Search This Blog

Tuesday 20 December 2022

TUKIO LA UJAMBAZI LILILOFANIKIWA ZAIDI, KUSISIMUA NA KUUSHANGAZA ULIMWENGU - 5

   


http://pseudepigraphas.blogspot.com/2020/06/tukio-la-ujambazi-lililofanikiwa-zaidi_10.html

Simulizi : Tukio La Ujambazi Lililofanikiwa Zaidi,  Kusisimua Na Kuushangaza Ulimwengu 

Sehemu Ya Tano (5)

reroute) naamini watu wa umeme na fizikia watelewa vizuri..

Kwahiyo baada ya kufanya hii reroute ilimaanisha kwamba umeme uliokuwa unatoka kwenye alarm system unaishia hapo kwenye 'bridge' na kurudi nyuma na umeme uliokuwa unatoka kwenye vifaa vya ulinzi ulikuwa hauvuki hiyo bridge!! Kwa kifupi ni kwamba mawasiliano kati ya alarm system na vifaa vya ulinzi yalikuwa hayapo hivyo haikujalisha nini kilikuwa kinatokea ndani ya vault, alarm system isingeweza kudetect..


Baada ya hapo wote wakaingia ndani na kuanza kazi ya kufungua visanduku vidogo vilivyopo ukutani vilivyokuwa na almasi.. Walitumia drill ambayo ilitengenezwa na The king of keys nyumbani.! Kwa kila kisanduku walitumia kama dakika tatu kukidrill mpaka kufunguka hivyo mpaka mida ya saa kumi na moja alfajiri walifanikiwa kufungua visanduku 109 kati ya 120 vilivyopo ndani ya ile vault.. Ili kuogopwa kukutwa na watu maana kitongoji cha Antwerp kuanzia majira ya saa kumi na mbili na nusu mitaa inaanza kufurika watu! Kwahiyo wakajiridhisha kuwa wana mali ya kutosha wakabeba mzigo wao wakatokomea..




#3


WIKI CHACHE BAADE..


Natarbatolo alikamatwa wiki chache baadae kwa kuhusika na tukio hili!

Kukamatwa kwake kulikuwa ni kwa kizembe mno, walitupa taka taka za vifaa vyao vya maandalizi nje kidogo ya mji wa Antwerp na walipuuzia kuzichoma moto wakiamini hakuna mtu atakayeziona.. Katika takataka hizo pia kulikwa na kipande cha Sandwich ambacho Natarbartolo alikibakisha alipokuwa anakula.. Polisi walitumia kipande hicho cha sandwich kupima DNA na kukuta inamatch na DNA ya Natarbartlo..



MAMBO YENYE UTATA MPAKA LEO HII


Kuna vitu kadhaa ambavyo mpaka leo havitapata majibu sahihi..


i) yule myahudi aliyempa dili Notarbartolo ni nani?? Kuna watu wanadai kuwa Natarbartolo anajificha identity ya huyu mtu kwasababu inawezekana ni mpwa wake Benedetto Capizzi ambaye mwaka 2003 aliteuliwa kuwa Capo dei capi, ambacho ni cheo cha juu kabisa katika mtandao wa kihalifu wa Sicilian Mafia..

Natarbartolo anakataa kabisa mpwa wake kuhusika katika tukio hili..


ii) Natarbartolo anadai kuwa wao wenyewe waliingizwa mkenge na yule myahudi kwasababu anahisi kuwa yule myahudi na wenzake walitengeneza insurance scum ili waweze kujipatia fedha kutoka kwenye kampuni ya Bima.

Yaani iko hivi, polisi wanadai kuwa almasi iliyoibiwa zilikuwa na thamani ya dola milioni 100 lakini Natarbartolo anadai kuwa viboksi vingi wakivyovifungua ndani vault vilikuwa havuna kitu kana kwamba watu waliambiws wasiweke alamsi siku hiyo.. Natarbartolo anadai kuwa almasi walizozikuta zilikuwa na thamani isiyozidi dola milioni 20.!! Natarbatolo anahisi kuwa yule myahudi alipanga dili na wenzake wamshawishi aende akaibe lakini siku moja kabla yule myahudi na wenzake wengi wakatoa almasi kwenye vault, kwahiyo baada ya tukio lile la wizi watu wote wenye visanduku kwenye vault wataenda kulipwa na kampuni ya bima lakini huku almasi zao zikiwa ziko nyumbani wamezificha kwani walizitoa siku moja kabla ya tukio! Kwahiyo wanakuwa wamepata hela ya bima na almasi zao wanazo..


iii) Hizi almasi zilizoibiwa hazijapatikana mpaka leo, na hazijulikani ziko wapi licha ya Natarbattolo kukamatwa..



MWISHO




    0 comments:

    Post a Comment

    Blog