Search This Blog

Saturday 5 November 2022

SAUTI YAKE MASIKIONI MWANGU - 4

 








Simulizi : Sauti Yake Masikioni Mwangu

Sehemu Ya Nne (4)







afanya? Nauliza ni uchafu gani huu unafanya ndani ya nyumba yangu? Hapana haiwezekani.” Akawaka. Akatoa simu yake, akabofyabofya kumpigia mume wake.



“Shemeji naomba nikueleweshe....” akataka kujitetea Mkuki lakini wapi,

“Sitaki kusikia chochote kutokwa kwako. Sitaki kuongea na wewe. Hunijui sikujui.” Akasema Onyuletwa, alikuwa ameshikwa na jazba kweli kweli.

Simu ikapokelewa.

“Meja naomba njoo nyumbani sasa hivi.” Akasema kisha akaa kimya kusikiliza upande wa pili.

Akaendelea.

“Nimekwambia njoo nyumbani sasa hivi, kama huwezi hutonikuta. Nafunga mizigo yangu naondoka na mwanangu nakuachia nyumba.”

Akasikiliza upande wa pili.

“Nimekwambia njoo. Siwezi kuvumilia huu uchafu siwezi. Kumbe nyinyi Watanzania ni wafuska namna hii, hapana. Najuta kukujua, najuta kuishi na wewe. Naondoka Meja.” Akabatwa Onyuletwa kisha akata simu.

Hakutaka kuzungunza na Mkuki hata kidogo, akaenda chumbani kwake akimuacha Mkuki na Mei Lee pale sebuleni wamepigwa bumbuwazi kama wachawi waliokutwa wakicheza cheketucheketu.

Punde Onyuletwa akatoka na begi moja la nguo akaliweka sebuleni, akarudi chumbani tena na dakika tano baadae akatoka na begi lingine, hakumsemesha mtu, alikuwa amenuna na kukunja sura kweli kweli.

Mara ya tatu akatoka na begi lingine na akarudi tena ndani na papo hapo mlango ukafunguliwa, Meja akaingia, alipomuona Mkuki na Mei Lee tu akagundua kwamba mke wake aliwakuta na akahisi kwamba huenda Mkuki aliingiza mwanamke huyo baada ya wao kutoka.

Akanyamaza Meja, akasimama palepale mlangoni akimtazama Mkuki na Mei Lee kana kwamba hata yeye ilikuwa ni mara ya kwanza kuwatia machoni. Hakutaka mke wake afahamu kwamba anayo taarifa kuhusu huyo mgeni wa Mkuki, alielewa kwamba hilo lingefanya mke wake amuone 'kilaza' wa mbingu ya saba.

Punde mke wake akaja sebuleni akiwa begi dogo. Akamuona mume wake.

“Meja? Umemleta huyu ili afanye huu ufuska kwenye nyumba yangu? Sasa mimi naondoka, nawaachia nyumba, siwezi kukaa na mshenzi wa hivi. Hebu mtazame mwanamke mwenyewe kwanza, sura ya ajabu kama....” hakumalizia, Meja akamkatishaa.

“Basi mke wangu.” Alisema Meja kisha akamgeukia Mkuki. “Kaka ndo nini hiki unafanya? Unaingizaje mwanamke ndani ya nyumba yangu bila kunitaarifu?” Akauliza Meja. Mkuki akamuelewa kwamba alikuwa anajitoa kwenye ‘msala’.

“Meja naomba watoe watu wako sasa hivi. Sitaki kuwaona na kama itakuwa haiwezekani mimi nionodoke na mwanangu.” Akasema.

Sasa agizo hilo ndilo lilimtoa kijasho chembachemba Meja; mtihani aliopewa na mke wake ulikuwa ni mzito zaidi ya ule wa utaamua yupi kati ya simba na chui ukiwa na bastola yenye risasi moja tu.

Shida ilikuwa ni kwamba Mkuki alikuwa ni rafiki yake tena kipenzi wakati mke wake pia alikuwa ni muhimu kwake kama ambavyo Mei Lee alikuwa muhimu kwa Mkuki. Onyuletwa ndiye aliyemasaidia Meja kupata kazi pale anapofanya, kabla ya kuwa na uhusiano naye Meja alikuwa si lolote si chochote, hana kazi, ni kama goigoi anyetangatanga mtaani tu.

“Mke wangu, naomba tulizungumze hili.”

“Sitaki kuongea chochote Meja. SITAKI. SITAKI. Unawondoa ama niondoke?”

Meja akatulia kidogo, hapa akiupa nafasi ubungo wake uchakate jibu la kutoa juu ya lile swali aliloulizwa, bila shaka alihitaji ujasiri katika kutoa jibu hilo.

“Mkuki.” Akaita Meja. Mkuki akamtazama usoni kama ishara ya kwamba anamsikiliza. “Nenda kaka.” Akazungumza kwa kiswahili Meja. Aliumia sana moyoni, hakutaka kuzungumza vile, yale hayakuwa maamuzi yake, bali alisukumwa na matakwa ya mke wake. Ilikuwa ni lazima amsikilize ili kuiokoa ndoa yake, kuokoa familia yake na kumnusuru mtoto wake na madhara ya kulelewa na mzazi mmoja.

Basi Mkuki akasimama bila kusema neno

Akaenda moja kwa moja hadi chumbani na punde akatoka akiwa na begi dogo lenye nguo, ni nguo zake alizonunuliwa akiwa pale kwa Meja.

“Twende.” Akamwambia Mei Lee. Binti akasimama na kumfuata.

Mkuki akafungua mlango walipoufikia, akampisha Mei Lee atangulie kutoka kisha naye akafuata, lakini kabla hajarudisha, akamgeukia Meja na kumtazama kwa jicho ambalo ni kama alikuwa akimlaani kwa kile alichomfanyia, alimtazma hivyo kwa sekunde kumi kisha akafunga mlango, akaondoka.





********************************

Walifika nje, kwa pamoja, Mkuki na Mei Lee walitembea bila kusemeshana. Kila mmoja aliogopa kwa sababu wote wawili walikuwa wanajiona wakosefu na kwamba ndio chanzo cha yale yanayoendelea.

Mkuki alihisi bila yeye Mei Lee asingukuwa pale China akidhalilika kiasi kile wakati Mei Lee naye alijiona ndiyo sababu ya Mkuki kutimuliwa kama mbwa pale alipokuwa akiishi kwa kufadhiliwa.

Lakini Mei Lee alifurukutwa mno moyoni, alihisi kuna ulazima wa kuzungumza chochote juu ya kile kilichotokea, hata kuomba msamaha ikibidi.

“Mkuki?” Aliita Mei Lee katikati ya safari, Mkuki akamtazama kuashiria kwamba anamsikiliza.

“Samahani...” akasema.

“Usiseme. Hakuna ukichokosea. Mimi ndiye nastahili kukuomba msamaha.”

“Hakuna ulichokosea, ni mimi.”

Mkuki akajitabasamisha kidogo. “Basi si wewe si mimi, sote hatuna kosa, hatustahili kuombana msamaha,” akasema Mkuki kisha akapiga kimya kidogo akimtamza Mei Lee usoni huku wakiendelea kitembea.

Akaendelea kuzungunza Mkuki.

“Nadhani kilichotokea ni kama kukohoa. Kinaonekana si kitendo kizuri machoni mwa watu lakini huwezi kikuzia. Mimi na wewe hatuwezi kukizuia, ilikuwa ni lazima kitokee.”

Mei Lee akatabasamu, alifurahishwa na kauli za Mkuki, zilimfanya ajihisi mwepesi, asiye na mzigo wowote moyoni.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“Tunakwenda wapi?” Akauliza.

Mkuki akatabasamu kidogo kabla ya kumjibu. “Popote Mungu atakapotupeleka.”

Mei Lee akacheka.

“Lakini natakiwa niende kazini. Ninakwenda kukuacha sehemu kisha tutaonana jioni nikitoka.” akasema Mkuki.

Safari iliendelea huku sasa hali ya hewa ikionekana si rafiki kwa matembezi ya kawaida—yaani kulikuwa na dalili zote za kunyesha mvua kubwa. Wakapita mitaa miwili, wakatokea kwenye mtaa mwingine uitwao Cheynun Temple. Mtaa huu ulikuwa na barabara ndogo yenye kupita magari machache.

Basi wakiwa pembezoni mwa barabara walimuona bibi mmoja akivuka barabara mbele yao, alikuwa ni mzee kweli kweli na hata mwendo wake ulithibitisha hilo. Lakini mbele ya bibi huyo waliona gari ndogo ikija kwa kasi kana kwamba ilikuwa ikiendeshwa na mwendawazimu.

Mkuki alihisi jambo, alifikiria kwamba huenda gari lile litafika alipo bibi kabla ya kuvuka na kama ni hivyo basi ni wazi kwamba litamgonga.

Basi ghafla Mkuki akatimua mbio kuelekea alipo bibi hata alimshitua Mei Lee naye akataka kukimbia bila kujua kwanini mwenzake alifanya hivyo. Lengo la Mkuki ilikuwa ni kumfikia yule bibi na kumuoka na ajali iliyokuwa karibu kumkumba.

Kabla Mkuki hajamfikia bibi gari lilikuwa limeshamkaribia bibi na hapo Mkuki akagundua kuwa njia pekee iliyobaki ya kumnusuru kikongwe yule na umauti ni kujirusha na kumsukumia pembeni.

Hata bibi mwenyewe aliliona gari, lakini hakuwa na cha kufanya zaidi ya kufumba mambo asishuhudie jinsi atakavyozolewa juu juu na gari lile liendelo kasi sana.

Basi kabla gari halijamkumba bibi, Mkuki alijirusha, akamsukuma bibi na wote wawili wakaangukia pembeni mwa barabara, gari ikapita kwa kasi na ikawa imewakosa.

Bibi alichunika kidogo, lakini ni heri majeraha kuliko umauti.

Mkuki akasimama, akamuinua na bibi na wakati huo Mei Lee naye ndiyo alikuwa anafika pale.

“Mmeumia? Bibi umeumia?”

“Hapa tu.” Akajibu bibi huku akionesha kiwiko cha mkono wake wa kulia ambacho kilikuwa na mchubuko. Kisha akamgeukia Mkuki ambaye alikuwa karibu yake, akamtazama kana kwamba ni bubu asiye na maneno yoyote ya kumwambia, kisha ghafla bibi akajichoropoa, akamkumbatia Mkuki huku akilia kwa furaha.

“Asante mjukuu wangu. Asante sana.” Akasema.

Kabla hata Mkuki hajajibu radi likarindima, na mvua ya rasharasha ikaanza kunyesha; iliwanyeshea.

Mkuki akajitoa kwenye kumbato la bibi. “Unaenda wapi bibi?” Akamuuliza.

“Nyumbani.”

“Ni wapi?”

“Hapo mtaa wa nyuma.”

“Basi twende tukupeleke haraka kabla mvua haijawa kubwa.” Akasema Mkuki na hicho ndicho kilichoafanyika. Walimchukua bibi wakampeleka hadi kwake. Hapakuwa mbali na pale, ilikuwa ni mtaa wa nyuma tu.

Bibi huyu alikuwa akiishi kwenye jengo nambari 11 la mtaa huo. Jengo la ghorofa nane, wakati yeye alikuwa akiishi ghorofa ya sita. Walipanda lifti, bibi akatangulia kwa msaada wa kushikwa mkono na Mei Lee hadi mbele ya mlango wa chumba anachoishi bibi huyo.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Bibi akachukua funguo kutoka katika pochi yake ndogo, akampa Mkuki amsaidie kufungua, Mkuki akafanya hivyo kisha bibi akatangulia kuingia ndani, Mei Lee akafuata na Mkuki akawa wa mwisho.

Bibi alikuwa akiishi kwenye nyumba ya hadhi kubwa kweli kweli, sebule yake ilikuwa na fanicha tena za kisasa na ilipendeza mno.

“Karibuni.” Yakamtoka.

“Asante bibi. Tunaomba twende.” Akasema Mkuki.

“Haraka kiasi hicho? Kaeni niwapatie kahawa wanangu.”

“Hapana bibi. Siku nyingine tutakauja, tunawahi kazini.”

“Hata kama. Kazi ni bora lakini si bora zaidi ya kupokea shukurani.” Akasema bibi.

“Siku nyingine bibi.”

“Kweli!? Mnafanya wapi kazi?”

“Kwenye mgahawa wa Huan.”

“Nyote  wawili?”

“Ndiyo.” Akaongopa Mkuki.

“Kweli?” akahoji bibi kana kwamba kuna kitu alikuwa akifahamu.

“Ndiyo, lakini leo mwenzangu anapumzika. Naenda mimi peke yangu.” Akasema Mkuki, aligundua ile hali ya utambuzi aliyokuwa nayo bibi, kwahiyo alijitahidi kuendana na kasi yake.

“Anhaa!  Basi naona itakuwa vyema kama huyu binti atabaki hapa  na mimi hadi utakaporudi kazini…..” akasema  bibi lakini Mkuki alimkatisha.

“Hapana bibi…..” Bibi akamkatisha pia.

“Mjukuu wangu? Mwanangu? Niko mwenyewe hapa nyumbani, sina mtu wa kuzungumza naye. Naomba mnisaidie katika hili pia kama ambavyo mlinisaidia kule barabarani.” Akasema bibi.







Ni kama kile alichokizungumza kilikuwa na barafu kali, kilimgandisha Mkuki na kumfanya sasa afikirie kwamba inawezekana hiyo ikawa ni fursa pekee ya kumuacha Mei Lee pale na kumfuata jioni akiwa ameshafikiria ni wapi watakwenda. Lakini nafsi yake ilikinzana yenyewe ndani kwa ndani, alifikiria kumuacha Mei Lee pale, tena bila ya kukubaliana ama kumuuliza kwamba hilo litampendeza ilikuwa ni sawa na nusu ya kumtelekeza.







“Usijali bibi, tutakuja siku nyingine.” Akaamua Mkuki.

“Sawa. Nawashakuru sana kwa kunisaidia. Kwa sasa sina cha kuwapa lakini nawaahidi nitawaandalia kitu kizuri mtakapokuja hiyo siku nyingine.” Akasema Bibi, na baada ya hapo Mkuki na Mei Lee wakatoka wakimuacha bibi akifunga mlango na kurudi kuketi kwenye kiti chake akipendacho zaidi mle ndani.

Punde mlango ulibishwa hodi, bibi aliinuka kwenda kufungua na hapo akakutana na Mkuki na Mei Lee—waliamua kurudi baada ya kukubaliana kwamba ni vyema Mei Lee akabaki pale hadi jioni.

“Bibi, naomba mwenzangu abaki hapa. Nitamfuata jioni.” Akasema Mkuki na hilo halikuwa ombi kwa bibi, bali ni zawadi kubwa na ya muhimu sana ya kumuondolea ile hali ya upweke, hali ya kuwa mwenyewe kwa siku nzima.

Yeye alikuwa akiitwa Pin Ping, bibi kikongwe wa miaka takriban 80. Alikuwa akiishi peke yake kwa sababu kuu moja ambayo mwenyewe aliifanya kama siri.

Awali alikuwa akiishi Guanzouh na si hapa Hong Kong alipo leo, bali alikimbilia huko baada ya mwanae kumpelekea akaishi katika nyumba ya kulelea wazee. Hakuwa akiyataka maisha ya huko lakini hakutaka kuwakwaza wanawe na maamuzi yao. Alichoamua ni kutoroka akiwa huko kituoni, na akatumia pesa zake alizozihifadhi kwa siri kuhama Hong Kong, kupanga nyumba na kuanzisha maisha kwa kujificha ingawa alifahamu fika kwamba maisha ya aina hiyo yana ukingo wake.

“Sawa. Anaweza kubaki hapa.” Akasema bibi Pin Ping, hapo Mei Lee akamuaga Mkuki na kuingia ndani, kisha mwanaume akaondoka mbio mbio hadi mgahawani.

Alichelewa mno, na siku hiyo ilikuwa ni manusura afukuzwe kazi isipokuwa Meja alimtetea kwamba alikuwa na matatizo ya kiafya na ilibidi apite hospitali kwanza.

Kisha baada ya hapo Meja akamuita pembeni Mkuki na kumuomba msamaha zaidi wa kile kilichotokea. Hakika kilimuumiza lakini hakuwa na jinsi, ilikuwa ni lazima aegemee upande wa familia yake, upande wa mke wake.

Hata hivyo Mkuki sasa alimuelewa, hakuwa na kinyongo naye wala chuki dhidi yake, alijtahidi kusahau kila kilichotokea, na kuamua kuangalia mbele tu.

******************************

Jioni Mkuki alirudi kwa bibi Pin Pong, alibisha hodi na mlango ulifunguliwa na Mei Lee.

“Karibu.” Akasema Mei Lee. Mkuki akapita ndani, akaketi kwenye kiti.

“Bibi yuko wapi?” Mkuki akauliza.

“Kalala.” Akajibu Mei Lee.

“Muamushe umuage tuondoke.” Akasema Mkuki, alikuwa amepanga kwenda kulala na Mei Lee kwenye hoteli ndogo, alikuwa amepata vipesa kidogo siku hiyo.

“Mkuki, nimezungumza vitu vingi sana na bibi, nimemueleza kila kitu kuhusu maisha yetu, kasema tunaweza kuishi naye hapa.” Akaeleza Mei Lee huku akimtazama Mkuki machoni.

Mkuki alimtazama kana kwamba hakuelewa kile kilichosemwa; lakini ukweli ni kwamba alikipenda ingawa aliogopa kwa kiasi fulani kutokana na kwamba hawakuwa wakimfahamu uzuri yule bibi.

Lakini Mkuki hakuona sababu ya kupinga ofa ile hasa ukizingatia kwamba ilionekana hata bibi alikuwa anawahitaji, yaani kila mmoja alikuwa na umuhimu kwa mwenzake; bibi alichoka maisha ya upweke na Mkuki na Mei Lee hawakua na pahala pa kuishi.

********************************

Mkuki, Mei Lee na bibi Pin Ping walitengeneza familia bora sana yenye furaha hata kila mmoja akasahau mahangaiko aliyopitia. Na hivi ndivyo Mungu alivyo, mara zote hufanya njia pale pasipotarajiwa ili kuthibitisha uwepo na uwezo wake mkubwa wakufanya kile atakacho ndani ya nukta moja tu

Mkuki sasa akawa ndiye mleta huduma wa familia kama ambavyo alikuwa kwenye familia ya mzee Wong na hilo lilizidisha umuhimu wake katika familia hii.

Walikaa na bibi Pin Ping kwa miezi miwili; na kwa wiki ya kwanza ya kipindi chote hicho bibi Pin alipata kugundua kipaji kikubwa cha kuimba alichokuwa nacho Mei Lee. Mara kadhaa alimsifia na kuonesha hisia zake za wazi za jinsi ambavyo anafurahishwa na uimbaji wa msichana huyo, hata ukajengekea utamaduni wa kwamba kabla ya kulala ilibidi aimbiwe, aisikie sauti ya Mei Lee masikioni mwake ndipio usingizi uje.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Siku moja, baada ya miezi miwili ya kuishi kama familia , bibi Pin Ping alimuuliza Mei Lee  jambo kuhusiana na muziki wake.

“Unajua kupiga  chombo gani?” aliuliza bibi.

“Chombo cha muziki?”

“Ndiyo.”

“Hapana. Sijui kupiga chochote.”

“Mh! Kwanini?  Hupendi?”

“Hapana. Napenda. Sikupata nafasi ya kujifunza tu.”

“Basi ngoja.” Akasema bibi Pin Ping, kisha akainuka kuelekea chumbani kwake akimuacha Mei Lee pale sebuleni walipokuwa. Punde alirejea akiwa  na kitu fulani mkononi, ala  ya muziki ambayo ilikuwa ni miongoni mwa ndoto za Mei Lee kwamba siku moja aimiliki na ajue kuitumia.

Lilikuwa ni gitaa, ala maarufu yenye kutengeneza muziki kwa kuvutwa nyuzi zake. Hili alilokuja nalo bibi Pin Ping lilikuwa ni gitaa lisilotumia umeme, lenyewe lilikuwa limetengenezwa kwa mbao nyepesi na kunakishiwa kwa rangi nyeusi, huku likiwa na vumbi kiasi kana kwamba lilihifadhiwa  mahala kwa muda mrefu bila kutumika.

“Shika,” bibi akasema huku akimkabidhi Mei Lee lile gita. “Nenda kalisafishe, lifute vumbi kisha uje nalo.” Akamuelekeza.

Mei Lee akapokea, akainuka nalo na kwenda chumbani kwake akimucha bibi mwenyewe pale sebuleni. Alirudi sekunde chache baadae akiwa na gitaa lisilokuwa na vumbi sasa, alikwenda huko ndani kwa ajili ya kuchukua kitambaa kikubwa na kulisafisha.

“Tayari.” Akasema Mei Lee huku akimkabidhi bibi lile gitaa. Bibi akapoke taratibu, akalipaka kwenye mapaja yake akilitazama kwa makini kana kwamba lilimkumbusha jambo fulani murua lenye kusisimua lililopata kutokea katika maisha yake. Akafumba na macho kama mtu anayevuta  hisia tamu, na hapo kiganja chake cha mkono kilipapasa gitaa lile.

Sekunde chache baadae akashusha pumzi ndefu, akafumbua macho, akamtazama  Mei Lee.

“Hili gitaa linaitwa Caihong (Upinde wa Mvua),” akazungumza polepole na kwa hisia kali bibi Pin Ping na kuendelea. “kwangu ni kitu cha thamani zaidi kilichobaki kwenye uso wa dunia. Nilipewa kama zawadi na mume wangu, alinunua Uingereza alipokwenda kusoma. Sijui alifikiria nini hata akaamua kuniletea zawadi ya aina hii kwa sababu mimi na yeye, sote hatukuwahi kuwa wanamuziki; lakini niliipenda.

Basi nilitafuta mwalimu, akanifundisha jinsi ya kulitumia kwa usahihi na nilipohitimu tu nikawa nikitengeneza melodi nzuri kwa ajili ya kumliwaza mume wangu kila usiku.

Alifurahia sana, hata aliandika kwenye wosia wake kwamba akifa kabla yangu nimpigie melodi kadhaa kwenye mazishi yake.” alisimulia  bibi Pin Ping na hadi kufikia hapa hisia zilimzidi. Akashindwa kujizuia, akajikuta akitokwa machozi.

Kile alichokisimulia kilimkumbusha mbali sana, kilimpa kumbukumbu za kusisimua za  mapenzi. Alimkumbuka Lau, mwanaume aliyemuoa kwa ndao halali, ndoa iliyochochewa na upendo wa dhati wa kila mmoja kwa mwenzake. Alifariki kipindi ambacho bibi Pin Ping bado alikuwa ni mwanamke mwenye nguvu, hivyo baada ya pale alipata kuwa na wanamume wengine na hata kuolewa pia lakini bado nafasi ya Lau ilibaki kama ilivyo; hakuna shababi aliyefanikiwa kumfunika mwanaume huyo.

Bibi aliendelea kulia kwa machozi, Mei Lee alikuwa pale lakini hakuthubutu kusema neno, alielewa wakati mgumu namna ile aliokuwa akipitia bibi yake, hivyo aliamua kumpa uhuru wa kufanya vile alivyoamua, kutoa sumu za kumbukumbu zote za raha alizowahi kupewa na mumewe kipenzi Lau.

Baadae bibi alitulia mwenyewe, hapa sasa Mei Lee akapata nguvu ya kumsemesha na bibi akamuunga mkono kwa kumjibu na kisha mazungumzo mengine yakashika hatamu ambayo yalikuwa na sentensi mbili tu za kati kabla ya bibi kufikia kuelezea kwanini alikuja na lile gitaa.

“Ninataka nikufundishe kupigia gitaa.” Akasema bibi Pin Ping na hivyo ndivyo ilivyokuwa.

Bibi Pin Ping alimfunza barabara Mei Lee jinsi ya kutumia gitaa, na ndani ya wiki nne tu binti akawa tayari na uwezo wa kuchezesha vizuri vidole vyake na kutengeneza muziki mzuri. Alilielewa kwa muda mfupi sana hasa ukilinganisha na watu wengine jinsi ambavyo huchukua kipindi kirefu cha kujifunza matumizi ya dubwana hilo; lakini bila shaka yeye alifanikiwa kutokana na kiu aliyokuwa nayo.

Sasa ikawa kila jioni, baada ya chakula Mei Lee aliwaimbia Mkuki na bibi Pin Ping huku akipiga gitaa. Alifanya hivyo kwa ustadi mkubwa sana na hakika kila mmoja alifarikija kusikiliza nyimbo zake.

****************************************

Mei Lee alikuwa akilala chumba kimoja na bibi Pin Ping; na huko kikongwe huyo aligundua kitu nyeti kuhusu mjuu wake huyu ambacho ni zaidi ya sauti nzuri na kipaji kikubwa alichokuwa nacho.

Aligindua kwamba Mei Lee alikuwa na mapenzi makubwa mno na Mkuki, na si mapenzi ya kawaida, mapenzi ya kaka na dada, bali mapenzi ya Adam na Hawa; mapenzi yaliyopelekea leo hii dunia kuwa na idadi kubwa mno ya watu.

Hili halikuwekwa wazi na Mei Lee mwenyewe, isipokuwa bibi Pin Ping alikuwa shuhuda wa kuweweseka kwa Mei Lee na ndoto zake za kila siku usiku alizokuwa akiota na huku akimtaja Mkuki.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



*************************





Hilo halikuwa jambo geni kumtokea Mei Lee, isipokuwa bibi Pin Ping aliligundua mara walipoanza kuwa wanalala pamoja, lakini ukweli ni kwamba Mei Lee alianza kuchanganyikiwa juu ya Mkuki tangu alipozungumza naye kwa kirefu kwa mara ya kwanza; ile siku alipomuonesha sura yake na Mkuki akampatia zawadi ya cheni. Tangu hapo moyo wake ulimuangukia mtoto wa kiume, alihisi kumpenda sana kiasi kwamba alishafunga naye ndoa, wakaanzisha familia na kuzaa watoto lukuki huko huko ndotoni.



Mkuki yeye hakuwa na mawazo hayo kabisa, alimchukulia Mei Lee kama dada yake kwa jinsi ambavyo alikuwa akimuheshimu sana marehemu mzee Wong na ule msaada aliompa.

Sasa bibi Pin Ping aliona kuna kila sababu ya kumsaidia mjukuu wake wa kike. Yeye aliyaelewa mapenzi sanjari na hisia za kumpenda mtu ambaye haonekani kuwa na dalili za kukufikiria kwa namna hiyo; hivyo mara moja akaanza kuandaa mipango ya kuhakikisha Mei Lee anafanikiwa, lakini alifanya hivi kimya kimya.

**************************************

Jiono moja Mkuki alirudi nyumbani na taarifa nzito, taarifa kwa ajili ya kubadilisha maisha ya Mei Lee sambamba na yeye pia.

Alirudi akiwa na karatasi ndogo ya rangi ya manjano mkononi, ilikuwa ni kipeperushi chenye kutangaza shindano kubwa la kusaka vipaji vipya vya waimbaji wa aina zote za muziki. Shindano lilikuwa likiitwa 'Chinese Singers Search', na lilikuwa likifanyika jijini Beijing.

“Inabidi twende Mei Lee. Ni lazima ushinde hili shindano.” Alimwambia lakini jibu alilolitoa Mei Lee lilimchosha.

“Hapana. Siwezi kwenda.”

“Kwanini? Hii ni nafasi yako Mei Lee, fursa kubwa ya kutimiza ndoto zako za na kubadilisha maisha pia.”

“Hapana. Siwezi.” Akasisitiza binti asieleze sababu za kukataa, lakini ukweli ni kuwa si kwamba hakuwa akipenda kushiriki shindano hilo, bali alikuwa akifikiria jinsi ambavyo atasimama mbele ya kundi kubwa la watu akiimba huku ile sura yake anayoichukia yenye makunyazi ikitazamwa na kila mmoja. Alijiona akikumbwa na fedhea kubwa kama atathubutu kufanya hivyo;  hakika alijithibitishia kwamba hakuwa na ujasiri wa kiasi hicho.

Lakini Mkuki hakukata tamaa, alimbembeza na kumlazimisha kwenda kwa sababu aliamini kama Mei Lee atashinda shidano hilo watakuwa  matajiri wakubwa kwa sababu mshindi wa kwanza wa shindano huogeshwa pesa si mchezo. Hata hivyo aligundua kuwa peke yake asingeweza, hapa akaamua kumshirikisha na bibi Pin Ping ambaye kimsingi ndiye aliyeweka nguvu kubwa na hata mwishowe Mei Lee alikubali kwenda ingawa kwa shingo upande.

Pia kukubali kwa Mei Lee ilikuwa na maana ya kwamba Mkuki aache kazi, na kwa pamoja, yeye na Mei Lee waongozane kutoka hapo Hong Kong hadi Beijing lilipokuwa likifanyia shindano hilo, kwa ajili ya kuweka kambi huko kipindi chote cha miezi miwili hadi litakapomalizika shidano;  hivyo watamuacha na bibi Pin Ping mwenyewe pia.

Hakika suala la kaucha kazi kwa Mkuki lilikuwa ni gumu sana kwa kufukirika kwa akili ya kawaida, lakini kwa sababu ya kuthamini ndoto za Mei Lee na lile donge nono kama zawadi kwa mshindi vilimjaza  matuamini na hakuogopa kupoteza kibarua chake-- alikuwa na imani kubwa na kipaji cha Mei Lee.

**********************************

Basi siku ya safari iliwadia, hakika ilikuwa ni siku chungu kuliko zote alziowahi kuishi bibi Pin Ping, ukiondoa ile siku aliyompeoteza mume wake kipenzi. Alikuwa amewazoea sana Mkuki na Mei Lee, kuondoka kwao ilikuwa ni kama kuchomolewa kiungo muhimu mwilini mwake.

Alishindwa kujizuia kulia bibi huyo wakati Mkuki na Mei Lee wanamuaga kwa mara ya mwisho, wanachukua mabegi yao na kuondoka—tena si kulia tu, bali aliangusha kilio kikubwa mno kilichoanzia moyoni.

Kubwa lililomliza ni jinsi ambavyo Mei Lee na Mkuki walishi naye kwa kumjali kana kwamba walikuwa ni familia moja yenye uhusiano wa kibailojia kabisa. Mei Lee na Mkuki walimuonesha upendo mkubwa bibi Pin Ping zaidi ya ambavyo mwanae wa kumzaa ambaye mara baada ya mama yake kuzeeka alimsukumia kwenye kituo cha kulelea wazee akaishi huko; hivyo maisha yake bila Mkuki na Mei Lee yasingekuwa na sababu ya msingi sana ya kuendelea kuwepo, bibi alitamani kutomokea mbali na dunia kuanzia siku ile.

Ili kuonesha upendo na thamani kubwa kwa yale waliyomfanyia kwa kipindi chote walichoishi pamoja alimuachia Mei Lee lile gita, alimpa kama zawadi akaitumie huko aendeko na hakika jambo hilo lilikuwa na maana kubwa kwa wote wawili hasa ukizingatia thamani ya lile gitaa analoliita ‘Caihong’ katika maisha ya Pin Ping.

Basi walifanikiwa kutoka nje ya Hong Kong na wakafika Beijing kwa gari. Huku walichukua chumba kimoja kwenye hoteli ya hadhi ya kawaida na kukilipia kwa siku saba—Mkuki alikuwa na pesa ya kutosha ya kumudu maisha ya kawaida kwa kipindi chote cha wao kuwa huko Beijing.

Usaili wa kwanza wa shindano ulikuwa ukifanyika kesho ya siku waliyofika, hivyo iliwalazimu waamke asubuhi kwa ajili ya kuelekea aneo ambalo zoezi zima lilikuwa likifanyika.

Usiku Mei lee hakutaka hata kufanya mazoezi, akili yake ilikuwa haifanyi kazi, alikuwa akifikiria jinsi ambavyo atasimama mbele ya kundi la watu huku uso wake ukiwa wazi—mashaka yake makubwa yaliishi katika hili.

********************************

Asubuhi ilifika, baada ya kupata kifungua kinywa Mkuki aliongozana na Mei Lee kuelekea lilipokuwa likifanyika shindano; hapakuwa mbali na hoteli waliyokodi hivyo walitumia miguu kufika huko.

Lilikuwa ni shindano kubwa na la aina yake, lilikuwa na mtindo tofauti na mashindano mengi ya aina hiyo hiyo. Wenyewe walikuwa wakifanya usaili mbele ya macho ya dunia nzima, yaani walirusha zoezi hilo 'mubashara' kwenye televisheni lakini pia kundi kubwa la hadhira huruhusiwa kuhudhuria ukumbini kutazama hatua ya awali kabisa ya upatiakanaji wa washiriki wa shindano.

Walifika ukumbini, lilikuwa ni shindano kubwa kweli kweli.  Washiriki lukuki walijazana kwenye mstari baada ya kujaza fomu za ushiriki wakisubiri kupanda jukwaani ili kuonesha walichokuwa nacho.

Mkuki alimsindikiza Mei Lee kwenye kuchukua fomu ya ushiriki na akajaza; baada ya hapo wakaachaana—Mkuki alikwenda kuketi kwa mashabiki wakati Mei Lee alikwenda kupanga foleni ya washiriki wanatakiwa kupanda jukwaani, kuimba.

Namba yake ilikuwa ni 69, hiyo ni sawa na kusema kwamba yeye alikuwa ni mshiriki wa sitini na tisa kupanda jukwaani na hadi kufikia wakati huo tayafi washiriki arobaini walishaimba na saba tu kati yao walifuzu kwa kupata kura za ndio kutoka kwa majaji wote watatu waliobobea kwenye suala zima la muziki.

Sasa alipanda mtu wa arobaini na moja, aliposhuka akaja anauemfuatia, akaja mwingine na mwingine. Kadri zamu ya Mei Lee ilivyokaribia ndivyo ambavyo alizidi kuchanganyikiwa. Alihisi joto lisilosemekana akiwa pale mstarini na gitaa lake. Tena ili kuficha fedhea juu ya uso wake aliufunika kwa nywele jambo ambalo Mkuki alimkataza sana kulifanya.

Mungu si Athumani zamu yake ikafika, mshehereshaji wa shindano akataja namba yake pamoja na jina na uraia kwa sababu shindano hilo hurusu watu kutoka Thaiwan na nchi nyingine za jirani pia. Akatoka kuelekea jukwaani taratibu huku akitetemeka si mchezo. Mapigo ya moyo yalimwenda kasi kana kwamba alimeza injini ya treni ya umeme, kile alichokiwa anakwenda kukifanya kilikuwa ni kizuri kwa maisha yake lakini kilihitaji kujiamini zaidi ya alivyokuwa yeye.

Akafika jukwaani akiwa na gita lake, hapo Mkuki akamuona kutokea kule alipoketi, akawa anamuomba Mungu amjaze ujasiri Mei Lee na kujiamini pia ili aweze kuunoesha uwezi mkubwa aliokuwa nao.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“Mei Lee. Karibu?” Jaji mkuu wa shindano akamkaribisha—mwanamume wa makamo, chotara wa kichina na Kimarekani, mrefu, mnene kidogo, mwenye nywele zilizonyolewa ungaunga (kawaida), aitwaye Will Chan; na alimuita jina kwa sababu majaji walikuwa na nakala ya fomu ya kila mshiriki aliyepanda jukwaani, kwahiyo alisoma jina lake huko.

“Asante.” Mei Lee akaitikitia lakini ni kwa sauti ya chini sana kiasi kwamba hata kuna wengine hawakusikia ingawa sauti ilipenya kwenye kipaza sauti kilichosimamishwa jukwaani, mbele ya kiti cha mguu mmoja maalum kwa ajili ya washiriki wanaopenda kuimba wakiwa wameketi.

“Utatuimbia nini leo?” Akauliza jaji Will Chan lakini kabla ya Mei Lee kuendelea jaji mwingine wa kiume pia aitwaye Zoe Zhing akaingilia mazungumzo yao.

“Kabla hatujajua atakachoomba tungependa tuione sura yake.” Akasema Jaji Zoe Zhing kwa sababu Mei Lee alikuwa amefunika uso wake kwa nywele; jambo ambalo Mkuki alishamkataza kubisa kulifanya.







“Sawa. Mei Lee tungependa utuimbie huku tukikuufahamu kwa sura.” Akasema Jaji Will Chan kwa mtindo wa kumbembeleza. Lakini Mei Lee hakujibu chochote juu ya suala hilo, badala yake alikuwa kimya kama bubu huku akiinamnisha kichwa chini mithili ya kondoo.



“Hei! Vipi? Kama unaona aibu toka hapo mbele waje wenzako. Shindano si kwa ajili mtu mmoja. Usitupotezee muda.” Akabatwa jaji Zoe Zhing lakini Will Chan akamtuliza kiutuzima; yeye alikuwa na mtazamo tofauti juu ya kile alichokuwa anaendelea kukiona kwa Mei Lee; alishaanza kufikiria kwamba huenda kulikuwa na tatizo linalomfanya yule msichana awe vile, hivyo ni lazima angehitaji msaada badala ya kupelekwa kijeshi kama ambavyo jaji Zoe Zhing alifanya.

“Mei Lee, umekuja na mtu yeyote hapa?” akauliza jaji Mkuu, Will Chan.

“Ndiyo.” Akajibu Mei Lee kwa sauti ya upole.

“Anaitwa nani?”

“Mkuki.”

“Ni nani yako?”

Mei Lee akapiga kimya, swali hilo lilikuwa gumu sana kwake, hakuwa akijua amtambulishe vipi Mkuki.

“Will huyu anatupotezea muda, tuna washiriki lukuki huko nje wanasubiri jukwaa hili hili. Atoke waje wengine.” Akasema jaji Zoe Zhing lakini kabla hata ya neno lingine la ziada halijazungumzwa kutoka kwake Mkuki alifika karibu na jukwaani, akaonana na mshereheshaji na kumuomba apate nafasi ya kuzungumza na msichana huyo kwa maana ni ndugu yake na ana matatizo fulani ya akili—alidanganya.

Mshehereshaji akaingilia kati.

“Majaji, mtu aliyekuja na Mei Lee yuko hapa, anaomba kusogea jukwaani azungumze naye, anasema ana matatizo.”

“Mruhusu aje.” Akasema jaji Will Chan, jambo ambalo lilimboa sana Zoe Zhing na wakaanza kuzozana wenyewe kwa wenyewe hata jaji Zoe akafikia hatua ya kusiamama na kutoka kwenye kiti cha ujaji kwa hasira, akaenda kukaa huko nyuma ya jukwaa akiahidi kurudi baada ya jaji mkuu kumaliza kumpendelea Mei Lee kwa kumpa fursa ya kupoteza muda namna ile.

Mkuki akapita akiwa na kipaza sauti mkononi, akasogea na kwenda kusimama karibu na Mei Lee.

“Wewe ndiye umekuja na Mei Lee.” Jaji Will akauliza swali ambalo tayari alikuwa na jibu lake—alitaka kuthibitisha tu.

“Ndiyo.” Mkuki akajibu.

“Ni nani yako.” Akauliza jaji.

“NI MPENZI WANGU.” Akajibu Mkuki tena kwa kujiamini mno kana kwamba yeye na Mei Lee walikuwa na uhusiano wa aina hiyo kwa miaka kumi sasa.

Jibu lake lilimshitua sana Mei Lee mwenyewe hata ilibaki kidogo aanguke na azirai kwa kile alichokisikia.  Kwa taarifa yako tu mi kwamba kilimfurahisha mno, alihisi mashamushamu na raha tele moyoni mwake. Hakuwahi kuitwa mpenzi na mwanaume yeyote tangu kuzaliwa kwake; lakini leo Mkuki Salumu Goigoi amefanya hivyo tena mbele ya dunia nzima, hakika alijihisi ni malaika, asijue Mkuki alifikiria nini hata kutamka maneno yale.

“Sawa. Zungumza naye aonyeshe sura na aanze kuimba. Ana dakika moja tu kuanzia sasa.” Akasema jaji Mkuu, wakati wote huo mashabiki walikuwa wakitamani kuona tamati ya ile filamu fupi isiyokuwa na ‘script’ inayochezeka pale jukwaani.

Basi Mkuki akamsogelea karibu zaidi Mei Lee, akasimama mbele yake, akanyanyua mkono wake mmoja na kumshika kidevuni, akamuinua uso ili wawe kama wanatazama, alifanya hivyo bila kumfunua nywele.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“Nakupenda Mei Lee. Nakupenda sana.” Akamwambia, tena kila mtu alisikia kwa sababu sauti yake ilipenya kwenye kipaza sauti alichoshika.

Kisha baada ya hapo Mkuki akafunua mywele za Mei Lee taratibu na kuzirudisha nyuma, halafu akasogeza mdomo wake polepole karibu na mdomo wa msichana huyo na bila dada mwenyewe kutarajia alinyonywa mate mbele ya hadhara kwa sekunde kadhaa.

Hakikuwa ni kitendo chenye maadili kwa nchi kama China lakini niamini mimi kwamba kilifanya kila mtu pale ukumbini ampende Mkuki na kumuona ni mwanaume timilifu hasa baada ya kumuachia, na uso wa Mei Lee kumulikwa na kamera na kufanya wote wagundue sababu ya binti huyo kukataa kuachia nywele zake—watu walijiuliza na hawakupata jibu la Mkuki alimpendaje, na huko kutokuwa na majawabu ndiko kulipelekea wamuone Mkuki ni shujaa haswa?

Baada ya pale Mkuki aliteremka jukwani akiwa amemuachia Mei Lee ujasiri mkubwa mno; lile busu mubashara alilopewa lilikuwa ni tiba haswaa; lilikuwa ni busu lake la kwanza la mdomo kwa mdomo tangu aumbwe na Mungu Mwenyezi.

Mkuki alifanya vile kwa sababu kuu moja; bibi Pin Ping alikwishamueleza kila kitu kitu kuhusu upendo wa Mei Lee juu yake; hivyo Mkuki alikuwa anafahamu yote, anafahamu kiu ya kupendwa aliyokuwa nayo Mei Lee na ndiyo maana alifanya vile ili kumpa ujasiri.

Binti akaketi kwenye kiti akielekea kipaza sauti, akapiga gitaa kidogo, kisha akafungua kinywa na kuimba. Ni nani kati ya waliomsikia alikuwa na kiburi kiasi kwamba angepinga ubora wa binti huyo kwenye kuimba na ule utamu wa sauti yake—hakuwepo hakika, wote walimuelewa sana, alipigiwa shangwe za ‘kufa mtu’ zilizoufunika ukumbi mzima.

Siku ile aliimba wimbo wake mwenyewe uitwao RANGI YA HUBA. Wimbo alioundika akiwa na ndoto za kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Mkuki, na mashahiri yake yaliendana kabisa na lile tukio lililotokea siku ile.

“Umeimba vizuri sana. Una pointi tatu kutoka kwangu.” Alisema jaji Mkuu na mtazamo wake ulikuwa sawa na jaji namba tatu ambaye alikuwa ni mwanamke; na ili kufuzu usaili huo mshiriki yeyote alihitaji jumla ya pointi sita huku kila jaji akiwa na uwezo wa kutoa pointi zisizozidi tatu tu, hiyo ilikuwa ni sawa na kusema kwamba ingawa maamuzi ya Mei Lee yalitoka kwa majaji wawili, lakini alifuzu kutokana na kwamba majaji wote wawili walimpa pointi tatu kila mmoja.

Baada ya pale Mei Lee aliteremka jukwaani akisindikizwa na makofu ya pongezi kutoka kwa hadhara waliohudhuria tukio lile; na ratiba ilikuwa ni kwamba baada ya hapo washiriki wote watakaofuzu watafanyiwa semina kabla ya kitumbukizwa kwenye shindano rasmi ambapo sasa raia watapewa ruhusa ya kupiga kura kwa njia ya simu za mkononi.

Aliposhuka chini Mei Lee alikutana na Mkuki, hapa Mei Lee alishindwa kujizuia kumkimbilia, kumkumbatia na kumpiga busu refu la mate kwa mate kwa mara nyingine—alikuwa ni kama amewehuka.



“Nakupenda Mkuki. Nakupenda sana.” Alimwambia baada ya kujichomoa kutoka kwenye lile kumbatio, kisha akamkumbatia na kumbusu tena.

Walipotoka nje ya ukumbi ilikuwa ni kasheshe, walikutana na kundi kubwa la waandishi wa habari wanaotaka kuzungunza na Mei Lee, si kwa sababu aliimba vizuri bali ni kutoka na ile hitulafu iliyo usoni mwake—waliamini habari iko hapo.

Hata hivyo mwenyewe hakuwa tayari kuzungunza lolote na kwa msaada wa Mkuki walifanikiwa kuwachenga waandishi wote na wakarejea hotelini.

Walifika hotelini huku mioyo yao ikiwa imejaa furaha na raha lakini zaidi ilikuwa ni kwa Mei Lee. Yeye aligubikwa na lindi zito la huba kwa kiasi kwamba nishati iliyotokana na hali penzi iliyozalishwa na moyo wake ingeweza hata kufanyiza umeme kwa ajili ya matumizi ya nyumbani.

Walipoingia ndani tu Mkuki alimkamata Mei Lee, akambeba na kwenda kumuanguashia kitandani. Kisha naye akaja juu yake, akaanza kumpiga denda huku akimpapasa taratibu kwenye maeneo mengine ya mwili wa binti huyo.

Binti alihisi raha iliyoje, raha isiyosimulika, raha ambayo bado haijapata msamiati wa kuidadavua kwa uzuri zaidi.

Mtoto wa kiume akaendelea na mashambulizi, na sasa wakafikia hatua ya kuchojoana nguo kabisa. Mkuki alipukitisha kiwalo kimoja baada ya kingine cha Mei Lee kana kwamba alikuwa akimchuna ngozi na tamati binti alibaki mtupu kama alivyozaliwa.

Hiyo ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Mkuki kushuhudia tupu ya Mei Lee, mtu ambaye awali alikuwa akimtazama kama dada yake. Mtoto wa kike alikuwa na mwili mzuri kweli kweli, ngozi laini kama hariri, kama aliyekoga mafuta ya jibini.

Basi Mkuki hakutaka kupepesa katika hili, alikwenda moja kwa moja kifuani, eneo ambalo lilikuwa na matiti saa sita yenye chuchu zilizosimama kama ncha ya msumari. Hapo akazinyonya taratibu kwa mahaba huku akitega sikio lake kusikiliza mrejesho wa jinsi ambavyo Mei Lee alikuwa akiugulia.

Ilikuwa ni raha tu, na utamu ulikamalika baada ya Mkuki kuingiza roketi yake pangoni mwa binti, na tangu hapo historia ikaandikwa kuwa ilikuwa ni mara ya kwanza kwa msichana huyo kuonja utamu wa ‘tunda la edeni’.

Tangu siku ile maisha yalibadilika sana hasa kwa Mei Lee, sasa alikuwa akijiona ni binadamu kamili, mwanamke asiye na kasoro. Mkuki alijitahidi sana kuwa mwanaume muungwana kwake na alifanya hivyo akisukumwa na upendo wa dhati ulioibuka ghaflla juu ya Mei Lee.

**************************





Siku ya semina kwa ajili ya wa washiriki wote waliofuzu ilifika; washiriki wapatao thelethini wa shindano lile walihidhuria akiwemo Mei Lee. Yeye alisindikizwa na Mkuki kama kawaida na alikuwa nje ya ukumbi wa semina akimsubiri.

Baada ya semina washiriki waliruhusiwa kuondoka huku sasa wakifahamu kwamba shindano litaanza kurindima wiki moja baadae.

Wiki haikuwa mbali namna hiyo; iliwadia na shindano lilianza mara moja, tena lilianza moto kweli kweli. Washiriki wote thelathini walikuwa na vipaji vikubwa lakini amini kwamba kwa Mei Lee wote walikuwa ni cha mtoto tu.

Mei Lee aliimba vizuri mno, sauti yake na ujuzi wa kupiga gita vizuri kulimfanya awe wa pekee sana kulinganisha na wenzie

Shindano lilikatiza wiki nne, na sasa walisalia washiriki 18 kwa sababu kila wiki moja walikuwa wakitoka washiriki watatu wenye kura chache zaidi  za mashabiki.

Hata hivyo dalili zilioneyesha wazi kwamba Mei Lee alikuwa anakwenda kuwa mshindi kwa sababu yeye alikuwa na kura nyingi sana ukilinganisha na washiriki wengine.

Baada ya wiki nane walisalia washiriki sita tu akiwemo Mei Lee ambao hao wangeimba kwenye onesho la nusu fainali na angetoka mshiriki mmoja na watano watakaosalia watakwenda moja kwa moja fainali.

Kabla ya nusu fainali Mei Lee alipata ofa kubwa ambayo ilikuwa ni kama ngekewa ya kubadilisha maisha yake. Ilikuwa ni kitu ambacho pengine alitamani kiwezekane kwa muda mrefu lakini alishindwa kukimudu kutokana na gharama.

Ilikuwa ni ofa kutoka hospitali ya YUN; hospitali ambayo ilikuwa imeshehenei madaktari bingwa hasa waliobobea katika suala zima la kufanya upasuaji.

Walimpa ofa ya kimsaidia kufanya uchunguzi wa tatizo alilonalo usoni na kama watagundua kuwa linaweza kutibika basi watampa matibabu na kuhakikisha anapona kabisa na walimchagua yeye kwa sababu waliamini kama atashinda atakuwa ni msanii mkubwa kwa hivyo anaweza kuwa balozi wao nambari moja.

Alimpa taarifa hiyo mpenzi wa maisha yake, Mkuki Salumu Goigoi ambaye naye alikubali bila shida huku akiomba Mungu tatizo la Mei Lee lipate matibabu ili naye apate kuona urembo halisi wa msichana huyo uliofichwa nyuma ya makunyanzi yake.

Basi Mkuki alimsindikiza hospitalini siku ya vipimo, binti akaingia chumba cha dakatari na baada ya mazungumzo ya hapa na pale alichukuliwa na kupelekwa chumba cha vipimo. Huko madaktari walifanya wanachofanya na tamati walikuja na jibu kwamba kuna uwezekano mkubwa wa kupona kabisa kupitia upasuaji watakaomfanyia ambao kimsingi ulikuwa ni upasuaji wa gharama kubwa mno.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Aliambiwa tatizo lilikuwa kwenye leya ya ndani ya ngozi, iliathiriwa na sumu ya Holocen ambayo hupatikana kwenye seli za viumbe wa baharini hasa samaki na kupitia hilo daktari alithibitishia kwamba huenda Mei Lee alipata tatizo baada ya kula samaki mwenye sumu hiyo.

Baada ya pale alipangiwa siku ya zoezi lenyewe la upasuaji na ilikuwa ni kesho kutwa ya siku hiyo ambayo itakuwa ni siku nne kabla ya nusu fainali ya shindano kufanyika; hivyo madaktari walimuhakikishia kwamba upasuaji hautaathiri uwezo wake wa kuimba.

Basi tangu pale waliona ni kama muda haukwendi, umesimama. Si yeye Mei Lee si mpenzi wake Mkuki, waliona siku ya upasuaji ni kama ilipangwa miaka miwili mbele. Lakini huo ulikuwa ni mtazamo wao, muda ulikwenda kama kawaida na hatimaye siku ikafika.

Mkuki alismindikiza tena mpenzi wake hadi hospitalini; huko Mei Lee akakutana na wale madaktari, wakamchuka hadi kwenye chumba cha upasuaji na shughuli ikaanza mara moja. Ulikuwa ni upasuaji mkubwa, uligharimu zaidi ya saa tatu hadi kukamilika na baada ya hapo Mei lee alifunikwa na kitu kama bandeji nyeupe usoni na kuingizwa kwenye mashine fulani ambayo hii ilikuwapo maalum kwa ajili ya kukamilisha matibabu.

Alitakiwa kukaa katika mashine hiyo kwa dakika thelathini na baada ya hapo angetoka akiwa Mei Lee mpya, Mei Lee halisi.

Basi hizo dakika thelathini zilikuwa ni kama miaka mia nane kwa Mkuki. Alikuwa na hamu ya kumuona Mei Lee baada ya matibabu, aliwashwa sana na mashumumashamu ya kuiona sura halisi ya msichana huyo—unajua hakuwahi kumuona hata kwenye picha.

Dakika thelathini nazo hazikuwa kitu, zilikatika na sasa ukawa ni muda muafaka kwa binti kutolewa kwenye ile mashine, kuvuliwa ile bandeji na kuwa yeye kama yeye.

Daktari aliyekuwa akimshuhulikia Mei Lee aliingia kule alipokuwa mgonjwa, akabofya kitufe na mashine ikafunguka, na taratibu akaanza kuondoa ile bandeji usoni mwa Mei Lee.

Zoezi lilikamlika, dokta akamuomba Mei Lee asimame taratibu, asogee mbele ya kioo na ajitazame kuona jinsi alivyokuwa.

Mei Lee akafanya hivyo, akashuka kitandani na kwenda kusimama mbele ya kioo kikubwa. Alitulia wa sekunde kadhaa akijitazama lakini ghafla alianza kulia kilio kikubwa mno, kilio cha furaha, kilo ambacho kilitafisri shukrani aliyokuwa nayo kwa Mungu na wale madktari waliofankisha zoezi la matibabu yake—hakuwahi kutarajia kwamba kuna siku tatizo lake  litapata kikomo.

Baada ya hapo aliombwa kutoka nje, kwenye kordo ambapo Mkuki alikuwa akimsubiri.

Basi Mkuki akiwa hapo akaona mlango ukifunguliwa, akatoka msichana ambaye Mkuki alijithibitishia kabisa kwamba ni Mei Lee wake. Hakika alihisi furaha moyoni kumtazama, hakuwahi kufikiria hata siku moja kwamba Mei Lee atakuwa ni msichana mrembo namna ile hasa ukizingatia kwamba si wasichana wengi wa kichina na hata Thaiwan ambao waliwahi kumvutia machoni. Mei Lee alikuwa na sura murua, ndogo ndogo ya duara, yenye kipua , vimacho, na vidomo viduchu-duchu.

Mkuki alisamama wakati Mei Lee akimfuata taratibu. Akamfika, akasimama mbele yake akimtazma bila aibu yoyote lakini ghafla alimvamia na wakakumbatiana.

“Nakupenda Mkuki. Nakupenda sana. Yote haya ni kwa sababu yako.” Alisema Mei Lee huku akilia kilio cha furaha mno. Yeye aliamini kwamba bila Mkuki kila kitu kisingekuwa kama kilivyo, asingefanikiwa kwa kiasi kile.

Hakika ile ilikuwa ni siku ya maana kubwa kwa wote wawili, siku ya kujitambua na kujifahamu, siku ambayo kila mmoja aligundua waziwazi sababu ya yeye kuwepo duniani.



**********************************

Siku ya nusu fainali iliwadia, watu walijazana ukimbini kama ilivyo kawaida na walianza kupata burudani taratibu kutoka kwa washiriki wa shindano lile.

Washiriki wote walipanda jukwaani na kuimba na Mei Lee akawa wa mwisho. Walifanya hivyo kwa sababu walitaka kuwashamgaza mashabiki kwa kile kilichotokea kwa kuwa hakuna mtu yeyote aliyefahamu kama anakwenda kufanya upasuaji wa kurekebishwa sura yake.

Basi alivyopanda jukwaani ziliibuka shangwe za kufa mtu, huku wengine hasa wanawake wakishindwa kuzuia hisia zao kiasi kwamba walilia mno kana kwamba walikuwa na undugu wa damu na Mei Lee. Walikuwa wakimpenda sana, walikuwa wakipenda anavyoimba, walipenda anavyopiga gita lakini pia walipenda haiba yake, na sasa wakajikuta wanaongezewa kitu kingine cha kupenda toka kwake—ile sura yake nzuri ya kitoto.

Niamini mimi kwamba baada ya hapo Mei Lee alikuwa na aslimia mia moja za kuwa mshindi wa shindano lile, hakukuwa na cha kumzuia asilani, aliwaongoza wenzake kwa kila kitu.

Baada ya mtanange wa nusu fainali kwisha na Mei kuwa ni miongoni mwa washiriki watakaokwenda fainali alitoka na Mkuki mpaka nje ya ukumbi ambapo huko Mei alivamiwa na kundi kubwa la mashabiki wakiomba kupiga naye picha na kupata saini yake kwenye nguo zao.

Kundi la mashabiki lilikuwa ni kubwa mno kiasi kwamba wasingeweza kuwamudu kwa namna yoyote ile; yaani kwa Mei Lee kukubali kupiga nao picha au labda kuwakimbia.

Hapo ilibidi wapate msaada kutoka kwa walinzi wa ukumbi lilipokuwa likifanyika shindano, lakini pia hawakufanikiwa kitu; watu waliendelea kumzonga Mei Lee pamoja na Mkuki pia.

‘Paaa’ mara mlio wa risasi ukasikika, risasi ambayo ilipigwa na askari mlinzi aliyeoona kuwa labda hiyo ndiyo njia pekee ya kuwasaidia kina Mei Lee.  Ghafla watu wakaonekana kuchanganyana huko na huko jambo ambalo kidogo lilifanya Kina Mei Lee wawe huru.

Papo hapo akatokea mwanaume mmoja, akamkamata mkono Mei Lee na kuanza kumvuta kwa kuelekea eneo ambalo halikuwa na mashabiki.

“Twendeni huku.” Akasema mwanaume huyo akimwambia Mkuki pamoja na Mei Lee, nao wakamfuata bila kujua wapi wanapelekwa na ni nani huyo aliyewaongoza.

Kwa msaada wa mwanaume yule walifanikiwa kuwatoka mashabiki na wakaifikia gari ya kisasa aina ya Rolls Royce yenye rangi nyeusi, jamaa akafungua mlango wa nyuma na kuwataka Mkuki na Mei Lee waingie kisha na yeye akaingia akiwa wa mwisho—upande huo wa  nyuma ulikuwa na viti wiwili vinavyotazama huku kila kiti kikitosha kukaliwa na watu wawili.

Yule mwanamume akaketi upande ambao alikuwa akiwatazama kina Mkuki uso kwa uso kisha papo hapo akamuamrisha dereva aendeshe gari na mambo yakawa hivyo, safari ya kusipojulikana ikaanza.

Kimya kifupi kilitawala mle ndani, jamaa alitazama na kina Mkuki kana kwamba walikuwa wakipanga mipango ya kukamilisha biashara fulani ya haramu.

Alikuwa ni mwanamume wa kichina mwenye umri unaocheza katikati ya  miaka 25 hadi 30, mrefu ukimlinganisha na wachina wengi lakini mfupi kwa Mkuki. Alikuwa amevalia suruali ya jinzi, raba miguuni na shati la mikono mirefu alilolivaa ndani ya koti la suti la rangi nyeusi. Nywele zake hazikuwa za kawaida, zilikuwa na mtindo wa ajabu kana kwamba alikuwa ni msanii wa muziki, pia alikuwa na hereni ndogo  kwenye sikio lake la kushoto, cheni kubwa shingoni, pete kidoleni na makorokoro mengi ya kufanana na bangili mikononi.

“Unajisikiaje? Umaarufu ni mtamu?” Akaamua kufuta ukimya jamaa  huyo kwa kumuuliza Mei Lee.

Mei Lee hakumjibu, alitabasamu.

“Samahani; umetusaidia lakini hatujui tukushuru kama nani, tunaweza kutambuana?” Akasema Mkuki. Hapa alikuwa akitaka kumfahamu mtu huyo baada ya ile sintofahamu iliyokuwemo baina yao hasa ukizingatia kwamba aliwaokoa kwa kutumia njia ya hatari sana ambayo hata hivyo hurusiwa kutumika zinapotokea hali za namna ile.

“Naitwa Leehom; bila shaka si jina linalohitaji ufafanuzi zaidi.” Akasema mwanaume huyo huku muda wote akionesha uso wa tabasamu—alikuwa na sura ya kuvutia pia.

“Sio vibaya ukitufafanulia.” akasema Mkuki; alikuwa akijiamini kweli kweli.

“Sawa. Nitafanya kama mnavyotaka.” Akasema jamaa  huyo aliyejitambulsiha kwa jina la Leehom na kuendelea. “Leehom ni moja ya nembo za taifa hili, sina tofauti na bendera yetu au labda ukuta mkuu wa Uchina. Kazi yangu ninnanyoifanya ni lulu masikioni mwa watu wengi, na kuna watu nje ya ardhi hii wananifahamu mimi zaidi ya wanavyoijua China.” Akasema Leehom; alitumia mtindo wa kona kona katika kujitambulisha.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“Kama nimekuelewa basi unamaanisha wewe ni  mwanamuziki, sio?” Mkuki akauliza.

“Bila shaka jibu ni ndiyo. Mimi ni mwanamuziki.” Akasema.

“Sawa. Kwahiyo utatupeleka hadi wapi? Kwa maana sisi tunaishi katika hoteli ya Nei Pei, ni karibu na pale ukumbini.”

“Najua. Najua kila kitu kuhusu nyinyi wawili. Najua pia hamtakuwa na pingamizi endapo nitawaomba kwamba kituo cha safari hii kiwe ni nyumbani kwangu, tupate mvinyo laini na chakula cha jioni kisha nitawariduisha hotelini kwenu.” Akasema Leehom.

********************************









ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog