Search This Blog

Thursday 27 October 2022

KAHABA YUAN LIANG - 3

 









    Simulizi : Kahaba Yuan Liang

    Sehemu Ya Tatu (3)





    Makao makuu ya polisi;



             Kamanda Junior pamoja na kamanda Amiry walikuwa wameketi mbele ya meza, huku Kamanda kendrick na wenzake wakiwa upande wa pili wa meza, pamoja na waziri wa ulinzi bwana Saidi Mbeku.



    “,swali la kwanza, raisi aliwambia anaenda kuonana na nani? “,



    “,hapana, lakini alitwambia mgeni wake ni mwanamke “,



    “,alitegemea mgeni wake atamjeruhi? au ni mtu mbaya kwake ?…”,



    “,Hapana, ndiyo maana alitwambia tusogee mbali na chumba chake, alimwamini mgeni wake kwa asilimia mia moja…”,



    “,mgeni huyo alikuwa ni mzungu, Muafrika, na alijiamini kiasi gani? ,”



    “,Alikuwa mzungu, alijiamini sana …”,



    “,Asanteni kwa ushirikiano wenu, kwa upelelezi tulio ufanya awali, tukilinganisha na huu, nyie hamna hatia, waziri wa ulinzi kwa vile yuko hapa, muachiwe haraka iwezekanavyo, muendelee na majukumu yenu ya kulijenga taifa, pia serikali iwalipe fidia, mtuhumiwa ni mwanamke, mzoefu wa mauaji, mwenye tabia za kujigeuza geuza, tutamkamata kwani tuna watalaamu wa kompyuta mahali hapa, twendeni tukaonane na raisi Jonsoni Mtemvu, kisha tukamtafute mtuhumiwa mahali alipo kabla ya saa kumi na mbili jioni …”,



    Jopo lote la maaskari wapelelezi wakasimama, wakaondoka, huku kamanda Amiry na mwenzake Junior wakiachiwa huru kwa amri ya waziri wa ulinzi,Saidi Mbeku, baada ya ukweli kuhusu muuaji aliyemjeruhi raisi na kumuibia kufahamika.



    Mexic; 11;00am



          Yuan Liang alikurupuka kutoka usingizini, alikuwa amechoka sana kwa purukushani za hapa na pale usiku uliopita, aliiba, akaua na kutoroka eneo la kasino ya Casabranka hoteli, lililopatikana katika mji mdogo wa Huwei, akakimbilia kilomita tano, katika mji mdogo wa Mexic, kaskazini mwa jiji la Costa, nchini Goshani.



    “,Nimelala sana, haijawahi kunitokea hata siku moja, I have to look for money, muda wa kazi sasa …”,Yuan Liang alijigeuza kitandani, akanyanyuka, akaisogelea simu yake, katika kabati chakavu, kama ujuavyo hoteli za uswazi, akaitazama simu yake, “11;00” saa yake ilisomeka, ilikuwa saa tano asubuhi, akapigwa na butwaa akishangaa jinsi masaa yalivyofyatuka kama umeme.



    “,Ngo ngo, ngo ngo, hodii! wenyewe! “,



    “,karibu, nakuja! “,



    Muda mfupi tu, akiwa bado amesimama akitafakari, mlango wa chumba chake ukaanza kugongwa, akaitika, akausogelea mlango wake, akachungulia kupitia tundu la mlangoni, akajiridhisha, aliyegonga mlango hakuwa adui yake, akafungua mlango.



    “,Umelala sana, pole na uchovu …”,



    “,Asante, “



    “,Jana umetoa pesa nyingi, hapa tunatoa huduma ya chakula pia, sijui nikuandalie chakula gani siku ya leo? “,



    “,Oooh, ok, nisubili kidogo, nakuja …”,



    Yalikuwa ni mazungumzo kati ya Yuan Liang pamoja na mwanamke aliyempokea usiku uliopita, Yuan Liang akarudi ndani, akasogelea mabegi yake mawili, akafungua, akachukua noti tano za elfu kumi kumi, akarudi tena mlangoni, kuzungumza na mwenyeji wake.



    “,Jana nilikupatia elfu hamsini, ile ni kwa ajili ya chumba, hii hapa ni kwa ajili ya chakula, “



    “,Sawa dada, hapa kuna chapati, ndizi nyama, wali,pamoja na chipsi, sijui tukuletee msosi gani? “,



    “,Asubuhi chapati na chai, mchana chipsi, usiku niletee ndizi nyama! “,



    “,Ok dada, asante! “,



    Mama yule aliongea, akamuaga Yuan Liang,akaondoka zake. Yuan Liang akafunga mlango wa chumba chake, akabonyeza bonyeza  simu yake, akaweka sikioni.



    “,Haloo “,Yuan Liang aliongea.



    “,Hallow nani mwenzangu? “,upande wa pili wa simu uliitikia.



    “,Saa tano usiku nipate pesa zangu, mpate diski yenu, mtanikuta Mexic, mji mdogo kaskazini mwa Goshani, nitawambia pesa mumpatie nani, na diski mtaipataje, “Yuan Liang aliongea.



    “,Haloo, haloo, halooo! “,upande wa pili wa simu ukaongea, simu haikujibiwa, Yuan Liang akabonyeza tena simu yake, akakata simu.



    “,Mshenzi kabisa, anazani natania, niko siliasi, ngoja aone,”Yuan Liang aliongea, akachukua kompyuta yake, akakaa kitandani, akaendelea na shughuli zake za kuchezea kompyuta yake.



    …………………………………



    Ikulu; Saa moja iliyopita



             Waziri mkuu Januari Sasamba, alikuwa ameketi kitandani, pembeni na rafiki yake kipenzi, raisi Jonsoni Mtemvu. Walikuna vichwa vyao, wakatafakari bila kupata majibu, walitafakari kuhusu namna ya kurudisha diski yenye siri nyingi haramu,irudi katika himaya yao.



    “,Kachukue pesa, anza safari ya kuelekea huko, hakikisha haumwambii mtu yoyote yule …”,



    “,lakini mkuu, vipi kuhusu makachelo hawa kutoka Tanzania,situwaachie wafanye kazi wao! “,



    “,Itakua vizuri zaidi tukiipata sisi kama sisi, bila kupitia wao, kwani wakiipata wao wanaweza kuichunguza diski hiyo, mambo yakawa mabaya zaidi, “



    “,Sawa bosi, nimekuelewa “,Januari Sasamba aliitikia, akasimama kutaka kuondoka, huku raisi akiipokea simu yake iliyoonekana ikiita kwa muda mrefu, bila kupokelewa.



    “,Haloo,nani mwenzangu? “,raisi aliongea, akasikiliza maelezo kutoka upande wa pili wa simu.



    “,Haloo, haloo, halooo!”,Jonsoni Mtemvu aliongea, akaongea tena, alikuwa amepagawa, simu ilikuwa tayali imekatwa, waziri mkuu Januari Sasamba alikuwa bado hajaondoka, alikuwa amesimama mlangoni, akisikiliza maongezi kati ya raisi, pamoja na mtu aliyempigia simu bila kumfahamu.Akajongea taratibu, akarudi katika kitanda alicholazwa rafiki yake.



    “,Kapiga tena! “,



    “,Anasemaje? “,



    “,kasisitiza kuhusu pesa zake, anasema pesa zipelekwe katika mji mdogo wa Mexic, atatutarifu mahali pa kuonana naye …”,



    “,duuuh, haina jinsi, ngoja nikajiandae, nifike huko …”,



    “,Sawa,jitahidi, kazi njema! “!



    Januari Sasamba alimaliza kuongea, akaagana na rafiki yake, akasimama, akaondoka zake.



    …………………………………

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    12;45pm



                The super three soldiers walirejea tena ikulu, wakiongozana na kamanda Gupta, pamoja na kamanda Yasini. Waka keti katika sofa, karibu kabisa na kitanda cha mheshimiwa raisi Jonsoni Mtemvu.



    “,unaendeleaje mheshimiwa? “,



    “,naendelea vizuri, nipe ripoti! “,



    “,Upelelezi unaendelea vizuri, mtuhumiwa ni hatari sana, walinzi wako hawahusiki na chochote kile, tunaomba utusaidie saa yako, saa ndio kila kitu kwa sasa, tumalizie hatua ya mwisho ya uchunguzi! “,



    Kamanda Kendrick aliongea,akitoa ripoti ya upelelezi kwa raisi Jonsoni Mtemvu, dakika mbili tu, raisi akavua saa yake mkononi,kamanda Philipo akaipokea, akaipachika katika kifaa kidogo kilichokua na taa nyekundu, taa nyekundu ikiwaka na kuzima.



    Kamanda Philipo akachukua kompyuta yake, kwenye begi dogo, akaifungua, akachomeka waya wa USB, akaunganisha na kifaa kidogo, kifaa kilichokuwa na saa ya raisi, akaanza kazi yake, kamanda Catherine akiwa pembeni yake, wote walikuwa wataalamu wa kutumia kompyuta.



    “,Connection loading ……”,kioo cha kompyuta kilisomeka kwa kizungu.



    “,Vipi, mahali ilipo diski ya saa mmepatambua? “,kamanda Kendrick aliuliza.



    “,hapana, bado inasachi,ngoja tusubili …”,kamanda Philipo aliongea.



    ‘,link connected, the related disc available in Mexic,Costa, Goshani “,(imeunganishwa, diski inayohusiana inapatikana Mexic, Costa, Goshani …)”,maandishi yalisomeka tena katika kioo cha kompyuta,picha kubwa ya ramani ikaonekana.



    “,tayali, sogeeni muone,diski iko Mexic, bila shaka mtuhumiwa yuko huko Mexic…,”Catherine aliongea, macho yake yakiwa bize kutazama kompyuta.



    “,Mexic!! “,raisi alishtuka, alisikia jina ambalo lilitajwa awali kwenye simu na mtu aliyempigia, akihitaji pesa apatiwe diski yake, akatafakari jambo, katika kichwa chake.



    “,Basi kamateni silaha, tuondoke! “,kamanda Catherine aliongea, kamanda Philipo na wenzake wakaacha kutazama ramani katika kompyuta, wakasimama, “tunaondoka mheshimiwa, salutii “,kamanda Kendrick aliongea, wakapiga saluti, wakatoka nje, kuelekea Mexic, kaskazini mwa jiji la Costa, nchini Goshani.



    Mara tu baada ya the super three soldiers kutoka nje ya chumba chake, alichokuwa anapatiwa matibabu,mheshimiwa raisi, Jonsoni Mtemvu alichukua simu yake, akalitafuta jina la waziri Januari Sasamba,akapiga simu, simu ikaita, ikaita tena na tena bila mafanikio.



    “,huyu vipi, mbona hapokei simu? “,aliongea, akapiga tena, dakika mbili tu, ikapokelewa.



    “,Haloo, niko ndani ya gari, ndio maana sikusikia simu, nambie, “upande wa pili wa simu ulisikika.



    “,Kuwa makini, makamanda wanakuja huko,mitambo yao inaonesha mtuhumiwa yuko huko, hakikisha unachukua diski kabla yao, ikishindikana, wakawahi kuichukua, hakikisha wanakupatia kabla hawajagundua siri zetu, mpaka najuta kwanini niliwaleta, tukizubaa watatugeukia!!”Jonsoni Mtemvu aliongea, akakata simu.



    “,Usjali mkuu, nitakua salama …”,upande wa pili wa simu uliongea, simu ikakatwa, angalau raisi Jonsoni Mtemvu akawa na amani moyoni.



    …………………………………



    Gari lilikanyagwa mafuta, kamanda Gupta kama kawaida yake, alifahamu kila kona za jiji la Costa, alikuwa ameshika uskani,barabara kuu, kuelekea nje ya mji, kaskazini mwa jiji la Costa.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kadri walivyozidi kusafiri, masaa yakazidi kwenda, ndivyo kilomita za eneo, mahali diski ilipo, ziliweza kupungua.



    “,Bado kilomita kumi, endelea kukanyaga mafuta, tukifika mji unaoitwa Huwei, tutaupita, tutasogea kilomita tano mbele, tutafika eneo la Mexic, mahali diski ilipo, “kamanda Catherine aliongea, akifuatilia ramani kupitia kompyuta yao.



    “,Sawa mkuu, nusu saa inatosha, tutafika …”!,kamanda Gupta aliwatoa hofu, akaendelea kukanyaga mafuta ya difenda yao, gari ikafyatuka kama umeme, na kuwaacha midomo wazi, raia pamoja na askari wa usalama barabarani kandokando ya barabara, king’ora juu ya gari kilipiga kelele na kutahadharisha watumiaji wengine wa barabara kuwa makini na gari hilo la polisi.



    …………………………………



    Huwei;



          Kikundi cha majambazi, maarufu kama “Casablanca gang ” ,kikichomilikiwa na bilionea Xavery, mfanyabiashara wa madawa ya kulevya, silaha pamoja na filamu chafu za ngono,kilianza safari kutoka Huwei, kuelekea Mexic, mahali iliposemekana Yuan Liang alitorokea huko.



    Vijana sita, wawili wazungu, mmoja mjapani, na watatu Waafrika tena waswahili wa nchini Goshani, walikuwa wamepanda pikipiki zao, miwani rangi nyeusi pamoja na suti nyeupe, wakielekea kumtafuta Yuan Liang, wamshawishi ajiunge nao kwa lazima au hiari, kama walivyoelekezwa na bilionea Xavery.



    Mexic; 1;00pm



            Yuan Liang alikuwa ameketi kwenye kitanda chake,machale yalimcheza, kichwa chake hakikutulia hata kidogo, muda wote alikuwa anasimama na kuchungulia dirishani, kuchunguza usalama wake.



    “,Siko sawa, kuna kitu sio bure! ninapaswa kujiandaa, muda wowote kuna kitu kinaweza kutokea …”,Yuan Liang aliongea, akatelekeza kompyuta yake pembeni, akasogelea mabegi yake ya nguo pamoja na vifaa muhimu. Akavaa jinsi yake aliyoitumia siku zote kwenye mauaji, akavaa mkanda wenye visu vidogo vidogo maarufu kama “magic knives ,akachukua bastola yake, akaiweka kiunoni,akavaa koti lake kubwa lililokaribia kumfika miguuni, akachukua miwani yake,akaivaa,akasogelea viatu vyake vyenye visigino



    virefu,akavivaa,dakika tano tu zilitumika, tayali alikuwa amekamilika.



    Akapekua tena begi lake, akauona mkoba wake, akaufungua, akachukua diski, kisha akarudisha mkoba na kulifunga tena begi lake, akatoka nje na kutokomea.



    “,Hapa si salama tena, ngoja niondoke, nitarudi baadae, “aliongea baada ya kufunga mlango wa chumba chake, akaanza kupita koridoni, akakunja kushoto, akakunja kulia, akatoka nje ya hoteli aliyokuwa amepanga, akachukua pikipiki yake, mahali alipokuwa amepaki,akawasha, akaondoka haraka sana eneo lile kama upepo.



    Akakamata barabara kubwa ya kuelekea mji wa Huwei,alikuwa anatafuta mahali salama, aweze kufanya biashara na serikali ya raisi wa nchi, bwana Jonsoni Mtemvu, ampatie diski, kisha yeye apate bilioni kumi kama walivyokubaliana.



    “,Kuna kibanda cha baa, nilikipata jana, nikifika pale, nitamjulisha aniletee pesa mahali hapo, maana ni nje ya mji, hakuna watu wengi,tunaweza kufanya biashara vizuri tu, akinizingua, na mimi namzingua! “,Yuan Liang aliongea, akiwa amekamatilia pikipiki yake, akatoweka mbali na mji mdogo wa Mexic,akiwa ameshika njia ya kurudi jijini Costa, kupitia mji wa Huwei.



    Baada ya robo saa, akiwa ametembea kilomita tatu, zikiwa zimesalia kilomita mbili tu afike mji wa Huwei, alifika katika baa aliyokuwa akiifikiria, akapunguza mwendo wa pikipiki yake,akapaki pikipiki yake, akashuka, akaisogelea kaunta.



    “,Samahani dada,nikusaidie nini! “,muhudumu wa baa aliuliza.



    “,Konyagi pamoja na maji,shilingi ngapi? “,Yuan Liang akauliza.



    “,elfu kumi na tano tu …”,muhudumu akajibu, Yuan Liang akaingiza mkono mfukoni, akatoa noti mbili za elfu kumi kumi,akampatia muhudumu, kisha akarudishiwa shilingi elfu tano..



    “,hapana, hiyo baki nayo, itakusaidia! “,Yuan Liang aliongea.



    “,asante dada yangu …”,muhudumu akashukuru, akachukua chupa ya konyagi iliyojaa vizuri, akampatia na chupa ya maji ya Uhai kutoka nchi jirani ya Tanzania, akampatia. Yuan Liang akapokea, akasogelea meza moja yenye viti takribani sita, akaketi mahali hapo, akachanganya konyagi na maji kwenye glasi, akaanza kunywa, huku mziki wa rumba taratibu ukipigwa katika baa hiyo, na kupenya vilivyo katika moyo wa Yuan Liang.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “,Nilipopatwa na ajari, nililia sana, fanya hima, nisaidieee!,”,



    “,wanaume tumeumbwa, matesoo ,matesooo, kuhangaikaa! “,



    Ni moja ya mistari iliyopenya katika nafsi ya Yuan Liang, japo hakuwa mwanaume, lakini nyimbo ilimgusa bila kutegemea, akajikuta anatikisa kichwa kufuata biti la wimbo huo, ulioimbwa na bendi maarufu ya Msondo ngoma, kutoka nchini Tanzania, Afrika ya Mashariki. Akaendelea kunywa, akisubili muda ufike, aweze kumjulisha raisi Jonsoni Mtemvu, aweze kuleta pesa zake, ajipatie diski yake kabla hajaivujisha na kuweka mambo yote hadharani.



    …………………………………



    Huwei;



           Kamanda Gupta aliendelea kukanyaga mafuta,wakafika mji wa Huwei, wakakata kona kidogo, wakanyosha barabara kubwa iliyopita pembeni ya jengo kubwa la Casablanca kasino, hawakusimama, wakanyosha moja kwa moja kuelekea mji ndogo wa Mexic, kilomita tano kutoka Huwei.



    “,Kuweni makini, oneni! diski imehamishwa tena, adui yuko kilomita tatu kutoka mahali alipokuwa awali,kilomita mbili kutoka hapa tulipo, bila shaka machale yamemcheza! “,kamanda Philipo aliongea, wote macho yao yakahamia katika kompyuta.



    “,Huyu mpuuzi anaonekana ni hatari eee!, lakini leo itakua mwisho wake! “,kamanda Kendrick aliongea,huku akiikoki bastola yake.



    “,Bado dakika tano, tufike eneo hilo, kilomita mbili kutoka Huwei, lakini tutajuaje mahali diski ilipo?, na nani anayo? “,kamanda Gupta aliuliza.



    “,tukifika,kompyuta itaonyesha,kumjua mtuhumiwa, itabidi tutumie mbinu za kipelelezi pamoja na uzoefu, muuaji anajulikana popote pale …”,kamanda Catherine alisisitiza, kisha ukimya ukatawala,safari ikaendelea …



    dakika tano zikakatika,walikuwa bado hawajafika, dakika saba sikafika, ” ,link connected, the disc related is available in this area …,”limeunganishwa,diski inayohusiana inapatikana eneo hili)”,maandishi yalitokea katika kompyuta,ikaonesha ramani ndogo,ambayo hawakuielewa vizuri.



    “,Tumefika,lakini hatuoni majumba mengi mahali hapa,hebu paki gari hapo baa,tuanze upelelezi…”,kamanda Catherine alitoa maelekezo,wakazima kin’gora wasiwashtue watu,wakachukua silaha zao ndogo,bastola pamoja na vizu,wakaweka katika nguo zao,wakatoka na kuisogelea baa,wakiwa makini kupeleleza kila sura waliyo iona!”,



    …………………………………



    Yuan Liang aliendelea kunywa bia yake,lakini ghafla alisikia mlio wa king’ora cha polisi kwa mbali,kelele za king’ora zikaongezeka kadri muda ulivyozidi kwenda,difenda ya polisi ikafunga breki kwa fujo, king’ora kikazimwa, difenda ya polisi ikakata kona na kupaki pembeni ya baa.



    “,Shit! damu itamwagika, mimi ni wa kuniletea polisi? Jonsoni Mtemvu are you serious?, kwa nini umekiuka maagizo yangu, why? “,Yuan Liang aliongea pekeyake, akiwa amejaa na hasira ghafla, polisi wakashuka na kuingia ndani ya baa, waka angaza huku na kule, wakasogea kaunta, “muhudumu, tupatie juisi kila mmoja, mi pia nipatie na maji, “Kamanda Kendrick aliongea, macho yake yakiwa bize kumtazama raia wa kichina, aliyekuwa ameketi mita takribani tano kutoka eneo la kaunta…



    “,Huyu namuhofia, wageni wote wa raisi, walikuwa raia wa kigeni! tena wanawake kama huyu, harafu mavazi ya mwanamke huyu si ya binadamu wa kawaida ,”kamanda Kendrick alipiga mahesabu kichwani mwake, akimtazama mwanamke ambaye alikuwa bize kunywa bia yake, bila wasiwasi wowote.



    “,Saa yake ni ya kipelelezi, miwani yake ni automatiki mashine, inabatani mkono wa kulia wa jicho, viatu vyake, kisigino chake kinafanana na kile kisigino cha kiatu, katika hoteli zote mbili, nina wasiwasi na mwanamke huyu, tukienda vibaya, hakuna atakaye rudi salama nchini Tanzania “,kamanda Catherine aliwaza.



    “,Huyu mwanamke mavazi yake, kama komandoo, sio huyu kweli, mbona koti kubwa kama jambazi, ila wachina sio watu wazuri, wanapiga karate kama mashine, tusipokuwa makini, kama ni yeye atatushambulia kabla hatujashtukia …”,kamanda Philipo aliwaza.



    “,Gupta, Guptaa! yule mwanamke mi namuhofia, anaonekana tu ni hatari, kama sio yeye muuaji, ninani sasa eneo hili …?”kamanda Yasini alimnongoneza kamanda Gupta.



    “,Hakuna, atakua ni yeye tu! “,kamanda Gupta aliitikia kwa sauti ya chini, mazungumzo ambayo hakuna mtu yoyote aliyasikia, zaidi yake na kamanda Yasini. Wote walikuwa bize wakitafakari,fikra zikiwatuma kuwa mwanamke aliyekuwa mbele yao, ndiye muuaji waliyekuwa wakimtafuta.



    “,Vipi wateja wangu, vinywaji nimeshawaletea muda mrefu, chukueni mkanywe,!”,



    “,aaa…a…aah sawa kabisa, asa…nte …”,http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Muhudumu aliwashtua, wote wakashtuka, wakaitikia kwa kigugumizi,wakachukua vinywaji vyao, wakaenda kuketi meza moja na Yuan Liang, muuaji mkatili, chotara wa kichina,walikaa karibu naye, ili wampeleleze kwa undani zaidi.



    “,Samahani dada, sijui unaitwa nani? “,



    “,Hwan Lee …”,



    “,Ohoo, kumbe unajua kiswahili, we unatokea nchi gani hapa Afrika mashariki …”,.



    “,Goshani is my mother land, China is my father land! “,.



    “,ohoo, nice! ,kumbe mchina pia, unaonekanaa…”,



    “,Hahaahaa “,



    Wote walicheka kwa kicheko cha kinafki, Catherine alikuwa ameshagundua mtu aliyekuwa mbele yao alikuwa ni hatari sana, aliuona mkanda wenye visu, visu ambavyo alivitambua vizuri sana, kisu kimoja cha aina hiyo kilitumika kukata kioo katika hoteli ya Serena, mapigo ya moyo wake yakaanza kukimbia kwa kasi sana.



    “,Mbona mna maswali mengi, nyinyi ni polisi? “,



    Yuan Liang aliwauliza swali la mtego, huku fikra zake zikiwa tayali kwa mashambulizi,kamanda Kendrick na wenzake hawakutegemea swali hilo, wakakosa jibu la kumpatia kwa haraka, wakaangaliana, wakakonyezana, Yuan Liang alizitambua fikra zao, akaendelea kujifanya mjinga mbele yao, awatie adabu vizuri, bila kujua kuwa askari mbele yake sio askari mdebwedo aliowazoea.



    “,Uko chini ya ulinzi!, usitikisike, kaa hapo hapo …”,ghafla, bastola sita zilikua kichwani mwake, akatii maelekezo, akipiga mahesabu namna ya kuwashambulia, kisha atokomeee.



    …………………………………



    Vijana sita wa kundi la Casabranka gang walipoteza mwelekeo,hawakufanikiwa kumuona adui yao maeneo ya Mexic walikoelekezwa, hoteli zote kubwa za starehe walikagua bila mafanikio, wakafunga safari kurudi katika makazi yao ya Huwei, kumpatia ripoti bosi wao, bilionea Xavery.



    Walifika katika baa waliyopita awali, wakataka wapoze kiu zao kwa mara nyingine tena,ghafla wakashtuka, kabla hawajapaki pikipiki zao, waliona gari la polisi, wakaogopa kupaki pikipiki zao, walipochunguza kwa makini, walimuona msichana waliyemtafuta, kwani jibaba wa mlango wa kasino alimtambua vizuri,akawajulisha wenzake…



    “,Nd’o yeye!, wamemkamata!, shambulieni, muokoeni! “,



    Jibaba lile la mlango wa kasino la Casabranka lilipiga kelele, liliitambua vizuri sura ya Yuan Liang,wote wakashambulia, wakiwa bado juu ya pikipiki zao..



    Yuan Liang akiwa amenyoshewa silaha, ghafla alisikia mlio wa pikipiki nje, alipogeuza shingo lake kutazama pikipiki hizo, alimtambua mmoja kati ya vijana sita, walivalia miwani myeusi na suti nyeupe, walipoiona sura yake, wakachomoa silaha zao, wakashambulia askari waliomnyoshea silaha Yuan Liang, Yuan Liang akatumia fursa hiyo kujiokoa, aliruka serekasi mara mbili, akapiga mateke sita,Catherine akapangua,bastola yake ikadondokea kule, kamanda Kendrick akalipangua teke hilo, lakini likamzidi nguvu, akaangukia upande wa pili, Gupta, Yasini pamoja na Philipo wakatandikwa na kuangukia kule, Yuan Liang alikuwa ameshika rimoti ya pikipiki yake, akaibonyeza huku anakimbia, pikipiki ikawaka, akakimbia na kuirukia, akapanda, akaondoka, huku vijana wa Casabranka gang wakimsaidia kushambulia, wakapiga risasi taili za difenda ya polisi, wakatoweka zao …



    “,Yalaaa, inaumaaa, wamenipiga risasi wajinga hawa……!!”,Kamanda Kendrick alipiga kelele…



    “,Jikaze, jikaze, ngoja nikusaidie, tayali wametuponyokaaa,ama zao ama zetu…”,kamanda Catherine aliongea, akasogea kumsaidia kamanda Kendrick, risasi ilipenya katika bega lake, alipojaribu kumzuia Yuan Liang asikimbie, akajikuta anagaagaa kwa uchungu.



    Mexic;



         Waziri mkuu, Januari Sasamba, alikuwa na masaa mawili, akiwa ndani ya mji mdogo wa Mexic. Alikodi chumba cha kifahari kwa siku moja tu,katika hoteli ya kitalii maarufu kama” Mexic garden hotel “,hoteli yenye mandhari mazuri ya kuvutia, hasa maua yenye rangi nyekundu na njano, yaliyopandwa kuzunguka maeneo yote ya hoteli,vipepeo wakiruka na kuzidi kupendezesha uzuri wa eneo hili.



    Wageni wote katika hoteli hii walikuwa na nyuso za furaha,isipokuwa mtu mmoja tu, ambaye muda wote alijishika kichwani, akijikuna kipara chake, midomo yake ilicheza cheza, bila shaka alikuwa akiongea mwenyewe, si mwingine, ni waziri mkuu wa nchi ya Goshani, waziri ambaye alitambulika kila kona kwa utendaji wake mzuri serikalini, licha ya kuwa na siri nyingi moyoni mwake, siri ambazo iwapo zitagundulika, hakustahili kuendelea kuishi, adhabu ya siri zake nzito alizozificha ni kunyongwa …



    “,Usafi uimarike,mpatieni huduma nzuri, aitangaze vizuri hoteli yetu …”



    “,Sawa bosi! “,



    “,Haya mnaweza kwenda, kuendelea na majukumu yenu …!”,



    Alikuwa ni meneja wa hoteli ya Mexic garden,akizungumza na wafanyakazi wake, baada ya kuitisha kikao cha dharula,walipopata mgeni mkubwa kutoka serikalini, ndani ya dakika kumi tu, kikao kifupi kilimalizika, wote wakatawanyika …



    ……………… …………………



    Waziri Januari Sasamba alisimama, akatembea huku na kule, akachungulia dirishani, hakuona chochote kile, zaidi ya vipepeo walioruka kufurahia maua, pamoja na watu wachache walioketi katika bustani, wakifurahia na familia zao, akatoka katika dirisha, akaketi kwenye sofa ndani ya chumba chake, chumba namba tatu, akachukua simu yake, akaanza kupangusa kioo cha simu yake,bila shaka alichunguza kitu fulani …



    “,Mbona hapigi? Mbona hasemi nimkute mahali gani?, ok, let me call him, ngoja nimpigie! “,



    Waziri, mheshimiwa Sasamba aliongea,akanyenyua simu yake, akaweka sikioni, akapiga, simu ikaanza kuita, ikaita tena mpaka ikakata,haikupokelewa,akapiga tena, ikaita, sekunde mbili tu ikapokelewa …



    “,Haloo, naitwa Waziri Januari Sasamba, nimetumwa na muheshimiwa raisi kuleta pesa zako, kisha unipatie diski, nikuletee pesa wapi?? “,waziri mkuu, mheshimiwa Sasamba aliongea.



    “,Pumbavu kabisa, wewe na raisi wako nyote mtakufa, nitawaua, kisha nitaanika kila kitu wazi! Haiwezekani mniletee polisi mimi, mnataka kuniua?, I say you can’t, you can’t kill me, hamuwezi kuniua hata siku moja! “,upande wa simu uliongea kwa kufoka, kisha simu ikakatwa.



    “,Haloo, haloo, haloo! “,Januari Sasamba aliongea, akaongea tena, simu ilikuwa imeshakatwa. Hakuamini alichokisikia, mwili wake ukafa ganzi, akaanza kutetemeka kwa woga.



    “,Nini kimetokea? mbona sielewi?, au the super three soldiers walitaka kumnasa?, tumekwishaa! bora tusingewaleta! kazi imekua ngumu kwelikweli!,”Januari Sasamba aliongea mwenyewe, kama mtu angemtazama, alivyokuwa akiongea peke yake, hakuwa na tofauti na kichaa, mheshimiwa waziri siku zote hakua mwepesi kukata tamaa, alinyanyua simu yake kwa mara nyingine tena, akampigia simu jambazi hatari wa kike,ambaye hakuwahi kumuona uso kwa uso hata mara moja, japo yeye ndiye alikuwa chanzo cha matatizo, kwa kumtafuta kahaba huyu kupitia mtandao wa Instagram ili amridhishe rafiki yake, raisi Jonsoni Mtemvu, bila kutambua kuwa mwanamke huyo alikuwa zaidi ya hatari, jambo ambalo lilimfanya ajutie kila siku iendayo kwa Mungu …



    “,Nimesema sitaki maongezi na nyinyi! sitaki pesa zenu! hukumu yenu ni kifo tu, ……”,sauti ya kufoka ilisikika, simu ikakatwa, waziri Sasamba akanyongonyea, maneno aliyoyasikia yalikuwa machungu na mazito.Hakuwa na haja ya kupiga tena simu, alijilaza kwenye sofa bila kupenda,akiwa hajui nini cha kufanya…



    ………………………………



    Nusu saa iliyopita;



             Yuan Liang alifanikiwa kuponyoka mikononi mwa the super three soldiers, kwa msaada wa kikundi cha uhalifu, kikundi kilichojihusisha na biashara haramu maarufu kama Casablanca gang,wote kwa pamoja waliendesha pikipiki zao kwa kasi sana,wakanyosha barabara moja kwa moja,kuelekea mji wa Huwei,baada ya dakika kumi,walikuwa tayali wamekimbia kilomita mbili,wakafika katika kasino lao,makao makuu yao yaliyopatikana katika jengo lao kubwa la hoteli,wakaingiza pikipiki zao,wakaingia mafichoni,chini ya ardhi,kwenye mahandaki yaliyojengwa kwa siri miaka mingi iliyopita…



    “,Nahitaji kuondoka!,nambie niwalipe  kitu gani,pesa au kitu gani,kwa msaada mlio nipatia…!”,



    “,Tunataka ujiunge na sisi,nd’o lengo kuu la sisi kukutafuta na kukusaidia…”,



    “,Hapana,hilo halitawezekana!”,



    “,tunaomba utii maagizo yetu,bila hivyo utakufa!”,



    “,Mnanitisha si ndio?,death is nothing to me,siogopi kufaaa!,kabla sijafa mimi,nyote mtakua mmeshaoza na kuanza kunuka!”,



    “,Unatutukana si ndio?”,



    “,drii,drii,drii……”,



    “,Hebu niache nipokee simu,cool down please!”,



    Mazungumzo yaliendelea kati ya bilionea Xavery,kundi lake pamoja na Kahaba Yuan Liang,walishindwa kufikia makubaliano,Yuan Liang alikataa kujiunga nao,wakaanza kumtisha kifo,na yeye akawa mkali,hakuogopa mtu yoyote chini ya jua,aliahidi kuwaua kabla yeye hajafa kama wakijaribu kumshambulia,ghafla simu yake ikaita,akaipokea,kisha akaiweka sikioni.Ndipo alipokuwa mkali kama pilipili,mtu aliyempigia alikuwa na hasira naye,kwa kumtumia polisi,tofauti na walivyokubaliana,akakataa pesa zao,akakataa kuwarudishia diski yao,akaahidi kuwaua wote na kuweka siri zote hadharani…



    Kundi  la bilionea Xavery walisikiliza mazungumzo kati ya Yuan Liang pamoja na serikali ya raisi Jonsoni Mtemvu,wivu ukawajaa,tamaa ya pesa ikawaingia,wakawa na shauku kubwa ya kuungana na Yuan Liang,ili baadae wamgeuke,pesa wakizipata ziwe zao,akikataa wamteke,kisha awaambie mahali diski ilipo,waichukue wao…



    “,Tutakupatia bilioni tano,ungana na sisi binti,unataka matatizo ee?”,



    “,Wee mzee nakuheshimu ujue,nimesema sitaki sitaki,narudia tena sitaki,sitaki kushirikiana na nyinyi……”,



    “,Unaleta jeuri ee?,fungeni milango yote ya chumba cha siri,mkamateni hakikisheni hatoki ndani…!”,



    Milango yote ya chumba cha siri,milango ya umeme ikafungwa,vijana wa bilionea Xavery,vijana takribani arobaini wakamzunguka Yuan Liang,vijana wawili walikuwa wazungu, mmoja mjapani na wote waliobakia walikuwa Waafrika weusi, wenye miili iliyoshiba ipasavyo.



    Yuan Liang alijiweka sawa kwa mapambano, aliingiza mkono kwenye mkanda wake, akachomoa kisu kimoja, akakishika kikamilifu, akavua miwani yake, alitaka isivunjike, akaiweka kwenye mfuko wa koti lake, akakunja ngumi, miguu yake ilijikunja kama inge, alijiandaa kwa mapigano, yoyote atakaye msogelea amtie adabu …



    …………………………………



    “,Haloo, haloo bosi, mambo yameharibika,mwizi wa diski kashambuliwa na polisi, anasema sisi ndio tumewatuma hao polisi, kwahiyo ameahidi kutuua muda wowote, harafu kila kitu atakiweka wazi kwa wananchi!! “,



    “,Unasema? “,



    “,Ndiyo bosi, niko hotelini nimelala tu, nimeshindwa nifanye nini, kesho narudi, tutazungumza vizuri! “,



    “,Ok, ok, nitaj……”,



    Mheshimiwa Jonsoni Mtemvu alipigiwa simu na rafiki yake, aliipokea haraka sana, aweze kujua nini kilikua kinaendelea, alichanganyikiwa, kazi ya kurudisha diski yake katika mikono yake ilizidi kuwa ngumu, alijuta kwanini alitaka kuchepuka na kuangukia katika mikono ya kahaba Yuan Liang, alijuta kwanini aliwaleta the super three sordiers nchini kwake kufanya upelelezi wa kesi yake …



    “,What!, hawa wanataka nini tena, sina pesa za kuwalipa kwa sasa, nina mambo mengii ……”,



    “,Haloo bosi! “,

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “,Haloo vijana! “,



    “,Polee na matatizo, naskia diski yako imeibiwa, ina siri zote zako, mbaya na nzuri! “,



    “,Ndio vijana, lakini sina pesa za kuwalipa! “,



    “,Usjali, wewe ni mwenzetu, tumefanya biashara ya silaha na madawa ya kulevya muda mrefu,sina haja na pesa ndugu yangu, kesho natuma vijana, watatoka msituni katika maficho yetu, watakuja kukusaidia, diski itakuwa mikononi mwako! “,



    “,Nitashukuru sana,sasa hivi ananitishia mpaka kifo,kama vita na iwe vita,poteleaa mbalii……”,



    “,Sawa kabisa,itabidi afe huyo mwanaharamu,hawezi kukudhalirisha kiasi hiki…”,



    “,kweli kabisa,ok,kwaheri bosi!”,



    “,sawa,sawa,kazi njema!”,



    Kikundi cha kigaidi cha M27,kikundi cha magaidi 27,magaidi waliouziwa silaha za serikali na mheshimiwa Jonsoni Mtemvu walisikia tetesi za mteja wao kujeruhiwa na kuibiwa diski yake muhimu,wakampigia simu,wakaahidi kumsaidia,akafurahi sana,hakutegemea msaada huo,aliwaamini sana magaidi hawa kwa umakini katika kazi,hawajawahi kumuangusha hata siku moja,mheshimiwa Jonsoni Mtemvu akatabasamu,akaketi kitandani,akaanza kufanya mazoezi ya shingo yake,akageuka huku,akageuka kule,moyo wake ulipata matumaini mapya kwa mara nyingine…



    Casablanca hoteli;



          Yuan Liang alizungusha macho yake kila kona,akitafuta upenyo wa kupita, haukuwepo, vijana arobaini wa bilionea Xavery walimzunguka ipasavyo, hakukuwa na uwazi wowote kumruhusu hata panya kupita.



    “,Mkamateni! tukimpata tutapata pesa nyingi, amekataa kujiunga na sisi, sawa!, lakini inasemekana ana diski, mkamateni atwambie diski ya serikali ameificha wapi?,tukiipata mambo yatakua yamenyooka”,bilionea Xavery aliongea.



    Vijana wake wakapata nguvu, mioyo yao ikajaa shauku ya kupata pesa nyingi, mikononi mwao walishika mapanga, visu na wengine nyundo ndogo, wakamvamia Yuan Liang wote kwa pamoja …



    “,Kwachaaa! “,



    “,Yalaaa …”,



    “,Kwachaaa …”,



    “,Uwiiiii …”,



    “,Kwacha, kwachaaa …”,



    “,Msimuogope, mvamieni nyote, shambulia! mwanamke mmoja tu ndiyo anawashinda, shambulia washenzi msipomkamata na nyie mnakufa! “,



    “,Kwachaaa! “,



    “,Yalaaa, uwiiii! “,



    “,Kwachaaa, kwachaa! “,



    “,Puuu, puuu “,



    Vijana wa kundi la Casabranka gang, walimavia Yuan Liang, bila kutegemea, aliruka serekasi, akawapiga mateke yaliyovunja shingo zao,wakalia kwa uchungu,wakamvamia tena, huku wengine wakigaa gaa chini, wakampiga na panga zao akakwepa, wakampiga tena, akakwepa, akaruka serekasi na kutua upande wa pili,wakamfuata, wakarusha mateke yao akakwepa, wakarusha tena, akadaka mguu wa mmoja wao, akaupiga na kifuti, mguu ukavunjika,jambazi la kiafrika lenye kiduku kichwani likapiga kelele za uchungu, dakika kumi tu, vijana takribani kumi na tano, vijana wa bilionea Xavery walikuwa wamelala chini wakiugulia maumivu. Bilionea Xavery akafoka, akawahimiza vijana wake waendelee kumshambulia Yuan Liang,huku wengi wao wakisogea nyuma, Yuan Liang akaingiza mfukoni mikono yake, akatoa gloves,gloves zake hatari zenye misumali midogomidogo, akazivaa,kijana wa kijapani akiwa ameshika panga lake, akamsogelea Yuan Liang, Yuan Liang akaruka mateke mawili, yote yakapanguliwa, akaruka serekasi ya kinyume nyume, kisha akarudi na mateke manne mfululizo, matatu yakapanguliwa, moja likampata shingoni, kisigino cha kiatu chake kirefu kikamjeruhi,akaangukia upande wa pili kama mzigo, shingo yake ikivuja damu, vijana wote wakamvamia tena Yuan Liang, hapo ndipo walijuta kuzaliwa, walipigwa gwala, mateke, ngumi nyingi mfululizo, mapigo ya karate za kichina,wote wakadondoka chini, vijana wawili wa kizungu licha ya kupigwa mateke vifuani na kudondoka chini, walisimama tena, hawakukubali kushindwa, wakatupa visu vyao, wakakunja ngumi …



    “,Nawaomba mniache niende, nitawafanya kitu kibaya, sitaki kuua mtu siku ya leo ……!”,Yuan Liang aliongea, huku jicho lake la kushoto likimtazama bilionea Xavery, jicho lake la kulia likiwatazama vijana wawili wa Kizungu, vijana ambao walikuwa wamesimama kizembe, huku wakipepesuka, Yuan Liang licha ya kuwapiga na mateke vifuani, alikuwa ameshawategua miguu yao ya kulia …



    “,Hutoki humu ndani malaya weee! “,



    “,You call me malaya eee!, mnanijua maskini wa kizungu nyie! “,



    “,Yes, wewe malaya!,your finished, we are going to kill you now,fuck you son of bitch…! “,



    Majambazi mawili ya kizungu yalijitamba, yalimtukana Yuan Liang matusi ya nguoni, matusi ambayo Yuan Liang aliyachukia siku zote,siku zote waliomtukana na kumwita malaya waliambulia kichapo kikali, sura ya Yuan Liang ilikuwa imekunjamana kwa hasira,akajitayalisha kutoa pigo kali la kuua mtu, wazungu wale wakamvamia, wakaruka mateke mawili angani,akapangua mateke yote, wakaruka tena, alikuwa anawasoma staili zao za mapigano, akapangua tena mateke yao…



    “,Tayali nimeshaweka mapigo yao kichwani, wakijiroga wakaruka tena mateke, wamekwisha!”,



    Yuan Liang aliongea peke yake moyoni mwake, bila kutambua fikra za Yuan Liang, wazungu wale wakaruka tena mateke, Yuan Liang akakwepa kwa kuinama chini kidogo  ,kabla hawajatua chini, wakiwa bado hewani, akadaka miguu yao, akawagonganisha,wakapigana vikumbo, wakadondoka chini kama mizigo wakiugulia maumivu, akaruka serekasi, akatua kwenye matumbo yao, akachomoa visu viwili hatari, kutoka kwenye mkanda wake, akawachoma kwenye macho yao, macho yao yakatoboka, yakatokeza kwa nje, wakafa palepale, kifo cha kikatili …



    “,Mnaniita malaya, hata huko kuzimu mlikoenda, msisuthubutu kuniita Malaya, nitawafuata huko huko, haya na wewe bosi wao!!, bado hutaki kuniacha nikaenda zangu ……”,



    “,Hapa…ana, sita…ki tena kuku…kamata, wewe ne…nda tu, nen…da kw…a ama…ni.. ……”,



    Bilionea Xavery aliongea kwa kigugumizi,hakufahamu Yuan Liang kama alikuwa mtu hatari kiasi kile, akamruhusu kwa shingo upande, akipiga mahesabu yake kichwani, bila kutambua kuwa Yuan Liang alikuwa na uwezo wa kufikiria fikra za mtu, kama akimtazama macho yake …



    Yuan Liang akaanza kuondoka, baada ya kufika umbali wa mita tano, bilionea Xavery akanyanyua bastola yake,akajiandaa kumshambulia kwa risasi kahaba Yuan Liang,alipotaka tu kuvuta taiga ya bastola yake, Yuan Liang alichomoa kisu chake, akaruka serekasi na kurusha kisu hewani, kisu kikatua kwenye mkono wa bilionea Xavery, kikafyeka vidole vyake vinne, damu zikamwagika kama maji, bastola yake ikadondokea kule, akapiga kelele za uchungu na maumivu.



    “,Siku nyingine ukisamehewa uwe na adabu, jinga kabisa wewe! “,Yuan Liang alitukana,akaondoka zake, akafika kwenye mlango wa chumba hiki cha siri, chumba kilichojengwa chini ya ardhi katika hoteli ya Casablanka, “,Shiit! milango ni ya chuma, tena imefungwa kwa umeme! anyway! hakijaharibika kitu,”Yuan Liang aliongea, akachukua kisu chake kimoja, kisu aina ya magic knife, kisu cha maajabu, visu vilivyojipatia umaarufu vita ya pili ya dunia kwa umahili wake, akaanza kukata chuma cha mlango, akatengeneza duara dogo lililomuwezesha kupita, dakika kumi tu alimaliza, akatoka nje na kutoweka, kurudi katika hoteli yake, hoteli ya hadhi ya chini, katika mji mdogo wa Mexic, kilimita tano kutoka mji wa Huwei.



    ……………………………… …







    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog