Search This Blog

Monday 19 December 2022

QUEEN MONICA (3) - 5

  





Simulizi : Queen Monica (3)
Sehemu Ya Tano (5)

 

 

Huyu ni kiongozi wa ukoo mmoja na alikuwa anatafutwa kwa kuchochea watu wa ukoo wake kuvamia na kuwachinja kikatili watu wa ukoo mwingine.Hussen alikuwa ni mtu tajiri sana na ilituchukua muda kufahamu maficho yake.Tulivamia nyumba yake na yakatokea mapambano makali baina yetu na walinzi wake,kati kati ya mapambano hayo Hussein akafanikiwa kutoroka.Tulipoipekua nyumba yake tulikuta kuna chumba kimejazwa fedha .Hatukuacha hata senti moja.Tulikuwa watu kumi na tano,tukagawana fedha zote na ndizo ambazo nilizitumia kujenga jumba hili kwa siri bila ya mke wangu kujua.Amarachi ndiye aliyekuwa akisimamia ujenzi wa jumba hili wakati nikiwa Darful hadi lilipokamilika kwa hiyo hakuna mtu wangu yeyote wa karibu anayefahamu kuwa jumba hili ni langu zaidi ya Amarachi.Hii ni siri yako Austin hatakiwi mtu mwingine kufahamu kwani tulichokifanya haikuwa sahihi” akasema Job na wote wakacheka.Job akamtembeza Austin sehemu mbali mbali za jumba lile kisha wakaagana “Usiku wa leo nitakuwa na kazi moja tu ya kufanya usafi humu ndani na kuweka mazingira safi kabla hamjahamia humu” akasema Job ,Austin akaondoka alipotoka kuonana na Austin,Boaz alimrejesha Maria hotelini kisha akakodisha gari la hotelini hapo na kuondoka.Usiku huu alikuwa na miadi ya kuonana na aliyekuwa waziri mkuu. “Austin amepewa kazi gani na rais? Amekataa kabisa kuniweka wazi ni kazi ipi anaifanya .Ujio wa Austin Tanzania unaweza kuwa na uhusiano na hiki alichokifanya rais Ernest? Nimefikiria sana kuhusu jambo hili kwani baada tu ya Austin kuja Tanzania ndipo rais alipobadilika ghafla.Sina hakika sana kuhusu jambo hilo lakini linatakiwa lifanyiwe uchunguzi .Natakiwa kufahamu ni kazi gani ambayo Austin anaifanya hapa Tanzania.Kuna mtu mmoja tu ambaye ninaamini anaweza kunisaidia kupata jibu.Wilson Mukasha.Huyu ni mtu wa karibu mno na rais na nina uhakika lazima atakuwa anafahamu kazi ambayo Austin anaifanya hapa Tanzania.Nitaongea naye baada ya kuonana na waziri mkuu” akawaza Boaz akiwa njiani kuelekea katika makazi ya waziri mkuu aliyevuliwa madaraka “Bado suala la Marcelo linaniumiza kichwa changu mno.Amejificha wapi? Anashirikiana na akina nani? hii ni vita nyingine imeanzishwa ambayo lazima niipigane ili kukipata kitabu pamoja na Austin.Kitabu kile ni muhimu mno na endapo hatutakipata mimi na wenzangu tutakuwa katika hatari kubwa.Kwa vyovyote vile lazima kitabu kipatikane.Kwa nini lakini Dr Richard ametufanyia hivi? Kwa nini ametusaliti kiasi hiki? Nilimuamini mno na hakuna aliyetegemea kama siku moja angeweza kutuuza kiasi hiki.Kwa hiki alichokifanya ni fundisho kwangu kuwa sitakiwi kumuamini mtu yeyote tena.Unayemuamini leo huyo ndiye atakaye kuangamiza kesho.Tulifanya kosa kubwa kumuamini Dr Richard na kosa hilo linakwenda kutugharimu. Akaendelea kuwaza Boaz Aliwasili katika makazi ya aliyekuwa waziri mkuu na kupokewa kwa furaha na mwenyeji wake mheshimiwa Jeremiah “Karibu sana Boaz.Karibu tena nyumbani” akasema Jeremiah akimuongoza Boaz katika chumba cha maongezi “Ahsante sana Jeremiah” “Hebu nipe siri yako Boaz,miaka inazidi kusonga lakini huzeeki.Whats your secret? Akauliza Jeremiah na wote wakacheka “Nitakueleza siku nyingine Jeremiah mzizi ninaoutumia” akajibu Boaz “Pole sana Jeremiah kwa hiki kilichokutokea.Sote tumestuka sana kwa mambo yanayoendelea.Nini kimemfanya Ernest akabadilika ghafla namna hii? “Ahsante sana Boaz.Kilichotokea kimemstua kila mtu ni kitu ambacho hakuna aliyekuwa amekitegemea.Ni jambo lililotokea ghafla sana.Hatujui ni kitu gani kilichomfanya Ernest akabadilika namna hii.Hata hivyo tunaendelea kujipanga kukabiliana naye” akasema Jeremiah “Mpaka sasa kuna hatua zozote mlizochukua? Makao makuu ya Alberto’s wanasemaje? “Hicho ndicho kilichonifanya nikuite hapa Boaz.Toka limetokea jambo hili hakuna chochote kilichofanyika zaidi ya kukaa kikao ambacho hakikuwa na suluhu yoyote ya maana ya kulikabili suala hili.Hatujui Ernest anashirikiana na akina nani ila tunachojua ni kwamba he’s not alone.Kikao kiliamua kulipa muda suala hili kwa ajili ya kufanya uchunguzi kufahamu ni akina nani anashirikiana nao.Kanuni za jumuiya zinaeleza wazi kwamba yeyoye anayekwenda kinyume au kukiuka masharti au kufanya usaliti adhabu yake ni kuuawa lakini cha kushangaza mwenyekiti wetu kwa makusudi amezuia hilo lisifanyike eti kwa lengo la kufanya uchunguzi kubaini watu ambao Ernest anashirikiana nao.Huu ni upuuzi mkubwa kwani hatuna uhakika uchunguzi huo utachukua muda gani na kipindi hicho uchunguzi unafanyika Ernest atazidi kujiimarisha na kuitokomeza kabisa Alberto’s hapa nchini.Mimi,makamu wa rais na mke wa rais tumekutana na kulijadili suala hilo kwa upana wake na tukafanya maamuzi kwamba ili tuweze kuiokoa jumuiya hapa Tanzania basi mwenyekiti Obi auawe haraka sana na kisha ifanyike kampeni na mimi nichaguliwe mwenyekiti wa muda na hapo nitaidhinisha rais auawe mara moja.Baada ya Ernest kuuawa makamu wa rais atakaimu nafasi ya rais kwa muda na katika kipindi hicho atakachokaimu atatengua maamuzi yote aliyoyafanya Ernest.Ataurudisha tena ule muswada ukajadiliwe bungeni pia atanirejeshea wadhifa wangu wa waziri mkuu na atamrejesha mkuu wa majeshi.Hilo likifanyika sote tutakuwa salama.Biashara zenu zote zitafanyika kwa uhuru na amani .Endapo hilo halitafanyika nakuhakikishia Boaz kuwa hatutabaki salama.We’ll all go down.Ernest amekwisha onyesha dhamira ya wazi ya kuifuta Alberto’s katika uso wa Tanzania.We have to act very