Search This Blog

Tuesday 20 December 2022

D.B. COOPER TUKIO HALISI LA KUSISIMUA LILILOGEUKA HADITHI YA 'ALFU LELA ULELA' - 4

   


http://pseudepigraphas.blogspot.com/2020/06/db-cooper-tukio-halisi-la-kusisimua_10.html


Simulizi :  D.b. Cooper Tukio Halisi La Kusisimua  Lililogeuka Hadithi Ya 'alfu Lela Ulela'

Sehemu Ya Nne (4)


Mtoto wa miaka 8 aliyeitwa Brian Igram akiwa kwenye vacation na familia yake kwenye beach ya mto Columbia alikuwa akichimba chini ili kusaidia familia kuwasha moto waote. Igram alikuwa akichimba kwa mikono kama watoto wafanyavyo na akachimba shimo refu kiasi na akiwa anachimba alikutana na makaratasi. Baada ya kuyatoa hayo makaratasi kutoka kwenye shimo alilochimba wazazi wake waligundua kuwa zilikuwa na vibunda vitatu vya hela.


Baada ya kuzichunguza kwa makini wazazi wakahisi kuwa inawezekana fedha hizo zinahusiana na D.B Cooper tukio ambalo lilitawala kwenye vyombo vya habari kwa kipindi hicho. Hivyo basi wazazi wakawasiliana na vyombo vya ulinzi na baada ya FBI kuzisoma serial number za noti hizo wakathibitisha kuwa ni kweli noti hizo ni sehemu ya fedha alizopewa D.B Cooper mwaka 1971. Swali, je zilifikaje pale?


Hivyo basi FBI ikatumia wataalamu wake ili kupata mwanga kidogo.

Kwanza vibunda vyenyewe vya hela vilikuwa kama ifuatavyo; kila kibunda kilikuwa peke yake kinajitegemea kimoja kilikuwa na noti 100 zilizofungwa pamoja kwa rubber band isipokuwa kibunda kimoja tu ambacho kikikuwa na noti 90 lakini nazo zilifungwa pamoja kwa rubber band.


Pia licha ya kuwa noti zilikuwa zimefungwa pamoja kwa rubber band lakini zilikuwa zimekaa hovyo hovyo katika umbo la mviringo na wataalamu wa FBI wakatoa conclusion kwamba zilikuwa zimekaa hovyo hivyo kwa umbo mviringo kwasababu zilikuwa zime 'kururuka' na maji ya mto kutoka mahali fulani na kuna kunasa hapo.


Na hakika huu ndio ufafanuzi ambao angalau ulikuwa unaingia akilini.

Lakini swali linakuja; inawezekanaje vibunda vitatu vya hela ambavyo havijaungana kila kimoja kinajitegemea 'vikururuke' na maji alafu vije vyote vinase sehemu moja? Kitu kama hicho ni almost imposible.


Kutokana na kesi hii kuteka vyombo vya habari kipindi hicho kugundulika kwa noti hizi kuliteka hisia za watu na hii ikapelekea mtaalamu wa jiolojia aliyeitwa Leonard Palmer kutoka chuo kikuu cha Portland kufanya tafiti katika beach ambayo vibunda hivi vitatu vilipatikana na matokeo ya utafiti wake ndio yalishangaza zaidi FBI.


Kwanza kabisa kumbukumbu zilionyesha kuwa sehemu kubwa ya mto Columbia ikiwemo sehemu vinunda hivi vya hela vilipatikana ilifanyiwa dredging mwaka 1974. Dredging ni vile wanatumia vifaa maalum kutoa udongo chini ya mto na pembezoni mwa mto na kuumwaga kwenye beach ya mto. Kitendo hiki huwa kinafanyika ili kuongeza kingo za mto au kuboresha ubora wa beach.


Sasa basi, alichokigundua huyu mtaalamu ni kwamba katika lile shimo ambalo mtoto Igram alichimba na kukuta vinunda vya hela za Cooper chini yake kulikuwa na matabaka mawili ya udongo na ukichimba tena unakutana na tabaka la tatu ambalo lina udongo wa mfinyanzi ambao ndio udongo unaopatikana baada ya kufanya dredging. Sasa hii ina maana gani? Maana yake ni kwamba hivyo vibunda vya hela za Cooper vilikuwa deposited hapo baada ya dredging kuwa imeshafanyika. Sasa kumbuka kuwa dredging ilifanyika mwaka 1974 na tukio la Cooper likitokea mwaka 1971.


Kuna tofauti ya miaka miatatu hapo. Sasa je hivi kweli inawezekana hela zikururuke na maji miaka mitatu na kwa bahati mbaya au nzuri isiyomithilika bibunda vitatu vyote vikwame sehemu moja?


Kama hiyo haitoshi; kumbuka kuwa mtaalamu anasema kuwa chini ya shimo alilochimba mtoto Igram kulikuwa na matabaka mawili ya udongo ndipo ufikie tabaka la udongo mfinyanzi uliotokana na dredging hii inamaanisha kuwa baada ya dredging kufanyika mwaka 1974 ilipita miaka kadhaa amabapo yale matabaka mawili mengine yakajitengeneza kwa juu ya udongo mfinyanzi ndio hivyo vibunda vya hela za Cooper zikawa deposited hapo.


Na mtaalmu alikisia hivyo vibunda vya hela vimekuwa deposited hapo labda miaka miwili tu iliyopita. Sasa huo ulikuwa ni mwaka 1980, miaka miwili nyuma maana yake ni 1978 na kumbuka tukio la Cooper lilitokea mwaka 1971.! Kuna tofauti ya miaka saba hapo katikati. Na hili lilikuja kuungwa mkono na kikosi kazi maalum kilichoundwa baadae na FBI kilichojulikana kama Cooper Research Team kuwa vibunda vya hela lazima vilikuwa deposited hapo miaka kadhaa baada ya tukio la sivyo rubber band walizozikuta vimeshikilia noti zingekuwa zimeharibika kabisa.


Ugunduzi huu uliwapa maswali na kuwachanganya zaidi FBI badala ya kuwasaidia kwasababu haiingii akilini hela zikururuke na maji miaka saba.

Kumbuka umbali kutoka mto Columbia na 'Vector 23' (njia ambayo ilipita ndege ya akina Cooper siku ya tukio) kulikuwa na umbali wa kilometa 20.


Hivyo basi hata kama maji yangekuwa yanatembea taratibu isingechukua zaidi ya dakika 40 kwa vibunda hivyo kufika hapo. Kwahiyo kwa namna yoyote ile isingewezekana kwa sehemu ya kuchukua dakika 40 itumike miaka saba, na kwa namna yeyote ile habadani haiwezekani vibunda vitatu ambavyo havijashikana vije vikwane exactly sehemj moja!


Katika ofisi ya FBI maswali na mafumbo yalikuwa mengi kuliko majibu! Hizo fedha za Cooper zimefikaje pale? Zimekuja na maji? Mtu kaziweka? Kama ni mtu kwanini aziweke pale? Je, fedha nyingine ziko wapi? Kwnini vibunda viwili vina noti 100 kila kimoja na kibunda kimoja kina noti 90 tu? Noti kumi zimeenda wapi? Na hii inatoa clue gani kuhusu D.B Cooper?


Baada ya miaka sita ya kitendawili kuhusu fedha zilizookotwa zimetoka wapi hatimaye mwaka 1986 FBI ikanyoosha mikono juu na kusalimu amri kuwa fedha hizo zilizookotwa haziwezi kuwasaidia kumpata Cooper. Hivyo basi wakafikia makubaliano ya kuziganya fedha. FBI wenyewe wakachukia noti 14 kama kidhibiti na noti zilizobaki zikagawanywa kwa kijana Igram aliyeziokota na nyingine wakapewa kampuni ya Bima waliowalipa fidia Northwest Orient Airlines.

Igram aliziuza kiasi kidogo cha baadhi ya noti zake mwaka 2008 katika mnada wa hadhara kwa thamani ya Dola 37,000.


Mpaka leo hii noti nyingine zilizobakia ambazo Cooper alipewa mwaka 1971 (takribani noti elfu tisa na mia saba) hazijulikani zilipo.


SAIKOLOJIA YA MKAKATI WA COOPER


Baada ya miaka mingi ya upelelezi na kujiuliza maswali mengi hatimae mwaka 2007 FBI walitangaza kwa umma baadhi ya mambo waliyoyabaini katika mkasa mzima wa D.B Cooper.


Kwa mfano siku ya tukio Cooper alihitaji parashuti moja tu ili aweze kuruka lakini aliwaagiza kuwa anahitaji maparashuti manne. FBI wanaamini kuwa Cooper alitoa maagizo ya dizaini hii ili kupandikiza wazo kwa vichwani mwa maofisa wa FBI kuwa kulikuwa na uwezekano akaruka na mateka ambao watatumia maparashuti mengine matatu yaliyobaki. Hii iliwalazimu FBI kumpatia maparashuti manne ambayo hayana hitilafu au ubovu wowote. Na iliwachukua muda sana kubaini kuwa Cooper alicheza na akili zao bila wao kujua.


Pia uchaguzi wa kuiteka Northwest Orient Flight 305 haukuwa wa bahati mbaya. FBI wanaamini kuwa Cooper alifanya uchunguzi wa kina na kuchagua kuiteka ndege hiyo. Kumbuka kuwa Orient Flight 305 ilikuwa ni aina ya ndege ya Boeing 727.


Kwa kipindi hicho Boeing 727 ndio zilikuwa ndege pekee ambazo zilikuwa na uwezo wa kufunguliwa mlango wa nyuma mkiani ikiwa bado iko angani. Kitu hiki kilikuwa hakijulikani kwa raia na hata watu wa ndege wenyewe walikuwa hawafahamu jambo hili.



    0 comments:

    Post a Comment

    Blog