Search This Blog

Thursday 27 October 2022

MVUVI BRUNO (BRUNO THE FISHERMAN) - 3

 









    Simulizi : Mvuvi Bruno (Bruno The Fisherman)

    Sehemu Ya Tatu (3)





    Bruno na mzee Todd walikuwa wakitembea kwa kasi kuelekea Upande wa Kaskazini, vichwa vyao vilikuwa vikifikiria maisha yao yangekuwaje nchini Afrika Kusini huku yeye, Todd akitafutwa dunia nzima kwa makosa ambayo hakuwahi kuyafanya.

    Kichwa chake kilimfikiria mke wake na mtoto wake, aliwakumbuka, alitamani kuungana nao tena lakini kwa kipindi hicho haikuwezekana kabisa. Ukiachana na yeye, Bruno kichwa chake kilikuwa kikimfikiria mpenzi wake, Sharifa tu.

    Hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea huko, alitamani kurudi haraka nchini Kenya ili kwenda kuonana naye kwa mara nyingine lakini hilo halikuwezekana kabisa. Hakujua ni kwa jinsi gani angeweza kurudi nchini humo na wakati mfukoni mwake hakuwa na pesa yoyote ile.

    Hapo Cape Town walitembea kwa kujificha sana mpaka walipofika katika kituo cha treni za umeme cha Bellstar Junction. Hapo walitaka kupanda treni na kuondoka jijini Cape Town na kuelekea Johannesburg ambapo huko waliamini kwamba wangepata msaada wa kuondoka nchini humo.

    Hawakuwa na pesa mfukoni lakini mzee Todd alikuwa na pesa nyingi katika akaunti yake. Aliogopa kwenda benki na kuchukua pesa kwani sura yake ilikuwa dili kila sehemu na watu walimtafuta kwa nguvu kubwa.

    “Ninataka kuelekea benki kuchukua pesa, ila nahisi nitakamatwa. Unadhani unaweza kwenda kwa ajili yangu?” aliuliza Todd huku akimwangalia Bruno.

    “Kwenda benki?”

    “Ndiyo!”

    “Sawa. Benki gani?” aliuliza.

    “Barclays!”

    “Haina shida.”

    Alichomwambia ni kwamba alitakiwa kwanza kwenda huko kwa lengo la kuchukua karatasi ya kuandikia hundi (cheque) na yeye kuipeleka benki. Hilo halikuwa tatizo, akaelekea benki ambapo huko akakutana na dada mmoja wa Kizulu na kuanza kuongea naye.

    Alizungumza naye huku akionekana kuwa mchangamfu mkubwa, alijua kumteka mtu kupitia mazungumzo yake kiasi kwamba msichana huyo aliyeitwa kwa jina la Susan akabaki akikenuua tu kwani kila neno alilolizungumza Bruno kwake liliukuna moyo wake.

    “Umetoka wapi?” aliuliza Susan, hakuwahi kukutana na mwanaume aliyekuwa akiongea kama Bruno.

    “Kenya!”

    “Ooh! Kumbe Afrika Mashariki. Nawapenda watu wa huko, wanaongea sana, ni wachangamfu mno. Si ndiyo ilipo Tanzania?” aliuliza msichana huyo.

    “Ndiyo!”

    “Ninawapenda sana Afrika Mashariki!”

    Hilo likampa uhakika wa kukamilisha kile alichokitaka. Akamwambia kwamba lengo la kufika mahali hapo lilikuwa ni kuchukua kitabu cha hundi. Hilo halikuwa tatizo, Susan akampa kitabu hicho na Bruno kuondoka mahali hapo.

    Huko alipokwenda, alimfuatan mzee Todd na kumpa kile kitabu. Mzee huyo akakichukua na kuandika kiasi cha dola milioni moja apewe mkononi. Bruno alipokichukua kitabu hicho na kuangalia, hakuamini, alimwangalia vizuri mzee Todd, alihisi kama kiasi kile cha pesa alichoandikiwa kilikuwa ni uongo.

    “Dola milioni moja?”

    “Ndiyo! Hakikisha unakwenda na kufungua akaunti yako. Utazichukua hizi pesa na kuziingiza kwenye akautnti yako, tutakuwa tunazitumia kupitia akaunti yako,” alisema mzee huyo.

    Bruno alichanganyikiwa mno, hakuamini alichokuwa akikisoma kwenye cheki ile. Kiasi kile, kwa pesa za shilingi ya Kenya kilikuwa ni sawa na bilioni moja, milioni mia mbili na senti kadhaa huku kwa shilingi ya Kitanzania ikiwa ni zaidi ya shilingi bilioni mbili.

    Akaondoka mahali hapo na kumuacha mzee huyo akiwa sehemu amekaa kwa kujificha sana. Alipofika, kama kawaida yake akamfuata Susan na kuanza kuongea naye. Kitu cha kwanza alichohitaji kilikuwa ni kufungua akaunti.

    “Una randi elfu ishirini?” aliuliza Susan.

    “Ya nini?”

    “Kufungulia akaunti!”

    “Sina! Ila nitakuwa nazo baada ya kufungua akaunti!”

    “Kivipi?”

    Alichokifanya Bruno ni kumuonyeshea Susan ile hundi aliyokuwa ameandikiwa. Msichana huyo hakuamini, kilikuwa kiasi kikubwa cha pesa ambacho kilitakiwa kuingia mara baada ya kufunguliwa kwa akaunti hiyo.

    Haraka sana Susan akampeleka sehemu ya kupiga picha, akafanya hivyo na kufuata taratibu zote na kiasi hicho cha pesa kumlipia yeye mwenyewe kwani aliamini kwamba angelipwa kwa fadhilla alizokuwa ameonyesha.

    Mchakato ulipokamilika, hundi ile ikachukuliwa na pesa kutolewa katika akaunti ya mzee huyo na kuingizwa katika akauti ya Bruno, akatoa kiasi cha dola elfu ishirini na dola elfu moja na kumpa Susan kisha kuondoka zake.

    Hilo likamfurahisha mzee Todd na kuona kwamba walikuwa wakienda kufanikiwa kile walichokuwa wakikitaka. Wakawa na pesa, walichokifanya ni kukata tiketi na safari ya kuelekea Johannesburg kuanza.

    Njiani, mzee Todd alikuwa na kofia, hakutaka kugundulika na mtu yeyote yule kwani aliamini kwamba dunia nzima ilikuwa ikifahamu kama alikuwa akitafutwa. Treni hiyo ilichukua saa moja mpaka kufika katika Jiji la Johannesburg ambapo wakateremka na kufikiria kwenda kupumzika hotelini.

    Kitu walichokifanya ni kununua simu. Kila mmoja akanunua yake pamoja na laini ambazo zilisajiliwa kwa jina la Bruno. Kila kitu kilipokamilika, kwa kuwa namba ya mke wake aliifahamu, akaanza kumpigia.

    Simu haikuita muda mrefu ikapokelewa na mkewe. Sauti yake haikuwa ya kawaida, alikuwa akizungumza huku akilia. Alihitaji msaada kwani pale alipokuwa hakukuonekana kuwa salama kabisa.

    Wakati akizungumza naye, mara simu akapokonywa na sauti ya mwanaume kusikika kutoka upande wa pili. Iliongea kibabe, sauti ambayo haikuonekana kuwa na mchezo hata kidogo.

    “Tunakuhitaji ndani ya saa arobaini na nane. Mbali na hilo, utaziona maiti za familia yako ufukweni. Una saa arobaini na nane kujisalimisha kwetu,” alisema mwanaume huyo kwa sauti yenye utetemeshi.

    “Wewe nani?”

    “Si lazima unifahamu. Fanya kama nilivyokwambia,” alisema mwanaume huyo na kukata simu.

    Mzee Todd akabaki akitetemeka, hakujua mwanaume huyo aliyekuwa akizungumza upande wa pili alikuwa nani. Akachoka, akatulia kwenye kiti huku akitetemeka kupita kawaida.

    Hakujua ni kitu gani alitakiwa kufanya. Maneno aliyozungumza mwanaume huyo yalionyesha kabisa kwamba familia yake haikuwa salama huko ilipokuwa.

    “Halo...halo...” aliita lakini hakukuwa na sauti iliyosikika upande wa pili.

    Bruno alibaki akimwangalia mzee huyo, alikuwa akilia, machozi yalitiririka mashavuni mwake. Alionekana kuumizwa na kile kilichokuwa kimetokea. Aliipenda familia yake na mara kadhaa alikuwa akiizungumzia kwamba aliikumbuka na alitamani sana kuonana nayo.

    Akamuuliza kilichokuwa kimetokea, akamwambia kwamba familia yake ilitekwa na mtu asiyemfahamu na alimuhitaji ndani ya saa arobaini na nane kitu ambacho kilikuwa ni vigumu kufanyika.

    “Kwa hiyo?” aliuliza Bruno kwa sauti ya upole.

    “Sijajua ni kitu gani kinatakiwa kufanyika. Familia yangu itauawa! Familia yangu itauawa!” alisema mzee Todd huku akilia kama mtoto.

    ***

    Hakukuwa na mtu aliyekuwa muhumu kwa kipindi hicho kama mzee Todd. Maofisa wa CIA walikuwa wakimtafuta kila kona, walimtaka mzee huyo kwa udi na uvumba.

    Walihangaika kila kona kumtafuta lakini hawakujua mahali alipokuwa. Wakati mwingine waliambiwa kwamba alikuwa nchini Msumbiji, walisafiri na kwenda huko lakini hawakufanikiwa kumpata.

    Mzee huyo aliwasumbua kichwa kupita kawaida. Dunia ilikuwa kimya, kila mmoja alitaka kuiona nguvu ya Marekani kwamba kama ingeweza kumpata mwanaume huyo au la.

    Walihangaika, kwenye simu hakuwa akipatakana na hata walipojaribu kuitraki simu yake hawakuambulia kitu chochote kile. Walisumbuka kwa muda wa wiki nzima ndipo siku moja wakafanikiwa kuiona simu ya mke wake ikiita, ilikuwa ikipigiwa na simu kutoka nchini Afrika Kusini.

    Waliifuatilia simu ya mkewe bila yeye mwenye kugundua. Walijua kwamba ilikuwa ni lazima kwa mzee huyo kuwasiliana na familia yake na ndiyo maana walikuwa makini sana kuhakikisha wanakamata mawasiliano kutoka kwa watu hao.

    Simu iliyopigwa katika simu ya mwanamke huyo ilitoka Afrika Kusini walichokifanya ni kuiunganisha na kuanza kusikiliza mazungumzo ya watu hao. Maneno waliyoyasikia yaliwashangaza, Juddie alisikika akilia huku akiomba msaada kuonyesha kwamba alikuwa kwenye hatari na baada ya hapo wakasikia sauti ya mwanaume ikimwambia kwamba alimpa saa arobaini na nane tu awe amejisalimisha.

    Maofisa wa CIA hawakujua kilichokuwa kikiendelea, hawakujua ni kitu gani kilikuwa nyuma ya pazia. Ili kujua kile kilichokuwa kikiendelea ilikuwa ni lazima kumkamata Todd na kumuuliza kuhusu hayo yote yaliyotokea na huku wakiwa wameandaa kesi kwa lengo la kumpeleka mahakamani.

    “Simu imetoka Afrika Kusini karibu na kituo cha treni cha Johannesburg Park. Waambie vijana waende huko, wamuwahi mzee huyo na kumtia mikononi mwao,” alisema mwanaume mmoja, haraka sana simu ikapigwa Afrika Kusini, maofisa wa CIA waliokuwa huko, wakawataarifu kwamba mahali walipokuwa hakukuwa mbali na kituo hicho, hivyo walikuwa wakienda haraka sana kuhakikisha mzee huyo anatiwa mikononi.
    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Johannesburg haikuonekana kuwa sehemu salama kwa maisha yao, ilikuwa ni lazima waondoke nchini humo huko Bruno akimwambia mzee Todd kwamba walitakiwa kuelekea nchini Kenya kwani alikuwa akizijua sehemu nyingi za kujificha ikiwemo kijijini kwake.

    Hilo halikuwa tatizo, lakini kabla ya kuondoka kuelekea nchini humo ilikuwa ni lazima wapate mtu ambaye angewaunganishia na meli yoyote ile ili waondoke kuelekea Kenya. Kwa Bruno, kwake lilionekana kuwa suala kubwa na gumu kwani humo Afrika Kusini, hakuwa na ndugu, rafiki au mtu yeyote yule.

    Walitamani kukutana na mtu yeyote ambaye angewaambia mahali pa kwenda kwani kwa jinsi mzee Todd alivyokuwa akitafutwa, walijua kabisa kwamba wasingeweza kupanda ndege, ilikuwa ni lazima kuondoka nchini humo kwa kutumia gari au meli.

    “What should we do?” (Tufanye nini?) aliuliza mzee Todd.

    “Let’s go to Soweto. I’m sure there are people who can help us out,” (Au twende Soweto, naamini huko kuna vijana wengi ambao wataweza kutusaidia,” alisema Bruno.

    Hakuwahi kufika Soweto lakini alisikia tu kwamba huko kulikuwa ni uswahilini mno, kulikuwa na wahuni wengi ambao walikuwa wakipanga madili yao ya kuvamia benki na hata kufanya uchafu wa kila aina. Ilikuwa ni lazima kwenda huko kama tu walikuwa wakihitaji msaada wa kuondoka nchini humo.

    Soweto ilikuwa ndani ya Johannesburg hivyo haikuwa vigumu kwao kufika huko. Kwa kuwa walikuwa na kofia, miwani hawakuhofia kumuuliza mtu yeyote mahali ilipokuwa Soweto. Walipouliza kwa mtu mmoja tu, akawaambia mahali kulipokuwa na kuanza kwenda huko.

    Walikuwa na hofu, waliijua Soweto, kulikuwa na fujo za kila aina, watu walikuwa wakiuawa kila siku, haikuwa sehemu salama ya kuishi kwani watu wote waliokuwa wakiishi humo walikuwa waswahilini ambao waliamini zaidi katika fujo.

    Baada ya dakika kadhaa, wakaingia Soweto. Sehemu hiyo haikutofautiana na sehemu nyingine za uswahilini. Kulikuwa na nyumba mbovu, barabara za vumbo na kitu pekee ambacho kilipendezesha mtaa huo ni uwanja wa timu ya Orlando Pirates.

    Kila mtu alikuwa akiwaangalia jinsi walivyokuwa wakitembea mtaani. Walikuwa wakiangalia huku na kule, kwa kuwaangalia tu ilikuwa ni rahisi kugundua kwamba watu hao walikuwa wageni. Walitembea kwa kujishtukia huku muda mwingi wakiangalia huku na kule.

    Walitembea mpaka walipokuta sehemu iliyokuwa imefungwa kamba kwa mbele. Hiyo ilikuwa ni kuingia ndani kabisa ya mtaa huo wa Soweto. Watu waliokuwa wakipita hapo walikuwa wale wa kitambo au wahuni ambao kutoa roho za watu ilikuwa ni sawa na kuua mbu.

    Magari yote yaliyokuwa yakiibwa mjini, yalipitia hapo na kamba ile kufungwa. Hao ndiyo walikuwa chanzo cha mashirika ya umeme kuanzia mfumo wa luku kwa kuwa hawakuwa wakilipa na kila siku watu wa umeme waliokuwa wakienda huko walikuwa wakipigwa na wengine kuuawa.

    Walisimama pale barabarani huku wakijifikiria kama iliwezekana kuvuka mahali pale au la. Kwa kupaangalia, palionekana kuwa pa kawaida, hakukuwa na mtu yeyote, barabara ya vumbi haikuwa hata na gari moja.

    “Kuna kamba! Hii inamaanisha haturuhusiwi kuingia?” aliuliza Bruno, hakujua maana ya kamba ile.

    “Nahisi kwa magari! Sisi tuingie,” alisema mzee Todd.

    Hicho ndicho walichokifanya, wakaingia kwa kuivuka kamba ile, wakateembea kwa mwendo wa kawaida kusonga mbele huku kila mmoja akionekana kuogopa mno. Walipopiga kama hatua mia moja, mbele wakamuona mwanaume akijitokeza na kusimama barabarani.

    Mkono wa kulia alishika panga huku wa kushoto akiwa na bunduki aina ya AK-47. Mwanaume huyo alivalia usongo kichwani kama Rambo huku akiwa na kaoshi na kipenzi kilichokuwa kimechanikachanika.

    Wakasimama na kuanza kuangaliana na mwanaume yule. Kabla hawajachukua hatua yoyote ya kufanya, wakageuka nyuma, wanaume wengine waliokuwa na muonekano kama wa mwanaume yule aliyekuwa mbele yake wakatokea, walikuwa zaidi ya wanne.

    Mpaka kufikia hapo, wakajua maana ya Mtaa wa Soweto. Walisikia tu kwamba ndani ya mtaa huo mauaji yalikuwa waziwazi, halikuwa jambo la kushangaza kuwaona watu wakipigwa au miili yao kutupwa barabarani kama mizoga.

    “Hey! White! What are doing here?” (Hey! Mzungu! Unafanya nini hapa?) lilikuwa swali la kwanza alilouliza mmoja wa wanaume waliokuwa nyuma yao.

    Hakukuwa na Mzungu aliyejaribu kwenda Soweto. Watu hao hawakupendwa huko kwa kuwa weusi waliamini kwamba walikuwa katili na ndiyo waliokuwa wakiwatesa watu weusi wengi nchini humo.

    Kulikuwa na mapigano ya chini kwa chini baina ya Wazungu na watu weusi. Walitafutana kimya kimya, Wazungu walikuwa wakiokotwa wakiwa wamekufa na hata wakati mwingine nao watu weusi waliokotwa wakiwa wamekufa.

    Hakukuwa na mtu aliyemaliza uhasama huu, ulikuwa ukiendelea huku kila mmoja akijiona kuwa sahihi na kusingekuwa na mtu yeyote wa kumbabaisha.

    Soweto haikuwa na maendeleo makubwa na watu hao waliamini kwamba Wazungu ndiyo waliokuwa wakiinyima maendeleo kwani pamoja na kuwa katika jiji la biashara la Johannesburg lakini uswahilini bado kuliendelea kuwa Soweto.

    Wazungu wengi waliwahusisha wanawake weusi katika biashara ya ngono. Walikuwa wakiwachukua na kuwapeleka katika madanguro ya Kizungu na hata cassino na kuanza kuwafanya walivyotaka.

    Wanawake hao walitafuta pesa, walijua kwamba walikuwa wakijidhalilisha lakini hawakuwa na jinsi, kwa kuwa walikuwa wakaiingiza pesa, kwao

    Kitendo cha mzee Todd kuonekana humo ilikuwa ni hatari kwa maisha yake, aliulizwa swali lakini hakuwa na jibu lolote lile. Wakawasogelea na kuanza kuwaangalia vizuri, waliporidhika, wakawachukua, wakawafunga kamba na kuanza kuondoka nao.

    Wote wakajua huo ndiyo ulikuwa mwisho wao, walikuwa na hofu na kuona kwamba huo ungekuwa mwisho wao. Walipitishwa mitaani, kila mtu aliyekuwa akiwaangalia, alishangaa na zaidi kuliko yote walikuwa wkaimshangaa mzee Todd, ilikuwaje ajiamini aende Soweto na wakati Wazungu wote walikuwa wakiogopa kwenda huko?

    Ni mwendo wa dakika tano tu wakafika katika jumba moja bovu na kuingizwa humo na kuamriwa watulie kwani kulikuwa na kiongozi wao aliyetakiwa kuwaona na kuwauliza maswali machache kabla ya kutoa uamuzi kwamba baada ya kuuawa huyo Mzungu, naye Bruno alitakiwa kuuawa au la.

    “Do they want to kill us?” (wanataka kutuua?) aliuliza mzee Todd huku akionekana kuchanganyikiwa.

    “Yeah! They really want to kill us. Let’s get prepared,” (Ndiyo! Wanataka kutuua hasa. Tujiandae tu) alisema Bruno kwani kwa jinsi watu wale walivyokuwa wakionekana, walionyesha kila dalili za kutaka kuwamaliza watu hao.

    Kitu walichokifanya ni kuwapokonya simu zao na kwenda kuzifungia ndani. Wakawapekua na kuwakuta na pesa, dola aambazo napo wakazichukua na kadi ya benki ambayo kwao ilikuwa muhimu kuliko kitu chochote kile.

    “How much do you have?” (mna kiasi gani?) aliuliza mwanaume mmoja huku akiwa ameshika kadi ya ATM.

    “We have nothing...” (hatuna kitu) alijibuu Bruno.

    “You must be kidding me,” (utakuwa unanitania)

    “Serious brother, we have nothing,” (siriazi kaka, hatuna kitu) alijibu Bruno, hakutaka kumuacha mzee Todd aongee kwani kwa hofu aliyokuwanayo ingekuwa rahisi kusema kiasi chote kilichokuwa kwenye akaunti na wakati yeye mwenyewe alikuwa akikitaka.

    “Give me the password,” (nipeni namba ya siri) alisema mwanaume huyo.



    Hilo lilikuwa jambo gumu ambalo lisingeweza kufanyika. Kitendo cha kumpa mwanaume huyo namba ya siri ya kadi ile ilimaanisha kwamba wangekwenda kuchukua kiasi chote cha pesa ambacho kilikuwa kikubwa mno.

    Bruno hakutaka kukubali, kwake, zile pesa zilikuwa kila kitu, alizitaka na ndiyo maana aliamua kumpambania mzee Todd kumfikisha salama alipokuwa akipataka yeye lakini si kuona akipoteza pesa zile.

    Jamaa huyo aliona kama alifanyiwa kiburi kwa kutopewa namba ya siri ya kadi ile, akachukua bastola yake na kuwanyooshea huku akitaka aambiwe kuhusu namba hizo.

    Wakati kila mmoja akijua kwamba walikuwa wakipigwa risasi, ghafla mlango ukafunguliwa na wanaume wawili kuingia humo. Mmoja alikuwa yule kiongozi wao aliyekwenda kuitwa kwa lengo la kuja kuwaona watu waliokuwa wamewakamata.

    Kiongozi huyo alipofika hapo, akawaangalia watu hao. Ghafla, akashtuka, hakuamini kumuona mtu huyo mahali hapo. Hakuwa mzee Todd, bali alikuwa Bruno.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Akamsogelea na kumwangalia vizuri. Alimfahamu mtu huyo japokuwa ilipita miaka kumi hawakuwa wameonana. Bruno alibaki akimshangaa mtu huyo, hakumfahamu na aliona kabisa kwamba siku hiyo ndiyo ilikuwa ya kwanza kumuona mbele ya macho yake.

    “Bruno!” aliita mwanaume huyo kitu kilichomfanya Bruno kushtuka, si yeye tu bali hata watu wengine waliokuwa mahali hapo.

    “Who the hell are you?” (wewe nani?) aliuliza Bruno huku akimwangalia mwanaume huyo.

    “Niangalie! Hunijui kweli?” aliuliza mwanaume huyo kwa Kiswahili kilichomfanya Bruno kugundua kwamba mtu huyo alitoka Afrika Mashariki.

    Bruno alimwangalia, hakuweza kumkumbuka mwanaume huyo, kwake, alionekana kuwa mgeni kabisa. Aliyaangalia mavazi aliyokuwa ameyafaa, yalimuonyesha jinsi alivyokuwa katili na mtemi katika mtaa huo.

    “Bruno! Umenisahau Ibrahim Onyango! Kiongozi wa watoro shuleni!” alisema mwanaume huyo.

    Alipolitaja jina la Onyango tu, kumbukumbu za Bruno zikaanza kurudi nyuma. Akamkumbuka mwanaume huyo, aliwahi kusoma naye sekondari mpaka pale walipomaliza shule na kufeli vibaya huku yeye akianza kazi ya uvuvi.

    Onyango alikuwa kiongozi wa watoro shuleni kwao, hakupenda kusoma, kila siku aliwaambia wazazi wake kwamba shule ilimkataa na ilikuwa ni lazima kuondoka Kenya na kuelekea Afrika Kusini kutafuta maisha.

    Wazazi wake walizungumza naye sana, walikuwa ni wazazi waliokuwa na uuwezo mkubwa, walimpa kila kitu lakini Onyango hakutaka kukubali, mali zile alisema ni za wazazi wake na yeye ilikuwa ni lazima kutafuta mali zake, hakuona sehemu ambayo angepata maisha mazuri zaidi ya kwenda Afrika Kusini.

    Alitoroka Kenya na kuelekea Afrika Kusini. Watu walishangaa lakini yeye aliamua kuwa na maisha yake. Miaka zaidi ya kumi ilikuwa imepita, leo, Bruno alikutana na Onyango Afrika Kusini huku akiambiwa kwamba huyo ndiye alikuwa kiongozi wao.

    “Unafanya nini huku?” aliuliza Onyango huku akimwangalia Bruno.

    “Ni habari ndefu sana! Tunaweza kwenda sehemu kuongea nje ya hapa manake hizi bunduki zinanikosesha amani kabisa,” alisema Bruno.

    “Haina noma!”

    Bruno hakutaka kubaki peke yake, aliamini kwamba kama angemuacha mzee Todd ndani ya chumba kile basi angepigwa mikwara na kutoa namba za siri za kadi, alichokifanya ni kuondoka na mzee huyo kwenda uani na kuanza kuzungumza na Onyango.

    Waliongea kwa furaha, walicheka na kukumbushiana mambo mengi ya nyuma. Muda wote huo mzee Todd alikuwa akiwasikiliza tu, hakuelewa Kiswahili, alibaki kimya huku mawazo yake yakiwa yanaifikiria familia yake tu.

    “Ikawaje?”

    “Washikaji wakanitosa baharini! Mtu wangu nilipiga mbizi mpaka nikaokolewa na Warusi,” alisema Bruno.

    “Na huyu mzee vipi?”

    “Nilimkuta kwenye meli hiyo, wana walitaka kumuua, ila nilipotoroka, nikatoroka naye!”

    “Wewe ninja! Yaani ulitoroka kwenye meli, wewe ninja mchizi wangu,” alisema Onyango huku akitoa tabasamu pana.

    Waliendelea kukaa uani na kuendelea kuzungumza. Wakati mazungumzo yakiwa yamepamba moto, wakaanza kusikia kelele kutoka mtaani, hawakujua kulikuwa na nini. Wakati wakiwa wanajiuliza, wakaanza kusikia milio ya risasi, ilikuwa ni kama milio ya majibizano.

    Kila mmoja akaogopa, Onyango akachukua bunduki yake, akapanda ukuta na kuangalia kwa nje kuona kulikuwa na nini. Macho yake yakatua kwenye gari moja jeusi, lilikuwa jipu, kulikuwa na Wazungu wanne waliovalia suti ambao walikuwa wakipambana na vijana wake.

    “Kuna nini?” aliuliza Bruno huku akiogopa.

    “Wazungu! Wamekuja kupambana! Sijui kuna nini!”

    “Tufanye nini?”

    “Njooni huku!”

    Aliwachukua na kuwapeleka katika mlango mwingine wa kutoka ndani ya eneo la nyumba hiyo na kuwaambia wakimbie kwani hawakujua watu hao walikuwa wakina nani na walihitaji nini.

    Hilo halikuwa tatozo, wakaagana na kuanza kukimbia mahali hapo. Milio ya risasi iliendelea kusikika kila kona. Wazungu wale walikuwa hatari, walikuwa na shabaha kupita kawaida, kila risasi iliyokuwa ikitoka, ilitoka kwa malengo na kumpata mtu.

    Japokuwa Soweto kulizoeleka kusikika milio ya risasi lakini siku hiyo hali ilionekana kuwa tofauti. Soweto ilibadilika na kuwa kama uwanja wa mapambano. Watu weusi wengi waliuawa na hakukuwa na mtu aliyejua sababu iliyowafanya Wazungu hao kufika humo na kuanza kushambulia.

    Bruno na mzee Todd waliendelea kukimbia, hakukuwa na mtu aliyesimama, kila mtu alikuwa akiokoa maisha yake. Wakakimbia mpaka mlimani na kuanza kuangalia kwa chini kwa mbali.

    Waliwaona watu wakipambana, milio ya risasi iliendelea kusikika kwa sauti kubwa huku watu wengine wakikimbilia kule walipokuwa.

    “Mungu wangu! Nimesahau kadi ya ATM kwa yule jamaa,” alisema Bruno mara baada ya kujipekua mifukoni kuangalia kadi ile.

    “Unasemaje?”

    “Kadi na simu! Tumesahau ndani ya nyumba ile,” alisema Bruno huku akionekana kuchanganyikiwa, kwake, ilikuwa ni afadhali kusahau simu lakini si kadi ya ATM.

    “Tuondoke! Achana navyo! Tuondoke!” alisema mzee Todd, kwake, pesa zilizokuwa katika akaunti aliyofungua Bruno kilikuwa kiasi kidogo sana cha pesa.

    “Haiwezekani!”

    “Bruno! Tuondoke!”

    “Siwezi kuondoka na kuacha kadi ile. Ni lazima nirudi!”

    “Urudi?”

    “Ndiyo!”

    “Kule kwenye mapambano?”

    “Hukohuko!”

    “Haiwezekani!”

    “Siwezi kuendelea mbele pasipo ile kadi. Kuna hela nyingi sana, hatuwezi kuacha kadi kiholelea,” alisema Bruno.

    Walikuwa wakivutana, mzee Todd alimwambia Bruno kwamba walitakiwa kuondoka lakini kijana huyo hakutaka kuelewa kitu chochote kile. Alichomwambia ni kwamba amsubiri pale na yeye kwenda kule kuchukua kadi.

    Alikuwa akikimbia kuteremka mlima. Alipishana na watu waliokuwa wakipandisha, kila mmoja alikuwa akimshangaa, wao walikuwa wakikimbia risasi lakini ndiyo kwanza Bruno alikuwa akizikimbilia. Walimuona kama mtu aliyechanganyikiwa lakini mwenyewe hakuwa tayari kuona akirudi nyuma, kwake, kadi ile ilikuwa muhimu kuliko kitu chochote kile.

    Milio ya risasi iliendelea kusikika lakini hakujali, alipofika, akaanza kupita kwenye vichochoro. Alikuwa peke yake, watu wengine walikuwa wamejifungia vyumbani mwao na wengine kukimbia.

    Hakukumbuka mahali nyumba ile ilipokuwa lakini baada ya kukumbuka kwamba ndipo mahali watu wale walipokuwa wakipambania, akaanza kufuatilia milio ya risasi hiyo.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Alitembea harakaharaka kwa kujificha mpaka alipofika mahali ilipokuwa nyumba ile. Hakutokea kule ilipokuwa nyumba ile bali alipotokea ni nyuma ya gari la Wazungu wale waliokuwa wakipambana. Akawaangalia vizuri Wazungu wale, jinsi walivyokuwa wakipambana na hata kukwepa risasi, akagundua kwamba hawakuwa watu wa kawaida hata kidogo, mafunzo waliyokuwa nayo yalikuwa hatari mno.

    “Who the hell are these people?” (hawa ni wakina nani?) alijiuliza swali alilokosa jibu, kijasho chembamba kilikuwa kikimtoka mfululizo.

    ***

    Mawasiliano yakafanyika haraka sana kutoka nchini Marekani, maofisa wa CIA waliokuwa nchini Afrika Kusini walitakiwa kwenda kule simu ilipopigwa ambapo wakaelekezwa na kuelekea huko. Walipofika katika kituo cha treni jijini Johannesburg ambapo ndipo mzee Todd alipokuwa amepiga simu, hawakuweza kumuona mzee huyo.

    Haraka sana wakawapigia simu maofisa waliokuwa nchini Marekani na kuwaambia kile kilichokuwa kikiendelea kwamba mwanaume huyo hakuwa mahali hapo. Hilo halikuwa tatizo, kwa kutumia satalaiti yao kwa mfumo wa GPS, wakaweza kuiunganisha simu ya mzee Todd na wao kuweza kuona jinsi simu ile ilipokuwa kipindi hicho.

    Waliona ikiwa inatoka sehemu moja kwenda nyingine, hawakutaka kubaki mahali hapo kwani kutoka katika kituo hicho mpaka mahali simu hiyo ilipokuwa hakukuwa mbali. Wakaondoka na kumfuata mahali alipokuwa kwani simu ile ilionyesha kwamba ilikuwa katika Mtaa wa Soweto.

    Hawakuchukua muda mrefu wakawa wanakaribia kuingia katika mtaa huo. Walipoangalia tena kifaa chao wakaona kwamba simu imetulia sehemu moja kitu kilichowafanya kujua kwamba ilikuwa imewekwa ndani, sehemu fulani na watu hao kutulia.

    Waliijua Soweto, walijua tabia za watu wa huko kwamba hawakuwa na mchezo hata mmoja, walizijua chuki zao kali dhidi ya Wazungu, walijua kabisa kama wangekwenda kimama basi ilikuwa ni lazima kuuawa.

    Wakakaanda bastola zao na kuingia ndani huku wakiwa na gari lao ambalo vioo vyake havikumruhusu mtu wa nje kuona ndani. Walipofika katika eneo ambalo halikuwa mbali na mahali simu ilipokuwa, wakasimamisha gari lao.

    Nyumba iliyokuwa mbele yao ndiyo ambayo ilikuwa na mtu waliyekuwa wakimtafuta, nje ya nyuumba ile kulionekana vijana mbalimbali wakifanya mambo yao, wengine walikuwa wakipiga stori na wengine kujitenga pembeni huku wakivuta bangi.

    “Tufanye nini?” aliuliza jamaa mmoja.

    “Tukavamie!”

    “Ila tuwe makini kwanza, tunaweza kufa na mbaya zaidi hatujui wale jamaa wana nini,” alisema mwingine.

    Wale vijana waliokuwa nje ya nyumba ile walionekana kulishuku gari lile, lilikuwa limekuja mahali pale na kusimama, hawakujua kulikuwa na kitu gani kilichokuwa kikiendelea lakini wakahisi kabisa kwamba watu waliokuwa humo ndani hawakuwa watu wema.

    Wakachukua bunduki zao na kuanza kulisogelea. Maofisa wale wa CIA walipowaona wanakuja, wakaziandaa bastola zao kwa lengo la kushambuliana kwani walijua kwamba kama wale vijana wangejua kwamba ndani ya gari lile walikuwemo wao, Wazungu basi ilikuwa ni lazima kuwamaliza.

    “Paa!” ulisikika mlio mmoja wa risasi, jamaa mmoja wa pale Soweto miongoni mwa wale vijana waliokuwa wakipiga hatua akaanguka na damu kuanza kumtoka kifuani.

    Vijana wale wakashtuka na kugundua kwamba kweli watu wale hawakuwa wazuri kwao, wakajificha na kuanza kushambuliana nao. Milio ya risasi ilisikika kila kona mahali hapo, wale waoga, wakakimbia lakini waliokuwa na bunduki nao wakajiweka sawa na kuanza kupambana na watu hao.

    Bruno alikuwa amekwisharudi na kuwa nyuma ya gari la maofisa wale wa CIA, hakujua ni kitu gani alitakiwa kufanya kwani kwa jinsi alivyokuwa mweusi, kama angejitokeza mbele ya watu wale ilikuwa ni lazima kumuua kwa kuwa wangehisi kwamba naye alikuwa adui.

    Hakuondoka mahali hapo, alijibanza kwenye ukuta huku akifuatilia kila kitu kilichokuwa kikiendelea. Baada ya dakika kadhaa, milio ya risasi ikaacha, Wazungu wale wakajua kwamba watu weusi waliokuwa wakipambana nao, wote walikuwa wamekufa na hivyo kuanza kuingia ndani.

    Walipofika, ni maiti tu ndizo zilizokuwa zikionekana huku zikiwa zimetapakaa damu. Ndani ya nyumba ile, wakaanza kumtafuta mzee Todd ambaye walijua kwamba alikuwa humo kwa kuwa bado GPS ilionyesha kwamba simu ile ilikuwa humo ndani.

    Wakafanikiwa kuipata lakini kitu cha ajabu, mzee huyo hakuwepo. Wakaanza kuangalia katika kila chumba, wakafungua milango na kuingia ndani lakini hawakuweza kumuona mzee huyo ambaye walifika hapo kwa lengo la kumtaka yeye tu.

    Walipohakikisha kwamba hakuwepo, hawakutaka kupoteza muda kubaki mahali hapo, walichokifanya ni kuondoka na kuziacha maiti mulemule ndani ya nyumba ile.

    Wakati wanatoka, wanaingia ndani ya gari lao na kuondoka mahali hapo, bado Bruno alikuwa amejibanza kwenye kile kiukuta, alipoona gari limeondoka mahali hapo, haraka haraka akatoka na kwenda ndani ya nyumba ile.

    Hali aliyoikuta humo ilimuogopesha mno, hakuwahi kufikiria hata siku moja kwamba katika maisha yake kuna siku angeweza kuziona maiti nyingi zikiwa zimetapakaa kama ilivyokuwa siku ile.

    Akaziruka na kumfuata yule mwanaume ambaye aliichukua ile kadi na kuanza kumpekua mifukoni mwake, akabahatika kuikuta kadi ile ambayo aliichukua na kuondoka zake.

    Bado mtaa ulikuwa kimya, hakukuwa na mtu aliyethubutu kutoka ndani ya nyumba yake kwa kuhofia maisha yake, kila mtu alibaki ndani huku dakika zikiendelea kwenda mbele.

    Bruno alipoondoka hapo, moja kwa moja akaelekea kule mlimani, alikuwa akikimbia, alichoka lakini hakutaka kusimama, kwake, mzee Todd alikuwa kila kitu, alihitaji kumsaidia mzee huyo kwa kuwa alionekana kuhitaji msaada kupita kawaida.

    Alipofika kule juu, akamkuta pale pale alipomuacha na kumuonyeshea kadi ile kwamba alifanikiwa kuipata kitu kilichoonekana kumfurahisha mzee yule.

    “Kwa hiyo?” aliuliza mzee Todd.

    “Tuondoke tukapange vyumba hotelini,” alisema Bruno na kuanza kuondoka hapo.

    Mzee Todd hakutaka kuvua miwani wala kofia aliyokuwa ameivaa, hakutaka kugundulika na mtu yeyote yule, alijua kwamba alikuwa akitafutwa kila kona hivyo kama angeendelea kujificha hivyo basi ingemsaidia kuwa salama mpaka siku ambayo angefanikiwa kufika nchini Marekani.

    Alijua kwamba kutafutwa kwake ni Maxwell ndiye alikuwa amefanya hivyo, alihisi kitu hicho kwani mbali na kuwa na urafiki wa mashaka lakini kila mmoja alihitaji kuwa na nguvu ya kibiashara kitu kilichoonekana kuvuruga kila kitu.

    Hawakuchukua muda mrefu wakafika sehemu iliyokuwa na hoteli ndogo iitwayo Elizabeth Royal, moja kwa moja wakaelekea mpaka mapokezi ambapo wakafanya harakati za kuchukua chumba.

    “Tutakaa kwa siku tano,” alisema Bruno ambaye akachukua ile kadi na kumpa dada wa mapokezi ambaye akaingiza namba za kadi katika kompyuta yake na kuchukua kiasi kilichotakiwa kama malipo kwa muda huo. Alipomaliza, akawapa kadi zilizotumika kama funguo na kuondoka mahali hapo kuelekea vyumbani kupumzika.





    Maxwell alichanganyikiwa, mpaka kipindi hicho hakujua mahali mzee Todd alipokuwa. Alihisi kabisa kichwa chake kikichanganyikiwa, mwanaume huyo alikuwa muhimu mno kwake, alimtaka kwa udi na uvumba na ndiyo maana alihangaika kwa nguvu zote kuhakikisha kwamba anauawa kwa gharama yoyote ile.

    Vijana waliokuwa nchini Afrika Kusini nao hawakuweza kumsaidia kwa chochote kile, kila alipowapigia simu walimwambia kitu kimoja kwamba bado waliendelea kumtafuta na hawakujua mahali alipokuwa.

    Alikuwa na familia yake, ilikuwa ni lazima kuhakikisha kwamba watu hao hawaondoki mikononi mwake, alihakikisha kwamba anawafanyia umafia wa nguvu hata kama mzee huyo hakuonekana.

    Alimpa saa sabini na mbili ambazo zilikuwa ni siku tatu, alijua kwamba kwa jinsi alivyokuwa akiipenda familia yake, ilikuwa ni lazima mzee Todd afanye kila liwezekanalo kufika nchini Marekani.

    Siku ya kwanza ikakatika, ya pili ikaingia na kukatika lakini bado majibu yalikuwa yaleyale kwamba Todd hakuonekana na vijana wake walikuwa wakiendelea kumtafuta kila kona bila mafanikio.

    “Kwa hiyo?” aliuliza kijana mmoja kwenye simu, alitaka kusikia kutoka kwa bosi wake kama ilikuwa ni muhimu kuimaliza familia yake hata kama hakuwa amerudi au walitakiwa kusubiri.

    “Tuongeze siku mbili, inawezekana akafika,” alisema Maxwell.

    Hawakuwa na jinsi, wakaongeza siku mbili huku wakiendelea kuitunza familia yake kwa chakula na vitu vingine. Kila siku Juddie alikuwa kwenye maumivu makali, hakujua mahali mume wake alipokuwa, alitamani kumuona, hata kama asingemuona akiwa hai basi aione hata maiti yake na kujihakikishia kwamba mume wake alifariki dunia.

    Siku hizo zilipokwisha, Maxwell hakuwa na jinsi, akamwambia kijana yule awamalize na kisha kuipiga picha miili ya watu hao ili baadaye amtumie mzee Todd na kumwambia kwamba aliiteketeza familia yake na alibaki yeye tu, na ilikuwa ni lazima amtafute na kumuua.

    “Kill them both,” (waue) alisema Maxwell kwenye simu.

    “Hakuna shida bosi!” alisema kijana huyo na kukata simu, utekelezaji ulitakiwa kufanyika mara moja.

    ***

    Japokuwa walikuwa wamepatana kukaa mahali hapo kwa muda wa wiki moja lakini mpaka kipindi cha mwezi nzima Bruno na mzee Todd walikaa ndani ya hoteli hiyo waliyokuwa wamechukua chumba.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Hawakuonekana kuwa na hofu yoyote ile kwani kwa jinsi walivyokuwa ilikuwa vigumu sana kumgundua mzee Todd kwamba alikuwa mtu aliyekuwa akitafutwa mno kutokana na sakata la madawa ya kulevya lililokuwa likimkabiri.

    Waliishi kwa amani japokuwa muda mwingi mzee huyo alikuwa akimfikiria mke na mtoto wake. Hakujua kama watu hao walikuwa hai au la kwani tangu alipopewa muda wa saa sabini na mbili mwezi uliopita, hakuwasiliana nao tena.

    Hakuonekana kuwa na raha hata kidogo, kichwa chake kilikuwa na mawazo tele. Alitamani kuondoka barani Afika, hakutaka kuendelea kuishi huko na wakati hakujua familia yake ilikuwa ikiendeleaje nchini Marekani.

    Dada wa mapokezi, Thandi ambaye aliwapokea katika hoteli waliyokuwa wamechukua chumba alionekana kuwa na wasiwasi na wateja hao. Mtu aliyemtia hofu alikuwa mzee Todd ambaye muda wote aliokuwa akiongea, kofia na miwani haikutoka mwilini mwake.

    Alikuwa akijiuliza mambo mengi kuhusu mtu huyo, hakujua sababu ya kufanya hivyo, alijaribu kumwangalia vizuri zaidi lakini hakupata jibu juu ya mwanaume huyo, hakujua alikuwa nani na kwa nini hakutaka kuondoa kofia wala miwani aliyokuwanayo.

    Alijaribu kuvumilia, alitaka kuona kama ingetokea siku moja mzee huyo kuvua kofia yake lakini jambo hilo halikuweza kutokea, kila alipokuwa akitoka chumbani kwake kofia yake ilikuwa kichwani.

    Japokuwa lilionekana kuwa jambo la kawaida lakini kwa mhudumu huyo likaonekana kuwa jambo moja kubwa sana kwani katika kipindi hicho kulikuwa na matukio mengi ya kigaidi yaliyokuwa yakitokea nchini Afrika Kusini, akahisi kwamba inawezekana mzee yule alikuwa mmoja wa magaidi waliotaka kuilipua hoteli yake.

    Kukosa amani kwake kukampeleka kumuhadithia mpenzi wake nyumbani. Alimwambia ukweli kuhusu wageni hao waliokuwa wamechukua mwezi mzima kazini kwake lakini katika kipindi chote hicho hakuwahi kuona kofia ikitoka kichwani mwa mzee Todd.

    “Mwezi mzima?” aliuliza mpenzi wake.

    “Ndiyo! Ni mwezi mzima ile kofia ipo kichwani,” alijibu Thandi.

    “Mmh! Labda kuna kitu hapo, umejaribu kufuatilia kwa karibu kujua sababu?” aliuliza mpenzi wake.

    “Hapana! Ila anaonekana ana pesa sana kwani hivyo vinywaji anavyokuywa, ni balaa,” alisema Thandi kwa lengo la kumsifia mzee Todd.

    Wakati wakizungumza mambo kuhusu wageni hao, kichwa cha mpenzi wake kikaenda sehemu nyingine kabisa. Yeye alikuwa mmoja wa vijana waliokuwa wamewekwa nchini Afrika Kusini kwa lengo la kumtafuta mzee Todd. Alikuwa kijana wa Maxwell ambaye aliamua kuwatawanya wengi nchini humo kwa kuamini kwamba mzee Todd alikuwa ndani ya Afrika Kusini.

    Alipoambiwa na Thandi kuhusu jambo hilo, hakutaka kubaki nalo bali alichokifanya ni kwenda kuwaambia vijana wenzake kile alichoambiwa na mpenzi wake kwani hata naye alikuwa na hofu tele kwa kuhisi kwamba inawezekana huyo Mzungu alikuwa ni yule Todd waliyekuwa wakimtafuta.

    “Sasa kofia si jambo la kawaida tu,” alisema mwenzake baada ya kupewa taarifa.

    “La kawaida? Unajua kwamba inawezekana akawa Todd tunayemtafuta?”

    “Ni vigumu! Hivi Todd anavyotafutwa anaweza kuwa hotelini kweli?”

    “Inawezekana kwani hayupo peke yake, yupo na kijana mwingine. Mmesahau tulivyoambiwa kwamba kwenye meli Todd alikuwa na kijana mwingine wa Kiafrika?” aliuliza mpenzi wa Thandi.

    Hilo kidogo likawaingia vichwani mwao. Ilitakiwa kuanza kufuatilia na kujua watu hao walikuwa ni wakina nani na kwa nini mwanaume huyo wa Kizungu alikuwa akivaa kofia muda wote.

    Walichokifanya ni kuwatuma vijana wawili na kuanza kuwafuatilia katika hoteli hiyo. Vijana hao wakaenda na kupanga vyumba huku wakitakiwa kufuatilia kila hatua ambayo watu wale walikuwa wakichukua.

    Baada ya siku mbili, vijana hao wakafanikiwa kumuona Bruno na mzee Todd wakiendelea na maisha yao kama kawaida hotelini pale. Kwa kumwangalia mzee Todd, kwao halikuwa na ugumu kugundua kama huyo alikuwa mzee huyo.

    Haraka sana wakawaambia wenzao kwamba walimwangalia mzee huyo na kugundua kwamba alikuwa yuleyule waliyekuwa wakimtafuta na hivyo vijana hao kupiga simu kwa Maxwell na kumwambia kilichokuwa kikiendelea.

    “Safi sana! Hakikisheni haondoki ndani ya hoteli hiyo,” alisikika Maxwell kwenye simu.

    “Kwa hiyo tumuue au?”

    “Hapana! Atekwe, msimuue hapo hotelini, watu wakikusanyika mnaweza kukamatwa na kuniletea matatizo,” alisikika Maxwell.

    Mipango ya kutekwa kwao ikapangwa, hawakutakiwa kutekwa wakiwa vyumbani mwao bali walitakiwa kutekwa wakati wakiwa katika mgahawa wa hotelini hapo walipokuwa wakila.

    Hilo wala halikuwa tatizo, walichokifanya ni kusoma ratiba yao kwanza. Wakagundua kwamba watu hao wawili walikuwa wakishuka mgahawani saa nne asubuhi, saa sita mchana na saa mbili usiku, hivyo kama walitaka kuwateka basi hiyo ndiyo mida yao waliyokuwa wakitoka kwenda kula.

    “Tuwatekeni usiku, nadhani hiyo itakuwa salama zaidi,” alisema kijana mmoja na kukubaliana. Siku iliyofuata ndiyo ilikuwa siku ya kufanya tukio hilo, kuanzia asubuhi mpaka jioni walikuwa wakiwafuatilia kwa makini sana.

    Majira ya saa moja hata kabla hawajakwenda kwenye mgahawa, tayari vijana hao walikuwa wamefika mahali hapo huku wakiwa na bastola zao viunoni.

    Wakati Bruno na mzee Todd wakishuka kwenda kula, walikuwa wakiwaangalia tu, wakawaona wakiifuata meza moja, wakakaa na kuanza kula huku sehemu yote hiyo ikiwa na watu.

    “Kwa hiyo? Tuwafuate sasa hivi?” aliuliza jamaa mmoja.

    “Umewaambia washikaji waandae gari?”

    “Ndiyo! Walisema gari lipo tayari hapo nje ya hoteli,” alijibu mwingine, walikuwa wakiongea kwa sauti ya chini.

    “Basi sawa. Twende!”

    Wakainuka na kuanza kuwafuata watu hao, walipowafikia katika meza ile, wakatoa bastola zao kisiri sana na kuwaambia wasimame. Kwanza walitaka kubisha lakini hata kabla ya kufanya hivyo, wakaziona bastola hizo kitu kilichowafanya kuogopa.

    Waafrika Kusini hawakuwa watu wa mchezo, waliwafahamu, walikuwa na michezo ya kutisha na bastola zao, walikuwa wepesi kuua, kwao, kumwaga damu ilikuwa ni kama kumchinja kuku au kumuua panzi.

    Wakainuka na kuanza safari ya kuelekea nje ya mgahawa ule huku wakiwa wametangulizwa mbele. Hakukuwa na mtu yeyote aliyegundua kitu kilichokuwa kikiendelea mahali hapo, walichokiona ni marafiki wanne walikuwa wamewafuata wenzao na kuondoka mahali hapo.

    Walipofika nje, tayari wenzao walikuwa katika gari moja mahali hapo, walichokifanya ni kuwataka kuingia garini na baada ya hapo, gari likawashwa na kuondoka mahali hapo kwa mwendo wa kawaida kana kwamba hakukuwa na kitu kibaya kilichokuwa kimetokea.

    Hata kabla hawajafika mbali, kijana mmoja aliyekuwa amebaki ndani ya gari lile na dereva akachukua simu yake, akabonyeza namba fulani, baada ya sekunde kumi akaanza kuzungumza na mwanaume wa upande wa pili ambaye alikuwa Maxwell.

    Alimwambia kwamba mtu aliyekuwa akihitajika alikuwa mikononi mwao hivyo walitaka kufuata maelekezo ya juu ya nini cha kumfanya mtu huyo.

    “Just kill him,” (muueni tu!)

    “And the other guy?” (na huyu mwingine?)

    “Who is he?” (nani huyo?)

    “He was with him, should we kill him too?” (alikuwa naye, naye tumuue pia?) aliuliza.

    “Kill them both,” (waueni wote)

    “Ok sir,” (Sawa bwana mkubwa) alisema kijana yule na hapohapo akaanza kuikoki bunduki yake, kilichotakiwa kufanywa ndani ya gari hilo ni mauaji tu.

    Bruno na mzee Todd walijua kile kilichokuwa kikienda kutokea kwani waliisikia sauti iliyokuwa ikizungumza na kijana yule, wakajua kabisa kwamba walikuwa wakienda kufa humo garini.

    Walitamani kuruka kupitia dirishani lakini walishindwa, vioo vilifungwa na mbaya zaidi walikuwa wamewekwa mtu kati hivyo wasingeweza kufanya kitu chochote kile.

    Wakaanza kuomba msamaha, hawakutaka kufa kikatili ndani ya gari. Bruno ndiye aliyekuwa akilia sana, moyoni mwake alimkumbuka mpenzi wake, Sharifa, ilikuwa ni lazima aondoke Afrika Kusini kwenda nchini Kenya kumuona mpenzi wake aliyekuwa akimpenda kwa moyo wa dhati. Wakati wakiwa wanasali sala zao za mwisho, tayari vijana waliokuwa mule garini walikwishamaliza kuzikoki bastola zao na kilichosikika baada ya hapo ni milio ya risasi tu huku gari likiwa kasi.

    “Paaa! Paaa! Paaa!” milio ya risasi ikasikika na damu kutapakaa garini.

    ***

    Bado msichana Thandi alikuwa na hofu tele juu ya watu waliokuwa wamefika katika hoteli yao na kuchukua chumba, mwanaume yule wa Kizungu kila siku alikuwa na kofia kichwani mwake na miwani, hakutaka kuitoa, alipokuwa akifika mapokezini, alikuwa na vitu hivyo na hata alipokuwa akiingia ndani ya gari pia alikuwa na vitu hivyo.

    Hilo lilizidi kumtia hofu msichana huyo, hakutaka kukubali, aliona kabisa kwamba ilikuwa ni lazima amwambie bosi wake juu ya kile kilichokuwa kikiendelea kwani kwa muda wa mwezi mzima mwanaume huyo kuwa hivyohivyo, lilionekana kuwa jambo gumu.

    Mbali na kuzungumza na mpenzi wake, akazungumza na meneja wa hoteli hiyo ambaye naye akaanza kufuatilia na kugundua kwamba kulikuwa na ukweli kwa kile alichokuwa akiambiwa.

    Hakutaka kuchelewa, meneja huyo akazungumza na polisi na kuwaambia kila kitu kilichokuwa kikiendelea. Polisi hao walitaka kuthibitisha kile kilichokuwa kikiendelea na hivyo kwenda katika hoteli hiyo kujionea kwa macho yao.

    Siku ambayo walikwenda na kuonyeshewa watu hao ndiyo siku ambayo Bruno na Todd walikuwa kwenye mgahawa wakila. Polisi waliokuwa na nguo za kiraia walikuwa mahali hapo, bastola zilikuwa viunoni mwao, walijiandaa na kitu chochote kile ambacho kingetokea mahali hapo.

    Baada ya dakika kadhaa, wakawaona wanaume wawili wakisimama na kuwafuata watu wale waliowafuata, walisimama karibu nao na kuanza kuzungumza nao. Walikuwa polisi, walijua kila kitu alichokuwa akikifanya adui. Japokuwa watu wengine hawakuwa wameziona bunduki walizozionyesha watu hao kisiri na kuwataka kusimama, wao waliziona vizuri kabisa.

    “What the hell is going on?” (nini kinaendelea?) aliuliza polisi mmoja huku jicho lake likiangalia kule kwa wizi.

    “I don’t know, let’s keep waiting,” (sijui, hebu tuendelee kusubiri) alijibu mwenzake.

    Baada ya sekunde kadhaa wakawaona watu wao wakisimama na kuanza kupiga hatua kwenda nje huku wale jamaa wakiwafuata kwa nyuma. Haikuwa ngumu kwao kugundua kwamba watu wale walikuwa wamewekwa chini ya ulinzi na hivyo kuanza kuwafuatilia.

    Walipofika nje, wakawaona wakiingia ndani ya gari na kuondoka mahali hapo. Nao hawakutaka kubaki, wakaingia ndani ya gari lao na kuondoka kwa kulifuatilia gari lile.

    Walilifuatilia gari hilo ambalo lilichukua Barabara ya Western Bypass ambayo ilikuwa ikielekea Upande wa Kaskazini mahali kuitwapo Woodmead kulipokuwa na makorongo makubwa. Magari yalikuwa yakitembea kwa mwendo wa kawaida, hawakusubiri sehemu yoyote ile, ilikuwa ni lazima kulifuatilia na kujua mwisho wa safari hiyo ilikuwa wapi.

    Hawakuwa mbali kutoka katika gari hilo, ilikuwa ni sawa na hatua tano za miguu ya binadamu. Wakati wakiwa wamekwishafika Bryston, wakashangaa kuona mwanaume mmoja akitoa bastola yake ndani ya gari. Hawakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea lakini waliangalia vizuri kabisa na kumuona mtu huyo akiwa na bastola yake dakika chache baada ya kuongea kwa simu.

    “Stephen, take your gun and do the work,” (Stephen, chukua bastola yako ufanye kazi) alisema mwanaume aliyekuwa akiendesha gari.

    Hilo halikuwa tatizo kwa huyo mtu aliyeambiwa kwani alikuwa miongoni mwa polisi waliokuwa na shabaha kubwa, alichokifanya, kama muvi vile akatokeza nusu ya mwili wake nje ya gari kupitia dirishani na kisha kunyoosha mkono wenye bastola kuelekea katika gari lile.

    Watu waliokuwa pembeni walishangaa, hawakujua sababu ya mwanaume yule kufanya hivyo lakini hata kabla hawajapata majibu, Stephen akaachia risasi kadhaa ambazo zilipenya katika kioo cha nyuma, mwanaume mmoja akapigwa risasi ya shingo kwa nyuma, kwa kupagawa, wenzake wakaanza kurushiana risasi na Stephen ambaye alikuwa kwa nyuma na alikuwa akiwaona vizuri kabisa.

    Kila mmoja akawasahau watu wao na hivyo kuanza kupambana na Stephen aliyeonekana kuwa si mtu wa mchezo hata kidogo. Mwenzake aliyekuwa ameshikilia usukani alijua vilivyo namna ya kupambana na watu waliokuwa kwenye gari hivyo alichokifanya ni kuendesha kwa kasi na kusimama upande wao wa kulia na hivyo kumpa nafasi Stephen kufanya kile alichokitaka.

    Watu waliokuwa pembeni wakaanza kukimbia, kila mtu alikuwa akiyaokoa maisha yao kwani hali ilionekana kutisha na ilionekana kabisa kwamba muda wowote ule risasi zile zingewapata.

    “Deal with the driver,” (shughulika na dereva) alisema dereva.

    Hilo halikuwa na tatizo hata kidogo, haraka sana Stephen akaanza kushughulika na dereva aliyekuwa ameambiwa. Ni ndani ya sekunde thelathini tu, risasi mbili zikaingia katika mikono ya dereva, hakuendelea kuushikilia usukani na hivyo gari hilo kutoka barabarani na kuanza kuingia korongoni kwa kasi.

    ***

    Abdul na Sharifa walikuwa wakikimbia kwa kasi, nguo ya harusi tena huku akiwa amepambwa vizuri ilikuwa mwilini mwa Sharifa lakini hakutaka kujali, alikuwa akikimbia huku akimfuata Abdul ambaye alimwambia kwamba mpenzi wake, Bruno alikuwa hai na hakufa kama alivyokuwa ameambiwa.

    Moyo wake ulikuwa kwenye majonzi mazito, hakuamini kama alithubutu kukubali kuolewa na mwanaume mwingine na wakati hakuwa na uhakika kama mpenzi wake aliyempenda kwa mapenzi ya dhati alikufa kweli au la.

    Walichukua dakika kumi kukimbia, wakasimama nje ya nyumba moja ambapo Abdul alimwambia kwanza wapumzike kwani walikuwa wamekaribia kufika kule alipoambiwa kwamba bruno alikuwepo.

    Walipumzika pasipo kuongea kitu chochote kile, baada ya dakika kadhaa, ikambidi Sharifa aulize vizuri kama kweli kile alichokuwa amemwambia kule harusini kilikuwa kweli au alimdanganya.

    “Bruno yupo wapi?” aliuliza Sharifa huku akimwangalia Abdul.

    “Nimeambiwa alipiga simu. Twende kwa Alfred, yeye ndiye aliyepokea simu kutoka kwake na kumwambia kwamba Bruno yupo hai,” alisema Abdul.

    Sharifa alionekana kukakasirika lakini hakuwa na la kufanya, walichokifanya ni kuanza kwenda kwa huyo Alfred huku akitaka kujua ukweli juu ya kile alichokuwa ameambiwa.

    Walipofika, kijana huyo akawaweka kwenye kochi na kuanza kuzungumza nao. Aliwaambia kwamba alipokea simu kutoka kwa Onyango na kumwambia kwamba Bruno alikuwa hai, tena aliongea naye mwenyewe.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Onyango?” aliuliza Abdul huku akionekana kutokuamini alichokisikia.

    “Ndiyo! Onyango huyohuyo!”

    “Yule aliyekimbilia Afrika Kusini?”

    “Ndiyo! Sijui wamekutana vipi lakini inaonyesha kwamba Bruno naye yupo Afrika Kusini,” alisema Alfred maneno yaliyomfanya kila mtu kushtuka.

    “Afrika Kusini?” aliuliza Sharifa huku akionekana kutokuamini.

    “Ndiyo!”

    Hilo halikumuingia akilini hata kidogo, alijaribu kufikiria namna ambavyo mpenzi wake huyo kufika Afrika Kusini kutoka nchini Kenya, alijaribu kujifikiria na kuunganisha safari ya kufika nchini humo lakini alikosa jibu kabisa, alibaki akishangaa, aliuliza mara nyinginyingi na Alfred alimwambia vilevile kwamba alikuwa Afrika Kusini.

    “Kuna kingine sasa! Kama unashangaa yeye kuwa Afrika Kusini, basi hili jingine utazimia,” alisema kijana huyo.

    “Lipi?”

    “Bruno ni bonge moja la bilionea!” alisema Alfred.

    “Bilionea?” aliuliza Abdul.

    “Ndiyo!”

    “Kivipi yaani?”

    “Huo ni umbeya niliopewa na Onyango, kawa bilionea kivipi, sijui, ila ni bonge la bilionea. Atakapotoka nchini Marekani, atakuja Kenya,” alisema Alfred.

    “Nchini Marekani?”

    “Ndiyo!”

    “Sasa Alfred unatuchanganya. Umesema Afrika Kusini, ukasema ni bilionea, sasa hivi unasema nchini Marekani, mbona hueleweki?” aliuliza Sharifa huku akimwangalia Alfred kwa macho yaliyojaa mshangao mkubwa.

    “Yaani hata mimi mwenyewe sikumuelewa Onyango mpaka pale aliponihakikisha kwamba jamaa kweli ni bilionea,” alisema.

    “Kivipi?”http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Alimwambia Onyango kwamba anahitaji namba yangu ya akaunti ili akutumie pesa. Nahisi zitakuwa zimefika manake nimeona mlio wa meseji, nafikiri ni pesa hizo,” alisema Alfred.

    “Mimi ndiyo sikuelewi kabisaaaa, naona kama unaongea Kirumi,” alidakia Abdul.

    “Hebu subiri!” alisema Alfred, akaingia mkono mfukoni na kutoa simu yake.

    Kulikuwa na ujumbe wa simu umeingia, hapohapo akaufungua na kuanza kuusoma. Uso wake ukajawa na tabasamu pana, baada ya hapo, akampa Sharifa ausome ujumbe huo, ulikuwa ujumbe mfupi uliosomeka ‘You have received 100,000 dollars from bank account number 0987225677890, (umepokea kiasi cha dola laki moja kutoka akaunti ya benki namba 0987225677890).

    “Umeona! Amesema hizi pesa amezituma kwa ajili yako,” alisema Alfred, hilo likawachanganya zaidi. Wakahisi kama kile kilichokuwa kikiendelea kilikuwa ni ndoto ambapo baada ya mudua mfupi wangeamka na kujikuta wakiwa kitandani.







    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog