Search This Blog

Saturday 24 December 2022

OPERATION BARRAS - 3

  http://pseudepigraphas.blogspot.com/2020/06/operation-barras.html

Simulizi :  Operation Barras

Sehemu Ya Tatu (3)



Katika mkutano wao huu wa kwanza upande wa Uingereza uliongozwa na Luteni Kanali Simon Fordham na uoande wa West Side Boys uliongozwa na kiongozi wao mkuu 'Brigedia' Foday Kallay.

Walipokutana, Fordham aliweka msimamo kuwa hawezi kuongea kitu chochote na Kallay mpaka pale ambapo atapewa uhakika kuwa Wanajeshi waliotekwa bado walikuwa hai.


Walibishana kwa muda wa dakika nyingi sana ambapo Brigedoa Foday Kallay akisisitiza kuwa wanajeshi waliotekwa wako hai lakini Luteni Kanali Simon Fordham aliendelea kusisitiza kuwa hawezi kuamini maneni tupu, anataka uthibitisho halisi.



Ili kuepusha mazungumzo yasivunjike, Kallay aliamuru wanajeshi wawili waliotekwa waletwe kutoka kijijini Mgbeni mpaka hapa kikaoni.


Ndani ya dakika chache tu, wapiganaji wake waliwaleta mateka wawili hapo kikoni, kiongozi wa ule msafara uliotekwa ambaye aliitwa Meja Allan Marshall na mwanajeshi mwingine Kapteni Flaherty.


Ukweli ni kwamba negotiators hawa walikuwa wanajua kuwa wanajeshi wao waliotekwa walikuwa hai kabla hata ya kufika hapa, lakini walikiwa na lengo la siri ndani ya akili zao kutaka waletwe hapa wawaone kwa macho yao.


Walipokuwa wakisalimiana na wenzao baada ya kuletwa hapo kikaoni, walipokuwa wanapeana mikono kwa ustadi mkubwa na weledi wa kijeshi Luteni Kanali Simon Fordham alimpa kikaratasi kwa siri Kapteni Flaherty. Karatasi hii ilikuwa ni ramani ya kijiji chote na majengo ya kijiji cha Gberi Bana ambacho mateka hao 11 wa kijeshi walikuwa wanashikiliwa.


ada75e1beb2c40f92d64a8bda8c95cfa.jpg


Kikao kiliendelea na hoja kuu mezani ilikuwa ni kusikiliza 'demands' za West Side Boys wanazotaka kutimizwa ili waweze kuwaachia mateka wa kijeshi walionao.


Orodha yao ilikuwa ni ndefu kweli kweli, kana kwamba matatizo yao yote walikuwa wanataka yaishe kulitia tukio hili. Katika uhalisia wa kawaida ilikuwa ni kama haiwezekani kutimiza matakwa yao yote japokuwa serikali ya Uingereza mwanzoni walikuwa na dhamira nzuri ya kumaliza suala hilo mezani.


Licha ya orodha ya wavitakavyo kuwa ndefu sana, lakini vitu vyenye uzito zaidi vilikuwa ni hivi vifiatavyo;


1. Kupatiwa vifaa vya mawasiliano, hasa simu za satelaiti.


2. Madawa ya matibabu


3. Wapatiwe kinga ya kisheria kuwazuia serikali kuwashitaki wakiamua kuweka mitutu chini.


4. Kufanywa marekebisho kwenye mkataba wa Lome (Lóme Peace Accord)…. Mkataba juu ulisainiwa mwaka 1999 kati ya serikali ya Rais Ahmad Tejan Kabbah na kiongozi wa RFU Bw. Foday Sankoh.


5. Kuachiwa kwa mateka wote wa kikundi cha West Side Boys waliopo kwenye jela za serikali.


6. Kupewa scholarship kwa kiongozi wa juu wa West Side Boys waliokuwa wanataka kwenda kusoma chuo kikuu nchini Uingereza.



Matakwa haya yalikuwa ni ya kiwendawazimu… lakini ndicho ambacho West Side Boys walikuwa wanakitaka ili waweze kuwaachia mateka waliokuwa nao.


afa62cf87baebcc7b94317ddfc3dccc0.jpg


Kikao cha pili kilifanyika siku ya tarehe 31 August.


Katika kikaoni hiki upande wa Uingereza walitimiza matakwa mawili ya West Side Boys… waliwasilisha simu za satelaiti pamoja na madawa ya matibabu.


Kutokana na kutimiza matakwa hayo mawili, West Side Boys walikubali kuwaachia wanajeshi watano kati ya wale 11.


Matakwa haya mawili ya West Side Boys yalikuwa yanatekelezeka tofauti na yale mengine, na ndio maana Uingereza walianza nayo. Yale matakwa mengine yaliyosalia kiuhalisia yalikuwa hayatekelezeki au kama yangetekelezwa basi yangeleta mgogoro mkubwa kuliko ambavyo mgogoro waliokuwa wanataka kuumaliza.



Kwa hiyo ilikuwa dhahiri kabisa kwamba jambo mbadala lilikuwa linahitajika kufanyika.



Uzuri ni kwamba kikundi cha West Side Boys wenyewe walikuwa wamefanyaakosa mawili bila kujijua.



Kosa la kwanza lilikuwa ni mateka wale watano ambao waliwaachia. Walikuwa hawajua kuwa kwenye kile kikao cha kwanza walikabidhiwa kwa siri kikaratasi cha eneo lote ambalo walikuwa wameshikiliwa. Kwa hiyo mpaka siku hii walipokuwa wanaachiwa walikuwa wamekusanya intelijensia ya kutosha kuhusu kijiji cha Gberi Bana.



Kosa la pili, lilitokana na haiba ya ujivuni wa viongozi wa West Side Boys. Walipokabidhiwa tu simu za upepo moja kwa moja waliporejea makao makuu yao walipiga simu kwenda kituo cha habari cha BBC na kufanya mahojiano LIVE kujigamba na kusisitiza kuhusu demands zao zilizosalia.


Kitu ambacho hawakukijua ni kwamba jeshi la Uingereza lilikuwa linafuatilia mawasiliano haya na kufanya 'triangulation' ili kujua kwa ufasaha zaidi simu ilikuwa inapigwa kutoka wapi.



Mateka wale wa kijeshi walioachiwa siku hiyo hiyo haraka sana walisafirishwa kwa chopa mpaka kwenye meli ya kijeshi ya RFA Sir Percivale ambayo ilikuwa pwani ya Africa magharibi ili kwenda kuwasilisha intelijensia waliyo nayo kuhusu kijiji ch a Gberi Bana kwa makamanda wa kijeshi waliokuwa kwenye meli hiyo kutoka Uingereza.




Matakwa ya West Side Boys yalikuwa hayatekelezeki. Jambo mbadala la haraka lilikuwa linatakiwa kufanyika.


Operation Barras ilikuwa inaelekea kuzaliwa.



e907b8985d97d635eb0b6de5ae99f66a.jpg

RFA Sir Percivale ambayo ilikuwa imepaki kwenye pwani ya Afrika Magharibi



OPERATION BARRAS (SEHEMU YA TATU)

OPERATION BARRAS

SEHEMU YA TATU

Kabla sijaendelea mbali sana, nieleze kidogo kuhusu SAS na 1 PARA vitengo vya weledi ambavyo vililengwa na jeshi la Uingereza kutumika katika oparesheni ya uokozi wa wanajeshi waliotekwa na wapiganaji wa West Side Boys.

SPECIAL AIR SERVICES (SAS)

SAS ni kitendo maalumu cha weledi cha jeshi la Uingereza. Kitengo hiki kiliundwa mwaka 1941 kikiwa kama ‘regiment’ na baadae mwaka 1950 kilibadilishwa kuwa ‘corps’.

Nieleze kidogo hii tofauti ya regiment na corp katika mifumo ya kijeshi.

Katika mfumo wa vitengo vya kijeshi, ‘category’ ya vitengo/kikosi na namna kinavyopewa jina inategemea na kazi ya weledi pamoja na idadi ya wanajeshi kwenye kitengo?kikosi hicho.

Kwa mfano;

FIERTEAM – Inakuwa na watu 3 mpaka 4 na kiongozi wao mara nyingi huwa ni Koplo.

SQUAD – Inakuwa na watu 8 mpaka 12 na kiongozi wao huwa ni Sajenti.

PLATOON – Huwa na watu 15 mpaka 30 na kiongozi wao huwa ni Luteni.

COMPANY – Huwa na watu 8 mpaka 150 na kiongozi wao huwa ni Kapteni au Meja.

BATTALION – Huwa na watu 300 mpaka 800 na kiongozi wao huwa ni Luteni Kanali.

BRIGADE (REGIMENT) – Huwa na watu 2000 mpaka 4000 na huongozwa na Kanali au Brigedia Jerenerali.

DIVISION – Huwa na watu 10,000 mpaka 15,000 na huongozwa Meja Jenerali.

CORPS – Huwa na watu 20,000 mpaka 40,00 huongozwa na Luteni Jenerali

JESHI (FIELD ARMY) – Huwa na watu 80,000 na kuendelea na huongozwa na Jenerali.

KIKUNDI CHA MAJESHI (ARMY GROUP) – Inaundwa na Majeshi (field Army niliyotaja hapo juu) mawili au zaidi. Huongozwa na Field Marshal au Jenerali wa nyota Tano.

REGION/THEATER – Huu ni Mkusanyiko wa ‘Army Groups’ (nilizotaja hapo juu) Nne au zaidi. Huongozwa na Jenerali mwenye nyota Sita au Amiri Jeshi Mkuu (Mara nyingi huwa ni Mkuu wa Nchi).

NB: Idadi ya wanajeshi kwenye vitengo hutegemea na mifumo ya kijeshi na utartibu wa nchi husika japo karibia nchi zote duniani hutumia mfumo huu katika kutambua/kutoa majina kwa vikundi/vikosi vyake na viongozi wa vikosi/vikundi hivyo.

Kwa hiyo ninaposema kuwa SAS iliundwa mwaka 1941 kama ‘regiment’ na mwaka 1950 ilifanywa kuwa ‘corps’ naamini kuwa unanielewa kwa ufasaha kabisa.

Mizizi ya SAS unaweza kuipata kuanzia mwaka 1941 na kipindi cha Vita Kuu ya Pili ya Dunia. Lakini mwaka 1947 iliundwa upya kama sehemu ya Territorial Army na kupewa jina la 21st Special Air Services Regiment (Artists Rifles).

SAS hupata watu wake kutoka katika vitengo vingine vya jeshi la Uingereza na mara nyingi huchukua wanajeshi ambao wana mafunzo ya ukomando tayari au ‘Airborne Foce’.

Kazi kubwa ya SAS ni kufanya ‘Covert Reconnaissance’ (hii ni kufanya ushushus wa eneo maalumu (mara nyingi eneo la adui vitani) na kupata kujua jografia ya eneo la adui, na namna aduai alivyojipanga). Pia SAS hufanya couter-terrorism, mashambulizi ya weledi dhidi ya adui (direct action) na uokoaji wa mateka.

SAS ilijipatia umaarufu mkubwa mwaka 1980 katika tukio la uokoaji wa mateka kutoka kwenye ubalozi wa Iran, tukio ambalo lilirekodiwa na kuirushwa kwenye runinga.

Nitaongelea kuhusu hili tukio huko mbeleni kwenye nfululizo huu huu wa makala ya Operesheni za kijasusi zilizofanikiwa zaidi.

1 PARA

1st Battalion, Parachute Regiment (1PARA) ni sehemu ya Kitengo cha usaidizi kwa vikosi vya weledi wa majeshi ya Uingereza (Special Forces Support Group – SFSG).

1PARA mizizi yake inaweza kupatikana kuanzia miaka ya 1940 kipindi cha Vita Kuu ya Pili ya Dunia ambapo kikosi maalumu cha No. 2 Commando chenye ukubwa wa batalioni kilipewa mafunzo maalumu ya parashuti katika kambi ya kijeshi ya Cambria maeneo ya Perham Down, karibu na Tidworth, Hants.

Kikosi hiki kilikuwa na ‘troops’ nne – A, B, C na D. baadae kikaongezewa mpaka kufikia troops 11. Baadae makomando hawa wa kitengo hiki wote walibadilishiwa majukumu na kupelekwa SAS huku jeshi likitengeneza kikosi kingine kipya cha No. 2 Commando.

Baada ya kikosi hiki kipya kuundwa muda mchache baadae kilisukwa upya na kupewa jukumu jipya na jina jipya la 1st Parachute Battalion.

Tangu kipindi hicho mpaka sasa 1 PARA imekuwa na jukumu kuu la kufanya usaidizi maalumu katika oparesheni za kijeshi zinazohusisha vikosi vya weledi kwenye oparesheni maalumu.

Hii ndio sababu ya 1 PARA katika mifumo ya kijeshi kuwekwa kwenye ‘category’ ya Special Opareations Light Infatry ikiwa na maana ya kwamba… kwenye miaka ya zamani kabisa kwenye medani za kivita, light Infatry walikuwa ni wanajeshi wa miguu wenye kubeba silaha nyepesi ambao walikuwa wanatumika kama ‘chambo’ kabla ya wanajeshi wenye silaha nzito kuanza mashambulizi. Lakini katika ulimwengu wa kisasa. Light Infatry imeboreka zaidi na kuwa ni wanajeshi ambao katika medani za kivita weledi wao mkubwa ni katika kasi na mnyumbuko wa haraka wa uendeshaji wa majukumu yao pasipo kutegemea zaidi silaha nzito. Na mara nyingi Light Infatry inakwenda sambamba na ukomando na matumizi ya Parashuti.

TURUDI KWENYE OPERATION BARRAS…

Nilikuwa najaribu kueleza ni kwanini jeshi la Uingereza liliamua kutumia SAS ikisaidiwa na 1 PARA kutekeleza oparesheni ya uokoaji wa mataeka wa kijeshi walichukuliwa na wapiganaji wa West Side Boys nchini Sierra Leon. Na nimeeleza kuwa sababu kuu ya kuamua kuwajumuisha 1 PARA ni kutokana na makao makuu ya West Side Boys kuwepo kwenye vijiji viwili tofauti ambavyo vimegawanywa kwa mto (kijiji cha Mgbeni na Gberi Bana).

Kwa hiyo,


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog