Search This Blog

Monday 24 October 2022

KIMBIA, KIMBIA! [RUN NIGGER, RUN!] - 4

 

     







    Simulizi : Kimbia, Kimbia! [Run Nigger, Run!]

    Sehemu Ya Nne (4)





    “Samahani mama.” Hughes alianza kusema bila kumtazama mbwa aliyemsogelea na kuanza kumnusa miguuni huku sasa akiwa ameacha kufoka mara baada ya Diana kufungua mlango.

    Diana hakujibu.

    “Mimi ni mgeni wa Janet.”

    Hapo mama alibibitua midomo, kisha akaachia kicheko kifupi, kicheko cha dhihaka.

    Hughes alibakia akimtazama, kwamba wakitazamana.

    Mara kidogo, mama alijikuta akishindwa kumtazama na hivyo kupelekea kukilegeza kichwa chake hata kiliangalia chini, kwani ndivyo dhihaka ilitimka ikifukuzwa na aibu iliyoanza kukua kwa namna ya kushangaza!



    “Mama, sijui Janet yupo?” Hughes alirejesha ulizo lake baada ya ukimya wa sekunde chache huku akitabasamu.

    Diana aliinua kichwa bila kumtazama Hughes na kujibu kwa sauti ya chini, sauti ya taratibu huku akianza kufanikiwa kuitawala aibu yake, “hupajui kwake?”

    “Nime…?”

    Diana alimkatiza mara; ndio, alimkatiza kwa namna ingedhaniwa alikamata ujasiri fulani wa ghafla ndani ya zile jeuri na dhihaka zake, “hujamuona? Hapana…elewa nina shughuli za kufanya kiasi sihitaji kujua nani yupo ndani ya nyumba yangu na nani hayupo!”

    Hughes hakujali ufidhuli wa majibu, isipokuwa alianza kueleza kuhusu jinsi alivyomtafuta Janet kwa kumpigia simu bila mafanikio ikiwa ni pamoja na kueleza alivyogonga mlango wa eneo lake kwa muda mrefu bila kupata majibu yoyote zaidi ya kusikia sauti ya mziki.

    Kadri alivyozidi kueleza, ndivyo Diana alianza kuonyesha kubadilika hali kwa kujipiga mapajani huku akipumua kwa shida kutokana na kuonekana ishara za kujitahidi kujikaza ili kuzuia kasi ya kuhema ilivyokuwa ikimjia kama dalili za kukereheka na maelezo ya Hughes ambaye alimtazama mithili alikuwa ni ‘mteja aliyenona wa Janet’.

    “Skiliza mwanaume…narudia! Mimi sifuatilii wala sijali kujua wapangaji wangu wakiwa hawapo ndani mwao! wanawake ni wa burudani tu! Demu wako anaweza kuwa na mwanaume mwingine eneo fulani! Nenda zako huko, mwanaume!”

    Hughes alishikwa na butwaa asiamini kama maneno hayo yalitoka kwa mama huyu aliyemuona akithamini utu na uzee wake; hatahivyo, hakujulisha mshangao wake zaidi ya kufanya hivyo ndani ya mawazo yake!

    “Grab another pussy…hey! Be a man!”

    Baada ya kitambo kidogo cha kutafakari, Hughes alikamata uelewa fulani ambao hata ulimfanya ajikute akiingizwa kumueleza Diana kwa ujasiri huku akianika zile tabasamu zichomazo, “wakati mwingine umri si habari…acha upepo uingie kwako, au wasemaje?”

    Diana hakujibu zaidi ya kufanya utumbuzi wa macho kwa namna kama hakuelewa Hughes alimaanisha nini kwa usemi wake huo ingawaje huko ndani mwake alihisi kuziona nafasi za kujongelewa kinamna kama siyo sasa alikuwa akidhihakiwa yeye.

    “Mama hujazeeka nisikutamani!” Hughes aliirekebisha njia ya maana aliyosema awali.

    Diana aliacha kutumbua!

    Sasa alijua aidha tafsiri moja ilikuwa sahihi, kwamba alitakiwa afikirie ‘kujirudisha’ kwa saa kadhaa ndani ya ule uwanja wake ambao hakusita kumvuta mwanaume yoyote pindi alipoingia katika anga zake; lakini ile tafsiri ingine ilimfanya atulie kwanza na kuutazama upepo wenyewe ili kama ndivyo ulikuwa, basi naye angejibu vikali kwani hapo alikuwa nyumbani kwake na haki zake.

    Hughes alivyoona hata alianza kutazamwa kwa kurembuliwa macho, ndivyo kwa ndani alijisemesha hakuwa amekosea ingawaje pia aliitikia hoja yake fulani kwamba dunia ilikuwa ikielekea ukingoni…the big crunch!



    Kidogo na kwa sauti ya chini kiasi na kwa taratibu ndivyo Diana alijibu; ni kwamba, alijibu akidhihirisha huko awali ilikuwa ni kweli alijawa na husuda kwa mpangaji wake, “huko tulistaafu, ila ningewahi nafasi hii mchekewa yenye kuchezewa na asiyejua unono wa mwanaume.”

    Sasa akihakikisha alimuelewa Diana.

    Alisema tena huku pia akimshika mikono, “natamani urudi kazini kwa ajili yangu. Nadhani bado upo imara kuachia nisiyowahi kupewa.”

    “Wewe?” Diana aliuliza, lakini hakugoma kushikwa.

    “Mpigaji huingizwa ndani ili kuhudumia.” Hughes alisema tena huku akimsogelea Diana ambaye naye alianza kurudi nyuma akiingia ndani na hivyo kufanya Hughes pia aingie ndani.

    Hughes alikubali Diana alibadilika!

    Ndio, alikubali alibadilika kwasababu kadri sekunde zilivyokuwa zikitembea halikadhalika alipandwa joto!

    Lakini ukubali huo haukuwa eti alizembea kazi!

    Hapana, si kweli alizembea!

    Hapana pia si kweli hapo alitamani!

    Ila ni kweli kwa mwendo huo alikuwa kazini vilevile!







    Deborah Evans na George Boofy (mpenzi wake) walikuwa hospitali ya Muhimbili ndani ya jengo lililoandikwa juu yake, INSTITUTE FOR THE HUMAN BRAIN. Huko walikuwa eneo la wagonjwa mahututi katika chumba alichowekwa Marlon Evans lakini wakiwa ofisi ya Dr Holmes Dude ambaye alikuwa miongoni mwa madaktari bingwa kuhusu muundo na shughuli za ubongo wa mwanadamu.



    “Daktari, tafadhali naomba jitahidi kaka apone! Nahitaji kumuona amepona hata kama atakuwa ni kilema au vyovyote vile, kwani nitamuhudumia kwa hali zote…please, Doctor! Make it happens to your best!” Deborah alisema kwa masikitiko.

    Dr Holmes alitoa miwani yake, kisha alianza kusema huku sasa akimtazama Deborah; mikono yake iliacha kubonyezabonyeza vitufe katika sahani ya kompyuta yake iliyokuwepo pembeni ya meza yake kubwa, “nakubali ni kweli nimebobea katika habari za ubongo wa mwanadamu. Ni kweli pia hivi karibuni nimekuwa katika kiu kubwa ya kutafiti reconstructive brain surgery.” Aliacha kusema kwa muda, akawa akiisafisha miwani yake kwa kitambaa cheupe alichokuwanacho mkononi. Aliendelea kusema baadaye, “kama siyo risasi ya taya aliyopigwa kaka yako, basi nafasi yake ya kupona ilikuwa kubwa sana.”

    “Ina maana…sikuelewi…hatapo…?”

    “Nisikilize vizuri.” Holmes alimkatiza, “ile risasi ilitikisa kichwa chake kiasi mifupa kadhaa iliyovunjika iliweza kutumbukia ndani ya ubongo wake ambao pia umevurugika kwa kiwango kibaya.”

    Deborah alitingisha kichwa kwa masikitiko makubwa.

    “Napenda ujue…I’ll do the most kwasababu imani yangu ipo katika kupenda kusaidia watu. Ndio, habari ya Marlon hainihitaji kujua au kupata maelezo ya maisha yake ili niweze kumsaidia. Kwani sijali yeye ni nani ikiwa ni pamoja na kutojali kujua kwanini alipigwa risasi. Najali kujua maelezo ya kuumia kwake ili niweze kutoa maamuzi ya kitaalamu endapo tutaweza kumponyesha au la!”

    George Boofy alitulia kimya huku akiwa kauvuta mkono mmoja wa Deborah katika mapaja yake akibonyezabonyeza vidole vyake; na mawazoni mwake fikira zilimtupa katika kuona Dr Holmes alikata tamaa kumponyesha shemeji yake.

    “Tayari najua tungemshughulikia vyema kama sio hiyo risasi ya taya…bado natathmini hali aliyonayo sasa huku tukiendelea kumuacha kwa muda akisaidiwa kuishi kwa msaada wa mashine.” Dr Holmes alisema zaidi.

    “Kitu kinachonipa nguvu kwamba ninayo nafasi ya kuokoa maisha ya kaka yako ni hii,” Holmes aliendelea kusema; na sasa aliongeza sauti yake, “kwanza nimeweza kuondoa karibu vipande vyote vya mifupa, na mpaka nitavitoa vyote. Pia utafiti wangu umenipatia njia za kuweza kurekebisha maeneo ya ubongo yaliyoharibika kwa kuongeza nguvu zaidi kwa yale maeneo mazima ili kuchukua nafasi za traumatized tissue katika kutenda.”

    “Ninaamini Backup system ya ubongo haina ukomo, kwani taasisi iliweza kugundua huko nyuma kwamba endapo kipande kimoja cha ubongo kikishindwa kufanya kazi zake, basi ndivyo kipande kingine huweza kuziba nafasi yake. Tuseme, licha ya kila kipande cha ubongo huweza kufanya kazi zote za vipande vingine, pia kipande hicho kinaweza kufanya kazi zote peke yake kikilazimika!”

    Hakuna aliyesema kitu; wote walisikiliza kwa shauku huku Deborah akiomba kimoyomoyo Mungu amuwezeshe Dr Holmes kuweza kumponya kaka yake.

    “Ila tumaini hili lina vikwazo ambavyo bado taasisi haijaweza kupata maelezo ya kuridhisha kama inawezekana kukishawishi kipande kilichoharibika kuweza kutokata tamaa ya kuweza kurejea katika kutekeleza wajibu zake ili kuboresha nguvu za vile vipande vizima vya ubongo.”

    “Tatizo hili maana yake ni kwamba kama tutashindwa kukifanya kipande kilichoshindwa kutimiza majukumu yake, basi ndivyo wasiwasi mkubwa unakuwepo kwa vipande vingine kuweza kutekeleza majukumu yote kwa pamoja bila kushuka chini ya mstari wa ufanisi unaotakiwa…vipi kaka akiishia kuwa dhaifu au mlemavu katika meneo kadhaa kwasababu hivyo vipande vizima vinaishiwa nguvu kutenda mambo kikamilifu?”

    Hawakusema chochote.

    “Ndio. Kwani upo uwezekano, hatimaye kipande kimoja baada ya kingine katika vile vizima vitapata hitilafu pia kabla ya vyote kuharibika! This is the problem I must tell if we shouldn’t let him die normally!”

    “Wengi hawaamini inawezekana kuukarabati ubongo wa mwanadamu bila kumuua…mimi nitathibitisha, tunaweza! Nendeni mkiamini Marlon ataamka tena ingawaje zipo sehemu chache sana ninaweza kutofanikisha katika kurejesha katika awali yake. Marlon atatembea, Marlon atasema, Marlon atajitegemea akiwa na akili timamu.”

    “Thank you.” Wote walijibu kwa kuchanua furaha zao.

    “Mimi pia nitashukuru nimefanikisha,” Dokta alijibu huku akivaa miwani yake. Kisha alisema tena, “katika surgery iliyofanyika tayari, mgonjwa ana uwezekano wa asilimia 50 kurejewa na akili zake huku tukibakiza uwezekano wa asilimia 0.02 kwa surgery ambayo bado haijafanyika. Hapa yapo mambo kadhaa ya kitaalamu ili kuipandisha asilimia hii ili angalau kwa ujumla niwe nimerudisha hali yake kwa asilimia 80 hivi ya utendaji wake kabla ya janga lake kumpata.”

    George Boofy alikurupuka kusema huku akitumbua macho, “Dr! Sasa ukiishia asilimia 50 au hata huko 80…mmh! Yaani, huoni tayari shemeji atakuwa taahira? Vipi, ataweza kukumbuka mambo? Ataweza kujiendesha kwa akili zake? Kweli itawezekana Dr? Kwakweli naona…aah…?”

    Dr Holmes Dude alimkatiza; lakini bado alisema kwa utaratibu huku uso wake ukibakia vilevile wenye alama za ujali na umakini wa kazi, “Usijali. Najitahidi utahira usiwepo…you know, the fact so many areas in his brain are already dead! But it’s this…nataka kumfufua!”

    “Mmh?”

    “those areas are clinically dead!”

    “Kwahiyo ni marehemu? Dr?” Deborah alidakia mazungumzo huku akisimama; tayari alihisi hali za kizunguzungu kutaka kumnyemelea.

    Boofy alimshika mkono na kumuomba atulie, “cool down babe! Get on chair!”

    “Kaka amekufa?” Alirudia kuuliza huku akielekea kuanza kutii kuketi huku ishara za Boofy kutaka kuinuka pia zikijianika kutokana na mwili wake kuanza kutotuliatulia kama awali.

    “Sijasema amekufa, isipokuwa zipo asilimia amekufa!” Daktari alijibu kwa sauti kubwa kiasi.

    Boofy alishusha pumzi nzito, na kisha ndipo aliketi huku uso wake ukinyon’gonyea hasa; na macho yake yalijaa mashaka!

    “Usiwe na shaka, tutafanya! Nitafufua kiasi kizuri katika zilizokufa kwa kuziimarisha tissues zilizo nzima ili ziambukize uzima palipo ufu au ubovu!”

    Deborah alitetemeka!

    “Upo uwezekano wa asilimia 20 kuzikarabati sehemu zilizoharibika ili ziweze kurejea majukumu yake.”

    Hapo Deborah na Boofy walijikuta wakitazamana bila kusema chochote huku macho yao yakionyesha kuwasiliana kwa namna ambayo haikuweza kujulikana.

    Daktari aliona yote, lakini hakujali; aliendelea na maelezo yake, “his probability of partial recovery is at least 20 percent.”

    Boofy aliacha kumtazama Deborah, na kisha aliuliza vilevile kimkurupuko, “una maana gani?”

    “Tunazungumzia uwezekano kwa kuanzia kwamba, Marlon ataweza kupumua mwenyewe, ataweza kujua mazingira yanayomzunguka huku akiweza kuwasiliana na ulimwengu nje ya mwili wake. Ninaamini chini ya hapa siwezi kuita mgonjwa amepona ingawaje anaweza kuwa technically conscious. Ndio, bado ninamchukulia Marlon amezirahi ingawaje ni kweli najisikia si kitendo chema cha kibinadamu kumuacha aendelee kuishi ndani ya maumivu makali haya kwa madai eti haumii kwakuwa hawezi kuyawasilisha! Kwangu haya mazingira aliyomo ni mabaya sana yasiyoweza kubebeka hata kwa siku mbili! Machine zinalazimisha aendelee kuumia kwasababu zipo ili kugoma asife wakati tayari eneo zingine zimekufa tayari!”

    “And fully recovery?” Boofy aliuliza tena huku umakini wa kusikiliza ukionekana katika utazamaji wake.

    “Too much tissue has been destroyed, there will be no total healing! Ni kwamba, I’m…aah, we’re trying to recover a remarkable number of his faculties! (Sehemu nyingi zimeharibika, haiwezekani kurekebisha kwa asilimia mia!)” Aliishika pua yake kidogo, kisha akavaa miwani yake kabla ya kuanza kumtambaza ‘panya wa kompyuta’ huku akisema kwa sauti ya chini kiasi, “Narudia. Atatembea, atasema, atafikiri, ataona, atasikia…mmh, hata hisia atakuwanazo! Mmh, ndio…emotion, emotion! Yees, he’ll have emotion or he could recover any combination of those abilities.”

    Holmes Dude hakusema tena, isipokuwa aliinamisha kichwa chini akitafakari maneno aliyoeleza hasa habari ya uwezo wa kumrejeshea mgonjwa ‘hisia zake’.

    Kuona hivyo, Boofy alifanya mithili alivuta ndani makamasi lakini huku macho ya udadisi yenye ishara kadhaa za ubishi yakizalisha utazamaji wake kwa kumkodolea daktari ambaye bado aliinamisha kichwa.

    Lakini, hatahivyo, Holmes hakufanya sana kwani hakusogea kwa zaidi ya dakika tayari aliweza kuahirisha fikiri hizo ili zisiweze kuleta dhana mbaya kwa wateja; na ndivyo aliinua kichwa chake hata kufanya macho yake kukutana na yale ya Boofy. Wakati huo, Deborah alikuwa kainamisha kichwa huku kakilaza kiasi pembeni mwa bega la Boofy; na mikono yake iliziba uso wake kwa namna kwamba alikuwa akilia mithili akiamini kaka yake asingeweza kupona kama daktari alivyojaribu kueleza







    ALHAMISI, 9/11/1989:

    Pamoja na uso wa John Hughes kuzalisha tabasamu zaidi mara baada ya kumaliza kuurejesha mahala pake mkono wa simu ya mezani, hatahivyo, bado hali hiyo haikuwa lile tabasamu ambalo huliachia awapo ndani ya ridhiko zake; ndio, hapo haikuwa hivyo pamoja na kutabasamu huko. Isipokuwa hapo alikuwa bado hajatolewa ndani ya sumbufu za mawazo kuhusiana na kesi ya mauaji ya Brigitte; na ndivyo ilikuwa mara baada ya kujiachia kwa kukilalia kiti chake, sumbufu za mawazo ziliichukua tena ile sehemu iliyomfanya atabasamu kiasi.

    Sekunde chache baadaye, alijiondoa katika huo mkao kwa kuketi wima huku macho yake yakikodolea faili moja lililokuwepo mezani kwake kwa namna kwamba wazo fulani hivi ndani ya mawazo yake lilikuwa limemchota.

    Tena akarejeshwa kutabasamu.

    Naam, ni zaidi alitabasamu akitazama hapo.



    Ni kwamba, ile simu ilitoka kwa Dr. Dickman aliyempigia ili kumpatia maendeleo ya mtuhumiwa Michelle Obrien tangu wamalize kumfanyia operesheni. (Tangu Obrien na Marlon kulazwa hospitali ilikuwa sasa yapata zaidi ya miezi miwili huku bado kitendawili cha kujua ni kwanini na akina nani walihusika na mauaji ya Brigitte kikiwa hakijaweza kuteguliwa, kwani ugumu zaidi uliongezeka kutokana na utokezaji wa utata kadhaa.)

    Daktari alieleza si kwamba Obrien aliondolewa ndani ya chumba cha wagonjwa mahututi ambako alikuwa akiishi kwa msaada wa mashine hadi pale alipomaliza kufanyiwa operesheni, bali sasa alikuwa amezinduka ingawaje bado alihitaji muda zaidi wa kupumzika ili kuruhusu kumbukumbu zake kuweza kumrejea kama kawaida!

    Hili ndilo lilimfanya Inspekta Hughes aweze kufurahi kidogo, kwamba taarifa hizo aliziona kuwa zilifanya mchango mkubwa katika kumsogeza karibu zaidi na hitaji zake za kufikishwa kumhoji Obrien, ingawaje kwa upande mwingine akili zake zilisita kwa kutahadharisha kuwa bado nafasi hiyo aliyokuwa akihitaji sana ingeweza pia kuwa ‘ukuta mwingine’ katika kumrejesha nyuma kwa kumsimamisha palepale kama siyo kumtupa mbali zaidi na habari alizotegemea kuzinyaka kutoka kwake.

    ‘Nikiweza kupata majibu safi kama kweli huyu atapona, basi pengine nitaweza kujua ni kwanini huyu Mbilikimo anamficha Edwin kwa kutetea hayupo nchini wakati ushahidi mwingi unaeleza vinginevyo.’ Hughes aliwaza, ‘halafu, Janet Babatz kauawa!’

    Mawazo hayo yalimsukuma kubadilika mara, na hivyo kasi ya tabasamu lake kuanza kurudishwa nyuma huku hasira zikiashiria kuanza kuchukua mkondo. Na alipomfikiria Marlon Evans, hapo ndipo alijikuta akikunja ngumi na kujipigiza mezani huku sauti ya kufoka ikimtoka!

    “Ni kwanini lakini?”



    Lakini kidogo tena…alisikia sauti!

    Akatazama mlangoni!

    Akaduwaa kwanza!

    Wala hazikupita sekunde zaidi ya kumi hivi, tayari alibadilika akijikuta akitulia huku mapigo ya moyo yakianza kurejea ndani ya kawaida huku mdomo ukiicheza tabasamu fulani, tabasamu iliyotengenezwa kwa hisia za mahaba na ikijazwa mahaba!



    ***

    Mlango ulifunguliwa, akaingia mama mmoja mnene aliyevalia mavazi ya kipolisi; na huyo alifika mbele yake, akaivua kofia yake huku tayari kasimama wima.

    Saluti kali ikamtoka!

    John Hughes akatabasamu huku akimtania, “pamoja na ukweli sipendi hunifanyie hivyo, hatahivyo unapendeza sana hivyo unavyofanya!”

    “Bosi si vema kuweka masihara kazini hata kama sisi ni wapenzi…wanoko watatunusa.”

    “Tusiishi kwa kuogopa sana, mapenzi ni uhuru wetu,” alijibu Hughes huku akiinuka, “ebu sogea nikuguse. Acha hizo mpenzi!”

    “Honey, mbona hunigusa kuliko hata mume wangu asiyechoka kusafirisafiri!” Julieta alijibu; bado alikuwa kasimama ingawaje sasa alifanya kwa kujilegeza kiasi huku macho yake makubwa yakifanywa kusinziasinzia.

    Sasa Hughes alikwishatoka ule upande mwingine wa meza, kule kwenye kiti chake; na baada ya kumsogelea karibu, alishika mikono ya Julieta na kumvuta huku mdomo ukijitayarisha…

    Ndivyo kofia ilidondoka!

    “Bosi…bosi, ebu acha kwanza,” Julieta alisema kwa kulalama huku sauti ikitokea puani, pia alijaribu kupeleka uso wake pembeni ingawaje kila alipofanya ndivyo Hughes alimvuta zaidi huku akimsogeza zaidi…

    Hata alipigwa!http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Hata naye alipiga!

    Yaani ilikwenda utadhani haikuwa kweli Julieta alikuwa mbishi kupigwa!

    Kwamba, ndivyo ndimi zao zilichokozana, zikikandamizana huku mihemo ya raha ikitengenezwa…

    Baada ya kukurukakara za kupeana mabusu, Julieta alijibandua kutoka mikono ya Hughes ambayo ilikuwa imepunguza nguvu za kumshika.



    Julieta alipiga hatua moja nyuma kabla ya kugeuka mwili mzima na kuanza kuinama chini ili kuiokota ile kofia.

    Hapo ndipo ‘mbinuko’ ulitazamika vyema huku mapaja yake yakifanya vurugu katika kusaidia mtikisiko!

    Mtu na ulafi wake vikazidisha mambo kiasi Hughes alijikuta akimsogelea tena kwa kupiga hatua moja mbele; na alipomfikia, taratibu, mikono iliivuta juu sketi…

    Hughes alihema sana baada ya mikono yake kukizunguka kiuno chake huku akimuinamia.

    Mikono ilipochezea tumbo, Julieta aliweweseka zaidi kiasi almanusura adondoke chini kama siyo kuzuiwa na ile mikono ya Hughes!

    “Mpenzi niache!” Alilalama Julieta.



    Kitambo kidogo, Hughes alimuachia.

    Julieta akainuka, akageuka na kumtazama Hughes kwa macho ya kitandani huku akiguna, “Uuh!”

    Hughes akaachia meno nje, kisha alisogea pembeni na kuikota kofia; lakini hakurudi mezani kama alivyopanga ili kuiweka kofia ile, kwani Julieta alimzuia kwa kumshika mkono kabla ya kuanza kumueleza kwa njia ya kubembeleza, “mpenzi, muda huu si mzuri.” Alinyamaza kidogo, akaacha kuushika ule mkono wake huku kabla ya kusema akiachia pumzi nzito ilifuatana na mguno ambao ulizungumza kwamba hata yeye tayari alitayarishika ili kupelekewa raha zake, “kwanza, afande Kanyengele anataka kukuona. Yupo ofisini kwangu…aah, ona sasa…zimeamka wakati mbaya!”

    Hughes pia alipumua zaidi huku akiduwaa!

    Julieta akamshika tena mkono, akishika ule mkono ulioshika kofia; kisha alisema tena, “mimi ni asusa wako, tukitoka kazini ukanicheze! Niruhusu niondoke…Kanyengele atahisi vibaya!”

    Hapo ndipo Hughes alikurupuka akisema huku akiruhusu mkono wake kupokonywa ile kofia, “kupenda huku…mh!”

    “Usidanganye bwana! Utapenda wangapi?” Wivu ulimkonyeza kidogo Julieta huku akiiweka sketi yake vyema baada ya kumaliza kuvaa kofia.

    Hughes hakujibu; alirejea kitini na kuketi akijitahidi kupunguza hemaji zake.



    “Mruhusu, mmh! Ndiyo…” Hughes alifikirifikiri, na kidogo tena aliendelea huku akiinua mkono wa simu ile ya mezani, “mmh, baada ya dakika tano hivi unaweza kuruhusu…halafu…ndio, halafu…eeh, mwambie nazungumza na simu muhimu. Sawa eeh?”

    Julieta alibibidua midomo yake, akageuka kwa madaha na kusema huku akianza kupiga hatua ambazo alijua huko nyuma ziliacha kizaazaa, “ungekuwa mume wangu, usiku wote ungekuwa ni…wow, shabash!”

    “Niwe mara ngapi?” Hughes alitania huku macho yake yakibandika tazamo katika ‘mbingiriko’ uliokuwa ukitemeshwa kashkash za aina yake kiasi zile hemaji zilisogea tena mbele katika kuzidisha ‘upashaji moto’.

    Julieta alipofika mlangoni alisimama, akashika kitasa cha mlango; na kabla ya kuufungua, alijigeuza kidogo huku kichwa kikigeuka zaidi kiasi cha kufanya macho yake yaliyokuwa yamerembushwa kwa makusudi kuweza kumtazama Hughes ambaye hadi wakati huo alikuwa bado ndani ya zile tazama zake na akishindwa kuzifikuza zile hemaji za kilafi.

    Kisha sauti ya kutokea puani ilimtoka tena Julieta, “mwee…hiyo mimacho…aku!”

    Hughes hakusema tena.



    ***

    Kanyengele aliingia ofisini kwa Hughes baada ya dakika saba hivi tangu kuondoka kwa Julieta; na wala hakutoa saluti kama ilivyo desturi. Alifika na kuketi kitini huku akiwa mwanzilishi wa kusalimiana kwao katika hali za kirafiki na matani.

    Ndipo punde kidogo, mazungumzo rasmi yalianza.

    “Nilikupigia simu ufike ili nikujulishe habari mbili za hii kesi yetu ambayo nasikitika sana hadi sasa hatujaweza kusogea hatua nzuri katika kuifikia tamati.” Hughes alisema taratibu huku sura yake ikijibu masikitiko hayo kwa namna alivyokuwa akionekana.

    “Afande, naamini hatupo mbali hivyo, kwani data tulizonazo zinaweza kutufungulia njia ili kuanza kuimaliza kesi kwa kasi ya kushangaza…but real difficulties are about to come against! Dem comin’ I sense!” Kanyengele alijibu kwa kujiamini.

    “Tuombe hivyo,” Hughes alianza kusema tena, “mkuu kanipatia taarifa kuhusu mtu mmoja ambaye mara nyingi ndiye huwa pamoja na Edwin.”

    Kanyengele alijilaza zaidi katika kiti chake kwa maana ya kutengeneza usikivu imara.

    “The grapevine is heard Edwin is hiding even from his family with the fact that he didn’t travel! (Minon’gono inasema Edwin amefichwa hata familia haijui huku ukweli ukijianika hakusafiri!)”

    “Hana kawaida ya kusafiri bila kuitaarifu familia…na pia mkewe ameanza kuonyesha hali za wasiwasi juu ya maisha ya mumewe kiasi minon’gono inadai kumsikia akilaani kukubali kusema uongo.”

    “Sometimes hearsay lead to reality…uongo upi huo?” Kanyengele aliuliza.

    “Eti alishinikizwa kusema uongo na rafiki wa Edwin ambaye ninayo picha yake hapa!” Hughes alisema, kisha alitoa picha na kumpatia Kanyengele.

    Katika picha hiyo alionekana mwanaume mmoja akiwa kifua wazi akidhihirisha alikuwa ni mtu wa mazoezi, kwani kwa kiasi kikubwa alikuwa pandikizi la baba ingawaje si kwa kiasi cha kutisha!

    Kanyengele aliendelea kuitazama picha bila kusema.

    “Pili,” Hughes alianza kusema tena kiasi alimfanya Kanyengele aache kuiangalia picha hiyo kwa muda ili kumakinisha bongo katika kile Hughes alichokuwa akieleza, “nimepigiwa simu muda si mrefu na dokta Dickman.”

    “Enhe?”

    “Obrien ameondoshwa intensive care!”

    “Yees!” Kanyengele alisema kwa kuropoka huku akianika meno nje kwa kuvamiwa na furaha.

    “Anahitaji mapumziko bado…kumbukumbu hazijamjia.”

    Hapo Kanyengele alinuna!







    “Halafu, mtu aliyetumwa kufuatilia nyendo za nyumbani kwa Edwin ana dukuduku kwamba Edwin amefichwa huku familia yake ikiwa pia haijui!”

    “Edwin amefichwa au amekimbia? Huyu bwana…kama vile kesi imebakia kumtafuta kwasababu ndiye muuaji tunayemsaka!” Kanyengele alifungua kinywa chake tena huku akionyesha kuwa ndani ya tumaini fulani ingawaje huko mawazoni mwake hilo lilisimamishwa kama tumaini lililokuwa upande wa pili wa kisu lenye kuweza kuumiza mtu kwa mbali sana huku uhakika wa kutomkata ukiwa zaidi ya asilimia mia.

    “Inawezekana, lakini sidhani ipo nafasi sisi kuanza kufikiri huko! Sawa. Obrien akipona ipo hatua nzuri tutakuwa tumepiga…naweza kushawishika ule ugomvi haukuishia De-paradise!”

    “Bado nina wasiwasi zaidi kwamba Edwin anaweza kuwa ndiye pia alimuua Janet ili kuziba ushahidi kabla hajajitokeza…halafu huyu mzee Kasonzo anaweza kuhusika kusaidia kujificha kwake kwakuwa Edwin anaonekana kuwa mtu wake muhimu sana hata kama bado dhana hii haijasimama sawasawa…ndio, angalia maelezo ya antidrug squad! Nakuambia, yanapeleka hisia hizi tusiziache hivihivi!”

    “Maybe.”

    “Sasa hii picha…hivi tuanzie wapi? De-paradise tena? Nyumbani kwa Edwin, hapana…huko tutaharibu mwendo! Mmh…vipi kwa yule demu wako wa…ooh…eeh, hukohuko De-paradise!” Kanyengele alisema huku akirejea kuiangalia picha ile.

    “Sawasawa…nitajisogeza zaidi kwa yule demu. I’ve the number.” Hughes alijibu huku akitabasamu; na hata Kanyengele alitabasamu pia. Baada ya sekunde mbili tatu hivi, Hughes aliendelea kusema tena, “wewe nenda nyumbani kwa marehemu Janet ukajaribu kumuulizia mama mwenye nyumba hasa yule mpangaji mwingine…ila yule mama sidhani kama anaweza kutusaidia! Siku ile nilipogundua mwili wa marehemu, niliona tabia zake za kuchukia polisi…some people bwana!”

    Lakini Hughes hakueleza alivyozijua tabia za yule mama mwenye nyumba (Diana); ndio, hakutaka kwasababu alihisi aibu Kanyengele kujua ukweli kwamba aliweza kumjua vizuri Diana kutokana na ‘kumbanjua’!

    Pia hakutaka kwenda huko kwasababu bado alikasirishwa na ishara za kuchukiwa baada ya kujulisha alikuwa askari aliyekuja kumuhoji Janet, kwani Diana alithibitisha kuzidisha majuto yake ya kujisogeza vile kwa Hughes kila alipokuwa akiombwa asaidie kupeleleza maisha ya Janet kabla hajagundua tayari alikuwa nyumbani kwake akiwa ameuawa kwa kupigwa risasi.



    ***

    Walipomaliza kuongea habari za kazi, Kanyengele alianzisha mwendo mwingine wa mazungumzo, “Bosi! Lakini huyu sekretari wako angekuwa sio mke wa mtu ningejaribu kumposa maana amekidhi sifa ninazohitaji.”

    “Unanitania sasa!”

    “Hapana afande…I’m seriously!” Kanyengele alijibu huku akijaribu kumsoma Hughes huku moyoni akisema si kweli angemposa mwanamke huyo kutokana na kushangazwa na ishara kwamba hata aina hiyo bado wapo wanaosaliti ndoa zao, kwani tayari alihisi uwepo wa mapenzi kati yake na Hughes isipokuwa ‘alikauka’.

    “Ok. Ok. Ni kwanini ungefanya?” Hughes aliuliza huku alama za mashaka zikijitengeneza katika utazamaji wake.

    Kanyengele alifikiri kidogo huku Hughes akimtazama. Kisha alijibu kwa kueleza kwamba kwa kulinganisha na wajihi na tabia za mwanamke aliyechorwa kichwani mwake, aliona Julieta alifanana na mwanamke huyo.

    “Unajua ili kuwa ndani ya sahihi katika mapenzi wa dhati kunahitaji kuijua vyema sanaa ya mapenzi, kwani mapenzi ni sanaa inayohitaji hekima na uelewa fulani wa hali ya juu ili kuweza kuibuka mshindi ingawaje bado ni vigumu sana kuendelea kudumisha huo ushindi.” Alisema zaidi Kanyengele.

    “Ushindi wa kuopoa au ushindi gani unaosema…you cut me off!” Hughes aliuliza huku wasiwasi fulani ukimtambaa mawazoni kwamba pengine tayari ‘mchezo wake’ na Julieta ulijulikana maana alimjua Kanyengele kwa mwendo wa mafumbo katika kujulisha habari.

    “Katika mapenzi ukiyafanya ndivyosivyo utaambulia mateso na wakati mwingine unaweza ukalaani kwanini ulikutana na mpenzi uliyenaye.” Kanyengele aliendelea zaidi huku akiboresha uchanuzi wa tabasamu, “nimebaini siku nyingi kwamba huyu dada alimiliki sifa hizi, lakini sasa naona zipo kasoro fulani!”

    “Kasoro?”

    “Afande kama ni wako, sitazoza!” Kanyengele alisema kwa macho makavu akikwepa kufafanua zaidi, kwani sasa aliona hadi hapo ilitosha kujulisha ili kuona kama hisia zake zilipatia au ndivyo yeye auanzishe mwendo aliohitaji aupatie kibali.

    Hughes akatumbua macho!

    Kanyengele naye akatumbua kwa makusudi!

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ndio, Kanyengele hakuwa ‘mroho’ kama Hughes ingawaje alitegemewa kuwa hivyo kutokana na kuwa bado aliishi ukapera. Isipokuwa, ni sahihi alikuwa ‘mroho’ pale alipozin’gamua sifa fulani zilizoshabihiana na mwanamke aliyetamani aishie kuwa mkewe; lakini bado alikuwa ‘mchoyo sana’ kwa mwanamke aliyekosa chini ya nusu ya sifa hizo katika kumlegezea tamaa zake ili zishinde hata kama ni yeye ndiye alikuwa mwanzilishi mtamani!

    Hapo alimuona Julieta alivaa sifa zilizokuwa na mvuto wa kusumbua ‘uroho wake’ ingawaje alijua huyo hakustahili kuwa mume wa mtu, kwani aliziona ishara za usaliti zikimtikisa sana hata kama ingekuwa si kweli hakuwa ‘mali’ ya bosi wake; na ndivyo, alitaka kupata uhakika kama alikuwa ‘mali ya bosi’ kama hisia zake zilivyotengeneza tafsiri hiyo ili ajue kama asitishe zoezi la kumfukuzia.

    Ni kwamba, kwake mwanamke safi alihitaji kuvaa sifa zote kama kichwa chake kilivyojua huku pia akitambua kwamba nafasi ilikuwa pana kwa mwanamke kuzivua, kuvuliwa au kupunguzwa sifa hizo kutokana na ushawishi na nguvu za mazingira aliyomo; lakini bado hata kwa mwanamke wa ‘kujirusha’, yeye alihitaji kumuona akiwa na angalau sifa ya kwanza na ya pili.

    Yaani, kwake mwanamke yoyote katika uhusiano wa kimapenzi alipaswa asipungue sifa mbili ambazo ndizo aliziweka katika daraja za juu huku akikubali zingeweza kupungua katika mazingira yaliyoletwa na hali za uvamizi wa uzee au mwanamke mwenyewe kuamua kuishi kwa kutojipenda na kujithamini na akiishi ‘mpaukaji kitandani’.

    Lakini katika hali yoyote kama mwanamke aliishi ‘mpaukaji kitandani’, basi yeye hasingemuhitaji; kwani vinginevyo, huyo alikuwa tayari ni mkewe ambaye uzee au ugonjwa usiotibika ndio umemtenda hivyo.

    Basi ndivyo alipomtazama Julieta alikubali alikuwa na sura nzuri na umbo la kuvutia huku akiziona ishara pevu kwamba sanaa ya mapenzi alijua kuitumia.

    Alikubali Julieta alikuwa mkarimu na mcheshi, akiwa hana vijitabia vya ajabuajabu. Lakini alikuwa na wasiwasi kama alikuwa mvumilivu na aliye tayari kwa raha na shida; na hii ilitokana na zile hisia zake kumsogeza katika kumuona alikuwa msaliti wa ndoa yake, jambo ambalo ndilo lilimfanya amuone angeweza kuwa ‘raha’ isiyomn’gan’gania katika kipindi hiki akiwa bado kapera akisubiri kutokea kwa ‘sahihi wake wa kuzikana’.



    “Wewe ni kijana wangu kikazi, halafu pia ni rafiki yangu ambaye huruhusu nichezee kitanda chako kwa ajili ya raha zangu.” Hughes aliamua kujibu, “ebu nieleze kama wapo wengine wanajua?”

    “Kujua nini?”

    Hughes alitulia kidogo, kabla ya kujibu kwa sauti ya utulivu na uhakika, “ni kwamba, mimi ndiye mswaki wa Julieta kutokana na mumewe kutokuwa na muda wa kutosha kumsukutua vyema!”

    “Duh…wewe ni afande kiboko!”

    “Wapo wengine wanajua?” Hughes aliuliza swali la awali huku akivuta kiti kuonyesha alikuwa makini ili kujua.

    Kanyengele hakujibu, kwani mawazo yake yalishangaa kwamba ni kweli hisia zake zilinena kwa kupatia!

    “Nijulishe basi.” Hughes alisisitiza ili kujibiwa.

    Kanyengele alitazama pembeni, kisha akaachia pumzi ya kusalimu amri kabla ya kuanza kujibu, “wewe ndiye umenijulisha ingawaje hisia zangu zilikuwa zikilazimisha nielewe hivyo umevyonijulisha…ok, endeleeni.”

    Kanyengele aliinuka, kisha alisema tena, “hisia zinasema mkuu wetu mpya anakuogopa kila mnapokutana…nahisi uhisi macho yako humvua nguo kila unampomtazama!”

    Hughes alicheka.

    “Unacheka?”

    Bado akichekacheka, Hughes alibadilisha mazungumzo, “nimefanya copy tayari, unaweza kuondoka na picha. Halafu, kwanza nakwenda home kucheki hali ya mama na mtoto.”

    “Bosi wangu ungetulia sasa, tuachie sisi vijana!”

    Hughes hakusema; alitabasamu.



    ***



    Baada ya dakika kumi hivi tangu Kanyengele alipotoka ofisini, Hughes alibonyeza kitufe fulani katika simu ya mezani ambapo ndani ya sekunde tano tayari ilisikika sauti ya Julieta kupitia spika za nje za simu hiyo.

    “Bado yupo hapo?” Hughes aliuliza.

    “Nani?”

    “Kanyengele.”

    “Aah…ndio, anatokomea! Kwani nini tena?”

    “Hamna kitu…ebu njoo.”

    “Afande…?”

    “Ebu njoo!” Hughes alimkatiza kwa sauti utadhani alikasirika, kisha alikata mawasiliano.



    Muda kidogo, Julieta aliingia ofisini huku kanuna; lakini alipogongana na tazamaji ya Hughes, kwa mwendo wa haraka alijikuta akijiondoa huko na kuanza kutabasamu huku akiumauma meno!

    Alipofika mezani, alisemeshwa kabla ya kuketi, “vipi kama ukifunga vizuri huo mlango?”

    “Hapana darling!” Julieta alipinga, na kisha aliketi bila kusubiri majibu huku tabasamu likiwa limepunguza mwendo kwani hata kujiumauma aliacha. Hatahivyo, alikwepesha macho yake kugongana na Hughes kwa kuangalia chini.





    Hughes alifikirifikiri kidogo kabla ya kusema tena kwa kuuliza swali jingine, “jumamosi utakuwa free?”

    Julieta aliinua kichwa, akamtazama kidogo; na alipoacha ili kurejea kutazama chini, mara kicheko kifupi kilimtoka kabla ya kujibu huku akirejea kujiumauma, akirudisha mwendo wa kutabasamu, “sijui nikujibuje.”

    “Au jamaa karejea?”

    “Hata akirejea, ni sawa na hayupo!” Julieta alisema kwa unyonge, lakini ajabu aliishia kucheka tena huku akirembua macho ambayo bado hayakuruhusiwa kumtazama Hughes.

    “Nakuhitaji jumamosi.”

    “Wee mwanaume…mkeo si akaribia kuzaa? Elewa angehitaji uwepo wako kipindi hiki…au unataka yeye pia awe kama mimi? Nyinyi wanaume…hapana!”

    Julieta alimtazama Hughes, akifanya kwa chati.

    “Nakuhakikishia niwapo na mke mkubwa kwa dakika kumi tu, basi uacha nimemtosheleza asihitaji baada ya siku kadhaa! Nampenda mke wangu. Nakupenda na wewe huku nikijua ninao wajibu katika kuhakikisha dozi zote unazipata ili usihuzunike kwamba mahitaji yako hayakidhiki…ok?”

    “Lakini mkeo haitaji hayo mahitaji, anahitaji wingi wa uwepo wako…au ndivyo bado unamliza? Wewe?”

    Hughes alicheka kwanza, kisha ndipo aliachia sauti yake huku akitalii utazamaji wa Julieta, “nikisema humtosheleza, sina maana hiyo! Ni kwamba, nikiwa naye uhakikisha nimemchezea hata ujichokea na kulala zake akiwa hoi mithili zeze lilichezwa!”

    Julieta alihema akihisi raha, kwani sehemu ya maneno hayo iliweza kuzitekenya awaa zake za nafsi kiasi alizidi kukiri alimzidi sana mumewe mbele za mahitaji yake!

    Kweli alitekenyeka!

    “Sasa nenda…utanipigia simu kesho ili nipate muda wako mzuri hiyo jumamosi ni upi! Anza kujitayarisha kwamba tutapambana mechi ya kufa mtu!”

    Hakujibu zaidi ya kujiinua taratibu; kisha alimtazama Hughes kwa macho ya usingizi huku bado akihema zaidi ya kawaida.

    Hughes alinyoosha mkono wake wa kulia; Julieta pia alifanya, lakini yeye alimpelekea hadi ukashikwa.

    Hughes akauvuta hata aliubusu.

    “Nakupenda.”

    Julieta alihisi kunyeshewa mvua kiasi aliuvuta mwili wake kindani kwa namna ya kujikunyata; kwani tayari alijichukua msalimishwa mbele ya himaya ya Hughes huku hisia zake zikiridhika huko ndipo ilikuwa sahihi kwa mwili wake kuendeshwa kwa kudhibitiwa!

    Mtekenyo ulikuwa maridhawa sana kiasi alihisi pengine hata alianza kuvuja!

    “Nakupenda.” Hughes alinena tena huku akiuvuta zaidi mkono wa Julieta katika kufanya mwili wake uanze kumjongelea; na ndipo hata mkono mwingine ulipeleka usaidizi, kwamba, kichwa kikasogezwa huku midomo miwili ya pua ikisikika ikivuma sana.

    Kwamba, wote walipwitwa huku wakibandikana hisia za kuzidiwa na uchokozi wa kurarua…!



    ***

    Katika uhusiano wa kimapenzi lolote huweza kuwa uongozi: kwamba, mwanamke anaweza kujikuta akimpenda mwanaume ambaye si yule aliyemchora mawazoni mwake, yaani hivyo hujikuta akifanya pengine ni kwasababu aidha yeye ni kichaa wa mapenzi au pengine amempenda kwasababu anatimiziwa ndoto zake kadhaa za kiuchumi na mengineyo hata kama hivyo inakuwa ni kwa muondoko wa kudhalilishwa. Lakini pia, anaweza kumpenda mwanaume kwasababu ameamua kumpenda jinsi alivyo bila kuvutwa na chochote zaidi ya uamuzi wake wa kumpenda bila masharti.

    Ndivyo, (baadhi yao hasa ‘wachunaji’) anayeona amempata mpenzi wa kumtimizia ndoto zake kadhaa za kiuchumi, huyo uhakikisha akijitahidi kuzijua mbinu za ‘kumkuna’ mwenzake vilivyo ikiwa ni njia ya kujihakikishia usalama wa kutokimbiwa hadi huyo amalizike; lakini wapo ambao (ni wachache sana) kwa mwendo huo hujikuta taratibu nao wakizama kuwapenda hao waliowachukulia kuwa ni ‘wakuchunwa’ kwasababu hata mwanaume anapopenda pia hujitahidi kuzalisha muonekano pamoja na viashiria vyake kwamba yeye kapenda kikwelikweli – yaani hapo jibu hutengenezwa kwamba kila upande hujivuna unapojulishwa kwa hisia na vitendo kwamba unapendwa, unahitajiwa, na unathaminiwa!

    Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa kijana Susan Orbin ambaye pamoja na kumkubali Hughes kama ‘buzi lake la wakati’ huku akijua alitongozwa kwasababu maalumu za kiupelelezi, ndivyo alianza kujikuta akijipokea alikuwa akisogea kumpenda kikwelikweli kutokana na ‘kukunika barabara’ kila walipokutana kwa shughuli hiyo!

    Kwamba, alimpokea kibiashara!

    Kwamba, alimpokea alilipwa vyema!

    Ndivyo hata alimpokea alijua kumkuna!

    Lakini sasa alimkubali, alijiachia, kwani alimpenda!

    Kumkubali huku kulifanya akubaliane na mafunzo fulani ya mama yake kwamba wanaume na wanawake hutofautiana katika mambo mbalimbali, lakini tofauti hizo hazipo kuhusu kuwa na mshawasha na wasiwasi wanapokuwa ndani ya mapenzi. Ndio, ukubali huu ulizidi kumbainishia kuwa ilikuwa ni sahihi yeye kujua kumfurahisha John Hughes wakati wote ili aanze kumpenda badala ya kule kuhisi kutakiwa kwasababu za kusaidia upelelezi wake, kwani alikuwa na wasiwasi wa kuja kutemwa na hivyo kuikosa misaada mbalimbali aliyokuwa akipewa; lakini kwa kadri alivyokuwa akihakikisha akimkuna vyema, ndivyo halikadhalika naye alijikuta akipokea alikuwa akikunwa barabara na hivyo kujikuta akijongea kuanza kumpenda kikwelikweli tofauti na kumpokea kwasababu ya kuhudumiwa kiuchumi!

    Ndivyo, sasa alishikwa na vyote!

    Akishikwa na wasiwasi!

    Akishikwa na mshawasha!

    Sasa alifanywa ajifunze zaidi ili kuwajibika kwa alama za juu zaidi kwa maana alimpenda na akitamani yeye pia apendwe ikibidi mume wa mtu aporwe kupitia ‘udatishi’; na kwa mjongeo huo ndivyo alichukua elekezi kutoka ‘popote’ kwa maana ya kuamua kutekeleza vyote kadri alivyoweza bila kuzingatia masharti ya mkataba wake wa kukodisha mwili, kwakuwa sasa wasiwasi ulishika awe makini asimkose huku mshawasha nao ukishika atende ili asimkose aliyempenda bila masharti!

    Hughes…ooh, John Hughes!

    Ndio, sasa aliweka katika vitendo yote aliyojua, kwamba alipaswa kufahamu jinsi ya kumfanya Hughes ajihisi ni hodari huku yeye akimshangaza kwa mambo yake kwa mapigo yake; na tena alijua alipaswa kuweka urahisi na umakini kwa maana ya kutokuwa mrahisi sana huku ukiwa si mgumu pia – kwamba, hapo alijua wapendanao wanapokutana kwa ajili ya mapenzi, hao wanapaswa kufahamu kuwa tendo linalofanyika ni tendo la kusisimua miili ambalo ni upeo wa upendo baina yao!

    Ndio, sasa aliweka katika vitendo yote aliyojua, kwamba, halikadhalika, alipaswa kujua kuweza kumkuna Hughes vilivyo ingetemea pia na jinsi anavyomuonyesha anavyomuhitaji huku akijua kuzisoma hisia zake ikiwa ni pamoja na kuzipatia jawabu katika nafasi muafaka. Ni kwamba, alijua akimuonyesha anamuhitaji ndivyo angevyochangia vyema katika kumpatia nguvu na ari ya kurahisisha kumfanya ashikwe na hisia za kujibu mapigo hata kama bado yeye hatakuwa tayari ametumbukia ndani ya nafasi zile za kuhakikisha akimkuna vilivyo pale panapomuwasha!

    Hivyo ndivyo alijua!

    Hivyo ndivyo alitenda bila kuacha!



    ***

    NI KWAMBA, Susan Orbin alitulia chumbani akisikiliza mziki tulivu kupitia Radio-Clouds akiwa amejilaza kitandani kifudifudi lakini kivivuvivu. Hapo alivalia kisketi kifupi sana huku matiti yake madogo mithili ya embe dodo yakiwa wazi yakilalia mto uliokumbatiwa.

    Chini katika kapeti la mpira, karibu kabisa na kitanda, zilikuwepo chupa tatu za pombe aina ya safari-lager ambapo kati yake moja ilikuwa tupu huku nyingine ikiwa imebakia nusu ambayo pia ndiyo ilisimama katikati.

    Taratibu alianza kuugeuza mwili, kisha alinyoosha mkono wake wa kulia kwa kuupeleka sakafuni hadi alishika ile chupa ya katikati na kuanza kuibeba huku akianza kukisogeza pia kichwa chake kama vile alihitaji kuchungulia...

    Alikunywa pombe kwa kupiga mikupuo miwili ya harakaharaka, kisha aliirejesha mahala pake chupa ile; sasa alijilaza chali, lakini kwanza alilishika tumbo lake kwa kulibinyabinya kidogo huku akichanua tabasamu, na ndipo baadaye kidogo aliuchukua mto na kuukumbatia huku akiendelea kusuuzwa na mashairi matamu ya mziki.

    “Watasema nakuchuna…ay!” Aliigiza ubeti mmoja wa wimbo huo na kufuatia na mwingine uliosema, “watasema nimebahatika…ooh!”

    Ala zilipopigwa peke yake ndivyo alitikisa kichwa huku mikono ikibinyabinya mto mithili ni mpenzi ndiye alishikwa akibembelezwa; lakini sauti iliporejea tena, aliigiza tena kuimba, “wakijua hawatasema nimeshikwa, kwani wananiita malaya.”

    “Hawajui malaya pia hupenda, malaya pia hupendwa…uuh!” Alimalizia kuuigiza ubeti mmoja huku macho yake yakizidi kulegea, kwani wakati pombe ilifanya ndivyo kungumanga aliyokula ilifanya halikadhalika.



    Mziki uliisha kwa kuingiza matangazo kadhaa ya biashara ambapo yalifanya ajigeuze tena ili mkono wake uweze kuchukua chupa ile ya pombe ambayo bado ilikuwa haijaisha.

    Alipiga fundo kadhaa kabla ya kuirudisha mahala pake chupa ile huku sasa hisia zake zikizidi kumvuta katika kuiwazia ‘raha ya pipi’ kutoka kwa Hughes; na ndivyo, mara baada ya kujilaza kama mwanzo, alijikuta akiachia sauti laini kwa kuimba sehemu ya wimbo fulani kutoka kwa mtunzi wa riwaya hii…

    Amependa Malaya,

    Amependwa Malaya,

    Wote wamedata, Wote wajidatisha





    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    SUSAN alikuwepo nyumbani kwakuwa alikuwa ‘off’ siku hiyo ya alhamisi; na pia hakutaka kutoka kutokana na kuombwa na Hughes (buzi lake) asiondoke hadi wakutane. Na kwakuwa alikuwa na ule wasiwasi ambao sasa ulifunikwa blanketi la mshawasha, ndivyo alijua kusubiri huku akipenda kusubiri kwasababu hata huko aliingizwa ndani ya raha.

    Ndio, kusubiri kulikuwa ni raha kabla ya kushereheka!



    Hadi wakati huo ilikuwa majira ya saa 12.37 jioni; zaidi ya dakika arobaini kupita muda ambao alielezwa alipaswa kukutwa hapo.

    Alipapasa sehemu fulani kitandani, akaigusa simu ya mkononi na kisha aliichukua. Alifungua mfuniko wake simu na kisha alibonyeza namba kadhaa; na ndipo baada ya sekunde tano hivi alianza kuongea na ‘buzi hilo’.

    “Mpenzi unaponiita mwili tayari unajipeleka…please, usikawie sana! Naugua! Naugua unaninyima, naugua nakunyima haki yako!”

    “Usijali endelea kumbembeleza mtoto, mdanganye kwa kidole chako anyonye hadi nitakapomletea pipi halisi…darling, ndani ya robo saa kweli nimefika!” Hughes alisema, na kisha ndipo waliagana.

    Lakini badala ya kuirudisha simu, ndivyo Susan alianza kumuandikia ujumbe mfupi akisema, ‘mtoto alizwa akimlilia mzee, alizwa akipenda akoshe! Alizwa…uh!’

    Kisha ujumbe ukatumwa!



    SAUTI ya kugongwa mlango ilisikika vizuri huko chumbani alipokuwa Susan ambaye moja kwa moja alimbashiri Hughes kuwa ndiye mgongaji. Hivyo, alijitoa kitandani na kuanza kutembea kukitoka chumba hicho ili kuelekea chumba cha pili ambacho ndicho kilikuwa baraza lenye mlango wa kuingilia ndani.

    Alipofika mlangoni, alisimama kwanza akijitazama kwa sekunde kumi hivi ndipo taratibu mkono wake ukaanza kuondoa komeo huku tayari sura ikin’gaa tabasamu.

    Kisha alifungua mlango!

    Macho yakagongana!

    Wote walisisimka huku mmoja akivuta pumzi zaidi kabla ya kuziachia ambapo alifanya kifua kilichobeba matiti yaliyosimama kisawasawa kijikusanye kabla ya kutanuka tena na kurudia hali hiyo mara kadhaa!

    Kwamba, Susan alihemahema!

    Kwamba, Hughes alisisimka akihema zaidi huku harufu nzuri ikizitekenya pua!



    Hali hiyo ilichukua sekunde chache kabla ya Susan kujikuta akimrukia Hughes ambaye alimbeba juujuu na kuingia naye ndani.

    “Ooh, my my!” Hughes aliweweseka kimahaba huku akigeuka na kuufunga mlango.

    Bado Susan alibebwa.

    Hughes akambeba hadi chumbani ambapo huko alimuachia akidondoka kitandani kwa mwendo wa chali kabla ya kumfuatia kwa kujilaza juu yake.

    Walitomasana kwa muda kabla ya Hughes kuinuka na kuondoa nguo zake zote ikiwa ni pamoja na kuizima taa yenye nuru mkubwa; na kisha taa dhaifu kuwashwa...

    Aliiweka simu yake katika meza ya kitanda kabla ya kuinama na kuchukua ile chupa ya pombe iliyokuwa haijafunguliwa.

    Susan alipotaka kuinuka, Hughes alimkataza kwamba angejihudumia mwenyewe bila wasiwasi; na ndivyo kwa kutumia meno alifungua kifuniko cha chupa hiyo, na kisha ndipo alikunywa kiasi kikubwa cha pombe.



    ******

    ILIPOFIKA majira ya saa mbili hivi, Susan alikuwa amemlalia Hughes akizichezea nywele zake huku wakiwa ndani ya maongezi ya kawaida ambayo yaliendelea hadi pale Susan alipobadilisha ‘upepo wake’ kwa namna ambayo Hughes alipendelea zaidi kutokana na mvumo wake kulandana kabisa na eneo lililofanya ajifikishe hapo.

    “Mpenzi…bosi wangu ananidodosa sana juu yako kiasi nakosa raha!” Susan alianza kusema kwa sauti ya puani.

    “Nini tena?”

    “Aah, si unajua ule ugomvi uliokuwa ukiulizia?”

    “Kwani imekuwaje tena?” Hughes aliuliza.

    “Hapana. Ila naona bosi kama vile ana wasiwasi.”

    “Wasiwasi?” Hughes aliuliza akijifanyisha kushangaa zaidi kiasi hata alimuondoa Susan kwa kumsukuma pembeni ili aketi hapo kitandani.

    “Ana wasiwasi sijui kuibashiri.”

    Akiwa ameketi, Hughes alifikirifikiri.

    “Nataka nitafute kazi sehemu nyingine. Sipendi kusumbuliwa…la sivyo, nirudi kijijini!” Hapo Susan alisema kwa sauti kali kiasi huku naye akijivuta kuketi lakini kwa kumuegamia Hughes mgongoni kwa namna ya kumkumbatia kwa nyuma.

    Ndipo Hughes alimtaka radhi kidogo na kujiondoa kitandani kabla ya kuokota shati lake lake lililokuwa si mbali sana na zilipokuwa zile chupa tatu za pombe.

    Susan alitulia akitazama.



    Hughes aliingiza katika mfuko na kutoa picha; na kisha tena, aliwasha taa yenye nuru kubwa…Susan akashikwa na mshangao ingawaje haukuwa mbali ya kawaida kwasababu kama ulivuka, basi ulivuka kiduchu sana!

    Hughes aliona badiliko hilo, lakini akijifanya hakuona ndivyo alirejea kitandani ambapo alimpatia Susan picha ile bila kusema chochote.

    Ulegevu wa mwili wa Susan ulijisema vyema ukisaidiwa na zile tazama zake.



    Baada ya kuipokea picha ile, Susan alisema, “hii ya pili unanipatia…nadhani unataka nimtambue kama nilivyomtambua yule…eeh, yule nanihi…nani vile?”

    “Polisi ni mwema. Halafu mimi ni mpenzi wako ninayeishi kwa ajira hii huku wewe pia ukifaidika. Si ndivyo? Au unasemaje?” Hughes alisema tofauti na muondoko wa sentensi ya mwenzake ambayo iliishia kwa kuachia swali.

    Susan aliitika kwa kichwa huku akiibibidua midomo; na wakati huo akimjongelea Hughes kwa kujivuta.

    Bado aliitazama picha.

    “Asikusumbue, kwani huko mbele nitahakikisha ukifanya shughuli ya maana kama sio kukupatia mtaji ujiajiri. Take it…jichukue umepata bahati ya kupendwa na mtu anayependa kuona mpenzi wake akiburudika katika nafasi zote kuanzia kitandani hadi nje yake. Mimi ni hitaji ulilopenda kupata.”

    “That’s why nakupenda Hughes.” Susan alijibu huku akidhihirisha alifurahi sana; na ndivyo hata alikitupa kichwa katika kifua cha Hughes kwa kumuegamia baada ya kuwa tayari alimsogelea.

    Hughes hakujua iwapo alikuwa sahihi jinsi alivyomuahidi au ndivyo zilikuwa sehemu za laghai zake ndani ya ngono. Hatahivyo, alipuuzia fikira hizo kwa kuendelea kumuuliza Hughes kama aliitambua picha ile huku akimhakikishia hakukuwa na namna mbaya ingemtumbukiza matatizoni.

    Susan aliitazama zaidi picha ile kabla ya kuachia mguno mfupi ukifuatia na kusema kwake, “usikasirike sweetie! Huyu aliwahi kunitongoza ingawaje hakutokea tena! Au sijui kwakuwa niligoma!”

    Hughes alijifanya kumtazama kiwivu.

    “Inabidi nieleze isijekuwa unaniuliza kwa mwendo huuhuu wa wivu ambao naona jinsi unavyoniangalia! Hakuna uhusiano, lakini namtambua.”

    “Usijali sana, kwani namtafuta kikazi. Hivi…hakuwepo katika ule ugomvi?”

    Suzan alichelewa kujibu huku akimtazama Hughes kidadisi lakini kwa kuendelea kuichanua tabasamu ambayo nyakati fulani ilin’garishwa kwa njia ya kuchezesha na kujilamba mdomo. Ndio, ilikuwa tabasamu mithili ya mtu aliyekuwa ndotoni akiota vizuri.

    Hughes aliinua mkono na kusogeza kidole cha shahada hadi kuanza kukipitisha juu ya mdomo wa Susan huku akimsemesha kimahaba katika kusukuma aelezwe iwapo ni kweli huyo mtu katika picha aliyompatia alikuwepo katika ule ugomvi wa De-paradise.



    Susan alijibu taratibu kwamba mtu huyo alikuwepo katika ule ugomvi, kisha alikiinua kidogo kichwa chake kwa upande mmoja ili kumuwezesha kumtazama Hughes kwa jicho moja la chati huku kope zake zikijitahidi kufunguka na kufunga kiasi ndivyo vilizalisha ulegevu zaidi katika kutazama; na kisha alitoa ulimi nje kidogo na kuanzisha vurugu fupi za kukilamba kidole kile kiasi Hughes alijikuta akimeza mate kwa ashki.

    Kichwa kiliinuliwa zaidi; na ndivyo macho yote yakawa yakitazama ulegevu wa kutazama wa Hughes ambaye hata alitumbukiza kidole chake ndani ya mdomo wa Susan kabla ya kumtupia swali jingine kutaka kuelewa kama alijua mtu huyo aliitwa nani; lakini kuuliza huko alifanya baada ya kutulia sekunde chache akisikiliza jinsi kidole chake kilivyokuwa kikifyonzwa na hivyo kuhisi raha fulani ambayo ilifanya hadi masikio yake yahisi kutekenyeka kwa ndani.

    Susan hakujibu si kwamba hakusikia; isipokuwa hakujibu kwakuwa mdomo ulikuwa katika hekaheka za kufyonza mithili ya mtoto na unyonyaji wa kidole chake katika kudanganya hamu zake za kutaka kunyonya maziwa ya mama. Lakini, hatahivyo, kidogo tena alijikuta akiwa ameachishwa kunyonya kutokana na Hughes kukichomoa kidole ambapo alifanya kwa mwendo wa kusuasua huku akisikiliza jinsi kilivyokuwa kikivutwa na kuonyesha mnyonyaji na mnyonywa waliburudika kwa pamoja.



    Kidole kilipotoka, Susan aligugumia kwa raha huku mikono yake ikimkumbatia Hughes kwa nguvu kwa kumzunguka mgongoni!

    “Anaitwa nani?” Hughes aliuliza tena huku mgongo wake ukisuguliwa na mikono ya Susan ambaye sasa aliitupa picha kitandani katikati ya mito miwili.

    “Mmh?” Susan aliuliza kimguno.

    “Huyu jamaa ni nani?”

    “Aah!” Susan aliguna tena, kisha akajibandua kumkumbatia; lakini bado hakuacha kukituliza kichwa chake katika kuegamia kifua cha Hughes. Ndipo akajibu kwa kutoa sauti hafifu ya mahaba akijulisha mtu yule katika picha aliitwa Bob Collin.

    Jibu liliongeza kiwango cha tabasamu huku maswali mengine yakifuatia katika kuhitaji kujua huyo Collin aliishi wapi akishughulika na nini.

    “Hayo sijui. Ila namtambua kama mteja ingawaje sikuhizi haonekani tangu ule ugomvi kutokea.”

    Hughes akifurahishwa na majibu ndivyo alijikuta akishuhudia mikono yake ikimnyanyua Susan kupitia kumshika mabega.

    Susan alisaidia kwa kujiinua.

    “Sasa tufurahi.” Hughes alisema huku akimtazama Susan ambaye mara alishusha pumzi ndefu huku macho yake yakilegea zaidi kiasi uzito wa kope kama vile uliongezeka katika kumfanya aonekane mwenye kujitahidi zaidi kuzisimamisha.

    Macho yalibadilika hali; yaliiva!

    Huku mwili ukizidi kupashika!

    Huo ukitetemeka!

    Huo ukitekenyeka!



    ******



    Ilikuwa majira ya mchana siku iliyofuatia: Hushly Collin aliendelea kuendesha gari (BMW) kwa mwendo mdogo hata alipokwishakata kona kuingia mtaani kwake. Alipunguza zaidi mwendo alipokuwa katikati ya barabara hiyo huku akiitoa simu yake ya mkononi iliyokuwepo katika kichumba chake katika gari na kisha kuanza kubonyeza namba kadhaa. Lakini si kwamba alipiga simu; bali alikuwa akibinya namba za siri ili mlango wa geti la kuingilia jumba ufunguke ingawaje bado angeweza kupiga honi ambayo ingemjulisha mlinzi wake na hivyo kumfungulia mlango.

    Gari lilipofika mbele ya jumba, tayari lango la kuingilia lilikuwa limefunguka huku mlinzi akionekana pembeni; na ndivyo, alilingiza gari hadi mbele ya eneo la baraza la kuingilia nyumba kubwa iliyokuwa katikati ya nyumba ndogo mbili huku mojawapo iliyokuwa imeingia kwa ndani zaidi ikiwa gereji.

    Alipotoka nje, mlinzi alimkimbilia.

    “Samahani mkuu.” Mlinzi alisemea kwa mbali huku akikazana kumkimbilia.

    Collin alisimama.

    Alipofika tayari alikuwa akihema ingawaje haikuwa kwa sana. Hatahivyo, Collin alitania, “mazoezi baba! Kila mara nakusisitiza…punguza wanawake!”

    “Hapana mkuu.”

    “Hapana wakati naona ulimi unataka kujiachia nje…ok, lete habari.”

    Mlinzi alitulia kimya kwa sekunde tano hivi ndipo alianza kusema, “majira ya saa nne hivi baada ya kutoka kwako alikuja mtu akidai anakuhitaji sana.”

    “Mtu?”

    “Ni askari.”

    Collin hakuonyesha alishtuka; hatahivyo, moyoni mwake alifanya kiasi alihisi mithili alichanwa kiasi!

    “Unatakiwa ukaripoti polisi.”

    Collin alishika pua na kufanya kama vile alikuwa akizisawazisha tundu zake ili kuweza kupumua vyema; na kisha ndipo aliitikia kwa kichwa huku akianza kuondoka.

    “Mkuu, ni kwema?”

    Alisimama kabla ya kujibu, “everything is under control…be normal but don’t forget our usual alertness!”

    Kisha alianza kuondoka tena.

    Lakini alipomaliza kupiga hatua tano hivi alisimama huku akigeuka taratibu.





    “Bonnet!” Aliita kwa sauti; na wakati huo mlinzi alikuwa tayari ndani ya banda la ulinzi pembeni ya lango la kuingilia eneo la jengo hilo.

    Mlinzi alitoka na kumfuata kwa kumkimbilia kama alivyofanya mwanzo.



    Alipofika, alitoa saluti kali.

    “Sijajua. Natakiwa makao makuu au ni kituo kipi natakiwa niripoti? I hope they told you exactly.”

    “Kituo cha tabata. Huko kimanga.”

    “Thanks.”

    Collin aligeuka bila kujali kapuakapua za mlinzi; na ndivyo alianza kuondoka…



    COLLIN hakukaa nyumbani kwa zaidi ya saa moja, kwani hatimaye mawazo yalimjia ilikuwa ni busara kuripoti polisi mapema ili kuweza kujua kwa uhakika ni nini aliitiwa.

    Hatahivyo, kabla ya kuamua kuondoka alimpigia simu mzee Kasonzo ili kumjulisha habari hiyo ikiwa ni pamoja na kuhitaji kujua pengine mzee huyo angekuwa na dokezo au angempatia maelezo au amri yoyote.

    Simu ilipoitika, alimfanyia msichana wake wa ndani ishara ya mkono kwamba akimtaka aondoke.

    Sauti ya mzee iliposikika, Collin alimsalimia; na kisha mara moja alimjulisha habari nzima kama alivyojulishwa na mlinzi wake.

    “Usipokuwa makini, huu ni mzozo.” Sauti ya masikitiko ya Kasonzo ilisema.

    “Master! Narudia kuomba samahani!”

    “Samahani si habari kama hutaweza kurekebisha!” Sauti ile ilisema tena, “ni kweli unasakwa kuhojiwa baada ya makachero kuubaini ule ukaribu. Remember…I’m the patient bird, the vulture on wait!”

    Collin aliduwaa kitambo, akitetemeka huku mawazo yakichota kwa ghafla kutoka ndani ya kumbukumbu zake habari nzima, habari iumizayo!

    Aliposhtuka, tayari simu ilikatika!http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Akailani habari nzima!

    Akijuta sana!



    Ndivyo aliitikia wito; lakini safari ya kwenda huko hakuifanya kwa kutumia gari lake, kwani alipiga simu ili kufuatwa na taxi ambayo mara nyingi ilimuhudumia kila alipoona hakuhitaji kutumia usafiri wake.



    *****

    Mara baada ya kuitwa na mkuu wa kituo na hatimaye kumuhoji Hushly Collin aliyefika kituoni hapo kuitikia wito, ndivyo Hughes hakukaa sana ofisini; kwani aliamua kwenda kumtembelea Susan Orbin ambaye alizidi kujikubali alikuwa akimvuta sana kimapenzi kiasi cha kujitambua alimpenda tofauti na ilivyokuwa mwanzoni. Ndio, aliamua kuondoka mapema kutokana na kutoridhishwa na maelezo ya Collin tofauti kabisa na tarajio zake kwamba pengine hapo wangeweza kupata fununu nzuri ya kumuhusu Edwin ambaye sasa iliamuliwa taarifa rasmi zitolewe za kutafutwa kwake nchi nzima kama mshukiwa wa mauaji ya Brigitte.

    Collin alieleza ni kweli alikuwa rafiki wa Edwin, hatahivyo alimaka hakuwa mshirika wake kikazi huku pia akisema alikuwa safarini kitambo na kwamba alirejea yapata wiki mbili hivi zilizopita; na alipoulizwa mara ya mwisho kuonana au kuwasiliana na Edwin ilikuwa lini, hapo alisema asingeweza kukumbuka!



    *****

    Majira ya saa tano Hughes aliwasili nyumbani kwake lakini kwa lengo la kuondoka baadaye tena, kwani aliamua siku hiyo angelala kwa Susan!



    Kama kawaida, alifunguliwa mlango na mkwewe ambaye alimkaribisha kwa kumrukia na kumkumbatia huku akichuchumia kwa vidole vya miguu ili kujikaribisha kupeana mabusu; na ndivyo ilikwenda, lakini kwa kuanzia mama mkwe kunyanyuliwa ambaye naye aliinua miguu na kuizungusha kiunoni mwake!

    Baada ya dakika tatu hivi ndipo waliachana huku mkwe akiwa mwanzilishi wa mazungumzo yaliyomwaga ishara za wivu huku hata tazama zake zikiin’garisha.

    “Ukichelewa nasikia vibaya!”

    Hughes alikuna kidevu kabla ya kujibu; na tayari alikuwa akiingia ndani, “kibarua mama!”

    “Mmh!” Mama Lana aliguna huku akichezesha macho, na kisha alisema kivivuvivu, “jitahidi uwe unawahi bwana…nimekuzoea utadhani huu mume wangu!”

    Akichekacheka, Hughes aliyekuwa nyuma yake alimvuta na kumkumbatia kwa kuibana mikono yake; na kisha aliinama na kumbusu shingoni!

    Ndivyo mama wa watu alijikuta akihema sana huku akijiachia, mwili ukilegea sana; na sauti laini, sauti yenye kusikika kwa mbali ilipiga kuta za ndani za masikio ya Hughes, “nasikia raha!”

    Kisha tena…mama mkwe aliachiwa; kwanza, kwa kugeuzwa mwili ili watazamane kabla ya kusemeshwa kwa kitambo kifupi huku kashikiliwa mikono. Kwamba, alimueleza atangulie chumbani, kwani alihitaji kuingia chumbani kwa madai ya kuchukua kitu.

    “Ukiingia huwezi kutoka…hapana, usifanye! Usiende bwana!” Mama mkwe alipinga huku akijaribu kubadilisha hali kwamba yeye ndiye awe alimshika mikono; kwani alitamani asisitize kwa kumvuta kinyumenyume.

    Hughes akiruhusu ashikwe mikono huku akijibu baada ya kumbusu katika paji la uso, “nitanyata, hawatajua!”

    “Aah, kwanini usichukue kesho?”

    “Skliza. Leo sitalala. Nimekuja kwa ajili yako na kuchukua hicho kitu.” Hughes alinyamaza kwa sekunde chache na kisha aliendelea kusema, “kuna kazi maalumu inatakiwa ifanyike kabla ya mapambazuko!”

    Hapo mkwewe aliacha kumshika!

    “Nenda, nakuja!”

    Mama mkwe aliinua mikono hadi katika mashavu ya Hughes na kuitikia kwa kuachia sauti ya kinyonge, “nimesikia mpenzi! Lakini taadhari usiisahau, kwani nampenda sana mwanangu.”

    “Taadhari?” Hughes aliuliza, kisha aliuliza tena kabla ya kujibiwa, “eeh…nisiisahau? Ipi hiyo?”

    “Huko kunyata! Unyate ukijua kunyata ili usiharibu ukashindwa kurudi nikupatie chakula chako cha usiku!” Mama Lana alijibu kwa sauti ya puani huku akigeuka taratibu.

    Hughes akakenua meno, “una maneno matamu ingawaje huwa ni matamu zaidi uwapo kitandani ukifinyanga!”

    Mama alikatisha kugeuka kwa kurejea haraka katika kutizamana, na kisha alikonyeza huku mdomo ukilambwa na ulimi…halafu, aliikunjua khanga yake iliyokuwa pekee katika kuustiri mwili wake; na kisha tena alijifunga huku akibadilisha mtazamo mithili aibu ilimchukua…

    Hughes akisisimka kiasi pumzi nzito ilimshuka kabla ya kuhemea juu juu!

    Mwanamke huyo pia alihema huku akikamilisha kujifunga vizuri hiyo khanga yake huku macho ya mahaba yakizalisha ukunaji ndani ya hisia za Hughes ambazo zilitekenyeka kiasi!

    “Mama…mmh, wajua! Wajua kutayarisha, wajua kuvuta!”

    Mama hakujibu kwanza: aligeuka kwa mikogo huku kichwa kikichelewa kuufuata mwili kutokana na kule kumtazama kiwiziwizi huku macho yakizungurushwa kinamna; na kichwa kilipomalizia kugeuka, ndipo taratibu kwa kujinyonganyonga alianza kuondoka huku akisema, “mfinyanzi atajulikana kitandani!”



    Hughes pia aliondoka akimfuata kwa nyuma huku ukodoaji ukitalii mtetemeko wa umbo ambao ulifanya kila mara khanga iwe ikivutwa na kukunjwakunjwa kiasi pande mbili za ‘bambataa’ zilionekana zikipigana vikumbo.

    Ndio, aliendelea kumfuatia kwa nyuma hadi alipoikaribia korido ndipo alibadilisha muelekeo na kuanza kukifuata chumba chao; lakini hivyo alifanya kwa kuvuruga raha za hisia zake ambazo ziliburudishwa sana ‘mitetemeko ya bambataa na tingishika zingine za mwili’!

    Alipofika mlangoni mwa chumba, alisimama na kusogeza sikio lake la kushoto karibu na tundu za funguo katika mlango, na kisha alitulia hivyo kwa robo dakika hivi akijaribu kusikiliza kama kulikuwa na hali zilizoonyesha waliopo huko hawakulala.

    Alipopata ishara alizotegemea alikenua meno na halafu ndipo aliondoa sikio lake. Mara akaanza kufungua mlango kwa taadhari sana katika kuhakikisha hakuna sauti iliyosikika; na ndipo hata alijitoma ndani…



    Vilevile, akiwa ndani alihakikisha ujio wake haukusumbua, kwamba, haukufanya waliomo wajitoe usingizini na hivyo kuvuruga mipango yake ya kujifua na mkwewe kama ambavyo sasa alipenda kwa sana.

    Taa yenye mwangaza hafifu ndio ilikuwa ikiwaka kiasi ilijulisha hali za wote waliokuwemo katika vitanda viwili.

    Alisogea katika kitanda cha mkewe na kufurahi kwamba alilala usingizi. Halafu aliongoza njia hadi katika kitanda kingine ambacho alilala Jackline; hapo alisikitika kidogo kwasababu hisia za kumtamani zilijitokeza!

    Huku akitazama uzuri wa sura ya Jackline alijipatia matumaini kwa kudai kwakuwa tayari aliridhia kwamba alipenda kupelekwa basi ndio alishika uhakika upo wakati angeanza kumfaidi na akiwa ndiye muanzilishi. Hatahivyo, alijisifu tayari alikuwa akiuchezea sana mwili huo huku akipatiwa kibali kufika popote mikono ilipohitaji!

    Bado aliifurahia mipango ya mkwewe kwamba Jackline angeanza kulala chumba chao ili kuhakikisha usalama wa afya ya mkewe kutokana na kukaribia muda wa kujifungua, kwani mpango huo ulikuwa ni kuacha nafasi nzuri kwa wao ‘kuvinjaliana’ nyakati za usiku kabla Hughes hajajitokeza kwamba alirejea nyumbani; lakini mpango huu (nafsini mwa Hughes) pia ulikuwa nafasi kwa kurahisisha msogezo wa kumtafuna Jackline!

    Ndivyo, Hughes alijisemea moyoni kwa matumaini kwamba kuanzia wiki ijayo angesimama kulala na mkwe ili ‘kumpiga mweleka’ Jackline kuanzwe kwa mikakati ambayo alijua wangeichora wote wawili, yaani, mpigaji na mpigwaji.



    Ndipo kidogo tena, alifuata kabati lake na kufungua kwa taadhari zilezile. Alitoa burugutu la fedha na kuziweka katika droo kabla ya kufunga mlango.

    Kisha sasa alitoka…



    LAKINI, Hughes hakujua; halikadhalika, mama mkwe!

    Kwamba, Hughes hakujua Jackline alikuwa macho, kwani huyo alisikia mlango wa kuingilia ndani ulipofunguliwa na hivyo kuushtukia ujio huo!

    Hivyo, kwanza alijifanya alilala, lakini si kwamba alilala hakutaka kujulikana alikuwa macho; bali hivyo alifanya kwasababu maalumu akihisi angechokozwa kuamka!

    Sasa hakupenda alivyoona haikufanyika!

    Akishangaa iweje hata hakuguswa!

    Akishangaa iweje Hughes aliingia akinyata!

    Na kwakuwa alibaini Hughes alipokuwa akitoka chumbani, ndivyo aliona amfuate hukohuko akiwa na dhamira, safari hii ‘amenywe’! ndio, hakutaka aendelee tena kuishia akihisi akimenywa, bali sasa alitamani kuwa shuhuda yeye mwenyewe akimenywa kwa mara ya kwanza hata kama alishikwa hofu za kuhisi kasheshe zingevyokuwa!

    Ndivyo aliamka huku mwili ukitetemeka, lakini huku mawazoni akijiwa na maswali machache kuhusu kwanini Hughes aliingia akinyata na akitoka akinyata!

    Alitulia kitandani akipunguza kasi za kuhema kwa sekunde kadhaa kabla ya kujiondoa kitandani kabisa na kusimama kama mtu aliyekuwa akifikirifikiri!

    Kidogo tena, alianza kutembea kwa mwendo mdogo na kwa kunyata hadi katika mlango; akasimama tena!

    ‘Kwanini alinyata? Ananikimbia?’ Alijiuliza.



    Sasa, taratibu alifungua mlango na kutoka; kisha aliurudisha kwa kuufunga taratibu!

    Akaanza kutembea, akitembea kwa kunyata na tayari akijenga hisia kwamba Hughes alikuwa maliwatoni ambapo aliona ni vyema kumfuata hukohuko…

    Wakati huo, yale maumivu ya muda mrefu ya kuumizwa na ashki zake zilizokuwa zikiishia kuchokozwa na ndivyo yalikuza mzuka wa hofu!

    Kwa mzuka huo si kwamba alihofu kupigwa; bali hofu ilikuwa ni kwakuwa hivyo ingekuwa ni mara yake ya kwanza kama angefanikisha kuhakikisha akiwa ameondoka amepigwa!

    Hivyo alimezwa na hofu ya kuhitaji kupigwa!

    Kupigwa kwa hamu!

    Kupigwa kwa raha!



    Alipofikia chumba cha mama Lana, alijikuta akisimama kwanza, kwani wakati macho yaliona mlango haukufungwa ndivyo alihisi huko mbele alikuwa akija mtu!

    Akarudi nyuma kwa haraka na kuingia katika korido la kuelekea barazani; hapo akajibanza bila kuchungulia kwanza, lakini masikio yake yalikuwa imara sana!

    Ndani ya sekunde tano, akafanya!

    Alichungulia!

    Mama…!?



    Hakuamini macho yake yalipomtazama Mama Lana aliyekuwa uchi wa mnyama!

    Mmh!

    Hata akaacha kuchungulia huku akirejewa kuhema sana huku mawazo ambayo hakutegemea yangemjia yalikuja kwa kufukuzana!

    Hisia zikasema!

    Akasononeka sana akipandwa na wivu ambao tena ulimvuta arejee kuchungulia!

    Akafanya…

    Lakini sasa hakuona kitu!

    Hisia zikamjulisha tena, ‘ameingia!’

    ‘Wapo wote!’ Hizo zikazidi kujulisha.

    “Sasa?” Akili iliuliza kwa kuruhusu sauti ndogo sana kupenya nje ya mdomo; na kwa kipindi hichohicho, hisia zilinon’gona tena, kwamba, zilimvuta katika kuona alipaswa akahakikishe kwa kusogea mlangoni.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Akili hazikubisha, kwani ndivyo alifanya!





    Alipofika mlangoni, alisinyaa kwa sekunde kwani mzuka wa hofu ulianza kusumbuliwa na kuhofia! Kwamba, alianza kuhofia kuendelea kudadisi huku bado mwili ukiwa umechemshika tayari…mara alijikuta akisogea zaidi ambapo alibaini mlango haukufungwa kutokana na kuona mwangaza wa taa hafifu aliyoijua ilikuwa imewashwa!

    Akisogea tena, zaidi akijivuta!

    Mara…akashtukia amesukuma mlango ambao ulifunguka zaidi bila kutoa kelele!

    Hapo alirudi nyuma hatua mbili tatu hivi huku hofu ikimyumbisha sana kiasi alitetemeka zaidi!

    Mara kasimama!

    Hapo alihema sana!

    Lakini tena, akajikuta akinyata, akisogea na kuusukuma mlango taratibu huku akijitahidi kupunguza sauti ya kuhema ambako kulidhihirisha alikuwa ndani ya wivu mkali uliokuwa ukimchana moyoni!

    Kwanza alikitanguliza kichwa katika kuchungulia…



    Ule mwangaza wa ndani ya chumba hicho licha ya kuwa ulikuwa hafifu sana, lakini bado aliweza kubaini kitanda kililaliwa na zaidi ya mtu mmoja!

    Hili alibaini wazi!

    Hili lilimsikitisha sana huku mwili mzima sasa ukiingia ndani bila kujua hivyo alifanya!

    Bado, baada ya kujiingiza hivyo, ndivyo halikadhalika alijikuta akibadilika hali kwasababu mzuka wa hofu ya kuhitaji kupigwa kimapenzi ulianza kutimua mbio kwa spidi kali katika kumchomoka na hivyo kuruhusu ujio wa maumivu ya moyo yaliyokuwa tayari yameibeba hasira ya wivu iliyoongeza kuumia kwake!

    Alipumua sana, kwani hata kwa sauti alifanya bila kutaraji angesababisha nini!



    Hali hiyo ambayo Jackline alishindwa kuikabili, hiyo ilifanya waliokuwa wamelala ‘wakigaragara’ hata washtuke; kwani Hughes aliyekuwa akijiandaa ‘kuupanda mlima’ ndiye alikuwa wa kwanza kusikia uhemaji ukitokea nyuma yake na hivyo kugeuka na kutazama kimshangao!

    Aliona; lakini bado hakumjua huku hisia zake zikirukia angekuwa ni mkewe!

    Lakini akatazama zaidi huku mama mkwe akishangazwa kuona mkurupuko wa kugeuka kwake…

    “Sweetie, nini?” Mama mkwe aliuliza huku akimshika Hughes shingoni na kujaribu kumvuta.

    Mama mkwe alishangaa tena hadi kuuliza mara ya pili, kwani shingo ya Hughes iligoma kuvutika!

    “Tu…tu…tumeshikwa!”

    Mama mkwe alikurupuka kwa kuamka huku akimuuliza kwamba alikuwa akisema nini; lakini Hughes hakujibu, na badala yake alijitoa kitandani na kuanza kuelekea mlangoni na hivyo kufanya mama mkwe naye ajiinue kidogo ili kuweza kusafirisha tazamo lake!

    Hughes alifanya hivyo huku bado hakuvaa!

    Akisogea, akisikitika!

    Lakini akiwa katikati ya chumba katika kusogea huko ndipo alibaini…duh, akashusha pumzi zake huku sasa akiongeza kasi ya kutembea…



    Wakati Jackline alitupwa zaidi mawazoni mwake kiasi hakuweza kumuona Hughes aliyekuwa akimjia!

    Na aliposhtuka, tayari alishikwa mikono!

    “Niache!” Jackline alisema kwa sauti kali.

    “Usifanye hivyo, tulia!” Hughes alianza kumbembeleza huku akifunga mlango wa chumba kwa kutumia mkono mwingine.

    “Wewe muhuni, sitaki tena!”

    “Mama alishikwa haja akaniomba nimsaidie. Ebu sogea katotoo!” Hughes alijitahidi kusema alivyoweza katika kushawishi huku akiwa hana uhakika kama alipatia kuwekeza nguvu za ushawishi imara.

    Jackline alipotaka kupiga kelele, alimziba mdomo!

    Na wakati huo mama mkwe alikuwa ametoka kitandani akiangalia bila kuamini macho yake; bado alikuwa amevurugwa sana akilini kiasi asijue sahihi ilikuwa ipi katika kutenda!

    “Tulia nikupe mahitaji. Wewe ni mwanamke sawasawa na hawa…leo utapata haki, utaijua haki!” Hughes alimueleza Jackline kwa sauti tulivu huku akimbeba kwa nguvu hadi kitandani.

    Jackline alijitahidi kujibandua katika ushikwaji na ubebwaji ule, lakini alishindwa kuzuia; na kwakuwa alikuwa akitumia nguvu nyingi ndivyo alijikuta akiishia akishuhudia amezidiwa nguvu, kwamba alianza hatimaye kulegea hata kabla ya kufikishwa kitandani ambapo aliachiwa akiangukia!

    “Hughes niache! Nihurumieeh!” Jackline alijikuta akisema maneno hayo bila kutoa sauti kali na kubwa kama alivyofanya kipindi kilichopita ingawaje bado alitamani apige kelele kwasababu hapo mdomo haukuzibwa wakati mikono mikubwa yenye nguvu ya Hughes ilipokuwa ikivua gauni lake la kulalia.

    Mama mkwe bado alisimama, akishangaa.



    Hughes alipomaliza kumuweka Jackline katika kuwa hakuvaa chochote kama alivyokuwa yeye, ndivyo alizidisha kumueleza kwamba hakukuwa na jambo lililoharibika kwani hata yeye atakuwa akitimiziwa kiu zake na hivyo kutakiwa asiwe na wasiwasi tena. Na wakati huo, tayari alianza kuitembeza mikono yake akitomasa maungo, ikipapasa ngozi ya mapaja yaliyokuwa nyororo na yakimetameta kutokana na kuakisiwa na ule mwangaza hafifu; isitoshe, mishiko na mipapaso ya mikono ilisaidiwa sana na mihangaiko ya uchokozaji wa kucha ya kidole chake kimoja ambacho alihakikisha kiliishi hivyo kwa ajili ya habari hizohizo.

    Kwamba, uti wa mgongo ulichokozwa na ukucha ule uliokuwa ukipita kwa utaratibu na upole; halikadhalika, ukucha huo ulipitia kwa nyakati zake katika kuchezea matiti mabichi ambapo mdomo wa Hughes uliposogea, basi ndivyo uliibaini harufu fulani, harufu ya kitoto.

    Hatimaye, Jackline aliwehuka hasa huku mama mkwe akifanywa mtazamaji bila kutaraji, kwamba, hivyo alifanya akijiachia kwa kujinyonganyonga mikononi mwa Hughes ambaye sasa alifurahi sana kwamba nafasi murua ilijitengeneza yenyewe ili wote awe ‘akiwararua’ bila kuhofia mwingine kujua!

    Sasa, kadri raha ilivyomtambaa Jackline, ndivyo mwili wake haukuisha kushtukashtuka, akisisimka kiasi hata alihisi machozi yalichungulia kutaka kumwagika, yaani, alihisi angelia kabla hata utepe haujakatwa!

    Lakini ni kweli, kwani ndivyo wakati fulani alijikuta akilia kutokana na jinsi alivyopatiwa kwa kuzamishwa ndani ya hofu za kuogopa yatakavyokwenda hatimaye huku hisia na mwili vikitamani sana mwendo uanze ili aujue uhondo wa kupelekwa akipeleka!

    Sasa hakufikiri alivyofumaniza!

    Hapo alijawa na hitaji!

    Akipenda kutunguliwa huku akihofia sana!

    Akipenda kuijua raha aliyokuwa akihofia sana!



    Huku Jackline akitetemeka sana ndivyo mama mkwe alipandwa zaidi na ashki kiasi cha kuona hapo alikuwa akiteseka haijapata kutokea maishani; lakini, hatahivyo, chache za akili zilikuwa bado zimeinuka na zikijulisha hivyo ndivyo ilimpasa kutulia kama alihitaji ‘habari isivuje’!

    Kweli, mama aliumia ingawaje alijua alipaswa kukubali kutazama bila kupinga huku akielewa ingeweza kuja nafasi ambayo angelazimika kufanya usaidizi katika kulazimisha uelekeo wa muondoko huo endapo Jackline’ angegoma kupelekwa!

    Hatahivyo, kwa Jackline (sawa na ilivyokuwa kwa Hughes) haikuwa mwendo huo, kwani sasa alikuwa haumizwi kwa maana ya kutekeseka; isipokuwa alikuwa akipokea akishwa raha iliyokuwa awali maumivu!



    Wakati Hughes akiisogelea ‘shabaha’ na tayari akiwa amejivisha kinga mpya, ndivyo mwili wa Jackline ulizidi maradufu kutetemeka huku kitanda cha futi sita kwa sita kikionekana hakiwatoshi, kwani kutokutosha huko kuliletwa na hali ya muondoko ambapo Jackline alianzisha tabia ya kusogea nyuma kila ‘shabaha’ ilipokuwa katikati ya kunaswa; na kwa hali hivyo ndivyo Hughes hakuacha kufukuza ingawaje hakupenda kutumia msuri wa simba mwenye njaa mbele ya swala katikati ya makucha yake!

    Jackline alihema sana!

    Hughes alihema sana!

    Halikadhalika, mama alifanya hivyo huku akishindwa kuacha kukodoa; lakini hapo tayari alikuwa katika kilele cha uchu huku kukata tamaa kukimnukia!



    Ndio, hatimaye, mama mkwe alianza kujihisi vibaya huku akiruhusu ashki iliyokuwa kileleni ikiporomoka.

    Hata ndivyo alipokea hakupaswa kushuhudia ‘hayo’ ili aumizwe moyoni na mwanaume ambaye alimpokea kwa tafsiri mbili zenye alama za juu – kwani, ni kweli alimpenda sana Hughes kama mpenzi wake wa kitandani huku akikiri halikadhalika alimpenda sana kama mume wa bintiwe mwenye kuitunza familia yake vyema!

    Sasa alihisi makosa huku akili zikichota uchambuzi kwamba angependa azijue namna za kuweza kuepukana na hali hii kwani ni kweli alichukia ‘muondoko wote’ huku akiwa hajui iwapo alimchukia Hughes na Jackline; kwani hapo, hatahivyo, aliingiza utambuzi kuwa yawezekana ni muda mrefu Hughes alimfukuzia Jackline ambaye hapa alishangaza jinsi ilivyokwenda kirahisi katika kutulizwa; na ndivyo hisia zilianza kushika kwamba Hughes alikuwa mpenzi ambaye alipenda kutembea na wengine!

    Kwahiyo, angezijua mbinu za kujinasua ni dhahiri kipindi hiki angefanya; lakini, maskini hakujua na hivyo kuishia kusikitika kwa ndani huku akifahamu habari chache ambazo hatahivyo hazikusimama ili kumsaidia katika kuitimiza dhamira yake hiyo iliyomjia hapo!

    Mama mkwe alifahamu jinsi ya kulisema tatizo; lakini hakujua angelitatuaje kama mwendo ulikuwa ni kujinasua huku akizidi kukiri alimpenda sana Hughes katika tafsiri zile mbili; lakini pamoja na yote hayo alijua zipo elekezi katika kumpeleka mwanamke kujinasua kutoka kwa mwanaume aliyempenda mwenye kupenda kuwa na wanawake wengine katika kuwabadilisha mithili ya nguo.



    Nini alifahamu sasa?

    Kwamba, alipaswa kuepuka vipindi vya ukimya akijua kusema, kusubiri na kusikiliza bila kukatisha mazungumzo.

    Kwamba, alipaswa kujua kutomlazimisha mpenzi wake kubadili kile alichokusudia kukielezea baada ya kusema alichohitaji kijulikane; na yote haya alipaswa kuujua uvumilivu wa usikivu ili kumuwezesha kujua mbivu na mbichi za mwenzake na hatimaye kusogezwa katika kuelewa wapi angesimamia kwa lengo la kuingia hatua ya kutafuta nguvu na msukumo wa kuanza kutatua tatizo.

    Hivyo kuelekea katika kujua ni wapi angesimamia haikuwa shida kwake; isipokuwa shida ilikuwa ni habari za kukamata ujasiri wa kujinasua kama bado angeendelea kusimamia katika uamuzi huo kama suluhisho muafaka la kukamilisha utatuzi wa tatizo.



    ******

    Ilikuwa jumatano ya 27/12/1989 wakati Michelle Obrien alipojikuta akiamka ghafla huku akiachia uyowe utadhani hatari ndio ilimshtusha, kwani hata alitetemeka sana huku mwili ukitema jasho kiasi shuka lililoana! Ndivyo akipapasa macho, alijikuta akitaka kukurupuka; lakini alipothubutu aliishia kushindwa!

    Akajaribu tena…vilevile, alishindwa!

    Ndivyo akatazama zaidi, akiangaza pembezoni mwake hata…aah, hata alivutwa kushangaa zaidi, kwani alishuhudia mikono na miguu yake ikiwa imefungwa pingu katika mifumbati ya kitanda; hofu ikafinya zaidi, akikumbuka zaidi, akiumia zaidi!



    *******

    Akiwa bado ndani ya tafakari, mara waliingia watu wawili, mmoja mwanaume na mwingine mwanamke; hao walivalia makoti meupe yaliyopitiliza hadi magotini.

    Yule mwanaume ambaye pia alivaa miwani, alimsalimia huku uso wake ukiendelea kuizungumza tabasamu iliyoonekana kuwepo hata kabla ya ujio wake humo chumbani, “habari mgonjwa? Wajisikiaje?”

    Mwanamke naye alitoa salamu.

    Obrien hakujibu mapema; bado mshangao ulimchapa.

    Tabasamu la yule mwanaume lilibadilika mara, lakini halikubadilika kwamba alikasirishwa au vyovyote yenye kushabiana na hilo; bali huyo alibadilisha tazama zake kwa kuachia sura iliyotafsirika aliongezeka kumuhurumia!

    Ndipo Obrien alitoa sauti ndogo ya mguno, akifurahi kutazamwa vile huku akihisi kukumbuka jambo fulani lililokuwa na ubavu kiasi wa kutuliza fikra zake kwa muda.

    Ndio, ni kweli alikumbuka ingawaje bado bakora za mshangao zilinena kwa vuma zake; alikumbuka alimtambua mwanaume huyo! Na hata alikumbuka upole na ujali wa mwanaume huyo mbele zake tangu atolewe katika kile chumba cha wagonjwa mahututi akiwa hajui nini kilimsibu.

    Mkumbukwa alikuwa Dr Dickman.



    “Dokta hapa ni hospitali!” Obrien alisema kwa sauti kubwa kiasi na kwa mwendo wa kuropoka; lakini vile alisema kwa tafsiri ya kutambulisha kuwa sasa alijua alikuwa wapi.

    Dr Dickman hakutia neno zaidi ya kuchezesha kichwa kuonyesha ukubali uliobebwa ndani ya ujali.

    Michelle Obrien aliitazama mikono yake kwa kitambo kifupi kabla ya kurejesha tazamo lake kwa daktari huku akitengeneza ishara kwamba hali hiyo mpya ambayo haikuwepo wakati akiletwa chumba hiki ilimshangaza.

    Daktari yule aliachia tabasamu dogo katika kujulisha alielewa mgonjwa wake aliwaza nini, na kisha alisema, “tulia upate tiba. Afya yako ndio habari muhimu zaidi kwa sasa. Stay patient.”



    Wote kwa pamoja, daktari na Nesi walianza kazi ya kumpima; na walipofikia hatua fulani waliridhika huku Daktari akimaliza kwa kutoa maagizo kwa Nesi. Kisha Obrien aligeukiwa tena na kusemeshwa kwa sauti ya huruma sana, “Pumzisha mawazo, kwani ndivyo utarahisisha kupona haraka zaidi.”







    ITAENDELEA 

0 comments:

Post a Comment

Blog