Search This Blog

Tuesday 20 December 2022

TUKIO LA UJAMBAZI LILILOFANIKIWA ZAIDI, KUSISIMUA NA KUUSHANGAZA ULIMWENGU - 4

   


http://pseudepigraphas.blogspot.com/2020/06/tukio-la-ujambazi-lililofanikiwa-zaidi_10.html

Simulizi : Tukio La Ujambazi Lililofanikiwa Zaidi,  Kusisimua Na Kuushangaza Ulimwengu 

Sehemu Ya Nne (4)



Shughuli ikabaki kwenye kufungua mlango kwa kutumia funguo.! Funguo iliyokuwa inatumika hapo sio kama funguo hii ya kuweka mfukoni.. Ilikuwa ni funguo kubwa yenye size sawa na mguu wa binadamu!

Sasa ilikuwa ni zamu ya The king of keys kufanya miujiza yake... Kumbuka kuna kifaa chao kile kilichopo kwenye fire extinguisher kinachorekodi kila kinachoendelea kwenye vault kwahiyo kabla ya siku hii ya tukio walikuwa na Picha halisi ya funguo ya mlango ilikuwa inafananaje.. Kwahiyo alichokifanya The king of chains ni kutengeneza funguo inayofanana kabisa na ile funguo halisi.. Lakini kabla hawajaijaribu hii funguo yao ya bandia The king of keys akawaeleza kuwa kwenye zile Picha za video walizonazo aligundua kitu kuwa kabla mlinzi hajafungua mlango ilikuwa lazima aende kwenye chumba kilichopo karibia na hiyo vault na The king of keys alitaka kujua alikuwa anaenda kufanya nini.. The king of keys alipoenda katika chumba kili hakuamini alichokikuta, ulikuwa ni uzembe wa kiulinzi ambao hakuutegemea utokee Antwerp.. Funguo halisi ya kufungua mlango wa vault ilikuwa imewekwa pale inaning'inia.

The king of keys alichukua funguo halisi akarudi kwenye vault na kuwasisitiza wenzake kuwa angeoenda watumie funguo ile halisi.. Kwahiyo wakachomeka funguo na kuizungusha kisha wakazungusha ringi (usukani) wa mlango wa vault na mlango ukafunguka bila hiyana.. Kwahiyo kwa nje ya vault walikuwa wamepita vizingiti vyote na kikibakia geti la Chuma lililopo baada ya mlango.. Geti hili ni mageti fulani hivi yanayotumika kwenye vault nyingi lenyewe linakuwa lina nondo dizaini kama madirisha yetu uswahilini ya nondo na mbao tofauti tu ni kwamba hili lilikuwa ni nondo na chuma pekee hakuna mbao.. Kwakuwa tayari walikuwa wamedisable kifaa cha kumonitor hili geti (pale ukutani unapoingiza tarakimu nne) kwahiyo hapa wakatumia nguvu tu kuliharibu na kuingia ndani..


Kwahiyo kwa walikuwa wamefanikiwa kupita matabaka yote ya ulinzi nje ya vault na wakibakiwa na matabaka machache ya ulinzi ndani ya vault ambayo ni Kamera ya ulinzi, sensor ya mwanga (light sensor) na sensor ya mjongeo na joto (heat & motion sensor)




#2


NDANI YA VAULT..


Baada ya ya kufanikiwa kufungua mlango wa vault kwa mafanikio kabisa sasa changamoto ilibaki ndani ya vault kukabiliana na matabaka matatu ya ulinzi kabla ya kuanza kufungua visanduku vya vilivyohifadhi almasi ambavyo navyo vilihitaji funguo na namba za siri..


Kumbuka kuwa siku moja kabla Natarbartolo alikuwa amepulizia hair spray kifaa cha kuhisi joto na motion! Lakini ile spray ingesaidia labda kwa dakika tano tu kama mtu angeingia na baada ya hapo ingeweza kuhisi kuna mabadiliko ya joto.. Kwahiyo kama wote watatu wangeingia maana yake labda kwa dakika moja au mbili za mwanzo isingehisi kitu lakini baada ya hapo ingeling'amua kuwa kuna mabadiliko makubwa ya joto.. Hivyo badi ilikuwa inatakwa mtu mmoja tu aingie na aweze kudisable system nzima ya zile alarm na hapo ndipo ilikuwa zamu ya The monster ambaye alikuwa ni mtaalamu wa umeme na mekanika (mechanics) kufanya miujiza yake..


The monster alitembea hatua kumi na moja mpaka katikati ya vault kama ambavyo alikuwa amefanya mazoezi kwa takribani miezi mitank kwenye replica waliyokuwa nayo nyumbani.. Baada ya kufika katikati ya vault aliinua mikono juu kugisa dari la vault ambalo hapo juu kulikuwa na kiboksi cha umeme ambaco chenyewe ndicho kilikuwa kinakusanya electric pulse kutoka kwenye vifaa vyote vya ulinzi ndani ya vault na kupeleka kwenye system ya alarm.. Yaani kwa mfano kama light sensor ikihisi kuna mwanga kwenye vault basi itatuma electric pulse mpaka kwenye kifaa hiki na chenyewe kitatuma taarifa juu kwenye system ya alarm na alarm italia..


Kwahiyo alichokifanya The monster ni kufungua mfuniko wa kifaa hiki kisha akazichuna plastiki ya juu inayofunika nyaya na hatimae zile nyaya zikawa wazi, kisha akachukua kipande cha nyaya alichokuja nacho na kufunga kwa ustadi kuunganisha nyaya hizo na kutengeneza 'bridge' ya umeme (alikuwa anafanya 



    0 comments:

    Post a Comment

    Blog