Simulizi : Mimi Na Rais (The President And I)
Sehemu Ya Tatu (3)
Franco-Domino-Chi ni ‘code’ ya kiusalama ya mawasiliano kati ya Macha na Meshack. Maneno yale yalimtaka Meshack afanye mambo matatu makubwa, kwanza yalimpa taarifa kuwa Macha hatafanya jambo lolote la ajabu kwa hiyo Meshack asiogope, pili abakie akiwa amejikita katika majukumu yake kwa utulivu na tatu, siri yake bado haijagundulika hivyo asihofu kwa sasa.
Watu wa usalama mara nyingi hutumia maneno machache kumaanisha kurasa nzima. Hii huwasaidia kuwasiliana ndani ya muda mfupi lakini mambo mengi. Huweza kuamua kufanya kidole kimoja kikinyooshwa basi kumaanisha mambo matatu mpaka manne.
Meshack alimwelewa Macha na kukubali. Meshack alikuwa sehemu ya mpango mkakati lakini akitumiwa na Macha kwa siri na utaalamu mkubwa. Yeye aliwekwa aje kuwa kiungo mmaliziaji lakini bahati mbaya mambo yamekwenda ndivyo sivyo hadi kufikia wakati ule.
Macha alishaelewa kuwa Meshack atakuwa katika hali mbaya hivyo alihitaji kumtia moyo na kumfanya atulie asije akashawishika kutamka lolote katika kujihami ama kujisafisha mbele ya Rais. Japo mpango mzima na wahusika wote alikuwa nao Macha na Joe tu na hata baadhi ya wahusika wenyewe hawajuani.
************************************
Baada ya Rais Sylvester Costa kupata mpango ule na kusikia zile sauti alizotumiwa na Jenerali Ernest Nduta alichanganyikiwa.
Alimwagiza mkuu wa majeshi haraka aongeze ulinzi pale Ikulu, alimkabidhi Sabinasi Paulo aongoze intelijensia ya Idara ya Usalama wa Taifa na kuhakikisha kama kuna uwezekano wa kuwajua wahusika wengine basi haraka hilo lifanyike. Kwa ufupi aliona ni kama anapinduliwa muda huo.
Rais Costa alikuwa akizungukazunguka meza ya ofisi yake huku aking’ata kucha asijue nini kinatokea. Taarifa zile zilimchanganya sana. Hupenda kusema kazi ya Urais inamchosha sana lakini wakati ule alionyesha fika ni kwa jinsi gani anapenda cheo kile na kamwe hayupo tayari kukiachia.
Alikuwa akipiga simu kila mahali na kila saa kuulizia nini wameweza kukigundua kingine. Mathalani, alitaka sana kuongea na Pius lakini jitihada zote za kumpata zilikuwa zikishindikana.
“Kimweri vijana wako wameshafanikiwa kufika uwanja wa ndege wa Shenyang?”, Rais Costa aliwasiliana na balozi Kimweri kutoka Beijing China.
“Ndiyo Mkuu, wamefika lakini kamera zimeonyesha alitoka nje ya uwanja ndio bado tunafuatilia” Kimweri alijibu.
“Fanyeni hima mniambie kijana wangu Pius yupo wapi kama mnashindwa niambieni nitapiga simu Ikulu”, Rais Costa aliongea kwa ghadhabu.
“Tunajitahidi mkuu”, Kimweri alijibu
Wakati anamalizia kuongea na simu mlango wa ofisi ya Rais Costa ulifunguliwa na alikuwa ni Meshack akimwingiza Stanley Macha.
“A traitor”(Msaliti), Rais Costa alifoka kwa hasira na kumkaribia kwa kasi Stanley Macha na kumpiga ngumi ya uso.
“Mh. Rais”, Macha alijibu kwa unyenyekevu na kujishika alipopigwa na kutulia.
Rais Costa alikuwa amefura kwa hasira.
“How did you manage to fool me all along? It has been a long time Macha, for the past 8 years I believed you were protecting me and the best interest of our nation, and you were conspiring to overthrow constitutionally, legitimate president who was elected through democratic processes? How could you? Son of a bitch”.
http://pseudepigraphas.blogspot.com/
(Uliwezajie kunidanganya kwa kipindi chote? Ni muda mrefu Macha, kwa miaka nane sasa niliamini unanilinda na kulinda maslahi ya nchi yetu, kumbe ulikuwa unakula njama za kumpindua Rais halali aliyechaguliwa kwa misingi ya katiba, aliyechaguliwa kwa michakato ya kidemokrasia? Mwanaharamu mkubwa!), Rais Costa alizidi kung’aka kwa hasira.
Hakika haikuwahi kutokea hata siku moja Rais kuonekana katika hasira ya namna ile. Ilimtisha kila mtu, hakuna aliyeongea wala kumsogelea. Macha alibaki kimya.
“Nimekukosea nini mimi? Nimekunyima kitu gani? Tell me, tell me now Macha”, Costa aliendelea kuongea huku macho yake yakiwa mekundu kama yaliyojaa damu. Hasira ilimzidi kipimo.
“Am I not doing enough for this country? Am I not delivering? then why? Why are you doing this? Then do it, am here. Do it, tell me to get out and I will leave this office and let you be if that is what you wanted. Is it not what you want?”.'
(Je sifanyi vya kutosha kwa ajili ya nchi hii? Sitekelezi? Kwanini lakini? Kwanini unafanya haya? Haya, nipindue, nipo hapa. Nipindue, niambie nitoke nje na nitaondoka nikuachie Urais huu kama ndicho utakacho. Sivyo?), Rais Costa aliongea mfululizo huku akizungukazunguka ndani ya ile ofisi.
Macha alibaki kimya akiwa ameinamisha kichwa chini.
“Mh. Rais…”
“Shut up” (Nyamaza), Costa alimkatiza Macha alietaka kuongea jambo.
“Meshack hakikisha familia ya huyu mbwa na ya Joe zote zimewekwa chini ya ulinzi popote zilipo na mtoeni huyu mbele yangu. I don’t have timen to listen to traitors. Just get him out of my sight”. (Sina muda wa kusikiliza wahaini. Mtoe machoni mwangu sasahivi), Rais Costa aliagiza kwa hasira kuu.
Vijana wawili walimshika Macha mkono ili wamwelekeze mahali wanapokwenda kumuhifadhi kwenye moja ya nyumba za siri za idara ya usalama wa taifa ambapo atakaa huko muda wote wa uchunguzi chini ya uangalizi mkali.
Meshack alipotaka kutoka tu Gideon msaidizi wa Rais aliekuwa akifuatilia kasheshe lile alitia neno.
“Meshack subiri. Mh. Rais, kitendo wanachokifanya hawa kina Joe na Macha ni kitendo cha ajabu sana, kwanza umefanya hekima sana kumsitiri mimi ningeshapiga mtu risasi”. Gideoni kama kawaida yake alianza unaa.
“Gideon, nimekasirika sana na hawa watakiona cha mtema kuni. Kama Joe nilimfanyia vile kwa miaka miwili bila kugusa roho yake akaniona mimi ni mjinga wakati huu naua mtu”, Rais Costa alijikuta anaropoka azma yake ya kumuua Macha na Joe popote atakapopatikana.
“Lakini sasa Mh Rais nilikuwa nashauri, mambo haya unajua mara nyingi hayafanywi na watu wawili ama watatu ni mnyororo mrefu na watu wa kukufanya ujue mnyororo huo ni Macha na Joe hivyo nashauri usiwapoteze mapema…….
Tunawahitaji sana. Huyu Macha aingizwe kwenye mahojiano yenye mateso makali mpaka aseme nani wanashirikiana nae. Joe nae atafutwe, najua vijana wetu hawashindwi kumpata ndani ya muda mfupi. Hata hivyo kumbuka kina Joe wametoka kwenye misheni huko Korea unahitaji kupata mrejesho. Siku mbili tatu hizi Rais Kim atataka kusikia kutoka kwako utamjibu nini?”
“Unaongea kweli Gideon lakini taarifa zote alikuwa amebeba Pius, anazo. Nitazipata”, Rais Costa alijibu kwa majigambo.
“Sawa utazipata lakini bado ninashauri familia za hawa mabwana zisiguswe kabisa. Kufanya hivyo utasababisha taharuki na watu watataka kufahamu nini kimetoka. Ninashauri jaribio hili lisijulikane kabisa, tena hata Mkuu wa Majeshi mwambie afanye siri. Wakuu wake wa vikosi wasijue maana kumbuka ni wao walitaka kukupindua kipindi cha nyuma na kina Joe na Macha wakazima lile jaribio sasa huwezi jua kuna masalia yao na wakijua utaamsha tena hisia”, Gideon aliendelea kuchangia.
Wakati wa mazungumzo yote hayo Meshack alikuwa amesimama pale akisubiria maelekezo mengine.
Rais Costa alitafakari ushauri wa Gideon na kuunga mkono japo roho ilimuuma sana kuziacha familia za Joe na Macha bila kuzipa shida.
“Meshack ziache familia zao kwanza nitakupa maelekezo baadae”, Rais Costa alimalizia na Gideon na Meshack walitoka na kumwacha Rais Costa mwenyewe.
Akiwa bado amesimama ghafla aliingia Jenerali Ernest Nduta Mkuu wa Majeshi.
“Nduta, tell me what’s going on” (Nduta niambie nini kinaendelea), Rais Costa alimpokea Nduta kwa swali.
“Mpaka sasa taarifa za kiintelijensia zinaonyesha hali ni shwari. Tumefanya full intel scan kwa miezi zaidi ya sita nyuma na hakuna mawasiliano yoyote yaliyobainisha mpango huu.
Actually, timu yangu inaendelea kukagua kama kuna mawasiliano yoyote kutoka nje na watu wa ndani ili kujua labda kuna mkono wa nje, lakini kwa sasa hali ni shwari. Nadhani ulikuwa ni mpango ambao bado ulikuwa ni mchanga sana”, Nduta alimpa taarifa fupi Rais Costa.
Wakiwa bado wanaongea ghafla simu ya Sabinasi Paulo, kijana aliyekaimishwa ukuu wa Idara ya Usalama wa Taifa baada ya Macha kuwekwa chini ya ulinzi iliingia.
“Mh Rais, tumempata Luteni Jenerali Pius” Sabinasi aliongea kwa kifupi.
“Put him through” (Muunganishe hewani), Rais Costa alitaka kuunganishwa nae.
“Mh. Rais Salamu”, Pius alisikika akiongea kwa sauti ya unyonge.
“Pius, upo salama? Pole sana kijana wangu”, Rais Costa aliongea kwa sauti ya upole na mahaba mazito kwa Pius.
Alimuona ni shujaa kuliko mashujaa wote aliowahi kuwasoma kwenye historia. Kitendo cha kuweza kumpenyezea taarifa kuwa mtu kama Macha anaemwamini anapanga mipango miovu dhidi yake kilikuwa ni msaada mkubwa kupitiliza. Alitamani hata palepale atoe amri vitabu vyote vya mitaala vya historia viwafute watu kama kina Mkwere na Njelilila wanaoonekana ni mashujaa na kumwandika Pius Kihaka.
“Nipo salama Mkuu, japo nina maumivu makali sana shingoni nadhani walinipiga na kitu kizito. Sasa nipo hapa ofisi zetu za ubalozi wananipatia huduma ya kwanza”, Pius aliongea kwa unyonge sana.
Pigo la jug-eun halikumwacha salama. Alihisi amepondwa na chuma kizito kumbe ni mkono tu.
“Pole sana. You have the package of your visit to North Korea, right?” (Una nyaraka zote zinazohusu safari yenu ya Korea Kaskazini, si kweli?) Rais Costa aliuliza kwa shauku.
“Hapana Mh Rais walichukua taarifa zote”, Pius alijibu.
“Son of a bitch! ****” (Mwanaharumu huyu), Rais Costa alitukana kwa kummaanisha Joe.
“Sabi, andaa mpango wa kuhakikisha Joe anapatikana ndani ya wiki moja akiwa hai ama amekufa. Kama kuna chochote utahitaji kwangu nikusaidie ama kuidhinisha niambie. Huyo kijana wa mawasiliano aliyekuwa akishirikiana na Macha hapo Idarani nae apelekwe ‘sehemu salama’ hata kama alikuwa akifuata maagizo ya mkuu wake, akamatwe na awekwe kizuizini haraka. Nahitaji safu nzima ya vijana wako hapa ikulu ibadilishwe na ianze kuchunguzwa haraka.
Nduta, naomba baada ya siku tatu unipe uhakika kuwa hakuna kikosi ama mkuu wako yeyote wa kikosi aliyekuwa akihusika na mpango huu. Nawategemea ninyi.” Rais Costa alitoa maagizo.
“Sawa mkuu”, wote kwa pamoja Sabinasi na Nduta waliitikia huku Nduta akiwa ameitika kwa kupiga saluti.
“Kimweri, andaa mpango Pius afanyiwe matibabu kama yatahitajika na afike Stanza haraka”, Rais Costa alimwagiza balozi Kimweri aliyekuwa kwenye simu akifuatilia mazungumzo yale.
“Sawa mkuu”, Kimweri aliitikia.
Simu ilikatwa na Nduta alitoka na Rais Costa kubaki ofisini mwenyewe. Alichukua simu na kumpigia tena Sabinasi.
“Sabi, andaa mpango Sara arudi Stanza haraka. Na safari zangu zote za kimataifa zifute mpaka hapo nitakaposema vinginevyo. Sitoki kwenda popote. Sawa?”, Rasi Costa aliagiza.
“Sawa mkuu” Sabinasi alijibu.
Sara ni mke wa Rais Costa na alitajwa na Joe kuhusika katika mpango huo. Wakati hayo yakitokea alikuwa amekwenda Ontario Canada kuhudhuria mkutano wa wiki moja wa wake wa Marais Duniani.
Rais Costa alishindwa kumvumilia arudi, alitaka arudi haraka na ahojiwe na kutaja wanaohusika kama anawafahamu. Japo alishindwa kuamini ni kwa vipi mke wake anaweza kuhusika kutaka atolewe madarakani. Alichukizwa sana.
Aliwaza sana jinsi anavyompa mke wake kila anachohitaji lakini bado anahusika katika mipango miovu dhidi yake. Alitaka afike hata siku hiyo hiyo.
Isitoshe, Rais Costa aliagiza safari zote zifutwe, hakutaka kutoka nje ya mlango wa Ikulu. Alijiona hayupo salama hata kidogo. Hakumwamini yeyote na alihisi saa na wakati wowote anapinduliwa na hivyo alitaka abaki kuhakikisha hali inakuwa shwari.
Rais Costa kichwa kilimuuma sana siku ile.
“Shit”, Costa alijikuta akitamka kwa hasira huku akipiga ukuta pale ofisini kwake alipokuwa mwenyewe.
***************************************
“Meshack, niambie hali ikoje huko”. Joe alikuwa akiongea na Meshack kwa njia ya WhatsApp call kupitia namba ambayo Meshack huitumia kwa kazi maalum tu.
“Hali ni tete mkuu, we are almost cornered. Sabinasi kapewa kitengo na wewe unamjua alivyokuwa haivi na wewe na Macha”, Meshack alijibu
“Damn it! Ila wakati nikifikiria namna ingine ya kufanya nakutegemea wewe uendelee kunipa taarifa”, Joe alimwambia Meshack
http://pseudepigraphas.blogspot.com/
“Tumebadilishwa wote, hivi ninapoongea na wewe nimepangwa nikawe afisa usalama jimbo la Kinyunyu. Yani Joe huu mpango achana nao kaka. Umeshindwa vibaya”, Meshack aliongea kwa kukata tamaa.
“****”, Joe nae alijikuta akitukana. Hakika aliwekwa pabaya. Kwa mara ya kwanza aliona kushindwa kukiwa mbele yake.
Jimbo la Kinyunyu ni moja ya majimbo yaliyopo pembezoni kabisa mwa Stanza, mpakani na nchi ya Rangaba inayosifika kwa warembo barani Afrika. Ndipo huko Sabinasi alipomtupa Meshack baada ya kupangua maafisa usalama wa pale Ikulu. Kiufupi alipangua haswa.
“Ok Meshack nitakutafuta tena”, Joe aliagana na Meshack kiunyonge.
“Una maanisha Meshack alikuwa Sehemu ya mpango”, Habibu aliekuwa akisikiliza ile simu alihoji.
“Ndiyo, ila huyu kazi yake ingekuwa mwishoni sana. Sasa ndio hivyo tena”, Joe kwa mara ya kwanza alimjibu Habibu katika hali ya kukata tamaa.
Habibu nae kwa mara ya kwanza alianza kumsikitikia Joe badala ya kujisikitikia yeye. Alimwangalia Joe katika hali ya kumwonea huruma. Aliona nia njema iliyopo ndani ya Joe lakini inayoendea kushindwa.
“Joe, you still have power brother. Una taarifa muhimu ambazo Rais Costa atazihitaji. Unaweza kuzitumia hizo kukaa nae mezani”, Habibu alimpa moyo Joe.
Yale makabrasha yote ya safari ya Korea Kaskazini alikuwa ameyashika Joe. Rais Kim alikuwa akisubiri simu ya Rais Costa kukiri kupata majibu na hivyo mambo mengine yaendelee.
Kauli ya Habibu ilimpa moyo Joe kwa kiasi fulani.
“Ni kweli Habibu”, Joe alijibu kwa tabasamu la kulazimishia. Hakutaka kumvunja moyo Habibu aliyeona ameshaanza kupata moyo.
“There is one person left untouched. If he gets caught, then I will declare this a mission impossible and surrender” (Kuna mtu mmoja tu amebaki bila kuguswa. Kama na huyu akishtukiwa na kukamatwa nitakiri rasmi mpango huu kushindwa na nitajisalimisha) Joe alimwambia Habibu huku akichukua simu yake na kufungua ‘game’ yaClash Royale.
Clash Royale ni ile ile ‘game’aliyokuwa akiitumia kuwasiliana na Macha kwa siri, na huyu anaetaka kuwasiliana nae ni mtu wa tatu mwenye ile game katika mpango ule. Wakiwa watatu tu yaani Joe, Macha na huyu anaewasiliana nae sasa ndio haswa ‘masterminds’ wa mpango huu.
“Who is that? (Nani huyo?), Habibu aliuliza kwa shauku.
“Just pray that he is still in position to carry on with the mission Habibu or else consider yourself screwed”, (We omba sana huyu jamaa bado awe kwenye nafasi nzuri ya kutusaidia kuendelea na misheni Habibu, tofauti na hapo jihesabu umekwisha) Joe alijibu kwa jibu lililotoka moyoni kabisa. Wazungu wangesema ‘a sincere reply’
******************************
?
Stanley Macha Ahojiwa. Askofu Begere Amvuruga Julius Kebwe
“Macha, mimi si mpelelezi wa shauri lako hili, lakini kwa heshima uliyokuwa nayo ndani ya vyombo vya ulinzi na usalama nimekuja mwenyewe. Nimekuja kusikia kutoka kwako mwenyewe, nataka uniambie ni nini kilikusibu, na utueleze kwa mapana ipi ilikuwa nia ya wewe na wenzako kutaka kumpindua Rais halali wa nchi yetu aliyechaguliwa kidemokrasia na kwa kufuata matakwa ya Kikatiba na anayeungwa mkono karibu na watu wote.
Mlikusudia nini na unashiriki wewe na nani? Ni vyema ukasema yote na kuwataja wenzako kabla njia nyingine hazijaanza kutumika’’, Alikuwa ni Inspekta Mabubi Majita akimhoji Stanley Macha kwa mara ya kwanza huku akimshushia na mkwara kidogo.
Stanley Macha alichukuliwa na kuwekwa ndani ya nyumba maalumu ya siri ya Idara ya Usalama wa Taifa Stanza, wenyewe wakiita‘safe house’ iliyopo karibu na fukwe za bahari katika eneo linalofahamika kama Khanama akiwa ameshikiliwa huko kwa kosa la uhaini kwa kushirikiana na Joe.
Pamoja na nyumba hii kuwa maeneo ya makazi wanapoishi matajiri na viongozi wa ngazi za juu serikalini, hakuna aliyekuwa anafahamu matumizi yake na wala hakuna aliyewahi kuitilia shaka. Hata baadhi ya viongozi wa juu wa serikali hawakuwa wanafahamu kazi yake zaidi ya maafisa usalama walioingia na kutoka mara kwa mara kwa shughuli maalumu.
Kabla ya kutumia njia za mateso, Jeshi la Polisi liliamua kujaribu mbinu za kidiplomasia kwani wanafahamu wazi ugumu wa kumfanya mwanausalama kusema lolote ambalo hataki kusema. Kuna wanausalama wengi hufa kwa mateso bila kusema hata tone la siri ambayo kwao wanaona haipaswi kumfikia mtu asiyepaswa.
Inspekta Majita alikuwa maarufu na mashuhuri sana katika kufuatilia masuala ya kiuchunguzi. Ni miongoni mwa ma afisa wa jeshi la Polisi watatu tu Stanza waliopata mafunzo nchini Pakistan, Cuba, Marekani na Israeli. Nchi zote katika nyakati tofauti.
Mathalani, Inspekta Majita ni miongoni mwa wataalamu wachache walioitwa kuunda kikosi cha kuchunguza tukio la ulipuaji wa balozi za Marekani katika nchi za Afrika ya Mashariki yaani Tanzania na Kenya mwaka 1998. Ni baada ya tukio lile Marekani ilimpa nafasi ya kwenda kuongeza ujuzi katika shirika lao la uchunguzi, Federal Bureau of Investigation maarufu kama FBI.
Inspekta Majita alikuwa ni mrefu, watoto wa mjini wangesema amepanda hewani, alipenda kufuga ndevu nyingi na kuvuta sana sigara hasa anapokuwa kwenye kazi maalumu. Alipendelea pia kuvaa shati lenye mikono mirefu na kisha kuikunja huku akivaa mkononi saa yake inayotumia mapigo ya moyo kutembea. Sauti yake ilikuwa nzito sana na yenye kukwaruza, hali hii ilichangiwa na uvutaji sana sigara uliopitiliza tangu akiwa mtoto wa miaka 16 tu.
Majita hakuwa muongeaji sana na hakuonekana mara kwa mara, hata serikalini na kwenye taasisi za kiusalama, wanausalama wenzake humuita Kakakuona, kwasababu kuonekana kwake kulikuwa kwasababu maalumu na kwa kazi maalumu tu. Alipendelea kufanya kazi bila kuonekana na watu wala vyombo vya habari.
Inspekta Majita hakuwa na magenge ya marafiki ndani au nje ya taasisi za usalama, alipendelea kuwa na mahusiano ya kikazi pekee. Tabia hii ilisababisha asioe na hakuwa na mtoto. Kwasababu hiyo hakuwa amezoeana na Stanley Macha hata kidogo japo walikuwa wakijuana na mara kadhaa Stanley Macha akiwa kama bosi wake alishawahi kumtuma kazi kadhaa na alizitekeleza vyema.
Stanley Macha anamfahamu fika inspekta Majita na uwezo wake. Leo ni zamu yake kuwekwa kitimoto.
“Majita, unajua unachofanya hapa ni kutaka kukamua maji kutoka kwenye mwamba. Hakuna mpango kama huo”, Macha alimjibu Majita wakiwa wamekaa meza ya mahojiano.
“Labda mimi ni nabii Mussa, huwezi kujua Macha. Nahitaji maji yatoke kwenye mwamba niwanyweshe wana wa Mungu. Rais Costa anahitaji majibu sasa, ukisema hakukuwa na mpango kama huo mimi siwezi kukuelewa na Rais hawezi kunielewa pia”, Majita nae alijibu kwa utaratibu huku akipuliza moshi wa sigara kutoka puani.
“Unajua nilitii na kuwa mkimya kwa sababu nilitaka kujiridhisha lakini ukweli ni kuwa mimi na Joe tulikuwa katika mpango wa kumpima Pius kama kweli yupo thabiti katika kumlinda na kumtetea Rais na Bahati nzuri matokeo ndio haya tumeona alivyo”, Macha alimjibu Majita.
“Macha stop that nonsense man. Both you and I know that is not it. Unampima mnadhimu mkuu wa Jeshi kama ana utii kwa Rais? Unampima kwa kibali cha nani? Kwanini? Kwanini umpime kwa njia hiyo?” Majita aliuliza huku akisimama na kuelekea dirishani.
“Majita zipo sababu nyingi. Kwanza ikumbukwe Pius yupo nafasi ya pili baada ya mkuu wa Majeshi na labda siku moja au siku za usoni yeye atashikilia nafasi hiyo kubwa ndani ya jeshi. Kwa kumbukumbu tu, mipango ya uasi wa jeshi miaka miwili iliyopita Pius alikuwa karibu na mkuu wa kikosi cha mizinga pamoja na anga ambao ilikuja kuthibitika kuwa ndiyo waliokuwa wapanga mipango ya kutaka jeshi liasi.
Ni mimi na Joe ndio tuliuzima mpango ule, unajua historia hiyo. Pius sasa hivi anahusika katika misheni ya kisualama ya Korea Kaskazini, yeye ndiye atakuwa akihusika sana kama kiungo ni muhimu tukajua ama kwa hakika yupo thabiti kumtetea Rais na kulitetea taifa na hana tamaa”, Macha alimalizia utetezi wake wa kuungaunga usio hata na kichwa wala miguu.
“Macha, wewe ndio ulinipendekeza kwa mara ya kwanza kwenda Cuba kusomea haya mambo. Ukanipeleka na Israel na Pakistan. Sasa leo unaponigeuza poyoyo unanikosea sana bosi wangu. I need the truth and only truth. Haya rudia tena”. Majita alimjibu Macha huku akiwa dirishani anaangalia nje. Hakuwa hata anamwangalia, alimpa kisogo. Majibu ya Macha yalimkera.
“Majita, unataka kuamini kweli kuwa mimi naweza kupanga njama za kumpindua Rais Costa? Kwasababu zipi? Ili nipate nini? Mimi nilimnusuru kwenye tukio la kwanza halafu tena leo nipange kumpindua? Come on guys mnanikosea sana. Hata Joe mnamkosea sana anafanya kazi kubwa iliyowashinda wote kwenye serikali hii”, Macha nae alijibu kwa dharau.
“Kama kweli ilikuwa ni kumpima Pius kwanini simu yako uliifanyiaHard reset? Kwanini taarifa zako za simu na za mawasiliano hazipatikani popote. Umezifuta. Faili hili hapa zimetoweka dakika tatu kabla ya kusimamishwa kwenye korido za Ikulu kwa kumtumia kijana wako Daudi.
Amefuta mpaka kwenye server za idara. Nikaagiza kufanyike hard backup nikakuta hakuna kitu. Kila kitu umefuta halafu unaniambia haukuwa mpango wenye nia mbaya? Macha ninakuheshimu, don’t push me to the corner that you would not wish for. Heshima ninayokupa itunze”, Majita aliongea kwa hasira jambo lililomshtua Macha.
“Majita, I have worked in intelligence community since I was in high school, keep that in mind. Maswali unayoniuliza hayana maana. Kuhakikisha taarifa zangu zipo salama ni kosa? Kwani hiyo si kanuni namba moja uliyofundishwa?”, Macha nae alijibu mapigo kwa kufoka.
“Sio ndani ya muda mfupi namna ile toka ujulikane mpango wako ovu” Majita alijibu.
“Kwa hiyo unasemaje”, Macha alijibu kwa hasira
“You are leaving me with no option than applying enhanced interrogation techniques on you Macha. I know both you and I do not wish for that”, Majita alijibu.
http://pseudepigraphas.blogspot.com/
“Nimeihudumia serikali hii kwa miaka 30. Nimemlinda na kumtetea Rais Costa kwa mwaka wa 12 sasa. Kama hii ndiyo gharama ya uaminifu wangu kwa Mh Rais na kwa taifa hili, basi nipo tayari kuilipa”. Macha alijibu kwa kupayuka huku Inspekta Majita akiwa anatoka nje na kutotaka kumsikiliza.
“I will show you some love and you’ll fall in love with the show. I will be back to say hello soon”, Inspekta Majita alijibu na kutupa kipisi cha sigara chini na kisha kutoka.
**********************************
??? ? ?? ?? o-eseo mwo deul-eoss ni? (Umesikia lolote kutoka kwa Joe?). Rais Kim alimuuliza Waziri En wakiwa wamesimama kibarazani kwenye jumba la Ryongsong, makazi maalum ya Rais Kim.
???, ??? ???? ???? ????? ?????? ?? ???aniyo, geudeul-i beijing-e anjeonhage dochaghaessdago hwag-indoeeossjiman geuui tag-wolham(Hapana Kamaradi, japo nilithibitishiwa kuwa walifika salama Beijing), Waziri En alijibu huku akiwa ameinamisha kichwa kidogo.
??? ?????. ??? ???? ???? ?? ??? ???? ?????? igeos-eun eosaeghabnida. koseuta daetonglyeong-eun haegmugie daehan saeng-gag-eul joh-ahaji anh-assseubnikka? (Hii ni ajabu sana, au Rais Costa hakupenda wazo letu la silaha za kinyuklia?) Rais Kim alionesha mashaka yake kwa ukimya wa serikali ya Stanza.
?? ?? ???? ???? ???.naneun geuui tag-wolham-eul hwagsinhaji moshanda. (Sina hakika Kamaradi), Waziri En alijibu kiufupi.
??? ????? . Joe? ??? ??? ??? ???? ?? ????. geugeos-eul chaj-eusibsio. Joewa non-uihan naeyong-i yeojeonhi yuhyohanji algo sipseubnida. (Fuatilia na uje unihakikishie kuwa tuliyoyaongea na kuyapanga na Joe yapo katika mchakato au kuna mabadiliko yoyote), Rais Kim alimalizia.
Waziri En aliondoka.
******************************
Toka siku ile Waziri wa Sheria na Masuala ya Bunge bwana Kinyamagoha afukuzwe na Rais kwa sababu ya kushindwa kusukuma kwa nguvu muswada uingie bungeni wa kubadili umri wa mtu kugongea u Rais kutoka miaka 40 mpaka 55, hakuwahi hakuonekana hadharani tena.
Alitoka pale na moja kwa moja alielekea kijijini kwao Kwamchae ili kwenda kufanyiwa “maarifa”. Kama kuna mtu dunia hii aliamini uchawi na uganga basi Kinyamagoha aliongoza.
Aliamini misukosuko ile ni kwasababu mwaka huu hakuwa ametoa kafara. Kafara ya Kinyamagoha ilihusisha watoto wachanga wasiozidi umri wa siku moja. Kinyamagoha akishirikiana na baadhi ya manesi anaowalipa pesa nyingi aliua watoto hasa wakati mama anapokuwa anajifungua. Wakati ule huhakikisha kwa namna yoyote hata kwa kumziba mtoto asipumue ama vinginevyo basi huua mtoto kama sehemu ya hitaji la waganga wake.
Baada ya kuua na mama aliejifungua kuambiwa na kuhuzunika nesi hujifanya anaenda kumsafisha ili wamfunge kwa mazishi lakini kabla ya humchanja yule mtoto na kutoa damu kiasi ambayo kuikinga na kupelekwa kwa Kinyamagoha kisha kuipekea kwa mganga.
Iikuwa ni ngumu kuamini hasa kutokana na tabia ya Kinyamagoha kupenda kuandaa makongamano ya dini akihusisha maaskofu ama mashehe. Tena mara kadhaa utamuona akiwa misikiti mbalimbali akishiriki swala ya Ijumaa ama kusaidia vituo vya watoto wasiojiweza.
Kinyamagoha alikuwa fisi ndani ya ngozi ya kondoo. Lakini pia, Kinyamagoha alikuwa ni kama alama ya wanasiasa walio wengi na hata wanajamii walio wengi kwa ujumla. Wengi walikuwa na dini zao lakini hawakuacha kushiriki masuala ya kishirikina au vinginevyo, kama si ya kishirikina basi waliendelea kutekeleza dini zao za asili, maarufu kama dini za Kiafrika zinazohusisha uganga na matambiko ya aina mbalimbali
********************************
“Tunamshuru sana Mh. Rais na serikali yake kwa kukubali kutoa kibali cha Ujenzi wa hospitali kubwa kule Kilungululu. Hii siyo tu inaonyesha nia njema ya Rais katika kuunga mkono jitihada za kanisa, lakini pia nia yake njema ya kutaka wananchi wa Stanza wapate huduma bora za afya.
Ni rai yangu basi waamini wenzangu kumuunga mkono Mh. Rais hata katika mambo mengine anayoyafanya ambayo ni tija kwa taifa letu. Hii tabia ya kumzodoa, kumkatisha tamaa na kumtusi tuiache, haisaidii wala haijengi.
Wapo wanaosema hafuati sheria wala katiba, tena haheshimu utawala bora. Mimi nasema Roma haijajengwa kwa siku moja, tutafika huko. Sasa hivi sio muda wa kufanya siasa, ni muda muafaka sasa wengine wote tuweke mikoba yetu na ya vyama vyetu chini tushirikiane na tuunge mkono juhudi njema za Mh Rais anazofanya kwa maslahi ya taifa letu. Hata nafsi tatu za Mungu hutenda kazi pamoja, kama kila moja ingekuwa ina kazi ya kumkosoa mwenzake basi hata leo tungekuwa hatujakombolewa”, Askofu Damian Begere aliendelea.
Ilikuwa ni siku ya Jumapili akiwa katika ibada ya kiaskofu akitoa mahubiri yake kikanisa huitwahomilia. Hakuna aliyeamini kama kweli maneno yale anayatamka Askofu Begere. Watu kanisani walikuwa wakinong’onezana sana wakiulizana kulikoni. Hakuna aliyemzoea askofu Begere na mahubiri ya mtindo ule yenye sifa kedekede kwa Rais Costa. Waswahili husema usilolijua ni sawa usiku wa giza.
Kama ilivyo ada, baada ya ibada ya misa Askofu hutoka nje ya saktestia(chumba maalumu cha Padri au Askofu kujiandaa kabla na baada ya ibada) na kisha kusalimiana na baadhi ya watu na kuongea nao mawili matatu.
Julius Kebwe, kiongozi mkuu wa siasa za upinzani nchini Stanza alienda kumsalimu Muhashamu baba Askofu Damiani Begere.
“Tumsifu Yesu Kristu baba Askofu”, Julius alisalimia huku akibusu pete ya askofu.
“Milele amina Julius. Haujambo?” Askofu Begere aliitikia huku akitabasamu.
Askofu Begere na Julius ni marafiki wakubwa. Urafiki wao ulianza tangu Julius akiwa kiongozi wa chama cha kitume cha wanafunzi wakatoliki mashuleni kijulikanacho kamaSYCMS (Stanza Catholic Movement for Students). Ni kutokea huko askofu Begere alimkuza Julius tena akitaka amfanye aingie seminari na kuwa padri lakini Julius alikataa.
Baada ya Julius kuingia kwenye siasa, askofu Begere amekuwa msaada mkubwa sana katika kumtia moyo na kumpa ushujaa na kumtaka kutoogopa kusimamia anayoamini ila tu iwe haki na kweli. Askofu Begere ni mtoa hamasa mkuu kwa Julius.
“Baba leo umeniacha njiani. Sijakuona kabisa”, Julius alianza kumtania askofu Begere.
“Siku zetu zinakaribia kwisha Juli”, Askofu Begere nae alijibu kiujanja kwani alijua Julius anamaanisha na kulenga nini.
“Lakini siku zikikaribia kwisha si ndo mnatakiwa wazee mtuachie wosia?” Julius nae alidodosa harakaharaka.
“Sometimes, you need to compromise for a greater cause”, askofu Begere alijibu kiutu uzima.
“Should I compromise as well?”, Julius nae alihoji.
“Njoo nyumbani tuzungumze Julius”, Askofu Begere alimwalika Julius kwenye makazi yake.
Julius alitabasamu na kumuhakikishia askofu kuwa ataenda kuonana nae kesho yake siku ya Jumatatu. Maswali ya Julius yalimwingia Askofu Begere na hakika aliona alichoongea kinajifunga sana na uhalisia wake na uhalisia wa mambo pia. Ila angefanyaje?
Anataka aonane na Julius.
*************************************
Joe alimwita Habibu asogee karibu na simu yake ili aweze kusoma mazungumzo watakayokuwa wanaandikiana Joe na huyo mtu mwingine kupitia game ya Clash Royale.
“Hii application inaitwaje Joe?”, Habibu alipoona tu kwanza aliuliza.
“Mapema kwa sasa wewe kufahamu ila subiri tuone kama atajibu kwanza”, Joe alimjibu Habibu huku akiwa ameandika salamu akisubiria jibu.
“Na huyu unayewasiliana nae ndio anaitwa Saddam Hussein?”, Habibu alihoji kwa mshangao.
“Hapana. Hilo ni jina analotumia huku”, Joe alijibu na ghafla ile salamu yake ilijibiwa.
“Aisee nimekwama na sijui naanzia wapi. Nimeambiwa Meshack nae kashapigwa pini, vipi Tigerwamempeleka wapi?” Joe aliandika kwenye ujumbe.
http://pseudepigraphas.blogspot.com/
“Tiger yupo kama sio nyumba namba 3 basi ni wamempeleka red square”. Yule mtu alieandikwa kama Sadam Hussein alimjibu Joe kwa ujumbe.
Muda wote huo Habibu nae alikuwa akifuatilia mawasiliano yale akiwa ameachwa njiapanda asijue Joe anaongea na nani ila alijua nyumba namba 3 na red square ni kati ya nyumba za siri za Idara ya Usalama wa Taifa Stanza, kizungu wanaziitasecret detention facilities au kama zinatumika kwa kuhifadhi mtu kwa ajili ya usalama wake huitwa ‘safe houses.’
Alijaribu kuuliza Tiger ndio nani lakini Joe alimwambia atamwambia asijali.
“Kwa hivyo haujapata kujua chochote kinachoendelea kwa Tiger?”, Joe alihoji.
“Ndio, si unajua Sabinasi ndio sasa kapewa kitengo? Anajiona yeye niIgor Kostyukovu, pumbavu sana. Taarifa anazificha balaa”, Yule mtu alieandikwa kama Saddam Hussein alijibu.
Igor Kostyukovu ndio mkuu wa Idara ya Inteligensia ya Taifa la Urusi. Mmoja kati ya jasusi nguli duniani.
“Hakikisha familia yangu haiguswi Saddam. Wewe sasa ndiye uliebakia kunisaidia kumalizia kugurudumu hili. Nimeshapoteza mengi na siwezi kurudi nyuma maana haitosaidia tena. This time around ni mimi ama yeye.” Joe aliandika.
“Sawa Che, lakini huoni kama hakuna namna nyingine? Kwanza nakuomba mwache Habibu arudi. Hakuna sababu ya kumuharibia maisha huyo kinda”, Yule aliyejiita Sadam aliandika.
Joe alimwangalia Habibu aliekuwa akisoma kila kitu. Habibu alipoona ameangaliwa alitikisa kichwa kuashiria kuwa hataki kurudi na anataka awe pamoja na Joe.
“Una hakika Habibu”, Joe alimuuliza.
“Ndiyo”, Habibu alijibu na kupeleka macho kwenye simu ya Joe ili aone maongezi yataendeleaje?
“Habibu hayupo tayari kurudi Stanza.Ameamua kuendelea na mkakati huu”. Joe alimuandikia Saddam.
“Che, nitakurudia baadae kidogo” Saddam aliandika na kutoka hewani.
“Tiger na Che ndio kina nani?”, Habibu alihoji baada ya kuona la Sadam Hussein hajibiwi.
“Tiger ni Stanley Macha na Che Guevara ni mimi”, Joe alimjibu kiufupi.
“Na huyo Sadam Hussein je?” Habibu aliuliza kwa hamu kubwa.
“Sadam Hussein ni Gideon”, Joe alijibu na kumwacha Habibu hoi asiamini alichosikia.
*******************************
Gideon Kalumanzila, mshauri wa karibu na kipenzi cha Rais Sylvester Costa na Joseph Kaduma ni marafiki wa siku nyingi. Urafiki wao haukuwa ukifahamika sana miongoni mwa wengi katika serikali ya Rais Costa. Hii ilitokana na ukweli kwamba ni watu waliokuwa wakisukuma agenda nyingi nyuma ya pazia katika serikali ya Stanza hivyo waliafiki kutokuweka wazi urafiki wao.
Ilikuwa ni ngumu kufatilia uhusiano wao na kujua umeanzia wapi maana kwenye rekodi zao hakuna mahali inaonekana kufahamiana kwa namna yoyote ile. Kuanzia makabila yao, shule walizosoma, vyuo na nchi walizowahi kuishi hakuna mahusiano hata kidogo. Ni hali hii iliwapa nafasi nzuri sana ya kusukuma mambo serikalini na mtu asijue kabisa kama ni nguvu ya pamoja.
Si hivyo tu, hata mitazamo yao mbele ya viongozi wenzao wa Stanza ilitofautiana sana. Yeye Gideoni alionekana kama mtu mwenye kuunga mkono kila haja ya Rais Costa wakati Joe yeye huhoji kila suala na wakati mwingine kupingana na Rais Costa.
Si mara moja wala mbili Gideon alionekana kumchongea Joe kwa Rais Costa ili achukuliwe hatua za kinidhamu katika masuala mbalimbali. Ni yeye aliyeshauri na kushupalia haswa Joe avuliwe ubalozi na kupewa kesi ya uhujumu uchumi iliyomtesa kwa miaka miwili. Jambo hili lilifanyika kwa umaridadi mkubwa ili Gideon azidi kuwekwa karibu na Rais Costa.
Kwa macho ya nje, Gideon alifanikiwa sana kujitenga na Joe na hakika kama tungekuwa kwenye medani za kishushushu basi Gideon alifuzu viwango vyote vya kuitwaundercover agent. Joe alihakikisha Gideon hagunduliki hata kwa thumni na hilo walifanikiwa sana.
Watu hawa walijuana vipi?
Ilikuwa ni katika miaka ya 1991 wakati Joe akichukua shahada ya Uzamili katika Diplomasia ya Kimataifa kutoka chuu kikuu chaWarwick huko Uingereza na Gideon akichukua shahada ya Uzamili katika Sayansi ya Siasa kutoka chuu kikuu cha Melbourne huko Australia walipokutana katika fainali za kombe la dunia la mchezo wa Rugbyzilizofanyika Ufaransa.
Gideon akiwa miongoni mwa waliounda kikosi cha timu ya Australia yeye Joe alikuwa ni mmoja wa kamati ya ufundi kwenye timu ya Uingereza. Ni katika mechi ile ambayo Australia waliibuka mabingwa wa dunia kwenye mchezo wa Rugby na kwa shauku kubwa Joe alipenda kujua muafrika mmoja tu aliyekuwa akiunda timu ile iliyoibuka na ushindi alitokea wapi.
Joe, alishangaa alipojua kuwa Gideon ni Mstanza. Gideon alikuwa ni Mstanza pekee labda mpaka nyakati hizi aliewahi kushiriki kombe la dunia la mchezo wa Rugby na timu yao kuibuka kidedea.
Ni baada ya mechi ile Joe aliongea na Gideon na kuanzisha mahusiano ya kirafiki. Japo hawakuwa wakiwasiliana mara kwa mara lakini mahusiano yao yalidumu. Ni Joe alieanza kurudi Stanza na kuingia serikalini. Baada ya miaka mitano Joe akiwa kwenye mkutano wa kimataifa Brusells Ubelgiji alikutana na Gideon kwenye moja ya migahawa ambapo wakati huo Gideo alikuwa Ubelgiji akifanya tafiti.
Joe aliongea kwa kirefu sana na Gideon juu ya siasa za Stanza na ni hapo Joe alivutiwa sana na mitazamo ya Gideon juu ya maendeleo ya nchi za kiAfrica. Alimsihi Gideon arudi Stanza na angefanya kila jitihada kumfanya awe mshauri wa Rais kwani aliona kabisa mawazo yake yangeisaidia Stanza kwa namna nyingi.
Gideon alirudi Stanza na kuteuliwa kuwa mshauri mdogo wa Rais Costa katika masuala ya kimataifa kwa ushawishi wa Joe. Wakati huo urafiki kati ya Rais Costa na Joe ulikuwa katika viwango vya hali ya juu labda kuliko mtu yeyote katika serikali ya Rais Costa.
Mienendo ya siasa na uendeshwaji wa nchi ya Stanza vilimchosha sana Gideon. Aliona ni bora arudi zake ughaibuni akaendelee na mambo yake kuliko kukaa kwenye nchi ambayo ushauri wa kitaalamu unaonekana ni takataka na badala yake umbea ndio unathaminiwa.
Joe alimsihi Gideon kuwa hapaswi kuondoka badala yake yafaa abaki ili wasaidiane kurekebisha hali ya utawala nchini Stanza. Ni hapo ndipo walipokubaliana namna bora ya kufanya.
Wakati wakiwa katika mpango ule ndipo Rais Costa alipoanzisha mpango wa yeye kuendelea kubaki madarakani kwa muhula wa tatu kwa kupeleka marekebisho ya katiba bungeni. Joe alipingana nae na kusababisha chuki dhidi yake na Rais Costa.
Joe alimsisitiza Gideon hata katika hali ile asiache kuwa karibu na Rais Costa na kuhakikisha analinda urafiki na ukaribu wake na Rais hata hapo muda muafaka utakapofika. Gideon alifanikiwa sana katika hilo na hakika kama kuna watu Rais Costa anawahusudu basi Gideon ni nambari moja.
Ni Gideon na Stanley Macha waliohakikisha wanamrudisha Joe kwenye picha na kumfanya aongoze ujumbe kule Korea Kaskazini. Baada ya yote kutokea ni yeye Gideon amebakia kama kimbilio la mwisho na mtu pekee anaeweza kuifanya misheni hii ya kumtoa Rais Costa madarakani ikamilike ama ishindikane. Gideon Kalumanzila, macho yote ya Joe, Habibu na Stanley Macha yanamwangalia yeye.
***********************************
Joe na Habibu waliendelea kubaki katika ardhi ya China. Walichagua kupumzika katika mgahawa waShenang, uliojengwa pembezoni mwa mto Chachiu ambao una vivutio vingi ikiwemo aina mbalimbali za ndege na maua.
Pamoja na kuwa katika msukumo mkubwa wa kiakili kufikiria ni hatua gani wangefuata baada ya mpango wa awali kukwama, Joe na Habibu waliamua kupumzika katika eneo hilo kusafisha akili zao na kupata mawazo mapya.
Wakati wakiendelea na tafakuri na kupata chakula cha mchana, Joe alisikia milio miwili tofauti katika simu yake kuashiria kuingia kwa jumbe mbili kwa mifumo miwili tofauti jambo lililomshtua kidogo.
Kupitia program ya Clash Royale, alipokea ujumbe kutoka kwa Gideon ulioandikwa kwa kifupi tu ‘’I have got an idea, let the movie begin. The plan B is taking off’’. Gideon alikuwa amemrudia Joe kama alivyomuahidi hapo awali.
Wakati Joe akiendelea kutafakari ujumbe wa Gideon, alikumbuka kuwa kuna ujumbe mwingine uliingia katika simu yake. Alipangusa kioo cha simu yake kwa kushusha chini na aliona ujumbe kutoka kwa Waziri En ukimuuliza ni nini kinaendelea na kwanini hawajasikia kutoka Stanza tangu waondoke Korea Kaskazini.
Ujumbe wa Waziri En ulitumwa kwa njia mahsusi, ni simu ya Joe peke yake iliwezeshwa kwa codesmaalumu ambazo ingeweza kupokea ujumbe akiwa sehemu yoyote duniani bila kujali kuwa ana mtandao au hana, hata kama amezima simu yake. Ujumbe ungekuja na mhuhusika akishausoma, basi ungetoweka katika simu yake. Ili aweze kujibu, ingempasa abofye namba maalumu alizopewa na kujibu kisha ujumbe wake ungefutika pia na kutoacha aina yoyote ya hustoria kuwa watu wao walishawasiliana.
Joe alikuwa na jumbe mbili za kujibu kutoka watu wawili muhimu katika kuleta matumaini mapya ya mkakati wa kuleta mabadiliko ya kiutawala nchini Stanza.
********************************
imkakati
Ujumbe wa Gideon ulimfariji Joe, hakika aliona yupo na mshirika
mwaminifu na mwanamkakati wa dhati. Ujumbe aliousoma kwa Waziri
En ndio uliomtia wazimu kidogo.
“Comrade, what is the progress? We haven’t heard from you for some
days now. Is President Costa not happy with our agreement?”
(Kamaradi, maendeleo yakoje? Hatujasikia chochote kutoka kwako kwa
siku kadhaa sasa au Rais Costa hakua?ikiana na makubaliano yetu?”
Ujumbe wa Waziri En uliuliza.
Ujumbe ule ulimchanganya kichwa Joe kwa sababu jibu atakalolitoa
hapo litaamua swali au hatua itakayofuata kwa Korea Kaskazini.
Alijua akisema mambo yapo sawa wakati hayapo sawa ingeleta shida.
Lakini akisema hayapo sawa ingezua maswali kwa En na hakuwa tayari
kwa hilo kujulikana kwa sasa. Aliwaza sana lakini mwisho alipata cha
kueleza. Aliwaza kuwa dawa ya moto ni kuumwagia maji na sio
kuwasha moto mwingine. Aliwaza, kama Pius aliamua kuwasaliti basi
acha ammalize kabisa kabisa kwenye sura ya Korea Kaskazini.
Alijua kwa vyovyote Rais Costa angemtumia Pius kuendelea na misheni
na yeye angekuwa hana maana tena hata kama akifa, wazungu
wanasema ‘He will be of no relevance’. Alijua hakuna kitu kibaya kwenye
maisha kama kupoteza thamani ya uwepo wako mahali fulani kwa
sababu utatemwa au wazungu wanasema ‘you will be rejected’.
Alifahamu hata ndoa huvunjika baada ya mwanandoa mmoja kupoteza
thamani mbele ya mwenzake, mtu hufukuzwa kazi baada ya kupoteza
thamani yake kwenye kampuni/shirika/o?isi hiyo n.k
Joe hakukubali thamani yake kwenye serikali ya Stanza ipotezwe
kirahisi. Alijua ku ‘deal’ na matukio ya namna hiyo.
“Comrade, things are not ?ine. Pius has informed the president that I
have a secret mission with you that’s why we have agreed the
involvement of nucler weapons in our agreements. Now I am under the
extreme hunt together with Habibu to be terminated. This is the reason
why you don’t hear from me neither from the President”
(Kamaradi, mambo hayapo sawa. Pius amemtaarifu Rais kuwa nina
mpango wa siri na ninyi na ndio maana tumekubaliana nanyi juu ya
mpango wa silaha za kinyuklia. Sasa hivi nipo kwenye msako mkali ili
niuawe mimi na Habibu. Hii ndio sababu kwanini husikii lolote kutoka
kwangu wala kwa Rais). Joe alimjibu Waziri En.
“This is ridiculous, how could the soldier of the higher rank like Pius
behave like that? So you haven’t even arrived in Stanza?” (Hili jambo
linanishangaza sana, inawezekanaje askari wa cheo cha juu kama Pius
afanye mambo kama hayo? Kwa hiyo bado huja?ika Stanza?) Waziri En
aliuliza kwa shangao.
“He has surprised all of us. Yes, We are still in Beijing” (Ametushangaza
wote. Ndio bado tupo Beijing) Joe alijibu.
“Africa has never stop to amaze us. So where are you and how can we
help you because you remember what we discussed?” (Africa haijawahi
kuacha kutushangaza. Kwa hiyo upo wapi na tukusaidieje kwa sababu
unakumbuka lile suala tulilojadili?) Waziri En alimuliza Joe.
Joe alianza kumwandikia Waziri En yote anayoona yanafaa ili
kuhakikisha yupo salama na misheni yake inaendelea. Mambo mengi En
alipingana nayo kwani kwa hakika yalikuwa yanaingilia uhuru na
utawala wa Stanza (Sovereignity interference). Waziri En alijua kwa
kufanya yale Joe aliyokuwa anamuomba angeibua hisia kubwa kwa
mataifa ya magharibi na ungekuwa ni uchokozi wa bayana kabisa
ambao ungekosa utetezi.
Waziri En alimwambia Joe asijali, kwanza atamtaarifu Rais Kim
kilichotokea na kisha atamrudia kumweleza nini wame?ikiria wanaweza
kusaidia. Waziri En alikuwa makini sana katika kila jambo alilopewa
kulisimamia na serikali yake ya Korea Kaskazini.
*******************************http://pseudepigraphas.blogspot.com/
“Mh. Rais umeona watu wanavyopiga kelele huko nje baada ya lile suala
la kodi kuanza kufanyiwa kazi?”, Gideon alikuwa akiongea na Rais Costa
asubuhi o?isini kwake ambapo Rais Costa hupenda kupitia kila nyaraka
anayoikuta mezani kwake asubuhi, huo ukiwa ni utaratibu wake.
Gideon alikuwa akimkumbusha Rais juu ya ule mpango aliowahi
kumshauri wa kuhakikisha anaweka kodi koro?i kwa wafanyabiashara
wa Stanza kwa kisingizio cha kuongeza mapato lakini hakika zikiwa
zinawatesa wananchi na kuua mitaji yao ya biashara. Agizo hilo lilikuwa
lipo katika utekelezaji na wananchi walikuwa wakilalamika na
kunyanyaswa sana na mamlaka ya makusanyo ya taifa wakishirikiana
na askari polisi pamoja na mgambo.
“Gideon, hizi kelele zimekuwa nyingi mpaka zinaanza kunipa hofu.
Ninataka bunge lipitishe muswada wa kutaka kubadili umri wa mtu
kugombea Urais ambapo tunauongeza, muswada huu utaleta kelele
nyingi kutoka kwa wapinzani sasa nahitaji wananchi wawe na amani na
mimi ili watu wangu watakapokuwa wanautetea wananchi waunge
mkono. Sasa, hili wazo lako naona linanichonganisha na wananchi tu
bila sababu”, Rais Costa alijibu huku akimalizia kusoma moja ya barua
alizozikuta pale mezani kwake ambayo aliiona haina maana akaiweka
kando.
“Mh. Rais, yani katika jambo litakupa ‘kiki’ ni hili, utakuja kunishukuru
baadaye. Wakati muswada ukiendelea kuandaliwa na huku tukisubiri
kipindi cha bunge kuanza ndio wakati huu wananchi watasumbuliwa
sana na watu wa Mamlaka ya Mapato na Makusanyo. Nimeona kila
halmashauri ya jimbo inawatumia mgambo kufanikisha makusanyo na
mgambo hawa wananyanyasa watu sana na kuzidisha chuki na hasira
kwa serikali na kwako.
Sasa hali hii iache iendelee na ikiwezekana kwenye mawasiliano yako
na wakuu wa mamlaka na wakuu wa mikoa na wilaya wasisitize kuwa
bado hujaona wakifanya jitihada vya kutosha ili wakazidi kutesa watu.
Sasa kipindi cha bunge kikianza tu ambapo muswada wako ndio
utajadiliwa wapinzani najua wataibuka na hoja nzito sana sasa wewe
ndio unatokea pale kuwavuruga kwa kusitisha kila aina ya manyanyaso
yanayoendelea kwa wafanya biashara juu ya ukusanyaji kodi. Tena ili
kuwamaliza kabisa toa tamko la kufuta mgambo wote kwenye miji yote.
Nakuhakikishia, ukifanya hivi utabadili upepo na muswada utapita bila
hata wananchi kuelewa na utapendwa kuliko ulivyowahi kupendwa.
Yani kwa ufupi ni kuwa, wakati wapinzani wakiwa na hoja ya muswada
wa umri wa kugombea uRais wewe unaibuka na suala la kutatua kero
za wananchi. Unakuwa ‘busy’ kupambana na hili suala la kodi koro?i na
hivyo umakini wote wa wananchi unahamia kwako kama mkombozi
wao. Wakati wanagutuka tayari muswada umeshapita, na hapo
unakuwa umeua ndege wawili kwa jiwe moja. Kwanza umeongeza
mapenzi kwa wananchi na pili muswada wako umepita bila kelele.
Wapinzani utakuwa umewapiga kile tunaita ‘Bao la kisigino” Gideon
aliendelea ‘kumjaza upepo’ Rais Costa
“Hujawahi kuacha kunishangaza Gidi. Ha ha ha! Leo ndiyo nimekuelewa
vizuri, hasa hiyo ‘timing’ ulivyoiweka”, Rais Costa alionekana
kufurahishwa sana.
“Ndiyo kazi yangu Mh. Rais, kukushauri”. Gideon alijibu kwa nidhamu.
“Kha! Huyu kijana ameipata wapi hii ‘issue’ ya mimi kununua kisiwa cha
kitalii huko U?ilipino?”. Rais Costa alionekana kuuliza kwa kushangaa na
hasira mara baada ya kusoma gazeti la kiingereza la STANZA TODAY
lililomnukuu Julius Kibwe akisema amepata Ushahidi kuwa Rais
Sylvester Costa anamiliki moja ya visiwa vya kitalii huko nchini
U?ilipino.
“Kwani ni kweli mkuu habari hizi?”, Gideon alihoji.
“Hilo ni swali gani Gideon? Kuna kosa gani mimi kuwapa maendeleo
wananchi na mimi kujipa maendeleo?”, Rais Costa alijibu kiutu uzima.
Gideon aligutuka kuwa kuzidi kuuliza ni kukoro?ishana na Mh. Rais na
hilo si jambo lililompeleka o?isini asubuhi ile.
“Mh. Rais huyu kijana yafaa adhibitiwe mapema na ninakumbuka mara
ya mwisho ulisema ungeongea na Macha na Waziri wa Polisi walifanyie
kazi, wali?ikia wapi?”, Gideon alidodosa.
“Macha ndiye aliyesema angemdhibiti sasa ndiyo huyohuyo tena
mhaini. Hauwezi kuwaaamini binadamu, hata kama ni ndugu zako wa
damu. Nadhani nitamwambia Waziri wa Polisi aendelee na mpango
wake”, Rais Costa alijibu huku akikazana kuisoma ile habari.
Kwa kawaida kila siku Rais huwa na kikao kidogo asubuhi ili kuelezwa
kwa ufupi mambo yote yanayoendelea kwenye habari na mitandaoni,
wananchi wanazungumza nini na kadhalika. Akiwa hapo o?isini wakati
ule alikuwa akisubiriwa ili apewe taarifa kwa kina juu ya ile habari
aliyoisoma kwenye gazeti.
“Mh. Rais ulipomtaja Macha umenikumbusha jambo, mahojiano naye
yame?ikia wapi, yamevuna taarifa gani muhimu?”, Gideon aliuliza.
“Macha hataki kuongea, anadai kuwa hakukuwa na jaribio lolote la
mapinduzi. Nimemwagiza Majita amtese hadi aseme mpango wote, na
kama kufa afe tu, sitaki upumbavu. Joe nae nimeshatoa amri popote
atakapoonekana auawe. Sitaki hata kuona sura yake katika maisha
yangu”. Rais Costa alionekana kutibuliwa hasira na Gideon mara baada
ya kuulizwa habari juu ya Macha.
Gideon aliposikia Macha yupo chini ya Inspekta Majita roho ilimruka.
Anamfahamu Majita kwa uhodari wake wa kuua watu katika mateso,
hana mzaha. Suala la Rais kutoa amri ya Joe kuuawa popote
atakapopatikana lilimshtua pia. Alifahamu kuwa makachero wa Stanza
walishawahi kutumwa katika misheni mbalimbali duniani na kuua
maadui wa Rais Costa tena kwa kutumia njia ambayo haiachi alama
yoyote kuwa ni tukio la mauaji.
Gideon aliona amefanikiwa suala moja la kuhakikisha familia za Joe na
Macha hazibughudhiwi, lakini taarifa aliyoisikia kwa Mh Rais kuwa
ameagiza wauawe ilimpa mshtuko mkubwa. Alijiona kabisa ana haki ya
kuwasaidia wenzake katika misheni. Isitoshe suala la Rais Costa
kumiliki kisiwa U?ilipino nalo lilimuacha mdomo wazi.
Alianza kuunganisha nukta kwa kujiuliza kumbe ndio maana Rais huwa
ana fedha za holela tu bila hata kujua anazipata wapi na wala
kutokuwapo kwenye utaratibu wa kawaida wa bajeti. Kwa mara ya
kwanza alijua huko anapozipata hizo za kugawa ndio huko huko
huchota za kwenda kununulia visiwa vya kitalii nchi za ughaibuni.
Kwasababu yeye huambatana na Rais Costa katika ziara zake nchini
Stanza, pia alikumbuka kuwa Rais hugawa mamilioni ya fedha kila
anapojisikia akiwa kwenye mikutano ya hadhara.
Alikumbuka pia taarifa ya Mwanamahesabu wa Serikali zilizotolewa
miaka mitatu iliyopita na kuonesha kuwa kuna fedha nyingi zilitumika
katika miradi hewa na matumizi yake hayakufuata sheria wala
utaratibu. Ali?ikiria masuala mengi, lakini pia alijifunza kuwa ukiwa
kwenye nafasi ya mamlaka ya juu unaweza kufanya jambo lolote bila
yeyote kukuuliza.
“Mh. Rais, nina?ikiri inawezekana nikasaidia katika kupata taarifa
kutoka kwa Macha. Kama hutojali na inawezekana, ningependa
kufahamu ni wapi Macha ameshikiliwa na mkaniruhusu nizungumze
nae katika njia Ra?iki, pengine anaweza akanipa ushirikiano Zaidi ya
hapa na kunieleza kiundani zaidi”, Gideon aliomba.
“Sijui wapi wamempeleka ila Sabinasi atakuja asubuhi hii nitamwambia
akupe ‘clearance’ ya kwenda kuongea nae”. Rais Costa alijibu huku
akisimama ili watoke aelekee kwenye kikao cha kupata taarifa za
habari, wao hukiita Media Brie?ing.
Wakiwa ndio wanataka kutoka mara aliingia Sabinasi Paulo, Mkuu mpya
wa Idara ya Usalama Wa Taifa Stanza aliepewa nafasi hiyo mara tu
baada ya Stanley Macha kuwekwa chini ya Ulinzi.
“Mkuu, nimeleta ile orodha ningeomba unisaidie kuidhinisha”, Sabinasi
aliongea kwa ufupi.
Haraka Rais Costa alipokea ile karatasi na kuiweka mezani na kupitisha
macho kwa haraka. Ilikuwa na majina kama ya watu watano hivi na
chini kuna Sehemu ya Rais kuweka sahihi na yeye Sabinasi.
Gideon alikuwa amesimama kwa mbali kidogo hivyo alishindwa
kuisoma vizuri lakini alifanikiwa kusoma maneno ya juu yaliyoandikwa
‘Order to kill’ yenye maana Amri Ya Kuua. Halafu kwa sababu Rais
aliweka mkono juu ya ile karatasi hakuweza kusoma majina yote lakini
alifanikiwa kusoma jina moja la mwisho lililosomeka Sylvanus Majura.
Rais Costa alimaliza kusaini na kumpa Sabinasi na kisha kumwagiza
Sabinus ampeleke Gideon kwenye nyumba walipomuhifadhi Macha.
Baada ya Rais Costa kutoka kwanza kama utaratibu ulivyo, Gideon na
Sabinasi nao walitoka. Sabinasi alimwambia Gideon asubiri palepale
Ikulu na kuwa gari maalumu lingekuja kumchukua na kumpeleka
kuonana na Macha. Gideon alia?iki.
**********************************
Sara, mke wa Rais Costa alikuwa kwenye sintofahamu kubwa
alipotaari?iwa kuwa anatakiwa kurudi Stanza haraka. Alimuuliza
msaidizi wake ambaye ni Sehemu ya Usalama wa Taifa Stanza kama
kuna lolote analolijua lakini msaidizi yule alisema kwa hakika hana
taarifa zozote.
Wakiwa Safarini kutokea Canada alijawa na mawazo mengi sana kwa
sababu hata alipoongea na mume wake Rais Costa alimwambia tu
anamtaka arudi nyumbani haraka na hakumpa sababu.
Alidhani labda mtoto wao wa pekee Brian Sylvester Costa amepata
tatizo lakini alipompigia simu Brian anayesoma nchini Denmark
alimwambia mama yake kuwa yupo salama. Sara alipata wasiwasi lakini
alishindwa kutambua tatizo ni lipi linalomfanya kutakiwa kurudi nchini
kwake haraka.
Asubuhi ile alitua uwanja wa Kimataifa wa ndege Stanza na msafara
ulimpokea kama kawaida ili kumpeleka Ikulu.
***********************************
“Tumsifu Yesu Kristu Baba Askofu”, Julius Kibwe alimsalimia
Muhashamu Baba Askofu Damian Begere alipomtembelea kwenye
makazi yake kama walivyokubaliana siku ya Jumapili.
“Milele amina Kibwe. Unaendeleaje?” Askofu Begere alimjibu Julius
huku akimshika mkono kumwelekeza mahali wanapokwenda kukaa
kwa mazungumzo kwenye bustani maridadi zilizozunguka makazi yale.
Makazi ya Askofu Begere yalivutia sana. Kulikuwa na usa?i na utulivu wa
hali ya juu. Bustani zilishamiri maua ya kila aina na ya kuvutia. Kukiwa
kumetengenezewa njia maalumu za kutembelea ili kujivinjari kwenye
bustani zile, kulijaa ndege kama Tausi, Kanga na Kasuku
walioning’inizwa kwenye vivuli vya miti kwenye vitenga vyao.
Mathalini, katikati ya njia na kwenye bustani zile kuliwekwa sanamu
nzuri za kuvutia za watakatifu na taa nzuri zilizowaka na kuzifanya
sanamu zile zivutie sana. Tena hapakukosa kile wakatoliki wanaita
Groto, yaani Sehemu iliyotengenezwa vizuri kama pango hivi ambapo
kuna sanamu nzuri ya Bikira Maria na ambapo watu kama watano
huweza kukaa na kufanya ibada.
Upande wa kulia kuliwekwa sehemu inayorusha maji na kutiririka
kwenye njia zake maalumu zilizotengenezwa na kufanya kama vijito
hivi. Miti mingi ya vivuli na matunda ilizunguka makazi yale. Uki?ika
kwenye makazi ya Askofu Begere basi ilikuwa ni vigumu sana
kutofautisha msimu wa kiangazi na wa mvua ama msimu wa joto na
baridi. Muda wote palijawa na unyevunyevu na kiubaridi. Ilikuwa ni
pepo iliyopo Stanza.
“Julius umeibuka na hili la Rais Costa kumiliki kisiwa cha kitalii huko
U?ilipino. Limekaaje hili” Askofu Begere alimuuliza Julius katika hali ya
ucheshi.
Alirejea taarifa aliyoisoma na yeye kwenye gazeti la STANZA TODAY
lililomnukuu Julius akisema ana ushahidi usio na shaka wa Rais Costa
kumiliki kisiwa cha kitalii nchini U?ilipino.
“Baba Askofu ndiyo maana Jumapili iliyopita nilishangaa mahubiri yako,
hayakuwa katika hali uliyotufundisha na ya ukweli. Labda wewe ndiyo
uanze kunieleza mimi nini kimekupata maana ulinijibu tu kuwa wakati
mwingine mtu huhitajika kubwaga manyanga chini”, Julius ni kijana
mdogo kiumri lakini mwenye uwezo mkubwa wa kujenga hoja katika
mijadala alimuuliza Askofu Begere kwa jicho la umakini.
“Hili lako ndilo la muhimu Julius. Ha ha ha!” Askofu Begere alisisitiza
huku akicheka.
“Baba Askofu, kwa kifupi tu ni kuwa kwa sasa tangu tuanze awamu hii
ya tatu ya Rais Costa, amekuwa akichukua pesa kwenye Kibubu Cha
Taifa kinyume na utaratibu. Amekuwa akitoa ‘Presidential Order’
kuidhinisha pesa kwa kisingizio kuwa anatekeleza miradi ya maendeleo
na kuwa taratibu za bunge ni ndefu na zinazorotesha kasi ya maendeleo
anayoitaka. Bahati mbaya bunge lina wabunge wengi wa chama chake
ambao hawataki kuhoji taarifa yoyote, ama kwa kuogopa au kwa
makusudi kwakuwa tu anayetenda hayo ni Mwenyekiti wa chama cha
Ukombozi Stanza.
Pesa hizi anazochota 25% anazichukua moja kwa moja ile 75%
inayobaki anaiingiza kwenye mradi lakini hao wanaotekeleza mradi
wanamwingizia asilimia 15% tena kwenye akaunti zake zilizopo Uswizi.
Kwa hiyo kwa mradi mmoja pesa zinazotoka kwa amri yake karibu 40%
humrudia yeye mwenyewe.
Isitoshe kila kampuni kubwa hapa nchini imekadiriwa kodi ya kihalali
kabisa na baada ya kujua ni kiasi gani kwa uhalali kampuni inatakiwa
kulipa basi kwa kutumia vyombo vyake hurekodi kwenye mamlaka ya
makusanyo ya taifa 25% pungufu ya uhalisia. Hii asilimia 25
huchukuliwa na kuingizwa kwenye akaunti zake.
Kwa maneno mengine kama kodi ya kampuni husika inatakiwa ilipwe
Milioni mia moja katika mwaka wa fedha huo basi italipa Milioni 75 na
ile Milioni 25 iliyobaki itaingizwa kwenye akaunti binafsi za Rais Costa.
Najua hayo watu wengi hawafahamu, ila nimepenyezewa na watu
ninaowaamini kutoka Idara za Makusanyo ya kodi na hata wandani wa
Rais.
Lakini pia, toka tulipoingia awamu hii ya tatu ya utawala wa Rais Costa
amejikusanyia ukwasi mkubwa kuliko aliokusanya awamu zote mbili
alizokaa madarakani. Sasa basi, ninazo taarifa za visiwa alivyonunua
huko U?ilipino na Majengo na makazi aliyonunua huko Finland. Tena
hisa zake kwenye makampuni ya hisa ya nchi za Scandinavia pia tayari
taarifa ninazo”, Julius alimalizia.
Askofu Begere alikuwa amebaki mdomo wazi asiamini anachokisikia.
“Nimeshangaa sana Julius kama haya ni kweli. Lakini sasa huogopi
kuyatamka haya? Huogopi atakudhuru?”. Askofu Begere alihoji kwa
sauti ya chini sana.
“Ataua wangapi? Mimi nimeaga kwetu kuwatumikia wana Stanza. Kama
ni kufa sote tutakufa, hata yeye. Sintokuwa binadamu wa kwanza kufa.
Hakuna haja ya kuwa na hofu”, Julius Kibwe alijibu kijasiri.
“Kwa kweli kijana wangu kama una moyo wa kijasiri namna hiyo
nakupongeza. Si wengi wameumbwa na ujasiri huo. Mpo wachache
sana. Mimi nilisikitika sana kwa kitendo alichonifanyia Costa.
Aliamua kuzuia miradi yote mikubwa ya maendeleo ninayotaka
kuifanya. Ile yote niliyoitangaza kanisani aliizuia na imebidi nikubaliane
na matakwa yake ili iendelee.” Askofu Begere alimalizia na kutulia
kimya.
“Baba Askofu kuliko kuongea vile ni bora ungekaa kimya ama
kumsukumia msaidizi wako aongee. Kauli yako ina uzito sana na sasa si
vyema kuharibu uzito ule katika siku zako hizi za mwisho za utumishi”,
Julius aliongea kwa kumshauri Askofu Begere.
“Julius, sisi Wajesuiti tuna msemo unaosema kwa kilatini ‘dum in sua
non est super’ yaani ‘hatujamalizana mpaka tumalizane’. Askofu Begere
alimwambia Julius huku akimninia chai iliyokuwa imeletwa pale
bustanini na mmoja wa masista wa makazi yale.
“Sijakuelewa baba”, Julius alitaka ufafanuzi.
“Ha ha ha ha! The ?ight for justice is not over, not just yet. My son,
resistance to tyranny is obedience to God. What is going to unfold next
is bigger than he ever expected”. (Ha ha ha ha! Mapambano kwa ajili ya
haki hayajaisha, bado. Mwanangu, kukataa udhalimu ni kumtii Mungu.
Kinachofuata ni zaidi ya alichowahi kukitarajia maishani mwake’’),
Askofu Begere alijibu tena kimafumbo.
Alimkaribisha Chai na waliendelea na habari nyingine mchanganyiko
ikiwemo Askofu Begere kumwelezea kwa kina kisa kizima cha yeye na
Rais Sylvester Costa.
*******************************
ITAENDELEA
0 comments:
Post a Comment