fast.Nimekuita hapa kukupa taarifa hiyo na kukuomba msaada wako.Nafahamu wewe unafahamiana na watu wengi hivyo naomba unisaidie kumpata mtu atakayefanya kazi ya kumuua mwenyekiti Obi.I need someone very professional.Can you help me with that? Akauliza Jeremiah.Boaz aliyekuwa anasikiliza kwa makini akasema “Nimekuelewa Jeremiah na kwangu mimi hilo si tatizo.Ninafahamu watu wengi wenye ujuzi wa hali ya juu wa kuifanya kazi yako kwa ufanisi.Lakini nina swali moja nini kitatokea endapo Alberto mkuu akifahamu juu ya njama hizi? Ukumbuke pia kwamba Alberto mkuu ni mtu mwenye nguvu kubwa na uwezo wa kung’amua mambo nina wasi wasi hata mpango huu wa kumuua mwenyekiti wenu anaweza akalifahamu na sote tukaingia katika matatizo makubwa.Kwa upande Fulani nadhani mwenyekiti wenu anatumia busara kwani ni wazi Ernest kuna watu anashirikiana nao na hao ndio wanaompa ujasiri na nguvu ya kufanya hayo anayoyafanya.You have to be sure about what you want to do Jeremiah” akasema Boaz.Jeremiah hakuonyesha kufurahishwa na maneno yale ya Boaz akasema “Nielewe vizuri Boaz hali imechafuka .Kila kitu kimesimama na hatujui nini mipango ya kesho ya Ernest.Biashara yenu inafanyika na kufanikiwa kwa mwavuli wa Alberto’s na kama Alberto’s hawapo basi hata ninyi hamtaweza kufanya tena biashara zenu.You are nothing without us.Suala hili si langu peke yangu ni suala letu sote.Alberto mkuu yuko Italia na sisi tuko hapa Tanzania.Hii ni nchi yetu na endapo tutashindwa kufanya mabadiliko basi misaada itakatwa na tutawekewa vikwazo vya kiuchumi.Taifa hili litazidi kudidimia katika umasikini.We have to fight for our nation.Hata Alberto mwenyewe endapo atagundua na halafu akaona faida za tulichokifanya ninaamini atatupongeza kwani lengo lake kubwa ni kuibadili dunia na katika Afrika Tanzania ni nchi anayoipa umuhimu mkubwa mno.So are you going to find me what I asked or not? Akauliza Jeremiah.Boaz akamtazama kwa muda kisha akasema “I’ll find someone to do your job” “Thank you.Unadhani kufikia lini utakuwa umempata ? “Nipe siku mbili” “Good” akasema Jeremiah na ukimya mfupi ukapita.Boaz akasema “Jeremiah kuna jambo nimelifikiri kwa haraka haraka na sina uhakika kama linaweza kuwa na maana yoyote kwako” “Nieleze Boaz.Kwa hali ya sasa kila ushauri una maana kwangu”: “Baada ya kuyasikia maelezo yako nimegundua kuwa tatizo hapa ni rais Ernest Mkasa.Kama hivyo kwa nini basi isitafutwe namna ya kuweza kumuondoa Ernest na kumaliza matatizo yote bila ya kumgusa mwenyekiti Obi? Hii inaweza kuwa njia muafaka kabisa ya kuepusha mambo mengine yasitokee ndani ya jumuiya” Jeremiah akavua miwani akatoa kitambaa na kufuta macho kisha akasema “Boaz wazo lako ni zuri na la msingi ,lakini tatizo lililopo ni kwamba kwa mujibu wa taratibu zetu mwenyekiti wa jumuiya nchini ndiye mwenye uwezowa kutoa ruhusa ya kumuua mtu ambaye amekwenda kinyume na jumuiya na ndiyo maana nataka nishike nafasi ya uenyekiti ili kusitokee mkwamo wa aina yoyote .Kwa hiyo Boaz nitafutie huyo mtu wa kuifanya hiyo kazi yangu” akasema Jeremiah halafu wakaendelea na maongezi mengine na baadae Boaz akaondoka kwenda kupumzika “Mhh !! hili jambo linakoelekea limeanza kunitisha.Hii ni kama filamu ya usaliti.Dr Richard ametusaliti wenzake na kutuuza kwa mwanae Marcelo,Ernest Mkasa amewasaliti Alberto’s na sasa Jeremiah na wenzake wanataka kufanya usaliti mwingine kwa kwenda kinyume na makubaliano ya kikao chao cha pamoja.Sifahamu nini mwisho wa filamu hii lakini huko tunakoelekea si kuzuri hata kidogo.Watu wamechanganyikiwa hawafikiri sawasawa.Mimi nadhani suluhu pekee hapa ni kumuua rais ambaye ndiye anayeonekana kuwa kikwazo.Tukiendelea kumuacha hai hatujui nini malengo yake.I’m confused!! Akawaza Boaz.Kwa upande wangu nadhani nisijiingize sana katika mambo haya ya Alberto’s bali nijikite katika kujihakikishia usalama wetu mimi na wenzangu.Tuhakikishe kitabu kinapatikana na papo hapo tuanze kubuni mikakati ya kuifanya biashara yetu iendelee endapo mambo hayatakuwa mazuri.Tunatakiwa tujenge uwezo wa kuendesha mambo yetu bila ya kuwategemea sana Alberto’s.Hata hivyo nina uhakika mkubwa Alberto’s hawatakubali kushindwa na Ernest.Nina imani huko makao makuu yao hivi sasa watakuwa wanapanga mikakati mikubwa namna ya kufanya” akawaza Boaz na kukumbuka kuwa alihitaji kuongea na Wilson Mukasha.Akachukua simu na kuzitafuta namba za Mukasha akapiga “Boaz !! akasema Mukasha kwa mshangao “Hallo Wilson” “Hallo Boaz.Nimestuka kidogo ,sikutegemea kama ungenipigia mida hii” akasema Mukasha. “Usistuke Mukasha.Unafahamu mimi huja na kuondoka kama mvua.Samahani kwa kukupigia mida hii .Bado uko kazini? “Hapana nimefika nyumbani muda huu” “Poleni sana kwa mambo yaliyotokea na yanayoendelea kutokea” “Ahsante Boaz.Ni kweli kuna upepo mbaya unavuma sasa hivi na hali si nzuri sana” akasema Mukasha “Hicho ndicho hasa kilichonirudisha nyumbani haraka.Kwa namna mambo yanavyokwenda unadhani yanaweza yakatulia hivi karibuni? Akauliza Boaz “Hapana sina uhakika Boaz.Hii ni vita ngumu.Ernest amejipanga sana kwa mapambano.Ni wakati wa kuwa waangalifu mno” “Nalifahamu hilo Wilson na tayari tumekwisha anza kuchukua tahadhari.Wilson kilichonifanya nikupigie usiku huu ni kutaka kufahamu jambo moja” “ Jambo gani Boaz? Ni kuhusu Ernest na Austin.Unaweza kufahamu Ernest amempa Austin kazi gani? Boaz akauliza “Ernest ni mtu wangu wa karibu sana na siri zake nyingi amekuwa ananieleza ila kwa hili amekuwa mgumu kidogo kunieleza.Ni siri yake na Austin pekee kwani hata wanapozungumza hawataki mtu mwingine awe karibu na asikie wanachokiongea.Ninachoweza kuhisi lazima kuna jambo kubwa ambalo Austin analishugulikia kwani ilimlazimu Ernest kulipa ujira mkubwa ili Austin aweze kumfanyia kazi yake.Kwa hiyo naweza kusema kazi ambayo Austin anamfanyia Ernest ni kazi yenye umuhimu mkubwa sana kwa Ernest” akasema Mukasha “Umesema kuna ujira Ernest ametoa? Ni kiasi gani amemlipa Austin? “Ndiyo kuna ujira ametoa lakini si pesa ila kuna kitu kikubwa amemfanyia Austin na ndicho kilichomfanya Austin akubali kuifanya kazi hiyo ya Ernest” “Alimfanyia jambo gani? akauliza Boaz.Mukasha akavuta pumzi ndefu na kusema “ Alimtoa Linda mdogo wake Austin gerezani nchini China.” Boaz akahisi kama vile amemwagiwa maji ya barafu ghafla gari likayumba kidogo kwa mstuko alioupata ikamlazimu kuegesha pembeni. “Boaz are you there? Akauliza Mukasha “ Wilson I’m....I’m just shocked.Hii ni taarifa ambayo imenistua sana.Amewezaje kumtoa Linda? “He’s a president kwa hiyo ametumia madaraka yake kufanya hilo liwezekane.Amebadilishana wafungwa na seriali ya China.Kwa hiyo hivi sasa Linda yuko huru” akasema Mukasha.Boaz akavuta pumzi ndefu “Wilson nimestuka sana.Sikutegemea kabisa kama lingetokea jambo kama hili.Yule binti anafahamu mambo yangu mengi na anaweza akamueleza kaka yake kila kitu kuhusu mimi kuwa ndiye niliyemuingiza katika biashara hii ya dawa za kulevya .Kwa hivi sasa yuko wapi? “Kwa hivi sasa anaishi kwa balozi wa Tanzania nchini China” akasema Mukasha. “Wilson tafadhali naomba unishauri nifanye nini? Linda hapaswi kuwa huru.Ni hatari mno kwangu.Austin hapaswi kufahamu chochote kuhusu mimi na mambo yangu.Endapo atafahamu mambo yangu basi tutakuwa maadui wakubwa na kazi zangu nilizompa azifanye hazitafanyika.Hiki ni kipindi ambacho ninamuhitaji mno Austin.Kuna kazi nyingi ambazo nahitaji azifanye” akasema Boaz “Boaz kitu pekee ambacho unaweza kukifanya hapa ni kumuua Linda” “Wilson hilo si jambo rahisi hata kidogo kwani kuingia katika ubalozi wetu na kumuua Linda si jambo dogo.Hata hivyo niachie mimi nitajua nifanye nini.Ninahitaji kujua kitu kimoja ambacho kinaweza kunipa picha .Wewe ndiye uliyenitambulisha kwa rais.Mimi na yeye hatukuwa tukifahamiana.Ilikuaje hadi akafahamu kuwa mimi niko na Austin? “Boaz I don’t think that’s necessary.Kuna mambo mengi ambayo tunapaswa tuyajadili kwa sasa na si suala hilo” akasema Mukasha “Wilson jambo hili ni muhimu sana kwangu.I want to know the bottom of this.I want to know how it started? Wilson akavuta pumzi ndefu na kusema “ Ernest met with this woman...” “ What woman? Boaz akauliza “ Anaitwa Janet mwamsole.Huyu ni rafiki wa siku nyingi wa Ernest na huwa wanakutana mara kwa mara .Ni watu wanaofahamiana kwa miaka mingi toka wakiwa shuleni.Baada ya kutoka kuonana na na Janet ndipo alipotaka nimtafutie mtu mwenye sifa maalum amfanyie kazi yake na ndipo nilipomkumbuka Austin.” Akasema Mukasha “Unadhani huyo mwanamke alimueleza nini Ernest? Unahisi anaweza kuwa na mahusiano na hiki alichokifanya Ernest? Siwezi kuwa na uhakika sana wa hilo labda tufanye uchunguzi” akasema Mukasha “Hakuna haja.Tujikite katika masuala ya msingi.Kuna jambo nataka kukufahamisha.Unamkumbuka marehemu Dr Richard? “Ninamkumbuka uliwahi kunikutanisha naye ukatutambulisha lakini si kuwahi kuwa na ukaribu naye.” “Usingeweza kuwa na ukaribu naye kwa kuwa wewe si mwanachama wa Alberto’s.Dr Richard alikuwa anahusika na wafuasi wa Alberto’s pekee.Leo hii nimeipata barua ambayo kabla hajafa alimuandikia mwanae Marcelo.Katika barua hiyo alimueleza kila kitu kuhusu Alberto’s na sisi pia.Mwisho wa maelezo yake akamtaka ahakikishe anapambana kufa na kupona kuwafyeka Alberto’s na sisi pia tunaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya.Alimuachia kitabu Fulani ambacho kina orodha ya wafanya biashara wote wa dawa za kulevya hapa nchini ,mahala walipo ,mali zao na hadi mtiririko wao mzima wa fedha.Dr Marcelo ametoroshwa na watu wasiojulikana na mpaka sasa hatujui yuko wapi.Tunachofahamu ni kuwa hayuko peke yake kuna watu anaoshirikiana nao.Kwa hiyo hivi sasa ninajiandaa kwa operesheni nzito kuhakikisha ninampata Austin na hicho kitabu .Bila kumpata Austin au hicho kitabu basi hatutakuwa salama.Kuna watu ambao wanajipanga kutuzimisha kabisa” akasema Boaz “ Hizo ni taarifa za kustusha sana.Una sehemu yoyote ya kuanzia kufanya uchunguzi huo? Akauliz Mukasha “Ninazo tetesi Fulani ambazo ninazifanyia kazi .Nina imani ndani ya siku mbili nitakuwa na jibu la uhakika .Ninachokuomba Mukasha endelea kufanya uchunguzi ufahamu ni kazi gani ambayo rais amempa Austin.Ni muhimu sana kwangu” “Sawa Boaz mimi nitajaribu kufanya uchunguzi wangu na chochote nitakachokipata nitakutaarifu” “Ahsante Mukasha.Kuwa makini sana hasa katika nyakati hizi.Jitahidi kadiri uwezavyo kuendelea kuwa karibu na rais ili asigundue upande wako wa pili” “Ahsante Boaz nitajitahdi” akasema Wilson Mukasha na kukata simu.Boaz aliyekuwa ameegesha gari pembeni ya barabara akawasha gari akaendelea na safari ya kurejea hotelini “Habari ya Linda kutolewa gerezani ni habari ambayo naweza kusema ni mbaya zaidi.Yule binti anafahamu mambo yangu mengi kwani nilikuwa namtumia kimapenzi na kumuingiza katika biashara ya dawa za kulevya.Endapo akipata nafasi ya kumueleza Austin mambo anayoyajua kuhusu mimi sijui nini kitatokea.Ninachotakiwa kufanya kwa sasa ni kumuhimiza Austin anifanyie kazi zangu haraka haraka na baada ya kumaliza I’ll have to kill him.Sitaki apate nafasi ya kuonana na Linda.Nikiruhusu hilo litokee basi nimekwisha na Austin ataniua kwani nmaamini lazima Linda amueleze kila kitu wakionana .Austin must die” akawaza Boaz ustin alirejea katika makazi yake tayari ilikwisha timu saa saba za usiku.Mara tu alipoingia ndani akaenda moja kwa moja kubisha hodi katika chumba cha Marcelo.Mlango haukufunguliwa akaingiwa na wasi wasi akaitoa bastora yake na kukinyonga kitasa mlango ukafunguka akaingia ndani.Marcelo alikuwa amelala usingizi mzito sana.Austin akashusha pumzi,akamfuata Marcelo na kumuamsha. “Austin you are back” akasema Marcelo kwa uchovu huku akipiga mwayo.Austin akamtazama kwa makini na kusema “Marcelo huu si muda wa kulala namna hiyo.Huu ni muda wa mapambano ni muda wa kukesha macho .Ni muda wa kujilinda .Si muda wote utakuwa na mimi kwa hiyo unapokuwa peke yako unapaswa kujilinda .Ni vipi endapo ni adui ndiye aliyegonga mlango na akaufungua bila hata ya kustuka? Don’t do that next time” akasema Austin “Nimekuelewa Austin.Hii imetokana na hizi dawa ninazotumia zina nguvu sana.I’m sorry it wont happen again” akasema Marcelo “Good!!! Akasema Austin na kwenda kuketi katika kochi dogo lililokuwamo mle chumbani “Nilikuahidi kwamba tutaongea nitakaporejea kwa hiyo naomba unisikilize kwa makini sana.” Akasema Austin na kumtazama Marcelo kwa makini sana akasema “Naitwa Austin January.Ni mtanzania mwenye uraia wa Afrika kusini.Nimerudi Tanzania kwa ajili ya kazi maalum” akatulia kidogo halafu akaendelea “Miaka kadhaa iliyopita nilikuwa nafanya kazi katika idara ya usalama wa taifa kitengo cha ujasusi wa kimataifa .Nimefanya kazi nyingi na za hatari nilizotumwa na nchi yangu.Kazi ya mwisho niliyoifanya ilikuwa kuongoza kikosi maalum kilichokwenda kuwakomboa watanzania waliotekwa na wanamgambo wa Alshabaab nchini Somalia.Katika operesheni hiyo nilipigwa risasi na mmoja wa wenzangu nilioongozana nao nikatelekezwa hapo na kuchukuliwa na Alshabaab.Kilichosababisha nitake kuuawa ni baada ya kugundua mpango wa kumuua rais Ferdinand uliosukwa na watu ndani ya serikali” akatulia na kumeza mate akaendelea “ Nilikombolewa toka kwa Alshabaab na mtu mmoja anaitwa Boaz ambaye ni baba wa mpenzi wangu Maria.Kwa msaada wake nimefanikiwa kuanza maisha mapya na yeye ndiye sababu mimi kuwa hapa nilipo leo.Sikuwahi kurejea tena Tanzania hadi hivi sasa nilipoitwa na rais kwa kazi maalum.Jioni ya leo kama utakumbuka nilikuomba uende chmbani kwako kwa kujua kuwa rais amekuja.Hakuwa rais kama nilivyotegemea bali alikuwa mlinzi wake aliyekuwa ametumwa kuwaleta wageni ambao ni Boaz na mpenzi wangu Maria.Nilistuka sana kwani sikuwa nimewatarajia kabisa.Boaz aliniomba tuongee pembeni na akanieleza kilichomleta.Amekuja kuniomba nimfanyie kazi yake moja.Alinieleza kwamba aliwahi kuwa na rafiki yake anaitwa Dr Richard ambaye kwa sasa ni marehemu” “Dr Richard ?!! ..Dr Marcelo akastuka sana “Ndiyo Dr Richard .Alisema kwamba walikuwa na mahusiano ya kibiashara .Walikuwa na miradi ambaye Dr Richard walikuwa na miradi kadhaa ya pamoja ambayo Dr Richard ndiye aliyekuwa msimamizi mkuu.Alipofariki Dr Richard alimuachia majukumu yote mwanae anaitwa Dr Marcelo .” “What??!! Dr Marcelo akazidi kushangaa “Subiri nimalize Marcelo” akasema Austin “Dr Macelo ndiye aliyekuwa msimamizi mkuu wa miradi yote baada ya baba yake kufariki.Kwa mujibu wa maelezo ya Boaz ni kwamba Marcelo alibadilika na kutaka kujimilikisha miradi ile ya ubia jambo ambalo halikumfurahisha.Anadai kwamba Aliwatuma vijana wake wakamuhoji lakini akawafyatulia risasi na wao ikawalazimu wajibu na kumjeruhi kwa risasi akaenda kulazwa hospitali lakini ghafla akatoweka hapo hospitali alikokuwa amelazwa na hajulikani yuko wapi .Boaz anadai kwamba kuna kitabu ambacho Dr Richard alimkabidhi Marcelo ambacho ndicho kina maelekezo yote kuhusiana na miradi hiyo ya ubia baina yao.Marcelo ametoweka na kitabu hicho.Kazi aliyonipa Boaz ni kumsaka Marcelo na kuhakikisha ninampata yeye na hicho kitabu.Kunirahisishia kazi zaidi amenipa majina ya watu wawili ambao ana uhakika mkubwa kuwa wanafahamu mahala ulipo.Ametaka niwateke ,niwatese waonyeshe mahali alipo kisha niwaue.Watu hao ni Daniel Swai na mwingine anaitwa Monica Benedict” “No!!...No!!...noo !! akasema Marcelo. “Let me finish Marcelo” akasema Austin.Uso wa Marcelo ulikuwa umeloa jasho “Nilimkubalia kufanya kazi yake kwa hiyo hivi sasa niko katika zoezi la kumsaka Marcelo.Natumai Marcelo ambaye Boaz anamtafuta si wewe...” “Austin please dont do it! Mimi ndiye Marcelo ambaye huyo Boaz anamtafuta.Dr Richard ni baba yangu na kweli amekwisha fariki” akasema Dr Marcelo .Kwa dakika mbili Austin na Marcelo wakabaki wanatazamana “Please don’t do it” akasema Marcelo huku macho yake yakichuruzika machozi “Boaz alipomtaja Dr Marcelo nilistuka sana na nilifahamu moja kwa moja kuwa ni wewe ila sikumueleza chochote kama ninakufahamu.Ninachotaka unieleze kwa ufasaha kabisa historia yako na mahusiano yako na Boaz na kama alichokizungumza Boaz ni kitu cha kweli .I need to hear the truth..” Dr Marcelo akafuta machozi na kusema “ Baba yangu marehemu Dr Richard alikuwa ni daktari bingwa wa saratani na vile vile alikuwa na uwezo mkubwa katika mambo ya upasuaji.Ni daktari aliyejizolea sifa kubwa kutokana na umahiri katika kazi yake.Alinivutia sana kwa kazi zake na mimi nikajikuta nikivutiwa kuwa daktari .Naweza kusema kwamba sikutumia muda mwingi kuwa na baba kwani mara nyingi alikuwa ni mtu wa kusafiri katika nchi mbali mbali mimi muda mwingi nilikuwa masomoni.Nikiwa masomoni China nilipigiwa simu kuwa baba ni mgonjwa sana na anahitaji kuniona.Nilirudi haraka sana kuonana naye.Hakuwa na matumaini ya kupona hivyo akanieleza mambo kadhaa ya muhimu ambayo alitaka niyatekeleze baada ya yeye kufariki.Alinipa vile vile kitabu alichokisema ni mwongozo katika kazi zangu za kitabibu.Alisema kwamba kila nitakapokuwa na tatizo lolote katika kazi yangu basi nitampata ufumbuzi wake katika kitabu hicho.Alinipa vile vile namba za simu akasema kwamba nizipige kabla sijaanza kukitumia kitabu hicho ili niweze kupewa maelekezo na huyo mtu aliyenipa namba zake.Alinitaka nisikifungue kitabu kile hadi atakapokuwa amefariki.Hata baada ya baba kufariki sikuwahi kukifungua kitabu kile wala kumpigia simu huyo mtu aliyenielekeza nimpigie.Nilikihifadhi kitabu kile katika kasiki na sikuwahi kukigusa hadi hivi majuzi nilipokuta kasiki langu limefunguliwa na baadhi ya nyaraka zangu zikachukuliwa likiwemo faili langu la matibabu.Nilipochunguza vizuri nikagundua kwamba hata kitabu hicho alichonipa baba nacho kilikuwa kimechukuliwa.Jioni ya siku hiyo nikapigwa risasi na watu nisiowafahamu nashukuru madaktari walifanikiwa kuokoa maisha yangu.Nikiwa hospitali nilimuona mtu mmoja aliyewahi kuwa na urafiki na baba na ambaye aliwahi kunionya kwamba nisiwe na mazoea naye kabisa .Niliogopa sana nikajua tayari maisha yangu yako hatarini ikanilazimu kuomba msaada kwa mtu ambaye ninamuamini naye ni Monica Benedict ambaye Boaz anataka umtafute umpate.” “Monica Benedict ? akauliza Austin “Ndiyo” akajibu Marcelo “Ok endelea” akasema Austin “Nilimuomba Monica anisaidie niweze kutoka pale hospitali bila mtu mwingine yeyote kueleza sikutaka hata ndugu zangu wafahamu.Monica aliahidi kunisaidia lakini ghafla akapotea na sikuonana naye tena hadi leo hii.Sielewi nini kilitokea hadi David Zumo akapata taarifa zangu akamuomba rais wa Tanzania ambaye alikutuma wewe ukaja kunitoa pale hospitali.Kwa hiyo Austin simfahamu Boaz ,sijawahi kumuona na wala baba hakuwahi kunieleza au kunitajia jina kama hilo.Mambo yote aliyokueleza siyafahamu na ninaweza kusema kwamba si ya kweli.Nakuomba tafadhali usifanye alichokuomba ufanye.Usiwafanye chochote Daniel na Monica,hawafahamu chochote kuhusu mahali nilipo na zaidi ya yote ni watu wangu wa karibu mno.Naomba uniamini Austin” akasema Dr Marcelo.Austin akamkazia macho Marcelo kwa muda kidogo na kusema “Ofcourse I believe you” “Ahsante sana Austin kwa kuniamini” akasema Marcelo “Nilifahamu toka awali Boaz alikuwa ananidanganya.Hapa lazima kuna jambo linaendelea ambalo Marcelo halifahamu.Kuna jambo limefichwa katika hicho kitabu ambacho Boaz anaonekana kukihitaji kwa gharama zozote.Boaz asingeweza kufunga safari kuja kuniomba nimfanyie kazi yake hii kama haina umuhimu mkubwa kwake” akawaza Austin akiendelea kumtazama Dr Marcelo “Marcelo unadhani ni nani aliingia chumbani kwako akafungua kasiki na kuchukua kitabu na nyaraka zako nyingine? Unaweza kumuhisi mtu yeyote? Akauliza Austin “Toka lilipotokea tukio lile nimekuwa najiulza sana nani anaweza akafanya kitendo kile? Nimetafakari mno lakini mpaka sasa sina yeyote niyaweza kumuhisi. “Unahisi na nani nyumbani kwako? “Ninahisi peke yangu ila ninaye mfanyakazi wa ndani ambaye ni mtu mzima anayejiheshimu na hawezi kufanya kitu kama hicho.Huja asubuhi na kuondoka saa kumi jioni.Hajawahi kuingia chumbani kwangu hata mara moja.” “Huna mke? “Hapana sina” “Je mpenzi ambaye huja na kuondoka mara kwa mara? “Hata mpenzi sina” Austin akaonekana kushangaa “ Marcelo nitafurahi endapo utakuwa mkweli kwangu ili nitafute namna ya kukusaidia.Right now I’m your only help. So tell me the truth” akasema Austin “Nimekueleza ukweli Austin,sina mke wala mpenzi.Mbona unaonekana kushangaa? “Inashangaza kidogo kwa mtu kama wewe kukosa mke au hata mpenzi. “Sikiliza Austin ,sababu ya mimi kukosa mke au mpenzi ni kwa kwamba mimi ni mgonjwa.Ninasumbuliwa na kansa ya damu kwa hiyo sitaki kujiingiza katika mahusiano yoyote.Ila niliwahi kuwa katika mahusiano na msichana mmoja anaitwa Lily wakati fulani” akasema Marcelo “Nini kilitokea? “It didn’t work” “Where is she now? Akauliza Austin “I don’t know.Tulipoachana hatukuwahi tena kuwasiliana “ Aliwahi kuingia chumbani kwako?Anazifahamu namba za siri za kufungulia kasiki? “Tulikuwa wapenzi kwa hiyo chumbani kwangu kulikuwa ni kama chumbani kwake.Alikuwa akija mara kwa mara.Kuhusu namba za kufungulia kasiki hazifahamu” Austin akafikiri kidogo na kusema “Tell me about Monica Benedict.Una mahusiano gani naye? Are you two dating? “Mimi na Monica ni marafki wa kawaida na hatuna mahusiano ya kimapenzi.Nimefahamiana na Monica siku si nyingi .Daniel ndiye aliyenitambulisha kwake na toka tulipoonana tumekuwa watu wa karibu sana.” Akajibu Marcelo “Inavyoonyesha Boaz anazo taarifa zako zote.Kila unachokifanya anakifahamu na ana uhakika mkubwa kwamba mmoja kati ya hawa watu wawili Daniel na Monica anafahamu mahala ulipo.Inaonekana amekuwa anakufuatilia au ameweka watu wa kukufuatilia kila ukifanyacho bila wewe kufahamu. Inaonekana anachokitafuta toka kwako ni kitu kikubwa na ninahisi miongoni mwa watu wako wa karibu kuna mtu kapandikizwa ili kukuchunguza.Unapaswa uchekeche akili na ujue ni nani ambaye unahisi anaweza akawa ni pandikizi la Boaz? “Austin nakubaliana nawe kwamba inawezekana katika watu wangu wa karibu kuna mtu anayenichunguza lakini nakuomba ufanye kila uwezalo kuwalinda Daniel na Monica.Dont let anybody hurt them especially Monica” akasema Marcelo kwa msisitizo “Nitajitahdi kadiri niwezavyo kuwalinda hao rafiki zako lakini kuna mambo mawili ninajiuliza .Kwanza kitabu ulichopewa na baba yako ambacho Boaz anakitafuta ambacho kimeibwa kwako lakini Boaz hajakipata nani anacho? Ninahisi aliyekichukua kitabu hicho hana mahusiano na Boaz na ndiyo maana Boaz hafahamu kama kitabu hicho kimeibwa.Nini kilichomo ndani ya hicho kitabu na kukifanya kiwe na thamani kubwa namna hii? Jambo la pili najiuliza rais wa Cngo David Zumo ameingiaje katika suala hili? Marc......” Austin akakatishwa na mlio uliotoka katika saa yake ya mkononi “Somebody is at the door” akasema na wote wakashangaa “ Una miadi ya kuonana na mtu usiku huu ? akauliza Marcelo “Hapana ni usiku mwingi tayari na sitegemei mgeni yeyote.” Akasema Austin na kuchukua kile kifaa kidogo mithili ya simu ya mkononi alichokuwa amemuachia Marcelo akakibonyeza na picha kutoka katika kamera zikaanza kuonekana.Kamera ya getini ilionyesha kulikuwa na mtu amesimama,alikuwa ni mwanamke.Austin akastuka na kuongea kwa sauti ya mshangao “ Maria?!! “ You know her? Akauliza Marcelo “ Amekuja kutafuta nini usiku huu? Akajiuliza Austin halafu akamgeukia Marcelo “ Marcelo ujio wa Maria usiku huu unanipa mashaka sana.Chukua bastora ile niliyokupa na utajificha katika maua karibu na mlango mkubwa wa kuingila sebuleni.You are going to cover me.” Akasema Austin wakatoka mle ndani na kuelekea nje.Marcelo akajificha katika maua kama alivyoelekezwa na Austin na kwa tahadhari Austin akaelekea getini.Akachungulia katika kijitundu kidogo akamuona Maria akiwa amesimama akisubiri kufunguliwa geti.Hakukuwa na mtu mwingine hapo karibu.Taratibu na kwa tahadhari kubwa Austin akaufungua mlango mdogo wa geti na kutoka bastora ikiwa mkononi “Austin don’t shoot!! its me Maria !! akawahi kujitambulisha Maria baada ya kuona namna Austin alivyotoka pale getini. “Are you lone? “Yes I’m alone.Nililetwa na gari ya hotelini lakini tayari imeshaondoka” akasema Maria .Austin akamtaka aingie ndani haraka na kufunga geti “I’m sorry Austin” akasema Maria kwa sauti ya woga “Twende ndani” akaamuru Austin na Maria akamfuata .Dr Marcelo aliyekuwa amejibanza katika maua kama alivyokuwa ameelekezwa na Austin alihisi mwili kuingiwa baridi baada ya kumtazama mwanamke Yule aliyekuwa ameongozana na Austin “Lilian??!! Akajiuliza “Sidani kama ninaota.Japokuwa ni muda mrefu hatujaonana lakini macho yangu hayanidanganyi that’s Lily.What is she doing here? Amefahamianaje na Austin? Ama kweli milima haikutani binadamu hukutana.Baada ya miaka hii yote kupita hatimaye leo ninakutana tena na Lily! Akawaza Marcelo .Austin na Maria walipoingia sebuleni,Marcelo akatoka katika maua na kusogea mlangoni akajibanza kusikia walichokuwa wanakizungumza Austin na Maria “Maria why are you here? Why are you back? akauliza Austin mara tu walipoingia sebuleni. “Maria !!!...Her name is Maria? Mbona mimi namfahamu kwa jina la Lilian? Halafu ana jina lingine anaitwa Shamim” Dr Marcelo akazidi kushangaa. “Nisamehe Austin lakini imenilazimu kurudi tena.I need answers.What are you doing here and why you don’t want me to be here with you? What are you hiding? akauliza Maria huku macho yake yakiingiwa machozi.Kabla Austin hajajibu kitu Marcelo akaingia pale sebuleni.Austin na Maria wakastuka wote wakageuka na kumtazama. “Lilian !! akasema Marcelo “Marcelo !! akasema Maria kwa sauti yenye kitetemeshi.Alionekana kustuka na kuogopa sana. “Do you know him? Austin akauliza kwa mshangao.Maria akaitika kwa kutikisa kichwa.Wote watatu wakabaki wanatazama “Habari yako Lily.Habari za miaka mingi?Akasema Dr.Marcelo huku akitabasamu kwa mbali.Kabla Maria hajafumbua mdomo wake kujibu chochote Austin akauliza kwa mshangao “ Lilian ? Austin na Marcelo wakatazamana kisha Marcelo akasema “Austin tunaweza kuzungumza pembeni tafadhali? “Sure” akajibu Austin kisha wakaingia katika chumba cha pembeni chenye mlango wa kioo “Marcelo umefahamiana wapi na Maria? Akauliza Austin “Ni hadithi ndefu kidogo lakini mimi na Maria tuliwahi kuwa na mahusiano ya kimapenzi.Huyu ndiye mwanamke ambaye nilikueleza kuwa niliwahi kuwa naye katika mahusiano lakini tukaachana.Ninamfahamu kwa jina la Lily.Ni muda mrefu hatujaonana hadi nilipomtia machoni usiku huu.Anafanya nini hapa? Akasema Marcelo.Austin alionekaa kushanagzwa na habari ile ya Marcelo. “Huyu haitwi Lilian anaitwa Maria.Huyu ni mtoto wa Boaz mtu anayekutafuta kwa udi na uvumba na ndiye mpenzi wangu kwa sasa.Huyu ndiye aliyemshawishi baba yake anikomboe toka Alshabaab kwa kiasi kikubwa cha fedha” akasema Austin na wote wakaendelea kutazamana.Marcelo akasema “Umesema anaitwa Maria” “Ndiyo anatwa Maria” “Hii imenishangaza kidogo kwani mimi ninamfahamu kwa jina la Lilian.Ninazihamu nyaraka zake zote zina jina la Lilian Bakile.Pasi zake za kusafiria ,kadi zake za benki,na vyeti vyake mbalimbali vyote vinaonyesha kwamba jina lake ni hilo.Kitu ambacho kilisababisha mimi na Lily kushindwa kuelewana na hatimaye kutengana ni pale nilipogundua kuwa ana pasi nyingine ya kusafira yenye jina la Shamim.Nilipohoji kuhusu hilo ukaibuka mkwaruzano na tukatengana.Nimestuka kidogo kusikia anaitwa Maria. ” Akasema Marcelo Austin akainama akafikiri kidogo na kusema “Nimeshangaa sana kwanza sikufahamu kama wewe na Maria mnafahamiana na kwamba mpenzi wangu aliwahi pia kuwa mpenzi wako.Mimi ninamfahamu kwa jina la Maria .Nyaraka zake zote zinaonyesha anaitwa Maria Boaz Abrahams. Kwa hili uliloniambia kuna taa nyekundu imewaka kichwani kwangu.Kuna kitu Maria anakificha.Kwa nini awe na majina zaidi ya moja? Nadhani kuna ulazima wa kumfahamu vizuri.Nadhani bado sijamjua vizuri mtu ninayedhani ni mpenzi wangu.Ahsante Marcelo kwa kunifumbua macho” akasema Austin “Tutafanya nini Austin? Huyu ni mtoto wa Boaz na tayari amekwisha niona na akitoka hapa lazima ataenda kumueleza baba yake kuwa niko hapa.Naomba unisaidie Austin” “Usijali Marcelo.She wont get out of here” Austin akafungua mlango na kutoka akamuendea Maria na bila kupoteza hata sekunde akatoa bastora na kumuelekezea Maria “Nataka unieleze what’s your real name? Are you Maria,Lilian or Shamim? Akauliza Austin kwa ukali.Maria hakujibu kitu akabaki anamtazama Austin kwa woga. “Answer me !! what’s your real name? akauliza tena Austin kwa ukali lakini Maria hakujibu kitu akabaki anatetemeka .Austin aliyekuwa amefura kwa hasira akamnasa kibao kikali Maria “Answer me !! akasema Austin.Maria hakujibu kitu akaendelea kulia.Austin akamuinamia pale sofani “Nafahamu unanidanganya kuhusu mambo yako mengi lakini leo ni siku yako ya kunieleza ukweli, wewe ni nani? I don’t care how much you love me but I want to hear the truth.Kwa nini uwe na jina zaidi ya moja? Kwa nini una pasi zaidi ay moja za kusafiria? Jina lako halisi ni lipi?Usiponieleza ukweli nakuhakikishia nitakufanyia kitu kibaya sana.Look at me !! Look at me ! akasema Austin kwa ukali na kumlazimisha Maria amtazame usoni “Right now,I’m not Austin you know.I’m at work and when I’m doing my job I become a monster so if you don’t tell me the truth I’ll do smething very painfull to you.Usinilazimishe nikufanyie hivyo Maria tell me who are you ?Kwa nini ubadilishe majina ? akauliza Austin lakini Maria hakujibu kitu akaendelea kulia “Maria tafadhali usinilazimishe nikufanyie jambo ambao sikuwa nimekusudia kulifanya.Niambie ukweli kuhusu wewe.” “Austin give her a chance to expl....” Marcelo akataka kusema kitu lakini Austn akamzuia “Marcelo nenda chumbani kwako kajiandae.We’re leaving this place” akasema Austin halafu akachukua waya akamfunga Maria mikono na miguu na kumfunga kitambaa usoni. “Austin why are you doing this to me? Akauliza Maria huku akilia “I warned you don’t come to Dar es salaam because I didn’t want this to happen to you.Now I don’t have a choice I have to do this.Wewe utakuwa chanzo cha kupata kile ninachokihitaji” “Nani kakubadilisha namna hii Austin hadi ukanifanyia haya? Nini unakitafuta toka kwangu? “The ruth !! akasema Austin kwa ukali “I want to know who you real are? Kwa kuwa umekuwa mgumu wa kunieleza ukweli unanifanya niamini kwamba kuna mambo mengi ambayo bado umenificha kuhusu wewe .Inaniuma kukufanyia hivi lakini hata kama angekuwa ni mama yangu mzazi lazima ningemfanyia hivi.I don’t have a soul whem I’m doing my job” akasema Austin na kupanda kwa hasira ghorofani akakusanya vitu vake vyote vya muhimu akavipakia katika gari halafu akambeba Maria na kumpakia katika gari. Akamuamuru Dr Marcelo aingie garini wakaondoka Austin akaongeza sauti ya muziki hakutaka kusikia Maria alivyokuwa akilia. “ I hate this job.Sikufikiria kama siku moja nitamfanyia hivi mwanamke ninayempenda .Maria ni sababu ya mimi kuwa hapa nilipo leo lakini hayo yote lazima niyaweke pembeni kwanza kuna vitu ambavyo natakiwa kuvifahamu toka kwake.Kwa nini awe na majina matatu?Kwa nini hajawahi kunieleza kuhusu majina yake mengine? Kuna kitu gani anakificha na ambacho hataki kukiweka wazi? Ninahisi kuna jambo haliko sawa hapa.Ngoja nitaufahamu ukweli kabla hakujapambazuka” akawaza Austin Wilson Mukasha alishindwa kupata usingizi akainuka na kwenda kusimama kibarazani.Alionekana kujawa na mawazo “Rais amempa kazi gani Austin? Si kawaida yake kunificha jambo lolote lakini katika hili ameniweka pembeni.Kwa nini hataki nifahamu kazi aliyompa Austin? Amehisi nini hadi asinishirikishe katika jambo hilo wakati mimi ndiye niliyemsaidia akampata Austin? Sina hakika kama atakuwa amehisi kitu juu yangu kwani endapo angekuwa amehisi au kusikia kitu chochote basi asingefikiria kunichagua kuwa waziri mkuu wa Tanzania.” Akawaza Mukasha “ Ujio wa Austin umekuwa kama na mkosi kwani ni baada ya yeye kuja ndipo rais alipobadilika ghafla.Sifahamu nini kinaendelea kati yao lakini nahisi lazima Austin atakuwa anahusika katika mabadiliko haya ya ghafla ya rais.Jambo hili si la kupuuzia kwani bila kuchukua tahadhari mambo mengi yanaweza yakafichuka hapa.Nimeanza kuwa na wasi wasi sana na Austin.Nitachunguza nijue kazi anayoifanya hapa Tanzania na nikitaka kujuia ni kazi gani natakiwa kumuhoji Janet kwani baada tu ya rais kutoka kuongea naye ndipo alipoanza kumtafuta mtu mwenye sifa kama za Austin.Nina hakika Janet kuna kitu atakuwa anakifahamu” akawaza Mukasha ********************* Austin aliwasili katika makazi ya Job. “Job imenilazimu kuja mapema zaidi ya nilivyotegemea” akasema Austin baada ya kushuka garini “Hakuna tatizo Austin.Hapa unakaribishwa muda wowote.Nini hasa kimetokea? “Something happened Job.Tutaongea baadae lakini ndani ya gari kuna watu wawili ambao nitakuwa nao hapa” akasema Austin na kuufungua mlango wa gari na kumtaka Marcelo ashuke “Huyu anaitwa Dr Marcelo” Austin akamtambulisha Marcelo kwa Job halafu akamfungua Maria kitambaa usoni na waya aliomfunga miguuni akamuamuru ashuke “Huyu anaitwa Maria” akasema kwa ufupi kisha wakaingia ndani “Austin you are a devil.Sikutegemea kama siku moja ungeweza kunifanyia hivi.Yaani kukupenda kwangu kumbe nilifanya kosa na leo hii unanifanya mimi kama mhalifu? Nilifanya kosa kubwa sana kukupenda shetani kama wewe.I swear Austin you’ll pay for this..!!!! akasema kwa hasira Maria “Shut up !!! Austin akafoka Austin akawataka Maria na Marcelo waketi pale sebuleni halafu yeye na Job wakapanda ghorofani. “Austin what’s going on? Who is that woman? Job akauliza.Austin akavuta pumzi ndefu na kusema Anaitwa Maria.Ni mtoto wa Boaz na ndiye mpenzi wangu niliyekueleza awali” “Your girlfriend? Nini kimetomkea hadi akawa katika hali ile? Austin akamsimulia Job kila kitu kilichotokea “ Dah ! Austin una akili nyepesi sana ya kutambua mambo.Ninakubaliana nawe kuwa hapa kuna kitu kimejificha.Haiingii akilini awe na majina mawili tofauti,awe na pasi zaidi ya moja?.Kuna kitu gani anakificha? Ni vipi endapo atakuwa na majina zaidi ya hayo matatu? Tunapaswa tumchunguze huyu mpenzio.Inawezekana yeye na baba yake kuna mambo wanayafanya.” Akasema Job “ Boaz ndiye pekee ambaye anaweza akatupa taarifa tunazozitaka kuhusiana na Mukasha na ili kumfanya Boaz atupe tunachokitaka tunatakiwa kumtumia Maria .Anampenda mno mtoto wake na hatakubali jambo lolote limtokee Maria kwa hiyo atatueleza kile tunachokitaka.Kesho nitampata Boaz na atatueleza kila kitu.” Akasema Austin Job akamtazama Austin kwa makini na kusema “Austin are you sure about this? What we’re going to do is not easy so you must be sure that you are going to hurt the woman you real love.” Austin akavuta pumzi ndefu na kusema “ Yes ! I’m sure” Job akamuongoza katika chumba maalum cha mahojiano kilicho ndani ya jumba lile.Ni chumba kilichojengwa kisasa sana kiasi kwamba ukiwa nje unaweza kumuona mtu aliyemo ndani kupitia kioo maalum bila ya yeye kukuona. Sebuleni Dr Marcelo alikuwa ameketi akitazamana na Maria.Hakuna aliyekuwa akimsemesha mwenzake.Bastora ambayo Marcelo alipewa na Austin kwa ajili ya kujilinda ilikuwa mezani. “Marcelo nimefurahi sana kukuona.Ni muda mrefu hatujaonana.Nimekuwa nakukumbuka sana lakini sikujua ningekuona vipi.kwa sasa mimi makazi yangu ni afrika ya kusini na huja mara chache hapa Dar es salaam kibiashara.Umefahamiana vipi na Austin? Maria akauvunja ukimya uliokuwepo pale sebuleni “ Shut up lily !! akasema Marcelo “ Marcelo tafadhali usinifanyie hivi.Usiwe kama Austin .Tena nakushauri Marcelo usiwe na urafiki na huyu mtu he’s a monster.Siamini kama anaweza akamfanyia jambo kama hili mwanamke anayempenda.Kwa taarifa yako mimi ndiye sababu ya yeye kufika hapa alipofika leo lakini ameyasahau hayo yote na ananifanyia hivi.Sintomsamehe kamwe katika maisha yangu” akasema Maria huku akilia machozi.Marcelo akaonekana kuguswa na kumuonea huruma. “Lilian pole sana .Lakini kwa nini usimueleze ukweli kuhusu wewe na mkayamaliza mambo haya? Anakupenda sana na haachi kukuzungumzia kila dakika lakini umemchanganya wewe mwenyewe kutokana na utata wa majina yako.Hata mimi umenishangaza sana.Who you real are? Akauliza Marcelo akati nikiwa nawe nilikufahamu kama Lilian baadae nikagundua jina lako la Shamim na sasa unaitwa Maria ,what’s your real name? Did you change your name? haya ndiyo mambo ambayo Austina anahitajiku yafahamu .Funguka na mambo haya yatamalizika amani itakuwepo.Hata mimi sifurahi kukuona katika hali hii” akasema Marcelo.Maria akamtazama kwa huruma na kusema “Fine.Nitawaeleza kila kitu .Mnataka ukweli basi mtaujua lakini naomba kwanza unifungue nikajisaidie.Nimebanwa sana” akasema Maria huku akiibana miguu kuonyesha namna alivyobanwa. “ Siwezi kufanya hivyo.Wasubiri akina Austin wanakuja sasa hivi” akasema Marcelo “Marcelo nimebanwa sana tafadhali.Usiniache nikajisaidia hapa .Mimi si mhalifu na sistahili kufanyiwa hivi.Nimesema nitawaeleza kila kitu kwa hiyo basi naomba unifungua Marcelo nikajisaidie.Una bastora hapo ,itume endapo nitafanya jambo lolote la kipuuzi.Ninakwenda kujisaidia na nikimaliza utanifunga kamba zenu.” Akasema Maria.Marcelo akamtazama kwa wasi wasi mwingi “Amebanwa sana na halitakuwa jambo jema kumuacha akajisaidia hapa.Ngoja nimfungue akajisaidie” akawaza Marcelo na kwenda kumfungua Maria waya aliofungwa mikononi. “Thank you Marcelo for this.You are real a gentleman.Show me the toilet” akasema Maria na Mara tu Marcelo alipogeuka bila kutarajia akajikuta amepigwa pigo zito kichwani lililompeleka chini na kumpoteza fahamu. Haraka haraka akaichukua bastora iliyokuwa juu ya meza. “Its my turn now.He wants to know who I am and now the time has come to know who I real am” akasema Maria kwa sauti ndogo na kwa tahadhari akaenda kuchungulia dirishani “Sioni mtu yeyote nje.What is this place? I need to get out of this place now before these monsters comes down” akasema Maria kwa kunong’ona na kwa haraka akaenda mlangoni akakinyonga kitasa kwa lengo la kuufungua mlango “Stop right there !! ikasema sauti kali ya Austin aliyekuwa amesimama katika ngazi akitokea ghorofani. “Slowly put your gun down and push it to me !!!.akasema Austin kwa sauti kali Taratibu Maria akaushusha chini mkono uliokuwa na bastora kwa lengo la kuiweka chini kama alivyoamriwa lakini kabla bastora ile haijagusa chini kukatokea kitendo ambacho Austin hakuwa amekitarajia.Kwa wepesi wa aina yake Maria akageuka na kuvurumisha risasi upande aliokuwa amesimama Austin ambaye alianguka huku akivuja damu.Bastora yake ikifuka moshi Maria akamuendea Austin aliyekuwa amelala akivuja damu,machozi yakamtoka “I’m sorry my love.Sikutegemea kama siku moja tungefika hapa.Ni afadhali nikuue kuliko kukupa nafasi ya kunifahamu mimi ni nani.I love you Austin and God will forgive me for what I’m going to do” akaema Maria kwa sauti ndogo na kuelekeza bastora katika kichwa cha Austin na ukasikika mlio wa risasi. AUSTIN ANAPIGWA RISASI NA MPENZI WAKE MARIA,NINI HATIMA YAKE? MARIA NI NANI NA KWA NINI HATAKI AUSTIN AMFAHAMU? MCHAKATO WA NDOA YA RAIS DAVID ZUMO NA MONICA BENEDICT UMEANZA ..JE WATAFANIKIWA LENGO LAO? MPENZI MSOMAJI KUPATA MAJIBU HAYA NA MENGINE MENGI USIKOSE QUEEN MONICA SEASON 4

 

 

MWISHO


0 comments:

Post a Comment

Blog