Search This Blog

Saturday 5 November 2022

I DIED TO SAVE THE PRESIDENT - 1

 




IMEANDIKWA NA : PATRICK CK



*********************************************************************************



Simulizi : I Died To Save The President

Sehemu Ya Kwanza (1)





I DIED TO SAVE MY PRESIDENT



Shughuli zote zilizopangwa kufanyika katika kikao cha bunge zilikamilika na kabla ya kusitisha shughuli za bunge kwa siku hiyo hadi siku inayofuata,spika wa bunge akamuita waziri anayeshughulika na bunge mheshimiwa William Kangoga ili aweze kutoa hoja ya kutengua kanuni “Meshimiwa Spika, naomba kwa ruhusa yako sasa nitoe hoja kwamba bunge lako tukufu litengue kanuni ya bunge ili kuwaruhusu vijana wetu wanafunzi waliofanya vizuri katika mithani yao ya kidato cha nne waweze kuingia bungeni hapo kesho.Mheshimiwa spika naomba kutoa hoja” Baada ya hoja ile kutolewa wabunge wote wakasimama na kuiunga mkono halafu spika akawahoji na wote wakakubalianana hoja ile kwamba kanuni ya bunge itenguliwe na kuwaruhusu wanafunzi ishirini waliofanya vizuri katika mitihani yao ya kidato cha nne waweze kuingia bungeni ili waweze kupongezwa na bunge. “Ahsanteni sana waheshimiwa wabunge kwa kukubali watoto wetu waje bungeni tuwapongeze na kuwatia moyo ili waweze kufanya vizuri zaidi huko mbele waendako.” Akasema spika wa bunge halafu akasitisha shughuli za bunge hadi siku inayofuata saa tatu za asubuhi ********************* Ni saa tano za usiku sasa lakini bado Patricia hakuwa na usingizi.Yeye na mama yake walikuwa katika chumba kilichoko ghorofa ya nne ndani ya hoteli hii kubwa mjini Dodoma ijulikanayo kama Dodoma view hotel.Ni moja kati ya hoteli yenye hadhi ya juu kabisa mjini Dodoma na ambayo wabunge wengi wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania hupenda kufikia . “Patricia mbona hulali?Si unajua siku ya kesho itakakuwa ndefu? Jitahidi ulale ili usije ukasinzia katika ukumbi wa Bunge” akasema Bi Doroth Mwaukala mama mzazi wa Patricia “Mama nashindwa kabisa kupata usingizi siku ya leo.Usiku nauona mrefu sana” akasema Patricia binti aliyejaaliwa uzuri wa kipekee mno “Una wasi wasi? “Ndiyo mama lakini si sana.Nawaza kuhusu kesho sijui itakuaje pale nitakaposhikana mkono na mheshimiwa waziri mkuu huku nikionekana katika televisheni nchi nzima.Mama sikuwahi kuota siku kama ya kesho itakuja kunitokea katika maisha yangu.Bado siamini hadi hapo nitakaposhikana mkono na waziri mkuu ndipo nitaamini ni kweli.Mama kesho ni siku yangu kubwa mno” akasema Patricia.Mama yake aliyekuwa akimtazama mwanae akatabasamu na kusema “Usiwe na hofu Patricia.Hii si ndoto bali ni kitu cha kweli kinachokwenda kutokea hapo kesho.Kama ingekuwa ni ndoto tusingekuwa hapa Dodoma mida hii katika hoteli kubwa na nzuri kama hii.Patricia unapaswa kujivunia mafanikio yako haya makubwa uliyoyapata.Mwanangu umenitoa kimaso maso mimi mama yako kwani hakuna aliyetegemea kama mwanafunzi aliyeshika namba moja nchini Tanzania atakuwa ni kutoka katika familia masikini kama ya kwetu.Umeidhihirishia nchi na dunia kwamba hata mtoto wa masikini anaweza akafanya mambo makubwa na ya kushangaza.Umelipandisha kileleleni jina la familia yetu na kwa sasa sisi si watu wa kudharaulika tena kama ilivyokuwa hapo awali.Laiti baba yako angekuwa hai kushuhudia tukio hili sipati picha angekuwa na furaha ya namna gani…” akasema Bi Doroth. “Mama sifa na shukurani zimwendee mwenyezi Mungu kwa neema na Baraka zake nyingi kwangu lakini sifa na shukrani za pekee pia ni kwako wewe mama.Wewe ndiye kila kitu kwangu na ndiye uliyefanikisha haya yote yakawezekana.Umenipa ushirikiano mkubwa.Maongozi na maelekezo yako yameniweka katika nafasi hii nilipo sasa.Mama unastahili sifa za kipekee kwa kunijali na kuwa nami na kunivumilia hata katika nyakati zile ngumu kabisa.Umejinyima mambo mengi ili mwanao niweze kusoma na haya ndiyo matunda yake” akasema Patricia halafu akainuka na kuelekea dirishani ,akalifungua na kuutazama mji wa Dodoma ulivyokuwa usiku hii. “ Huu ni mwanzo wa safari yangu ndefu ya maisha.Nina ndoto nyingi sana za kutimiza maishani na ndoto ya kwanza ni kuiondoa familia yangu katika umasikni huu mkubwa tulionao.Namuonea huruma mama yangu namna anavyohangaika kunisomesha.Lazima nikiri kwamba si kazi rahisi kwake lakini amejitahidi kwa kila namna na kuhakikisha kwamba hakuna siku nimekosa shule.Huyu ni mama anayestahili sifa za pekee kabisa.” Akawaza Patricia halafu akalifunga dirisha na kurejea kitandani “ Patricia jitahidi ulale.Muda umekwenda sana.Kesho tunatakiwa tuamke asubuhi na mapema” akasema Bi Doroth “ Mhh ! mama sijui kama nitaweza kupata usingizi.Sijazoea kulala sehemu laini kama hii” akasema Patricia na wote wakacheka “ Patricia unatakiwa uanze kuzoea vitu kama hivi.Huu ni mwanzo wako wa safari ndefu ya maisha yako.Siku moja vitu kama hivi utaviona vya kawaida.Jitahidi ulale” akasema Mama yake halafu akamfunika shuka vizuri akaenda kuzima taa wakalala. ********************* Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Patricia kuingia katika viwanja vya bunge.Aliustaajabia uzuri wa eneo hili.Hakukaukiwa na tabasamu.Siku hii alikuwa amependeza mno.Alivaa gauni lenye rangi nyeupe chini na juu likiwa na rangi nyeusi.Miguuni alivaa viatu virefu vilivyoendana na gauni alillolivaa.Mavazi haya ya gharama alizawadiwa na Juliana mwanamitindo maarufu hapa nchini ambaye alifurahishwa mno na matokeo ya Patricia. Wanafunzi bora ishirini walipokewa na katibu wa bunge halafu wakakabidhiwa kwa wafanyakazi wa bunge ambao walianza kuwatembeza sehemu mbali mbali za bunge .Patricia alionekana kuwa na furaha pengine kuliko wengine wote kwa sababu hakujua kama siku moja angeweza kufika mahala pale.Kati ya wanafunzi ishirini waliofanya vizuri mtihani wa kidato cha nne wengi walionekana kutoka katika familia bora zenye kujiweza kifedha.Ni Patricia pekee ambaye alitoka katika familia iliyo masikini zaidi lakini pamoja na umasikini wa familia yake iliyokuwa ikiishi katika chumba kimoja tu cha kupanga ,aliweza kuwaongoza wanafunzi wote nchini waliofanya mtihani wa kidato cha nne na kushika nafasi yakwanza. Kwa siku ya leo ingekuwa vigumu kuamini kwamba Patricia anatoka katika familia duni kwanamna alivyokuwa amependeza kwa mavazi aliyozawadiwa na mwanamitindo Juliana.Wakati amekaa na wenzake wakisubiri kuingia katika ukumbi wa bunge mara akatokea mama yake na kumuita pembeni “ Mama kuna nini mbona umefurahi namna hiyo? “ Patricia huwezi amini.Juliana amekuja .” “ Juliana?! Patricia akastuka “ Ndiyo “ Amekuja kufanya nini? “ Amekuja kukusapoti katika siku yako kubwa.” “ Kweli mama ?!! akauliza Patricia huku akiruka ruka kwa furaha “ Ndiyo Patricia.Anasema kwamba hakutaka kukutaarifu mapema kwamba atakuja alitaka akushangaze” “ mama yuko wapi dada Juliana? Nipeleke nikaonanane naye” akasema Patrcia na kwa haraka wakatembea hadi katika maegesho ya magari ambako Juliana alikuwa garini na rafiki yake aishiye mjini Dodoma.Mara tu Patricia alipotokea,Juliana akatoka garini na kumkumbatia “Wow ! Dada Juliana sikujua kama utakuja Dodoma”akasema Patrcia.Juliana akatabasamu na kusema “Sikutaka kukutaarifu mapema kama nitakuja Dodoma.I wanted to surprise you.Siwezi kukosa katika siku yako kubwa na muhimu kama hii ya leo.Patricia najua una wasi wasi sana na nimeona katika orodha ya watoto ambao utaambatana nao leo bungeni ,wote ni kutoka katika familia zenye uwezo mkubwa.Usiwe na wasi wasi you have a huge support” akasema Juliana na kumshika mkono Patricia wakaingia garini,akafungua mkebe mkubwa wa poda na kuanza kumremba halafu akavua heleni zake nzuri za dhahabu akamvisha.Akamuangalia na kutabasamu. “Now you look like a princes.Go now.Tutaonana baadae” akasema Juliana , Patricia akakimbia kwenda kuungana na wenzake.Uso wake ulikuwa na tabasamu zito.Baada ya Patricia kuondoka,Juliana akaagana na Bi Doroth kwa ahadi ya kuonana jioni ya siku hiyo katika sherehe ya kuwapongeza akina Patricia . “Juliana nakushukuru sana kwa msaada wako mkubwa.Umeweza kunifuta aibu kubwa siku ya leo. Bila wewe sijui Patricia angeonekanaje leo.Lakini kwa saabu yako leo Patricia ameng’aa na kupendeza kuliko wenzake wote” akasema Bi Doroth “ Mama hupaswi kunishukuru .Patricia ni kama mdogo wangu.Mimi ni mmoja wa watu walioguswa sana na matokeo yake mazuriNinathamini sana elimu hasa kwa mtoto wa kike na ndiyo maana nimeamua kwa moyo wangu kujitolea kumsaidia Patricia ili aweze kutimiza malengo yake.Bado ana safari ndefu sana na ili afikie malengo yake anahitaji sana sapoti yetu sisi sote” akasema Juliana halafu akaagana na Bi Dprpth na kuondoka kwa ahadi ya kukutana jioni . *************** Kipindi cha maswali na majibu kilimalizika , Spika wa bunge akasoma baadhi ya matangazo ikiwa ni pamoja na kuwatambulisha wageni waliofika hapo bungeni kwa mafunzo halafu akamuita katibu ili aweze kusema ni kitu gani kilichokuwa kinaendelea.Katibu akasimama na kulitaarifu bunge kwamba ni wakati wa kuwaruhusu wanafunzi waliofanya vizuri waingie bungeni wakabidhiwe vyeti na waziri mkuu.Spika wa bunge akasimama na kusema “Waheshimiwa wabunge ,jana tulitengua kanuni ya bunge ili kuwaruhusu watu ambao si wabunge kuingia ndani ya ukumbi wetu huu.Wageni tuliowaalika ni wanafunzi ishirini bora katika mtihani wa kidato cha nne .Naombeni wakati vijana wetu wakiingia humu ukumbini,muwashangilie kwa makofi kwani wamefanya kazi kubwa sana” Akasema Spika na kumuamuru askari wa bunge awaongoze wanafunzi kungia ukumbini .Lango kuu likafunguliwa na wanafunzi wakaingia wakiwa katika mistari miwili,mmoja wa wanaume na mwingine wa wanawake.Makofi mengi ,vigere gere pamoja na meza kugongwa vikasikika.Kilikuwa kipindi cha furaha sana kwa wabunge kuwashuhudia wanafunzi wale ishirini bora.Spika wa bunge akaomba utulivu halafu akamkaribisha waziri mkuu ili aweze kusema machache kabla ya kuwakabidhi vyeti.Waziri mkuu wa Tanzania mheshimiwa Thobias Kangeba kengaiza akasogea mbele na kusema “ Mheshimiwa spika naomba nikushukuru sana kwa kunipa nafasi hii niweze kusema machache kuhusiana na tukio hili.Napenda nikushukuru wewe na bunge lako kwa kukubali kutengua kanuni ili wanafunzi hawa waweze kukaribishwa bungeni na kupongezwa.Binafsi ninafuraha kubwa sana kuwaona wanafunzi hawa ingawa ningefurahi zaidi kama kungekuwa na uwiano sawa baina ya wavulana na wasichana kwa sababu naona kati ya wanafunzi bora ishirini wasichana ni nane tu na kumi na mbili ni wavulana.Kuna haja ya kuendelea kuwekeza zaidi katika elimu ya mtoto wa kike ili kuwe na uwiano sawa wa ufaulu.Pamoja na hayo ,kwa niaba ya serikali napenda kutoa pongezi zangu nyingi kwenu wanafunzi kwa ufaulu huu mzuri.Haikuwa kazi rahisi .Yalikuwa ni mapambano na leo hii mmeibuka vinara..Nawapongeza pia walimu na wazazi wenu kwa ushirikiano wao wa kuwasaidia kuwafikisha hapa mlipofika.” “Mheshimiwa spika,mfumo wetu wa elimu bado unakabiliwa na changamoto nyingi kama vile uhaba wa walimu,vitabu,vifaa vya kufundishia na kujifunzia,lakini serikali imekuwa ikjitahidi kutatua changamoto hizi na leo hii tunashuhudia mwanafunzi wa kwanza Tanzania ametoka katika shule ambazo zimejizolea umaarufu kama shule za kata ambazo zimekuwa na changamoto nyingi.” Makofi mengi yakapigwa halafu waziri mkuu akaendelea Mheshikiwa spika,ninaomba niseme kwamba hata kama tukifanikiwa kutatua changamoto zote zinazoikabiili sekta ya elimu hapa nchini lakini bila juhudi binafsi za wanafunzi wenyewe kamwe hakutakuwa na ufaulu mzuri.Kuna shule zenye walimu wa kutosha na vifaa vya kufundishia na kujifunzia lakini hazikufanya vizuri .Kwa hiyo basi naomba niwaase wanafunzi waongeze kasi ya kujisomea .Mwalimu ana nafasi yake lakini mwanafunzi pia ana nafasi yake.Ni vyema kila mmoja akaitumia vyema nafasi yake.” “Mheshimiwa spika naomba nimalizie kwa kutoa pongezi zangu nyingi kwa niaba ya serikali na kuwatakia kila la heri wanafunzi hawa katika safari yao ndefu.Someni kwa bidii na taifa linawasuri mje kulitumikia.Hongereni sana” akamalizia nasaha zake mheshimiwa waziri mkuu,wabunge wakamshangilia kwa kugonga meza halafu spika wa bunge akasimama “Tunakushukuru sana mheshimiwa waziri mkuu kwa nasaha zako.Natumai wanafunzi wote wamekusikia na watayafanyia kazi yale uliyowaasa Waheshimiwa wabunge kinachofuata sasa ni mheshimiwa waziri mkuu kuwakabidhi vyeti vijana wote ishirini.” Akasema Spika na zoezi la kutoa vyeti likaanza.Wa kwanza kuitwa kwenda kupokea cheti alikuwa Patrcia.Ukumbi wote wa bunge ukalipuka kwa makofi na kushangilia wakimpongeza msichana huyu kwa kushika namba moja.Zoezi lilipomalizika baadhi ya wabunge walipata nafasi ya kusema machache na kuwaasa wanafunzi kusoma kwa bidii.Kila aliyesimama hakuacha kumpongeza na kumtolea mfano





Patrcia.Kila mbunge alikunwa vilivyo na uwezo wa kipekee aliouonyesha binti huyu Hatimaye shughuli zote zilzopangwa kufanyika katika kikao cha asubuhi zikamalizika na spika akasitisha shughuli za bunge hilo hadi saa kumi na moja za jioni. Nje ya ukumbi wa bunge ,kila mbunge alitaka kumpa mkono na kumpongea Patricia.Waandishi wa habari hawakubaki nyuma katika kumuhoji Patricia na wenzake kuhusu siri ya ushindi wao.Baada ya zoezi lile kukamilika Patricia na mama yake wakaingia katika gari na kurudishwa hotelini ambako walipata chakula cha mchana kisha wakaenda chumbani kwao kupumzika na kujiandaa kwa ajili ya sherehe za pongezi zitakazofanyika jioni . “ Nimepokea simu nyingi toka kwa majirani zetu wote pale mtaani wakisema kwamba wamekuona katika teleisheni.Dah !http://deusdeditmahunda.blogspot.com/ Sikutegemea kama lingekuwa ni tukio kubwa namna hii” akasema Bi Doroth mama yake Patricia. “ Mama siku ya leo ni siku yangu ya furaha sana.Nashindwa niielezaje furaha niliyo nayo.Leo nimeshikaka mkono kwa mara ya kwanza na waziri mkuu.Ninaona ni kama muujiza.Nahisi ni kama ndoto” akasema Patrcia akiwa amekishika cheti alichopewa na waziri mkuu.Mama yake akatabasamu na kusema “ Haya pumzika Patricia .Bado kuna shughuli nyingine leo jioni.” akasema bi Doroth ******************* Saa kumi na mbili za jioni mrembo Juliana akawasili katika hoteli waliyofikia Patrcia na mama yake Wow !Patricia my dear …!!!” akasema Juliana kwa furaha na kumkumbatia Patricia “Karibu sana dada Juliana.” Akasema Patricia “ Ahsante sana Patrcia.Congraturations.It was your first time to enter that building and you showed a great confidence.Nilikuwa nakuangalia kupitia Luninga.Everybody is talking about you.Congraturations again” akasem Juliana “ Ahsante sana dada Juliana.Jumba lile ndiyo maana likaitwa tukufu.Linatisha kwa ndani kama ni mara yako ya kwanza kuingia” akasema Patricia “ Unavaa nini jioni ya leo? akauliza Juliana.Patricia akamuonyesha nguo ambayo alipanga kuivaa jioni hiyo Hapana usivae hiyo.You have to look like a queen .All eyes must be on you tonight” akasema Juliana na kufungua begi alilokuja nalo akatoa gauni refu jeusi lenye k u m e r e m e t a “Utavaa hili” akasema halafu akatoa vifaa vya urembo na kuviwe ka me zani akaanza kumremba Patricia.Baada ya k u m a l i z a k u m r e m b a akamuangalia na kutabasamu. Patricia you are blessed with the natural beauty.You deserve a miss world crown” akasema Juliana na wote wakacheka Baada ya kumaliza kumremba Patricia Juliana akaanza kumremba na Bi Doroth “ Ahsante sana Juliana kwa kuja kwako.Bila wewe sijui tungeonekana vipi” akasema Bi Doroth “ Usihofu mama.Nisingeweza kukosa tukio kubwa kama hili kwa ajili ya mdogo wangu “ akasema Juliana Saa moja na nusu za jioni tayari walikwisha jiandaa,wakaingia garini na kuelekea mahala inakofanyikia sherehe ya kuwapongeza akina Patricia.Endapo ungebahatika kumshuhudia Patricia jioni ya leo ungedhani ni mwanamitindo maarufu sana hapa nchini kwa namna alivyokuwa amependeza Waliwasili ukumbini wakapokelewa na kuelekezwa sehemu za kukaa. Patricia akawaacha mama yake na Juliana kwa ajili ya kwanda kukaa katika sehemu waliyokuwa wameandaliwa kwani Kulitengwa sehemu maalum ya wanafunzi kukaa . “ Patricia don’t be nervous.Always put a smile on your face.” Juliana akamnong’oneza Patricia sikino wakati akienda kuungana na wenzake katika sehemu waliyoandaliwa.Kama alivyokuwa ametazamia Juliana ndivyo ilivyokuwa ,Patrica alikuwa anameremeta na kila mtu alimtupia jicho. Bado waheshimiwa wabunge na wageni mbali mbali waliendelea kuwasili.Aliyekuwa akisubiriwa ni mgeni rasmi ambaye ni waziri mkuu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.Katika sherehe hii alikuwepo pia mke wa rais bi Bernadetha Jumbo ambaye ni mwanamke anayepambana sana kuhusiana na elimu ya mtoto wa kike. “ Hi” Patricia akasalimiwa na kijana mmoja mweupe mtanashati aliyevaa suti nzuri nyeusi iliyomkaa vyema.Kijana Yule alikuwa ni moja kati ya wanafunzi waliofanya vizuri.Patricia akageuza shingo na kumuangalia kijana Yule .Wote wawili wakatabasamu na kisha Patricia akasema “ Hi” Kijana Yule aliyekuwa na sura nzuri na vishimo mashavuni anapotabasamu akamnyooshea mkono Patricia na kusema “ Hongera sana”. Patricia akatabsamu na kusema “ Hongera nawe” Sisi sote tunapaswa kukupa wewe hongera kwani ndiye uliyetuongoza.” Akasema Yule kijana na kumfanya Patricia azidi kutabasamu “ Sote tumeshinda.Sote tuko katika kundi moja la ishirini bora” akasema Patricia halafu kikapita kimya kifupi Yule kijana akasema “ By the way I’m Elvis.” “ I’m Patricia.” Akajibu Patricia. “ Huna haja ya kujitamblisha Patricia.Hakuna mtu asiyekufahamu kwa sasa hapa nchini.Wewe ni mmoja wa watu maarufu sana hapa nchini” akasema Elvis na kumfanya Patricia atabasamu.Kabla hajasema kitu mwanamama mmoja ambaye ni mbunge akamsogelea na kusema Patricia nilikutafuta mchana pale bungeni sikukuona.Kuna jambo ambalo nilitaka nikufahamishe. Ni kwamba umechaguliwa kutoa neno la shukrani kwa niaba ya wenzako wote” “ Mimi ..?!! Patricia akauliza kwa mshangao “ Ndiyo wewe” “ Mheshmiwa sidhani kama nitaweza kuongea mbele ya umati huu mkubwa wa viongozi.Tafadhali naomba utafute mtu mwingine afanye hivyo mimi sintaweza” “ Hapana Patricia utaweza tu.Wewe ndiye uliyeshika namba moja kati ya wenzako wote kwa hiyo unapaswa kuwaongoza wenzako pia katika kutoa shukrani.” Patricia akafikiri kidogo na kusema “ Nitaenda kusema kitu gani? Akauliza Patricia kwa wasi wasi “ Say anything.Ili mradi liwe ni neno la shukrani.You can do it Patricia.Show all these people that you deserve to be number one” akasema Yule mbunge na mara Elvis aliyekuwa kimya akifuatilia maongezi kati ya Patricia na Yule mbunge akaingilia kati na kusema “ Madam usihofu nitamsindikiza mimi ili kumpa sapoti na kumfanya asiogope” akasema Elvis “ Good.Hilo ni jambo zuri.Patricia atakapoitwa utamshika mkono na kumuongoza mpaka pale mbele” akasema mbunge na kumgeukia PatriciaStart preparing yourelf.Itumie vyema nafasi hii” akasema Yule mbunge na kuondoka.Patricia alionekana kuingiwa na woga mwingi “ Usiogope Patrcia.You can do it” akasema Elvis. “ Sijawahi kuongea mbele ya hadhira kubwa kama hii tena kukiwa na viongozi wa juu wa serikali.” Akasema Patricia “ Patricia kama umeweza kuwazidi akili wanafunzi wote wa Tanzania na ukashika namba moja ,huwezi kushindwa kuongea neno pale mbele.Just say anything you want to say” “ C’mon Elvis,ule ulikuwa ni mtihani na hatufanyi kwa kuongea.I don’t know what I have to say” Elvis akamtazama Patricia usoni akatabasamu na kusema “ Unataka nikuandikie kitu cha kwenda kuongea pale mbele? “ No ! don’t do that” akasema Patrcia na kuinuka akaelekea katika meza waliyokuwa wamekaa mama yake pamoja na Juliana.Akamuita Juliana pembeni “ Patricia whats wrong? Naona sura yako imebadilika.Unaogopa nini? “ Dada Juliana kuna kitu nimeambiwa muda huu ambacho kimenistua kidogo” “ Kitu gani Patrcia? “ Nimeambiwa kwamba mimi ndiye nitakayetoa neno la shukrani kwa niaba ya wenzangu .Nimestukizwa na sijafanya maandalizi yoyote.Sielewei nitasema nini pale mbele ya viongozi hawa wakubwa wa kiserikali.” Akasema Patrcia “ Kwa nini hawakukutaarifu toka mapema ukafanya maandalizi? Akauliza Juliana “ hata mimi sielewi ni kwa nini wamefanya hivi .This is unfair.Wangenieleza toka mapema ili nijiandae akalalama Patricia.Juliana akatabasamu akamshika bega na kusema “ Relax my dear.Relax.Put back your smile .Usikwazike na hilo.Wamekuchagua kwa sababu wanajua una uwezo mkubwa kwa hiyo ukiitwa pale mbele nenda kawaonyeshe kwamba unaweza na unastahili kuwa namba moja Tanzania.Waonyeshe kwamba hukubahatisha kushika nafasi hiyo.Jambo lingine jihadhari na matumizi ya lugha.Usichanganye lugha.Ongea Kiswahili fasaha na kilichonyooka.I believe in you Patrcia.You can do it.Go and make your mom proud.make us all proud my dear” akasema Juliana na kumfanya Patricia atabasamu. “ dada Juliana nitaenda kusema nini pale mbele? I’m a bit scared” Akauliza Patricia “ say anything you want to say.Ongea neno lolote la shukrani unalolijua.This is your time.Waandishi wa habari wako hapa na wote watayaelekeza macho yao kwako.Wamekupa nafasi hiyo makusudi ili kukupima kwa hiyo wadhihirishie kwamba unastahili” akasema Juliana na mara ikasikika sauti ya muongoza shughuli akiwataka watu wote walio nje ya ukumbi kuingia ndani kwani muda wowote sherehe zinarajia kuanza. “ Watu waliokuwa nje wakaingia ukumbini na sherehe zikaanza.Ilikuwa ni sherehe nzuri iliyoambatana na hotuba za viongozi mbali mbali akiwemo waziri mkuu na mke wa rais.Baada ya hotuba za viongozi kikafuata kipindi cha utoaji wa tuzo na zawadi kwa wanafunzi wote na shule zilizofanya vizuri zikatolewa. Baada ya zoezi lile kukamilika ,muongoza shughuli akawafahamisha watu kwamba ni wakati wa chakula na baada ya chakula Patricia akaitwa mbele ili aweze kutoa neno la shukrani kwa niaba ya wenzake.Ukumbi wote ukalipuka kwa shangwe baada ya Patrcia kuinuka na kuanza kuelekea mbele ya ukumbi akiwa ameongozana na kijana mtanashati sana Elvis.Uso wake haukukaukiwa tabasamu.Akafika mbele na kukabidhwa kipaza sauti.Ilikuwa ni mara yake ya kwanza kukishika na kukitumia.Mikono ilikuwa inamtetemeka na midomo kumcheza kiasi kwamba alishindwa aanze vipi.Watu wote wakakaa kimya tayari kumsikiliza .Mara maneno ya Juliana yakamjia kichwani. “Wamekuchagua kwa sababu wanajua una uwezo mkubwa kwa hiyto ukiitwa pale mbele nenda kawaonyeshe kwamba unaweza na unastahili kuwa namba moja Tanzania.Waonyeshe kwamba hukubahatisha kushika nafasi hiyo” I have to do it..I can do it” akasema moyoni na kwa ujasiri akakishika vizuri kipaza sauti akakohoa kidogo kurekebisha koo na kusema “ Mheshimiwa waziri mkuu,mpendwa mama yetu mke wa rais,waheshimiwa mawaziri ,wabunge na viongozi wengine wa serikali,walimu ,wazazi , wanafunzi wenzangu,wageni waalikwa mabibi na mabwana,ninapenda kumshukuru sana mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutujalia wote kuwepo hapa usiku huu.” Maneno haya ya utangulizi yakazidi kumpa ujasiri .Akaendelea “ Waheshimiwa viongozi ,wageni waalikwa mabibi na mabwana nimesimama mbele yenu kwa unyenyekevu mkubwa ili kutoa neno la shukrani kwa niaba ya wanafunzi wenzangu wote tulioko hapa usiku huu” Akatulia kidogo halafu akaendelea “ Baba yangu alifariki nikiwa darasa la tano.Alifariki kwa ajali ya gari.Kifo chake kiliacha pengo kubwa sana kwangu na kwa familia yangu .baba yangu hakuwa tajiri kwa hiyo alipofariki hakutuachia mali yoyote hali iliyomlazimu mama yangu ashike nafasi zote mbili yaani kama baba na kama mama.Mama yangu Bi Doroth ambaye niko naye hapa usiku huu,hakuwa na kazi ya maana zaidi ya kufua nguzo katika majumba ya wahindi.Pamoja na kazi hiyo yenye ujira mdogo lakini bado alielekeza nguvu zake zote katika kuhakisha kwamba hata hicho kidogo alichokuwa akikipata katika kazi zake za ufuaji anakitumia katika kuniendeleza kielimu.Aliamini kwamba elimu pekee ndiyo itakuwa mkombozi wangu.” Patricia akanyamaza na kuitazama hadhira ile iliyokuwa kimya ikimsikiliza halafu akaendelea “Nilichaguliwa kuendelea na elimu ya sekondari katika moja ya shule zile zenye umaarufu kama shule za kata.Ni shule yenye changamoto nyingi,hatukuwa na walimu wa kutosha,vifaa vya kutosha vya kujifunzia n.k.Pamoja na hali hiyo bado mama yangu aliendelea kuniunga mkono katika kila hatua niliyopiga.Alininunulia vitabu na kunilipia masomo ya ziada.Kuna nyakati ilimlazimu kukaa nami hadi usiku katika sehemu niliyokuwa nikijisomea aidha na wenzangu au masomo ya ziada ili kuhakikisha kwamba ninarudi nyumbani nikiwa salama .Alikuwa mkali sana kila pale ambapo sikufanya vizuri shuleni jambo ambalo lilinifanya niongeze bidii sana katika masomo na hatimaye leo hii nimesimama mbele yenu enyi waheshimiwa sana nikiwa mwanafunzi niliyeshika namba moja katika mtihani wa kidato cha nne nchini Tanzania” Makofi mengi na vigere gere vikapigwa.Bi Doroth mama yake Patricia alishindwa kujizuia kutokwa na machozi..Patricia akaendelea







Najua mtajiuliza ni kwa nini nimeyasema haya yote.Nimeyasema haya yote kwanza kutoa shukrani zangu za kipekee kwa mama yangu kipenzi ,walimu wangu na walezi wangu walionisaidia mimi binafsi kufika hapa nilipofika.Ni wengi wamenisaidia na sintaweza kuwataja wote kwa majina lakini kwa ujumla wao ninasema ahsanteni sana” makofi mengi yakapigwa “ Pili nimeyasema haya yote ili kuonyesha wazi kwamba mafanikio ya mtoto yanachangiwa na mambo mengi lakini kubwa ni ushiriki wa mzazi.Pamoja na umaskini wake mama yangu ameshirikiana nami katika kila hatua niliyopiga.Pale nilipoanguika alikuwa mtu wa kwanza kunipa moyo nikainuka nikasonga mbele.Mama huyu ni mfano wa kuigwa na wazazi wote.Kushindwa kwa wanafunzi wengi kunachangiwa kwa kiasi kikubwa na ushirikiano mdogo wa wazazi .Sisi wanafunzi ishirini tulioko hapa tulioko hapa usiku huu tumepata mafanikio haya kwa juhudi za wazazi wetu.Ahsanteni sana wazazi wote mlioko hapa kwa juhudi zenu na ushirikiano mnaowapa watoto wenu.Kwa wale wazazi na walezi ambao hawako karibu na watoto wao,ni wakati wenu wa kubadilika.Watoto wenu wanawahitaji sana.Kwa niaba ya wenzangu wote tunawashukuru nyote kwa mapokezi mazuri,pongezi mlizotupa na zawadi nzuri mlizotuzawadia.Tumejifunza mengi toka kwenu na tutasoma kwa bidii sana kwani tumetambua nchi yetu inatuhitaji sana.Tunawatakia nyote afya njema na mafanikio katika kufanikisha majukumu mliyonayo kwa taifa.Ahsanteni na Mungu awabariki.” Patricia akamaliza na kumkabidhi muongoza shughuli kipaza sauti.Watu wote walikuwawamesimama wakipiga makofi.Wote walikunwa na maneno yale na kuduwazwa kwa uwezo mkubwa aliokuwa nao Patricia.Patriciai akaongozwa akaenda kupeana mkono na waziri mkuu ,kisha mke wa rais na viogozi wengine wa meza kuu halafu akageuka na kuanza kupiga hatua kurejea kitini lakini muongoza shughuli akamzuia Ndugu wageni waalikuwa ,mabibi na mabwana,nadhani nyote mmeshangazwa na uwezo mkubwa alio nao binti yetu Patricia.Ameongea maneno mazito sana na nina imani kila mmoja wetu hapa ameguswa .Miongoni mwa watu walioguswa ni mama Bernadetha Jumbe mke wa rais wetu ambaye anataka kusema neno.Karibu sana mama”akasema muongoza shughuli na makofi mengi yakapiga.Bi Bernadetha Jumbo mke wa rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania akasimama na kuelekea mbele akapewa kipaza sauti. “ Waheshimiwa wageni waalikwa mabibi na mabwana,nimesimama mbele yenu tena kutokana na kuguswa na maneno mazito aliyoyasema binti yetu Patricia.Ni maneno yenye ukweli na ametukumbusha wajibu wetu sisi kama wazazi, ambao wengi wetu tumeusahau.Napenda kuchukua nafasi hii kumpongeza kwa namna ya pekee kabisa Patricia kwa ufaulu wake mzuri.Ameonyesha njia na kuwa mfano wa kuigwa na wengine hasa watoto wa kike.Ninampongeza kwa namna ya pekee pia kwa sababu amepitia changamoto nyingi sana katika maisha yake hadi hapa alipofika,changamoto ambazo zingepelekea yeye ashawishike kuingia katika mambo yasiyofaa na kumuharibia kabisa muelekeo mzima wa maisha yake lakini yeye hakuanguka na alielekeza akili yake katika kitu kimoja tu ,kusoma.Watoto wengi wa kike hushawishika kuingia katika mambo yasiyofaa kutokana na changamoto mbali mbali wanazokutana nazo katika maisha yao ya kila siku na wakati mwingine ni tamaa tu ya kutaka kuishi maisha yasiyolingana na uwezo wao . “Binafsi nimeguswa sana na historia ya Patricia na kuanzia sasa ninatangaza kwamba nitagharamia mimi gharama zote za masomo yake hadi atakaposema imetosha.” Makofi mengi na vigere gere vikapigwa halafu akaendelea “Mama yake Patricia ni mama wa mfano.Ametufundisha namna bora ya kulea watoto wetu.Pamoja na changamoto kubwa ya kipato inayomkabili ,ameweza kufahamu umuhimu wa elimu kwa mtoto wake na akaelekeza nguvu zake zote katika kuhakikisha kwamba mwanae anasoma.Hongera sana mama Patricia na ninakuomba kokote ulipo sogea hapa mbele. Tafadhali” Mama yake Patricia akasimama na kuanza kusogea mbele huku akishangiliwa kwa nguvu.Akakumbatiana na mke wa rais kwa furaha “ Hongera sana mama Patricia.Juhudi zako zimeonekana.Wazazi wote natumai wataiga mfano wako na kuwekeza kila walichonacho katika elimu ya watoto wao.” Akasema Bi Bernadetha huku akimpa mkono wa pongezi mama Patricia halafu akaendelea “ waheshimiwa wageni waalikwa mabibi na mabwana,mimi pia ni mama na ninaufahamu ugumu uliopo katika ulezi wa familia na hasa ukiwa peke yako.Kwa maana hiyo ninamuunga mkono mwanamke mwenzangu kwa kumpatia mtaji wa biashara wa shilingi milioni tano ili aachane na kazi ya ufuaji anayoifanya na afungue biashara ambayo itamuwezesha kujikimu yeye na familia yake.” Bi Bernadetha akashangiliwa kwa nguvu sana na kelele zilipopungua akaendelea “ Najua wengi wenu hapa mmeguswa kama nilivyoguwa mimi kwa hiyo kama nawe unajisikia kumsaidia chochote mama Patricia unakaribishwa kufanya hivyo.Pita hapa mbele umpongeze mama huyu ambaye ninaweza kumuita ni jasiri” Kauli ile ya mama Bernadetha ilikuwa ni kama imewasha moto kwa waheshimiwa wabunge kwani ndani ya dakika chache Patricia na mama yake walikuwa wanaoga pesa.Elvis na Juliana walikuwa na kazi ya kukusanya fedha walizotunzwa Patricia na mama yake. Baada ya zoezi lile kumalizika mama Patrcia akapewa kipaza sauti ili aweze kutoa neno la shukrani kwa niaba ya wazazi wote “ Sina maneno mengi ya kusema ila ninaomba nimshukuru sana mama Bernadetha Jumbo kwa moyo wake wa huruma na kwa msaada wake mkubwa kwangu.Kwa kweli changamoto ni nyingi sana ukiwa kama mzazi mmoja na kubeba majukumu yote ya ulezi peke yako lakini namshukuru Mungu nimeweza kuvuka vikwazo vyote na mwanangu ameweza kusoma japo kwa shida.Naomba nikiri kwenu kwamba haikuwa kazi rahisi lakini kwa kuwa ninaamini kwamba elimu ndiyo urithi pekee ninaoweza kumpatia mwanangu basi nilijifunga mkanda kuhakikisha kwamba mwanangu anasoma.Kuna nyakati ilinilazimu kusoma pamoja naye japokuwa nilikuwa nafunua tu vitabu na kutazama picha bila kuelewa chochote” Watu wote ukumbini wakaangua kicheko “ Nawasihi wazazi wenzangu wote mlioko hapa na wale walioko majumbani,tujenge urafiki na watoto wetu na tuwe nao karibu katika kuwapa msaada wanaouhitaji kila mara.Tuwasaidie hawa watoto hasa wa kike ambao wanakabiliwa na vishawishi vingi sana.Mwisho napenda kuwashukuru nyote kwa michango yenu wote.Mungu awabariki sana” akasema mama Patricia na kwa mara nyingine tena akashikana mkono na mke wa rais halafu akarejea kukaa mahala pake akifuatana na Juliana aliyekuwa amebeba pochi lililojaa fedha. Zoezi lililofuata lilikuwa ni burudani toka katika kikundi cha sanaa za ngoma za asili. “ Hongera sana Patricia ulifanya vizuri..Usiku wa leo umedhihirisha kwamba unastahili kuwa namba moja..” akasema Elvis wakati burudani ya ngoma ikiendelea.Patricia akatabasamu na kusema “ Ahsante sana Elvis.Ulinisaidia sana kuniondolea uoga” akasema Patricia. “ Usijali Patricia .Ni jambo la kawaida kuwa na uoga unaposimama mbele ya hadhira kubwa kama hii.Pamoja na uoga wote uliokuwa nao lakini umeweza kuongea maneno mazito yaliyomgusa kila mmoja na hata mimi niliguswa pia.Umenikumbusha baba yangu alikuwa ni rafiki yangu mkubwa.Ilikuwa ni ndoto yake siku moja nifike mbali sana kielimu.”akasema Elvis “ Alikuwa ?! ..Patricia akashangaa Ndiyo.Baba yangu alifariki mwaka juzi.Mimi na wewe sote tumebakiwa na mzazi mmoja tu” “ Dah ! pole sana Elvis” “ Ahsante.Pole nawe” akasema Elvis halafu kimya kikapita “ Patricia unaishi wapi kwa sasa? Akauliza Elvis “ Naishi Kimara Baruti Dar es salaam.Wewe unatokea wapi? “ Mimi natokea Arusha .Ninaishi Njiro.Karibu sana Arusha uje utembee siku moja.Karibu uje utembelee mbuga za wanyama na vivutio mbali mbali vya kitalii” akasema Elvis na kumfanya Patricia atabasamu “Nitakuja kutembea siku moja.Natamani sana kufika Arusha” “ Ukija nitakuwa mwenyeji wako” akasema Elvis Ahsante ila naomba nikupe tahadhari mapema kwamba sintakuwa na hela ya kukulipa kama muongozaji watalii” Elvis akacheka sana na kusema “ Sintakutoza fedha nyingi kwa kuwa wewe ni mtalii wa ndani.Tuna nyumba Dar es salaam Mbezi,na mimi siku moja nitakuja Dar na wewe utakuwa mwenyeji wangu” “ Usijali kuhusu hilo.Nimezaliwa na kukulia Dar kwa hiyo ninalifahamu vyema jiji” akasema Patricia. Baada ya burudani ya ngoma za asili kumalizika mheshimiwa waziri mkuu akafungua muziki na watu wote wakajumuika ukumbini kulisakata rhumba. “ wakati wa muziki sasa.Can we dance? Akauliza Elvis.Patricia alionekana kuogopa na kuona aibu.Wanafunzi wenzao walikuwa wanainuka na kujumuika na wabunge katika kuusakata muziki “Ninaogopa sijawahi kucheza hata mara moja.” Akasema Patricia Wakati Elvis akimuomba Patricia waende wakacheze muziki mara akatokea mama yake akiwa ameongozana na ndugu wengine watano. “ Elvis sherehe imemalizika.Ni wakati wa kuodnoka sasa.Tunatakiwa tupumzike kwani kesho tuna safari ndefu ya kurejea Arusha.Sitaki kuendesha gari nikiwa nimechoka. Akasema mama Elvis “ Mama kabla ya yote kutana na Patricia.Yeye ndiye aliyetuongoza wote na kushika namba moja.Ni rafiki yangu wa kwanza kukutanana naye ambaye nitakuwa naye pale J.Y.Makamba school of science.” Elvis akamtambulisha Patricia kwa mama yake “Patricia huyu ni mama yangu anaitwa Mrs Tarimo na hawa wengine ni ndugu zangu walionisindikiza kwa ajili ya sherehe hii” Patricia akainuka na kwa adabu akamsalimu mama Elvis. “ Shikamoo mama” “ Marahaba Patricia.Nafurahi kukutana nawe.Hongera sana kwa kufanya vizuri” “ Ahsante sana mama.Hata mimi nafurahi kukutana nawe.Hongera pia kwa Elvis kwani naye amefanya vizuri sana” Amejitahidi ameshika namba nane.Nilitegemea labda angekuwepo katika nafasi tatu bora.Kwa kuwa mtakuwa wote shule moja naomba umkazanie sana mwenzio aongeze juhudi na kidato cha sita nyote muwe katika nafasi tatu za juu” akasema mama Elvis. Usihofu mama.Kidato cha sita Patricia hatanishinda tena.Nitamshusha toka namba moja” akasema Elvis na wote wakacheka “ Patricia unaishi wapi? “ Mimi natokea Dar es salaam” “ Ouh vizuri sana.Sisi tunaishi Arusha japokuwa hata Dare s salaam tuna nyumba pia.Karibu sana Arusha ututembelee siku moja” Ahsante sana mama.Tayari Elvis ameshanialika nije Arusha siku moja na nitakuja pale nipatapo nafasi” “Ouh kumbe ameshakukaribisha.Huyu naye huwa hachelewi.Haya ukipata nafasi tafadhali njoo ututembelee” “ Ahsante sana mama nitakuja siku moja” “ Haya Patricia sisi tunaondoka,tunatakiwa tukapumzike kesho asubuhi tuna safari ya kurejea Arusha.Nakutakia safari njema ya kurejea Dar es salaam” “ Nashukuru sana mama.Nami nawatakia safari njema ya kurejea Arusha” akasema Patricia. “ Mama tangulieni katika gari nitakuja baada ya muda mfupi.Nataka kuagana na Patricia “ akasema Elvis na mama yake huku akitabasamu akaondoka kuelekea garini “ Mama yako mcheshi sana” akasema Patricia “ Usimuone akiongea kwa upole namna ile.Ni mkali sana akiwa nyumbani.Tuachane na hayo,Patricia nashukuru sana kukutana nawe .Kwa kuwa sote tunakwenda kuendela na masomo katika shule moja,nina imani tutazidi kuwa marafiki sana.” “ Hata mimi nafurahi sana kukutana nawe Elvis.” Akasema Patricia “Patricia najua hatutaonana tena hadi tutakapokutana shuleni.Unaweza ukanipa namba yako ya simu ili mara moja moja niwe nikikupigia simu na kukujulia hali” Patricia akatabasamu na kusema “ Sina simu Elvis” “ Huna simu?!....Elvis akashangaa “ Ndiyo sina simu” akajibu Patricia. “ C’mon Patricia ina maana hufanyi mawasiliano? “Nikitaka kuwasiliana na mtu hutumia simu ya mama” “Ok..! Ok ! ..Nipe basi namba ya simu ya mama” “ Hapana Elvis.Nipe wewe namba zako na nitakupigia simu mimi nikipata nafasi.” Elvis akaandika namba zake za simu na kumpatia Patricia halafu wakaagana na kuondoka.Watu bado waliendelea kujimwaga ukumbini wakilisakata rhumba.Patricia akamfuata mama yake aliyekuwa amesimama na kundi la wabunge wanawake wakimpongeza Sherehe zilipomalizika Patricia na mama yake wakarejeshwa hotelini “Dah ! ilikuwa ni siku ndefu sana” akasema mama Patricia. “ Ilikuwa siku ndefu lakini nzuri.Mama nimefurahi sana leo.Hii ni siku kubwa katika maisha yangu” akasema Patricia “ Hata mimi nimefurahi sana.Unajua pale ulipoitwa uende mbele kuongea neno la shukrani nilistuka sana kwani nilijua hujajiandaa kitu cha kuongea lakini Juliana alinitoa wasi wasi na kuniambia nisihofu.Ulipoanza kuongea kijasho kilikuwa kinanitoka lakini mwishowe nilijikuta nikitoa machozi.Patricia Mungu amekujalia akili ya kipekee kabisa.Ahsante sana kwa maneno yale mazito ambayo yalichoma mioyo ya kila mmoja pale ukumbini.Ni kwa maneno yale mazito tumefanikiwa kupata kiasi hiki cha fedha.Bado siamini macho yangu.” Akasema mama Patricia na kulifungua pochi lake kubwa na kumwaga pesa kitandani. “ Wow ! ..Patricia akatabasamu “ Patricia tunapaswa kumshukuru sana Mungu kwa muujiza huu mkubwa.Jana tulikuwa hatuna hata fedha ya kununua sukari lakini leo hii tuna fedha hizi nyingi.Ouh Mungu ahsante sana kwa jambo hili kubwa” akasema mama Patricia na kuanza kuzihesabu fedha zile..Jumla zilikuwa ni shilingi million mbili laki saba na sabini.Bi Doroth hakuamini macho yake.Machozi ya furaha yakamtoka.Akakumbatiana na mwanae “ Basi usilie mama.Ni wakati wetu wa kufurahi na kumshukuru Mungu kwani maisha yetu yanaanza kuonyesha nuru.Pesa hizi na zile alizokuahidi mama Bernadetha zinatosha sana kuanzisha mradi wowote ambao utatuwezesha kujikimu na kututoa katika lindi hili la umasikini mkubwa” akasema Patricia “ Patricia mwanangu lazima nilie kwa sababu nikikumbuka taabu nilizozipata katika kukusomesha.Mungu pekee ndiye anayejua.Ninawashukuru wote waliotuchangia fedha hizi ambazo ni nyingi na zinatosha kabisa kuanzisha bashara.Tunatakiwa tukae na tubuni biashara ya kufanya.Mimi nina wazo moja.Siku ya jumatano







nitakapokwenda kuonana na Mama Bernadetha katika taasisi yake kama alivyonitaka,nitamuomba anisaidie nipate walau shamba au kiwanja ili niweze kuanzsha mradi wa ufugaji kuku.Unaonaje kuhusu wazo hili? “ Hilo ni wazo zuri sana mama lakini nina imani utakapoonana naye na kumweleza hali yako ,yeye mwenyewe anaweza akatafuta njia bora zaidi ya kukusaidia” akasema Patricia huku akiuvua mkufu wa dhahabu na mara akamkumbuka Juliana “ Dada Juliana amefanya kazi kubwa sana na amenifanya nipendeze na kusifiwa na kila mtu leo ” akasema “ Ni kweli Patricia.Tunapaswa kumshukuru mno Juliana kwa wema wake kwetu.Amesafiri toka Dar es salaam hadi huku Dodoma kuja kuungana nasi.Ana moyo wa huruma sana Yule binti.” Akasema mama Patricia halafu akanyamaza kana kwamba kuna kitu anakikumbuka,akauliza “ Patricia Yule kijana aliyekusindikiza pale mbele ulipokwenda kutoa shukrani ,mnafahamiana? Swali lile likamstua kidogo Patricia “ Unasema Elvis? “ Simfahamu kwa jina .Umesema anaitwa Elvis? “ Ndiyo mama anaitwa Elvis.Nimefahamiana naye pale pale katika sherehe.Yeye ameshika namba nane na anatokea Arusha.Kitu ingine ni kwamba wote tumechaguliwa kuendelea na kidato cha tano katika shule moja.Kuna tatizo lolote mama? “ Hapana hakuna tatizo lakini kama unavyofahamu kwamba sitaki ulewe sifa na kubadilika.Safari yako ndiyokwanza imeanza.Masuala ya vijana mimi sitaki kuyasikia.Kama ni urafiki uwe ni wa kusaidiana katika masomo tu na si vingnevyo.Nitakuwa mkali sana katika hilo na ninakuomba usinione mbaya.Nataka ufahamu kwamba utakapokwenda huko shuleni utakuwa peke yako.Hautakuwa na mimi tena.Kwa hiyo zingatia yale yote ambayo nimekuwa nikikuelekeza japokuwa una uwezo wa kufanya maamuzi yako mwenyewe kwa sababu wewe ni binti mkubwa sasa na unafahamu jema na bayaa.Unazifahamu ndoto zako kwa hiyo pambana ili kuzitimiza.” Akasema mama Patricia.Patricia akatabasamu na kumsogelea mama yake. “ Mama usiwe na hofu na mimi hata kidogo.Ninajitambua mimi ni nani na malengo yangu ni nini kwa hiyo nakuomba usiwe na wasi wasi hata kidogo.Sintakuangusha mama yangu.Naomba uniamini” Patricia akasisitiza “ Nakuamini Patricia lakini lazima nikukumbushe mara kwa mara kwamba kwa sasa wewe ni binti mkubwa na unazidi kuwa mrembo.Urembo wako ni kama ua lenye harufu nzuri ambalo huvutia nyuki wengi kulifuata.Urembo wako ukichanganya na jina ambalo umelipata hivi sasa ni vichocheo tosha kabisa kuwafanya wanaume wengi ,vijana kwa wazee kuanza kukuzengea na katika umri huu mwili nao hukumbana na vichocheo na vishawishi vingi.Wasichana wengi huanguka vishawishini katika kipindi hiki. Patricia mwanangu,umeweza kujilinda kwa miaka minne na nina imani utaweza pia kwa hiyo miaka miwili na mingine mingi utakayokuwa masomoni.Kamwe usikubali kuanguka vishawishini.Mapenzi yapo na utaondoka utayaacha.Tengeneza kwanza maisha yako na mambo mengine yatafuata baadae.Naomba usiyasahau maneno haya ambayo ni kwa faida yako wewe mwenyewe” akasema Bi Doroth “ Mama siwezi kuyasahau.Siku zote maneno yako yamekuwa ni dira na ngao yangu.Nakuhakikishia mama kwamba siwezi kuanguka na nitamuweka Mungu mbele siku zote.Usichoke kuniombea” “ Mimi nitakuombea bila kuchoka lakini hata wewe pia unatakiwa usimame imara katika maombi” Ulikuwa ni usiku mrefu sana kwa Bi Bernadetha na binti yake.Waliongea mambo mengi sana kuhusiana na maisha yao.Walikumbushana mambomengi kuhusu waliyoyapitia katika maishayao na ilipotimu saa tisa za usiku wakalala. ********************** Siku sita zimekwisha pita toka Patricia arejee toke Dodoma.Maisha yao yalianza kuwa na mabadiliko.Tayari Bi Doroth amekwisha onana na mke wa rais na akampatia kiasi cha fedha alichomuahidi.Mke wa rais pia alikwenda mbali zaidi na kuahidi kumpatia kiwanja ili aweze kujenga nyumba walau nyumba ndogo ya kushi yeye na mwanae Patricia pamoja na kufanya kazi ya ufugaji kama alivyokuwa amepanga.Mwanga ulianza kuonekana katika maisha yao Ni siku ya Ijumaa saa nne asubuhi mrembo Juliana akawasili nyumbani kwa akina Patricia.Akashuka toka ndani ya gari lake aina ya Mercedece Benz jeusi na kuwasalimu akina mama waliokuwa kibarazani wakiendelea na shughuli za usafi halafu akanyoosha hadi katika chumba cha akina Patricia akagonga na mama Patricia ndiye aliyefungua mlango “ Ouh ! Juliana ! Karibu sana” akasema Bi Doroth “ Ahsante sana mama.Shikamoo” akajibu Juliana “ Marahaba Juliana.karibu sana.Karibu ndani” akasema mama Patricia huku akiweka vitu vizuri ili Juliana aweze kupita “ Karibu sana Juliana.Habari za toka majuzi? Habari nzuri mama .Habari za hapa? “ habari za hapa nzuri.Sijui huko kwenu” “ Kwetu kwema mama.Vipi Patricia hajambo? Hajambo ,nimetuma hapo dukani atarejea muda si mrefu” “ Mama leo ndiyo ile siku niliyokuwa nimeamuandalia Patricia ile sherehe ndogo ya kumpongeza nyumbani kwetu.Watakuwepo marafiki wachache tutakaojumuika pamoja” akasema Juliana “ Juliana ahsante sana lakinu utanisamehe kwani sintaweza kuhudhuria.Hivi unavyoniona nina miadi ya kuonana na mama Imelda Kulangwa ambaye ameelekezwa na mke wa rais aende akanionyeshe kiwanja alichoninunulia.Utakwenda na Patricia” Patricia akatabasamu na kusema “ Ouh hizo taarifa njema sana mama.Kama umepata kiwanja tutasaidiana masuala ya ujenzi.Nina rafiki yangu mmoja ana duka la vifaa vya ujenzi tutamtumia huyo kupata vifaa vya ujenzi” “ ahsante sana Juliana” akajibu Bi Doroth na mara mlango ukafunguliwa Patricia akaingia “ wow ! Dada Juliana” akasema kwa furaha na kumkumbatia Juliana “ Karibu sana dada Juliana” akasema Patricia “ Ahsante sana Patricia” akajibu Juliana halafu akamfahamisha Patricia kwamba amekuja kumchukua ili aende akashinde nyumbani kwao ambako kuliandaliwa sherehe ndogo ya kumpongeza.Patricia alijiandaa haraka haraka halafu akapanda katika gari la Juliana wakaondoka.Breki ya kwanza ilikuwa Sabina beauty saloon ambako Patricia alirembwa “ Wow ! Patricia you are so beautifu.You are amazing” akasema Juliana baada ya Patricia kumaliza kurembwa.Toka hapo walielekea katika maduka ya nguo na urembo ambako Juliana alimnunulia Patricia vitu mbali mbali halafu wakaelekea nyumbani kwa akina Juliana Geti kubwa jeusi lilifunguliwa wakaingia katika jumba kubwa lenye rangi nyeupe.Patricia akatabasamu kwa uzuri wa jumba lile. “ Patricia hapa ndipo ninapoishi.Kwa sasa ninaishi mimi, mdogo wangu Godson pamoja na binamu zetu wawli.Baba mama na mdogo wetu wa mwisho wanaishi nchini Afrika kusini ambako baba nafanya kazi katika shirika moja la kimataifa.” Akasema Juliana kabla ya kushuka garini “ Nafurahi kupafahamu nyumbani kwenu dada Juliana.Ni nyumba nzuri sana nimeipenda” akasema PatriciaLaiti mama angeweza kukubali ningekuchukua tukaishi wote hapa kwetu lakini mama katu hawezi kukuachia” akasema Juliana huku akicheka halafu wakashuka na kwa kupitia mlango wa nyuma wakaingia ndani na moja kwa moja wakaelekea chumbani kwa Juliana.Patricia akapatwa na mshangao baada ya kuingia katika chumba kile kikubwa na kizuri. “ Patricia hiki ni chumba changu cha kulala.Nimekuleta huku moja kwa moja ili mtu yeyote asikuone kabla ya sherehe kuanza.” Akasema Juliana huku akitabasamu “ Dada Juliana una chumba kizuri mno.Sijawahi kuingia katika chumba kikubwa na kizuri kama hiki katika maisha yangu” “ Usijali Patricia.Hivi ni vitu vya kawaida tu na utakapovizoea utaviona ni vya kawaida .Kwa sasa usiwaze kuhusu maisha kama haya.Una kazi ngumu ya kusoma” akasema Juliana halafu akafungua kabati kubwa la nguo na kuanza kumchagulia Patricia nguo nzuri itakayompendeza kwa jioni ya siku ile.Alimchagulia suti nzuri nyeupe na kumpa aijaribu Patricia hakuna nguo utakayoiweka mwili mwako isikupendeze.Kama isingekuwa bado ni mwanafunzi ningekushauri uingie katika ulimwengu wa mitindo.Una umbo la kiuanamitindo na nina hakika ungeweza kufika mbali sana lakini usiwaze mambo kama haya kwa sasa.Elekeza akili yako katika masomo” akasema Juliana halafu akamuacha Patricia mle chumbani akaenda kuungana na rafikize katika kuandaa sherehe ile ndogo ya kumpongeza Patricia.Bado maandalizi yalikuwa yanaendelea.Wengine walikuwa jikoni wakiendelea kupika na http://deusdeditmahunda.blogspot.com/wengine walikuwa bustanini wakipamba sehemu itakapofanyikia sherehe “ Wakati pilika pilika zikiendelea huko nje, Patricia yeye alikuwa chumbani kwa Juliana akiendelea kutazama filamu.Wakati akiendelea kuifurahia filamu ile nzuri mara mlango ukafunguliwa taratibu.Patricia alidhani ni Juliana ndiye aliyeufungua mlango ule lakini ghafla akapatwa na mshangao alipoelekeza macho yake mlangoni.Kijana mmoja mweupe mwenye sura nzuri na aliyefanana sana na Juliana alikuwa amesimama akitabasamu.Walitazamana kwa sekunde kadhaa Patricia akaingiwa na woga.Kijana yule akaanza kupiga hatua taratibu kumuendea Patricia. “ helo Patricia” akasema Yule kijana huku akinyoosha mkono wake na kumsalimu Patricia ambaye alipatwa na uoga mkubwa.Alimtazama kijana Yule mwenye sura nzuri aliyekuwa akitabasamu naye akajilazimisha kutabasamu na kunyoosha mkono akasalimiana na Yule kijana “ I’m Godson” akasema kijana Yule halafu akakaa katika sofa lililoelekeana na lile alilokaa Patricia “ Tafadhali usiogope Patricia Juliana hawezi kuja sasa hivi.Nimemsikia akiwaambia wenzake kwamba uko huku chumbani kwake amekuficha na kwa kuwa nilikuwa na hamu ya kukuona nikaona ninyate ili nije nikusalimie.Nimefurahi sana kukuona na kukufahamu” akasema Godson “ dada Juliana aliniambia ana mdogo wake anaitwa Godson ndiye wewe? Akauliza Patricia. “Ndiye mimi” akajibu Godson. Nimefurahi kukuona Godson.Umefanana sana na Juliana.Nilipokuona tu nilijua lazima utakuwa ndugu yake” akasema Patricia na kumfanya Godson atabasamu.Kimya kifupi kikapita .Patricia akaendelea kumtupia jicho la wizi Godson akimchunguza.Alikuwa ni kijana mwenye sura nzuri sana na ya kuvutia sana.Alikuwa na mwili uliojengeka vyema.Fulana ile aliyovaa iliyokatwa mikono ilionyesha michoro aliyojichora katika mabega yake.Kwa ujumla alikuwa ni kijana mwenye kuvutia mno ambaye kila binti angetamani kuwa naye.Kwa mara ya kwanza katika maisha yake Patricia akajikuta akisisimka mwili “ Patricia ! ..akaita Godson na kumstua Patricia “ Juliana ameniambia kwamba umeshika namba moja katikamatokeo ya mtihani wa kidato cha nne” “ Ndiyo Godson” akajibu Patricia “ Hongera sana Patricia.Unastahili pongezi” “ Ahsante sana Godson.Namshukuru sana Mungu kwa hilo” “ By the way,umekwisha pangiwa ni shule gani unakwenda kuendelea na kidato cha tano? “ Ndiyo.Nimechaguliwa kuendelea na kidato cha tano na sita katika shule ya J.Y.Makamba school of science iliyoko Bumbuli Tanga.Ni shule mpya kabisa na nzuri.” “Safi sana kama umechagua mchepuo wa sayansi.Katika dunia ya sasa sayansi ndiyo inayoongoza.Hata mimi napenda sana masomo ya sayansi .Unafikiria kuwa nani huko mbeleni? Napenda niwe daktari” akajibu Patricia “ That’s great.Mimi pia nilisoma shule ya sayansi lakini nimejikita zaidi katika teknolojia ya kompyuta.” “ Ouh safi sana.Hata mimi nina hamu sana ya kujua kompyuta “ “ Katika shule uliyosoma hakukuwa na somo la kompyuta? “ Somo la kompyuta lilikuwepo lakini hakukuwa na kompyuta hata moja shuleni kwa hiyo ilikuwa vigumu kuelewa.Nafahamu kuna vitu vinaitwa keyboard,monitor lakini sijawahi kuvitumia “ Uko tayari nikufundishe kompyuta walau kwa siku hizi chache kabla ya kwenda shuleni? Nina hakika itakusaidia sana katika masomo yako.” “ Niko tayari Elvis.Natamani sana kujua kompyuta” Basi usihofu kuhusu hilo.Nitakufundisha katika kipindi hiki kifupi kabla ya kuelekea shuleni.” Akasema Godson na mara mlango ukafunguliwa akaingia Juliana.Alishikwa na mshangapo mkubwa baada ya kumkuta Godson mle chumbani “ Godson !!!!!..akasema Juliana “Nini kimekuleta chumbani kwangu?Please get out of here now” akafoka Juliana. Huku akitabasamu Godson akainuka na kumsogelea dada yake. “ Calm down big sister.Nilikuja kumsalimu Patricia.Nimeshindwa kuvumilia hadi jioni” akasema Godson. “ Ok go out now” akasema Juliana na Godson akageuka na kumtazama Patricia “ Bye Patricia.See you later” akasema Godson na kutoka mle chumbani. sorry Patricia.Huyu mdogo wangu ni mtundu sana.Hajakwambia neno lolote la kukukwaza? “ Hapana dada Juliana.Hajanitamkia neno lolote baya.Alitaka kunisalimu tu na tulikuwa tukiongea mambo ya kawaida ya masomo.Godson ni mcheshi sana” akasema Patricia “ Sikutaka mtu yeyote akuone kabla ya muda haujawadia.I wanted to surprise them.Lakini huyu Godson kajipenyeza mpaka amekuja kukuona.” Akasema Juliana na kumfanya Patricia acheke kidogo “ Dada Juliana ,Godson ameniambia kwamba yuko tayari kunifundisha kompyuta” akasema Patricia na kumstua Juliana “ Godson anataka kukufundisha kompyuta? “ Ndiyo dada JulianaAmesema atakufundishia wapi na lini? “ Bado hajasema ni lini na wapi.Mbona umestuka hivyo dada Juliana? Hana uwezo wa kunifundisha? Akauliza Patricia Juliana akavuta pumzi ndefu na kusema “ Godson amesoma kompyuta na anaifahamu vyema .Ni hivi majuzi tu amerejea toka nchini Marekani alikokuwa akisomea sayansi ya kompyuta.” Akasema Juliana na kumtazama Patricia . “ Are you sure you want to learn computer? Akauliza Juliana.Huku akitabasamu Patricia akajibu “ Ndiyo dada Juliana” “ Ok hakuna shida .Nitaongea naye ili tuone namna tutakavyoweza kufanya kuhusu somo hilo lakini kabla ya yote lazima mama akubali” Mama hatakuwa na shida ,mara zote huwa hana shida linapokuja suala la masomo.” “ Nitaongea naye jioni ya leo nitakapokurudisha” akasema Juliana Ilikuwa ni siku nzuri sana na ya kupendeza kwa Patricia na kwa wote waliohudhuria sherehe ile ndogo ya kumpongeza .Chakula kitamu kiliandaliwa na vinywaji vya kila aina vilikuwepo Ilipotimu saa mbili za usiku Juliana akamuomba Patricia ajiandae ili aweze kumrejesha kwao.Patricia akaagana na wote waliohudhuria sherehe ile ,akawashukuru kwa kufika kwao na kwa zawadi walizomzawadia halafu akaingia garini yeye Patricia na Godson ambaye aliomba akapafahamu nyumbani kwa akina Patricia Waliwasili nyubani kwa akina Patricia lakini mama yake bado alikuwa hajarejea.Juliana na Godson hawakukaa sana wakaondoka huku Juliana akiahidi kuongea na mama yake Patricia simuni kuhusu suala la mafunzo ya kompyuta “ Ilikuwa ni siku nzuri sana kwangu kiasi kwamba ninaiona kama imekuwa fupi mno.Sijui nitamlipa nini dada Juliana kwa wema wake huu mkubwa.Ametokea kunipenda sana na kunijali kama ndugu yake wa damu.Ana roho nzuri sana ya upendo na ndiyo aana anafanikiwa.” Akawaza Patricia na mara picha ya chumba kikubwa cha Juliana ikamjia kichwani akatabasamu “ Nimekipenda sana chumba cha Juliana.Kina kila kitu ambacho mwanamke anakihitaji.Natamani siku moja na mimi niishi maisha kama yale ya Juliana lakini yote haya yatawezekana tu kama nitaongeza juhudi katika masomo.Familia yangu ni masikini na haina uwezo wa kunifanya niishi maisha kama yale ya Juliana.Kitu pekee kitakachonifanya niishi maisha kama yale ni elimu..” akawaza Patricia huku akiendelea kufungua zawadi alizopewa picha ya Godson ikamjia kichwani “ What a handsome guy.Kusema kweli sijawahi kuona kijana wenye sura nzuri kama Godson.Uzuri wake hata mimi umenigusa.Ana sura nzuri,mwili laini na na hata tabia yake inaonekana ni nzuri japokuwa Juliana alisema kwamba ni mtndu.Alikuwa akiongea nami kwa lugha laini.he’s so sweet” akawaza Patricia huku akitabasamu na kuendelea kuzifungua zawadi zake







Elvis Tarimo alikuwa amejilaza kitandani chumbani kwake baada ya chakula cha usiku.Mkononi mwake alikuwa ameshika kipande cha gazeti lenye picha ambayo alikuwa akiitazama huku akitabasamu.Picha ile ilipigwa siku ya sherehe ya kuwapongeza iliyofanyika Dodoma.Katika picha ile Elvis alionekana akiwa pembeni ya Patricia . “ Naona siku haziendi ili shule zifunguliwe nimuone tena Patricia.Toka nlipokutana naye Dodoma sura yake imekuwa ikikitawala kichwa changu.Napatwa na hisia na msisimko wa aina yake kila nikimkumbuka.” “ Akawaza Elvis halafu akaitazama tena picha ile katika gazeti “Patricia ni msichana mwenye sifa zote.Amebarikiwa kuwa na uzuri wa kipekee kabisa.Najiona ni mtu mwenye bahati sana kusimama pembeni ya msichana kama huyu.” Elvis akaliweka pembeni gazeti lile akainuka na kuegemea kabati la nguo “ Siku zote mama amekuwa akinionya sana kuhusu kujihusisha na masuala ya mapenzi wakati ninasoma lakini toka nilipokutana na Patricia najisihi siwezi tena kuzizuia hisia zangu za mapenzi.Nahisi kupenda Patricia.Nimekutana na wasichana wengi wazuri na wanaotoka katika familia bora lakini sijaona hata mmoja anayeweza kumfikia Patricia kwa sifa.Siwezi kuendelea kujizuia tena kwa Patricia.Tayari amekwisha niingia moyoni na siwezi kumtoa tena” akawaza David “Nimempenda sana Patricia na kwa hili siwezi kuendelea kubishana na moyo wangu.This is my first time to fall in love.I’m deeply in love” akasema Elvis kwa sauti ndogo “ Sina hakika kama patricia anatambua uzuri alio nao.Laiti angejua kwamba ana uzuri wa asili usioelezeka angekuwa ni msichana mwenye majivuno sana lakini yeye hayuko hivyo.Ni msichana mcheshi,hana maringo na mwenye adabu.Mama yake anastahili sifa kubwa kwa namna alivyomlea na kumfanya awe na tabia hii njema.Kwa wasichana wa umri wake wenye uzuri na akili kama yake,mara nyingi wanakuwa katika hatari kubwa ya kuanguka vishawishini lakini Patricia yuko tofauti.Anaonekana ni msichana ambaye anajitambua mwenye msimamo na hadanganyiki kirahisi.Ninafahamu nitakumbana na kigingi kikubwa lakini sikati tama.Nitambana na kuhakikisha Patricia anakuwa mpenzi wangu.Hata kama itanigharimu sehemu kubwa ya maisha yangu niko tayari kusubiri hadi pale Patricia atakapokubali kuwa wangu.I’ll never give up.I’ll die trying” akawaza Elvis na kushika tena kile kipande cha gazeti akaitazama picha ile kubwa iliyokuwa mbele na kutabasamu “ Kokote uliko Patricia ninakupeda zaidi ya ninavyoweza kukueleza.I’m dying to see you” akasema Elvis ******************* Juliana na mdogo wake Godson walikuwa garini wakirejea nyubani baada ya kumrejesha Patricia kwao.Safari yao ilikuwa ya kimya kimya.Godson aliyekuwa amekaa pembeni ya Juliana akamtazama dada yake halafu akakohoa kidogo na kusema “ Big sister,I’m sorry.Najua umechukia kwa kitendo cha kuingia chumbani kwako bila ruhusa .I’m so sorry for that” akasema Godson “Kwa nini ulifanya vile Godson? Kwa nini uliingia chumbani kwangu bila ruhusa yangu? Akauliza Juliana “ Sister najua umechukia.Tafadhali naomba unisamehe.It wont happen again.I did that because …..because…” Godson akasita “ Because of what? Akauliza Juliana “ Because I wanted to see Patricia” akasema Godson na kumfanya Juliana acheke kidogo “ wewe ni mtundu sana.Kwa nini ulitaka kumuona Patricia wakati muda wa haujawadia?Ulijuaje kama yuko chumbani kwangu wakati nimemuingiza kwa kificho? “ Nilikuwa bustanini wakati unashuka garini.Nilistuka sana nilipomuona Patricia japo nilikuwa mbali.Niliamua kumfuata kule chumbani ili nikahakikishe kama nilichokiona ni cha kweli au macho yangu yalinidanganya.” Juliana akacheka kidogo na kusema “ Kwani Patricia yukoje? “ Ouh Big sister,Patricia amebarikiwa uzuri usioelezeka.Nimekutanana wasichana wengi tofauti tofauti lakini sijawahi kukutana wa aina ya Patricia.That girl is so hot” akasema Godson.Juliana akatabasamu akapunguza mwendo wa gari na kusema “ Kwa hilo hata mimi nakubali.Patricia ni msichana mrembo sana.Ana uzuri wa asili.Anafaa sana kuwamwanamitindo.Nina imani iwapo angekuwa mwanamitindo angekuwa maarufu sana” “ Kwa nini usimshauri aingie katika fani hii ya mitindo na urembo? Akauliza Godson “Hapana Godson.Patricia ni msichana mwenye malengo mengi ya maisha yake.Anatakiwa kuelekeza akili na nguvu zake zote katika masomo.Ndoto yake kubwa ni kuiondoa familia yake katika umasikini mkubwa walionao na ndiyo maana anasoma kwa bidii kubwa.Halafu aliniambia kwamba unataka kumfundisha kompyuta? “ Ndiyo .Anapenda kujua kompyuta na nina imani itamsaidia sana katika masomo yake.” Akasema Godson na kuinama .Kuna kitu alikuwa anawaza “ Unawaza nini? Akauliza Juliana Big sister kuna kitu nataka nikwambie lakini tafadhali naomba usichukie” “ Kitu gani hicho Godson? “Ni kuhusu Patricia” “ Patricia ?!! akauliza Juliana “ Ndiyo Sister” “ Patricia kafanya nini tena? Godson akavuta pumzi ndefu na kusema “ I don’t know how to say it but the truth is….” Akasema Godson na kusita kidogo “ Godson una tatizo gani? Akuliza Juliana “ Juliana wewe ni dada yangu na siwezi kukuficha jambo lolote.Ukweli ni kwamba nimetokea kuvutiwa sana na Patricia na nd……” Kabla hajaendelea Juliana akamkatisha “ Stop it right there Godson.Tafadhali naomba futa kabisa mawazo yako kuhusiana na Patricia.I wont allow you this time” akasema Juliana “ Big sister najua unafahamu mambo yangu mengi lakini yote hayo yamekwisha pita.Nimeshakua sasa na nimeachana na yale mambo ya zamani.” “ Vyovyote utakavyosema Godson sikubaliani nawe hata kidogo.You are a player and a liar.Unawaumiza watoto wa watu kwa ulaghai wako.Unaitumia sura yako nzuri inayopendwa na wasichana kuwalaghai na kuwaumiza mioyo yao.Siwezi kuruhusu ufanye ulaghai wako kwa Patricia” akasema Juliana “ Sikiliza big Sister…” akasema Godson lakini Juliana hakutaka kumpa nafasi ya kusema chochote “ Godson this conversation is over.Tutaongea tukifika nyumbani” akasema Juliana akionekana kukasirika.Safari ikaendelea kimya kimya hadi walipofika nyumbani.Wakashuka garini na kungia ndani. “ Big sister hatukumaliza mjadala wetu ndani ya gari.Tafadhali naomba unipe na mimi nafasi unisikilize ninachotaka kukisema’ akasema Godson “ Godson forget about Patricia.Sitaki umguse.Ana ndoto nyingi sana maishani mwake na sitaki uyaharibu aisha yake.Stay far away from her” akafoka Juliana “Sister naelewa hofu yako lakini naomba nikiri kwamba ni kweli hapo awali nilikuwa na tabia chafu .Sikuwa na mapenzi na msichana yeyote yule japokuwa wengi wa wasichana niliokuwa nao walikuwa wakinipenda kwa dhati ya mioyo yao.Niliwadanganya kwamba ninawapenda ili niweze kuwapata tu na baadae niliwaachawakiteseka.Ule ulikuwa ni utoto lakini kwa sasa nimekwisha kuwa mkubwa.Soon I’ll get a job and start my new life so I need someone I can love with all my heart and that someone is Patrcia” “ Godson ishia hapo hapo.Tafuta msichana mwingine utakayemchezea lakini si Patricia.Siwezi kusahau ulivyowatesa Penina,Pendo,Salma,Agatha,Maria mu,Agnes na Salome.Hawa ndio wale niliowashuhudia wakimwaga machozi kwa namna ulivyowatenda.Wengine walidiriki kufuamaniana na kupigana humu humu ndani.Tabia kama zile wafanyie wasichana wengine lakini si Patricia.Kama huna lingine la kusema this conversation is over.I need to sleep” akasema Juliana na kuanza kuondoka “ Please Juliana don’t go.Naomba unisikilize na unielewe.Nahitaji msaada wako.I’m changed now.Toka nimerudi Marekani hakuna msichana yeyote ambaye umemuona nimemleta humu ndani.Hii ni dalili tosha ya kuonyesha kwamba nimebadilika.I’m not the same Godson of three years ago.For the first time in my life I feel love.Nimetokea kuvutiwa sana na Patricia .Please sister don’t let me down .Nisaidie nimpate Patricia.” Akasema Godson “ Godson No ! Sitaki upuuzi wowote kwa Patricia.Ni binti mwenye kujiheshimu ,mwenye ndoto na malengo makubwa katika maisha yake.Stay far away from her” akasema Juliana “ Ok Big sister .Najua hutaki kuniona nikiwa na Patricia lakini naomba ujue kwamba Patricia ndiye mwanamke ninayempenda na nitafanya kila niwezalo nimpate.I think you understand when I say I’ll do anything” akasema Godson na kumstua Juliana “ Godson please sina nia ya kutaka usiwe na Patricia lakini binti Yule bado anasoma.Kama kweli unampenda Patricia muache amalize shule kwanza.Ukimuingiza katika masuala ya mapenzi kwa sasa hivi utakuwaunamchanganya na kumfanya apoteze mwelekeo” akasema Juliana “ Juliana sina lengo la kumuharibia Patricia maisha yake.I love her and I want her to be my girlfriend.I love her not because of sex but just because I want to be with her “ akasema Godson.Juliana akamuangalia kwa makini na kusema “ Kama ndiyo hivyo go and tell her that you love her” akasema Juliana Its not that simple big sister” akasema Godson “ So what do you want me to do? “ I need details of her,like what she likes…etc” Juliana akainama akafikiri na kusema “ Next Saturday is her birthday.Suprise her” akasema Juliana na kuelekea chumbani kwake “ Godson akidhamiria kitu lazima atakipata tu.Kama amedhamiria kumpata Patricia basi ni lazima atafanya kila awezalo hadi ahakikishe amempata.Siwezi kumzuia kwani inaonekana amempenda Patricia sana.Pamoja na hayo lazima niwe makini sana ili asije akamuharibia mtoto wa watu muelekeo wake.Namfahamu vizuri Godson he’s a player” ******************** Siku ya Jumatatu ilianza kwa Patricia kufuatwa nyumbani na Godson kisha wakaelekea nyumbani kwa akina Juliana kwa ajili ya kuanza rasmi mafunzo ya kompyuta.Godson alijtahidi kutumia kila aina ya utaalam ili kumfanya Patricia aifahamu kompyuta ndani ya kipindi kifupi.Patricia alikuwa mwepesi na alielewa kwa haraka sana Wakati somo likiendelea Godson alikuwa akijitahidi kupenyeza utani wa hapa na pale lengo likiwa ni kutaka kumzoea Patricia. Patricia alikuwa ni msichana mcheshi sana na alijibu vizuri na kwa ufasaha kila alichoulizwa na Godson.Kuna nyakati ilibidi somo lisimame na kuyapisha maongezi yachukue nafasi.Ndani ya kipndi kifupi wote wawili walijikuta wakizoeana sana.Godson alimuuliza Patricia mambo mengi kuhusiana na maisha yake naye alimjibu bila kumficha kitu chochote. Patricia aliendelea kujifunza kompyuta kwa bidii kubwa. Ilikuwa ni siku ya alhamisi baada ya kumrejesha Patricia nyumbani,Godson alikuwa na maongezi na dada yake Juliana “ Mnaendeleaje na somo la kompyuta? Patricia anaelewa? Akaanzisha maongezi Juliana “ Juliana naomba nikiri kwamba katika muda huu mchache niliokaa karibu na Patricia nimegundua vitu vingi.Patricia ni msichana wa ajabu kwani ana akili ya kiwango cha juu mno.Huwezi amni ndani ya kipndi hiki kifupi Patricia ameweza kutumia kompyuta kama mtu ambaye amejifunza kwa muda mrefu.Hata mimi mwenyewe ninapomfundisha huwa makini sana kwani mara nyingi huwa ananikosoa ninapokosea.Pamoja na hayo yote lakini kuna jambo nataka kukwambia” “ Jambo gani Godson? “ I want to make a surprise party for her on her birthday.I need your help” akasema Godson “ Unataka nikusaidie nini Godson? Akauliza Juliana. “ Nataka unisaidie namna ya kuandaa pati hiyo ndogo.Sina uzoefu wowote wa kuandaa vitu kama hivi so I real need your help” Juliana akainama akafikiri na kusema “Ok ! I’ll help you but in one condition” akasema Juliana “ Naomba unihakikishie kwamba endapo itatokea Patricia akaridhia ombi lako la kutaka muwe wapenzi ,hautamshawishi mfanye vitendo vya ngono hadi hapo atakapokuwa amemaliza masomo yake.Can you promise me that? Akauliza Juliana Big sister I give you my word.” “Ok I’ll help you but don’t break your promise” akasisitiza Juliana







Ni Patricia pekee ambaye hakuwa na ufahamu wa kilichokuwa kinaendelea kuhusiana na sherehe ya siri ya siku yake ya kuzaliwa iliyokuwa ikiandaliwa na Godson akishirikiana na dda yake.Mama yake alikwisha fahamishwa na Juliana kuhusu kinachoendelea.Toka amezaliwa Patricia hakuwahi kufanya sherehe ya kukumbuka siku yake ya kuzaliwa.Sherehe hii ingekuwa ni ya kwanza katika maisha yake. Siku ya Jumamosi ilianza vizuri na Patricia aliendelea na kazi ya kufua nguo.Hakuwa na habari yoyote kuhusiana na siku yake ya kuzaliwa na wala haikuwa siku muhimu kwake na ndiyo maana hakuwa hata na kumbu kumbu yoyote kwamba siku hiyo ndiyo siku aliyoingia duniani. Ilipotimu saa tisa za alasiri bi Doroth akamwambia Patricia asitishe shughuli zote alizokuwa akifanya na ajiandae kwani Juliana angekuja kuwachukua kuna mahala wanakwenda jioni ya siku hiyo.Bila kuuliza chochote Patricia akaoga na kuvaa vizuri.Wakati akiendelea kujiandaa mama yake akaingia mle chumbani na kujikuta akitabasamu “Mbona unatabasamu mama? Nimefurahi kwa namna ulivyopendeza leo.Mwanangu hakuna nguo inayokukaa vibaya.Mwili wako unakubali kila aina ya nguo.” Akasema mamayake Patricia halafu naye akaanza kujiandaa.Patricia alijaribu kumdadisi mama yake ni wapi walikuwa wakielekea lakini hakupewa jibu la uhakika Saa kumi na mbili za jioni Juliana akafika na kuwachukua wakaelekea moja kwa moja nyumbani kwao. “ Patricia utabaki hapa nyumbani na Godson .Mimi na mama tunakwenda sehemu Fulani muhimu.Godson atakuchukua katika gari na mtatoka kwenda kupata chakula cha usiku sehemu yoyote utakayopenda.” Akasema Juliana halafu yeye na bi Doroth wakaendelea na safari yao “ Patricia hatuna sababu ya kuendelea kukaa hapa .Twende tuingie garini tukatafute mahala pazuri tukae tupate chakula cha usiku.”Akasema Godson na kuingia ndani akachukua funguo za gari halafu nao wakaondoka. Tunalekea wapi Godson? Akauliza Patricia. “ Tunaenda matembezini.Kuna sehemu ambayo umekuwa ukiiota na ungependa kuingia? Kama ipo basi leo niambie nitakupeleka.” Akasema Godson na kumfanya Patricia atabasamu “ Godson muda mwingi wa maisha yangu ninautumia kwa kusoma kwa hiyo sifahamu chochote kuhusiana na starehe wala sehemu za burudani.Nina ndoto nyingi sana za maisha yangu “ akasema Patricia “ Patricia wewe ni msichana wa aina yake kabisa.Wasichana wengi wa umri wako wenye uzuri kama wako wamejikuta wakitumbukia katika anasa na starehe na kusahau malengo yao.Wewe uko tofauti kabisa.Hongera sana kwa msimamo wako usioyumba” akasema Godson Nakubaliana nawe Godson,wengi wa wasichana wanaingia katika tamaa na kushawishiwa kuingia katika tabia zisizofaa na hatimaye hujikuta wakipoteza kabisa mwelekeo.Sikatai hata mimi nakutana na vishawishi vingi sana lakini najitahidi kuvishinda vyote na kuelekeza akili yangu katika ndoto zangu.Najikubali kwamba nimetokea katika familia masikini na ninayakubali maisha yangu kwa hiyo siko tayari kurubuniwa na mtu eti kwa kigezo cha umasikini wangu.Nnaamini endapo nitajitahidi kusoma kwa bidii siku moja nitaachana naumasikini .Nitakuwa na maisha mazuri” akasema Patricia “ Patricia mwanaume atakayekuoa atakuwa na bahati sana kuliko wanaume wote wa dunia hii” akasema Godson na kumfanya Patricia acheke kwa nguvu “ Umenifurahisha sana Godson.Suala la kuolewa ni suala la mwisho kabisa na hata katika akili yangu halipo kwa sasa” “ Vipi kuhusu boyfriend? Akauliza Godson.Patricia akatabasmau na kusema “ Kama unamaanisha mpenzi,jibu ni sina lakini kama unamaanisha marafiki wa kawaida wa kiume ninao wengi sana na mmoja wao ni wewe” akasma Patricia na kumfanya Godson acheke kidogo. “ Patricia samahani kuna kitu nataka kukuuliza” “ Bila samahani Godson” akajibu Patricia “ Have you ever fall in love? “ What ? akauliza Patricia kana kwamba hakusikia alichoulizwa Nimekuuliza kwamba umeshawahi kumpenda mvulana yeyote ? Patricia akatabasamu na kusema “ Hapana sijawahi.Hicho ni kitu ambacho ninakikwepa sana lakini nina uhakika muda utakapofika nitajikuta siwezi tena kujizuia na nitampenda tu kijana mmoja kwani hata mimi ni binadamu mwenye hisia kama wengine.Ninaomba sana nitakapoanguka mapenzini iwe ni wakati nimekwishamaliza masomo.Sitaki kuchanganya mambo kwa sasa” akasema Patricia “Ahsante Patricia kwa kuwa muwazi na mkweli” akasema Godson “ What about you? Are you in love with someone? Akauliza Patricia Patricia kwa kuwa umekuwa muwazi kwangu naomba na mimi niwe muwazi kwako.Ni kweli nimewahi kuzama mapenzini na wasichana kadhaa lakini niligundua kwamba hawakuwa ni wa wa saizi yangu” “Nini kilitokea? Were they from poor family? “ Hapana si hivyo.Kila niliyekutana naye nilijikuta moyo wangu unakataa kuendelea naye.Sikufanikiwa kumpata Yule ambaye ataufanya moyo wangu ubadili mapigo yake .Wengi wao walinipenda kwa sababu nimetoka katika familia inayojiweza kiuchumi na si kwa mapenzi ya kweli toka moyoni.Kwa hivi sasa kuna msichana mmoja ananinyima usingizi kabisa.Akili yangu yote ipo kwake .Kila nimuonapo mapigo ya moyo wangu hubadilika.I love this woman with all my heart” akasema Godson.Patricia akanyamaza akameza mate na kusema “ Umeshamueleza huyo msichana ukweli wa moyo wako? “ Hapana bado sijamueleza na hafahamu chochote” “ Unasubiri nini kumueleza.Go and tell her the truth.Pengine naye anakupenda pia” “ Its not that’simple Patricia.But I’m waiting for the right time to tell her the truth and I hope she’ll understand me.Akasema Godson kisha akawasha indiketa ya kushoto kuashiria kwamba anataka kuingia katika hoteli moja tulivu ijulikanayo kama Ruby hotel “ Twende tuingie hapa Ruby hotel tukapate chakula cha usiku halafu turejee nyumbani tukawasubiri akina Juliana” akasma Godson akaegesha gari wakashuka na kuinghia hotelini wakachukua meza halafu Godson akainuka na kumwambia Patricia kwamba amsubiri hapo hapo kwani anakwenda maliwatoni.Patricia alikuwa na wasi wasi mwingi kwani ilikuw ani mara yake ya kwanza kuingia katika hoteli kuwa na tulivu kama ile.Godson alizunguka nyuma ya hoteli akatoa simu na kuwasiliana na Juliana akamfahamisha kwamba tayari wamekwisha fika.Juliana akampa maelekezo yote ya namna ya kufanya halafu Godson akarejea mezani alikomuacha Patricia “ Patricia nimepata meza nzuri zaidi huko ndani.Twende tuhame hapa” akasema Godson.Patricia akainuka na kumfuata Godson wakatembea kuelekea ndani zaidi ya hoteli.Wengi wa watu waliokuwamo humu hotelini walitoka mataifa ya kigeni Walifika katika mlango mmoja uliokuwa na kibao Masama hall.Godson akakiminya kitasa cha mlango ukafunguka akaingia ndani.Kulikuwa na giza “ Godson mbona kuna giza ? Huku ndiko tuendako? Akauliza Patricia kwa wasi wasi akiwa amesimama nje ya mlango “ Usihofu Patricia hii ni njia tu ya kupita.Tafadhali usiogope.” Akasema Godson na kumshika Patricia mkono akamuingiza ndani “Godson unanipeleka wapi? Akauliza Patricia kwa uoga na ghafla taa zikawaka na ukumbi wote ukawa mweupe.Nusura Patricia aanguke kwa mstuko.Mwili wote ulikuwa unamtetemeka kwa alichokiona.Alitamani kuamini kwamba ilikuwa ni ndioto lakini haikuwa hivyo.Kilichokuwa mbele yake ni kitu cha kweli kabisa “ Happy birthday Patricia ..!!!!!!! Sauti za watu waliokuwemo mle ukumbini zikasikika.Patricia alishindwa kuongea midomo ilikuwa inamtetemeka .Macho yake yaliloa machozi.Akahisi miguu inamuisha nguvu akakaa chini.Wote waliokuwemo ukumbini wakaendelea kupiga makofi na kushangilia kwa nguvu Juliana akamfuata akamshika mkono akamuinua na kumkumbatia “ happy birthday Patricia” Patricia hakujibu kitu.Alishindwa kuongea akaaendelea kulia.Juliana akachukua kitambaa na kumfuta machozi “ Nyamaza kulia Patricia.Today is your very big day.Smile and don’t cry” akasema Juliana “Dada Juliana ..nashindwa cha kusema.Nimekosa neno la kusema”akasema Patricia na kuendelea kulia.Juliana akamshika mkono na kumtoa nje ya ukumbi “ Patricia nyamaza usilie.Leo ni siku yako kubwa sana .Futa machozi” akasema Juliana “ Dada Juliana kwa nini hukuniambia kama kuna sherehe umeiandaa? “ Hii ni surprise party Patricia.Ameiandaa Godson kwa ajili yako” Patricia akajikuta akiendelea kulia “ Usilie Patricia.Just relax.Endelea kutabasamu “ Nashindwa kujizuia kulia dada Juliana.Sijawahi hata mara moja kukumbuka siku yangu ya kuzaliwa.Hii ni mara ya kwanza katika maisha yangu.” “ Basi usiendele kulia Patricia.” Akasema Juliana na kuingia tena ukumbini akachukua pochi yake kubwa na kutoka akamfuataPatricia akatoa mkebe wa poda na kuanza kumremba “Don’t drop any tears again.You’ll ruin your make up” akasema Juliana.Uso wa Patricia ulikuwa unang’aa sasa.Juliana akamshika mkono akamuingiza tena ukumbini.Watu wote wakashangilia kwa nguvu.Mama yake Patricia akamsogelea wakakumbatiana kwa furaha “ Hongera Patricia” akasema Patricia hakujibu kitu zaidi ya kumkumbatia mama yake kwa nguvu.Watu mbali mbali waliohudhuria sherehe ile wakampongeza Patricia kwa kutimiza umri wa miaka kumi na sita.Ilikuwa ni sherehe ndogo lakini iliyofana sana. ****************** Inakaribia saa tisa za usiku lakini bado Patricia hakuwa hata na chembe ya usingizi.Kitendo kile cha kufanyiwa sherehe ya kukumbuka siku ya kuzaliwa kiliendelea kujirudia kichwani.Alikumbuka namna alivyostuka baada ya taa kuwashwa na watu wakashangilia.Akahisi msisimko wa aina yake. “Kwa nini Godson amenifanyia sherehe ile .Do I deserve such a surprise? Akajiuliza Patricia halafu akainuka na kukaa “ Sielewi kwa nini ameamua kunifanyia jambo kubwa kama hili.Godson ana roho nzuri kama ya dada yake Juliana ambaye toka amefahamiana na sisi amekuwa akitusaidia katika mambo mengi sana.Nina deni kubwa la kuwalipa kwa wema wao mkubwa kwetu” akawaza Patricia na sura ya Godson ikamjia kichwani akazidi kutabsamu Kuna kitu nimekiona cha tofauti sana.Toka nilipokutana na Godson na kuwa karibu naye ninahisi kuwa na furaha ya ajabu.He makes me happy.Ninapokuwa karibu yake nahisi kama vile nina uwezo na nguvu ya kufanya jambo lolote..” akawaza Patricia halafu akajilaza kitandani “I’ve never felt this way before.Sijawahi katika maisha yangu yote kuwa na furaha kama ninayoisikia sasa baada ya kukutana na Juliana na Godson.He’s so sweet” akaendelea kuwaza huku sura ya Godson ikiendelea kujirudia kichwani kwake “ Sura ya Godson haifutiki kichwani.Kila dakika ni yeye tu ninayemuwaza.Nahisi kama akili yangu haitaki kuwaza kitu kingine zaidi ya sura ya Godson.Ouh gosh Godson anaanza kuniingia taratibu moyoni mwangu.Ameanza kuziteka fikra zangu” akainuka na kuelekea msalani “Mungu wangu naomba unisaidie niweze kulishinda jaribu hili kubwa na gumu .Godson anazidi kuniingia katika ubongo wangu.Najihisi kuanza kumpenda kwa nguvu sana na nina wasi wasi ninaweza nikajikuta nimeanguka mapenzini.” Patricia akaomba kimya kimya “ Siwezi kubishana na moyo wangu kwamba tayari nimeanza kumpenda Godson.Sijawahi kuwa na hisia kama hizi hapo kabla kwa mvulana yeyote Yule.Ouh No ! I have to control my feelings now.Siwezi kuendelea kumuwaza Godson kiasi hiki” Ulikuwa ni usiku mrefu sana kwa Patricia.Mawazo mengi yaliendelea kumuandama na kumfanya akose kabisa usingizi ******************* Siku zilienda kwa kasi kubwa na hatimaye muda wa Patricia kuondoka kuelekea shuleni ukawadia.Siku iliyotangulia siku ya kuondoka kwake alifika nyumbani kwa akina Juliana kwa ajili ya kuwaaga.Saa nne asubuhi ilimkuta Patricia ndani ya jumba hili kubwa ambalo kwa wiki kadhaa amekuwa akifika hapa karibu kila siku kwa ajili ya kujifunza kompyuta.Juliana hakuwepo nyumbani alikuwa ametoka asubuhi sana kuwahi miadi yake muhimu ya kibiashara.Pale nyumbani alikuwepo Godson peke yake.Sura ya Patricia ilionyesha mshangao baada ya kumkuta Godson akiwa katika hali isiyo ya kawaida. “ Godson unaumwa? Akauliza Hapana Patricia.Usiku wa kuamkia leo sikuweza kabisa kupata usingizi” “ Pole sana.Una tatizo lolote lililokufanya ukakosa usingizi? “ Ndiyo lakini si tatizo kubwa.Ni mawazo tu ndiyo yananisumbua” “ Mawazo gani hayo yanayokusumbua Godson? Unamuwaza Yule msichana uliyeniambia kuwa unampenda? Akauliza Patricia.Uso wa Godson ukachanua tabasamu “Ni kweli.Siachi kumuwaza yeye ndiye anayeninyima usingizi” Patricia akameza mate na kumtazama Godson kwa makini usoni kisha akasema “ Pole sana Godson.Inaonekana huyo msichana unampenda sana.Usiendelee kuteseka namna hiyo,mfuate na umweleze ukweli wa moyo wako anaweza akakuelewa.Usiendelee kujiweka kifungoni kuwa wazi kwake.Huwezi kujua pengine naye anakupenda na anasubiri umuanze wewe kumwambia” akasema Patricia.Godson akatabasamu “ Ahsante sana Patricia kwa ushauri wako mzuri.Nadhani ni wakati muafaka wa kumueleza ukweli wa moyo wangu.Sitaki kuendelea kuteseka tena.Naomba unisubiri dakika mbili nikabadili nguo kuna sehemu nataka unisindikize” akasema Godson “ Godson nilikuj……” Patrica akataka kusema neno lakini Godson akamkatisha “ Najua unachotaka kukisema Patricia.Umekuja kutuaga.Hata mimi nataka kukuaga lakini kabla ya hatujaagana kuna sehemu nataka unisindikize” akasema Godson na kukimbia hadi chumbani kwake akabadili nguo na kurejea sebuleni Twende tuondoke” akasema na kuongozana na Patricia hadi garini wakaondoka Walielekea moja kwa moja Sabana beach hotel moja ya hoteli kubwa jijini Dar iliyo pembezoni mwa bahari.Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Patricia kuingia katika hoteli kubwa kama hii iliyosheheni raia wa kigeni wengi wao walikuwa katika mavazi ya kuogelea.Patricia alishangaa na kujisikia aibu alipowaona wanawake kwa wanaume wakiwa katika mavazi ya nusu utupu wakicheza ndani ya maji na wengine wakijilaza katika mchanga .Hakuwahi kuyashuhudia mambo haya kwa macho. Godson akamuongoza hadi katika jiwe moja kubwa wakapanda juu yake.Paricia akaonekaa kuifurahia sana mandhari ile Huwa unakuja hapa mara kwa mara? Sehemu hii ni nzuri sana.bahari inaonekana vizuri mno” akauliza Patricia “ Mara nyingi huwa nakuja hapa kupumzika hasa nikiwa na mawazo mengi.Sehemu kama hii hunisaidia sana kutuliza akili yangu” akasema Godson “Unajisikiaje kuwaona watu wakiwa wamevaa nusu utupu namna ile? Nimetetemeka sana kwani sijawahi kushuhudia kwa macho mambo ya namna ile” Godson akatabasamu akacheka kidogo na kusema “ Huna haja ya kuhofu Patricia.Wengi wa watu uliowaona hapa ni kutoka katika tamaduni tofauti na zetu na ndiyo maana kwao kuvaa namna ile ni kitu cha kawaida.Kadiri unavyozidi kuendelea na safari ya maisha yako mambo kama haya utakutana nayo sana na utayaona ni ya kawaida. Kitu cha muhimu ni kwamba usijaribu kuiga.” Akasema Godson halafu kikapita kimya kifupi Wote walikuwa wameyaelekea macho yao baharini .Ni Patricia ndiye aliyeuvunja ukimya “ Godson leo nimekuja kuwaaga ,kesho ninaondoka kuelekea shuleni” “Ninafahamu Patricia na ndiyo maana nimekuleta hapa ili nipate nafasi ya kukaa nawe japo kwa muda huu mfupi uliobakia.I feel so sad Patricia.Nimekuzoea sana.Nimezoea kukuona kila siku.I’ll miss you a lot .Naomba nikiri kwamba toka tumefahamiana umekuwa ni rafiki yangu mkubwa.”akasema Godson.Patricia akainama kwa sekunde kadhaa halafu akainua kichwa na kusema “I’ll miss you too Godson.Ahsante sana kwa kunisaidia kuifahamu vyema kompyuta.Ahsante pia kwa surprise party.Ulinifanyia kitu kikubwa sana ambacho sikukitegemea na ambacho siwezi kukisahau katika maisha yangu.Ahsante sana Godson kwa yote.I’ll miss you a lot.You are a wonderfull guy” akasema Patricia “ Patricia kuna jambo ambalo ninataka kukueleza na ndiyo maana nimekuleta sehemu hii yenye utulivu mkubwa” akasema Godson “ Usihofu Godson.Nieleze tu unachotaka kunieleza” “ Kabla sijakueleza naomba kwanza nikuombe usikasirike wala kukwazika kwa nitakachokueleza” “ C’mon Godson,kwa nini nikasirike?Usihofu niambie unachotaka kuniambia “ akasemaPatricia.Godson akavuta pumzi ndefu na kusema Patricia unakumbuka tukiwa nyunbani ulinipa ushauri kwamba nimueleze ukweli wa moyo wangu Yule msichana ninayempenda? “ Nakumbuka Godson.Nadhani ndiyo njia pekee ya kujiweka huru.Msichana huyo anapaswa kufahamu kwamba moyo wako umemuangukia yeye” “ Ahsante sana kwa ushauri wako Patricia.Ninataka kufanya kama ulivyonishauri” “ wow ! that’s good.Go and tell her how much you love her” akasema Patricia huku akiwa ameinama chini.Moyoni alikuwa anaumizwa sana na maneno yale kwani tayari alikwisha anza kumpenda Godson. Godson akatabasamu na kusema “ Sina haja ya kwenda Patricia” akasema Godson na kumstua Patricia Umebadili mawazo? Hutaki tena kumweleza ukweli? “ Si hivyo Patricia,bali msichana ambaye amekuwa akinitesa na ambaye ninataka kumweleza ukweli wa moyo wangu yuko hapa pembeni yangu.” Akasema Godson na uso wa Patricia ukabadilika “usistuke Patricia.Wewe ndiye Yule msichana ambaye nimekwa nikikosa usingizi kwa ajili yake.” “ Godson ..!!!!!!..akasema Patricia kwa mshangao huku akiinuka “Patricia please don’t say anything now.Just listen to what I want to tell you.” Akasema Godson na kumshika Patricia mkono ambaye aliusukuma na kusimama huku akimuangalia Godson kwa macho makali “ I cant believe this” akasema Patricia kwa sauti ndogo “ Patricia please don’t say anything.Nilijuanitakukwaza na ndiyo maana nikatanguliza samahani.Naomba unielewe Patricia,sina nia wala lengo la kukukwaza.Ninachokwambia ni ukweli mtupu wa moyo wangu.Patricia wewe pekee ndiye msichana ambaye toka uvunguni mwa moyo wangu ninakiri kwamba ninakupenda kwa moyo wangu wote.” “ Godson please stop that !..Kumbe umenileta huku kwa ajili ya kunieleza mambo hayo? Akafoka Patricia “ Patricia tafadhali naomba usikasirike na wala usinielewe vibaya .Sina lengo baya nawe wala kucheza na hisia zako.Wewe ndiye chaguo la moyo wangu,wewe ndiye msichana wa maisha yangu” “ Godson please stop that ..!!! Mimi bado mwanafunzi na sitaki kujihusisha katika masuala hayo.Naomba uniache nisome .Nina ndoto nyingi kubwa za maisha yangu na zaidi ya yote I’m not of your type.I’m from poor family unlike you.You are so cute Godson and every woman would dream to be loved by y ou.You are rich,you have everything so you deserve someone better than me.Keep on searching Godson but I’m sorry I’m not the one” akasema Patricia halafu akainama.Machozi yalikuwa yanamtoka kwanza kwa Godson kumtamkia kwamba anampenda na pili kutokana na hali halisi inayomfanya asimkubali Godson. “ Nimetokea kumpenda Godson .Nimekuwa nikimuwaza yeye kila siku kumbe hata yeye amekuwa na hisia kama zangu.Ouh gosh ! I don’t know what to do..I’m confused.Ninatamani na mimi niwe na mpenzi kama huyu lakini mazingira ya sasa hayaniruhusu.Nasikitika sana kumkoa kijana kama huyu lakini sina namna nyingine y akufanya siwezi kukubali kuingia katika mahusiano kwa sasa” akawaza Patricia na mara Godson akamsogelea na kumshika bega. “ Patricia nyamaza usilie.Sikuwa na lengo la kukukwaza na kukutoa machozi.Lengo langu ni kukueleza ukweli tu wa moyo wangu .Nafahamu bado unasoma na ninafahamu una ndoto nyingi sana mbele yako na si lengo langu kutaka kuingilia maisha yako na kukuharibia maisha yako.Naomba unielewe hivyo Patricia and please don’t say anything for now.Nilichohitaji ni kuutua huu mzigo mzito uliokuwa umenielemea.” Akasema Godson.Patricia akainua uso wake na kusema “ Godson I’m sorry..Naomba ufahamu kwamba………” Patricia akataka kusema kitu lakini Godson akamzuaShhhhhhhh…!!!.Dont say anything.I understand you” akasema Godson halafu akachukua kitambaa kisafi na kumpa Patricia afutie machozi “” Godson naomba unipeleke nyumbani” akasema http://deusdeditmahunda.blogspot.com/Patricia kisha wakaanza kutembea kimya kimya mpaka mahala waliokoegesha gari wakaingia na kuondoka kurejea nyumbani. “ Toka siku yakwanza nilipokutana na Godson nilihisi kuna kitu kati yetu.Nilimpenda Godson toka dakika ile na toka wakati huo hajawahi kunitoka akilini.Kila siku ninajikuta nikizidi kumpenda na sikujua kama naye ananipenda pia.Pamoja na hayo siwezi kumkubalia ombi lake la kwamba tuwe wapenzi kwa sasa.Sitaki kuchanganya mambo mawili kwa wakati mmoja. I’m so confused.Ninampenda Godson na sitaki kumpoteza.Lakini ngoja kwanza niachane na mambo haya yatanichanganya akili yangu na kunipotezea mwelekeo.Kama Godson ananipenda kweli basi atakuwa tayari kunivumilia hadi hapo nitakapomaliza masomo yangu.Endapo akiendelea kunishawishi tuwe wapenzi nitampa mtihani huo kwamba anisubiri hadi hapo nitakapomaliza masomo yangu.” Patricia akastuska toka mawazoni baada ya gari kusimama nje ya jengo moja kubwa lenye maduka mengi “ Naomba unisubiri humu humu garini.” Akasema Godson akaufungua mlango na kushuka.Patricia akamtazama kwa makini Godson alivyokuwa akitembea kuingia katika jengo lile kubwa moyo ukamuuma sana “ Ouh jamani ninampenda sana Godson lakini mazingira yananifanya nishindwe kuwa naye…Sina hakika kama anaweza akaamua kunisubiri hadi hapo nitakapokuwa nimemaliza masomo yangu kwani vijanawengi wa siku hizi hawana uvumilivu huo.Wanachokitaka wao ni kufanya ngono tu kwa maana hiyo basi itanilazimu kuchagua kati ya Godson au masomo na maisha yangu na linapokuja suala la kuchagua basi lazima niachane na kila kitu nichague masomo.Nasikitika kumkosa Godson lakini dunia bado imejaa wavulana wazuri na nina hakika siku moja nitampata mtu ambaye nitampenda kwa moyo wangu wote zaidi ya ninavyompenda Godson.” Akawaza Patricia. Baada ya kama dakika kumi hivi Godson akarejea akiwa na maboksi matatu “Patricia hii ni simu nimekununulia.Ukiwa shuleni tutakuwa tukiwasiliana” akasemaGodson huku akitoa simu na kumkabidhi Patricia.Ilikuwa ni simu nzuri sana na ya kisasa “ Godson ahsante sana kwa zawadi hii lakini nasikitika kwamba sintaweza kuipokea.” Akasema Patricia na kumfanya Godson aonyeshe mshangao wa dhahiri. “ Godson ninajua kwamba umenipa simu hii kwa moyo mkunjufu kabisa ili iweze kunisaidia kwa mawasiliano.Kinachonifanya nisiipokee ni kutokana na taratibu nilizojiwekea mimi mwenyewe.Sihitaji kuwa na simu kwa sasa.Sina chanzo chochote cha mapato kitakachoniwezesha kupata pesa ya kununua muda wa maongezi zaidi ya yote sina watu wengi wa kuwasiliana nao.Mtu pekee ambaye ninataka niwe na mawasiliano naye ni mama yangu tu” Jibu lile la Patricia likamyong’onyeza Godson kwa shingo upande akaichukua simu ile ya gharama na kuirudisha katika boksi “ Kama umekataa simu naomba upokee hii kompyuta ndogo.Hii itakusaidia sana katika masomo yako.Tayari nimekwisha kununulia kifurushi kikubwa cha internet na nitakuwa nakununulia mara kwa mara na kukuongezea katika laini yako ili upate kujifunza mambo mengi zaidi kupitia mtandao.” Akasema Godson na kumkabidhi Patricia kompyuta ndogo mpya kabisa “ Ahsante sana Godson.Umenisaidia kitu kikubwa sana.Nina imani kompyuta hii itaniwezesha kujifunza mambo mengi sana kupitia mtandao” akasema Patrica.Godson akatabasamu na kusema Katika boksi hili linguine kuna vitu vidogo vidogo ambavyo utakuwa unavitumia shuleni” akasema Godson “ Ahsante sana Godsn.Naomba usijisike vibaya kwa kuikataa ile simu” “ Usijali Patricia nimekuelewa.Lakini pamoja na hayo kuna jambo nataka nikuombe” “ Jambo gani tena Godson? “Nitafurahi sana kama nitapata walau dakika tatu kila siku za kuongea nawe kupitia mtandao wa skype.Naomba niwe mtu wa mwisho kuongea nawe kabla hujalala” “ Patricia akatabasamu na kusema “ Usijali Godson.Nitajitahidi kufanya hivyo.Hata mimi nitafurahi pia kuwasiliana nawe.Wewe ni mmoja wa marafiki zangu wakubwa.” Akasema Patricia kisha Godson akawasha gari wakaondoka **********







J.Y.Makamba school of science ni shule ya ainayake hapa nchini ya mchepuo wa sayansi iliyoko Bumbuli Tanga.Shule hii ambayo huchukua wanafunzi waliofanya vizuri zaidi katika masomo ya sayansi imesheheni walimu wa kutosha wenye ujuzi,vifaa vya kujifunzia na kufundishia,maabara zenye vifaa vya kutosha na kila kitu kinahitajika katika kujifunzia au kufundishia sayansi. Geti la kuingilia shuleni hapa siku hi ya Jumatatu lilikuwa na pilika pilika nyingi.Ni siku ambayo wanafunzi wapya walikuwa wakiwasili shuleni.Saa tatu za asubuhi gari moja aina ya Toyota surf lenye rangi nyeusi likaruhusiwa kupita getini na kuelekea moja kwa moja katika jengo la utawala.Ndani ya gari hili alikuwemo mwanamitindo maarufu sana nchini na afrika mashariki,Juliana ambaye hakuwa peke yake bali alikuwa na Patricia na mama yake bi Doroth.Ni siku ya Patricia kuripoti shuleni tayari kwa kuanza masomo yake ya kidato cha tano hivyo Juliana na bi Doroth waliamua kumsindikiza hadi shuleni ili kuhakikisha amefika salama. Walishuka garini wote watatu na kuelekea katika ofisi ya mkuu wa shule msaidizi bi Eunice Kakwala.Walipokewa vizuri na Patricia akasajiliwa na kuelekezwa bweni ambalo atakuwa akikaa.Juliana akamsaidia Patricia kushusha mabegi yake katika gari na kuongozana naye kuelekea bwenini.Bi Doroth yeye alielekea katika ofisi ya mhsasibu kwa ajili ya kukamilisha taratibu za usjali ikiwa ni pamoja na kulipa karo na michango mingine. Bweni alilopangiwa Patricia lilikuwa ni bweni zuri na la kisasa lililokuwa na vyumba ishirini.Kila chumba kilikuwa na wanafunzi wane.Kila mwanafunzi alikuwa na kabati lake kwa ajili ya kuwekea nguo na vifaa vingine.Kulikuwa pia na kijichumba kidogo chenye meza na viti vinne kwa ajili yakujisomea Juliana akamsaidia Patricia kupanga vitu vyake kabatini halafu wakatoka mle chumbani na kuelekea katika jengo la utawala walikomuacha bi Doroth. “ Patricia safari imeanza.Nakusihi weka pembeni kila kitu na uzingate suala moja tu la kusoma.Mama yako ana matumaini makubwa sana nawe.Soma ili uje uikomboe familia yako toka katika hali duni ya sasa.Soma ujikomboe wewe mwenyewe.Tafadhali usimuangushe mama.Najua vishawishi ni vingi sana hasa kwa mrembo kama wewe lakini katu usikubali kuanguka wishawishini.Endapo utahitaji kitu chochote wasiliana nami.Godson aliniambia kwamba alikupa simu ukaikataa” “ Ndiyo dada Juliana.Godson alinipatia simu kwa bahati mbaya sikuipokea lakini si kwa ubaya bali ni kutokana tu na taratibu zangu nilizojiwekea ” “ Ok That’s great.I love that.Nitakuwa nikiwasiliana nawe kwa kutumia simu ya shule.Hata fedha nitakuwa nikikutumia kwa kupitia mwalimu mkuu msaidizi.” “ ahsante sana dada Juliana.Nakuahidi nitafanya vizuri sana katika masomo na akili yangu yote nitaielekeza katikakusoma tu” akasema Patricia Bi Doroth akiwa nje ya ofisi ya mhasibu wa shule mara akasikia mtu akimuita “ Mama Patricia !.... Bi Doroth akageuka nakutazama aliyekuwa akimuita.Kijana mmoja mtanashati alikuwa amesimama huku akitabasamu.Mara moja Bi Doroth akamkumbuka kijana Yule.Ni mmoja wa vijana waliofanya vizuri katika mtihani na walikutana Dodoma katika sherehe za kupongezwa . “ Shikamoo mama” akasema Yule kijana “ Marahaba mwanangu hujambo? “ Sijambo mama.Habari za siku nyingi? Bado unanikumbuka mama? Ninakukumbuka vizuri sana.Tulikutana Dodoma katika sherehe za kupongezwa lakini jina lako nimelisahau” “ Naitwa Elvis..” “ Ouh Elvis.Kumbe nawe umechaguliwa kujiunga na shule hii pamoja na Patricia? “ Ndiyo mama.Patricia yuko wapi? “ Patricia yupo.Tayari amekwisha sajiliwa na ameelekea bwenini kupeleka mizigo yake.” “ Sawa mama.Nitakuwa na Patricia hapa shuleni na tutakuwa tukisaidiana katika masomo na katika matatizo mbali mbali.Hajawahi kusoma shule ya bweni kwa hiyo kwa siku za mwanzoni mazingira yanaweza kumpa taabu kidogo lakini usijali nitamsaidia na atayazoea” “ Ninashukuru sana Elvis kwa msaada huo kwa mwanagu.Ninamfahamu Patricia.Linapokuja suala la kusoma huwa anajikuta akisahau kila kitu .Naomba wakati mwingine uwe ukimsihi apumzike kwa sababu anaweza akasoma kutwa nzima bila hata kupumzika” “ Nitafanya hivyo mama.Naomba pia unipe namba zako za simu ili niwe nikiwasiliana nawe kama kuna tatizo lolote na kuna nyakati hata Patricia mwenyewe angependa kuwasiliana nawe kwa sababu aliniambia kule Dodoma kwamba hana simu.Kwa kuwa mimi nina simu basi tutaitumia simu yangu katika mawasiliano” akasema Elvis Mama Patricia akampatia Elvis namba zake za simu na mara Patricia na Juliana wakatokea.Patricia akafurahi san a baada ya kugonganisha macho na Elvis. “ Elvis..!!...akasema Patricia huku akitabasamu Patricia ..!!akasema Elvis huku naye akitabasamu “ Habari za siku Patricia? “ habari za siku nzuri sana Elvis.Habari za Arusha? “ Arusha kwema .Karibu sana Bumbuli.Mimi nimefika hapa siku mbili zilizopita .Nimetaka niwahi ili nianze kuyazoea mazingira.” Akasema Elvis Juliana na Bi Doroth hawakuwa na sababu ya kuendelea kuwepo pale shuleni kwani tayari kila kitu kilikwisha kamilika.Ilikuwa ni siku ngumu sana kwa bi Doroth kuyaanza maisha mapya bila ya Patricia.Alimzoea sana mwanae.Alimkumbatia na kumuaga. “ Patricia mwanangu zingatia yale yote niliyokwambia” akasema mama Patricia “ Nitayazingatia mama” akajibu patricia huku machozi yakimtokaIlikuwa ni mara yake ya kwanza kutengana na mama yake Juliana na Bi Doroth wakaingia garini na kuondoka maeneo yale ya shule.Patricia bado alikuwa amesimama akilitazama geti kubwa jeusi likifungwa baada ya gari la Juliana kutoka. “ Usijali Patricia utazoea tu.Twende sehemu ya kupumzikia” akasema Elvis na kumuongoza Patricia hadi sehemu ambayo imetengwa maalum kwa ajili ya wanafunzi ,walimu , wafanyakazi na wageni kupumzika.Ilikuwa ni bustani nzuri na yakupendeza.Palikuwa na duka la kuuza vinywaji baridi ,pamoja na vitu mbali mbali.Elvis akaenda kununua vinywaji wakaendelea na maongezi “ Nimefurahi sana kukuona tena Patricia.Nilitamani sana kuwasiliana nawe kwa simu lakini sikuwa na namba yako ya na wewe hukukumbuka hata kunijulia hali.What happened Patricia? Kwa nini hukutaka hata kunitumia ujumbe wa maneno kunisalimu? Akauliza Elvis “ Naomba unisamehe Elvis.Hata mimi nilikukumbuka sana na nikataka kukusalimu lakini nilipoitafuta namba yako sikuiona tena.” Patricia akadanganya “ Usijali Patricia.Nafurahi nimekuona tena” “ Lakini naomba usichukie Elvis.Sikufanya makusudi” akasema Patricia huku akimtazama Elvis kwa macho yake mazuri. “ Siwezi kuchukia Patricia lakini ni kweli nilikwazika sana kwa kutokuwasiliana nawe .” akasema Elvis . Waliendelea na maongezi na baadae Elvis akamchukua Patricia na kuanza kumuonyesha mazingira ya shule.Ndani ya muda huu mfupi walikwishazoeana kama marafiki wa muda mrefu sana. Baada ya chakula cha usiku,Elvis na Patricia wakaagana na kila mmoja akaelekea bwenini kwake.Chumba alichopangiwa Patricia kulikuwa na vitanda vinne lakini wasichana wawili tu waliokuwemo mle chumbani .Msichana mwingine aliyekuwa chumbani na Patricia ni Shamim toka Zanzibar. “ Halow Shamim” Patricia akamsalimu Shamim baada ya kuingia mle chumbani na kumkuta Shamim amejilaza kitandani akiwa na kompyuta yake..Shamim akavua spika za masikioni alizokuwa amevaa akatabasamu na kusema “Hallow Patricia” “ Hukwenda kupata chakula? “ No Patricia I’m full.kwa siku ya leo sihitaji chakula .Nina juice yangu inanitosha sana” akasema Shamim na kuinuka akakaa kitandani “ Naona mwenzangu tayari umekwisha pata mwenyeji” akasema Shamim huku akitabasamu “Mwenyeji gani tena? Akauliza Patricia huku naye akitabasamu “ Kuna Yule handsome boy ,mmoja nimekuona uko naye toka mchana” Patricia akacheka na kusema “ Elvis?! “ Sijui anaitwa nani ila ninamfahamu kwa jina moja tu la handsome.He’s real handsome pengine kupita vijana wote hapa shuleni” akasema Shamim “ Elvis nilikutana naye Dodoma tukawa marafiki.Toka hapo hatujaonana tena mpaka tulipokuja kuonana leo hi” akasema Patricia He’s so cute.You have a cute boyfriend” akatania Shamim “ He’s not my boyfriend.Ni rafiki yangu wa kawaida” akasema Patricia “ Gosh ! Usiseme hivyo.Siku nyingine mbele za watu.They’re gonna take him away.Usiache msichana mwingine akamchukua Elvis.” Akasema Shamim “Shamim,hakuna kinachoendelea kati yangu na Elvis.Sisi ni marafiki wa kawaida tu” akasema Patricia “ Ouh Patricia my dear you real wanna make me cry..If you don’t want him give him to me” akasema Shamim “ You can take him.Mimi mambo hayo ya mapenzi sijihusishi nayo kwa sasa” akasema Patricia na kumshangaza Shamim “ Patricia unataka kuniambia kwamba huna mpenzi? Sina” akasema Patrica .Shamim akacheka kicheko kikubwa “What a liar.Msichan mzuri kama wewe haiwezekani ukakosa mpenzi.Unaishi vipi bila kuwa na mpenzi? “ Nakuambia kweli Shamim.Sina mpenzi” “ Hapana si kweli” “ Believe what you have to,but that’s the truth.Akili yangu yote nimeielekeza katika masomo.Sitaki kuchanganya mambo mawili kwa wakati mmoja.Mapenzi na shule kamwe haviendi sambamba.” Akasema Patricia.Shamim akacheka kicheko kikubwa na kusema “ Usinichekeshe Patricia.Nani alikwambia kwamba ukiwa na mpenzi unafeli masomo? Si kweli hata kidogo.Mimi nina mpenzi wangu anaishi Oman.Niko naye toka nikiwa kidato cha kwanza natazama nimefaulu vizuri masomo yangu na tuko wote hapa katika hii shule ya wanafunzi wenye vipaji vya pekee.Abdul amekuwa ni msaada mkubwa kwangu na kwa masomo yangu.Patricia usidanganywe na mtu kwamba kuwa na mpenzi kutakufanya ufeli masomo.Unachotakiwa kufanya ni kutenga muda vizuri kwa masomo na mambo mengine.Elvis ni kijana mzuri sana ukimuacha wenzako watamchukua” akasema Shamim.Patricia akavuta pumzi ndefu na kujitupa kitandani.Shamim akamtazama halafu akainamia kompyuta yake “ Haya maneno anayoyasema Shamim yanaweza kuwa na ukweli.Ninajitahidi sana kupambana na hisia kali za mapenzi ambazo zimekuwa zikinijia kila mara.Ninahisi kutaka kuwa na mpenzi kama wasichana wengine na kila mara linapokuja suala la kufikiria kuhusu mpenzi ,mtu wa kwanza anayekuja kichwani kwangu ni Godosn.Tayari amenitamkia kwamba ananipenda na anataka tuwe wapenzi.Pamoja na kumkataa lakini bado moyo wangu unaniambia kwamba yeye ndiye mwanaume wa maisha yangu.Ninampenda sana Godson.Anazidi kuniingia katika kila mshipa wa mwili wangu..Ouh Mungu wangu nitafanya nini? “ akawaza Patricia “ Ngoja kwanza niwasiliana naye katika mtandano pengine inaweza kunisaidia kunipunguzia mawazo mengi niliyo nayo juu yake.” Patricia akachukua computer yake ndogo akaiwasha na kuingia katika mtandao wa skype ili aweze kuwasiliana na Godson lakini kwa bahati mbaya Godson hakuwepo mtandaoni. Gosh ! Hayupo mtandaoni.” Akawaza Patricia.Akavuta pumzi ndefu halafu akaizima kompyuta yake na kujilala kitandani. “ Sioni kama kuna ubaya endapo nikiwa na mpenzi.Marafiki zangu wote wana wapenzi na maisha yao yanaendelea vizuri tu.Kitu cha msingi ni kujitahidi mapenzi yasinivurugie malengo yangu .” akawaza Patricia akiwa amejilaza kitandani. MIEZI MINNE BAADAE Miezi minne imekwisha katika toka Patricia aliporipoti shuleni J.Y.Makamba school of science.Masomo yaliendelea vizuri na kama kawaida yake aliendelea kuwa gumzo kwa wenzake kutokana na uwezo mkubwa aliokuwa nao darasani.Bado aliendelea kuwaongoza wenzakena kushika namba moja katika kila mtihani na majaribio.Patricia alikuwa ni msichana mwenye akili ya kiwango cha juu mno. Maisha ya shule yalikuwa mazuri na tayari alikwisha yazoea mazinginra .Kila mwanafunzi alimpenda sana kutokana na ucheshi na uchangamfu wake .Ilikuwa ni shule yenye wanafuzni mia moja.Wavulana hamsini na wasichana hamsini.Pamoja na kuwa na marafiki wengi,wavulana kwa wasichana ,lakini rafiki yake mkuu hapa shuleni alibaki kuwa Elvis.Walisoma pamoja na waliachana pale tu kila mmoja alipoelekea bwenini kwake.Mawasiliano baina yake na Godson yaliendelea kama kawaida.Waliwasiliana karibu kila siku usiku kabla ya kulala kupitia mtandao wa Skype.Tayari kulikuwa na ukaribu mkubwa sana baina yao. Kila jumamosi ya kwanza ya mwezi huwa ni siku ya wanafunzi kwenda matembezini nje ya shule pamoja na kujinunulia mahitaji mbali mbali.Ni saa mbili na nusu za usiku wakati wanafunzi wakiwa vyumbani mwao,Elvis na na Patricia walikuwa katika bustani ya shule wakibadilishana mawazo huku kila mmoja akiwa na kompyuta yake .Wakati wakiendelea na maongezi,mara Godson akaingia mtandaoni.Haraka haraka Patricia akamuona na kuvaa spika za masikioni akampigia simu. “ Hallow Patricia” akasema Godson “ Hallow Godson.Unaendeleaje? “ Nina endelea vizuri.Vipi wewe unaendelaje?Habari ya weekend? “ Weekend nzuri tu Godson” “ Nafurahi kusikia hivyo.” Akasema Godson “ dada Juliana hajambo? Juliana hajambo.Alisafiri kwenda Nairobi anategemea kurejea kesho.Vipi kuhusu masomo? “ Masomo yanaendelea vizuri .Unaendeleaje na kazi zako? “ Kazi zinakwenda vizuri.Changamoto ni nyingi lakini ninajitahiidi kukabiliana nazo.Hata hivyo kuna kampuni moja nimetafutiwa na baba nchini afrika kusini ambayo natakiwa kwenda kufanya usaili.Endapo nitakapa nafasi katika kampuni hiyo basi itanilazimu kuondoka na kwenda kuishi Afrika kusini” akasema Godson.Patricia akastuka na kuvuta pumzi ndefu halafu akasema “ Umechoka kufanya kazi Tanzania? “ Si hivyo Patrica.Ninapenda kufanya kazi Tanzania lakini endapo nitapata kazi katika kampuni hii ninayokwambia basi nitalipwa mshahara mzuri sana tofauti na ninaolipwa sasa.Kikapita kimya halafu Godson akamstua Patricia “ Patricia ! akaita Godson “ Sema Godson” “ Kuna jambo ambalo limekuwa linaniumiza sana kichwa changu” “ Jambo gani Godson? “Unakumbuka siku ile iliyotangulia siku ya kuondoka kwako kwenda shule,tukiwa ufukweni kuna jambo nilikueleza? “ Ndiyo nakumbuka “ “ Basi suala lile ndilo ambalo limeendelea kuniumiza sana kichwa changu” Patricia ninakonda kwa kukuwaza wewe.Umeniingia hadi ndani kabisa mwa kila mshipa wa mwilini mwangu .Wewe ndiye mwanamke wa pekee kabisa katika maisha yangu.Umeiteka akili yangu na kuifanya ikufikirie wewe tu.NakupendaPatricia,Nakupenda sana.Tafadhali naomba usinipuuze na unikubali ili tuwe wapenzi.Sintakutenda jambo lolote baya.Nitakuthamini na kukuheshimu katika siku zote za maisha yangu.Nikubali niwe wako Patricia ili moyo wangu uweze kutulia” akasema Godson na kumfanya Patricia ashushe pumzi.Uso wake ukabadilika.Hakujua atoe jibu gani.Kimya kikatanda “ Patricia ..!! akaita Godson “ Godson,tuliongea kuhusu suala hili na tukalimaliza.Nadhani unakumbuka nilichokuambia” “ Ni kweli Patricia.Ulinieleza msimamo wako na nikakuelewa lakini kadiri siku zinavyozidi kwenda najikuta nikishidwa kuvumilia.Nakupenda Patricia .Moyo wangu unakuhitaji wewe tu.Najua una malengo mengi ya maisha yako na lengo langu mimi sikukuharibia masomo au maisha yako.Nataka tuwe wapenzi na mambo mengine yatasubiri hadi hapo utakapomaliza masomo yako.Niko tayari kukukusubiri .Patricia naomba ufahamu kwamba ninakupenda ,nakuheshimu na ninakuthamini.Kamwe sintaweza kukufanyia jambo lolote lile la kipuuzi tofauti na matakwa yako” akasema Godson Patricia akainama akafikiri na kusema “ Godson najua kwamba unanipenda na lengo lako ni zuri.Toka tumefahamiana umekuwa ni mtu mwema sana kwangu .Wewe ni kijana wa aina yake na ambaye kila mwanamke angependa kukupata.Pamoja na hayo yote Godson,lakini bado nitaendelea kuwa kinyuma na ombi lako nikimaanisha kwamba hatuwezi kuwa wapenzi.Gods………” Kabla hajamaliza alichotaka kukisema Godson akasema “ Kwa nini unanifanyia hivyo Patricia? Am I not good enough for you? Kama nina tatizo lolote naomba unieleze.Tell me anything and I can do.Your word is my command” akasema Godson “ Godson mimi bado mwanafunzi.Sitaki kuchanganya mambo mawili kwa wakati mmoja.Siku zote mapenzi na masomo hayaendi pamoja.Tafadhali naomba uniache nimalize masomo halafu kama ni mambo mengine ndipo yafuate lakini sipotayari kwa sasa” akasema Patricia “ Patricia ninaelewa unachokimaanisha lakini naomba uelewe kwamba sina lengo baya nawe” “ Ninajua huna lengo baya nami,lakini naomba uelewe pia kwamba nimeamua hivi kwa faida yangu mwenyewe .Nakuomba Godson kama kweli unanipenda kama unavyosema,niache nimalize masomo yangu.Bado nina safari ndefu sana mbele yangu.Wewe umebahatika kuzaliwa katika familia yenye uwezo tofauti na mimi.Familia yangu imezungukwa na umasikini mkubwa na mkombozi wangu pekee ni elimu” akasema Patricia “ Patricia ninaelewa kwamba wewe bado mwanafunzi na unahitaji kuielekeza akili yako yote katikakusoma.Ni lengo langu pia kuhakikisha kwamba unatimiza malengo yako yote.Nataka kuwa ni sehenu ya mafanikio yako.Naomba uufungue moyo wako na uniruhusu niingie ndani .Niruhusu nikuonyeshe ni namna gani ninavyokupenda Patricia” Patricia akavuta pumzi ndefu na kusema Godson nakosa jibu la kukupa.Sielewi nikwambie kitu gani ili unielewe” “ Patricia kuna kitu kimoja tu ambacho ninataka uniambie” “ Kitu gani hicho? Godson akavuta pumzi ndefu na kusema “ Naomba uwe muwazi kwangu na uniambe kitu kimoja.Je katika moyo wako hakuna hisia zozote juu yangu? Naomba uwe muwazi kwangu kama mimi nilivyokuwa muwazi kwako” Swali lile likamchanganya Patricia akabaki anatazama kompyuta yake.Hakujua aseme nini “ Mbona hunijibu Patricia? Akauliza Godson “ Godson swali lako gumu sana na sielewi nikujibu nini” akasema Patricia “ Nataka kuusikia ukweli wa moyo wako.I’m your friend so be honest with me.Tell me the truth and I’ll understand.Patricia nipe ukweli wa moyo wako and I swear I’ll never bother you again” akasema Godson.Patricia alilengwa na machozi.Alikuwa katika wakati mgumu sana.Alimpenda Godson lakini aliogopa kujiingiza katika mahusiano “ Answer me Patricia” akasema Godson. “ Huu ni mtihani mgumu na sielewi ni kwa nini niendelee kuteseka kwa jambo hili .Mbona hapa shule karibu kila msichana ana mpenzi wake? Hakuna dhambi yoyote kuwa na mpenzi.Ninampenda Godson na sitaki kumkosa.Ngoja tu nimkubalie lakini nitajichunga ili nisije poteza mwelekeo” akawaza Patricia.Akakohoa kidogo na kusema Ninakupenda Godson.Ninakupenda sana.Sitaki kuku…….”Hakumalizia sentensi yake Godson akaruka kwa furaha “ Ouh Patricia,thank you,thank you so much.I real love you with all my heart” akasema Godson “ Ahsante kwa jibu lako Patricia.Ni hilo tu ndilo nilikuwa nahitaji kulisikia toka kwako.Ahsante kwa kunipenda.Nitakupenda daima.I’ll never make you cry” akasema Godson “ Godson ninakupenda na niko tayari kuingia kwa maraya kwanza katika mahusiano ya kimapenzi lakini kwa sharti kwamba utayaheshimu malego yangu ya maisha na kwamba hautafanya jambo lolote la kunivurugia masomo au maisha yangu” “Niko tayari kwa masharti hayo Patricia na ninakuahidi kwamba nitakupenda daima .Nitafanya kila utakachoniamuru nikifanye.” “ Ahsante Godson kwa ahadi yako.Natumai utaitimiza.Tutapata wasaa mzuri wa kuongea kuhusiana na mambo haya nitakaporejea Dar es salam wakati wa likizo,lakini kwa sasa naomba uniache nielekeze akili yangu katika masomo” “ Patricia narudia tena kusema ahsante sana kwa kunikubali niwe mpenzi wako.Umeyafanya maisha yangu yawe na furaha.Umenipa furaha ambayo sijawahi kuipata toka nimezaliwa” Godson akasema kwa furaha.Wakaagana na Patricia akaizima kompyuta yake.Kijasho kilikuwa kinamtoka.Alipogeuza shingo yake Elvis hakuwepo. “ Elvis kaondoka muda gani? Kwa nini hakunifanyia ishara kama anaondoka? Yawezekana alikerwa na maongezi yangu na Godson? Akawaza Patricia halafu akaegemea kiti akavuta pumzi ndefu “Ouh Godson,umenifanya niuvunje mwiko wangu.Ni kweli nakupenda sana na sijawahi kumpenda mvulana yeyote kama ninavyokupenda wewe.Kwa sababu yako ninaufungua ukurasa mpya wa mapenzi katika maisha yangu.Natumai hautakuwa sababu ya mimi kupoteza dira na mueleko wa maisha yangu.” Akawaza Patricia na kutabasamu baada ya picha ya Godson kumjia kichwani. “ He’s such a handsome guy.Nampenda sana .Sura yake inanijia kila dakika na kuufanya ubongo wangu usitulie.Sikujua kama ukitokea kumpenda mtu unakuwa namna hii” akawaza Patricia na kuinuka akaeleeka bwenin.





I’m so stupid..!!! akasema kwa hasira Elvis na kujipiga kofi kichwani “ Why could I be so stupid? I’m so coward.” Akasema kwa hasira huku machozi yakimtoka.Ilikuwa ni muda mfupi baada ya kuondoka bustanini alikokuwa amekaa na Patricia ambako ilimlazimu kuondoka baada ya kumsikia Patricia akiongea masuala ya kimapenzi na mvulana mwingine kupitia mtandao wa Skype “ Siku zote nimekuwa karibu na Patricia nikijaribu kujenga urafiki wa karibu ili siku moja nimueleze kwamba ninampenda lakini kumbe nilikuwa najidanganya.Yote niliyoyafanya ni kazi bure.Patricia ana mtu wake anayempenda Aaaaggghhhhhh….!!!!!!! Akapiga ukelele kwa hasira “ Kwa nini siku hizi zote asiniambie kama ana mtu wake anayempenda? Lakini siwezi kumlaumu kwani ni kosa langu.Ningemwambia mapema kwamba ninampenda nisingeumia namna hii.Pamoja na hayo,bado sijapoteza matumaini.Nitaendelea kupambana hadi dakika ya mwisho.Nitapambana kuhakikisha kwamba Patricia anakuwa wangu.Yeye ndiye mwanamke pekee ninayempenda katika maisha yangu.” Akawaza Elvis halafu akaenda katika sinki akafungua maji akanawa uso kisha akatoka na kueleka tena bustanini mahala alikokuwa amekaa na Patricia lakini Patricia hakuwepo.Akaketi kitini na kuinua kichwa akatazama juu angani. I swear in heaven and earth,Patricia will be mine.She will love me and no one else will make us apart.To win Patricia’s heart is my major goal for now.” Akasema Elvis kwa sauti ndogo.Akatoa simu yake akafungua mahala anakohifadhia picha akaitazama picha ya Patricia “ You’ll be mine Patricia.You’ll be mine.You’ll love only me”Akasema halafu akainuka na kuelekea bwenini ******************** Kitendo cha Elvis kutoonekana darasani kilimchanganya sana Patricia na kumfanya awe na mawazo mengi.Haikuwa kawaida ya Elvis kukosa darasani.Saa nne na nusu kengele ikagonga kuashiria kwamba ni wakati wa mapumziko ya asubuhi.Patricia akatoka kwa haraka na kumfuataMartin ambaye ndiye anaishi chumba kimoja na Elvis “ Martin samahani,kuna jambo naomba kukuuliza” akasema Patricia kisha wakasogea pembeni “ Jambo gani Patricia? “ Ni kuhusu Elvis.Mbona leo hajaingia darasani? Ana matatizo? “ Hajaingia darasani? Martin akauliza. “Ndiyo na si kawaida yake kukosa darasani.Ana matatizo yoyote? “ Sina hakika kama ana matatizo kwa sabau mimi niliwahi kuamka asubuhi nikamuamsha ili naye ajiandae lakini akaniambia kwamba nitangulie yeye atafuata baadae” “ Ok ahsante ngoja nikamuangalie” akasema Patricia huku akianza kutembea kwa kasi kuelekea katika bweni la akina Elvis Patricia huruhusiwi kuingia katika bweni la wavulana.Ukionekana kule unaweza kupewa adhabu kali” akasema Martin “ I don’t care .Nataka kujua ni kwa nini Elvis hajaingia darasani leo.He’s my friend and I need to know if he’s having a problem.” Akasema Patricia na kuchomoka hadi katika bweni la wavulana.Anafahamu namba ya chumba cha akina Elvis akanyoosha moja kwa moja na kukinyonga kitasa cha chumba namba sita akaingia ndani lakini Elvis hakuwemo “ Ouh gosh ! Elvis amekwenda wapi? Mbona humu hayumo? Akajiuliza Patricia halafu akatoka mbio mle chumbani “ Nimekumbuka kitu.Kuna sehmu moja ambayo huwa anapenda sana kwenda kupumzika.Ngoja nikamuangalie kule” akawaza Patricia huku akikimbia kuelekea katika msitu wa shule.Pembeni ya msitu ule kulikuwa na maporomoko madogo ya maji na hii ndiyo sehemu ambayo Elvis hupenda sana kwenda kupumzika. Kama Patricia alivyokuwa amehisi ni kweli Elvisa alikuwa amekaa juu ya jiwe. “ Elvis…!!!!” akaita Patricia na kumstua Elvis aliyekuwa amezama katika mawazo mengi. “ Patricia !! akasema Elvis kwa mstuko wa kumuona Patricia maeneo yale.Kwa haraka akainuka na kumfuata “ Patricia what are you doing here? Akauliza Elvis “ Elvis nimekutafuta kila mahala nikakukosa nikajua lazima utakuwa huku.” “ Patricia tafadhali usithubutu siku nyingine kupita humu msituni peke yako.Kuna hatari nyingi humu.Hakuna usalama ukiwa mwenyewe” “ Usijali Elvis,sintafanya hivyo tena.Nimelazimika kufanya hivyo kutokana na wasi wasi niliokuwa nao kwa kutokuona darasani leo.Si kawaida yako kukosa darasani.Una matatizo gani? Tell me Elvis I’m your friend and I do care about you.Una matatizo gani? Kwa nini hujaingia darasani leo? Unaumwa? Akauliza Patricia “ Hapana siumwi Patricia ila sikujisikia tu kuingia darasani leo na ndiyo maana nimekuja huku ili kutuliza kichwa changu.” Patricia akamshika Elvis mkono wakatazamana “ Elvis niambie una matatizo gani leo? Nini kinakusumbua? Tafadhali naomba unieleze” Elvis akavuta pumzi nefu akamtazama Patricia na kusema “ Ni kweli nina matatizo Patricia Kuna jambo linaniumiza sana kichwa changu lakini nasikitika kwamba sintaweza kukwambia.Thank you for your concern” akasema Elvis “ Elvis you do trust me right? Akauliza Patricia “ Ofcourse I do” akajibu Elvis “ Kama unaniamini naomba unieleze ni jambo gani linalokusumbua? Akasema Patricia.Elvis akamtazama kisha akasema “What about you Patricia ,do you trust me ? “ I do trust you Elvis.Kwa nini umeniuliza hivyo? “Nina wasi wasi na jibu lako Patricia.Sina hakika kama unaniamini na ndiyo maana umekuwa msiri sana” “ Siri?! Patricia. Akashangaa “ Ndiyo” “ Elvis mbona nimekuwa nikikueleza kila jambo linalonihusu? Hakuna jambo ambalo nimewahi kukuficha.Wewe ndiye mtu pekee unayefahamu kuhusu undani wa maisha yangu” akasema Patricia “ You didn’t tell me that you have a boyfriend” “ boy friend? Patricia akashangaa “ Ndiyo.Kwa nini kila siku tulipokuwa tunaongelea kuhusu mambo haya ya mahusiano ulisema kwamba huna mpenzi? Kwa nini ulinidanganya? Akauliza Elvis.Patricia akashikwa na kigugumizi akashindwa ajibu nini.Akakumbuka kwamba wakati akiongea na Godson jana usiku Elvis alikuwepo karibu.” “Mimi nilidhani ni rafiki yako ambaye unaweza ukanieleza kitu chochote lakini kumbe si mtu muhimu kwako hata kidogo.” Akasema Elvis “ Elvis,I’m sorry.Jana ulisikia maongezi yangu na Godson pale bustanini.Samahani kama nilikukera na samahani kwa kutokueleza kuhusu jambo hili kwani niliona halikuwa na umuhimu wowote wa kukueleza kwani ni la kibinafsi zaidi.” Akasema Patricia “ Patricia halikuwa na umuhimu kwako lakini kwangu mimi lina umuhimu mkubwa.Kama rafik yako nilihitaji kujua kama uko katika mahusiano au vipi” akasema Elvis “ Elvis kuna mambo ambayo ni ya ndani sana na ambayo si lazima kuyaweka hadharani kwa kila mtu.” “ Ni kweli ni suala binafsi lakini kulikuwa na ulazima wa kunieleza ukweli ili nifahamu.Hukupaswa kunificha” “ Samahani kwa hilo Elvis.Naomba basi nitumie nafasi hii kukueleza ukweli” akasema Patricia halafu akamshika mkono Elvis na kwenda kuketi juu ya jiwe “Mtu niliyekuwa nikiongea naye jana usiku anaitwa Godson.Ni mdogo wake Juliana.Nilikutana naye siku Juliana aliponifanyia sherehe ndogo ya kunipongeza nyumbani kwao.Toka siku ile tukatokea kuwa marafiki .Ukaribu wetu ulizidi pale alipoanza kunifundisha kompyuta.Siku moja kabla sijaondoka kuja shuleni Godson alinipeleka ufukweni na ndipo aliponieleza kwamba ananipenda na anataka tuwe wapenzi.Nilimkatalia kwamba hatuwezi kuwa wapenzi kwa sababu bado ninasoma.Alionyesha kunielewa na akaniomba tuendelee kuwa marafiki.Nimekuwa nikiwasiliana naye karibu kila siku na jana wakati nikiongea naye alinikumbusha kuhusu ombi lake la mimi na ye ye kuwa wapenzi” Akasema Patricia.Elvis akavuta pumzi ndefu.Maelezo yale yalionekana kumchoma sana . “ So you said Yes? Swalilile likambabaisha kidogo Patricia akajikaza na kusema “ Yes.I said yes .Nilimkubalia tuwe wapenzi.” Akasema Patricia halafu ukimya mzito ukatanda. “ I said yes because I cant handle these feelings anymore” akasema Patricia.Elvis akageuka na kumtazama halafu akasema “ This guy,do you love him? Patricia akatabasamu na kusema “ Yes I do love him so much.Toka nilipoonana naye nimetokea kumpenda sana.Huyu ni mwanaume wa kwanza kumpenda katika maisha yangu” akasema Patricia maneno ambayo yalizidi kumnyong’onyeza Elvis “Patricia nakushukuru kwa kunieleza ukweli.Pamoja na hayo kuna mambo nataka nikuase.Kwanza naomba ufahamu kwamba mapenzi yapoo na kila binadamu hupenda na hakuna anayekuzuia kupenda kwa hiyo kama huyo Godson ndiye mtu ambaye una imani moyo wako umemchagua basi nakupongeza ila kuwa makini sana kwani siku hizi walaghai wengi .Wengi wamekuwa wakitamani badala ya kupnda.Kitu kingine ninachotaka kukushauri ni kwamba umeufungua ukurasa mpya wa mapenzi katika maisha yako.Umeingia katika mapenzi na siku zote mapenzi huwa ni upofu na hivyo unapaswa kuwa mwangalifu sana ili yasije yakakuchanganya na kukupotezea mwelekeo mzima wa maisha yako.Mwisho naomba unifikishie salamu zangu kwa huyo kijana.Mwambie kwamba umempa moyowako autunze na asithubutu kukutoa chozi.Siku akifanya jambo lolote la kukuumiza he’ll answer to me” akasema Elvis halafu akamshika Patricia mkono “ Twende tuondoke” akasema Elvis.Patricia akamuangalia kwa mshangao na kumuuliza “ Elvis bado hujanieleza ni jambo gani linalokusumbua kiasi cha kukufanya usiingie darasani siku ya leo? Naomba nawe uwe muwazi kwangu kama nilivyokuwa muwazi kwako” akasema Patricia “ Patricia umesema mwenyewe kwamba kuna mambo ambayo si lazima kuyaweka wazi kwa hiyo nasikitika kwamba sintaweza kukwambia ni kitu gani kinachonisumbua.Ni siri yangu.Twende tuondoke” akasema Elvis wakaondoka. “Bado sijakata tamaa kwamba siwezi kumpata Patricia.Nilifanya makosa kutokumweleza ukweli mapema kwamba ninampendalakini pamoja na hayo bado nitaendelea kuwa karibu naye.Patricia atakuwa wangu tu muda utakapofika” akawaza Elvis wakiwa njiani wakirejea shuleni “ Kitu gani kinamshumbua Elvis? He looks so strange.Sijawahi kumuona akiwa katika hali hii toka nimemfahamu.Lazima kuna kitu kinamsumbua kichwa chake.Halafu kuna kitu nimekigundua inaonekana hakufurahishwa na kitendo cha mimi kumwamba kwamba nimemkubali Godson tuwe wapenzi.Ninahisi hii inaweza ikawa sababu ya mabadilio yake ya ghafla.Kama ni kweli kwa nini basi akwazike na jambo hili? Whats going on with him? Is he in love with me? Patricia akajiuliza “ Ouh No ! That cant happen.Elvis ni rafiki yangu mkubwa na hata siku moja sjawahi hata kuota kwamba mimi naye tunaweza kuwa wapenzi.Siku zote nitaendelea kumuheshimu na kumthamini kama rafiki na mtu wa karibu sana.Kama ni kweli ana hisia hizo za kunipenda anatakiwa azifute kwa sababu tayari nimeufungua moyo wangu kwa Godson” akawaza Patricia ******************** Siku zilikwenda kwa kasi na hatimaye muhula wa kwanza wa masomo ukamalizika na shule zikafungwa.Katika mthani wa kumaliza muhula kama kawaida yake Patricia alishika nafasi ya kwanza.Elvis alishika nafasi ya kumi na tatu.Yalikuwa ni matokeo ya kustusha sana kwa mtu kama Elvis ambaye katika majaribo ya kila mwezi hakuwahi kutoka nje ya nafasi tano za juu Usiku uliotangulia siku yakufunga shule Patricia na Elvis walikuwa bustanini wakibadilishana mawazo.Pamoja na maongezi lakini kuna jambo lililokuwa linamuumiza kichwa Patricia .Ni kuhusu kuporomoka ghafla kwa kiwango cha Elvis toka kushika nafasi tano za juu hadi nafasi ya kumi na tatu “ Patricia mbona unanitazama namna hiyo? Akauliza Elvis baada ya kugundua kwamba Patricia amekuwa akimuangalia usoni kwa muda mrefu “ Elvis kuna jambo ambalo nataka kukuuliza” “ Uliza tu usihofu” “ Elvis nimestushwa sana na matokeo yako katika mtihani wa kumaliza muhula.Sikuwahi kuota kama ungeweza kushika namba ya kumi na tatu.Nini kimetokea? Elvis ninakufahamu vizuri na ninaufahamu uwezo wako na kila mtu anashangaa ni jambo gani limetokea hadi uporomoke namna hii? Elvis akatabasamu na kusema “ Patricia nakushukuru sana kwa ku0nyesha kuguswa na tatizo hili.Ni kweli nimeporomoka sana darasani kiasi cha kushangaza lakini hakuna hata mtu moja aliyeonekana kuguswa na matokeo hayo na kutaka kujua kulikoni zaidi yako.Ni wewe pekee ambaye umeonyesha kunijali.Wewe ni rafiki wa kweli na ndiyo namna marafiki wanapaswa kuwa” akasema Elvis halafu akameza mate na kuendelea “ Patricia siwezi kukuficha kwamba ni kweli nina matatizo na ndiyo yaliyonipelekea kushuka kwa kiwango changu namna hii.” Matatizo gani hayo Elvis? “ Utanisamehe Patricia lakini sintaweza kukwambia kwa sababu ni matatizo binafsi.Nitajitahidi niendapo likizo niyamalize matatizo yangu na nitakaporudi muhula ujao nitakuwa katika kiwango changu cha kawaida” akasema Elvis “ Nafurahi kusikia hvyo Elvis.Nitakuwa nikiwasiliana nawe kila siku ili nijue maendeleo yako na tafadhali kama kuna jambo lolote ambalo ninaweza kulifaya linaloweza kukusadia katika matatizo yako naomba uniambie na niko tayari kukusaidia” akasema Patricia “ Nitafurahi sana kuwasiliana nawe mara kwa mara Patricia lakini kuna kitu kimoja ambacho nataka kukukumbusha.Ni kwamba unarudi nyumbani na nina hakika huko utaonana na mpenzi wako Godson.Tafadhali kuwa muangalifu sana .Dunia ya sasa imejaa ulaghai mwingi.Sitaki upatwe na tatizo lolote Patricia.Sitaki kukuona ukiumia,sitaki ujutie maamuzi yako” “ Ahsante sana Elvis kwa kunikumbusha wajibu wangu.Nakuahidi nitakuwa makini” akasema Patricia wakaagana na kila moja akaelekea bwenini kwake kujiandaa na safari ya kesho ****************** Ni jumamosi tulivu siku ambayo mwanamitindo Juliana alikuwa akisherehea siku yake ya kuzaliwa.Ni wiki ya pili toka Patricia arejee nyumbani kwa likizo.Patricia alikuwa ni mwenye furaha sana kwanza ni kwa kuonana tena na mama yake kipenzi pamoja na watu wake wa karibu kama Juliana na wengineo,pili alikuwa na furaha kwa kuendelea kushika nafasi ya juu kabisa katika mitihani yake, na tatu alikuwa mapenzini na Godson ambaye wa sasa anafanya kazi katika mtandao wa simu wa MasaiTell. Wageni waalikwa waliendelea kuwasili nyumbani kwa akina Juliana ambako sherehe ya kumbu kumbu ya kuzaliwa kwa mrembo huyu inafanyika.Patricia na mama yake walikuwpo hapa kuanzia asubuhi wakisaidia katika shughuli mbali mbali za uandaaji wa sherehe hii Saa moja za joni sherehe ikaanza.Juliana akajitokeza bustanini akiwa amependeza vilivyo kwa gauni zuri alilolibuni yeye mwenyewe.Alikuwa anatembea taratibu katika zuria jekundu huku akisindikizwa na muziki laini.Watu wote walikuwa wamesimama wakimshangilia Godson aliyekuwa amependeza ndani ya suti nzuri nyeusi,ndiye aliyempokea jukwaani wakakumbatiana “ Happy birthday Juliana” akasema Godson na kumuongoza dada yake hadi katika meza iliyokuwa na keki iliyotengenezwa kwa ustadi mkubwa.Godson akawasha mishumaa iliyokuwa juu ya keki ile halafu Juliana akaisogelea ,akafumba macho na kuizima ile mishumaa,makofi mengi na vgere gere vikasikika Zoezi lililofuata ni kuwalisha keki wageni waalikwa na baada ya hapo kikafuata kipindi cha zawadi na pongezi.Baada ya zoezi hilo kukamilika,ukawadia muda wa chakula na baadae ukafika wakati wa vinywaji na muziki.Vinwaji vya kila aina vilikuwepo.Juliana akafungua muziki na Godson mdogo wake halafu watu wengine nao wakajumuika kulisakata rhumba.Patricia alikuwa amesimama katika moja ya nguzo akitabasamu na kufurahi namna watu walivyokuwa wakijimwaga na muziki.Mara akafunikwa macho na viganja vya mikono,akaipapasa halafu akacheka kidogo baada ya kugundua alikuwa ni Godson “ Pole sana Patricia “ akasema Godson akiwa na glasi yake ya kinywaji mkononi “ Pole ya nini Godson? “ Umefanya kazi kubwa sana leo kuandaa sherehe hii.Sherehe imefana sana hongera” akasema Godson na Patricia akatabasamu “ Its nothing Godson compared to what Juliana has done to me” akasema Patricia na kumfanya Godson atabasamu “ Unapenda kucheza muziki? Akauliza GodosnHapana sijui hata huo muziki wenyewe unachezwaje.Ninafurahi tu kuwaona watu wakicheza” “ Mimi mwenyewe sijisikii kucheza .Twende tutafute mahala tukae tuongee wakati watu wakiendelea kuserebuka” akasema Godson na kumshika Patricia mkono wakazunguka nyuma ya nyumba wakaenda kukaa katika majani mazuri .Mwanga haukuwa mkali eneo hili walilokaa hivyo kwa mtu kuwaona mahala walipokaa itakulazimu usogee karibu zaidi.Patricia alionekana kuogopa kuwepo kule peke yao “Godson,itakuaje tukikutwa huku peke yetu wakati wengine wote wako katika sherehe? I’m scared people might get suspicious.Sitaki watu wafahamu kuhusu mahusinao yetu” akasema Patricia kwa wasi wasi.Godson akamuwekea kidole mdomoni Shhhhhh!!!!,,Usiogope my angel.Mimi ndiye mfalme wa mahala hapa na isitoshe hakuna mtu yeyote atakayekuja huku.Patricia nafahamu toka umerudi mama yako amekuwa anakuchunga sana. Na hivyo kufanya makutano yetu kuwa magumu.Nina mambo mengi ya kuongea nawe kuhusu mustakabali mzima wa mapenzi yetu.I want to show you how much I love you” akasema Godson “ Ni kweli Godson .Hata mimi nina hamu sana ya kupata wasaa mzuri wa kukaa nawe tukaongea na kufurahi pamoja.Nitajitahidi katika wiki hii nipate siku moja ambayo itakuwa maalum kwa ajili yetu” Godson akasogea karibu zaidi ya Patrcia halafu akauzungusha mkono wake wa kushoto shingoni mwa Patrcia na kumfanya astuke .Wote wawili wakabakiwanatazamana halafu Godson akasema “ Patricia kuna zawadi ambayo nimekuandalia,twende ndani nikakupatie” akasema Godson akamshika Paricia mkono na kwa kupitia mlango wa nyuma wakaingia ndani.Nyumba ilikuwa kimya kabisa,watu wote walikuwa bustanini wakilisakata rhumba.Godson aamuongoza Patricia hadi chumbani kwake na kumkaribisha.Patricia akasita kuingia “ Usiogope Patricia.Hakuna mtu yeyote aliyekuona wala atakayejua kwamnba uko humu chumbani.Ingia tafadhali kabla hajatokea mtu na kukukuta hapa mlangoni” akasema Godson na kwa wasi wasi mwingi Patricia akaingia .Kilikuwa ni chumba kikubwa na kizuri.Patricia akatabasamu Chumba chako kizuri sana.Nimezipenda picha zako za ukutani” akasema Patricia.Godson akacheka kidogo halafu akamkaribisha Patricia sofani.Akaenda katika kabati lake kubwa akalifungua na kutoa kiboksi kidogo chenye rangi nyekundu ,akamshika mkono Patricia na kumuoongoza hadi katika kioo kikubwa. “ Patricia you are blessed with natural beauty..Do you know how beautiful you are? Akauliza Godson aliyekuwa amesimama nyuma ya Patricia ambaye uso wake ulionyesha woga mwingi .Alihisi msisimko wa aina yake pale mikono ya Godson ilipoigusa shingo yake.Alihisi mapigo ya moyo wake yakibadilika na kuanza kwenda kwa kasi kubwa Toka ndani ya boksi Godson akatoa mkebe mdogo halafu akaufungua na ndani yake kulikuwa na mkufu wa thamani kubwa.Akamvisha Patricia shingoni.Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Patricia kuvaa shingoni mkufu wa gharama kubwa namna ile.Kwa furaha akageuka na kusema “ Ahsante sana Godson kwa mkufu huu mzuri.Nimeupenda sana” akasema Patricia huku uso wake ukionyesha furaha isiyoeleza.Godson akamvuta karibu yake zaidi halafu akampiga busu moja zito linalomfanya Patricia aweweseke.Ilikuwa ni http://deusdeditmahunda.blogspot.com/mara yake ya kwanza kupigwa busu na mwanaume.Mwili wote ukamsisimka.Midomo yake ikabaki inacheza akashindwa kuongea akabaki anamtazama Godson.Taratibu Godson akaushusha mkono wake wa kulia akivipitisha vidole vyake kati katiya utiwa mgongo hadi sehemu za kiunoni.Patricia akastuka na kutoa mguno Alihisi kama macho yake yanaanza kuona giza.Alisikia raha ya ajabu “G..go…gods…on” akaita kwa taabu Patricia huku akihema kwa kasi na mara akashikwa sehemu Fulani ambayo inamfanya asikie raha isiyoelezeka.Akalegea kabisa Ilikuwa ni mara yake ya kwanza kusikia raha ya namna ile.Godson akamuinua na kumuweka kitandani “ God..gods..on…N ..Dont/…..” akasema Patricia kwa sauti dhaifu lakini Godson tayari alikwishapandwa na midadi akaendeleza autundu katika mwili wa Patricia ambaye aliendelea kutoa miguno ya kusikia raha.Godson alimfanyia Patricia kila aina ya utundu na kumpagawisha vilivyo.Baada ya kuona Patricia hajiwezi tena,Godson taratibu akaanza kufungua vifungo vya blausi ya Patricia na akahisi kuchanganyikiwa baada ya kukishuhudia kifua cha Patricia kilichobeba matiti madogo yaliyosimama.Mwili ulizidi kuchemka kwa ashki,akainama na kuyabusu matiti yale ambayo hayakuwahi kuguswa na mwanaume yeyote hapo kabla.Akayabusu na kuanza kuyachezea.Patricia aliendelea kutoa miguno kila pale alipoguswa.Taratibu Godson akafungua zipu ya sketi aliyokuwa ameivaa Patricia na kuivua.Patricia akabakiwa na nguo ya ndani pekee.Godson akazidi kuchanganyikiwa alipoushuhudia mwili ule mwororo .Akausogeza mkono na kuishika ile nguo ya ndani na alipotaka kuivua Patrcia akamshika mkono . “God..Godson..No….” akasema Patricia huku akiibana miguu yale.Godson akamsogelea halafu akatoa ulimi na kuuingiza sikini mwa Patricia kwa ufundi sana.Patricia akatoa ukelele.Godson akaendelea kuuzungusha ulimi wake ndani ya sikio la Patricia na taratibu akamwambia “ Usiogope mpenzi wangu.Ninakupenda na hautaumia” “ Godson akaedelea kuuchezesha ulimi sikioni mwa Patricia na wakati huo huo kwa kutumia mkono wake wa kulia akaishika ile ngupo ya ndani ya Patricia akaivua.Baada ya kuhakikisha kwamba Patricia ameandaliwa vya kutosha Godson akavua nguo zake na kubaki mtupu.Uume wake ulikuwa umesimama wima tayari kwa shughuli.Akachukua chupa ya mafuta laini na kuupaka ili asimuumize Patricia .Akapanda kitandani na kumuweka Patricia katika mkao mzuri na kisha akamuingiza rasmi katika ulimwengu wa mapenzi.Patricia alitoa ukelele na miguno.Alikuwa ameondolewa bikira yake . “ Ouh gosh ! I cant believe this.Patricia..!! Ouh my angel,I love you…I love you so much” akasema Godson akiwa juu ya mwili wa Patricia akinedelea na utundu . Baada ya kufika mshindo,Godson akajitupa pembeni ya Patricia “ Ouh gosh,Ive never met a sweet girl like you Patricia” akasema Godson huku akimbusu Patricia ambaye machozi yalikuwa yanamtoka.Godson akamfuta kwa mikono yake. “ Nyamaza kulia Patricia.Usilie mpenzi wangu” Godson akambembeleza Patricia ambaye bado aliendelea kulia.Godson akainuka na kwenda kuchukua kitambaa akamfuta machozi Usilie Patricia.Usilie mpenzi wangu” akasema Godson huku akimbusu Patricia shavuni “Godson kwa nini umenifanyia hivi? Akauliza Patrcia huku akilia “ Shhhhh..!!!!!...Patricia tafadhali usikasirike.Huu ni mwanzo mzuri wa mapenzi yetu.” “ Godson tulikubaliana kwamba hatutafanya mapenzi hadi nitakapomaliza masomo yangu.Kwa nini umevunja ahadi yako na kunilaghai hadi tukafanya ? “ Nisamehe Patricia.Nisamehe mpenzi wangu.Ni kweli hatukukubaliana hivi na hata mimi sielewi imetokeaje tukajikuta tukifanya” Akasema Godsn na Patricia akazid kutoa machozi “ Umenitoa bikira yangu ambayo ilikuwa ni zawadi kwa manaume wangu wa kwanza nitakayempenda ambaye ningemtunzia hadi tutakapofunga ndoa.Kwa sasa sintakuwa na thamani tena kwako” akasemaPatricia na kuendelea kuangusha machozi “Tafadhali usiseme hivyo Patricia.Hujui ni kwa kiasi gani ninakupenda malaika wangu.Wewe ndiye kila kitu kwangu ,nakupeda zaidi ya ninavyoweza kukueleza.Usiwe na hofu yoyote kuhusu mimi” akasema Godson “ Godson nimekuwa na mashaka kama kweli unanipenda kwa dhati au lengo lako lilikuwa kunitumia kimwili kwa tamaa zako.Kama unanipenda kwa namna ambayo umekuwa ukiniambia kila siku basi usingenishawishi tukafanya mapenzi.” Akasema Patricia na kukaa kitandani na mara akastuka baada ya kukumbuka kitu Fulani Gosh..!!! haukutumia hata kinga.” Akasema Patricia kwa ukali huku akimpiga Godson makofi mgongoni. “ Patricia i’m sorry lakini hakuna tatizo.Ninajiamini na sina matatizo yoyote” akasema Godson .Patricia akainama na kulia “ I’m so stupid..How could I be so stupid .Kwa nini nimemuacha Godson akanifanyia hivi? akalia kwa uchungu Patrcia.Godson akamtazama na kusema “ Patricia inuka ukaoge ujiweke vizuri.Wanaweza wakaanza kututafuta akina Juliana” akasema Godson Patricia alishikwa na hasira kiasi cha kushindwa kuongea tena.Akainuka kitandani akajitazama na kuitazama damu kidogo iliyokuwa katika shuka jeupe lililotundikwa kitandani .Akazidi kuumia Gosh ! Ameniondolea usichana wangu.Nimejitunza kwa miaka hii yote lakini leo hii nimenaswa kama ndege aliyeloa.I’m so stupid” akawaza Patricia huku akivaa nguo zake “ Bafu lile pale Patricia,hutaki kuoga? Akauliza Godson.Patricia akamuangalia kwa jicho kali sana halafu akaufungua mlango na kutoka.Moja kwa moja akaelekea chumbani kwa Juliana akajitazama katika kioo na kulia sana “I’m so stupid” hili ndilo neno alilobaki akilisema.Akaufungua mlango wa bafuni na kuingia kuoga.Bado picha ya tukio zima lililotokea ikaendelea kumjia kichwani. “ Patricia msichana ambaye ninaheshimika sana kwa uwezo wangu mkubwa darasani lakini leo hi nimenasa mtegoni.I’m so fool.I’m so stupid.How could I let that bastard do that to me? Tena hakutumia hata kinga.Vipi kama akiniambukiza magonjwa hatari ya zinaa? Ouh gosh how could I be so stupid? Kibaya zaidi ninaweza hata kupata mimba” Mwili wote ukamsisimka pale wazo la kupewa mimba lilipomjia kichwani. “ Help me God mambo haya yasinitokee.Juhudi zangu zote za miaka hii yote za kujitunza,na kujituma kusoma vyote vitakuwa kazi bure.Ndoto zangu zote za maisha zitapotea.” Patricia akasema taratibu halafu akamaliza kuoga akavaa nguo zake.Wakati akiwa katika meza ya vipodozi mara mlango ukafunguliwa akaingia Juliana.Akastuka baada ya kumkuta Patricia mle chumbani “ Patricia uko huku? “ Ndiyo dada Juliana.Nilisikia joto kali nikaona nije huku kuoga.Mbona umeloana hivyo? Kuna rafiki zangu wamechelewa wamefika muda si mrefu ndio walioniogesha hii shampeni.” Akasema Juliana huku akilivua ganuni lake zuri na kuvaa lingine halafu akaongozana na Patricia kuelekea bustanini kuendelea na sherehe. Sherehe ziliendelea hadi ilipotimu saa saba za usiku.Wageni wakaondoka zao.Baadhi ya wageni ambao hawakujisikia kuondoka usiku ule wakapewa nafasi ya kulala katika vyumba vya wageni kwani jumba lile lilikuwa kubwa na vyumba vingi vya kulala.Mama yake Patricia yeye alipewa chumba chake maalum cha kulala halafu Patricia yeye akaenda kulala chumbani kwa Juliana “Ouh thank God sherehe imekwisha.Patricia nashukuru sana kwa msaada wako mkubwa katika kuifanikisha sherehe hii ambayo imependeza sana” akasema Juliana wakati wakijiandaa kulala “ Ouh Dada Juliana please don’t mention.Sijafanya chochote kulinganisha na wema wako kwangu.” Akasema Patricia “ Ninafurahi sana kufahamiana nanyi.Japokuwa wazazi wangu wako mbali lakini kuwa karibu na mama yako ninajiona ni kama vile niko na wazazi wangu” akasema Juliana .Patricia hakujibu kitu akatabasamu.Juliana akamsogelea akamtazama Patricia usoni halafu akasema “ Patricia I’ve noticed you’ve changed suddenly.Umekuwa mkimya na hata uso wako umebadilika kitu ambacho si kawaida yako.What happened? Kuna kitu kimakukwaza mdogo wangu? Are you not happy here? Akauliza Juliana .Patricia akashindwa kujizuia kutoa machozi .Juliana akazidi kuwa na wasi wasi “ Patricia are you ok? Akauliza “ I’m ok” “ Mbona unalia? What happened? Kitu gani kinakuliza? “Sina atizo lolote dada Juliana.I’m just too emotional today.Kila nikikumbuka mambo yote ambayo umenifanyia toka tumefahamiana nashindwa kujizuia kutokwa na machozi.You are very kind” akasema Patricia.Juliana akamkumbatia halafu akamuomba Patricia alale apumzike “ Patricia ananidanganya.Something is worng with her.Kitu gani kinachomsumbua na kumtoa machozi? Anyway nitatafuta nafasi niongee naye vizuri ili anieleze kitu gani kinachomkwaza.Kwa sasa ngoja apumzike amefanya kazi kubwa sana siku ya leo” akawaza Patricia Ulikuwani usku mrefu mno kwa Patricia.Ilimchukua muda mrefu upata usingizi kutokana na mawazo mengi aliyokuwa nayo. Hatimaye kulipambazuika na baada ya shughuli za usafi kumalizika Patricia na mama yake wakaanza kujiandaa ili warejee nyumbani kwao.Kabla hawajaondoka Patricia akamuita Juliana chumbani kwake halafu akatoa mkufu wa dhahabu mfukoni na kumpatia “Dada Juliana naomba umpatie Godson mkufu huu.Alinipatia kama zawadi lakini siwezi kuuvaa” akasema Patricia.Juliana akamuangalia na kusema “ Patricia tell me what happened? Godson amefanya kitu chochote cha kukukwaza?Tell me please” akasema Juliana “ Hapana dada Juliana.Hajanifanyia jambo lolote baya isipokuwa alinipatia mkufu huu ambao una thamni kubwa tofauti na mimi.Sina thamani ya mkufu huu wa gharama kubwa” akasema Patricia na kuzidi kumshangaza Juliana “ Patricia wewe ni mdogo wangu.Please be honest with me.Did you and Godson had a fight? Godson aliniambia kwamba umemkubalia muwe wapenzi sasa nashangaa nini kimteokea? Patricia akavuta machozi na kusema “ Ni kweli tulikuwa wapenzi but not anymore.” Akasema Patricia “ Patricia mbona hutaki kunieleza nini kimetokea? Godson amekufanya nini? Patricia akainama akakosa neno la kusema .Akainua kichwa na kusema Dada Juliana thank you for everything.I have to go” akasema Patricia ,akageuka akafungua mlango na kutoka.Juliana alibaki anashangaa .Akachukua funguo ya gari na kuwarudisha Patricia na mama yake nyumbani.Garini Patricia alikuwa mkimya sana.Kichwa chake kilikuwa na mawazo mengi sana “ I’m so stupid.Ilikuaje nimruhusu Godson anivue nguo na kunifanyia vile.? I’m so weak and stupid.Nilimepnda sana Godson lakini kwa sasa simtaki tena kwa kushindwa kuyaheshimu mapatano yetu ambayo tulikubaliana kwamba hatutafanya mapenzi hadi pale nitakapokuwa nimemaliza masomo yangu.Lakini amenishawishi hadi tukafanya mapenzi.It was my first ime and I didnt know what to do.Sitaki tena kusikia suala la mahusiano.Sitaki tena kusikia suala la mapenzi.From today,I erase Godson from my heart and evey fibre of my body” akawaza Patricia akiwa garini Kwa siku zote zilizofuata Patricia hakuwa akitoka numbani.Alikuwa mkimya sana na muda mwingi aliutumia kujisomea.Hakuwasiliana tena na Godson na hakutaka tena kuonana naye licha ya Godson kujitahidi kumtafuta kwa juhudi zote ili waongee kuweka sawa mambo *****************







 ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA “Kwanini sikuhizi zote asiniambie kama ana mtuwake anayempenda? Lakinisiwezikumlaumu kwani ni kosa langu.Ningemwambia mapemakwamba ninampendanisingeumia namna hii.Pamoja na hayo,bado sijapoteza matumaini.Nitaendelea kupambana hadi dakikayamwisho.Nitapambana kuhakikisha kwamba Patriciaanakuwa wangu.Yeye ndiye mwanamke pekee ninayempenda katika maisha yangu.” AkawazaElvis halafu akaenda katika sinkiakafunguamaji akanawauso kisha akatoka na kuelekea tenabustanini mahala alikokuwa amekaana Patricia lakiniPatriciahakuwepo.Akaketi kitini na kuinua kichwa akatazamajuu angani. “Iswearin heaven andearth,Patricia willbe mine.She willfall in my hands andloveme andno one elsewillmake us apart.To win Patricia’s heartis my major goal for now.” Akasema Elvis kwa sauti ndogo.Akatoasimuyake akafunguamahala anakohifadhia picha akaitazama picha yaPatricia “You’ll be mine Patricia.You’ll be mine.You’ll love onlyme? Akasema Elvishalafu akainukana kuelekea bwenini ENDELEA……………………………. Kitendocha Elviskutoonekana darasani kilimchanganya sana Patriciana kumfanyaawe na mawazo mengi.Haikuwa kawaida yaElviskukosa darasani.Saa nnena nusukengele ikagonga kuashiriakwamba ni wakati wamapumziko yaasubuhi.Patricia akatoka kwa haraka na kumfuata Martinambaye ndiyeanalala chumba kimoja na Elvis “Martinsamahani,kuna jambo naomba kukuuliza”akasemaPatricia kisha wakasogeapembeni “Jambo gani Patricia? “Ni kuhusu Elvis.Mbona leo hajaingia darasani? Ana matatizo? “Hajaingiadarasani? Martinakauliza. “Ndiyo na si kawaida yake kukosa darasani.Ana matatizo yoyote? “Sinahakika kama ana matatizo kwa sababumimi niliwahi kuamkaasubuhi nikamuamshaili nayeajiandaelakini akaniambia kwamba nitangulie yeye atafuatabaadae” “Okahsante ngojanikamuangalie” akasema Patriciahuku akitembea kwa kasikuelekea katika bwenilaakina Elvis “Patriciahuruhusiwikuingiakatika bwenilawavulana.Ukionekana kule unawezakupewa adhabu” akasema Martin “Idon’t care.Natakakujua ni kwa nini Elvishajaingiadarasani leo.He’s my friendandI need toknowif he’s havinga problem.” Akasema Patriciana kuchomokahadi katika bwenila wavulana.Anafahamu namba ya chumbacha akina Elvis akanyoosha moja kwa moja na kukinyongakitasa cha chumbanamba sita akaingiandani lakiniElvishakuwemo “Ouhgosh ! Elvisamekwenda wapi? Mbona humu hayumo? Akajiuliza Patriciahalafu akatoka mbio mle chumbani “Nimekumbukakitu.Kuna sehmu moja ambayo huwa anapendasana kwenda kupumzika.Ngoja nikamuangalie kule” akawazaPatriciahuku akikimbia kuelekeakata msituwa shule.Pembeni yamsituulekulikuwana maporomoko madogoyamaji na hiindiyosehemu ambayo Elvishupenda sana kuja kupumzika. KamaPatriciaalivyokuwa amehisi ni kweli Elvisaalikuwaamekaajuu yajiwe. “Elvis…!!!!”akaita Patriciana kumstua Elvisaliyekuwa amezama katika mawazo mengi. “Patricia” akasema Elvis kwa mstuko wakumuona Patricia maeneo yale..Kwa haraka akainukana kumfuata “Patriciawhatareyou doing here? AkaulizaElvis “Elvisnimekutafuta kilamahala nikakukosanikajualazima utakuwa huku.” “Patriciatafadhaliusithubutusiku nyinginekupita humu msituni peke yako.Kunahatari nyingi humu.Hakuna usalamaukiwa mwenyewe” “UsijaliElvis,sintafanya hivyo tena.Nimelazimika kufanyahivyo kutokana na wasi wasiniliokuwa nao kwa kutokuona darasanileo.Sikawaida yako kukosadarasani.Una matatizo gani? Tell me ElvisI’m your friendandI do careabout you.Una matatizo gani? Kwanini hujaingia darasanileo? Unaumwa? Akauliza Patricia “Hapana siumwiPatriciaila sikujisikia tukuingiadarasani leo na ndiyomaana nimekuja huku ili kutuliza kichwa changu.” Patriciaakmshika Elvis mkono wakatazamana “Elvisniambie unamatatizo gani leo? Nini kinakusumbua? Tafadhalinaomba unieleze” Elvisakavuta pumzindefuakamtazama Patriciana kusema “Ni kweli nina matatizo PatriciaKuna jambo linaniumiza sana kichwa changu lakininasiktikakwamba sintaweza kukwambia.Thankyouforyour concern” akasema Elvis “Elvisyou do trustme right?Akauliza Patricia “OfcourseI do.Whatabout you do you trustme ? “Ido trustyou Elvis.Kwa nini umeniuliza hivyo? “Nina wasiwasi na jibu lako Patricia.Sina hakika kama unaniamini na ndiyomaanaumekuwamsiri sana” “Siri?! Patriciaakashangaa “Ndiyo? “Elvismbona nimekuwa nikikueleza kilajambo linalonihusu? Hakunajambo ambalo nimewahikukuficha.Wewe ndiye mtupekeeunayefahamu kuhusu undani wamaishayangu”akasema Patricia “Youdidn’t tell me that you havea boyfriend” “boyfriend? Patriciaakashangaa “Ndiyo.Kwa nini kila sikutulipokuwa tunaongeleakuhusu mambo hayaya mahusianoulisema kwamba huna mpenzi? Kwa niniulinidanganya? AkaulizaElvis.Patricia akashikwana kigugumiziakashindwa ajibu nini.Akakumbuka kwamba wakati akiongeana Godsonjanausiku Elvis alikuwepokaribu. “Mimi nilidhani ni rafikiyako ambaye unawezaukanielezakitu chochotelakini kumbesi mtumuhimukwako hata kidogo.” Akasema Elvis “Elvis,I’m sorry.Jana ulisikiamaongezi yangu na Godson palebustanini.Samah anikama nilikukera na samahani kwa kutokukuelezakuhusu jambo hili .Niliona halikuwana umuhimuwowote wa kukuelezakwani ni lakibinafsi zaidi.” Akasema Patricia “Patriciahalikuwana umuhimukwako lakinikwangumimi lina umuhimu mkubwa “akasemaElvis “Elviskunamambo ambayo ni ya ndani sana na ambayo silazima kuyawekahadharanikwa kila mtu.” “Ni kweli ni suala binafsi lakini kulikuwa na ulazima wakunieleza ukweli ilinifahamu.Hukupaswa kunificha” “Samahanikwa hilo Elvis.Naomba basi nitumie nafasihii kukuelezaukweli” akasema Patriciahalafu akamshika mkonoElvis na kwenda kuketijuu ya jiwe “Mtu niliyekuwa nikiongea nayejana usikuanaitwaGodson.Nimdogo wake Juliana.Nilikutana nayesikuJuliana aliponifanyia sherehe ndogo ya kunipongezanyumbani kwao.Toka siku ile tukatokeakuwa marafiki .Ukaribu wetuulizidipalealipoanza kunifundisha kompyuta.Siku moja kabla sijaondoka kujashuleni Godsonalinipeleka ufukweni na ndipo aliponieleza kwamba ananipendana anataka tuwe wapenzi.Nilimkatalia kwamba hatuwezi kuwawapenzi kwa sababu bado ninasoma.Nimekuwa nikiwasiliana naye karibukilasikukwa njia yamtandao na janawakati nikiongeanaye alinikumbushakuhusu ombilake la mimi na yeye kuwa wapenzi”Akasema Patricia.Elvis akavutapumzi ndefu.Maelezo yale yalionekana kumchoma sana . “So you said Yes? Swalilile likambabaisha kidogo Patricia akajikazana kusema “Yes.I said yes .Nilimkubalia tuwe wapenzi.” Akasema Patriciahalafu ukimya mzitoukatanda. “Isaidi yes because I cant handle these feelings anymore” akasema Patricia.Elvis akageukana kumtazama halafu akasema “Thisguy,do you love him? Patriciaakatabasamu na kusema “YesI do love him somuch.Toka nilipoonananayenimetokeakumpenda sana.Huyuni mwanaume wakwanza kumpendakatika maisha yangu” akasema Patriciamanenoambayo yalizidikumnyong’onyeza Elvis “Patricia nakushurukwa kunieleza ukweli.Pamoja na hayokuna mambo nataka nikuase.Kwanzanaomba ufahamu kwamba mapenzi yapona kila binadamu hupendana hakuna anayekuzuia kupendakwa hiyokama huyo Godsonndiyemtuambaye una imani moyo wako umemchagua basi nakupongezaila kuwa makinisana kwani sikuhizi walaghaiwengi.Wengi wamekuwawakitamanibadala ya kupenda.Kitu kingineninachotaka kukushaurini kwamba umeufungua ukurasampyawa mapenzi katika maishayako.Umeingiakatika mapenzi na sikuzote mapenzi huwa ni upofuna hivyo unapaswa kuwamwangalifu sana iliyasijeyakakuchanganyana kukupotezea mwelekeo mzimawa maishayako.Mwishonaomba unifikishie salamuzangu kwa huyo kijana.Mwambie kwamba umempa moyo wako autunze na kamwe asithubutukukutoa chozi.Siku akifanya jambo lolote la kukuumizahe’ll answer tome”akasemaElvis halafu akamshika Patriciamkono “Twendetuondoke” akasema Elvis.Patricia akamuangalaiakwa mshangaona kumuuliza “Elvisbadi hujanielezani jambo gani linalokusumbuakiasi cha kukufanya usiingiedarasanisiku yaleo?Naomba naweuwemuwazi kwangu kama nilivyokuwauwazi kwako” akasema Patricia “Patriciaumesemamwenyewe kwamba kunamamboambayo si lazima kuyawezkawazi kwa hiyonasikitika kwamba sintawezakukwambiani kitu gani kinachonisumbua.Ni siri yangu.Twende tuondoke” akasema Elvis wakaondoka. “Bado sijakata tamaa kwamba siwezi kumpata Patricia.Nilifanya makosa kutokumwelezaukweli mapema kwamba ninampendalakinipamoja na hayobado nitaendelea kuwa karibu naye.Patricia atakuwa wangu tumuda utakapofika” akawaza Elviswakiwa njiani wakirejea shuleni “Kitu gani kinamshumbua Elvis? He looks sostrange.Sijawahi kumuona akiwakatika hali hii toka nimemfahamu.Lazima kunakitu kinamsumbua kichwa chake.Halafu kuna kitunimekigunduainaonekana hakufurahishwana kitendo cha mimi kumwambakwamba nimemkubali Godsontuwewapenzi.Ninahisi hii inaweza ikawasababuya mabadiliko yake yaghafla.Kamani kweli kwa nini basi akwazikena jambo hili?Whats going on withhim?Is he nlovewith me? Patriciaakajiuliza “OuhNo! That cant happen.Elvis ni rafikiyangu mkubwa na hatasiku moja sijawahihatakuota kwamba mimi naye tunawezakuwa wapenzi.Siku zote nitaendelea kumuheshimu na kumthaminikama rafiki na mtuwa karibusana.Kamani kweli ana hisiahizo zakunipendaanatakiwaazifutekwa sababutayarinimeufungua moyo wangu kwa Godson” akawazapatricia TUKUTANESEHEMU IJAYO………………





Siku zilikwenda kwa kasi na hatimaye muhula wa kwanza wa masomo ukamalizika na shule zikafungwa.Katika mthani wa kumaliza muhula kama kawaida yake Patricia alishika nafasi ya kwanza.Elvis alishika nafasi ya kumi na tatu.Yalikuwa ni matokeo ya kustusha sana kwa mtu kama Elvis ambaye katika majaribo ya kila mwezi hakuwahi kutoka nje ya nafasi tano za juu

Usiku uliotangulia siku yakufunga shule Patricia na Elvis walikuwa bustanini wakibadilishana mawazo.Pamoja na maongezi lakini kuna jambo lililokuwa linamuumiza kichwa Patricia .Ni kuhusu kuporomoka ghafla kwa kiwango cha Elvis toka kushika nafasi tano za juu hadi nafasi ya kumi na tatu

“ Patricia mbona unanitazama namna hiyo? Akauliza Elvis baada ya kugundua kwamba Patricia amekuwa akimuangalia usoni kwa muda mrefu

“ Elvis kuna jambo ambalo nataka kukuuliza”

“ Uliza tu usihofu”

“ Elvis nimestushwa sana na matokeo yako katika mtihani wa kumaliza muhula.Sikuwahi kuota kama ungeweza kushika namba ya kumi na tatu.Nini kimetokea? Elvis ninakufahamu vizuri na ninaufahamu uwezo wako na kila mtu anashangaa ni jambo gani limetokea hadi uporomoke namna hii?

Elvis akatabasamu na kusema

“ Patricia nakushukuru sana kwa ku0nyesha kuguswa na tatizo hili.Ni kweli nimeporomoka sana darasani kiasi cha kushangaza lakini hakuna hata mtu moja aliyeonekana kuguswa na matokeo hayo na kutaka kujua kulikoni zaidi yako.Ni wewe pekee ambaye umeonyesha kunijali.Wewe ni rafiki wa kweli na ndiyo namna marafiki wanapaswa kuwa” akasema Elvis halafu akameza mate na kuendelea

“ Patricia siwezi kukuficha kwamba ni kweli nina matatizo na ndiyo yaliyonipelekea kushuka kwa kiwango changu namna hii.”

“ Matatizo gani hayo Elvis?

“ Utanisamehe Patricia lakini sintaweza kukwambia kwa sababu ni matatizo binafsi.Nitajitahidi niendapo likizo niyamalize matatizo yangu na nitakaporudi muhula ujao nitakuwa katika kiwango changu cha kawaida” akasema Elvis

“ Nafurahi kusikia hvyo Elvis.Nitakuwa nikiwasiliana nawe kila siku ili nijue maendeleo yako na tafadhali kama kuna jambo lolote ambalo ninaweza kulifaya linaloweza kukusadia katika matatizo yako naomba uniambie na niko tayari kukusaidia” akasema Patricia

“ Nitafurahi sana kuwasiliana nawe mara kwa mara Patricia lakini kuna kitu kimoja ambacho nataka kukukumbusha.Ni kwamba unarudi nyumbani na nina hakika huko utaonana na mpenzi wako Godson.Tafadhali kuwa muangalifu sana .Dunia ya sasa imejaa ulaghai mwingi.Sitaki upatwe na tatizo lolote Patricia.Sitaki kukuona ukiumia,sitaki ujutie maamuzi yako”

“ Ahsante sana Elvis kwa kunikumbusha wajibu wangu.Nakuahidi nitakuwa makini” akasema Patricia wakaagana na kila moja akaelekea bwenini kwake kujiandaa na safari ya kesho

***************************

Ni jumamosi tulivu siku ambayo mwanamitindo Juliana alikuwa akisherehea siku yake ya kuzaliwa.Ni wiki ya pili toka Patricia arejee nyumbani kwa likizo.Patricia alikuwa ni mwenye furaha sana kwanza ni kwa kuonana tena na mama yake kipenzi pamoja na watu wake wa karibu kama Juliana na wengineo,pili alikuwa na furaha kwa kuendelea kushika nafasi ya juu kabisa katika mitihani yake, na tatu alikuwa mapenzini na Godson ambaye wa sasa anafanya kazi katika mtandao wa simu wa MasaiTell.

Wageni waalikwa waliendelea kuwasili nyumbani kwa akina Juliana ambako sherehe ya kumbu kumbu ya kuzaliwa kwa mrembo huyu inafanyika.Patricia na mama yake walikuwpo hapa kuanzia asubuhi wakisaidia katika shughuli mbali mbali za uandaaji wa sherehe hii

Saa moja za joni sherehe ikaanza.Juliana akajitokeza bustanini akiwa amependeza vilivyo kwa gauni zuri alilolibuni yeye mwenyewe.Alikuwa anatembea taratibu katika zuria jekundu huku akisindikizwa na muziki laini.Watu wote walikuwa wamesimama wakimshangilia

Godson aliyekuwa amependeza ndani ya suti nzuri nyeusi,ndiye aliyempokea jukwaani wakakumbatiana

“ Happy birthday Juliana” akasema Godson na kumuongoza dada yake hadi katika meza iliyokuwa na keki iliyotengenezwa kwa ustadi mkubwa.Godson akawasha mishumaa iliyokuwa juu ya keki ile halafu Juliana akaisogelea ,akafumba macho na kuizima ile mishumaa,makofi mengi na vgere gere vikasikika

Zoezi lililofuata ni kuwalisha keki wageni waalikwa na baada ya hapo kikafuata kipindi cha zawadi na pongezi.Baada ya zoezi hilo kukamilika,ukawadia muda wa chakula na baadae ukafika wakati wa vinywaji na muziki.Vinwaji vya kila aina vilikuwepo.Juliana akafungua muziki na Godson mdogo wake halafu watu wengine nao wakajumuika kulisakata rhumba.Patricia alikuwa amesimama katika moja ya nguzo akitabasamu na kufurahi namna watu walivyokuwa wakijimwaga na muziki.Mara akafunikwa macho na viganja vya mikono,akaipapasa halafu akacheka kidogo baada ya kugundua alikuwa ni Godson

“ Pole sana Patricia “ akasema Godson akiwa na glasi yake ya kinywaji mkononi

“ Pole ya nini Godson?

“ Umefanya kazi kubwa sana leo kuandaa sherehe hii.Sherehe imefana sana hongera” akasema Godson na Patricia akatabasamu

“ Its nothing Godson compared to what Juliana has done to me” akasema Patricia na kumfanya Godson atabasamu

“ Unapenda kucheza muziki? Akauliza Godosn

“ Hapana sijui hata huo muziki wenyewe unachezwaje.Ninafurahi tu kuwaona watu wakicheza”

“ Mimi mwenyewe sijisikii kucheza .Twende tutafute mahala tukae tuongee wakati watu wakiendelea kuserebuka” akasema Godson na kumshika Patricia mkono wakazunguka nyuma ya nyumba wakaenda kukaa katika majani mazuri .Mwanga haukuwa mkali eneo hili walilokaa hivyo kwa mtu kuwaona mahala walipokaa itakulazimu usogee karibu zaidi.Patricia alionekana kuogopa kuwepo kule peke yao

“Godson,itakuaje tukikutwa huku peke yetu wakati wengine wote wako katika sherehe? I’m scared people might get suspicious.Sitaki watu wafahamu kuhusu mahusinao yetu” akasema Patricia kwa wasi wasi.Godson akamuwekea kidole mdomoni

“ Shhhhhh!!!!,,Usiogope my angel.Mimi ndiye mfalme wa mahala hapa na isitoshe hakuna mtu yeyote atakayekuja huku.Patricia nafahamu toka umerudi mama yako amekuwa anakuchunga sana. Na hivyo kufanya makutano yetu kuwa magumu.Nina mambo mengi ya kuongea nawe kuhusu mustakabali mzima wa mapenzi yetu.I want to show you how much I love you” akasema Godson

“ Ni kweli Godson .Hata mimi nina hamu sana ya kupata wasaa mzuri wa kukaa nawe tukaongea na kufurahi pamoja.Nitajitahidi katika wiki hii nipate siku moja ambayo itakuwa maalum kwa ajili yetu”

Godson akasogea karibu zaidi ya Patricia halafu akauzungusha mkono wake wa kushoto shingoni mwa Patrcia na kumfanya astuke .Wote wawili wakabaki wanatazamana halafu Godson akasema

“ Patricia kuna zawadi ambayo nimekuandalia,twende ndani nikakupatie” akasema Godson akamshika Patricia mkono na kwa kupitia mlango wa nyuma wakaingia ndani.Nyumba ilikuwa kimya kabisa,watu wote walikuwa bustanini wakilisakata rhumba.Godson akamuongoza Patricia hadi chumbani kwake na kumkaribisha.Patricia akasita kuingia

“ Usiogope Patricia.Hakuna mtu yeyote aliyekuona wala atakayejua kwamba uko humu chumbani.Ingia tafadhali kabla hajatokea mtu na kukukuta hapa mlangoni” akasema Godson na kwa wasi wasi mwingi Patricia akaingia .Kilikuwa ni chumba kikubwa na kizuri.Patricia akatabasamu

Chumba chako kizuri sana.Nimezipenda picha zako za ukutani” akasema Patricia.Godson akacheka kidogo halafu akamkaribisha Patricia sofani.Akaenda katika kabati lake kubwa akalifungua na kutoa kiboksi kidogo chenye rangi nyekundu ,akamshika mkono Patricia na kumuoongoza hadi katika kioo kikubwa.

“ Patricia you are blessed with natural beauty..Do you know how beautiful you are? Akauliza Godson aliyekuwa amesimama nyuma ya Patricia ambaye uso wake ulionyesha woga mwingi .Alihisi msisimko wa aina yake pale mikono ya Godson ilipoigusa shingo yake.Alihisi mapigo ya moyo wake yakibadilika na kuanza kwenda kwa kasi kubwa

Toka ndani ya boksi Godson akatoa mkebe mdogo halafu akaufungua na ndani yake kulikuwa na mkufu wa thamani kubwa.Akamvisha Patricia shingoni.Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Patricia kuvaa shingoni mkufu wa gharama kubwa namna ile.Kwa furaha akageuka na kusema

“ Ahsante sana Godson kwa mkufu huu mzuri.Nimeupenda sana” akasema Patricia huku uso wake ukionyesha furaha isiyoeleza.Godson akamvuta karibu yake zaidi halafu akampiga busu moja zito linalomfanya Patricia aweweseke.Ilikuwa ni mara yake ya kwanza kupigwa busu na mwanaume.Mwili wote ukamsisimka.Mid

omo yake ikabaki inacheza akashindwa kuongea akabaki anamtazama Godson.Taratibu Godson akaushusha mkono wake wa kulia akivipitisha vidole vyake kati katiya utiwa mgongo hadi sehemu za kiunoni.Patricia akastuka na kutoa mguno Alihisi kama macho yake yanaanza kuona giza.Alisikia raha ya ajabu

“G..go…gods…on” akaita kwa taabu Patricia huku akihema kwa kasi na mara akashikwa sehemu Fulani ambayo inamfanya asikie raha isiyoelezeka.Ak

alegea kabisa Ilikuwa ni mara yake ya kwanza kusikia raha ya namna ile.Godson akamuinua na kumuweka kitandani

“ God..gods..on…N ..Dont…..” akasema Patricia kwa sauti dhaifu lakini Godson tayari alikwishapandwa na midadi akaendeleza autundu katika mwili wa Patricia ambaye aliendelea kutoa miguno ya kusikia raha.Godson alimfanyia Patricia kila aina ya utundu na kumpagawisha vilivyo.Baada ya kuona Patricia hajiwezi tena,Godson taratibu akaanza kufungua vifungo vya blausi ya Patricia na akahisi kuchanganyikiwa baada ya kukishuhudia kifua cha Patricia kilichobeba matiti madogo yaliyosimama.Mwili ulizidi kuchemka kwa ashki,akainama na kuyabusu matiti yale ambayo hayakuwahi kuguswa na mwanaume yeyote hapo kabla.Akayabusu na kuanza kuyachezea.Patricia aliendelea kutoa miguno kila pale alipoguswa.Tara

tibu Godson akafungua zipu ya sketi aliyokuwa ameivaa Patricia na kuivua.Patricia akabakiwa na nguo ya ndani pekee.Godson akazidi kuchanganyikiwa alipoushuhudia mwili ule mwororo .Akausogeza mkono na kuishika ile nguo ya ndani na alipotaka kuivua Patrcia akamshika mkono .

“God..Godson..No….” akasema Patricia huku akiibana miguu yale.Godson akamsogelea halafu akatoa ulimi na kuuingiza sikini mwa Patricia kwa ufundi sana.Patricia akatoa ukelele.Godson akaendelea kuuzungusha ulimi wake ndani ya sikio la Patricia na taratibu akamwambia

“ Usiogope mpenzi wangu.Ninakupenda na hautaumia”

“ Godson akaendelea kuuchezesha ulimi sikioni mwa Patricia na wakati huo huo kwa kutumia mkono wake wa kulia akaishika ile ngupo ya ndani ya Patricia akaivua.Baada ya kuhakikisha kwamba Patricia ameandaliwa vya kutosha Godson akavua nguo zake na kubaki mtupu.Uume wake ulikuwa umesimama wima tayari kwa shughuli.Akachukua chupa ya mafuta laini na kuupaka ili asimuumize Patricia .Akapanda kitandani na kumuweka Patricia katika mkao mzuri na kisha akamuingiza rasmi katika ulimwengu wa mapenzi.Patricia alitoa ukelele na miguno.Alikuwa ameondolewa bikira yake .

“ Ouh gosh ! I cant believe this.Patricia..!! Ouh my angel,I love you…I love you so much” akasema Godson akiwa juu ya mwili wa Patricia akiendelea na utundu .

Baada ya kufika mshindo,Godson akajitupa pembeni ya Patricia

“ Ouh gosh,Ive never met a sweet girl like you Patricia” akasema Godson huku akimbusu Patricia ambaye machozi yalikuwa yanamtoka.Godson akamfuta kwa mikono yake.

“ Nyamaza kulia Patricia.Usilie mpenzi wangu” Godson akambembeleza Patricia ambaye bado aliendelea kulia.Godson akainuka na kwenda kuchukua kitambaa akamfuta machozi

“ Usilie Patricia.Usilie mpenzi wangu” akasema Godson huku akimbusu Patricia shavuni

“Godson kwa nini umenifanyia hivi? Akauliza Patrcia huku akilia

“ Shhhhh..!!!!!...Patricia tafadhali usikasirike.Huu ni mwanzo mzuri wa mapenzi yetu.”

“ Godson tulikubaliana kwamba hatutafanya mapenzi hadi nitakapomaliza masomo yangu.Kwa nini umevunja ahadi yako na kunilaghai hadi tukafanya ?

“ Nisamehe Patricia.Nisamehe mpenzi wangu.Ni kweli hatukukubaliana hivi na hata mimi sielewi imetokeaje tukajikuta tukifanya”

Akasema Godson na Patricia akazidi kutoa machozi

“ Umenitoa bikira yangu ambayo ilikuwa ni zawadi kwa manaume wangu wa kwanza nitakayempenda ambaye ningemtunzia hadi tutakapofunga ndoa.Kwa sasa sintakuwa na thamani tena kwako” akasemaPatricia na kuendelea kuangusha machozi

“Tafadhali usiseme hivyo Patricia.Hujui ni kwa kiasi gani ninakupenda malaika wangu.Wewe ndiye kila kitu kwangu ,nakupeda zaidi ya ninavyoweza kukueleza.Usiwe na hofu yoyote kuhusu mimi” akasema Godson

“ Godson nimekuwa na mashaka kama kweli unanipenda kwa dhati au lengo lako lilikuwa kunitumia kimwili kwa tamaa zako.Kama unanipenda kwa namna ambayo umekuwa ukiniambia kila siku basi usingenishawishi tukafanya mapenzi.” Akasema Patricia na kukaa kitandani na mara akastuka baada ya kukumbuka kitu Fulani

“ Gosh..!!! haukutumia hata kinga.” Akasema Patricia kwa ukali huku akimpiga Godson makofi mgongoni.

“ Patricia i’m sorry lakini hakuna tatizo.Ninajiamini na sina matatizo yoyote” akasema Godson .Patricia akainama na kulia

“ I’m so stupid..How could I be so stupid .Kwa nini nimemuacha Godson akanifanyia hivi? akalia kwa uchungu Patrcia.Godson akamtazama na kusema

“ Patricia inuka ukaoge ujiweke vizuri.Wanaweza wakaanza kututafuta akina Juliana” akasema Godson

Patricia alishikwa na hasira kiasi cha kushindwa kuongea tena.Akainuka kitandani akajitazama na kuitazama damu kidogo iliyokuwa katika shuka jeupe lililotundikwa kitandani .Akazidi kuumia

“ Gosh ! Ameniondolea usichana wangu.Nimejitunza kwa miaka hii yote lakini leo hii nimenaswa kama ndege aliyeloa.I’m so stupid” akawaza Patricia huku akivaa nguo zake

“ Bafu lile pale Patricia,hutaki kuoga? Akauliza Godson.Patricia akamuangalia kwa jicho kali sana halafu akaufungua mlango na kutoka.Moja kwa moja akaelekea chumbani kwa Juliana akajitazama katika kioo na kulia sana

“I’m so stupid” hili ndilo neno alilobaki akilisema.Akaufungua mlango wa bafuni na kuingia kuoga.Bado picha ya tukio zima lililotokea ikaendelea kumjia kichwani.

“ Patricia msichana ambaye ninaheshimika sana kwa uwezo wangu mkubwa darasani lakini leo hi nimenasa mtegoni.I’m so fool.I’m so stupid.How could I let that bastard do that to me? Tena hakutumia hata kinga.Vipi kama akiniambukiza magonjwa hatari ya zinaa? Ouh gosh how could I be so stupid? Kibaya zaidi ninaweza hata kupata mimba” Mwili wote ukamsisimka pale wazo la kupewa mimba lilipomjia kichwani.

“ Help me God mambo haya yasinitokee.Juhudi zangu zote za miaka hii yote za kujitunza,na kujituma kusoma vyote vitakuwa kazi bure.Ndoto zangu zote za maisha zitapotea.” Patricia akasema taratibu halafu akamaliza kuoga akavaa nguo zake.Wakati akiwa katika meza ya vipodozi mara mlango ukafunguliwa akaingia Juliana.Akastuka baada ya kumkuta Patricia mle chumbani

“ Patricia uko huku?

“ Ndiyo dada Juliana.Nilisikia joto kali nikaona nije huku kuoga.Mbona umeloana hivyo?

‘Kuna rafiki zangu wamechelewa wamefika muda si mrefu ndio walioniogesha shampeni.” Akasema Juliana huku akilivua ganuni lake zuri na kuvaa lingine halafu akaongozana na Patricia kuelekea bustanini kuendelea na sherehe.

Sherehe ziliendelea hadi ilipotimu saa saba za usiku.Wageni wakaondoka zao.Baadhi ya wageni ambao hawakujisikia kuondoka usiku ule wakapewa nafasi ya kulala katika vyumba vya wageni kwani jumba lile lilikuwa kubwa na vyumba vingi vya kulala.Mama yake Patricia yeye alipewa chumba chake maalum cha kulala halafu Patricia yeye akaenda kulala chumbani kwa Juliana

“Ouh thank God sherehe imekwisha.Patri

cia nashukuru sana kwa msaada wako mkubwa katika kuifanikisha sherehe hii ambayo imependeza sana” akasema Juliana wakati wakijiandaa kulala

“ Ouh Dada Juliana please don’t mention.Sijafanya chochote kulinganisha na wema wako kwangu.” Akasema Patricia

“ Ninafurahi sana kufahamiana nanyi.Japokuwa wazazi wangu wako mbali lakini kuwa karibu na mama yako ninajiona ni kama vile niko na wazazi wangu” akasema Juliana .Patricia hakujibu kitu akatabasamu.Juliana akamsogelea akamtazama Patricia usoni halafu akasema

“ Patricia I’ve noticed you’ve changed suddenly.Umekuwa mkimya na hata uso wako umebadilika kitu ambacho si kawaida yako.What happened? Kuna kitu kimakukwaza mdogo wangu? Are you not happy here? Akauliza Juliana .Patricia akashindwa kujizuia kutoa machozi .Juliana akazidi kuwa na wasi wasi

“ Patricia are you ok? Akauliza

“ I’m ok”

“ Mbona unalia? What happened? Kitu gani kinakuliza?

“Sina atizo lolote dada Juliana.I’m just too emotional today.Kila nikikumbuka mambo yote ambayo umenifanyia toka tumefahamiana nashindwa kujizuia kutokwa na machozi.You are very kind” akasema Patricia.Juliana akamkumbatia halafu akamuomba Patricia alale apumzike

“ Patricia ananidanganya.Something is worng with her.Kitu gani kinachomsumbua na kumtoa machozi? Anyway nitatafuta nafasi niongee naye vizuri ili anieleze kitu gani kinachomkwaza.Kwa sasa ngoja apumzike amefanya kazi kubwa sana siku ya leo” akawaza Juliana







Ulikuwani usku mrefu mno kwa Patricia.Ilimchukua muda mrefu upata usingizi kutokana na mawazo mengi aliyokuwa nayo.

Hatimaye kulipambazuika na baada ya shughuli za usafi kumalizika Patricia na mama yake wakaanza kujiandaa ili warejee nyumbani kwao.Kabla hawajaondoka Patricia akamuita Juliana chumbani kwake halafu akatoa mkufu wa dhahabu mfukoni na kumpatia

“Dada Juliana naomba umpatie Godson mkufu huu.Alinipatia kama zawadi lakini siwezi kuuvaa” akasema Patricia.Juliana akamuangalia na kusema

“ Patricia tell me what happened? Godson amefanya kitu chochote cha kukukwaza?Tell me please” akasema Juliana

“ Hapana dada Juliana.Hajanifanyia jambo lolote baya isipokuwa alinipatia mkufu huu ambao una thamni kubwa tofauti na mimi.Sina thamani ya mkufu huu wa gharama kubwa” akasema Patricia na kuzidi kumshangaza Juliana

“ Patricia wewe ni mdogo wangu.Please be honest with me.Did you and Godson had a fight? Godson aliniambia kwamba umemkubalia muwe wapenzi sasa nashangaa nini kimteokea?

Patricia akavuta machozi na kusema

“ Ni kweli tulikuwa wapenzi but not anymore.” Akasema Patricia

“ Patricia mbona hutaki kunieleza nini kimetokea? Godson amekufanya nini?

Patricia akainama akakosa neno la kusema .Akainua kichwa na kusema

“ Dada Juliana thank you for everything.I have to go” akasema Patricia ,akageuka akafungua mlango na kutoka.Juliana alibaki anashangaa .Akachukua funguo ya gari na kuwarudisha Patricia na mama yake nyumbani.Garini Patricia alikuwa mkimya sana.Kichwa chake kilikuwa na mawazo mengi sana

“ I’m so stupid.Ilikuaje nimruhusu Godson anivue nguo na kunifanyia vile.? I’m so weak and stupid.Nilimepnda sana Godson lakini kwa sasa simtaki tena kwa kushindwa kuyaheshimu mapatano yetu ambayo tulikubaliana kwamba hatutafanya mapenzi hadi pale nitakapokuwa nimemaliza masomo yangu.Lakini amenishawishi hadi tukafanya mapenzi.It was my first ime and I didnt know what to do.Sitaki tena kusikia suala la mahusiano.Sitaki tena kusikia suala la mapenzi.From today,I erase Godson from my heart and evey fibre of my body” akawaza Patricia akiwa garini

Kwa siku zote zilizofuata Patricia hakuwa akitoka numbani.Alikuwa mkimya sana na muda mwingi aliutumia kujisomea.Hakuw

asiliana tena na Godson na hakutaka tena kuonana naye licha ya Godson kujitahidi kumtafuta kwa juhudi zote ili waongee kuweka sawa mambo

**************************************

Hatimaye likizo ikamalizika shule zikafuguliwa .Safari hii Patricia alikwenda shule kwa basi.Hakutaka kupelekwa tena na Juliana kwani alitaka kujizoesha kusafiri mwenyewe.Vile alitaka kuanza kupunguza mahusiano na akina Godson taratibu.

Ilikuwa ni furaha kubwa kwa Elvis kuonana tena na Patricia.Urafiki wao ukaendelea kama kawaida.

Ilikuwa ni siku ya Jumatano ya wiki ya pili toka walipofungua shule Patricia alisikia kizungu zungu akiwa darasani hivyo ikamlazimu kuondoka na kurejea bwenini ambako alikunywa dawa za kutuliza maumivu na kulala.Siku hiyo yote alishinda kitandani na hakuwa na hamu ya kula kitu chochote

Jioni ya siku hiyo alienda kuonana na Elvis bustanini ili kumtoa wasiwasi kuhusiana na hali yake.Elvis akamchukua na kumpeleka hadi katika mgahawa wa shule ambako huuzwa vyakula mbali mbali akamnunulia sahani moja ya chipsi pamoja na kuku wa kukaanga

“ Patricia siku nyingine usirudie tena kushinda bila kula chakula.Masomo ni magumu sana kwa hiyo unaposhinda bila kula chochote lazima utasikia hiyo hali ya kizungu zungu.Kwa sasa punguza muda wa kusoma hadi hapo hali yako itakapokuwa nzuri tena” akasema Elvis.

“ Elvis sikufanya makusudi kushinda bila kula chochote siku ya leo lakini sikuwa nikijisikia kula kitu chochote kile.Mchana wote nilikuwa najisikia vibaya sana lakini usijali kwa sasa najisikia vizuri .Nadhani hali hii ni kutokana na kusoma sana” akasema Patricia

“ Patricia pamoja na hayo lakini nakushauri pia kwamba kuna ulazima wa kupima na kujua kama unasumbuliwa na maralia.Toka tulipofungua shule nakuona kama umebadilika sana.Umekuwa mtu wa kulala s……” kabla hajamalizia sentensi yake Paticia akainama chni na kutapika.Elvis akaogopa

“ Patricia unaumwa twende nikupeleke katika zahanati ya shule usiku huu huu” akasema Elvis

“ Hapana Elvis.Ngoja kwanza nikalale kwa sababu kuna dawa tayari nimekwisha tumia.Kesho asubuhi kama bado hali yangu haitakuwa nzuri basi nitakwenda zahanati kupima.”

“ Hapana Patricia.Hali yako si nzuri na siko tayari kukuacha ukalale ukiwa katika hali hiyo. Ninakufahamu kwa muda mrefu na sijawahi kukuona ukitapika toka tumefika hapa shuleni” akasema Elvis

“ Nadhani ni kwa sababu ya hii harufu ya kuku” akasema Patricia na kumfanya Elvis ashangae

“ Harufu ya kuku? Mbona tumekuwa tukila kuku hapa shuleni mara kwa mara na hata mara moja haujawahi kuniambia kwamba unadhurika na harufu ya kuku? Akauliza Elvis

“ Hili tatizo nimenza kuliona baada ya kufungua shule.Kuna baadhi ya vyakula ambavyo hapo awali nilikuwa nakula bila matatizo lakini kwa sasa vimeanza kunishinda kabisa na kimojawapo ni kuku wa kukaanga.”

Elvis akamtazama Patricia kwa makini kama kwamba kuna kitu anakisoma usoni kwa Patricia

“ Ouh my gosh ! This cant be..” akanong’ona

“ Nini Elvis? Mbona unaongea mwenyewe? Akauliza Patricia.Elvis akamsogelea akamshika mkono akamuangalia usoni

“ Patricia ! akaita

“ Nini Elvis? Mbona unaniangalia namna hiyo hadi ninaogopa?

“ Usiogope Patricia.Mimi na wewe ni marafiki na tumekuwa tukishirikiana katika kila jambo.Tunalia na kucheka pamoja.Ugonjwa wako ni ugonjwa wangu pia.Binafsi ninakuamini kuliko hata mama yangu mzazi na ninaweza kukueleza kila kitu .Kuna kitu nataka kukuuliza Patricia na ninakuomba uwe muwazi kwangu.Just this once be honest with me Patricia” akasema Elvis

“ Elvis kuna nini? Patricia akauliza

“Ulikutana n a Godson wakati ukiwa likizo?

“ Ndiyo nilikutana naye japo si mara nyingi kwa sababu kwa sasa anafanya kazi katika kampuni ya simu kwa hiyo muda wake ni mchache sana na mimi mwenyewe nilikuwa nimebanwa na kazi nyingi”

“ Katika siku hizo chache mlizokutana mliwahi kufanya mapenzi?

“ What ?! Patricia akastuka

“ Nauliza mliwahi kufanya mapenzi ?

Patricia akainama akajawa na mawazo.Machozi yakaanza kumtoka

“ Ouh my gosh ! you did it” akasema Elvis kwa sauti ndogo.Patricia akaendelea kulia

“ Elvis yes we did it”akasema Patricia huku akifuta machozi.Elvis akashika kichwa kwa mikono yake alihisi miguu yake inaisha nguvu.

“ Patricia mlitumia kinga wakati wa kufanya mapenzi?

Swali lile likamfanya Patricia azidi kutoa machozi na kushindwa kujibu

“ Answer me Patricia….” Akasema Elvis huku naye machozi yakianza kumlenga

“ I’m so stupid Elvis.Hatukutumia kinga.Sielewi ni kwa nini nilijikuta nikikubali kufanya mapenzi na Godson na kusahau kabisa habari ya kinga”

“ Ouh gosh Patricia how could you do that?

“ I’m so fool Elvis” akasema Patricia na kuzidi kulia

“ Nyamaza kulia Patricia lakini naomba niwe muwazi kwako kwamba ulifany a kosa kubwa sana.”

“ What are you trying to say Elvis” akauliza Patricia

“ Patricia wewe ni rafiki yangu mkubwa na siwezi kukufica kitu.Inawezekana ukawa mjamzito”

“ What?!..That cant happen..” Patricia akahamaki

“ Inawezekana Patricia kama mlifanya mapenzi bila kutumia kinga.

“ Ouh Mungu wangu..nitafanya nini mimi kama ni kweli nina mimba? Please help me God” akasema Patricia na kuhisi miguu yake inaisha nguvu akakilaza kichwa chake mezani.Alilia machozi mengi sana.Elvis ambaye alihisi kuchanganyikiwa akamshika begani na kumuinua kichwa.

“ Patricia usilie tafadhali.Bado hatuna uhakika kama ni kweli.Hizi ni hisia tu lakini kuna ulazima wa kufanya vipimo na kubaini kama ni kweli au si kweli na kama ni kweli tujue namna ya kufanya” akashauri Elvis

“ I’m finished Elvis.I’m finished if it’s true.” Akasema Patricia

“Usihofu PatriciaKesho nitaongea na Thadei Yule dereva wa shule na atakwenda kutuletea kipimo cha kupimia ujauzito na baada ya kupima tutapata jibu.Kwa sasa naomba uende ukapumzike” akasema Elvis na kumshika mkono Patricia akamuongoza kuelekea bwenini .





Elvis nimechanganyikiwa.Sielewi nitafanya nini kama ni kweli nina mimba.” Akasema Patricia huku akilia

“ Patricia tafadhali nyamaza.Hizi ni hisia tu na bado hatuna uhakika kama ni jambo la kweli.Kesho baada ya kufanya kipimo tutabaini ukweli wa jambo hili lakini kwa sasa nakuomba usiwaze sana..” akaema Elvis

“ Sina hakika kama nitaweza hata kuupata usingizi Elvis.Nimestushwa sana na jambo hili.Kama ni kweli ina maana juhudi zangu zote nilizozifanya kwa miaka hii yote zitakuwa zimeishia hapa? Ndoto zangu zote zitapotea kwa starehe ya dakika kumi tu? Ouh gosh !.” akasema Patricia kwa uchungu

“ Patricia naomba futa hayo mawazo.Hata kama ikiwa ni kweli lakini hautakuwa ndio mwisho wa ndoto zako.Naomba nenda kapumzike na tafadhali usiwaze sana kuhusu suala hili” akasema Elvis

Bila kuongea kitu ,Patricia akainuka na kuanza kuelekea bwenini.Elvis akamsindikiza hadi karibu na bweni

“ Patricia mimi naishia hapa,lakini naomba usiwaze chochote kuhusiana na suala hili.Tutapata majibu yote kesho” akasema Elvis na bila kuongea kitu Patricia akatembea kwa unyonge kuingia bwenini kwao.Elvis akabaki amesimama akimtazama

“ Ouh Patricia kwa nini ulikubali kudanganyika na ukafanya mapenzi yasiyo salama?Kwa nini unataka kupoteza ndoto zako zote ?Kwa nini unataka kuyaharibu maisha yako? Akasema Elvis kwa sauti ndogo huku akielekea bwenini kwao.

Baada ya kuingia chumbani kwake Patricia akajitupa kitandani na kuendelea kulia.

“ Nina hakika lazima nitakuwa mjamzito.Nimeanza kuona mabadiliko makubwa katika mwili wangu toka nilipofanya mapenzi na Godson.Masikini mimi ,nimekwisha sasa.Sijui nitauficha wapi uso wangu kwa aibu hii kubwa” akawaza Patricia

“ Nitamwambia nini mama ? Najua akisikia kama mimi ni mjamzito anaweza akaanguka na kufariki hapo hapo kwa mstuko atakaoupata.Ana matumaini makubwa na mimi na endapo akisikia kuhusu suala hili sielewi nini kitatokea.” Akaendelea kuwaza

Machozi mengi yakaendelea kumtoka alichanganyikiwa hakujua afanye nini.Kwa upande wake Elvis baada ya kuachana na Patricia akaelekea moja kwa moja chumbani kwake huku naye akiwa na mawazo mengi.Suala la Patricia kuwa mjamzito lilimstua sana

“ Patricia how could you do that?Kwa nini umeyachezea maisha yako namna hii? Kwa nini unataka juhudi zako zote zipotee bure?Nimeumia sana.Umeniumiza mno kwa sababu ninakupenda na siku zote ndoto yangu ni kukuona unafika mbali na kufanikiwa katika maisha yako na kuiondoa familia yako katika lindi la umasikini lakini kama ni kweli utakuwa mjamzito kuna wasi wasi ndoto hizi zisitimie.Kweli nimeamini ule msemo usemao when it comes to love,smart people are idiots.” Akawaza Elvis

“ Pamoja na chochote kitakachotokea lakini siwezi kumuacha Patricia peke yake.Yuko katika wakati mgumu sana na anahitaji mno msaada wangu.She’ll never walk alone.Nitasimama pamoja naye katika hili” akasema Elvis huku akijtupa kitandani.

*******************************

“ Saa saba za mchana siku iliyofuata dereva wa shule akarejea na kumpatia Elvis kipimo cha kupimia ujauzito alichokuwa amemuomba amnunulie.Baada ya kukipokea kipimo kile akakiangalia na kuvuta pumzi ndefu .Muda wa mapumziko ya mchana ulipomalizika na wanafunzi wakarejea madarasani Elvis alibaki chumbani kwake amekaa akitafakari halafu akainuka na kuchungulia nje.Eneo lote lilikuwa kimya kabisa wanafunzi wote walikuwa madarasani.Elvis akatoka mle bwenini kwao na kuelekea katika bweni la akina Patricia ambaye hakuingia darasani siku hiyo

Elvis alikwenda kwa tahadhari kubwa ili asijeonwa kwani ni kosa kwa mwanafunzi wa kume kuonekana katika maeneo ya bweni la wasichana bila sababu ya msingi.Baada ya kufanikiwa kuingia mle bwenini moja kwa moja akaelekea katika chumba cha akina Patricia akagonga mlango mara tatu lakini hakujibiwa akaamua kinyonga kitasa na kuufungua mlango taratibu.Patricia alikuwa amelala kitandani ,aliposikia mlango ukifunguliwa akainua kichwa ili aangalie ni nani aliyekuwa ameingia mle chumbani akastuka baada ya kukutana na Elvis.

“Elvis !..akasema Patricia na kuinuka akakaa kitandani

“What are you doing here? Akauliza Patricia

“ Patricia nimekuja kukutazama.Unae

ndeleaje?

“ Elvis huruhusiwi kuonekana maeneo haya na endapo ukikutwa humu chumbani sote wawili tunaweza kupewa adhabu” Akasema Patricia kwa woga halafu akainuka na kwenda kuufunga mlango kwa funguo

“ Usijali kuhusu hilo Patricia .Vipi maendeleo yako?

“ Ah ! hivyo hivyo tu.Bado najisiki a vibaya sana.Nafikiria niende zahanati nikapime niangalie kama nina maralia.” Akasema Patricia ambaye macho yake yalikuwa yamemvimba

“ Pole sana Patricia.Nim…..” kabla hajamalizia alichotaka kukisema zikasikika hatua za mtu

“ Kuna mtu anakuja huku” akasema Elvis na mara mlango wa chumba cha akina Patricia ukagongwa

“ Patricia !!..Ikaita sauti toka nje

“ Ouh my gosh .Ni Matron!! Akanong’ona Patricia.

“ Tutafanya nini? Akauliza Elvis

“ Jifiche chini ya kitanda” akasema Patricia na kwa haraka Elvis akaingia chini ya kitanda.Patricia akaenda kuufungua mlango na kukutana na mwalimu mlezi wao.

“ Patricia kwa nini unafunga mlango na funguo?Milango hii haitakiwi kufungwa na funguo” akasema mwalimu Anastela Kipisa

“ Samahani mwalimu sintafanya hivyo tena”

“ Unaendeleaje? Akauliza mwalimu Anna

“ Bado sijisikii vizuri na ninataka niende zahanati nikapime maralia.”

“ Ok vizuri.Ukisha pima tumia dawa utakazopewa na kama hali itaendelea kuwa mbaya zaidi tutaelekea hospitali ya wilaya kesho kwa vipimo zaidi” akasema malimu Anna

“ Sawa mwalimu” akasema Patrica

“ Ok endelea kupumzika na endapo hali itabadilika nitumie taarifa mara moja.Baadae nitamtuma mpishi akuletee chakula.Unapenda kula chakula gani leo wakuandalie?

“ Chakula chochote tu mwalimu nitakula” akasema Patricia na mwalimu Anna akaondoka.Baada ya kuhakikisha kwamba amaeondoka kabisa maeneo yale ya bwenini Patricia akamwambia Elvis atoke uvunguni

“ Elvis hii ni hatari sana.Ungekutwa humu chumbani tungekuwa katika matatizo makubwa.Tafadhali naomba usije tena huku chumbani.Kama ni kuonana tutakuwa tukionana bustanini kama tulivyozoea” akasema Patricia

“ Usihofu kuhusu hilo Patricia.Nimeku

letea kile kipimo.” Akasema Elvis na kutoa kile kipimo akampatia Patricia ambaye alikitazama na kushusha pumzi

“ Help me God ! ,akasema Patricia.Elvis akamuangalia na kusema

“ Weka mkojo katika chombo kikavu halafu ingiza hicho kipimo na kama una ujauzito basi kitaonyesha.

“ I’m so scared Elvis” akasema Patricia

“ Usiogope Patricia.Be strong” akasema Elvis.Patricia akainuka na kuelekea chooni.Akachukua kopo kavu na kukojolea ndani yake halafu akakifungua kile kipimo .Mikono ilikuwa inamtetemeka.Mapigo ya moyo yalikuwa yanamuenda kwa kasi kubwa.

“ Please help me God” akasema Patricia na taratibu akaanza kukiingiza kile kipimo katika kopo lenye mkojo halafu akakitoa.Mwili ukamuisha nguvu alipokitazama ,akajikuta akikaa chini

“ Nimekwisha sasa.I’m totally finished.I’m pregnant.” Akasema Patricia.Alishindwa kulia.Akakiangalia tena kile kipimo halafu akaushika ukuta na kurejea tena chumbani.

“Majibu yanasemaje Patricia? Akauliza Elvis lakini Patricia midomo ilikuwa mizito kufunguka.Akamtupia Elvis kile kipimo ambaye alistuka sana

“ My gosh ! .” akasema Elvis na kukaa kitandani

“ what are we going to do Patricia?

Patricia akainua kichwa akataka kusema neno lakini sauti haikutoka.Elvis akainuka na kuegemea kabati.

“ Elvis ndoto zangu zote za maisha zimekomea hapa” akasema Patricia

“ Usiseme hivyo Patricia.Bado ni mapema sana kukata tamaa.There must be a way”

“ Elvis hakuna namna nyingine nitakayoweza kukwepa jambo hili lisijulikane.Likifika kwa uongozi wa shule lazima nifukuzwe shule.Sina hakika nini kitatokea endapo mama akisikia kwamba nimepata mimba.Ana matumaini makubwa sana na mimi na siku zote amekuwa akinionya kuhusu kujitumbukiza katika mahusiano akiogopa suala hili hili la kupata mimba.” Akasema Patricia.

“ Kusema ukweli Patricia hata mimi suala hili limenichanganya sana.Bado najiuliza ni kwa nini ulifanya vile?

“ Elvis I’m so stupid.Ididnt think what will happen.I wasn’t thinking clearly.I’m so fool”

“ Usijilaumu sana Patricia.Kinachotakiwa kwa sasa ni kutafuta namna ya kufanya kulishughulikia suala hili”

“ Elvis nimekwisha fikiri hadi akili yangu imefika mwisho wa uwezo wake wa kufikiri lakini bado sijapata jibu namna ninavyoweza kulitatua tatizo hili”

Elvis akavuta pumzi ndefu na kusema

“Huyo boyfriend wako umewasiliana naye na umempa taarifa hizi?

“ Sina mawasilianao naye kwa sasa.Nilipogundua kwamba lengo lake lilikuwa ni kunichezea tu na hakuwa na mapenzi ya kweli nami nimekata mawasiliano naye.”

Elvis akamtazama Patricia na kumwambia

“ Inabidi afahamishwe kuhusu jambo hili kwani yeye ndiye muhusika mkuu”

“ Elvis I’m so scared kwa sababu sijui nitaanzaje kumueleza” akasema Patricia.Elvis akamsogelea karibu na kumwambia

“ Patricia huu si wakati wa kuogopa au kumuonea mtu aibu.Kama hukumuogopa wala kumuonea aibu na ukakubali kumvulia nguo kwa nini basi uogope kumweleza matokeo ya kile mlichokifanya?Usiogope.Leo jioni tukutane bustanini nitakupa simu yangu utawasiliana naye”

Kimya kikatanda wakatazamana

“ Patricia kwa sasa pumzika tutaonana jioni.Tafadhali usimweleze mtu yeyote suala hili kwa sasa” akasema Elvis halafu akainuka na kutoka.Alipofika mlangoni Patricia akamuita

“ Elvis !

Elvis akageuka

“ Naomba samahani kwa kukuingiza katika matatizo haya”

“ Usijali Patricia.Rafiki wa kweli siku zote huyabeba matatizo ya mwenzake kama ya kwake na husimama na rafikiye hata katika nyakati zile ngumu kabisa.Endelea kupumzika ila usisahau jioni tukutane bustanini.” Akasema Elvis na kutoka.Baada ya Elvis kutoka Patricia akajitupa kitandani

“ Siamini kama maisha yangu yanakwena kuharibika namna hii.Kitendo cha dakika chache kimeharibu kabisa muelekeo mzima wa maisha yangu.Juhudi zangu zote nilizozifanya kwa miaka hii yote za kuyatengeneza maisha yangu zimenifikisha hapa.Mama yangu amejitolea sana katika kunifikisha hapa nilipofika itakuaje akizipata taarifa hizi? Yote haya yamesababishwa na Godson kwani ndiye aliyenishawishi tukafanya mapenzi.I hate that Bastard.Yeye ndiye aliyeyaharibu maisha yangu” akawaza Patricia

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



Godson kwani ndiye aliyenishawishi tukafanya mapenzi.I hate that Bastard.Yeye ndiye aliyeyaharibu maisha yangu” akawaza Patricia Kichwa cha Patricia kilijaa mawazo mengi hali ilIyosababisha kianze kuuma na kumlazimu kumeza dawa za kutuliza maumivu.Akaitupia macho meza ya kusomea iliyopo mle chumbani iliyosheheni vitabu vingi “ Hapana siwezi kukubali maisha yangu yaharibike kirahisi namna hii.Kitu pekee cha kufanya kwa sasa ni kuitoa hii mimba angali bado mapema ili niweze kuendelea na masomo yangu bila matatizo.I’ve worked so hard and I cant end up here.Godson anatakiwa anisaidie katika zoezi hili la kuitoa mimba hii” akawaza Patricia “ Najua ni njia hatari na ni dhambi kubwa kufanya hivi lakini sina namna nyingine lazima niitoe hii mimba” akawaza Patricia ************************** Saa moja za jioni wakati wanafunzi wakiwa katika bwalo la chakula wakipata mlo wa jioni,Patricia na Elvis walikutana bustanini mahala ambako wamekuwa wakikutana mara nyingi “ Umeshindaje Patricia? “ Hivyo hivyo Elvis.” “ Ulijitahidi kula chakula walau kidogo? “ Ndiyo nilijitahidi” Ok Good.Usiwe na mawazo mengi sana tutapata muafaka wa suala hili” “ Elvis nimefikiria sana na muafaka pekee niuonao mimi ni kuitoa hii mimba” akasema Patricia na kumstua Elvis “ Patricia ..!!! “ Ndiyo Elvis.Hiyo ni njia peke iliyopo kwa sasa.Vinginevyo itanilazimu nikatishe masomo na kurejea nyumbani kuilea mimba hii,kitu ambacho siwezi kukubali kitokee.” Akasema Patricia “ Patricia naomba unisikilize vizuri.Usifanye maamuzi ya haraka haraka namna hii.Hili si suala la kufanyia maamuzi ya haraka.Tuliza akili na tulitafutie suluhisho lenye kufaa na si kufikiria kwenda kuitoa hii mimba” akasema Elvis “ Elvis,naomba ufahamu kwamba tunaongelea kuhusu maisha yangu na siko tayari kuona maisha yangu yakiharibika kwa sababu ya hii mimba.Potelea mbali lazima nikaitoe tu” akasema Patricia “ Patricia mimi sikubaliani na wazo hilo hata kidogo.Ni jambo la hatari na linaloweza kukusababishia matatizo makubwa” “ I don’t care Elvis.Kitakachotokea na kitokee tu lakini siko tayari kuona maisha yangu yakiharibika.Niko tayari kukabiliana na lolote lile” akasema Patricia Elvis akamuangalia Patricia akakosa neno la kusema.Msimamo wake haukuonekana kutetereka.Alikwisha dhamiria kuitoa ile mimba “ Naomba simu niwasiliane na Godson” akasema Patricia.Elvis akampatia simu,akaandika namba za Godson na kupiga.Simu Ikaanza kuita “ Hallow “ ikasema sauti ya upande wa pili ambayo Patricia aliitambua ilikuwa ya Godson “Hallow Godson,Patricia hapa ninaongea” “ Ouh Patricia my angel,how are you? How’ve u been?I’ve been dying t o hear from you again .Why are you doing this to me my love? Why are you avoding me? Nakupenda sana Patricia Nakupenda sana.Patr…….” “ Godon !!...” Patricia akasema na kumkatisha Godson ambaye alikuwa akiongea mfululizo “ Godson nimekupigia simu si kwa ajili ya ya kuongelea mambo yaliyopita.Kuna matatizo yametokea” “ Matatizo gani Patricia.Niambie una matatizo gani nikusaidie? Sitaki kukuona mtoto mzuri kama wewe ukiwa katik matatizo” Patricia akavuta pumzi ndefu na kusema “Godson I’m pregnant” “ What ?! Pregnant?!... Godson akastuka “Ndiyo.Nina ujauzito” akasema Patricia halafu kikapita kimya kifupi.Godson akasikika akivuta pumzi ndefu “Godson umenisikia nilichokwambia? Akauliza Patrcia “ Patricia nimekusikia lakini ninachotaka kufahamu ni nani muhusika wa hiyo mimba? “ Godson hakuna haja ya kuanzisha mjadala wakati ukweli unaufahamu wewe mwenyewe.Mimba hii ni ya kwako” akasema Patricia “ Patricia unanichanganya sana.Inawezekanaje? Nitaaminije kama hiyo mimba ni ya kwangu? “ Godson mambo gani haya unayonieleza? Unataka kusema nini? Patricia umenichanganya sana.Ni vigumu kuamini kama mimba hiyo unayoisema ni yangu kweli .Nitaaminije kama hukuwa na wanaume wengine huko shuleni? Huku akifuta machozi Patricia akasema “ Godson sitaki malumbanonawe.Nimekueleza ukweli kwa sababu wewe ndiye mwanaume wangu wa kwanza na sijawahi kuwa na mwanaume mwingine zaidi yako.Sasa naomba unisikilize vizuri.Nina kila ushahidi wa kuthibitisha kwamba wewe ndiye mwenye hii mimba na endapo utajaribu kuleta ujeuri wako nitakuwa tayari kuharibu masomo yangu lakini wakati huo na wewe utakuwa unatumikia kifungo gerezani.Viongozi wengi wa serikali wananifahamu kwa hiyo suala hili litakapofika kwao litashughulikiwa kwa uzito mkubwa sana.I will destroy you Godson” akasema Patricia kwa ukali huku machozi yakimtoka “ Patricia calm down .Naomba tusifike huko unakotaka tufike.Samahani kama nimeongea neno baya lakini ni kutokaana mstuko nilioupata.Sikuwa nimezitegemea taarifa hizi .Naomba tuongee suala hili kwa utulivu na tufikie muafaka” “ Sihitaji muafaka nawe wowote Godson.Ninachotaka kukwambia ni kwamba ninaitoa hii mimba kwani siko tayari kukatisha masomoyangu .Siwezi kukubali juhudi zangu zote zipotee kwa ajili ya mtu kama wewe.Ninachotaka nitumie pesa za kwenda kuitoa hii mimba haraka sana kabla haijajulikana kwa uongozi wa shule” akasema Patricia na kimya kikatanda “ Godson umenisikia? Nimekuelewa Patricia .Hilo ni wazo zuri sana kwani hata mimi siko tayari kwa majukumu yoyote ya kulea mtoto kwa sasa na vile vile siko tayari kuanza kuvutana na vyombo vya sheria kwa kosa la kumpa mimba mwanafunzi.Kwa maana hiyo basi kesho asubuhi nitaanza safari ya kuja Tanga.Nitafanya mipango ya kutoa mimba hiyo na baada ya kufanikisha nitakuja Bumbuli kukuchukua na tulimalize suala hili.Umenielewa Patricia? “ Nimekuelewa.Tafadhali fanya haraka kwani nina wasi wasi suala hili linaweza likagunduliwa na walimu halafu yakawa mambo mengine” “ Usihofu Patricia.Kesho kutwa nitashughulikia mambo yote na kisha nitakufuata shuleni.Kwa sasa kuwa kimya na usimueleze mtu yeyote kuhusu suala hili.It’s just me and you” Ok Godson ukifanikisha utawasiliana nami kwa kutumia namba hii ya simu ili nami nifanye mpango wa ruhusa” “ Nitafanya hivyo Patricia.Narudia tena kukukumbusha katika siku mbili hizi jitahidi kila kitu kiwe kimekamilika” akasema Godson .Patrcia akakata simu “ I hate you Godson.I hate you so much.Kwa sababu yako ninafanya mambo ambayo sikuwahi kufikiria kuyafanya.Godson you are a monster” akasema Patricia baada ya kukata simu “ It’s ok Patricia.Usiumie sana” akasema Elvis “ Elvis I’m so tupid.I’m so fool.Akasema Patricia.Elvis akamtazama na kusema “ Patricia are you sure you want to do this? Patricia akafuta machozi na kusema “ Do you have another alternative Elvis? Elvis akakaa kimya “ Elvis ninafanya hivi kwa sababu sina namna nyingine ya kufanya Siwezi kukubali maisha yangu yaharibike kirahisi namna hii.Naona huafikiani nami katika suala hili .Kama kuna njia mbadala naomba unieleze lakini kama huna niache nifanye ninavyoona ni muhimu kwangu.Hata nikisema nilee mimba na nizae mtoto how wili I feed the baby? Elvis thank you for your concern but for this matter let me stand alone.” Akasema Patricia na kuinuka akaelekea bwenini.Elvis naye akakosa neno la kusema na kumuacha aende zake ********************* Ni saa sita za mchana ,Patricia na Godson wamo katika chumba cha kupumzika wagonjwa wa dharura ambamo Patricia aliwekwa apumzike baada ya zoezi la kumtoa mimba kukamilika. “ Pole sana Patricia” akasema Godson.Patriciaaliyekuwa amelala kitandani akamtazama na kusema “ Ahsante Godson kwa kunisaidia suala hili limekwisha” “ Usijali Patricia” akasema Godson “ One more thing..” akasema Patricia “ Tutakapoachana hapa me and you we’re finished.Naomba tusijuane tena.Nimenusurika kuyaharibu maisha yangu na sitaki tena kufanya mchezo .Nakushukuru kwa kunionyesha upendo kwa kipindi kifupi tulichokuwa pamoja” akasema Patricia huku akikunja uso kwa maumivu aliyokuwa akisikia “ Patricia nakushukuru kwa kuwa muwazi .Nimeyapokea maamuzi yako na ninayaheshimu.Utanisamehe sana Patricia kwa jambo hili lililotokea ambalo nusura liharibu kabisa masomo yako.Baada ya mambo haya kutokea hata mimi kuna jambo ninataka kukwambia.Nimeamua kwenda nchini Afrika ya kusini.Ninaenda kufanya kazi katika ile kampuni niliyokwambia wakati ule.Itanichuka muda mrefu kuonana nawe tena lakini dunia hii ni ndogo kama kijiji kwa hiyo tunaweza kuonana tena muda wowote.Pamoja na yote yaliyotokea kuna jambo moja nataka kukuomba” “ Jambo gani ? “ Ninaomba tuendelee kuwa marafiki badala ya kuwamaadui.Nitakapofika afrika kusini nitamuomba Juliana akupatie mawasiliano yangu na tuendelee kuwasiliana .Muda wowote utakaokuwa na hamu ya kuongea nami au ukiwa na tatizo lolote usisite kuwasiliana nami.Nitakusaidia “ akasema Godson .Patricia hakujibu kitu Saa nane za mchana,Patricia akaruhusiwa kutoka .Akapewa dawa za kutumia kwa muda wa siku saba.Wakaingia katika gari alilokuja nalo Godson na safari ya kurejea shuleni ikaanza.Ilikuwa ni safari ya kimya kimya.Maongezi yalikuwa machache sana Baada ya kuwasili shuleni,Patricia na Godson wakaagana.Godson akamuachia kiasi cha shilingi laki tano kwa ajili ya matumizi na kisha akaondoka zake.Patricia akaelekea moja kwa moja bwenini kulala.Alikuwa amechoka sana Siku iliyofuata Patricia aliingia darasani alikuwa akijisikia vizuri.Elvis alifurahi kumuona tena msichana ampendaye.Baada ya chakula cha mchana tumbo likaanza tena kumsumbua Patricia hivyo ikamlazimu kwenda bwenini kulala. Kwa muda wa siku nane mfululizo Patricia aliendelea kuwa kitandani akisumbuliwa na tumbo.Alipata matibabu katika zahanati ya shule lakini hakuweza kupata nafuu hali iliyowalazimu uongozi wa shule kuamua kumpelea Tanga mjini katika hospitali kubwa kwa ajli ya uchunguzi zaidi wa kubaini ni kitu gani kilihokuwa kikimsumbua.Mchana wa siku iliyotangulia siku ailiyopangwa Patricia apelekwe Tanga mjini kwa uchunguzi,Elvis na Patricia wakakutana wakati wa chakula “ Elvis nina wasi wasi sana na Yule daktari aliyenitoa mimba nawezekana kuna kitu alikosea kwa sababu maumivu ninayoyasika ni makubwa sana.Kuna nyakati ninahsi kama ninataka kufa” akasema Patricia “ Patricia pole sana.Hii ndiyo sababu iliyonifanya nisikubaliane na kitendo cha kwenda kuitoa mimba ile.Kuna binamu yangu aliwahi kupoteza maisha akiwa katika harakati za kutoa mimba.KItendo kile bado kinanuma mpaka leo na ndiyo maana niko kinyume kabisa na suala hilo” akasema Elvis “Lakini Elvis sikuwa na namna nyingine ya kufanya zaidi ya kuitoa.Nina wasi wasi endapo nitapelekwa hospitali kwa uchunguzi nitabainika kwamba nilitoa mimba na hii inaweza ikaniletea matatizo pia” akasema Patricia What are we going to do then ? akauliza Elvis “ Sijui nitafana nini.NImechanaganyikiw ana sielewi la kufanya” akasema Patrica .Elvs akainama akafikiri na kusema “ Patricia kuna kitu nakifikiria” “ Kitu gani hicho? “ Ni kweli endapo utapalekwa hospitali ya mkoa kwa uchunguzi itabainika kwamba umetoa mimba.Ninafikiria kwamba kabla ya jambo hili halijafika hatua hiyo basi tumueleze mwalimu Anna” “ Elvis !!! Patricia akastuka “ Najua ni jambo gumu kueleza ukweli lakini itakuwa vyema endapo ataufahamu ukweli kabla ya uchunguzi kufanyika” “ No Elvis..I cant do that” akasema Patricia halafu akainama na kugugumia kwa maumivu makali ya tumbo Patricia naomba uelewe kwamba mwalimu Anna ni mwelewa sana na endapo atalifahamu suala hili kabla ya kwenda hospitali anaweza akatafuta njia nzuri ya kukusaidia ili jambo hili lisijulikane” akasema Elvis na kuzidi kumchanganya Patricia “ Elvis unayoyasema ni ya kweli .Toka nimeanza kuumwa mwalimu Anna amekuwa akinitembelea kila siku na kunijulia hali.Anawapenda wanafunzi na nina hakika anaweza akanielewa lakin tatizo ni namna ya kuanza kumueleza kuhusu usala hli hadi anielewe” “ Sikliza Patricia.mwalimu Anna ni mama.Naye pia ana watoto na mambo ama haya anayafahamu.Niachie mimi ndiye nitakayeongea naye.Nitamfuata nyumbani kwake leo jioni na kuongea naye.Nina hakika atanielewa” akasema Elvis na baada ya mongezi kidogo Patricia akakubali kwamba Elvis aende akaonane na mwalimu Anna Saa moja za jioni wakati wa chakula cha jioni Elvis akachepuka na kuelekea nyumbani kwa mwalimu Anna ambaye anaishi katika moja ya nyumba za shule.Aligonga mlango wa mbele ukafunguliwa na mtoto mdogo wa kike wa mwalimu Anna ambaye alimkaribisha ndani na kwenda kumuita mama yake aliyekuwa jikoni akiandaa chakula cha usiku “ Ouh Elvis ! Karibu” akasema mwalimu Anna baada ya kuingia sebuleni na kumkuta Elvis.Mwalimu Anna alikuwa mkarimu sana na alipendwa na wanafunzi wote “ Pole na masomo Elvis” akaanzisha maongezi mwalimu Anna Ahsante sana mwalimu” akajibu Elvis halafu kikapita kimya kifupi “ Elvis ulisema una tatizo unataka kunieleza? “ Ndiyo mwalimu Anna.Kuna jambo nataka kukueleza lakini si kuhusu mimi bali Patricia” “ Patricia ?! “ Ndiyo mwalimu” “ Patricia ana tatizo gani? Kwanini asinieleze yeye mwenyewe wakati mimi ndiye mlezi wao? “ Ni kweli mwalimu Anna.Yeye mwenyewe ndiye aliyepaswa kukueleza kuhusu matatizo yake lakini kwa hali aliyonayo imekuwa vigumu kufanya hivyo na ndiyo maana nimekuja mimi badala yake.Mimi na Patricia ni marafiki wakubwa .Tunaishi kama ndugu kwa hiyo nitakachokueleza mimi ni sawa na ambacho angekueleza Patricia” akasema Elvis Haya nieleze ni tatizo gani alilo nalo Patricia” Elvis akashusha pumzi na kusema “ Mwalimu Anna naomba tuongee kama mtoto na mzazi wake na si kama mwanafunzi na mwalimu” “ Elvis mbona unanipa wasi wasi? Mna matatizo gani nyie vijana? “ Mwalimu Anna unamfahamu vizuri Patricia.Ni mwanafunzi mwenye akili ya kiwango cha juu sana na ni mtu mwenye kujituma na mwenye msimamo usiotetereka.Patricia anatoka katika familia duni .Baba yake alifariki muda mrefu hivyo kwa miaka mingi Patricia amekuwa akilelewa na mama yake .Hilo ni jambo ambalo limemfanya awe ni mtu mwenye ndoto nyingi sana na anyejituma ili kuzitimiza na moja ya ndoto yake kubwa ni kuiondoa familia yake katika hali duni iliyonayo” akasema Elvis halafu akanyamaza akanywa funda moja la soda aliyowekewa mezani na kuendelea “ mwalimu Anna kama walivyo wasichana wengine wa rika la Patricia na wenye uzuri kama wa kwake,Patricia naye amekuwa akisumbuliwa na wanaume wenye kumtaka kimapenzi.Amekuwa akikumbana na vishawishi vingi na amekuwa na msimamo imara lakini kwa bahati mbaya alijikuta akitetereka kidogo baada ya kujikuta akimpenda kijana mmoja aitwaye Godson.Ilikuwa ni mara yake ya kwanza kuingia mapenzini.Wakati wa likizo huyo rafiki yake wa kiume akamualika katika sherehe ya kuzaliwa dada yake na hapo ndipo akamshawishi Patricia wakafanya mapenzi.Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Patricia kufanya mapenzi.Kwa bahati mbaya Patricia na huyo rafikiye walifanya mapenzi yasiyo salama na kwa bahati mbaya Patricia akashika mimba” “ Jesus Christ ..Mwalimu Anna akastuka.Alimtazama Elvis kana kwamba ameona kitu cha kutisha.Elvis hakujali mstuko ule wa mwalimu Anna akaendelea “ Baada ya kugundua kwamba ni mjamzito hakuwa na njia nyingine ya kufanya zaidi ya kuitoa hiyo mimba ili aweze kuendelea na masomo.Mara tu alipofanya zoezi hilo ndipo tumbo lilipoanza kumsumbua hadi hivi leo” “ Ouh Mungu wangu !! akasema mwalimu Anna na kuendelea kumkazia macho Elvis “ Elvis nimekosa neno la kusema.Haya yote unayonieleza ni ya kweli? ...







ukweli mtu mwalimu.Hauna mtu mwingine anayefahamu suala hili hapa shuleni zaidi yangu” “ Jesus Christ !!..Patricia !!!..bado siamini kama anaweza kweli akafanya jambo kama hili” “ Naomba uniamini mwalimu Anna” “ Kwa nini alikimbilia kwenda kuitoa hiyo mimba bila hata kuja kuniuona na kuniomba ushauri? Siku zote nimekuwa mlezi wao.Nimejishusha na kuwa kama rafiki yao ili wakiwa na tatizo lolote wasisite kunieleza kwa nini hakunifuata akanieleza tatizo lake nimsaidie ? “ Mwalimu Anna suala hili ni gumu na alikuwa amechanganyikiwa kwa hiyo akaona njia pekee ya kufanya ni kwenda kuitoa” “ Ulifahamu kila kitu kwa nini basi na wewe hukuja kunieleza hadi umesubiri hali imekuwa mbaya? “ Mwalimu ,hili ni suala linalomuhusu mtu na siwezi kufanya lolote bila ruhusa yake” “C’mon Elvis,she’s your friend and you need to be there for her.What’s the meaning of friendship if you cant help each other in times like this? Akauliza mwalimu Anna.Elvis akashindwa kujibu “Hiyo mimba aliitolea wapi? “Alikwenda kutolea Tanga mjini.Mimi sikuambatana naye.Huyo rafikiye aliyempa ujauzito ndiye aliyekuja kumchukua na kumpeleka kwenda kuitoa hiyo mimba” “Nyie watoto mnafanya mambo ya hatari sana.Hili si suala la kufanyia mchezo hata kidogo.Ni suala zito sana.Inaonekana mimba hiyo alitolewa vichochoroni na mtu ambaye si mtaalamu .Kama ni hivyo inabidi aende akasafishwe upya vinginevyo anaweza akapoteza maisha.Ouh jamani mambo gani haya yanamtokea mwanafunzi ninayempenda? Akasema mwalimu Anna “ Mwalimu Anna ndiyo maana nimekuja hapa kukuomba utafute namna yakumsaidia Patricia ili aweze kusafishwa na pili suala hili lisifike kwa uongozi wa shule .Wewe ndiye mama unayetulea hapa shuleni tukiwa na matatizo kama haya wewe ndiye kimbilio letu.Naomba ulichukue suala hili kama mama na umsaidie Patricia aweze kupona na aendelee na masomo yake .Bila msaada wako hali yake itakuwa mbaya na tunaweza tukampoteza” akasema Elvis “ Elvis umeichanganya sana na sijui nifanye nini.Patricia ni mwanafunzi ninayempenda mno na siku zote ndoto yangu ni kuona akitimiza ndoto zake.Ouh jamani Patricia” akasema mwalimu Anna na kuvuta pumzi ndefu.Akainama akafikiri na kusema “ Elvis suala hili ni gumu na siwezi kutoa jibu la moja kwa moja ni namna gani nitaweza kumsaidia Patricia.Kesho nitampeleka hospitali na kule atafanyiwa uchunguzi ili kubaini ni jambo gani linalomsumbua.Baada ya uchunguzi wa madaktari ndipo tutajua ni namna gani ya kumsaidia” “ Hapondipo penye tatizo mwalimu Anna.Endapo atapimwa na ikagundulika kwamba ametoa mimba taarifa hii inaweza kumletea matatizo kwa uongozi wa shule na familia yake pia.Mwalimu Ana suala hili halitakiwi kufika kwa uongozi wa shule au mtu mwingine .Nimekuja hapa kukuomba kama mama tafadhali msaidie Patricia ili aweze kupona na aendelee na masomo yake” “ Elvis kama nilivyosema siwezi kutoa jibu la moja kwa moja kuhusu namna gani nitaweza kumsaidia Patricia.Naomba uniache kwa usiku huu nitafakari nini nitafanya.Kesho asubuhi tayari nitakuwa na jibu.Hata mimi ninampenda Patricia na nitafanya kila niwezalo kumsaidia . Mama yake amekuwa akinipigia simu mara kwa mara na kuniuliza maendeleo ya mwanae,ana matumaini makubwa sana na mwanae huyu wa pekee.Kama mama nitamsaidia wmanamke mwenzangu ili mwanae aweze kupona” akasema mwalimu Anna “Mwalim Anna kuna ambo lingine nataka kukuomba” “ Jambo gani Elvis? “ Ninaomba kesho utakapompeleka Patricia hospitali ,niambatane nawe” Usijali kuhusu hilo.kama uko tayari tutakwenda sote” “ Ahsante sana mwalimu Anna na samahani kwa taarifa hizi nilizokuletea ambazo najua zimekustua sana lakini wewe ndiye mama yetu mlezi hapa shuleni kwa hiyo tunapokuwa na matatzio wewe ndiye mtu pekee tunayeweza kukukimbilia” “ Ahsante kwa Elvis kwa taarifa hizi.Umefanya jambo la maana sana kuja kunieleza lakini ulipaswa kunieleza mapema ili nione namna gani ya kumsaidia.Ningejua mapema yasingefika hapa yalipofika” akasema mwalimu Ana na Elvis akaondoka “ Watoto hawa kwa nini wanafanya mambo ya hatari namna hii kuhatarisha maisha yao?Bado siamini kama Patricia mtoto mwenye bidii kubwa na akili ya ajabu anataka kuyaharibu maisha yake.Itanilazimu nifanye kila niwezalo ili kumsaidia.Kama asiposaidiwa kila alichokifanyia kazi kwa miaka hiyo yote kitapotea” akawaza mwalimu Anna halafu akaifungua bahasha aliyopewa na Steve na kukuta bunda la noti nyekundu akastuka “ Hizi za nini tena?akajiuliza huku akizihesabu fedha zile. “ Elvis hakupaswa kunipa fedha hizi ili nimsaidie Patricia.Hata bila ya fedha nilazima nimsaidie Patricia lakini kwa vile amenipa mwenyewe siwezi kuzikataa” akawaza walimu Anna halafu akatoka na kuelekea katika bweni la wasichana kuangalia maendeleo ya Patricia.. ******************** Uso wa mwalimu Anna ulionyesha mstuko mkubwa wakati akitoa katika chumba cha daktari mkuu wa hospitali ya mkoa ambako Patricia alipelekwa kwa ajiliya kufanyiwa uchunguzi.Alionekna kuchanganyikiwa.Elvis ambaye alikuwa nje akimsubiri akashangazwa na hali ile ya mwalimu Anna akamsogelea “ Mwalimu Anna daktari anasemaje? Vipimo vinasemaje? Akauliza Elvis.Mwalimu Anna hakusema kitu akamshika Elvis mkono na kuelekea katika benchi la kupumzikia wakakaa “ Elvis nimechangnyikiwa na sijui nifanye nini” “ Kwa nini mwalimu Anna? Daktari anasemaje? “ Elvis tatizo ni kubwa sana tofauti na tulivyokuwa tukifikiria” “ Daktari anasemaje? Vipimo vinaonyeshaje? “ Elvis nimetetemeka sana kwa taarifa ya daktari” Niambie mwalimu Anna.Daktari anasemaje? Patricia na tatizo gani? “ Tatizo la Patricia ni kubwa.Imegundulika kwamba daktari aliyemtoa mimba hakumsafisha vizuri hivyo kupelekea kizazi chake kuoza” “ Ouh Mungu wangu..!!....Elvis akastuka na kuweka mikono yake kichwani “ Kwa hiyo daktari anasemaje?Watamsafisha upya? “ Suluhisho pekee hapa la kuyanusuru maisha ya Patricia ni kumfanyia upasuaji na kuondoa kizazi” “ What ?! …Patricia atolewe kizazi? Ina maana hatakuwa na uwezo wa kupata mtoto katika maisha yake yote? “ Ndiyo Elvis.Kama akiondolewa kizazi basi hatakuwa na uwezo wa kupata mtoto katika maisha yake yote yaliyobaki” Ouh Masikini Patricia.kwa nini yanamtokea haya? Ndoto yake nyingine kubwa ni siku moja kuwa na familia.Kama akitolewa kizazi ndoto hii haitatimia.Jamani Patricia ataishi vipi? Akawaza Elvis na kumgeukia mwalimu Anna aliyekuwa ameinama akitafakari “ Mwalimu Anna hakuna njia nyingine ya kuweza kumsaidia Patricia zaidi ya kuondoa kizazi? Akauliza Elvis “ Hakuna Elvis.Hakuna njia nyingine ya kumsaidia Patricia.Kwa mujibu wa daktari ni kwamba hali yake si nzuri na inatakiwa afanyiwe upasuaji huo haraka iwezekanavyo.” “ Tutafanya nini basi mwalimu Anna? Wewe umaeamua nini? “ Patricia atalazwa hapa hospitali.Taratibu zinafanyika ili aweze kupelekwa wodini .Suala la upasuaji itabidi lisubiri kwanza hadi mzazi wake na uongozi wa shule ufahamishwe.Hili ni suala kubwa na kwa ngazi iliyofikia sasa inabidi wazazi na uongozi wa shule wafahamu” akasema mwalimu Anna “Mwalimu Anna hatuwezi kuendelea kulifanya jambo hili kuwa siri? Nina wasi wasi mkubwa endapo taarifa hizi zitamfikia mama yake na uongozi wa shule” akasema Elvis “ Elvis hili ni suala zito na linalohusisha uhai wa wanafunzi ambaye mimi ndiye mlezi wake kwa hiyo jukumu langu ni kutoa taarifa sahihi kwa wazazi na walimu.Endapo nitaficha juu ya ugonjwa wa Patricia na baadae ikagundulika kwamba nilisema uongo nitajiweka katika matatizo makubwa.Wewe unataka tufanye nini Elvis? Akauliza mwalimu Anna ninachotaka ni kuendelea kulifanya suala hli liendelee kuwa siri.Ongea na daktari na aandike tatizo lingine kabisa ili kumuepusha Patricia na matatizo mengine.Mama yake hatakiwi kujua chochote” “ Elvis hilo ni suala gumu kwa sasa.Kwanza sina hakika kama daktari atakubali ,pili hata kama akikubali nani ambaye atamuuguza Patricia hapa hospitali? Patricia atafanyiwa upasuaji mkubwa kwa hiyo anahitajika mtu wa karibu wa kumuuguza hadi hapo atakapopona.Kazi hii anatakiwa kufanya mtu wake wa karibu “ Usiogope kuhusu hilo mwalimu Anna.Hapa Tanga mjini ninaye binamu yangu moja anafanya kazi katika benki ya NMB.Ni mtu ambaye ninaelewana naye sana kwani amekulia nyumbani kwetu.Endapo nitaongea naye nina hakika lazima atakubali kumsaidia Patricia kwa sababu kwa hivi sasa yuko likizo kwa hiyo atakuwa na nafasi nzuri ya kumuhudumia .Kuhusu daktari usiwe na shaka wale tutaongea nao kwa pesa tu” “ Hapana Elvis usifanye hivyo,.Naomba usitumie pesa yoyote tafadhali.Pesa uliyompa jana inatosha kabisa” “ Usijali mwalimu Anna,pesa ile ya kwako .Nisubiri dakika mbili niende hapo nyuma” akasema Elvis na kutoka mbio kueleka katika ATM ilikuwa pale hospitali akachukua fedha kiasi cha shilingi laki tatu na kurejea akamkabidhi mwalimu Anna “ Elvis kwa nini unafanya haya yote? “kwa sababu Patricia ni rafiki yangu na nilimuahidi kwamba nitakuwa naye katika nyakati zote,lazima nitimize ahadi yangu.Muda unakwenda mwalimu Anna nenda kaonane na daktari ili tujue atatusaidiaje.Mimi nawasiliana na binamu yangu nimfahamishe kuhusu sula hili” akasema Elvis mwalimu Anna akainuka na kuelekea ofisini kwa daktari.Elvis akachukua simu na kumpigia binamu yake Scola “ hallow Elvis habari ya shule?Nimepanga nije wiki hii kukusalimia hapo shguleni nikuletee na zawazi zako” akasema Scola baada ya kupokea simu “ Habari nzuri Scola.Nimekuja mjini leo.Niko hapa hospitali ya mkoa” “ Uko hospitali? Kuna nini? Unaumwa? Akauliza Scola “ Hapana siumwi Scola,ni rafiki yangu ndiye anayeumwa.Uko wapi hivi sasa? “ Niko Saluni natengeneza kucha” “ Unaweza kuja hapa hospitali? Kuna tatizo gani? “ Siwezi kukueleza katika simu.Naomba uje sasa hivi hapa hospitali” akasema Elvis “ Ok nakuja sasa hivi.Umeniogopesha sana Elvis” akasema Scola na kukata simu “ Elvis akaenda kukaa katika bench lililokuwa nje ya ofisi ya daktari.Baada ya kama dakika ishirini muuguzi akaja na kitanda cha magurudumu na kuingia nacho ofisini kwa daktari na baada ya muda akatoka akikisukuma kitanda kile ambacho juu yake alikuwa amelala Patricia.Daktari pamoja na mwalimu Anna nao wakatoka ,mwalimu Anna akamuomba Elvis waongozane kuelekea wodini ambako Patricia akapewa kitanda.Wakati akiwa nje ya wodi,simu yake ikaita ,alikuwa ni Scola,akamuelekeza amfuate katika wodi Elvis kuna nini? Mbona uko huku? Unaumwa? Akauliza Scola ambaye alikuwa na sura iliyojaa wasiwasi.Elvis akamvuta pembeni na kumueleza kila kitu kuhusiana na matatizo ya Patricia “ Ouh my gosh ! anaendeleaje? Akauliza Scola kwa wasi wasi “ hali yake si nzuri” akasema Elvis na mara mwalmu Anna akatoka mle wodini.Elvis akamtambulisha kwa Scola wakasalimiana “ mwalimu Anna daktari amesemaje? Akauliza Elvis “ Amepokea ule mzigo na amekubali kutusaidia.Kutokana na hali ya Patricia kuendelea kuwa mbaya usiku wa leo itabidi afanyiwe upasuaji. Kwa maana hiyo itanilazimu nisirejee shuleni leo ili niendele kufuatilia sula hili” akasema mwalimu Anna na wote wakabaki kimya Napatwa na wasi wasi sana mtoto wa watu kufanyiwa upasuaji mkubwa namna hii bila ya mzazi wake kufahamishwa.”akasema mwalimu Anna “ Usihofu wmalimu Anna.Patricia mwenyewe hataki mama yake afahamu kuhusu suala hili.” “Kwa hivi sasa Patricia yuko katika maumivu makali na hana uwezo wa kufanya maamuzi yoyote kuhsu suala hili” akasema mwalimu Anna “ Kama ni hivyo basi sisi ndio tunapaswa kubeba jukumu lote.Tunatakiwa tuwe majasiri na tukubaliane na chochote kitakachotokea” akasema Scola MIEZI MITATU BAADAE Miezi mitatu imekwisha pita toka Patricia afanyiwe upasuaji na tayari amekwisha pona na kurejea masomoni.Hali yae ilikuwa nzuri na hakuna aliyefahamu chochote kuhusiana na kilichokuwa kinamsumbua na kusababisha afanyiwe upasuaji.Ilibaki ni siri yao pekee yeye Patricia,Elvis , mwalimu Anna na Scola binamu yake Elvis ambaye alifanya kazi kubwa sana ya kumuuguza Patricia wakati alipofanyiwa upasuaji. Japokuwa alikuwa anaendelea vizuri na masomo yake lakini kuna jambo moja kubwa ambalo lilikuwa linamtesa sana.Ni suala la kutoweza kupata mtoto tena katika maisha yake yaliyobakia.Elvis ambye aliifahamu siri hii alijitahidi sana kumpa moyo na kumfariji Siku zilikatika na hatimaye ukafika wakati wa kumaliza shule.Bado ukaribu wao ulikuwa mkubwa sana.Pale shuleni kila mtu alifahamu kwamba lazimaPatricia na Elvis wana mahusiano ya kimapenzi lakini ukweli ni kwamba walikuwa marafiki wa kawaida na hawakuwa wapenzi kama watu walivyodhani.Japokuwa Elvis aliendelea kumpenda Patricia kila uchao lakini alivuta subira ili kuacha kwanza kidonda cha Patricia kipone.Hakutaka kumuingiza tena kwa haraka katika mahusiano kwani siku zote katika maongezi yao Patricia aliweka wazi ni jinsi gani anavyoyachukia mapenzi.Aliweka wazi kwamba hatapenda tena kwani haoni umuhimu wa kuingia mapenzini na kuumizwa tena “ Yalikuwa ni makosa yangu hadi nikawa katia hali hii.Nastahili niubebe mzigo huu mimi mwenyewe” Hiyo ndiyo ilikuwa kauli ya kila mara ya Patricia wakiwa katika maongezi yenye kuhusisha mambo ya mahusiano. Elvis aliyaona mateso na machungu ya moyo aliyokuwa nayo Patricia kila alipofikiria kwamba hataweza kupata mtoto katika maisha yake yote,akaumuoea huruma sana.Patricia alizidi kumuingia moyoni na ndiye mwanamke pekee ambaye aliupeleka mbio moyo wake.Hakuwahi kutokea mwanamke aliyempenda kama alivyompenda Patricia na aliweka nadhiri ya kuhakikisha anafanikiwa kuwa naye maishani Jioni moja wakiwa wamekaa bustanini sehemu waliyopenda sana kukutana ,Patricia akamuuliza swali Elvis “ Elvis,kuna jambo limekuwa linanikwaza sana na kunishangaza” “ jambo gani Patricia? “ Toka nimekufahamu siku zote nimekuwa nikitegemea kwamba lengo lako kubwa ni kuwa mwana sayansi,daktari au mhandisi na sikutegemea hata simu moja kwamba unataka kusoma mambo hayo ya upelelezi unayotaka kwenda kuyasomea.Kwa nini usiwe daktari au hata rubani? Au kwa nini usiwe mhandisi?Mimi binafsi hainiingii akilini kwa mtu kama wewe kwenda kusomea mambo kama hayo sijui ya ujasusi sijui mnayaitaje..” akasema Patricia na kumfanya Elvis acheke kicheko kikubwa “ Patrcia si wewe peke yako unayeniuliza swali hili.Hivi sasa nina ugomvi na mama yangu kuhusiana na maamuzi yangu ya kutaka kujiunga na mafunzo ya usalama wa taifa.Ukweli ni kwamba nilipenda sana kufanya kazi hii toka nikiwa mtoto mdogo.Baba yangu alikuwa kanali wa jeshi kwa hiyo nilipenda sana mambo haya ya usalama na ndiyo maana ndoto yangu kubwa ni kuingia katika kazi hii ya ujasusi.Ninaipenda kazi hii toka moyoni na kuna baba yangu mdogo anayefanya kazi katika idara ya usalama wa taifa amekuwa ananipa moyo sana kwamba kama ninaipenda kazi hii basi atakuwa tayari kunisaidia” akasema Elvis “ Sikuzuii kuifanya kazi hiyo Elvis lakini sina hakika kama umefanya chaguo sahihi.Muonekano wako si mtu wa kufanya kazi kama hizo ambazo ni za hatari kubwa.” “ Usihofu Patricia.Ninaipenda kazi hii na ndiyo pekee ambayo ninataka kuifanya katika maisha yangu” akasema Elvis na kumfanya Patricia aendele kumtazama kwa macho makali. *********************** Hatimaye baada ya kumaliza masomo yao ya kidato cha sita Elvis na Patricia walifanikiwa kupata kazi ya muda katika hoteli ya kitalii wakati wakisubiri matokeo yao .Kwa sasa Elvis alikuwa akiishi jijini Dar es salaam katika nyumba yao iliyoko Mbezi.Urafiki baina yao uliendelea kuwa mkubwa na wakaribu zaidi hata baada ya kumaliza masomo. Ilikuwa ni siku ya ijumaa wote wawili wakiwa katika zamu ya usiku siku ambayo wageni walikuwa wachache sana hapo hotelini hivyo Patricia na Elvis wakapata wasaa wa kukaa pamoja na kuzungumza mambno yao ya maisha.Walienda kukaa katika viti vya kupumzikia pembeni ya bwawa la kuogelea.Siku hii Patricia alionekana kuwa na mawazo mengi “ Patricia unawaza nini? Akauliza Elvis bada ya kumuona Patricia yuko kimya na ameyaelekeza macho yake juu angani. “ Ninawaza mambo mengi sana.Nawaza kuhusu safari yangu ya maisha.Nafikiria ndoto zangu nyingi ambazo natakiwa nizitimize ,nyingine hazitawezekana tena lakini nitajitahidi niweze kutimiza asilimi 98 ya malengo yangu.” Akasema Patricia “ Patricia wewe ni mwanamke wa aina yake na usiyekubali kushindwa na jambo.Toka nimekufahamu nimejifunza mambo mengi kupitia kwako.Umenifundisha namna ya kupambana kufikia malengo ya maisha.Nimejifunza kupambana na changamoto zozote zinazojitokeza katika kuyakamilisha malengo binafsi.Nashukuru sana kwa elimu hii ya bila darasa”akasema Elvis .Patricia akatabasamu na kumshika mkono Elvis “ Elvis haya yote yamewezekana kwa sababu yako ya watu wenye mapenzi na mimi ukiwamo wewe.Huwezi kujua una nafasi gani kwangu.Wewe ndiye umekuwa kama malaika wangu mlinzi.Umekuwa nami hata katika nyakati zile ngumu ambazo hakuna mtu ambaye angeweza kuwa nami lakini wewe ulisimama pamoja nami,ulihuzunika nami,ukacheka na kufurahi nami.Kuna nyakati huwa ninajiuliza kwa nini unanifanyia haya yote? Ninajiuliza bila kupata jibu nitakulipa kitu gani kwa mambo haya makubwa uliyonifanyia.Nimekuwa nikitafuta siku nyingi nafasi ya kukuuliza ni kwa nini unanifanya haya? Why me? akauliza Patricia.Elvis akatabasamu halafu akakohoa kidogo na kusema Patricia may be its right time now to know the truth” “ Truth ?! What truth? Akauliza Patricia huku sura yake ikionyesha wasi wasi “ Itis the truth about me and my heart” akasema Elvis huku Patricia akimuangalia kwa wasiwasi.Elvis akameza mate na kusema “Patricia kwa muda mrefu nimekuwa nikitafuta nafasi kama hii ambayo nitakueleza kile kilichomo moyoni mwangu na kwa nini nimeyafanya haya yote niliyoyafanya.Sikuweza kukueleza mapema kutokana na na kukabiliwa na mambo mengi ya masomo na kimaisha” Elvis akatulia kidogo akamtazama Patricia halafu akaendelea “ Patricia ni ukweli huu nitakaokwambia ndio utakaoniweka huru toka kifungoni” Ni ukweli gani huo Elvis? Please tell me” akasema Patricia “ Patricia Mungu ametuumba na kutuweka duniani tufurahi na kuutukuza uumbaji wake na katika maisha haya ametupa kila mmoja na mtu wake ambaye ataambatana naye na kuwa mwili mmoja.Patricia moyo wangu umekuona wewe na kutua kwako kiasi ambacho hauwezi kubanduka tena.Ninakupenda Patricia kwa moyo wangu wote Nina hakika kwamba wewe ndiye mwanamke pekee katika dunia hii ambaye umeumbwa kwa ajili yangu.Nguvu ya pendo langu kwako ndiyo inayonifaya niweze kusimama nawe hata katika nyakati zile ngumu.Tafadhali Patricia naomba uufungue moyo wako na unikubalie niwe mpenzi wako” akasema Elvis.Patricia akabaki ameduwaa alikosa neno la kuongea.Walitazamana kwa dakika kadhaa kisha Patricia akasema “ Elvis nmekosa neno la kusema.Sijui nikujibu nini .” akasema Patricia na mara macho yake yakajaa machozi. “ Tafadhali usitoe machozi Patricia.Futa machozi halikuwa lengo langu kukukwaza.” akasema Elvis “ Hujanikwaza Elvis lakini nimepatwa na mstuko mkubwa sana kwa mtu kama wewe kunipenda mtu kama mimi.Siamini na haikuwahi kuniingia akilini hata siku moja kwamba utatokea kunipenda. Ahsante kwa kunipenda Elvis lakini nasikitika kwamba umeniambia ukweli wako kwa kuchelewa” “ Kwa nini unasema hivyo Patricia? “ Kwa sababu moyo wangu hauna hata chembe ya mapenzitena kwa mwanaume yeyote.Zaidi ya yote Elvis unahitaji kuwa na mwanamke mwenye mapenzi ya kweli nawe,ambaye anatoka katika familia bora kama yako ,mwanamke amb……..” akasema Patricia lakini Elvis akamkatisha “ Sikiliza Patricia,sihitaji mwanamke mwingine ,nakuhitaji wewe pekee.Siko tayari kuwa na mpenzi ambaye si wewe” akasema Elvis.Patricia akafuta machozi na kusema “ Elvis you were there beside me all the time and you know exactly what I went through.I don’t think I’m the right woman for you” Akasema Patricia.Elvis akatabasamu na kusema “ Patricia ni kwa sababu ya upendo wangu usiopimika kwako ndiyo maana niko nawe toka tulipofahamiana na ni kwa sababu ya upendo huo huo ndio maana niko nawe hapa sasa hivi









kwamba wewe ndiye mwanamke wa pekee ninayekupenda na ninayekutaka maishani mwangu.Patricia najua uliumizwa na mambo yale yaliyokupata wakati ule lakini naomba ufahamu kwamba mambo yote yaliyotokea si kigezo cha kunizuia mimi kukupenda wewe” “ Elvis ni ukweliulio wazi kwamba lengo la watu wawili kuingia katika mahusiano ni ili siku moja waishi pamoja na waanzishe familia.Mimi sina uwezo wa kupata mtoto katika maisha yangu yote yaliyobaki hapa duniani kwa hiyo sina thamani kwa mwanaume yeyote Yule katika dunia hii.Siku zote matarajio ya mwanaume kwa mke wake ni kumzalia watoto na kutengeneza familia iliyo bora,uwezo huo mimi sina tena na ndiyo maana suala la mahusiano nimekwisha lifuta katika akili yangu” akasema Patricia “ Patricia nakupenda wewe na kila ulicho nacho.Suala la kupata mtoto si suala ambalo linaweza kunifanya nishindwe kuwa nawe” akasema Elvis “ Elvis hili si suala dogo kama unavyodhani.Hili ni suala zito sana na linaloniumiza mno kila nikilifikiria.Sitaki mtu kama wewe uumizwe na makosa niliyoyafanya mimi.Elvis wewe ni mtu mwenye upendo wa ajabu sana ,you deserve someone better than me.Si haki hata kidogo ukaishi maisha yako bila kuwa na familia” “ Patricia maneno yako yanazidi kuniumza zaidi” akasema Elvis “ Samahani Elvis lakini huo ndio ukweli .I made a mistake once and I have to pay for my mistake for the rest of my life.I’m not that woman who can be loved by anyone.I’m valueless.Samahani kwa maneno haya lakini hivyo ndivyo ninajisikia mimi moyoni mwangu” akasema Patricia “ Patricia ninafahamu umeumizwa kwa kiasi kikubwa sana na ninayahisi pia maumivu yako.Tafadhali nipe nafasi ya kukuonyesha upendo wangu kwako,nipe nafasi ya kukufanya malkia wa ulimwengu wangu na kukufanya uwe mwanamke mwenye furaha kupita wote duniani.Nipe nafasi katika moyo wako.Nomba uufungue moyo wako na uuruhusu kupenda tena” Maneno yale yakaonekana kumuingia Patricia na kumfanya atoe machozi.Akamtazama Elvis na kusema “ Elvis ni bahati ilioje kupendwa na mwanaume kama wewe lakini nasikitika kwamba moyo wangu hauna hata chembe ya mapenzi ndani yake na itanichukua muda mrefu kupenda tena .I’m sorryElvis” akasema Patricia.Elvis akamtazama usoni na kusema “ Patricia haujawahi hata mara moja kuwa na hisia zozote juu yangu? Patrcia akainama akafikiri halafu akajibu “ No ! sijawahi kufikiria chochote kuhusu wewe kuhusiana na suala la mapenzi.Kwangu wewe ni rafiki yangu mkubwa sana kupita wote” akasema Patricia halafu akainama chini “ Patricia naomba unitazame usoni” akasema Elvis na Patricia akainua uso wake na kumtazama Elvis “ Nitazame machoni na uniambie kwamba hujawahi kuwa na hisia zozote juu yangu.Tell me the truth and I swear I’ll believe you” “ Ouh Elvis ……!! Patricia akashindwa kujizuia akainama na kuanza kulia.Elvis akambembeleza Elvis you don’t know how much I love you and I’ve been dreaming how happy I could be if you were my man.Nilipokutana nawe Dodoma kwa mara ya kwanza moyoni mwangu nilihisi kuna kitu kipo kati yetu lakini niliporudi Dar nikakutana na Godson nikajikuta nikimpenda na kuamini kwamba ndiye mwanaume wa maisha yangu.Baada ya kutengana naye taratibu ulianza kuniinga moyoni mwangu nikaanza kuvutiwa nawe na kukupenda lakini tayari nilikwisha chelewa.Tayari nilikwisha yaharibu maisha yangu.Nimekuwa nikipigana na moyo wangu ili usiendelee kukuwaza lakini kadiri siku zinavyozidi kwenda nimejikuta nikishindwa na hilo limekuwa linanitesa mno.Nakupenda Elvis.Nakupenda sana kiasi ambacho siwezi kukuelezea lakini ….” “ Lakini nini Patrica…?! Akauliza Elvis.Patricia akashindwa kuongea kitu akabaki anamtazama Elvis “ Patricia ahsante kwa kuwa muwazi kwangu.Ahsante kwa kunipenda.kwa mara ya kwanza katika maisha yangu ninajiona ni mtu wenye bahati sana kupendwa na mtu kama wewe” akasema Elvis na kumkumbatia Patricia. “ Patricia kwa kuwa sote tunapendana hakuna kitu kinachoweza kutuzuia mimi na we tusiwe wapenzi.Naomba tuwe wapenzi na hatimaye siku moja tuweze kufanikiwa kufunga ndoa kwani ndoto yangu kubwa ni kuwa nawe katika maisha yangu yote hadi kifo kitutenganishe.Nataka uwe malkia wa moyo wangu.Nataka nikufanye mwanamke mwenye furaha kubwa duniani” akasema Elvis.Patricia ambaye machozi yalikuwa yanamtoka akamtazama Elvis usoni na kusema “ Elvs najua unanipenda na sina shaka hata kidogo na upendo wako kwangu,lakini pamoja na kunipenda nadhani unafahamu fika kwamba mimi ni mwanamke ambaye siko kamili tena ,ina maana sina tena uwezo wa kuzaa jambo ambalo najua hata kama tukiwa wapenz litakuumiza sana.Ninapata mashaka ya kuingia tena katika mahusiano nikiwa katika hali hii kwa kuogopa kumuumiza mwenzangu na mimi mwenyewe kuumia pia. “ akasema Patricia “ Patricia I love you with all my heart .Nakupenda ulivyo.Ninayafahamu matatizo yako na niko tayari kuyabeba pamoja nawe.Hilo si suala ambalo linaweza kutufanya mimi nawe tusiwe pamoja na wala si suala linaloweza kutufanya tukakosa furaha.Tafadhali nikubali niwe wako Patricia.Niruhusu nikuonyeshe namna gani ninakupenda ewe malaika wangu” akasema Elvis.Patricia akashindwa kuwa na kigugumizi tena kwani alimpenda Elvis na ndoto yake ilikuwa ni siku moja yeye na Elvis wawe wapenzi lakini alikuwa akisita kila alipofikiria kwamba hakuwa tena na uwezo wa kuzaa jambo lililomfanya kukata tamaa kabisa ya siku moja kuwa na maisha ya furaha akiwa na mwanaume ampendaye. Ukurasa mpya ukafunguliwa kati ya Elvis na Patricia.Waliingia rasmi katika ulimwengu wa wapendanao MIAKA 13 BAADAE Miaka 13 imekwisha pita sasa toka Elvis na Patricia walipoufungua ukurasa wa mapenzi kati yao na kuwa wapenzi. mapenzi yao yalikuwa mazito na ya kutiliwa mfano.Walipendana kwa dhati ya mioyo yao Patricia alihitimu shahada yake ya kwanza ya udakatari katika chuo kikuu cha sayansi na tiba cha Muhimbili na baadae akaenda tena nchini Marekani kuendelea na masomo zaidi katika fani yake hii .Kwa sasa anafanya kazi katika hospitali kuu ya magonjwa ya fahamu. Elvis kwa upande wake alijiunga na jeshi la wananchi wa Tanzania kwa mafunzo ya kijeshi ya miaka mitatu na baadae akapelekwa na serikali kwa mafunzo ya http://deusdeditmahunda.blogspot.com/ujasusi katika chuo cha ujasusi cha CIA university nchini Marekani ambako alihitimu kwa kiwango cha juu na cha kushangaza sana.Baada ya kuhitimu mafuzo yake akarejea nchini na kujiunga rasmi na idara ya ujasusi ya taifa akiwa ni jasusi wa kiwango cha juu kabisa nchini.Alifurahi sana kuifanya kazi hii ambayo amekuwa akiota kuifanya toka akiwa mdogo Tayari Elvis na Patricia wamehitimisha ile ndoto yao kubwa na ya siku nyingi ya kuishi pamoja baada ya kufunga ndoa.Maisha yao yalijaa furaha na amani na waliendelea na kazi zao kama kawaida.Patricia akiwa ni daktari katika hospitali kuu ya magonjwa ya akili na vile vile alikuwa ni daktari aliyekuwa akimtibu mke wa rais aliyekuwa akisumbuliwa na tatizo la kupooza mwili upande mmoja na kwa msaada mkubwa wa Patricia hali yake imekuwa ikiendelea vizuri naviungo vyake vilivyokuwa vimepooza vimeanza kufanya kazi tena.Kila siku kabla ya kuelekea kazini kwake Patricia hupita kwanza ikulu kumjulia hali mgonjwa wake na kukagua maendelo yake kitendo kilichojenga ukaribu mkubwa sana kati yake na familia ya rais Siku ya kumbu kumbu ya miaka kumi na tisa toka alipofariki kanali Braison Tarimo baba mzazi wa Elvis iliwadia.Ndugu wengi ,marafiki na jamaa wa karibu walikutana katika ibada maalum inayofanyika kila mwaka kwa ajili ya kumuombea heri kanali Tarimo ili mwenyezi Mungu aweze kumrehemu.Baada ya kumalizika kwa ibada ya misa takatifu,ndugu wote wakaelekea katika makaburi alikozikwa kanali Tarimo ambako waliwasha mishumaa katikakaburi lake ishara ya kuendelea kumkumbuka Toka makaburini watu wote waliohudhuria kumbu kumbu hii wakiongozwa na mjane wa marehemu Bi Carmelita tarimo mama mzazi wa Elvis wakaelekea nyumbani kwa marehemu Mbezi kwa ajili ya kumalizia shughuli zilizobaki.Bi Carmelita kwa sasa amekwisha staafu kazi yake ya uuguzi aliyokuwa akiifanya jjini Arusha na kwa sasa anaishi jijini Dar es salaam katika nyumba yao iliyoko mbezi akiendela kuisimamia miradi mbali mbali iliyoachwa na marehemu mume wake. Nyumbani kwa marehemu kuliandaliwa chakula na vinywaji. Watu walikula na kunywa wakifurahia maisha aliyoyaishi kanali Tarimo hapa duniani.Wakati watu wakiendelea kula na kunywa huku wakikumbushana mambo mbalimbali ambayo kanali Tarimo amewahi kuyafanya katika enzi za uhai wake,Bi Carmelita akamuita mwanae Elvis wakaelekea bustanini “ Elvis nashukuru sana kwa kupata nafasi hii ya kukaa nawe leo.Ni muda mrefu hatujapata nafasi ya kukaa pamoja na kuongea kwa uhuru na nafasi kuhusiana na mambo yanayotuhusu” akasema Bi Carmelita “ Kweli mama ni muda mrefu hatujapata nafasi ya kukaa pamoja kama hivi na kuongea.Kazi yangu inanibana sana na ndiyo maana tunashindwa kuonana” “ Nalifahamu hilo Elvis lakini nashukuru kwa kuwa haujawahi kupitisha hata siku moja bila ya kunipigia simu kunijulia hali.Nashukuru sana kwa hilo” akasema Bi Carmelita na kumfanya Elvis atabasamu “ Mama usijali kuhusu kutokuniona.Kila nitakapokuwa nikipata muda nitakuwa nikija kukusalimu” “ Ahsante sana Elvis.Vipi maisha yako na mkeo yanaendeleaje? “ Tunashukuru Mungu tunaendelea vizuri sana mama.Hatuna tatizo lolote” “Nafurahi kusikia hivyo Elvis lakini kuna jambo mimi binafsi linaniumiza sana moyo wangu” “ Jambo gani mama? Akauliza Elvis “ Elvis mimi na baba yako tulikupata kwa taabu sana.Tulikwisha kata tamaa kabisa ya kupata mtoto maishani mwetu na ndipo tulipofanikiwa kukupata na baada yako hatukufanikiwa tena kupata mtoto mwingine na ndiyo maana unaona uko peke yako.Kama tungefanikwa kupata watoto zaidi hivi sasa mngekuwa hata zaidi ya kumi kwani baba yako alipenda sana kuwa na watoto wengi.” Akasema Bi Carmelita na kumfanya Elvis acheke kidogo. “ Baba yako alipofariki alituachia mali nyingi na mrithi pekee ni wewe .Kitu kinachoniumiza mimi ni kwamba muda mrefu sasa umepita toka umefunga ndoa na Patricia lakini hakuna dalili zozote za kuniletea mjukuu.Unawaza nini kuhusu suala hili? Akauliza Bi Carmelita. Swali lile likaonekana kumstua sana Elvis kwani hakuwa amelitegemea. “ Mambo yameanza..Wamenza kudai toto wao ..!! akawaza Elvis “ Elvis ! akasema Bi Carelita na kumstua Elvis aliyeanza kuzama mawazoni Ndoto yangu kubwa ni kukuona ukiwa na familia kubwa na hatinaye tupate warithi wa kuziendeleza mali hizi.Sitaki kuingilia masuala yako ya ndani ya ndoa kwani sijui kinachoendelea kati yako na mkeo lakini ninachotaka ni kupata maoni yako kuhusu nini unafikiria kuhusiana na suala hili la mtoto? Elvis akainama akatafakari na kusema “ Mama naomba tafadhali usiumize kichwa kwa suala hili.Nafahamu kiu yako ya kupata mjukuu lakini naomba usiwe na hofu.Muda utakapowadia utampata mjukuu” akasema Elvis huku akijitahidi kutabasamu. “ Mwanangu ni miaka zaidi ya mitatu sasa imepita toka mmefunga ndoa kitu gani mnachokisubiri? Mnasubiri hadi ipite miaka mingapi? Bado tunajipanga mama kabla ya kuamua kupata mtoto” “ Kitu gani unachokisubiri Elvis? Nyote wawili mna kazi za maana.Mna kila kitu mnachokihitaji.Mnataka kujipanga nini? Mnataka hadi muwe na ndege yenu binafsi? “ Mama kuna mambo mengi ambayo tunatakiwa kufanya kabla ya kumleta kiumbe duniani” akasema Elvis “ Elvis ni maandalizi gani hayo mnayoyafanya?Kama ni fedha niambieni kiasi gani mnachokitaka ili niwapatie” “ Tatizo si pesa mama.Yapo mambo mengi tu ya kujipanga” Akasema Elvis.Mama yake akamtazama usoni na kusema “ Elvis niambie ukweli kuna tatizo lolote katika ndoa yenu? Kuna mmoja wenu ana matatizo katika masuala ya uzazi? Kama kuna tatizo lolote kati yenu naomba niweke wazi ili kwa pamoja tutafute namna ya kufanya.” Akasema Bi Carmelita.Elvis akatabasamu na kusema “ Huko unakofika mama ni mbali sana.Hakuna mtu mwenye tatizo kati yetu.Sisi sote tu wazima kabisa.Naomba unipe muda kidogo tuweke mambo sawa na utafurahi mwenyewe” akasema Elvis na mara Jackline binamu yake Elvis akaingia.Akakumbatiana na Elvis kwani ni muda mrefu hawajaonana “ Elvis habari za siku? Nimefurahi sana kukuona” “ Habari nzuri Jack.Ninaendelea vizuri tu.Vipi maendeleo yako? “ Ninaendelea vizuri hata mimi ila nasikitika sana hukuweza kuhudhuria katika harusi yangu” Utaisamehe Jack.Nilikuwa nje ya nchi lakini mke wangu alifika kuniwakilisha” “ Usihofu Elvis.Namshukuru Mungu mambo yalikwisha salama na mambo ni mazuri” akasema Jack huku akitabasamu na kulishika tumbo lake kubwa.Elvis akatabasamu “ Wow ! hongera sana Jack.Nahisi muda si mrefu mambo yatakuwa mambo” akasema Elvis “ Kweli kabisa Elvis.Mambo yatakuwa mazuri hivi karibuni” “ Hongera sana Jack.” Akasema Elvis “ Ahsante sana Elvis.What about you?What are you waiting for? Akauliza Jack “ Hilo ndilo jambo ambalo hata mimi nilikuwa namwambia hapa sasa hivi.Umekuwa ni muda mrefu sasa na hatuoni chochote.Nadhani ni wakati muafaka sasa kwa Elvis kutuletea mtoto.Ninahitaji kumuona mjukuu wangu kabla sijafa” akasema Bi Carmelita “ Ni kweli Elvis hayo ninayoyasema shangazi.Ni wakati muafaka sasa wa kutafuta mtoto” akasema Jack Elvis akatabasamu na kusema “ Nimekwisha ongea na mama na kumuahidi kwamba nitalifanyia kazi suala hilo.Hata mimi na mke wangu tuna mipango yetu ya ndani na suala hili tunalifahamu na liko katika mipango yetu kwa hiyo nawaomba muwe na subira na muda muafaka utakapowadia tutafanya mnavyotaka” akasema Elvis “ Sawa Elvis ,hatutaki kuingilia masuala yenu ya ndani lakini ni muhimu kama ukalifanyia kazi suala hili.” Akasema Bi Carmelita “ Usijali mama .Nitalifanyia kazi kama nilivyokuahidi” akasema Elvis halafu akaondoka pale bustanini na kuwaacha mama yake na Jack,akaenda kuungana na ndugu zake.Kichwa chake kilijaa mawazo mengi sana kutokana na maongezi yake na mama yake. “ Mpaka mama amefikia hatua ya kunieleza wazi wazi kuhusiana na suala la mtoto basi lazima litakuwa ni suala ambalo limemsumbua na kumuumiza sana kichwa chake.Nilitegemea mambo kama haya kujitokeza na sasa yameanza,natakiwa nikabiliane nayo” akawaza Elvis “ Lazima nikabiliane na suala hili na shinikizo lolote toka kwa ndugu.Lazima nihakikishe kwamba Patricia haumizwi na suala hili.Nilikubali kumuoa Patricia hali nikifahamu kabisa kwamba hana uwezo wa kupata mtoto na nilifanya hivyo kwa sababu ninampenda kwa moyo wangu wote na suala la kutokupata mtoto kwangu mimi si kigezo cha kushindwa kumpenda Patricia.Nitasimama imara na sintakubali mtu yeyote Yule awe ni mama au ndugu yeyote aingilie masuala yangu ya ndani ya ndoa.” Akawaza Elvis Saa mbili za usiku Elvis na mkewe Patricia wakaondoka na kurejea nyumbani kwao. ******************** Ni siku ya jumatatu ,baada ya kutoka ikulu kuangalia maendeleo ya mke wa rais ,Patricia akaelekea kazini kwake.Mara tu alipowasili akapata taarifa kwamba kuna mgeni wake aliyekuwa akimsubiri toka saa mbili asubuhi.Moja kwa moja akaelekea kwanza ofisini kwake akavaa koti lake la kitabibu halafu akaelekeakatika kantini ya hospitali ambako aliekezwa kwamba ndiko aliko mgeni wake. Alipofika kantini,Patricia akapigwa na butwaa baada ya kukutana na mama mkwe wake yaani Bi Carmelita mama yake Elvis.Nywele zikamsisimka na kwa kiasi Fulani akaogopa.Haikuwahi kutokea hata mara moja kwa Bi Carmelita kumfuata pale hospitali.Mara nyinig awapo na tatizo lolote au akihitaji msaada wa aina yoyote huwasiliana kwa simu lakini kitedo cha kumfuata pale hospitali kilimstua na kumshangaza sana Patricia. “ Mama shikamoo..” akasema Patricia akimsalimia mama mkwe wake kwa adabu “ Marahaba Patricia.Unaendeleaje?Samahani kwa kuja ghafla bila taarifa .Nilikuwa na shughuli hapo jirani na hospitali yenu hivyo nikaona ni vyema endapo nitapita hapa na kukusalimu .Nilipofika hapa nikaambiwa kwamba kila siku lazima upite kwanza ikulu kumuangalia mke wa rais “ “ Ndiyo mama kila siku asubuhi lazima nipite ikulu kumjulia hali mke wa rais na kuangalia maendeleo yake.Alipatwa na tatizo la kupooza mwili upande mmoja ” akasema patricia “ Vipi maendeleo yake? “ Anaendelea vizuri kwa sasa na viungo vyake vinaweza kufanya kazi tena.” “ Nafutahi kusikia hivyo.Lakini naomba unisamehe mwanangu kwa kuja namna hii bila kukutaarifu” “ Usihofu mama.Hakuna tatizo lolote .Karibu sana.Utapenda kutumia kahawa? “ Ouh ahsante sana Patricia lakini tayari nimekwisha hudumiwa kila nilichokihitaji.Wahudumu walipoambiwa kwamba mimi ni mgeni wako wamenichangamkia na kunipatia kila nilichohitaji.Ahsante sana Patricia” akasema Bi Carmellita.Patricia akamuita muhudumu na kumuomba amletee kahawa. “ Patricia mwanangu utanisamehe pia kwa kutumia muda wako wa kazi lakini kuna jambo moja ambalo limenileta hapa kwako asubuhi hii” akasema bi Carmelita “ Usijali kuhusu muda mama .Kuna tatizo gani? Akauliza Patricia “ Si tatizo bali ni suala dogo tu ambalo nataka niongee nawe kama mama na mwanae” “ Nakusikia mama endelea..” “ Patricia kama unavyoniona haliyangu mimi mama yako nimekwisha kuwa mzee.Nguvu zinaniisha taratibu.Nafurahi kwa Elvis kumpata mke ambaye hata kama nikifa leo basi sina wasi wasi hata kidogo ninajua mwanagu amebaki katika mikono salama” akasema bi Carmelita.Patricia akatabasamu “ Patrcia moyo wangu una furaha kubwa kwa wewe kukubali kuolewa na mwanangu.Kwa dunia ya sasa kupata mwanamke kama wewe ni jambo la bahati sana.Toka ndani ya moyo wangu ninakuhakikishia kwamba ninakupenda sana” “ Ouh ahsante sana mama.Hata mimi ninakupenda pia na ninashukuru kumpata mume kama Elvis na mama mkwe mwenye upendo kama wewe.Ninafurahi sana mama “ akasema Patricia .Bi Carmelita akatabasamu na kusema “ Ahsante sana Patricia.Nafurahi kusikia hivyo.Pamoja na hayo kuna jambo moja dogo tu ambalo napenda tuliongee” Jambo gani mama? Akauliza Patricia “Ni kuhusu mtoto “ Patricia aliposikia neno mtoto likitajwa,alisikia kitu kama nyundo nzito ikiupiga utosi wake.Moyo wake ukabadili mapigo na kuanza kwenda kwa kasi ya ajabu .Kijasho chembamba kikamtoka.Mstuko alioupata ulikuwa wa dhahiri kiasi kwamba hata mama mkwe wake aligundua. “ Samahani Patricia kama nimekustua lakini nimeona nikutane nawe ili tuongee nijue kama kuna tatizo lolote kuhusiana na suala hili.Kama unavyojua ni zaidi ya miaka mitatu sasa imepita toka mmeoana na hatujaona dalili zozote za kutuletea mjukuu.Kuna tatizo gani mwamangu?Au bado mnajipanga? Akauliza Bi Carmelita.Patricia akainama akashusha pumzi ,akafikiri na kusema Mama umewahi kuzungumza na Elvis kuhusiana na suala hili? “ Ndiyo nimewahi kuzungumza naye lakini jibu alilonipa halikunifurahisha na ndiyo maana nimekuja kwako ili tuongee na uniambie mna mipango gani au kama kuna tatizo basi nifahamu ili tuweze kulitafutia ufumbuzi.” Akasema Bi Carmelita.Patricia akavuta pumzi ndefu akafikiri kidogo na kusema “ Mama kwa kweli hakuna tatizo lolote.Tumechelewa kwa sababu ya kujipanga na kuweka mazingira mazuri” akasema Patricia “ Patricia mwanangu nilipoongea na Elvis naye alinipa jibu kama hilo kwamba muda haujafika na kwamba bado mnajipanga.Mnasubiri miaka mingapi ndiyo muwe tayari? Mnajipanga kitu gani? Akauliza bi Carmelita.Patricia jasho likaendelea kumtoka mama kuna masuala mengi ya kujipanga kabla ya kumleta mtoto duniani.Tunashughulikia suala hili na muda utakapofika utafurahi mwenyewe.Naomba utupe muda mama” akasema Patricia “ Patricia kuna jambo ambalo limeanza kunipa wasi wasi .Inaonekana kuna jambo ambalo hamtaki kuliweka wazi.Kuna tatizo gani? Kuna mmoja wenu ana tatizo lolote? Kama kuna mmoja ana tatizo kuweni wazi ili tuangalie ni namna gani ya kumsaidia kwani masuala haya ni ya kawaida sana hivi sasa” kauli ile ya bi Carmelita ikaendelea kumtoa jasho Patricia na kukitonesha kidonda ambacho kimekwisha pona tayari..Akajikaza na kusema “ Mama tatizo linalotufanya tusiwe tayari kwa sasa ni majukumu ya kikazi na zaidi ya yote nimechaguliwa kwenda kuendelea na masomo nje ya nchi kwa muda wa miaka mitatu.Elvis naye kuna kazi anatarajiwa kuifanya nje ya nchi na hatujui itamchukua muda gani kwa hiyo hilo ndilo suala linalotupa ugumu kwa sasa.Tunataka tutakapokuwa tayari kupata mtoto sote tuwe na muda wa kutosha kwa kumlea mtoto huyo” akasema Patricia “ Kama mkiweka mbele majukumu ya kazi zenu ni lini basi nafasi hiyo itapatikana? akauliza bi Carmelita “ Sote tunajaribu kutafuta uwezekano wa kuomba kusitishwa au kuahirishwa kwa safari hizo.Tayari nimekwisha wasiliana na viongozi wangu na nimekwisha wasilisha kwao maombi yangu na wanayafanyia kazi .Elvis naye amekwisha fanya hivyo lakini bado hajapatiwa majibu” akasema Patricia





Ahsante nimekuelewa Patricia.Ninawaombea Mungu maombi yenu yakubaliwe ili muweze kupata nafasi nzuri ya kutafuta mtoto.Kitu kingine ambacho nataka kukuomba ni kwamba muda wowote kama kuna tatizo lolote usisite kunifahamisha na tukatafuta ufumbuzi wa haraka” akasema bi Carmelita huku akiinuka “ Nitafanya hivyo mama usijali” akasema Patricia huku naye akiinuka wakaagana na bi Carmellita na kisha akaeleka ofisini kwake. Miguu ilikuwa mizito hata kupiga hatua .Alihisi kama amebeba kitu kizito kichwani.Mambo aliyoongea na mama mkwe wake yalimstua mno.Baada ya kuingia ofisini kwake Akakaa kitini na kuvuta pumzi ndefu Ouh Mungu wangu ! Mambo yameanza.Nilitegemea tu lazima mambo kama haya yatatokea siku moja na sasa yametimia.Ndugu wameanza kudai mtoto wao.Mpaka ifikie hatua ya mama mkwe kunieleza wazi wazi basi lazima suala hili liwe limekwisha jadiliwa sana katika ngazi ya ukoo na wameamua kunieleza wazi wazi. Ouh Mungu wangu nitafanya nini mimi? Nitamtoa wapi mtoto wanayemtaka? Akawaza Patrica .Alihisi kama kichwa chake kinataka kupasuka kwa mawazo .Alichanganyikiwa na hakujua afanye nini. “ Sina uwezo wa kuzaa tena na hakuna muujiza wa kuniwezesha kupata mtoto.Kama ndugu wameanza shinikizo la kudai mtoto basi furaha yote ya ndoa yangu iko hatarini kutoweka.Nampenda sana Elvis na sitaki mtu yeyote anitenganishe naye.Yeye ndiye kila kitu kwangu.Nimetoka naye mbali sana ,ananifahamu vizuri,anayajua matatizo yangu na amekubali kuishi nami kwa sababu ananipenda na hata siku moja hajawahi kunitamkia au kuniuliza chochote kuhusiana na suala la mtoto.Amenifanya ni mwenye furaha na nijisikie ni moja kati ya wanawake wenye bahati duniani lakini nimeanza kuingiwa na shaka kama ataendelea kuivumilia hali hii ya kukosa mtoto hadi kifo kitutenganishe kutokana na shinikizo la ndugu zake.Nina wasi wasi anaweza akaamua kutafuta mwanamke mwingine ili kuwaridhisha ndugu zake na hapo ninahisi penzi lake kwangu litakuwa limefika ukomo.Hatakuwa tayari kunipenda tena mtu ambaye sina faida yoyote kwake.Ouh gosh I’m so scared” akawaza Patricia kichwa chake kikajaa mawazo kiasi kwamba alishindwa hata kufanya kazi.Akavua koti lake la kidaktari na kutoka mle ofisini bila kuongea na mtu yeyote akapanda gari lake na kuelekea moja kwa moja kanisani.Milango ya kanisa ilikuwa wazi akaingia akapiga magoti na kuanza kusali huku machozi mengi yakimtoka “ Ee Mungu wangu nimekuja mbele zako ,najua nimekukosea sana.Najua wewe ni mwema sana na ninafahamu umekwisha nisamehe kosa langu kubwa nililolifanya la kutoa mimba,lakini bado naendelea kukulilia ee Mungu wangu endelea kuwa nami katika matatizo yangu.mambo yameanza kuniharibikia na furaha ya maisha yangu iko mbioni kutoweka.Ndugu za mume wangu wanaanza kudai mtoto na mimi sina uwezo wa kuzaa mtoto.Ee Mungu naomba uinusuru ndoa yangu isivunjike.Elvis ndiye kila kitu kwangu na sijui maisha yangu yatakuwaje bila ya kuwa naye.Nipe nguvu na ujasiri wa kulibeba jambo hili mpaka mwisho wake” akaomba Patricia huku akilia.Alitoa machozi mengi hadi kifua chake kikaloa machozi halafu akapanda gari lake na kurejea nyumbani akajifungua chumbani ******************** Saa moja za jioni ,Elvis akarejea nyumbani na kushangazwa na kitendo cha kumkuta mke wake akiwa chumbani amelala.Siku zote Patricia hakuwa mtu wa kupenda kulala lala. “ Hallo darling..Unaumwa? Si kawaida yako kuwa kitandani mida kama hii” akasema Elvis huku akimbusu mkewe katika paji la uso. “ Siumwi Elvis ,ila najisikia uchovu sana siku yaleo” akajibu Patrica huku akinuka na kukaa “ Matilda ameniamia kwamba leo umerejea mchana.Kulikoni? Una matatizo gani? Akauliza Elvis “ Ni kweli nimewahi sana kurudi leo,sikuwa nikijisikia vizuri.Pole na kazi” “ Ahsante sana mke wangu.Pole nawe.Unajisikiaje sasa hivi? “ Hivi sasa ninajisikia vizuri.Nimekunywa dawa najisikia afadhali.” Akasema Patricia kisha akamsaidia mume wake kuvua nguo halafu wote wakaingia bafuni kuoga.Kisha oga wakaenda kupata chakula cha usiku kilichoandaliwa na Matilda mfanyakazi wa ndani.Kisha kula wakaenda chumbani kwa mapsumziko. Mama alikuja leo kazini” akasema Patricia akiwa amekaa na mumnewe kitandani. “ Mama alikuja kazini kwako?! Elvis akashangaa “ Ndiyo.Nilipofika tu hospitali baada ya kutoka ikulu nilimkuta pale akinisubri” “ Asubuhi namna hiyo? Alikuwa anataka nini? Anaumwa? Akauliza Elvis “ Hapana haumwi chochote.Alipita tu kunisalimu na kuniletea ujumbe” “ Ujumbe ? Ujumbe gani? Akauliza Elvis kwa mshangao.Patricia akatabasamu na kusema “ Mama anataka mtoto” Kauli ile ikayafanya mapigo ya moyo wa Elvis yabadilike ghafla na kuanza kwenda kwa kasi isiyo ya kawaida Kwa nini wanataka kuanza kuingilia maisha yangu? Akasema Elvis kwa hasira “ Calm down my love.Calm down” Patricia akasema akijaribu kumtuliza mumewe “ Pole sana Patricia najua uliumia mno na ndiyo maana ukawahi kurudi nyumbani leo.Wewe ulimjibu nini? “ I lied to her.Nilimdanganya kwamba sote tumechaguliwa kwenda kimasomo na kikazi nje ya nchi kwa hiyo suala la mtoto litasubiri hadi hapo tutakapokuwa na nafasi yakutosha.I’m so sorry that I lied to your mother.” Akasema Patricia huku machozi yakimtoka “ Usihofu Patricia.You did the right thing na ninakuomba tafadhali usiumie wala usihofu kuhusu suala hili.Hauna mtu yeyote mwenye ruhusa ya kukuuliza jambo lolote kuhusanana suala la mtoto.Mimi ndiye niliyekuoa na ninafahamu tatizo lako na siko tayari ukose furaha kwa sababu tu ya suala hili la mtoto.Nitasimama dhidi ya yeyote Yule ambaye atakunyooshea kidole” akasema Elvis na kumkumbatia mke wake.Patricia akafuta machozi na kusema “ Elvis najua unanipenda na sina shaka hata kidogo na upendo wako kwangu .Najua uko tayari kwa lolote kwa ajili yangu.Elvis hata mimi nakupenda sana zaidi ya ninavyoweza kukueleza.Pamoja na upendo huu mkubwa tulio nao ambao nina hakika hauwezi kutetereka lakini ninafahamu toka ndani kabisa mwa moyo wako utakuwa unaumia sana kwa kukosa mtoto na kutokuwa na tumaini kabisa la kupata mtoto katika maisha yako.” “ Patricia !!..Elvis akamkatisha Patricia ili asiendelee kusema alichotaka kukisema “ Elvis tafadhali naomba unisubiri nimaize kusema kile ninachotaka kukwambia.Hata mimi mwenyewe suala hili linaniumiza sana Elvis.Natamani kukuona ukiwa na furaha ,ukiwa na mtoto nawe ukiitwa baba.Natamani kuona nyumba yetu ikiwa imechangamka ikiwa na furaha lakini ninaumia sana kwa kuwa niliyepaswa kuyafanya yote haya yakamilike na mimi na sina uwezo huo tena.,Siwezi kukuzalia mtoto na siwezi kuikamilisha furaha yako .Kwa kuwa ninakupenda zaidi ya kitu chochote kile sitaki kukuona ukikosa furaha kwa hiyo kuna jambo nimelifikiria” “ Patricia what are you trying to say? Mawazo gani hayo unayoyawaza? Akauliza Elvis Elvis,let me be honest,you’ll never be happy in your lfe without a kid” “ Stop it Patricia…please don’t ever say that again.Sitaki kusikia mambo kama hayo tena.Please my love this conversation is over” akasema Elvis “ Elvis naomba unisikilize ninachotaka kukwambia.Ninachokisema ni ukweli mtupu,najua wewe unaweza kuvumilia kwa sababu unanipenda lakini sina hakika kama ndugu zako wanaweza wakavumilia hali hii na lazima litatokea shinikizo toka kwako la kukutaka utafute mtoto.Najua itafika wakati ambao utashindwa kuvumilia.Sitaki kusubiri hadi wakati huo ufike.Nataka tutafute suluhisho la jambo hili sasa kabla suala hili halijachukua sura mpya kwani tayari moshi umeanza kufuka.” “ Hakuna suluhisho lolote la suala hili Patricia.Mjadala huu tumekwisha ufunga muda mrefu sana.Niliyekuoa ni mimi na si ndugu yangu yeyote kwa hiyo masuala ya ndani ya ndoa yangu hakuna yeyote anayepaswa kuyaingilia.” “ Nalifahamu hilo Elvis mpenzi ,lakini sitaki ukose amani mume wangu kwa sababu ya shinikizo la ndugu .Nataka kukuona ukiwa na furaha na amani siku zote katika maisha yako kwa maana hiyo nimefikiria sana na kufikia maamuzi kwamba utafute mwaname ambaye utazaa nae mtoto ili usikose mrithi wa mali zako .Naomba usistushe na jambo hili.Haya ni maamuzi yangu na sintakuwa na tatizo lolote lile.Moyo wangu mweupe kabisa.Mtoto huyo utakayempata nitampenda na kumlea kama mwanangu” akasema Patrcia .Elvis akamtazama na kucheka kidogo kisaha akasema “ patricia unawaza nini leo? Mawazo hayo umeyatoa wapi? Kitu gani kinakufanya uwaze mambo kama hayo? Akauliza Elvis akiwa amemkumbatia mkewe “ Elvis usinielewe vibaya mume wangu lakini hili ndilo suluhisho pekee la kunusuru ndoa yetu.Ninakupenda sana Elvis .Nakupenda zaidi ya ninavyoweza kukueleza na sitaki hata siku moja nikukose katika maisha yangu.Wewe ndiye kila kitu kwangu.Wewe ndiye maisha yangu.Please my love do that for me” “ Patricia..!!..akasema Elvis “ Please my love naomba ukubali kufanya hivyo.Tafuta mwanamke ambaye utazaa naye mtoto.Sintakuwa na tatizo lolote hata kidogo na mwanamke huyo na siku zote nitamuheshimu.Bila mtoto I swear we’ll never be happy na ndoa hii itavunjwa na ndugu zako.” Akasema Patricia.Elvis akacheka “ Mbona unacheka mpenzi? Jambo gani limekufurahisha? Akauliza Patricia.Elvis akambusu na kusema “ Ninacheka kwa sababu sijawahi kusikia au kutegemea kama siku moja ungeongea jambo la ajabu namna hii” akasema Elvis “ Elvis,hili si jambo la utani hata kidogo.Ninaamaanisha ninachokiongea “ “Patricia mke wangu hata kama unamaanisha unachokisema lakini naomba nikuhakikishie kwamba jambo hilo unalolitaka katu haliwezekani.Siwezi kufanya jambo la namna hiyo na ninaomba tusiendelee kuliongelea suala hilo.Let’s talk about your coming birthday this week” “ Elvis hatuwezi kuliacha jambo hili hivi hivi.Naomba unielewe mume wangu,nimeamua hivi kwa sababu nakupenda na ninakujali.Tafadhali naomba unikubalie ombi langu hili.Endapo tutapata mtoto haijalishi ni kwa namna gani lakini itanusuru ndoa yetu” Elvis akamtazama mke wake machoni kwa makini na kugundua kitu Fulani.Akaacha mzaha na kusema “ Naomba unisikilize Patricia.Mimi ndiye niliyekupenda na kukuoa.Toka awali nililifahamu tatizo lako na kwa moyo wangu mmoja nikakubali kulibeba tatizo hilo kwa sababu ya upendo wangu kwako usio na kipimo.Nilikupenda kabla hata ya kupatwa na matatizo yale na sikufahamu wakati ule kama una uwezo wa kuzaa au huna.Nilikuwa nawe wakati wa matatizo yale nilisimama pamoja nawe kwa sababu ninakupenda.Nakuomba usiendelee kujilaumu kwa kilichotokea.Hupaswi kuadhibiwa kwa makosa ya wakati ule kwa sababu hukuwa na namna nyingine ya kufanya zaidi ya vile ulivyofanya .Patricia nakupenda mno na nina furaha kubwa kuwa nawe.Maisha yetu yana furaha kubwa kwa hiyo nakusihi usiwape watu nafasi ya kuingilia maisha yetu ya furaha.Haya ndiyo maisha yetu na hatuna kitu kingine cha ufanya zaidi ya kukubaliana na hali halisi kwamba hatuwezi kuwa na mtoto katika maisha yetu” akasema Elvis.Patricia akatabasamu lile tabasamu lake adimu sana ambalo siku zote huwa lina mpagawisha Elvis “ Siku zote maneno yako matamu yamekuwa yakiupagawisha moyo wangu.Nashukuru kwa maneno hayo mazito uliyonambia nami nakuahidi kwamba sintaacha kukupenda hata kwa sekude moja.Pamoja na hayo yote lakini bado moyo wangu unakosa amani.Nina hakika lazima kutakuwa na shinikizo kubwa toka kwa ndugu zako pale watakaogundua kwamba sina uwezo wa kuzaa mtoto kwani hutaweza kuificha siri hii milele.” “ Patricia ,tulikula kiapo kanisani kwamba tutapendana katika shida na raha hadi kifo kitutenganishe.Nitasimama katika kiapo hicho hata siku moja sintakwenda kinyume na kiapo nilichoapa cha kukupenda wewe peke yako na kukuvumilia hadi kifo kitutenganishe.Naomba tafadhali ufute kabisa wazo kama hilo.Siwezi kufanya jambo kama hilo unalotaka nilifanye.Nakupenda sana Patriciana katu siwezi kukufanyia jambo la ajabu namna hiyo.Naomba mjadala wa suala hili uishie hapa ” Akasema Elvis na kumbusu Patricia halafu wakaendelea na maongezi mengine kuhusiana na sherehe ya siku ya kuzaliwa kwa Patricia. ************************* Saa saba za mchana siku iliyofuata ,Patricia akataarifiwa kwamba kuna mgeni wake.Alikuwa na miadi ya kukutana na rafikiye Doreen..Akavua koti lake na kutoka ofisini kwenda kuonana na Doreen kisha wakaelekea Papino Restaurant kwa ajili ya kupata chakula cha mchana.Maongezi yalikuwa mengi huku wakiendelea kupata chakula halafu Patricia akabadili maongezi. “ Doreen nimekuita kuna jambo ambalo ninahitaji sana msaada wako ndugu yangu” Jambo gani Dr Patrica? Wewe ni rafiki yangu mkubwa na niko tayari kukusaidia katika tatizo lolote” akasema Doreen msichana mwenye uzuri wa kipekee.Binti huyu ambaye mama yake ni mzungu toka ufaransa na baba mtanzania alikuwa ni rafiki mkubwa wa Patricia ambaye walikutana masomoni nchini Marekani.Doreen kwa sasa ni mfanyakazi wa kampuni moja ya simu hapa nchini “ Doreen nina matatizo makubwa ndugu yangu” “ Matatizo gani Patricia? Naomba unieleze tafadhali” “ Kwa kuwa wewe ni rafiki yangu wa karibu nitakueleza ni jambo zito na la ndani sana kuhusiana na maisha yangu kwa hiyo naomba tutakachoongea hapakibaki kuwa ni siri yetu” akasema Patricia .Doreen akanywa funda moja kinywaji na kusema “ Patricia mimi nawe ni zaidi ya marafiki.Mambo mengi ya siri tumekuwa tunaambiana.Naomba uniamini na uniambie jambo lolote lile linalokusumbua” Patricia akavuta pumzi ndefu na kuanza kumsimulia Doreen historia ya maisha yake hadi alipopata ujauzito akiwa shuleni hadi alivyotoa mimba ile na kuhatarisha maisha yake jambo lililomsababishia atolewe kizazi na kupoteza uwezo wa kuzaa. Doreen jasho likamtoka.Pamoja na kumfahamu Patricia kwa muda refu lakini hakuwahi hata siku moja kulifahamu tatizo lile alilokuwa nalo.Alitoa kitambaa na kujifuta kijasho kilichoanza kumchuruzika usoni. “ Pole sana Patricia.Kwa kweli suala hili ni gumu sana na sikuwahi kujua kama unaweza kuwa na tatizo kama hili” akasema Doreen “ Ahsante sana Doreen.Ndiyo maisha yalivyo” akasema Patricia “ Matatizo kama haya ni ya kawaida na yanaweza kumtokea mtu yeyote.Nijambo lenye kuumiza sana hasa ukifahamu kwamba hutaweza tena kupata mtoto katika maisha yako.Namshukuru sana Elvis kwani analifahamu fika tatizo langu lakini amekubali kulibeba kwa moyo wake wote.Pamoja na hayo kuna tatizo limejitokeza” akasema Patricia “ Tatizo gani Patricia? Akauliza Doreen “ Ndugu za Elvis tayari wameanza kudai mtoto” “ Gosh ! Tayari imeshafika hapo? “ Mambo tayari yameanza Doreen.Tayari ndugu wameanza kuhisi kuna tatizo na wameanza kudai mtoto.Jana mama mkwe alinifuata kazini na kunihoji kwa nini mpaka leo hatujapata mtoto” “ Ouh my gosh ! Umemjibu nini? “ Nilikosa cha kumjibu ikanilazimu nimdanganye” “ Ina maana mama mkwe hajui chochote kuhusiana na tatizo hili? Doreen akashangaa “ Hakuna anayefahamu chochote kuhusiana na tatizo hili.Hata marehemu mama yangu ambaye sikuwa nikimficha chochote hakuwahi kuifahamu siri hii.Ni siri yangu mimi na Elvis kwani wakati mambo haya yanatokea yeye ndiye aliyekuwa pamoja nami na kwa sababu ananipenda aliamua kunioa hivyo hivyo.Wewe ndiye mtu pekee ambaye nimekuamini kukwambia siri hii na nina imani utanisaidia” “ Niko tayari kukusaidia Patricia kwani nafahamu ni namna gani suala hili linavyotesa.Kuna rafiki yangu mmoja ninafanya naye kazi anateseka sana kwa kukosa mtoto.Ananyanyaswa mno na ndugu za mume.Kwa hiyo umepanga kufanya nini Patricia? Akauliza Doreen.Patricia akanywa maji kidogo akamtazama Doreen na kusema “ Doreen kuna jambo nimefikiria kulifanya kunusuru ndoa yangu ambayo sina hakika kama itadumu endapo hakutakuwa na mtoto” “ Umefikiria kufanya nini Patricia? Nimechanganyikiwa mwenzako na sijui nifanye nini” akasema Doreen “ Kuna kitu nataka nikifanye Doreen japokuwa ni kugumu lakini sina budi kukifanya” “ Niambie Patricia ni kitu gani hicho unachofikiri kukifanya? “ Doreen wewe ni zaidi ya rafiki na ndiyo maana ninakuomba msaada wako” Niambie Patricia niko tayari kukusaidia kwa jambo lolote lile” “ Nashukuru kusikia hivyo.Ninakuomba uzae na Elvis” akasema Patricia Doreen akastuka na kuinuka akashika kiuno na kumshangaa Patrica “ Patrica.!!! akasema Doreen kwa mshangao.Patricia akainuka akamshika mkono na kumetisha kitini Doreen akatoa kitambaa akafuta jasho “ Calm down Doreen.Najua nimekustua na kukushangaza sana.Naomba usistuke ndugu yangu” “ Patricia ni kweli umenistua sana” “ Usistuke Doreen.Usistuke ndugu yangu” akasema Patricia.Doreen akavuta pumzi ndefu “akasema Tafadhali Patricia naomba ukirudie tena kile ulichokisema.Pengine sikusikia vizuri” Patricia akamtazama Doreen kwa makini na kusema “ Doreen matatizo yangu ni kama nilivyokueleza.Nina tatizo kubwa sana ndugu yangu.Ndoa yangu iko mashakani baada ya ndugu za Elvis kuanza kudai mtoto.Sina uwezo wa kuzaa mtoto kwa hiyo kuna hatari ndugu wakamshinikiza Elvis atafute mwanamke mwingine ili azae naye mtoto.Na pindi ikitokea hivyo basi ndoa yangu itakuwa matatani na ndiyo maana ninakuomba wewe unisaidie kwa hilo.Naomba uzae na Elvis ili ndugu watulie baada ya kusikia Elvis ana mtoto” akasema Patricia.Doreen akacheka kidogo na kusema “ Patricia that’s impossible.Hicho ni kitu ambacho hakiwezekani kabisa na sijui mawazo haya umeyatoa wapi” “ Doreen inawezekana .Naomba unisaidie ndugu yako niko katika matatizo makubwa.Najua si jambo rahisi kutokea lakini mpaka nimefikia hatua ya kukueleza jambo kama hili ujue kwamba mambo yamenifika shingoni.Naomba unisaidie Doreen.Bila msaada wako nitamkosa Elvis” Doreen akainama akafikiri na kusema “ Patricia nimekosa neno la kusema.Naumia moyoni kwa mateso unayoyapata na ninatamani kukusaidia lakini nasikitika kwamba katika suala hili sintaweza kukusaidia.Siwezi kuzaa na mumeo.Hilo ni jambo lisilowezekana kabisa.Utanisamehe Patricia.Mimi kama rafiki yako sikushauri ufanye hivyo unavyotaka kufanya Mpango huo ni hatari zaidi kwa ndoa yako kwani huwezi kujua nini kitatokea baada ya mwanamke mwingine kumzalia mtoto Elvis.Lakini kama unataka kuendelea na mpango wako basi nakushauri tafuta mwanamke ambaye unamuamini kwamba ataendelea kukuheshimu hata baada ya kumzalia mtoto mumeo na hatakuwa na tamaa ya kutaka kuchukua nafasi yako kama mke wa pili” akasema Doreen.Patricia akatabasamu na kusema “Ahsante kwa ushauri wako lakini naomba ufahamu kwamba haya ni maamuzi magumu niliyoyaamua kuyafanya katika maisha yangu na niko tayari kwa chochote kitakachotokea.Najua ni suala lenye changamoto nyingi na ndani yake lazima kutakuwa na maumivu mengi na makubwa lakini niko tayari kuyakabili yote hayo kwa lengo moja tu la Elvis apate mtoto.Ninampenda sana Elvis na yeye ndiye kila kitu kwangu na japokuwa hawezi kunieleza wazi wazi ninaamini ndani ya moyo wake anaumia kwa kukosa mtoto” akasema Patricia “ Patricia sikukatazi kufanya hivyo unavyotaka kufanya lakini nina mashaka kidogo kama maisha yako na Elvis yataendelea kuwa sawa baada ya kitendo hiki kufanyika.Are you sure things will continue to be the same? Patricia akainama akafikiri na kusema “ Elvis loves me so much and will never do anything to hurt me.As much as we love each other I hope we’ll continue to be the same” akasema Patricia kwa kujiamini “ Ahsante sana kwa kujiamini kiasi hicho lakini pamoja na hayo nakusihi tafuta mtu ambaye unamuamini na ambaye atakuwa na moyo wa kukusaidia kwa tatizo lako na si bora mtu.Hili si jambo rahisi sana kwa mtu kukubali kulifanya” “ Ndiyo maana nimekuamini na kukuchagua wewe Doreen” akasema Patricia “ Patricia let me be honest with you darling,I cant do such a thing to you.Kuniambia nizae na mumeo ni sawa na kuniambia nizae na ndugu yangu jambo ambalo haliwezekani .Patricia wewe ni zaidi ya rafiki kwa hiyo siwezi kufanya jambo kama hili kwa mtu kama wewe ambaye ninakuchukulia kama dada yangu so I cant do that” “ Yes you can do it Doreen” akasisitiza Patricia “ No Patricia I cant” “ Yes you can” akasema tena Patricia “ If you love me and you value our friendship you are gong to help me in this.I trust you so much that’s why I’ve chosen you.Naomba unisaidie Doreen ninateseka mwenzio” akasema Patricia huku macho yake yakilengwa na machozi.Doreen akamtazama rafiki yake akamuonea hurma sana.Alitamani kumsaidia lakini suala lile lilikuwa gumu sana kwake.Alihisi kama kuchanganyikiwa “ Doreen endapo hutanisaidia kuna hatari kubwa maisha yangu yakaharibika endapo Elvis atashindwa kuvumilia shinikizo la ndgu zake na kuamua kutafuta mwanamke mwingine wa kuzaa naye.Ikiwa hivyo sintakuwa tena na thamani kwa ndugu zake na hawatataka kuniona tena.Sitaki jambo hilo linitokee na ndiyo maana ninakuomba unisaidie wewe mtu ambaye ninakufahamu na ambaye nina uhakika mkubwa hata baada ya kuzaa na mume wangu bado hakuna kitakachobadilika kati yetu” akasema Patricia Doreen akamtazama Patricia usoni na kusema “Why do you trust me that much? “ I don’t know Doreen but I do trust you,my heart trust you “ akajibu Patricia Kimya kifupi kikapita kila mmoja akiwaza lake “ Are you going to help me? Akauliza Patricia “ Patricia unaniweka katika wakati mgumu sana.Nashindwa nifanye nini.Ninaumia unavyoteseka na ninatamani kukusaidia lakini……” “ Lakini nini Doreen? Kitu gani ambacho kinakupa ugumu? “ Suala hili si rahisi kama unavyolichukulia Patricia.Hili ni suala zito sana na gumu.Siku zote nilipanga kwamba nitazaa mtoto na mwanaume ambae nitafunga naye ndoa,kwa hiyo endapo nitakubali kuzaa na mumeo basi ndoto yangu hii haiwezi kukamilika.Nitakuwa nimeharibu mfumo mzima wa maisha yangu” “Nalifahamu hilo Doreen.Nafahamu changamoto zake na ndiyo maana ninakuomba toka moyoni mwako ukubali kunisiaidia.Sina mtu mwingine ambaye ninaweza kumkimbilia kwa wakati huu” Doreen akainama akafikiri na kusema “ Patricia kila ninapojaribu kuufanya moyo wangu ukubaliane nawe lakini unakataa kabisa” “ Doreen uko tayari kuiona ndoa yangu ikivunjika? Elvis ndiye kitu pekee kinachonipa furaha na sababu ya kuishi .He’s all I’ve got now.I don’t have a father or mother but I have Elvis.Sina uwezo wa kupata mtoto kwa hiyo mtoto wangu ni Elvis pekee.Endapo nikimkosa yeye basi sintakuwa na sababu nyingine ya kuendelea kuishi tena.Tafadhali naomba unisaidie Doreen” “ Patricia siko tayari kuiona ndoa yako ikisambaratika..” “ Kama hauko tayari basi naomba nisaidie” Doreen akainama akafikiri na kusema “ Mumeo anajua chochote kuhusiana na mpango huu? “ Nilimwambia…..” akasema Patricia na kusita kidogo “ Akasemaje? Alikubali ? “ Hapana hakukubaliana nami.Hayuko tayari kufanya kitu kama hicho” “ Kama hakubaliana nawe utautekelezaje basi mpango huo? Huoni kwamba unaweza ukazusha tena suala lingine gumu? “ I Have a plan how I’m going to do it” akasema Patricia Bila ya mumeo kufahamu? “ Ndiyo.Elvis hataelewa chochote na atakapokuja kugundua hatakuwa na la kufanya tena kwani tayari kitendo kitakuwa kimeshafanyika” “ Patricia huoni kama unafanya jambo la hatari sana? kulifanya jambo hili kwa siri bila ya mumeo kujua ni hatari.Hata kama nikiamua kukusaidia siwezi kufanya hivyo bila ya mume wako kujua kwani endapo atagundua jambo ulilomfanyia atakuwa na hasira sana na jambo hili linaweza kuzua matatizo makubwa” “ Doreen namfahamu vizuri Elvis katu hatakubali kufanya jambo hili kwa ridhaa yake na ndiyo maana kuna mpango nimeubuni” “ Mpango gani huo Patricia? Patrcia akanywa maji halafu akakohoa kidogo na kusema “ Siwezi kukwambia kwa sasa mpaka nitakapokuwa na uhakika kwamba uko tayari kunisaidia.Naomba ukubali Doreen I’ll take care of you.I’ll do everything for you.Nitakupa hata kiasi chochote cha pesa utakachohitaji” “ Patricia kama nikiamua kukusaidia si kwa sababu ya pesa lakini ni kwa sababu ya moyo wangu umekubali kufanya hivyo.Patricia wewe ni mtu ambaye niko tayari kufanya chochte kwa ajili yako lakini kwa jambo hili najaribu kuwaza bila kupata majibu” “ Jambo gani linakusumbua? Doreen akavuta pumzi ndefu na kusema “ Ninawaza endapo nitakubali kuzaa na Elvis nini kitafuata baada ya hapo? What if Elvis falls for me? Siombi jambo hili litokee lakini linawezekana kabisa kutokea na linaweza kuleta mgogoro mkubwa kati yetu.Pili jamii itanielewaje? Familia yangu itanichukuliaje? Vipi kuhusu maisha yangu? Mambo mengi nitakuwa nimeyapoteza.Sina maana kwamba nahitaji fidia lakini tayari nitakuwa nimepunguza vigezo vya kumpata mwanaume wa ndot zangu kwani wanaume siku hizi hawapendi kuoa mwanamke ambaye amekwisha zaa mtoto na mwanaume mwingine.Kitu kingine vipi kuhusu marafiki zetu na wanaotufahamu wakigundua kwamba nimezaa na mumeo? Itakuwa ni aibu kubwa mno kwetu .Tutazificha wapi nyuso zetu? Patricia jambo hili ni gumu sana na ndio maana inaniwia ugumu hata kukubali kukusaidia” akasema Doreen.Patricia akafikiri kidogo na kusema “ Doreen naomba nikutoe hofu kwamba Elvis hawezi akahamisha mapenzi kwako.Ninamfahamu vizuri na nina uhakika hawezi kufanya jambo hilo kwa hiyo usiwe na shaka na hata kama ikitokea hivyo nina uhakika kwamba huwezi kukubali litokee.Naomba nikuhakikishie vile vile kwamba kwa pamoja tutamlea mtoto huyo na atakapofika umri wa kuanza shule tutamchukua na kuishi naye nawe utapata nafasi ya kuendelea na maisha yako ya kawaida na ninakuomba nikutoe hofu kuhusu kuolewa.Siku hizi wanaume wanapenda kuoa mwaname ambaye ana uwezo wa kuzaa.Mwanamke kama mimi ambaye sina uwezo huo katu siwezi kupata mume wa kunioa ndiyo maana ninamuona Elvis kama malaika wangu kwa sababu pamoja na kufahamu hali yangu lakini bado amekubali kunioa nakunifanya nami nionekane mwanamke katika jamii.Kuhusu familia ndugu na marafiki wanaotujua ni lazima watakuwa na mengi ya kusema lakini siku moja watanyamaza, hakuna haja ya kuwajali sana.Kwa hiyo umeamuaje Doreen,utanisaidia? “ Patricia nashindwa kukupa jibu la m0ja kwa moja kwasasa.Naomba unipe mda wa kulitafakari suala hili halafu nitakupa jibu baada ya tafakari ya kina.Hili si suala la kulitolea maamuzi ya haraka.Naomba unipe siku mbili nikalifikirie” akasema Doreen kisha wakaendelea na maongezi mengine halafu wakaondoka. ******************* Jumamosi tulivu mwisho wa wiki ,wengi wa wafanyakazi wakiwa katika mapumziko ,nyumbani kwa akina Elvis kulikuwa na pilika pilika nyingi.Ni siku ya kumbu kumbu ya kuzaliwa kwa Patricia.Toka asubuhi Patricia alionekaa ni mtu mwenye furaha kubwa.Sherehe iliandaliwa katika eneo kubwa la bustani yao. Pamoja na furaha aliyokuwa nayo hakuna aliyefahamu kilichokuwamo ndani ya moyo wake.Alikuwa na furaha iliyochanganyika na wasiw asi. Kilichokuwa kikimfanya awe na wasi wasi ni kwamba siku hii ni siku ambayo alitazamia kuutekelza mpango wake alioupanga.Pamojana wasi wasi huo alikuwa nao katika kuutekelza mpango wake alikuwa na furaha pia kwa rafikiye Doreen kukubali ombi lake la kuzaa na mumewe Elvis.Patricia na Doreen ni marafiki wakubwa sana na





ambao wamekuwa wakisaidiana katika mambo mengi na ndiyo maana baada ya kutafakari sana Doreen aliamua kukubali kumsaidia rafiki yake ambaye alikuwa katika wakati mgumu sana. “ I’m so scared but I have to do it today.Elvis will get angry at me but I have to make it looks like an accident.Endapo zoezi hili likienda vizuri na Doreen akifanikiwa kupata ujauzito amani itakuwepo katika ndoa yangu” akawaza Elvis wakati akiwa saluni akitengeza nywele kwa ajili ya sherehe itakayoanza jioni.Mara picha ya mama yake ikamjia “ Laiti mama yangu angekuwepo angekuwa ni mfariji wangu mkubwa katika wakati huu mgumu nilionao.Mama yangu alifariki bila kufahamu chochote kuhusiana na siri yangu ya kutokuwa na uwezo wa kupata mtoto.Aliniusia endapo nitapata mtoto nimuite jina lake,hakujua kama sina uwezo huo” machozi yakamlenga Baada ya kumaliza kupambwa akapanda gari lake na kurejea nyumbani ambako wageni tayari walianza kuwasili.Miongoni mwa wageni waliokuwa wamewasili alikuwemo pia Doreen ambaye kwa siku hii ya leo alikwa amependeza sana akiwa ndani ya ganun refu jekundu .Kwa uzuri Doreen alijaaliwa uzuri wa kipekee kiasi kwamba amekuwa akiwatoa udenda wanaume wengi kupagawishwa na uzuri wake Patricia akawasalimu wageni waliokwisha wasili halafu akamshika mkono Doreen wakaelekea pembeni “ Nashukuru sana umekuja Doreen.Nilikuwa na wasiwasi sana pengine ungeweza kuogopa na kuahirisha” akasema Patricia Doreen akacheka kidogo na kusema “ Siwezi kuahirisha shoga yangu.Siwezi kukuangusha ingawa nina wasi wasi sana” “ Usiogoipe Doreen.Ni kweli si jambo rahisi and I don’t know if I’m doing the right thing but we have to do it today” akasema Patricia ‘Patrica how are we going to do it? Bado hujaniambia ni namna gani tutakavyofanya .Are we gong to talk to him? Akauliza Doreen.Patricia akatabasamu na kusema “ relax Doreen.Sherehe zikianza nitakuambia.Tulia ,pata kinywaji na uendelee kusubiri” akasema Patricia halafu akaelekea chumbani kwake kujiadaa. “ Uphhhh…!!!!!!” Doreen akavuta pumzi ndefu akachukua glasi yake iliyojaa mvinyo akanywa funda moja Patricia ana tatizo kubwa na nimekubali kumsaidia.Ouh gosh ! suala hili ni zito sana.Nimeingia katika mgogoro mkubwa lakini kwa ajili ya kumsaidia rafiki yangu.I don’t now what’s going to happen but then I have to do it.Patricia is my friend and I must help her” akawaza Doreen. “ Wow ! my angel you are so amazing today” akasema Elvis aliyeingia ghafla chumbani na kumkuta Patricia akijiremba.Akamsogelea na kumbusu “ You are so pretty my queen.I love you” akasema Elvis “ Thank you my love.I love you too” akasema Patricia huku akitabasamu Saa moja za jioni ,wageni wote walioalikwa tayari walikwisha wasili na aliyekuwa akisubiriwa ni Patricia pekee ajitokeze ili sherehe zianze “ It’s time .let’s go” akasema Elvis aliyekuwa chumbani na Patricia akamshika mkono wakaanza kutoka chumbani “ Are you nervous? Akauliza Elvis “ Not much” akasema Patricia kisha wakatoka nje na kuanza kutembea katika zuria jekundu lililotandikwa kuanzia mlangoni.Muziki laini ulikuwa unapigwa wakati Patricia akiwa ameshikwa mkono na mumewe wakielekea bustanini.Watu wote walisimama huku wakiwapigia makofi Haikuwa sherehe kubwa sana lakini ilifana vilivyo.Kila aliyehudhuria sherehe ile alisuuzika moyo wake.Kila kitu kilikwenda kwa mujibu wa ratiba na hatimaye zoezi la mwisho likawa ni muziki.Patricia na mumewe Elvis wakafungua muziki Walikumbatiana na kucheza kwa mahaba mazito “ Patricia,you’ll forever be my one and only true angel.Nakupenda zaidi ya ninavyoweza kukueleza” akasema Elvis wakati wakicheza halafu akambusu “ Ahsante sana Elvis kwa maneno hayo mazito.Hata mimi nakupenda na nitakupenda hadi pumzi yangu ya mwisho” akasema Patricia kisha wakakumbatiana kwa nguvu zaidi Wageni waalika nao wakajiunga na akina Elvis kulisakata rhumba huku wakiendelea kunywa vinywaji .Kulikuwa na vinywaji vya kila aina.Wakati muziki ukiendelea,Patricia akamvuta pembeni Doreen “ Sikiliza Doreen.Elvis si mnywaji sana wa pombe.Glasi mbili tu za mvinyo huwa amelewa na kawaida yake alewapo basi hulala usingizi mzito .Toka akiwa chumbani nimeanza kumnywesha pombe kali na mpaka sasa hivi bado anaendelea kunywa kwa maana hiyo muda si mrefu toka sasa atazimika.Unamuona anavyocheka? Akasema Patrica na wote wawili wakaelekeza macho yao mahala alikokuwa amekaa Elvis na wenzake wakipata kinywaji. “ Basi ile ni dalili tosha kwamba tayari amekwisha lewa.Nitakuwa ninamtupia macho kwa karibu na nikisha ona tayari amezidiwa nitamchukua na kumpeleka chumbani halafu nitazima taa na kumuacha amelala.Wewe utaingia chumbani na utalala naye.Utafanya kila uwezalo ili ufanya naye mapenzi.kwa kuwa hizi ni siku zako za hatari kama ulivyoniambia basi nina hakika kabisa kwamba ukifanikisha kufanya naye mapenzi utashika mimba na mpango wetu utakuwa umefanikiwa.Najua atakapostuka asubuhi na kukuta umelala naye atapandwa na hasira lakini utajitetea kwamba ulikuwa umelewa na hukuwa ukielewa chochote na ndiyo maana ukajikuta mle chumbani .” akasema Patricia “ Patricia I’m so scared” akasema Doreen kwa wasi wasi.Patricia akavuta pumzi ndefu na kusema “Nafahamu hilo Doreen hata mimi ninaogopa vile vile lakini hakuna namna nyingine lazima tufanye hivyo.” Akasema Patricia halafu wakarejea tena katika sherehe na moja kwa moja Patricia akaenda katika meza ya vinywaji akachukua chupa ya pombe kali na kwenda nayo katika meza aliyokuwa amekaa Elvis na rafiki zake.Gentlemen hii ni zawadi yangu kwenu” akasema Patricia na kuiweka mezani ile chupa ya pombe kali. “ Wow ! Whazard !..akasema moja wa marafiki wa Elvis kwa furaha.Patricia akatabasamu na kuifungua pombe ile na kuanza kuimimina katika glasi. “ I’m not going to take that.Its too strong for me” akasema Elvis.Patricia akamfuata akambusu na kumnong’oneza sikioni. “ My love this is my gift to you so you have to drink it .I want all of us to drink it “ akasema Patricia huku akiendelea kumimina pombe ile katika glasi halafu kila mmoja akashika glasi yake mkononi halafu wakagonganisha na kumtakia Patricia maisha marefu yenye furaha.Baada ya kama dakika kumi hivi Elvis akainamia meza.Hakuwa akijiwezatena.Tayari alikwisha lewa kupindukia “ Ngoja nimpeleke Elvis chumbani akapumzike” akasema Patricia huku akimuinua Elvis na kumsaidia kutembea kuelekea chumbani.Elvis alikuwa amelewa sana na walipofika tu chumbani akajitupa kitandani kama furushi .Patricia akamvua nguo na viatu akamlaza vizuri na haikuchukua muda mrefu Elvis akaanza kukoroma Patricia akatabasamu akazima taa na kutoka “ Now its time” akasema Patricia na kumfuata Doreen. “Tayari nimekwisha mpeleka chumbani na hafai kwa usingizi.Tusubiri muda kidogo halafu utaenda chumbani .Mimi nitajifanya nimelewa sana na nitalalala sebuleni” akasema Patricia halafu wakaendelea na vinywaji na ilipotimu saa saba za usiku Patricia akamfanyia ishara Doreen aelekee chumbani .Doreen aliondoka pale shereheni huku akionekana kuyumba kwa kuzidiwa na kilevi.Kila aliyemuona aliamini kwamba alikuwa amelewa sana.Doreen akaingia ndani na kutazama kila upande kuhakiki kwamba hakuna mtu yeyote mle ndani halafu akaelekea moja kwa moja katika mlango w a chumba cha akina Elvis.Taratibu akakinyonga kitasa cha mlango na kuingia ndani.Taa ya chumbani ilikuwa imezimwa lakini chumba kilikuwa na mwanga hafifu wa kumuwezesha kuona uliotoka katika taa iliyokuwa nje.Kwa hatua za taratibu Doreen akatembea hadi kitandani na kumshuhudia Elvis akiwa amelala fofofo.Mapigo ya moyo yalikuwa yakimuenda kwa kasi ya ajabu.Mwili ulikuwa unamtetemeka. Ouh gosh ! This is too hard for me but then I have to do it” akawaza Doreen huku akimtazama Elvis pale kitandani “ If you love me and you value our friendship you are going to help me.I trust you so much that’s why I’ve chosen you.Naomba unisaidie Doreen.Ninateseka sana mwenzio.” Maneno haya ya Patricia yakamjia tena kichwani “ I have to help her.Nilikubali kumsaidia na lazima nifanye hivyo” akawaza Doreen akavua viatu na kupanda kitandani akajifunika shuka na kumkumbatia Elvis “ I must do it” akawaza Doreen halafu akaanza utundu wa kuyaamsha mashetani ya Elvis. Wakati Doreen akiwa chumbani na Elvis,wageni wachache waliobaki nao wakaaga na kuondoka wakabaki Patricia na mtumish wao wa ndani .Patricia akaenda sebuleni na kujitupa sofani.Akaijkunja mikono yake na kuiweka kifuani.Alikuwa na wasi wasi mwingi kuhusiana na inachoendela chumbani kati ya mume wake na rafikiye Doreen. “ I’m so scared whats happening in there.Ninafanya jambo la hatari sana kumuacha mume wangu alale na mwanamke ambaye ni rafiki yangu kipenzi.Ninamuamini vipi Doreen kama yuko salama na hana maambuki ya hili gonjwa letu la siku hizi au hata magonjwa mengine? Ni vipi kama atampa Elvis penzi la kiwango cha juu na kumfanya anogewe na kutaka tena na tena? Ni vipi kama Doreen naye atanogewa na kutaka kuendelea kwa siri na Elvis s ….ouh No ! hawezi kufanya hivyo.Ninamuamini sana Doreen.Ingawa wanadamu hawaaminiki lakini sina namna nyingine ya kufanya .Nataka Elvis apate mtoto.Nataka awe na furaha kwa kupata mtoto hata kama ni kwa mwanamke mwingine kwa sababu sina uwezo wa kumzalia mtoto.Lakini hata kama akizaa na mwanamke mwingine lazima awe ni mwanamke ninayemjua na kumuamini ili isije ikatokea akanipora mume wangu ninayempenda sana na ndiyo maana nikamchagua Doreen.Ni rafiki yangu wa muda mrefu,tunapendana na kuaminiana sana.Nina hakika Doreen amekubali kunisaidia kwa moyo mmoja” akawaza Patricia n a kujilaza sofani Doreen alijifunika shuka huku akiwa na uoga mwingi.Mwili ulimsisimka alipogusana na Elvis. “ Ninaogopa sana kwa jambo hili ninalotaka kulifanya.Lakini nimekwisha amua kulifanya na tayari niko kitandani na mume wa rafiki yangu.Sina ujanja tena,I have to do it” akawaza Doreen halafu akaunyoosha mkono wake na kuanza kumpapasa Elvis kifuani.Akapatwa na msisimko wa aina yake,akafumba macho na kuhisi raha ya ajabu sana “ Nimemtamani Elvis kwa muda mrefu sana.Ni mmoja kati ya wanaume wanaonivutia na kunisisimua sana kila nikimuona.Kwa kiasi Fulani huwa ninamuonea sana wivu Patricia kwa kumpata mwanaume kama huyu ambaye kila mwanamke ana ndoto za kuwa naye.Siamini kama leo niko naye kitandani japo si kwa ridhaa yake lakini ninahisi raha ya ajabu.” Akawaza Doreen huku akiendelea kumpapasa Elvis .mwili wote ulimsisimka na tayari mzuka ulikwisha mpanda na alitamani sana kufanya mapenzi na Elvis.Taratibu akaupeleka mkono wake hadi katika bukta aliyovaa Elvis,akaishika na kuishusha chini hadimagotini halafu akaitoa nguo ya ndani ya Elvis na kuingia ikulu.Alisisimkwa sana pale mzee alipokasirika na kusimama kwa hasira.Mara Elvis akageuza kichwa,Doreen naye akastuka na kuacha alichokuwa anakifanya.Kwa sauti ya uchovu na ulevi,Elvis akasema “ Patricia my angel,I’mso tired today,tutafanya kesho,.Niache nipumzike.” Akasema Elvis kwa suati ya kilevi na kugeukia upande wa pili .Baada ya Elvis kuanza kupitiwa na usingizi Doreen akaanza tena utundu wake lakini pamoja na jitihada zake zote bado Elvis hakuwa tayari kufanya mapenzi usiku ule. “ Juhudi zangu zote zimeshindikana.What am I going to do? Ina maana kutapambazuka bila ya kufanya kile kilichonileta hapa? Akajiuliza Doreen “ hapana lazima nifanye kila linalowezekana kabla hakujapambazuka.Nina hamu sana na Elvis kwani tayari mashetani yangu yamekwisha panda.Ni muda mrefu sijakutana na mwanaume.kwa sasa ngoja kwanza nimuache alale na baadae ulevi ukianza kumtoka lazimanihakikishe nimetimiza malengo yangu.Hakutapambazuka leo bila kufanya mapenzi na Elvis.Gosh mwanaume huyu ni mzuri sana jamani I wish angekuwa ni mwanaume wangu.Kwa bahati mbaya sana watu kama hawa huwa hawatupati watu kama sisi.Kitu gani alimpendea Patricia mwanamke ambaye hana hata uwezo wa kumzalia watoto? Lakini anyway ngoja niache kuwaza hayo mambo,Patricia ni rafiki yangu na amenitaka nimsaidie.Ngoja nimsaidie ” Akawaza Doreen na kugeuka akaupeleka mkono wake kifuani kwa Elvis na kumkumbatiaakafumba macho.Alijiona kama yuko katika sayari nyingine ******************* Kengele ya saa ndogo iliyoko katika meza ndogo iliyo pembeni mwa kitanda,ikalia na kumstua Elvis toka usingizini.Ni saa kumi na nusu za alfajiri.Muda huu Elvis huamka kwa ajili ya kufanya mazoezi mepesi ya viungo.Akainuka na kukaa kitandani akainama akashika tama.Alihisi kichwa kizito sana. “ leo siwezi kufanya mazoezi.Ngoja nipumzike.Jana nilikunywa sana pombe.Sijui kwa nini nilikunywa pombe na kulewa namna ile,si kawaida yangu.” Akawaza na kujitupa tena kitandani .Hakuwa na usingizi akageuka na kumkumbata Doreen akidhani ni mkewe patricia. jana usiku nakumbuka Patricia alikuwa ana hamu sana na mimi lakini nilishindwa hata kumpatia haki yake kutokanana kuzidiwa kwa ulevi.Najua atakuwa aliteseka sana usiku .Ngoja nijikongoje walau nimpatie hata mzunguko mmoja kumkata kiu yake ya jana” akawaza Elvis halafu akaanza kumpapasa katika sehemu mbalimbali za mwili wake.Bado chumbani hakukuwa kumewashwa taa.Kulikuwa na mwangaza mdogo uliotoka katika taa iliyokuwa karibu na dirisha. Kadiri Elvis alivyoendelea kumpapasa Doreen ndivyo damu ilivyozidi kumchemka.Doreen ambaye tayari alikwisha amka ,akatoa migumo na kuzidi kumpandisha mzuka Elvis.Akamvuta kwake na kumkumbatia kwa nguvu akaanza kumporomoshea mabusu mfululizo.Ikulu ya Elvis ilikuwa imechachama na tayari mzee alikuwa amefura kwa hasira. “I have to use this chance.Siwezi kuipata tena nafasi kama hii” akawaza Doreen na bila kupoteza muda akaishika na kuielekeza mahala husika. Alitaka kuwehuka kwa raha aliyoisikia pale mzee alipoanza kuzama taratibu.Akatoa ukulele ambao ulimstua Elvis.Akajinasua na kwenda kuiwasha taa. “ Ouh Mungu wangu !!!.....akasema Elvis kwa mstuko huku akihema kwa nguvu.Hakuamini alichokiona kitandani.Aliingiwa na hofu kubwaThis cant be..Doreen !!..akasema Elvis kwa sauti ndogo “ How it happened? Akajiuliza huku bado akiendelea kumshangaa Doreen aliyekuwa amekaa kitandani amejifunika shuka sehemu za kifuani macho yake yakiwa yamejaa aibu. “ Usiku wote nimelala na Doreen.Ouh My God..!! where is my wife? Patricia yuko wapi? .jambo hili limetokeaje? akaendelea kujiuliza Hakutaka kuendelea kupoteza muda hadiPatricia atokee , akamfuata Doreen pale kitandani “ Elvis ,I’m sorry…akasema Doreen alipomuona Elvis akimfuata pale kitandani huku uso wake ukionekana kuwa na hasira kali Doreen why are you here? Akauliza “ Hata mimi sifahamu Elvis,nimejikuta nikiingia humu chumbani.Nilikuwa nimelewa sana jana na nikamwamba Patricia kwamba ninakwenda kulala akanielekeza chumba cha kulala .Nilipotea chumba na kujikuta nikiwa humu.Samahani sana Elvis.” “ Doreen kama ulizidiwa na kilevi na ukapotea chumba Kwa nini ulitaka kufanya mapenzi na mimi? Ulimfahamu mtu uliyetaka kufanya naye mapenzi? Akauliza Elvis.Doreen akainama chini kwa aibu “ Answer me Doreen,kwa nini ulitaka kufanya nami mapenzi jana ? Elvis I’m sorry.Haikuwa dhamira yangu,nilikuwa nimelewa sana na nilipostuka nikakuta kuna mtu pembeni yangu nikapandwa na hisia nikajikuta nikitamani,I’m so sorry Elvis, please don’t tell Patricia about this.” akasema Doreen huku machozi yakimtoka.Elvis akamtazama na kusema “ Ok go now kabla Patricii hajaingia humu chumbani.Chumba cha wageni ni cha tatu mkono wa kulia kutoka hiki.Go now” akasema Elvis.Kwa aibu Doreen akainuka.Bado alikuwa mtupu.Akaichukua nguo yake na ndani na kuivaa.Mwili wote wa Elvis ukamsisimka alipoushuhudia mwili ule mwororo wa Doreen. she’s so sexy !! akawaza Elvis akimshuhudia Doreen akivaa nguo zake. “ Go now,kuna watu wamelala hapa wasije wakaamka na kukushuhudia ukitoka humu chumbani .” Akasema Elvis huku akiufungua mlango taratibu na kuizima taa ya kwenye varanda ili Doreen asionekane. “ Its clear,go now” akasema Elvis.Doreen akatoka na kuingia katika chumba alichoelekezwa .Elvis akaenda kukaa kitandani alikuwa na mawazo mengi sana “ Sielewi jambo hili limetokeaje.Ni ulevi gani huo aliokuwa nao Doreen hadi afikie hatua ya kupotea na kuja kulala chumbani kwangu? Tena akadiriki hata kuniamsha hisia ili tufanye mapenzi.Hapana siamini kabisa kama kwelialikuwa amelewa.Mtu aliyelewa na kuhsindwa kujitambua hadi kupotea mahala anakokwenda asingeweza kunifanyia mambo kama aliyonifanyia jana Doreen.Inaonekana alikuwa amedhamiria kufanya vile.Patricia yuko wapi ? Anafahamu chochote kuhusiana na alichokifanya rafiki yake? Akajiuliza na kuikumbuka picha ya Doreen akivaa nguo yake ya ndani “dah ! pamoja na yote lakini Doreen anasisimua sana .Kila nikimfikiria nahisi mwili unanichemka.Ni mwanamke aliyeumbwa hasa akaumbika.Dah ! nashukuru niliwahi kustuka na sikuendelea zaidi na mchezo ule.Nina hakika kwa uziri aliokuwa nao yule mwanamke kama ningeendelea basi ningekuwa katika matatizo makubwa kwani ningetamani kuendelea tena na tena .Uzuri wake ni kama ua lenye harufu nzuri inayowavuta nyuki kuling’ang’ania .Hili ni jaribu kali kuwahi kulishinda katika maisha yangu”akawaza Elvis huku akihisi ikulu kukiwa hakuna usalama kila alipoikumbuka picha ile ya Doreen akiwa mtupu “ Doreen ananitia majaribuni. No ! I cant do that.I love my wife so much.Niliapa kumpenda Patricia na sintamsaliti hata siku moja ,mbaya zaidi na rafiki yake mkubwa.” Akawaza Elvis na kutoka mle chumbani akaelekea sebuleni kumtafuta mke wake.Patricia alikuwa amelala sebuleni katika sofa huku kukiwa na chupa za pombe pembeni yake “ masikini Patricia unywaji gani huu wa pombe? akawaza Elvis huku akimuinamia na kumbusu “ nadhani alikunywa pombe nyingi jana kutokana na furaha aliyokuwa nayo na vile vile ili kupunguza mawazo ya jambo linalomsumbua sana kwa sasa la kukosa mtoto.Patricia hatakiwi kuumiza kichwa chake kwa sauala hili kwani nimekwisha muhakikishia kwamba hakuna yeyote mwenye mamlaka ya kumuuliza chochote kuhusiana na mtoto.Nilimuoa huku nikijua kabisa kwamba hana uwezo wa kupata mtoto na nimekubaliana na hali hiyo kwa sababu ninampenda.Kama mimi ambaye ndiye mumewe ninakubaliana na hali yake ,basi si mama wala mtu mwingine yeyote ambaye ana ruhusa ya kuingia katika ndoa yetu na kuanza kudai mtoto.Hakuna mahala tumeandikiana mkataba kwamba baada tu ya ndoa nitawazawadia mtoto.”akawaza Elvis huku akimuamsha mkewe. “ patricia..!! Patricia.!!!..” akaita Elvis.Patricia akafumbua macho. “ Ouh Elvis ! akasema kwa sauti ya uchovu.Bado alionekana kulemewa na ulevi. “ Wake up Patricia.Wake up my love,kumepambazuka.Twende ukalale chumbani” akasema Elvis huku akimsaidia kuinuka wakaelekea chumbani “ Elvis kichwa kinaniuma sana.Nilikunywa pombe nyngi jana” akasema Patricia “ Mkewangu ,usirudie tena kunywa pombe nyingi kiasi hiki.Hata mimi jana nilikunywa na kulewa sana na sijui hata nilifikaje kitandani” “ Mimi ndiye niliyekuleta baada ya kukuona umezidiwa na haujiwezi “ akasema Patricia “ Ahsante sana mke wangu.Anyway kunywa maji kwanza halafu endelee kulala ujipumzishe.Ngoja nikakuandalie supu” akasema Elvis na kutoka akaelekea jikoni.Patricia alijilaza pale kitandani akiwaza.. “Sijui kama mambo yalienda kama tulivyokuwa tumepanga.Natamani kujua kama mpango wetuulifanikiwa.Natamani kufahamu nini kilitokea baada ya Elvis kuamka na kujikuta akiwa amelala na Doreen? Ingawa uso wake hauonyesh kama kuna jambo la tofauti lililotokea lakini kuna aina Fulani ya wasi wasi katika sauti yake. Ngoja nijipumzishe kwanza nitapata jibu kwa Doreen baadae” Elvis alikuwa jikoni akimuandalia supu mkewe lakini bado tukio la kujikuta akiwa amelala na Doreen kitanda kimoja tena wakiwa watupu liliendelea kumtesa sana. “ Bado naendelea kujiuliza kuhusiana na tuko lile .Bado sielewi nia ya Doreen ilikuwa nini.Inawezekana Doreen akawa ananitamani sana na alipomuona Patricia amezidiwa na kilevi akaamua kuingia chumbani kwangu kwa lengo la kutaka kufanya mapenzi nami? .lakini kwa nin I afanye hivyo wakati akifahamu kabisa kwamba mimi ni mume wa rafiki yake kipenzi? Ingekuwaje iwapo Patricia angemkuta chumbani kwetu? Utetezi wake eti kwamba alikuwa amelewa na akajikuta mle chumbani hauingiiakilini.Mtu aliyelewa kiasi cha kutojitambua aliwezaje kuvua nguo zote na kufanya juhudi za kutaka kufanya mapenzi na mtu aliyemkuta hapo kitandani bila kufahamu mtu huyo ni nani? Bado hainiingia akilini kabsa..Nina imani kabisa Doreen alidhamiria kufanya vile.Dah ! wanawake” akawaza Ninaanza kuwa na mshaka kidogo kuhsusiana na tukio hili.Juzi Patricia aliniambia kwamba anataka nipate mtoto na akanipa uhuru wa kuzaa na mwanamke mwingine yeyote nitakayeona anafaa.Nina wasi wasi huu usije ukawa ni mpango wake nilale na rafiki yake ili nizaie naye.Kama ni hivyo atakuwa amekosea sana.Siko tayari kufanya hivyo.Ninampenda jinsi alivyo na kama ni mateso yake basi tutayabeba sote.Siko tayari kumsaliti mke wangu eti kwa kigezo cha mtoto.Niliapa siku ile kanisani kwamba niko tayari kumpenda katika hali zote,na ndivyo ninavyofanya.Hata nikishinikizwa na dunia nzima siko tayari kumkosea heshima mke wangu na kwenda kuzaa nje ya ndoa yangu.Kama mwanamke ninayempenda hana uwezo wa kupata mtoto huo ni msalaba wangu na lazima niubebe.Hakuna njia ya mkato hapa.” Akawaza na kwa mara nyingine picha ya Doreen akiwa mtupu ikamjia “ Nitaifutaje picha hii kichwani kwangu? naona kama inajirudia kwa kasi kubwa kila dakika.Sitaki jambo hili linitie majaribuni.Sitaki picha ile ya Doreen akiwa mtupu iendelee kukitawala kichwa changu na kunisababishia niwaze mambo mengine mabaya.Lakini hata hivyo mwenyezi Mungu anastahili sifa kwa uumbaji wake.Doreen ni mwamanke aliyependelewa uzuri wa kipekee kabisa.Japokuwa nimeoa na ninaishi kiapo change cha ndoa na siwezi kutoka nje ya ndoa yangu lakini lazima nikiri kwamba Doreen ni mwanamke mwenye mvuto wa ajabu sana na anayeweza kumfanya mwaume yeyote afanye jambololote kumpata.Amenifanya nikasisimka mno .Dah ! .” akawaza Elvis. ********************







Ni saa tano za asubuhi,siku ya jumapili bado Patricia na Elvis wako kitandani wakijipumzisha kutokana na uchovu wa siku iliyotangulia.Wote walikunywa pombe nyingi katika sherehe ya kuzaliwa Patricia.Mlio wa simu liyokuwa ikiita ndio uliomstua Elvis akainuka na kwenda mezani.Ilikuwa ni simu ya Patricia iliyokuwa ikiita.Katika kioo cha simu iliandika “ Dharura kaziniElvis akaichukua simu ile na kumuamsha mke wake “ mmhh my darling,niache nilale kidogo .Nimechoka sana” akasema Patricia huku macho yake yakionyesha wazi kwamba alikuwa na uchovu mwingi “ Pokea simu hii darling,imepigwa katika namba ya dharura ya kazini kwako” akasema Elvis.Neno dharura likamstua Patricia akainuka haraka na kuichukua simu akabonyeza kitufe cha kupokelea “ Hallow “ akasema “ Dr Patricia kuna dharura imetokea” “ Jambo gani limetokea Amanda?akauliza “ Cindy amezinduka” “ Cindy?!! Patricia akashangaa Ndiyo amezinduka sasa hivi” “ Anaweza kuongea? Anajifahamu? “ Ndiyo anafahamu zake na anaweza kuongea japo anasikika kwa mbali ” “ Ok nakuja sasa hivi” akasemaPatricia na kukata simu .Akavuta pumzi ndefu “ Kuna nini kimetokea? Akauliza Elvis “ Kuna mgonjwa mmoja ambaye aliletwa pale hospitalini kwetu akitokea hospitali ya taifa ya Muhimbili akiwa hana fahamu.Kwa mujibu wa taarifa iliyotoka Muhimbili ni kwamba mwanadada huyo aliokotwa na wasamaria wema na kupelekwa pale akiwa hana fahamu .Baada ya kumchunguza wakaamua kumleta pale kwetu ili tumfanyie uchunguzi wa kina kuhusianana nini kinamsumbua kichwani” “ Nini kilimpelekea apoteze fahamu? Akauliza Elvis “ Kwa mujibu wa uchunguzi tuliomfanyia,alipoteza fahamu kwa sababu ya kupigwa sana hasa sehemu za kichwani.Inaonekana watu waliompiga walikuwa na lengo la kumuua.” “ Dah jamani dunia hii imejaa watu makatili sana”: akasema Elvis “ Kwa muda wa miezi miwili amekaa bila fahamu na katika muda huo wote hakuna hata ndugu yake mmoja aliyejitokeza ndiyo maana nikaamua kumpa jina la Cindy” akasema Patricia “ So are you going there? Akauliza Elvis Yes ! I have to go there” akasema Patricia “ I’ll go with you.Umechoka sana na siwezi kukuacha ukaendesha gari ukiwa katika hali hii.Nitakupeleka kazini na kukurudisha” akasema Elvis .Wakaingia bafuni kuoga kisha wakaelekea katika chumba cha kulia chakula wakapata kifungua kinywa “ Sylvie,Doreen bado hajaamka? Patricia akamuuliza mtumishi wao wa ndani “ Aliamka ,akaomba kahawa kisha akarudi tena kulala” akajibu Sylvie “ Ok ngoja nikamuangalie kabla hatujaondoka.Jana alikuwa amelewa sana” akasema Patricia na kuinuka akaelekea katika chumba cha wageni alikolala Doreen.Bila kubisha hodi Patricia akaingia chumbani na kumkuta Doreen amejilaza kitandani “ Bado umelala? Inaonekana shughuli ya jana ilikuwa nzito sana” akasema Patricia huku akitabasamu.Doreen akainuka na kunyoosha mikono akamfanyia ishara Patricia akae kitandani “ Enhee nipe habari shoga.Mambo yalikwendaje? “ Mhhhhh..!!!!” Doreen akaguna “ Mbona unaguna? “ Mambo hayakwenda kama tulivyopanga” akasema Doreen “ What happened? Doreen akainuka na kukaa kisha akasema ” Nilijitahidi sana kadiri niwezavyo bila mafanikio.Elvis alikuwa amelala fofofo.Alikuwa amezidiwa na kilevi” “ Dah ! So what happened? Alikuona? “ Nilijikuta nimepitiwa na usingizi na nikastuka asubuhi Elvis akiwa amewasha taa ananishangaa.Shoga ninasikia aibu sitaki hata kuonekana huko nje hadi atakapoondoka.Sijui nitamtazamaje Elvis usoni “ “ Alisemaje alipokuona? Akauliza Patricia huku sura yake ikionyesha wasiwasi mwingi “ Alistuka sana.Sura yake ilipata wasiwasi mkubwa.Hakuamini kilichotokea.Nilimuomba samahani nikaondoka haraka kuja huku.Patricia tumefanya jambo la aibu sana.Nasikia aibu mno” akasema Doreen “ samahani sana Doreen kwa kukuingiza katika jambo hili” “ Usijali Patricia ,yote hii ilikuwa ni katika kutafuta suluhisho la matatizo yako.” Patricia akakaa kimya akafikiri na kusema “ So what are we going to do now? Akauliza “ I don’t know Patricia.I’m so scared to do it again” akasema Doreen.Patricia akainama akatafakari na kusema “ Ahsante Doreen kwa kujitolea kunisaidia.kwa sasa naelekea hospitali kuna dharura imetokea.Nitakuja kukuona jioni tutaongea zaidi”akasema Patricia “ Elvis naye anatoka? Ninaogopa hata kumtazama usoni” akasema Doreen “ Elvis naye anaondoka.Ndiye anayenipeleka hospitali.” “ Ok hata mimi ngoja nijiandae niondoke niende nyumbani nikapumzike .Leo sintatoka kabisa” akasema Doreen Patricia akatoka mle chumbani akamuelekeza mtumishi wake kazi za kufanya kisha yeye na mumewewakaingia garini na kuondoka kuelekea hospitali ‘ Patricia ,hivi Doreen anaishi na nani?akauliza Elvis.Patricia akastushwa kidogo kwa swali lile “ Unauliza Doreen anaishi na nani..? “ Ndiyo.Doreen anaishi na nani? Ana mume? “ Hana mume anaishi peke yake.Kwa nini umeuliza? Nilihitaji tu kufahamu kwa sababu nilishangaa uliponiambia kwamba alilala pale nyumbani nikajiuliza angewezaje kufanya hivyo kama tayari ana mume wake” Patricia akacheka kidogo na kusema “ Doreen hana mume na ndiyo maana yuko huru kufanya jambo lolote” “ Ok sawa.Uliionaje sherehe ya jana? “ Sherehe ilipendeza sana kiasi kwamba siwezi hata kuielezea.Japokuwa matatizo madogo madogo kama ya kulewa kupitiliza yalikuwepo lakini kwa ujumla wake shertehe ilikuwa nzuri sana.” “ jana ulikunywa pombe nyingi sana” akasema Elvis Kweli nilikunywa sana.Baada ya wageni kuondoka tulibaki tunaendelea kunywa mimi na Doreen na sikumbuki hata mwenzangu aliondoka saa ngapi kwenda kulala.Sitaki tena kurudia unywaji pombe wa namna ile” akasema Patricia.Elvis akacheka kidogo na kusema’ “ Kitugani kilikufanya unywe pombe namna ile? “ Ni furaha tu niliyokuwa nayo jana.Nilitaka nifurahi kwa sababu kwa siku za hivi karibuni kichwa changu kimekuwa na mambo mengi sana kwa hiyo jana nikaona ni bora niitumie siku ile kujisahaulisha mambo yote na kufurahi.” Akasema Patricia.Elvis akageuza shingo na kumtazama mkewe Patricia naomba tafadhali usiwaze chochote kuhusiana na mambo yale aliyokwambia mama.Niachie mimi suala hili nitalishughulikia kama nilivyokuahidi.” akaema Elvis.Patricia akatabasamu bila kusema chochote safari ikaendelea Walifika hospitali Patricia akampeleka mumewe sehemu ya kupumzikia akamuomba amsubiri pale “ I must do something” akawaza Elvis halafu akachukua simu yake na kuzitafuta namba za simu za Doreen akampigia “ Hallow Elvis” akasema Doreen baada ya kupokea simu “ Doreen nahitaji kukuona ,umeshaondoka hapo nyumbani? Nimeshaondoka niko njiani kuelekea nyumbani kwangu.Kuna tatizo lolote Elvis? “ Hakuna tatizo ila nahitaji kukuona.We need to talk” “ Sawa Elvis,unataka tuonane wapi? Nielekeze sehemu unakotaka tukutane” “ Usisumbuke Doreen ninakuja nyumbani kwako” akasema Elvis huku akishuka ngazi na kuelekea lilipo gari lake. “ Najua Elvis anataka kuongelea kuhusiana na lile tukio la jana.Niliuona uso wake namna alivyokuwa akinitazama.Patricia ameniingiza katika mgogoro mkubwa.I’m so stupid.Nimekubali kufanya jambo kama lile na kujidhalilisha namna ile.Ninaona aibu sana na sijui nitamtazamaje Elvis”akawaza Doreen lakini maraakatabasamu baada ya kukumbuka kitu “ Pamoja na mambo kutokwenda kama tulivyotaka lakini kuna jambo nililiona usoni kwa Elvis.Japokuwa alistuka sana aliponiona lakini alikuwa ananitamani.Kuna kila dalili kwamba Elvis alitamani sana kufanya nami mapenzi lakini alikuwa akimuogopa mke wake.Yawezekana hilo ndilo jambo linalomleta kwangu.” Akawaza Doreen na kukumbuka picha ya tukio la jana “ Mwili wangu ulipogusana na Elvis nilipatwa na msisismko wa aina yake.Nilihisi ni kama nimelala na mwanaume wangu.Elvis ni mwanaume anayesisimua sana.Tayari tulikwisha anza kufanya mapenzi kama nisingepiga ule ukulele kwa raha ya ajabu niliyoisikia basi asingestuka..Sijui nitafanya nini kumpata Elvis tumalizie pale tulipoishia http://deusdeditmahunda.blogspot.com/.Ouh jamani sijui kwa nini mawazo kama haya yananijia.Lakini yote haya ameyataka Patricia mwenyewe ” akawaza Doreen na kukumbuka msisimko alioupata wakati akizichezea nyeti za Elvis. “ Ni muda mrefu nilimtamani Elvis lakini sikuwa na mawazo yoyote kwamba siku moja mimi na yeye tunaweza kulala kitanda kimoja tena katika hali ya utupu.Elvis ni mume wa rafiki yangu kipenzi na siku zote nimeliheshimu hilo..Ni Patricia mwenyewe ndiye anayenisbabishia niwaze mawazo ya namna hii baada ya kunitaka nilale na mumewake.Japokuwa Elvis ni mwanaume ninayemtamani sana lakini sikuwa tayari kulala naye lakini Patricia alinilazimisha sanahadi nikakubali na baada ya Elvis kuuona utupu wangu sina cha kuogopa tena.Lazima ndoto yangu itimie.Lazima nitembee naye.” akawaza Doreen wakati akikata kona kuingia nyumbani kwake .Martha mtumishi wake wa ndani alimfungulia geti akaingiza gari halafu akaelekea moja kwa moja chumbani kwake ambako alioga haraka haraka na kujiandaa kwa ajili ya kukutana na Elvis.Alipomaliza kujiandaa akapanda kitandani na kujilaza.Picha ya tuko la jana haikuacha kumjia kichwani. Nina hakika kinachomleta Elvis ni kuhusianana tukio la jana tu.yawezekana anataka kuja kuende………….”alikatishwa mawazo yake na mtu aliyebisha hodi katika mlango wake.Akainukana kwenda kuufungua Alikuwa ni mtumishi wake wa ndani “ Dada yule mgeni uliyesema akija nimkaribishe sebuleni tayari amekwisha fika” akasema Martha mtumishi wa ndani wa Doreen “ Ok Martha mpeleke katika chumba cha maongezi” akasema Doreen kisha akaufunga mlango wake na kuuegemea.Mapigo ya moyo wake yalibadilika na kuanza kwenda kasi “ Naona aibu sana kukutana tena ana kwa ana na Elvis.” Akawaza halafu akaenda katika meza yake ya vipodozi akajitazama usoni “lakini kwa nini niogope w akati ni mke wake ndiye aliyesababisha haya yote? Sikuwa nikihitaji jambo kama hili litokee lakini Patricia amelazimisha hadi limetokea.Elvis amekwisha uona utupu wangu na nina hakika hataacha kunifuata kama nyuki .Potelea mbali litakalotokea nalitokee tu siwezi kuendelea kumuogopa ,kama akitaka penzi mimi nitampatia tu kwani tayari nimeruhusiwa na mke wake na hata hivyo Elvis ni mwanaume niliyemtamani siku nyingi sana.” Akawaza Doreen kisha akafungua mlango akatoka na kuelekea katika chumba cha maongezi aliko Elvis Elvis ! karibu sana” akasema Doreen huku akijilazimisha kutabasamu “ Doreen samahani sana kwa kukusumbua .Najua muda huu ulikuwa unapumzika” “ Usijali Elvis,karibu sana.” Akasema Doreen huku akijitahidi kuyaficha macho yake yasikutane na yale ya Elvis. “ Uhhm Doreen nimelazimika kuja kukuona ili tuzungumzie suala lile lililotokea jana usiku.Bado ni….” Akaanzisha mazungumzo Elvis lakini Doreen akamkatisha “ Elvis utanisamehe sana kwa tukio lile la aibu.Hata mimi mwenyewe sielewi lilitokeaje.Naomba samahani sana Elvis na tafadhalinaombausimweleze Patricia “ akasema Doreen “ Doreen najua ni pombe mlizokunywa jana ndizo zilizosababisha jambo lile litokee.Sote tulikuwa tumelewa sana jana.Lakini ninachojiuliza ni kwa nini ukaacha vyumba vingine vyote na kuingia kwangu? Ni kwa nini ukanivua hadi nguo yangu ya ndani na kunipandisha hisia ili tufanye mapenzi? Kwa nini ulifanya vile? Doreen ni sisi pekee tunaofahamu nini kilitokea na wala sintomueleza mke wangu kwa hiyo tafadhalinaomba unieleze ukweli,ni kweli ulikuwa umelewa au ulidhamiria kufanya vile? Niambie ukweli nitakuelewa Doreen “ akasema Elvis “ Elvis kusema ukweli sikuwa nikijitambua kutokana na pombe nilizokuwa nimekunywa.Baada ya sherehe kumalizika na wageni wote kuondoka nilikuwa nimelewa sana na kwa hiyo Patricia akanishauri kwamba nilale pale pale nyumbani.Tuliendelea kunywa pombe hadi usiku mwingi nikamwambia Patricia anionyeshe chumba nikalale lakini alikuwa amelewa hajitambui hivyo nikainuka mwenyewe na kuanza kutafuta chumba kilipo nikajikuta nimeingia katika chumba chenu.Elvis sina maelezo ya kutosha kulielezea jambo hili kwa sababu kuna mambo hata mimi sikumbuki yalitokeaje”akasema Doreen “ Natamani sana kukubaliana nawe Doreen lakini kitu ambacho hakiniingi akilini ni kwamba kama ulikuwa umelewa kiasi chakutojitambua kwa nini basi ukavua nguo zako zote na kuziweka sofani kisha ukapanda kitandani mtupu? Pale kitandani ulimkuta mtu amelala kwa nini ukaanza kumchezea kwa madhumuniya kufanya mapenzi? Akauliia Elvis.Swali lile likambabaisha Doreen akashindwa kujibu “Naomba unijbu Doreen.Ni kweli ulikuwa umelewa au ulidhamiria kufanya vile? Akauliza Elvis “ Elvis,..” Doreen akataka kusema kitu lakini akaogopa “ Tell me please” akasisitiza Elvis “ Naomba uniambie ulijisikiaje uliponiona asubuhi ni mimi ndiye niliyelala nawe na si mkeo Patricia? Elvis akamuangalia Doreen kwa mshangao mkubwa “ I was angry,very angry….” Doreen akatabasamu kidogo na kusema “ No Elvis,hukuwa umekasirika.Ulikuwa unamuogopa mkeo Patricia asijue .I saw your face.You needed it.You needed me ,right? Akasema Doreen na kumfanya Elvisi azidi kumshangaa. “ Doreen mambo gani hayo unayasema.Wewe ni rafiki mkuwa wa mke wangu,unadhani Patricia angesema nini endapo angekukuta chumbani kwake tena ukiwa mtupu? Halafu ulijua kabisa kwamba umelala kitandani na mume wa rafikiyako kipenzi na wakati nikijiandaa kufanya tendo la ndoa nikidhani niko na mke wangu wala hukuonekana kustuka.Ni wazi ulikuwa umedhamiria jambo lile litokee.Kwa nini Doreen.kwa nini ulitakakufanya vile? Kwanini ulitaka kumsaliti rafiki yako kipenzi? Akauliza Elvis.Doreen akamtazama na kuuliza “ Elvis why are you here? Akauliza Doreen huku akimsogelea Elvis. “ I’m here to find answers” akajibu Elvis “ No Elvis.You are not here for answers” akasema Doreen huku akimkaribia zaidi Elvis na kukigusisha kifua chake katika kifua cha Elvis na kuyafanya mapigo ya moyo ya Elvis yabadilike You are here because you need something.Tell me what do you want Elvis?Usiogope Elvis tuko hapa peke yetu,mkeo hayupo wala hakuna anayetuona.So tell me what do you want?” akasema Doreen .Elvis aliendelea kumtazama akashindwa aseme nini. “ Why are you doing this Doreen.” Akauliza Elvis “ Elvis mbona unauliza maswali mengi sana.Niambie bila kunificha ni kitu gani umekifuata hapa kwangu?Kama hutaki kuniambia basi nitakwambia .” Akasema Doreen na taratibu akafumba macho na kuusogeza mdomo wake karibu na mdomo wa Elvis,akambusu na ghafla Elvis kama mbogo majeruhi akamshika Doreen kwa nguvu na kuanza kunyonyana nadimi. Doreen tayari alipandisha mashetani yake ,alikuwa akihema haraka haraka.Hakutaka kupoteza muda akaanza kufungua vifungo vya shati la Elvis.Ghafla Elvis akakurupuka na kumsukuma “ Elvis,why? What happened? “ No I cant do this.I real cant” “ Elvis,usinifanyie hivyo tafadhali.Nafahamu umekuja kunifuata mimi.Sasa unaogopa nini? Hakuna atakayefahamu na wala mkeo Patricia hatajua lolote.Please Elvis I need you” akasema Doreen huku akimsogelea Elvis “ No Doreen stop.!..akasema kwa ukali Elvis huku akihema kwa nguvu. Walisimama kwa sekunde kadhaa wakitazamana kila mmoja akihema kwa nguvu.Vifungo vya nguo aliyokuwa ameivaa Doreen vilikuwa vimefunguka na hivyo kuifanya sehemu ya matiti yake mazuri kuonekana na kumpa wakati mgumu sana Elvis “ Hili ni jaribu kali sana.Sijui ni kitu gani hasa kilichonileta huku kwa Doreen.” Akawaza Elvis huku akiendelea kumtumbulia macho Doreen “ Elvis tafadhali naomba usiogope kitu.Nafahamu unanitaka lakini unaogopa.Hakuna atakayefahamu chochote kuhusiana na jambo hili.I need you and I’ll give you everything that you want hata vile ambavyo umeshindwa kuvipata kwa mkeo kwangu nitakupa” akasema Doreen .Kauli ile ikamstua kidogo Elvis akauliza “ Doreen,kuna jambo lolote ambalo Patricia amekueleza kwa siku hizi za karibuni? “ Jambo gani hilo? “ Hajakueleza jambo lolote kuhusiana na mambo ya ndani ya ndoa yetu? “ Kuna jambo Fulani alinieleza” ” Jambo gani? “ “ Ni kuhusiana na yeye kutopata mtoto” Elvis akashusha pumzi akamuangalia Doreen na kumuuliza “ Alikueleza sababu za yeye kutokupata mtoto? “ Ndiyo alinieleza kila kitu” Elvis Akakaa kimya kidogo kisha akasema siku chache zilizopita ,ndugu zangu wakiongozwa na mama walianza kuhoji kuhusiana na kwa nini toka tumeoana hadi leo hii hatujafanikiwa kupata mtoto.Hakuna anayefahamu ni kwa nini sisi hatuna mtoto hadi leo hii.” akanyamaza kidogo akatazama chini halafu akainua kichwa na kuendelea “ Kitendo cha ndugu zangu kuanza kuulizia kuhusiana na masuala ya mtoto kimemkosesha amani mke wangu .Juzi aliniambia kitu ambacho kilinishangaza sana.Aliniambia kwamba yuko tayari mimi nizae na mwanamke mwingine nje ya ndoa.Nilimkatalia kuhusiana na jambo hilo lakini hakuonekana kuridhika.Tukio lililtokea jana linanifanya nianze kuhisi kwamba yawezekana mlikuwa mmepanga litokee.Hiyo ndiyo sababu nimekuja hapa kwako ili niweze kuupata ukweli wa tukio lile.Ni kweli mlikuwa mmepanga na Patricia kwamba nilale nawe? Naomba usinifiche Doreen” akasema Elvis.Doreen alionyesha wasi wasi mwingi.Alishindwa ajibu nini.Kwa mbali macho yake yakaonekana kulengwa na machozi “ Elvis naomba nikwambie ukweli.” Akasema Doreen halafu akainama akafikiri kwa muda na kusema “ Elvis tafadhali naomba usikasirike lakini ukweli nikwamba lile lilikuwa ni tukio la kupangwa..Tulilipanga mimi na Patricia.” Ouh Mungu wangu !!akasema Elvis na kusimama akashika kichwa chake.Doreen akaendelea “ Patricia alinifuata akanieleza matatizo yake na namna anavyoteseka kwa kukosa mtoto.Aliniambia kwamba anataka uwe na furaha maishani mwako na furaha hiyo ingekamilika endapo tu ungekuwa na mtoto.Patricia anaogopa kwamba siku moja shinikizo toka kwa ndugu zako litazidi na utaamua kuzaa na mwanamke ambaye yeye hamfahamu na hivyo kuhatarisha ndoa yenu na kwa sababu anakupenda ndiyo maana akaona ni vyema kama atakupa nafasi ya kuweza kuzaa na mwanamke ambaye yeye anamuamini .Ulipokataa kufanya hivyo alikuja kwangu na kuniomba nimsaidie katika tatizo lake hili,.Aliniomba nizae nawe .Nilimuuliza kama uko tayari kwa jambo hilo akasema kwamba alikueleza lakini haukuwa tayari.Kwa upande wangu sikuwa tayari kufanya jambo kama hili hasa kutokana na namna tunavyoheshimiana lakini Patricia alinililia sana nikamuonea huruma na kukubali kumsaidia ndipo tulipopanga ule mpango na yakatokea yale yaliyotokea.Elvis naomba unisamehe sana,nilifanya vile kwa ajili ya kumsaidia rafiki yangu “ akasema Doreen.Elvis akamtazama kwa macho makali na kusema “ Siamini kama ni kweli mmefikia hatua hii.How could you do this?Mnafahamu madhara yake? Nilikwisha mwambia Patricia kwamba asiumize kichwa chake na jambo hili lakini hataki kunielewa,.What else should I do to prove to her that I love her with all my heart? Akasema Elvis kwa ukali.Jambo lile lilionekana kumchukiza mno. “ Elvis tulikuwa tunajaribu kutafuta suluhu ya tatizo hili.Cant you see how Patricia is suffering right now? Akasema Doreen naye sauti yake ilionekana kuanza kuwa kali “ so this is the solution? You are making things worse than solving the problem.” Akasema Elvis “ Elvis,Patricia loves you so much na ndiyo maana yuko tayari kufanya jambo kama hili kwa ajili ya kukupatia wwewe furaha.Do you think this is easy for her? Akauliza Doreen “ Nafahamu mke wangu ananipenda sana na lengo lake ni kuniona nikiwa na furaha lakini njia hii anayotaka kuitumia si sahihi hata kidogo.Mimi ninampenda kwa jinsi alivyo na wala suala la kukosa mtoto halipunguzi hata chembe moja ya upendo wangu kwake.Siku zote nimekuwa nikimuasa kwamba maneno mengi yatasemwa lakini anatakiwa awe mvumilivu .Kukosa mtoto si mwisho wa maisha” akasema Elvis.Doreen akamtazama kwa makini na kusema “ Hongera kwa msimamo huo lakini nina hakika moyoni mwako utakuwa ukiumia sana kwa kukosa mtoto japokuwa hutaki kuweka wazi.Nina hakika vile vile kwamba siku moja itafika utashindwa kuvumilia na utaamua kuzaa nje ya ndoa yako.Patricia tayariamekwisha liona hilo na ndiyo maana amekubali kwamba uwe na mtoto wan je ya ndoa lakini toka kwa mwanamke anayemfahamu na kumuamini na katika hilo amenichagua mimi.” akasema Doreen.Elvis akainama akafikiri na kusema “ Iwas there when it happened.Nilikuwepo na kushuhudia wakati Patricia anapoteza uwezo wa kuzaa.Nilisimama pamoja naye .Nilimpenda hata kabla ya matatizo yale kumkutana nitaendelea kumpenda siku zote za uhai wangu.Nilimuoa Patricia kwa sababu ninampenda kwa moyo wangu wote na siumizwi kwa hali yake ya kukosa mtoto kwa sababu nililifahamu jambo hili toka awali na nikawa tayari kukabiliana nalo.Kuhusu kuzaa mtoto na mwanamke mwingine hilo ni jambo ambalo sintaweza kulifanya.Sijali kama ni yeye anayetaka ama nani lakini siwezi kufanya hivyo.”akasema Elvis “ Kwa nini unafanya hivyo Elvis? Kwa nini hutaki kumsikiliza mkeo? Kwa nini hutaki kumuona Patricia akiwa na furaha? I beg you, do what she wants you to do and you can make her happy” akasema Doreen “ Ninampenda sana mke wangu na ndiyo maana sitaki kufanya hivyo anavyotaka nifanye kwa sababu ninafahamu lazima ataumia sana moyoni.Halafu ni kwa nini unanisisitiza sana kuhusu kufanya jambo hili? Akauliza Elvis “ Its because I’m a woman and I know how a woman feels pale anapundua kwamba hana uwezo wa kuzaa mtoto” akasema Doreen “ Think about it Elvis and if you want to do what your wife wants ,I’ll be right here waiting” akasema Doreen.Elvis akamtzama usoni akataka kusema jambo lakini kabla hajatamka chochote simu yake ikaita,akaitoa mfukoni akatazama mpigaji.Alikuwani Patricia mke wake “ Hallow Patricia” “ Elvis uko wapi? Mbona sikuoni hapa nilipokuacha? Akauliza Patricia Elvis akamtazama Doreen halafu akasema “ Nimetoka kidogo kuna mtu nimekuja kumtazama mara moja.Tayari umeshamaliza shughuli nije nikuchukue? “ Elvis kuna tatizo limejitokeza na hakuna mtu mwingine ninayeweza kumueleza zaidi yako” “ Tatizo gani Patricia? “ Ni kuhusiana na huyu msichana Cindy niliyekuja kumtazama.Ni kweli amezinduka na anaweza kuongea kidogo .Wakati niko naye nikimuhudumia kuna jambo amenieleza limenistua kidogo” “ amekueleza nini” akauliza Elvis. “ Ameninong’oneza kwamba anataka nimsaidie kumuondoa pale hospitali kwani maisha yake yako hatarini” “Maisha yake yako hatarini? Kivipi? “ Anadai kwamba kuna watu wanaotaka kumuua.Anasema kwamba endapo atagundulika yuko pale hospitalini basi lazima atauawa..” “ Amekueleza nini sababu ya maisha yake kuwa hatarini na ni akina nani wanaotaka kumuua? “ Hapana hajanieleza chochote.How are we going to help her? Elvis akafikiri kidogo na kusema “Nakuja hapo sasa hivi “ akasema na kukata simu “ Kuna tatizo limetokea? Akauliza Doreen “ Kuna mtu ana tatizo ngoja nikamuangalie” akasema Elvis Before you go” akasema Doreen.Elvis akageuka na kumtazama “ Nahitaji unijibu kwa nini umemdanganya mkeo alipokuuliza uko wapi? Kwa hukumweleza ukweli kwamba uko na mimi? “ Sitaki ajue kama nimekuja kwako na ninaomba Doreen suala hili Patricia asilifahamu” “ Usijali Elvis,hakuna atakayejua .Hata kama tutafanya Patricia hatajua chochote” akasema Doreen na kumstua kidogo Elvis “ Umesema nini Doreen? “ Nimesema kwamba muda wowote ukinihitaji niko hapa nakusubiri” akasema Doreen “ stop this Doreen.I have to go.We’ll talk later” akasema Elvis na kuondoka Namlaumu sana Patricia kwa kitu anachotaka kukifanya.Hakupaswa kufanya vile kwa sababu ninampenda na sikuzote atakuwa ni mwanamke peke e ninayempenda kuliko wote hapa duniani na siko tayari kuzaa mtoto na mwanamke mwingine.Najua alifikia maamuzi haya kutokana na maneno yanayoanza kusemwa na ndugu.Nitasimama imara siku zote kumtetea na sintakubali mtu yeyote yule amseme vibaya mke wangu” akawaza Elvis akiwa njiani kuelekea hospitalina mara sura ya Doreen ikamjia akatabasamu “ Sielewi ni kwa nini Doreen alikubali kirahisi namna hii ombi la Patrica la kutaka kuzaa na mimi. Si jambo rahisi kwa mwanamke kukubali kuzaa mtoto na mume wa mtu lakini kwa Doreen ameonekana kutokuwa na tatizo lolote kuhusiana na suala hili .Napata mashaka kama kweli ana nia ya dhati ya kumsaidia rafikiyake au ana sababu zake kwani hata maongeziyake ukiyasikia unagundua kabisa kuna kitu anakitafuta.Hata hivyo dah ! Doreen is so hot.Anasisimua sana.Kwa mara ya pili leo kama nisingekuwa jasiri basi ningefanya naye mapenzi leo kwani tayari mashetaniyangu yalikwisha amka.Ananiweka katikamajaribu makubwa ” Akawaza Elvis halafu akakumbuka jambo aliloambiwa na Patricia “ Huyo msichana ana matatizo gani? Nani anayetishia maisha yake? Ngoja nikamsikilizenione kama nitaweza kumsaidia lakini ninahisi ni suala ambao linatakiwa kuripotiwa polisi.” Akawaza Elvis Alifika hospitali akamtaarifu mkewe ambaye alfika mara moja akamchukua na kumpeleka hadi sehemu Fulani “ Hii ni sehemu pekee ambayo hakuna kamera za ulinzi zilizoelekezwa tofauti na kila kona ya majengo ya hospitali hii”akasema Patricia “ Elvis kuna jambo yule msichana amenieleza limenistua kidogo” “ Jambo gani hilo? amekwambia nini? “ Msichana yule ana matatizo na anahitaji msaada.Amenieleza kwamba maisha yake yako hatarini na kwamba kuna watu wanaomtafuta ili kumuua” “ Ni watu gani hao wanaotaka kumuua na kwa nini? “ Hajanieleza kwa undani kuhusu suala hilo ila ameniomba nimtoe hapa hospitali kwani anaogopa wanaomtafuta wakigundua kwamba yuko hapa basi watafika na kumuua” “ Patricia ninapata wasiwasi kidogo kama huyo msichana tayari amekwisha rejewa na fahamu zake kamili.” Akasema Elvis “ Hakuna tatizo katika fahamu zake.Anakumbuka kila kitu na nimemfanyia vipimo yuko safi.Kumbukumbu zake zote ziko sawa” “ Anakumbuka ni kitu gani kilimsababisha apoteze fahamu kwa muda wa miezi miwili? Nimejaribu kumuuliza lakini anaonekana kukumbuka jambo Fulani halafu huogopa na kuanza kulia.Anaonekana kuna kitu ambacho hataki kukiweka wazi” Elvis akafikiri na kusema “ Naweza kuruhusiwa kumuhoji kidogo ili nione ni namna gani tunavyoweza kumsaidia? “ Kwa sasa itakuwa vigumu kumuhoji kutokana na mazingira ya hospitali kwanihutaruhusiwa kuingia mahala aliko kama si daktari au muhusika wa hospitali hii.” “ So what are we going to do? Akauliza Elvis “ I don’t know Elvis” Elvis akainama akafikiri kwa muda kisha akasema “ Are you sure you want to help her?akauliza “ Elvis msichana yule anaonekana wazi ana tatizo kubwa na inaonekana kuna kitu kikubwa anakifahamu na ndiyo maana amenililia na kuniomba nimsaidie .Nadhani kuna ulazima wa kumsaidia” “ Vizuri kama uko tayari kumsaidia basi njia pekee ni kumuondoa hapa hospitali.Hilo linawezekana ? “ Anaweza kuruhusiwa lakini kuna taratibu za kufuata” “ Hapana hatuwezi kusubiri hizo taratibu zikamilike .Yawezekanani kweli anaweza kuwa katika hatari kubwa.We have to save her” “What are we going to do? Akauliza Patricia Kama kweli tunataka kumsaidia tunatakiwa tumuondoe hapa hospitali kimya kimya bila ya mtu kufahamu “ “ Hilo ni jambo gumu sana Elvis.Kamera za ulinzi zimefungwa kila kona ya hospitali hii kwa hiyo hatuwezi kumtorosha bila ya kuonekana.I’mso confused” “ Anaweza kutembea japo kidogo? “ nadhani anaweza kutembea japo bado dhaifu sana” “ Ok good.Kitu cha kufanya hapa mvue mavazi yale ya wagonjwa na umvishe mavazi ya kawaida.Baada ya hapo mtoe nje kwa kisingizio kwamba anakwenda kupunga upepo .Utampeleka hadi chini ya ule mti uliopo eneo la megesho.Mimi nitalitoa gari nje ya geti halafu nitamtuma kijana wa piki piki ambaye atamfuata na kumtoa nje kisha nitampakia garini na kuondoka naye.Hakuna mtu yeyote ambaye atahisi kwamba umemtorosha mgonjwa bali itaonekana ametoroka mwenyewe”akasema Elvis .Patrcia akafikiri kidogo kisha akasema “ Ok ! Ngoja tufanye hivyo ili kumsaidia yule msichana.Anaonekana ni kweli ana tatizo kubwa” ********************** “ Cindy yuko wapi? Akauliza Patricia baada ya kuwasili nyumbani akiwa katika gari ya kukodi.Gari lao aliondoka nalo Elvis katika harakati za kumtorosha Cindy Yuko chumba cha wageni anapumzika.Vipi hospitali hakuna tatizo lolote? Akauliza Elvis “ Hakuna tatizo lolote.Nimeripoti kwa uongozi kwamba mgonjwa amepotea.Na jambo zuri nimeripoti kwamba mgonjwa aliyepotea ana matatizo ya akili.Hakuna mtu anayetilia maanani kupotea kwako hasa baada ya kusikia kwamba ana matatizo ya akili” akasema Patricia na kuvuta pumzi ndefu ‘ Umefanya jambo zuri sana la kijasiri Patricia.” “ Ahsante sana Elvis.Ni kweli tumefanya jambo la kijasiri japokuwa halikuwa rahisi.Ahsante kwa kunipa ujasiri wa kulifanya jambo lile nilikuwa naogopa sana.Kwa sasa Cindy yuko huru na ni jukumu letu kufahamu kilichomsibu na kumsaidia” “ Nadhani ni wakati muafaka wa kumuhoji na kujua kila kitu kumuhusu yeye.Tufahamu ametokea wapi na akina nani wanaotaka kumuua..” akasema Elvis kisha wakainuka na kuelekea katika chumba cha wageni alimokuwamo Cindy ambaye alikuwa amekaa kitandani “ Unajisikiaje hivi sasa? Akauliza Patricia “ Ninajisikia afadhali sana.Kidogo ninajisikia kupata nguvu.Ahsante sana dokta kwa msaada wako” akasema Cindy “ Vizuri sana.Utapona tu usiwe na wasi wasi” akasema Patricia .Cindy akamshika mkono na kusema Dokta ninarudia tena kukushukuru kwa msaada wako .Umeyaokoa maisha yangu.Watu wale wangejua niko pale hospitali wangenifuata na kuniua” akasema Cindy .Patricia akageuka na kumtazama Elvis halafu akamshika Cindy begani “ Cindy huyu hapa ni mume wangu anaitwa Elvis.Kwa pamoja tumeguswa sana na tatizo lako na tuko tayari kukusaidia lakini ili tukupe msaada unaostahili tunataka tulifahamu tatizo lako.Tunataka tufahanu nini kilikutokea na kusababisha upoteze fahamu kwa muda wa miezi miwili? Tunataka kufahamu ni akina nani wanaotaka kukuua na kwa nini? Tafadhali kuwa muwazi kwetu na usiogope kitu hapa uko katika mikono salama.” Akasema Patricia.Cindy akafumba macho kana kwamba kuna kitu anakumbuka.Michirizi ya machozi ikaonekana mashavuni “ Usilie Cindy.Kuwa jasiri.Tueleze kitu gani kilikusibu? Akasema Patricia.Cindy akakohoa kidogo na kusema “Jina langu naitwa Elizabeth.Nilitokea Iringa na kuja kufanyakazi za ndani jijini Dar e s salaam.Nilifanya kazi kwa mama mmoja anaitwa mama Shamim na alipoondoka kwenda arabuni akanikabidhi kwa mtu mmoja anaitwa Pascal Situmwa ambaye mke wake alikuwa amefariki na kumuachia watoto wawili wadogo.Pascal alikuwa akitafuta mtu wa kuwalea watoto wake.” “ Hebu ngoja kwanza Elizabeth.” akasema Elvis huku sura yake ikionyesha mshangao Fulani “ Unasema ulikabidhiwa kwa Pascal Situmwa? “ Ndiyo .Nilikabidhiwa kwa Pascal Situmwa.Nilikuwa nafanya kazi kwake.” Akasema Elizabeth kwa sauti dhaifu.Elvis akafikiri kidogo kisha akasema “ Endelea” “ Vipi mbona umestuka Elvis ? Do you know him? Akauliza Patricia “ hapana simfahamu” akajibu Elvis.Elizabeth akaendelea “ Nilianza kufanya kazi kwa Pascal Situmwa na aliniamini sana.Niliwalea watoto wake vizuri bila matatizo.Siku moja Pascal alikuja na rafiki zake wakanywa sana pombe sebuleni hadi usiku mwingi.Asubuhi nilipoamka niliokota pochi ndogo sebuleni nikaifungua na kuangalia kilichokuwamo ndani yake.Kulikuwa na kadi tatu mfano wa kadi za benki,fedha taslimu shilingi laki tatu pamoja na dola mia mbili za marekani.Vile vile kulikuwa na kitu Fulani kama memory kadi ya simu halafu kukawa na flash disc yenye GB 8.Sikuwa na shida na vifaa vile shida yangu mimi ilikuwa ni zile fedha tu.Sikutaka kuziweka fedha zile chumbani kwangu nikaichukua ile pochi na kwenda kuifukia chini ya mti nyuma ya nyumba.Pascal alipoamka asubuhi alianza kuitafuta ile pochi akaniuliza lakini nilikana kuiona.Aliendelea kutafuta pochi ile kila mahali lakini hakuipata.Baada ya kuitafuta sana na kuikosa akaniita na kunionya kwamba niirudishe pochi ile kwani hakuna mtu mwingine anayeweza kuichukua pochi ile zaidi yangu.Alinipa muda wa dakika thelathini niwe nimeirudisha pochi yake.Niliendelea kukataa kwamba sifahamu mahala iliko hiyo pochi yake.Baada ya nusu saa akaja tena na kuniomba nimrudishie vitu vilivyokuwamo ndani ya ile pochi ila fedha nizichukue.Niliendelea kukataa akanishika na kunipeleka chumbani kwangu akaanza kupekua kila mahala lakini hakuiona pochi wala hela,akanivua nguo zote na kunisachi kila mahala hadi sehemu za siri lakini hakuona kitu.Hakunisemesha kitu tena.Ilipofika saa tisa alasiri wakaja watu wanne ambao sikuwahi kuwaona wakanichukua na kunipeleka sehemu Fulani katika shamba moja wakanitesa sana wakanipiga sana ili niwaeleze mahala ilipo pochi hiyo .Walinipiga mno hadi nikapoteza fahamu na sikujua tena kitu chochote kilichoendelea hadi nilipozinduka na kujikuta pale hospitali.Wale watu walidhamiria kuna kabisa kwani kabla sijapoteza fahamu niliwasikia wakijadiliana mahala watakapokwenda kunitupa baada ya kuniua” akasema Elizabeth .Elvis na Patricia wakatazamana. “ Pole sana Elizabeth.Kuanzia sasa usiwe na wasi wasi wowote kuhusu maisha yako.Hapa uko sehemu salama na hakuna mtu atakayejua kama uko hapa.Kwa sasa pumzika tutaongea zaidi baadae” akasema Elvis halafu akatoka na kulekea chumbani akamuacha Patricia akimpa dawa Elizabeth.Kichwa chake kiliwaza jina moja tu Pascal Situmwa “ Pascal Situmwa !..akasema Elvis kwa sauti ndogo “ Pascal Situmwa kwa nini atake kuua Elizabeth kwa sababu tu ya pochi? Katika pochi hiyo kulikuwa na nini? Nashawishika kuamini kwamba katika pochi hiyo kuna jambo kubwa .Ninamfahamu Pascal Situmwa,mpaka afikiri hatua ya kutaka kumuua huyu msichana lazima iko sababu kubwa.Inawezekana kuna jambo analificha ambalo anahisi pengine huyu msichana amelifahamu” akawaza Elvis na mara Patricia akaingia “ Elvis mbona ulistuka uliposikia Elizabeth akilitaja jina la aliyekuwa mwajiri wake? Do you know him? Akauliza .Elvis akamshika mkono mkewe na kumketisha kitandani “ Ninamfahamu Pascal Situmwa.Ni mfanyakazi wa idara ya usalama wa taifa.Ana nafasi kubwa katika idara ile” “ Kwa nini basi atake kumuua Eliza? Hivyo vitu vilivyokuwa ndani ya hiyo pochi yake vina thamani gani? “ I dont know my love but I need to find out “ akasema Elvis na kumstua mke wake “ Find out ? How? akauliza Patricia







Nitakwenda nyumbani kwa Pascal na kuitafuta hiyo pochi mahala alipoificha Eliza na nikiipata nitajua kilichomo ndani yake” “ Elvis !!...pauline akastuka “ Please don’t do that.Leave this matter as it is,Huyu Pascal huwezi kujua ni kwa nini alitaka kumuua Elizabeth kwa sababu tu ya pochi.Naomba usijihusishe na suala hili hata kidogo.Huyu msichana tutamrejesha kwao Iringa.” Akasema Patricia kwa uoga “ Usihofu kitu Patricia,nataka tu kufahamu kilichomo ndani ya hiyo pochi na baada ya hapo sintakuwa na tatizo tena na Pascal ” akasema Elvis “ Sawa Elvis lakini mimi moyo wangu hauafiki kabisa suala hili lakinikwa kuwa umenihakikishia kwamba hakutakuwa na tatizo lolote basi nakuruhusu ufanye hivyo unavyotaka k ufanya” “ Ahsante kwa kukubaliana nami.Lengo langu ni kutaka tu kufahamu kwa nini Pascal alitaka kumuua Elizabeth kwa sababu tu ya pochi? Kuna kitu gani kikubwa ndani ya hioyo pochi? “ Utafanya nini ukigundua kwambandaoi ya hiyo pochi kuna jambo kubwa? Akauliza Patricia “ Naomba nisikujibu kwa sasa mke wangu hadi hapo nitakapokuwa nimeipata hiyo pochi na kujua kilichomo ndani yake.” Kazi zetu sisi huwa zimetawaliwa na usiri mkubwa.Tunatembea na siri nyingi za taifa kwa hiyoyawezekana katika pochi hiyo kuna siri kubwa” “ Umepanga kwenda lini huko kwa Pascal? “ Tonight.Ninapafahamu nyumbani kwake,nimewahi kwenda sikumoja na mkurugenzi wangu wa zamani.Ninachohitaji ni huyu msichana anielekeze mahala alikoificha hiyo pochi ili nikaichukue” akasema Elvis ******************* Saa mbili na nusu za usiku ,Elvis akasimamisha gari nje ya Akwinabe Bar halafu akashuka na kuingia ndani ya baa ile maarufu hasa kutokana na idadi kubwa ya wasichana wanaouza miili yao.Alikwenda kaunta akanunua chupa kubwa ya maji ya kunywa halafu akatoka.Watu walikuwa wengi kama kawaida ya mahala hapa. Akiwa na chupa yake ya maji mkononi Elvis akaangaza angaza pande zote kama kuna mtu anayemfuatilia halafu akaanza kupiga hatua akaondoka na kuishika barabara iliyokuwa ikielekea ilipo nyumba ya Pascal.Ni nyumba ya nne toka Akwinabe bar. Kwa mujibu wa maelekezo aliyopewa na Elizabeth ni kwamba njia rahisi ya kuingia ndani ni kwa kupitia mlango mdogo ulio nyuma ya nyumba ambao hufungwa saa tano za usiku.Saa nne usiku mbwa hufunguliwa na kutolewa n je kujisadia na saa tano za usiku huingizwa tena ndani na mlango huo hufungwa Elvis akapita katika uchochoro mdogo uliolitenganisha jumba la Pascal na nyumba ya jirani akazunguka hadi nyuma ya nyumba hakukuwa na mtu yeyote kule nyuma,akatoa glovu nyeusi akavaa halafu akachukua na kitu mfano wa soksi kubwa akaivaa kichwa na kubakisha eneo la macho tu kisha akaambaa ambaa na ukuta hadi katika mlango ule mdogo akajaribu kuusukuma ukafunguka.Taratibu na kwa tahadhari ya aiana yake akaingia ndani bastora yake ilikuwa mkononi tayari kukabiliana na chochote ambacho kingejitokeza.Hakukuwa na mtu yeyote kule nyuma ya nyumba.Taa za ndani zilikuwa zinawaka kuashiria kwamba kuna watu walikuwemo ndani Moja kwa moja akaelekea katika mti alioelekezwa na Elizabeth ambako ndiko alikoificha ile pochi ya Pascal.Mwangaza haukuwa mkali sana eneo hilo kutokana na matawi ya miti na hakuweza kuonekana kiurahisi kutokana na mavazi meusi aliyoyavaa.Akavua begi alilokuwa amevaa mgongoni akatoa kitu Fulani kigumu chenye ncha kali na kuanza kuchimba.Wakati akiendelea na zoezi lile la kufukua ,ghafla mlango ule mdogo ukafunguliwa na kijana mmoja akaingia na bila kuhisi kitu chochote akaelekea moja kwa moja ndani.Elvis aliyekuwa amejibanza pembeni ya mti akaendelea na zoezi lake la kuchimba .Baada ya muda akakutana na kitu kama mfuko wa nailoni na ndaniyake kulikuwa na pochi.Kwa haraka haraka akaiweka pochi ile katika begi lake halafu akaishika bastora yake akatazama usalama wa eneo lile kisha akaondoka kwa tahadhari kubwa.Akaufungua mlango mdogo lakini kabla hajatoka mlango wa kuingilia ndani ukafunguliwa na kwa haraka akajirusha nje.Mara akasikia msichana akipiga kelele akiwaita watu waliokuwemo ndani akawafahamisha kwamba ameona mtu akitpoka pale mlangoni .Elvis akavua ile kofia aliyokuwa ameivaa kichwani halafu akatoka mbio hadi barabarani na kuelekea moja kwa moja katika baa mahala alikoacha gari lake akaingia garini na kuondoka kwa kasi ****************** Saa tano na dakika tatu za usiku Elvis akawasili nyumbani kwake.Patricia mke wake ndiye aliyemfungulia geti. “ Thank you lord you are back” akasema Patricia na kumkumbatia mumewe.Elvis akambusu mkewe na kumshika mkono wakaingia sebuleni. “ Nilikuwa na wasi wasi sana na ndiyo maana nimeshindwa hata kupata usingizi”akasema Patricia “ Samahani kwa kukuweka roho juu mpenzi wangu lakini hakukuwa na sababu yoyote ya kuwa na wasi wasi.Ilikuwa ni kazi ndogo sana” “ Usiseme hivyo Elvis.Ilikuwa kazi ndogo kwako lakini ya hatari kubwa kwangu.Kazi yako naiogopa sana.Kila siku namuomba Mungu watume malaika zake wakutangulie kokote uendako.Sitaki upatwe na tatizo lolote .I love you so much Elvis,you are my everything.” Akasema Patrician na kukilaza kichwa chake katika kifua cha mumewe.Elvis akainama akambusu na kusema “ I love you too Patricia.I love you so much ” wakakumbatiana .Baada ya muda kidogo Patricia akauliza “ Umeipata pochi hiyo uliyokwenda kuitafuta? “ Ndiyo nimeipata” akasema Elvis halafu akainuka na kulifungua begi lake akatoa pochi ndogo akaifungua.Ndani ya pochi ile kulikuwa na kila kitu alichokisema Elizabeth “Kila kitu ni kama alichokisema Elizabeth. Hizi fedha sina haja nazo,tutampatia Elizabeth zitamsaidia katika matatizo yake.Vitu ambavyo vilipelekea Pascal afikie maamuzi ya kumuua Elizabeth ni hivi viwili tu .Hii flash disc na h ii memory card.” Akasema Elvis “ Kuna nini ndani yake mpaka afikie hatua ya kutaka kuutoa uhai wa mtu kwa ajili ya vitu hivi?” akauliza Patricia “ I don’t know yet.I’ll find out” akasema Elvis “ Elizabeth anaendeleaje? “ Anaendelea vizuri.Ninaendelea kumpa dawa.Hali yake inazidi kuboreka” Good.Hali yake ikisha boreka itabidi tumsafirishe kumrejesha kwao Iringa akaanze maisha mapya.Hapa mjini hatakiwi kuonekana kabisa.Ni hatari kubwa kwake” “ Hilo ni wazo la msingi sana.Tutampatia mtaji wa biashara akaanze maisha yake huko kijijini.Hatupaswi kuendelea kumuweka hapa kwa muda mrefu” Elvis akamshika mkono mkewe wakaelekea chumbani.Elvis akamtazama mkewe kwa makini bila kumsemesha. “ Vipi mbona unanitazama hivyo Elvis?akauliza Patricia.Elvis akamsogelea akambusu na kusema “ You are blessed my love.You are so beautifull than all women in this world.I want to remind you again of how much I love you and how important you are in my life” akasema Elvis Patricia akamkumbatia kwa nguvu kisha wakaanza kupeana mabusu mazito na haukupita muda wakahamia katika ulimwengu wa huba ************************* Saa sita za usiku Pascal alirejea nyumbani kwake kama kawaida yake.Mida hii ndiyo huwa anarejea nyumbani kila siku. Arejeapo nyumbani usiku huu familia yote huwa imelala na hivyo hufungua geti kwa kutumia remote control.Aliingiza gari katika gereji halafu akaingia sebuleni na kushangaa kuwakuta Salvatory mdogo wake pamoja na mtumisi wa ndani wakiwa sebuleni jambo ambalo halikuwa la kawaida. “Bado hamjalala mpaka mida hii? Akauliza Pascal “ Kaka tumeogopa kulala kuna shida kidogo imetokea” “ Shida gani imetokea? “ Prisca anasema kwamba alimuona mtu akiwa na mavazi meusi akitoka ndani kwa kupitia mlango wa nyuma” “ Mtu ? !!..Pascal akashangaa “ Ndiyo kaka” akajibu Prisca mtumishi wa ndani “ Ulimuona mtu huyo alikuaje? “ sikumuona usoni.Nilimuona kwa nyuma wakati akitoka.Alikuwa amevaa mavazi meusi pamoja na begi mgongoni” Mmejaribu kuangalia kama kuna sehemu yoyote kumevunjwa au kuna kitu chochote kimeibiwa? “ Tumeangalia lakini hakuna sehemu yoyote iliyovunjwa au kitu chochote kilichoibiwa.” Akasema Salvatory.Pascal akafikiri kidogo na kusema “ Ok msiogope. Yawezekana wakawa ni vibaka waliokuta mlango uko wazi wakaingia ili kutafuta cha kuiba wakakosa.Msiache mlango wazi tena ,muwe mkiufunga muda wote” akasema Pasca na kuzunguka nyumba yote kuchunguza na kuhakikisha hakuna sehemu iliyovunjwa halafu akaingia katika chumba chake ambacho hukitumia kuhifadhia vitu vyake vya siri lazima atakuwa ni kibaka aliyekuwa akitafuta nafasi ya kuiba.Sina hakika kama ni mtu aliyekuwa na nia yoyote mbaya na mimi.Kama angekuwa ni mtu mwenye kutafuta chochote toka kwangu basi angeingia ndani.Hata hivyo kuna ulazima wa kufunga kamera za ulinzi hapa nyumbani.Toka yule msichana alipoipoteza ile pochi yangu yenye vitu vyangu vya muhimu nimekosa amani kabisa.Nashukuru niliwahi kummaliza na nina hakika siku ile ile hakutoka kabisa nje ya nyumba hii kwa hiyo kama kuna mtu alimtuma basi hakupata nafasi ya kuonana naye tena.Lakini sina hakika sana kama kuna mtu yeyote anayeweza kumtumia msichana kama yule kuniibia vitu vyangu,najua shida yake ilikuwa ni fedha tu na vitu vingine vyote akavitupa.Kama angenieleza ukweli ningemsamehe lakini aligoma kuwa mkweli na kunilazimisha nimkate pumzi” Akawaza Pascal ******************** Kumepambazuka siku ya jumatatu,wiki mpya imeanza.Saa kumi na mbili za asubuhi Elvis na Patricia waliamka na kuelekea katika chumba cha mazoezi na kufanya mazoezi mepesi ya viuongo .Kisha maliza maozezi wakaingia bafuni wakaoga na kujiandaa kwa ajili ya kuelekea makazini.Kabla ya kutoka wakapata kwanza kifungua kinywa My love,sintoungana nawe mchana wa leo kwa chakula .Nitakuwa na kazi nyingi leo kutokana na ujio wa rais wa Marekani hapo kesho.Ugeni huu ni mkubwa na idara zote za usalama wa nchi zinahusika kikamilifu” akasema Elvis wakiwa mezani wakipata kifungua kinywa “ Usihofu darling.I’ll miss you a lot today”akasema Patricia “I’ll miss you too my angel.Kama kutakuwa na tatizo lolote hospitali kuhusiana na Elizabeth nitaarifu mara moja ili tujue namna ya kufanya” “ Usihofu Elvis.Sina hakika kama kutakuwa na tatizo lolote.No body cares for her.Kwa muda wote aliokuwa hospitali hana fahamu hakuna hata mtu mmoja aliyejitokeza kumtafuta .Kila mtu pale hospitali anafahamu kwamba ana matatizo ya akili kwa hiyo hakuna anayejali kupotea kwake.Kama kutakuwa na tatizo lolote basi nitalimaliza mwenyewe huko huko.” Akasema Patricia.Baada ya kumaliza kupata kifungua kinywa kila mmoja akaingia katika gari lake na kuondoka kuelekea kazini Saa mbili kasorobo Elvis akawasili ofisini na moja kwa moja akaiwasha kompyuta yake.Kabla hajaanza kufanya kazi yoyote akatokea Sabina mmoja kati ya wafanyakazi wapya wa idara hii.Sabina alikuwa ni mtaalamu wa kutegemewa wa masuala ya kompyuta “ Hello handsome” akasema Sabina.Elvis akageuka huku akitabasamu na kusema Hello queen of Africa” Akasema Elvis huku akicheka .Yeye na Sabina ni watu waliozoeana sana na mara nyingi wamekuwa wakitaniana. “ How was your weekend? Utanisamehe Elvis nilishindwa kabisa kufika katika birthday party ya mkeo,niliitwa mara moja Morogoro anakosoma mdogo wangu.Sherehe ilikwendaje? “ Ilikuwa nzuri sana.We had fun.Watu wengi walihudhuria,tukala na kunywa.Kwa ujumla ilikuwa nzuri” akajibu Elvis “ Nafurahi kusikia hivyo .Its timefor work Elvis.Tal k to you later “akasema Sabina na kuelekea katika meza yake. “Now its time to find the truth. “ akawaza Elvis halafu akaichukua ile flash disc akaichomeka katika kompyuta yake na kuifungua.Kulikuwa na mafaili matatu ndani yake .Akafungua faili la kwanza na la pili na la tatu yakamstua sana .Zilikuwa ni nyaraka za kijeshi zilizohusiana na silaha mbali mbali za kivita.Kulikuwa na picha mbali mbali za silaha nzito za kivita na maelezo yake.Kulikuwa na ndege vita tatu,vifaru tisa vya kisasa ,na aina mbali mbali za bunduki zenye nguvu na mabomu.Mwanzoni mwa kila faili kulikuwa jina la Pascal kwa kalamu.. “Nyaraka za jeshi.Pascal anahuska vipi na nyaraka hizi nyeti za jeshi? Ninavyofahamu mimi mambo ya silaha hasa silaha nzito na kivita kama hizi huwa ni mambo ya siri ya kijeshi.Kwa nini basi Pascal ambaye si mwanajeshi awe na nyaraka kama hizi? Kuna kitu anakichunguza ndani ya jeshi? Hapana sina hakika kama kuna kitu anachokifanyia uchunguzi ndani ya jeshi.Ninavyofahamu mimi kama kuna tatizo lolote ndaniya jeshi basi wana taratibu zao za kufanya uchunguzi na si kwa kuwatumia watu wasio wanajeshi kama Pascal .Kama ni hivyo , Pascal amezipata wapi nyaraka nyeti kama hizi za kijeshi? akawaza Elvis “ Sasa ninaanza kupata picha ni kwa nini Pascalalitaka kumuua Elizabeth kwa kuificha pochi yake.Hakutaka nyaraka hizi zionekane kwa watu wengine.Kwa ninialiogopa? Ngoja kwanza nifahamu Pascal ana daraja gani katika idara yake hadi kuwa na nyaraka nyeti kama hizi ambazo wahusika wake ni viongozi wakuu wa nchi na wa jeshi ” Akawaza Elvis na kuzitafuta namba Fulani akapiga “ Hallow Elvis” Habari za siku?ikajibu sauti ya mwanadada upande wa pili “ Nzuri Imelda,unaendeleaje? Umepotea sana siku hizi”akasema Elvis “ Nipo Elvis wewe tu ndiye umepotea kabisa hata simu siku hizi hutaki kunipigia” “ Ni kweli Imelda sijawasiliana nawe kwa kipindi kirefu kidogo lakini ni kutokana na kubanwa sana na kazi” “ sawa Elvis,unahitaji nini leo ? Kwa sababu ukinipigia simu ni lazima utakuwa na shida na unahitaji msaada.” Akasema Imelda halafu wote wakacheka “ Mbona unacheka Elvis? Ni kweli hayo ninayoyasema? Huwa hunikumbuki hadi upatwe na tatizo” “ Kweli Imelda nina shida kidogo naomba unisaidie” “ Una tatizo gani? “ Imelda nahitaji kufahamu Pascal Situmwa ana daraja gani katika idara yenu ya usalama wa taifa? “ Daraja la PascalSitumwa? Imelda akauliza “ Ndiyo .Nahitaji kufahamu daraja lake ndani ya idara yenu” akasema Elvis “ Elvis siwezi kujua kwa sasa Pascal ni daraja gani hadi niingie katika kompyuta ya mkurugenZi kwani haya huwa ni mambo ya siri “ “ Ok do it for me Imelda” akaomba Elvis “ Ok naomba unipe dakika tano nitakupigia” akasema Imelda na kukata simu.Elvis akaendelea kuziangalia silaha zile na baada ya kama dakika nne Imelda akapiga “ Elvis ,Pascal situmwa ni mfanyakazi wa daraja la tatu yaani daraja la kawaida sana na hana cheo chochote ndani ya idara.” “ Kama Pascal ni mtu wa daraja la tatu na hana cheo chochote ndani ya idara ya usalama wa taifa,kwa ninibasi awe na nyaraka nyeti kamahizi za kijeshi? Akajiuliza Elvis “ Elvis are you there ? Akauliza Imelda baada ya kuona kumekuwa kimya Nipo Imelda.Ahsante sana kwa msaada wako lakini kuna jambo lingine dogo nataka unisaidie tena” “ semaElvis ni jambo gani unahitaji? “ Naomba unisaidie namba ya simu ya Pascal” “ Elvis Pascal kafanya nini? Kuna nini unataka kukifanya kwake? Nakufahamu vizuri mpaka umfanyie uchunguzi mtu lazima kuna jambo” akauliza Imelda “ usihofu kitu Imelda,hakuna tatizo lolote.Kuna kitu kidogo nilichohitaji kukifahamu kuhusiana na Pascal” Imelda akamtumia Elvis namba za simu za pascal “ Ninachotaka kukifahamu mimi ,nyaraka hizi za kijeshi zimefikaje mikononi mwa Pascal? Inaonekana nyaraka hizi zina umuhimu mkubwa sana kwake na ndiyo maana alikuwa tayari hata kuutoa uhai wa mtu ili kuhakikisha kwamba hazitui katika mikono ya mtu mwingine.Nahitaji kulifanyia uchunguzi jambo hili.Nataka kufahamu uhalali wa pascal kuwa na nyaraka nyeti kama hizi.” Akafikirikidogo halafu akainuka na kuelekea katika ofisi ya Sabina “ Sabina ninatoka kidogo kuna mahala ninaelekea” “Unaelekea wapi Elvis? Mkurugenzi alisema kwamba asubuhi ya leo tunatakiwa wote katika kikao mumu cha kazi” “ Please sweet baby,cover for me.Ninakwenda sehemu Fulani muhimu sana na sintakawia kurudi ” akasema Elvis na kutoka akaingia garini .Kabla hajaondoka akazitafuta namba za simu za Doreen akampigia “ hallo Elvis,habari za asubuhi?” akasema Doreen baada ya kupokea simu “ habari nzuri sana Doreen.Ukowapi mida hii? “Niko ofisini .Kuna tatizo lolote Elvis? “ Ninahitaji kukuona .Ninakuja huko ofisini kwako sasa hivi”akasema Elvis na kumstua sana Doreen “ Kuna tatizo gani Elvis?akauliza Doreen kwa wasi wasi.Elvis akacheka kidogo na kusema “ Hakuna tatizo Doreen.Nahitaji kukuona kuna jambo nahitaji msaada wako”





Elvis alifika katika ofisi za kampuni ya Tanzacom anakofanya kazi Doreen.Aliegesha gari na kushuka akaelekea moja kwa moja ofisini kwa Doreen ambaye kwa wakati huo alikuwa ana mteja ndani akimuhudumia hivyo kumlazimu Elvis kusubiri nje hadi mteja yule alipotoka ndipo alipoingia “ Hallow Elvis!! Doreen akasema huku akisimama na kumpa mkono Elvis halafu akaufunga mlango wa ofisi yake hakutaka watu wasikie maongezi yake na Elvis “ karibu sana Elvis,habari za toka juzi? “ habari nzuri sana Doreen.Unaendelaje? Ninaendelea vizuri sana Elvis.” Akasema Doreen halafu kimya kifupi kikapita wote wawili wakiangaliana “ uhhm Elvis ulisema una tatizo.Ni tatizo gani nikusaidie? Akauliza Doreen “ Doreen nimekuja nina tatizo na ninahitaji msaada wako”akasema Elvis “ I can do anything for you Elvis.Hata vile ambavyo unafikiri kwamba siwezi ninaweza.” akasema Doreen huku akitabasamu.Elvis naye akatabasamu na kusema “ Nafurahi kusikia hivyo Doreen.Ahsante kwa kuwa tayari kunisaidia kwa jambo lolote.Kilichonileta hapa muda huu ni hiki”akaingiza mkonomfukoni na kutoa kijikaratasi akampata Doreen “ Nahitaji kupata mawasiliano ya namba hizi ya mwezi mmoja ulipita.”Doreen akaegemea kiti na kumtazama Elvis kwa makini “ Umenipa mtihani mgumu sana Elvis but let me see what I can do for you” akasema Doreen na kutoka.Baada ya kama dakika kumi hivi akarejea akiwa na flashi disc mkononi akampatia Elvis “ Kila kitu unachokihitaji kiko humu ndani” akasema Doreen na kumpatia Elvis ile flash disc iliyokuwa na taarifa za mawasiliano ya Pascal kwa muda wa mwezi mmoja uliopita “ ahsante sana Doreen.Ahsante kwa msaada wako huu mkubwa” usijali Elvis,niko tayari muda wowote kukusaidia.Kwa sababu yako niko tayari kufanya jambo lolote hata lile la hatari”akasema Doreen na kumfanya Elvis atabasamu “ Ahsante sana Doreen.Tutaonana baadae”akasema Elvis huku akitoka na kumuacha Doreen akiwa bado amesimama “ Sikuwa nimepanga kuja kuonana na Doreen kwa sababu kila ninapomuona mwili wangu hunisismka sana na kunikumbusha usiku ule.Hili ni jaribu zito katika ndoa yangu ambalo sina budi kulishinda.Ngoja kwanza nishughulike na suala hili la msingi ndipo niligeukie suala hili la Doreen” akawaza Elvis wakati akiingia garini “Baada ya kuondoka katika ofisi za Tanzacom,moja kwa moja akaelekea nyumbani kwake.Akaichomeka flash disc aliyopewa na Doreen katika kompyuta yake na kuanza kuipitia taarifa Iile lenye mawasiliano ya pascal.Ilikuwa ni taarifa ndefu iliyomchukua zaidi ya nusa saa kulipitia.Katika orodha ya simu zote ambazo Pascal alipiga na kupigiwa kuna namba mbili ambazo zilionekana kuwasiliana naye mara nyingi zaidi.Hakujua namba zile ni za akina nani kwani zilikuwa ni za mtandao tofauti na ule wa Pascal.Bila kuchelewa akachukua tena simu na kumpigia Doreen akampatia zile namba mbili na kumuomba amsaidie kufahamu ni za akina nani.Baada ya dakika mbili Doreen akampigia simu “ Elvis,namba ya kwanza ni ya Edna jumbe na ya pili ni Franck kwaju” Elvis akastuka baada ya kulisikia jina la pili la Frank Kwaju “ Umesema Frank kwaju? “ Ndiyo .kwani kuna tatizo gani? Akauliza Doreen “ Doreen ahsante sana kwa msaada wako” akasema Elvis na kukata simu.Akaegesha kiti chake halafu akainuka na kwenda kuchungulia nje “ Brigedia jenerali Frank kwaju !! akasema Elvis huku akizunguka zunguka mle chumbani Sasa nimeanza kupata picha kwa nini nyaraka zile za kijeshi zimemfikia Pascal.Lazima kuna kitu kinachoendelea kati ya Pascal na Brigedia jenerali Frank Kwaju.kwa mujibu wa taarifa hii ya mawasiliano ya Pascal,inaonekana kwamba pascal na Frank wamekuwa wakiwasliana mara nyingi zaidi.Hata katika orodha ya simu alizopokea inaonyesha kwamba amepokea simu nyingi zaidi toka kwa Frank kwaju…Something is going on here.I need to find out.” Akawaza Elvis “ Nakumbuka wakati nikiwa jeshini kabla ya kwenda masomoni nje ya nchi kuna kijana mmoja namkumbuka kwa jina la David Elifariji ambaye alituhumiwa kumbaka mtoto wa Frank.Wakati naondoka kueleka Marekani nliacha bado kesi ile ikiunguruma na sikuwahi kufuatilia tena ili kujua nini ilikuwa hatima yake.Ninavyokumbuka kesi ile ilijaa utata mkubwa.Natakiwa kufahamu nini kilitokea katika kesi ile.Nahisi kuna kitu Fulani hakikuwa sawa na ambacho natakiwa kukifahamu.” Akawaza Elvis halafu akatoka na moja kwa moja akaelekea ofisini kwao mara tu baada ya kluegesha gari akashuka na kuelekea moja kwa moja katika ofisi ya mkurugenzi wake ambaye alishangaa kumuona Elvis mida ile “ Elvis,what are you doing here? Akauliza mkurugenzi “ Mkurugenzi nina shida kidogo ya dharura na ndiyo maana niko hapa “ Shida gani Elvis? Akauliza mkurugenzi “ Mzee ,wakati nikwia jeshini kuna mwanajeshi mmoja aliyejulikana kwa jina la David Elifariji ambaye alikuwa na kesi ya kumbaka mtoto wa Brigedia jenerali Frank kwaju.Niliondoka na kuelekea Marekani na kuiacha kesi ile ikiendelea kuungurma na sikuifuatilia tena.Nahitaji kufahamu hatima ya kesi ile na maamuzi yaliyotolewa” “ Elvis kwa sasa rais wa Marekani yuko angani akija Tanzania na jukumu letu ni kushirikiana na vyombo vingine vya usalama kuimarisha ulinzi na sina wakati wa kufuatilia kesi zilizokwishapita miaka mingi.Timu yote iko kazini muda huu ni wewe tu ambaye uko hapa” akasema mkurugenzi “ Mzee,jambo hili ni la muhimu sana na ndiyo maana niko hapa ninahitaji msaada wako” Mkurugenzi akamtazama Elvis kwa makini na kusema “ Unafuatilia jambo gani? “ Kwa sasa ni mapema mno kukueleza ninachokifuatilia mzee lakini naomba unipe muda kidogo ,kuna mambo nayakamilisha halafu nitarudi kwako na kukupa taarifa kamili.Ili kuikamilisha taarifa hiyo nahitaji msaada wako na ndiyo maana niko hapa” Mkurugenzi akaendelea kumkazia macho Elvis halafu akasema “ Unataka nikusaidie nini Elvis? Nataka unipatie barua ambayo itaniwezesha kulipata faili la keshi ya ubakaji iliyomkabili David” “ Elvis kitu unachokiomba ni kigumu sana.Inawekana tu kufanya hivyo endapo kuna jambo zito ambalo tunalifuatilia” “ Naelewa hivyo mkurugenzi na nisingeweza kuja hapa kwako kukuomba kitu hicho kwa jambo ambalo si la muhimu” “ Unataka kuona nini katika faili hilo? Akauliza Mkurugenzi “Kuna kitu nahitaji kukiangalia “ Mkurugenzi akafikiri kwa muda na kusema ‘ Ok ! Nitakuandikia hiyo barua kwa sababu ninakuamini na ninaamini kuna jambo la muhimu unalolifuatilia.Naomba taarifa mara moja ya jambo hilo unalolifuatilia mara tu umalizapo uchunguzi wako.Mara nyingi sipendi mtu afanye uchunguzi wa jambo nisililolifahamu lakini kwa vile ninakuamini ninakuruhusu uendelee na uchunguzi wako .Vile vile nataka ufuatilie suala hili la faili kwa muda wako lakini kwa sasa nataka ukaungane na wenzako katika kuimarisha ulinzi.”akasema Mkurugenzi na kumuandikia Elvis barua itakayomuwezesha kulipata faili analolihitaji “ Tafadhali Elvis naomba uelekee moja kwa moja uwanja wa ndege”akasisitiza mkurugenzi wakati akimpatia Elvis barua “ Usijali mzee wangu ,ninaelekea huko “akasema Elvis na kutoka ,akapanda gari lake na kuondoka kuelekea uwanja wa ndege kuungana na wenzake “ Sifahamu ni kitu gani ninachotaka kukiangalia katika faili hilo lakini nahitaji tu kuliona.Kuliona jina la Frank Kwaju katika orodha ya watu waliowasiliana na Pascal mara nyingi kumenitia shaka kidogo na kunilazimisha nianze kumfanyia uchunguzi “akawaza Elvis akiwa njiani kuelekea uwanja wa ndege ******************* Kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania ulinzi mkali na wa aina yake ulishuhudiwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere .Hii ilitokana na ujio wa rais wa Marekani anayefanya ziara ya siku nne nchini Tanzania.Ulinzi huu wa aina yake ulihusisha vikosi maalum vya ulinzi toka Marekani ,makachero toka shirika la ujasusi la marekani C.I.A na wale wa F.B.I bila kusahau vikosi mbali mbali vya ulinzi vya hapa nchini Tayari rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr Samweli Mhamba alikwisha wasili uwanjani kumlaki mgeni wake .Pamoja naye alikuwepo pia rais wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar Dr Makame Abdallah ,makamu w a rais wa Tanzania,waziri mkuu pamoja na viongozi wengine wakubwa wa serikali.Tayari viongozi wote walikwisha jipanga mstari ishara kwamba mgeni wanayemtegemea yuko karibu kuwasiliEneo la uwanja lilijawa na heka heka za walinda usalama waliokuwa makini wakizunguka huku na kule kuhakikisha kwamba hali ya amani na usalama inaimarika kabla na baada ya mgeni kuwasili.Hali ya uwanjani hapo ilikuwa tulivu na mandhari nzima ilivutia sana .Bendera za Tanzania na Marekani zilipepea katika kila kona ya uwanja huu.Vikundi mbali mbali vya ngoma za kiutamaduni viliendelea kutumbuiza wakati mgeni akisubiriwa. Vilikuwepo pia vikundi mbali mbali vya akina mama na vijana waliokuwa wamevalia sare maalum zenye picha ya Kiongozi huyu wa taifa kubwa duniani huku wakiwa wameshika bendera za taifa la marekani na Tanzania mikononi kwa jumla hali ya uwanjani hapo ilikuwa ni ya kupendeza mno. Saa tano na dakika arobaini juu ya alama dege maarufu sana duniani lijulikanalo kama Air force one likaonekana angani.Uwanja wote ukalipuka kwa shangwe .Kila mtu aliyekuwapo pale uwanjani alijikuta akiwa na furaha kubwa ya kutaka kumshuhudia kiongozi huyu mashuhuri duniani. Hatimaye dege lililombeba rais wa marekani likaigusa ardhi ya Tanzania na kwenda umbali mrefu kisha likaanza kurudi pole pole na mwishowe likasimama.Mlango ukafunguliwa na baadhi ya maofisa wa usalama wakaingia ndani ya ndege Baada ya dakika kama ishirini toka dege lile lisimame uwanja ukarindima kwa shangwe na nderemo baada ya mgeni aliyekuwa akisubiriwa kwa hamu kujitokeza katika mlango wa ndege na kupunga mkono.Alikuwa ameambatana na mkewe na binti yao Shanon Dr samweli Mhamba akampokea mwenyeji wake wakasalimiana kisha akaanza kumtambulisha kwa viongozi wengine wa kitaifa waliokuwepo pale uwanjani.Baada ya utambulisho ule ,rais wa Tanzania na mgeni wake wakaelekea katika jukwaa lililoandaliwa wakasimama na nyimbo mbili za taifa za mataifa haya mawali zikapigwa na baada ya hapo rais wa Marekani akakagua gwaride maalum lililoandaliwa kwa ajili yake.Alipomaliza akaongozwa na mwenyeji wake katika kukagua vikundi mbali mbali vya ngoma na burudani vilivyokuwapo pale uwanjani.Rais wa Marekani na ujumbe wake walionekana kujawa na furaha sana kwa burudani iliyokuwepo pale uwanjani.Kisha kagua vikundi vile vya ngoma na burudani misafara ya marais ikaondoak pale uwanjani na shughuli za uwanjani hapo zikawa zimemalizika .Elvis na timu yake nao hawakuwa na cha kufanya tena pale uwanjani “ Ni muda sasa wa kwenda kulifuatilia lile faili.” Akawaza Elvis akawaaga wenzake na kuondoka ********************** Saa mbili za usiku Elvis akarejea nyumbani .Tayari Patricia alikwisha rejea muda mrefu na alikuwa asebuleni akimsubiri ili wale wote chakula cha usiku “ Hallow my love umeshindaje leo? Akauliza Patricia huku akimkumbatia mumewe na kumbusu “ Nimeshinda salama Patricia.Tulikuwa na shughuli nzito leo ya ulinzi lakini nashukuru Mungu imekwenda salama” “ Pole sana mume wangu.I missed you so much.” Akasema Patricia na kumsaidia Elvis kuvua koti halafu akamuongoza hadi chumbani na kisha wakaingia bafuni kuoga.Kisha oga wakapata chakula cha usiku halafu wakaingia tena chumbani kwao.Waliongea mambo mengi kuhusiana na siku ilivyokuwa hadi pale Patricia alipopitiwa na usingizi.Elvis alihakikisha mkewe amepitiwa kabisa na usingizi halafu akainuka taratibu akatoka na kuelekea katika ofisi yake ya nyumbani.Akaufungua mkoba wake na kutoa faili moja akalifungua na kuanza kulipitia taratibu.Hili ni falili la kesi iliyokuwa ikimkabiili Private David Elifariji Muda wa masaa mawili sasa Elvis aliendelea kulipitia falili lile kwa umakini mkubwa,na alipomaliza akaegemea kiti “ David Elifariji alikutwa na hatia ya kumbaka Graca mtoto wa Frank na akafungwa miaka thelathini gerezani.Ninapata mashaka makubwa kuhusiana na namna kesi hii ilivyoendeshwa.Ni kweli David alimbaka huyu mtoto wa Brigedia Frank? Akajiuliza Elvis halafu akasimama na kukaa juu ya meza “ Natakiwa kumuona David gerezani na kumuhoji kuhusiana na jambo hili.Nataka niufahamu ukweli.Hii ni sehemu nzuri sana kuanzia kumfahamu Frank Kwaju.Kuna kitu lazima nitakipata baada ya kuonana na David”akawaza Elvis halafu akarejea chumbani kwake na kulala Saa mbili za asubuhi siku iliyofuata Elvis tayari alikuwa katika ofisi ya mkurugenzi wake .Alikuwa ni mtu wa kwanza kuonana na mkurugenzi “ Habari za toka jana Elvis”akauliza Mkurugenzi Habari nzuri mzee.” “ Elvis nashukuru kwa kazi mliyoifanya jana.Mpaka hivi sasa hakuna tishio lolote la usalama na kila kitu kinakwenda vizuri.Pamoja na hayo lazima tuendelee kushirikiana na vikosi vingine vya usalama kuhakikisha hali inaendelea hivi hadi mgeni atakapoondoka.Hatutakuwa na muda wa kupumua kwani ugeni huu ni mkubwa na kama unavyojua nchi ya Marekani ina maadui wengi duniani.Ulifanikiwa kulipata lile faili ulilokuwa ukilihitaji ? ” akauliza mkurugenzi “ Ndiyo mzee nilifanikiwa lakini nina shida nyingine naomba msaada wako” “ Shida gani tena Elvis? Mtuhumiwa mwenye faili lile alihukumiwa miaka thelathini gerezani kwa kosa la ubakaji,nahitaji kuonana naye.Kuna mambo ambayo nahitaji kuyafahamu toka kwake.” akasema Elvis “ Elvis ni kitu gani kinaendelea? Unachunguza jambo gani? “ mzee kuna jambo ninalolifuatilia .Ni jambo kubwa na sitaki kuliweka wazi kwa sasa mpaka hapo nitakapokuwa na taarifa za kutosha.” “ Elvis unachokifanya ni kinyume kabisa na taratibu za idara yetu.Kila kitu kinachofanyika hapa katika idara hii ninapaswa kukifahamu hata kama ni cha hatari kiasi gani ili niweze kuona kama kinafaa kuchunguza ama vipi.lakini wewe unajifanyia uchunguzi wako kimya kimya bila kumshirikisha mtu yeyote na bado unahitaji msaad wangu.Ninakusaidia kwa vile ninakuamini tu lakini naomba haraka iwezekanavyo unitaarifu ni kitu gani hasa unachokichunguza” akasema Mkurugenzi “ Mzee kwanza nashukuru kwa kuniamini na kunisaidia japokuwa nimetoka nje ya taratbu zetu za kazi.Ninakuahidi mara tu baada ya kumaliza uchunguzi huu nitakuja kwako na kukueleza kila kitu” akasema Elvis Mkurugenzi akainama akatafakari kidogo kisha akasema “ Ok nitawasiliana na uongozi wa gereza alilofungwa na watakuruhusu uonane na mtu unayemuhitaji” Bila kupoteza muda Elvis akaingia garini na kuondoka kuelekea gereza la Uwangwa kuonana na Private David Elifariji *************** Taarifa za ujio wake tayari zilikwisha fika katika ofisi ya mkuu wa gereza la Uwangwa hivyo baada tu ya kufika Elvis alipelekea moja kwa moja katika sehemu ambayo angekutana na David Elifariji.Kilikuw ani chumba chenye ukubwa wa wastani chenye meza na viti viwili Baada ya dakika kadhaa mlango ukafunguliwa na David Elifariji akaingizwa mle ndani “ Ouh my God !.....Elvis akasema kwa sauti ndogo ya mstuko baada ya kumuona David.Alikuwa amekonda sana na kupauka “ Afisa ,mtu uliyemuhitaji huyu hapa.Uko huru kuongea naye.Kamera za ulinzi za chumba hiki zimezimwa kutokana na maelekezo ya mkuu wa gereza.Mkishamaliza maongezi yenu utagonga mlango nitakuwepo hapo nje”akasema askari magereza aliyemleta David mle ndani “ Ahsante sana Afande.”akajibu Elvis na yule askari akatoka akawaacha yeye na David pekee “ Hallow david”akasema Elvis huku akimpa mkono david “ “halow “ akajibu David “ Pole sana david” “ahsante sana kaka” akajibu David .Kimya cha sekunde kadhaa kikapita kisha Elvis akasema “ David sina hakika kama unanikumbuka kwa sababu ni muda mrefu umepita.Ninaitwa Elvis ninatoka katika idara ya ujasusi ya taifa kitengo kipya cha kuzuia na kupambana na ugaidi.Mimi na wewe tulimaliza wote mafunzo ya kijeshi na niliondoka kuelekea marekani kwa mafunzo zaidi ya ujasusi na namna ya kupambana ugaidi.Wakati ninaondoka niliacha bado kesi yako ikiendelea na sikujua nini kilitokea huku nyuma.Jana nililazimika kulipitia tena faili la kesi yako na leo nimelazimika kuja kukuona.Nimekuja hapa ili kuongea nawe kuhusiana na kilichotokea na kupelekea ukafungwa gerezani kifungo kirefu.Tafadhali nieleze kila kitu unachokifahamu bila kunificha.Nini hasa kilitokea? Ni kweli ulimbaka mtoto wa Frank Kwaju? Kuwa huru kuniambia kile unachokifahamu.Kwa pamoja tunaweza kupata kitu ambacho kinaweza kukusaidia na kukutoa humu .I’m here to help you”” Akasema Elvis.David akamtazama Elvis kwa macho ya huruma na kutoa machozi “Jikaze Elvis.Niambie ukweli” akasema Elvis “ Elvis nakosa hata sehemu ya kuanzia lakini nakushukuru sana kwa kuja kwako.Japokuwa ni muda umepita lakini bado sura yao naikumbuka.Ahsante sana kwa kuja ndugu yangu.Nimefarijika mno moyoni kwani toka nimefungwa hajawahi kutokea mtu yeyote ambaye ametaka kufahamu nini kilichotokea.Wewe nimtu wa kwanza kutaka kuufahamu ukweli na nitakueleza kila kitu” akasema David halafu akanyamaza kimya akafikiri kwa muda na kusema Ilianza oale tu tulpomaliza mafunzo ya kijeshi na kupangiwa kituo cja kazi.Siku ya kwanza tu,niliporipoti kambini nikiwa katikalindo la jioni ndipo nilipokutana naGraca Frank ambaye baadae nilikuwa kumfahamu kwamba ni mtoto wa brigedia jenerali Frank kwaju.Siku hiyo alikuwa akitaka shuleni.Aklijuwa na mabegi mawili mazito nikamsaidia moja na siku hiyondipo uradfiki wetu ulipoanza.Nilijikuta nikimpenda Graca halikadhalika naye akatokea knipenda.Tukajikuta tukianzisha mahusiano ya kmapenzi .Graca bado alikuwa ni mwanafunzi kwahiyo mahusiano yetu yalikuwa ni ya siri sana” Daid akanyamaza akainama kana kwamba kuna kitu anakumbuka halafu akainua kichwa na kuendelea. “ Siku moja Graca alinipigia simu na kuniomba nionane naye.Siku hiyo alionekana kuwa muoga na mwenye wasiwasi mwingi.Mkononi alikuwa ameshika begi dogo.Alinipa begi na kuniamba kwamba nikalifiche lile na nisimuonyeshe mtu yeyote na wala nisijaribu kufungua na kuangalia kilichomo ndani.Nilichukua begi lile na kwenda kulificha kwangu na sikuwahi kulifungua kuangalia ndani yake kulikuwa na nini” David akanyamaza kidogo kishaakendelea “ Baada ya wiki mbili toka unipatie lile begi,akanipigia simu usiku na kuniuliza kama begi lile ninalo,nikamjibu kwamba badoninalo akakata simu.Nilistushwa na sauti yake usiku ule.Haikuwa sautile niliyoifahamu “ Ilikuaje sautiyake? Akauliza Elvis “ Ilionekana kana kwamba alikuwa analia.Sikutaka kumuuliza kilichomsibu lakini nilistuka sana.Saa kumi na mbili siku ilifuata Graca alinifuata saa kumi na moja alfajiri.Nilistuka sana kwa hali aliyokuwanayo.Macho yake yalikuwa mekundu na yamevimba kwa kulia.Mwili wake ulikuwa umemvimba ilionekana alikuwa amepigwa.Nilijaribu kumuuliza kilichompelekea awe katika hali ile lakini hakunijibu zaidi ya kulia.Aliniomba nimpatie lile begi alilinipa nimuhifadhie.Nilimuuliza kilichokuwamo ndani ya lile begi akasema kwamba itakuwa vyema kwa usalama wangu endapo nisingefahamu katika begi ile kulikuwa na kitu gani.Nilimpatia lile begi akaondoka” David akanyamaza kidogo kisha akaendelea Saa kumi na mbili za asubuhi nilikamatwa na kuwekwa katika mahabusu ya kambi.Nilituhumiwa kwa kosa la ubakaji.Niliambiwa kwamba nilimbaka Graca.Nilistushwa mno na jambo hilo na nikajieleza vya kutosha kwamba sikufanya kitendo kile lakini hakuna aliyeonekana kuniamini.Nilifunguliwa mashitaka ya kijeshi nikakutwa na hatia hivyo nikafukuzwa kazi na kufunguliwa mashitaka mahakamani.Mpaka leo hii sielewi nini kwa nini nilibambikiwa kesi ile lakini ukweli ni kwamba sikumbaka Graca na hata mwenyewe anajua hilo.Nimefungwa sina hatia ninaozea gerezani kwa kosa ambalo sikulitenda.Mpaka leo sielewani kitu gani niliwafanyia Brigedia Frank na mwanae Graca kiasi cha kuniadhibu namna hii.” Akasema David kwa uchungu.Elvis akamtazama akamuonea huruma sana na kusema “ Katika faili lile la kesi yako kuna cheti kinaonyesha kwamba Graca ana matatizo ya akili.Katika kipindi hicho ulichokuwa na mahusiano naye ulimuonaje? Kweli ana matatizo ya akili? “ Hapana.Sikubaliani na mtu yeyote anayesema kwambaGraca alikuwa na matatiozo ya akili.Jambo hilo nimelisikia baada ya kesi yangu kuanza.Ninachofahamu mimi Graca alikuwa mzima kabisa na sikumuona kama ana tatizo lolote la kiakili kama inavyodaiwa.Kuna mtu aliniambia kwamba baada tu ya mimi kuhukumiwa kwenda jela miaka thelathini ,Graca alipelekwa nchini afrika kusini katika hospitali ya magonjwa ya akili iitwayo Nxhasa mental hospital.” akasema David “ Unahisi ni kitu gani hasa kilichomfanya Brigedia frank akubambikie kesi ile ya ubakaji na kukusababishia kifungo hiki? Akauliza Elvis “ Sifahamu kaka.Nimejaribu sana kujiuliza ni kitu gani hasa kilichosababisha hadi nikafungwa gerezani kwa kosa ambalo sikulitenda lakini nimekosa jibu.Nimeamuachia Mungu yote yeye ndiye anayeufahamu ukweli” akasema Davis .Elvis akaendelea kumtazama kwa makini na kumuuliza “ Unahisi ndani ya lile begi alilokupa Graca kulikuwa na nini? “ Sina hakika kulikuwa na nini lakini kwa namna lilivyokuwa ilionyesha ndani yake kulikuwa na kompyuta ndogo.” “ unahisi kilichokuwamo ndani ya hilo begi ndicho kilichopelekea wewe kufikwa na tatizo hili? “ Sina hakika sana lakini ninahisi inawezekana ikawa hivyo.Graca alinisisitiza sana kwamba nisifungue ndani kuangalia kuna nini .Inaonekana kulikuwa na kitu cha muhimu mno ambacho alikuwa anakificha watu wasikione.Hata siku ya mwisho alipokuja kulichukua begi lile nilijaribu kumuuliza kuna nini ndani lakini hakuwa tayari kuniambia.Ninahisi kilichokuwamo ndani ya mkoba ule kina uhusiano wa moja kwa moja na Brigedia Frank.Ninahisi huenda Frank alifahamu kwamba begi lile liko kwangu na kwamba tayari ninafahamu kilichomo ndani yake na ndiyo maana akanifanyia hivi.” Akasema David “ David ahsante sana kwa maelezo yako.Umenipa mwanga mkubwa sana” “ Ndugu yangu nimekueleza ukweli wote bila kukuficha hata kitu kimoja kwa sababu ninakuamini.Tafadhali naomba unisidie kama utaweza ili niweze kutoka humu gerezani.Sina hatia yoyote na mateso ninayopata humu ni makubwa” akasema David “ Pole sana David.Nitakusaidia.Nitafanya kila ninaloweza kuhakikiksha kwamba unatoka humu gerezani.Nimeumizwa sana na kitendo alichokufanyia Frank.Nitakuja kukuona tena baada ya siku chache zijazo lakini kwa sasa naomba usimweleze mtu yeyote kile ulichonieleza.” akasema Elvis halafu akaagana na David akaondoka. “ David amefungwa bila hatia.Nimemtazama machoni.He’s telling the truth.Kwa nini Frank amfanyie hivi? Akawaza Elvis akiwa garini “ Katika faili lile la kesi kuna uthibitisho toka hospitali ukithibitisha kwamba ni kweli Graca alibakwa na David.Dr Herman Mapunda ndiye aliyefanya uchunguzi huo na kuthibitisha kwamba Graca alibakwa.Natakiwa kumtafuta daktari huyu niongee naye” akawaza Elvis na kuongeza mwendo wa gari huku maneno aliyoambiwa na David yakizidi kujirudia kichwani “ Kwa mujibu wa David ni kwamba Graca hakuwa na matatizo yoyote ya kiakili katika kipindi chote cha mahusiano yao.David anadai kwamba baada tu ya kesi yake kuanza ndipo ugonjwa wa Graca ulipoanza.Ninapatwa na wasi wasi mkubwa kuhusiana na jambo hili.Ngoja kwanza nikaonane na Dr Herman halafu nitajua nini kitafuata” Elvis alifika katika hospitali ambako ndiko iliandikwa kwamba Graca alifanyiwa uchunguzi na kubainika kwamba alibakwa.Akashuka na kuelekea ndani ya hospitali.Kulikuwa na wagonjwa wengi na mara akamuona muuguzi mmoja aliyekuwa anongea na simu akamsogelea na kumsubiri hadi alipomaliza kuzungumza na simu akamsabahi “samahani dada yangu.” akasemaElvis.Muuguzi yule aliyevaa vazi lililomkaa vyema akatabasamu na kusema “ Bila samahani kaka yangu,nikusaidie nini? “ Ninahitaji kuonana na Dr Herman Mapunda.Unaweza ukanielekeza mahala ninakoweza kumpata? Akasema Elvis na kumstua yule muuguzi “ Dr Herman?!! Yule dada akashangaa “ Ndiyo .Mbona umeshangaa.Humfahamu? “ Kwani kaka wewe umetokea wapi? Akauliza yule muuguzi “ Nimetokea nje ya nchi .Kuna wakati niliwahi kuwasiliana naye na akaniambia kwambanikija tanzania nije nimtafute hapa” akasema Elvis “ Dah pole sana kaka yangu.Dr DrHerman unayemtafuta hayupo tena katika hospitali hii.” “ Yuko wapi? Amehama kituo cha kazi? Akauliza Elvis “ Dr Herman alikwisha fariki dunia muda mrefu” “Amefariki dunia?..Elvis akashangaa “ Ndiyo amefariki dunia” “ Nini sababu ya kifo chake? “ alianguka ghafla na kufariki.Uchunguzi unaonyesha kwamba moyo wake ulipasuka lakini kuna tetesi kwamba alipewa sumu” Elvis akavuta pumzi ndefu Ahsante sana dada yangu kwa kunipa taarifa hii“akasema Elvis na kuondoka huku yule muuguzi akiendelea kumshangaa “ Dah ! Dr Herman naye amekufa.Ninaanza kuwa na uhakika na hisia zangu kwamba kuna kitu hapa kinachoendelea.Yeye ndiye anayedaiwa kumfanyia uchunguzi Graca na kuthibitisha kwamba ni kweli amebakwa na David.Inawezekana akawa ameuawaa ili kuendelea kuuficha ukweli kuhusiana na kubakwa kwa Graca.Ili kuupata ukweli wa jambo hili natakiwa kuonana na Graca.Yeye ndiye mwenye majibu kuhusiana na kizungumkuti hiki” akawaza Elvis halafu akawasha gari na kuondoka na moja kwa moja kwa akelekea ofisini kwao





akabisha hodi katika ofisi ya mkurugenzi wake “ Elvis unafanya nini hapa mida hii?Unatakiwa uungane na timu ya wenzako” akasema mkurugenzi “ Samahani sana mzee.Nimelazimika kuja kukuona kuna jambo nataka kuongea nawe.Nahitaji tena msaada wako” Mkurugenzi akamtazama kwa makini na kusema “ Evis kuna kitu gani unachokifuatilia?Kitu gani kinachoendelea ambacho hutaki kuniambia? Elvis akavuta kiti na kuketi halafu akasema “ Mzee najua unahitaji sana kujua kitu ninachokichunguza.Nahitaji sana kukueleza ni kitu gani lakini inaniwia ugumu kwa sababu hata mimi mwenyewe bado sijapata undani hasa wa kile ninachokifuatilia.Nahitaji uchunguzi zaidi ili niweze kupata taarifa zenye kutosheleza na ndipo nitakapokuja kwako kukueleza ” akasema Elvis.Mkurugenzi akamtazama na kusema “ Elvis ninakuamini sana kijana wangu na niko tayari kukusaida msaada wowote unaouhitaji lakini nimeanza kuingiwa na shaka kuhusiana na usiri wako katika jambo hilo unalolichunguza” “ Mzee nafahamu kwamba ninakwenda kinyume na taratibu kwa kuchunguza jambo bila kukushirikisha kwanza wewe.Jambo ninalolichunguza ni jambo kubwa na ninahitaji bado kufahamu mambo kadhaa ili niweze kulileta mezani kwako likiwa limekamilika .Naomba muda kidogo ili niweze kukamilisha uchunguzi wangu”akaomba Elvis.Meshack Jumbo akasema “ What do you need this time? “Nahitaji kwenda Afrika ya kusini”akasemaElvis “ Afrika ya kusini? “ Ndiyo mzee “Kufanya nini? “ Kuna mtu ambaye nahitaji kwenda kumuhoji.Nina uhakika yeye ndiye mwenye majibu yote ya kile ninachokichunguza”akasema Elvis “ Kwa hiyo unahitaji nini? “ nahitaji ruhusa ya kwenda huko na endapo nitahitaji msaada wowote nikiwa huko basi nitakufahamisha.Mzee suala hili ni muhimu sana.Utimilifu wa jambo zima ninalolichunguza unategemea sana safari hii” akasema Elvis .Mkurugenzi akafikiri kidogo na kusema “ Umeniacha nikiwa sina uamuzi mwinginezaidi ya kukuruhusu uende huko afrika ya kusini.Pamoja na hayo ukumbuke siku zote kwamba ninakuamini kila unachoniambia kwa niyo pindi ukamilishapo uchunguzi wako ujekwangu mara moja kunieleza” “ Mzee ahsante sana kwa kuniamini .Nakuahidi nitakaporejea nitakuwa na kitu muhimu cha kuweka mezani kwako” Akasema Elvis “ Elvis Kitu kingine ninachotaka kukufahamisha ni kwamba safari hii ni ya siri kati yangu nawe na haitakuwepo katika orodha ya kazi za ofisi kwa hiyo jitahidi asifahamu mtu mwingine yeyote..” akasema mkurugenzi “ Ahsante sana mzee.Ninategemea kuondoka kesho asubuhi na baada ya siku mbili nitarejea.” “ sawa Elvis.Nakutakia kila la heli. Nitaongea na Bongani Makath ambaye ni mtu wetu kule afrika kusini na atakupatia kila aina ya msaada unaouhitaji ukiwa kule” “ Ahsante sana mzee.Tutaonana nitakaporejea” akasema Elvis na kuondoka ili kuanza maandalizi ya safari yake ya kuelekea afrika kusini.







ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA “ Samahani sana mzee.Nimelazimika kuja kukuona kuna jambo nataka kuongea nawe.Nahitaji tena msaada wako” Mkurugenzi akamtazama kwa makini na kusema “ Evis kuna kitu gani unachokifuatilia?Kitu gani kinachoendelea ambacho hutaki kuniambia? Elvis akavuta kiti na kuketi halafu akasema “ Mzee najua unahitaji sana kujua kitu ninachokichunguza.Nahitaji sana kukueleza ni kitu gani lakini inaniwia ugumu kwa sababu hata mimi mwenyewe bado sijapata undani hasa wa kile ninachokifuatilia.Nahitaji uchunguzi zaidi ili niweze kupata taarifa zenye kutosheleza na ndipo nitakapokuja kwako kukueleza ” akasema Elvis.Mkurugenzi akamtazama na kusema “ Elvis ninakuamini sana kijana wangu na niko tayari kukusaida msaada wowote unaouhitaji lakini nimeanza kuingiwa na shaka kuhusiana na usiri wako katika jambo hilo unalolichunguza” “ Mzee nafahamu kwamba ninakwenda kinyume na taratibu kwa kuchunguza jambo bila kukushirikisha kwanza wewe.Jambo ninalolichunguza ni jambo kubwa na ninahitaji bado kufahamu mambo kadhaa ili niweze kulileta mezani kwako likiwa limekamilika .Naomba muda kidogo ili niweze kukamilisha uchunguzi wangu”akaomba Elvis.Meshack Jumbo akasema “ What do you need this time? “Nahitaji kwenda Afrika ya kusini”akasemaElvis “ Afrika ya kusini? “ Ndiyo mzee “Kufanya nini? “ Kuna mtu ambaye nahitaji kwenda kumuhoji.Nina uhakika yeye ndiye mwenye majibu yote ya kile ninachokichunguza”akasema Elvis “ Kwa hiyo unahitaji nini? “ nahitaji ruhusa ya kwenda huko na endapo nitahitaji msaada wowote nikiwa huko basi nitakufahamisha.Mzee suala hili ni muhimu sana.Utimilifu wa jambo zima ninalolichunguza unategemea sana safari hii” akasema Elvis .Mkurugenzi akafikiri kidogo na kusema “ Umeniacha nikiwa sina uamuzi mwinginezaidi ya kukuruhusu uende huko afrika ya kusini.Pamoja na hayo ukumbuke siku zote kwamba ninakuamini kila unachoniambia kwa niyo pindi ukamilishapo uchunguzi wako ujekwangu mara moja kunieleza” “ Mzee ahsante sana kwa kuniamini .Nakuahidi nitakaporejea nitakuwa na kitu muhimu cha kuweka mezani kwako” Akasema Elvis “ Elvis Kitu kingine ninachotaka kukufahamisha ni kwamba safari hii ni ya siri kati yangu nawe na haitakuwepo katika orodha ya kazi za ofisi kwa hiyo jitahidi asifahamu mtu mwingine yeyote..” akasema mkurugenzi “ Ahsante sana mzee.Ninategemea kuondoka kesho asubuhi na baada ya siku mbili nitarejea.” “ sawa Elvis.Nakutakia kila la heli. Nitaongea na Bongani Makath ambaye ni mtu wetu kule afrika kusini na atakupatia kila aina ya msaada unaouhitaji ukiwa kule” “ Ahsante sana mzee.Tutaonana nitakaporejea” akasema Elvis na kuondoka ili kuanza maandalizi ya safari yake ya kuelekea afrika kusini.ENDELEA…………………….. Saa tano za asubuhi ndege ya shirika la ndege la afrika ya kusini ikatua katika uwanja wa ndege wa kimtaifa wa Oliver thambo jijini Johannesburg Afrika ya kusini.Ni siku ya Ijumaa iliyopendezeshwa na kijua kitamu .Elvis akiwa ni mongoni mwa abiria waliosafiri na ndege hii kutokea jijini Dar es salaam alishuka ndegeni na kukamilisha taratibu za kiuhamiaji halafu akatoka na kupokelewa na Bongani Makath wakala wa idara ya ujasusi ya Tanzania nchini Afrika ya kusini.Kisha salimiana wakaongia garini na safari ya kuelekea nyumbani kwa Bongani ikaanza. Bongani alikuwa na jumba kubwa na zuri.Elvis akakaribishwa ndani na maongezi ya kikazi yakaanza. “ Elvis karibu sana afrika ya kusini” akasema Bongani ‘ Ahsante sana Bongani.Nyumba yako nzuri sana nimeipenda” akasema Elvis “ Ahsante sana Elvis.Habari za Dar es salaam? Ni muda mrefu hatujaonana” “ Dar es salaam kwema.Ni kweli ni muda mrefu hatujaonana” akasema Elvis.Kikapita kimya kifupi Bongani akasema “ Nimelifanyia kazi lile suala ulilonieleza na tayari nimekwisha ongea na uongozi wa hospitali ile na wametoa ruhusa ya kuonana na mgonjwa unyemtaka.Kwa mujibu wa melezo yao ni kwamba mgonjwa huyo hali yake inaendelea vizuri kwa sasa na ana uwezo wa kuhojiwa jambo lolote”akasemaBongani Bila kupoteza muda Bongani na Elvis wakaingia garini na safari ya kuelekea hospitali ikaanza ***************** Saa saba za mchana katika uwanja wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam dege la shirika la ndege la Qatar airways linatua .Miongoni mwa abiria walioshuka walikuwepo watu wawili waliokuwa wamevalia nadhifu sana.Watu wale walikamilisha taratibu za uhamiaji na kuruhusiwa kuingia nchini.Katika sehemu ya kupokelea abiria wanaowasili watu wane walikuwa wakiwasubiri wale jamaa wawili na walipowaona wakawapokea na kuwaongoza hadi katika gari mbili zilizokuwa nje ya uwanja wakaingia na kuondoka na moja kwa moja wakaelekea Silvano hoteli moja ya hoteli inayosemekana kwamba ni kubwa na ya ghali kuliko zote nchini Tanzania. Dakika kama ishirini toka wawasili pale hotelini gari moja jeusi likawasili na akashuka Brigedia Jenerali Frank Kwaju akiwa ameongozana na watu wawili na miongoni mwao alikuwepo Pascal Situmwa.Chrispine Akwite akawapokea na kuwaongoza hadi ghorofa ya juu waliko wale wageni wawili.Brigedia Frank na ujumbe wake wakasalimiana na wale jamaa “ Karibuni sana Tanzania” akasema Frank “ Ahsante sana Frank.Tunashukuru” wakajibu wale jamaa kwa pamoja “ Habari za Tanzania? Mambo yanakwendaje hapa? Akauliza mmoja wa wale jamaa “ Habari za hapa ni nzuri na kila kitu kinakwenda kama kawaida.Mheshimiwa Daudi Sichoma tayari nimekwisha wasiliana naye na jioni ya leo tutakuwa naye katika kikao.Msiwe na wasi wasi kila kitu kitakwenda vizuri.” Akasema Frank .Baada ya maongezi kidogo wakaagana kwa ajili ya kwenda kujiandaa na kikao kitakachofanyika jioni ya siku hiyo.Frank akiongozana na Pascal pamoja na mtu mwingine wakaingia garini na kuondoka “ Frank wewe ni rafiki yangu na kila kitu tunafanya pamoja lakini nashangaa mpaka sasa hivi hujanieleza chochote kuhusiana na wale jamaa.Who are they? Frank akamtazama na kusema “ Usiwe na haraka Pascal.Utafahamu kila kitu katika kikao cha pamoja leo jioni” Pascal akavuta pumzi ndefu na kusema “ Frank mimi na wewe tumekuwa ni washirika wakubwa sana na kwa muda mrefu.Kila jambo tumekuwa tukilifanya pamoja na hatujawahi kufichana jambo lolote.Kama mshirika na mtu wako wa karibu nina haki ya kufahamu ni kitu gani kinachoendelea kabla hata ya hicho kikao” akasema Pascal “ Pascal ni kweli wewe ni mshirika wangu mkubwa lakini nasikitika kwamba sintaweza kukueleza kwa sasa ni kitu gani kinachoendelea.Naomba uvute subira hadi jioni kuna jambo zuri sana utalifahamu” akasema Frank “ Frank unanishangaza.Haijawahi tokea hata siku moja ukanificha jambo.Kuna nini kinachoendelea? Halafu umenistua sana ulipomtaja Daudi Sichoma kwamba naye atahusika katika kikao cha jioni.Huyu ni waziri mkuu mstaafu anahusikaje na sisi? Tafadhali naomba uniweke wazi Frank”akasema Pascal “ Pascal naomba usiwe na haraka sana lakini kwa kukudokeza tu ni kwamba kuna jambo zito lililowaleta wale jamaa na ndiyo maana waziri mkuu mstaafu Daudi Sichoma naye atashiriki katika kikao.Vuta subira kidogo tu na utafahamu kilakitu” akasema Frank na Pascal hakutaka kuuliza tena wakaendelea na safari yao ******************** Geti la hospitali ya magonjwa ya akili iliyopo nje kidogo ya jiji la Johannesburg likafunguliwa na gari aina ya range rover yenye rangi nyeupe ikaingia na kusimama katika kibanda cha walinzi kwa ajili ya ukaguzi.Mlinzi mmoja aliyevalia sare za kampuni binafsi ya ulinzi akalisogelea lile gari na Bongani aliyekuwa akiendesha akashusha kioo akasalimana naye kwa lugha ya kizulu wakaongea kidogo halafu akamruhusu apite “ Unafahamiana na yule mlinzi?akauliza Elvis “ Hapana sifahamiani naye.Nimemchangamkia tu ili kujenga mazoea naye.Siku zote ukitaka watu kama hawa wasikubughudhi basi jishushe na ujiweke chini yao”akasema Bongani na kuegesha gari katika maegesho ya hospitali kisha wakashuka na kuingia katika jengo la utawala .Moja kwa moja wakanyoosha hadi katika mlango uliokuwa na kibao kidogo juu Dr Susan Ndaba Dlamini.Bongani akagonga mlango na sauti toka ndani ikawaruhusu wapite.Wakaingia na kukutana na mwanamke mmoja mrembo sana mwenye tabasamu la kuvutia.Aliwasalimu kwa furaha na kukakaribisha “Karibuni sana” akasema Dr Susan “ Ahsante sana Susan.Huyu hapa ni yule mwenzangu toka Tanzania anaitwa Elvis.Tumekuja kuhusiana na lile suala nililokwambia .Tunataka kuongea machache na Graca” akasema Bongani.Dr Susan akaweka chini kalamu yake na kuwatazama akina Elvis kwa makini kisha akasema “ Hali ya Graca kwa sasa inaendelea vizuri na anazidi kuimarika siku hadi siku tofauti kabisa na wakati alipoletwa.Kinachonishangaza kidogo ni kwamba kuna nyakati anakuwa mzima kabisa na kuna nyakati huwa ana badilika na kumshangaza kila mtu.Nikimuangalia sana Graca ninahisi kuna jambo analo moyoni.Haonekani kama ni mgonjwa wa akili niliowazoea.Ninasema hivyo kwa sababu nimekuwa karibu naye sana toka alipoletwa na ninamfaamu vizuri” Akasema Dr Susan na kuinuka na kuwaomba akina Elvis wamfuate.Waliongozana hadi katika bustani kubwa iliyokuwa na viti vizuri na maua ya kupendeza.Kulikuwa na sehemu nyingi za kukaa kupumzika na baadhi ya wagonjwa walionekana wakiwa wamekaa na madaktari wao.Dr Susan akawaambia akina Elvis waketi katika mojawapo ya sehemu za kupumzikia na wamsubiri akamlete Graca “ Unafahamiana na Dr Susan?akauliza Elvis baada ya Dr Susan kuondoka.Bongani akatabsamu na kusema “ Ndiyo ninafahamiana naye ni mtu wangu wa karibu sana ndiyo maana umeona imekuwa rahisi kuruhusiwa kuingia huku na kuonana na mgonjwa.Kwa kawaida kuja kumuona mgonjwa hapa huwa ni jambo lenye utaratibu mrefu kidogo lakini kwetu sisi imekuwa rahisi” akasema Bongani huku akitabasamu “ Hata mimi nimeshangaa kutokana na urahisi huutulioupata tofauti kabisa na nilivyokuwa nimetazamia” akasema Elvis na mara kwa mbali akatokea Dr Susan akiwa amemshika mkono binti mmoja mrefu mwembamba mweupe.Walikuwa wakitembea huku wakiongea na kucheka kama marafiki wakubwa “ Thats Graca” akasema Elvis.Bongani akamtazama na kusema Unasemaje Elvis? “ Sikutegemea kama ni binti mzuri kiasi hiki”akasema Elvis huku bado akiendelea kumkodolea macho Graca aliyekuwa akija taratibu akiongozana na Dr Susan.Baada ya kufika mahali pale walipokuwa wamekaa Bongani na Elvis wakasimama,Elvis akamvutia Graca kiti akaketi .Dr Susan akakohoa kidogonakusmea “ Bongani na Elvis huyu ndiye Graca.Ni mrembosana.Mnamuonaje? akatania Dr Susan na wote wakatabasamu “Ni kweli ni mrembo sana” akasema Elvis huku akiendela kumkodolea macho niti yule mwenye macho ya aibu.Graca alikuwa anaonekana ni mzima wa afya na ilikuwa vigumu kuamini kwamba alikuwa mgonjwa wa akili “ She’s so pretty” akawaza Elvis akiendelea kumtazama Graca kwa macho ya kuibia “ Graca hawa ni wageni wako” akasema Dr Susan “Huyu hapa anaitwa Mr Bongani ni mwenyeji wa Johannesburg na huyu hapa anaitwa Elvis toka jijini Dar es salaam.” Dr Susan akafanya utambuliso “ Karibuni sana” akasema Graca kwa sauti ndogo na laini “ Ahsante sana” wakajibu kwa pamoja Elvis na Bongani “ Elvis nadhani itakuwa vyema tukiwaacha wewe na Graca muongee.Graca hana matatizo yuko katika hali nzuri leo na atakujibu kila kitu unachokihitaji toka kwake” akasema Dr Susan halafu yeye na Bongani wakainuka wakaelekea katika benchi lililokuwa mbali kidogo. “ Pole sana Graca.Unaendeleaje ? akaanzisha maongezi Elvis “ Ahsante sana Elvis.Ninajisikia vizuri sana.Umetokea Tanzania? Akauliza Graca “ Ndiyo nimetokea Tanzania.” “Umenifahamuje? Tumewahi kuonana? “ Hatujawahi kuonana ila nimekufahamu kupitia kwa David Elifariji” Graca akastuka mno baada ya kusikia jina la David likitajwa. Umesema David Elifariji? Unamfahamu? ”akauliza Graca “ Ndiyo ninamfahamu .Nmeonana naye kabla sijaja huku” “ Anaendelaje? Akauliza Graca “ Anaendelea vizuri” akajibu Elvis.Graca akainamisha kichwa machozi yakamtoka “ Ninaitwa Elvis tarimo”akasemaElvis na Graca akainua kichwa akamtazama “Ninafanya kazi katika idara ya ujasusi nchini Tanzania.Nilihitimu mafunzo ya kijeshi na David halafu nikaondoka kuelekea nchini Marekani kwa mafunzo zaidi” Elvis akanyamaza akamtazama Graca kisha akasema “ Hivi majuzi kulitokea tukio moja ambapo mwanamke mmoja alipoteza fahamu kwa muda wa miezi miwili.Alipozinduka nilifanikiwa kumuhoji na akasema kwamba aliyeamrisha apigwe hadi auawe ni mwajiri wake ambaye ni mfayakazi wa idara ya usalama wa taifa.Nilimfanyia uchunguzi mtu huyo na ndipo nilipogundua kwamba alikuwa na mahusiano ya karibu na baba yako Brigedia jenerali Frank kwaju.Nilijiuliza maswali mengi kuhusiana na ukaribu huo na ndipo nilipomkumbuka David.Wakati naondoka kuelekea Marekani kwa mafunzo,kesi ya David ilikuwa bado ikiunguruma kwa hiyo sikujua hatima yake.Ilinilazimu kumfuata David gerezani na kuonana naye” akasema Elvis “ Nimeonana na David,nimeongea naye na amenieleza mambo mengi .Amenieleiza mkasa mzima uliompelekea afungwe gerezani.Toka ndani kabisa mwa moyo wake amekiri kwamba hakutenda lile kosa na alibambikiwa ile kesi ya ubakaji.Nilimuamini na kuahidi kumsaidia na ndiyo maana nimelazimika kuja kuonana nawe.Kuna mambo ambayo nahitaji kuyafahamu toka kwako ambayo yatatusaidia katika kumsaidia David anayetumikia kifungo cha miaka thelathini gerezani” akasema Elvis.Graca akainama na kutoa machozi na kusema “ Unataka nini toka kwangu? “ Graca nimelisoma faili la kesi.Kuna ushahidi mzito uliotolewa ukiwemo wa daktari aliyekufanyia uchunguzi na kuthibitisha kwamba ni kweli ulibakwa na David.Daktari huyo aliyeithibitishia mahakama tayari amekwishafariki na inasemekana alifariki kwa sumu.Kilichonileta hapa ni kufahamu ukweli toka kwako kwani wewe ndiye muhusika mkuu wa sakata hili.Ni kweli David alikubaka? Ni kweli wewe una matatizo ya akili kama faili lako linavyoonyesha? akauliza Elvis.Graca akainama na kuanza kulia.Elvis akatoa kitambaa kisafi na kumpatia Futa machozi .naomba tafadhali nieleze kila kitu unachokifahamu kuhusiana na sakata hili.Ukweli wako ndio utakaonipa nguvu ya kumsaida David kutoka gerezani” akasema Elvis.Graca akafuta machozi na kusema “ Sifahamu chochote .Ulichokisoma katika faili ndicho sahihi” akasema Graca huku machozi yakimtoka. Elvis alimtazama Graca kwa makini na kisha akasema “ Graca please tell me the truth.Nimelipitia faili la kesi na nimegundua mambo mengi ambayo nina mashaka nayo.Nimeongea na David amekiri kwamba hakutenda lile kosa and I do believe him.Ninataka nisikie pia na kwa upande wako,unasemaje? Ninataka nimsaidie David ambaye anateseka gerezani kwa kosa ambalo naamini hakulitenda .Tafadhali naomba unieleze ukweli” akasema Elvis.Graca akaendelea kulia.Elvis akainuka na kwenda kumshika bega. “ Please Graca I need to know the truth” akasema Elvis.Graca akamtazama Elvis kwa makini usoni na kusema “ Kwa sababu ya David nitakueleza ukweli” “ Ahsante GracaYou are doing the right thing” Sekunde kadhaa zikapita Graca akiwa kama mtu anayekumbuka jambo halafu akasema kwanza kabisa naomba nikuweke wazi kwamba hauongei na mgonjwa wa akili.Mimi si mgonjwa wa akili na sikuwahi kuwa na ugonjwa huo” akasema Graca “ Reall !!? Elvis akashangaaa “ usishangae Elvis.Hakuna anayejua jambo hili zaidi yangu na nitakueleza baadae ni kwa nini nimeletwa kutibiwa katika hospitali hii ya magonjwa ya akili”akasema Graca “ tell me everything” akasema Elvis Graca akamtazama Elvis usoni na kuendelea “ Siku moja mama alifanikiwa kuingia katika chumba cha baba ambacho hukitumia kama ofisi yake ndogo awapo nyumbani.Katika chumba hicho hakuna yeyote ambaye anaruhusiwa kuingia.Sifahamu aligundua nini lakini alinipa mkoba uliokuwa na kompyuta ndogo mkononi akaniomba nikaufiche mahala ambako hakuna yeyote anayeweza kuona.Jioni ya siku hiyo kulitokea mzozo mkubwa baina ya baba na mama.Nilimsikia mama akimlaumu baba kwa kujiingiza katika biashara haramu .Sikuelewa mara moja ni biashara zipi alizokuwa akiongelea mama .Baada ya siku tatu toka utokee mzozo ule mama alifariki dunia katika ajali ya gari akiwa safarini kuelekea Morogoro.Gari lake lilipasuka tairi na kupinduka” Graca akainama na kufuta machozi halafu akaendelea “ Baada ya mama kufariki,baba alinifuata na kuniuliza endapo mama aliwahi kunipa mzigo wowote nikaufiche.Nilikataa kumweleza ukweli ikamlazimu atumie vitisho na ndipo nilipochukua lile begi na kwenda kulificha kwa David ambaye kwa wakatio huo tulikuwa katika mahusiano ya kimapenzi.Vitisho vilizidi na siku moja baba alinikamata na kunitesa sana akatishia kuniua endapo nisingemuonyesha mahala lilipo begi lake.Alinitesa sana usiku huo.Kulipopambazuka alfajiri nilidamka na kwenda kuchukua lile begi kwa David.Sikujua kama kuna watu waliokuwa wananifuatilia.Nilipotoka niliona kuna watu wawili wakishuka garini.Niliwafahamu watu wale ni washirika wa baba ikanilazimu kupenya dirishani na kukimbia na kwenda kulifcha begi lile sehemu ninakojua.Saa tatu za asubuhi nilipata taarifa kwamba David amekamatwa kwa kosa la ubakaji.Niliogopa sana kwani baba alikwisha ahidi kufanya jambo lolote kuhakikisha kwamba begi lake linapatikana.Kwa namna alivyonitesa na kunitisha niliogopa kuna uwezekanao anaweza hata kuniua hivyo ikanilazimu kujifanya kama nimechanganyikiwa hivyo kuwafanya watu wamtaarifu baba ambaye alinikamata na kunipeleka katika hospitali ya taifa kitengo cha magonjwa ya akili.Pamoja na kulazwa pale bado baba aliendelea kuwasisitiza madaktari kwamba wajitahidi ili niweze kupata nafuu haraka lengo lake nikamuonyeshe mahala lilipo begi lake.Niliendelea kujifanya mgonjwa wa akili na sikuonyesha dalili zozote za kupata nafuu na ndipo baba alipoamua kunileta huku afrika ya kusini na kunitupa hapa.Toka aliponileta hajawahi hata siku moja kuja kuniangalia au hata kunijulia hali.”akasema Graca na kuanza kulia.Elvis akainuka na kumshika bega akambembeleza anyamaze.Graca akafuta machozi na kuendela. “Ukweli ni kwamba David hakutenda kosa hilo alilodaiwa kulifanya,hakunibaka na wala asingeweza kufanya hivyo kwa sababu upendeo wake kwangu hauna kipimo.Ninasikitika sana Elvis kwa kuishi maisha haya .Ninapewa madawa mengi makali na kunifanya nidhoofu namna hii.Sielewi nitaishi hivi mpaka lini.Sitaki kujifanya nina nafuu kwani baba atatarifiwa naatakuja kunitoa hapa” Graca akashindwa kujizuia kuangua kilio.Elvis akainuka tena na kwenda kumbembeleza “ Nyamaza kulia Graca.” akasema Elvis “ Inauma sana Elvis.Ninasikia maumivu makali ya moyo.Uchungu ninaoupata huelezeki” Pole sana Graca”akasema Elvis halafu ukimya ukatawala “ Kwa sasa nina hakika lazima katika hilo begi kuna siri nzito ambayo inamfanya brigedia Franka asiwe hata na huruma kwa mwanae.Mpaka Graca kuamua kujifanya ni mgonjwa wa akilini wazi aligundua kwamba baba yake angeweza hata kumuua.Ninachotaka kufahamu toka kwa Graca kuna nini ndani ya hilo begi? akawaza Elvis halafu akakohoa kidogo na kuita kwa sauti ya upole “ Graca !!.. Graca akainua kichwa akamtazama Elvis . Machoyake yalikuwa mekundu . “ Graca nimechomwa sana na maelezo yako .Naelewa uko katka kipindi kigumu na cha mateso makubwa.Nakuahidi kufanya kila lililo ndani ya uwezo wangu kukusadia wewe na David na kuwaondoa katika mateso haya mliyo nayo” akasema Elvis halafu akavishika viganya vya mikono ya Graca na kusema “ Please trust me.I’ll do anything I can to help you.I give you my word” akasema Elvis “ Ahsante sana Elvis .Naomba kama una uwezo wa kunisaidia tafadhali nisaidie.Mateso ninayoyapata ni makubwa.Nimechoka kuishi maisha haya ya mateso lakini naogopa kuondoka hapa kwani baba akinipata atanifanyia jambo baya.Nina hakika mpaka aleo hii bado atakuwa akitaka kufahamu

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/





ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog