Search This Blog

Tuesday 20 December 2022

SHETANI' MTANASHATI NA AMRI KUU 10 - 3

  http://pseudepigraphas.blogspot.com/2020/06/shetani-mtanashati-na-amri-kuu-10.html


Kisha Lustig anamueleza zaidi kuwa kiboksi hicho kina uwezo wa kuprint noti moja ya dola 100 kwa kila masaa 6. Kutokana na mtu kuhisi kuwa atapata faida kubwa akiwa na kiboksi hicho chenye uwezo wa kumpatia dola 100 kwa kila masaa 6 pasipo kuvuja jasho hivyo walikuwa wakinunua kwa moyo mkunjufu kabisa na Lustig aliwauzia kiboksi hiki kwa dola elfu thelathini za marekani kwa kiboksi kimoja.


Kumbuka hapa wako ndani ya meli inayosafiri kuelekea Paris, Ufaransa kwahiyo huyu mtu akishanunua kiboksi baada ya masaa sita kiboksi kile kitaprint noti ya dola 100, baada ya masaa sita mengine kitaprint noti nyingine ya dola mia.. Lakini baada ya hapo kitaanza kuprint karatasi za kawaida nyeusi na hapa ndipo mtu hushituka kuwa amekwisha tapeliwa lakini kwa muda huu meli inakuwa imeshafika Paris na Lustig ameshashuka kwenye Meli na kutokomea.


efa8a23754df1ada8d957bd178cd859b.jpg

Eiffel Tower: mnara uliouzwa mara mbili na Lustig kwa wafanyabiashara mashuhuri jijini Paris.


Kuna siku Lustig alikuwa Paris, akiwa ameshashuka kwenye meli baada ya kumuuzia mtu mashine ya kuprint hela. Katika mizunguko yake akakutana na habari kwenye gazeti ambayo ilimsisimua. Habari hii ilikuwa inahusu taarifa ya serikali ikizungumzia kuhusu ni jinsi gani ilivyokuwa inaingia gharama kubwa kutunza mnara wa Eiffel.


Makala hii lengo lake hasa ilikuwa ni serikali wanajitetea baada ya raia kulalamika kuwa serikali hawako makini kuutunza mnara huo kwani umekuwa mkuu kuu na haupendezi tena. Katika makala hiyo serikali ilijitetea kuwa hata kuupaka rangi mnara huo ni gharama kubwa mno kwahiyo wananchi wawe wapole tu.


Taa ikawaka kichwani kwa Lustig.. Akang'amua hii ilikuwa ni fursa adhimu kwake kujitajirisha.


Lustig akaandaa vitambulisho na nyaraka za kugushi za serikali ya ufarasa ambazo zilimtambulisha yeye kama Naibu Mkurugenzi katika Wizara ya Mawasiliano akishugulikia masula ya Posta na Telegram. Kisha akaenda katika hoteli de Crillon ambayo kwa kipindi hicho ilikuwa ndio hoteli ya hadhi ya juu kabisa katika mji wa Paris na akakodi chumba na ukumbi kwa wageni wenye hadhi (executives).


Baada ya hapo akawasiliana na wafanya biashara wakubwa sita wenye makampuni makubwa zaidi ya biashara ya vyuma chakavu na akawaalika hotelini kwa mazungumzo maalumu.


Bila kusita wafanyaniashara hao wakawasili hotelini na moja kwa moja mazungumzo na Lustig yakaanza. Lustig akajitambulisha na kuwaeleza kuwa kikao hicho ni cha siri na serikali imewateua wao kwa ajili ya zoezi maalumu. Akawaeleza kuwa kama wanavyoona kwenye vyombo vya habari gharama za kutunza mnara wa Eiffel imekuwa kubwa kiasi kwamba serikali imeshindwa na hivyo suluhisho pekee ni kuubomoa. Hivyo basi serikali inataka kuwapa mmoja wapo kati yao deal ya kuubomoa mnara huo na kuchukua vyuma vitakavyo patikana.


Lakini akawasisitiza kuwa suala hilo ni aibu kwa serikali ndio maana hawakutaka hata kutangaza tenda hadharani hivyo anaomba ishu hii anayoongea nao iwe ni siri kubwa kwani serikali haitaki hilo suala lifahamike mpaka pale itakapofikia siku chache kabla ya kuubomoa. Akawaeleza kuwa tenda hiyo atapewa yule ambaye ataweka dau kubwa kuliko wenzake (highest bidder).


Baada ya mazungumzo hayo Lustig akawachukua kwa kutumia gari ya kifahari ya Limousine aliyokuwa ameikodi na kuwapeleka mpaka kwenye mnara wa Eiffel kwa ajili ya kuukagua pamoja na kupeana maelekezo zaidi.


Baada ya kufika kwenye mnara wakiwa bado wanapeana maelekezo, Lustig pia akatumia mwanya huu kuwasoma wafanyabiashara hao ili kujua yupi mwenye shauku zaidi ya dili hiyo na yupi itakuwa raisi kwake kumtapeli. Baada ya kuwachunguza kwa kina karata yake ikaangukia kwa mfanyabiashata aliyeitwa Andre Poisson.


Baada ya kumaliza zoezi hili kesho yake wafanyabiashara hao wote waliwasilisha bids zao na kwa kuwa Lustig tayari alikuwa amemlenga Andre Poisson hivyo aliwasiliana naye huyu pekee kumtaarifu kuwa serikali imempitisha na kumpa hiyo deal.





0 comments:

Post a Comment

Blog