Search This Blog

Tuesday 20 December 2022

D.B. COOPER TUKIO HALISI LA KUSISIMUA LILILOGEUKA HADITHI YA 'ALFU LELA ULELA' - 5

   


http://pseudepigraphas.blogspot.com/2020/06/db-cooper-tukio-halisi-la-kusisimua_10.html


Simulizi :  D.b. Cooper Tukio Halisi La Kusisimua  Lililogeuka Hadithi Ya 'alfu Lela Ulela'

Sehemu Ya Tano (5)


Na taarifa hii ilifichwa kwasababu kwa kipindi hiki haikuwa kitu cha kawaida kwa ndege ya abiria kuwa na ubunifu wa aina hii.

Watu pekee ambao walikuwa wanafahamu suala hili na kuwahi kutumia advantage ya ubunifu huu walikuwa ni CIA ambao walitumia ndege kama hii kudondosha mizigo na maafisa wao katika maeneo husika katika vita ya Vietnam.


Pia injini za Boeing 727 zilikuwa juu kidogo tofauti na ndege nyingine za abiria ambazo injini zake zilikuwa chini chini karibia usawa wa madirisha. Kumbuka kuwa injini ya ndege ikiwashwa ikiwa inazunguka kitu chochote kikipita mbele yake kinavutwa na kumezwa kwenye injini na kuharibiwa au injini yenyewe kupata hitilafu. Hivyo basi uchaguzi wa kuruka kutoka kwenye Boeing 727 ilimaanisha kuwa ilipunguza hatari ya mrukaji kuvutwa na kumezwa na injini.


Pia FBI wanaamini kuwa Cooper alifahamu kuwa Boeing 727 ilikuwa na teknolojia mpya ambayo iliruhusu kujaza mafuta kwenye matanki matatu ya ndege kwa kutumia tundu moja tu. Kama isingekuwa na teknolojia hiyo hiyo ya kujaza mafuta kwa tundu moja tu FBI wangeweza kutumia mwanya wa gari la kujazia mafuta likiwa linazunguka upande mwingine wa ndege kupenyeza maafisa wao.


Pia Boeing 727 ilitoa advantage nyingine katika ufunguaji wa mlango wa nyuma wa ya mkia wa ndege ambapo ukiwasha tu kifaa cha kufungua mlango huo hata rubani aliye mbele hawezi kuufunga. FBI wanaamini Cooper alilifahamu hili ndio maana baada ya kuwafungia watu aliobaki nao kwenye chumba cha rubani. Alifungua mlango wa nyuma kwa kujiamini na kuruka.


Pia Boeing 727 ilikuwa na ubunifu mwingine adhimu tofauti na ndege nyingine kwa kuwa ilikuwa unaweza kucontrol speed na mwinuko wa ndege 'manually' hata ukiwa katika sehemu ya kukaa abiria, pia kwa kipindi hicho Boeing 727 ndio ilikuwa ndege pekee ya abiria ambayo ilikuwa na uwezo wa kugeuza mabawa yake ili yakae katika nyuzi 15.


FBI wanaamini kuwa Cooper alifanya utafiti wa kina na kuweka mkakati kabambe kabla ya kutekeleza tukio na alitumia advantage zote hizi za ndege ya Boeing 727 ili kutekeleza tukio lake kwa ukamilifu wa 100%.


Lakini jambo lingine la muhimu zaidi ilikuwa ni uchaguzi wa siku ya tukio. November 24.


Kwanini? Baada ya tukio FBI kugundua Cooper alikuwa ameruka nyikani wazo mojawapo ambalo walilipata ni kwamba kwakuwa sehemu aliyoruka ilikuwa mbali mno na makazi ya watu, hivyo basi ingemchukua Cooper takribani siku hata tatu kusafriri ili kurudi mtaani.


Kwahiyo FBI walidhani kwa kuwa Cooper asingeliwezakutumia siku moja kusafiri kurudi mtaani hivyo basi kama kesho yake wangembelea kila ofisi na maeneo ya kazi kukusanya orodha ya watu ambao hawajatokea kazini lazima watu hao mmoja wao angekuwa ni Cooper.


Lakini hii ilikuwa haiwezekani! Kwanini? Kwasababu November 24 usiku wake ulikuwa ni sikukuu ya 'Thanks giving' maana yake ni kwamba kesho yake haikuwa siku ya kazi. Mbaya zaidi November 24, 1971 ilikuwa ni siku ya Jumatano kwahiyo kesho yake alhamisi pamoja na ijumaa zilikuwa siku za sikuu na siku zilizofuata zilikuwa ni weekend. Kwahiyo hii ilimpa Cooper siku nne za kutosha kabisa kusafiri kutoka nyikani mpaka mtaani. Na kama alikuwa mfanyakazi ofisi fulani maana yake Jumatatu aliingia ofisini kama watu wengine! FBI wakapiga saluti.


"MAISHA BAADA YA TUKIO LA D.B COPPER"


Baada ya tukio la utekaji la Cooper kutokea na FBI kuonekana dhahiri kuwa wameshindwa kufikia mwisho wa kutengua kitendawili cha tukio hili hali ilikuwa tete katika viwanja vya ndege na kusababisha marekebisho mengi ya protokali za ulinzi na utoaji huduma katika viwanja vya ndege nchini marekani.

Kwanza kabisa serikali ya marekani ilitilia mkazo uanzishwaji upya na kuboresha programu ya maaskari wanaosindikiza ndege za abiria (Sky Marshal Program).


Pia serikali ilichukua hatua kali zaidi kwa mara ya kwanza kabisa kuanzisha mpango wa kupekua mizigo ya abiria kabla hawajapanda kwenye ndege. Hatua hii ilisababisha mvutano mkali kati ya wananchi wa marekani na serikali yao katika miaka ya sabini ambapo ilifikia hatua kesi za kikatiba zilifunguliwa dhidi ya serikali ya marekani kwa madai ya kwamba kupekua mizigo ya abiria ilikuwa inavunja Kipengele/Marekebisho ya Nne ya katiba ya marekani (Fourth Amendment) kipengele kinachomlinda raia wa marekani dhidi ya upekuzi na kuingiliwa faragha yake. Lakini mwishoni serikali ilishinda kesi hizi na tangu hapo imekuwa ni jambo la lazima kwa mizigo kukaguliwa kabla ya abiria kupanda ndege.


Si hivyo tu, serikaki kupitoa idara ya usafiri wa anga nchini marekani (FAA) ikaenda mbali zaidi kwa kuzitaka kampuni zote za usafiri wa anga zinazotumia ndege aina ya Boeing 727 wafunge kifaa maalum cha kuzuia mlango wa nyuma mkiani mwa ndege kufunguka pindi ndege ikiwa angani. Kifaa hiki kilipewa jina 'Cooper Vane'.


Na pia FAA walitoa maagizo kuwa ndege zote ziwekwe matundu maalum ya kuchungulia (peepholes) katika mlango wa chumba cha marubani ili kuwawezesha waweze kuona kinachoendelea upande wa abiria.


Pia, mwaka 2013 Earl Cossey mmliki wa kituo cha kufundisha Skydiving sehemu ambapo maparashuti manne yaliazimwa na FBI na kumpa Cooper mwaka 1971 alikutwa ameuawa nyumbani kwake. Bw. Cossey alikuwa ameajiriwa na FBI mara tu baada ya tukio la Cooper akiwa kama mshauri muelekezi (consultant) katika juhudi za kumtafuta Cooper na alihusika katika hatua zote za upelelezi.


Ziko nadharia nyingi zinazoamini kuwa vyombo vya usalama vya marekani vinahusika katika kifo cha Cossey na watu wanadhani kuwa kuna jambo la siri ambalo alikuja kulibaini katika upelelezi huo wa tukio la Cooper na FBI walihofia labda Bw. Cossey asingeliweza kutunza siri hiyo, hivyo basi suluhisho jepesi wakaona ni kumwondosha.


Hatimaye..


Mwezi July mwaka huu 2016 tarehe 14, shirika la upelelezi la FBI walifunga jalada la kesi ya Cooper na kukivunja kikosi kazi maalum cha kuchunguza tukio la Cooper (Cooper Research Team) kwa madai kuwa haukukuwa na tumaini lolote la kufikia hitimisho katika upelelezi huo.


Walifunga jalada wakiwa bado hawafahamu kama Cooper yuko hai au ameshafariki, hawajui kama hilo ni jina lake halisi au la kubuni, hawafahamu fedha alizopewa zimekwenda wapi na wala hawafahamu ni namna gani binadamu mmoja alifanikiwa kutekeleza tukio kwa usahihi wa asilimia mia moja kama tukio hili.


Tukio la Utekaji la Cooper ndilo limeingia kwenye orodha ya kumbukumbu ya shirika la FBI kama kesi iliyotumia muda mrefu zaidi kufanyiwa uchunguzi (miaka 45) na tukio hili limeingia kwenye vitabu vya historia ya nchi ya marekani kama tukio pekee la utekaji wa anga (hijacking) ambalo limeshindikana kufikia hitimisho.


Kwa hivi sasa katika maeneo mbalimbali nchini marekani na hasa eneo la Airel, mjini Washington kila mwaka mwezi November watu husherehekea 'Cooper day' kukumbuka tukio hilo la kihistoria nchini marekani lilotekelezwa na binadamu mmoja peke yake ambaye kutokana na ustadi alioutumia kufanikisha azma yake amebakia kwenye vitabu vya historia, na umahiri wake umemfanya kugeuzwa kutoka kuwa binadamu wa kawaida mpaka kuwa 'binadamu wa kusadikika'! Mwenyewe alijitambulisha kama D.B Cooper!


Mwisho.


    0 comments:

    Post a Comment

    Blog