Search This Blog

Tuesday 20 December 2022

SHETANI' MTANASHATI NA AMRI KUU 10 - 5

  http://pseudepigraphas.blogspot.com/2020/06/shetani-mtanashati-na-amri-kuu-10.html



Noti zao feki zilitengenezwa kwa umahiri wa hali ya juu kiasi ambacho hata tellers katika benki walishindwa kuzitofautisha na zile halisi.


'Biashara' hii ilimfanya Lustig kuwa milionea kwa haraka sana na akaishi maisha ya anasa. Na biashara hii ndio iliyomfanya asakamwe na serikali wakimuwinda kila kona wamkamate kwani noti zake bandia zilizagaa kiasi kwamba baadhi ya nchi zilianza kukataa kupokea dola kutoka marekani wakihofia kuwa zinaweza kuwa feki.


Taarifa za idara ya Huduma za Siri (Secret Service) ambayo iliundwa kipindi hicho kwa lengo kuu la kupambana na kutokomeza fedha bandia (walikuja kubadilishiwa majukumu miaka ya baadae na kupewa jukumu la kulinda viongozi wakuu wa nchi) taarifa hizo zinasema kwamba tatizo la fedha bandia za Bw. Lustig lilikuwa kubwa kiasi ambacho ilifikia hatua ilikuwa kana kwamba kuna 'serikali' nyingine ndani ya Marekani iliyokuwa inashindana na Serikali halali katika kuchapa noti za fedha. Hivyo basi kumkamata Lustig ikawa ni kipaumbele namba moja cha Secret Service.


Lustig alikuwa na hawara aliyeitwa Billy May, na Lustig alifanya kosa la kuanzisha mahusiano ya siri na msaidizi wa ndani wa Billy May aliyeiitwa Marie. Kutoka na uchungu wa kusalitiwa, mwanamama Billy May aliwasiliana na polisi na kuwaeleza Lustig alipo na hii ikafanikisha kukamatwa kwake.


Baada ya kukamatwa Lustig alipelekwa katika gereza lililopo Manhattan na akakaa hapo kwa wiki kadhaa kabla ya kuwatoroka kwa njia ambayo hwakutarajia.


Lustig alitumia mashuka katika selo yake kutengeneza kamba ndefu. Kisha akakata vyuma vya dirisha la selo yake (haijulikani alikataje) na akatumia kamba kushukia chini upande wa nje ya gereza. Kutokana na gereza kuwa karibu na barabara, Lustig alikuwa anashuka ukutani taratibu huku akizuga kusafisha vioo ili asitiliwe shaka ma wapita njia kwanini yuko juu ya ukuta.


Alishuka kwa mtindo huu taratibu taratibu huku akisimama kila mara kufuta vioo mpaka alipofika chini kisha akatokomea kusikojulikana.


Askari magereza walipokuja kukagua selo yake wakakuta amewaachia kipande cha karatasi chenye Ujumbe aliouandika kutoka katika kitabu cha Les Miserables. Ujumbe huo ulisema;


"Aliruhusu apelekwe katika ahadi; Jean Valjean alikuwa na ahadi. Hata kwa mfungwa, naam tena mahsusi kwa mfungwa. Inaweza kumpa mfungwa kujiamini na kumuongoza katika njia ya haki. Sheria haikuandikwa na Mungu na binadamu aweza kukosea."


Baada ya kutoroka ulianzishwa msako mkali na miezi michache baadae alikamatwa tena na safari hii bila kuchelewa alihukumiwa kifungo cha miaka 20 jela na kutokana na rekodi yake ya kutoroka akaamuliwa akatumikie kifungo katika gereza la Alcatraz. Gereza hili lilikuwa linaogopwa haswa kipindi hicho, lilikwa kama Guantanamo kutokana na mateso yake.


Gereza lilikuwa kisiwani, hivyo limezungukwa na maji pande zote hivyo hata mfungwa angesema atoroke asingeweza kuogelea mpaka kukutana na nchi kavu.


Lustig alifariki miaka michache baadae kutokana na baridi kali lililopitiliza katika gereza la Alcatraz ambalo lilimsababishia pneumonia kali.


Baada ya kifo chake, mchunguzi na mwanahistoria mashuhuri Tomas Andel alifanya kazi kubwa ya kwenda kupeleleza na kutafuta nyaraka katika nchi ya Austria-Hungary pamoja na nchi nyingine za jirani na baada ya uchunguzi wake wa muda mrefu akatoa sentesi moja tu ya kuhitimisha: hakuna mahali popote duniani kwenye nyaraka hata chembe inayothibitisha au kuonyesha kuwa Lustig alizaliwa hapo.


Badala ya majibu uchunguzi wa kufukua historia ya aisili ya Lustig unatoa maswali zaidi! Ina maana hakuzaliwa?? Kama alizaliwa je alizaliwa wapi??


Lakini ukweli wote ambao hakutaka kumwambia mtu yeyote alikufa nao yeye mwenyewe Victor Lustig, 'mpigaji' wa Daraja la Kwanza kuwahi kutokea katika historia.




Jiunge na Group langu la WhatsApp kusoma simulizi mpya kila siku. Kuna malipo ya 5,000/- kwa mwezi. Wasiliana nami 0759 181 457



The Bold.




0 comments:

Post a Comment

Blog