Search This Blog

Friday 28 October 2022

JINI MWEUPE - 2

 









    Simulizi : Jini Mweupe

    Sehemu Ya Pili (2)





    Ofisi ya ukombozi; 9:20pm



    Kamanda Catherine alipaki gari lake dogo aina ya escudo, akatoka, akalisogelea jengo la China plaza, huku akiwa makini. “,Niangalizie gari langu, baada ya dakika kumi nitarejea, “alichomoa shilingi elfu kumi, akampatia mlinzi wa kimasai,kisha akausogelea mlango wa jengo la China plaza, akaufungua, akaanza kupandisha ngazi kuelekea juu.



    “,Paaaaa! “,mlio ulisikika, akapepesuka huku na kule, akaanguka chini kama mzigo.



    “,Samahani sana dada, samahani …”,raia aliyeonekana kuwa wa kigeni alimuomba samahani Catherine, wote walikuwa wameanguka chini baada ya kugongana, kijana yule alinyanyuka harakaharaka, akatoka nje.



    “,Muwe makini mkiwa mnashuka ngazi, nisingekuwa mstaarabu tungetwangana makonde sasa hivi, fyuuu ……”,kamanda Catherine alisonya,akajipangusa vumbi, kisha akaendelea na hamsini zake.



    …………………………………



    “,Someone tried to unlock the door “,(kuna mtu alijaribu kufungua mlango) “,kamanda Catherine alijaribu kufungua mlango, akaingiza neno siri ikagoma, akaingiza tena ikagoma, ilikua imeshavurugwa, akabonyeza batani nyekundu iliyoandikwa “RESET KEY “,baada ya kubonyeza akaingiza neno siri ikakubali,maandishi mekundu yakaonekana kwenye mlango uliyotengezwa kwa teknolojia ya hali ya juu …



    “,Nani alijaribu kufungua mlango? “,kamanda Catherine aliongea, akasubili kidogo, ujumbe ukarudi kwa mara nyingine kwenye kifaa kidogo karibu na mlango, kifaa cha kuingizia neno siri ili mlango kufunguka.



    “,Someone tried to unlock your door “,(Kuna mtu alijaribu kufungua mlango wako …)”,ujumbe ulisomeka, picha ya muhusika ikaonekana, sura haikua ngeni katika macho yake, akajishika kichwa, akaitafakari, akaikumbuka,hakuwa na haja ya kuingia ndani ya ofisi tena, alifunga  mlango kwa mara nyingine tena,akashuka ngazi harakahara kwa kasi ya ajabu …



    dakika kumi baadae, tayali alikuwa nje ya jengo la China plaza,aka angaza barabara ya Karume hakuona mtu zaidi ya walinzi pamoja na watu waliokuwa wamejifunika mashuka na kulala kandokando ya magorofa.



    “,Samahani mlinzi, kuna kaka mweupe,ana sura ya kisomali, kichwani kafuga rasta,kaelekea wapi? “,kamanda Catherine aliongea, huku akitoa noti mbili za elfu kumi kumi akampatia mlinzi yule wa kimasai, kama ujuavyo mjini kuuliza pesa, usipotoa pesa basi utapotezwa.



    “,Alikuja na gari dakika kumi kabla ya wewe hujafika, akapanda juu ghorofani, lakini wewe ulipoingia tu, nilishangaa akitoka nje akihema kwa kasi, akapanda gari, akatoweka,bila shaka wame elekea mitaa ya mabibo…”,mlinzi yule aliongea.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kamanda Catherine akaisogelea gari lake,alipotaka kuingia,akashtuka!,akatazama kwa makini gari lake,lilikuwa limetolewa upepo,akakasirika,akamsogelea mlinzi wa kimasai aliyemuachia gari alinde…



    Akachomoa bastola,akamuwekea kichwani,”Niambie,nani katoa upepo kwenye gari langu,nazani unajua kila kitu,nambie kabla sijasambaratisha ubongo wako!”,kamanda Catherine alifoka.



    “,Nisamehe,nitasema,usiniue,nipesa tu mwanangu ndio zimesababisha nishindwe kulinda gari yako kikamilifu.”,mzee yule wa kimasai alilia,kelele zilizowaamsha raia waliokuwa wamelala nje,wengine walitimua mbio baada ya kuona silaha,walizani ni majambazi.



    “,Acha siasa mzee,sema kabla sijatoa uhai wako”,kamanda Catherine aliendelea kuchimba mkwala.



    “,Walinipatia laki moja,niwaruhusu watoe upepo kwenye gari lako,nikawaruhusu,pia waliniambia ukiniuliza nikudanganye,hawajaelekea mabibo,wameelekea makao makuu ya jeshi la polisi,kuna mfungwa wao!”,mzee yule alinyosha maelezo,kamanda Catherine akafurahia ukweli wa mzee yule,aliona shida nyingi katika macho ya mzee yule,akamuonea huruma,akafungua pochi yake,akampatia laki mbili taslimu,pesa halali za Kitanzania,mzee akashukuru.



    “,Siku nyingine kuwa mwaminifu,”Kamanda Catherine aliongea,akasogelea kando ya barabara,akaita bodaboda,hakuna aliyeweza kumsogelea,wote walimwogopa,wengi walishuhudia alipokuwa anamchimba mkwala kwa kutumia bastola mzee yule,waliogopa kumsogelea,wengine walihama vituo vyao vya maegesho…



    “,Nikupeleke wapi kamanda,”bodaboda mmoja aliongea,huku akiisogeza pikipiki yake karibu na kamanda Catherine Obadia,bodaboda huyu hakuwa muoga kama wenzake.



    “,Nipeleke makao makuu ya polisi,”kamanda Catherine aliongea.



    “,Makao makuu ya mbezi au Temeke?”,bodaboda yule aliongea.



    “,Temeke,endesha haraka sana,usiogope trafiki yoyote yule…”,kamanda Catherine aliongea,kichwani akitafakari watu waliokuwa wakimnyemelea muda mfupi uliopita…



    “,Hawa ni D47,hakuna wengine,hawatuwezi,lazima tuwatie nguvuni…”,aliongea kwa sauti.



    “,Kamanda kuna shida?”,bodaboda aliuliza,baada ya kusikia Catherine akiongea peke yake kama mwendawazimu.



    “,Aaaah,hakuna shida usjali,endelea kukanyaga mafuta…”,Catherine aliongea,huku akijishangaa,hakuwa anatambua kama aliongea kwa sauti ikiyosikika kwa mtu asiyestahili,mawazo yake yalikuwa mbali sana.



    …………………………………



    Gano;



            Donald Mbeto akiwa amepanda spidi boti,alivua sura yake ya bandia, sura ya kike,akavua sura ya bandia,akanywa maji kwa wingi,sauti ikaanza kurudi taratibu,huku safari ya kuelekea katikati ya bahari,kilomita kumi kutoka ufukwe wa nchi ya Gano ikiendelea…







    Baada ya kutembea takribani kilomita sita,machale yalianza kuwacheza,maji yalikuwa yamechafuka yakiwa yamebadirika rangi na kuwa meusi,wakapunguza mwendo wa boti yao,wakaisogeza taratibu eneo la tukio.



    “,Shit,wameshambuliwa,wameripuliwa!”,Donald Mbeto aliongea,akiwa amechukia,akachukua simu yake,akabonyeza namba kadhaa,akapiga,simu ikaita,simu ikaita tena,kisha ikapokelewa.



    “,Haloo,Donald Kazi inaendeleaje?”,upande wa pili wa simu ulisikika.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    “,Kazi imekwisha,lakini nimerudi nimekuta Nyambizi imeripuliwa…”,Donald Mbeto aliongea.



    .



    “,Yap,imeshambuliwa na askari wa Tanzania,wamemkamata D47 namba sabini,kapelekwa Tanzania,tumeshawapatia maelekezo aweze kuuawa haraka sana kabla hajatoa siri za kutuangamiza…”,upande wa pili wa simu ulizungumza.



    “,Hapo sawa,sasa sisi tunarudije?niko na D47 namba kumi,hawezi kurudi Gano lazima atatiwa nguvuni kwa mikasa hii,hali haijatulia huko……”,Donald Mbeto aliongea.



    “Sogeeni mpaka kilomita ishirini mbele,rada zisiweze kuisoma kwa urahisi helikopta yetu,inakuja kuwachukua”,upande wa pili wa simu uliongea.



    “,Sawa bosi,”Donald Mbeto aliongea,akakata simu.



    …………………………………



    Makao makuu;.



              Helikopta ya jeshi la Tanzania ilitua katika uwanja wa jeshi la upelelezi na kupambana na ugaidi nchini Tanzania. Askari walipanga foleni, huku silaha zao zikiwa begani, walisimama wima, hawakutikisika.



    Kamanda Kendrick, akiwa na nyota tatu begani,pamoja na mwenzake kamanda Philipo walishuka ndani ya helikopta, wakapigiwa saluti, risasi tatu za heshima kulingana na idadi ya nyota zao zikapigwa hewani, walipokelewa kwa heshima kubwa, kwani wali iwakilisha vema nchi katika medani ya Kimataifa.



    “,Kamanda Catherine yuko wapi?, mtuhumiwa wa ugaidi aliyekamatwa yuko mahali gani? “,kamanda Kendrick aliongea baada ya kusogelea ofisi za jeshi.



    “,Ameelekea katika ofisi yenu, ofisi ya ukombozi saa moja iliyopita ,mtuhumiwa yuko mahabusu, mnaweza kwenda kumuona! “,



    Kabla hata hawajapumzika na kupeleka mabegi yao nyumbani kwao, walianza kazi usiku huu, hali ya nchi haikua shwari, huku mabegi yao yakipelekwa na askari wadogo wenye vyeo vya chini.



    “,Huyo hapo amefika, mmh mbona anakuja anakimbia? “,kabla hata mazungumzo hayajaendelea zaidi, askari wa zamu aliongea, wote wakageuka, walimshangaa kamanda Catherine.



    “,Ulinzi uimarishwe mahali hapa, bora mmefika, askari yoyote yule asiende kulala ,nimetoka ofisi ya ukombozi nimekoswa kifo, kundi la mtuhumiwa wa ugaidi wanatutafuta watuue, wanamtafuta pia mtuhumiwa wamuue, tunapaswa kumuhoji, inaonekana anafahamu mambo mengi zaidi. “,kamanda Catherine aliongea, akaeleweka, askari walinzi wakachukua bunduki zao na kukaa lindoni, huku the super three soldiers wakielekea mahabusu kumuhoji mtuhumiwa, kwa upande wa masaa, ilikuwa takribani saa saba usiku.



    …………………………………http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Mahabusu.;



         Hawakuamini walichokiona,walimgusa kidogo mtuhumiwa alipokuwa ameketi na kuegemea ukuta, akadondoka chini,povu lilikuwa linatoka mdomoni kwa wingi, alikufa muda mrefu uliopita..



    “,Nani kauwa? bila shaka amekufa kwa sumu, aliyeleta chakula au maji kwa mtuhumiwa akamatwe, atatueleza ukweli “,Kamanda Kendrick aliongea, alikuwa sahihi, wote wakakubaliana naye, wakatoka katika chumba cha mtuhumiwa wa ugaidi, huku vichwa vyao vikijiuliza maswali mengi bila majibu.



    Bahari ya hindi; masaa matano yaliyopita …



            Harakati ziliendelea makao makuu ya kundi la kigaidi D47,katikati ya bahari. Baadhi ya askari walifanya kazi ya kupakia madawa , kupakia silaha kwenye maboksi, makundi mengine yaliendelea na mazoezi, huku chumba cha mawasiliano kikiendelea kuifuatilia nyambizi yao iliyokuwa safarini kumpeleka Donald Mbeto nchini Gano, kisha imrudishe tena baada ya kazi kukamilika.



    “,bosi! “!,



    “,nambie kijana, kuna tatizo? “,



    “,ndio bosi “



    “,tatizo gani? “,



    “,nyambizi yetu imetekwa kama unavyo ona,kisha imeripuliwa,wote wamekufa isipokuwa D47 namba sabini,amekamatwa sijui kapelekwa wapi!”,



    “,unasemaje?kwahyo hata Donald amekufa?”,



    “,hapana,yeye bado yuko kazini nchini Gano,walikuwa bado  wanamsubili akamilishe kazi warudi naye…”,



    “,ok,sasa angalia kwa kutumia kompyuta yako,tujue ni jeshi gani limemkamata mtu wetu,”



    “,sawa bosi.”,



    Yalikuwa ni mazungumzo kati ya kiongozi wa kundi la kigaidi la D47,bwana Paresh Kumar,pamoja na mtaalamu wake aliyehusika na idara ya mawasiliano na teknolojia,Paresh Kumar alipomaliza kumpatia maelekezo,mtaalamu wake akaendelea kuchezea kompyuta yake,baada ya dakika mbili akamgeukia tena.



    “,bosi!”,



    “,yes Benard,nambie”,



    “,jeshi la Tanzania ndio limemkamata…”,



    “,ok sawa,ngoja niwajulishe wenzetu wa Tanzania wamuokoe,ikishindikana wamuue…”,



    “,ameshatoa siri zetu,haina haja ya kubakia mzima…”,



    “,oooh,kumbe katoa siri zetu,basi ngoja wamuue…”,



    Paresh Kumar alimaliza kuzungumza na mtaalamu wake wa teknolojia aliyeitwa Benard,akachomoa simu yake,akabonyeza namba kadhaa,akaweka simu sikioni,simu ikaita,sekunde mbili tu ikapokelewa.



    “,haloo D47 namba sitini,Dar es salaam.,Tanzania,



    “,nambie mkuu,kuna jipya?”,



    “,ndiyo,mwenzetu,D47 namba sabini kakamatwa ,ameletwa Tanzania,hakikisha halioni jua la kesho,”



    “,sawa bosi,saa moja tu linatosha,atakua amekata kamba…”,



    “,ok,ok,pesa za kazi nawaingizia benki…”,



    “,ok mkuu…”,



    Mazungumzo kati ya Paresh Kumar,bilionea katili wa kihindi,mmiliki wa kundi la kigaidi la D47 pamoja na kijana wake kutoka Tanzania yalimalizika,akakata simu,akarudisha simu yake mfukoni,sekunde mbili tu,simu ikaita tena,akaichukua katika mfuko wake wa suruali,akaitazama,Donald Mbeto alikuwa amepiga,wote waliokuwa karibu naye wakatazamana,walitaka kujua nini kinaendelea,akapokea simu harakaharaka,akaiweka sikioni.



    “,Haloo Donald, kazi inaendeleaje? “,Paresh Kumar aliuliza swali baada Ya kupokea simu ya Donald Mbeto, akajibiwa swali alilouliza.



    “,Yap, imeshambuliwa na askari wa Tanzania, wamemkamata D47 namba sabini, kapelekwa Tanzania, tumeshawapatia maelekezo aweze kuuawa haraka sana kabla hajatoa siri za kutuangamiza …”,Paresh Kumar aliendelea kukuongea na Donald Mbeto kwa kutumia simu, kisha akakaa kimya, alikua akisikiliza maelezo kutoka kwa kijana wake mtata Donald Mbeto.



    “,Sogeeni mpaka kilomita ishirini mbele, rada zisiweze kuisoma kwa urahisi helikopta yetu, inakuja kuwachukua …”,Paresh Kumar aliongea, kisha akakata simu.



    “,Chukueni helikopta, seahawk, nendeni mkamchukue Donald Mbeto na mwenzake, kuweni makini …”,Paresh Kumar alitoa maelekezo kwa vijana wake, wakatoweka mbele yake, akabaki peke yake akiwa na Benard, katika chumba cha mawasiliano ,makao makuu ya kundi lake, katikati ya bahari ya hindi.



    …………………………………



    Dar es salaam;



         “,Wawili waende makao makuu ya polisi, wengine waende Kariakoo kwenye ofisi ya hawa washenzi, lazima tutajua chochote kuhusu mahali alipo mwenzetu “D47 namba sitini aliongea.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “,Sawa bosi, tuondoke “,wenzake wakaitikia, kisha wakasambaratika, wakaondoka katika makazi yao yaliyoko kimara, ndani ya jengo la kifahari, lisilo na panya wala mende ndani yake.



    …………………………………



    Temeke; Makao makuu



             Kundi la kwanza lilipaki gari lao karibu kabisa na kituo cha polisi, makao makuu ya askari wapelelezi nchini Tanzania.Mmoja akabaki ndani ya gari, mwingine akatoka,akaangaza huku na kule hakuona kitu, akaanza kutembea kusogelea ofisi za jeshi, uso kwa uso akakutana na mtu aliyemkusudia, askari mamluki.Siku zote alichukua taarifa za serikali na kuwapatia magaidi,ili kujipatia donge nono na kukidhi njaa zake.



    “,Mwenzetu amekamatwa,hatujui kapelekwa mahali gani, sijui unaweza kutusaidia …”,



    “,yupo mahali hapa, kaletwa muda sio mrefu, kuwasaidia naweza lakini nyinyi hamuwezi kwenda, ulinzi ni mkali mno”,



    “,basi tufanyie kazi, sumu hii hapa…”,



    “,Sawa, lakini na mimi mnifikiliee, “



    “,Aaaah bwanaa, wewe tena, kesho asubuhi benki akaunti yako itajaa pesa …”,



    “,Sawa ndugu,kazi njema, mimi naondoka …”,



    D47 namba sitini aliagana na askari wa zamu,wakapeana sumu kwa siri, hakuna aliyewaona, kisha kila mtu akachukua hamsini zake, askari wa zamu akarudi kituoni, gaidi akatoka eneo la kituo cha polisi, akavuka barabara, akapanda gari lao, wakaondoka zao …



    ………………… ………………



    Kariakoo;



        Gari ya kifahari aina ya BMW ilipaki pembeni mwa barabara ya Karume, nje ya jengo la China plaza. Gaidi mwenye sura ya kisomali, rasta ndefu kichwani mwake, alishuka ndani ya gari, alionekana kuwa na haraka sana, akaingia ndani ya jengo, akapanda juu harakaharaka, ndani ya dakika kumi, alifika ghorofa ya tano, nje ya ofisi ya Ukombozi, ofisi ya kundi la wapelelezi wa Tanzania, maarufu kama the super three soldiers.



    Gaidi D47 namba ishirini, akaanza kufungua mlango kwa kutumia utundu wake, aliingiza neno siri katika mlango ukagoma kufunguka, akakadilia tena, akaingiza ukagoma, akatafakari, akaingiza tena mlango ukagoma kufunguka, ghafla simu yake ikaanza kuita, akaichukua, alikuwa ni mkuu wake wa kazi, akaipokea.



    “,Njooni kambini haraka, kazi tayali imekamilika, “sauti ilisikika upande wa pili wa simu, akakata simu, akairudisha mfukoni, akaanza kushuka ghorofani bila kutambua tayali alipigwa picha naa kifaa cha kuingizia neno siri mlangoni, baada ya kukosea neno siri mara tatu mfululizo.



    “,puuuu, “kishindo kilisikika, walipamiana na mwanamke ambaye alimtambua vizuri sana,alitwa kamanda Catherine, alimanusura amkute ndani ya ofisi yake, wakatupiana maneno, akasimama na kutoweka zake, akafika nje, akampatia maelezo kazaa mlinzi, akampatia pesa, akatoa upepo wa gari, kisha akarudi makao makuu ya kundi lao nchini Tanzania.Huku wakimdanganya mlinzi kuwa akiulizwa aseme walielekea Mabibo au makao makuu ya polisi.



    …………………………………



    Makao makuu ya polisi;



          Askari wa zamu alichukua chakula kama kawaida yake,kuwapatia mahabusu chakula, akaweka sumu kwenye chakula cha mfungwa wa ugaidi,kisha akamuita askari ambaye alikuwa lindo, bila shaka alimzidi cheo.



    “,vipi Afande, kuna tatizo? “,



    “,nina kazi nyingi, nisaidie kuwapa hao mbwa watatu chakula, tayali nimeonja hakina shida …”,



    “,sawa afande …”,



    Afande aliitikia kwa mbwembwe, bila kujua kuwa tayali aliuziwa kesi, akachukua chakula kimoja baada ya kingine, akawepelekea mahabusu, akiwemo gaidi D47,mshatakiwa wa kesi ya ugaidi anayetafutwa kuuawa kwa udi na uvumba.



    …………………………………



    Gano; 8;20am



            Hospitali ya jiji la Gano ilikuwa imejaa watu kama kawaida, wagonjwa, madaktari pamoja na watu mbalimbali hospitalini walijaa na taharuki kubwa, wengine walijadiri kuhusu mripuko wa gari uliotokea usiku uliopita bandarini, wengine wakijadirinana kuhusu karatasi iliyokutwa imebandikwa katika vyoo vya kike hospitalini, ikiwa na maneno yaliyojaa utata,maandishi yaliyoandikwa kwa wino wa damu, neno JINI MWEUPE.



    “,naitwa Efreza, mwandishi wa Gano tv,unalizungumziaje swala la karatasi hii iliyobandikwa hospitalini…?”,



    “,hii karatasi ilibandikwa mwaka 2008 mahali hapa, baada ya muda vifo vingi vikatokea hospitalini, mwaka 2016,karatasi yenye neno hili ilibandikwa katika hospitali ya taifa la Tanzania, baada ya masaa kadhaa, watu wakafa kama nzige hospitalini, mpaka leo mtuhumiwa anatafutwa bila mafanikio ,kwahiyo naiomba serikali ifanye uchunguzi bila hivyo tutakufaa……”,



    “,Aaaaa, achaa uongo bwana, mbona hatujawahi kusikia, hahaaa ……”,



    Watu walimcheka mwanaume mwenye mavazi yaliyolaruka na kujaa viraka, hawakutafakari maneno yake aliyozungumza wakati wa kuhojiwa, siku zote maskini hawana sauti na maneno yao hupuuziwa, baada ya kumaliza kuhojiwa, aliondoka zake, mwandishi wa habari akaendelea kuhoji watu wengine, nusu saa baadae vifo vikaanza kutokea hospitalini, idadi ya vifo ikaongezeka kila baada ya nusu saa, hawakujua chanzo ni nini, madaktari walikimbia huku na kule, waandishi wa habari wakaanza kujaa hospitalini, polisi wakazagaa kila kona ya hospitali, haikusaidia chochote kile, wagonjwa waliendelea kufa, huku miili yao ikifanyiwa uchunguzi ili kujua chanzo cha vifo vyao, maneno ya tahadhari kutoka kwa masikini aliyehojiwa masaa mawili yaliyopita yakawa na mashiko ndani yake.



    Makao makuu ya polisi; masaa sita yaliyopita;



         The super three sordiers, walitoka mahabusu, wakiwa na maswali mengi kichwani, maswali ambayo yalipaswa kujibiwa na askari wa zamu, pamoja na askari wa lindo …



    “,Kamanda wa zamu, mtuhumiwa wa ugaidi amepoteza maisha, bila shaka yoyote amekufa kwa sumu, maana povu jingi linamtoka mdomoni, unaweza kutwambia nani kauwa? “,kamanda Catherine aliuliza,akiwa amesimama sambamba na wenzake, kamanda Philipo pamoja na kamanda Kendrick.



    “,Mtuhumiwa amekufa!, sijui chochote, ndiyo taarifa hii ninaisikia kutoka kwenu “,askari wa zamu alijitetea, alikuwa ameketi kwenye meza yake, karibu kabisa na mlango wa kuingilia kituoni.



    “,Uongo kabisa, uongo huo, wewe ndiye uko hapa mezani, mapokezi, yoyote yule anayeingia kituoni au mahabusu lazima aombe kibali kutoka kwako, wewe kama askari wa zamu, kwanini unasema hujui?, “kama Kendrick aliuliza.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “,Mambo mengi bosi, muda mwingine nitatoka kwenda toileti,wakati mwingine nakuwa bize napekua mafaili ya kesi mbalimbali kabatini, kwahyo inawezekana walitumia fursa hiyo, wakapenya, wakasababisha mauaji! “,askari wa zamu aliendelea kujitetea.



    “,Ok sawa, sawa kabisa, umejitetea vizuri, lakini ,wewe kama askari wa zamu, unahusika pia na kuwapelekea chakula wagonjwa?, ulionja chakula hicho ?,…”,Kamanda Kendrick aliuliza, askari wa zamu akasita kujibu, akakaa kimya kwa takribani dakika tano, kisha akafungua mdomo wake,bila shaka alitaka kunena jambo.



    “,Nilikuwa bize na kazi?, kamanda Agrey, askari wa zamu kulinda mahabusu, nilimuomba anisaidie kuwapa chakula badala yangu …”,askari wa zamu alijitetea.



    “,What!, wewe unahusika, unahusika na mauaji, tangu lini ukawa bize mpaka ukakosa dakika tano za kuwapatia chakula mahabusu, tena watatu tu?  ,anyway! tuyaache hayo, namuomba kamanda Agrey aje hapa! “,kamanda Catherine aliongea,alikuwa na hasira kupita kiasi, dakika mbili tu kamanda Agrey alifika mbele yao, akapiga saluti …



    “,Nimeitikia wito Afande “,kamanda Agrey aliongea, akiwa amesimama wima kwa heshima, bila kutikisika …



    “,Ulipeleka chakula mahabusu? “,kamanda Catherine aliuliza …



    “,Ndiyo, nilipeleka? “,kamanda Agrey alijibu



    “,Ulionja chakula ?”,Catherine aliuliza tena.



    “,Hapana, askari wa zamu aliniambia kiko salama, alikuwa tayali ameonja …”,alijibu kwa ufasaha.



    “,Unaaminije kama alionja, ulimuona? “,Catherine aliuliza.



    “,Hapana, sikumuona …”,kamanda Agrey alijibu …



    “,Baada ya mahabusu kumaliza kula, nani alitoa vyombo? “,kamanda Catherine aliuliza …



    “,Alitoa askari wa zamu, “Agrey alijibu …



    “,Ulimuona wakati anatoa vyombo, kwanini atoe vyombo,hakua bize kama alivyosema awali? wakati chakula cha Wafungwa kinaliwa kwa dakika tano tu? “,kamanda Catherine aliuliza.



    “,Sijui afande, swali hilo labda umuulize yeye mwenyewe …”,Agrey alijibu.



    “,Unajua sababu ya kukuuliza maswali haya yote? “,Catherine aliongea.



    “,Hapana!, sijui Afande! “,Agrey alijibu.



    “,mshatakiwa wa Ugaidi, aliyeletwa usiku huu amekufa kwa sumu? “,kamanda Catherine aliongea.



    “,Unasemaje?, amekufa! “,kamanda Agrey aliongea,alishangaa sana kwa taarifa aliyopatiwa, hakujua chochote kile kilichokuwa kinaendelea.



    “,Najua haujaua, lakini utawekwa rumande kwa uzembe, naomba uvue mkanda, pamoja na kofia,haiwezekani uwe zamu kulinda mahabusu, harafu mahabusu afe bila wewe kujua chochote kile, that is nonsense! “,kamanda Catherine aliongea kwa hasira,siku zote akiongea, ameongea, habadili msimamo hata siku moja …



    “,Hapana afande,familia inanitegemea, msiniweke rumande pliizi naomba, afande Kendrick, afande Philipo nisaidieni …”,kamanda Agrey alijitetea



    “,Ukikaa rumande kwa wiki moja, i hope next time utakua makini, lakini kwa huyu askari wa zamu, awekwe chumba cha mateso, asulubiwe mpaka aseme nani kauwa? ,maelezo yake yanaonesha anajua kila kitu …”,kamanda Kendrick aliongea, huku askari baadhi wakiitwa, wakawakamata askari wote wawili, kila mmoja akapelekwa katika chumba chake,kadri amri zilivyotolewa na the super three soldiers …



    …………………………………



    Masaa manne yaliyopita; Bahari ya Hindi



             The seahawk, helikopta ya kivita, helikopta ya kutegemewa na kundi la magaidi la D47,ilitua kwa mara nyingine tena, katika meli kubwa inayoitwa D47paraquat, meli yenye uwezo wa kubeba ndege za kivita mia moja, vifalu hamsini,isitoshe ilikuwa na uwezo wa kujigeuza kama nyambizi ikazama chini ya bahari, sifa kubwa kuliko zote, ilikuwa na uwezo wa kupaa angani kama ndege zingine zozote zile …



    “,Karibu sana, welcome my hero! kazi imekwisha, kilichobakia ni kusikia tu vifo kesho asubuhi ……”,



    bosi wa kihindi, mmiliki wa kundi la D47 maarufu kama Paresh Kumar, alimpokea Donald Mbeto kwa heshima, mara baada ya helikopta kurejea, ilipowafuata kilomita therathini ,katikati ya bahari, kutoka kisiwa cha Gano, baada ya Nyambizi aliyokwenda nayo awali kuripuliwa.



    “,Kweli bosi, nimefanikiwa kukamilisha kazi,nitazidi kutikisa dunia, watanitafuta mpaka wanazeeka, hawatanipata!! “,Donald Mbeto alishuka kwenye helikopta, akashikana mikono na bosi wake, huku akiongea maneno ya kejeli kwa mataifa yote duniani yaliyomtafuta kila kukicha.



    “,Hahahaa, “wote wakacheka, meno yote yakaonekana kwa nje, walijawa na furaha, kwa kukamilisha kazi kubwa kwa muda mfupi tu.



    “,Sasa hapo lazima wajute,lazima wajute kwanini walinikataza nisimiliki migodi ya almasi katika nchi zao, nikapoteza pesa nyingi kuhonga viongozi wakubwa katika serikali zao, lazima wajute kula pesa zangu, harafu nikose migodi ya dhahabu, ok kijana wangu, unatorokea Amerika au wapi! “,Paresh Kumar aliongea, akaeleza sababu ya kijana wake kufanya mauaji Tanzania, Ufilipino,Gano pamoja na nchi zingine, huku baadhi ya nchi Donald Mbeto akiwa amefanya mauaji mara mbili mfululizo.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “,Siendi popote pale, wewe ni mama na pia ni baba yangu!! “,Donald Mbeto aliongea, licha ya umri wake wa miaka sitini, umri uliopelekea awe na mnvi nyingi kichwani na kidevuni, mnvi zilizosababisha ajiite Jini Mweupe, sababu ya mwonekano wake,alimuheshimu sana bosi wake, bosi kijana wa kihindi, bilionea Paresh Kumar mwenye umri wa miaka arobaini tu …



    “,Sawa kijana, nafurahi kuskia hivyo, twende ukaburudike …”,bosi Paresh Kumar aliongea, akamchukua Donald Mbeto, wakaelekea katika vyumba vyao vya starehe, vyumba vilivyojaa starehe zote, bila kusahau wanawake wa kila aina, wazungu, waafrika, wachina na wajapan …



    …………………………………







    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog