Search This Blog

Sunday 20 November 2022

VIPEPEO WEUSI: FROM ZURICH WITH RULES - 5

 





    Simulizi : Vipepeo Weusi: From Zurich With Rules

    Sehemu Ya Tano (5)









    Gari ambayo tulikuwa tunaitumia tulikuwa tumeikodi kutoka kwa kampurufu ya ukodishaji magari hapa Zurich inayoitwa ILOM. Nililipia dola za kimarekani 388 gharama kukodi gari pamoja na kodi kwa ajili ya kuwa nayo hii gari kwa muda wa wiki nzima. Ilikuwa ni gari aina ya Nissan Juke AWD.



    Nilikuwa nahisi kwamba katika siku hizi zijazo tutakuwa na mizunguko mingi sana hapa Zurich na sikutaka kutumia usafiri wa umma kwa kuhofia labda kuna uwezekano polisi wakawa wananitafuta kutokana na kifo cha Luke na kunikuta nyumbani kwake juzi na kuwapa taarifa zangu za uongo.



    Tulikuwa tumepaki gari ng'ambo ya barabara mkabala na nyumba ambayo juzi usiku nilikuwa hapa kuipekua, nyumba ile mtaa wa Affolterntrasse. Nyumba hii hii ambayo pia Jimmy amekieleza kuwa ndipo ambapo Luke na Ivanka waliishi na wazazi wao waliowaasili, Bwana Delani na mkewe Zarah.



    Leo ilikuwa ni siku ya pili tumekuja tena hapa. Siku ya jana tulishinda hapa siku nzima pasipo kuona mtu yeyote akiingia ndani ya nyumba hii.



    "Nobody is gonn' come mate!" Jimmy aliniambia tena wasiwasi wake kwa mara nyingine tena karibia ya ishirini.



    Hakuwa anaamini kwamba kuna mtu ambaye alikuwa anakuja kwenye nyumba hiyo. Aliamini moyoni mwake kwamba tangu nyumba hiyo itelekezwe na Delani na mkewe hakukuwa na mtu ambaye anaishi humo.



    Nilikubaliana naye kwamba pia nilikuwa naamini hakukuwa na mtu anayeishi humo. Lakini nilikuwa na hakika kabisa kuna mtu lazima awe anaitunza. Kwa sababu ndani mwake imepangiliwa maridhawa mno na ni kusafi kana kwamba ni kila siku nyumba hii kuna mtu ambaye alikuwa anaifanyia usafi.http://pseudepigraphas.blogspot.com/



    Lakini kuna upande fulani moyoni nilikuwa natamani nikubaliane na Jimmy kwamba hakukuwa na mtu ambaye anaitunza nyumba hii. Nilihisi kama hisia zanhu hazikiwa sahihi tulikuwa tunapoteza muda mwingi sana hapa badala ya kufuatilia taarifa nyingine. Lakini kuna upande mwingine moyoni mwangu ulizidi kunitia moyo kwamba lazima kuna mtu anayefanya matunzo ya hii nyumba. Kwa nini barua ambayo niliandika nikiwa Tanzania kuja anuani hii ipokelewe? Kwa nini ndani kuwe kusafi namna ile? Hapana… nilijipa moyo kwamba hisia zangu ni sahihi?



    "If someone comes, then what?" Jimmy aliniukiza.



    Nilikuwa sina uhakika sana ni nini hasa nitakifanya kama mtu akitokea kweli na kuingia kwenye nyumba hiyo… ni kipi ambacho nitakifanya.



    "Not so sure of what I will do… lets wait and see!"



    "You are insane mate… we spend two days out here and you……"



    "…quite… look… look.!"



    Nilimkatisha Jimmy alichokuwa anaongea na kumuonyesha ng'ambo ya barabara. Kulikuwa na gari imefika na kupaki barabarani nje ya ile nyumba.

    Ilikuwa ni gari ndogo aina ya Volkswagen Polo nyekundu. Ilisimama barabarani karibu na ile nyumba. Akashuka binti mmoja mweusi, mrefu kiasi… alikuwa amevalia suruali ya jinzi ya buluu yenye kubana na juu alivaa blauzi kama ya rangi ya kahawia. Mkononi alikuwa amebeba mifuko kadhaa… kama mifuko mitatu hivi ya plastiki ya rangi ya maziwa ikiwa na vitu ndani yake kana kwamba ni mtu ametoka supermarket na sasa alikuwa anarejea.



    "Is it her?" Jimmy aliniuliza.



    "I don't know… let's see!"



    Alikuwa ni binti ambaye nilikadiria kwamba hawezi kuzidi umri wa miaka ishirini na tatu au ishirini na nne.

    Alifunga mlango wa gari na kisha kuanza kutembea mpaka kwenye ile nyumba. Alipofika mlangoni alisimama na kugeuka nyuma. Aligeuka na kisha kukaza macho kutazama gari yetu. Ilikuwa kana kwamba alikuwa ana mashaka hivi na gari yetu hapa ilipopaki. Aliitazama kwa muda wa karibia dakika nzima. Kisha akageuka na kuingia ndani ya nyumba.



    "Shiiiit.! She saw us!!" Jimmy aling'aka



    "It dosn't matter… we got her!" Niliongea huku natabasamu.



    Nilitabasamu kwanza kwa kusikia raha moyoni kwamba kwa mara nyingine tena hisia zangu zilikuwa sahihi. Lakini pia nilitabasamu kwa kuwa sasa nilikuwa nahisi kabisa nakaribia kutatua kitendawili ambacho kiko mbele yangu na kilichosababishe nije hapa Zurich.



    "Let's go!" Nilimuamuru Jimmy



    "Wait… wait! Go where?"



    "Let's go talk to her..!"



    "And tell her what exactly? Nah mate… i will wait here.! You go ahead."



    Jimmy alikuwa anagoma kuongozana nami kwenda kwenye ile nyumba. Uzuri sikuhitaji sana uwepo wake japo nilipendelea zaidi kama tungeongozana wote.

    Nikawa najiandaa kufungua mlango wa gari ili nielekee kwenye ile nyumba. Lakini kabla sijafungua mlango wa gari nilitupa jicho kwenye ile nyumba na kuona mlango ukifunguliwa. Mlango ulifunguliwa na kisha yule binti kutoka. Alitoka pamoja na ile mifuko yake ya plastiki yenye vitu ambayo alikuwa ameingia nayo. Alipotoka safari hii hakuangalia gari yetu kama mara ya kwanza. Alikuwa anatembea kana kwamba haoni gari yetu hapa ilipo, alitembea huku anatazama chini kwa hatua za haraka mpaka kwenye gari yake.



    "Is she leaving? She has been inside for only like two minutes!!" Jimmy aliongea kwa kunong'ona huku wote wawili macho yetu tunaangalia nje kutazama yule binti.



    Alifungua mlango wa gari yake, akakwea ndani na kisha kung'oa gari.



    Sikupoteza muda. Niliacha gari yake iondoke na kututangulia mbele kama sekunde ishirini tu hivi kisha na mimi nikang'oa gari na kuanza kumfuata kwa nyuma.



    Kichwani nilikuwa najiuliza, kwa nini huyu binti ameondoka haraka haraka kwenye ile nyumba? Au ametushitukia? Na kwa nini aogope watu kupaki gari karibu na ile nyumba?

    Nilikuwa na hakika kabisa kwamba huyu binti ndiye ambaye anaitunza ile nyumba kama ambavyo kilikuwa na hisia tangu juzi kwamba kuna mtu lazima anatunza ile nyumba.



    Kutoka mtaa huu wa Affolterntrasse kuna barabara inanyooka moja kwa moja kama umbali wa kilomita tatu hivi na kisha kukutana na barabra kuu. Ukiifikia barabara kuu ukipinda kulia unakutana na barabara inayoelekea katikati ya mji wa Zurich na kama utapinda kushoto unarudi kwenye maeneo yenye mitaa kama Hardstrasse.



    Huyu binti alipofika hapa kwenye makutano ya barabara akapunguza mwendo kidogo na kisha kusimama kabisa. Na mimi nikasimamisha gari nikimuacha umbali wa kama mita mia moja hivi mbele yetu.



    Alisimama pale kwa muda wa kama dakika moja hivi kisha akang'oa tena gari.



    Alipong'oa gari alipinda kona kwenda kulia barabara ambayo inaelekea katikati ya mji wa Zurich. Nami nikapinga kona kulia.

    Aliendesha mwendo wa kama dakika mbili hivi kisha akasimama tena. Nami nikasimamisha gari nyuma yake umbali wa kama mita mia moja.



    "What the **** is she doing!" Jimmy Aliuliza huku amekodoa macho kwa mshangao.



    "She trying to see if she is being followed!" Nikamjibu



    Nilishaelewa ni nini hasa huyu binti alikuwa anakifanya. Inaonekana pale kwenye ile nyumba alipotoka kwenye gari yake na kisha kutembea mpaka mlangoni na kugeuka kututazama tayari alikuwa na mashaka na gari yetu. Ndio maana hakukaa sana ndani alitoka na kuondoka. Aliposimamisha gari mara ya kwanza alitaka kuona kama sisi tutampita na hii ingemfanya ajue kwamba atumfuatilii. Lakini kitendo cha sisi kusimama nyuma yake yeye aliposimama kilimuhakikishia kwamba tunamfuatilia. Sikuelewa kwa nini aliamua kusimamisha gari tena kwa mara ya pili.



    Ghafla tuliona mlango wa ile gari ukifunguliwa na yule binti kushuka. Aliposhuka alianza kutembea kwa haraka kuja lilipo gari letu.





    "Mate… mate! Mate.!! She is coming for us.!" Jimmy alihamaki huku anataka kufungua mlango atimue mbio.



    "Hey! Relax.!" Nilimtuliza



    Siku zote nimekuwa naamini katika dhamira. Ukiwa na dhamira safi huwezi kudhulika. Unaweza kukutana na simba mwituni na kuangaliana naye macho kwa macho… ukiwa na dhamira safi na huna nia ovu juu yake anaweza kabisa kuona usoni mwako kwamba dhamira yako ni safi. Atageuka na kuelekea njia nyingine na safari yake.

    Ndivyo vivyo hivyo pia ilivyo kwa binadamu.



    Nilikuwa na uwezo wa kung'oa gari kuondoka kumkimbia huyu binti. Lakini sikutaka kufanya hivyo japo alikuwa anatembea kwa hasira kuja hapa tulipo akionekana dhahiri kabisa anakuja kwa shari.

    Siwezi kumkimbia, kwanza nataka kuzungumza naye na pia sina nio ovu dhidi yake.

    Nikatulia na kumwambia pia Jimmy atulie.



    Yule binti alifika kwenye gari yetu na kugonga kioo cha pembeni kwa nguvu kwa hasira. Nikashusha kioo.



    "Pourquoi me suivez-vous.!?" Binti alifoka kwa kifaransa mara tu baada ya kushusha kioo.



    "Sorry mam i don't speak french!" Nilimjibu kwa kutabasamu japo kwa kifaransa changu cha kuungaunga nilikuwa nimeelewa kabisa nini ambacho alikuwa anafoka.



    "Why are you following me?" Alifoka kwa kingereza safari hii.



    Niliweza kusikia lafudhi ya bara la Afrika safari hii alipoongea kingereza. Hii ilinifanya niwe 'curious' zaidi. Africa??



    "Sorry mam, we just want to talk!"



    Sikutaka kukataa kwamba tulikuwa tunamfuatilia. Niliona ni vyema tu niongee ukweli.



    "Then why don't you just come and talk to me! This is a third time you just park your car there and watch me.! Listen, If you don't stop following me I am to report you to the police… Bastard.!!"



    Yule binti alifoka na kisha kugeuka kwa hasira kurudi kwenye gari yake.



    "Third time?" Nilijikuta akili yangu imenasa neno hilo tu. Hii si mara ya tatu tunamfuatilia. Hii ni mara ya kwanza. Huyu binti anaongea kitu gani?

    Nikashuka haraka kwenye gari na kumkimbilia.



    "Hey miss! Sorry… Hey miss!" Nilimsimamisha kwa kumshika bega.



    "Don't touch me you bastard!" Aling'aka kwa hasira na kuendelea kutembea haraka kuelekea kwenye gari yake.



    "Miss I am trying to help you here… listen, your life could be in danger!"



    Nilipoongea kauli hii alishtuka kidogo. Alisimama na kugeuka kuniangalia. Alikuwa amefika kwenye gari yake tayari na alikuwa anajiandaa kufungua mlango. Lakini nilipomwambia kuwa maisha yake yako hatarini hakufungua mlango, aligeuka kuniangalia.



    "What are talking about?" Aliniuliza akiwa na taharuki usoni.



    "You said this is a third we have been following you… No, actually this is our first time… someone else is following you and you could be in great danger!"



    "What? Who are you then and why are following me… are you the police?"



    "No we are not… we just want to talk to the owner of that house!"



    "I am not the owner!" Alinijibu kifupi



    Moyoni nilijipa 'tano'. Nilikuwa sahihi. Kuna mtu kazi yake ni kuitunza tu ile nyumba.



    #314

    "I know! I just want to talk.!"



    "I don't understand… who are you people?" Akauliza kwa kingereza chake kilichojaa lafudhi ya bara la Africa huku uso wake ukionyesha mashaka aliyonayo juu yetu.



    "My name is Ray and that is my friend Jimmy… if you could give us just a few minutes of your time we will really appreciate it… please!"



    Nilijitahidi kuongea kistaarabu na unyenyekevu wote uliomo ndani yangu. Nilitaka ajue ni kiasi gani ilikuwa muhimu sisi kuongea naye.



    Alinikazia macho kwa muda mrefu kana kwamba alikuwa ananisoma dhamira yangu. Kwa muda wa karibia dakika nzima hakuingea chochote, alikuwa ananitazama tu usoni.



    "Ok.!" Hatimaye akakubalikubali.



    "Thank you mam! Let's go over there.!" Nilimuonyesha mgahawa mmoja ambao ulikuwa karibu na barabara.http://pseudepigraphas.blogspot.com/



    Jimmy hakutoka ndani ya gari na sikutaka kumlazimisha afuatane nasi. Nilihisi kama vile alikuwa hapendi kuonekana hadharani.

    Mimi na yule binti tuliingia kwenye mgahawa ulio karibu yetu na kuagiza kahawa.



    "Make it quick, am running late!" Yule binti aliongea huku akipiga funda la kwanza la kahawa baada ya kuletwa.



    Nilijiandaa kuanza kuongea huku nikipiga hesabu haraka haraka vitu gani vya kumuambia na kumuuliza huyu binti.



    Yule binti kwa kiasi fulani alikuwa 'amerelax' tofauti na zile hasira zake za mwanzo alivyoshuka kwenye gari na kuja kutugongea kwenye kioo.

    Alikuwa amenitambulisha jina lake kwamba anaitwa Winnie Akoh. Alikuwa ni mwanafunzi kutoka nchini Senegal na yuko hapa Zurich kama mwanafunzi akisomea "Banking and Finance" katika chuo kikuu cha Zurich.



    "What are doing in that house?" Nakumbuka nilimuuliza.



    Winnie alinieleza kwamba miaka miwili iliyopita alipowasili hapa Zurich kwa ajili ya masomo kama ilivyo kawaida ya wanafunzi wengi ughaibuni ilimlazimu kutafuta kibarua ambacho atakuwa akifanya katika muda wake wa ziada ili aweze kuingiza kipato cha kumuwezesha kujikimu.



    Winnie alinieleza, kwamba aliomba kazi kadhaa mtandaoni… kuanzia uhudumu kwenye mgahawa, uhudumu kwenye kituo cha kutunza wazee, kuwa mtu wa mauzo wa kampuzi za vipodozi na kadhalika na kadhalika. Alinieleza kwamba aliomba kazi nyingi sana na kusubiri aone ipi ambayo atapata majibu. Katika mlolongo wa huo wa kuomba kazi mtandaoni aliona tangazo lenye maelezo mafupi tu likisema "Earn $ 3000/month cleaning a house".



    Winnie alinieleza kwamba mwanzoni alihisi labda ni utani au tangazo la uongo kama ambavyo yamejaa huko mitandaoni. Lakini akaamua kutuma tu maombi aone kama ni kweli au la.

    Anasema kwamba siku tatu baadae alipigiwa simu na mtu aliyejitambulisha kuwa ni muwakilishi wa kampuni walioweka tangazo lile ambalo yeye aliomba kazi.



    "Did he tell you the company's name?" Nilimuuliza.



    "Yes! REMODO HOLDINGS." Winnie alinijibu.



    "Can I have their adress?" Nilimuuliza.



    "I might still have their business card in my car…!" Winnie alinijibu.



    Kisha akaendelea kunieleza kwamba mtu huyo alimuhoji maswali kadhaa kuhusu taarifa zake na kisha akamtaka waonane baada ya siku moja.



    "Did you meet him?" Nakumbuka nilimuuliza.



    "Yes! We did meet two days after the phone call."



    "Where did you guys meet?"



    "Freacht West Street… there is a fancy chinese restaurant there."



    "Chinese restaurant??"



    Nilishtuka sana aliponitajia kwanza Freacht West Street. Huu ndio mtaa ambao kuna Radison Blu Hotel ambayo nilifikia nilipoingia hapa Zurich na ndio mahala ambako siku mbili zilizopita yamefanyika mauaji ya Luke na Ivanka. Lakini nilishtuka zaidi aliponitajia mgahawa wa kichina… kwa sababu niliamini kabisa alikuwa anaongelea mgahawa ule ambao niliwahi kufika siku ya kwanza na kuchomwa sindano ya kemikali na kupoteza fahamu na baadae kujikuta nimeamka kwenye lile jengo mtaa wa Hardstrasse.



    "Is everything ok?" Winnie aliniuliza baada kuona mshtuko wangu.



    "Everything is ok! I was just thinking about that meeting place… it seems like an odd choice." Nilijitahidi kumzuga. Sikutaka ajue chochote kile ambacho nakifahamu kuhusu sehemu hizo.



    "Why is that?" Aliniuliza



    "No! Nothing… what happened next?"



    Akaendelea kunieleza kwamba, mtu huyo alichukua nakala zake za hati ya kusafiria, kitambulisho cha uanafunzi chuoni pamoja na namba yake ya akaunti ya benki. Kisha akamlipa dola elfu moja tasilimu papo hapo na kumwambia kuwa anatakiwa kuanza kazi kesho yake.



    "What was the job about… what where you suppose to do?" Nilimuuliza.



    Alinijibu kwamba, alikuwa anatakiwa kufika kwenye ile nyumba ya mtaa wa Affolterntrassemara mbili kila wiki kwa ajili ya kufanya usafi na kupokea barua zozote ambazo zitatumwa kwenye anuani ya nyumba hiyo. Hiyo ndio ilikuwa kazi yake.



    "Thats it?" Nilimuuliza.



    "Yap! Thats it.." alinijibu huku anatabasamu.



    #324

    "Did you ever got his name?"



    "I dont really remember… Eddie or Edgar something like that." Winnie alinijibu.



    "Don't you find it odd and curious to be paid all that money just to clean a house twice a week?" Nilimuuliza tena.



    "At first I was curious… but after doing it for two years, now I am comfortable with it... I just assume may be the house belongs to some rich folks and the house hold some wonderful memories and they dont want it to get dusty… I dont I am just comfortable with it now… but that was until theree weeks ago!"



    "When someone started following you!" Nikamsadia kumaliza sentensi.



    "Yap! Then I started to be curious again… why am I being followed? Do you know who they are?"



    "Not really! That's what we are trying to figure out.!" Nikamjibu. "So how do you get paid?"



    Winnie alinijibu kwamba kila mwisho wa mwezi anaingiziwa fedha kwenye akaunti yake kiasi cha dola elfu tatu. Nikamuomba anipe namba ya akaunti ambayo inatumika kumtumia hizo fedha.

    Winnie akachukua simu yake nakuanza kubofya bofya akitafuta mahala ambako alihifadhi namba hiyo ya akaunti ya benki. Baada ya kama dakika moja hivi aliipata na kunisomea huku na mimi nikiandika kwenye simu yangu.





    "AECD0210000000693123456"





    "Winne I can not thank you enough! Thank you very much!"



    "Its ok! I hope this is information I have given you is not going to get me into any trouble."



    "Not at all!" Nilimfariji lakini moyoni nikiwa na mashaka hasa nikikumbula vifo vya Luke na Ivanka siku mbili tu zilizopita.

    "Jus one last question…"



    Kabla hajaondoka nikamuuliza swali la mwisho. Kwamba alinieleza kuwa mtu ambaye alionana naye alimuelezakuwa jukumu lake ni kufanya usafi kwenye ile nyumba pamoja kupokea barua. Nikamuuliza hizo barua anazifanyia nini?



    "I forward them… he gave me a forwarding address." Alinijibu.



    "Can I have that address?"



    "Its actually their company's address… as I said, I think I still have thier business card in my car."



    Nikamshukuru Winnie tena na tena kwa taarifa hizi zote ambazo alikuwa amenipatia. Sasa nilikuwa najihisi kabisa kwamba nimeanza kupiga hatua kutegua fumbo hili ambalo lilikuwa limenileta hapa Zurich.



    Tukatoka pale mgahawani na kutembea kuelekea pale ambako tulikuwa tumeyaacha magari. Winnie walau sasa alikuwa anatabasamu tofauti na hasira ambazo nilimuona nazo awali alipokuja kutugongea kioo cha gari. Ni muda huu ndipo ambapo nilipata kutambua uzuri aliokuwa nao. Alikuwa ni binti mrembo haswa. Mrefu kiasi, mwenye umbo zuri haswa la kuvutia, uso mwembamba kiasi na macho mazuri ya kutamanisha mwanaume yeyote. Tukiwa tunatembea nilijaribu kufanya utani wa hapa na pale ili 'arelax' zaidi. Kila mara ambapo alitabasamu au kucheka kutoka na utani niliokuwa naufanya nilijikuta nafurahi moyoni kuona tabasamu lake la bakshasha na namna ambavyo meno yake meupe peee yalivyo pangika kwa uzuri kinywani mwake.



    Gari lake alikuwa amelisimamisha mbele ya gari yetu kama, kama umbali wa mita mia moja hivi. Kwa hiyo tulilipita gari letu tukiongozana nikimsindikiza kuelekea kwenye gari lake. Jimmy bado alikuwa ndani ya gari. Alituangalia tu tulivyopita bila kusema chochote.



    Tulitembea mpaka tukalifikia gari lake. Tukiaganana kutakina heri na kuahidiana kwamba tutaonana tena siku za karibuni. Kwa kiasi fulani nilihisi pia Winnie alikuwa amefurahia 'kampani' yangu kwa dakika chache zile. Sikujua kama ni kwa sababu mimi ni Mwafrika mwenzake au vipi. Maana Waafrika ikitokea mkikutana ughaibuni mnajikuta mnafurahi kama vile ndugu mliopotezana siku nyingi.

    Sikujua ni kwa nini lakini ilikuwa dhahiri kabisa kwamba Winnie alifurahia muda ule tuliokuwa wote.





    #325

    "Let me get that card!"



    Alifungua mlango wa gari na kuingia ndani akianza kupekua pekua kutafuta ile business card ambayo alihisi kuwa bado anayo.



    "Here you go!" Aliibuka kutoka kwenye gari akiwa ameshikilia business card na kunikabidhi.



    Alipobikabidhi tu macho yangu moja kwa moja yalianza kudadisi ile kadi hasa anuani yake.





    REMODO HOLDINGS

    HARDSTRASSE 201

    1985

    ZURICH

    SWITZERLAND



    Nilisikia moyo unalipuka kama vile unataka kutoka kifuani. Nilijitahidi kweli kweli Winnie asigundue mshituko wangu.

    Hii ilikuwa ni anuani ya lile jengo ambalo kwa sasa naishi ndani yake. Jengo lile la mtaa wa Hardstrasse.



    "Are you ok?" Winnie aliniuliza kwa udadisi.



    "I'm ok! So when can I see you again.." nilijaribu kuhamisha mjadala huku nikilazimisha tabasamu usoni.



    "I don't know… we will see about that!" Winnie alinijibu huku anatabasamu.



    Tulibadilishana namba za simu kisha akakwea kwenye gari lake na kuondoka.



    Nilibakia pale nikilitazama gari likiondoka. Nililitazama mpaka ambapo lilipotea kwenye upeo wa macho yangu. Kichwani nilikuwa nawaza vitu vingi sana lakini kikubwa kikiwa ni usalama wa Winnie. Taarifa kwamba kuna watu walikuwa wanamfuatilia kabla yetu iliniumiza moyo sana na kunipa wasiwasi. Nilikuwa na mashaka juu usalama wake. Nilitamani ningekuwa na uwezo nimchukue na kurudi naye Hardstrasse.

    Kwa muda mchache tu baada ya kuonana na Winnie nilikuwa nimejikuta najihisi nina jukumu la kuhakikisha yuko salama. Sikujua ni nini hasa kilikuwa kinatokea moyoni mwangu. Nimempenda?? Nikatingisha kichwa kuondoa hilo wazo kichwani mwangu.



    Nikatupa macho tena mkononi kwenye ile business card ambayo ina anuani ya jengo la Hardstrasse. Moyo ukaanza tena kwenda mbio.

    Nikatembea haraka kurejea kwenye gari yetu.



    Jimmy alikuwa ananitazama huku anatabasamu nilipoingia ndani ya gari.



    "I think you said you were married mate!"



    "Yes, I am!"



    "I saw the way you look at that girl… not cool mate… not cool..!" Jimmy aliongea akitingisha kichwa huku anatabasamu kwa utani.



    "Shut up you idiot!" Nikajikuta nashindwa kuficha tabasamu fulani la aibu. Alichokuwa anakisema Jimmy kilikuwa na kiasi fulani cha ukweli.



    "So what did your girlfriend say?" Jimmy aliniuliza huku bado akiwa na tabasamu la utani.



    Nilimsimulia kila kitu kuhusu maongezi yangu na Winnie. Namna alivyopata kazi. Maagizo aliyopewa. Namna anavyolipwa. Mpaka ile anuani ya kampuni.



    "What does all this mean?" Jimmy aliniuliza taharuki.



    Hata yeye alishitushwa kuona anauani ya kampuni iliyomuajiri Winnie kufanya usafi kwenye ile nyumba ya mtaa wa Affolterntrasse ni anuani ile ile ya jengo ambalo kwa sasa tunakaa mtaa wa Hardstrasse.



    Lakini binafsi taa ilikuwa inawaka kwa nguvu kichwani. Nilihisi nukta zinaungana. Hatua kwa hatua nang'amua hili fumbo.



    "Have you ever heard of the word 'shell company'?" Nilimuuliza Jimmy.



    "I might have.. I dont really know though what it means.!"



    Nikaanza kumueleza Jimmy kile ambacho nilikuwa nakihisi na kwa sababu gani nilipewa lundo la zile nyaraka. Na kwa nini anuani ya hii kampuni inaonyesha ipo jengo la Hardstrasse.



    Nilimueleza kuhusu shell companies. Kwamba kampuni hewa zinazoanzishwa kwa lengo la kuficha umiliki wa kampuni nyingine au kupitisha rasilimali tu kwa lengo la kuficha umiliki wa hizo rasilimali na zilikotoka. Kwamba unaweza kuanzisha msururu wa 'shell companies' ambazo kampuni moja inamiliki nyingine na nyingine na nyingine inamiliki nyingine. Vivyo hivyo kwa lengo la kuficha wamiliki halisi.



    Hiki ndicho ambacho nilihisi kilikuwa kimefanyika. Na ndio sababu ya lundo la nyaraka nilizopewa kule mtaa wa Wipkeng na watu wa Hudini kuwa zimesheheni ananuani na namba za akaunti.



    "So what we do now?" Jimmy aliniuliza.



    "We find a loophole.!" Nilimjibu huku nimeanza kung'oa gari.



    "What is that?" Jimmy aliniuliza tena.



    "This bank account, this adress amd this woman, Winnie... that's our loophole!" Nikamjibu huku nikitabasamu na kuingiza gari barabarani tayari kurejea Hardstrasse.



    Nilikuwa na hakika kabisa bila shaka anuani hii, yaani jengo lile ambalo tunaishi pamoja na namba ya benki account ambayo Winnie alinipatia zilikuwa zinatosha kabisa kujua ni nani ambaye yuko nyuma ya hili suala. Na nikimfahamu mtu huyo, ndio wasaa ambao nitafahamu hasa kwa nini mzee alinitaka kuja hapa Zurich. Nini ambacho alitaka nikione.





    Majengo ya chuo kikuu cha Zurich yalikuwa yanapendeza haswa. Yalikuwa yanaakisi kwa uzuri kabisa umahiri wa stadi za uhandisi wa majengo wa karne ya kumi na tisa. Muda mchache uliopita nilikuwa nimemtumia Winnie ujumbe mfupi wa maandishi kumfahamisha kwamba nimeshafika hapo chuoni na alinijibu kwamba nimsubiri kwenye eneo la kuingilia kwenye Campus ya chuo ambayo lina sanamu maarufu sana la kutambulisha chuo hiki. Ilikuwa ni sanamu ya mwanamke aliyekaa juu ya jiwe huku akiwa amejitanda kwa shuka upande mmoja huku upande mwingine wa kifua ukiwa wazi titi moja likionekana. Mkono wa kulia kulikuwa na sanamu nyingine ya mwanaume ambaye naye pia alikuwa amekaa juu ya jiwe akiwa kifua wazi na huku amejifunika na shuka kuanzia kiunoni. Sanamu hizi zilikuwa zina umaridadi wa kuvutia mno kwa macho kutokana na kudhihirisha ustadi wa sanaa ya ufinyanzi ambayo ilitamalaki mno kwenye nchi za ulaya kwenye karne ya kumi na saba, kumi na nane na karne ya kumi na tisa.



    Chini ya viambaza vyenye kushikilia sanamu hizi kulikuwa na maneno yaliyoandikwa kwa herufi kubwa katika lugha ya kijerumni, “UNIVERSITAT ZURICH ZENTRIUM” yakimaanisha “Zurich University Center” kwa umombo.



    Nilisogea mpaka kwenye benchi dogo la kumpumzika ambalo lilikuwa karibu na sanamu hizi. Nilikuwa nimeomba kuonana na Winnie ili nimuhoji maswali kadhaa ambayo nilihisi kuwa yanaweza kunisaidia. Kwa siku mbili zilizopita nilikuwa nimekesha kuchambua nyaraka nilizonazo nikijaribu kutafuta uhusiano kati ya zile nyaraka nilizonazo na namba ya akaunti ya benki ambayo Winnie alikuwa amenipa. Mwanzoni nilihisi ingekuwa kazi rahisi tu lakini kwamuda wa siku mbili nilikuwa kama nazunguka mbuyu tu hivi. Waliondaa nyaraka zile walikuwa wamefanya kazi ya umaridadi sana kuficha uhalisia wa wahusika wake. Ni kama ambavyo nilikuwa nimemueleza Jimmy kuhusu ‘shell companies’. Kampuni moja ilifichwa ndani ya kampuni nyingine kivuli na nyingine ndani ya nyingine vivyo hivyo tena na tena.



    “where is your bodyguard?”



    Nilisikia mtu akinisemesha, nikainua shingo kutazama.Nilitabasamu, alikuwa ni Winnie akinitazama kwa kutabasamu na kisha kukaa pembeni yangu pale kwenye benchi.



    “bodyguard?” nilimuuliza huku nikijifanya kana kwamba sikuelewa anaumuongelea nani.



    “yes, your bodyguard... that serious guy!”



    Nilimuelewa kabisa kwamba alikuwa anamuongelea Jiimy na alikuwa anaongea kwa utani tu.



    “he is not my bodyguard… he is a friend!” nilimjibu huku natabasamu.



    #366

    Winnie alionekana kuwa nilivyomuomba tukutane alitegemea kwamba ningekuja na Jimmy kama siku ile ya kwanza. Hata mimi nilitamani kuja na Jimmy. Nilikuwa nafurahia kuongozana nae huku mtaani kwasababu ni kawaida kuwa unapata ujasiri fulani hivi ukizurura mitaani sehemu ya ugenini ukiwa na mwenyeji wa eneo hilo. Lakini Jimmy siku moja iliyopita alinieleza kwamba hawezi kuendelea kuishi na mimi kwenye lile jingo la Hardstrasse. Ati kwamba hajazoea maisha hayo… kwamba anarudi mtaani. Nilielewa wazi kabisa kwamba kuna kitu Jimmy anakificha, kuna sababu ya huu uchokoraa wake, au labda kuna kitu kilimtokea huko nyuma kwenye historia yake… kuna sababu fulani hivi ambayo inamfanya aishi mitaani. Sikutaka kumbana kwa maswali na kumuhoji ni nini hasa kinamsibu, huu haukuwa muda sahihi. Nilihitaji akili yangu kwa sasa kujisumbua kung’amua hiki kilichonileta hapa Zurich.

    Tulikubaliana na Jimmy kwamba kila siku jioni nitaweza pizza kwenye boksi na kuiacha nje ya mlango wa nyuma wa jengo lile la hardstrasse. Kama nitakuwa namuhitaji anisaidie chochote kile basi nitaweka karatasi wenye ujumbe ndani ya boksi hilo la pizza.



    “what’s up?” Winnie alinisalimia baada ya kukaa kwenye benchi.



    Sikumuuliza kama alikuwa ametokea mazoezini ama vipi lakini kwa muonekano wa namna ambavyo alikuwa amevaa alionekana kama vile ametoka ‘gym’. Alikuwa amevalia ‘leggings’ ya rangu ya kijivu ndefu… suruali fulani nyepesi ya mazoezi yenye kushika maungo ya mwili. Juu alikuwa amevaa fulana fupi nyeusi ambayo nayo ilikuwa inabana mwili kiasi.

    Macho yangu yalikosa pazia na kushindwa kujizuia kukodolea mwili wake na namna ambavyo ulikuwa umepangika vyema na kuvutia. Hakika alikuwa ni mrembo haswa.



    “how have you been?” hatimaye nilimsalimia.



    “Great.. how are you?”



    Tulisalimiana na kuongea maongezi madogo ya hapa na pale huku nikijibaraguza kujaribu kumuonyesha ni kiasi gani nilikuwa nimekipenda chuo chao na kadhalika. Hatimaye nilianza kumueleza namna ambavyo kwa siku mbili zilizopita nimekuwa nikihangaika kujaribu kutafuta undani wa namba ya akaunti ambayo alikuwa amenipa bila mafanikio yoyote yale.



    “how can I help?” aliniuliza.



    “I want to know anything that you know about this account number… holders name, the bank and anything else that could be helpful.!” Nikamjibu.



    “you couldn’t figure it out yourself? Its very easy.. come here!” Winnie aliongea na kuchukua simu yake na kuanza kubofya.



    Nikajivuta na kusogea karibu yake. Akafungua kwenye uwanja wa kuandika ujumbe mfupi na kisha kuiandika ile namba ya akaunti ambayo alinipa juzi.





    AECD0210000000693123456



    Winnie akaanza kunionyesha umahairi wake wa masula ya benki ambayo alikuwa anasomea hapo chuoni.

    “You see… this is IBAN.!” Alianza kuongea



    “what is that.!” Nikamuuliza



    “International Bank Account Number,!” alinijibu huku anatabasamu kwa mimi kushindwa kutambua kitu rahisi hivyo.



    “ok ok… continue!”



    Akaendelea kunieleza kwamba namba zote za akaunti za benki za kimataifa zinakuwa na ‘digits’ ishirini na tatu ambazo zimegawanywa katika makundi mawili. Namba nne za kwanza zinajulikana kama “Header” na namba kumi na tisa zinazofuata zinajulikana kama “BBAN”.



    “what is BBAN” nilimuuliza tena huku nikijihisi mbumbumbu hasa kwa haya maswali yangu.



    “that’s a Basic Bank Account Number.” Winnie alinijibu tena huku anatabasamu.



    “Ok ok..!”



    Winnie akaendelea kunieleza kwamba katika akaunti hizi za kimataifa, tarakimu zile nne za mwanzo kwenye akaunti hizi za kimataifa ambazo ndio zinaitwa ‘Header’, tarakimu mbili za mwanzo zinatumika kutambullisha nchi ambayo akaunti hiyo ipo. Kwa hii namba ya akaunti ambayo alinipa ni herufi ‘AE’ ambayo Winnie alinieleza kwamba ni ‘ISO country code’ ya nchi za United Arabs Emirates (UAE). Kisha akanieleza kwamba herufi nyingine mbili ambazo zinafuata, yaani ‘CD’ zilikuwa ni ‘check digits’.

    Winnie akaendelea kunieleza kwamba zile tarakimu kumi na tisa ambazo zinafuata ambazo zinajulikana kama BBAN nazo zinagawanyika kwenye sehemu mbili. Sehemu ya kwanza ina tarakimu tatu baada ya ‘Header’ ambapo kwa hii namba yetu ya akaunti ni 021. Alinieleza kwamba hii inaitwa ‘Identifier’ na inatumika kutambulisha benki ambayo akaunti hiyo ipo.



    “so which bank is it in this case?” nilimuuliza Winnie.



    Winnie alianza kubofya bofya simu yake akitafuta kitu Fulani, nikamuona akifungua file ambalo linamfululizo wa namba na kisha akanijibu.



    “It’s Citi Bank.”



    Baada ya hapo akaendelea kunieleza kuwa zile ‘digits’ kumi na sita ambazo zinafuata ni namba ya akaunti ya mteja kwenye hiyo benki husika. Winnie akamaliza kueleza.



    “are we together?” akaniuliuza huku anatabasamu tena akijua kabisa kwamba siwezi kuwa nimeelewa kwa asilimia mia.



    “only half of it!” nikamjibu huku nikitabasamu pia na kukuna kichwa.



    #368

    Japo maelezo ya kina na ya kiufundi ambayo alikuwa amenipa nlikuwa sijayaelewa sawa sawa lakini nilikuwa nimepata mwanga juu ya hii akaunti. Kwamba akaunti hii inamilikiwa na mtu ambaye yuko UAE katika tawi la Citi Bank.



    “Is there a way we can know the account holder’s name?” nilimuuliza



    “yes ofcourse.!” Winnie akaitikia na kasha kuanza tena kubofya simu yake.



    Sikujua alikuwa anaangalia nini lakini baada ya kama dakika mbili hivi akanionyesha jina la mwenye hiyo akaunti.



    “Here!” akasogea karibu yangu kunionyesha.



    “Dr. Athumani R. Chande.”



    Moyo ulinilipuka ghafla. Nilijiuliza kama ni majina tu yalikuwa yamefanana au huyu ambaye nilikuwa namfikiria ndiye?



    Nilikuwa nafahamu kwamba Waziri Mkuu wa Kwanza wa Tanzania, ndugu Chande Ramadhan Chande ambaye pia ndiye alikuwa Mwenyekiti wa Kwanza wa Jumuiya ya The Board alikuwa na watoto watatu. Mtoto wake wa kwanza wa kiume, Jamal Chande alikuwa ni mfanyabiashara maarufu jijini Dar es Salaam. Mtoto wake wa pili wa kike, Khadija Chande alikuwa ni mbunge wa jimbo la Dodoma mjini. Na mtoto wake wa mwisho wa kiume, Athuman Chande alikuwa anaishi uarabuni na sikuwahi kufuatilia hasa alikuwa anaishi nchi gani.

    Nilijiuliza kama ulikuwa ni mfanano tu wa majina au alikuwa ni yeye haswa.



    “are you ok?” Winnie aliniuliza.



    “I think I know who this is!” niliongea bila kumuangalia Winnie. Macho yangu bado nilikuwa nimeyakaza juu ya kioo cha simu ambako alikuwa ananionyesha jina la mwenye ile akaunti.



    “Who is he.?” Winnie aliniuliza huku nikianza kuhisi taharuki kwenye sauti yake.



    “He is the son of our first Prime Minister!” nikamjibu kwa kifupi tu nikimtazama safari hii.



    Winnie alitoa macho kweli kweli kwa taharuki. Aliachama mdomo kama vile alitaka kuoongea kitu lakini alishindwa. Alibaki amenikodolea macho kwa mshangao.



    “What’s going on Ray?” kwa mara ya kwanza nilihisi mtetemo wa woga kwenye sauti yake.



    Nahisi alianza kuelewa ni kwa namna gani labda amejikuta amejitumbukiza kwenye suala zito pasipo yeye mwenyewe kujua. Sikujua nimjibu nini. Kama nimwambie ukweli au ni maelezo gani ya maana nimpe.

    Nikiwa nimekodoa macho bado nikitafari nini cha kuongea, mbele yetu pale tulipokaa ng’ambo ya barabara kulikuwa na taxi imesimama. Japo nilikuwa sijatilia maanani sana lakini nilihisi kama ile taxi imesimama pale kwa muda mrefu kuzidi kawaida.



    “For how long has this car been here?” nilimuuliza Winnie huku nikumuonyesha ile gari.



    #369

    “a long time… why?” Winnie aliniji bu huku ananitazama kwa udadisi.



    Nilianza kupata hisia mbaya juu ya hii taxi. Nikakaza macho kuitazama. Nikatazama dirisha la siti za nyuma ya abiria. Nilihisi kama kuna sura ya mtu ambaye namfahamu. Nikaanza kuinuka taratibu. Nikaanza kupiga hatua taratibu kwenda pale barabarani ambako taxi ilisimama kando.



    “Ray! Are you ok?” Winnie aliuliza



    Sikujibu kitu, niliendelea kupiga hatua taratibu kuifuata ile taxi huku macho nimeyakaza dirisha la siti ya nyuma ya abiria. Kadiri nilivyokaribia ndivyo ambavyo ilizidi kuwa dhahiri kwamba kwenye ile siti ya nyuma kulikuwa na mtu ambaye namfahamu japo hata kwa sura.

    Niliendelea kupiga hatua za taratibu mpaka kufika kama umbali wa mita tano tu kutoka mahala ambako taxi ilikuwa imepaki. Ndipo hapa ambapo niling’amua mtu Yule kwenye siti ya nyuma alikuwa ni nani.



    Ni jamaa yule yule ambaye nimemuona mfululizo kwa siku kadhaa zilizopita, mapokezi ya Radison Blu Hotel, kwenye eneo la tukio la Luke alipopigwa risasi, na eneo la tukio ambalo pia Ivanka alipigwa risasi. Jamaa Yule Yule, mwenye kovu upande mmoja wa sura, kofia ya pama rangi ya kijivu kichwani na koti refu jeusi.

    Tuliangaliana kwa kukaziana macho kwa karibia nusu dakika. Nilikuwa Napata hisia kwamba nimewahi kumuona huyu mtu… lakini sikuweza kukumbuka ni wapi. Nikapiga hatua nyingine tena mbele kuifuata gari lakini mara moja taxi iliondokakwa mwedo wa kasi. Kichwani nilikkuwa najiuliza ni nani huyu mtu? Anahusika vipi na mfululizo wa haya matukio? Yuko hapa kumfuatilia Winnie au mimi?

    Nillibaki pale nikiitazama mpaka ilipopotea kwenye upeo wa macho yangu… niliweza kuishika kichwani namba ya ile taxi, ZH 45789.



    “Ray! Are you ok?” Winnie alikuwa amesimama na kuja mpaka hapa nilipo.



    “Come with me!” Nilimshika mkono Winnie na kuanza kuondoka pale kwa haraka.





    “where are you taking me?” Winnie alilalamika huku anajaribu kujitoa mkono wake kutoka katika mkono wangu.



    “I think you are in great danger!” nilimwambia tena kwa mara nyingine.



    “Danger from what? You keep saying that..!”



    Nilikuwa nashindwa kupata maneno sahihi ya kumueleza Winnie ili anielewe. Yule jamaa mwenye kofia ya pama ambaye alikuwa kwenye taxi dakika chache zzilizopita alikuwa amenifanya niwe na wasiwasi sana juu ya usalama wa Winnie. Kwa kiasi kikubwa rohoni mwangu nilikuwa naamini kwamba anahusika kwa kiwango fulani na vifo vya Lukena Ivanka. Watu ambao siku chache tu baada ya kuonana na mimi walipoteza maisha. Sikutaka Winnie naye aende na maji.



    “I have strong reasons to believe that the man who was in that car is the one who has been following you..!”



    “How do you know that?”



    Nikajikuta Napata tena kigugumizi cha nini hasa nimwambie. Tulikuwa tumetembea mpaka eneo la ndani ya chuo baada ya kumvuta kutoka pale nje kwenye benchi ambalo tulikuwa tumekaa awali. Sikuwa nataka kumwambia Winnie masuala yote kuhusu mimi au ni nini hasa kilikuwa kinaendelea. Kwanza kwa sababu sikutaka aniogope na pili sikuona busara ya kumueleza siri hizo mtu ambaye bado sijamjua kwa undani. Lakini nilikuwa naona kabisa kuna hatari mbele yake.



    “I belive that man was involved it two deaths that happened this week.!”



    Winnie alitoa macho na kuachama mdomo huku akijiziba kwa kiganja cha mkono.



    “Whaaat??” Winnie alitaharuki huku amenitolea macho.



    “Two shootings happened this week and two people were killed and I have strong reasons to believe that guy was involved.!”



    “Do the poliece know about this?”



    “No! probably not..!”



    “Then we should inform the police!”



    “No no no! we can’t do that..”



    #372

    “Why not?”



    Nilijikuta Napata tena kigugumizi nini hasa nimwambie. Nilijua jibu ambalo nitampa lazima litaleta madhara kwenye huu ukaribu tulio nao.



    “aah… you see, aah!” kigugumizi kilikuwa kimenishika roho ikisita kutamka nilichokuwa nataka kumwambia Winnie. Nahisi Winnie alikuwa ameona kusitasita kwangu na alianza kupata wasiwasi.



    “what is it Ray? Why you don’t want us to inform the police?” aliniuliza huku ananiangalia kwa macho ya mashaka.



    “Winnie… I think the police believe that I did it.!” Nilimjibu kwa uso mkavu huku nikimtazama usoni nione namna ambavyo atakuwa amepokea taarifa hii.



    Winnie alitoa macho kama vile mjusi aliyebanwa na mlango. Alinitazama kwa mshituko kama vile ilikuwa ni mara yake ya kwanza kuniona. Nilimuona akianza kusogea nyuma taratibu kama vile ananiogopa.



    ”Winnie look… I have nothing to do with it, I swear to God… it’s a long story, I will explain!” niliongea hukunikijaribu kumsogelea ili niweze kumtuliza wasiwasi ambao ulimpata ghafla juu yangu/ ubaya wa kujitetea ni kwamba kadiri unavyojitetea ndivyo ambavyo unaonekana una hatia. Kila hatua ambayo nilikuwa napiga kumsogelea naye alikuwa napiga hatua moja nyuma.



    “I am sorry Ray but I think I have to inform the police about this… someone is following me for the past three weeks and now you are telling me that two people died… I am sorry but I have to talk to the police about this!”



    “Please Winnie don’t do that!”



    “I am sorry Ray!”



    Winnie aliongea kwa sauti ya unyonge huku akiniangalia kwa huruma na kisha akugeuka na kuondoka kwa hatua za haraka. Nilimtazama anaondoka mpaka nikijilaumu moyoni. Kwa nini nimemueleza suala hili? Lakini sikuwa na chaguo lingine… nia yangu ilikuwa ni kuokoa maisha yake. Japo ulikuwa ni wendawazimu kumuomba tuondoke wote na mimi lakini sikuwa na njia nyingine ya kumsaidia zaidi ya hiyo. Nilijihisi kuwa atakuwa salama zaidi akiwa pamoja na mimi kule hardstrasse kuliko kuwa peke yake hapa chuoi. Hivyo nilipaswa kumuambia kuhusu vifo vya Luke na Ivanka ili aelewe juu ya ukubwa wa hatari ambayo ilikuwa juu ya maisha yake.

    Nilijua fika kabisa nilikuwa nimebakiwa na muda mchache sana, kama kweli Winnie atakwenda kuongea na polisi kuhusu kufuatiliwa na watu wasiojulikana pamoja na taarifa yoyote kunihusu mimi basi muda wowote na sekunde yeyote nitatiwa korokoroni.



    Nilitembea mpaka barabarani na kupanda taxi kurejea hardstrasse. Kichwani nilikuwa na mambo mawili ambayo nilikuwa nimeyapa kipaumbele kwa sasa. Kwanza ni taarifa hii ambayo nimetoka kuifahamu kwamba akaunti inayotumika kumlipa Winnie inamilikiwa na mtoto wa Marehemu Waziri Mkuu Chande ambaye anaishi uarabuni, lakini suala la pili nilikuwa nimedhamiria kufahamu japo lolote kuhusu Yule jamaa mwenye kofia ya kijivu ya pama ambaye nahisi amekuwa akifuatilia nyendo zangu.



    #373

    Nilipofika tu kwenye jengo la hardstrasse na kuingia ndani moja kwa moja nikachukua simu yangu na kuanza kuperuzi mtandaoni. Nilikuwa nahitaji kujua taarifa za kutosha kuhusu Dr. Athumani R. Chande mtoto wa marehemu waziri mkuu Chande ambaye pia aliwahi kuwa mwenyekiti wa jumuiya ya The Board. Kitu pekee ambacho nilikuwa nakijua haraka haraka kumuhusu ni kwamba anaishi uarabuni kwa miaka mingi sasa.



    Nilifungua simu na kuanza kuperuzi kwa kuandika jina lake kwenye mtandao wa google na kisha kuanza kupitia matokeo ambayo yaliletwa. Habari nyingi ambazo zilikuwa zimeletwa baada ya kubofya kitufe cha kutafuta zilikuwa zinakuhusu marehemu baba yake, nyingine zilimuhusu dada yake Khadija Chande mbunge wa jimbo la Dodoma mjini, habari nyingine zilimuhusu kaka yake Jamal Chande. Niliperuzi karibia nusu saa nzima pasipo kukutana na habari yoyote ile ambayo ilikuwa inamuhusu yeye moja kwa moja.



    Nikiwa nakaribia kabisa kukata tamaa ya kuendelea kuperuzi, hatimaye jicho langu lilitua kwenye habari ambayo ilionekana imeandikwa kama siku tatu zilizopita kwenye moja ya blogu maarufu nyumbani Tanzania. Habari hii ilinionyesha pale juu kwamba ndani yake kulikuwa na jina hili ambalo niliandika pale juu kwenye sehemu ya kufatuta, yaani jina “Athumani R. Chande”.

    Haraka nikafungua habari hiyo.



    Habari ilikuwa inahusu uwekaji wa jiwe la msingi katika ujenzi wa kiwanda cha kuchakata na kusindika gesi (LNG – Liquefied Natural Gas) ujenzi ambao ulikuwa unafanyika huko mkoani Lindi katika kijiji cha Likong’o. habari hiyo ilieleza kwamba uzinduzi huo umefanywa na Mheshimiwa Rais Albert Kafumu kuashiria kuanza kwa ujenzi huo ambao ulikuwa unasuasua kwa miaka kadhaa sasa. Habari iliendelea kueleza kuwa ujenzi huo unafanywa chini ya shirika la mafuta la Tanzania, TPDC kwa kushirikia na kampuni zote za utafutani gesi ambazo zimepewa vitalu nchini Tanzania, yaani kampini ya Statoil, BG Group, Exxon Mobil, Royal Dutch Shell, Ophir Energy na Pavilion Energy.

    Jina la Athumani R. Chande katika habri hii liliibuka mahali ambapo habari ilizungumzia kampuni ambayo imepewa zabuni ya kufanya ujenzi huo wa kiwanda. Kampuni hiyo iliitwa PETROFAC Emirates ambayo ilikuwa inatokea huko nchi za Falme za Kiarabu. Kwa mujibu wa habari hiyo, nilisoma namna ambavyo Rais Kafumu aliimwagia sifa kedekede kampuni hiyo ya PETROFAC kwamba wana uzoefu na weledi wa kutosha kuhakikisha kwamba kiwanda hicho kinajengwa kwa umaridi, viwango vya kimataifa na ndani ya muda mfupi.

    Kwenye hotuba hiyo pia Rais Kafumu aliongea kwamba alikuwa anajivunia kuona kwamba kuna mtanzania ndani ya bodi ya wakurugenzi ya PETROFAC na hii ilikuwa inampa imani kwamba hatimaye sasa “rasilimali za nchi zinakuwa kwenye mikono sahihi”, rais alinukuliwa na habri hiyo.



    Habari hiyo pia ilimnukuu Dr. Athumani Chande mwenyewe akiongea na wanahabari na kuwaeleza kwamba alikuwa anajisikia fahari kampuni yao kumteua yeye kuja kusimamia mradi mkubwa kama huu hapa nyumbani. “Najisikia fahari na kuwa na imani kwamba sasa rasilimali za nchi zinaelekea kuwa katika mikono sahihi.” Dr. Chande alinukuliwa.

    Kwa haraka nikagundua namna ambavyo Dr. Chande alikuwa amechagua maneno. Alikuwa ametumia maneno yenye kufanana kabisa na yale ambayo Rais Kafumu alikuwa ameyatumia katika hotuba yake.



    Nikahisi labda ni bahati tu kufanana uchaguzi huo wa maneno, lakini pia upande mwingine wa akili ulihisi labda kulikuwa na maana iliyojificha. Nikahifadhi wasiwasi wangu huu akilini.



    Nikatoka kwenye blogu hiyo na moja kwa moja kwenda kufungua tovuti ya kampuni ya PETROFAC Emirates. Katika tovuti ya hiyo kampuni moja kwa moja niliingia kwenye sehemu ambayo ilikuwa



    #374

    mahususi kwa ajili ya historia fupi za viongozi wa kampuni hiyo na uzoefu wao. Kulikuwa na orodha ndefu sana lakini nilishuka chini mpaka nilipolikuta jina la Dr. Athumani Chande. Kama ilivyo kwa majina mengine yote kulikuwa na maelezo mafupi tu kwa kila jina, hasa hasa kuhusu elimu yake, uzoefu wake na mawasiliano yake ya barua pepe na simu ya ofisi.

    Maelezo yalionyesha kwamba Dr. Athumani Chande alikuwa ni msomi mkemia wa mafuta, yaani Petro-chemist ka umombo akiwa na shahada ya uzamivu ambayo aliipata katika chuo kikuu cha Aberdeen nchini Uingereza. Maelezo hayo pia yalionyesha kwamba Dr. Chande amewahi kufundisha masomo ya kemia ya mafuta katika Khalifa University kilichopo Abu Dhabi lakini pia amewahi kuwa mjumbe wa bodi ya maendeleo ya Elimu nchini Rwanda. Hapa nilishituka kidogo. Rwanda? Kwanini? Huyu si Mtanzania. Tena anaishi uarabuni kwamiaka mingi? Haya mafungamano na Rwanda yameokea wapi?

    Sikuweza kupata jawabu la haraka lakini moyoni nilikuwa nimefarijika kiasi kwamba angalau nilikuwa nimemfahamu huyu mtu… mtu ambaye akaunti yake ya benki inatumika kumlipa Winnie, binti ambaye amepewa kazi ya kufanya usafi na kuhifadh barua kwenye anuani ambayo inatumiwa na kikundi cha siri cha HUDINI.



    Kuna muda ambao ukikaribia kufanya uvumbuzi fulani unasikia kabisa damu inachemka na mwili wote unakusisimka. Ndivyo ambavyo nilikuwa najiskia muda huu.

    Kazi ambayo ilikuwa imebaki mbele yangu ilikuwa ni kuunganisha nukta ili nipate kuelewa Dr. Athumani Chande alikuwa na mfungamano gani na HUDINI mpaka kumtumia kufanya miamala hii ya benki.



    Nikiwa natafakari hatua za kuchukua kutokea hapa mara simu yangu ikaita… nikatupa jicho kwenye kioo, alikuwa ni Winnie.



    “Haloo.!!” Nilipokea simu harak haraka



    “…hallo…”



    “Hallooo.!!” Niliita tena kwa mara ya pili. Sauti ya Winnie ilikuwa chini sana na nilikuwa namsikia kwa mbali mno.



    “…ray…” aliongea tena taratibu. Safari hii niligundua kwamba alikuwa ananong’ona kwa makusudi. Alikuwa hataki kuongea kwa sauti kubwa.



    Moyo ukanilipuka.



    “Winnie are you ok?” nilimuuliza huku nahema



    “someone is following me!” Winnie alinong’ona tena



    “where are you right now?” nilimuuliza huku nasimama haraka haraka mkono mmoja nikishikilia simu na mkono mwingine nikitumia kuvaa viatu.



    “I am at Freatch West Street!” alijibu tena kwa kunong’ona.



    “What? What are doing at Freatch West? I told you to…. Damn it!” nilijikuta nashindwa hata kumalizia sentensi. Winnie anafanya nini Fretch West? Nilimuacha chuoni na nilimueleza kwamba awe makini mno kwa sababu nilihisi kabisa yuko hatarini. Sasa hivi ananiambia kuwa yuko mitaa ya Freatch West



    amefuata nini? Kwa makisio hii ilikuwa yapata kama saa moja na nusu au saa mbili usiku. Anafanya nini Freatch West?

    “where exactly are at?” nikamuuliza

    http://pseudepigraphas.blogspot.com/

    “there is a chinese restaurant that I told about so…!”



    “I know the place, stay put. I am on my way!” sikutaka hata amalize sentensi. Alivyonitajia tu mgahawa wa kichina nilielewa kwa hakika kabisa ni wapi alikuwa.



    Nilihisi ni lazima Winnie atakuwa kwenye hatari kubwa mpaka kunipigia simu mimi ukizingatia namna ambavyo tulikuwa tumeachana pale chuoni masaa machache yaliyopita. Sikutegemea kama angewasiliana nami tena au kutaka kuwa karibu nami. Kwa hiyo kama mpaka imemlazimu kunipigia simu mimi tena ni lazima atakuwa kwenye hali ya hatari haswa.

    Kitu ambacho kilikuwa kinaniumiza kichwa ni nini hasa kilimpeleka huko Freatch West? Sikutaka kupoteza muda, nikatoka nje na kutafuta taxi tya kunipeleka Freatch West.







    Nilifika mtaa wa Freatch West karibia majira ya saa mbili na nusu usiku. Mtaa ulikuwa kimya tofauti na kawaida kama ambavyo niliufahamu kipindi bado nakaa hoteli ya Radison Blu. Nilihisi labda ni kutokana na matukio ya maujai ambayo yametokea ndio yalifanya watu wawe na hofu kutembea usiku katika mtaa huu. Nilishuka kwenye taxi umbali wa kama hatua ishirini kutoka mahala ambako ule mgahawa wa kichina ulipo ambapo Winnie alinielekeza kuwa yuko ndani yake. Nilihitaji kuyasoma mazingira kabla ya kuingia ndani ya mgahawa huu.



    Nilitembea na kufika kama hatua kumi kutoaka ulipo malango wa mgahawa. Uzuri ni kwamba upande huu wa barabarani wa mgahawa kama ilivyo desturi ya migahawa mingi ya nchi za magharibi ulikuwa ni wa kioo tupu kwa hiyo niliweza kuona ndani bila wasiwasi kabisa. Japo kuwa ilikuwa ni mapema kabisa saa mbili unusu usiku, lakini ndani ya mgahawa kulikuwa na watu wachache sana. Niliweza kumuona Winnie akiwa amekaa kwenye meza ya peke yake kukiwa na kikombe cha kahawa mezani. Winnie alikuwa amevalia sweta la mikono mirefu na alikuwa amelivuta mpaka kufunika viganja vya mikono. Kwa namna ambavyo alikuwa amekaa tu mtu yeyote angeweza kuhisi woga ambao Winnie alikuwa nao.



    Meza kama ya tatu kutoka aliko Winnie alikuwa amekaa mzee wa kichina na mkewe ambao walionekana wanapata mlo wa jioni kama kawaida. Meza nyingine kulikuwa na kijana wa kizungu, mwanaume ambaye pia alikuwa anapata kahawa. Nilijaribu kuangaza macho huku na huko labda niweze kung’amua huyo mtu ambaye Winnie alidai anamfuatilia lakini sikuweza hata kuhisi… nje ya mgahawa kulikuwa hakuna mtu yeyote yule na watu wote ambao walikuwa ndani ya mgahawa hakuna ambaye alinifanya nimtilie mashaka.

    Nikaufuta mlango wa ngahawa na kuingia ndani.



    “Hey… you ok?” nilimuuliza Winnie huku nikikaa kwenye kiti baada ya kufika kwenye meza ambayo aliketi.



    “No I’m not… I’m far from ok!” Winnie aliongea kwa wasiwasi huki analivuta vuta sweta lake viganjani.



    “What are you doing here?” nilimuuliza. Ilikuwa ni jambo la ajabu sana kwangu Winnie aliponiambia kuwa yuko kwenye mgahawa huu hasa baada ya kuonana tu na mimi masaa machache yaliyopita.



    “They called me again!” alinijibu huku ananiangalia kwa uso wa wasiwasi



    “Who called you?”



    “The guy who gave me the job… the one I told you about earlier today!” Winnie alinijibu.



    Nilimuelewa kwamba alikuwa anamaanisha yule jamaa ambaye alimpigia simu miaka miwili iliyopita na wakakutana katika mgahwa huu huu na kumpa kazi ya kusafisha nyumba ile ya mtaa wa Affoltentrasse.



    Nilijiuliza kichwani kama hii ilikuwa ni bahati mbaya ama vipi? Kwa nini mtu huyo ampigie simu Winnie siku ya leo baada ya Wiinie kuonana tu na mimi?



    “What did he want?” nikamuuliza Winnie huku kichwani nikiendelea kuchekecha mfululizo huu wa utokeaji wa matukio.



    “it’s strange.. he called me and wanted to meet him up here and then he only said one sentence and then he left.!”



    “What didi he say?” nikauliza kwa shauku.



    “He just said… ‘don’t invite anyone inside the house’.!”



    “What!!”



    “That’s all that he said and then he left!”



    “He could have said that over the phone… why did he want to meet!”



    “I don’t know… am really confused!”



    Ilikuwa haiingii akilini kwamba mtu huyo alitaka kuonana na Winnie ili aongee sentesi moja tu kwamba ‘winnie asiruhusu mtu yeyote kuingia ndani ya nyumba’. Alikuwa anaweza kumwambia suala hilo kupitia simu, kwa nini alitaka waonane. Au huu ulikuwa ni mtego ? Mtego wa nini?



    “You said someone was following you?” nikamuuliza Winnie kwa kunong’ona.



    “Yes.. that guy over there!” Winnie aliongea kwa kunionyesha kwa ishara ya macho.



    Nilifuata uelekeo wa macho ya Winnie na alikuwa ananionyesha kwenye ile meza ambayo alikuwa amekaa kijana wa kizungu ambaye alikuwa anakunywa kahawa. Kwa mara hii ya pili baada ya Winnie kunionyesha na kumuangalia vizuri yule kijana ndipo ambapo sura yake ikaanza kuingia kwenye akili yangu na kuhisi kama nimewahi kumuona mtu huyu mahala fulani japokuwa alikuwa anaonekana ni wa kawaida kabisa ambaye mtu usingelimtilia mashaka. Alikuwa amevalia suruali ya jinzi na sweta lenye kofia waitazo ‘hood’ kwa umombo.



    “Are you sure?” nilimuuliza Winnie.



    “Hundred percent sure… I saw that guy’s car when I was on my way here… and then after I got here he also parked outside and has since been sitting there. I think he is waiting for me to leave so that he can do the same!”



    Nikainua tena shingo kumtazama yule kijana wa kizungu. Hakika nimewahi kumuona mahali, japo kumbukumbu ilikuwa inakuja na kuondoka.



    “What is going on Ray?” Winnie aliniuliza kwa sauti ya woga.



    “I don’t know… did you call the police like you said earlier today?” nikamuuliza

    “I wanted to but I couldn’t.”



    “Why?”



    “Well you said it might get you into trouble if the police get involved in this!” Winnie alinijibu huku ananiangalia kwa macho ya huruma.



    Moyoni niliumia kweli kweli. Binti huyu japo tumejuana kwa siku chache tu lakini alikuwa anajali usalama wangu kiasi hiki. Alikuwa anahatarisha maisha yake kwa kutotoa taarifa hii ya kufuatiliwa na watu wasiojulikana polisi na anafanya hivyo ili tu kunilinda nisiingie kwenye matatizo na polisi. Na sasa mimi ndiye mtu pekee ambaye ni tegemeo lake kumnasua kwenye kizaazaa hiki ambacho amejikuta yumo. Moyo ulikuwa unaniuma kwa kuwa nilikuwa sijui nifanye nini, nilikuwa bado sijui hata adui yetu halisi alikuwa ni nani.



    Nikiwa nawaza hivi ghafla mlango wa mgahawa ulifunguliwa na aliingia binti mrembo wa kizungu. Alikuwa amevalia kigauni kifupi sana cha rangi nyekundu. Kigauni kilikuwa kifupi kiasi kwamba sehemu kubwa ya mapaja yake yalibakia wazi. Chini alikuwa amevalia viatu virefu vya rangi nyekundu pia. Shingoni alikuwa amevalia mkufu wenye kumeremeta kwa vito vya thamani ambao ulionyesha ulikuwa wa bei ghali si kidogo. Nilipomtazama usoni macho yetu yaligongana, akatabasamu. Naama ndipo hapa ambapo niling’amua, nimewahi pia kumuona huyu binti… yes, nimewahi kumuona. Nilibakia nimemkodolea macho tu… binti alitembea kwa mwendo wa madaha kama mwanamtindo na kwenda kukaa kwenye kiti pale ambapo yule kijana wa kizungu ambaye Winnie alisema kuwa alikuwa anamfutilia alikuwa ameketi. Naam, sasa kumbukumbu yangu ilinijea sawia kabisa, niwahi kuwaona hawa watu… ni siku ile pale Radisson Blu Hotel… siku ile ambapo nilikuwa nabishana yule muhudumu Erica, pale kwenye eneo la kupumzika pale mapokezi kulikuwa na mama mwenye mtoto, alafu kulikuwa na yule jamaa mwenye kuvaa kofia ya pama na koti refu jeusi na pia kulikuwa na hawa wapenzi wawili. Ni hawa hawa ambapo nilipochukua taxi na kuondoka nao walichukua taxi nyingine na kunifuatilia kwa nyuma. Kisha nilipomuamuru dereva asimamishe gari nao walimama kwa muda wa kama dakika moja hivi na kisha kuamua kuondoka wakitupita kwa kasi pale tuliposimama. Naam, ni hawa hawa. Mapigo ya moyo yalinienda mbio.



    “What is it?” Winnie aliniuliza.



    Alikuwa ameona namna ambavyo nilibadilika mara baada ya yule binti wa kizungu kuingia humu mgahawani na kwenda kuketi pale kwa yule kijana wa kizungu.



    “I know them!” nilimjibu bila kumuangalia. Macho yangu bado nilikuwa nimeyakaza kuwatazama wale vijana wa kizungu.



    “Who are they?” Winnie aliniuliza kwa shauku.



    “I don’t know who they are but this is not the first time I see them!”



    Nikiwa najiuliza kichwani ni nini kilikuwa kinaendelea na watu hawa ni akina nani, mara yule kijana wa kiume alimuita muhudumu na kisha kumlipa. Wakainuka yeye na mwenzake yule binti aliyekuja hapa dakika chache ziliopita na kisha wakatoja nje ya mgahawa na kuondoka.

    #419

    Nilihisi kichwa kinataka kupasuka, nilihisi maluweluwe mbele yangu. Kwa nini waondoke? Si Winnie amenieleza huyu kijana amekuwa anamfuatilia.? Kwa nini wameondoka na kutuacha hapa?

    Nikawaza haraka haraka lakini sikupata jawabu.

    Kwa nini huyo mtu aliyemuita Winnie waje kukutana kwenye mgahawa ule ule ambao mimi niliitwa pia siku ya kwanza tu nilipowasili hapa Zurich na kutolewa damu na kudungwa sindano ya usingizi? Lakini Winnie anadai pia ni mgahawa huu huu ambao aliitwa miaka miwili iliyopita, hii maana yake kwamba yeye alishawahi kufika hapa hata kabla ya mimi kufikiria kuja Zurich.

    Lakini kwa nini mtu huyo amuite tena leo hii, baada ya mimi na Winnie kuonana mchana, na kwa nini amuite ili kuongea sentesi moja tu? Papo hapo Winnie afuatiliwe, na ghafla tu wanaomfuatilia waondoke?



    Kuna mtu alikuwa anacheza na akili yangu. Sikujua alikuwa na lengo gani lakini ilikuwa dhahiri kwamba alikuwa hatua elfu kadhaa mbele yangu. Alikuwa ananichezesha ngoma ambayo nilikuwa siijui.



    “It’s a trap!” nilimwambia Winnie huku nikiangaza macho mle ndani ya mgahawa huku na huko kama vile kuna kitu natafuta.



    “What?” Winnie aliniuliza kwa mshangao.



    “This is a trap! Come with me.” nilimwambia tena huku namshiika mkono na kuanza kuinuka kutoka pale ambako tulikuwa tumekaa.







    “Where are we going Ray?” Winnie aliniuliza huku ametoa macho anashangaa.



    Nilielewa mshangao wake. Alikuwa anategemea kwamba tungetoka nje ya mgahawa tofauti na nilichokuwa nakifanya kumvuta kuelekea nyuma ya ‘kauta’ ambako kuna jiko. Kitendo cha wale vijana wawili wa kizungu ambao niliwahi kuwaona Radison Blu Hotel kuwepo hapa mgahawani na kisha kuondoka ghafla tu kilinipa mashaka. Kulikuwa na mtego ambao ulikuwa mbele yetu. Sikuelewa kwa haraka ni kwa nini walikuwa wanafanya haya lakini kwa mbali nilikuwa nimeanza kupata wazo mazingira ambayo yalikuwa yanatengenezwa. Ilikuwa haiingii akilini watu hawa kunifuatilia mimi au Winnie, kwa sababu nilikuwa na hakika kabisa wanajua mahala gani naishi na walikuwa wanajua pia Winnie anaishi wapi. Nilikuwa na hakika kabisa wanajua mambo mengi kuhusu mimi na hata kuhusu Winnie. Kwa nini walikuwa wanatufuatilia? Kulikuwa na jawabu moja tu ambalo lilikuwa na mashiko…



    “stop being stubborn… just come with me.!” Niliongea huku naendelea kumvuta Winnie mkono kuelekea kule jikoni kwa huu mgahawa.



    “Please explain it to me… what’s going on here?”



    “I will explain later… we don’t have much time… just come!”



    Tulifika mpaka kwenye malango wa jiko la mgahawa. Kulikuwa na kijana wa Kichina ambaye alikuwa amevalia suti nyeusi na mwili wa miraba minne uliojengeka kwa mazoezi alikuwa amejaa mlangoni akituzuia tusipite. Nikamuangalia kwa kumkazia macho nikimaanisha kwamba asogee pembeni na kunipisha nipite lakini hakutikisika wala kupepesa macho. Kitendo chake cha kubakia kuziba mlango tu ili tusiingie jikoni lakini kushindwa kutuondoa pale kwa nguvu kilinipa moyo kwamba mtu huyu hakuwa na hakika hasa kichwani mwake kama atuondoe au aturuhusu kuingia.



    “Step aside.!” Niliongea kwa kujiamini huku nimemkazia macho. Winnie alikuwa amesimama pembeni yangu kwa utulivu mkubwa na kwa uoga.



    Yule kijana wa kichina bado alikuwa amesimama pale mlangoni bila kutikisika wala kupepesa macho.



    “I need my dragon wings.!!” Niliongea kwa sauti kubwa nikitaka watu walioko huko jikoni wanisikie.



    “What are talking about??” Winnie alihamaki huku ametumbua macho akishangaa kile ambacho nilikuwa nimekisema.



    “Shut up! Just wait and see…!” nilimnyamazisha Winnie “I need my dragon wings.!!” Nilirudia tena kuita kwa sauti.



    “Let him in.!” sauti iliyojaa lafudhi ya kichina iliongea kutokea ndani ya jiko.



    #421

    Winnie alibakia ametumbua macho asielewe kile ambacho kilikuwa kinaendelea. Hakuelewa kuhusu hili neno la fumbo ambalo nilipewa siku yangu ya kwanza tu kuingia Zurich ambapo nilitakiwa kufika kwenye mgahawa huu na kuwaambia wahudumu waniletee ‘dragon wings’. Siku ambayo hapa hapa mgahawani baada ya kuwaambia neno hilo la siri nilikutanishwa na yule mzee wa kichina ambaye alinichoma sindano ya kemikali na kupoteza fahamu na kujikuta nimeamka kwenye lile jengo mtaa wa Hardstrasse.



    Yule kijana wa miraba mine alisogea pale mlangoni na kutupisha tuingie jikoni. Lilikuwa ni jiko la kisasa la ukubwa wa wastani. Kulikuwa na wapishi kama watano hivi wakiwa na ‘apron’ zao za upishi kila mmoja akioneakana kuwa ‘bize’ kuandaa chakula. Katika wapishi hawa watano mmoja wao alikuwa yule mzee wa kichina ambaye nilikutana naye hapa nilipokuja siku ile ya kwanza.



    “Give us some privacy!” yule mzee aliongea na wapishi wengine na wote kwa haraka na heshima kubwa walitoka jikoni.



    Yule kijana wa miraba mine ambaye awali alikuwa ametuzuia tusiingie pale mlangoni alifunga mlango kwa ndani. Kwa hiyo ndani ya jiko tulibakia mimi, Winnie, yule mzee na kijana huyu wa miraba minne. Winnie taharuki iliongezeka usoni mwake baada ya mlango wa jiko kufungwa.



    “PUUUUUUUUHH.!!!” Nilikuwa nimegeuka nikimuangalia yule kijana akifunga mlango na ghafla nilishitukizwa kwa ngumi nzito ya uso iliyonifanya nijiinamie nikishikilia mdomo na kugugumia kwa maumivu.



    “That’s for Ivanka!” yule mzee wa kichina aliongea huku nikimuona akivuta kasi ili kunidondoshea ngumi nyingine.



    “PUUUUUUUUHH.!!!” Alinidondoshea ngumi ya pili ambayo ilinipata tumboni.



    Nilidondoka chini na kujinyongorota kwa maumivu.



    “That’s for Luke…” mzee aliongea kwa kukereka.



    “what…the ****…are you doing!” niliongea kwa taabu nikijinyongorota kwa maumivu pale chini sakafuni.



    “stupid kid… get up!” mzee alifoka na kuja kuninyanyua mzobe mzobe na kunikalisha kwenye moja ya kiti pale jikoni. Alikuwa ni mzee wa makamo lakini nilishangaa namna ambavyo alikuwa mkakakamavu.



    Nilikaa kwenye kitu huku nikiwa kama niko ‘disorriented’. Nilikuwa naona maluweluwe tu. Alikuwa amenishambulia kwa kunishtukiza na sikuwa namuelewa maana ya kile ambacho alikuwa anakisema.



    “I told you to go back to the hotel and wait motherfucker! Is that hard?” mzee alifoka huku amenikwida shati uso wake akiwa ameusogeza karibu kabisa na wa kwangu.



    Nilibakia nimetumbua macho tu nisijue ni kitu gani hasa niongee. Nakumbuka mara ya mwisho tulipoonana alinipa maagizo hayo. Siku ile ambayo nilikuta mgahawa umefungwa na kuzunguka mlango wa nyuma. Kijana wake wa ulinzi aliponikamata nilimueleza kuwa nimetumwa na ‘melchizedek’. Baadae aliniuliza swali la mtego ambalo nililijibu kwa usahihi. Na kisha akanieleza “go back to the hotel and wait”. Lakini nilipofika hotelini na kukuta chumba kizima kinanukia harufu ya windex na pia kukuta kopo hilo la dawa ya windex imesahauliwa chumbani kwangu niliamua kuondoka na kuhamia kwenye jengo la Hardstrasse. Ni kweli sikufanya kama vile ambavyo alikuwa amenieleza, lakini sikuelewa hiki kipigo chote na kunitajia majina ya Ivanka na Luke alikuwa na maana gani hasa.



    “do you know what you have done you son of bitch!! You killed them both..!” mzee alifoka huku akiniachia kwa nguvu shati ambalo alilkuwa amenikwida na kunifanya nisukumwe nyuma nusura nidondoke tena ardhini.



    “I don’t understand!” niliongea kwa sauti ya kutetema kwa hasira na uoga.



    Yule mzee alienda mpaka upande mmoja wa jiko ambako kulikuwa na makorokoro akapekua pekua na kisha kutoka na bahasha mbili za kaki.

    Akatembea haraka haraka kwa hasira mpaka pale nilipo. Kwa hasira kubwa aliweka zile bahasha mbili kwenye meza ya karibu yangu. Kisha nikamuona anafunua lile apron lake la upishi na kisha anapeleka mkono wake kiunoni. Alipotoa mkono alikuwa ameshikilia bastola mkononi.

    Sikujua kama nikimbie au nifanye nini. Wote wawili, mimi na Winnie tulibakia tumetumbua macho huku tukitetemeka kwa hisia ambayo tulikuwa nayo kichwani yule mzee alichokuwa anataka kukifanya.

    Lakini ajabu ni kwamba aliigeuza ile bastola na kuishika mdomoni huku mshikio akiuelekeza kwangu kwa maana ya kwamba alikuwa ananikabidhi ile bastola. Niliipokea huku mikono inatetemeka. Akachukua na zile bahasha mbili ambazoa likuwa ameziweka pale mezani awali nazo pia akanikabidhi.



    “this is the package that I delivered for you at Radison Blue but you were not there.!” Mzee aliongea kwa hasira huku amenikazia macho.



    “I don’t understand!” nilimjibu huku bado nikiwa natetemeka.



    “Now you are on your own Ray! Don’t ever come back here… if I ever see you here again I swear to God I’m gonn’ skin you alive!” mzee aliongea kwa hasira na kwa msisitizo akionekana kumaanisha kila neno ambalo alikuwa analiongea.



    Nilibakia nimemkodolea macho kwa karibia nusu dakika. Niligeuka kumuangalia Winnie, alikuwa ananiangalia kwa woga kama vile ameona kifo mbele yake.

    Nikageuka kumuangalia tena yule mzee.



    “I don’t understand!” nikamweleza tena.



    “Get the **** out of here before I cut off your haed!” mzee aliongea huku ameanza kupiga hatua za taratibu kunifuata tena.



    “Let’s go Ray!” Winnie aliongea kwa upole huku ananishika mkono kuniondosha. Nahisi alikuwa amegunduka kwamba kutokana na kilichokuwa kimetoka hapa haraka haraka, akili yangu ilikuwa imesizi ghafla na sikuwa nawaza sawasawa, nilikuwa kama niko kwenye bumbuwazi na uwepo wangu hapa ulikuwa unaendelea kumtia hasira huyu mzee.



    Tulitoka jikoni na moja kwa moja kutokea sehemu ya mbele ya mgahawa ambayo tulikuwa tumekaa awali. Tulitembea haraka haraka na kutoka nje mpaka kwenye gari ya Winnie ambayo alikuwa amekuja nayo na kuingia ndani haraka.



    #422

    Ulipita ukimya wa karibia dakika tatu nzima tukiwa ndani ya gari pasipo yeyote kusema neno wala kung’oa gari. Nilikuwa nimefumba macho na kujilaza kwenye siti nikijaribu kuiweka akili yangu iwaze vyema sawa sawa. Nilishtushwa na mikono laini ambayo ilikuwa imenigusa usoni kama inanipapasa.



    “Let me take a look at that!” Winnie alikuwa amenishika kichwa na kukigeuza kutaka kuangalia vyema lile aneo ambalo yule mzee alikuwa amenipiga ngumi. Mwanzoni pale jikoni sikutambua ila sasa hivi ndio niligungua kuwa palikuwa pamechanika na kulikuwa na damu kidogo zilitoka japo kwa sasa zilikuwa zimekoma kutoka.



    “Leave it alone… its ok!” nilimtoa mikono yake usoni na kuinuka na kukaa vyema wima.



    Kilipita kimya kingine cha dakika moja nzima bila yeyote kuongea lakini wote wawili tulijua kabisa ni kitu gani ambacho tunapaswa kukizingumza.



    “what’s going on Ray?” Winnie aliuliza hatimaye na aliuliza kwa sauti ya upole kabisa na utulivu kana kwamba alikuwa ananionea huruma.



    “I don’t even know where to start!” niliongea huku nimefumba macho.



    “Start from where you said this was a trap!”



    Nilitafakari kwa muda wa kama sekunde ishirini hivi kisha nikaanza kumueleza Winnie. Kwanza nilimueleza kwa kifupi kuhusu uwepo wa kikundi cha HUDINI na namna ambavyo wanapaswa kunipa taarifa ambazo zimenifanya nije hapa Zurich. Kisha nikamueleza wasiwasi wangu kwamba kuna uwezekano kuna watu wengine nje ya HUDINI nao walikuwa wanaitaka taarifa hiyo ambayo HUDINI wanayo. Nilimueleza ni kwa namna gani ambavyo maelezo alinipa juzi kwamba kuna watu wamekuwa wakimfutilia kwa muda wa wiki tatu zilizopita kwa kupaki gari nje barabarani kwenye ile nyumba mtaa wa Affoltranasse. Nilimueleza kwamba nina imani kubwa waliomuajiri ni mawakala wa HUDINI kwa hiyo hawana sababu ya kumfutilia kwa hiyo hii ilimaanisha kwamba watu ambao wanamfuatilia ni wengine nje ya HUDINI. Nikamweleza Winnie pia kwamba HUDINI hawana sababu ya kunifuatilia mimi kwa sababu walikuwa wanajua naishi wapi hapa Zurich na mambo mengine yote. Kwa hiyo kitendo hiki cha kufuatiliwa kilikuwa kinaonyesha dhahiri kabisa kwamba kulikuwa na watu wengine wapinzani wa HUDINI. Lakini pia nilimweleza kuhusu mauaji ya Luke na Ivanka siku mbili tu baada ya mimi kuonana nao iliashiria dhahiri kabisa kwamba Ivanka na Luke kuna uwezekano mkubwa walikuwa ni mawakala wa HUDINI na waliuwawa na wapinzani wao.

    Baada ya hapo nilimueleza kwa nini nilihisi kwamba kuitwa kwake hapa kulikuwa ni mtego… kwanza kabisa nikamueleza kwamba ahiingii akilini mtu amuite kumwambia sentesi moja tu kuwa “kamwe asimruhusu mtu kuingia ndani ya nyumba ile ya mtaa wa Affoltrenasse”. Kwa hiyo hisia yangu ni kwamba HUDINI walikuwa wanafanya ‘counter-survaillance’, kwamba walikuwa hawajui kinagaubaga adui yao ni nani kwahiyo walimtumia yeye kumuita hapa wakijua kuna uwezekano mkubwa na yeye kuniita mimi hapa ili wote tukiwa sehem moja ni chambo kizuri cha hao watu wanaotufuatilia kufanya hivyo na papo hapo HUDINI kutumia mwanya huo kuwang’amua wabaya wao.



    Nakumbuka Winnie aliniuliza kwa nini HUDINI wasinipe tu hiyo taarifa ninayotakiwa kuwa nayo ili niondoke na kuepusha madhila yote haya. Nikamjibu kwamba hisia yangu ni kwamba HUDINI walikuwa wanaogopa kunipa taarifa hiyo kienyeji au kirahisi rahisi kwa kuhofia taarifa hiyo inaweza kuchukuliwa kwa urahisi kutoka kwangu na hao maadui zao.



    #423

    “I know it doesn’t make any sense but that’s what is in my head!” nilijitetea baada ya kuhisi ufafanuzi wangu ni wa kuunga unga mno.



    “No, actually it make sense some how.” Winnie akanitia moyo japo sikudhani kama alikuwa anamaanisha kweli maana hata mimi mwenyewe nilikuwa na wasiwasi na nadharia yangu.



    “So what made you go to the kitchen and get your ass beaten?” Winnie aliongea huku anatabasmau. Tulijikuta wote tumeangua vicheko.



    “I have this principle… stall, confuse, deflect!”



    Nikamueleza ni namna gani ambavyo mara nyingi nikiwa kwenye mazingira ninayohisi kuwa natumika kama chambo au nashawishiwa nichukue hatua fulani huwa napenda kufanya kitu ‘random’ ambacho huyo mtu anayenifuatilia alikuwa hakitegemei ili kumchanganya asiweze kuelewa hatua ambayo niyaichukua tena baada ya hapo.



    “stall, confuse, deflect! I like that!” wote tukatabasamu. “so what’s up with those envolopes and the gun.”



    “that part I tottaly don’t understand… it was a surprise even to me!”



    Aliponiuliza kuhusu zile bahasha nilihisi huu ulikuwa muda muafaka wa mimi kuzifungua bahasha hizo kujua kulikuwa na nini ndani yake.

    Nikaifungua bahasha ya kwanza.ndani yake kulikuwa na picha ya Delani na mkewe wakiwa pamoja na Luke na Ivanka wakiwa watoto. Ilikuwa ni picha sawasawa kabisa na ile picha ambayo niliichukua siku ile kwenye nyumba ya kule Affoltranasse.



    “I know this photo!” Winnie alihamaki.



    Naam sikushangaa Winnie kusema anaijua picha hii kutokana na uwepo wa picha kama hii kule kwenye nyumba ya Affoltrenasse ambayo niliiba siku kadhaa zilizopita.

    Nikafungua bahasha ya pili. Ndani yake kulikuwa na picha ya Delani akiwa pamoja na yule jamaa ambaye nimekuwa nikimuona mara kadhaa, yule jamaa anayevaa kofia ya pama na koti refu jeusi. Tofauti pekee kwenye picha alikuwa anaonekana hana lile kovu alilonalo sasa usoni.

    Nikamweleza Winnie kwamba ninazo piacha nyingine kadhaa zikimuonyesha Delani akiwa na watu wengine tofauti tofauti. Nilihisi kwamba siri yote ambayo natakiwa kuijua imefichwa kwenye hizi picha. Natakiwa kuzitazama picha zote hizi na kisha kujaribu kutafsiri kile ambacho kimejificha kwenye picha hizi maana ndicho kitu pekee kinachoonyesha kina umuhimu mkubwa kwenye kisanga chote hiki.



    “I agree with you but we need to get a safe place and rest for the night!” Winnie alinijibu.



    “Sure! The problem is I don’t think if its safe anymore for me to go back to Hardstrasse or for you to go back to your place!”



    “you said stall, confuse, deflect! That’s what we going to do… I have an idea.!” Winnie aliongea huku anatabasamu kwa bashasha na kung’oa gari.



    Japokuwa tulikuwa kwenye dhahama kubwa lakini kulikuwa na kitu fulani kikubwa juu ya Winnie kilikuwa kinajengeka moyoni mwangu. Nilihitaji ‘upako’ wa ziada niweze kumshinda shetani kwenye kile ambacho nilihisi kinaweza kutokea kati yangu na Winnie siku si nyingi.







    Winnie ndiye ambaye alikuwa amekaa kwenye usukani akiendesha gari na mimi nikiwa kwenye siti ya abiria. Alikuwa amekata kona kuingia mtaa wa Affoltrenasse. Kichwani nilikuwa tayari nimehisi ni wapi ambapo tulikuwa tunaelekea. Alipokata kona tu kuingia mtaa wa affoltrenasse nilimuangalia na kutabasamu na yeye alinikata jicho na kutabasamu pia. Tulikuwa tunaelekea kwenye ile nyumba ambayo ameajiriwa kufanya usafi, nyumba ambayo masaa machache yaliyopita alionywa kwamba asimkaribishe mtu yeyote yule ndani.

    Tangu ambapo tulitoka kule kwenye mgahawa wa kichina mpaka kufika hapa affoltrenasse kulikuwa na ukimya fulani umetawala kati yetu. Ukimya ambao ulikuwa kana kwamba unabembeleze kitu fulani kisemwe. Kitu ambacho hakipaswi kusemwa na hakikuwa na ulazima wa kusemwa kwa sababu wote kati yetu kilianza kujengeka mioyoni mwetu. Kitu kilichokuwa kinafanya ukimya huu kati yetu kwa dakika chache kuwa kama bakshikshi ya kuchochea uthibitisho wa kile ambacho tulikuwa tumeanza kukihisi mioyoni mwetu lakini tukifanya juhudi za kutaka kukizima.



    Tulikuwa tayari tumefika mbele ya nyumba mtaa wa affoltrenasse na kupaki gari. Kulikuwa na kimvua fulani chepesi kimeanza kunyesha.http://pseudepigraphas.blogspot.com/

    Tulikaa kimya kwenye gari kwa karibia dakika tatu nzima bila yeyote kati yetu kusem chochote. Sikujua kama Winnie alikuwa anatafakari namna ambavyo tulikuwa tunaelekea kuvunja agizo alilokuwa amepewa kwamba asimkarinishe mtu ndani ya nyumba ile au kama alikuwa anawaza kile ambacho nilikuwa nakiwaza mimi kichwani mwangu… nini kitatokea kati yetu leo hii gizani?



    “are you ready for this?” Winnie aliniuliza nikiamini kwamba alikuwa anamaanisha kuhusu kuingia ndani ya ile nyumba kinyume na maagizo ambayo alikuwa amepewa.



    “not so sure!” nilimjibu huku natabasamu.



    “Let’s do this!!” aliongea na mara moja akafungua mlango na kutoka nje ya gari, nami nikafanya hivyo.



    Kutokana na ile mvua ndogo ambayo ilikuwa inanyesha Winnie alikuwa amejikumbatia mikono akiiweka kifuani mwake huku anakimbia kuelekea kwenye mlango wa nyumba. Sijui kama ni kwasababu ya mvua au kutokana na umbo lake lakini nilihisi kama vile nguo zake zimekuwa nyepesi zaidi mwilini mwake na kumfanya akiwa anakimbia mwili wake ulivyokuwa unatikisika kufanya nisikie kama cheche zinapita mwilini mwangu. Nilijikuta nasikia wivu namna ambavyo matone ya mvua yalikuwa yanatiririka mwilini mwake nikitamani kana kwamba matone yale ya mvua yangelikuwa ni kiganja changu cha mkono kikiambaa ambaa mwilini mwake namna ile.



    “Are you coming or what?” Winnie alinigutusha kutoka kwenye mgagaziko uliokuwa umenikuta ghafla nikivuta hisia na kujikuta nimesimama bila kutembea katikati ya mvua nikimtazama bila kujijua.

    #432

    “Coming.!” Nikaanza kukimbia kutoka kwenye mvua na kuelekea kwenye mlango wa nyumba.



    Pembezoni mwa nyumba kulikuwa kuna maua ambayo yalikuwa yamaeoteshwa kwenye bakuli kubwa za udongo za urembo. Winnie alitembea mpaka kwenye bakuli kama ya nne hivi kutoka mlangoni na kuifunua na kisha kuingiza mkono chini yake na kutoka na funguo.



    “Oh so there is where you keep the keys!” nilongea kwa utani.



    “Yap! For emergencies..” Winnie alijibu huku anakimbia kutoka pale kukwepa mvua na kurudi mlangoni.



    “Emergencies!?”



    “Yeah! Like today.”



    Tukacheka kisha Winnie akafungua mlango tukaingia ndani.



    “I’m such a bad girl!” Winnie aliongea kwa sauti ya utani.



    “Why is that?” nikamuuliza



    “First date and I’m taking you back home.” Akaoongea tena kwa utani



    “I like naughty girls!” nikamjibu pia kwa utani.



    Yalikuwa ni maneno ya utani lakini kichwani mwangu nilikuwa namaanisha kila neno ambalo nililisema. Nilitamani kwamba naye kchwani mwake awe japo na asilimia fulani ya kumaanisha kwa haya maneno ya utani ambayo ameyasema.



    “Don’t turn on the lights.” Niliongea kwa sauti ya kunong’ona.



    “why?”



    “that’s the easiest way for someone to know that we are inside.”



    “I bet they already know we are inside.” Winnie alinijibu lakini hakuwasha taa kama ambavyo nilitaka.



    Japokuwa kulikuwa na giza lakini niliweza kuona kwa mbali mule ndani. Kulikuwa kama ambavyo nilipaona siku ya kwanza. Nadhifu na pamepangiliwa sawia kabisa kana kwamba kuna watu wanaishi ndani yake.

    Nilikuwa natamani kuichunguza hii nyumba nukta baada ya nukta nikiamini kabisa kwamba kuna baadhi ya maswali ambayo nitayapatia majawabu. Lakini nilikuwa nashindwa kabisa kubandua macho yangu kutoka kwa Winnie ambaye alikuwa amesimama kwenye moja ya dirisha kuangalia nje barabarani kana kwamba anahakikisha hakukuwa na mtu ambaye alikuwa anatufuatilia.

    Kutokana na giza ambalo lilikuwa humu ndani lilifanya pale dirishani ambapo alikuwa amesimama na mwanga hafifu ukimmulika kutokea nje kulifanya apendeze zaidi kumuangalia umbo lake ambalo nguo zilikuwa zimeshika mwili sawia kutokana na mvua ndogo ile ambayo ilikuwa imemnyeshea.



    Damu illikuwa imeanza kunichemka nikisikia mshawasha wa cheche ukitembea mwilini.

    “what are you looking at!” Winnie aliongea kwa sauti ya nyororo ya ushawishi kama ananong’ona bila kugeuka kuniangalia. Nilihisi kabisa namna ambavyo hata yeye mwili wake unawaka moto wa matamanio muda huu.



    Sikujibu. Nilipiga hatua za taratibu kumfuata pale dirishani ambako alikuwa amesimama. Nilikuwa nahema taratibu lakini niliusikia moyo namna ambavyo ulikuwa unadunda kwa nguvu kama unakaribia kutoka nje ya kifua. Winnie alinisikia namna ambavyo nilikuwa namsogelea lakini hakugeuka, aliendelea kusimama vile vile akiwa amenipa mgongo.

    Nilisogea mpaka kufika nyuma yake kabisa tukigusana, makalio yake yakinigusa katikati ya mapaja yangu, uso wangu ukiwa nyuma ya kichwa chake ukiparaza nywele zake laini. Winnie hakusogea wala kutikisika, kitu pekee ambacho nilikisikia ni namna ambavyo alikuwa anahema kwa nguvu kama vile anapanda mlima. Taratibu nikapenyeza mikono yangu ubavuni kwake mpaka mbele kifuani kwake na kumkumbatia kwa nguvu nikimvuta kwangu. Japokuwa alikuwa ameloa kiduchu na ile mvua lakini mwili wake ulikuwa ni wa moto kana kwamba alikuwa amebanikwa kwenye jiko la mkaa.

    Niliusikia namna ambavyo mwili wake ulikuwa unaitika kwa kulegea nyang’anyang’a kana kwamba ulikuwa unapasuka vipande vipande. Nilihisi namna ambavyo alikuwa ameishiwa nguvu… akalaza shingo yake begani kwangu.



    “you are so beautiful!”



    Nilimnongoneza taratibu sikioni kama vile namng’ata. Niliusikia mwili wake namna ambavyo ulisisimkwa nilipokuwa nanong’ona sikioni mwake. Alikuwa anahema kwa nguvu nikihisi ameishiwa nguvu kiasi kwamba alikuwa kuna kitu anataka kusema lakini alishindwa na kuishia kutoa miguno tu…



    “Mmmmmhhhh.!”



    Nilimkumbatia kwa nguvu zaidi huku mikono yangu kifuani kwake nikiipa uhuru wa kubinya chuchu za matiti yake taratibu. Alikuwa anajinyonganyonga kana kwamba anataka kujinasua mikononi mwangu lakini kwa namna ambavyo utamu ulikuwa umemkolea nilihisi alikuwa anataka zaidi.

    Akaanza kwa kupeleka mkono wake mpaka juu ya suruali yangu na kuanza kuushika mkuki akipeleka mkono juu na kurudisha chini. Nilihisi kama vile suruali ilikuwa inakaribia kuchanika kwa namna ambavyo mkuki ulichachamaa ndani ya suruali. Nikamvuta tena kwangu kwa nguvu zaidi… bado tulikuwa hatuangaliani uso kwa uso. Alikuwa amegeukia dirishani na mimi nimekumbatia mgongoni.

    Nilikuwa nimepandwa na mori iliyochanganya hasira na matamanio na hamu kubwa haswa ya kutaka kuusulubisha mwili wake usiku mzima wa leo.

    Nilimvuta kwa nguvu haswa na kuzama shingoni mwake nikiilamba na kuimungunya shingo kama pipi. Winnie alikuwa anajinyonga nyonga kama vile nyoka aliyemwagiwa mafuta ya taa huku anatoa miguno mikubwa akiendelea kuhema kwa taabu sana. Taratibu niliusikia mkono wake akiuzamisha ndani ya suruali yangu na kwenda kuushika mkuki akifanya kama mwanzoni akiupeleka mkono juu na kuushusha chini.

    Uzalendo ulinishinda nikamkamata kwa nguvu na kumgeuza tukawa tunaangaliana.



    Alikuwa anahema kwa nguvu kama anataka kukata roho. Nilijikuta ghafla kwa hasira na mori ya matamanio nimeikamata blauzi yake na kuichana kwa nguvu kutoka kifuani mwake. Sikujua kama Winnie alikuwa hajavaa braa au kama niliichana pamoja na ile blauzi, lakini ninachokumbuka ni Winnie alikuwa mbele yangu kifua wazi matiti yakiwa yamesimama kama kigoli wa miaka kumi na saba. Hii ilikuwa ni moja ya nyakati chache ambazo niliweza kusifu ufundi na umaridadi wa aliye juu katika uumbaji wake. Katika wakati huu kama ningepewa kontena lililojaa dhahabu na mwili wa Winnie, hakika



    #434

    ningelichagua mwili huu ambao ulikuwa mbele yangu muda huu nikiutazama. Namna ambazo matiti yake yalikuwa yamejaa sawia kifuani mwake, chuchu zikiwa zimesimama kama mwali wa kimanga, na tumbo lake tambarare kama sakafu ambalo lilijiunga vyema kwenye kiuno chembamba ambacho kilikuwa kinashawishi kukimata na kukisulubisha … kwa hakika alipoumbwa muumbaji alitulia.

    Winnie alikuwa bado anahema kwa nguvu… alinishika shingoni kwa nguvu na kunivuta midomoni mwake. Niliibusu midomo yake na kuinyonya ndimi yake kana kwamba ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kwenye maisha. Morali na mshawasha ambao tulikuwa nao ulifanya tunyonyane ndimi kama vile tulikuwa tunapigana. Mkono wake ulizama tena ndani ya suruali yangu na mimi nilikuwa natembeza mikono yangu mgongoni mwake, kushuka mpaka kiunoni na mpaka chini ya kiuno kwenye ‘mitungi’ miliwi iliyounganishwa na kiwili wili chake chini ya kiuno. Nikaanza kumvua kisuruali chake taratibu mpaka ilipofika magotini ambako alimalizia mwenyewe kuivua kwa kuikanyaga na upande mmoja na mguu na ilipovuka upande mmoja akakanyaga tena upande mwingine.



    Winnie alikuwa amesimama mbele yangu akiwa mtupu kabisa isipokuwa nduo ya ndani tu. Mimi nilikuwa kifua wazi na suruali mkanda ukiwa tayari umefunguliwa. Tulikuwa tunanyonyana ndimi kwa nguvu na morali huku mkono wangu mmoja ukipapasa ‘mitungi’ yake na kumvua nguo ya ndani taratibu.

    Sijui ni nini ambacho kilinitokea lakini nilipoanza kumvua Winnie nguo ya ndani sura ya mkewangu Hasnat, Cheupe wangu ghafla ilikuwa inanijia akilini… nilijikuta nimejinasua kukota kwenye mikono ya Winnie.



    “I can’t do this!” niliongea huku nahema.



    Winnie akafanya kama vile hajanisikia. Alinirukia na kunivuta tena mdomoni mwake na kuingiza tena mkono ndani ya suruali.



    “No no no! stop..!” nilijinasua tena kutoka mikononi mwake huku nikihema kwa nguvu.



    Winnie naye alikuwa anahema kwa nguvu huku amenikodolea macho akishangaa akiwa haamini kile ambacho nilikuwa nakisema.

    Sikujua ni kitu gani ambacho kilikuwa kinanisibu lakini haijalishi ni kwa kaisi gani nilijitutumua kiume kupoteza nisimuwaze cheupe kwa wakati huu nilishindwa na sura yake ilikuwa imejaa kwenye akili yangu. Nilijisikia hatia moyoni kiasi kwamba hata morali ya ‘kumsulubisha’ Winnie ilipotea. Ule mshawasha wa mapenzi wote uliyeyuka ghafla… nilibakiwa na hatia tu moyoni.



    “I’m so sorry Winnie! I can’t do this..!!” niligeuka pembeni kwa aibu.



    Hakuna kitu kibaya kama kumvua nguo zote mwanamke alafu uhairishe kufanya tendo lenyewe. Nilimuona Winnie akijisikia aibu kiasi kwamba nilihisi alitamani akimbie kutoka mle ndani. Alikaa chini na kujikunyata akificha matiti yake kwa viganja vya mikono huku anazoa zoa nguo zake kutoka sakafuni. Sidhani kama nimewahi kujisikia aibu kwa kiasi kile. Nilijisikia aibu na hasira kwa nafsi yangu kwa hiki ambacho kilikuwa kinatokea.



    “I’m sorry!” niliomba tena radhi huku nikienda upande mwingine wa sebule na kukaa chini nikijiinamia.



    Winnie hakusema chochote kile, nilimsikia tu akiwa na purukushani za kuvaa nguo haraka haraka. Alipomaliza kuvaa nguo naye alikaa chini sakafuni lakini hakujiinamia… alikuwa ananitazama kwa hasira bila kusema chochote. Nilikosa hata ujasiri wa kumuangalia. Nikajiinamia chini.

    Tulikaa hivyo kwa muda wa kama dakika kumi nzima bila yeyote kati yetu kuongea. Winnie akiwa ananitazama kwa hasira na mimi nimejiinamia chini.

    Nikamsikia Winnie amesimama na anagusa gusa funguo mkononi.



    “There is something I want to show you… I think might help us… come with me!” aliongea bila kuniangalia huku anaanza kutembea.



    Nilishtuka kutoka kwenye kujiinamia kwa mawazo na kuinuka na kuanza kumfuata ambako alikuwa anaelekea… kwenye ‘basement’ ya nyumba.









    "…wanasema tunajifunza kwa makosa ya awali, si kweli. Tunafanya makosa, tunahisi tumejifunza, kesho tunafanya makosa tena, tunahisi tena tumejifunza lakini mtodogoo tunafanya makosa kwa mara nyingine. Ni asili ya mwanadamu, kupungukiwa utimilifu. Japokuwa ni asili ya binadamu lakini bado haiondoi maumivu tunayoyasikia pale udhaifu wetu wa asili unaposababisha machozi kwa wale ambao wanatupenda zaidi, haiondoi kujuta pale ambapo udhaifu wetu unapopelekea usaliti na kuumiza nafsi za wanaotupenda sawa sawa na maisha yao. Ni maumivu haya ambayo yanafanya tukiona machozi ya watupendao tuhisi kama uhai umetutoka nafsini mwetu, tusikie hatia mioyoni mwetu kiasi kwamba tunasikia mpaka harufu ya kifo.

    Ni nini basi cha kutuokoa na udhaifu huu wa asili? Je tunapaswa kuishi tukiukubali udhaifu huu? Tuendelee kufanya makosa? Tuendelee kuwaumiza wanaotupenda? Labda pengine maumivu haya yanasababishwa na ulimwengu kutegemea makubwa kutoka kwetu. Labda ujasiri wanaona tunao unawafanya wadhani ni watimilifu, labda wingi wa akili tulizonazo unawafanya wahisi hatupaswi kukosea na pengine labda vipawa adhimu tulivyojaaliwa vinawapofusha wasione ukweli, ukweli dhahiri kabisa, ukweli usiopaswa kupuuzwa kwamba licha ya ujasiri wote, licha ya akili zote, licha ya vipawa vyote…. *I am only human.!!* Tunakosea, tunajifunza, kesho tunakosea tena, tunajifunza… na iko siku tutakosea tena..!"







    *Mtaa wa Hardstrasse, Zurich*



    Nilikuwa nimeamka tena kwa mara ya pili hii ndani ya siku hii hii moja. Ilikuwa inakaribia saa kumi jioni, na kilichoniamsha ilikuwa ni mlio wa simu. Simu ilikuwa imeita mara mbili hapo awali na sikuijibu lakini safari hii niliamua niamke ili kuijibu.



    "still sleeping?" Ilikuwa ni sauti ya Winnie upande wa pili wa simu.



    "I was… morning!" Nilimjibu huku napiga mihayo.



    "Its evening idiot! Are you coming?" Winnie aliongea kwa sauti ya utani aliponiuta 'idiot' lakini aliponiuliza kama naenda sauti ilibadilika akionekana kumaanisha.



    "Did you get it?" Nikamuuliza kwa shahuku.



    "Yap… got it!"



    "On my way!" Nikakata simu.



    Tangu awali ambapo simu ilikuwa inaita japo sikuangalia lakini nilijua kabisa lazima simu hiyo itakuwa ya Winnie. Nafsini mwangu nilikuwa sina ujasiri kabisa wa kuongea nae kutokana na kile ambacho kilitokea baina yetu jana usiku. Nilikuwa nasikia mzigo wa hatia moyoni. Japokuwa hatukufanya tendo la ngono kabisa lakini kitendo cha kutomasana tu kiasi kile ambacho tulifikia moyoni nilikuwa nasikia hatia ya kumsaliti mkewangu Cheupe. Nilitamani niinue simu nimtwangie mkewangu nyumbani Tanzania lakini moyo ulikuwa haupati ujasiri.

    Lakini pia kila ambapo nilifikiria kuonana tena na Winnie moyo wangu ulikuwa unapasuka vipande. Nawezaje kumtazama tena usoni? Ajabu ni kwamba sikuwa nasikia aibu kwa kutomasana vile bali nilikuwa najisikia aibu kwa kumchombeza na kumtomasa na kisha kuishia njiani bila kufanya tendo lenyewe.



    #449

    Lakini hii ilikuwa ni tofauti kabisa na winnie kwa namna ambavyo alikuwa anaongea kwenye simu utadhani kama vile hakukuwa na chochote kile kilichotokea jana usiku. Nilihisi kwamba hakutaka kuwe na 'tension' katikati yetu ukizingatia hii dhahama tuliyonayo. Alikuwa anajitahidi kwa nguvu zote kufanya mazungumzo nami kwa namna ya kawaida kana kwamba hakuna chochote ambacho kimetokea.



    Tangu jana usiku tulipoishia katikati ya mchezo ambao tulikuwa tunataka kuufanya Winnie hakuwahi kuniuliza kwanini sikutaka kufanya nae ngono wala kugusia kwa namna yoyote ile mazungumzo yenye mlengi huo. Badala yake jana ile usiku alichepusha maongezi na kunipeleka kwenye basement ya ile nyumba ya mtaa wa Affoltrenasse. Kwenye basement ambayo alinionyesha vitu ambavyo mpaka muda huu ubongo wangu umekuwa mzito nikiogopa hata kuviwaza.



    Wazo hili la kumbukumbu ya vitu ambavyo niliviona kwenye basement lilivyoanza kurejea kichwani niliacha kulifikiria haraka na kuinuka kutoka kwenye sofa ambayo ndio naitumia kama kitanda changu kwenye jengo hili la hapa Hardstrasse. Niliinuka haraka haraka na kuanza kuvaa nguo ili niweze kuelekea chuo kikuu cha Zurich alipo Winnie. Kwa hakika kabisa nilikuwa sitaki abadani kuonana na Winnie lakini taarifa ambayo alikuwa ananieleza kuwa anayo ilikuwa ni ngumu kuipuuza nisiende kutazama hicho alichokipata.



    Tulipoachana asubuhi kutoka pale affoltrenasse nilimueleza kwamba sikutaka kufikiria chochote kile kuhusu kile ambacho alikuwa amenionyesha kule chini kwenye basement. Nilikuwa nataka tufanyie kazi mfululuzo wa picha ambazo nimekuwa nazipata kuanzia zile ambayo niliikuta kwenye bahasha niliyoachiwa na marehemu mzee wangu, ile niliyopewa na Hudini na hii ambayo nilipewa jana na yule mzee wa kichina. Katika picha zile zote kulikuwa na kitu kimoja kikuu ambacho kiko kwenye picha zote… Delani. Yule mzungu anayeonekana kwenye picha akiwa na Rais Albert Kafumu kwenye eneo lenye makontena, ni yeye pia alikuwa kwenye ipe picha pamoja na Cheupe na baba yake na ni yeye pia alikuwa kwenye picha ambayo nilipewa jana na yule mzee wa kichina ambayo inamuonyesha Delani akiwa na yule jamaa mwenye kuvaa kofia ya pama na koti refu jeusi.



    Ilikuwa ni dhahiri kwamba kwa namna yeyote ile nilikuwa napaswa kuonana na Delani ambaye anaonekana ni kiunganishi cha watu wote hawa. Lakini kwa muda wa miaka miwili sasa hakuna ambaye anajua Delani yuko wapi. Wazo la pili ambalo tulilizungumza na Winnie ni kujaribu kumpata mmoja kati ya watu wale ambao anaonekana kwenye mojawapo ya zile picha. Ilikuwa haiwezekani kumpata Rais Albert Kafumu. Winnie akapendekeza nizungumze na Cheupe. Nikamkatalia. Cheupe alikuwa haungi mkono safari yangu ya hapa Zurich, kwahiyo napaswa kutafuta wakati mujarabu haswa ili kumuuliza kuhusu picha hiyo ya yeye akiwa mtoto pamoja na baba yake na bwana Delani.



    #450

    Kwa hiyo mtu pekee sahihi ambaye walau alikuwa ana uwezekano wa kumpata alikuwa ni yule jamaa wa kofia ya pama na koti refu jeusi. Walau huyu tulikuwa tunajua pasina shaka yeyote kwamba yuko hapa Zurich. Kama tukiweza kumtafuta na kumpata jamaa huyu walau tutakuwa na matumaini hata kiduchu na mwongozo wa kumpata Delani.

    Ndipo hapa ambapo tulikubaliana kutumia namba ya taxi ambayo yule jamaa wa kofia ya pama aliitumia kuja nayo pale chuoni na kupaki ng'ambo ya geti kuu la kuingilia chuo juzi wakati ambapo nilikuwa naongea na Winnie. Kwa bahati nzuri wakati taxi inaondoka nilifanikiwa kunakili namba yake, ZH 45789.



    Nilikuwa na imani kwamba kama nitaweza kumpata dereva taxi ambaye alikuwa anamuendesha yule jamaa siku ile basi naweza kumng'ang'aniza hata kwa hongo aniambie alimpeleka wapi yule jamaa walipotoka pale chuo na nikifahamu mahali ambako alimpeleka basi tunaweza kuanzia hapo kufuatilia nyendo za yule jamaa.

    Lakini ili tumpate yule dereva taxi, tunapswa kufahamu taxi ile ni ya kampuni gani, na ofisi zao ziko wapi na jina la dereva taxi ambaye alikuwa anaendesha taxi siku ile. Uzuri ni kwamba taarifa zote siku hizi ziko kwenye mifumo ya kompyuta. Lakini hatuwezi kuipata taarifa hiyo kwa urahisi pasipo ruhusa ya wenye kampuni. Tunapaswa kufanya uhuni mpaka tuipate.

    Winnie alinieleza kwamba chuoni kwao anawafahamu baadhi ya wanafunzi kutoka Nigeria ambao ni watundu wa mifumo ya Tehama.



    Tukakubaliana kwamba aipeleke namba hii ya taxi kwa wanafunzi wenzeke hao na wakimpa majibu stahiki ndipo anipigie ili tuanze mchakato wa kumtafuta huyo dereva taxi na hatimaye yule jamaa wa kofia ya pama.



    Maongezi haya tuliyaongea asubuhi wakati tunatoka kwenye nyumba ya affoltrenasse ambako tulilala jana usiku. Na sasa ilikuwa tayari saa kumi jioni na Winnie ananieleza kwamba tayari anayo taarifa kuhusu ile taxi ambayo yule jamaa wa kofia ya pama aliipanda juzi alipokuja pale chuoni.



    Nilichukua simu yangu tena na kuingia mtandaoni na kufungua tovuti ya kampuni ya uuzaji 'fast food' ambayo iko karibu na mtaa huu wa hardstrasse. Niliagiza pizza niletewe. Kama ambavyo tulikubaliana na Jimmy kwamba nikimuhitaji basi niweke boksi la pizza nje ya mlango wa jengo hilo na akiliona usiku atakuja hapa nikiwepo. Nilikuwa namuhitaji Jimmy, nilikuwa namuhitaji anisaidie kung'amua kile ambacho nilikiona kwenye basement ya nyumba ya kule affoltrenasse.



    Kama dakika saba baadae nilisikia mlango unagongwa. Uzuri nilikuwa nimemaliza pia kujiandaa. Nikachukua simu yangu na kutoka mpaka nje.



    "Keep change!" Nilimlipa kijana wa pizza na kuipokea. Alipoondoka nilifunua upande wa juu wa boksi kwa ndani na kuandika "i need a doctor". Nikiamini kabisa kwamba Jimmy atahisi kwamba nahitaji aje aniangalie kidonda changu cha risasi tumboni. Hii ingemfanye aje haraka na bila kukosa.

    Japo ilikuwa ni kweli nilimuhitaji aniangalie maendeleo ya kidonda… lakini nilimuhitaji zaidi kwa ajili ya kile ambacho nilikiona affoltrenasse. Mwili ulinisisimka kila ambapo nilikumbuka ile basement.



    Nikaweka boksi la pizza chini mlangoni na kuondoka kuelekea chuo kikuu cha Zurich kuonana na Winnie.







    Tofauti na juzi ambapo mimi ndiye nilikuwa wa kwanza kufika na kumsubiri Winnie, leo hii nilimkuta tayari amefika pale kwenye lango la kuingilia chuoni kwao akinisubiri.



    “you are late!” aliongea huku anatazama saa kwenye simu yake.



    “sorry! Had a few things to attend first!”



    Tuliongozana moja kwa moja na kuingia ndani ya eneo la chuo. Hostel zao wanazoishi zilikuwa kama mwendo wa dakika saba hivi kutoka pale kwenye lango kuu la kuingia ndani ya chuo. Muda wote huo ambao tulitembea kutoka pale getini mpaka kufika kwenye hosteli Winnie hakuongea neno lolote lile. Muda wote alikuwa anabofya simu yake.

    Mwanzoni nilihisi labda alikuwa anajisikia aibu kutokana na kile ambacho kilikuwa kimetokea jana usiku, lakini nilipomtazama usoni nilimuona akiwa anatabasamu kila mara huku anaendelea kubofya simu yake. Hii ilikuwa ni mara ya kwanza nikiwa na Winnie kumuona akiwa ‘bize’ na simu kana kwamba sikuwepo pale, nilisikia karoho kaniniuma kwa mbali lakini nikajitahidi kutoonyesha hisia zozote zile usoni. Tulitembea namna hiyo mpaka kwenye jengo la hostel ambalo alikuwa anaishi.



    “Karibu.!” Winnie alinikaribisha kwa kuongea neno la Kiswahili fasaha kabisa tulipofika nje ya chumba chake. Nilitabasamu na kumjibu



    “Asante sana!” nikamjibu pia kwa Kiswahili.



    Tukaingia ndani.



    kilikuwa ni chumba cha ukubwa wa wastani, kama futi kumi kwa futi kumi. Mtindo wake wa namna ambavyo kilipangiliwa ulikuwa unafanana sana na vyumba vya wanafunzi nyumbani Tanzania na kwa dakika kadhaa nikajikuta nakumbuka nilipokuwa mwanafunzi chuo kikuu Mzumbe miaka kadhaa iliyopita. Kulikuwa na kitanda cha futi nne kwa sita kwa namna ambavyo nilikadiria haraka haraka. Tofauti kubwa ya chumba hiki na nikikumbuka vyumba vya hosteli zetu za Mzumbe kilikuwa na nyongeza ya sehemu ya jiko, bafu na unadhifu wa vyumba hivi. Nilipotupa jicho kwenye meza yake ya kusomea nilijikuta napatwa na hasira fulani ya ghafla. Kulikuwa na mtu, mwanaume amekaa na kompyuta mpakato akibofya bofya.



    “Ray! This is Dafa… he is the one who is helping us with the issue.!” Winnie alinitambulisha mara baada ya kuingia.



    “hey man! Nice to meet you!” nilimpa mkono kumsalimia huku nikilazimisha kutoa tabasamu. Nilikuwa nachukia hali ya wivu ambayo ilikuwa inanikaba rohoni kumuona mwaume mwingine kwenye chumba cha Winnie.

    “So what have you got?” nikamuuliza huku navuta kiti kilicho karibu na kukisogeza karibu yake pale mezani na kuketi.



    “it was tricky at first but then I figured out…” yule jamaa niliyetambulishwa kama Dafa akaanza kunielezea kile ambacho alikuwa amefanikiwa kukipata baada kupatiwa ile nambari ya gari.



    Kama ilivyo kawaida ya wataalamu wa mambo ya kiufundi, hasa wataalamu wa teknohama, alianza kubwabwaja masuala ya kiufundi ambayo nilikuwa siyaelewi wala sihitaji kuyajua. Akanieleza kuhusu namna ‘alivyocheza’ na proggramu za kompyuta mpaka kufikia kudukua taarifa kutoka kwenye mifumo ya serikali na hatimaye kwenye kampuni inayomiliki ile taxi.



    “Did you find our guy?” nikamuuliza kwa kukereka baada ya kumuona hamalizi kubwabwaja msuala ya kiufundi aliyokuwa ananieleza.



    “easy… easy! Found him… here!!” aliongea na kunionyesha kwenye kioo cha kompyuta.



    Nikaanza kusoma kwa makini. Maelezo pale kwenye kioo cha kompyuta ambayo yalionyesha kwamba, taxi ile yenye namba za usajili ZH 45789 inamilikiwa na kampuni ya usafirishaji hapa Zurich inayoitwa Alp Limo. Baada ya maelezo hayo kulikuwa na maelezo mengine mengi mno ambayo nilikuwa siyaelewi.



    “Where is our guy.!?” Nilimuuliza kwa mshangao kwa sababu kulikuwa na maandishi mengi sana yanayofuata baada ya jina la kampuni ambalo liliambatana na ile namba ya taxi.



    “Look closer.!” Aliongea huku ananionyesha kidole kwenye kioo cha kompyuta.



    Nikatazama tena kwa makini zaidi na ndipo ambapo nikagundua kuwa maelezo yale yalikuwa kama ‘log book’… ratiba fulani hivi au kumbukumbu. Ilikuwa inaonyesha taxi gani ilikuwa inaendeshwa na dereva gani na siku ipi. Nikaangaza macho yangu kwenye jedwali ambalo lilikuwa linaonyesha nambari za taxi. Nikayapepesa kwa kushuka chini mpaka nilipoiona namba ZH 45789. Nikaangaza pembeni yake mpaka siku ya juzi na kutazama jina la dereva ambaye alikuwa anaendesha taxi hiyo…



    “Vihaan Singh!” Nilisoma pale juu ya kioo na kumtazama Dafa. “Is this our guy?” nikamuuliza.



    “That’s your guy!” alinijibu huku anabofya bofya tena kompyuta… “found his address too… here it is!”



    Nilitoa simu yangu haraka haraka na kunakili anuani ambayo ilikuwa inaonekana pale kwenye kompyuta. Anuani ilikuwa inaonyesha kwamba Vihaan Singh anaishi mtaa wa Peterstrasse karibu kabisa na Uwanja wa ndege Zurich.



    “Thank you Dafa!” Winnie alimshukuru yule jamaa huku nikimuona akimkabidhi noti kadhaa za faranga za Uswisi.



    Yule jamaa lizipokea wakaagana na kisha akuondoka. Tukabakia mimi na Winnie pekee.



    “Thank you for this Winnie!”



    “It’s ok! We are in this together..” alinijibu huku anakaa kwenye kiti.



    #452

    “I think we should get moving right now!”



    “sorry Ray I won’t be joining you today… I have an appointment with someone!”



    “A date?” nilimuuliza kwa utani lakini ajabu ni kwamba nilimuona anajiinamia chini kwa aibu fulani hivi kumaanisha kwamba kile ambacho nilikuwa nakisema kilikuwa sahihi. Nilisikia kama vile moyo wangu unawaka moto.



    “My boyfriend is going to be in town today… I have to meet him.” Winnie aliongea huku akiwa amejiinamia chini.



    Nilisikia kama kisu cha moto kimepenya moyoni. Mithiri ya kisu cha moto ambacho kinapita kwenye siagi. Mimi na Winnie hatukuwa wapenzi rasmi, lakini kulikuwa na kitu fulani katikati yetu, kitu ambacho kadiri ambavyo tulikuwa tunaepuka kukiongea ndivyo ambavyo kilikuwa kinazidi kuwa na nguvu zaidi. Moyo uliniuma niliposikia ametamka “my boyfriend”.



    “Wow! Sounds cozy.” Nikajitahidi kuongea kwa sauti iliyo kawaida lakini kigugumizi kilikuwa dhahiri kabisa katika mwambo wa sauti. “so… see you later?” nikauliza kwa mashaka kabisa nikijua kabisa jibu ambalo nitalipata.



    “No! ’ll see you tomorrow.!” Alinijubu na kuinua kichwa kuniangalia.



    “send him my regards… will keep you posted!” Niliaga na kuanza kuondoka.



    Winnie hakunijibu chochote alijiinamia tena chini, hakuinuka hata kunisindikiza. Hatukuwa wapenzi lakini dhahiri kabisa alikuwa anajisikia aibu kunieleza kuwa leo ataonana na mpenzi wake na watalala wote. Niliondoka roho ikiwa inafukuta, moyo kama vile unawake moto. Nilijisikia hasira na aibu kwa wakati mmoja. Nilisikia hasira kwa kuwa na wivu ambao ulikuwa unanijia kila ambapo nikifikiria kwamba leo hii Winnie atakuwa mikononi kwa mwanaume mwingine. Lakini wakati huo huo nilisikia aibu kwa mume wa mtu, mume wa mwanamke ananyenipenda kwa dhati kabisa kuruhusu hisia za namna hii juu ya mwanamke mwingine kukua moyoni mwangu.



    “Stay focused kichwa… stay focused!” nilijisemesha mwenyewe nikiwa napanda taxi kutoka chuoni kwa Winnie kuelekea mtaa wa pertstrasse ambako Vihaan Singh alikuwa anaishi.



    Kama dakika kumi na tano baadae taxi ilikuwa imesimama kwenye mtaa wa peterstrasse. Nikalipa na kushuka kuanza kutafuta namba ya nyumba ambayo ilikuwa kwenye anuani. Nilitembea kama dakika mbili hivi mpaka hatimaye nikaipata. Nikasogea mlangoni na kubofya kengele mlangoni. Nilibofya kengele kama mara tatu hivi ndipo niliposikia mtu akifungua mlango.



    “Hello.!” Alikuwa ni mwanaume wa kihindi mtu mzima wa makamo ya kama katikati ya miaka arobaini hivi.



    “Hello… ’m looking for Mr. Vihaan Singh!”



    “This is him… who are you?” alinijibu kwa kingereza kilichojaa lafudhi nzito ya kihindi.



    #453

    “My name is Ray, would like to ask you a few questions.” Niliongea huku mwenyewe nikihisi kabisa nilitumia sentesi ambayo haikuwa sahihi sana. Niliuliza kama mtu mwenye mamlaka fulani hivi.



    “Who are you? Police?” aliniuliza kwa woga.



    “No no no! ’m not with the police… if we can just speak for a few minutes.”



    “what is it about?” aliniuliza huku ananiangalia kwa mashaka.



    “can I come in?”



    “No you can’t! what is it about?” aliniuliza huku nikiona kabisa mashaka yakiongezeka usoni mwake.



    Nilikuwa nimefungua maongezi haya kwa sentesi ambazo hazikuwa sahihi kabisa na sasa nilikuwa nimebananishwa kwenye kona.



    “its about a passenger you drove day befor…..”



    “No no no man! I can’t share with you that kind of information unless you are with the polce.!” kAlinikatisha kabla sijamaliza kuongea na aliongea kwa hasira na kisha kufunga mlango kwa nguvu.



    Nikabaki pale nje nimeduwaa tu. Taarifa ambayo nilikuwa nahitaji anipatie ilikuwa ni kinyume na maadili ya kazi yake kabisa na mbaya zaidi nilikuwa nimemuuliza kwa urahisi rahisi kama vile naomba maji ya kunywa. Nikachakata akili haraka haraka.



    “it’s a job offer… hundred francs per hour!” niliongea kwa msamiati wa fumbo nikiamini atanielewa kabisa kwamba nataka kumpa hongo ili anipatie taarifa hiyo.



    Ulipita ukimya wa kama sekunde thelathini hivi kisha nikasikia mlango unafunguliwa tena kwa nguvu.



    “What do you want man?” aliongea kwa hasira kiasi.



    Sikutaka kuchelewesha mambo. Nikaingiza mkono mfukoni na kuhesabu faranga hamsini haraka haraka na kumkabidhi mkononi, “You get another fifty after we talk.!” Niliongea huku nimemkazia macho.



    Vihaan aligeuka kuangalia kushoto na kisha kuangalia kulia na kisha kufungua mlango niingie.



    “you guys go to your room!” Vihaan aliwaambia watoto kama watatu ambao ambao walikuwa pale sebuleni mara baada ya sisi kuingia. “have a seat!” Vihaan alinikaribisha nikae kwenye sofa pale sebuleni. “what is your name again?”



    “It’s Ray.!”



    “Which customer exactly are you talking about!” aliniuliza huku naye akikaa kwenye sofa.



    Nilielewa wazi kabisa kwamba anahudimia watu wengi kwa siku kwa hiyo nilihitaji kumueleza kwa ufasaha mno mpaka kumkumbuka ni mteja gani hasa ambaye nilikuwa namlenga. Lakini ajabu ni kwamba nilipoanza tu kumueleza kuhusu safari yake ya juzi chuo kikuu chA Zurich alimkumbuka ni nani ambaye nilikuwa namlenga.



    “You want to know where I took that guy with a black hat and a long over coat?” aliniuliza huku anatabasamu.



    “yes yes.. that guy. Wow you have a good memory!”



    “Nah not good memory! I remember that guy well because you are not the first one to ask where I took him!”



    “what? Someone else asked you about him? Who?” nilipatwa na mshituko wa ghafla kiasi kwamba kama ningekuwa nimesimama ningeliweza kudondoka. Kuna mtu kabla yangu amekuja kwa Vihaan kuuliza kuhusu yule jamaa wa kofia ya pama na koti refu jeusi. “who?” nikamuuliza tena.



    “I will do this for three hundred francs!” Vihaan aliongea huku anatabasamu kifedhuli. Alijua kuwa amenibananisha kwenye kona na kwa muda huu nilihitaji taarifa hiyo zaidi ya nilivyokuwa nahitaji oksijeni.



    Sikutaka kufikiri mara mbili. Uzuri nilikuwa nimejiandaa tangu nilipotoka hardstrasse, nilijua kuwa lazima nitahitaji fedha kumshawishi dereva taxi ili anipe taarifa hizo kitendo ambacho ni kinyume kabisa na maadili yake ya kazi.

    Nikaingiza mkono mfukoni na kutoa kibunda cha fedha. Nikahesabu faranga mia tatu na kuziweka mezani.

    http://pseudepigraphas.blogspot.com/

    “Now tell me where you took him and who is asking questions about him?”





    MWISHO WA MSIMU WA PILI



    ENDELEA KUFUATILIA MSIMU WA TATU



    MWISHO

0 comments:

Post a Comment

Blog