Search This Blog

Monday 19 December 2022

QUEEN MONICA (2) - 3

  



Simulizi : Queen Monica (2)
Sehemu Ya Tatu (3)

haraka.Nashindwa nikujibu nini David ila naomba ufahamu kuwa wewe ni mwanaume bora kabisa.Haihitaji nguvu kubwa kufahamu namna ulivyo mkarimu na mwenye moyo wa huruma.Pauline amenieleza mambo mengi kuhusu wewe namna unavyompenda na kujali na nimemuamini alichonieleza.Pamoja na hayo yote lakini nasikitika kukueleza David kuwa bado sina hisia zozote za mapenzi nawe.Sitaki nikudanganye David labda unipe muda zaidi wa kulitafakari jambo hili” akasema Monica David akaivua kofia yake yenye manyoya ya Simba na kujifuta jasho kichwani “ Monica sina maneno mazuri na matamu ya kuulainisha moyo wako au laiti ningekuwa na uwezo wa kuyawezesha macho yako yaweze kuona namna moyo wangu unavyoteseka juu yako ungenionea huruma na kulikubali ombi langu.Monica sihitaji unipende.Ninachohitaji mimi ni kuwa nawe tu.Nipe nafasi Monica nikuonyeshe namna ninavyokujali na kukupenda.Najua hauna mchumba bado kwa hiyo tafadhali naomba usininyime nafasi hii.Yawezekana labda unaogopa kuwa mke wa pili lakini naomba usiogope.Tutafunga ndoa halali serikalini na utakuwa mke wangu wa halali.Hakuna tatizo kwa upande wa Pauline na tayari amekwisha kuthibitishia hilo.” Akasema David akainuka na kumshika mkono Monica wakatoka katika chumba cha chakula wakaelekea sebuleni wakaketi sofani.Mapigo ya moyo wa Monica yalikuwa yanakwenda kwa kasi ya ajabu “ Monica ninapokutazama machoni najiona mimi.Ninaiona kesho yangu.Ninaiona kesho ya Congo.Kesho yangu iko juu yako Monica kwa hiyo naomba usininyime nafasi ya kuiona kesho yangu.Nikubali nikuoe Monica nikuonyeshe namna ulivyo muhimu kwangu,namna ulivyo muhimu kwa Congo .Nchi yote ya Congo itakusujudu kama malkia wao.Niruhusu nikupe nafasi hii ya kuwa malkia wa Congo kwani naamini kutokea kwako atazaliwa mtawala mpya wa Congo baada yangu kwa hiyo wewe ni mtu muhimu sana kwa nchi hii.Ufungue moyo wako Monica na niruhusu niingie kama niivyoufungua wa kwangu na kukuruhusu uingie na utawale.” David Zumo akatamka maneno yale kwa hisia kubwa akiwa ameishika mikono ya Monica.Walikuwa wamekaribiana sana na maneno yale ya David yakaonekana kumuingia . “ Kuna sauti kubwa ninaisikia ndani mwangu inaniambia nimkubali David.Tayari nimekwisha pata picha ya maisha nitakayoishi nitakapokubali kuolewa na David.Ni maisha ya kifahari mno.Hakuna mwanamke katika dunia hii ambaye hataki kuishi kama malkia.Nitapoteza kitu gani nikimkubali David hata kama bado hajaniingia moyoni mwangu? Akajiuliza Monica “ Hakuna chochote nitakachopoteza nikikubali kuolewa na David Zumo.Ngoja tu nikubali kwani nafasi kama hizi hutokea mara chache sana duniani.Imekuwa ni kama bahati imeniangukia mimi,sipaswi kufanya mzaha katika jambo hi.................” Mara Monica akaondolewa mawazoni baada ya kuhisi kitu kama mkono ukipapasa na kuyatomasa matiti yake.Alistuka sana.Hakuwahi kutomaswa matiti yake na mwanaume yeyote “ David !!! akasema na kutaka kumsukuma lakini mikono yeye nguvu ya David ikamshika bara bara “ Monica tafadhali naomba usihamaki.Nimeshindwa kuvumilia.Najua umekwisha fahamu ninachokihitaji kwako na ninafahamu hata wewe unahitaji pia jambo hili kwa hiyo naomba Monica unipe heshima hii” akasema David kwa sauti ya kubembeleza huku akihema haraka haraka.Monica akashindwa afanye nini kwani tayari David alikwisha onyesha dhamira ya wazi ya kutaka kufanya ngono.David aliendelea na kuyapapsa maungo ya Monica na kumfanya ahisi msisimko wa aina yake “ Ni mara ya kwanza ninachezewa hivi na mwanaume.Nahisi raha ya aina yake.David ananigusa katika sehemu zile ambazo zinanifanya nipagawe.oh my gosh !!.Leo nimepatikana sina ujanja tena.I have to do it.Ngoja tu nimuachie afanye kile anachokitaka lakini ukweli utabaki pale pale kuwa I’m so weak and stupid.Nimejitunza kwa kipindi kirefu lakini leo nimenasa kwenye mtego kama kinda na siwezi kujinasua.” Akawaza Monica wakati David akiendelea kumfanyia utundu wa kila aina na kumfanya atoe migumo kwa raha aliyokuwa anaipata.Alihisi kuhamishwa dunia.Alilainika na hakuweza kufumbua hata ukope. SEHEMU YA 42 DAR ES SALAAM – TANZANIA Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Ernest Mkasa alipomaliza kuzungumza na David Zumo katika simu akamgeukia Austin “Austin sasa naomba unisikilize vizuri.” Akasema Ernest.Akatulia kidogo akamtazama Austin kwa makini na kusema “ Nina kazi mbili ambazo nataka unifanyie.Kazi ya kwanza kuna mtu Fulani anaitwa Dr Marcelo amelazwa hospitali ya mtakatifu Lucia.Nataka ukamtoe hapo hospitali kwani kuna watu wanataka kumuua.Nataka atolewe kimya kimya bila ya mtu yeyote kufahamu na baada ya kumtoa utamleta hapa kwako atakaa hapa hadi hapo nitakapokupa maelekezo mengine.” Akasema Ernest na kunyamaza “ Ni nani huyo Marcelo? Nani wanataka kumuua? Akauliza Austin “ Austin umepewa kazi ya kufanya tafadhali naomba uifanye.Sihitaji maswali katika jambo hili.” Akasema Ernest “ Mheshimiwa rais ,nimekuuliza maswali hayo kwa lengo la kutaka kufahamu kwa kina kuhusu jambo hili.Nataka kufahamu ni akina nani wanaotaka kumuua na kwa nini ili ninapokwenda huko niwe tayari ninafahamu nguvu ya hao wanaotaka kumuua Marcelo.Hata hivyo unataka lini kazi hiyo ifanyike? “ Soon as possible” akajibu Ernest kwa haraka “ kama kungekuwa na uwezekano hata usiku wa leo ungeifanya kazi hiyo lakini naomba uifanye kesho.Kama kuna chochote utakachohitaji utanitaarifu” akasema Ernest “ kazi ya pili ambayo ni kubwa” akaendelea “ Kuna msichana mmoja anaitwa Monica benedict mwamsole ambaye hivi majuzi ametajwa na jarida moja kubwa la mitindo la The Face kuwa ndiye mrembo kuliko wote Afrika.Enzi za ujana wangu niliwahi kuwa na mahusiano na mwanamke mmoja ambaye ni mke wa rafiki yangu na hivi karibuni mwanamke huyo amekuja kwangu akanieleza kwamba wakati ule tukiwa katika mahusiano aliwahi kupata mimba yangu ila akanificha.Mwanamke huyo akadai kwamba Monica ni mwanangu.Hapa nilipo sina mtoto hata mmoja kwani watoto wangu wote wamekwisha tangulia mbele za haki na nilipopewa taarifa hizi nilistuka sana na sijataka kuziamini moja kwa moja kwa hiyo nataka nifanya uchunguzi wangu wa siri kubaini kama kweli Monica ni mwanangu.Ninataka kufanya kipimo cha vinasaba ambacho kitanipa jibu kama kweli Monica ni mwanangu .Jambo hili ni la siri kubwa na sitaki mtu mwingine yeyote alifahamu zaidi yako.Nimekuamini na ndiyo maana nikafanya kila lililo ndani ya uwezo wangu kuhakikisha ninatimiza masharti yako ili unifanyie kazi hii” akanyamza na baada ya muda akaendelea. “ Nataka kupata sampuli kwa siri toka kwa Monica kwa hiyo basi nataka ujenge urafiki wa karibu naye .Nataka kuutumia ukaribu huo wako na yeye kumfahamu vizuri Monica ili hata kama ikitokea akawa kweli ni mwanangu iwe rahisi kujenga mahusiano mazuri naye.” Akanyamaza tena kidogo, akaendelea “ Tukisha ipata sampuli hiyo ,kipimo kitakwenda kufanyika nje ya nchi.Sitaki kipimo kifanyike hapa nchini kwa kuogopa udanganyifu.Austin nimekukabidhi jukumu hili lote ulisimimamie wewe mwenyewe na mwisho unipatie majibu .Nakuomba ufanye kila linalowezekana kufanikisha jambo hili.Chochote utakachokihitaji katika saula hili niambie nitakupatia.Kama nimeweza kumtoa ndugu yako kifungoni China siwezi kushindwa jambo lingine lolote.kwa hiyo Austion kaa na utafakari namna utakavyoweza kulifanikisha suala hili.Narudia tena chochote utakachokihitaji katika jambo hili utakipata na yale yote niliyokuahidi kuhusu dada yako yatatekelezwa.Natumai umenielewa Austin” Ukimya ukatanda wa takribani dakika mbili kisha Austin akasema “ Nimekuelewa mheshimiwa rais.Nitakufanyia kazi yako ila nina mambo mawili ya kukwambia kabla sijafanya kazi zako” akanyamaza kidogo na kusema “ Kwanza nataka kukuweka wazi kwamba baada ya kumaliza kazi zako mbili mkataba wangu na wewe utakuwa umemalizika na sintapokea tena kazi nyingine yoyote kwa hiyo kama una mawazo ya kunipa kazi nyingine baada ya hizi yafute kabisa mawazo hayo.” Akanyamaza kidogo halafu akaendelea “ Jambo la pili nilikuuliza kuhusu Alberto’s ukakiri kuwafahamu japo wewe si mmoja wao.Nimefurahi kusikia hivyo kwani kuna jambo nataka ulifanye.” Akanyamaza akameza mate na kuendelea “ Nimekuwa nikifuatilia habari za Tanzania.Ni siku ya tatu leo katika kila mkoa hapa Tanzania kuna makundi ya watu wake kwa waume ,wazee kwa vijana wanajiandikisha kwa ajili ya kufanya maandamano makubwa kuelekea bungeni mjini Dodoma ambako kunatarajiwa kuwasilishwa muswada wa kutetea haki za binadamu katika kikao kijacho cha bunge kitakachoanza hivi karibuni.Katika muswaada huo kuna vipengele ambavyo vinataja kutambua haki za baadhi ya makundi kadhaa ya watu wakiwamo watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja.Muswada huu unazitambua pia ndoa za jinsia moja na kama haitoshi musaada huu pia unatambua haki ya mwanamke kutoa mimba.Miswada ya aina hii tayari imekwisha pitishwa kuwa sheria katika nchi zaidi ya ishirini barani afrika.Lengo ni kuhakikisha nchi zote za Afrika zinakubaliana na mambo hayo .Imetumika nguvu kubwa kuufikisha muswada huu hapa ulipofika na toka maandalizi ya muswaada huu yalipoanza kumekuwa na kelele nyingi toka kwa wananchi wakiupinga lakini viongozi na wewe ukiwemo ,mmeziba masikio na mmeendelea na mchakato wake kwa kigezo cha manufaa kwa nchi.Mheshimiwa rais ninakueleza haya yote lakini unafahamu kila kitu kwani umeshiriki pia katika kuubariki muswada huu uende kujadiliwa bungeni na nina hakika uko tayari kuweka saini yako ili uwe sheria pindi utakapofikishwa katika ofisi yako baada ya kujadiliwa na bunge.Mheshimiwa rais wewe na wenzako hamuwezi mkawa sababu ya Tanzania kulaaniwa kwa mambo mnayotaka kuyafanya kwa hiyo utaitisha mkutano wa dharura wa watendaji wako kesho na utatangaza kuufutilia mbali muswada huo ,usipelekwe bungeni na wala usijadiliwe sehemu yoyote ile.” “ Austin.....!!! Ernest akataka kusema kitu Austin akamzuia “ Naomba usubiri nimalize mheshimiwa rais.” Akasema Austin “ Kesho hiyo hiyo baada ya kuufuta muswada huo wa haki za binadamu ,jioni utalihutuba taifa na kuwataarifu wananchi kuwa hakutakuwa tena na muswada huo na utaitumia nafasi hiyo kuitangazia dunia kuwa Tanzania haiko na haitakuwa tayari kukubaliana na masharti toka kwa taifa lolote kubwa au dogo na utamke wazi wazi kuwa mapenzi au ndoa ya jinsia moja ni marufuku nchini Tanzania.Mr president are you readuy for that? Akauliza Austin.Bila kukawia Ernest akasema “ Austin that’s impossible.Hilo ni jambo lisilowezekana na ninaomba tusiliongelee hilo kabisa !! akasema Ernest kwa hamaki “ Mheshimiwa rais naomba nikuweke wazi kwamba utimilifu wa kazo zako utategemea sana na wewe utakavyolipokea suala hili.Endapo utafanya kama nilivyokueleza nitakufanyia kazi yako tena kwa muda mfupi sana lakini endapo hautakuwa tayari kutekeleza hayo maagizo yangu basi sintoifanya kazi yako na nitaamini wewe ni mfuasi wa Alberto’s ambao ni maadui zangu kwa hiyo na wewe utakuwa mmoja wa maadui zangu.” Akasema Austin.Ernest akamtazama kwa macho makali na kusema “ Austin ninakuamini sana na ndiyo maana niko tayari kufanya kila lililo ndani ya uwezo wangu ili unifanyie kazi yangu vizuri.Nitafanya lolote utakaloniamuru nifanye lakini hili unalotaka nilifanye kesho ni jambo ambalo lipo nje ya uwezo wangu na sina mamlaka nalo kwa hiyo siwezi kulifanya” Akanyamaza akamtazama Austin halafu akasema “ Austin ninaamini mpaka hapa tayari unawafahamu Alberto’s ni watu wa namna gani.” “ Ndiyo mheshimiwa rais ninawafahamu” “ Basi naomba nikuweke wazi kuwa wao ndio walioniweka madarakani.” Sura ya Austin ikabadilika akapandwa na hasira . “ You lied to me.You are one of them!! Akasema Austin kwa hasira “I’m not one of them,ila walinisaidia nikaingia madarakani kwa makubaliano ya kuwasaidia katika mambo yao Fulani Fulani.Sikutegemea kama siku moja wangeweza kuja na muswada kama huu.Siwezi kuufuta muswada huu kwa sababu tayari nimekwisha weka makubaliano nao kuitumia ofisi yangu kufanikisha mambo yao na moja ya mambo hayo ni huu muswada unaotarajia kuwasilishwa bungeni hivi karibuni.Nitakapokwenda kinyume nao I’m dead.These people are powerfull and mosters.I can’t betray them.Naomba mambo haya tuyaache kama yalivyo na tuongelee kuhusu yale yanayohusiana na kazi yetu” akasema Ernest “ Hata hili linanihusu pia.” Akasema Austin na kumkazia macho Ernest kisha akasema “ Alberto’s are my enemies mr President.If you want me to do your job then they should be your enemies too.” Macho ya Ernest Mkasa yalionyesha woga mkubwa “ Austin hutakiwi kuweka uadui na hawa watu.Kama nilivyokueleza they are powerfull and monsters.Wako kila sehemu .Wamekita mizizi katika sehemu zote za muhimu za serikali na hivyo ni vigumu sana kupambana nao.Nakushauri Austin tafadhali achana kabisa na watu hawa kijana wangu” akasema Ernest “Mzee naomba nikuweke wazi kitu kimoja .Mimi kutaka kuuawa kule Somalia ulikuwa ni mpango wao na walitaka kuniua baada ya kuifahamu mipango yao miovu hapa Tanzania.Niliponusurika kifo niliamua kuachana kabisa na kazi hizi na sikutaka kujishughulisha nao.Nilichukizwa mno na kitendo kile na ndiyo maana nikaichukia Tanzania na sikutaka tena kurejea nikaamua kuchukua uraia wa Afrika kusini ambako ninaishi kwa amani.Uliponimbia nije Tanzania nilikubali kwa sababu ya mambo mawili kwanza kumkomboa dada yangu na pili niliamua kuja kuwakomboa watanzania wenzangu dhidi ya mambo machafu wanayofanyiwa na Alberto’s kupitia viongozi walioweka maslahi yao mbele na kusahau kuwahudumia wananchi.Mheshimiwa rais nimekuja kupambana na Alberto’s na ninaomba uniunge mkono.Macho yako yanaonyesha wazi kwamba hufurahishwi na mambo yanayofanywa na Alberto’s lakini huna namna ya kuweza kuwakatalia kwa sababu ya makubaliano yenu.Mheshimiwa rais imetosha sasa na umefika wakati wa kuachana nao.Wakati wako ni huu wa kufanya maamuzi yenye kufaa kwa mustakabali wa taifa letu.Nakuhakikishia mheshimiwa rais ukishindwa kufanya maamuzi leo na ukakubali taifa likatumbukia katika laana hii kubwa,siku ukifa kaburi lako litapigwa mawe .Liokoe taifa hili lisilaaniwe” akasema Austin .Ernest akainamisha kichwa akafikiri kwa sekunde kadhaa akasema “ Austi sina la kusema zaidi ya kurudia ushauri wangu kuwa achana na mambo hayo.Kama hutaki ushauri wangu na ukaamua kuendelea na hicho unachokiita mapambano dhidi ya Alberto’s naomba usinishirikishe tafadhali na nina wasiwasi sintakuwa na namna nyingine ya kukusaidia.Ninakushauri tena kama kijana wangu,fanya kazi zangu nilizokuagiza halafu urejee zako afrika ya kusini ukaendelee na maisha yako ya amani .Usitake kuyaharibu maisha yako kwa kutafuta ushujaa.” Akasema Ernest .Austin akamtazama kwa makini sana na kusema “ Mheshimiwa rais ,utajisikiaje iwapo ungekuwa na mtoto wa kiume ambaye umemlea kwa mapenzi makubwa na ukiwa na mategemeo kuwa atakuletea wajukuu lakini badala yake akageuzwa mke na mwanaume mwenzake? Au utajisikiaje iwapo ikatokea Monica akawa kweli ni mwanao halafu ukagundua kwamba ameolewa na mwanamke mwenzake? Ernest akainamisha kichwa akafikiri na kusema “ Ni wazi nitajisikia vibaya na ninaomba usiku na mchana laana hiyo ipite mbali na familia yangu.Siwezi kuvumilia upuuzi kama huo!!! Akasema Ernest “ Jinsi utakavyojisikia ndivyo watakavyojisikia vibaya wazazi ambao watoto wao watafanywa wenzi na wenzao wa jinsia moja pale tu utakaporuhusu muswada huo ukaingia bungeni na baadae ukatia saini kuufanya sheria.Tafadhali mheshimiwa rais usikubali jambo hili.Unazo nguvu za kuhakikisha muswada huu haupelekwi bungeni .Tumia madaraka yako kama rais” akasema Austin.Ernest akatumia zaidi ya dakika saba kutafakari kisha akasema “ Austin maneno uliyoyasema ni mazitoi na yameniingia barabara.Ninakiri kwako kuwa nilifanya kosa kubwa sana kukubali kutumiwa na watu hawa .Ni tamaa ya urais iliniponza.Kuna mambo mengi mabaya yamefanywa na watu hawa kwa wananchi ambao niliapa kuwatumikia na ninaumia sana kila ninapoona taarifa za habari na kusikia kasi ya saratani ya kizazi inaongezeka kila uchao kwa wanawake kutokana na madawa mengi yanayoingizwa kwa makusudi yanayosababisha saratani ya kizazi.Lengo hapa ni kupunguza idadi ya watu barani Afrika ili baadae kusiwe na nguvu kazi na wazungu waje waitawale tena Afrika.Kundi kubwa la vijana nguvu kazi ya taifa limeathirika na dawa za kulevya.Ninatamani nifanye kitu lakini mikono yangu tayari imefungwa .Nimekuwa rais kivuli ambaye ninatumiwa na watu wengine.I cant fight these people so do you.” Akasema Ernest kwa unyonge “ Mr President nimefarijika kuona kuwa una umizwa na mambo haya.Naomba usiogope tafadhali.Kuwa jasiri na ufanye leo maamuzi makubwa ambayo yatakufaya ukumbukwe na vizazi vingi vijavyo.Kuwa rais wa mfano na ufanye nchi hii iwe nzuri na salama kuishi kwa watoto wa watoto wetu” akasema Austin.Ilimchukua dakika zaidi ya tatu Ernest kuongea “Austin narudia tena kusema kuwa mambo uliyoyaongea ni mazito na yenye manufaa makubwa.Nimekuelewa kijana wangu na niko tayari kufanya maamuzi makubwa na magumu lakini ukae ukijua kuwa nitakapofanya hivyo unavyotaka nifanye basi tayari mimi na wewe tutakuwa katika hatari kubwa.Sitaki kukuingiza katika matatizo.Sitaki niwe chanzo cha maisha yako kuharibika tena” akasema Ernest “ Mheshimiwa rais umesoma faili langu na tayari umefahamu mambo mengi kuhusu mimi.Siogopi kuingia katika matatizo na wala maisha yangu kuvurugika.Kwa hiyo usihofu kuhusu usalama wangu na wako” akasema Austin.Ernest akafikiri tena kwa muda kidogo na kusema “ Austin nitafanya hivyo unavyotaka nifanye lakini kwa sharti moja” “ Sharti gani mheshimiwa rais? Akauliza Austin “ Nataka unihakikishie kwamba hautarejea tena Afrika kusini bali utabaki hapa hapa nchini.Austin I need you here to protect me” Mheshimiwa rais unao ulinzi wa kutosha kwa hiyo sioni sababu ya mimi kubaki Tanzania” “ Ni kweli Austin ninao ulinzi mkubwa lakini hakuna kati ya walinzi wangu mwenye uwezo mkubwa kama wewe.Umepata mafunzo ya hali ya juu katika nchi tofauti tofauti .Ni mtanzania pekee kati ya 10 uliyemaliza na kuhitimu mafunzo ya operesheni maalum katika chuo cha Navy seal nchini Marekani.”akasema Ernest “ Mheshimiwa rais nipe muda wa kulitafakari suala hili kwani siwezi kukupa jibu la haraka haraka kama ninaweza kulikubali ombi lako ama vipi” “ Austin ni wewe ambaye umenishawishi kuingia katika hii vita kwa hiyo lazima tupambane wote wawili.You are going to stay here for good.Nitakupatia kila unachokihitaji na utakuwa mlinzi wangu wa siri.Austin kazi hii huwezi kuikimbia ,haya ndiyo maisha yako.Yakubali na uyaishi.Mimi kesho nitafanya kama tulivyokubaliana na nina imani na wewe utatekeleza kwa upande wako” akasema Ernest “ Mheshimiwa rais ,ahsante kwa kunisikiliza na kunielewa.Kesho nitaanza kufanya kazi zako.Nitakupa orodha ya vitu nitakavyovihitaji kwa ajili ya kuikamilisha kazi hizo.Natumai tutakuwa tena na kikao kingine cha kuzungumzia kwa undani kuhusu vita hii tunayokwenda kuianza.Kwa sasa naomba uende ukapumzike na mimi uniache nitafakari namna nitakavyofanya kazi zako” akasema Austin akaagana na Ernest akaondoka “ hatimaye ninarejea tena rasmi katika kazi ambayo sikuwa ninataka kuifanya katika kipindi cha maisha yangu yote yaliyobakia lakini kama alivyosema rais kuwa this is my life ,this is my job,this is where I belong.Ni muda muafaka sasa umefika wa kupambana na Albertos na kuung’oa kabisa mzizi wake hapa Tanzania.Watu hawa walinifanya nikaichukia nchi yangu na hata kuapa kutokurudi tena,ninasema safari hii ni ama zao ama zangu.Siwaogopi tena.Nitapambana nao hadi mwisho wangu.Nashukuru kwa rais kuamua kuniunga mkono .Endapo kesho atafanya kama nilivyomuelekeza basi litakuwa ni pigo kubwa kwa Alberto’s.Hawataamini kilichotokea.Wakati wakiwa katika mshangao wakijiuliza juu ya kilichotokea nitawaondoa mmoja baada ya mwingine.Si kazi nyepesi hii lakini nitajitahidi kwa nguvu zangu zote na pale itakapobidi nitaomba msaada.Lazima nipambane nao ,lazima waondoke Tanzania.Hii ni nchi pekee ambayo wamehangaika kwa miaka mingi kuotesha mizizi yao na walifanikiwa baada ya kumsaidia Ernest Mkasa kuingia madarakani.Toka hapo nchi imebadilika sana na wamekuwa wakifanya yale ambayo wameyafanya katika nchi nyingine za afrika na dunia. Lakini ngoja kwanza niachane na mawazo hayo kuhusu vita na Alberto’s kwa sasa na nielekeze akili yangu katika kutafuta namna ya kuweza kumtoa Marcelo hospitali na namna nitakavyojenga ukaribu na Monica” akawaza Austine na mara akamkumbuka mpenzi wake Maria “ Natakiwa kuwasiliana na Maria nijue maendeleo yake.Nimekuwa namuwaza kutwa nzima ya leo.Ninampenda sana na moyo unaiuma kwa kitendo nilichokifanya cha kumdanganya kuhusu kazi iliyonileta Dar es salaam.Itanilazimu nimueleze ukweli wa kila kitu ili asije huku kwani mambo yanayokwenda kutokea siku si nyingi ni ya hatari sana kwa usalama wake na siko tayari kuyaweka maisha yake hatarini.” Akawaza Austin na kwenda kuchukua kompyuta yake akamtafuta Maria mtandaoni akampigia.Maria akapokea simu “ How’re you my love.Huwezi jua ni kwa namna gani nimeisubiri simu hii leo.Sijui kama ningeweza kulala bila kuisikia sauti yako nzuri.Nakupenda sana Austin na ndiyo maana ninakuwaza mno kuliko kitu kingine chochote.” Akasema Maria na kumfanya Austin atabasamu “ Hello malaika wangu, umeshindaje leo? Nisingeweza kulala bila kujua hali yako “ “ Nimeshinda salama mpenzi wangu na hali yangu ni njema sana.Leo nimeshindwa kusaini ule mkataba ,wanasheria wa Alnoor wanaweka sawa baadhi ya vipengele ila kesho nina uhakika tutasaini mkataba na baada ya hapo sintopoteza hata dakika moja ,nitapanda ndege kuja Dar es salaama kukutana nawe mfalme wangu” Akasema Maria na Austin akajikuta akikosa neno la kusema “ Mbona umekuwa kimya ghafla Austin? Hutaki nije Dar es salaam? Akauliza Maria.Austin akakohoa kidogo na kusema “ Uhhmm ! Maria bado unasisitiza kutaka kuja Dar es salaam? “ Ndiyo ninasisitiza Austin.Mbona unaonekana hujapendezwa na mimi kutaka kuja Dar es salaam?Kuna nini unanificha Austin? Tafadhali kuwa muwazi” akasema Maria.Austin akatabasamu na kusema “ Hakuna chochote ninachokificha Maria ila nina wasi wasi na usalama” “ Kama huna unachokificha basi hupaswi kuwa na wasi wasi.Nitakuja Dar es salaam mara tu baada ya kumalizana na Alnoor.Austin siogopi hatari yoyote kama kuna lolote baya basi litufike sote kwa hiyo ujiandae kunipokea kesho kutwa.Nitakutaarifu kesho ni ndege gani nitapanda ili unipokee uwanja wa ndege” akasema Maria wakaendelea na maongezi mengine na baada ya saa nzima wakaagana “ Nimeshindwa kumueleza Maria ukweli na hii ina maana lazima aje Dar es salaam.What can I do? Nifanye nini kumzuia asije? Ulimi umekuwa mzito kumueleza ukweli na endapo atakuja Dar lazima atagundua nimemdanganya na ataumia sana kwani mimi ni mtu anayeniamini kuliko hata baba yake mzazi.Nitaongea na baba yake pengine anaweza akanisaidia kwa namna yoyote ile kumfanya Maria asije Dar es salaam” akawaza Austin na kuanza kuwaza tena juu ya majukumu yaliyoko mbele yake “ Monica Benedict Mwamsole ,who is this woman? Kwa bahati mbaya mimi si mfuatiliaji sana wa habari za mambo haya ya urembo ndiyo maana simfahamu huyo Monca ni nani hadi kutangazwa kuwa mwanamke mrembo kuliko wote Afika.Haiwezekani atokee mwanamke mmoja awe mzuri kuliko mamilioni ya wanawake wa Afrika,awe mzuri kumshinda hata mpenzi wangu Maria.Mimi naamini Maria ni mwanamke mzuri kuliko wote Afrika na dunia “ akawaza Austin na kuanza kupekua mtandaoni kutafuta t aarifa za Monica. Alipata picha nyingi za Monica alizoweka mtandaoni na akabaki mdomo wazi “ What a beautiful woman.!!! She’s an angel..I was wrong,huyu anastahili kabisa kuwa mrembo kuliko wote afrika.” Austin akajikuta akiongea mwenyewe kwa sauti ndogo na kuendelea kupitia picha za Monica moja baada ya nyingine halafu akajiegemeza kitini “ Monica Benedict !!..akasema kwa suti ndogo “ Nilidhani labda ni mwanamke mwenye uzuri wa kawaida tu lakini kumbe ni mwanamke mwenye uzuri usioweza kuelezeka kwa maneno.Nawapongeza watu wa jarida la The Face walifanya kazi kubwa ya kusakanya na kumpata mtu sahihi kuwa malkia wa urembo Afrika.” Akawaza Austin huku akiendelea kuzitazama picha za Monica “ Mpenzi wangu Maria ni mzuri sana lakini nakiri hawezi kufikia uzuri wa Monica” Bado picha za Monica zilionekana kumsisimua mno “ Japokuwa kazi nimekubali kuifanya lakini nathubutu kukiri ina majaribu makubwa .Mara nyingi huwa sipendi kufanya kazi ambazo ndani yake kunakuwa na wanawake warembo kama Monica.Binadamu siku zote ni dhaifu na unaweza ukajikuta umeanguka kishawishini na kushindwa kuitekeleza kazi yako ipasavyo.Nitajitahidi sana hilo lisitokee.Nakumbuka nliwahi kutumwa kazi na rais aliyetangulia kabla ya Ernest kuwasaka watu waliotaka kumuua Boaz na nikajikuta nimezama mapenzini na mtoto wake Maria.Sitaki kilichotokea wakati ule kinitokee sasa na kusababisha kutetereka kwa mahusiano yangu na Maria.Ninampenda sana na sitaki kumuumiza.Yeye ndiye sababu ya mimi kuendelea kuwa hai hadi sasa.Yeye ndiye aliyemshawishi baba yake akalipa kiasi kikubwa cha pesa walichokitaka wanamgambo wa Alshabaab wakaniachia huru.Ninamuheshimu sana Maria na siku zote atabaki kuwa mwanamke wa pekee kabisa katika maisha yangu” akawaza Austin akainuka na kuelekea chumba cha kulaa.tayari umekwisha kuw ausiku mwingi wa sekunde kadhaa sasa David Zumo alikuwa amepiga magoti pembeni ya mwanamke mrembo kuliko wote Afrika Monica Benedict Mwamsole aliyekuwa amelala kifudi fudi huku wote wakiwa watupu sebuleni .David alikuwa anahema kwa kasi kubwa na jasho jingi likimtiririka.Macho yake aliyaelekeza kwa mwanamke aliyelala pembeni yake ambaye alikuwa analia kwa kwikwi “ Ni vigumu kuamini lakini ni kweli.Monica hajawahi kumjua mwanaume na mimi ndiye mwanaume wake wa kwanza.Huyu ni mwanamke wa kipekee kabisa .Wanawake wanaotunza bikira zao hadi umri kama huu wa Monica ni wachache mno katika ulimwengu wa sasa.Laiti ningejua Monica bado ni bikira ningesubiri hadi tutakapofunga ndoa kwani naamini kabisa hawezi kukataa” akawaza David “ Najisikia fahari kubwa kuwa mwanaume wa kwanza kumjua Monica.Hii ni heshima kubwa kwangu na lazima niitunze.Nitamuweka Monica katika nafasi ya juu mno.Nitampa heshima ya kipekee kabisa mwanamke huyu wa pekee ambaye sikuwahi kuota kama nitaweza kumpata katika maisha yangu.” Akawaza David huku akiendelea kumtazama Monica aliyekuwa amejilaza kitandani akilia kwa kwikwi.Akamuinua na kumfuta machozi “ Pole Monica.Tafadhali nyamaza kulia” akasema David akimfuta Monica machozi “ Najua umeumia Monica lakini nakuomba usiendelee kulia malaika wangu.” Akasema David Zumo.Monica akamtazama na kusema “ Umenishawishi tukafanya mapenzi na umeniondolea bikira yangu ambayo ilikuwa ni zawadi kwa mwanaume wa maisha yangu” akasema Monica na kuendelea kumwaga machozi “ Monica malaika wangu usilie tafadhali.Hata mimi ninajilaumu sana kwa hiki kilichotokea.Laiti kama ningejua mapema ningejitahidi kujizuia lakini tayari imeshatokea kwa hiyo nakuomba unifanye mimi niwe mwanaume wako wa kwanza.Nifanye mimi niwe mfalme wako.Monica wewe ni mwanamke wa pekee kabisa kuwahi kukutana nawe.Ni nadra sana kwa zama hizi kukutana na mwanamke aliyetunza usichana wake hadi kufikia umri kama wa kwako.Unastahili pongezi na heshima ya kipekee kabisa.Mimi kama mwanaume wako wa kwanza ninaomba unipe nafasi Monica ili nikupe heshima unayostahili mwanamke kama wewe.Naomba nikuonyeshe namna ninavyokupenda .Nipe ruhusa nikuinue juu ya wanawake wote wa dunia hii.Kubali kuolewa nami Monica “ akasema David Monica akaupeleka mkono sirini akautazama, ulikuwa na damu,akamtazama David na kusema “ Umenitoa bikira yangu ambayo nimeitunza kwa miaka hii yote kwa ajili ya mwanaume Yule ambaye atakuwa wa pekee kwangu,mwanaume ambaye nitamkabidhi moyo wangu autunze zaidi ya mboni ya jicho lake.Bikira hiyo imekuwa ikinipa ujasiri na subira ya kumsubiri mwanaume wa ndoto zangu .Ni kitu nilichojivunia na kukithamini mno lakini kwa sasa baada ya kuiondoa nimekua mtu wa kawaida nisiye na thamani tena.Kwa kuwa wewe ndiye uliyenitoa usichana wangu siwezi kulikataa tena ombi lako la kutaka kunioa.Ninakubali kuolewa nawe ila nomba yale yote uliyoniahidi yawe ya kweli.” Akasema Monica.David hakumpa nafasi ya kuendelea zaidi akapagawa kwa jibu lile la Monica akajikuta amemkumbatia kwa nguvu na kuanza kumporomoshea mabusu katika sehemu mbali mbali za mwili “ Ahsante Monica.Ahsante malaika wangu kwa kukubali ombi langu.Sijui nikwambie nini Monica kuhusu furaha niliyonayo kwa kulikubali ombi langu.Nakuahidi hautajutia uamuzi wako .Nakuahidi nitakupenda zaidi ya upendo wenyewe.” Akasema David na kumbusu Monica “ Sasa twende chumbani ukapumzike malaika wangu,siku yetu imekuwa nzuri na njema sana .Kesho tutakuwa na maongezi mengi zaidi kuhusiana na maisha yetu.” akasema David akambusu Monica na kumshika mkono akamuinua wakaelekea katika chumba cha kulala. “ Hiki ni chumba chako cha kulala malkia wa Congo.Panda kitandani upumzike ewe mzuri wa wazuri” akasema David Zumo akambusu Monica na kutoka mle chumbani.Monica akaingia bafuni kuoga.Kwa dakika kadhaa alikuwa amesimama bafuni akitafakari “ Sielewi nini kimenitokea hadi nikajikuta kwa hiari yangu nikimvulia nguo David.Nahisi huyu jamaa anatumia uchawi kwani mimi ni mtu mwenye msimamo mkali linapokuja suala la haya ya mapenzi lakini najishangaa kwani leo nimejikuta mwenyewe nikichojoa nguo na kufanya mapenzi.I’m so weak and stupid...” akawaza Monica huku akijipiga vibao shavuni “ So this is it.Bikira yagu imeondolewa na sina tena cha kujivunia.Imenilazimu nikubali kuolewa na David Zumo .Hata hivyo nikimtazama David anaonekana ananipenda kwa dhati ya moyo wake na hata mke wake pia amenikubali .Ngoja tu niolewe na David japokuwa nitakuwa mke wa pili lakini hakuna tatizo kwani Pauline mke wa David ameridhia jambo hilo “ akaendelea kuwaza Monica huku akioga “ David anaonekana kuchanganyikiwa kabisa na mimi .Sijui amechanganyikiwa na nini lakini nahisi lengo lake kubwa yeye na mke wake ni kupata mtoto kutoka kwangu.Sipati picha hiyo harusi yetu itakuaje.Mhh ..!! mwili wote unanisisimka.Halafu kuna jambo ambalo bado sijapata muafaka wake.Nikiolewa na David najua atanitaka niishi hapa Congo karibu naye lakini kama nitakubali kuishi hapa nitaendeshaje program zangu? Hapana sitaki kuishi Kinshasa ,nitaishi Tanzania” akawaza Monica.Picha nyingi za haraka haraka zikamjia kuhusiana na maisha atakayoyaishi baada ya kuolewa na David Zumo.Akatabasamu DAR ES SALAAM – TANZANIA Kijua tayari kimekwisha chomoza kuashiria mwanzo wa siku nyingine .Austin tayari alikuwa katika chumba cha mazoezi akiweka mwili sawa kuikabili siku.Alipomaliza kufanya mazoezi akatoka akaelekea jikoni akafungua mojawapo ya kabati akatoa kitu Fulani alichokitengeneza mara tu alipoamka asubuhi akakichunguza kwa makini halafu akakiweka katika boksi na kuliingiza boksi lile katika begi la mgongoni “ I’m back to work again.Sikutegemea kabisa kama nitarejea tena katika mambo haya” akawaza na kutoka mle jikoni akaenda bafuni akaoga halafu akarejea tena jikoni akaandaa stafstahi.Alikunywa chai kwa haraka akiwa amesimama na alipomaliza akachukua begi lake la mgongoni alimoweka lile boksi lenye kifaa Fulani ndani yake .Akaenda tena chumbani akafungua sanduku kubwa na ndani yake akatoka sanduku lingine la kadiri akalifungua.Lilikuwa limesheheni silaha ndogo ndogo.Akachukua bastora mbili pamoja na vifaa vingine vichache ambavyo vingeweza kumsaidia.Kabla hajatoka alihakikisha kamera tatu za ulinzi alizofunga zinafanya kazi vizuri.Kamera zile ndogo lakini zenye uwezo mkubwa ziliunganishwa na mfumo wa kompyuta ambao uliweza kutuma picha za kila kilichokuwa kinaendelea moja kwa moja katika miwani maalum aliyoivaa.Mara tu anapoivaa miwani hiyo na kugusa sehemu Fulani yenye kitu mfano wa doa jeusi sehemu moja ya miwani hiyo hubadilika na kuanza kupokea picha toka katika kamera zilizoko nyumbani kwa hiyo kumuwezesha kujua kinachoendelea .Hii ilikuwa teknolojia ya hali ya juu sana “ It’s perfect.” Akasema na kutoka akafunga nyumba na kuelekea katika maegesho zilikoegeshwa gari tatu mpya .Akachagua moja ambalo aliona lingemfaa kwa shughuli anayokwenda kuifanya kisha akaondoka “ Filimbi tayari imepulizwa sasa kinachofuata ni kuingia vitani.” Akawaza akiwa garini na mara akamkumbuka mpenzi wake Maria. “ Leo atasaini mkataba na Alnoor na kwa mujibu wa maelezo yake ni kwamba mara tu atakapomaliza masuala yaliyompelekea Dubai ,moja kwa moja atapanda ndege kuja Tanzania.Ni wiki ya tatu sasa hatujaonana na imekuwa ni kama miezi mitatu kwetu .She loves me a lot na hata mimi ninampenda mno zaidi ya ninavyoweza kueleza lakini suala la yeye kuja dar es salaam bado siliafiki kabisa kwani ni hatari mno kwake.mambo yatakayotokea ndani ya siku chache zijazo ni mambo ya hatari na sitaki mwanamke nimpendaye kuliko wote aingie katika hatari.Nasikitika kwamba sina cha kufanya kumzuia asije Tanzania.Nilishindwa kumueleza ukweli kwa hiyo lazima atakuja dar es slaam” akaendelea kutafakari akiwa amesimama katika taa za kuongozea magari. “ Kuna kitu kimoja ninachoweza kufanya ili kumzuia Monica asije dar .Ni kuacha kuwasiliana naye.Nikifanya hivyo hata kama akija Dar hatajua namna ya kunipata na ataondoka kurejea afrika ya kusini.Ni bora nikafanya hivyo kwa ajili ya usalama wake yeye mwenyewe ingawa najua ataumia na atanichukia sana lakini sina ujanja.Nitamuelewesha huko mbele ya safari naamini atanielewa.” Akaendelea kuwaza Austin na sura ya Monica ikamjia Sura ya binti malaika huyu inanijia kichwani kila mara.Ngoja kwanza nishughulikie kazi ya kwanza ya kumuondoa hospitali Marcelo na baada ya hapo nitajipanga wa ajili ya Monica.” Lango la kuingilia hospitali ya Mt Lucia lilikuwa wazi,watu na magari walikuwa wakipita bila kikwazo chochote.Hakukuwa na ukaguzi wowote japokuwa walikuwepo walinzi waliovalia sare za kampuni binafsi ya ulinzi .Kulikuwa na magari mawili mbele ya Austin yakiingia mle hospitali .Austin kwa haraka haraka akachunguza ulinzi ulivyo pale getini akatabasamu “ Hakuna ulinzi wowote wa maana hapa getini.Hawa walinzi wako hapa kutangaza kampuni yao tu” akawaza wakati akivuka geti na kukutana na kibao kilichomuelekeza sehemu ya kuegesha gari.Ilipata saa tatu na dakika ishirini na tayari eneo la maegesho lilisheheni magari .Austin akachukua kofia nyeusi akavaa pamoja na miwani ile ya kielektroniki yenye kuweza kufanya mambo kadhaa kwa wakati mmoja.Akahakikisha bastora zake zimekaa vizuri kisha akachukua begi akashuka.Ilikuwa ni mara yake ya kwanza kufika katika hospitali hii kubwa iliyokuwa na bango kubwa lenye ramani ya hospitali ikielekeza namna ya kufika katika sehemu mbali mbali za hospitali ile .Taratibu huku akiyasoma mazingira Austin akakamata njia iliyoelekea ziliko wodi za kulaza wagongwa.. “ Hospitali ya kisasa sana hii.Ina miundo mbinu mizuri lakini kuna kasoro moja tu kubwa,hakuna usalama” akawaza Austin akiwa amezifikia wodi . akakutana na bango lingine lililoelekeza namna mpangilio wa wodi ulivyo ukianzia na zile wodi za watu maalum.Kwa kufuata maelekezo ya lile bango akafika katika wodi za watu maalum.Kulikuwa na pilika pilika nyingi eneo hili hivyo hakuna yeyote aliyekuwa na muda wa kumfuatilia Austin.Alichunguza eneo la chumba alimolazwa Dr Marcelo na kuondoka akaelekea katika jengo la mapokezi.Lilikuwa ni jengo kubwa la ghorofa nne.Watu walikuwa wengi katika jengo hilo na Austin akajumuika nao huku akiyasoma mazingira ya mle ndani yalivyo.Alitoka mle ndani akaelekea katika bustani nzuri iliyokuwa karibu na jengo la mapokezi.Begi lake akaliweka pembeni na alioneka kama mtu aliyekuwa akisubiria huduma.Akapita kijana muuza magazeti akanunua gazeti moja akaanza kusoma huku akichunguza mazingira yalivyokaa.Alipohakikisha hakukuwa na mtu yeyote aliyekuwa anamtilia shaka akalifungua begi lake na katika lile boksi lililokuwa na kifaa ndani yake akabonyeza kidude Fulani kilichokuwa mithili ya saa kikaanza kuandika namba kwa haraka haraka,akalifunga begi na kuliweka pembeni na kwa kutumia mguu wake akalisogeza katika maua halafu akaangaza tena pande zote lakini hakukuwa na mtu yeyote aliyekuwa anamfuatilia.Taratibu akainuka akaingia tena katika jengo la mapokezi halafu akatoka na kuanza kuelekea ziliko wodi.Alipokaribia chumba cha Marcelo akatoa kitu Fulani mithili ya simu akabonyeza namba kadhaa na mara ukatokea mlipuko mkubwa karibu na jengo la mapokezi.Kizaa zaa kikubwa kikaibuka hapo hospitali watu wakaanza kukimbia hovyo kunusuru maisha yao. Taharuki ile ndiyo aliyokuwa anaihitaji Austin ili afanikishe kazi yake.Akachomoka kama mshale hadi katika chumba cha Marcelo.Hakukuwa na daktari yeyote mle chumbani ,alikuwemo Dr Marcelo pekee akiwa hajui afanye nini.Marcelo akastuka sana kwa namna Austin alivyoingia mle chumbani “ Are you Marcelo? Akauliza Austin “ yes “ akajibu Marcelo kwa wasiwasi “ Good.My name is Austin and I’m here to take you out of here.Naomba ufuate maelekezo yangu” akasema Austin “ Wewe ni nani? Umetumwa na nani? “ Marcelo ninao muda mchache sana wa kufanikisha zoezi la kukutoa hapa kwa hiyo nahitaji ushirikiano wako.” Akajibu Austin huku akimshika mkono Marcelo na kumtaka ainuke “ Siendi kokote bila kufahamu ni nani aliyekutuma” Marcelo akagoma “ What ??..akauliza Austin “ Najua umetumwa uje unichukue ukaniue.Naomba uniulie hapa hapa ila huko unakotaka kunipeleka siendi” akasema Marcelo. Austin akavua kofia na kumtazama Marcelo “ Nisikilze kaka.Kazi yangu ni kukuondoa hapa na kukupeleka sehemu salama kwa hiyo sina muda wa mabishano na wewe.Kuna mambo mawili ya kuchagua ,aidha ufuate maelekezo yangu nikutoa hapa au nikutoe humu kwa nguvu” akasema Austin kwa sauti ya ukali wakaendelea kutazamana “ Are we going or you want me to use force? Akauliza Austin.Marcelo akatikisa kichwa ishara ya kukubaliana na Austin Haraka haraka Austin akamuinua Marcelo akamuweka begani na kuchungulia nje ambako bado taharuki ilikuwa imetanda na watu wakikimbia hovyo kunusuru maisha yao.Akaangaza pande zote kuhakiki usalama “ It’s clear” akasema taratibu na kuingia katika gari lake akaondoka eneo lile akipishana na magari mawili ya zima moto yaliyofika kwa haraka sana huku magari matatu ya polisi yaliyosheheni askari yakifika kwa haraka “ Nini kimetokea hapa? Nimesikia kishindo kikubwa kama mlipuko na watu wakaanza kukimbia huku wakipiga makelele na ghafla ukatokea chumbani kwangu.Who are you? Nani kakutuma uje unitoe hapa hospitali? Unahusika na kilichotokea hapa? Akauliza Marcelo lakini Austin hakumjibu kitu akaendelea kuendesha gari kwa umahiri kuhakikisha hakuna mtu anayemfuatilia “ C’mon brother I deserve to know who are you? Who sent you and where are you taking me? Akauliza Dr Marcelo .Bado Austin hakumjibu chochote “ Huyu mtu ni nani? Ametumwa na nani aje anitoe pale hospitali?Ananipeleka wapi? Maswali haya yalimuumiza sana Kichwa Dr Marcelo “ Kuna mtu mmoja tu ambaye nilimueleza tatizo langu na nikamuomba anisaidie ambaye ni Monica.Inawezekana huyu jamaa ametumwa na Monica au ametumwa na wale jaama wanaotaka kuniua? Lakini nikimtazama kwa makini haonyeshi kama ana lengo la kuniua.Kama ni Monica ndiye aliyemtuma sijui nitamshukuruje kwani nisingemaliza siku mbili bila kuuawa.Asubuhi ya leo niliwaona watu wao wawili wakiongea na daktari na baada ya hapo daktari akaja akanipima na kuondoka.Kilichoniweka hai hadi sasa ni kwa sababu nilijifanya siwezi tena kuongea.Natakiwa niikimbie nchi kwani endapo nitaendelea kukaa humu nchini lazima watanisaka na kuniua.” Akawaza Dr Marcelo wakati gari likikata mitaa ya jiji huku akiwa hajui ni wapi alipokuwa anapelekwa. “ Nimewastua na mlipuko ule wa fataki wamechanganyikiwa kabisa.Kimetokea kizaa zaa cha kutisha pale hospitali” akawaza Austin huku akitabasamu kwa mbali “ Kazi ya kwanza kati ya mbili za rais nimeimaliza.Imekuwa ni kazi nyepesi mno zaidi ya nilivyotazamia japokuwa nimetumia nguvu kubwa kidogo lakini nimefanya vile ili kuwapoteza lengo watu waliokuwa na nia ya kumuua Marcelo.Ninaamini kabisa kama kweli huyu jamaa alikuwa anataka kuuawa basi lazima kuna watu waliowekwa pale hospitali kumfuatilia na nisingeweza kumtoa pale kirahisi bila ya kuonekana lakini kwa njia hii niliyoitumia naamini hata wao kama walikuwepo lazima walikimbia kunusuru maisha yao.Nasikitika kishindo kile cha mlipuko kinaweza kuwa kimesababisha madhara kwa baadhi ya wagonjwa hasa wenye matatizo ya moyo lakini sikuwa na namna nyingineya kufanya ili kumuokoa Marcelo.”akawaza Austin KINSHASA – DRC Muziki wa ala uliosikika kwa sauti ya chini ulimfanya Monica aote ndoto nzuri .Alikuwa katika uwanda mpana wenye nyasi nzuri za kijani.Vijito vya maji vikitiririka katika kila kona ya uwanda huu wa kuvutia mno.Ndege wa rangi mbali mbali wakubwa wa wadogo walikuwa wanaruka .Upande wa juu watu waliovalia nadhifu walikuwa wamejipanga katika mstari wakiimba na wengine walikuwa pembeni wakipiga vyombo vya muziki.Ulikuwa ni muziki mtamu ulioburudisha.Pembeni na pale alipokuwa amekaa kulikuwa na wanawake zaidi ya sita wakiwa tayari kumuhudumia kwa chochote akitakacho.Tabasamu halikukauka .Alikuwa amevaa taji la dhahabu pamoja na vito vingi vyenye kung’aa vya thamani kubwa.Alikuwa anameremeta .Ghafla akastushwa na kengele iliyolia akakurupuka toka usingizini.Kulikuwa na mtu mlangoni.Haraka haraka akajifunga taulo na kwenda kuufungua mlango akakutana na sura yenye tabasamu ya mwanamama mmoja wa makamo akamsalimiana kujitambulisha. “ naitwa Anna.Ni muhudumu mkuu wa rais katika jumba hili.Nimefurahi kukuona malkia wa wangu.Kuna chochote unahitaji asubuhi hii? “ hata mimi nimefurahi kukufahamu Anna.Nitakujulisha baadae endapo nitahitaji chochote” akajibu Monica na Anna akaondoka kwenda kuendelea na shughuli zake.Monica Akakaa kitandani na kuanza kutafakari kilichotokea usiku uliopita.” “Nilifanya ujinga mkubwa sana jana.Nilimkubalia David kirahisi kufanya mapenzi bila hata kutumia kinga.Oh my gosh ni vipi kama ana magonjwa? Akawaza na kushika kichwa “ Lakini hapana David ni mtu muungwana asingeweza kukubali kufanya nami mapenzi bila kinga hali akifahamu kuwa ana matatizo.” Akajipa moyo na kutabasamu baada ya kuikumbuka ndoto ile nzuri aliyoiota. “ Ilikuwa ndoto nzuri ajabu.Sijawahi kuota ndoto nzuri kama ile katika maisha yangu.Je ndoto ile inaashiria maisha yangu yatakavyokuwa huko mbeleni? Kama nilichokiota katika ndoto ndivyo maisha yangu yatakavyokuwa basi sikufanya makosa kukubali kuolewa na David Zumo.” Akawaza Monica halafu akamkumbuka Marcelo “ Marcelo..Hali yake ikoje sasa hivi?Jana David aliongea na rais wa Tanzania na akamuahidi kumsaidia kumtoa pale hospitali.Natamani kujua kama zoezi hilo limekwisha fanyika au vipi.Nikionana na David nitamuuliza kuhusu jambo hili” Akiwa bado amekaa kitandani huku akiwaza mambo mengi kengele ya mlango ikalia akaenda kufungua na kukutana na David Zumo “U hali gani Monica? Akauliza David Zumo aliyekuwa amesimama mlangoni akiwa amevaa mavazi yale aliyokuwa ameyavaa usiku yaani ngozi ya chui na kofia ya manyoya ya Simba. “ Hallow David” akasema Monica huku akitabasamau na kuona aibu kwa mbali.David akaingia ndani “ Umeamkaje malaika wangu? Akauliza “ Nimeamka salama kabisa ,sijui wewe” “ Hata mimi nimeamka salama kabisa.Vipi maendeleo yako?Una hali yoyote ya maumivu nimuite daktari? “ Ninahisi maumivu kwa mbali lakini nitatumia dawa za kutuliza maumivu tu na nitapona.” Akasema Monica “ Samahani sana Monica.” “ Usiogope David.Jambo hili limeshatokea na limepita kwani hata kama isingekuwa ni wewe basi angefanya mwanaume mwingine.Kwa sasa tuachane na suala hilo tuangalie mengine ya msingi lakini awali ya yote kuna kitu nataka kuuliza” “ Uliza Monica” “ jana tulipofanya mapenzi hukutumia kinga.Una hakika uko salama? David Zumo akatabasamu na kusema “ Nilitegemea ungeniuliza swali kama hilo.Naomba nikuhakikishie kwamba usiku wa jana ni usiku wa kwanza kwangu kufanya mapenzi na mwanamke ambaye si mke wangu.Toka nimefunga ndoa na Pauline sijawahi kujihusisha na mahusiano na mwanamke mwingine yoyote zaidi ya mke wangu.Mimi na Pauline tunapendana sana na tunaaminiana mno” akasema David wakatazamana kwa muda kisha David akasema “ Monica ni wakati wa kujiandaa kuna mgeni atakuja kuungana nasi hapa leo.Ukishaoga na kujiandaa pale ukutani kuna vitufe vitano,utabonyeza kitufe namba moja na watakuja watumishi kukuhudumia kisha baada ya hapo tutaungana kwa mlo wa asubuhi akasema David na kutoka mle chumbani akampa nafasi Monica kujiandaa “ Tayari maisha yangu yamebadilika.Monica wa jana si Monica wa leo.Ama kweli maisha yana maajabu makubwa.Sikuwahi kuota kama siku moja nitaishi maisha makubwa kama haya” akawaza Monica na kuingia bafuni kuoga.Alipomaliza kuoga akafuata maelekezo aliyopewa na David akabonyeza kitufe namba moja na haikumalizika dakika moja wakaingia wanawake zaidi ya sita kwa ajili ya kumuandaa Monica.Kila mmoja alikuwa na kazi yake.

ITAENDELEA


0 comments:

Post a Comment

Blog