Search This Blog

Saturday 24 December 2022

OPERATION BARRAS - 4

  http://pseudepigraphas.blogspot.com/2020/06/operation-barras.html

Simulizi :  Operation Barras

Sehemu Ya Nne (4)


Jeshi la Uingereza lilitoa maagizo kwa makao makuu ya 1 PARA kuandaa kikosi maalumu ambacho kitashiriki katika oparesheni hii ambayo ilikuwa inapangwa. Kiongozi mkuu wa batalioni hii ya 1 PARA akateua kikundi maaumu cha A COMPANY kinachoongozwa Meja Matthew Lowe, ambacho kwa wakati huo kilikuwa kwenye mazoezi nchi Jamaica. Japokuwa makomando karibia wote wa kikundi hiki cha A Company walikuwa ni wapya jeshini lakini viongozi wa 1 PARA waliamua kuwapa jukumu hili kwa kuzingatia kuwa wanajeshi wapya ambao ndio kwanza wametoka mafunzoni morali yao inakuwa iko juu sana. Walichokifanya ilikuwa ni kuwaongezea makomando wachache wenye uzoefu ili kuhakikisha kuwa uzoefu wa medani ya vita haikosekani ndani ya kikundi hiki cha A Company ambao walikuwa wanatarajiwa kupelekwa huko Sirrea Leon.

Baada ya hapo siku ya August 31, A Company walirudishwa kutoka Jamaica mpaka Uingereza na moja kwa moja kupelekwa kwenye kijiji kinachitwa South Cerney nchini Uingereza. Mpaka muda huu hakuna commando yeyote ambaye alikuwa anajua ni nini kinaendelea. Wote waliambiwa kuwa wamepelekwa kijijini hapo kwa ajili ya kufanya mafunzo maalumu ya kijejeshi yajulikanayo kama “readiness to move”. Mtu pekee ambaye alikuwa anajua kwa nini wako hapo alikuwa ni kiongozi wao Meja Matthew Lowe.

Kesho yake jioni baada ya kuwasili kijijini hapo, makomando wote waliitwa na simu zao za mikononi kukusanywa na kuzimwa. Baada ya hapa ndio walielezwa lengo hasa la kurudishwa kutoka Jamaica mpaka Uingereza.

Wakati huo huo…

Kule nchini Siera Leon wale makomando wa SAS waliopandikizwa kwenye timu ya negotiators walikuwa pia wameanza kufanya covert reconnaissance ya hali ya juu zaidi. Walikuwa wanajitahidi kuingia maeneo ya karibu na vijiji vya Mgbeni na Gberi Bana nyakati za usiku ili kusoma namna ya ulinzi ulivyo kwenye hayo makoa makuu ya West Side Boys, silaha walizonazo pamoja na nguvu yao ya idadi ya wapiganaji.

Baadae kitengo kingine maalumu cha jeshi la Uingerreza cha weledi wa majini kijulikanacho kama Special Boat service kilifanikiwa kupitisha kwa siri kubwa boti ndogo ya kijeshi kwenye mto Rokel ambao unatenganisha kijiji cha Mgbeni na Gberi Bana. Boti hii ilikuwa imepakia makoamndo wanne wa SAS ambapo boti ilipopita wao waliruka, makomando wawili kila upande mmoja wa mto.

Makomando hawa nao kazi yao ilikuwa ni kukusanya taarifa nyeti zaidi kuhusu West Side Boys pamoja na kutambua sehemu ambazo helikopta za kijeshi zinaweza kutua.

Ulifika muda ambapo Uingereza ilikuwa imepata Intelijensia ya kutosha kuhusu wapiganaji wa West Side Boys na kilichobakia kilikuwa ni utekelezaji tu wa Oparesheni. Lakini changamoto kubwa ilikuwa ni vyombo vya habari.

Media zote ulimwenguni na hasa hasa vyombo vya habari vya Uingereza na Marekani vilikuwa vimeanza kuripoti juu ya ‘mining’ono’ kuhusu jeshi la Uingereza kufanya Oparesheni ya uokozi. Hili lilikuwa ni suala baya mno kwani kama habari hii ingeendelea kuripotiwa na kuaminika kwenye jamii, basi West Side Boys wangeweza kuua mateka wote ambao walikuwa nao.

Hivyo basi jeshi la Uingereza lilikuwa linajitahidi kwa kila namna kuficha mno mwenendo wao na kutoonesha dalili yoyote kwamba walikuwa wanataka kufanya Operesheni ya Uokozi. Hii iliwafanya iwawie vigumu sana kuingiza A Company ya 1 PARA nchini Sierra Leon kutokana na vyombo vya habari kufuatilia nyendo zote na kuzingatia kwamba hata ndani ya jeshi kulikuwa na watu wanaovujisha habari.

Kwa hiyo chaguo la kwanza lilikuwa ni ‘kulaunch’ shambulio kutokea Uingereza. Yaani siku ambayo operesheni itatekelezwa basi makomando watokee moja kwa moja nchini Uingereza na kuelekea vijiji vya Mgbeni na Gberi Bana nchini Sierra Leon. Lakini hii pia ilikuwa na changamoto yake. Ingeachukua takribani masaa 14 kulaunch operesheni kutokea Uingereza mapaka Mgbeni na Gberi Bana. Kijeshi hii ilikuwa ni ‘risk’ kubwa sana kwani kulikuwa na uwezekano mkubwa wa West Side Boys Kushitukia mchezo wote kabla haujafanikiwa. Lakini pia safari ya masaa 14 ingewachosha sana makomando na ufanisi wao kwenye operesheni ungepungua sana.

Kwa kuzingatia hili, timu yote ya A Company ilisafirishwa mpaka Dakar nchini Senegal ili kuwe na urahisi wa kulaunch operesheni kutokea hapo kwa sababu nchi hiyo inapakana na Sierra Leon.

Pia ili kupunguza urasimu, balozi wa Uingereza nchini Sierra Leon ambaye alikuwa mjini Freetown, Bw. Alan Jones alipewa mamlaka yote ya kuamuru na kutoa kibali juu ya operesheni hiyo kwa niaba ya Waziri Mkuu. Pia Brigedia David Richards ambaye alikuwa ni kamanda wa vikosi vyote vya Uingereza ambavyo vilikuwa nchini Sierra Leon alipewa mamlaka yote ya kijeshi na kuwa na kauli ya mwisho ya kijeshi kuhusu operesheni hiyo.

Changamoto pekee ambayo walikuwa wamebakiwa nayo ilikuwa ni namna gani wataingiza nchini Sierra Leon makomando wa A Company kutoka 1 PARA pamoja na makomando wengine wa SAS pasio vyombo vya habari kugundua na pasipo kuvuja habari hiyo kutoka ndani ya jeshi.?

Katika hali kama hii ndipo ambapo suala la ‘uhuru’ wa kuripoti kila habari unaonekana kama ni ‘upuuzi’ kwa baadhi ya watu. Media zilikuwa zinataka stori na kila mtu akitaka kuwa wakwanza kuripoti habri hiyo bila kuzingatia ni kwa namna walikuwa wanakuwa kikwazo katika kuokoa maisha ya wale wanajeshi waliotekwa.

Upande wa pili wa mpaka, ndani ya Sierra Leon timu ya negotiators walikuwa wanaendelea ‘kununua muda’ kwa kuendeleza na kurefusha maongezi na West Side Boys ili kuwafanya waone kuwa Uingereza bado ilikuwa na nia ya kumaliza suala hilo mezani kwa maongezi.

Siku zilikuwa zimeyoyoma haswa… uvumilivu wa West Side Boys ulikuwa umeisha… walikuwa wanataka masharti yao yatekelezwe mara moja bila kuchelewa tena hata siku moja. Kadiri dakika zilivyyokuwa zinaenda mbele, ndivyo ambavyo wanajeshi mateka walikuwa wanakikaribia kifo cha kikatili mikononi mwa West Side Boys…

Lakini Brigedia David Richards alijiapiza kuwa kamwe hawawezi kupiga magoti na kuwaramba miguu West Isde Boys… Yaani ni kama waswahili tunavyosema, “inyeshe mvua au liwake jua” watawarudisha salama nyumbani kwa familia zao wanajeshi wao wote waliotekwa na watawashikisha adabu West Side Boys na watajutia kuvuka mpaka wa kuwagusa wanajeshi wa Uingereza.!!

Operation Barras ilikuwa imewiva!!

Itaendelea…






Operation Barras ilikuwa imewiva!!



Mkakati wa oparesheni ambao Uingereza walikuwa nao kichwani ulikuwa kama ifuatavyo;


Walilenga A Company ya 1 PARA ifanye uvamizi katika kijiji cha Mgbeni wakati ambao timu ya SAS itafanya uvamizi katka kijiji cha Gberi Bana upande wa pili wa mto.


Lengo kuu la A Company kupewa jukumu la kuvamia kijiji cha Mgbeni lilikuwa ni kuharibu silaha zote za West Side Boys ambazo zingeweza kutumika kuvuruga Oparesheni. Kumbuka kwamba kama ambavyo nimeeleza kuwa makao makuu ya wapiganaji hawa yako kwenye vijiji hivi viwili ambavyo vinatenganishwa na mto.


Kijiji cha Mgbeni ndicho ambacho kilikuwa kinatumika kama ‘kambi kuu’ ya wapiganaji hawa na ndipo hapo haswa ambapo silaha zao nyingi na vifaa vya kijeshi walikuwa wanavitunza. Kijiji cha Gberi Bana ng’ambo ya mto kilikuwa kinatumika kwa lengo kuu la kwanza kama makazi ya kiongozi wao Foday Kallay na makamanda wake wakuu.


Lakini pia jukumu kuu la pili ambapo A Company walilengwa kupewa lilikuwa ni kuwadhibiti wapiganaji wa West Side Boys wasiweze kuvuka mto mpaka kijiji cha pili cha wakati ambapo SAS watakuwa wanafanya uokozi wa mateka ambao wamehifadhiwa huko. Lakini pia jukumu la tatu ambalo walipewa lilikuwa ni kuokoa magari yote ya kijeshi ambayo yalitekwa pamja na wanajeshi wao wale 11.


Lakini changamoto ya pili ilikuwa ni mbinu ambayo watatumia kuingia kwenye vijiji hivi vya Mgbeni na Gberi Bana. Kulikuwa na mapendekezo kadhaa.


i. Overland Approach: ilifikiriwa kwamba makomando hawa wanaweza kuingia kijijini hapo moja kwa moja kwa kutumia gari za kijeshi. Japokuwa mbinu hii ilikuwa ni nzuri na ya uhalisia zaidi, lakini hasara yake ilikuwa ni kwamba, haikuwa rahisi kuingia kwenye vijiji hivi bila kushitukiwa mapema kabla hata ya kufika kijijini Mgbeni kutokana na West Side Boys kuweka vizuizi vingi kwenye barabara yote ambayo inaelekea kijijini Mgbeni.


ii. Water-borne Insertion: pia ilifikiriwa kwamba makomando hawa wangeweza kuingizwa kinyemela kwenye vijiji vyote viwili kwa kutumia njia ya maji kama ambavyo wale makomando wanne walivyopenyezwa kwa boti za SBS (Special Boat Services) kwa ajili ya kufanya reconnaissance . Njia hii ilikuwa ni murua lakini changamoto yake ilikuwa ni kwamba, mto Rokel ulikuwa na mchanga mwingi kwa hiyo isingewezekana kupita kwa kutumia boti kubwa. Lakini pia mto huu ulikuwa na mkondo unaoenda kasi sana. Sababu hizi zote zilimaanisha kwamba kulikuwa na uwezekano wa kutumia boti ndogo pekee, kwa maana ya kwamba ilikuwa inabidi kupeleka makomando wachache wachache kwa awamu. Hii haikuwa salama sana kwani ilikuwa inatoa mwanya kwa West Side Boys kushitukia ambacho kilikuwa kinaendelea kwenye mto Rokel.


iii. mwishoni ikaamuliwa kuwa njia bora zaidi itakuwa ni kutumia helikopta za kijeshi aina ya Chinook kutoka kitengo cha No. 7 Squadron cha jeshi la anga ambazo zilikuwa hapo hapo nchini Sierra Leon tangu kipindi cha Oparesheni Palliser ambayo nilieleza mwanzoni, raia wan chi za jumuiya ya madola walivyokuwa wanahamishwa kutoka nchini Sierra Leon kwenda makwao.




KUINGIA NCHINI SIERRA LEON


Katika sehemu iliyopita nilieleza ugumu ambao jeshi lilikuwa linaupata kuingiza makomando nchini Sierra Leon pasipo yeyote kung’amua kutokana na vyombo vya habari kufuatilia kila hatua ambayo jeshi la Uingereza walikuwa wanaichukua na pia ndani ya jeshi kwenyewe kulikuwa na maafisa mabao walikuwa wanavujisha habari kwa vyombo vya habari.


Ili kufanikiwa kwa oparesheni hii ilikuwa ni muhimu sana kwa wapiganaji wa West Side Boys waendelee kuamini kuwa Uingereza ilikuwa bado na nia ya kumaliza mzozo huu kwa mazungumzo. Kwa hiyo ulikuwa unachukuliwa umakini wa kupitiliza kuhakikisha kuwa hakukuwa na yeyote ambaye angeling’amua pindi makomando wa SAS na 1 PARA wangeingizwa nchini Sierra Leon.


Kwa hiyo ambacho Uingereza ilifanya ni kuingiza kikosi fulani cha makomando nchini Senegal na vyombo vyote vya habari walielekeza akili yao katika kufuatilia nyendo za kikosi hiki ambacho kilipelekwa Dakar.


Kutokana na vyombo vyote vya habari kuelekeza akili zao katika kufuatilia nyendo za kikosi hiki cha makomando pale Dakar, hii ilitoa mwanya kwa jeshi la Uingereza kupenyeza kwa siri kikosi cha makomando wa D Squadron ya 22 SAS bila chombo chochote kile cha habari kufahamu. Kwa mtindo huu huu pia jeshi la Uingereza liliingiza makomando wapatao 130 wa A Company katika vikundi vidogo vidogo.


Baada ya vikosi hivi viwili vya makomando kuingia nchini Sierra Leon kwa siri kubwa bila yeyote asiyehusika kufahamu, waliweka kambi katika eneo la Hasting, takribani kilomita 50 kusini mwa mji mkuu wa Freetown.


Wakiwa hapa, maandalizi muhimu ya mwisho mwisho yalifanyika kwa weledi mkubwa zaidi. Nia hapa ambapo walifanya mazoezi ya hatua ya mwisho kwa kutumia risasi halisi. Kwa kuwa tayari walikuwa na jiografia yote ya vijiji vya Mgbeni na Gberi Bana, kwa hiyo hapa hapa walipokuwa wameweka kambi na kufanya amzoezi ya maandalizi… kulitengenezwa vijiji vya kufanana kabisa na vile vya Mgbeni na Gberi Bana pamoja na mpangilio wa nyuma wa kufanana kabisa na jinsi zilivyo kule Mgbeni na Gberi Bana.


Wakiwa hapa Hasting wakifanya mazoezi ndipo ambapo waligundua kuwa walikuwa na changamoto nyingine ambayo hii hawakuwa na uwezo wa kuidhibiti kwa namna yoyote ile. Hali ya hewa.


Hali ya hewa ilikuwa ya joto mno kushinda hali ambayo walikuwa wameizoea nchini Uingereza.


Uzuri ni kwamba walau kidogo makomando wa SAS walikuwa na uwezo wa kuhimili hali yoyote ya hewa kutikana na mafunzo adhimu ya miaka kadhaa wanayopitia na moja ya mambo wanayofundwa ni namna ya kuhimili hali tofauti za hewa. Lakini makomando wa 1 PARA hawana mafunzo makubwa juu ya hili na makamanda wa Oparesheni walikuwa wanahofia wanajeshi wanaweza kuchemka (heat exhaustion) na hivyo kuathiri ufanisi wa oparesheni yote.


Hivyo basi uamuzi wa kwanza ambao makamanda wa oparesheni waliuchukua ni kutoa maagizo kwamba siku ya oparesheni, makomando wa A Company ya 1 PARA watabeba silaha na vichache kuliko ambavyo ilikuwa imepangwa awali. Yaani kwamba watabeba bunduki, risasi za akiba, maji na bandeji chache na dawa za kutibu majeraha. Walichokuwa wanakiona ni kwamba kama makomando wa 1 PARA watabeba begi za vita, silaha nzito na vitu vinginevyo watachoka mapema kuzingatia kiwango cha juu cha joto kilichopo.


Mwanzoni wazo hili liliungwa mkono, lakini baada ya kutafakari sana ulionekana umuhimu wa A Company kubeba kila kitu ambacho kilipangwa awali wawe nacho wakati wa utekelezaji wa oparesheni.


Baada ya kufanya uchunguzi wa kina zaidi kuhusu eneo ambalo wataenda kufanya oparesheni waikja kung’amua kwamba muda wa asubuhi hali ya hew inakuwa na baridi ya kuridhisha sana maeneo yote yanayozunguka mto Rokel ikiwemo vijiji vya Mgbeni na Gberi Bana. Kwa hiyo baada ya makamanda wote kujadiliana kwa kina walikubaliana kuwa badala ya kupunguza silaha na vifaa ambavyo vitabebwa na makomando wa A Company, badala yake oparesheni itekelezwe asubuhi sana mapema muda ambao hali ya hewa inakuwa ni ya kuridhisha zaidi, kwa maana ya kwamba joto linakuwa chini kabisa.


Siku zilipokuwa zinakaribia kwa ajili ya utekelezaji wa oparesheni, Mkurugenzi wa Vikosi vya Jeshi vya Weledi (Director of Special Forces), Brigedia John Holmes aliwasili kwa siri kubwa mjini Freetown akiwa ameambatana na Commanding officer wa 22 SAS, commanding officer wa D Squadron na maafisa watatu wa Jeshi la Anga la Uingereza kitengo za Technical Communications.


DSF, Brigedia John Holmes alifikia nyumba iitwayo Seaview, iliyoko karibu kabisa na makao makuu ya jeshi la Uingereza hapo mjini Freetown.


Tukumbuke kwenye sehemu iliyopita nilieleza kuhusu makomando wanne wa SAS ambao walipenyezwa kwa siri kwa kutumia boti ya SBS kupitia mto Rokel, makomando wawili kila upande wa mto. Makomando hawa muda wote huu mapaka sasa bado walikuwa bado msituni pembezoni mwa vijiji vya Mgbeni na Gberi Bana wakiendelea kufuatilia nyendo zote za wapiganaji wa West Side Boys. Nyendo zote hizi walizokuwa wanazichunguza walikuwa wanawasiliana na wenzao na kuwapa taarifa.




Kwa hiyo DSF, Brigedia John Holmes alipowasili Freetown moja kwa moja akafanya kikao kwa njia ya mawasiliano ya kimtandao kati yake, wale makomando wa SAS msituni, makamanda wa SAS na 1 PARA amabo wanafanya maandalizi kule Hasting pamoja na COBRA. Lengo la kikao hiki ni kufanya tathimini kama kuliwa na utayari na uhalisia wa kutoa ruhusa ya kufanyika kwa oaparesheni.



ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog