Search This Blog

Sunday 20 November 2022

NYUMA YAKO (4) - 1

 





    IMEANDIKWA NA : STEVE MOLLEL



    *********************************************************************************



    Simulizi : Nyuma Yako (4)

    Sehemu Ya Kwanza (1)





    ILIPOISHIA

    “Naomba unikumbushe maswali hayo,” akasema Kelly.

    “Sawa. Labda niyageuze na kuyafanya yawe ya moja kwa moja zaidi,” akasema Marshall na kuuliza, “Unamfanyia kazi nani?”

    Kabla Kelly hajajibu swali hilo, simu yake ikaita. Alikuwa ni Marietta. Alipokea simu hiyo na kuiweka sikioni.

    “Umefika?”

    “Ndio.”

    “Naomba niongee na Marshall.”

    Kelly alidhani amesikia vibaya. Marietta akarudia tena ombi lake. Anataka aongee na Marshall.

    Basi Marshall akapewa simu.

    ENDELEA

    "Marshall," Marietta akaita, kisha akajitambulisha na baada ya hapo akamweleza Marshall juu ya namna gani mambo yalivyo. Yeye ni mke wa Raisi na angemtaka Marshall amruhusu Kelly aende Morocco kumsaidia kumkomboa Raisi.http://pseudepigraphas.blogspot.com/

    "Najua nitakuwa nakuchanganya, Marshall. Mambo ni mengi muda ni mchache. Nitaeleza kila kitu nitakapopata muda."

    Kidogo Marshall alikuwa amekanganyikiwa. Ina maana Marietta alikuwa anajua mahali ambapo Raisi yupo? Muda wote ule?

    "Marshall, mimi ni mkosaji. Nataka tu nimkomboe mume wangu kabla ya kufa kwangu. Tafadhali."

    Basi Marshall akakata kwanza simu. Akawaza kwa kitambo kidogo kabla ya kuwashirikisha wenzake juu ya kinachoendelea.

    "Huko Morocco sehemu gani?" Marshall akamuuliza Kelly. Macho alikuwa ameyakaza kana kwamba mbogo aliyejeruhiwa.

    "Morocco kwa mwana wa mfalme," akasema Kelly. "Anaitwa Abdulaziz na ndiye yeye aliyemteka Raisi akimtumia Marietta na wengineo."

    "Kwahiyo una uhakika kuwa Raisi yupo huko?"

    "Uhakika ni asilimia zote. Hapa ninapokuambia, tayari vita ya madaraka ya kifalme imekwisha anza. Abdulaziz alituita kwenda kumsaidiza, mimi pamoja na K. Lakini mimi sikuwa upande wake."

    "Ndiyo maana ukamuua K?"

    "Ndio. Ilibidi niwahi kummaliza kabla yeye hajanimaliza."

    "Kwanini akumalize?"

    "Kwasababu mimi na yeye tuna interest tofauti."

    "Zipi hizo?"

    "Mimi namtumikia Marietta. Yeye anamtumikia Abdulaziz."

    Kukawa kimya kidogo. Ni kama vile watu walikuwa wamemezwa na bumbuwazi. Ilikuwa ngumu kuamini kinachotukia.

    Walipofikiri baada ya muda kidogo na kujadiliana, Marshall akapiga simu kuongea na Marietta.

    "Kama ni hivyo, nasi tunakuja huko," akaema maadhimio yao.

    "Lakini Marshall, huku si salama. Na pia ikigundulikana kuna mkono wa Marekani itazorotesha mahusiano ya kidiplomasia," Marietta akatoa angalizo.

    "Kama kungekuwa na haka ya kutunza mahusiano ya kidiplomasia, wasingemteka Raisi wetu. In fact, tunakuja huko kama genge na si watu waliotumwa na serikali ya Marekani.

    Na kuhusu usalama, hilo lisikupe tabu. Tumeshazoea maisha hayo kiasi kwamba tukiyakosa, tunahisi kupungukiwa."

    Kukawa kimya.

    "Kwahiyo tumekubaliana?" Marshall akauliza.

    "Ndio," Marietta akajibu. "Nitafanya namna ya kuwafikisha hapa," akaongezea na taarifa kabla ya kukata simu yake.

    "Tujiandae," Marshall akawaambia wenzake. "Safari ya kwenda Morocco ipo njiani!"

    Basi ndivyo muda ukaenda vivyo. Baadae, kama lisaa limoja lilipopita, Danielle akakutana na Marshall kando na kumweleza kumhusu bwana James. Bwana huyo amemfuata na kumtaka ampe ushahidi wote kumhusu Ian.

    Kama asipofanya vivyo, basi ataruhusu picha alizowapiga zitumike kwenye upelelezi.

    "Ametupata sehemu dhaifu hivi sasa," alisema Danielle. "Hatuna ujanja, Marshall. Ni lazima sasa tushirikiane naye."

    Marshall akawaza kidogo. Akashusha pumzi ndefu na kuuliza, "Unavyoona itakuwa threat kwetu?"

    "Sidhani," Danielle akajibu. "Kama ingekuwa threat basi angeshavujisha mpaka sasa."

    "Sasa tunafanyaje?"

    "Mimi nina wazo."

    Marshall akamtazama Danielle. Macho yake yalikuwa yanauliza kuhusu wazo hilo.

    "Inabidi tuwe karibu sasa na James."

    "Serious?"

    "Yah, Marshall. Serious. Kadiri James anavyokaa mbali nasi anaweza kutuumiza. Sasa kulidhoofisha hili yatupasa tukae naye karibu. Ni mtu mwenye lengo jema. Tunaweza pia kumtumia akatusafisha kila tunapoacha nyayo. Unaonaje?"

    Marshall akafikiri kidogo. Ni kweli mawazo ya Danielle yalikuwa yanaleta 'sense' ndaniye, basi akaridhia kufanyika kwa kile alichosema.

    "Lakini inabidi tuwe waangalifu sana, Danielle. Mtu yeyote anaweza akawa nyuma yako na kukuchoma kisu cha mgongo."

    Danielle akatabasamu. Alikuwa amebeba agizo hilo.

    Basi baadae ikiwa ni usiku wa saa nne, mwanamke huyo akasogeza gari lake mpaka mahali ambapo amekubaliana na James wakutanie. Hapo akazima gari na kuwasiliana na mlengwa wake kwa ujumbe.

    Muda si mwingi, James akafika eneo husika akiwa amekuja na bwana Smith. Lakini hakuwa ameongozana na bwana huyo bali alimwacha kwenye gari.

    "Umewahi!" Danielle akamkaribisha mwanaume huyo kwa tabasamu.

    "Nashukuru, nilikuwa nipo tenge tangu tumekubaliana kukutana muda huu," akasema bwana James. Bwana huyo alikuwa amevalia suti kama ilivyo kawaida yake. Lakini mara hii nywele zake alikuwa amezilaza vema akiwa amezipaka nywele dawa kana kwamba mate.

    Alipendeza.

    Alimtazama Danielle na kumuuliza kama amekuja kama vile walivyokubaliana. Danielle kabla ya kujibu akatabasamu.

    "Nawezaje kuja kama sipo kamili?"

    Naye James akatabasamu. Ni punde Danielle akatoa bahasha ya kaki na kumkabidhi mwanaume huyo. James akatazama ndani na kisha akatabasam tena.

    "Naweza nikakuamini?" Akauliza.

    "Bila shaka," Danielle akamhakiki. Basi James akaweka bahasha hiyo ndani ya koti lake na kisha akatazama mbele kuangalia gari alilokuja nalo.

    Kuna kitu alikuwa anawaza. Alishusha pumzi ndefu puani alafu akamtazama Danielle na kumuuliza, "Hamna kingine ungependa kunishiriki?"

    Danielle akatikisa kichwa. "Hapana." Akamtazama mwanaume huyo akiwa anajiuliza kitu kichwani. "Kwanini umeniuliza vivyo?"

    "Kwasababu nahisi una kingine."

    "Mimi?"

    "Ndio. Sikia Danielle, najua kuna mengi mtakuwa mnayafanya nyuma ya pazia. Sidhani kama itakuwa vema mtu mwingine akawa wa kwanza kuyaona kabla yangu. Itawaweka matatizoni."

    Danielle akawa kama mtu aliyeganda. Alibaki kumtazama James.

    "Ni sawa," akasema bwana James akishika kitasa cha gari. "Unajua wapi pa kunipata kama ukinihitaji." Aliposema hayo akaenda zake kwenda kukutana na Smith.

    Kitendo cha kufunga gari lake, Danielle akaondoka zake. Wakamtazama mwanamke huyo akiishia.

    "Vipi?" Smith akauliza. "Umefanikisha?"

    James akawasha gari wakaenda zao.

    **

    Saa nne usiku ...

    "Unahisi hapa tupo salama?" Aliuliza Marietta akimtazama Mahmoud.

    "Yah! Kiasi chake," akajibu Mahmoud akitafuna. Mkononi alikuwa amebebelea mirungi kana kwamba majani ya kumlisha sungura. Zainab yeye alikuwa ameketi jikoni akipika.

    Mazingira ya hapa yalikuwa pweke kiasi. Hakukuwa na nyumba nyingi, makazi machache yanayoweza kuhesabika. Makazi haya yalikuwa yanafanana kwa kiasi fulani kwenye muundo.

    "Kiasi chake?" Marietta akauliza. "Una maana gani kiasi chake?"

    Mahmoud akamtazama Marietta. Bado mwanaume huyo alikuwa anatafuna majani yake kana kwamba mbuzi.

    "Kwakuwa bado tupo Morocco hamna mahali itakuwa salama kwetu kwa kiasi hicho unachotaka. Abdulaziz ana mkono mrefu. Cha kufanya ni kwenda mahali ambapo itamchukua angalau muda kupajua."

    "Ndiyo hapa?" Marietta akauliza.

    "Ndio, Shanny. Hujaridhika napo?"

    Kabla Marietta hajajibu, Zainab akawa amefika na sinia lililobebelea vikombe vitatu vya kahawa. Akawapatia Mahmoud na Marietta kisha naye akachukua cha kwake na kuketi chini.

    Mahmoud akamtazama mkewe alafu akatabasamu. Alikuwa anafurahi kumwona mkewe papo. Naye mkewe alitabasamu kabla hajamtazana Marietta na kumuuliza,

    "Mmefikia wapi?"http://pseudepigraphas.blogspot.com/

    "Pazuri. Kama mipango yangu ikienda vema basi keshokutwa watu watakuwepo hapa."

    "Una hakika watakusaidia?"

    "Sana. Nimepata ziada ya watu, watanisogeza sana. Nadhani mipango yetu itakaa sawa endapo wakifika hapa."

    "Na vipi ule mpango Aziz?" Akauliza Zainab akimtazama Mahmoud. Mahmoud akabinua mdomo wake na kutafuna.

    Mpango wa Aziz ulikuwa ni wa kumtafuta kaka yake na Mahmoud kwa ajili ya kumshawishi awe upande wao kumshinda Abdulaziz.

    Aziz alikuwa ndiye 'crown prince', yaani mwana mfalme ambaye ndiye mwenye wakfu wa kuwa mfalme punde baba yake atakapochoka ama kufa.

    Kiuhalisia Aziz alikuwa ni mwana mwenye nguvu kuliko wote. Karibia robo tatu ya jeshi yote ilikuwa chini yake, kutimiza jeshi lote ingempasa mpaka pale baba yake atakapofariki ama kuachia madaraka.

    Basi mwana huyo kwakuwa ndiye ambaye anatazamia kupokea kijiti cha ufalme, ulinzi wake ni mkubwa. Si rahisi kumwingilia katika nyakati zote.

    Ana ushawishi mkubwa ndani ya nchi kama kiongozi ajaye.

    "Mke wangu," Mahmoud akaita akimtazama Zainab. "Unajua si rahisi kumpata Aziz. Mbali na mfalme yeye ndiye mtu anayelindwa zaidi. Jambo letu litachukua muda kidogo kutimia."

    "Laaziz," Zainab akaita akiuweka mkono wake juu ya kiganja cha Mahmoud. "Hatuna muda wa kungoja sana. Ni ngumu kumpata Aziz maana hajajua adhma ya wito wako. Laiti angelijua basi ni yeye ndo' angekuwa anakutafuta."

    "Saa tutafanyaje unadhani?"

    "Tafuta namna ya kuwasiliana naye. Njia yoyote ile. Mwambie una ujumbe wake nyeti."

    Mahmoud akashusha pumzi ndefu. Akamtazama Marietta na kumuuliza, "unasemaje, Shanny?"

    "Yuko sawa. Nadhani tumtafute yule mpambe wake. Yeye atakuwa njia nyepesi kumwingilia Aziz."

    Mahmoud akafikiri kidogo. Alikubaliana na wazo hilo lakini kulikuwa na tatizo kidogo.

    "Sikuwa nataka kwenda huko kabisa. Si salama kwangu. Ilaa ..... sina budi, nitafanya tu."

    "Lini?" Zainab akawahi kuuliza. Mahmoud akamshika mkono mwanamke huyo na kumtazama ndani ya macho. "Kesho ama keshokutwa."

    Alipomaliza tu hiyo kauli, akasikia vishindo vya mtu. Kutazama malangoni, akamwona mwanaume fulani aliyekuwa amevalia kanzu na kichwa chake amekifumba kiremba.

    Mwanaume huyo alikuwa ametoa macho, uso wake ulikuwa umebebelea hofu. Alishika kingo za mlango akaropoka, "wamefikaa!"

    Mwanaume huyo alikuwa anavuja damu mgongoni kwa wingi. Kitendo tu cha kumalizia kusema kauli yake, ikasikika sauti kubwa paaaaah! Kisha mwanaume huyo akadondoka chini vumbi la damu likimwagika toka shingoni!

    "Amka upesi upesi!!" Akafoka Mahmoud. Haraka akiongozana na Marietta na Zainab wakaenda chumbani ambapo huko walijifungia na mwanaume huyo akabonyeza kitufe fulani ukutani.

    Kitufe hicho kikasafirisha habari kwenye vijumba vyote vilivyokuwapo maeneo hayo. Kukawa na mlio wa king'ora kana kwamba gari la polisi.

    Na katika king'ora hicho zikasikika na sauti za risasi huku na kule. Zilikuwa zinarindima kana kwamba mvua! Wafuasi wa Mahmoud walikuwa wakipambana na wavamizi.

    Basi Mahmoud akiwa ndani ya chumba, akafungua mlango wa andaki wakazama humo. Lilikuwa ni andaki refu kama chemba ya kusafirishia maji machafu.

    Wakatembea humo kwa upesi Mahmoud akiwa amemshika mkono mke wake, Zainab. Kama baada ya hatua kadhaa, wakasikia sauti

    http://pseudepigraphas.blogspot.com/



    Na katika king'ora hicho zikasikika na sauti za risasi huku na kule. Zilikuwa zinarindima kana kwamba mvua! Wafuasi wa Mahmoud walikuwa wakipambana na wavamizi.

    Basi Mahmoud akiwa ndani ya chumba, akafungua mlango wa andaki wakazama humo. Lilikuwa ni andaki refu kama chemba ya kusafirishia maji machafu.

    Wakatembea humo kwa upesi Mahmoud akiwa amemshika mkono mke wake, Zainab. Kama baada ya hatua kadhaa, wakasikia sauti ya vishindo vikuu ndani ya handaki!

    ENDELEA

    Ilikuwa ni tafrani! Iliwapasa wakimbie zaidi na zaidi kwa ajili ya kukomboa nafsi zao. Lakini ndani ya humo humo handaki kulikuwa na mahali na mahali, kidogo walipokimbia, Mahmoud akasimama mahali na kubandua kitu ukutani. Kulikuwa na kama kadroo hapo.

    Mahmoud akachomoa bunduki humo, tatu kwa idadi, akamkabidhi kila mmoja wao silaha na kuwataka waikoki kwa ajili ya kujilinda.

    Baada ya hapo wakaendelea tena kukimbia na kukimbia. Walipofika tena mahali fulani, sasa wakiwa wamekaribiwa zaidi na watu wanaowakimbiza, bwana Mahmoud akaendea tena ukuta.

    Bwana huyu alikuwa na ramani yote ya handaki kichwani. Alikuwa anajua kila mahali na kwa kila hatua.

    Hapo ukutani akafunua tena. Humo hakukuwa na silaha tena kama mwanzoni bali kulikuwa na kifaa fulani cha mstatili, kilikuwa cheusi kwa rangi.

    Upesi Mahmoud akakifungua kifaa hicho na kubinya mahali, mara kifas hicho kikawaka na kuanza kuonyesha muda.

    Kwa haraka Mahmoud, akabinyabinya vitufe kutunza muda. Aliweka dakika mbili tu. Wakaendelea kukimbia na basi sasa kile kifaa kikawa kinazidi kuongeza sauti kulia ikihesabu muda chini.

    Punde muda ukawa umebakia sekunde thelathini. Kidogo tu, wakafika hapo wanaume watatu waliokuwa wamebebelea silaha kubwa.

    Walitambua hapo kuna kifaa kinacholia kwani kilikuwa kinatoa mwanga. Walipotazama ukutani - doh! - Wakabaini walikuwa wamekawia. Muda ulikuwa umewaishia!

    Lakini nani hukubali roho yake kutoka kwa urahisi? Basi mabwana hao wakakimbia kurudi walipotokea. Wasipige hata hatua nne, bomu likalipuka na kuwatupa haswa!!!

    Si kuwatupa hai, hapana, vipandevipande vya nyama na damu. Lakini pia kama haitoshi moto ukashika humo ndani ya handaki kwenda pande zote.

    Joto lilifukuta moto ukikimbia haswa.

    Mahmoud na wenzake walikuwa bado hawajatoka humo ndani ya handaki. Mlango ulikuwa kama hatua thelathini toka walipo, bado walikuwa wanaendelea kukimbia!

    Kwasababu ya bomu kulipuka humo, kulikuwa ma mtetemeko mkubwa na ilikuwa ni swala la muda tu kwa handaki zima kumomonyoka. Vumbi lilikuwa linateremka na pia vipandevipande vya mawe na vikokoto.

    "Kimbia! Kimbia!" Alifoka Mahmoud akiongeza ukubwa wa hatuaze. Walikimbia sana. Walipobakiza hatua kama nane hivi kufikia lango, mara jiwe likaporomoka toka darini na kumkita Zainab kichwani! Tih!

    Mwanamke huyo akadhoofu akipoteza fahamu! Alikuwa anatiririsha damu pomono kichwani. Ni punde tu hijab yake ikawa imetepeta damu!

    "Zainab!" Mahmoud akaita akiwa anamtazama mkewe. Alihofia sana uhai wa mwenza wake. Macho yake yalimezwa na hofu, woga.

    "Mahmoud twende!" Marietta akasihi. Alimvuta mwanaume huyo waende kwani hali ilikuwa inazidi kuwa mbaya humo. Joto ni kali na pia handaki lilikuwa linaelekea kumomonyoka.

    "Twende la sivyo tutakufa humu! Twendee!!" Marietta akaendelea kusihi. Mahmoud akanyanyuka na akiwa amembebelea mkewe akasonga wakikwepa mawe na mitaro ya vumbi iliyokuwa inatiririka toka juu.

    Walifikia lango wakakwea na kwenda nje. Walikuwa wametokea mahali ambapo palikuwa pametulia na pia pametingwa na msitu mkubwa.

    Hapo Mahmoud akamlaza mkewe chini akimtazama kwa huruma. Mwanamke huyo alikuwa ametulia kana kwamba maji mtungini.

    Basi alichokifanya Mahmoud ni kufungua hijab ya mkewe na kuifungia jerahani kisha akamtaka Marietta abaki hapo ingali yeye akienda kutafuta dawa hata ya mizizi.

    Mwanaume huyo akatoka upesi kuelekea mashariki. Alikuwa anakimbia huku akitupa macho yake huku na kule.

    Mpaka kuja kuona anachokitaka, ikawa imemchukua kama dakika sita hivi. Aliuendea mti lengwa alafu hapo akakata tawi na kuanza kulitumia kufukulia ardhi.

    Alifukua na kufukua mpaka kukuta mzizi. Akaung'ata na kuchomoa vipande alivyokuwa anavihitaji - vitatu kwa idadi!

    Mizizi hiyo ilikuwa michungu haswa. Na mbali tu na hivyo baada ya muda kidogo ilipoozesha kinywa cha Mahmoud kwa muda. Hakuwa anauhisi ulimi wake tena.

    Basi haraka akarudi kule alipowaacha wenziwe, ikamchukua kama dakika sita. Alipofika hakukuta mtu!!

    Akatahamaki.

    Akatazama kushoto na kulia kwake. Kidogo akahisi mlio wa risasi ukimpitia. Upesi akajificha nyuma ya mti kwa ajili ya usalama wake.

    Hapo akahema kwanguvu. Alihema kwa hofu lakini pia kwa kuchoka. Alijiuliza mkewe na Marietta watakuwa wapi akakosa kabisa majibu.

    Watakuwa hai ama watakuwa wameuawa? Alichomoza uso kuchungulia lakini kabla hajafanya jambo risasi ikatupwa upande wake! Upesi akarudisha uso kujificha.

    Moyo wake ulikuwa unakita ti-ti! Ti-ti! Ti-ti!

    Mawazo yake yote yalikuwa kwa mkewe. Kama yeye anawindwa hivi, mkewe huko atakuwa salama ukizingatia hali yake.

    Kidogo akasikia risasi zikirindima kwa kama sekunde tano mfululizo! Hapo naye akachungulia kujua kinachoendelea, mkononi akiwa ameshikilia bunduki yake.

    Kwa mbali kidogo akamwona mwanaume akikimbia. Alikuwa ni mwanajeshi. Mkononi mwake alikuwa amebebelea silaha. Alikuwa ndiye yule mwanaume aliyekuwa anamfyatulia risasi Mahmoud.

    Basi upesi Mahmoud akatoka hapo mtini na kuanza kumfukuza mwanaume yule. Alikimbia haswa. Kidogo akawa anamkaribia karibu na karibu.

    Ghafla mwanaume huyo akageuka nyuma, kabla hajafanya kitu, Mahmoud akamtupia rizasi na kumfanya mwanaume huyo awe 'helpless' chini.

    Alikuwa anavuja damu tu.

    Mahmoud akamjongea mwanaume huyo na kumuuliza, "mke wangu yuko wapi?"

    Alimkwida mwanajeshi huyo kwa nguvu. Alikuwa akimtikisatikisa kana kwamba kibuyu. Lakini mtu anayekufa anawezaje kuongea? Mwanajeshi huyo alikuwa anamimina damu mdomoni kwa wingi.

    Macho yalikuwa yamemtoka kwenda kifoni.

    "Mke wangu yupo wapi???" Mahmoud akaendelea kufoka. Kidogo tu mwanajeshi huyo akafa.

    "Shit!" Mahmoud akalaani. Akautupia mzoga huo pembeni kisha akaendelea kukimbia kwenda kule mwanajeshi yule alipokuwa anaenda.

    Akiwa anaenda akawa anaita jina la mkewe na pia la Shanny. Kidogo ndipo akakutana na walengwa wake, Marietta alikuwa amejilaza kando na mto, Zainab akiwa amepoa kabisa.

    "Shanny, nini kimetokea?" Mahmoud alifoka kuuliza huku akimkimbilia mkewe. Alipomfikia akamshika na kumuita mara kadhaa.

    "Ilibidi tukimbie. Maadui walikuwa wanatuwinda!" alisema Marietta.

    "Maadui gani?" Mahmoud akauliza. Marietta akanyooshea kidole upande wake wa magharibi. Huko Mahmoud alipotazama akaona miili minne ya wanaume ikiwa imelala mfu.

    "Samahani, Mahmoud. Nimeshindwa kumsaidia Zainab."

    Machozi yakaanza kummiminika Mahmoud mashavuni. Zainab alikuwa amekufa! Mwili wake ulikuwa unaelekea kuwa wa baridi.

    "Hapana!" Mahmoud akalia. "Hapana, Zainab! Hapanaa!!" Akalia kwa sauti kuu. Lakini wasidumu hapo kwa muda mrefu, wakasikia watu wakija.

    Hawakuwa na muda bali kuondoka hapo upesi.

    Lakini Mahmoud alikuwa amebebelea kinyongo kikubwa kifuani mwake. Alikuwa anahisi kifua chake ni kizito sana. Uzito kuliko mwili wa mkewe ambao ameubeba mgongoni.



    **http://pseudepigraphas.blogspot.com/



    Baada ya risasi moja kupiga, mtu alidondoka chini kana kwamba gogo. Abdulaziz alimtazama mtu huyo ambaye sasa alishakuwa marehemu akatoa agizo mwili huo ukatupiwe mbali.

    Basi wakaja wanaume wawili ambao waliuburuza mwili huo kwenda nao nje. Sakafu ikiwa inajaa damu.

    Walipotoweka, Abdulaziz akakaa kitako akiwa analaani. Akiwa anatusi. Alikuwa amekwazika. Jasho jembamba lilikuwa linamchuruza kwenye paji la uso.

    Macho yake yalikuwa mekundu haswa.

    "Jamal, mara hii sitau hawa washenzi wako. Nitakumaliza wewe!!" Abdulaziz akafoka akimtazama Jamal.

    Jamal alikuwa amekaa kama mbwa mwitu aliyepokonywa nyama.



    **

    Siku mbili baada ...



    Wimbi kubwa lilipiga chombo na kukiyumbisha haswa. Marshall aliyekuwa amelala kwenye chumba kidogo akaamka na kuangaza. Kidogo alikuwa aanguke toka kitandani.

    Alinyanyuka na kuangaza namna chombo chao kinavyoyumba. Ikachukua kama sekunde thelathini chombo hicho kutulia.

    Basi Marshall akatoka ndani ya chumba chake na kwenda koridoni. Akashika kingo ya boti na kutazama maji. Ilikuwa ni usiku. Maji yalikuwa yamechafukwa kiasi chake!

    Chombo kilikuwa kinaenda juu na kurudi chini ... chini tena na juu kwa kadiri mawimbi yalivyokuwa yanakwenda.

    Upepo nao haukuwa haba. Ulikuwa unapuliza sana.

    Basi Marshall akiwa hapo akasikia mtu akitapika. Akajikuta akipata hamu ya kujua, akasonga kutazama chumba kinachofuata, huko akamkuta Jack akiwa anatapikia kwenye mfuko. Tumbo lilimvuruga.

    Kajasho chembamba kalikuwa kanamchuruza.

    Marshall akiwa hapo anamtazama mwenzake, kabla hata hawajazungumza kitu, akastaajabu mwanga unammulika. Alipogeuza shingo yake kutazama, akaona boti kubwa umbali wa kama kilomita moja toka walipo.

    Mara kidogo sauti toka kwenye kipaza sauti ikapaza kwanguvu,

    "Mpo kwenye mpaka wa maji wa Morocco. Ninyi ni wakina nani?? Jitambulisheni na mtuonyeshe nyaraka zenu upesi!!"

    Marshall akang'ata lips yake ya chini kisha akasema, "oh God! Mbona mapema hivi?"



    **



    Marshall aliwaza cha kufanya na punde akaona ni vema akawataarifu wenzake kuhusu tukio hilo, lakini kabla hajafanya vivyo akabaini wenzake tayari wameshatoka ndani kutazama.



    Watu hao walikuwa ni watatu kwa idadi: Kelly, Danielle na Jack. Wote walikuwa wametoa macho wakijaribu kuelewa kuna nini kinachoendelea. Kidogo Kelly akasafisha koo lake kama ishara alafu akasema,



    “Acha niongee nao. I can handle this.”



    “Sure?” Marshall akapata shaka kidogo. Alimtazama Kelly anavyosonga karibu naye.



    “Yah! Si mara ya kwanza nafanya hivi,” akasema Kelly kwa kujiamini. Akasonga karibu kabisa na kushika kingo ya boti akitazama wale wageni wao. Muda si mrefu mwanamke huyo akakutana na hao wageni kwenye boti yao, boti ya serikali.



    Ilikuwa ni boti kubwa yenye maafisa kama kumi na tano kwa idadi. Wawili walikuwa ni manahodha, wengine watatu wakiwa ni watu wanaohusika na ufundi na wengineo waliobaki wakiwa ni kama walinzi. Hao ndo walikuwa wamebebelea bunduki na wapo tenge kwa lolote litakalotokea!



    Basi Kelly akiwa anatembea kwa madaha, akasonga mpaka kwa ‘captain’ wa boti na kumweleza kidogo kumhusu. Mwanamke huyo alijitambulisha kwa kusema kuwa yeye ni moja wa washiriki wa bwana Abdulaziz, mwana wa mfalme.



    “Bila shaka mimi si mgeni machoni mwako,” alisema Kelly akimtazama captain kwa kurembua. Captain akatabasamu kidogo, akamtazama mwanamke huyo na kumwambia, “ngoja!” kisha mwanaume huyo akaenda zake ndani kufanya mawasiliano.



    Kelly hakuwa na hofu. Haikuwa mara yake ya kwanza kukumbana na kadhia kama hiyo. Akiwa amerelax akangoja kwa kama dakika tatu kabla ya captain hajaja na kumwambia,



    “Sijapata uhakiki wake.”



    “Una maana gani hujapata uhakikiki wake?” Kelly akauliza upesi.



    “Simu haijapokelewa kwahiyo hatuwezi kuwaruhusu,” akasema captain kisha akatoa ishara kwa watu wake wa usalama, wale waliobebelea bunduki, punde mabwana hao wakafuata wakina Marshall na kuwaweka chini ya ulinzi.



    Wakawaamuru waende kwenye boti yao, nao walengwa wakatii.



    “Hamuwezi kutufanyia hivi!” akasema Kelly akikunja sura. “Punde Abdulaziz atakapojua mlichofanya mtakuwa mahali pabaya.”



    Hakuna aliyemsikiliza, wakasweka ndani ya chumba fulani na kufungiwa humo kwa komeo. Ndani kulikuwa ni kiza. Boti likawashwa na kutimka kuendelea na doria katika usiku huo.



    “Sasa tunafanyaje?” akauliza Marshall. Alikuwa haonekani bali kusikika tu. Kwa mbali sauti ya mawimbi ilikuwa inasikika yakiwa yanakatwa na ncha ya boti.



    “Tungoje kwanza,” akasema Kelly. “Nadhani hatuna haja ya kutumia nguvu hapa.”



    “Tutangoja mpaka muda gani?” Danielle akauliza. “Endapo jua likichomoza itakuwa ni hatari zaidi kwetu.”

    http://pseudepigraphas.blogspot.com/

    “Jua halitachomoza,” akasema Kelly kwa kujiamini. “Muda si mrefu Abdulaziz atapiga.”



    “Lakini ulisema wewe haumfanyii kazi bwana Abdulaziz,” Jack akatia neno.



    “Ndio, lakini bwana Abdulaziz hatambui hilo,” akasema Kelly. Basi wakangoja humo kwenye boti kwa kama robo saa, kimya. Wakaendelea kuvuta subra.



    Ilipopita dakika ishirini na tano, sasa hata Kelly na yeye akaanza kupata wasiwasi na ukimya ule, akanyanyuka aende kugonga mlango asikizwe. Kabla hajafika, mara boti ikayumba na kumdondosha chini! Puh!



    Boti ikayumba na kuyumba kwa muda kidogo kiasi kwamba akashindwa kabisa kusimama. Bahari haikuwa shwari.



    Hawakukaa sana mara maji yakaanza kuzama humo ndani! Boti ilikuwa inayumba sana kwa sasa! Mawimbi yalikuwa makubwa na upepo nao ulichachamaa.



    Boti ilipelekwa kushoto na kulia, juu na chini! Marshall pamoja na wenzake wakawa wanagongana na kuvamiana wakitupwa huku na kule.



    “Inabidi tufanye jambo!” akasema Marshall. “La sivyo tutakufa humu!”



    Ni wazi moja ya madirisha yaliyokuwa kwa chini humo chumbani yalikuwa yamepasuka. Maji yalikuwa yanazama ndani kila mara boti unavyoyumba!



    Kidogokidogo yalikuwa yanaongezeka!



    Punde kidogo mara king’ora kikaanza kulia. Boti ilikuwa imefungiwa mtambo wa kutambua hitilafu ya kuzamia kwa maji chomboni. Basi upesi wale mabwana wanaohusika na ufundi wakaanza kufanya namna kukabiliana na hatari hiyo.



    Kidogo ndipo wakabaini tatizo. Ni chumba cha chini!



    Basi upesi wakafungua mlango na kuanza kufanya marekebisho! Lakini haikuwa rahisi hata kidogo. Bado boti ilikuwa inayumbayumba kupelekeshwa na mawimbi. Utulivu ulikuwa ni mgumu kupatikana.



    Kuna muda bwana mmoja akajikuta akitupwa na kwenda kujikita ukutani, akapoteza fahamu papo hapo! Mwingine naye almanusura kudondoka kama isingalikuwa kujishikiza na nguzo.



    “Mmekamilisha?” akauliza captain. Akiwa amekaa karibu na usukani alikuwa amejishikza asiyumbe. Kulikuwa na sauti kubwa ya king’ora kwenye ‘system’ kumjulisha kwamba boti halipo salama.



    Alama ya tone la maji lenye rangi nyekundu ilikuwa inamwekamweka chini ya usukani wake.



    “Bado, hali si nzuri kabisa!” sauti ikamjibu toka kwenye ‘radio call’ ya boti. “hatupati utulivu wa kufanya kazi kabisa!”



    “Fanyeni upesi!” captain akafoka. “Hatuna muda mrefu hapa. Mpaka chombo kiz--” wimbi kubwa likachapa kioo cha mbele kabisa ya boti na kufanya chombo hicho kisimame karibia na kubinukia huko nyuma!



    Wimbi lilipopita, boti likarudi chini kwanguvu! Maji yakaruka juu na kuifunika boti hiyo kana kwamba mvua! Ni kheri boti ilisimama japo kwa mrama.



    Upande wa kushoto wa uso wa Captain ulikuwa unavuja damu. Alikuwa amechoka. Bega lake pia la kulia lilikuwa linamvuta kwa maumivu makali. Akashika chombo cha mawasiliano na kuuliza,



    “Mmekamilisha? --- mmekamilisha?”



    Akatambua kifaa hicho hakikuwa kinafanya kazi tena. Maji yalikuwa yanachuruza toka ndani yake. Akatupia kifaa hicho chini na kujaribu kusonga aende kuangalia kinachoendelea.



    Akamtaka mwenzake ashikilie usukani kurudisha chombo nchi kavu mara moja ingali yeye akitazama usalama.



    Akafika kule chumbani, japo kwa shida, akakuta chumba kikiwa kimejawa na maji mengi! Akamulika na kurunzi asione mtu yoyote humo.



    Akaita. Kimya.



    Kidogo akatambua kuwa kuna sauti inatokea upande mwingine. Alipoenda kutazama, akakuta watu wake wakiwa chini, wanne kwa idadi! Na upande wa kushoto wa kile chumba kilichokuwa kimejaa maji, pia kulikuwa kunapenyeza maji kwa vingi vilevile!



    Hajakaa muda mrefu pia akatambua kuwa boti haikuwa inakwenda kama vile alivyomuachia maagizo captain mwenzake! Kwa muda kidogo akashindwa kujua cha kufanya.



    Tih!!! maji yakachapa tena boti! Mara hii yalipiga kwanguvu sana kiasi kwamba captain hakuweza kumudu kujizuia. Alitupiwa ukutani na akapoteza fahamu mara moja!



    “Boti inazama! Narudia, boti inazama!” ilikuwa sauti ya captain aliyeachwa kwenye usukani. Hakuwa na kingine cha kufanya kuokoa chombo chao. Akiwa anaongozana na wenzake kadhaa wakanyofoa maboya na kujivika kisha wakatumbukia ndani ya maji.



    Hata hawakuwakumbuka wenzao.



    Walipookoa nafsi zao ndipo wakaanza kuulizana juu ya wengine.



    “Watakuwa wamekufa!” mmoja akasema. Alikuwa ameshikilia boya na huku pia ameshika bunduki, bunduki iliyojawa na kushiba maji.



    “Vipi tukaenda kuwatazama?” mmoja akauliza, lakini uso wake haukuwa unaonyesha kama kweli anamaanisha alichosema.



    “Tutaendaje kwenye boti inayozama?” akauliza mwingine. Kabla ya yule aliyetoa wazo hajaongezea neno, akahisi jambo. Alibinyabinya boya lake kisha akawatazama wenzake kwa macho ya mshangao na kusema,



    “Nahisi boya langu linapungua upepo!”



    Wenzake nao walipotazama yao, wakagundua wote walikuwa kwenye mkondo mmoja. Hawajakaa sawa, wakafunikwa na wimbi kubwa lenye urefu wa nchi zisizopungua kumi na tano!



    Bwaaaah!!





    **

    http://pseudepigraphas.blogspot.com/



    “Umefanya vema!” akasema Kelly akimgusa bega Marshall. Mwanamke huyo alikuwa ametoka kuchungulia kwenye vioo vya hadubini. “Hawataweza kudumu baharini. Watakufa kama wenzao!”



    Marshall akamtazama Kelly, mwanamke huyo hakukaa nao sana akaelekea ndani ya chumba. “Sasa tunaweza kuendelea na safari yetu,” ikawa ndo kauli ya mwisho ya Kelly kabla hajaufunga mlango.



    Kidogo kukawa kimya kwa mazungumzo. Danielle alimtazama Marshall kisha akamuuliza, “Una uhakika huyu ni mtu wa kumuamini?”



    Wakati akiwa anauliza vivyo alikuwa anatazama mlango alimozama mwanamke huyo.



    “Hatuna budi kuwa naye,” akasema Marshall. “Yeye ndo njia pekee ya kumpata Marietta, na hatimaye Raisi.”



    Marshall aliposema hivyo akawaacha wenzake hapo na kwenda kule alimo Kelly. Alifungua mlango na kuangaza, akamkuta mwanamke huyo anatapikia kwenye mfuko.



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog