Search This Blog

Saturday 5 November 2022

PENIELA (STORY YA KIJASUSI) - 1

 




IMEANDIKWA NA : PATRICK CK



*********************************************************************************



Simulizi : Peniela (Story Ya Kijasusi)

Sehemu Ya Kwanza (1)




Ni saa sita za usiku sasa bado jaji Elibariki chukuswa yuko sebuleni akiendelea kupitia kitabu chake cha sheria .Katika meza ndogo kulikuwa na vitabu vingine zaidi ya saba vya sheria.Aliendelea kufungua ukurasa baada ya ukurasa.Alionekana kuwa na mawazo mengi mno.Wakati akiendelea kupitia kurasa za kitabu kile mke wake akaingia pale sebuleni akiwa na kikombe cha kahawa, akakiweka mezani halafu akainama na kumbusu mumewe.



“ You need to take a rest now.Tommorow is your big day” akasema Flaviana mwanamke mwenye uzuri wa kipekee.Elibariki akakifunika kitabu chake na kumtazama mkewe ,akachukua kikombe cha kahawa akanywa kidogo na kusema



“ Natamani sana nipumzike lakini sina hakika kama nitapata usingizi.”

Mke wake akamuangalia kwa makini halafu akasema

“ Kuna jambo nataka nikuulize mume wangu”

“ Uliza usihofu ”

“ Najua kesi hii ni moja kati ya kesi kubwa na ngumu kwako.Hukumu unayotarajia kuitoa kesho inasubiriwa kwa hamu kubwa sana na umma wa watanzania.Wewe ni jaji na nina imani maamuzi yako utakayoyachukua ni sahihi kabisa,lakini swali langu ni je Yule msichana ana hatia?

Swali lile lilionekana gumu sana kwa jaji Elibariki.Akainama akafikiri kidogo halafu akachukua kikombe cha kahawa akanywa kidogo na kumtazama mkewe.



“ My love kesi hii ni ngumu sana na imejaa utata mwingi na ndiyo maana unaniona mpaka hivi sasa bado niko hapa.” Akasema Elibariki

Flaviana akamtazama mume wake na akagundua kwamba hakuwa tayari kumjibu swali alilouliza.Akas

imama na kusema



“ Sina wasi wasi na maamuzi utakayoyatoa kesho lakini nakuomba utoe haki kwa upande wenye haki.”

Elibariki hakumjibu kitu akabaki akimuangalia

“ Come to bed when you are done,but don’t stay till very late.You have a big day tomorrow.” Akasema Flaviana na kuelekea chumbani .Elibariki akavuta pumzi ndefu na kuchukua kitabu chake cha sheria akaendelea kukisoma.

“ Katika maisha yangu ndani ya sheria sijawahi kukutana na kesi ngumu yenye mitihani kama hii.Hata hivyo niliapa kusimamia sheria na kutenda haki kwa kila mwenye haki.



Katika maamuzi yangu ya kesho lazima nifanye kwa haki japokuwa nina hakika nitakuwa katika matatizo makubwa baada ya hukumu ya kesho lakini siwezi kupindisha sheria eti tu kwa sababu ya shinikizo toka kwa mtu au kikundi cha watu.Mungu ataniongoza na kunisimamia ili nitoe hukumu ya haki” akawaza Elibariki na kufunga vitabu vyake akaelekea chumbani kulala.tayari Flaviana mke wake amekwisha lala.Akamtazama kwa makini na kujisemea moyoni



“ Nina hakika hata wewe hautanitazama vizuri baada ya hukumu ya kesho,lakini sina namna nyingine zaidi ya kutenda haki.Utanisamehe mke wangu” akawaza Elibariki na kupanda kitandani kulala.



***********



“ Eli my love,amka kumekucha !! ..Ilikuwa ni sauti tamu na laini ya Flaviana akimuamsha mumewe.Jaji Elibariki ambaye asubuhi hii alionekana kuzama katika usingizi mzito akafumbua macho huku akiguna na kutazama saa ya ukutani.Ni saa kumi na mbili na dakika ishirini za asubuhi.

“ jana sikupata usingizi kabisa.Usiku wangu ulikuwa mrefu sana” akasema kwa sauti ya uchovu.



“ Please wake up honey.Today its going to be a very long day” akasema Flaviana.Elibariki akainuka na kuelekea katika chumba chake cha mazoezi akafanya mazoezi kidogo halafu akaelekea bafuni.Bado kichwa chake kiliendelea kuwa na mawazo mengi sana.Kisha oga akarejea chumbani na kukutana na suti nzuri aliyoandaliwa na mke wake akavaa na kujitazama katika kioo kikubwa kilichokuwamo chumbani mwao.Aliganda pale katika kioo hadi mke wake alipoingia naye akaanza kujiandaa.



“ Leo unakwenda kazini? Akauliza Jaji Elibariki.Flaviana akacheka kidogo na kusema

“ Usinichekeshe mume wangu,yaani niende kazini leo? Siwezi kufanya hivyo hata kidogo.Leo ni siku yako kubwa.Ni siku yetu kubwa.Ni siku ambayo jina lako litaingia katika vitabu vya historia kwa hukumu unayokwenda kuitoa.Vyombo vyote vya habari vitakuwepo mahakamani ,lazima na mimi niwepo nikuunge mkono pamoja na mdogo wangu Anna.” Akasema Flaviana.Elibariki hakujibu kitu akaendelea kujitazama katika kioo.



“Are you nervous my love? Akauliza Flaviana

“ No I’m not” akajibu Elibariki halafu wakaongozana kuelekea katika chumba cha chakula kwa ajili yakupata kifungua kinywa.Wakati wakiendelea na kupata kifungua kinywa simu ya Jaji Elibariki ikaita.Akaitazama ikiita akasita kuipokea.

“ Mbona hupokei hiyo simu? Akauliza Flaviana

“ Its your father.Mr President” akajibu Elibariki

“ Usiogope.Ongea naye .Si kawaida yake kupiga simu mida kama hii.Inawezekana ana jambo la maana la kukwambia” Akasema Flaviana.Elibariki akaichukua simu na kubonyeza kitufe cha kupokelea huku akiinuka na kuelekea sebuleni.



“ Hallo Mr President” akasema Jaji Elibarki

“ Hallo Jaji.Mnaendeleaje vijana wangu?

“ Tunaendelea vizuri mzee.Ninyi mnaendeleaje?

“ Tunaendelea vizuri sana”http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“ Nashukuru kusikia hivyo” akasema Elibariki na kimya kifupi kikapita

“ Elibariki,today its your big day” akasema Mheshimiwa rais.

“ Najua unakwenda kutoa hukumu katika kesi ngumu inayovuta hisia za watu wengi na hasa kwa kuwa binti wa rais naye kesi hii inamuhusu kwani mchumba wake ndiye aliyeuawa.Sikufundishi kuifanya kazi yako lakini fanya maamuzi ya haki kwa namna uonavyo wewe.Pamoja na hayo kuna jambo ambalo nataka kukuomba kijana wangu” Akasema Dr Joshua Johakim rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania.



“ Nakusikiliza mzee” akasema Jaji Elibariki kwa wasi wasi .

“ Nilikuteua kuwa jaji kwa sababu wewe ni msomi mzuri na unazifahamu sheria za nchi kwa hiyo sitaki kuingilia maamuzi yako lakini nakuomba kijana wangu,try in anyway you can to make my daughter Happy.Alimpenda sana Edson.Ni hilo tu ninalotaka kukuomba kijana wangu.Nakutakia siku njema” akasema mheshimiwa rais na kukata simu.Jaji Elibariki alibaki ameduwaa asijue afanye nini.Maneno yale ya rais ambaye ni baba mkwe wake yalimfanya ahisi kuchanganyikiwa.



“ Huu ni mtihani mgumu sana lakini Mungu atanitangulia nitatenda haki” akawaza Elibariki na kurejea mezani

“ Amekwambia nini baba? Mbona sura yako imebadilika namna hiyo? Akauliza Flaviana

“ Nothing.Just greetings” akajibu Elibariki na kuendelea kupata kifungua kinywa.Baada ya kumaliza akarejea chumbani na kujitazama tena katika kioo na kuvuta pumzi ndefu.



“ Please help me Lord.I’m in a very difficult situation” akasema Elibariki kwa sauti ndogo na mara mke wake akaingia mle chumbani

“ Its time my love.Are you ready?

“ Let’s go” akasema Elibariki ,wakatoka wakaingia garibni na kuondoka.



**********



Hakukuwa na nafasi tena ya kukaa ndani ya chumba cha mahakama kutokana na watu kujaa.Ni siku ya hukumu ya kesi ya mauaji inayomkabili mmiliki wa maduka makubwa ya mavazi ya Penny Fashion,Peniela Salimote.Kesi hii iliyovuta hisia za watu wengi na kuwafanya wafurike ili kuja kusikia hukumu ilikuwa inaonyeshwa moja kwa moja katika runinga.ILikuwa ni kesi ya kwanza kubwa kurushwa moja kwa moja katika runinga.Katika kila kona ya nchi watu walikuwa wakifuatilia matangazo ya moja kwa moja ya kesi hii ambayo hukumu yake ilikuwa inasubiriwa na watu wengi.



Ndani ya chumba cha mahakama ilikuwepo familia ya rais ikiongozwa na mke wa rais,Dr Flora Johakim ambaye alikuwa ameambatana na binti zake wawili Flaviana na Anna.Familia ya Edson Kobe kijana anayedaiwa kuuliwa na Peniela nayo ilikuwepo mahakamani hapo ili kuhakikisha kwamba haki inatendeka.Familia ya Edson na ile ya rais zilikuwa ni familia rafiki kwa muda mrefu sana.Kwa upande wa Penny hakukuwa na ndugu yake yeyote aliyefika mahakamani pale zaidi ya rafiki zake wachache.



Tayari mtuhumiwa amekwisha ingizwa mahakamani na aliyekuwa akisubiriwa ni jaji anayeisikiliza kesi ile aweze kuingia na kuisoma hukumu.Wakati wakimsubiri Jaji aingie,Jason Patrick mwanasheria anayemtetea Penny alikuwa akibadilishana mawili matatu na mteja wake .

“ Jason,kabla hukumu haijaanza ninaomba nikwambie kitu.” Akanyamaza kidogo na kuendelea.



“ Nakushukuru sana kwa kila kitu ulichonifanyia.Umenisimamia katika kesi hii kwa kila namna ulivyoweza.Najua chochote kinaweza kikatokea siku ya leo hivyo nakuomba endapo ikitokea nikakutwa na hatia na kufungwa kifungo cha maisha au kifo uhakikishe yale yote niliyokuandikia katika karatasi unayatimiza.Wewe ni zaidi ya rafiki.Wewe ni ndugu yangu pekee ninayekutambua.Ninakukabidhi kila kilicho changu endapo mambo yataenda kinyume na matarajio yetu." Akasema Penny huku machozi yakimtoka

“ Penny naomba usikate tamaa hata kidogo.Nimepambana vya kutosha kuhakikisha kwamba tunashinda kesi hii lakini kama mambo yataenda tofauti na matarajio yetu hautakuwa ni mwisho.Nitapambana hadi nihakikishe haki imepatikana.” Akasema Jason na mara jaji akaingia.



Wakati Jaji akiingia Penny akamnong’oneza Jason sikioni

“ I didn’t do it.I didn’t kill him”

“ I know Penny and I believe you” akasema Jason na mara mahakama ikaanza.”





Masaa manne yamekwisha katika sasa toka Jaji Elibariki alipoanza kuisoma hukumu .Ndani ya chumba cha mahakama kulikuwa na ukimya mkubwa kila mtu akifuatilia kwa umakini mkubwa kila alichokisema Jaji.Baada ya maelezo marefu kuhusiana na mwenendo mzima wa kesi ,hatimaye ukafika wakati wa kuhitimisha hukumu,wakati ambao ni mgumu kwa kila mtu mle mahakamani.Mke wa rais Dr Flora Joakin alishikana mikono na wanae Flaviana na Anna wakipeana moyo.Familia ya Edson halikadhalika walikuwa katika wasi wasi mkubwa kwani hakuna aliyejua jaji anakwenda kusema nini.



Toka alipoingia ndani ya chumba cha mahakama,Anna mtoto wa rais amekuwa akimtazama kwa hasira Peniela aliyekaa ndani ya kizimba kilichokuwa mbele kabisa ya mahakama.



“ Leo ndiyo siku yako ya mwisho kahaba wewe,mdanida waume za watu.Ndani ya muda mfupi ujao utayaanza maisha mapya gerezani paka wewe.Nilikuahidi kwamba utaozea gerezani na sasa utayaamini maneno yangu.Mwangalie kwanza alivyopauka na kukondeana kama muwa.” Akawaza Anna akiendelea kumtazama Penny kwa hasira

“ Ulinitenganisha na Edson mwanaume niliyempenda kuliko wote duniani.Urafiki wetu ulianza toka utotoni lakini ulivuruga kila kitu na mwishowe Edson akaniacha.Ninakuchukia wewe mwanamke na na laiti ningekuwa na uwezo ningekukata masikio “ Anna aliendelea kuwaza na akashindwa kuyazuia machozi kumtoka .Kitendo cha kumuona tena Peniela kilimrejeshea taswira ya Edson mwanaume aliywahi kumpena kupindukia.Akainama na kufuta machozi



Wakati kila mtu moyo ukimuenda mbio akisubiri maamuzi ya Jaji,Peniela alikuwa amefumba macho michirizi ya machozi ikionekana mashavuni pake.Alikuwa akiomba.



“ Ee Mungu baba,wewe ndiye mwenye uwezo wa kuona kila kitu hadi ndani ya mioyo yetu.Baba unafahamu sijatenda kosa hili ninaloshtakiwa nalo.Nimeteseka gerezani kwa mwaka mzima na hakuna anayeonekana kuniamini kwamba sikumuua Edson.Baba imetosha sasa na ninaomba kwa mapenzi yako itolewe hukumu ya haki”

Jason mwanasheria wake alikuwa amemuelekezea macho akimtazama na kumuonea huruma sana.



“ She’s Innocent.She didn’t kill him.Please Lord help her” akawaza Jason.Penny aliendelea kuyafumba macho yake machozi yakiendelea kumtoka na mikono yake akiwa ameifumbata kifuani .Jaji Elibariki aliendelea kumalizia kuisoma hukumu yake

Taratibu Penny alihisi miguu yake inaisha nguvu pale Jaji alipotamka kwamba upande wa mashtaka umeshindwa kuithibitishia mahakama kwamba Penny alimuua Edson licha ya kuwasilisha ushahidi na vielelezo vingi.Jaji Elibariki alikwenda mbali zaidi na kuainisha namna ushahidi uliotolewa mahakamani ulivyokosa nguvu ya kuweza kumtia hatiani mshtakiwa kwa hiyo kwa mujibu wa mamlaka aliyopewa anamuachia huru Penny.Alipotamka tu maneno hayo Penny akaanguka na kupoteza fahamu.



**********



Mtu wa kwanza kumtambua baada ya kurejewa na fahamu akiwa hospitalini alikuwa ni Jason mwanasheria wake.Mara tu alipopoteza fahamu baada ya Jaji kumuachia huru ,Penny alikimbizwa katika hospitali ya karibu kwa ajili ya huduma ya kwanza.



“ Jason ..!.akasema Penny kwa sauti dhaifu huku akitaka kuinuka lakini akashindwa mwili haukuwa na nguvu.

“ Penny relax ..!!!..Endelea kupumzika…” kabla hajamaliza sentensi yake Penny akapoteza tena fahamu.



“ Amepatwa na mstuko mkubwa huyu binti.Tunahitaji kumuweka hapa kwa muda tuendelee kumuangalia” akashauri daktari.

Jason Patrick mwanasheria anayemtetea Penny hata naye bado alikuwa katika kutoamini kama ni kweli Penny ameachiwa huru.Alifanya kazi kubwa ya kumtetea Penny lakini ushahidi uliowasilishwa na upande wa mashtaka ulikuwa mzito na uliotosha kabisa kumtia hatiani mteja wake.



Alimshukuru Mungu kwa muujiza ule mkubwa.Alimshuk

uru vile vile jaji Elibariki kwa maamuzi yale ya haki.

“ Haki imetendeka.Jaji Elibariki ameweka historia kwa kutoa hukumu ambayo wengi hawakuitegemea” akawaza Jason na mara daktari akamfuata na kumwambia kwamba kuna kundi la waandishi wa habari nje wanaohitaji kuongea na Penny.Akatoka na kwenda kukutana nao na kuwataarifu kwamba Penny hakuwa tayari kuongea na waandishi wa habari kwa wakati huo.



**********



Jaji Elibariki alipomaliza kutoa hukumu yake akatoka ndani ya mahakama huku nyuma yake akiacha vilio na mshangao kwa wengi hasa wale wa upande wa Edson.Asilimia kubwa ya wale waliokuwa waki fuatilia kesi ile waliamini kwamba lazima mahakama ingemkuta na hatia Penny. Flaviana mke wa Jaji Elibariki alikuwa amesimama amejishika kiuno asiamini kile kilichokuwa kimetokea



“ How could you do this to us Eli…!! Akasema kwa sauti ndogo na kupandwa na hasira alipomtazama mdogo wake Anna ambaye alikuwa ameanguka chini ameishiwa nguvu .Familia ya Edson nao hawakuamini kilichokuwa kimetokea.Walik



umbatiana na kulia kwa pamoja .Hawakuamini kama ni kweli mtu anayesadikiwa kumuua mtoto wao ameachiwa huru.

Dr Flora Joakim mke wa rais akakumbatiana na mama wa Edson na kumfariji akimuhakikishia kwamba huo haukuwa mwisho.Watapambana hadi haki ipatikane.



**********



Kitambaa cha mkononi cha jaji Elibariki kilikuwa kimeloa jasho lililokuwa linamtiririka kwa wingi licha ya ofisi hiyo kuwa na kipoza hewa.

“ I did it !!..” akasema kwa sauti ndogo

“ Nashukuru nimemaliza kesi.Penny hakuwa na hatia.Hakumuua Edson.” Akawaza huku akiendelea kujifuta jasho

“ Nimetoa hukumu ambayo wengi hawakuitarajia.Wengi waliamini lazima Penny angekutwa na hatia na kupewa adhabu kali akiwemo rais na familia yake.



Hata mke wangu akiwa ni sehemu ya familia ya rais naye alitegemea nimpatie Penny adhabu kali sana.Nimekwenda kinyume na matakwa yao kwa hiyo toka sasa nitaonekana msaliti na inanibidi kujiandaa kwa matatizo yatakayonikuta lakini sintoogopa kitu chochote kile kitakachonitokea kwa kuitenda vyema kazi yangu na wala sintafanya kazi kwa shinikizo la mtu au kikundi cha watu.Si rais wala mtu mwingine yeyote atakayenishinikiza nifanye atakavyo yeye” akawaza Elibariki na kujifuta jasho ,akainuka na kwenda dirishani akachungulia nje.



“Niliziona sura za familia ya mke wangu namna zilivyobadilika baada ya kutangaza kwamba Penny yuko huru.After today we’ll never be the same again” akawaza na mara sura ya Penny ikamjia, akatabasamu

“ Moyo wangu una furaha kwa kumrejeshea tena uhuru wake Penny ambaye ameteseka mwaka mzima gerezani bila hatia.Nisingeitendea haki taaluma hii kama ningekubali shinikizo la kumfunga maisha gerezani.”



Akainuka na kuanza kuzunguka zunguka mle ofisini

“ Kuna kitu nimekuwa nikijiuliza kwa mida mrefu bila kupata majibu.Ni kwa nini kumekuwa na shinikizo kubwa la kutaka Penny afungwe au ahukumiwe kifo? Toka ndani ya moyo wangu ninaamini kabisa Penny si muuaji wa Edson .Swali linakuja kama si yeye nani alimuua Edson? Akajiuliza Jaji Elibariki na kuvuta pumzi ndefu.Lilikuwa ni swali gumu lisilo na jawabu

“ Maswali haya ni magumu lakini yanahitaji majawabu.



Kesi tayari imekwisha lakini kuna kila ulazima wa kwenda mbali zaidi na kutafuta majibu ya maswali haya.Ninaamini kuna jambo linajificha hapa na bila kupata majibu ya maswali haya basi maisha ya Penny hayatakuwa salama.Kumuachia huru pekee haitoshi inabidi kuhakikisha pia na usalama wake baada ya kuwa huru.Atakuwa huru tukimpata muuaji wa Edson bila hivyo Penny atauawa tu” Akainuka na kwenda tena dirishani akachungulia nje



“ Sielewi ni kwa nini ninataka kujiingiza katika jambo kama hili ambalo ninajua lazima litaniletea matatizo makubwa lakini nafsi inanituma lazima nifanye hivi kwa ajili ya usalama wa Penny.Sina taaluma ya kuchunguza na kumpata muuaji lakini nitatumia kila mbinu ili niweze kufanikisha suala hili.I must dig deeper” akawaza Elibariki.



************



Ni saa tatu za usiku ,chupa ya mvinyo iliendelea kushuka taratibu.Toka aliporudi nyumbani Jaji Elibariki alikuwa amejifungia chumbani kwake akiendelea kupata mvinyo huku akitazama mpira katika runinga kubwa iliyokuwamo humo chumbani.Kazi kubwa aliyokuwa nayo usiku huu ni kupokea simu toka kwa watu mbali mbali marafiki zake waliokuwa wakimpongeza kwa hukumu ile ya kihistoria.



Wakati akiongea na mmoja wa rafiki zake simu nyingine ikaita,akatazama mpigaji alikuwa ni baba mkwe wake,Profesa Joshua Joakim rasi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.



“ Kazi imeanza” akawaza na kumuomba samahani Yule rafiki yake aliyekuwa akiongea naye na kuichukua simu ile iliyokuwa ikiita akabonyeza kitufe cha kupokelea.



“ Hallo mzee” akasema Jaji Elibariki.Zikapita kama sekunde kadhaa akasikia sauti ya rais.Haikuwa ile sauti yake aliyoizoea kuisikia







“ Hallow mheshimiwa Jaji habari za jioni?

“ Habari nzuri mheshimiwa rais.Pole na majukumu”

“Ahsante sana kijana wangu nimekwisha poa” akasema mheshimiwa rais halafu kimya kifupi kikapita.Rais akauvunja ukimya

“ Elibariki nimekupigia simu kuna jambo nataka tuongee”

“ Ndiyo nakusikiliza mzee”

“ Naomba kwanza nikupongeze kwa kuimaliza kesi ngumu iliyovuta hisia za watu wengi.Pamoja na pongezi hizo, naomba niwe wazi kwako kwamba sijafurahishwa hata kidogo na maamuzi uliyoyafanya.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



To ka awali nilikuomba ufanye kila linalowezekana ili shemeji yako Anna aweze kupunguza machungu ya kifo cha mpenzi wake Edson.Alimpenda sana Edson na walikuwa na ndoto nyingi siku za usoni.Sina maana ya kudharau maamuzi yako kama jaji,lakini kitendo cha kumuacha huru muuaji wa mpenzi wa mwanangu kimenifadhaisha sana mimi na familia yangu kwa ujumla.Elibariki umemuoa mwanangu kwa hiyo nakuhesabu nawe ni sehemu ya familia yangu.Kama mwanangu ulitakiwa kusimama upande wa familia yako na kumuadhibu muuaji lakini pamoja na ushahidi wote uliowasilishwa mahakamani bado umeupuuza ukamuachia huru Yule msichana.



Naomba tu ufahamu kwamba maamuzi haya yamenifadhaisha sana mimi na familia yangu kwa ujumla.Ni hayo tu niliyotaka kukwambia usiku huu.Kwa heri Jaji” akasema mheshimiwa rais na kukata simu.Jaji Elibariki alihisi kijasho kikimchuruzika.Akainua glasi yake ya mvinyo na kunywa fundo kubwa.



“ Nilijua tu lazima mambo kama haya yangejitokeza kwani rais na familia yake walitegemea ningefanya kama walivyokuwa wakishinikiza wao kwamba nimpatie Penny adhabu kali.Kwa maamuzi ya kumuachia huru nimekwisha tangaza vita na familia hii na nina hakika maisha yangu yatakuwa magumu sana kuanzia sasa.Lakini vyovyote itakavyokuwa siyajutii maamuzi yangu.Nimetenda haki na siku zote nitasimama katika haki.Nitatenda haki bila kujali uwezo wa mtu na sintokubali kufanya kazi yangu kwa shinikizo toka kwa mtu yeyote .



Si rais wa nchi wala mtu yeyote atanishinikiza nifanye kazi kwa matakwa yake.Ninafanya kazi kwa mujibu wa sheria za nchi.” Akawaza Jaji Elibariki akiwa na hasira na kunywa tena fundo lingine

“ Ndiyo maana ninataka nifanye uchunguzi ili kumbaini muuaji wa Edson.Hapo ndipo nitakapowadhihirishia kwamba maamuzi yangu ya kumuachia Penny yalikuwa sahihi kabisa.Nisipofanya hivyo nitajiweka mahala pabaya na hata Penny maisha yake hayatakuwa na amani na salama.Lazima watamuandama tu.”



Akiwa bado katika mawazo mara mlango ukafunguliwa na akaingia mke wake Flaviana.Bila kumsalimu mumewe akajitupa kitandani .Alionekana mchovu sana na usoni alionekana ni mwenye hasira.Baada ya dakika kama tano hivi za ukimya mle chumbani kitu ambacho hakikuwa cha kawaida kwao Elibariki akaamua kuuvunja ukimya na kumuuliza mke wake

“ Umechelewa wapi?



“ Nilikuwa nyumbani kwa baba nikilia na familia yangu” akajibu Flaviana kwa sauti ya ukali

“ Kwa nini hukunitaarifu kama utachelewa ili nisiwe na wasi wasi kuhusu usalama wako?

Flaviana akacheka kidogo kicheko cha dharau na kusema

“ Sikuona umuhimu wa kukutaarifu.”

Jibu lile likamstua sana Jaji Elibariki.Hata siku moja mke wake hakuwahi kumjibu kijeuri namna ile

“ Hukuona umuhimu wa kunitaarifu mahala uliko? Tabia hii imeanza lini? Akauliza Elibariki

“ Ndiyo sikuona umuhimu huo”

“ Flaviana naomba uwe makini na kauli zako.Mimi ni mumeo na ni lazima nijue kila kitu unachokifanya.



Mimi nina maadui wengi nitajuaje kama umedhurika huko njiani? Nimekaa hapa mawazo tele nikiwazia usalama wako” akasema Jaji Eli

“ Kwa maana hiyo unataka kumaanisha kwamba mimi ni wa muhimu kwako? Akauliza Flaviana

“ Maswali gani hayo unayouliza Flaviana? You are my wife and you are important to me”

“ Save your breath Eli.I’m not important to you at all.I mean nothing to you”

“Una hakika na hayo unayoyasema ? akauliza Eli

“ Ningekuwa ni wa thamani kwako basi ungeithamini na familia yangu pia na usingefanya maamuzi kama uliyoyafanya.Sikutegema kama ungemuachia huru Yule kahaba.



How could you let her go? Kahaba Yule alimuua Edson na kuna kila ushahidi wa kutosha ulikuwepo kumtia hatiani lakini kwa makusudi kabisa umeamua kumuacha huru.You have broken my sister’s heart and mine as well.I’m disappointed,very disappointed” akasema Flaviana kwa hasira.Elibariki akanywa fundo kubwa la mvinyo halafu akazima runinga na kumgeukia mkewe

“ Flaviana naomba iwe ni mwanzo na mwisho wewe na familia yako kuingilia kazi yangu.Mimi ndiye ninayehukumu na si mtu mwingine kwa mantiki hiyo basi hakuna anayeweza kunishinikiza nifanye anavyotaka yeye.Si wewe wala baba yako wala mtu yeyote Yule anayeweza akanifundisha namna ya kuifanya kazi yangu.Halafu naomba iwe ni mara ya kwanza na ya mwisho kumuita Penny kahaba.She’s a respectable woman and you’ll have to respect her” akasema kwa ukali Jaji Elibariki.



“ Huwezi kunizuia kuongea Eli. Nitaongea chochote nikitakacho na hutanifanya kitu.That woman is just a prostitute .Nashangaa unavyosimama na kumtetea kwa nguvu.Who is she to you? Akafoka Flaviana

Maneno yale ya mke wake yakamuumiza sana Jaji Elibariki akamsogelea mkewe

“ Flaviana nakupa onyo la mwisho.Naomba tafadhali usithubutu kunijibu namna hiyo.”



“Usinitishe Elibariki.Huwezi kunifanya lolote” .Flaviana akongea kwa ukali na kwa kujiamini.Elibariki akamshika shingoni kwa hasira

“ I married you because I love you,and not because you’re a president’s daughter so don’t dare disrespect me again.If you do that again I’ll forget that your father is the president and I’ll break your neck.” Akasema Elibariki kwa hasira na kutoka mle chumbani. Pamoja na ujasiri wote aliokuwa Flaviana akajikuta akiogopa ghafla kwani hakuwahi kumuona muwe akiwa amekasirika namna ile .



“ What a stupid husband” akasema kwa sauti ndogo Flaviana baada ya Eli kutoka mle chumbani

“ Sijawahi kudharauliwa kama alivyonidharau Flaviana leo.Lakini nilijua tu mambo kama haya lazima yatakuja.Ninachopaswa kufanya ni kukabiliana nayo,.Huu ni mwanzo tu.Mengi yatakuja makubwa zaidi ya haya.” Akawaza Jaji Elibariki akiwa amekaa sebuleni amefura kwa hasira



***********



Ilipata saa nane na dakika kumi na tatu za usiku kwa mujibu wa saa kubwa ya ukutani,hali ya chumba ikiwa ni ya ubariki uliotokana na kipoza hewa huku kukiwa na mwanga hafifu na muziki laini kwa mbali,msichana mrembo Peniela alikuwa amejilaza kitandani.Baada ya kusota gerezani kwa takribani mwaka mzima hatimaye leo kama ndoto amerejea tena katika chumba chake

Kwa muda wa masaa mawili sasa amekuwa simuni akiongea na wakili wake Jason Patrick



“ Penny muda umekwenda sana nadhani ni wakati sasa wa kukuacha upumzike.Siku ya leo ilikuwa ndefu sana” akasema Jason

“ Ouh C’mon Jason,unadhani ninaweza kupata usingizi leo? Siwezi kabisa kupata usingizi kwa furaha niliyonayo na pili bado niko katika mstuko.Bado siamini kama ni kweli niko huru.Itanichukua siku kadhaa ili niamini kama ni kweli niko huru.” Akasema Penny.Jason akacheka kidogo na kusema

“Penny amini kwamba kesi imekwisha na uko huru.Mahakama imekukuta huna hatia na imekuachia huru”



“ Nakubaliana nawe Jason lakini kwa upande mwingine bado nina wasi wasi sana na maisha yangu.Sina hakika kama maisha yangu yatakuwa sawa tena.”

“ Kwa nini unasema hivyo Penny?

“ Nimewashinda watu wakubwa waliotaka kuniangamiza .Ninaamni jambo hili halitaishia hapa.Wataendele

a kuniandama usiku na mchana hadi wahakikishe kwamba wametimiza lengo lao.Anna mtoto wa rais aliapa kwamba ataniangamiza na ndiyo maana umeshuhudia nguvu kubwa ikitumika katika kuhakikisha ninafungwa gerezani.Uliona wewe mwenyewe ushahidi mzito uliotolewa mahakamani lakini pamoja na jitihada zao zote Mahakama imeniachia huru.Nina hakika mapambano yetu hayatishia hapo tu.



Nitaendelea kuandamwa kokote nitakakokuwa.My life will be a living hell”

“ Penny nashukuru kama umelifahamu hilo.Kitu cha msingi unachotakiwa kufanya ni kujiweka mbali kabisa na mambo yoyote yale yanayoweza kuwafanya wapate sababu ya kufanya lolote juu yako.Najua watatumia uwezo wao kuyafanya maisha yako yawe magumu lakini usihofu wala usiogope.Mimi nipo pamoja nawe siku zote.Vita hii ni yetu na tutashinda sote” akasema Jason



Sijui nikushukuruje Jason kwa msaada wako mkubwa.Hata nikikulipa mamilioni ya pesa ,hayataweza kufikia ukubwa wa msaada ulionisaidia.Dunia nzima ilinitenga baada ya kuaminishwa kwamba mimi ni muuaji lakini wewe pekee ndiye uliyeniamni kwamba sikutenda kosa lile na ukasimama pamoja nami.Ahsante sana Jason “ akasema Penny na kwa mbali machozi yakamlenga akikumbuka namna Jason alivyompigania hadi akawa huru



“Penny toka siku ya kwanza nilipokuona machoni niliamini hukutenda kiosa hilo na ndiyo maana nimepambana kufa na kupona kuhakikisha kwamba binti malaika asiye na hatia anaachiwa huru. Hata hivyo hayo yameshapita na ninachokuomba uyasahu yote na tuangalie mambo ya mbele.Tunatakiwa kuangalia nini kitafuata baada ya wewe kuwa huru.Tutakaa pamoja na kuangalia ni namna gani tutafanya ili uweze kujiweka vizuri kiuchumi..Mwaka mzima uliokaa gerezani najua mambo yako mengi yameyumba lakini usihofu niko pamoja nawe ,nitakusaidia hadi hapo utakapoweza kusimama tena”



“ Ouh Jason,you are so sweet.Ahsante sana kwa kujitolea kunisaidia lakini naomba kwa hili niseme hapana.Jason umenipigania mpaka nimekuwa huru.Sitaki niendelee kuwa mzigo kwako” akasema Penny

“ Penny tafadhali usirudie tena kutamka hilo neno eti wewe ni mzigo kwangu.Ninajiona ni mwenye bahati sana kuwa na rafiki kama wewe.Zaidi ya yote wewe bado ni jukumu langu.Kukusaidia kushinda kesi bado haitoshi lazima nihakikishe kwamba umeweza kujiimarisha kiuchumi .Pesa ni vitu vya kupita kwa hiyo naomba ukubali nikusaidie Penny” akasema Jason.Penny akacheka kidogo na kusema



“ Jason siku zote hutaki kushindwa.Ok tutakaa na kuliongelea suala hili”

“ Ahsante sana Penny.Pumzika sasa tutaonana kesho” akasema Jason wakaagana na kukata simu

“ Afadhali sasa nitaweza kulala usingizi.Kesi ya Penny iliyokuwa ikininyima usingizi imekwisha “ akawaza Jason

“ Nitamsaidia kwa kadiri niwezavyo hadi nihakikishe amerejea katika maisha yake ya awali.Uchumi wake umeyumba sana baada ya kukaa mwaka mzima gerezani.Bado Penny anahitaji sana msaada wangu” Akawaza halafu akastuka baada ya kukumbuka kitu

“ Kuna kitu nimekuwa najiuliza sana kuhusu Penny.Toka nimemfahamu sijawahi kuwaona ndugu zake,wala wazazi wake.Mwaka mzima nimehangaika naye katika kesi na sijawahi kumuona ndugu yake yeyote wala hajawahi kutamka lolote kuhusu ndugu zake.Jambo hili linanifanya nijiulize maswali mengi kuhusiana na maisha yake.Je hana ndugu? Kama anao wako wapi?



Kwa nini walimuacha wakati wa kipindi kigumu alichokuwa nacho?Nadhani ninahitaji kumfahamu Penny kwa undani zaidi.Kuna mambo mengi kumhusu yeye ambayo nahitaji kuyafahamu” akawaza Jason







Jaji Elibariki aliamka asubuhi na mapema na kufanya mazoezi ya viungo kama ilivyo kawaida yake halafu akajiandaa kwa ajili ya siku hiyo na kuondoka akimuacha mkewe Flaviana akiwa bado amelala.Hakuweza kupata usingizi usiku huo kutokana na kichwa chake kuwa na mawazo mengi sana.

“ Siamini kama mimi na Flaviana tumefikia hatua hii.Dharau zake zimezidi.Dharau alizonionyesha jana zimevuka mipaka. Nadhani kinachompa kiburi na kumfanya awe na dharau ni kuwa mtoto wa rais na baba yake ndiye aliyeniteua kuwa Jaji.



Kwa kigezo hicho walitegemea wanitumie watakavyo.Hapana.Siwezi kukubali kutumika.Nimekwisha vumilia mambo mengi sana toka kwa Flaviana na sasa nadhani imetosha.Nilijitahidi kuvumilia ili kuinusuru ndoa yetu lakini kwa sasa litakalotokea na litokee tu.Kuna mambo mawili ambayo natakiwa kuyafanya .Moja ni kutafuta nani muuaji wa Edson.Pili ni kuanza maandalizi ya maisha mapya kwani nina hakika muafaka kati yangu na Flaviana hautapatikana. Akawaza Jaji Elibariki wakati akikata kona kuingia Mandarini Hoteli kwa ajili ya kupata kifungua kinywa

Alihudumiwa haraka haraka na wakati akiendelea kupata kifungua kinywa akachukua simu yake na kumpigia rafiki yake Stanley

“ Halo Stanley.



Habari za asubuhi?



“ Habari za asubuhi nzuri Jaji.Nimestuka kidogo kwa simu ya asubuhi asubuhi namna hii” akasema Stanley

“ Stanley nimekupigia ninakuomba msaada wako.”

“ Nakusikiliza Jaji”

“ Kuna Yule wakili wa Yule msichana Peniela ambaye kesi yake imekwisha jana akachiwa huru, anaitwa Jason Patrick,unaweza ukanisaidia kupata mawasiliano yake?

“ Usihofu.



Nitakupatia mawasiliano yake ndani ya nusu saa” akajibu Stanley na kukata simu

Jaji Elibariki akavuta pumzi ndefu na kuwaza

“ Nadhani Jason ni sehemu nzuri ya kuanzia uchunguzi wangu.Yeye ni wakili wa Penny na nina hakika kuna mambo mengi anayoyafahamu kuhusiana na maisha ya Penny.Ninaweza kupata kitu toka kwake kitakachonisaidia katika uchunguzi wangu.Nitapenda vile vile nionane na Peniela ana kwa ana lakini makutano yetu yawe katika sehemu ya siri.



Sitaki nionekane nikiongea naye watu wanaweza wakahisi vibaya kwamba pengine nilifanya makusudi kumuachia kwa kuwa nina mahusiano naye Fulani” akawaza Jaji Elibariki na kutabasamu baada ya kumkumbuka Penny.

“ Penny ni msichana mrembo sana aliyebarikiwa uzuri wa aina yake.Ningefanya kosa kubwa sana kama ningemfunga gerezani msichana kama Yule” akawaza jaji Elibariki halafu akamaliza kupata kifungua kinywa na kuondoka kuelekea ofisini kwake.



“ Clara sihitaji kuonana na mtu yeyote siku ya leo.” Akampa maelekezo katibu muhtasi wake kisha akajifungia ofisini kwake.Hakutaka kufanya kazi yoyote siku ya leo,kichwa chake kilikuwa na wazo moja tu kumtafuta muuaji wa Edson.



“ Sina hakika kama nitampata muuaji wa Edson lakini nitajitahidi kwa kila linalowezekana hadi nimpate.Si kazi rahisi na ni ya hatari sana lakini sina namna nyingine lazima niifanye.” Akawaza jaji Elibariki na mara simu yake ikaita alikuwa ni rafiki yake Stanley

“ Hallo Stanley” akasema Jaji Elibariki

“ Jaji tayari nimekwisha pata mawasiliano ya Jason Patrick na nitakutumia sasa hivi katika ujumbe mfupi” akasema Stanley.Baada ya dakika moja ujumbe mfupi ukaingia katika simu ya Elibariki ukiwa na mawasilinao ya Jason,kuanzia namba za simu barua pepe,n.k.



Jaji Elibariki akashusha pumzi na kuziandika namba za simu za Jason akapiga

“ hallow” ikasema sauti ya upande wa pili baada ya kupokea simu

“ hallow.Naongea na wakili Jason Patrick?

“ Ndiye mimi.Nani mwenzangu?

“ Jaji Elibariki.”

“ jaji Elibariki?!...



Jason akashangaa hakuwa ametegema hata siku moja jaji Elibariki angempigia simu kwani hawakuwa na mahusiano yoyote zaidi ya kukutana mahakamani

“ Ndiyo Jason.Ni mimi Elibariki”

“ Nafurahi kupata simu yako Jaji Elibariki.Nikusaidie nini?

“ Jason nina shida nahitaji kukuona.”

“ Shida gani hiyo? Hatuwezi kuzungumza katika simu kwa sababu leo nina mizunguko mingi”

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“ Ni jambo ambalo hatuwezi kuliongea simuni Jason”akasema Elibariki

Jason akafikiri kidogo na kuuliza

“ What is that about?

“ Its about Penny “ akajibu Jaji Elibariki

Jason akafikiri kidogo na kusema

“ Ok mheshimiwa.Tuonane wapi?

“ Tukutane Mandarini hotel saa tano asubuhi hii.Nitakuwa juu ghorofani ” akasema Jaji



“ Ok jaji nitajitahidi kufika kwa wakati” akasema Jason na kukata simu

“ Hii ndiyo hatua ya kwanza.Baada ya kuonana na Jason nitajua nini cha kufanya” akawaza Jaji Elibariki



************



Saa tano na dakika saba ,Jason akawasili Mandarini hoteli,akaegesha gari na kushuka akapanda hadi sehemu ya juu alikoelekezwa na Jaji Elibariki ambaye tayari alikwisha wasili kitambo

“Hallo Jason.Karibu sana” akasema Jaji Elibariki akimkaribisha Jason

“ Ahsante sana mheshimiwa jaji.”



Akasema Jason na kuvuta kiti .Muhudumu hakuchelewa akafika na kumuhudumia kinywaji

“ Jason samahani sana kwa kukuharibia ratiba zako,najua wewe ni mtu mwenye shughuli nyingi” akaanzisha mzungumzo Jaji Elibariki

“ Usijali mheshimiwa.Najua usingefanya hivyo kama kusingekuwa na jambo la msingi.Hata hivyo ninashukuru kukutana nawe ana kwa ana.Tumekuwa tunakutana tu katika kesi mahakamani.” Akasema Jason

“ Ni kweli Jason ,kuna jambo la msingi lililonifanya nilazimike kukuita hapa.Hata mimi kwa upande wangu ninafurahi pia kukutana nawe.Ulinifurahisha sana namna ulivyoisimamia kesi ya Penny.Katika maisha yangu ndani ya sheria sijawahi kukutana na wakili mahri kama wewe.You are the best Jason.Hongera sana” akasema Jaji Elibariki na wote wakaangua kicheko.



“ Ahsante kwa pongezi mheshimiwa.Hata mimi vile vile napenda nikupongeze kwa namna ulivyoiendesha kesi ile na hukumu ya haki uliyoitoa.Hukumu ile imedhihirisha kwamba mahakama iko kwa ajili ya kutoa haki bila kujali cheo cha mtu,uwezo rangi au mahala atokako.Nakupongeza sana mheshimiwa” akasema Jason ,wakainuka na kushikana mikono.



“ Ahsante sana Jason.Nilitoa hukumu ile kutokana na namna ulivyoweza kuithibitishia mahakama kwamba Penny hakutenda lile kosa.Upande wa mashitaka uliwasilisha ushahidi mwingi ambao ungeweza kumtia hatiani Penny lakini kwa umahiri wako uliweza kuufanya ushahidi ule ukose nguvu na hivyo Penny akaachiwa huru”Akasema Jaji Elibariki halafu kikapita kimya kifupi kisha akasema



“ Jason kuna jambo ambalo nimekuitia hapa linalohusiana na Peniela.” Akasema Jaji na kukaa kimya kidogo halafu akaendelea

“ Katika kesi iliyomalizika kulikuwa na nguvu kubwa iliyotumika kuhakikisha kwamba Penny anakutwa na hatia ya mauaji,lakini toka ndani ya moyo wangu ninaamini Penny hakutenda kosa lile” akasema Jaji

“ Nashukuru Jaji kwa kulitambua hilo.Nadhani ni mimi na wewe pekee ambao tunaamini kwamba Penny hakuua.” Akasema Jason

“ Kweli kabisa Jason.



Wengi wanaamini kwamba Penny alimuua Edson kutokana na mazingira yenyewe ya tukio.Lakini mwisho wa yote ukweli utabaki pale pale kwamba Penny hakuua.Lakini kuna swali ambalo nimekuwa najiuliza bila majawabu na ambalo limenifanya nikuite hapa asubuhi hii,je kama Penny hakuua nani basi alimuua Edson??



Kimya cha dakika mbili kikapita kila mmoja akifikiria halafu Jason akasema

“ Jaji Elibariki,swali hilo ni gumu mno.Hata mimi nimekuwa nikijiuliza swali kama hilo je nani aliyemuua Edson na kesi akaangushiwa Penny lakini nimekosa majibu”

“ Jason ,ukweli ni kwamba Penny yuko huru lakini hayuko salama na hata sisi ambao tumefanikisha yeye kuwa huru bado hatuko salama pia.Kuna jambo nalihisi litakua nyuma ya mauaji yale na ndiyo maana nikakuita hapa ili tujadili na kwa pamoja tushirikiane tumpate muuaji wa edson.Ni hilo tu ndilo litamuhakikishia usalmaa Penny na sisi sote.Bila kumpata muuaji ,sikufichi maisha ya Penny yatakuwa hatarini.”



“ Nakubaliana nawe Jaji.Hata yeye mwenyewe amekwisha anza kuhisi kwamba ,maisha yake hayatakuwa na amani kwani aliahidiwa na mtoto wa rais kwamba lazima atayafanya maisha yake yawe magumu”

Jaji Elibariki akatabasamu kidogo na kusema

“ hayo ni mambo ya kawaida kwa wanawake kwani inasemakana Edson alikuwa katika mahusiano ya kimapenzi na Anna mtoto wa rais kabla ya kuanzisha mahusiano na Peniela kwa hiyo vitisho kama hivyo ni vya kawaida .Tunachohitaji sisi ni kumtafuta muuaji halisi wa Edson.



Jason wewe umekuwa wakili wa Penny na ninatumai kuna mambo mengi ambayo amekueleza .Je hajawahi kukueleza chochote kwamba anahisi nani anaweza kuwa muuaji wa Edson?



“ Hapana mheshimiwa jaji.Penny hajawahi kunieleza chochote kuhusiana na nani anahisi anaweza kuwa muuaji wa Edson.Maelezo aliyonipa mimi siku zote ndiyo yale aliyoyatoa mahakamani kwamba alimkuta Edson ameanguka ametapakaa damu kifuani pake kulikuwa na bastora na kwa taharuki aliyokuwa nayo alijikuta akiishika ile bastora bila ya kujua kwamba inaweza kumtia hatiani kwani alama zake za vidole zilibaki katika ile bastora na ikasadikika moja kwa moja kwamba yeye ndiye muuaji.Mpaka leo hafahamu nani aliyemuua Edson” akasema Jason



“ Jason ninamuamini Penny.Inawezekana ni kweli hafahamu ni nani muuaji wa Edson lakini naomba mimi na wewe tushirikiane tufanye uchunguzi wetu na tumpate muuaji.Hiyo ndiyo itakuwa salama ya Penny na sisi sote.Toka nimeingia katika sheria sijawahi kukutana na kesi ambayo nguvu kubwa imetumika ili kuhakikisha mshtakiwa anapatikana na hatia kama hii.Hii inanishawishi kuchimba kwa undani zaidi kuhusiana na kifo cha Edson.”

