Search This Blog

Saturday 24 December 2022

OPERATION BARRAS - 2

  http://pseudepigraphas.blogspot.com/2020/06/operation-barras.html

Simulizi :  Operation Barras

Sehemu Ya Pili (2)







Taarifa hii ilikuwa ni ya kutia moyo mno kutokana na Group la vijana hawa wa West Side Boys kusumbua mno vichwa vya majeshi ya serikali pamoja na vikosi vingine ambavyo vilikuwemo nchini Sierra Leon. Kama ilivyo Ada ya wanajeshi wote wanapopokea taarifa hii inakuwa kana kwamba hakuna haja ya kusubiri zaidi mpaka pale ambapo watahakikisha kama ni kweli walichokisikia kilikuwa ni sahihi na labda ndani ya Mwezi huu jeshi la nchi hiyo litakuwa limepiga hatua kubwa na labda hatimaye Simulizi za kutisha za vijana wa West Side Boys hawatazisikia tena.






Kwa hiyo ulipofika muda wa kurejea kambini kwao Waterloo, kamanda wa msafara huu wa kikosi hiki cha STTT (1R IRISH) alishauri kuwa wajiridhishe kuhsu taarifa hiyo ya vijana na West Side Boys kuweka silaha chini.



a928e63aebd007ce89e657ee03e1df47.jpg

WEST SIDE BOYS



Sasa basi, ukiwa unatoka eneo la Masiaka kwenda Wasterloo au Waterloo kwenda Masiaka, maeneo fulani ya kati kati kuna barabara inachepuka kulekea kwenye kijiji cha Magbeni ambacho kama nilivyoeleza awali kuwa kilikuwa kinatumiwa na West Side Boys kama makao makuu yao.






Kwa hiyo, Meja Alan Marshall, kamanda wa msafara akaamuru kuwa wachepuke kufuata barabara hiyo mpaka kijijini Mgbeni ili kuthibitisha taarifa ambayo walikuwa wameipata kuwa vijana hao walikuwa wameweka silaha chini.




Msafara ukashika kasi kukaribia kabisa kijiji cha Mgbeni. Lakini wakiwa wamebakiza kama kilomita mbili tu kuingia kwenye kijiji hicho walishangaa ghafla tu mbele yao imetokeza gari aina ya Bedford ambayo imefungwa mizinga ya kudungua ndege imewaziba njia mbele yao. Kufumba na kufumbua kila upande… nyuma, mbele… kushoto, kulia… walikuwa wamezungukwa na mamia ya wapiganaji wa West Side Boys wakiwa wamewanyooshea bunduki.




Msafara wao (STTT) ulikuwa na wanajeshi 11 tu, lakini vijana hawa wa West Side Boys ambao walijitokeza ghafla walikuwa si chini ya 150 au 200. Kwa maana hiyo ilikuwa dhahiri kabisa hawakutakiwa kuanzisha mapambano ya risasi kwani ndani ya sekunde kadhaa tu wangeuwawa. Hivyo basi hawakuthubutu hata kuinui silaha zao na kuwanyooshea ‘vichaa’ hawa wa West Side Boys ili walau waonekane hawakuwa na nia mbaya yeyote ile.




Baada ya kuwekwa chini ya ulinzi, walinyang’anywa silaha zote pamoja na magari yao ya kijeshi aina ya Land Rover zenye ‘Wimik’ (Weapons Mount Installation Kit (Tazama picha)) na kisha wakaongozwa kwa miguu kutoka pale walipokamatwa na kuvuka mto Rokel na kuingia kijiji cha Gberi Bana ambako ndiko kwenye makazi ya kiongozi wa kikundi hiki, mwanajeshi mwenye mbwembwe na ukatili usiomithilika, ‘Brigedia’ Foday Kallay.






Baada ya wanajeshi hawa mateka wa STTT kufikishwa tu mbele yake, kitu cha kwanza ambacho ‘Brigedia’ Faday Kallay alikifanya ni kuinua simu na kupiga London, serikali ya Uingereza.




Simu ilivyopokelewa… Brigedia Faday Kallay hakutaka salamu au kujieleza sana… moja kwa moja akaelekea kwenye hoja zake.






“this is brigadier Foday Kallay…get a piece of peper and a pen.!” Kallay alijieleza kwa lafudhi yake mbovu ya kiafrica cha magharibi.




“what for?” aliyepokea simu akamuuliza.




“I want you to write down a list of my demands.!!” Brigedia Faday Kallay akongea kwa kujiamini.




“demands for what.!?” Aliyepokea simu aliuliza kwa mshangao zaidi.




“…I have eleven of your soldiers… and if you don’t comply to my demands they are going to be dead in 48 hours.!” Brigedia Fadaya Kallay aliongea kwa sauti thabiti na kujiamini kabisa.








Japokuwa kwa kiasi fulani vita ya wenyewe kwa wenyewe hapa nchini Sierra Leon ilikuwa inaishia ishia… lakini kwa upande wa nchi ya Uingereza, siku hii ya August 5, 2000 walikuwa kana kwamba wanaingia upya kwenye ‘vita’ ya kwao na kikundi cha West Side Boys.


Jambo baya zaidi vijana hawa walikuwa hawaogopi kifo… ilikuwa ni kana kwamba nafsi zao zilikuwa tayari ziko kuzimu na ni miili tupu ilikuwa inatembea… hivyo kama Uingereza ilitaka kuwapata tena wanajeshi wake wakiwa bado hai… basi walipaswa kupiga kila hatua kuanzia sasa kwa umakini na weledi uliotukuka.




df90bf7e3c948b0f91b128c820553af0.jpg

MFANO WA LAND ROVER YENYE 'WIMIK' AMBAZO ZILIKUWA KWENYE MSAFARA KUTOKA MASIAKA NA KUPITA KIJIJI CHA MGBENI NA KUTEKWA



Jana katika sehemu ya kwanza ya mfululizo wa makala hizi kuhusu Operesheni kubwa tano za kihisistoria nilianza kueleza kuhusu Oparesheni Barras.



Katika sehemu ile ya kwanza nilieleza kuhusu chimbuko la kikundi cha wapiganaji wa *West Side Boys* na namna ambavyo walishiriki katika vita ya wenyewe nchini Sierra Leon.

Mwishoni nilieleza juu ya mfululizo wa matukio mpaka kuelekea kuwateka wanajeshi wa kikosi cha STTT kijijini Mgbeni.



Tuendelee



8c6ebf39fc4b31561dd2236fd1cdefac.jpg





SEHEMU YA PILI




Baada ya serikali ya uingereza kupokea taarifa juu ya kutekwa kwa wanajeshi wake wa kikosi cha STTT jambo la kwanza kabisa ambalo walilifanya ilikuwa ni kutuma timu ya 'negotiators' kwenda nchini Sierra Leon.


Vichwani mwao walikiwa wakiamini kuwa walikuwa wanaweza kuwashaiwshi vijana wa West Side Boys kwa kuwapa vitu vya anasa ili wawaachie wanajeshi wao.



Timu hii ya negotiators iliongozwa na Luteni Kanali Simon Fordham ambaye ndiye alikuwa kamanda mkuu wa kikosi cha 1R IRISH (STTT) kilichopo nchini Sierra Leon.

Pamoja naye alikuwa na wasaidizi kadhaa ambao ni 'professional negotiators' kutoka Metropolitan Police nchini Uingereza.



Licha ya tukio hili kutoka ndani ya ardhi Sierra Leon, lakini Rais Ahmad Kabbah wa nchi alitoa ruhusu yote ya Uingereza wenyewe kuendesha juhudi za kuokoa wanajeshi wao kutokana na suala dhahiri kuwa Sierra Leon hawakuwa na weledi wa kutosha kwa namna yoyoye ile kufanikisha shughuli hiyo.



Kwa hiyo timu hii ya negotiators ikiongozwa na Luteni Kanali Simon Fordham walifanya mawasiliano na uongozi wa West Side Boys ili kuanza mazungumzo. Vijana hao walishikilia msimamo wao wa kutowaachia wanajeshi kwa madai kuwa waliwachokoza kwa makusudi kwa kuingia kwenye himaya yao kijiji cha Mgbeni.

Baada ya mazunguzo marefu sana hatimaye walikukubaliana makutano yao ya kwanza yawe siki ya August 29, 2000 nje kidogo ya kijiji cha Mgbeni kwenye barabara inayochepuka kwenda njia kuu ya Waterloo.


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog