Search This Blog

Tuesday 20 December 2022

D.B. COOPER TUKIO HALISI LA KUSISIMUA LILILOGEUKA HADITHI YA 'ALFU LELA ULELA' - 2

  


http://pseudepigraphas.blogspot.com/2020/06/db-cooper-tukio-halisi-la-kusisimua_10.html


Simulizi :  D.b. Cooper Tukio Halisi La Kusisimua  Lililogeuka Hadithi Ya 'alfu Lela Ulela'

Sehemu Ya Pili (2)


Kama nilivyoeleza awali kutoka Portland mpaka Seattle ni safari ya nusu saa kwa ndege lakini ndege ilikaa angani taribani masaa mawili ikiwa inazunguka tu ili kusubiria kule chini mamlaka usika ziandae vitu cooper alivyohitaji.


Ndani ya masaa mawili FBI walifanikiwa kukusanya noti za dola 20 zipatazo elfu kumi (jumla dola 200,000) kutoka bank za karibu na zote wakazipiga picha! Pia walifanikiwa kupata parashuti nne kutoka katika kituo cha jeshi la anga cha Tacoma kilichopo karibu na uwanja wa ndege wa Seattle! Baada ya kumaliza kufanya maandalizi yote haya mnamo majira ya saa kumi na moja dakika ishirini na nne wakawasiliana na ndege juu kumtaarifu Cooper kuwa vitu vyake vyote alivyohitaji viko tayari.


Baada kumpa orodha ya vitu hivyo Cooper akaamuru kuwa hataki parashuti za kijeshi anataka apewe parashuti za kawaida za kiraia na FBI wakafanikiwa kuzipata kutoka katika kituo cha kufunza watu skydiving.


Robo saa baadae (saa kumi na moja dakika 39) ndege ilitua katika uwanja wa Seattle na Cooper akamuamuru rubani aisimamishe ndege sehemu pweke na yenye mwanga wa kutosha. Pia akamuamuru rubani azime taa zote ndani ya ndege ili kuepusha wadunguaji (snipers) wa FBI kufanya yao.


Baada ya ndege kusimama mtumishi mmoja wa kampuni ya Northwest Orient Airlines aliyejulikana kama Al Lee akiwa amevalia kiraia ili kuepuka kumchanganya cooper asidhani ni askari akiwa amevaa sare za uwanja wa ndege, alikabidhiwa mabegi yaliyokuwa na fedha pamoja na maparashuti.


Al Lee akaisogelea ndege na Cooper akamuamuru muhudumu mwingine ndani ya ndege binti aliyeitwa Mucklow afungue mlango mdogo wa dharura pembeni ya ndege na kupokea mabegi hayo. Na Mucklow akatii.


Baada ya Cooper kuhakikisha kuwa fedha na kila kitu alichohitaji kiko sawa sawa akawaruhusu abiria wote washuke. Pamoja na abiria alimruhusu muhudumu Schaffner pamoja na muhudumu mwingine ambaye alikuwa anaonekana kuwa na umri mkubwa. Lakini akabaki na marubani wote wawili, yule binti mwingine muhudumu aliyeitwa Macklow pamoja na fundi wa ndege.


Kisha akaamuru gari la kujaza mafuta liletwe na kuwajazia mafuta.

Wakiwa wanawajazia mafuta Cooper aliwapa maagizo marubani kuhusu anakotaka waende na jinsi ambavyo anataka wasafiri. Kwanza akawaeleza kuwa anataka wafuate njia inayoelekea Mexico City na ndege iendeshe katika speed ya km 190/hour na ndege iruke umbali wa futi 10,000 kutoka ardhini.


Pia aliwaeleza kuwa anataka waondoe mgandamizo ndani ya ndege (cabin pressure) na wakiruka matairi yabaki kana kwamba wanatua, pia mlango wa nyuma ya ndege ubakie wazi kana kwamba mizigo inapakiwa na mabawa ya ndege ya pembeni yawekwe kwenye nyuzi 15.


Baada ya majadiliano kampuni ya Northwest Orient wakakataa ombi la cooper ndege iruke ikiwa imefunguliwa mlango wa nyuma mkiani au pembeni kwa madai kuwa itahatarisha usalama lakini Cooper kwa kujiamini kabisa akawaeleza kuwa ni salama na hakutaka kubishana nao sana kwani baada ya ndege kuruka tu aliufungua mlango wa pembeni mwenyewe.


