Search This Blog

Friday 18 November 2022

MZIMU UMERUDI TENA KULIPIZA KISASI - 3

 






Simulizi : Mzimu Umerudi Tena Kulipiza Kisasi
Sehemu Ya Tatu (3)


 Patrick akatoka mpaka nje na moja kwa moja akaenda mpaka uwani na kuchomoa Rand rover moja kali sana na yenye uwezo wa kwenda kwa kasi umbali mrefu bila hata kuchemka, aliwasha na kuanza kurudi nyuma taratibu mpaka sehemu yenye uwazi kisha akaigeuza na kulisogelea geti..



Mlinzi wa geti bwana Emanuel alishamwona mda mrefu sana hivyo akawahi kwenda kufungua geti kabla ya kupigiwa honi,, Patrick alipofika hapo alifunga breck na kushusha kioo,,



" Emanuel ikitokea Saida karudi bila mimi kufika mwambie asilete fujo humu ndani umenielewa?? ''

" Ndiyo nimekupata bosi ''



Patrick baada ya kujibiwa hivyo akapandisha kioo na kuipa land rover yake mafuta Huyooo!! Akapotea eneo hilo...

************************



Saida alikuwa amekaa kitandani akiyatafakari kwa kina maneno ya daktari huyo alieondoka humo ndani mda mfupi uliopita..



' Patrick umepatwa na nini mume wangu?? Mbona umekuwa hivyo lakini?? Kosa langu ni lipi usilotaka kuniambia?? Kiasi cha kufiki kunitesa namna hii?? Daaah! Ama kweli kuwa uyaone '



Ni mawazo mengi sana ya kusikitisha na kuumiza aliyokuwa nayo Mwanamama huyo, aliyafikiria kwa mda mfefu sana hatimae kwa mara ya pili machozi yalianza kumshuka mashavuni mwake..



" Mamaaa! Usilie mama yangu pole chukulia ni changamoto za kawaida tu katika maisha ''



Alikuwa ni yule nesi kama unakumbuka, kumbe hata docta lous alipotoka mle ndani yeye alibaki na Saida hakuwa anatambua uwepo wa nesi huyo humo ndani kutokana na kuwa na mawazo tele kichwani..



Hakuweza kumjibu chochote Nesi huyo zaidi ya kujiinamia tu na kuzidi kulia kwa kwikwi.. Yule nesi akamsogelea mama huyo na kuanza kum'bembeleza huku akimfuta machozi kwa kianganja chake cha mkono.. ''



" Pole sana mama angu, nakusihi usilie sana kwani kufanya hivyo ni kuhatarisha maisha yako,, tambua hii ndiyo dunia ya leo na hawa ndiyo wanaume wa sasa ''



Nesi huyo alizungumza huku akimtizama Saida usoni ambae pia hakuwa na neno lolote....



" Nikuletee chakula gani mama angu?? ''



Nesi huyo aliuliza kwa mara ya pili..



" Hapana mwanangu asante, kwa sasa hivi sijiskii kula chochote ''

" hata mazima mama?? ''

" usijali mwanangu nikihitaji nitakwambia.. ''



Nesi huyu alimtizama kwa mda mama huyo kisha akamuaga na kuondoka..



Saida alibaki katika tafakari nzito sana, alikuwa akiwaza ni njia gani aitumie ili mumewe huyo arudi katika hali yake ya zamani??



' Nimfanye nini huyu mwanaume?? Ili arudishe ule upendo wake wa zamani?? Hivi kweli ni huyu huyu Patrick nimjuaye au?? Mbona ananiumiza namna hii?? '



Yalikuwa ni maswali mengi yasiyo na majibu yaliyokuwa yakipita katika ubongo wa mwanamama huyo.. Wakati huo akiwa amejiinamia tu!



Mara kelele za mlango kufunguliwa zikamshtua, akainua kichwa kuona ni nani?? Macho yake yakakutana na nesi huyo huyo alietoka humo ndani mda si mrefu, Na sasa alikuwa amerejea huku mkononi alikuwa amebeba Themosi kubwa ya blue...



************************

Dakika thelathini zilimtosha Patrick kuwasili katika kituo cha Police Isman huku akiwa na wasi wasi mwingi sana!



Baada ya kufika cha kwanza anakutana na gari ya mkewe Saida, maswali yakazidi kumthonga kichwani maana endapo ataanza kuhojiwa kuhusu iyo ajali na mahali alipo mkewe pamoja na huduma yake kiujumla hatokuwa na jibu hata moja,



Patrick akapaki gari yake na kushuka kisha akaanza kutembea mwendo wa taratibu kuelekea ndani ya kituo hicho, wakati huo kila hatu anayopiga na mapigo ya moyo yaliongezeka pia..



" Karibu bwana Patrick ''



Mkuu wa kituo alimkaribisha Patrick baada ya kutia mguu mlangoni, nae bila kusita akaingia na moja kwa moja akaenda kuketi katika moja ya viti vilivyomo humo ndani...



" Karibu mzee wangu ''

" asante sana.. Asante sana.. ''

" za siku rafiki yangu ''

" aisee njema kabisa ndugu yangu..''

" mbona unapotea sana ndugu uko wapi siku hizi ''

" nipo.. Nipo ndugu yangu sema mizunguko ni mingi sana juzi nilikuwa mafinga hivi nimerudi jana tu! ''



Tayari Patrick alianza kutengeneza nafasi za uongo kwani ameshatambua fika wito wa hapo kituoni siyo salama.



" A'ahaa pole na majukumu ndugu yangu na pambana umaskini haunda ndugu rafiki ''

" nalijua hilo na ndiyo maana napigania... ''



" Vizuri.. Sasa ndugu yangu twende kwenye point ''



Patrick alianza kuhisi joto la mwili likianza kupanda..



" Ndugu Patrick.. ''

" ndiyo mkuu ''http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

" Nimekuita mimi hapa na bila shaka ndiyo umekuja kuripoti.. ''

" ndiyo mkuu ''

" umeiona iyo gari hapo nje?? ''

" ndiyo nimeiona ''

" bila shaka ni yako ''



Patrick akakaa kimya kwa mda akifikiria cha kumjibu..



" Hapana siyo yangu..! '' Patrick alikana gari hiyo.. Sasa sijui alikuwa na lengo gani?,, Mkuu wa kituo akamkazia macho Patrick kitendo kilichoanza kumtia uoga..



" Patrick... ''

" ndiyo mkuu.. ''

" nipo serious na hili spendi utani sawa?? ''



Mkuu wa kituo alibadilika gafla, na moja kwa moja Patrick akahisi huenda amejulikana yaani yeye mawazo yake yote yalikuwa kwa wale polisi waliomkosa kosa jana kule makonani, Patrick alishindwa kujizuia hofu kubwa ilimtawala alianza kupepesa macho huku na huko hii iliashiria ni kwa kiasi gani Patrick kachanganyikiwa..



" Niambie hiyo gari ni yako au siyo yako?? ''

" ni ya aliekuwa mke wangu ''

" ee?? ''



Taharuki ikahamia kwa mkuu wa kituo, neno " ni ya aliekuwa mke wangu " lilimchanganya, hakutaka kuamini kama watu hao ambao siku za nyuma walishirikiana katika kufuta kesi nyingi za mauaji na kumtunzia siri yake leo hii wameachana?? Hakutaka kuamini kabisa..



" Sijakuelewa hapo una maana gani?? ''

" Nimesema hiyo gari ni ya Saida mke wangu wa zamani ''

" Unataka useme umemwacha yule mwanamke?? ''

" ndiyo mkuu! ''

" kwanini sasa?? Hivi una amini utakuja kupata mke msiri na mtulivu kama yule?? ''

" Mheshimiwa sasa naona unataka kuniingilia kwenye maswala yangu ya ndani... We sema kama kuna la zaidi tulimalize ila kama kuhusu iyo gari, mimi sihusiki nayo kabisa ''



Patrick aliongea kwa kujiamini, kiasi cha kupelekea mkuu huyo wa kituo kukosa la kuongea kwa mda huo ukimya ukatawala humo ndani.. Wakati huo mkuu huyo wa kituo akitafakari cha kuongea maana mipango yake yote ya mwanzo imepanguliwa..



Je?? Mmeachana lini??



Mkuu wa kituo alimtandika Patrick swali murua kabisa, swali ambalo kwa Patrick liligeuka kitendawili maana hakuwa na jibu la haraka la kumpa kamanda huyo aliekuwa mbele yake akimtizama kwa makini sana.



" Hayo maswali siwezi kukujibu kwa maana nishakwambia hayo ni maswala yangu ya ndani mkuu! ''



Patrick alijitetea kinamna hiyo, lakini kwa upande mwingine alishanywea kabisaaa!!



" Mmeachana lini??? ''



Mkuu wa kituo alirudia tena swali hilo kwa mara ya pili ili kupima msimamo wa Patrick..



" Hivi we polisi huelewi kile nakwambia?? Ni vyema hayo maswali nikauliza mahakamani siyo hapa sawa?? Huwezi ukawa unanihoji kana kwamba wewe ni hakimu uliepewa maamuzi ya kutoa taraka umenielewa?? ''



Hatimae Patrick aliamua kumjia juu mkuu huyo wa kituo, na kwa wakati huo hakumjibu chochote alikuwa akimtizama tu! Anavyotoa povu..



" Patrick.. ''



Mkuu huyo wa kituo aliita kwa sauti ya chini huku akiwa kamtizama kwa umakini sana usoni kwake.



" Ndiyo nakusikiliza.. '' Patrick alijibu

" Hivi unapata wapi huo ujasiri wa kuropoka ujinga mbele yangu?? ''

" Lakini mk.... ''

" Ngoja kwanza!! Hivi ni mara ngapi nimekusaidia katika kesi zako za ajabu ajabu?? Na je? Mtu wa pili kukutunzia siri zako ni nani kama yule mkeo?? Unafikiri huyo mwanamke asingekuwa msiri kwa kuficha siri ambazo mimi nimekusaidia kuzitatua wewe leo ungekuwa wapi?? Kuwa na Adabu mpumbavu wewe ''



Mkuu wa kituo alizungumza maneno ambayo kwa Patrick yalikuwa ni kama msumari wa moto ndani ya kidonda kibichi, yalimchoma kweli kweli kiasi cha kushindwa kuzungumza chochote na kuishia kuinamisha kichwa chini..



Hapo ndipo mkuu huyo wa kituo kidogo cha police cha Ismani alipopata nguvu ya kuendelea kumkandamiza..



" na ukiendelea kunikoroga hakika nitafichua kesi zako zote tuone nani mjanja!! ''



Alitema mkwara!!!



" Samahani sana mkuu na usiende mbali tuishie kwenye point mkuu wangu ''

" Sasa sikia ''

" Ndiyo nakupata mkuu ''

" iyo gari si umeiona?? ''

" ndiyo naiona.. ''



" Na sisi tunatambua kuwa gari ni yako, na iyo gari imezua baraa huko makonani kiasi cha kupoteza uhai wa watu wengine pamoja na baadhi ya askari polisi ''



Patrick alipigwa na butwaa! Kwa maneno hayo moyo ulianza kumwendea mbio na asijue nini kinafuata! Na mda wote huo mkuu huyo alikuwa akimtizama usoni na kugundua tiyari jamaa kaingia kwenye kumi na nane zake..



" Sasa unasikia?? ''

" ndiyo... ''

" ukitaka usalimike katika baraa hili inatakiwa hii gari iondolewe kijanja hapa ''

" kivipi yani? Sijakuelewa hapo kamanda.. ''

" kwanza inatakiwa tuwazibe midomo wote waliopo hapa ili ifikapo saa kumi na mbili uondoke nayo hiyo gari ''

" bado sijakuelewa hapo kwenye kuwaziba midomo ''



Kabla mkuu huyo wa kituo hajaendelea, kwanza aliinua kichwa chake na kutizama maeneo yote ikiwamo nje kupitia madirishani kuona kama kuna mtu yeyote kasimama au kupita maeneo hayo.. Alipojirizisha na usalama wa eneo hilo alirudisha macho yake kwa Patrick alimtizama kwa sekunde kadhaa wakati huo Patrick kiti hakikaliki anahaha kusubili jibu kutoka kwa police huyo.



Mkuu huyo baada ya kumtizama kwa sekunde kadhaa akainua mkono wake wa kulika kisha akachezesha vidole vitatu!! Yaani dole gumba, kidole cha shahada pamoja na kile cha pili kinachofuata baadala ya kile cha shahada!! Police huyo alivichezesha vidole hivyo akiwa na maana ya mane!!! /pesa!!http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



Patrick alielewa maana nae ni mtu wa dili toka mda mrefu na katika madili mara nyingi ishara ndiyo huwa zinatumika sana baadala ya maneno! Kwani mpaka hapo Patrick kapitia dili nyingi na za hatari kama vile. Uuzaji wa madawa ya kulevya, biashara za mali za wizi, viungo vya albino, ngozi za binadamu n.k, na mara kibao amekuwa akikamatwa na vyombo vya dora lakini pia amekuwa hapewi adhabu kali kwani aliweza kushirikiana na Askari polisi huyo huyo alienae hapo kufutilia mbali kesi hizo..



Siri zote hizo Saida anazifahamu na kwa kuwa ni mwanamke msiri hajawahi kuzivujisha popote pale kwani aliamini ya kwamba hayo anayoyapitia mumewe ni mapito tu! Na ipo siku ataacha na kumrudia muumba wake.



" Ngapi mkuu tumalize chap chap kabla mambo hayajasambaa?? ''



Patrick aliuliza kwa shaukuu huku wasi wasi ukiwa umemshika mwili mzima, na anaachoomba ni wamalizane na Polisi huyo mapema ili aondoke hapo maana hapo alipo hana amani kabisa! Kwani anahisi anachokizungumzia polisi huyo ni kile alichokitenda, kumbe wala! Polisi nae alipanga lake!!



" Hapo bwana ukitoa jiwe tano nakusawazishia... '' Polisi alifunguka

" Jiwe tano?? Yaani laki tano?? ''

" Hapana ni (M) ''

" Duuuh! Mbona palefu mkuu?? ''

" Sikia ili hii Ishu isisambae inatakiwa kila mtu anaeijua alizike na alichopewa hapo utakuta kimyaa! Ila hivi hivi? Itakugharimu ''



Patrick alivuta pumzi ndefu na kisha kuishusha,, aliupa nafasi ubongo kufikiria kile alichoambiwa na Mkuu huyo wa kituo, alifikiria kwa mda wa dakika kadhaa kisha akaona ni heri atoe hiyo rushwa kuliko jambo hilo lisisambae na kumletea matatizo, Jambo ambalo hana uhakika kama ni lile analolijua yeye la kutaka kuwasababishia Askari polisi ajari au lipi?? Maana hata mkuu wa polisi kazungumza kimafumbo kwa maana tayari alishapanga kupiga pesa kwa tajiri huyo hivyo kaamua kuzusha tukio la kizushi ambalo pia kalizungumzia kimafumbo bila kulifafanua!



Patrick nae kwa kuwa ni mwoga sana katika maswala ya Pingu na vizimbani, alijikuta akikubali kutoa hongo hiyo pasipo kutaka kujua chochote....



Daaah!! Watu wanapigwa hela kizembe!!



" Nipo tayari kwa hilo ndugu yangu ili mambo yaende sawia ''

" Ayo ndiyo maneno ili hata siku nyingine tunaendelea kulindana au siyo bwana?? ''



Mkuu wa kituo aliongea huku meno yake yote 32 Yakiwa nje! Alikuwa na fulaha kubwa sana moyoni kuona mpango wake kabambe umekwenda sawia!



" Ni kweli bwana.. ''



Patrick alijibu kinyonge iyo hela ilikuwa inamuuma siyo kawaida, Hasira zote akazielekeza kwa Saida akiamini yeye ndiyo chanzo cha fimbo iyo kubwa anayokwenda kupigwa, bila kujua kuwa ujinga ni wake..



Akili ya Patrick iliganda kwa mda bila kufanya kazi, alibaki akiwa katumbua macho kama bundi aliefumaniwa na mwanga machoni pa watu..!! Maana milioni tano ni palefu siyo mchezo!!



" Ndugu yangu tunakwend na mda au unataka mpaka tushtukiwe huku ndani?? ''



Sauti hiyo ya mkuu wa kituo ilipenya vyema kabisa kunako ngoma za maskio ya Patrick na kumfanya ashtuke kutoka katika dimbwi lile kubwa la mawazo.



" A,a e..e.eeh!.. Ahaa Ok naomba akaunt namba.. ''



Patrick aliomba akaunt namba ya polisi huyo ili aweze kumhamishia kiasi hicho cha pesa kwa njia ya simu ili biashara iishe mapema!, bila hina mkuu huyo wa kituo alimtajia na Patrick akafanya muamala!! Milioni tano keshi!! Zikaingia katika akaunt ya polisi huyo..!!



" Sasa hapaaa.. Nafikiri mambo yote yamekaa sawa au kuna tatizo tena mkuu?? ''

" Mpaka hapa hakuna tatizo lolote!!...''

" Kwahiyo hapa ninachongoja ni mda ufike ili niondoke nayo? ''

" Hii hapaaa.. Hebu ngoja kwanza..''



Mkuu wa kituo Alinyanuka kitini na kumwacha Patrick hapo kisha akatoka nje! Na baada ya mda kidogo alirudi..



" Hapa ndugu mi nafikiri hii gari uondoke nayo tu! Maana watu niliokuwa nikiwahofia hawapo kwa sasa hivi wapo wachache ambao nishawapa maelekezo tayari.. ''



Akili mpya tayari alishaipanga polisi huyu, maana kama ni pesa tayari ameshapiga sasa bado nini?? Akatafuta njia ya kumtoa Patrick kijanja na korokoro lake!!



Mpaka hapo Patrick hakuwa na usemi wowote, zaidi ya kukubali kila alichokuwa akiambiwa maana mpaka hapo kachanganyikiwa kabisaa hana mbele wala nyuma!!



Basi walitoka mle ndani kisha mkuu huyo wa kituo akingîa katika stoo ya kituo hicho na kutoka akiwa kabeba chuma maarumu la kuvutia magari, Kisha akaenda kumsaidia kumfungia katika Rand rover aliyokuja nayo, baada ya hapo wakaagana na Patrick akaondoka kituoni..



' We malaya huko uliko unaona hasara uliyonitia huku??? Unaona?? Nguruwe weee!! Sasa ngoja nije utanitambua.. '



Patrick alikuwa akiongea kimoyo moyo huku akizidi kuipa gari mafuta kisawa sawa! Jamaa alikuwa amekasirika na kufura kama mbogo!!





Patrick alifika mpaka nyumbani hakika watu wote walishtuka kwa jinsi Patrick alivyokuwa kavimba, Kwanza mlinzi wake hakumsemesha chochote alimfungulia geti akapita huku nyuma akiwa anavuta na mkweche mwingine! Emanuel hatakutaka kuwa muulizaji saana kwani angeitwa mpelelezi japo rohoni ilimchonyota ila hakuwa na namna..



Patrick akaenda mpaka maegesho akapaki gari yake, wakati huo Ashura alikuwa bustanini akimtizama tu! Hata ile shughuli aliyokuwa akiifanya ya kumwagilia maua aliisitisha akabaki akimtizama Patrick aliekuwa kama mwendawazimu alianza kuzunguka zunguka hovyo pasipo na sababu maalumu,



Alizunguka zunguka weee mwishowe akaingia ndani, Ashura nae akaacha shughuli zake na kumfuata huko ndani ambako alimkuta akiwa amekaa sebleni kwenye masofa, kichwa chini mikono mashavuni..



" Baby mbona kama haupo sawa? '' Ashura aliuliza..



" Naomba uniache kwanza sipo sawa Ashura ''

" Sasa kama unanificha mimi nani mwingine wa kumwambia?? ''

" Haya ni maswala yangu ya kibinafsi naomba unielewe ''



Ashura akavuta pumzi ndefu na kuishusha kisha akamtizama Patrick kwa sekunde kadhaa kwa kuwa aligundua sababu ya mwanaume huyo kuwa katika hali ile. aliamua kuachana nae akaendelea na shughuli zake..



************************

Yule nesi alifika mpaka kitandani alipokuwa Saida kisha akafungua ule mfuniko mkubwa wa juu ya Themos ambao pia hutumika kama kikombe akamkabidhi Saida kikombe hicho, bila hiana nae alikipokea na kukishika vyema..



Yule nesi pia akafungua ule mfuniko wa pili ambao unakuwaga mdogo na wa mwisho, akawa tayari kwa kumimina kilichokuwa ndani..



" Shika vizuri kikombe hicho mama angu ''



Yule nesi aliongea nae Saida akakiweka sawa kikombe hicho na kukaza mkono, Taratibu nesi huyo akainua Themos ile na kumiminia uji mwepesi wa maziwa ndani ya kimbe hicho mpaka kikakaribia kujaa..



HIVI UNAUJUA UJI WA MAZIWA WEWE?? UNAKUWAGA MTAMU HUO! BARAA,



" Anza kunywa taratibu mama angu.. ''



Aliongea nesi huyo wakati huo anaifunga vizuri Themos hiyo ili ule uliosalia usipoe.. Saida taratibu alikipeleka kikombe hicho Kinywani na kutwaa funda moja...! mmmmh!! Alikutana na utamu usioisha hamu! Kwanza uji wenyewe haukuwa wa moto yaani ulikuwa na vuguvugu tu! Halafu jinsi ulivyomtamu sasa daaah!!



Alikunywa mpaka kikombe kikaisha kisha akamshukuru nesi huyo kwa msaada wake kwani mpaka sasa hakuna ndugu yeyote aliekuja hapo hii ni kutokana na mwanamama huyo kutokuwa na ndugu yeyote wa kueleweka zaidi ya mumewe ambae nae ndiyo ivyo tena kageuka adui..



SIKU ZIKASONGA HATIMAE WIKI IKAKATA..!



Yule Nesi ambae siku moja baada ya kupiga stori aliweza kujitambulisha kwa Saida kuwa anaitwa '' Felister '' Huyo nesi ndiye aliekuwa akimhudumia kwa kila kitu kipindi chote hicho cha wiki nzima hapo hospitalini, hatimae sasa Saida hali yake ilianza kutengemaa alianza kufanya mazoezi mepesi ya kutembea tembea mpaka nje kisha anarudi wodini, hali hiyo ilikuwa ikimfurahisha sana Felister. na aliamini kuwa hayo anayoyapitia mwanamama huyo ni mapito tu hata yeye huenda akaja kuyapitia na ndiyo maana akajitoa kumsaidia mwanamama huyo kwa moyo wake wote mpaka hali yake inakwenda kutengemaa..



Siku nazo zikazidi kusonga, Saida alianza kuyasahau yale yote aliyotendewa na mumewe alijipa imani kuwa huenda hasira zilimpitia tu, na kichwani Saida alipanga siku inayofuta arudi nyumbani kwa Suprise bila kumtaarifu..



Siku hii ilikuwa ni jumamapili moja tulivu sana ambapo hata msongamano wa watu hospitalini hapo ulikuwa ni mdogo siku hiyo, Ilikuwa ni majira ya asubuhi ndiyo jua linaanza kukomaa komaa, Saida aliinuka kitandani na kupata kifungua kinywa ambacho alikuta kimeandaliwa na Nesi Felister alikinywa baada ya kutosheka alijikongoja mpaka bafuni ambako alimkuta Felister akifua nguo huko.

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Basi wakungana kwa pamoja katika shughuli hiyo ya ufuaji huku stori za hapa na pale zikichukua nafasi yake sawia na vicheko vya furaha!



Hatimae beseni la kwanza likajaa nguo ambazo tayari zilikuwa zimeshatakata, ikabidi Felister akazianike hizo huku akimwacha Saida akiendelea kufua na kuweka kwenye beseni jingine.. Mwanamama huyu alikuwa na mikono miyepesi sana kwani hata ilo beseni halikukawia kujaa Felister aliporudi alikuta ameshalijaza tayari..



" Wapi kwa kuanika? '' Saida aliuliza..

" Huko nje '' Felister alijibu..

" Ngoja nami ninyooshe miguu nikazianike hizi we endelea kumalizia hizo.. ''

" Utaweza mama?? ''

" Naweza mwanangu ''

" Sawa sogea hapa dirishani.. ''



Saida alisogea mpaka hapo dirishani alipokuwa amesimama Felister..



" Unaziona zile kamba pale bustanini?? ''

" Ndiyo... ''

" Eheee! Ndiyo pa kuanika pale ''

" Sawa nimepaona ngoja nizipeleke... ''

" Kariri vizuri usije ukapotema mama hahaha.. ''

" Hahahaha...!! Mbona unataka kunivunja mbavu jamani khaaa!! Nipotee tena?? ''



Saida aliongea kwa furaha huku akijitwisha beseni hilo na kuanza kupiga hatu za taratibu kuelekea mlangoni...



" Haya mama hee kumbe hutaniwi ''



Felister aliongea hayo wakati huo mlango ndiyo unamalizia kujifunga Saida keshatoka! Nae bila hiana akaendelea kumalizia malizi zile nguo chache zilizokuwa zimebakia..



Saida alitoka mpaka nje, akatizama pande zote mpaka akaiona sehemu ambayo alitakiwa kwenda kuanika nguo hizo kwani sehemu hiyo ndipo palipokuwa na kamba pamoja na zile nguo alizokwenda kuanika Felister mda mchache uliopita.. Basi bila kupoteza mda akatembea mpaka hapo na kuanza kuzianika haraka haraka.



Mara akasikia muungurumo wa gari ikija, mwanzoni hakutaka kuitilia maanani gari hiyo kwani magari yanayoingia na kutoka ndani ya hospitali hii ni mengi hivyo alijua ni magari tu yanayoleta wagonjwa hospitalini hapo..



Akaendelea kuanika nguo Saida, lakini tayari moyo wake ulishaingiwa na shaka kuhusu gari hiyo, hatimae uvumilivu ukamshinda akainua kichwa na macho yake akayaelekeza iliko gari hiyo..



Paap!! Macho yake yanatua katika Land Cruiser yao moja makini sana ambayo waliinunua miezi minne iliyopita, moyo wake ukapiga kwa nguvu na kubadilisha kasi ya mapigo, Kwanza alishtuka Patrick kaja kwa lengo gani?? Ikiwa aliondoka hospitalini hapo wiki moja na siku kadhaa zilizopita tena aliondoka kwa hasira sasa leo kaja kwa lipi??



Mawazo na maswali kibao yalianza kutembea katika kichwa cha Saida na kumweka njia panda! Wakati huo gari hiyo inazidi kusogea maana ilikuwa bado iko mbali kidogo..



Sasa alipotupa macho kwa nyuma!! Ayaaaaa!! Anakutana na kisanga cha mwaka! anagundua kuwa Patrick kafunga ile VX aliyopata nayo ajari na yupo anaikokota kuja nayo hospitalini hapo.. Saida alizidi kupigwa na butwaa! Hakujua lengo la Patrick kwa mda huo,



Gari hiyo taratibu ikachepuka kuingia hospitalini hapo, Saida aliendelea kuitizama mpaka pale ilipokwenda kusimama katika geti kubwa la kuingilia Hospitalini hapo. Dakika moja mbele mlango wa Dreva ukafunguliwa na Patrick akashuka akiwa katika vazi la suti kali inayong'aa hatari..



Saida machale yakamcheza! Akahisi kitu, Aliendelea kumtizama mwanaume huyo ambapo alianza kupiga hatu za taratibu kuzunguka upande wa pili kana kwamba anakwenda kumfungulia mtu mwingine, Jambo lililomstaajabisha Saida aliekuwa akimtizama mda wote.. Alifika mpaka mlango wa pili na kuufungua..



Macho ya Saida yanashuhudia mwanadada mwenye mwili mnene kiasi na urefu wa wastani anaeng'aa kwa weupe pia nywele ndefu zilizokwenda kulala mgongoni, Akichomoza katika mlango wa upande huo hakuwa mwingi ni Ashura mtoto wa kishua!..



Moyo wa Saida ukaruka mpaka akahisi kama unataka kuchomokea mdomoni, joto la mwili lilianza kumpanda kwa kasi mpaka kupelekea jasho kuanza kumtililika mawazo ya kusalitiwa ndiyo yaliyokizonga kichwa chake kwa mda huo..



Baada ya maelezo mafupi, mlinzi wa geti hilo la Hospital hii aliweza kuwaruhusu Patrick na Ashura kuingia hospitalini hapo, Baada ya kuingia ndani ya uzio Patrick alianza kutupa macho katika bustani za Hospital hii. mara gafla macho yake yaliganda kwa mda upande wa mashariki baada ya kumwona yule aliekuwa akimfuata!, Basi bila hiana akamshika mkono Ashura kisha wote kwa Pamoja wakaanza kuelekea kule aliko Saida.



Kila hatua aliyoipiga Patrick na mapigo ya moyo wa Saida yaliongeza kasi kwani mpaka sasa hajajua lengo la mwanaume huyo ni lipi???.



Wakati wote huo Patrick na Ashura wakizipiga hatua kuelekea alipo Saida, Ashura alikuwa akiyatizama majengo ya hospital hii pamoja na watu waliokuwa wakiingia na kutoka, hivyo mpaka dakika hiyo hakuwa ameona kuwa kule mbele waendako kuna baraa, maana ake hata wanavyotoka nyumbani Patrick hakumwambia chochote hivyo kakokotwa tu kama gari bovu. Inavyoonekana huenda Ashura alizani wanakwenda gereji.. Kumbe! Pana jambo..



Macho ya Ashura yakaenda kutua juu ya paji la uso wa Saida, Ashura aliachia mshtuko wa nguvu mfano wa mtu aliegongwa na nyundo ya kichwa akiwa usingizini. Ni baada ya kutupa macho mbele wanakoenda! Uoga mwingi ukamvaa akasita na kutembea akasimama! Lakini Patrick akaendelea kumkokota!



Wakafika mpaka mahali alipokuwa amesimama Saida, mda huo mama wa watu hali yake ikiwa mbaya mpaka anahisi pumzi kutaka kumwishia!



" Habari yako mama?! ''



Sauti hiyo ya Patrick ilipenya kwa uzuri kabisa kunako ngoma za masikio ya Saida, ambapo alihisi kushikwa na tumbo mda huo! Kigugumizi kikali kikamkumba hali iliyopelekea kushindwa kujibu salamu hiyo na kubaki akiwa amewatumbulia macho wawili hao!



Patrick akaona siyo kesi salamu yake kutojibiwa kikubwa ni kukamilisha kile kilichompeleka pale, bila hiana akaingiza mkono mfukoni na kutoa karatasi iliyokunjwa vizuri sana akaitizama kwa mda kisha akanyoosha mkono wake kumpatia Saida, Saida nae akasita kuipokea asijue kuna nini ndani yake?



" Chukua zawadi yako hii.. ''



Patrick aliongeza kuongea huku akizidi kuunyosha mkono wake kwa mwanamama huyo..



Taratibu huku akitetemeka mwili mzima Saida akanyoosha mkono wake na kuipokea karatasi hiyo, haraka haraka tu akaifungua na kuanza kuisoma, wakati wote huo Patrick alikuwa akimtizama tu!



" Taalaakaaa???????!!!! ''



Saida alijikuta amepayuka kwa nguvu na kutokwa na maneno hayo huku na mengine kibao yakifuata! Ashura nae pia alishikwa na mshtuko wa ajabu kwani katika ajenda hiyo ya Patrick kwenda kudai talaka mahakamani hakushirikishwa kabisaa! Na hata hajui ni lini Patrick alikwenda mahakamani hivyo nae akabaki kinywa wazi..



" Ndiyo mama unashangaa?? ''



Patrick kwa sauti ya chiini iliyojaa zarau aliongea!, maneno ambayo kwa Saida yalikuwa machungu kama matango pori.



" Bado sijakuelewa ujue Patrick?? Ni kwani lakini mume wangu?? Kosa langu kubwa haswa ni lipi?? Na ni taraka gani hiyo ambayo umepewa pasipo mimi kushirikishwa kutoa maoni yangu?? Kwanini lakini um.....''



" Kelelee!!!! Shwain wee! Unaona gari yangu ulichoifanya?? ''

" Lakini mume wani si..... ''

" Shiii... Kwanzia sasa jina la mume kinywani mwako life umenielewa?? ''



" Patrick.....''



" Nimesema hivi.. Unaiona ile gari pale?? Imekufa kwiiisha hata mafundi wameshindwa waanzie wapi kuitengeneza, kifupi wameshindwa na wamesema uwezekano wa gari hii kupo ni mpaka Tokyo Japan, Sasa we una hiyo hela?? Kingine wakati nakwenda kuitoa kituoni nimepigwa milioni tano, na miamala hii hapa kama unabisha!!



Mpaka hapo Saida hakuwa na usemi wowote zaidi ya kumsikiliza Patrick anavyohubili hapo..



" Hivyo basi kufikia hapo nina mamlaka ya kusema mimi na wewe baaasii sawa?? Unamuona huyu?? Ndiyo kabadili nafasi yako!! ''



Mpaka hapo Saida alishindwa kujizuia machozi mengi yaliyoambatana na kamasi yepesi yalianza kumtoka kwa fujo pasipo yeye kulia..!!



" Kwaanzia hivi sasa nyumbani kwangu usitie unyayo wako tena!! Ukipona nenda kapange nawe uanze maisha yako, na iyo gari mimi nakwenda kuichoma moto sina mda wa kuhangaika nayo! ''



Patrick alipokwisha kusema hayo alimkumbatia Ashura mbele ya Saida na kumpiga busu la mdomo kisha akamshika kiuno na taratibu wakaanza kuondoka eneo hilo!



Saida alihisi kama moyo wake umetumbukizwa katika karai lenye mafuta ya moto! Maumivu aliyokuwa akiyapata hayaelezeki nguvu za kusimama zikaanza kumwishia na kuanza kuyumba yumba mfano wa mtu alielewa pombe.



***

Huku ndani nesi nae machale yakamcheza!



' Mbona haji huyu?? ' Alijiuliza Felister huku akianza kupiga hatua za haraka kuelekea nje, ebwana ee! Kufika mlangoni akatupa macho upande ule na kumshuhudia Saida akiyumba yumba huku akijitahidi kusimama lakini wapi.



Felister hakutaka kupoteza mda pale akachomoka mbiyo kali kwenda kumuokoa mama huyo ili asije akaanguka tena na hitlafu kumrudia. Akazidi kuongeza spidi lakini kule Saida hali ilishakuwa mbaya zaidi hatimae alikosa nguvu kabisa akaporomoka na kuanza kwenda chini kwa kasi. huyooooooooo!!



Akadakwa!! Daah!! Aisee halmanusura akapigize kichwa kwenye nguzo zilizofungwa kamba za kuanikia nguo!, lakini kutokana na wepesi aliokuwa nao Mwanadada huyu Felister aliweza kukimbia kwa kasi kubwa na alipofikia karibu alijirusha kwa nguvu kama kipa na kumdaka mama huyo baada ya kuona anakoenda kuangukia siyo.



" Uko salama?? ''http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



Nesi huyo alimuuliza Saida wakati huo nae mapigo ya moyo yakimwendea kwa kasi ya ajabu maana kitu alichoelekea kukishuhudia kisingefutika akilini mwake maisha yake yote.



************************

" Baby lakini mbona una maamuzi magumu kiasi hicho?? ''

" Huwa sipendi ujinga na isitoshe huyo mwanamke hazai halafu korofi yaani matatizo tu! ''

" Hazai?? ''

" Ndiyo kwani mpaka hapa ingebidi niwe na watoto ambao wanasoma vyuo vikuu ''

" Khaaa! Kwahiyo wataka kuniambia huna mtoto mpaka sasa?? ''

" Ndiyo baby nategemea wewe uje kunipatia mtoto na nitafulahi sana nakuahidi nitakupa chochote utakachotaka! ''

" Kweli?? ''

" Ndiyo nakuahidi.. ''

" Nashukuru kusikia hivyo.. ''



Yalikuwa ni maongezi kati ya Patrick na mkewe huyo mpya Ashura safari yao ikiwa imefika njia panda ya Kalenga na sasa wanaanza kuitafuta Iringa mjini, mara kwa mara Ashura alikuwa akifikiria ni kwanini mwanaume huyo kamua kumkatili mkewe kiasi hicho??



' Hivi ni kweli gari ndiyo sababu kubwa?? Au mimi?? Na je? Kama ndiyo tabia yake hii mimi ndiyo tutaishi nae?? '



Ashura alikuwa akijiuliza maswali lukuki kichwani kwake wakati huo mzee mzima Patrick akiwa bize na usukani akiipa gari mafuta kisawasawa,,



" Hivi Patrick nikuulize kitu baby?? ''

" Ndiyo upo huru wangu ''

" Hivi wakati unamuoa Saida mali hizi alikukuta nazo au? ''



Swali hilo kidogo lilimshtua Patrick lakini hakuwa na budi kudanganya ili mambo yaende sawa

" Ndiyo kwa sehemu kubwa alikuta nimechuma, kwanini umeniuliza?? ''



Patrick alijibu swali kisha tena akamtwanga swali Ashura.

" Hapana nauliza tu, inaweza kutokea mkeo akaenda mahakamani kupinga taraka iyo una habari iyo?? ''

" Hana ubavu huo nitahakikisha kesi inafutiliwa mbali. ''

" Mmh!! ''

" Mbona waguna??''

" Una maamuzi ya kiume kweli, safi na ndiyo inavyotakiwa, siyo mwanaume mzima unapandwa na mwanamke mpaka kichwani.. ''

" Umeona eee?! '' Patrick alisapoti huku meno yote 32 Yakiwa nje!!

" Ndiyo Baby napenda sana mwanaume mwenye msimamo katika mali zake ili zinufaishe familia yake ''

" Waoooh!! Safi sanaa! Mwanamke kama wewe ndiye niliekuwa namtafuta anaesapoti na kuchangia hoja safi sana!! ''

" Hahaha... Pati bwana!! Ila nami yasije kunitokea kama huyo mkeo..''

" Hapana kwako nimekufa nimeoza sitokufanyia kitu cha aina hiyo, kwanza yule mgumba nilikuwa simpendi ujue?? ''

" Kweli?? ''

" Saana yaani.. ''

" Usijali mi nitakuzalia mpaka nyumbani kwako pawe kama chekechea.. ''

" Waoooh! Nitafulahi sana,, hasa siku utakayonizalia mtoto nitakununulia Bughat mpyaa ''

" Khaah!! Acha utani.. ''

" Nakuapia si upo utaona.. ''

" Hahaha.. Ila kuwa makini tushaingia mjini hapa.. ''



Yalikuwa ni maongezi yenye fulaha na amani tele kati ya Ashura na Patrick, na sasa walishaingia changanyikeni Iringa mjini ikabidi na maongezi yao yakomee hapo ili Patrick awe makini na msongamano mkubwa uliokuwa mbele yao..

************************

Hospitalini Mambo yalikuwa siyo swari kabisa tayari Saida alishakuwa katika Hali iliyomwacha nesi wake njia panda. Kwani hakuwa akiongea Tena!!



" Saida nini tena mama angu?? Mbona ulitoka ndani mzima tu nini kimekukumba tena?? ''



Felister aliongea kwa huzuni kubwa wakati huo akijitahidi kumwinua mama huyo ili asimame vizuri kwani hajiwezi kabisaa udenda unamtoka hovyo tu mdomoni..



" Jumaaaa...! ''

" Naaam dada ''

" Nakuomba mara moja ''



Ilibidi Nesi huyo amwite mlinzi wa geti la nje katika hospital hii aje kumsaidia kum'beba ili wampeleke ndani. Chap kijana huyo mwenye kuvalia sare za mgambo aliwasili mahali hapo..



" Nakuomba tusaidiane kum'beba mama huyu tumpeleke ndani juma ''

" Poa tufanye haraka si unajua sitakiwi kutoka pale?? ''

" Dakika mbili tu, kaka angu ''

" ok mnyanyue huko.. ''



Wakamnyua ila kabla hawajaondoka.. Kuna karatasi ikadondoka mikononi mwa Saida. Nesi huyo akaiona..



" Juma ngoja kwanza... ''

" Nini tena?? ''



Hakumjibu, akamweka chini upande wa miguuni alikokuwa amem'beba kisha kwa haraka akaiokota karatasi hiyo na kuiweka katika mfuko wake wa shati, kisha wakam'beba na safari kuendelea mpaka ndani ya wodi yake ya siku zote, walim'bwaga juu ya kitanda chake kisha juma akatoka na kuwahi kwenye kibarua chake..



Felister alipomtizama vizuri Saida ayaaaa! akabaki ameduwaa asijue aanzie wapi maana hapo moja haikai wala mbili haikai yaani ni shiiidaa......



Kitu cha kwanza kukifanya Felister baada ya Saida kulazwa kwenye kitanda ni kupeleka sikio lake la kulia kifuani kwa mwanamama huyo kusikiliza mapigo ya moyo...



Ayaaaah! Moyo wa Felister ukaruka paaah!! Baada ya kukuta kimyaaa! Hee alichanganyikiwa hakujua aanzie wapi? Aishie wapi? Na leo ni siku ya jumapili hivyo kwa asilimia kubwa madaktari wengi wapo mapumziko. Wakati huo na yule mlinzi wa geti la nje Juma ameshatoka mle ndani. Nesi huyo alianza kuzunguka zunguka peke yake mle ndani na kuongea peke yake kama mwendawazimu..



Hatimae kuna wazo likamjia kichwani, hakutaka kulipotezea akatoka mle ndani kwa mwendo wa haraka haraka moja kwa moja akenda katika chumba cha dharura ambapo kuna daktari huwa anakuwapo pale masaa yote hata ikiwa ni usiku wa manane.



" Hey!! Vipi?? ''



Daktari huyo mkongwe aliuliza baada ya kuona mlango wa chumba chake kufunguliwa kwa fujo na mtu kujaa ndani pasipo hodi..



" Doctar.. Tafadhari kuna tatizo... ''



Felister aliongea huku akitetemeka mwili mzima, kijasho chembamba kikichukua nafasi yake kuanza kulowanisha gauni lako, pumzi nazo pia zikimtoka kwa fujo, hakika hata daktari mwenyewe alishtuka na kuweka kalamu yake juu ya daftari alilokuwa akililiandika, akaona haitoshi akavua na miwani kabisa..



" Umesemaje nesi??? ''



Doktar alimuuliza nesi huyo huku akimtizama usoni..



" Ndiyo kuna tatizo Doctar.. ''

" Tatizo gani tena?? ''

" Kuna mwanamama yupo wodini kule hali yake ni mbaya sana ''

" Hebu tuondoke mara moja ''



Daktari huyo mkongwe alichukua na baadhi ya vifaa vyake alivyoamini vitaweza kumsaidia katika hilo kisha wakatoka mle ndani kwa mwendo wa haraka..



Walifika mpaka katika wodi ambayo Saida alikuwa amelazwa, haraka sana dakatari huyo akavaa kifaa cha kusikilizia mapigo ya moyo masikioni mwake kisha ule upande mwingine akaugandamizia upande wa kushoto katika kifua cha mwanamama huyo na kuanza kusikiliza kwa utulivu na umakini wa hali ya juu!



Mda wote huo Felister alikuwa hatuu alikuwa akichezesha miguu mfano wa mtu anaeshambuliwa na siafu! Mda wote alikuwa akimtizama Daktari huyo kwa mashaka ya hali ya juu! Akihofia jibu atakalopewa..



' Ee! Mola simamia katika hili.. Muone mama huyu! Hastaili kufa '



Zilikuwa ni dua za nesi huyo aliekuwa akiongea kimoyomoyo huku akiwa na shaukuu kubwa ya kusikia jibu la Daktari,,



Punde si punde Daktari nae alikamirisha shughuli nzima ya upimaji, alionekana kuchoka pumzi nyingi akavuta na kuishusha kisha akakitupia pembeni kifaa alichokuwa amekivaa masikioni.



Hali hiyo ilizua taharuki kubwa kwa Felister, kigugumizi kikali kikamkumba akashindwa kunyanyua kinywa chake kumuuliza Daktari majibu ya mgonjwa huyo, akabaki akigonganisha meno tu!



" Binti.. ''



Sauti hiyo ya Daktari ilipenya vizuri kabisa katika masikio ya Felister na kumwachia msisimko wa aina yake! Mawazo yake yote akajua sasa wakati wa kupokea taarifa ya kifo cha mama huyo umefika,



" Abee.. '' aliitikia kinyonge..



" Huyu mwanamama hajafa bado ila ndiyo yupo katika hatua za mwisho mwisho, haina haja ya kuhangaika nae tena.. ''



" Nini Doctar??? Sijakuelewa ujue?? Yaani mtu bado hajafa we unasema tusihangaike nae?? ''



Felister alikuja juu baada ya kusikia Saida hajafa ila yupo katika hatua za mwisho na daktari anasema wamwache akate roho tu! Hakika uamuzi huo haukumpendeza mwanadada huyo.



" Sikiliza binti... Wewe kazi umeanza juzi sawa?? Sisi ni wakongwe wa kazi hii tumeianza mda mrefu, sasa unapokuja kupinga uamuzi wangu na kunifundisha kazi unakosea bint... ''



" Siyo kwamba nakufundisha kazi Doctar ila naona sasa unakwenda kinyume na taaruma yako, pia unakwenda kinyume na kiapo chako ulichokula kabla hujakabidhiwa rasmi kazi yako.. ''



" Kwahiyo sasa unaamua lipi maana naona unaongea maneno meengi yasiyo na point sasa amua utakavyo.. ''



Daktari huyo aliongea kwa ghadhabu kisha akatoka wodini hapo kwa hasira na kumwacha Felister akiwa ameduwaa asijue cha kufanya kwa mda huo. Maana hajajua aanzie wapi sasa kujaribu kuokoa uhai wa mwanamke huyo. Pumzi ndefu akaishusha...



' Ee mola nisaidie katika hili... '



Felister aliongea kimoyomoyo na bila kupoteza mda aliamua kupiga moyo kondo kujitolea kumsaidia mwanamama huyo, alianza kazi na sara, kwanza alichukua drip la maji na kumtundikia, baada ya hapo akachukua mashine ya OXYGEN Na kumfungia ili imsaidie kupumua kwani aliamini kapawa na mshtuko tu japo hajui chanzo ni nini??



Baada ya kuhakikisha amemfunga vizuri vifaa hivyo, alichuku Biblia na kwenda kukaa nayo pembeni na kuanza kuomba huku mara kwa mara akiyatupa macho yake kwenye drip la maji alilomtundikia mgonjwa wake na kulishuhudia jinsi maji yanavyoisha kwa kasi..



' Mmmh! Huenda na maji alikuwa ameishiwa mwilini '



Nesi huyo aliwaza hivyo na bila kupoteza mda akanyanyuka haraka na kwenda kutungua Drip la pili, haraka akianza kuliandaa Baada ya lile la mwanzo kuelekea kuisha.. Baada ya kukamilisha kuliandaa, moja kwa moja akaenda kulitoa lile la mwanzo na kumfungia jingine ambapo nalo lilianza kupungua kwa kasi ya ajabu,



Baada ya mda nalo pia likawa limebaki kidogo, Felister alichokifanya ni kumsogelea mgonjwa wake na kukita sikio kifuani kuona kama harakati zake zinazaa matunda.. Alisikiliza kwa mda mrefu kidogo, hatimae.. Kwa mbaali alianza kuyasikia mapigo ya moyo wa mwanamke huyo..



" Waoooooo!!!.. Amka mama angu amkaaa!! ''



Felister alijikuta amepayuka kwa fulaha....http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

***********************



Hatimae Ashura na Patrick waliweza kuuacha mji na msongamano kupungu, lakini licha ya hilo Patrick aliendelea kuwa kimya sana swala la Saida kupanda kizimbani na kwenda kupinga taraka hiyo lilianza kumtawala kichwani pia alianza kuingiwa na wasi wasi mwingi sana kwani tangu mwanzo anakwenda kudai taraka hiyo ambayo kwa upande mwingine tunaweza kusema ni ya bandia, hakuwa na wazo kwamba huenda Saida akaenda kuipinga mahakamani na wazo hilo alipewa na Ashura wakiwa njiani kurudi..



' Aa'aah hii inaweza ikanikost nini..?? '



Patrick alijiuliza kimoyomoyo wakati huo akikunja usukani kuiacha Barabara kuu na kuifata ile inayoelekea kunako makazi yake..



' A'h hakuna tatizo hata akifanya hivyo nitapambana nae tu.. '



Hatimae pia alijijibu mwenyewe, wakati huo akipiga honi ili mlinzi afungue geti, Bwana Emanuel mlinzi wa geti alikurupuka haraka kwenye kijibanda chake na kwenda kulifungua geti hilo, akilini mwake akijua huenda atamwona Saida maana ni siku nyingi sasa hajamwona nyumbani hapo, na kila akajalibu kumuulizia Patrick anamkuta ni mkali kama ng'e anaamu kumpotezea lakini roho inamuua vilivyo. Mama mpole na mwenye huruma kama yule leo hii asionekane kwenye mboni za macho yake? Aisee haikuwa ikimwingia akilini kabisa lakini pia hakuwa na la kufanya zaidi ya kukubali yote..



Emanuel alifunga geti baada ya Patrick kuingia, na kile alichokuwa akifikiria kuwa angemwona Saida Nayo pia ikawa ni ndoto tu!



Patrick hakwenda magesho bali aliingia na kumshusha Ashura kisha akageuza tena mpaka getini, Emanuel hakuwa ameondoka hivyo alifungua tena geti baada ya kuona bosi wake anakuja..



Patrick alipofika karibu akamwambia Mlinzi huyo apande na waondoke wote, mlinzi bila kuuliza wanakwenda wapi nae akajitosa ndani ya gari..



" Ashura funga geti hilo umesikia...?? ''

" Ndiyo mume wangu nimekusikia. ''



Baada ya kumweleza Ashura afunge geti hapo, Patrick aliludisha kichwa ndani ya gari na kuipa mafuta. Safari yao ilikuwa ni kutoka nje ya mji. Baada ya safari kama ya dakika Ishirini hivi Emanuel aliamua kumuuliza bosi wake maana anaona wanakwenda tu asipopajua!



" Eti? Boss tunaenda wapi?? ''

" Kuna kazi tunakwenda kuifanya.....''



Patrick alijibu kwa sauti fulani hivi ya kikauzu mpaka mlinzi alitishika kidogo..



" Wapi???.. '',



Emanuel alirudia swali wakati huo akianza kujenga wasi wasi juu ya safari hiyo..



" Nje ya mji wa Iringa... ?! ''

" Ee??! ''

" Ndiyo, mbona unanihoji?? ''

" A,a..ha hapana ''

" Wacha upumbavu lini nawe ukaanza kuwa na maswali ya kijinga namna hiyo?? ''

" Nisamehe bosi.. ''



Ilibidi tu Emanuel aombe msamaha kwa kosa asilolijua maana kakemewa kama mtoto mdogo, na mda huo gari inazidi kutokomea, hatimae wakaikaribia nduli, mzee mzima akakunja na kuiacha lami akaanza kufuata kijibara bara flani chakavu ambacho kilikuwa kikieleke msituni ndani ndani huko.. Eee!! Mlinzi akazidi kuogopa kwani kila akimtizama Patrick usoni anaona Dhahili anazidi kubadilika na kutisha mfano wa mwanajeshi alieuliwa familia yake.





Safari iliendelea, wakazidi kutokomea msituni zaidi, matumaini ya Emanuel kurudi salama yakatoweka moyoni mwake alianza kuhisi huenda boss wake amemhusisha kwenye tukio la kutoweka kwa mkewe Na sasa anakwenda kumuua. Emanuel hajui chochote mpaka sasa kuhusu Saida na mumewe japo anamuona Patrick anaingiza mwanamke mwingine ila hajui kama ameachana na Saida..



' Ni wapi tunakoelekea?? Na ni kwanini iwe porini?? Kuna usalama kweli?? Au boss anahisi nimemtorosha mkewe?? Sasa huku tunakokwenda anakwenda kunifanya nini?? Mmmh!! Ee mungu niokoe.. '



Yalikuwa ni maswali lukuki yasiyo na majibu kichwani mwa Emanuel mlinzi wa geti la Patrick, wakati huo gari inadhidi kutokomea msituni, Mara kadhaa Emanuel alikuwa akilitizama dirisha la mlango wa upande wake lililokuwa limeshushwa kioo, alitamani hata kuruka lakini alipotupa macho atakoenda kutulia anashuhudia majabali makubwa ya kutisha ambapo akithubutu kuruka tu! Habari yake inaishia pale.



Baadae kidogo gari ilisimamishwa, haraka Emanuel akaelekeza macho mbele na kuona sehemu yenye kijitambarare kidogo kisicho na miti wala nyasi, taratibu akayatoa macho yake huko na kuyaelekeza kwa Boss wake Patrick ambapo alishtuka kidogo baada ya kumuona akiwa kalaza uso wake juu ya usukani, Alishindwa kuelewa chochote mlinzi huyo wa geti..



" Boss.. ''



Emanuel aliamua kuvunja ukimya..



" Ndiyo Emanuel.. ''

" Kulikoni?? Mbona haupo sawa?? ''



Patrick hakumjibu wala hakuinua kichwa kwenye usukani, ila alichokifanya ni kupeleka mkono mfukoni na kutoa kiberiti, kisha mkono huo huo akaunyoosha kwa mlinzi wake..



" Chukua hiki kiberiti nenda pale kwenye ule weupe koka moto hapo.. ''

" Sawa.. ''



Emanuel akakipoke kiberiti hicho pasipo kuuliza chochote na kushuka ndani ya gari, Emanuel hakutaka kuuliza chochote kwani hata yeye haijui hatima yake hivyo yampasa tu kufuata kila agizo analopewa..



Alifika mpaka sehemu ambapo alitakika kukoka moto huo, kwanza kabla ya kuianza shughuli nzima ya ukokaji wa moto alizungusha macho kila upande kutizama usalama kwanza maana eneo lenyewe linatisha!



Alipojihakikishia kuwa usalama upo alianza kazi sasa, alikusanya nyasi pamoja na makuni ya nguvu kisha akakoka moto wa adabu!



Patrick baada ya kuona mlinzi wake kakamilisha agizo lake nae aliwasha gari na kuanza kulisogelea eneo hilo..



Sasa Emanuel ndipo alipokuja kugutuka kuwa Patrick tangu asubuhi alipoifunga ile gari mbovu na kuondoka nayo, hatimae aliludi nayo lakini pia waliondoka nayo mpaka katika msitu huo..



' Huyu jamaa mbona simwelewi?? Hili gari bovu ambalo nilizani anakwenda nalo gereji mbona karudi nalo?? Halafu tena tumekuja nalo huku mbona anazunguka nalo tu???... '



Maswali kibao yaliyokosa majibu yalimiminika katika kichwa cha mlinzi huyo wa geti na kumfanya aduwae kwa mda mpaka pale aliposhtuliwa na honi..



" Pi..piiiiii...!! ''

" Naam... Naam bosi..! ''



Emanuel aliitika kwa nguvu huku akihaha!!



" Njoo hapa mara moja.. ''

" Nimefika bosi.. ''

" Zunguka huko nyuma ifungue gari iyo.. ''

" Sawa.. ''



Haraka Emanuel akazunguka upande wa nyuma pale yalipofunganishwa magari hayo na kuanza kufungua haraka haraka wakati huo moto unazidi kushika kuni kisawa sawa!



" Tayari Boss... ''



Emanuel alimjuza boss wake kuwa tayari ameshafungua huko nyuma, Patrick nae bila kupoteza mda akaingiza gia na kuiondoa land cruiser yake mahali hapo na kwenda kuipaki mbali na eneo hilo kisha ye akashuka na kuja mpaka eneo hilo, Mlinzi wa geti lake alikuwa akimtizama tu asielewe chochote.



" Kazi yenyewe niliyokuletea huku ni hii hapa... Tusaidiane kulisukumia gari hili motoni.. ''



Emanuel alishtuka lakini hakutaka kuleta uzembe, moja kwa moja aliungana na Boss wake na kuanza kulisukuma gari hilo kwa nguvu kulisogeza motoni, wakati huo moto umeshika kasi ya hatari unaambiwa mpaka matawi ya miti yanaanza kudaka juu!



Juhudi zao zilizaa matunda robo ya gari kwa upande mbele ilishaingia motoni na mpaka hapo hawakuweza kuendelea tena kulisukuma kwani hata wao joto liliwazidia na kuanza kuungua, hivyo waliliachia hapo..



" Haraka tuondoke eneo hili ndani ya gari kuna dumu la petroli sasa hivi inalipuka... ''



Patrick alimwambia Emanuel, na bila kupoteza mda wakatimua mbio kali na kwenda kupanda katika Rand cruiser waliyokuja na kisha kwa kasi ya ajabu Patrick akaiondoa eneo hilo kama upepo!



Dakika tano mbali, mlipuko mkubwa ulisikika nyuma yao walipotizama kupitia vioo vya pembeni (Site mirror) waliona moto mkubwa wa kutisha ukianza kuuteketeza msitu ule mkubwa uliokuwa karibu na gari hiyo...



Patrick akazidi kuipa gari mafuta ipasavyo mpaka wakaikamata nduli na kuunga barabara kuu ya lami itokayo dodoma! Hapo sasa ndipo Emanuel alipokishuhudia kichaa cha bosi wake, kwani mwendo aliokuwa akitembea nao ulikuwa ni wa hatari..!! Mpaka Emanuel alishindwa kutizama mbele na kuinamisha kichwa chini kama kondoo! Kwa maana mbele hakutizamiki..!!



Dakika kadhaa mbele walishawasili nyumbani kwa tajiri huyo! Patrick alipiga honi, geti likafunguliwa na mkewe mpya Ashura.. Gafla wanaume wote wawili waliokuwamo ndani ya gari hiyo yaani Patrick na mlinzi walipigwa na butwaa! Na kubaki macho yakiwa yamewatoka pima mfano wa mijusi baada ya kumshuhudia Ashura akiwa katika vazi la ajabu huku maungo yake kwa asilimia kubwa yakiwa nje.. Ikichangia na alivyoumbika! Mmmmmmmmh!!!!



*************************

Felister alifulahi mnoo baada ya kuyasikia mapigo ya mwanamama huyo japo yalisikika kwa mbali lakini hali hiyo kwa upande fulani ilileta matumaini kwa dada huyo..



Taratibu Felister alijongea hadi mahali alipokuwa amekaa awali huku moyoni akiwa na fulaha kubwa saana!, aliendelea kusoma biblia yake huku mara kwa mara akimtizama Saida kama kafumbua macho au la!!



Mara! Akakumbuka wakati wanaanza kum'beba Saida kule nje kuna kikaratasi alikidondosha, na yeye ndiye aliekiokota na kukiweka katika mfuko wa shati lake. Haraka akaupeleka mkono katika kijimfuko hicho kilichokuwa kifuani na kuitoa karatasi hiyo..



Akaikunjua kwa pupa kutokana na uchu wa kutaka kujua kilichondani yake, Alianza kukisoma kikaratasi hicho kwa umakini mkubwa sana huku kila mstari anaoupitia ukimwachia mstuko na maswali kibao kichwani kwake..



Mpaka anaimaliza kuisoma alijikuta akisisimka mwili mzima! Maana makosa yaliyokuwa yameandikwa humo yanayomkabili Mwanamama huyo mpaka kufikia kupewa Adhabu ya talaka, yalikuwa hayaendani kabisa na mwonekano wa mwanamama huyo.



' Inamaana huyu mama ndivyo alivyo??? Mbona mwonekano wake hauendani kabisa na haya aliyoyatenda?? Mmmh! Ama kweli hata chui anaweza kuvaa ngozi ya kondoo na asijulikane kama ni chui.... '



Alijisemea moyoni maneno hayo Felister mwishowe akahitimisha na pumzi ndeefu! Kisha akaanza kuikunja vyema karatasi hiyo na kuirudisha katika kijimfuko alipokuwa ameiweka awali.



Alishaanza kumkatia tamaa mwanamke huyo kwani katika maisha yake yote Felister huwa hapendi watu wahuni, hivyo basi tayari na Saida alishamweka katika genge la watu wahuni baada ya kuisoma taraka yake na hakuwa na mpango nae tena,



Lakini pia kwa upande mwingine alianza kutafakari...



' Hii karatasi katoa wapi?? Maana hapo tangu alivyoamka aliishia kujifunga tenge je?? Hii karatasi kaitoa wapi?? Kama ni mikononi mbona alikuwa anafua hapa?? Na mara kwa mara tenge lake lilikuwa linataka kushuka analizuia sasa hiyo karatasi alikuwa kaiweka wapi??? Au kuna watu walimpatia huko nje?? na ndiyo maana kakawia kurudi??? '



Hayo yalikuwa ni maswali mengi kwa Felister yasiyokuwa na majibu sahihi. mwishowe aliamua kujituma mwenyewe kuwa atoke mpaka kwa juma aende kumuuliza kama kuna mtu yeyote kaja ndani ya saa hilo na kuonana na mwanamama huyo pindi alipokuwa akianika nguo kule bustanini.



Baada ya kupata wazo hilo hakutaka kulaza Damu aliweka biblia yake pembeni kisha akasimama na kujiweka sawa nguo zake, kisha akaanza kuondoka wodini humo.



Sasa ile anagusa tu! Kitasa cha mlango Saida akakohoa nyuma! Haraka akageuka macho yake yakagongana na macho ya Saida aliekuwa akimtizama kwa macho malegevu yenye kujaa usingizi.



Haraka Felister akaghairi safari yake na kurudi mpaka kitandani na kukaa kitako pembeni..



" Unajiskiaje?? Mama angu?? ''



Felister aliuliza, wakati huo macho yake yakiwa juu ya paji la uso wa Saida.



" Najisikia vizuri... ''



Saida alijibu swali hilo wakati huo akijaribu kuvuta kumbukumbu ili akumbuke nini tena kilichotokea mda huo?,



Felister hakutaka tena kuendelea kumghasi kwa mda huo kwani alitambua fika Saida bado hajawa sawa. Alichokifanya ni kujongea mpaka sehemu palipokuwa na jokofu na kutoa chupa moja yenye maji ya baridi akachukua na glasi kisha akarudi mpaka kitandani..



Kabla ya kukaa akakumbuka kitu tena, Haraka akainuka na kupiga hatua za haraka mpaka ilipo swichi ya AC Akiwasha na kuikadilia kiasi inachotakiwa kupulizia, kisha akarudi mpaka kitandani.

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Tayari alimkuta Saida akiwa keshaamka tayari na maji kanywa na sasa kajiinamia tu, Felister alikaa pia. Ukimya wa mda mfupi ukatawala mahali pale..



" Hivi una tatizo gani mama??? ''



Felister aliuliza, swali lililotegua kimya kifupi kilichokuwa kimetawala mle wodini..



" Maisha tu mwanangu.. ''

" Hebu niele, huenda nikawa msaada kwako.. ''



Saida alikaa kimya kwa mda akifikiria cha kumjibu dada huyo, hatimae alianza kujisachi kana kwamba anatafuta kitu, Felister alikuwa akimtizama tu!



" Hivi kuna karatasi utakuwa umeniokotea bint yangu??? ''



Swali hilo la Saida likamfanya Felister kuupeleka mkono wake mpaka kifuani mahali alipoiweka karasi hiyo ya taraka kwani aliamini moja kwa moja ndiyo inayotafutwa na Saida.



" Ni hii??.. ''



Felister alimuuliza huku akimwonesha..



" Ndiyo ni hiyo ninaniomba.. ''



Bila hiana Felister alimkabidhi Saida karatasi ile, Saida alipokoea huku tayari mikono ikianza kutetemeka, Alikunjulua na kuanza kuisoma upya kwa mara ya pili.



***

Kosa kuu lililopelekea yeye kutengana na mumewe inadaiwa kuwa Alikuwa ni mwanamke mhuni, malaya na mpaka hapo alipanga kutoroka na mwanaume mwingine na wakati anaondoka, inadaiwa aliiba kiasi cha Shilingi milioni mia moja tasilimu za kitanzania. Na taraka iyo inaeleza kuwa pesa hiyo alitoweka nayo mwanaume baada ya kuona wamepata ajali na Saida kuumia yeye alibahatika hakuumia na ndiyo alietoroka na pesa hiyo.



Patrick alipotakiwa kuidhibitishia mahakama kuhusu makosa hayo, alieleza kuwa mpaka mda huo Saida alikuwa hospitali na gari walilokuwa wakilitumia kutoroka lipo nyumbani kwake.



Basi mpaka kufikia hapo ikichangia na mkono wa nyuma (Rushwa) Mahakama iliweza kutoa taraka hiyo pasipo Saida kushirikishwa.

***



Saida akahitimisha kuisoma taraka hiyo kwa mara ya pili na kujihakikishia kama kile alichokisoma kule nje ndiyo kilichoandikwa kweli?? Maneno yalikuwa ni yale yale, hakukuwa na tofauti yoyote..



Machozi ya huzuni yalianza kumlenga lenga Saida kwa mbaali, mawazo mengi yakakizonga kichwa chake, moyo ukakosa utulivu! Akajutia kumwamini mwanaume huyo kiasi kile.



" Mama.. ''



Sauti hiyo nyororo ilipenya kwa ufasaha kabisa katika ngoma za masikio ya Saida na kumfanya ainue kichwa chake kumtizama bint huyo Felister..



" Binti yangu nina imani umesoma kila kitu kilichoandikwa katika karatasi hii, na labda nikuhakikishie tu, hii karatasi nimepewa mda mfupi baada ya kwenda kuanika nguo nje na.......... ''



" Hebu ngoja kwanza.. Umesema hii karatasi umepewa nje siyo?? ''

" Ndiyo.. ''

" Ni nani aliekupatia?? ''

" Mume wangu.. ''

" Ni kweli nimeisoma.. Na kwani umefanya hayo?? Huoni sasa maisha yako yanakwenda kuwa hatarini?? ''



" Mwanangu hayo yote yaliyoandikwa humo hakuna la kweli hata moja.. ''



" Hakuna la kweli hata moja??? Acha utani mama hivi unafikiri mahakama ni ya kijinga kumwazibu mtu pasipo kosa??? ''



Felister aliuliza kwa sauti kavu kidogo!!



" Kabla hujaamini hicho kilichoandikwa humo jiulize kwanza ni mahakama ya namna gani inayoweza kutoa maamuzi pasipo upande wa pili kuwepo??? ''



Saida alimzima nesi huyo kwa jibu murua lililo katika mfumo wa swali. Na mpaka hapo Felister alikosa cha kuongea..



Ngoja sasa nikusimulie kisa kidogo tu! Ambacho hata wewe ukija kuolewa usije thubutu kufanya kile nitakachokuhadithia..

--------------------------------------

SAIDA ALIELEZEA MKASA MZIMA KUHUSU MAISHA YAKE, ALIWEZA KUMWELEZA KILA KITU HAKUMFICHA CHOCHOTE NESI HUYO... MIMI SITORUDIA TENA KUKIANDIKA HAPA KISA HICHO KWANI TAYARI KIPO KATIKA SEHEMU ZILIZOPITA..

----------------------------------------

Felister alibaki kinywa wazi baada ya kuhadithiwa mkasa huo!!



" Mama hayo unayoyasema ni kweli au?? ''

" Na ndiyo maana sina mtoto mpaka leo hii.. ''

" Khaaa! Ulichukua maamuzi magumu sana ambayo malipo yake ndiyo haya.. ''

" Ni kweli yaani mpaka najuta kwanini nilimwamini mwanaume huyo kiasi kile... ''



" Pole sana mama, baadhi ya wanaume ndiyo walivyo ni kama mabeberu. Kila kundi atakaloliona lazima akafanye yake huko!!! ''



" Yaani sina usemi mpaka hapa. Akili imevurugika sina mbele wala nyuma.. ''

" Nitakusaidia usihofu mama.. ''

" Nitashukuru mwanangu na mwenyezi mungu atakubariki..

" Amina.. Sasa ngoja nikaandae chakula ee?? ''

" Sawa tangulia ngoja nivae nguo nitakuja kukusaidia ''

" Mmmmh! Mama pumzika bwana hali yako siyo nzuri.. ''

" Mi nataka kunyoosha miguu tu ''

" Sawa.. Kama unaweza hakuna tatizo.. ''



Felister alinyanyuka kitandani na kuelekea jikoni, huku nyuma tayari Saida aliingiwa na wazo fulani..



*************************

Patrick na mlinzi wake Bwana Emmanuel walidata kwa mda na kubaki wakimtizama mrembo huyo aliekuwa mbele yao. Maana alikuwa amevaa kituko mbele ya mwanaume yeyote alierijali..



Patrick alimpiga jicho la wizi mlinzi wake na kukuta hasomeki kabisaaa!. Ashura nae alibaki akiwatizama tu baada ya kufungua geti maana anaona hawaingii..



Patrick hakupendezwa na hali ile, akafungua mlango na kushuka kisha akapiga hatua za haraka mpaka alipokuwa Ashura..



" Weee! Nguo za aina hii vaa ukiwa chumbani na mimi sawa?? Huku nje huoni kama ni hatari??.. ''



" Ok samahani kwa hilo mi nilijua wenda unakuja peke yako.. ''

" Haya wahi ndani mara moja.. ''



Patrick akarudi mpaka kwenye gari...



" Nawe bwana Emmanuel,, huyu ni mke wangu sawa?? Sitofulahishwa kuona tena ukiwa unamwangalia kama ulivyokuwa ukimwangalia hapa umenielewa?? ''



" Ndiyo Boss... ''



" Na ukija kufanya ujinga wowote juu ya huyo dada halafu nikakubaini, tambua utakwenda kuchimbiwa kaburi.. ''



Emanuel alishindwa hata kujibu maana maneno anayoambiwa ni mazito mnoo! Kiasi cha kumfanya aanze kuingiwa na wasiwasi juu ya maisha yake hapo kazini..



" Shuka uendelee na kazi ''



Taratibu Emanuel akateremka garini na kumsubili Patrick aondoke ili afunge geti.



Patrick aliwasha gari yake na kuondoka huku nyuma mlinzi akafunga geti. Patrick alikwenda moja kwa moja mpaka sehemu husika na kupaki Cruiser yake, moja kwa moja akashuka na kuelekea ndani ya mjengo wake.



Alimkuta Ashura akiwa kakaa kinyonge sana, Hali ile kidogo ilimtia wasi wasi Patrick ikabidi aulize..



" Mke wangu mbona kama sikuelewi?? ''

" Ni kweli mume wangu nimepoke simu hivi punde kuwa mama yangu hali yake siyo nzuri na karudishwa tena nyang'oro.. ''

" Ufuuuuuh!! Pole kwahiyo tunafanyaje?? ''



Patrick alishusha pumzi ndefu kuondoa wasiwasi uliokuwa umejenga mwilini baada ya kujibiwa jibu tofauti na alivyokuwa akihisi.



" Hapa cha msingi natakiwa kwenda Ismani haraka iwezekanavyo.. ''

" Hakuna tatizo nitakupeleka jiandae twende.. ''



" Hapana Patrick wewe hutakiwi kwenda kule kwa maana sijakutambulisha bado na istoshe mama ni mgonjwa. Hatakiwa tena kubebeshwa mzigo mwingine wa mawazo juu yetu, kwa maana nirazima atashtuka mwanae kupata mwanaume.. ''



" kwahiyo hapo wasemaje?? ''

" Wacha niende halafu tutakuwa tukiwasiliana.. ''

" Sasa utaenda na nini?? ''

" Nitakwenda na Daladala japo nahisi nitachelewa ila hakuna jinsi.''



" Unajua kuendesha gari ili uwahi..''



Kudadek Patrick aligonga kwenye Point aliyokuwa akiitafuta kwa udi na uvumba Ashura, Mpaka alihisi msisimko wa ajabu mwilini mwake Na sasa aliona mpango wake unakwenda kutimia iwapo Patrick anakwenda kumpatia Gari aende nayo Ismani.





" Ndiyo ninajua kuendesha.. ''



Ashura alimjibu Patrick huku akiachia tabasam murua usoni mwake, jambo lililozidi kumchanganya Patrick.



" Basi nitakupatia gari yangu uende nayo ili ikuwahishe achana na adha za Daladala.. ''



Patrick alijibu, Jibu lililomwachia Ashura fulaha kubwa moyoni Fulaha ambayo alishindwa kuizuia akajikuta amekumbatia Patrick kwa nguvu! Hali iliyopelekea mengine!!

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

" Hivi Baby nikuulize kitu?? ''



Patrick aliuliza swali ambalo kwa upande fulani lilionekana ni la masikitiko fulani hivi..



" Ndiyo upo huru mume wangu.. ''



Ashura alijibu nae kwa kujifanya akifuatisha sikitiko la Patrick lakini moyoni alijibu kwa mikogo ya hali ya juu!



" Mbona kila siku hivi kwanini?? Huniamini?? Hii ni mara ya nne! Wakati taraka yule mpuuzi nishampa mbele ya macho iweje tuendelee kutumia marambo??



" Samahani kwa hilo, Ila tambua kuwa wanaume siyo wa kuwaamini haraka haraka kiasi unachofikiria wewe?? Unaweza ukanidunga mimba na kuniacha nitakuwa mgeni wa nani mimi?? ''



" Ashuuu nishakwambia kwako nimekufa nikaoza chochote ukitaka nitakupa ''



" Mmmh! Sawa ila nipatie mda zaidi kuhusu hili maana sina hata wiki tangu unichukue, kwahiyo mimi ni wako shaka ondoa.. ''



" Ashura bado sijaridhika kabisa mtoto mzuri kama wewe nitumie marambo?? Pili ninahitaji mtoto kwa udi na uvumba hebu usiwe hivyo eti?? Na tena ukinizalia nina zawadi yako spesho.. ''



" Kweli?? ''

" Ndiyo.. Sana tuu!! ''

" Basi subili nikirudi Ismani utakuja kuenjoy.. ''

" Unasema kweli Ashura?? ''

" Yea mi sina sababu ya kuendelea kukubania ikiwa unaniahidi hutonisaliti..''

" Hilo nakuapia kabisa sitolifanya kabisa Ashura ''

" Basi ondoa shaka nadhani sitokawia huko nitawahi kurudi.. ''

" Kwani unataka kwenda saizi?? ''



" Yaa hebu tizama simu yako inasema saa ngapi?? ''



Haraka Patrick akachukua simu yake na kutizama saa.



" Sasa hivi ni saa tisa na nusu.. (3:30 PM)

" Sawa wacha niwahi sasa hivi ili nikalale huko nikiona hali yake inaridhisha nitarudi kesho. ''

" Sawa jiandae uwahi basi ''



Basi Ashura akasima na kuelekea chumbani huku akimwacha Patrick katika tafakari nzito, kitu kinachomuumiza Patrick mpaka sasa ni kwamba hataki kukaa mbali na mwanadada huyo kiufupi ni kwamba tayari ameshajenga wivu juu ya mwanadada huyo.



Huku chumbani Ashura alikuwa akipiga pamba kali kali huku mda wote akiufikiria na kuuombea mpango wake kabambe usiingie dosari. Alivaa vitenge vya heshima kisha akamalizia na kujifunga kilemba cha kinafiki, baada ya kuona kakamilisha kwenye mavazi akakisogelea kioo alijitizama kwa mda kisha akaachia tabasama mwanana, Alibeba mkoba wake na kutoka mpaka sebleni.



Patrick macho yalimtoka pima kwa jinsi alivyokambwa na wivu..!



" Waaaah!!! Umependeza mke wangu!! ''

" Mhahaha!! Mbona kawaida tuu!! ''

" Weee!! Mpaka nakuonea wivu nahisi nakwenda kuibiwa... ''

" Hahaha.. Jamani hakuna kitu kama hicho ondoa shaka kabisa ''

" Sawa hebu twende nikupatie gari uwahi bado mapema.. ''



Taratibu wakaanza kutoka nje! Mpaka wanafika mlango wa nje tayari mlinzi wa geti alishawaona! Nae pia alishtuka kumwona Ashura katika hali ile kwani iliashiria alikuwa ni mtu wa safari.



' Au Saida anakuja ndiyo maana anamtoa huyu mdada nini??? '



Emanuel alijiuliza swali ambalo pia halikuwa na jibu kwake, hivyo alishia kuwasindikiza kwa macho mpaka mahali zilipopakiwa gari ndogo za kutembelea.. Macho ya mlinzi huyo yanashuhudiwa ikichomolewa " Prado '' moja kali yenye thamani ya pesa isiyopungua milioni mia moja na ishirini.. (1200,0000 Tsh ) Tasilimu za kitanzania...



" Hivi ni kweli unajua kuendesha gari wewe?? ''



Patrick alimuuliza Ashura huku akimkabidhi funguo za gari hilo.



" Tusiandikie mate wakati wino upo.. ''



Ashura alijibu huku akipokea fungu na kuzichomeka, akafunga mkanda na kuwasha gari, gia namba moja ikapangwa na gari kuondolewa sehemu ya paking. Wakafika mpaka getini mlinzi akawafungulia na kutoka..



" Ulijulia wapi kuendesha gari mke wangu??



Patrick aliuliza..



" Mwaka jana nilikuwa Dar es salaam nafanya kazi kwa mama mmoja ndiye alienifundisha na kuna mda nikawa nampeleka kazini kwake.. ''

" Oooh! Vizuri sana je? Una leseni?? ''

" Hapana.. Sijasomea mpaka niwe na leseni bali nilifundishwa tu ''



Mara wakawa wameingia barabara kuu iendayo Dodoma, na hapo ilimrazimu Patrick ashuke..



" Sasa sawa.. Wacha niteremkie hapa naa ukifika utanipigia ''

" Sawa mume wangu.. ''

" Safari njema mke wangu nakuombea urudi salama.. ''

" Asante na baiiii.. ''

" Baiiii pia.... ''



Waliagana namna hiyo kisha Ashura akaongeza gia na kukanyaga mafuta ipasavyo. Patrick nae akaanza kurudi nyumbani kwake taratiiibuu!



************************

Unaambiwa baada ya Felister kuondoka mle wodini Saida kuna wazo alilipata. Unajua ni lipi hilo?? Kwanza alijikagua mshono wake na kuona unakwenda vizuri yaani inashiria baada ya wiki mbili tena mbele atakuwa amepona kabisa..



' Nikipona lazima nikasimame kizimbani kudai haki yangu, Taraka ya namna gani hii?? Patrick kaamua kuniacha mimi?? Sasa nasemaje Hotel moja natoka nayo pale laa sivyo nitaungurumisha kesi mahakamani mpaka anishangae! Na isitoshe na siri zake nafichua nione kama hajakwenda kufia jela! '



Yaah!! Yalikuwa ni mawazo ya Mwanamama Saida ambapo anadai kuwa akipona atapanda kizimbani..!!



Daaah!! Ni shiidaaa!!



Papo hapo akakumbuka kuwa Felister alikwenda jikoni na alimwahidi kuwa anavaa nguo aende kusaidiana nae katika Swala zima la kuandaa chakula cha mchana huo, Basi alichokifanya kwanza ni kuingia bafuni kuoga maana tangu kumekucha mwili wake haujagusa maji jambo linalopelekea ahisi kwapa zinanata!!! Alioga kisha akarudi wodini na kuvaa nguo na moja kwa moja akaelekea jikoni..



Alimkuta mwanadada Felister akiwa katika heka heka za mapishi bila hiana nae akaingilia kati na kuanza kuipelekesha kazi hiyo mpute mpute! Baada ya nusu saa mbele chakula kilikuwa tayari..



" Mi nashauri tukalie wodini kwako mama au unasemaje?? ''

" Mi sina usemi mwanangu ila kule si hakuna meza?? ''

" Siyo lazima kuwe na meza, tunakwenda kukaa na kunyoosha miguu chini.. ''

" Hahahaha... We nae mbona una chekesha ''



Kicheko na sentesi ya Saida vilikuwa na mkanganyiko fulani maana ake alichopania kuongea hapo siyo hicho alichokizungumza.. Alikuwa anataka kusema.. ( We nae mbonanikumbusha mbali hivyo?? )



Yaaah! Ni kweli Ferister aliposema wangekwenda kukaa na kunyoosha miguu chini, pale pale kumbukumbu za Saida zilirudi nyuma mpaka mnano miaka ambayo yeye anaolewa na Patrick, alimkuta ni maskini wa kutupwa! Hata viti vilikuwa nadra sana! Chakula walikuwa wakilia kwenye mkeka chakavu ambapo pia huo huo ndiyo ulitumika kulalia!!



Kumbukumbu hiyo ilimzamisha Saida katika lindi kubwa la mawazo kiasi cha kupelekea kujipotea kabisaa! Ikawa Felister akiomba ampasie chombo chochote kilicho karibu nae mfano alisema...



" Mama hebu naomba sahani hiyo hapo.. ''



Sasa baadala ya kutoa sahani yeye akampa pakiti la chumvi..!! Felister alitaharuki kuona hali ile! Alimshangaa mara mbili mbili mama huyo kwa jinsi alivyojipotea!, Felister hakutaka kuamini kabisa akahisi huenda mama huyo hakusikia. Wakaendelea.....



Ikafika mda Felister akahitaji tena kijibakuli flani ambacho alikihitaji kwaajili ya kupakulia mboga, kibakuli hicho kilikuwa mikononi mwa Saida na alikuwa amekishika kama ulembo tu! Hakuna alichokuwa akikiifanya zaidi ya kuzunguka zunguka tu!



" Mama hebu naomba Kibakuli hicho nipunguzie Bamia hapa.. ''



Felister aliomba kibakuli hicho huku akimtizama mama huyo kuona kama yale ya mwanzo yangejiludia??



Tooba!!



Akaokota mwiko na kumpa! Felister akaupokea mwiko huo na kuuweka kando, kisha akamsogolea Saida na kumshika ipasavyo..



" Weweeeee!!!! ''



Felister alimpigia Saida ukelele mkali karibu na maskio yake! Saida alishtuka na kutaka kuruka ila Felister akamdhibiti na kumtuliza kifuni kwake mpaka pale Saida aliporejewa na hali yake ya kawaida..



Kwanza alimshangaa Felister kwa kuona akiwa amemkumbatia kwa nguvu mfano wa mlevi anaetaka kuleta fujo..



" Mwanangu angalia unaniumiza mshono wangu huko.. ''

" Oooh!! Mama pole sana hujaumia?? Hemu nione.. ''

" Hapana sijaumia lakini mbona ulikuwa umenikumbatia kwa nguvu namna hii kuna nini kinataka kutokea?? ''



Saida aliuliza swali ambalo pia lilimwachia Felister maswali lukuki, hakujua aanzie wapi? Au amjibu nini??





" A,a.. Unajua nani.. ' mama niliona kama unataka kuanguka hivi.. ''



Felister alichanganua akiri haraka na kupata jibu ambalo alihisi lingemwaminisha Saida. Lakini huyu ni mtu mzima bwana! Moja kwa moja akagundua kitu, Alianza kuvuta kumbukumbu ili ajue kabla ya yeye kuingia katika dimbwi hilo kubwa la mawazo walikuwa wanazungumza nini mwanzo??



Mwishowe akakumbuka!! Taratibu akakiinua kichwa chake na kumtizama Felister ambapo nae mda huo alikuwa akimtizama! Sasa wakabaki wakitizamana.



" Haya yote ni maisha.. Maisha ninayoishi leo hii ni kama Jehanamu, Sina raha, sina amani sitamani tena kuishi.. ''



Saida alijikuta akitokwa na maneno hayo bila hata kutarajia, Felister aliendelea kuzongwa na mishtuko chungu zima! Kila lililofanywa au kuzungumzwa na Saida kwake ilikuwa ni taharuki tu!



" Mamaa!! Kwanini uongee hayo?? Kwanini ujihukumu wewe mwenyewe?? Kwanini?? Achana na mawazo ya mwanaume, fanya yako tafuta pesa ya halali na uile pasipo na bughuza nadhani umenielewa vizuri mama?? ''

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

" Nakuelewa.. Lakini inauma tena sana kuona umetoa jasho lako mda mrefu halafu anakuja kulifaidi mtu mwingine baki? Kweli??? ''



" Pole mama na ninafahamu uchungu wake, ila naomba nikupe tahadhari usije ukafikiria kufanya chochote kuhusu huyo mumeo utakufa nakwambia.. ''



Felister aliongea maneno ambayo yalimchoma na kumuuzi Saida vilivyo kwani anachofikiri ndicho Felister alichomwekea tahadhari. Mpaka hapo alimwona kama amemshauri pumba tu! Hakutaka kuyatilia maanani kwanza aliyapotezea kabisa kilichobaki kichwani kwake ilikuwa ni apone akasimame kizimbani basi..



*************************
ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog