Search This Blog

Monday 19 December 2022

QUEEN MONICA (3) - 4

  





Simulizi : Queen Monica (3)
Sehemu Ya Nne (4)


“There is this new handsome guy from south Africa,Austin.Ni kijana mzuri.Japokuwa simfahamu tabia zake laini ni kijana mzuri mtanashati na ,mstaarabu .Yule jamaa nahisi anaweza akanifaa kwa sababu kwanza yeye si mkaazi wa hapa,makazi yake ni afrika kusini kwa hiyo hata kama nikifanya naye mapenzi hataweza kufanya matangazo na nikimtazama anaonekana ni kijana mwelewa.Isitoshe ana hadhi yangu.Tatizo ni namna ya kuweza kumpata kwani siwezi kukurupuka tu na kumfuata kumtaka tufanye mapenzi.Lazima nitafute njia itakayomfanya ashawishike kutaka kufanya nami mapenzi.Lazima nimsisimue.Tena nimekumbuka aliniomba kama tunaweza kutoka kwa chakula cha usiku nikamwamia kwamba nitampa jibu.Nadhani hapo ndipo sehemu nzuri ya kuanzia .Nitakubali kutoka naye kesho nitamchunguza nimfahamu ni mtu wa aina gani ” akatabasamu “Nadhani sasa nimepata muafaka na suluhisho la tatizo hili.Austin anaweza kunifaa.Najua sintakuwa namfanyia vizuri David lakini sina namna nyingine ya kufanya vinginevyo nitaikuta nimezidiwa na kufanya mambo mengine yasiyofaa.” Akachukua simu yake na kumuandikia Austin ujumbe mfupi wa kukubali ombi lake la kupata chakula usiku pamoja. Taratibu Monica akajilaza kitandani na kuanza kuutafuta usingizi alikuwa amechoka sana **************** Austin alikaribia sana kufika Rozana night club ukaingia ujumbe katika simu yake akapunguza mwendo wa gari na kuufungua akausoma kisha akatabasamu.Ujumbe ule ulitoka kwa Monica ambao ulisomeka “Dinner tomorrow. 8 Oclock” “Thank you Monica.Good night” Austin akaandika uumbe na kuutuma kwa Monica “Mambo yanazidi kukaa sawa.Monica amekubali ombi langu la kukutana naye kwa chakula cha usiku.Hii ni hatua kubwa na nzuri katika kuikamilisha kazi ya rais.Wakati mambo yangu yanakwenda vizuri Boaz na Maria wameibuka na wanataka kuharibu kila kitu.Hapana siko tayari kuifanya kazi ya Boaz.Eti nimteke Monica na kumtesa.Sintokubali kumgusa malaika Yule.Lazima nitafute namna ya kumlinda kwani hivi sasa tayari amekwisha anza kuwindwa na Boaz.Naona kuna mgogoro mkubwa unanukia kati yangu na Boaz.Nikiingia katika mgogoro na Boaz moja kwa moja nitakuwa nimeingia katika mgogoro na Maria.Dah ! sikutaka jambo kama hilo litokee lakini endapo itabidi iwe hivyo sintakuwa na namna nyingine zaidi ya kuingia katika mgogoro.Vyovyote itakavyokuwa lazima nimlinde Monica” akawaza Austin huku akipunguza mwendo akakata kushoto na kushika ujia ulioeleka Rozana night club.Kulikuwa na idadi kubwa ya watu na magari kutokana na klabu hii kutoa huduma ya burudani kwa saa ishirini na nne.Alielekea sehemu ya maegesho akaegesha gari na kushuka akaangaza huku na huku kuhakiki usalama akaridhika kila mtu alikuwa na hamsini zake “Pamechangamka sana mahali hapa.Burudani zipo za kutosha” akawaza Austin akaingia klabuni na kupanda ngazi kuelekea ghorofani kama alivyokuwa amekubaliana na Job.Watu walikuwa ni wengi ndani ya klabu na viti vyote vya kaunta vilijaa.Austin akapiga jicho pande zote na kuwaona watu wawili wakiinuka katika mojawapo ya meza iliyokuwa karibu na kaunta akaenda kuketi.Muhudumu aliyevalia nadhifu akafika haraka haraka na kumudumia kinywaji akaendelea kunywa taratibu huku akivuta muda akimsubiri Job.Mara akashikwa bega na mtu akageuka haraka haraka na kuiona sura iliyomstua “Jo......!!” akataka kusema neno lakini Yule mtu akaweka kidole mdomoni ishara ya kumtaka anyamaze halafu akamfanyia ishara kwa kichwa amfuate.Austin akainuka na kuangaza pande zote kisha akamfuata Yule mtu “Haya ni kama maajabu.Kweli Job ni jasusi wa hali ya juu.Mchana ni kichaa lakini usiku ni mtanashati namna hii kiasi kwamba ni vigumu hata kumtambua.Mchana anavaa matambara na usiku anavaa suti kali .Dah ! amenifurahisha sana kwa hii staili yake .Huyu haswa ndiye mtu ninayemuhitaji katika operesheni hii” akawaza Austin na kuendelea kumfuata Job aliyeelekea katika maegesho ya magari ,akaingia katika gari moja jeusi,Austin naye akaingia katika gari lake na kuondoka akilifuata gari alilopanda Job Walivuka daraja la Nyerere na kuingia Kigamboni halafu wakaelekea eneo la mto Kazi.Kwa kutumia kifaa cha kufungulia toka mbali Job akalifungua geti na kuingia ndani,Austin naye akafuata kisha geti likajifunga “Hapa ni wapi? Nani anaishi katika jumba hili kubwa? Austin akajiuliza maswali mara baada ya kushuka garini “Karibu Austin” Job akasema na kumfanyia ishara Austin amfuate wakaelekea hadi katika sebule kubwa ambayo karibu samani zake zilikuwa zimefunikwa na ilionyesha wazi kwamba hakukuwa na mtu aliyekuwa akiishi pale.Job akafunua kitambaa kilichofunika sofa na kupukuta vumbi “Karibu uketi Austin” “Job,first of all ,tell me what is this place? Nani anaishi hapa? Why are we here? Akauliza Austin “Relax Austin,utafahamu kila kitu lakini kabla ya yote kuna jambo nataka kufanya” akasema Job akatoka pale sebuleni na baada ya kama dakika tano akarejea akiwa na kompyuta ndogo akaiweka mezani akaiwasha na kuanza kubonyeza halafu akamgeukia Austin “Austin karibu sana .Utanisamehe kwani humu ndani hakuna kinywaji chochote.No body lives here” “Job you are amazing.How can ....” Kabla Austin hajamaliza alichotaka kukisema Job akadakia “I know what you want to say.I’m not crazy Austin.I repeat I’m not crazy” akasema Job huku akitabasamu “Hii ni nyumba yangu ya siri.Hakuna anayeishi humu ila huwa ninakuja mara kwa mara hasa nyakati kama hizi au wakati nina kazi za kufanya” “Umewezaje kufanya hili likawezekana na watu wasikutilie shaka? Akauliza Austin “Hahahaa!!!.Austin umenisahau kwamba mimi ndiye Job.Kwa kifupi tu ni kwamba imenilazimu kuishi katika maisha haya kwa miaka mitatu sasa na nmekuw anikija hapa mara kwa mara nyakati za usiku.Kila ni japo hapa huwa nachukua tahadhari kubwa.Ninazo kamera saba za siri ambazo nimezitega kwenye miti katika njia ya kujia hapa ambazo si rahisi kuonekana .Niingiapo hapa ndani huwa ninafuatilia kamera zote za njiani kuhakiki kama hakuna anayenifuatilia.Kwa hapa nyumbani pekee ninazo kamera kumi na tatu na hata niwapo kule kwa kaka huwa ninaweza kujua kila kinachoendelea hapa kupitia kifaa kidogo mithili ya simu ninachotembea nacho kila sehemu.” Akasema Job na kumuonyesha Austin mfumo mzima wa kamera ulivyo “That’s good.Kumbe umejizatiti haswa.” Akasema Austin “Nilinunua shamba hili toka kwa mama mmoja wa kiarabu ambaye kwa sasa anaishi Oman.Sikuwahi kumueleza mke wangu juu ya shamba hili .Ni eneo kubwa la ekari ishirini na saba.Kuna nyumba saba za waliokuwa watumishi wa huyo mama na niliponunua sikuwaondoa watu hao bali niliboresha zaidi makazi yao na kuwapatia kila mmoja sehemu ya kulima na kufuga kwa hiyo hawa pia ni walinzi wengine wazuri wa nyumba hii.Kwa hiyo Austin hayo ndiyo maelezo mafupi ya nyumba hii.Vipi unaendeleaje na maisha yako? Unaishi wapi kwa sasa? Akauliza Job halafu akamtazama Austin na kutikisa kichwa huku akitabsaamu “Nikikutazama siamini kama kweli ni wewe Austin.Nilipokuona leo nilipatwa na mstuko mkubwa nikadhani labda ni mzimu wako umenijia kwani sikutegemea kabisa kukuona tena katika maisha haya kutokana na taarifa ya mwisho niliyoipata kuwa ulipotea wakati wa operesheni ya kuwakomboa wale watanzania waliotekwa na Alshabaab nchini Somalia.Welcome back to life brother..” akasema Job huku akicheka.Austin naye akacheka kidogo na kusema “I’m back to life.They wanted me dead but now I’m back to haunt them.I’ll haunt each soul that signed for my death !! akasema Austin kwa hasira “What real happened brother? Please tell me how you survived” akasema Job akavuta pumzi ndefu akainama akawaza halafu akasema “Nilipata tetesi nikiwa katika kozi fupi nchini Korea kusini kuwa mke wangu Monalisa ana mahusiano na mwanaume mwingine.Sikuzipuuza tetesi hizo na nilipanga kufanya uchunguzi wangu pindi nitakaporejea nyumbani.Baada ya kumaliza mafunzo na kurudi nyumbani nilimkuta Monalisa akiwa na gari lenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni mia mbili.Nilistuka na kuuliza alikopata gari lile akanieleza kuwa amechukua mkopo benki na ameanza biashara ya madini inayomuingizia fedha nyingi na faida anayoipata ndiyo iliyomuwezesha kununua gari lile la kifahari.Ni kweli alikuwa na ofisi yake ya kununua na kuuza madini ya vito.Sikutaka kuonyesha wasi wasi wowote bali nilianza uchunguzi wangu kimya kimya ili kubaini ukweli.Nilipochunguza nikagundua kwamba ni kweli Mona alikuwa na mahusiano na mtu mmoja anaitwa Dogo Bill.Huyu ni mfanya biashara bilionea na jina hilo alipewa kutokana na kupata utajiri mkubwa akiwa bado kijana mdogo.Jina Dogo Bill lina maamisha Dogo Bilionea.Jina lake halisi ni Eliah Mkobweka.Niliendelea kufanya uchunguzi na kugundua kuwa huyu Dogo Bill ndiye aliyemnunulia gari lile na ndiye aliyempa mtaji wa biashara ya madini.Niliumia sana hasa nikikumbuka nilikotoka na Monalisa.Nilikwenda mbali zaidi na kugundua kuwa Dogo Bill ni mmoja kati ya wafanyabiashara wakubwa wa dawa za kulevya Afrika mashariki na kwa kiasi kikubwa utajiri wake unatokana na biashara hiyo.Niligundua kuwa huyu jamaa anaifanya biashara hiyo kwa siri kubwa kiasi cha kuwa vigumu kumfaham kuwa anahusika na biashara hiyo.Nilikwenda mbali zaidi nikagundua kuwa kuna mtandao ambao unafanya kazi ya kuteka watu toka mikoa mbalimbali kuwaua na kisha hutengeneza nyaraka Bandia za kuonyesha kuwa ni watu kutoka mataifa ya nje na husafirisha maiti hiyo kwenda nje ya nchi.Maiti hiyo hutolewa kila kitu ndani na kujazwa dawa za kulevya kisha husafirishwa.Kila mwezi maiti zaidi ya kumi zimekuwa zikisafirishwa kwenda nje ya nchi zikiwa zimejaa dawa za kulevya.Mtandao huu ni mpana na umesambaa katika sehemu zote muhimu na ndiyo maana hadi leo hii hakuna yeyote aliyewahi kuripotiwa kukamatwa kwa jambo hili.Kilichonistua zaidi ni kwamba kuna watu watatu wakubwa kabisa waliokuwa karibu na rais ambao nao wanajihusisha na biashara hii.Primusi Buke aliwahi kuwa waziri alifariki kwa maradhi ya kansa ya ini,Philipo Muro alifariki kwa ajali ya gari na ambaye yuko hai mpaka sasa ni msaidizi wa rais anaitwa Wilson Mukasha.Sina hakika kama rais anamfahamu huyu msaidizi wake ni mtu wa namna gani kwani kama angemfahamu naamini asingekubali kumuweka karibu yake.” Austin akasimama kwa mstuko alioupata “Vipi Austin mbona umestuka? “Umesema Wilson mukasha? Akauliza “Ndiyo,unamfahamu? Akauliza Job lakini Austin hakujibu kitu “ Austin !! akaita Job “ Umestuka baada ya kumtaja Wilson Mukasha ,unamfahamu? “yes I know him” akajibu Austin “Wakati nikiendelea na uchunguzi wangu ili kubaini mambo mengi yanayohusiana na mtandao huo,kuna kosa moja nililifanya ambalo lilisababisha niingie katika hali hii” akanyamaza akashusha pumzi na baada ya muda akasema “Niligundua kwamba ndani ya mtandao ule kulikuwa na watu wengine wakubwa zaidi ya akina Mukasha.Usiku moja niliondoka kuwahi jambo Fulani linalohusiana na uchunguzi niliokuwa naendelea kuufanya kumbe nilifanya kosa moja kubwa.Nilisahau kuuficha ushahidi wote nilioupata kuhusiana na mahusiano ya Monalisa na Dogo Bill.Huku nyuma Mona aliweza kugundua kuwa ninamchunguza baada ya kuuona ule ushahidi.Sikurejea nyumbani usiku ule na niliporejea oh my gosh !!..” Job akanyamaza “What happened Job? Akauliza Austin “My wife and my daughter were already gone.Aliondoka na kila ushahidi niliokuwa nimeupata kuhusu yeye na dogo Bill.I was left alone.Kwa kuwa simu yake tayari nilikuwa nimeiwekea program maalum ya kurekodi mawasiliano yake yote anayoyafanya niliweza kusikia mazungumzo ya mwisho kati yake na dogo Bill,Mona akimfahamisha Bill kwamba tayari nimegundua kuhusu mahusiano yao na Bill akamwambia kwamba wakati umefika kwa yeye kuondoka kwani kama angeendelea kukaa kwangu mambo yao yote yangeharibika.Mwisho alimuuliza Mona kama yuko tayari kuachana nami na bila kigugumizi Mona akajibu kuwa yuko tayari.Bill akamwambia kwamba aanze kujiandaa anatuma watu kwenda kumchukua.Mwisho kabisa alimhakikishia Mona kwamba asihofu nitashughulikiwa na sintakuwa kikwazo tena kwao.Hayo ndiyo yalikuwa maongezi ya mwisho ya mke wangu na simu yake ikazimwa.Haikuwahi kupatikana tena hadi leo hii na sielewi yeye na mwanangu wako wapi.Kwa mujibu wa mipango yao kilichokuwa kinafuata ilikuwa ni kunimaliza na kwa mtandao wao namna ulivyo mkubwa lazima wangenimaliza haraka sana hivyo ikanilazimu kujifanya nimerukwa na akili.Wengi walistushwa mno kwa hali ile ya ghafla lakini hakuna anayeufahamu ukweli .Wote wanajua kwamba nilipatwa na uchizi baada ya kuachwa na mke wangu.Ndugu zangu walinichukua wakanipeleka kwa mganga wa kienyeji kutibiwa wakiamini kuwa nimerogwa.Waliuza nyumba na vitu vyangu vyote yakiwamo magari mawili kwa kigezo cha kupata hela ya kunitibu lakini fedha yote waligawana wakijua kuwa mimi ni kichaa.Baada ya kuona kuwa sipati nafuu wakanihamishia kule kwa kaka ninakoishi na hakuna hata mmoja anayenijali tena.Wote wanajua kuwa tayari mimi ni kichaa na sintopona tena.Pamoja na hali yangu hiyo lakini nimekuwa nikiendelea na uchunguzi wangu kimya kimya” akanyamaza na kumeza mate “Unaendelea na uchunguzi upi? Akauliza Austin “Ukiacha wewe ,kuna mtu mwingine mmoja ambaye anafahamu kuwa mimi si kichaa.Anafahamu kuwa nini niko hivi nilivyo na ndiye ambaye ananisaidia katika uchunguzi.Naendelea kumchunguza Dogo Bill na mtandao wake ili nipate taarifa za kutosha kabla ya kuamua kufanya kitu.Mtu huyo ambaye ninashirikiana naye anaitwa Amarachi Inyike.Ni raia wa Nigeria lakini kwa sasa anao uraia wa Tanzania na anajulikana kama Winifrida Osward ama Winnie kama alivyozoeleka.Ninaye rafiki yangu mmoja anaishi nchini Nigeria aliniomba nimsaidie dada yake ambaye aliwahi kutekwa na kundi la Boko Haram akakaa msituni kwa miaka sita hadi yeye na wenzake sitini walipookolewa na majeshi ya serikali.Akiwa msituni,Amarachi aliozwa kwa mmoja wa kiongozi wa wanamgambo hao na akazalishwa mtoto mmoja.Kwa miaka sita wakiwa msituni walikuwa wanapewa mafunzo mbali mbali ya kijeshi wakiwaandaa kuja kuwa wanamgambo wa kikundi hicho.Walifundishwa namna ya kutengeneza na kutega mabomu,kutumia silaha nzito za kivita,mbinu mbali mbali za medani,kwa ujumla waliandaliwa kuwa magaidi na walikuwa wameiva barabara.Baada ya kukombolewa na kurudishwa uraiani,maisha ya Amarachi hayakuwa mazuri na yenye furaha.Jamii iliwatenga na hakuna aliyetaka kuchangamana nao.Mtoto wa Amarachi aliuawa na watu wasiojulikana kwa madai kwamba ni damu ya magaidi na siku moja naye angekuwa gaidi.Zaidi ya mara tatu Amarachi alinusurika kuuawa lakini alijinusuru kutokana na kuwa na uwezo mkubwa wa kujihami” Job akanyamaza kidogo halafu aakendelea “Nilipoombwa na kaka yake nimsaidie sikusita kufanya hivyo ikanilazimu nimuandalie nyaraka za kuweza kumuingiza na kumuwezesha kuishi nchini Tanzania.Kaka yake ni mtu mwenye uwezo mkubwa kifedha hivyo akamjengea hoteli kubwa hapa Dar inaitwa Silver peak hotel .Amarachi au Winnie ndiye pekee ambaye amekuwa akinipa msaada kila ple ninapohitaji.Ninapohitaji kuja hapa ni yeye ambaye huja kunichukua katika sehemu tuliyoipanga kukutana na hunileta huku nikafanya kazi zangu kisha hunirudisha .Amejitahidi kwa kadiri alivyoweza na amefanikiwa kujenga urafiki na dogo Bill na hivyo amekuwa akimchunguza lakini mpaka sasa hajawahi kumuona Bill akiwa na mke wangu Mona au hata kumtaja jina.Bado haijulikani kama Mona yuko hapa nchini au ameama nchi.Sijui kama yuko hai au amekufa lakini sitaki kuumiza kichwa kujua hali yake bali akili yangu ni kwa mwanangu Millen.Kwa kumtumia Amarachi nimeweza kupata taarifa nyingi za kuhusiana na mtandao wa akina Bill.Kwa ufupi hayo ndiyo yaliyonisibu na kunifanya niishi maisha kama haya lakini kilichomo moyoni mwangu ni kisasi kibaya sana.Nataka niumalize mtandao huu nikianzia na dogo Bill lakini nimechelewa kufanya hivyo nikitaka kwanza kufahamu alipo mwanangu Millen.Nitakapopata taarifa za uhakika za mahala alipo mwanangu wingu jeusi litatanda Dar es salaam kwani nitalisimamisha jiji wakati nikiwashugulikia watu hawa waliosababisha nikaishi maisha haya.Ninachofikiria kukifanya ni Mungu pekee anayefahamu.” “Pole sana Job.Haya ndiyo madhira tunayokutana nayo katika kazi zetu hizi.Tunajitoa mno kwa ajili ya kupigania usalama wa nchi yetu lakini kinachotupata ni majuto matupu.Mara nyingi huwa ninawaza na kujuta kwa nini niliingia katika kazi hii.Sikuwahi kufikiria eti siku moja nitaukana uraia wangu na kwenda kuishi nchi za ugenini.Naamini hata wewe haukuwahi kufikiri kuwa iko siku ambayo utaishi kwa kujifanya kichaa.Lakini haya yote yanasababishwa na watu wachache waliomo katika madaraka.Ukigusa maslahi yao they make your life a living hell” akasema Austin .Ukapita ukimya “Tell me why are you here Austin? What are you doing here? Aren’t you scared of them anymore? Akauliza Job.Austin akainuka na kwenda kufunua pazia akachungulia nje baada ya muda akageuka na kumtazama Job “Niko hapa kwa kazi maalum” akanyamaza kidogo halafu akasema “Kwa sasa mimi ni meneja wa kampuni ya A.A Safaris ltd nayomilikiwa na baba mkwe wangu.Ninaishi maisha mazuri nchini afrika kusini.Sikuwa nimepanga kurejea Tanzania tena au kufaya tena kazi hizi lakini nilipigiwa simu na rais Ernest Mkasa akaniomba nirejee Tanzania kuna kazi anataka kunipa.Sikuwa tayari kwa hilo lakini akanieleza jambo moja kuwa mdogo wangu Linda amefungwa nchini China kwa kosa la kujaribu kuingiza dawa za kulevya nchini China.Ernest aliahidi kunisaidia kumtoa mdogo wangu gerezani endapo ningekubali kumfanyia kazi yake.Kwa ajili ya mdogo wangu nilikubali kurejea Tanzania kuifanya kazi ya rais.Kama alivyoahidi alifanya kila aliloweza na mdogo wangu akatolewa gerezani kwa hiyo ni zamu yangu kufanya kazi yake” akanyamaza kidogo baada ya sekunde kadhaa akaendelea “Ernest Mkasa rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania anataka nimsaidie kupata sampuli toka kwa mwanamke mmoja ambaye ameelezwa kuwa ni mwanae,kwa ajili ya kufanay kipimo cha vinasaba kubaini kama kweli ni mwanae.Tayari nimeianza kazi hiyo ambayo si ngumu na nina uhakika wa kuikamilisha ndani ya kupindi kifupi kijacho lakini ndani ya kazi hiyo kumejitokea tena kazi nyingine ambayo ni kubwa zaidi na ambayo imenibadili msimamo wangu na kunirudisha tena kazini” akatulia kidogo halafu akaendelea “Nilikueleza awali kuwa sababu kubwa ya mimi kutaka kuawa ni baada ya kugundua mpango wa kumuua rais Ferdinand.Kuna kikundi kijulikanacho kama Alberto’s ambacho kimesambaa katika sehemu mbalimbali za dunia.Historia ya kikundi hiki kuna kiongozi mmoja wa kanisa aliyeitwa Alberto aliwahi kufukuzwa katika kanisa lake baada ya kuchochea uasi ndani ya kanisa kwa kutaka yafanyike mabadiliko ambayo hayapo katika imani ya kanisa hilo. Mambo ambayo Alberto alitaka yakubaliwe na kanisa ni kuwaruhusu makasisi na watawa kuoa na kuolewa,kukubaliana na kuhalalisha mapenzi ya jinsia moja.Utoaji Mimba,matumizi ya mihadarati n.k.Aliyekuwa kiogozi wa kanisa kwa wakati huo hakufurahishwa na jambo hilo hivyo akamvua daraja Alberto na kumtimua katika kanisa.Baada ya kufukuzwa alianzisha kikundi chake ambacho yeye anakiita jumuiya ya Alberto au the Alberto’s.Aliendeleza yale yaliyomfanya akafukuzwa na kanisa.Alianza kwanza kwa kuhakikisha wakuu wa mataifa makubwa yenye nguvu wanakuwa wafuasi wake.Alberto anatumia nguvu za giza kwa hiyo alifanikiwa kuwapata wakuu hao na mataifa mengi makubwa ya amerika na ulaya yakakubaliana na mambo yake ,wakayapa nafasi .Wamehalalisha mapenzi na ndoa za jinsia moja,utoaji mimba,matumizi ya mihadarati n.k.Baada ya kusambaa katika sehemu kubwa ya dunia Alberto’s walielekeza nguvu zao bara la Afrika ambako walianza ushawishi kwa viongozi wa mataifa ya Afrika wakiyatumia mataifa makubwa .Rais aliyekuwa madarakani wakati huo Ferdinand alikataa kata kata kushawishiwa na ndiyo sababu ya kifo chake ili nafasi ya rais ishikwe na mtu wanayemtaka wao” Austin akanyamaza na kumtazama Job “Sikufahamu chochote kuhusu suala hili” akasema Job “Si rahisi kufahamu kwani ni mambo yanayokwenda kwa siri kubwa na kwa kiapo kikali hivyo yeyote anayethubutu kwenda kinyume adhabu yake ni kifo” “Dah !” akasema Job kwa mshangao “Kabla ya kuianza kazi ya rais nilitaka kufahamu kama naye ni mmoja wa Alberto’s.Awali aligoma kunijibu lakini baadae akakiri kuwafahamu Alberto’s ila yeye si mmoja wao.Alinieleza kwamba Alberto’s walitumia nguvu yao wakamuweka madarakani ili waweze kumtumia katika kazi zao mbali mbali.Kwa ufupi ni kwamba rais Ernest yuko pale kama picha tu hana maamuzi yoyote.Anapangiwa kila kitu na Alberto’s.Makamu wa rais,waziri mkuu,mawaziri na wakuu wa vyombo vya usalama wote ni watu wa Alberto’s.Karibu sehemu zote za muhimu Alberto’s wamezishika .Alberto’s pia tayari wamewaweka katika himaya yao asilimia kubwa ya wabunge na hii inawafanya wawe na nguvu kwani miswaada yote yenye manufaa kwao itapita kirahisi bila matatizo yoyote.Wanatumia pesa nyingi kila mwezi kuwalipa wabunge hawa” akasema Austin kisha akanyamaza akavuta pumzi na kusema “Baada ya kujihakikishia kwamba nchi iko mikononi mwao waliandaa muswaada wa sheria ya haki za binadamu muswada ambao ndani yake una kipengele cha kutambua haki za wapenzi wa jinsia moja,haki za utoaji mimba ,haki za watumia mihadarati n.k.Muswada huo ulitarahjia kuwasilishwa bungeni hivi karibuni na kwa sababu tayari Alberto’s wana idadi kubwa ya wabnge basi muswada huo ungepita kirahisi na kuwa sheria.Nilimsoma Ernest hakuwa amependezwa na kitendo cha yeye kuwa kama rais picha asiye na maamuzi kuhusu masuala ya nchi.Niliona namna alivyokuwa na hamu ya kuondokana na jambo hilo.Niliamua kutumia fursa hiyo vizuri kwa kumpa darasa kuhusu athari za Alberto’s na nini kitatokea kwa kizazi kijacho endapo ataacha Alberto’s waendelee kuiongoza nchi hii.Aliona msingi wa kile nilichomueleza na akakubali kuungana nami kupambana na Alberto’s.Haikuwa kazi rahisi kumshawishi lakini nashukuru Mungu alikubali na kitu cha kwanza nilichomtaka akifanye ni kuufuta muswada ule usipelekwe bungeni na badala yake uandaliwe muswada mwingine unaotaja kuwa ni kosa la jinai kujihusisha na mapenzi au ndoa ya jinsia moja,matumizi ya mihadarati na utoaji mimba.Jambo la pili nililomtaka alifanye ni kumvua wadhifa waziri mkuu na kulivunja baraza lote la mawaziri ili ateue wapya ambao si wafuasi wa Alberto’s.Tatu nilimtaka amuondoe mkuu wa majeshi na nikamshauri mtu wa kumpa nafasi hiyo ambaye ninamuamini ni mzalendo wa kweli.Ernest alikubaliana na mawazo yangu yote na tayari amekwisha yafanyia kazi.Muswada umefutwa,waziri mkuu ameondolewa,baraza la mawaziri limevunjwa,mkuu wa majeshi ameondolewa na kwa haya aliyoyafanya tayari ametoa tamko la vita kati yake na Alberto’s” Austin akamtazama Job aliyekuwa ametulia akimsikiliza.Job akavua koti “Ninahisi joto.Mambo haya si mambo madogo.Ni mambo mazito mno” akasema Job “Ni kweli haya si mambo madogo.Hii ni vita kubwa lakini tumeamua kuipigana kwa ajili ya nchi yetu,kwa ajili ya vizazi vya sasa na vijavyo.Ni vita ngumu lakini lazima tuipigane huku Mungu tukimtanguliza mbele.Alberto’s ni mtandao mkubwa na wenye nguvu ,wana uwezo wa kufanya jambo lolote kwa wakati wowote wanaotaka kwa hiyo mimi na mheshimiwa rais tayari tumeyatoa maisha yetu kupambana na mashetani hawa na lolote litakalotokea tuko tayari.Tumeanza mapambano kwa kuukata mzizi mkuu wa Alberto’s hapa nchini ambao ni ofisi ya rais.Hii ni sehemu waliyokuwa wakitegemea mno .Tumekata mzizi mwingine ambao ni waziri mkuu na baraza la mawaziri.Tumekana mzizi mwingine ambao ni mkuu wa majeshi.Haya yote yamefanyika katika kipindi kifupi na kuwastua sana Alberto’s.Pamoja na mizizi hiyo mikubwa kukatwa bado kuna kazi kubwa inatakiwa kufanywa.Makamu wa rais ni mfuasi wa Alberto’s na kibaya zaidi hata mke wa rais naye ni mfuasi wa mtandao huu.” “Even first lady??!! Job akashangaa “Ndiyo.Tena yeye ndiye aliyetumiwa kumshawishi Ernest akubali kuwa rais” “Kama ni hivyo basi mheshimiwa rais yuko katika hatari kubwa!! Akasema Job “Ni kweli rais yuko katika hatari kubwa sana na muda wowote kitu chochote kinaweza kufanyika.Kabla ya kutoa hotuba yake ile aliyotangaza kulivunja baraza la mawaziri,watu wawili asiowafahamu waliingia chumbani kwake wakiwa na bastora na kumtisha asihutubie lakini kwa kuwa tayari amekwisha jitoa mhanga akaamua kuhutubia.He’s in great danger.Na hilo ndilo hasa lililonifanya nikakutafuta .Tayari nimeongea na rais nikamfahamisha hatari inayomkabili na yeye mwenyewe ameiona hatari hiyo kwa hiyo tumeshauriana kufanya jambo moja.Nitaunda kikosi kidogo cha watu wenye weledi mkubwa katika masuala ya usalama kwa ajili ya kumlinda rais.Alberto’s wamesambaa kila kona kwa hiyo hata walinzi wake wa sasa wanaweza wakatumika kumuua kwa hiyo kwa kutumia mamlaka yake atawaondoa walinzi wake wa sasa na tutaweka walinzi wapya tutakaowateua .I need you in that team.” Akasema Austin.Job akacheka kidogo na kusema “Austin you’re my brother.Mimi na wewe tumetoka mbali .Umenifundisha mambo mengi .I respect you so much but I cant be part of that team” “C’mon Job.This is serious. I need you” akasisitiza Austin “No Austin” akajibu Job “Kwa nini Austin? Wewe ni mmoja wa watu wachache ninaotaka kushirikiana nao katika hii vita.Hii vita si ya kwangu na rais pekee bali tunapigana kwa ajili ya nchi yetu kwa hiyo ungana nami tafadhali.Nakuhitaji sana uwepo katika kikosi cha kumlinda rais.Huyu ndiye mwangaza wetu katika mapambano haya hivyo anatakiwa alindwe.Ikitokea rais akauawa kabla hatujaimaliza vita hii then we’re done.The war will be over.Ili tusifike hapo tunatakiwa kumlinda rais kwa nguvu zetu zote.” Akasema Austin “Austin ninaelewa unachokisema na niko tayari kusaidiana nawe katika mapambano haya lakini naomba nisiwe sehemu ya timu ya kumlinda rais.Nitakusaidia katika upande mwingine” “Sikia Job.Vita hii si vita nyepesi.Inahitaji watu wenye ujuzi na uzoefu wa hali ya juu katika mapambano kama haya na mmoja wa watu hao ni wewe” akasema Austin na kuinamisha kichwa kisha kwa sekunde kadhaa halafu akamtazama Job “Kuna jambo ambalo sikuwa nimekueleza bado ambalo labda linaweza kukushawishi ukakubaliana nami” “Jambo gani hilo? Akauliza Job “Hata mimi sikuwa nalifahamu ni rais ndiye aliyekuja kunieleza.Ni kwamba katika kila nchi ambayo rais wake ni mfuasi wa Alberto anapaswa kuhakikisha anawalinda na kuwawezesha wafanya biashara wakubwa wa dawa za kulevya wafanye biashara yao kwa uhuru bila kubughudhiwa na chombo chochote cha usalama.Hiki ni chanzo kikubwa cha mapato kwa Alberto’s kwani wafanya biashara hao walio chini yao hutoa kiasi kikubwa cha fedha kama mchango wao kwa ajili ya kuendesha jumuiya.Ernest mkasa naye akiwa chini ya Alberto’s alipewa sharti hilo na amelitekeleza na ndiyo maana utaona katika kipindi cha uongozi wake biashara ya dawa za kulevya imeshamiri sana hapa nchini.Hii ni kwa sababu wafanya biashara hawadhibitiwi na wako huru kufanya biashara zao.Nilimtaka anipe orodha ya wafanya biashara hao ili tuweze kupambana nao na ameahidi kunipatia orodha hiyo .Baada ya kuisikia historia yako ninahisi kuna uwezekano mkubwa hata huyo dogo Bill aliyepelekea ukaishi katika maisha haya naye yumo katika hiyo orodha .It’s tme to fight back.Ni wakati wetu wa kuwa huru.Hatuwezi kuwa huru endapo hatutawaondoa wale wote waliotufanya tuishi maisha ya namna hii ,wale ambao wameibinafsisha nchi hii na kuifanya yao,hatutakuwa huru endapo hatutafanikiwa kuwaondoa Alberto’s hapa nchini.Mpaka lini nitaikimbia nchi yangu? Makaburi ya wazazi wangu yako hapa Tanzania kwa hiyo hata kama nitabadili uraia lakini sintaweza kuibadili damu ya Tanzania.Lazima mambo haya yafike mwisho na yatafika mwisho endapo tutaweza kuwaondoa Alberto’s na mizizi yake hapa nchini.Nani wa kuwaondoa Alberto’s hapa nchini? Ni mimi ,wewe na wazalendo wengine wachache walio tayari kuifia nchi yao.Tunaweza tusifanikiwe au tusifike mbali katika vita hii lakini tukianzisha tutaungwa mkono na watu wenye nia njema na nchi hii.Naomba usiogope Job,hii ni nafasi ya pekee imejitokeza ambayo itakusaidia kulipiza kisasi kwa wale wote waliofanya maisha yako kuwa hivi pia kupata ukweli kuhusu mke na mtoto wako walipo.This is our chance brother” akasema Austin .Michirizi ya machozi ikaonekana machoni mwa Job “Austin umenichoma mno moyo wangu na kuyaamsha tena machungu niliyonayo dhidhi ya Dogo Bill na kundi lake.Wamenifanyia unyama mkubwa kuniachanisha na mke wangu.I loved Mona so much lakini kwa tamaa ya pesa akachagua kunikimbia.You are right.Its pay back time.Austin nitaungana nawe katika haya mapambano lakini si kwa kuingia katika timu ya kumlinda rais.Nataka niwe pembeni yako tupambane kwa pamoja.Nitakusaidia kutafuta watu watakaounda hicho kikosi cha ulinzi wa rais.Nataka niwepo katika uwanja wa mapambano na nihakikishe ninamkamata dogo Bill kwa mikono yangu mwenyewe.Nikubalie kwa hilo Austin” akasema Job .Austin akamtazama kwa muda halafu akatabasamu na kumpa Job mkono “Karibu katika operesheni fagio.Tunakwenda kufagia nchi hii na kuuondoa uchafu wote na kuifanya safi tena kama ilivyokuwa awali enzi za waasisi wetu” akasema Austin “Mungu atusaidie “ akasema Job “Austin baada ya kuwa tumekuwa kitu kimoja naomba sasa unipe mikakati yako namna ulivyopanga kuiendesha operesheni hii.Lakini kabla hujanieleza chochote nina ombi moja kwako” “Omba chochote Job” akasema Austin “Ahsante sana.Naomba ukubali kumuingiza Amarachi katika operesheni hii.She’s a great asset to us” Austin akakuna kichwa akafikiri kidogo halafu akamtazama Job “ Job I have to be honest with you.Hii ni opereseni tofauti sana na nyingi ambazo tumewahi kuzifanya kwa hiyo napata ugumu kidogo kulikubali ombi lako.Tunakwenda kupambana na adui mwenye nguvu na mbinu nyingi kwa hiyo tunahitaji kuwa na watu wenye uwezo mkubwa kama wewe.Zaidi ya yote I cant work with people I don’t trust” akasema Austin “Nafahamu msimamo wako Austin lakini naomba uniamini ninachokwambia.This woman is wonderfull.Ana uwezo mkubwa kiasi cha kunishangaza hata mimi .Nakuhakikishia anaweza kuwa na msaada mkubwa kwetu.She’s well trained .Please let her in” Austin akafikri tena kidogo na kusema “Sawa Job ,nimekuelewa lakini kabla sijaamua chochote kama nimjumuishe ama vipi I’ll have to talk to her in person. I want her to understand how important this mission is for me,you and for our nation” akasema Austin “Thank you”akajibu Job “Ningetaka sasa nifahamu mikakati yako kuhusiana na suala hili” akasema Job “Kitu cha kwanza tunachotakiwa kukifanya ni kutafuta namna ya kumlinda rais.Nguvu aliyonayo ni msaada mkubwa sana kwetu kwa hiyo lazima tumlinde kwa nguvu zetu zote.Tunatakiwa haraka sana tupate kikosi kipya cha kumlinda.Kwa sasa tunaendelea kujipanga ,nitakapomaliza kazi aliyonipa rais tutakaa pamoja na kujadili nini cha kufanya na wapi kwa kuanzia.” Akasema Austin “Austin we have to make things faster.Tukizidi kuchukua muda mrefu tutawapa nafasi ya kujipanga na wakatuzidi maarifa.Naamni hivi sasa watakuwa katika mstuko mkubwa kwa hili lililotokea so we have to take them by surprise.Tusiwape nafasi” akasema Job “Uko sahihi Job,lakini watu hawa wamejiimarisha sana na mizizi yao tayari imesambaa katika sehemu kubwa kwa hiyo basi inabidi tukae chini tujipange namna ya kuwakabili.Kwa pamoja tutaamua namna bora ya kuwandoa” Austin akanyamaza kidogo na kusema “Job kuna jambo lingine ambalo nadhani itakuwa vyema endapo ukilifahamu.Ukiacha kazi aliyonipa rais ya kutafuta sampuli kutoka kwa Monica,alinipa pia kazi nyingine.Alinitaka nikamtoe hospitali daktari mmoja aliyekuwa katika hatari ya kuuawa anaitwa Dr Marcelo.Mtu huyu alipigwa risasi lakini kwa juhudi za madaktari waliyaokoa maisha yake.Watu waliotaka kumuua bado waliendelea kumfuata hadi hospitali na kutaka kummaliza ndipo rais aliponitaka nikamtoe kwa siri.Nilifanikiwa kwa hilo na Dr Marcelo niko naye mahala ninapoishi.Leo hii nikiwa sina hili wala lile,amekuja ghafla mpenzi wangu Maria akiwa ameongozana na baba yake Mr Boaz .Huyu Boaz ndiye aliyenikomboa toka mikono ya Alshabaab kwa hiyo ni mtu ninayemuheshimu na kumthamini mno.Ujio wake kwangu jioni ya leo ulikuwa ni kuniomba nimfanyie kazi yake.Amenipa kazi ya kumtafuta Dr Marcelo na kukipata kitabu ambacho anakihitaji toka kwake. Alinipa maelezo marefu kidogo kuhusiana na kitabu hicho na umuhimu wake.Boaz anafahamu kuwa Marcelo anashirikiana na watu Fulani na ndio waliomtorosha hospitali lakini hafahamu ni akina nani kwa hiyo amenipa jukumu la kuwafahamu pia watu hao .Alienda mbali zaidi na kunitaka niwatafute na kuwapata watu wawili wa karibu na Marcelo ambao ni Danel Swai rafiki wa karibu wa Marcelo na Monica Benedict ambao anahisi wanafahamu mahala aliko Marcelo.Anataka nikiwapata niwatese na waeleze wanachofahamu kuhusu Marcelo na kisha niwaue.Huyu Monica ndiye ambaye rais anataka athibitishe kama ni mwanae kwa kutumia sampuli aliyonipa kazi ya kuitafuta.” “Oh my God !!! akasema Job “Nimewekwa kati kati na sasa ni jukumu langu kuamua niende upande upi.Nikichagua upande wa Boaz ina maana nitakuwa nimemsaliti rais na mapambano dhidi ya Alberto’s hayataweza kufanikiwa.Nikichagua upande wa rais nitaingia katika mgogoro na mtu aliyeyaokao maisha yangu na kunifikisha hapa nilipoona endapo nitaingia katika mgogoro na Boaz moja kwa moja nitakuwa nimeingia katika mgogoro na Maria ambaye ni mwanamke ninayempenda kuliko wote.Hata hivyo nimechagua kusimama upande wa rais.Niko tayari kumkosa mpenzi wangu Maria kwa manufaa ya nchi.Haya ni maamuzi magumu sana nimeyafanya kwani mimi na yeye tutapita lakini Tanzania itabaki daima kwa hiyo nitapigana kwa ajili ya Tanzania.Kwa hiyo Job tuna kazi kubwa ya kufanya kumlinda Monica kwani endapo nitashindwa kutekeleza matakwa ya Boaz lazima atatafuta watu wengine wa kuifanya kazi yake .Sababu nyingine ya kumlinda Monica ni kwamba Alberto’s wanaweza wakafahamu kuwa Monica ni mtoto wa Ernest kwa hiyo wanaweza wakamtumia kama silaha katika kumlazimisha Ernest afanye yale wanayoyataka.” Austin akanyamaza kidogo kisha akaendelea. “Jambo la pili nikwamba baada ya kulivunja baraza la mawaziri,rais anahitaji kuunda upya baraza lingine.Kabla ya kuunda baraza jipya anahitaji kwanza kumpata waziri mkuu.Rais amekuwa na wakati mgumu wa kumpata mtu wa kumpa nafasi ya waziri mkuu ambaye atakuwa ni mzalendo na ambaye si mfuasi wa Alberto’s.Jana alikuja kwangu na kunipa taarifa kuwa tayari amefanya maamuzi nani awe waziri mkuu mpya wa jamhuri ya muungano wa Tanzania na mtu anayefikiria kumpa nafasi hiyo ni Wilson Mukasha” Job akapatwa na mstuko mkubwa akainuka na kumsogelea Austin “No ! That can’t happen!! Akasema kwa sauti ya juu “Hivyo ndivyo ilivyo Job.Mukasha ndiye ambaye rais amemuona anafaa kwa ajili ya kuwa waziri mkuu mpya wa Tanzania ndiyo maana uliponitajia jina hilo kuwa ni mmoja wa watu wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya nilistuka sana.” Akasema Austin “Austin rais atafanya kosa kubwa sana endapo atamteua Mukasha kuwa waziri mkuu.Hamfahamu vizuri Mukasha ni mtu wa aina gani.Austin you have to stop that.Do whatever you can to stop that from happening” akasema Job na kuinamisha kichwa “Nini kinatokea kwa hili taifa? Akasema kwa sauti ndogo halafu akamtazama Austin. “Austin we have to stop that.Tukiruhusu rais akafanya kitu kama hicho vita hii ambayo tumejitolea kuipigana itakuwa kazi bure.All our sacrifices will be for nothing !! “Nimekuelewa Job lakini kuna tatizo moja .Rais anamuamini mno Mukasha.Ni mmoja kati ya watu wachache ambao rais anawaamini mno.Ili tumzuie asifanye hicho alichokusudia kukifanya yaani kumteua Mukasha kuwa waziri mkuu yatupasa tuwe na ushahidi wa kutosha kumuhakikishia rais kuwa Mukasha hafai na anashiriki katika biashara ya madawa ya kulevya.Kumueleza kwa maneno matupu hataweza kutuelewa” akasema Austin “Austin una uhakika hata wewe ukimueleza hatakuelewa? Akauliza Job “Kwa muda mfupi niliomfahamu rais Ernest Mkasa nimeshuhudia namna anavyomuamini Mukasha.Hata akielezwa na nani itakuwa vigumu kumuamini bila kuwa na ushahidi wa kujitosheleza.Hivyo basi tunatakiwa kufanya juu chini kutafuta kila aina ya ushahidi utakaoweza kumfanya rais abadili maamuzi yake” “Hiyo nayo ni kazi nyingine akasema Job “Ni kazi mpya ambayo lazima tuifanye.Lazima tuzuie jambo hili lisifanikiwe.Tunapaswa kuanzia sasa kuanza kumchuguza Mukasha kwa siri.” Akasema Austin “Kwa nini tusiutumie ukaribu wako na rais kama sehemu ya kuanzia? Rais anakuamini kwa hiyo tafuta namna unavyoweza kuitumia nafasi hiyo kumchunguza Muk...” “Wait .! Austin akamkatisha Job “Kuna kitu nimekikumbuka .Wakati rais ananitambulisha kwa Mukasha alinieleza kwamba Yule ni rafiki yake ,msiri wake na ndiye aliyempa taarifa zangu.Hii ina maana kwamba Mukasha ananifahamu vizuri na anafahamu kuwa niko kwa Boaz na ndiye aliyewasiliana na Boaz.Nakumbuka suala la kunikomboa toka mikononi mwa Alshabaab lilikuwa la siri kubwa kwa hiyo endapo Mukasha anafahamu basi lazima atakuwa ameelezwa na Boaz.Lazima yeye na Boaz watakuwa na ukaribu.” Akasema Austin na kutabasamu “Boaz ni sehemu nzuri ya sisi kuanzia kumchunguza Mukasha.Hawa wawili kuna mambo wanashirikiana na endapo tutachimba kwa undani zaidi kuna mambo mengi tutayagundua” akasema Austin “Boaz is your father in law,right? Akauliza Job “ Yes he is” akajibu Austin “ Umekuwa naye karibu kwa kipindi kirefu,unaweza ukamuelezeaje? “Ninamfahamu Boaz ni mfanya biashara ambaye ni mbunifu na aliye tayari kufanya lolote linalowezekana ili mradi biashara zake zikue.Ni mtu mwenye ushawishi na malengo.Ni mtu mpambanaji.Toka nimefahamiana naye sijawahi kugundua jambo lolote baya na hata biashara zake nyingi ni halali,hana rekodi mbaya katika biashara zake ila ninafahamu kuna biashara chafu anazifanya ambazo hajawahi kuniweka wazi ila sikutaka kufuatilia kwa sababu sikutaka kuanzisha mgogoro na familia ile.kazi aliyoniomba nimfanyie leo imenipa mwanga kuwa Boaz ni mtu katili na hatari.Huu ni wakati muafaka wa kumfahamu ni nani hasa” akasema Austin Job akamtazama Austin kwa makini na kuuliza “Your girlfriend Maria,how much do you love her? “More that I can explain.Why do you ask? “Going after his father will complicate things between you two so I want you to be sure of what you want to do” Austin akainamisha kichwa akatafakari kidogo halafu akasema “Sijawahi kuzama mapenzini kama nilivyozama kwa Maria lakini kwa maslahi ya nchi ni tayari kwa lolote” “Good” akasema Job “Ninacho chumba cha mahojiano humu ndani ambacho tutakitumia kumuhoji Boaz.Kina zana maalum kwa ajili ya kumfanya mtu aseme kwa hiyo nakuhakikishia Boaz akiingizwa humo lazima atasema” “Nategemea muda wowote kuanzia kesho kuipata sampuli ninayoitaka toka kwa Monica ambayo itatuwezesha kufanya kipimo cha vinasaba na kuupata ukweli.Baada ya hapo tutaifungua rasmi operesheni fagio” “So tell me about this woman Monica Benedict.Is she pretty? “C’mon Job huu si muda wa kuwaza mambo kama hayo” akasema Austin “Its just a joke Austin” akasema Job huku akicheka “Job nadhani tumeongea mengi na ninahitaji kuondoka kwani natakiwa kumuhoji Dr Marcelo usiku huu.Kuna mambo ambayo nahitaji kuyafahamu toka kwake.Kabla sijaondoka kuna jambo nataka nikuombe” “ Jambo gani Austin? “ Kwa hali ya mambo inavyokwenda nahitaji kuhamisha makazi yangu na vile vile natakiwa kumlinda pia Marcelo na Monica.Pale mahala ninapoishi kwa sasa tayari pamekwisha julikana kwa kuwa katika nyumba hii hakuna mtu yeyote anayeishi unaonaje endapo nitaweka makazi ya muda humu mimi na Marcelo? Hii ni sehemu salama na inaweza kunifaa sana” “Hakuna tatizo lolote katika jambo hili Austin.Hata mimi nilikuwa nafikiria jambo kama hilo Karibu tuishi sote hapa.Ni nyumba kubwa ina vyumba vya kutosha na usalama ni mkubwa.Hata hivyo kuna jambo nataka ulifahamu” akanyamaza kidogo na kusema “ Sintarejea tena katika maisha yangu ya uwazimu.Nimechoka kuishi maisha yale.Nimeteseka sana Austin na ninashukuru kwa ujio wako ambao umenipa nguvu ya kuweza kuweka nukta katika maisha yale magumu.Sikuwahi kufikiri eti mtu kama mimi siku moja nitaweza kuokota chakula majalalani,laini imenilazimu kufikia hali hiyo ili kuwakimbia wanaonitafuta waniue.Mwanzoni hawakuamini na walikuwa nawaona wakinifuata na kunichunguza ili wapate uhakika kweli nimekuwa kichaa .Walinifuatilia kwa miaka miwili ndipo walipokata tamaa wakiamini kuwa kweli nimekuwa kichaa.Uchungu nilio nao siwezi kuuelezea Austin” Job akasema kwa hisia kali huku machozi yakimtoka “It’s ok brother,they‘ll all pay” akasema Austin “Sure they must pay.Kikubwa ninachokitaka kwa sana ni kufahamu aliko mwanangu kwani mateso yote haya ninayavumilia kwa ajili yake.” “Nakuhakikishia Job kati kati ya sinema hii utafahamu alipo mwanao” akasema Austin na wote wakacheka “By the way,umewezaje kujenga nyumba kubwa namna hii Job? Umepata wapi pesa? Akauliza Austin.Job akatabasamu na kusema “Niliwahi kushiriki katika operesheni moja huko Darfur kumtafuta mtu aliyeitwa Hussein Hafidh Abdullah.

 

ITAENDELEA


0 comments:

Post a Comment

Blog