Ndege iliruka kutoka kwenye uwanja wa ndege wa Seattle mnamo majira ya saa kumi na moja dakika arobaini ikiwa na watu watank pekee, yaani Cooper, muhudumu Macklow, fundi na marubani wawili! Watu watatu yaani fundi na marubani wawili walikuwa mbele kabisa kwenye chemba/chumba cha marubani kuendeshea ndege (cockpit) na Cooper pekee na muhudumu Macklow walokuwa kwenye sehemu ya abiria.


Mara tu baada ya ndege kuruka, ndege mbili za kivita aina ya F-106 kutoka kituo cha kijeshi cha McChord Air Force Base nazo ziliruka kuifuatilia ndege iliyotekwa na Cooper na ziliruka katika namna ambayo zisingeweza kuonekana na Cooper au mtu yeyote aliyeko ndani ya ndege, ndege moja ya iliruka juu nyingine chini ya ndege ya akina Cooper.


Baada ya mda kidogo kupita Cooper ali muamuru muhudumu aende mbele kwenye chumba cha marubani na akamfungia huko pamoja na wengine na akabaki peke yake katika sehemu ya kukaa abiria.


Takribani saa mbili kamili usiku alarm ikalia mbele kwenye chumba cha marubani kuashiria kuwa kifaa cha kufungua mlango wa nyuma kwenye mkia wa ndege kimehuishwa (activated). Dakika chache baadae sehemu ya nyuma ya ndege ilitikisika kwa nguvu na kuwa kama inainuliwa juu na marubaini wakabaini kuwa mlango wa nyuma kwenye mkia wa ndege ulikuwa umefunguliwa na ili kuepusha ndege isidondoke marubani iliwalazimu waishushe ndege chini na kutua kwenye uwanja wa ndege wa Reno, Nevada takribani majira ya saa nne na robo usiku.


Baada ya ndege kutua tu maofisa wa FBI na polisi waliizunguka na kuingia ndani kufanya upekuzi na ndani ya dakika chache wakagundua D.B Cooper hakuwepo ndani ya ndege.


MSAKO WA KIHISTORIA.


Baada ya FBI kujiridhisha kuwa Cooper hakuwa ndani ya ndege nadharia pekee iliyobakia ni kuwa aliruka ndege ikiwa angani kwani baada ya kuipekua ndege walikuta paradhuti mbili hazipo. Jambo la ajabu ni kuwa marubani wa ndege za kivita zilizokuwa zinaifuatilia ndege ya akina Cooper walisema kuwa hawakuona mtu akiruka kutoka kwenye ndege wala parashuti kufunguliwa.

Baada ya kutafakari kwa kina FBI wakaamua waitengeneza upya safari kama ile ile ambayo ilitokea siku ya tukio.


Hivyo basi kwa kutumia ndege ile ile na rubani yule yule FBI walorusha ndege kutoka uwanja wa Seattle kuelekea uwanja wa Rona, ndege ikiondoka Seattle muda unaofanana kabisa na ule ambao siku ile ya utekaji ndege iliondoka Cooper akiwemo ndani.


Kitendawili kikubwa ni mahali gani hasa ndipo kulikuwa na uwekano kuwa Cooper alitua ardhini. Lakini ili waweze kujua ni wapi alitua ilikuwa ni lazima wajua ni mahali gani ndege ikiwa angani aliruka na kufungua parashuti.


Na kitendawili kingine kama ikitokea wakagundua ni mahali gani angani ambapo aliruka itawapasa kung'amua ni muda gani Cooper alitumia kuwa katika 'mdondoko huru' (free fall) kabla hajafungua parashuti! Kwasabu mda mrukaji anaotumia kuwa katika free fall kabla hajafungua parashuti 'inadetermine' mahali anapotua ardhini.


Kwahiyo baada ya FBI kurusha ndege kutoka uwanja wa Seattle kuelekea uwanja wa Rona. Kwa kuzingatia maelezo waliyoyapata kuwa ndege ilitikisika majira ya saa mbili dakika kumi na tatu hivyo basi FBI wakafikia muafaka kuwa huo ndio muda ambao Cooper alifungua mlango wa nyuma ya mkia wa ndege na kuruka! Kwahiyo FBI nao wakarusha maafisa kadhaa katika usawa ule ule wa anga na walibakia katika free fall tofauti tofauti kabla hawajafungua maparashuti! Baada ya maafisa wote kutua wakatafuta mzingo (circumference) wa eneo hilo ambalo ndio eneo pekee lililokuwa na uwezekano wa Cooper kutua siku aliporuka.


    0 comments:

    Post a Comment

    Blog