Search This Blog

Saturday 24 December 2022

OPERATION BARRAS - 5

  http://pseudepigraphas.blogspot.com/2020/06/operation-barras.html

Simulizi :  Operation Barras

Sehemu Ya Tano (5)




COBRA ni nini?


Japokuwa kwa uhalisi wake inapswa kuitwa COBR lakini watu wamezoea kuita COBRA. Cabinet Office Briefing Room.


Hii nieleze kwa kifupi sana… kama kutakuwa na ulazima wa kuiandikia basi nitapokea maoni.


Hizi ni sehemu za siri sana ambazo vinafanyika vikao vya siri mno vya kamati mahususi kwa ajili ya kukabiliana na suala fualni la kiusalama la kitaifa au kimataifa dhidi ya nchi ya Uingereza.


Muundo wa kamati inayokutana mahali hapa inategemea na tishio husika la kiusalama… yaani kwamba kamati inayokutana inabadilika kutokana na tishio ambalo Uingereza wanakabilina nalo. Yaani kwamba wahudhuriaji ni wale ambao watakuwa na ‘input’ fulani kuhusu hatua stahiki ambazo zinapaswa kuchukuliwa ili kukabiliana na suala husika ambalo linakuwa linajadiliwa. Lakini mara zote kikao cha kamati hii kinakuwa chini ya uenyekiti wa Waziri Mkuu wa Uingereza au Waziri wa ngazi ya juu muandamizi.


Kwa hiyo ninaposema DSF, Brigedia John Holmes kwenye kikao chake kwa kutumia mawasiliano ya kimtandao pia walikuwepo COBRA hiki ndicho ambachi nina maanisha.




Wakati huo huo…


Timu ya negotiators walikuwa wanaendelea ‘kuwapoteza maboya’ West Side Boys na kuwafanya wajiamini kupitiliza. Labda ni kutokana na matumizi yaliyopitiliza ya mihadarati au labda ni haiba yao tu ya ujivuni na kujiamini kupitiliza… West Side Boys walikuwa wanongeza masharti kila uchwao.


Kwa mfano, siku ya Septemba 9… moja ya viongozi wa West Side Boys liyejiita “Kanali Cambodia” alitoa sharti jipya la kiwendawazimu kabisa safari hii. Alisema kwamba ili waweze kuwaachia wanajeshi 6 wa Uingereza walikuwa wanataka kuundwa kwa serikali mpya ya Sierra Leon ambayo nao watakuwa sehemu ya serikali hiyo.

Kwa namna yoyote ilesharti hili lilikuwa halitekelezeki. Hii ilikuwa inadhihirisha wazi kabisa kwamba hakukuwa na namna ambayo suala hili litaishia mezani kutokana na tabia ya ujivuni na haiba ya kuishi nje ya uhalisia ambayo West Side Boys walikuwa wanaionyesha.




Pia…


Wale makomando wanne wa SAS amabo walikuwa misituni karibu na vijiji Mgbeni na Gberi Bana ambao walikuwa wanafuatilia nyendo za West Side Boys waliripoti kwamba hawajawaona wanajeshi wao 6 waliotekwa kwa muda wa siku nne zilizopita.


Pia walisema kuwa walikuwa wanaona kama vile kuna nyendo zinazoashiria West SIDe Boys walikuwa wanataka kuhama kutoka kwenye vijiji hivyo na kuingia ndani zaidi ya msitu na kama hili litatokea basi wanaweza kuua wanajeshi hao mateka au kuwahamisha sehemu za ndani kabisa ya msitu ambako itakuwa vigumu zaidi kufanya uokozi.


Baada ya taarifa zote hizi mbili… ilikuwa dhahiri kwamba oparesheni ilikuwa inatakiwa kufanyika haraka iwezekanavyo.


COBRA wakamshinikiza Waziri mkuu wa kipindi hicho, Tony Blair kuhusu umuhimu wa Oparesheni hiyo kufanyika haraka iwezekanavyo na Tony Blair akatoa kibali kwa oparesheni kufanyika.


DSF, Brigedia John Holmes pia alifanya mazungumzo na Rais wa Sierra Leon Ahmad Kabbah na kupata kibali kutoka kwake juu ya opareshini hiyo. Kisha kwa kushirikiana na Army Legal Corps akafanya mazungumzo na viongozi wa juu wa jeshi la Sierra Leon na kupewa Baraka zao.


Baada ya oparesheni kupata ‘go ahead’ kutoka kila sehemu stahiki, Luteni Kanali Fordham yule ambaye alikuwa anaongoza timu ya negotiators alimpigia simu kiongozi wa West Side Boys, ‘Brigedia’ Foday Kallay na kumueleza kuwa wako tayari kutekeleza masharti yao lakini kabla ya kufanya hivyo alikuwa anataka uhakika kama wanajeshi wao wote sita wako hai.


Foday bila kuelewa mtego ambao alikuwa amewekewa… akaweka kwenye simu wanajeshi wote sita wanaowashikilia mateka wakamsalimia Luteni Kanali Fordham mmoja mmoja.


Wasiwasi walioupata baa ya makomando wa SAS walioko kule msituni kutowaona wanajeshi wao waliotekwa kwa siku nne na kudhani labda wameshauwawa ulikuwa umesawazishwa. Watu wao walikuwa hai… lakini hawatakuwa hai kwa muda mrefu kama hawatafanya kitu upesi…


DSF, Brigedia John Holmes akatoa idhini ya mwisho kwa vikopsi vya 22 SAS na A company ya 1 PARA… kwamba siku ya tarehe 10 alfajiri sana kabla hata jua kuonesha dalili ya kuchomoza wanapswa kutekeleza oparesheni.


Kwenye medani ya vita wanasema… ”MISSION IS A GO!!”


Kijijini Mgbeni


Chinook ya tatu iliruka moja kwa moja mpaka kijijini Mgbeni ikiwa imebeba nusu ya makomando wa A Company ya 1 PARA.


Helikopta ilitua nje kidogo ya kijiji mahala ambapo palipendekezwa na ile Observation Team ya SAS.


Katika mapendekezo yao kuhusu hii ‘landing zote’ walieleza kwamba sehemu hii licha ya kiwa ndio bora zaidi kwa ajili ya kutua lakini ina hali fulani hivi kama vile matope matope.


Kwa bahati mbaya sana walikuwa wameshindwa kukadiria ni kiasi gani cha matope kilikuwa katika eneo hili. Hii ilisababisha baada ya makomando wa A Company kushuka sehemu hii kwa mtindo ule ule wa ‘fast roping’ kujikuta wako ndani ya tope linalofika karibia na kifua na kuwafanya washindwe kuondoka kwa haraka kutoka eneo hili.


Idadi kubwa ya makomando walijivuta na kutoka ndani ya tope na kuanza kuelekea kijijini, lakini makomando wachache ambao walipewa jukumu la kulinda eneo hili la kutua iliwalazimu wabakie ndani ya tope.


Chinook ilipokuwa inarejea mara ya pili ili kuleta nusu ya pili ya makomando wa ACompany ilishitukizwa kwa kushambuliwa kwa risasi mfululizo kutoka kwa wapiganaji wa West Side Boys. Ili lazimu helicopter nyungine Lynx Attack Helikopta ipite kijijini Mgbeni kufanya ‘strafing’ kama ambavyo ilifanywa kule Gberi Bana.


Strafing ilifanyika mpaka walipohakikisha kuwa hakukuwa na mfululizo wowote wa risasi kutoka kwa wapiganajivwa West Side Boys ndipo ambapo Chinook ilirudi tena sehemu ile yenye tope na kushusha nusu ya pili ya makomando.


Baada ya nusu hii ya pili kutua ardhini kwa mtindo ule ule wa fast roping na kuungana na nusu ile ya kwanza moja kwa moja kwa haraka wakaanza kuingia kijijini Mgbeni.


Bahati mbaya nyingine ikatokea. Kuna mfululizo wa mabomu yalikuwa yanarushwa kutoka kwenye helicopter ile ambayo ilikuwa inafanya ‘strafing’ mara ya kwanza, safari hii ikifanya hivyo ili kuzuia wapiganaji wa West Side Boys wasitoe upinzani mkubwa kwa makomando wa A Company. Bahati mbaya sana moja ya mabomu ambayo yalikuwa yanaelekezwa upande wa Were Side Boys lilitua karibu kabisa na makomando wa A Company waliokuwa wanaingia kijijini Mgbeni kwa kasi na kusababisha makomando saba kujeruhiwa akiwepo Mathews Lowe, kamanda wao.


Tukumbuke kuwa kule kijijini Gberi Bana ambako makomando wa SAS walikuwa wametua muda mchache nyuma nako kulikuwa na majeruhi, komando Bradley Tinnions alikiwa amedunguliwa mara tu baada ya kutua ardhini kutoka kwenye Chinook.


Kwa kulikuwa na Chinook nyingine ambayo ilikuwa inarandaranda mahususi kabisa kwa ajili ya kutua muda wowote kuchukua mateka kama wakifanikiwa kuokolewa.


Ilibidi wawasiliane na hii Chinook ili iweze kutua na kuchukua majeruhi haraka ili oparesheni iweze kuendelea.


Baada ya majeruhi kuondolewa, akiwemo kamanda wao Matthew Lowe, oparesheni kijijini Mgbeni iliendelea ikiwa chini ya komando Danny Matthews ambaye ndiye walikuwa 2IC (Second In Command).


Baada ya majeruhi kuondolewa, 2IC Matthews aliwagawanya makomando wote katika platoons ambazo kila moja walikuwa na jukumu la kushambulia jengo mahususi kama ambavyo walikuwa wamefanya mazoezi kwenye kijiji walichokitengeneza Hastings kufanana kabisa na hiki cha Mgbeni.


Ndani ya dakika chache walifanikiwa kuliteka jengo la silaha la wapiganaji wa West Side Boys. Baada ya hapo kila platoon iliendelea kushambulia jengo lao mahususi ambapo walikuwa wamepangiwa.


Kila mpiganaji wa West Side Boys ambaye alijisalimisha aliwekwa chini ya ulinzi na kufungwa kamba. Wale wote ambao walileta upinzani au kutaka kupambana walitandikwa risasi bila huruma.


Baada ya kuhakikisha kuwa ‘wamesafisha’ majengo yote na hakuna tishio, makomando wachache walielekea kwenye msitu wa karibu kuwasaka wapiganaji ambao walikuwa wamekimbilia huko.




Wale waliosalia hapa walikaa katika mtindo ambao walikuwa kana kwamba wamezunguka kijiji chote ili kujihami na shambulio lolote kutoka nje.


Baada ya kukamata na kuua wapiganaji wote wa West Side Boys ambao walikiwa wamejificha msituni, makomando wa A Company walipanda ‘viazi’ (mabomu ya ardhini) kuzunguka eneo lote la kuingilia kijijini hapo.


Mpaka kufika majira ya saa mbili asubuhi, A Company walikuwa wameikiweka kijiji cha Mbeni mikononi mwao na kilikuwa salama.


Majira haya ya saa mbili asubuhi walianza hatua ya pili ya oparesheni yao.


Kwanza walichoma moto majengo yote na kuharibi silaha zote za West Side Boys pamoja na magari yao.

Tukumbuke kuwa siku ile ambapo wale wanajeshi wa Uingereza walitekwa, walitekwa pamoja na gari zao Land Rover za kijeshi (tazama Picha). A Company walipewa jukumu la kuhalikisha kuwa gari hizi nazo zinaokolewa na kurejeshwa kwenye jeshi la uingereza.


Kwa hiyo land rover hizi, zilifungwa kwamba katika mtindo maalumu na kisha ikapigwa simu zije kubebwa na Chinook (tazama Picha).


Baada ya zoezi lote kijijini Mgbeni kukamilika, makomando wa mwisho waliondoka hapo mnamo majira ya saa nane mchana.




Kijijini Gberi Bana


Makomando wa SAS walifanikiwa kumpandisha kwenye Chinook mwenzao Bradley Tinnions salama kabisa bila na moja kwa moja akapelekwa kwenye meli ya kijeshi iliyoko katika pwani ya afrika magharibi.


Tofauti na matarajio, makomando wa SAS walipoanza tu kushambulia kijiji cha Gberi Bana wapiganaji wengi wa West Side Boys walijisalimisha akiwemo kiongozi wao Foday Kallay.


Mara moja wakati wakomando wachache wakiwaweka chini ya ulinzi wapiganaji walijisalimisha na kuwafunga kamba na huku wakiwatandika risasi wale ambao walikuwa wanajaribu kukimbilia msituni, makomando wengine kwa haraka walielekea kwenye jengo ambalo mateka wanajeshi wa Uingereza walikuwa wanashikiliwa na kuwaondoa mara moja.


Luteni Musa Bangura alikuwa amewekwa mahala pengine peke yake. Walimkuta amefunikwa kwenye shimo ambalo lilikuwa linatumiwa na West Side Boys kumwaga mikojo na kinyesi.

Alikuwa amedhoofu afya yake kupitiliza na alikuwa ana majeraha mwili mzima kutokana na baadae kubainika kuwa West Side Boys walikuwa na desturi ya kumtoa shimoni na kumpa mateso kila baada ya siku kadhaa.


Mara moja Chinook iliwasili kuwachukua wale wanajeshi sita waliotekwa pamoja na luteni Bangura na kupelekwa kwenye hospitali ya dharura ya kijeshi iliyoko kwenye meli ya kijeshi bahari ya afrika magharibi.


Wale mateka raia wa Sierra Leon nao pia waliokolewa lakini wao jeshi walitumia tahadhari ya ziada katika kuwaokoa. Makomando wa SAS walikuwa wanahisi labda kulikuwa na uwezekano wa baadhi ya wapiganaji wa West Side Boys kujichanganya na raia mateka ili kujinusuru wasiuwawe. Kwa hiyo raia wote ambao walikuwa hapa kijiji cha Gberi Bana nao walifungwa kamba mikononi na kuwekwa chini ya ulinzi mkali na kusafirishwa kwa Chinook mpaka kwenye kambi ya wanajeshi wa nchi ya Jordna waliomo nchini humu kama sehemu ya majeshi ya umoja wa Mataifa kulinda amani mchini Sierra Leon (UNAMSIL).


Lengo la kuwapeleka hapa ni kuwafanyia mahojiano ya kina mmoja mmoja ili kuhakikisha kuwa hakuna wapiganaji wa West Side Boys ambao walikuwa wamejichanganya humu.


Baada ya hapa, makomando wa SAS walifanya kama kile ambacho kilifanywa kule kijijini Mgbeni na A Company. Walifanya msako msituni na kukamata wapiganaji wote wa West Side Boys ambao walikuwa wamekimbilia huko. Walijisalimisha walifungwa kamba mikononi na kurudishwa kijijini, na wale ambao walileta upinzani walitandikwa risasi.


Kisha wapiganaji wote wa West Side Boys nao wakasafirishwa kwa Chinook wakiwa chini ya ulinzi mkali kutoka hapa Kijijini Gberi Bana mpaka kambi ya UNAMSIL ya wanajeshi wa Jordan.



MWISHO


0 comments:

Post a Comment

Blog