Search This Blog

Tuesday 20 December 2022

D.B. COOPER TUKIO HALISI LA KUSISIMUA LILILOGEUKA HADITHI YA 'ALFU LELA ULELA' - 3

   


http://pseudepigraphas.blogspot.com/2020/06/db-cooper-tukio-halisi-la-kusisimua_10.html


Simulizi :  D.b. Cooper Tukio Halisi La Kusisimua  Lililogeuka Hadithi Ya 'alfu Lela Ulela'

Sehemu Ya Tatu (3)



Na baada ya kubaini ili eneo ambalo Cooper alitua, walibaini pia kuwa siku ya tukio eneo hili lilikuwa na mvua kali na kimbunga! Hivyo basi ukizingatia kuwa Cooper aliruka ndege ikiwa umbali wa futi 10,000 kutoka ardhini na siku ilikuwa na mvua kubwa iliyoambatana na kimbu na pia ilikuwa ni usiku wa giza totoro wakakubaliana kuwa hakukuwa na uwezekano wa Cooper kutua akiwa hai.


Pia walizingatia sababu nyingine kuwa kumbuka siku ya tukio Cooper aliletewa maparashuti ya kijeshi alafu akayakataa akadai apewe parushuti nne za kawaida na FBI wakenda kwenye kituo cha kufundisha skydiving na wakampatia. Sasa kwenye yale maparashuti manne, mawili yalikuwa kwa ajili ya kufundishia tu darasani na mawili ndio yalikuwa hasa yanaweza kutumika kuruka angani.


Kitu cha ajabu ni kwamba FBI wlikuja kugundua kuwa Cooper aliyaacha yale maparashuti mawili ambayo ndio yanayopaswa kutumia kurukia na na akaruka na yale mawili ya kufundishia darsani ambapo parashuti moja walidhani kuwa alivaa yeye na lingine alifunga begi la fedha.


Kwahiyo kama ilivyoelezwa awali kuwa siku hiyo ilikuwa na mvua kubwa na kimbunga kwahiyo FBI waliamini kuwa maparashuti hayo ya kufundishia yasingeweza kuhimili hali ya hewa ya siku hiyo na kumuwezesha Cooper kutua salama, hivyo walifanya kazi wakiwa na hisia kuwa Cooper hakutua salama.


Baada ya kubaini eneo ambalo ndilo lilikuwa na uwezekano mkubwa wa Cooper kutua, eneo ambalo lilikuwa nyikani kuzunguka mto Lewis karibu na ziwa Merwin! FBI kwa kutumia maofisa waliokuwa kwa miguu ardhini na helicopters angani wakafanya kazi ya kulikagua eneo lote hilo.


Lakini pia FBI wakatumia ndege na helicopters kukagua njia inayopitwa na ndege kutoka Seattle kwenda Rona (vector 23). Baada ya msako na upekuzi wa eneo lote hilo kwa siku kadhaa FBI hawakufanikiwa kumpata Cooper hai au amekufa, hakupata hata mabaki ya vifaa vya parashuti wala mabegi.


Pia walitumia submarine kutafuta chini ya sakafu ya Mto Lewis na Ziwa Merwin lakini kote hakukuwa na dalili ya Cooper wala mabaki ya vifaa alivyoruka navyo.


Baada ya mwaka mzima 1971 kuisha pasipo mafanikio yoyote ya kumpata kupa hai au mwili wake au hata mabaki ya vifaa alivyoruka navyo FBI ikabidi iombe msaada kutoka jeshi la marekani kusaidia msako huo. Hivyo basi jeshi la marekani wakatoa wanajeshi 200 kusaidia msako huo, pia wakapata msaada kutoka jeshi la Anga (Air force), pamoja na wanajeshi kutoka jeshi la ulinzi wa ndani ya nchi (national guard troops).


Kwa pamoja wakafanya msako wa kina zaidi katika eneo lote ambalo lilidhaniwa kuwa kuna uwezekano Cooper ndipo alipotua. Pia kampuni ya EEC ambayo inahusika na kufukua vitu vilivyozama majini (marine salvage firm), ilijitolea submarine ili kufanya msako chini ya ziwa Merwin kuona kama labda yeye Cooper au vitu alivyoruka navyo alizama umo.


Msako huu wa kina uliohusisha maafisa wa FBI, jeshi la marekani, makampuni binafsi pamoja na national guard troops ulifanyika kwa siku kumi na nane ndani ya mwezi march mwaka 1972 na pia ukafanyika tena mwezi April 1972 kwa siku kumi na nane nyingine.


Msako ulikuwa wa kina hasa kwani nukta baada ya nukta ilikaguliwa kwenye eneo lote ambalo walihisi cooper labda ametua ardhini na majini lakini mpaka msako huu unaisha ndani miezi miwili hiyo hawakufanikiwa kupata hata unywele au kipande cha nyuzi ya nguo ya Cooper au mabaki ya kitu chochote ambacho aliruka nacho siku ya tukio.


Kitendawili kikawa kigumu zaidi. Baada ya misako mingine mirefu zaidi bila mafanikio FBI ikawabidi waje na nadharia nyingine kwamba labda walikuwa wanafanya msako sehemu ambayo sio sahihi. Safari hii ikawabidi wafanye mahesabu ya kisayansi kabisa kwa kuzingatia kasi ya upepo siku ya tukio na uzito wa Cooper na mizigo aliyokuwa nayo na matokeo ya nadharia yao mpya ya mahesabu ya kisayansi ikawaambia Cooper atakuwa alidondokea eneo la kusini mashariki ya eneo walilokuwa wanafanya msako sasa. Eneo hili jipya walilolibaini kwa kuongozwa na hesabu za kisayansi lilikuwa linazunguka mto Washougul.


Hapa napo msako mkali ukafanyika kwa miezi kadhaa bila mafanikio yoyote.


Baada ya FBI kuona kuwa hakuna mafanikio yoyote katika misako yao ya maeneo ambayo walidhani labda cooper alitua ikawabidi wabadilishe nadharia yote. Sasa wakaweka nadharia mpya kuwa labda kuna uwezekano Cooper alitua salama salimini na yuko mtaani anatumbua hela zake.


Hivyo basi kwa kuwa FBI walizipiga picha noti moja moja ya fedha zote alizopewa Cooper (kumbuka walimpa noti 10,000 za dola 20). Kwahiyo walikuwa na serial number ya kila noti aliyopewa Cooper. FBI wakasambaza serial number hizi kwenye mabenki, macasino, maduka na kila sehemu ambayo fedha inatumika lengo ni kuwa kama noti hata moja ambayo Cooper alipewa itatumiaka mahali popote na kuingia kwenye mzunguko wa hela basi FBI watadetect na kutrace hiyo hela imetoka kwa nani.


Lakini wakasubiri miezi na miaka hakuna noti hata moja ambayo iliingia kwenye mzunguko wa hela.


Kitendawili kikazidi kuwa kikubwa zaidi! Kama Cooper hakufanikiwa kutua salama kwanini wameshindwa kupata mwili wake au mabaki ya vitu alivyoruka navyo ukizingatia kuwa wamefanya msako nukta baada ya nukta ya sehemu ambayo alitua. Na kama alitua salama na kuingia mtaani, kwanini hazitumii hela alizozipata maana hakuna noti hata moja kwenye mzunguko.


Fumbo hili liliwatesa FBI kwa miaka saba mpaka mwaka 1978 ambapo mwanga kidogo ulipatikana kuhusu tukio hili..


VIDHIBITI VINAFANYA FUMBO KUWA GUMU ZAIDI BADALA YA KUSAIDIA


Mwaka 1978 muwindaji mmoja aliokota kikaratasi chenye maelekezo ya namna ya kushusha mlango wa nyuma wa ndege aina ya Boeing 737 (Northwest Orient Flight 305 ilikuwa ni Boeing 727) na FBI wanaamini labda kikaratasi hiki kilidondoshwa na Cooper.. Lakini kidhibiti hiki hakikusaidia sana.


Kidhibiti ambacho kilikuwa na mchango mkubwa kwenye kuleta maswali zaidi kwa FBI kilipatikana mwaka 1980.



    0 comments:

    Post a Comment

    Blog