“ Nakubaliana nawe jaji.Niko tayari kuungana nawe ili kufanya uchunguzi na kumpata muuaji japokuwa si suala rahisi na ni la hatari kubwa.Je unashauri tufanye nini?



“ Ahsante sana Jason kwa kukubali.Kitu cha kwanza ambacho nataka unisaidie,nahitaji kuongea na Penniela ana kwa ana lakini katika sehemu yenye usiri .Sitaki kuonekana na watu niko naye kwani wataanza kuongea mambo mengine.”

“ Sawa Jaji nimekuelewa.Nitaongea na Penniela na kumuomba akutane nawe kisha nitapanga mahala ambako mtakutana na kuongea”



**********



Wakati akina Jason wakiwa katika mazungumzo hotelini juu ya kumpata muuaji wa Edson,Penny alikuwa amekaa sebuleni kwake akitazama runinga.Hakujisikia kutoka siku hii.Alitaka kubaki ndani akipumzika baada ya mwaka mzima kusota gerezani.Akiwa amejilaza sofani kengele ya mlangoni ikalia,akainuka akachungulia nje kupitia dirishani,na kukutana na sura ambayo ilimstua sana.



Alihisi mwili ukimtetemeka kwa uoga.





“ Ivan!!..akasema Penny kwa sauti ndogo .Bado mwili uliendelea kumtetemeka.Aliogopa sana.Kengele ya mlangoni iliendelea kulia,akavuta pumzi ndefu na kwenda kuufungua mlango .Mtu mmoja mwembamba mrefu ,aliyevaa suti nzuri nyeusi na miwani myeusi alikuwa amesimama mlangoni akiwa ndani ya tabasamu .Mkononi alikuwa ameshika lundo la maua mazuri.Wakatazamana kwa sekunde kadhaa



“ Welcome back Penny.I missed you so much.Even after a year in prison you are still as pretty as you used to be ” akasema Yule mtu.Penny hakuonekana kujali alichokiongea Ivan akamuuliza kwa ukali

“ What are you doing here Ivan?



“ Ouh Penny bado hujaacha machachari yako tu? Akasema Ivan huku akiendelea kutabasamu

“Ivan sema kilichokuleta tafadhali na uondoke mara moja.I don’t want to see you here” akasema Penny kwa sauti iliyoonyesha lwamba hakuwa na masihara

“ Hunikaribishi hata ndani Penny? Hatujaonana kwa muda mrefu “ akasema Ivan



“ Ivan tafadhali nakuomba sema kilichokuleta na uondoke.” Akasema Penny.Ivan akatabasamu na kusema

“ Ok Penny nimetumwa nikuletee mzigo huu”

“ Nani kakutuma?

“ Ivan hakujibu kitu akampa Penny ule mzigo wa maua.Penny akaupokea na kuuangalia kwa hasira

“ Kwa heri Penny.Nimefurahi kukuona tena” akasema Ivan na kuanza kupiga hatua kuondoka

“ Ivan please don’t come back here again” akasema Penny lakini Ivan hakugeuka akaingia katika gari lake na kuondoka,akimuacha Penny bado amesimama mlangoni

Baada ya Ivan kuondoka ,Penny akafunga mlango na kuyatupa yale maua mezani.Akayaangalia na kusema kwa sauti ndogo

“ After one year in prison,leo ndiyo ananikumbuka bazazi mkubwa Yule” Toka ndani ya maua yale kikaanguka kikadi kidogo chenye maandishi” welcome back”.Akiwa bado amesimama akitafakari mara simu ya mezani ikaita akaenda kuipokea

“ Hallow” akasema penny

“ Hallow Penny” ikasema sauti ya upande wa pili ambayo Penny aliitambua.



Kikapita kimya kifupi

“ What do you want from me? Akauliza Penny

“ Is that how you say hello to the love of your life? Akauliza mtu Yule.

“ Niambie tafadhali ni kitu gani unakitaka toka kwangu? Akauliza Penny

“ Penny naomba kwanza nikupe pole nyingi kwa masahibu makubwa yaliyokupata lakini vile vile napenda kukukaribisha tena uraiani.Tatu, leo jioni nataka kukutana nawe kwa chakula.Nitamtuma dereva aje akuchukue saa moja na nusu za jioni” akasema Yule mtu na kukata simu.Penny akabaki amesimama ameushikilia mkono wa simu.



Alizama katika mawazo.Akiwa bado amesimama akiwaza mara kengele ya mlangoni ikalia na kumstua.Haraka haraka akayakusanya yale maua na kuyafungia kabatini halafu akaenda kufungua mlango akakutana na wakili Jason

“ Jason” akasema Penny kwa mshangao kidogo kwani hakuwa ametegemea kama Jason angefika kwake mida ile

“ Hi Penny”

“ Hi Jason” akasema Penny na kumkaribisha Jason ndani.

“ Utanisamehe Penny nimekuja bila taarifa”

“ Bila samahani Jason.Hapa ni nyumbani kwako na una ruhusa ya kuja muda wowote na unakaribishwa bila hata kubisha hodi” akasema penny na kumfanya Jason atabasamu

“ Ahsante sana penny”

“ Jason unatumia kinywaji gani?

“ Ahsante Penny lakini kwa sasa sihitaji kinywaji chochote ila nimepita tu kutokana na suala la dharura lililojitokeza asubuhi ya leo”

“ Dharura gani hiyo?



Kuna tatizo? Akauliza Penny kwa wasi wasi

“ Jaji Elibariki alinipigia simu asubuhi akataka nionane naye”

“ Jaji Elibariki?!!..Penny akashangaa

“ Ndiyo “

“ Kuna tatizo gani tena? Akauliza Penny

“ Kuna suala nyeti ambalo aliniitia”

“ Suala gani hilo?

“ Anataka tumtafute muuaji wa Edson”

“ Muuaji wa edson? Penny akazidi kushangaa

“ Ndiyo Penny.Jaji Elibariki amekuwa akijiuliza swali ambalo hata mimi nimekuwa nikijiuliza bila kupata majbu,kwamba nani alimuua Edson ? Wote tuna hakika kabisa kwamba hukumuua lakini sasa nani alimuua? Tunahitaji kufanya uchunguzi na kulibaini hilo.Penny akamtazama Jason kwa sekunde kadhaa na kusema



“ Jason,siwezi kupingana na mawazo yako wala ya jaji Elibariki kwani hata mimi nimekuwa nikijiuliza swali kama hilo bila kupata jibu lakini kesi imekwisha na mahakama haijanikuta na hatia,ni kazi ya vyombo vya dola sasa kufanya uchunguzi na kubaini ni nani muuaji wa Edson?.Nadhani katika suala hili tuviachie vyombo vya uchunguzi vifanye kazi yake” akasema Penny



“ Nakubaliana nawe Penny kwamba mahakama haijakukuta na hatia na ndiyo maana ikakuachia huru lakini naomba nikuweke wazi kwamba hauko salama.Kulikuwa na nguvu kubwa iliyotaka kuhakikisha kwamba unakutwa na hatia lakini hilo likashindikana.Ni hilo ndilo lililomshangaza jaji Elibariki na kumfanya atake kufanya uchunguzi kuhusiana na tukio lile na kumbaini muuaji halisi wa Edson.Watu waliofanya kila jitihada kuhakikisha kwamba unakutwa na hatia ya mauaji watakuandama usiku na mchana hadi wahakikishe wamekuangusha baada ya kushindwa mahakamani.Kwa upande wangu nimekubaliana kabisa na jaji Elibariki kwamba kuna ulazima wa kufanya uchunguzi wa siri na kumpata muuaji.



Hiyo ndiyo itakuwa salama kwako na kwetu pia” akasema Jason.Penny akasema

“ Jason nakubaliana nawe kwa kila kitu na ninakushukuru lakini kuhusu hili sina hakika kama lina umuhimu mkubwa kwa sasa.Kuhusiana na maisha yangu usihofu kabisa.I’ll be fine.”

“ No Penny you are not fine and you’ll never be fine hadi hapo tutakapomjua muuaji wa Edson.Please Penny let us do this for you.This is for your own safety “ akasema Jason

Penny akainama akafikiri kwa muda na kusema

“Jason ninaogopa kwa sababu ninajitahidi kwa kila niwezavyo kuifuta kumbu kumbu ya Edson kichwani mwangu .Sitaki tena kujihusisha na mambo yoyote yanayohusiana na Edson.He’s gone for good and I have to forget him”

“ Penny nalielewa hilo lakini hautaweza kuifuta kumbu kumbu hiyo kichwani mwako bila ya kumpata muuaji wa Edson.Utakuwa unajiuliza swali hili mara kwa mara na hautakuwa na amani”

“ Jason this isn’t an easy thing.Ni jambo zito na la hatari kubwa.



How are you going to do it?

“ Ni kweli si jambo jepesi hata kidogo na sisi ni wanasheria na hatuna utaalamu wa kufanya uchunguzi wa jambo kubwa kama hii lakini tukiunganisha nguvu zetu sote watatu tunaweza tukafanikiwa”

Penny akanyamaza akafikiri na kusema

“ Sina kipingamizi hata kidogo kuhusiana na suala hili japokuwa sikuwa nataka kujihusisha katika kitu chochote kinachohusiana na Edson lakini wewe ndiye mwanasheria wangu naamini umeona umuhimu wa jambo hili kwa hiyo naahidi kutoa ushirikiano wangu”

“ Ahsante sana kwa kukubali penny.



Kwa kuanzia,Jaji Elibariki anahitaji kukuona ana kwa ana kwa maongezi ”

“ Kuhusu nini?

“ Ni kuhusiana na suala hili .Kuna mambo ambayo anahitaji kuyafahamu kutoka kwako kabla ya kuangalia tufanye nini tena.”

“ Lini anahitaji kuonana nami?

“ Ni jioni ya leo.Tayari nimekwisha andaa chumba ,Moniz 5 star hotel ambako ndiko mtakakokutania.Jaji Elibarii alitaka makutano yenu yawe ya siri kubwa bila ya mtu yeyote kufahamu”

Penny akainama akazama katika mawazo.



Alikumbuka jioni ya ana ahadi ya kuonana na mtu kwa chakula cha jioni

“ Mambo yanaingiliana.Watu wawili wote wanataka kuonana nami usiku wa leo.Nionane na nani? Akajiuliza Penny

“ Lakini ngoja nikaonane na Jaji Elibariki.Bila yeye hivi sasa ningekuwa kifungoni.” Akawaza Penny halafu akamgeukia Jason

“ Ok Jason.Nitakwenda kuonana na Elibariki jioni ya leo”

“ Ahsante kwa kukubali Penny.Nitakupitia saa moja za jioni nikupeleke mkaonane na Jaji Elibariki halafu nitakurejesha nyumbani”

“ Sawa Jason” akajibu Penny halafu wakaagana na Jason akaondoka



*********



Katika moja ya jengo refu kabisa jijini Dar ,watu saba wameizunguka meza ya duara ndani ya ofisi nzuri iliyo katika ghorofa ya kumi na mbili.Mtu mmoja mrefu na mwenye umbo la wastani alikuwa akiongea na wengine wakimsikiliza kwa makini

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“ Nimepigiwa simu na ofisi kuu asubuhi ya leo wakinionya kuhusiana na kutorudiwa tena kwa uzembe mkubwa uliopita kiasi cha kumuacha Penny akaingia katika matatizo makubwa na kuhatarisha mpango wetu wa miaka mingi.Endapo Penny angekutwa na hatia mahakamani na kufungwa ,kila kitu kingefikia mwisho.Juhudi zote za miaka zaidi ya ishirini zingekuwa ni kazi bure. Bila Penny kila kitu kitakwama .



Kwa hiyo basi maagizo niliyoyapata toka ofisi kuu ni kwamba tuhakikishe uzembe kama ule haujirudii tena na Penny apewe ulinzi wa kutosha na kumuepusha na mambo yote yanayoweza kumsababishia matatizo na kuhatarisha mpango mzima.Kazi kubwa imekwisha fanyika na tuko katika hatua za mwishoni.



Tunatakiwa kuongeza umakini maradufu.Tunatakiwa tufahamu na tuwepo kila mahala alipo Penny,tufahamu watu anaokutana nao na kwa kuanzia tunatakiwa kumfahamu Jaji Elibariki Chukuswa ambaye anakwenda kuonana na Penny jioni ya leo.”



Akasema Yule jamaa





Kwa mara ya kwanza baada ya kukaa gerezani kwa mwaka mzima,Penny alisimama mbele ya kioo kikubwa cha kujitazamia kilichopo chumbani kwake akijitazama namna alivyokuwa amependeza.Alikuwa amevaa gauni refu jekundu maalum kwa kutokea usiku.Alijiangalia na kutabasamu halafu akageuka na nyuma akajiangalia

“ Nothing have changed.I’m still the hot Peniela” akawaza Penny huku akiikoleza rangi ya mdomo.

“ sasa niko tayari kwenda kuonana na Jaji Elibariki” akawaza

Akiwa bado anamalizia kujiremba,kengele ya mlangoni ikalia,akatoka na kwenda kufungua mlango .



Kwa sekunde kadhaa akabaki akitazamana na Jason ambaye hakuamini macho yake

“ Wow ! “ akasema Jason

“ Umependeza mno Penny.Sikuwahi kukuona ukiwa umependeza kama ulivyopendeza leo.Kumbuka Jaji Elibariki ni mtu mwenye ndoa yake kwa hiyo chunga asije akachanganyikiwa na uzuri wako na kubadili mawazo” akasema Jason na wote wakaangua kicheko.



“ Ni muda mrefu sijapendeza Jason ndiyo maana kwa usiku wa leo nimeona nirudie enzi zangu”

Akasema Penny

“ Uko tayari? Akauliza Jason

“ Ndiyo Jason,niko tayari lakini naomba unisubiri dakika mbili kuna kitu nimesahau chumbani.” Akasema Penny na kuelekea chumbani kwake.Wakati akiwa bado chumbani kengele ya mlangoni ikalia .Jason aliyekuwa sebuleni akaenda kuufungua mlango na kukutana na kijana mmoja mrefu mwembaba,aliyevaa suti nzuri nyeusi iliyomkaa vyema.

“ Hallo” akasema Jason

“ Hallo” akajibu Yule jamaa ambaye sura yake ilionyesha mshangao kidogo kwa kumkuta Jason pale ndani

“Karibu ndani” akasema Jason na Yule jamaa akaingia ndani

“ Nimemkuta Penny? Akauliza

“ Ndiyo.



Penny yupo ,anakuja sasa hivi” akasema Jason halafu kikapita kimya kifupi

“ I’m Jason” akasema Jason

“ I’m Kareem” akasema Yule jamaa na kabla maongezi hayajaendelea zaidi Penny akatokea.

“ Kareem!!..akasema Penny kwa furaha

“ Penny..!!” akasema Kareem na kumfuata Penny wakakumbatiana.

“ Welcome back Penny”

“ Ahsante sana Kareem” akajibu Penny

“ Pole sana kwa matatizo.Nilikosa kabisa hata muda wa kuja kukuona.”

“ Usijali Kareem.Ninaelewa ugumu wa kazi zenu.Nashukuru Mungu matatizo yamekwisha”

“ Nashukuru kwa kulitambua hilo.




ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog