Search This Blog

Friday 28 October 2022

JINI MWEUPE - 1

 







    IMEANDIKWA NA : HAKIKA JONATHAN



    *********************************************************************************



    Simulizi : Jini Mweupe

    Sehemu Ya Kwanza (1)





    Manila; Ufilipino,



    Donald Mbeto,akiwa amevalia koti jeupe la kidaktari, machoni alivalia miwani, huku ndevu za bandia zikikipamba kidevu chake. Alitembea kufuata korido ndefu, alikata kona kushoto, kisha akakunja kulia, uso kwa uso akakutana na chumba kikubwa chenye mlango wa vioo. “pharmaceutical room”(Chumba cha madawa), chumba kile kilisomeka kwa lugha ya kizungu,Donald aliingiza mkono wake wa kulia mfukoni, huku akiangaza upande wa kulia na kushoto kwa umakini wa hali ya juu, alitoa mkono wake mfukoni, huku akiwa ameshika funguo yake ndogo iliyokuwa na uwezo wa kufungua mlango wowote ule.



    “Ooooh shit! kuna kamera!, hapa nikusambaratisha upumbavu wao, watawakamata wengine sio mimi ……”,Donald Mbeto  alizungumza, aliruka teke la kinyume nyume, sekunde tu kamera iliyokuwa juu ya mlango ilisambaratika vipande vipande.



    Umeme ulianza kuwaka na kuzima, haraka haraka alifungua mlango wa chumba, ukagoma,akafungua tena ukagoma!,ikabidi abadili mbinu maana funguo ilimcheleweshea kazi.



    “Hapa tayali shoti imetokea, ndani ya sekunde ishirini walinzi watakua mahali hapa, sikubali! lazima nikamilishe kazi! “,Donald Mbeto, muuaji wa kimataifa aliongea, huku akitazama taa ambazo ziliwaka na kuzima.



    “Yes, yes! kazi imekwisha! “!”,Donald alizungumza, akiwa na tabasamu usoni mwake. Alivuta waya wa kamera uliokuwa ukining’inia na kutoa cheche, akagusisha kwenye kitasa,vioo vikamcheka, mlango ukaachia.



    Bila kuchelewa, moja kwa moja akaingia stoo ya kuhifadhia madawa, akaingiza kwenye koti lake mkono wa kushoto,akatoa sindano yake iliyojaa sumu.



    “Sodium pentobarbital…!, kesho ni kilio na msiba mzito kwa taifa la Ufilipino, poleni wafiwa “,Donald Mbeto aliongea kwa kejeli huku akitabasamu kwa furaha, alichomeka sindano kwenye dawa zote aina ya kimiminika, na kuweka sumu hiyo hatari kwa maisha ya binadamu!



    “,done!, kazi imekwisha! “,alizungumza, akaangalia saa yake ya mkononi, sekunde tano tu zilitumika kukamilisha zoezi la kuweka sumu kwenye madawa.



    Alitoka nje, akarudisha mlango,na kuubana vizuri kama ulivyokuwa awali. Alipotazama huku na kule, hakuona mtu, zaidi ya taa ambazo ziliwaka na kuzima,kutokana na shoti ya umeme iliyosababishwa na kamera iliyopigwa teke na Donald.



    “Hawa walinzi wazembe kweli, anyway! ngoja nipotee mahala hapa …”,Donald Mbeto alizungumza, huku akipiga hatua kadhaa,ghafla rundo la walinzi walikua mbele yake, hakuwa na wasiwasi,aliweka koti lake vizuri kama daktari.



    “Hey doctor, what is the problem? “,(Hey daktari, kuna tatizo gani,?) ,mlinzi mmoja alimuuliza swali Donald Mbeto kwa kutumia lugha ya kizungu, baada ya kugundua alikuwa daktari wa kizungu na sio Mfilipini, kutokana na ndevu za kizungu, ndevu za bandia kidevuni mwake.



    “I don’t know anything”,(Sifahamu chochote kile …) ,Donald Mbeto aliwajibu kwa kifupi, akaendelea na safari yake, alinyosha korido aliyoingia nayo, akakunja kulia,moja kwa moja mpaka kwenye lifti,harakaharaka alibonyeza batani ukutani, lifti ikaanza safari ya kupandisha ghorofa za juu zaidi.



    ………………………………



    “Aim not sure if that person is a doctor of this hospital, let’s go back and look for him, aim sure is the one who did this ……”,(Sina uhakika kama mtu yule ni daktari wa hospitali hii, turudi tukamtafute ,nina uhakika ndiye aliyefanya hivi …”,mmoja wa walinzi aliongea, huku wakitazama kamera ambayo ilisambaratika vipande vipande.



    Ili kupata maswali ya majibu yao, kundi la walinzi lilirudi haraka sana huku kila mmoja akiwa amekamatilia silaha yake kikamilifu, tayali kwa ajili ya kumkabili bwana Donald Mbeto.



    Sekunde tano baadae, walikuwa katika eneo la lifti, walipotaka kuingia tu, ghafla mlio wa helikopta uliwashtua, kwa mbali waliona helikopta iliyokuwa ikiwaka taa mbalimbali, nyeupe na nyekundu, ikipotea kutoka juu ya jengo..



    “That bastard has gone…”,(Yule mwanaharamu ameondoka) “,mlinzi mmoja alizungumza, huku akitazama helikopta ambayo ilikuwa ikipotea machoni, kupitia vioo vya jengo ambavyo viliwawezesha kuona nje.



    “,Yes, but who is that person? “,(Ndio, lakini mtu yule ni nani? ),mlinzi mwingine alizungumza.



    “We don’t know, “(Hatufahamu) ,wote waliitikia.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “We have to be careful,anything can happen at any time “,(Tunapaswa kuwa makini, kitu chochote kinaweza kutokea muda wowote), mlinzi mmoja aliongea, kisha walipanda lifti kushuka chini kwenye wodi za wagonjwa kuendelea na majukumu ya ulinzi usiku huu uliojaa utata.



    …………………………………



    11;20am



         Uongozi wa hospitali ya mjii mkuu wa Manila, hospitali kubwa nchini Ufilipino, “Manila international hospital “,wanatangaza vifo vya watu zaidi ya elfu mbili, huku chanzo kikitajwa ni sumu aina ya Sodium pentobarbital iliyowekwa katika dawa zote aina ya kimiminika.



    Wagonjwa wote waliotumia dawa hizo, walikufa baada ya dakika moja tu. Waandishi wa habari, maafisa wa jeshi la polisi walizagaa pembe zote za hospitali kukusanya habari, huku walinzi wa usiku uliopita wakiwa washtakiwa namba mbili kwenye sakata hili,tayali wakiwa mahabusu kusubili kusomewa mashtaka yao ya kula njama na muuaji.



    “We are so sad to announce, more than two thousand people have died this morning,so ……”,(Tuna huzuni kubwa kutangaza, zaidi ya watu elfu mbili wamefariki dunia asubuhi hii, kwahiyo ……”,



    Kabla hata sentesi haijamalizika, kamanda Kendrick alishindwa kuvumilia, alizima tv yake, alichukua koti lake na kuanza safari kuelekea katika hospitali ya Manila, kwa ajili ya kujua ukweli kuhusu vifo vya zaidi ya watu elfu mbili ghafla kiasi kile.



    “Nina siku mbili tu tangu nitoke Tanzania, sijapata chochote kile kuhusu muuaji tunayemtafuta, lakini mbona matukio yanafanana, bila shaka ninaweza kugundua jambo fulani. ” ,kamanda Kendrick, askari mpelelezi namba moja wa kuaminika, miongoni mwa askari watatu wa “The super three Soldiers ” kutoka Tanzania, aliongea huku akishuka ngazi kutoka katika jengo la hoteli alilofikia mjini Manila, akiwa na shauku ya kutaka kujua chanzo cha mauaji ya wagonjwa zaidi ya elfu mbili katika hospitali ya kimataifa ya mji wa Manila.



    …………………………………



    01: 00pm



    “Kamanda Philipo,!, kamanda namba mbili ovaaa…!”,Kamanda Kendrick alizungumza kwenye simu, huku akiwa katika chumba cha mawasiliano katika hospitali ya Manila, kwa ajili ya ukaguzi wa kamera za siri zilizofungwa hospitalini bila kuonekana kwa urahisi.



    “,Kamanda Kendrick, kamanda namba moja, nakupata ovaaaa! “,upande wa pili wa simu uliongea.



    “,Muuaji aliyeweka sumu, katumia mbinu zilizotumika Tanzania, kichwani kaficha uhalisia kwa kutumia ndevu za bandia,nakuomba uje unisaidie kumtambua kama ndiye mtuhumiwa tunaye mtafuta au siye!”Kendrick alizungumza, huku askari wa Ufilipino wakimtazama bila kuelewa chochote kile, walichosubili ni taarifa tu watakayopewa na Kendrick kupitia lugha ya kingereza.



    “Sawa kamanda namba moja, dakika ishirini nitakua hapo! “,upande wa pili wa simu ulizungumza.



    “,Sawa ovaaa!, nakusubili “,Kamanda Kendrick alizungumza na kukata simu, akimsubili kwa hamu mpelelezi mwenzake aliyefikia hoteli nyingine, kamanda namba mbili, mtaalamu wa kompyuta wa kutegemewa katika kikundi cha “The super three Soldiers ” kutoka Tanzania, wakiwa na siku mbili tu tangu wafike nchini Ufilipino kwa lengo la kumtafuta muuaji, muuaji aliyeua watu kwa sumu nchini Tanzania.



    “Inspector, can you tell us what is going on? (Inspecta, unaweza kutwambia nini kinaendelea? “,),askari mmoja wa Kifilipini, askari mwenye cheo kikubwa kuzidi wenzake alimuuliza Kendrick.



    “,don’t wory boss, Few minutes to come, we will identify the killer …”,(Usjali mkubwa, dakika chache zijazo, tutamtambua muuaji,”) ,Kamanda Kendrick alizungumza, huku askari wa Kifilipini aliyeuliza swali akitikisa kichwa kuashiria kukubaliana naye



    …………………………………



    01:30pm



         “,What! kwanini anafanya hivi, kwanini anaua bila hatia? anataka nini?,ameua Tanzania, amekuja tena huku kaua, anataka nini? “,Kamanda Philipo aliongea kwa hasira, huku akitazama sura halisi ya muuaji akiwa na nywele zake za mnvi zilizomtapakaa kichwani pamoja na kidevuni, baada ya kuondolewa ndevu bandia, kwa kutumia kompyuta na kumtambua muuaji maarufu anayetafutwa kila kona, bwana Donald Bento aliyependa kujiita Jini mweupe.



    “,Tutamkamata tu, lazima tufahamu ukweli! “,Kamanda Kendrick aliongea huku akitazama kioo cha Kompyuta, baada ya Kamanda Philipo kutumia utalamu wake wa kompyuta ipasavyo.



    “,Is Donald Bento the one who killed people? “,(Donad Bento ndiye aliyeua watu? “,)askari wa Kifilipino aliyeuliza swali awali, aliuliza swali kwa mara nyingine huku wote wakiwa bize kutazama kioo cha kompyuta kilichopambwa na picha ya Donald Bento, pamoja na jina lake lililiondikwa kwa herufi kubwa, “DONALD MBETO”(JINI MWEUPE)



    “Yes boss, “(Ndio mkubwa), kamanda Kendrick alimjibu mkuu wa upelelezi kutoka Ufilipino, kamanda aliyekuwa nao bega kwa bega tangu waanze upelelezi wao nchini Ufilipino.



    Kamanda Kendrick alichoka, kamanda Philipo alichoka, jenerali pamoja na askari wote wa Kifilipino walichoka   ,hawakujua waanzie wapi kumtia nguvuni Donald Mbeto maarufu kama jini mweupe.



    “,Jambo la kwanza tunapaswa kujua Donald Mbeto yupo nchini, au ametorokea nchi zingine, tukitatua swala hili, kazi itakua rahisi kwetu ” ,Kamanda Kendrick aliongea, wote wakisubili taarifa kutoka kwa wataalamu wa rada uwanja wa ndege wa Manila, kuhusu ndege yoyote iliyotoka masaa kumi yaliyopita wakati wa usiku.



    “,Hapo umenena ,hujawahi kuniangusha kamanda namba moja! “,kamanda Philipo aliongea, vidole vyake vikichezea bastola yake, akafungua magazini, akapachika risasi, akafunga tena, akawa tayali kusubili amli kutoka kwa jenerali wa Kifilipini.



    “,Helikopta aina ya SH-60B Seahawk iliingia Ufilipino siku tano zilizopita, ikaweka kambi katika msitu wa Kijani kaskazini mwa Ufilipini,ilifika majira ya saa sita usiku katika hospitali ya Manila,baada ya kutua ghorofa ya mwisho, muuaji alipokamilisha kazi, ilitoweka nchini kupitia bahari ya hindi “,Kamanda Kendrick alisoma ujumbe mfupi, ujumbe ulioingia kwa lugha ya kifilipini na kutafsiriwa kwa Kiswahili, taarifa iliyotumwa na viongozi wa rada ya Ufilipini iliyo ongoza ndege zote zinazoingia na kutoka, baada ya kukamilisha uchunguzi wao.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    “,Inspector Kendrick and your fellow, go to look for the killer, i will help you if you need assistance, good luck! “,lkamanda Kendrick na mwenzako, nendeni mkamtafute Muuaji, nitawasaidia kama mtahitaji msaada, kila laheri! )”,jenerali Fernando alizungumza, kisha akasimama, akapigiwa saluti, akatoka katika chumba cha mawasiliano ndani ya hospitali ya Manila, baada ya kumtambua muhusika wa mauji, kupitia kamera za ziri zilizonasa zura ya bandia ya Donald Mbeto.



    “,Ok salute! “,kamanda Kendrick alizungumza, wote pamoja na kamanda Philipo wakapiga saluti kukubali amli, kazi waliyotumwa na taifa la Tanzania, pamoja na nchi ya Ufilipino kama heshima kubwa kwao.



    …………………………………



    Masaa kumi nyuma;



          Helikopta aina ya SH -60B Seahawk iliondoka usawa wa ghorofa ya mwisho, katika hospitali ya Manila saa kumi usiku, ikapaa usawa wa mita mia mbili za jengo kwa umbali wa kilomita mbili, ikapaa juu umbali wa mita mia mbili kumi na tano kutoka usawa wa bahari, ikapotelea angani.



    “,Hongera komandoo! kazi nzuri! pesa zako tumekuwekea katika akaunti yako ya siri katika benki ya dunia, ukikamilisha kazi hii ya mwisho, katika hospitali ya Gano, tutakupatia pesa zako zote trilioni moja, kisha utaenda kuishi mafichoni Amerika “,Paresh Kumar, bosi wa Kihindi alimpongeza Donald Mbeto, helikopta ikichanja anga kuvuka mipaka ya nchi kabla jua halijachomoza.



    “,Usjali bosi, omba Mungu nisife mapema kazi zako zikalala “,Donald Mbeto aliongea, sura yake halisi ikaonekana, alivua sura na ndevu zake za bandia, akabaki na mnvi zake kidevuni pamoja na rasta nyingi za mnvi kichwani zilizotoa tafsiri ya jina lake, jini mweupe.



    “,Hahahaaa, kweli wewe jini Mweupe, kiumbe hatari sana “,Paresh Kumar alikimudu kiswahili ipasavyo, alicheka kwa furaha huku akishika rasta nyeupe za Donald Mbeto kumpongeza.



    …………………………………



    Gano; 04;20pm



           Helikopta aina ya Seahawk ilitua bahari ya Hindi, katika meli kubwa aina ya MD47 Faaraquat inayomilikiwa na kundi kubwa la D47 ,kundi la kigaidi tajiri zaidi duniani.



    Donald Mbeto alishuka, akapokelewa kwa furaha na washirika wote wa kundi D47, kundi ambalo lilijishughulisha na kuuza madawa ya kulevya, silaha, pamoja na madini.



    “,Karibu White house! karibu makao makuu, pole na kazi, jiandae kwa kazi nyingine dakika kumi zijazo “,daktari mkuu wa kundi la D47 alimpokea Donald Mbeto, akamuongoza mpaka kwenye chumba cha upasuaji, huku akishangiliwa kwa furaha na wafuasi wa kundi hili waliokuwa katika mazoezi ya karate katika uwanja mkubwa melini.



    “,Umbo la kike litakua poa zaidi! ,meza dawa hizi, zinaitwa “voice changer “,zingatia, wakati wa kazi usinywe kinywaji chochote kile, sauti yako itarejea kuwa ya kiume “,dokta Govinda, daktari wa Kihindi, alifanikiwa kubadili mwonekano wa Donald Mbeto kwa dakika tano tu.



    Akiwa na makalio ya kike yaliyofungwa mwilini, chuchu za bandia pamoja na uso wa mwanamke wa kijapani aliovaa usoni, Donald Mbeto alikabidhiwa sindano ya sumu ile ile ya Sodium pentobarbital, sumu hatari iliyotumiwa na Donald Mbeto kufanya mauaji. Alitoka chumba cha upasuaji,akapigiwa magoti ya heshima na saluti, akapakiwa kwenye nyambizi,safari ikaanza kuelekea nchi ya Gano,kisiwa cha bahari ya Hindi Afrika ya Mashariki.



    Nyambizi ilizama futi ishirini kwenda chini, isije ikagundulika na kushambuliwa na helikopta za umoja wa mataifa, zilizofanya doria usiku na mchana katika bahari ya hindi kupinga ugaidi.



    “,Nyambizi itasimama kilomita tano kutoka nchi kavu, utachukua mitungi ya gesi, utaogelea baharini kama samaki! dakika kumi zinakutosha kukamilisha misheni hii, utarudi kwa kutumia spidi boti ya mvuvi ambaye ni mshirika wetu”,Kepteni wa Nyambizi alitoa maelekezo kwa Donald Mbeto.



    “,Haina shida! “,kwa sauti ya kike,baada ya kunywa vidonge aina ya “voice changer “,Donald Mbeto aliongea, huku akitikisa kichwa kuashiria kukubaliana na maelekezo aliyopewa. Nyambizi ikaendelea kupiga mbizi chini ya bahari.



    …………………………………



    Tanzania; 6:00 pm



           Kamanda Catherine, kamanda namba tatu wa kundi la wapelelezi watatu, “the super three soldiers “kutoka Tanzania, alihisi hali ya hatari katika bahari ya hindi na nchi zote za Afrika mashariki zilizopakana na bahari hii iliyojaa magaidi na maharamia.



    “Nyambizi hii mbona imeibuka ghafla tu! kwanini mwanzoni haikusafiri usawa unaoruhusiwa na umoja wa mataifa, nina wasiwasi! bila shaka imebeba magendo …”,kamanda Catherine aliongea, alinyenyua mkonga wa simu yake ya mezani, akabonyeza namba kadhaa kisha akaweka sikioni.



    “,Halloo kamanda, nakupata ovaa! “,upande wa pili wa simu uliongea.



    “,Kamanda namba tatu, nakupata ovaa! “,kamanda Catherine aliitikia kupitia simu yake ya mezani.



    “,Nikusaidie nini TSTS namba tatu …”,sauti ilisikika upande wa pili wa simu.



    “,Tuma ndege za kijeshi, kilomita kumi kuelekea kisiwa cha Gano, kuna Nyambizi imevuka usawa wa kimataifa, inaelekea Gano au huku Tanzania, nendeni mkaichunguze ……”,Kamanda Catherine, TSTS namba tatu alitoa maelekezo kwa jeshi la majini.



    “,Tumekupata mkuu, dakika ishirini tutakua eneo hilo “,sauti ilisikika upande wa pili, simu ikakatwa.



    Kamanda Catherine akabonyeza namba kadhaa za kimataifa, akampigia kamanda Philipo, namba haipatikani, akabonyeza tena, akampigia kamanda Kendrick, namba haipatikani, akatuma ujumbe kupitia saa zao maalumu za mkononi, “Network error “,(Mtandao unashida),saa ya kijeshi iliwaka taa nyejundu, huku ujumbe wa meseji ukionekana kwenye kioo chake.



    “,Kuna shida! sio bure, kuna shida! idara ya ulinzi haiko salama, “Kamanda Catherine alinyanyuka, alichukua bastola yake, akafunga kiatu chake pamoja na mkanda wa kijeshi, akafunga mlango wa ofisi yao ya siri kwa kutumia namba maalumu, akatoweka alikokujua yeye ……



    …………………………………



    Gano; 7;00pm



         Donald Mbeto alishuka ufukwe wa bahari nchini Gano, akavua mavazi na mitungi ya gesi akaitelekeza, akavaa nguo za kazi, suti ya kike,akavaa begi lake, akatokomea.



    “,Sista wapi? lakini umependeza, “dereva taksi eneo la bandari, alimuuliza Donald Mbeto.



    “,Hospitali ya taifa Gano! “!Donald Mbeto kwa sauti ya kike, alijibu kwa kifupi.



    “,Ohooo! lakini umependeza, ingekua vizuri ungenipatia namba yako, hata pesa zako sihitaji …”,dereva taksi alichombeza, huku akiliondoa gari kwa fujo eneo la bandari, kufuata barabara kuu ya jiji kuu la Gano.



    “,Mbona hunijibu, acha kulinga!”,dereva yule aliyekuwa amebabuka midomo, bila shaka alibugia unga kama sio bangi, alichombeza bila kujua uhalisia wa mtu anayemchombeza.



    Donald Mbeto alichomoa bastola, akaikoki, kisha akairudisha kiunoni. Akachukua kisu chake kidogo, akajichana kwenye kidole, damu zikatoka, akalamba, yote ni kumtisha dereva taksi.



    “,Basi inatosha, nisamehe tu dada, nilikua sijui! “,bila hata kuguswa, dereva taksi alijitetea, alishuhudia kila kitu Donald Mbeto alichokifanya.



    “,Ole wako useme uliyoyaona, nitakuua!Kwa sauti ya kike, Donald Mbeto alitoa onyo, akakunja nne, amani na ukimya ukatawala ndani ya gari.



    Masaa manne yaliyopita;



      TSTS (the super three soldier) namba moja, kamanda Kendrick, akiwa ameongozana na kamanda Philipo, TSTS namba mbili, walitoka katika hospitali ya manila, kichwani waliwaza kuelekea haraka sana kaskazini mwa jiji la Manila, helikopta aina ya Seahawk ilipotua mara ya kwanza, kabla ya kufika hospitalini kutekeleza tukio la kuweka sumu na kuua maelfu ya watu.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Waliamini wangegundua jambo lolote, ambalo lingewasaidia kugundua mahali ambapo Donald Mbeto alitorokea.



    Wakawasha gari, wakatoweka eneo la hospitali, wakiwa ndani ya gari, ni muda mrefu walikuwa wamezima simu zao,wakaamua kuziwasha, mlio wa meseji nyingi ukawapokea, meseji zilizotoka kwa “the super three soldier ” namba tatu, kamanda Catherine.



    “,Mipaka haiko salama, kuna nyambizi imeibuka ghafla na kuanza kuonekana usawa wa umoja wa mataifa baharini, kilomita kumi kutoka ufukweni, hatujui inaelekea wapi, Tanzania au Gano, isitoshe hatujui imebeba nini! “,meseji ilisomeka, ujumbe kutoka kwa kamanda mtata na mtaalamu wa tehama jeshini, kamanda wa kuaminika na serikali ya Tanzania, Catherine Obadia.



    “,Paki gari pambeni tufanye mawasiliano naye, kisha tutaendelea na safari! “,Kamanda Kendrick aliongea, kamanda Philipo akatii amri, akapaki difenda ya polisi pembeni. Kamanda Kendrick akabonyeza namba namba za kimataifa, akaweka simu sikioni, bila shaka alikuwa anampigia kamanda Catherine.



    …………………………………



    Tanzania;610pm, bandarini



              Jeshi la majini walikuwa bize, waliogopeshwa na taarifa waliyo ipokea muda mfupi uliopita, kuhusu usalama hafifu kilomita kumi eneo la bahari.



    “,Askari sita ndani ya nyambizi, sita ndani ya chopa, sita ndani ya spidi boti, hakikisheni nyambizi ya maadui haiwaponyoki!! mkuu wa jeshi la majini aliongea, akageuka ghafla, akakutana na sura asiyoitegemea, “Karibu bosi, saluti! “,akaongea, akapiga saluti, vijana wake wakafuatia, wakapiga saluti.



    “,Nikitoa kazi staki uzembe!,ndiyo maana nimekuja mwenyewe”,akaangalia saa, akaona nusu saa ilikuwa imepita tangu atoe taarifa.Akazidi kuvimba kwa hasira.



    “,Hapana bosi, nilikuwa na ……”,mkuu wa jeshi la majini aliongea.



    “,Hapana nini! staki uzembe kwenye kazi, nchi ikivamiwa sisi ndio wa kwanza kuulizwa, hebu kila mmoja apande kwenye usafiri wake tuondoke, haijalishi una nyota, una V mbili au praiveti, wote kazini! “,kamanda Catherine aliongea, licha ya kuwa na nyota tatu begani, hakuwa mzembe na kazi, aliweka vyeo vyake chini, akatanguliza kazi mbele, jambo ambalo lilipelekea kutunukiwa medali tano na umoja wa mataifa, kama mwanamke pekee wa wa Afrika mashariki kuingia vitani akiwa na kundi lake la the super three soldiers nchini Kongo, akafanikiwa kurudi salama.



    “,Sawa mkuu, saluti! “,askari wote wa majini waliitikia,ndege ya majini yenye askari sita pamoja na rubani akiwa wa saba, ilitembea kwenye maji kisha ikapaa angani, ikapaa futi hamsini kwenda juu., spidi boti ikafuatia ikaingia baharini na kupotea, kamanda Catherine akiongoza askari saba, akiwemo mkuu wa majeshi ya majini mwenye nyota moja begani, waliingia ndani ya nyambizi, nyambizi ikatembea baada ya dakika tano, kisha ikazama futi kumi kwenda chini, ikapotea kwenye uso wa bahari. Makundi yote yalivaa hedifoni masikioni, simu kubwa za kipolisi (redio call)  zilikua mikononi, wakiwasiliana na kujulishana kila hatua.



    “,Haloo, haloo, yoyote usawa wa helikopta, pokea simu ovaa! “,simu ilisikika kwenye helikopta, ikapokelewa, kisha ikasogezwa karibu na mdomo.



    “,Usawa wa nyambizi, nakupata ovaa! “,mmoja kati ya makamanda sita kwenye helikopta aliongea.



    “,baada ya kilomita kumi, simameni eneo hilo, makombola ya ndege yachomoeni kuangaza baharini, kuweni makini msishambuliwe! “,upande wa pili wa simu ulizungumza.



    “,Sawa kamanda, tumekupata ovaa! “,usawa wa helikopta ukajibu, kisha simu ikakatwa, tayali kifaa cha kupimia umbali, kilianza kuonyesha kilomita tisa zikiwa zimemalizwa,helikopta ikapunguza mwendo, makombola mawili kama mapembe yakachomoza kwa mbele, tayali kuishambulia nyambizi yoyote eneo hilo.



    …………………………………



    “,Sogeza karibu na Nyambizi hiyo, kilomita nne kutoka hapa! “,kamanda Catherine aliamua kuubeba mzigo mwenyewe, mtungi wa gesi ulikuwa mgongoni, miguuni na mikononi alivaa vifaa vya kumsaidia kuogelea, usoni alivaa helmenti iliyounganishwa na mtungi wa gesi, alitoa maelekezo huku akijiweka sawa.



    Dakika tano mbele, nyambizi ilifika eneo la tukio, wakaiona nyambizi kilomita tano mbele kwa kifaa maalumu, Nyambizi ya jeshi ikapandisha kidogo usawa wa bahari, mlango ukatokeza juu ya usawa wa bahari, Catherine akazima saa yake ili asinaswe na mawasiliano upande wa pili wa maadui, akatoka nje ya nyambizi yao, kisha ikazama tena, yeye akajitupa baharini na kuogelea kama samaki.



    …………………………………



    Tuko hatarini, nyambizi yetu imeshanaswa na jeshi la ulinzi, japo sijajua kama jeshi hilo ni la umoja wa mataifa, au jeshi la nchi ya Tanzania,au Gano, sijajua kabisa! “,Kepteni aliongea, akiwa na vijana wawili tu ndani ya nyambizi inayomilikiwa na kundi la kigaidi la D47.



    “,Hamna jinsi, wakitufikia lazima watuzidi nguvu, cha msingi ni kuwashambulia na makombola wakijaribu kutusogelea ili kuepuka kukamatwa……!”,gaidi kati ya wawili, akiwa na sura nyeusi, kipara chenye mafuta mengi kichwani, alitoa maoni yake kwa kepteni wa nyambizi.



    “,Sawa kabisa, ndege inayotutafuta imesimama juu eneo moja, hatuwezi kuchomoza usawa wa bahari, nyambizi yao pia iko kilomita tano kutoka hapa, imesimama pia inatunga sheria, hatuwezi kuondoka na kumwacha Donald Mbeto, lazima tumsubili, hawa wapuuzi wakitusogelea tunawashambulia kwa nyukilia zetu hawata amini macho yao! “,kepteni wa Nyambizi ya D47,aliendelea kujisifia, bila kujua mtego ambao waliwekewa, Catherine alikuwa anawasogelea bila kifaa chochote cha mawasiliano, asionekane katika mitambo yao na kuwanasa kirahisi.



    …………………………………



    Kamanda Catherine aliifikia Nyambizi, akatoboa kwenye injini, hakutosheka, akatafuta sehemu ya imejensi( imejensi chemba),sehemu ya kutokea kama kuna hatari yoyote, akabana mahala pale, huku akiwa na visu viwili mikononi, alibana, akisubili yoyote yule atakayetoka, aweze kumshughulikia.



    Aliendelea kusubilia, maji yakizidi kuingia ndani ya nyambizi,hakukata tamaa, hakukuwa na sehemu nyingine yakutokea kwa urahisi zaidi ya “emergency chamber “,aliendelea kusubili.



    …………………………………



    Ghafla hewa ilikuwa nzito ndani ya meli,injini ikazima, umeme ukazima,hofu ikamtawala kepteni pamoja na magaidi wawili waliokuwa ndani ya Nyambizi, wakashika bastola mikononi mwao, walitambua tayali walikuwa wamevamiwa,wakaanza kutembea kwa makini ndani ya Nyambizi,ghafla mawimbi yaliwasomba hakuna aliyekumbuka kuwahi boya wala mitungi ya kuogelea,kepteni akabamizwa na mawimbi kwenye chuma cha mlango wa kuelekea chooni akapasuka kichwa, akafa palepale, gaidi mmoja akajigonga huku na kule, akajitahidi kujitetea, maji yalimzidi nguvu, akazimia, gaidi wa tatu maji yalimsomba mpaka karibu na mlango, akaukamatilia vizuri, akaufungua, ukashindikana, ulikuwa umefungwa na komeo, akasogelea chemba ya kutokea kama kuna hatari, chemba karibu na mlango, akaipiga kwa nguvu na mguu, ikafunguka, akaanza kujitahidi kutoka, akishandana na maji yaliyokuwa yanaingia ndani ya nyambizi, akavutwa kwa nje, bila kujua mtu aliyemvuta.



    …………………………………



    Catherine baada ya kusubili kwa muda mrefu alitaka kukata tamaa, akataka kubadili mbinu,akiwa anatafakari, alishangaa mlango kusukumwa na mguu, akamvutia adui yake nje, akatupa bomu ndani ya nyambizi, likasaidiwa na maji mpaka ndani.



    Akamchoma visu vya miguu gaidi yule, akajuta kusaidiwa msaada wa kinafiki kwa kilio kikuu,nguvu hakua nazo tena, ujanja hakua nao tena, akaanza kupandishwa juu na mtu aliyemsaidia na kumshambulia akiwa hajitambui vizuri, Catherine aliogelea kama samaki aina ya papa kwa kasi ya ajabu, kabla bomu alilotupia ndani ya nyambizi ya D47 halijaripuka.



    …………………………………



    Nusu saa baadae;



           Mtuhumiwa alikuwa amepakizwa juu ya ndege,pembeni akiwa ameketi Catherine akimuhoji taratibu,”,Puuuu, puuuu!! “,bomu liliripuka, nyambizi ya D47 ikasambaratika vipande vipande baharini, hakuna chochote kilichosalia.



    “,Nitasema, nitasema! “,gaidi lilipiga kelele kwa maumivu. Catherine alimuunguza na sigara jichoni, alilia kama mtoto, Catherine hakua na huruma kazini.



    “,Sema, wewe ni nani, mmekuja kufanya nini? “,Catherine alifoka.



    “,Tumemleta Donald Mbeto, amekuja kukamilisha kazi ya mauaji nchini Gano, baada ya kutoka Ufilipino masaa kadhaa yaliyopita!! ” ,gaidi lile lilieleza kila kitu kwa huzuni.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “, Unasemaje, mmemleta Donald Mbeto kufanya mauji,?”,Catherine aliuliza akiwa haamini, alikuwa amechanganyikiwa, akachana kwa kisu shati la gaidi yule, akatazama mgongoni, kuna kitu alikua anahakikisha kama aliyo ambiwa ni kweli, “D47”,chata kubwa iliyozungushiwa duara ilikuwa mgongoni, aliamini kile alichoambiwa, askari wote ndani ya helikopta wakachanganyikiwa.



    Simu iliita, ikaita tena ikazima, hakuweza kuisikia, mawazo yalikua mbali, “mkuu pokea simu “,aliambiwa na askari pembeni yake, kamanda Catherine akashtuka, alipoangalia kwenye kioo akapokea haraka, “Kamanda kendrick “,kioo cha simu, jina la mtu aliyepiga simu ilionekana kwenye skrini.



    …………………………………



    Manila; Ufilipino.;



           “,Donard Mbeto yuko huku, rudini haraka, hapa tuko na gaidi tuliyemkamata, wamemleta na Nyambizi nchini Gano kufanya mauaji mengine, rudini haraka sana! “,kamanda Catherine aliongea.



    “,Unasemaje? “,kamanda Kendrick akauliza swali tena, hakuamini alichoambiwa.



    “,Rudini huku usiku huu, Donald Mbeto yuko huku Afrika Mashariki, njoeni kabla hajaua wengine! “,kamanda Catherine alimalizia,Kamanda Kendrick pamoja pamoja na Philipo hawakua na haja ya kuuliza tena, walijipakia kwenye gari na kutoweka walikokujua wao, kichwani walichanganyikiwa.



    Gano; 8:00



             Gari dogo ya abiria, ikiwa na bango dogo la prastiki rangi ya njano, lililosomeka “TAXI ”   kwa herufi kubwa, ilipaki nje ya hospitali kuu ya taifa nchini Gano, “tumefika bosi! “,kwa heshima, akiwa amejawa na wasiwasi, dereva taksi aliongea. Akafungua mlango wa taksi kwa rimoti ndogo iliyokuwa mikononi mwake, milango ikafunguka, Donald Mbeto akachomoa dola kumi, sawa na shilingi elfu ishirini, akampatia dereva taksi yule.



    “,Sina chenji bosi, “dereva taksi aliongea.



    “,Usjali, sihitaji chenji yako, naomba unisubili hapa hapa, “kwa sauti ya kike, Donald Mbeto aliongea, dereva taxi akiwa na tabasamu,akatikisa kichwa kukubali, alifurahi kupokea dili kubwa la pesa nyingi jioni hii, Donald Mbeto akaondoka zake, akapanda ngazi kuelekea Hospitalini.



    …………………………………



    Alikuwa mwanamke mrembo, hakuna aliyemfikiria vibaya,madaktari, manesi, pamoja na wagonjwa waligeuza shingo zao kumtazama, mwanamke huyu wa kijapani aliyetembea kwa maringo,chuchu zake, makalio yake, yalisababisha vidume wenye uchu wa ngono kummezea mate, hawakujua kuwa mwanamke yule alikuwa na makalio pamoja na matiti ya bandia yaliyofungwa kwa ustadi mkubwa,isitoshe hakuwa mwanamke, bali alikuwa mwanaume rijali kabisa.



    Nywele zake nyeupe za mnvi hazikuonekana tena, alivaa wigi kuzizuia,usoni alivalishwa sura ya bandia ya mwanamke wa kijapani, kazi iliyofanywa na daktari wa kundi la magaidi D47.



    Donald Mbeto alikata kushoto, akapandisha ngazi, alikuwa anaelekea katika choo cha kike, akafika, ramani yote ya jengo ilikuwa kichwani mwake, haikua mara ya kwanza kutekeleza mauaji yenye taswira ya kufanana katika hospitali hii. “,Nina dakika kumi tu, ninapaswa kukamilisha kazi na kutoweka eneo hili, ” Donald Mbeto aliongea, alifunga mlango wa choo kwa ndani, hakutaka mtu yoyote kumgundua.



    Akapanda juu, akakanyaga choo, akaufikia mfuniko juu kwenye dali, akaufungua, ukafunguka, akachomoa tochi yake, akapanda na kutumbukia ndani ya dali.



    Giza lilikuwa kali, popo walizunguka huku na kule, akachomoa tochi yake kubwa,akaangaza, popo wakakwepa mwanga, wakakimbia mbali”,chumba cha madawa kiko mbele, “aliongea, akaanza kutembelea tumbo polepole, akijivuta taratibu, dakika kumi baadae, akafikia mfuniko alioutarajia, akasogeza sikio karibu na mfuniko, akasikiliza kwa sekunde mbili, hakusikia sauti yoyote ile, “Hakuna mtu yoyote kwenye chumba cha madawa, “Donald Mbeto aliongea, akausogeza mfuniko pembeni, chumba cha kuhifadhia madawa kikaonekana, hakukuwa na mtu yoyote yule, Donald Mbeto akapenya kwenye tundu, akatumbukia ndani..



    Bila roho ya huruma, akachomoa sindano yake, sindano iliyojaa sumu aina ya Sodium pentobarbital, sumu Kali inayoua binadamu kwa dakika moja tu. Akaiingiza sumu katika dawa zote za maji, akachanganya, hakutaka mtu yoyote kuhisi dawa hizo, akasogea karibu na drip za maji,akaingiza sumu kwenye chupa takribani hamsini za drip ya maji, akasogelea chupa za drip ya quinine, dawa ya malaria, akaweka sumu ndani ya chupa takribani mia mbili, akazichanganya vizuri…



    Masaa mawili nyuma;

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

          Chopa ya jeshi la Tanzania, ilishuka makao makuu ya Jeshi, askari wakashuka, huku kamanda Catherine Obadia akishuka akiwa na mtuhumiwa wa ugaidi, mtuhumiwa ambae sura yake ilikuwa imefunikwa na kitambaa cheusi.



    “,Songa mbele mpuuzi wewe, lazima utuambie makao makuu yenu yako wapi, haiwezekani mtusumbue kila siku, kila matukio ni nyinyi ndio mnahusika, why? “,kamanda Catherine aliongea, huku akimsindikiza na mateke mtuhumiwa, mateke mawili yaliyomrushia ndani ya chumba cha mahabusu, akagagaa bila msaada wowote. Alimuacha akiwa na kitambaa chake usoni, akafunga mlango, akatokomea na funguo mahali alikokufahamu yeye …



    …………………………………





    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog