Search This Blog

Saturday 5 November 2022

PENIELA (2) - 2

 






Simulizi : Peniela (2)

Sehemu Ya Pili (2)





“ Nipeleke huko chumbani ”akasema Mathew na msichana yule akamuongoza katika chumba fulani wakaingia halafu wakaanza kushuka ngazi kuelekea chini.Kulikuwa na chumba fulani kilichokuwa kama mahabusu.Kulikuwa na mlango wenye nondo nzito na kufuli kubwa.Ndani ya chumba hiki Kulikuwa na kitanda na juu ya kitanda kile kuna msichana aliyekuwa amelala pale akiwa hajiwezi kabisa na mguu wake mmoja ulifungwa pingu

“ Ouh my God ! akasema Mathew na kumtikisa yule msichana pale kitandani lakini hakuamka .Hali yake haikuwa nzuri.Kwa hasira Mathew akamgeukia yule msichana na kumnasa kibao kikalikinachompeleka hadi chini



“ Mmemfanya nini huyu binti? Yule msichana hakujibu kitu zaidi ya kulia.Mathew akakipiga piga kile kidude cha mawasiliano alichokuwa amekichomeka sikioni

“ Anitha..do you read me?



“ yes Mathew.Whats going on? Akasema Anitha

“ I need your help.Kuna msichana mmoja ana hali mbaya sana amefungwa ndani ya hiki chumba.” Akasema Mathew

“ Unahitaji msaada gani?



“ We need to take her out of here.Njoo na gari usiogope ni sehemu salama.Watu wanne wako chini na mmoja hana fahamu.Njoo haraka”akasema Mathew na kumgeukia yule msichana



“ nani ana funguo za pingu hii? akauliza



“ Ni John” akajibu kwa uoga



“ Yuko wapi huyo John?



‘ Ni mmoja wa wale uliowapiga risasi”

“ Ok twende ukanionyeshe” akasema Mathew na kupanda haraka haraka hadi katika sehemu wale jamaa walipokuwa wameanguka .Damu ilikuwa imetapakaa .Yule msichana akam John mifukoni na kumkuta na funguo halafu wakakimbia na kwende kumfungua yule msichana.

“ Mathew nimekwishafika niko hapa nje” Anitha akamtaarifu Mathew ambaye alimuamuru yule msichana kwenda kufungua geti na Anitha akaingiza gari.Mathew akambeba yule msichana asiyejiweza akamtoa nje hadi katika gari

“ Gosh.! Wamemfanya nini ? Who are these people? akauliza Anitha huku akimsaidia Mathew kumuweka vizuri yule msichana ndani ya gari.

“ I don’t know yet.Lakini tutafahamu ndani ya muda mfupi.Bado kuna mtu tunayetakiwa kuondoka naye,yeye ndiye atakayetueleza kila kitu.” akasema Mathew na kuongozana na Anitha wakaingia ndani na kumchukua yule jamaa ambaye hakuwa na fahamu wakamfunga mikono na miguu wakampakia katika buti ya gari.Mathew akarudi tena ndani na kuichukua ile tablet na kumgeukia yule msichana aliyekuwa ameegemea ukuta ka woga

“ Wewe sintakufanya chochote lakini utaondoka nasi.Tutajua kitu cha kukufanya mbele ya safari” akasema Mathew na kumuongoza msichana yule hadi katika gari wakaondoka.

“ kaka naombeni msinifanye kitu chochote.Mimi ni mfanyakazi tu wa ndani katika ile nyumba na sifahamu chochote.” Akasema yule msichana huku akilia.



“ Mathew who are these people? Walikuwa wanafanya nini na huyu msichana ? akauliza Anitha.kabla Mathew hajajibu kitu yule msichana aliyedai nimfanyakazi wa ndani akasema

“ Huyu msichana alikuwa anashikiliwa mateka na wale jamaa.Wamekuwa na tabia ya kuteka watu na kuwafungia katika kile chumba cha chini.Mimi ndiye waliyenipa kazi ya kumuhudmia huyu dada kwa chakula na kila kitu”akasema

“ Nina wasi wasi yawezekana msichana huyu akawa ndiye yule ambaye aliniambia Eva” akasema Mathew



“ Umesema Eva? Akadakia yule msichana wa kazi .

“ unamfahamu? Akauliza Mathew



“ simfahamu Eva lakini kuna siku hapa katikati walimtesa sana huyu msichana na kumlazimisha aseme alikoweka sijui kitu gani wanachomlazimisha kila siku awaambie amekiweka wapi ndipo akamtaja Eva.Wakampa simu ampigie Eva lakini yeye hakuongea vile walivyotaka wao badala yake akamuomba Eva amuokoe. Wakamnyanga’anya simu na kumpiga sana.Wamekuwa wakimtesa kila siku wakimtaka awaelekeze mahala alikoweka hicho kitu wanachokitaka”akasema yule msichana wa kazi

“ Ouh my God, we’ve found her.Huyu ndiye msichana aliyemuomba Eva amsaidie.”akawaza Mathew na kisha akachukua simu na kumpigia Eva.

“Hallow Mathew”akasema Eva

“ Eva naomba uache kila unachokiganya hivi sasa tukutane nyumbani kwangu”

“ Kuna nini Mathew? Wewe uko wapi? akauliza Eva lakini Mathew hakujibu kitu akakata simu

“Mathew kwa nini tusimpeleke kwanza huyu binti hospitali? Hali yake si nzuri hata kidogo” akasema Anitha

“Hapana Anitha.Hatuwezi kufanya hivyo.Tutamuachia Eva yeye ndiye atakayetusaidia katika hilo.Anafahamiana na madaktari wengi na atatusaidia kumpata daktari wa kuweza kumuhudumia.Tukimpeleka hospitali tutahitajika kutoa maelezo na sisi hatuna maelezo yoyote.



“ Huyu binti ana siku ya tatu leo amegoma kula chakula na ndiyo hali yake ni mbaya .Walikuwa wanajadiliana wamtafute daktari “akadakia yule msichana ambaye alionekana muongeaji sana



“ Kuna kitu gani anacho huyu msichana kiasi cha kuwafanya wale jamaa wamteke na kumfungia na kumtesa kiasihiki ili awaonyeshe mahala alipokificha hicho kitu ? Lazima kitakuwa ni kitu muhimu sana.Ngoja tutafahamu muda si mrefu sana” akawaza Mathew

“Namuonea huruma sana huyu binti kwa namna walivyomtesa.Amedhoofu na ana makovu mengi ya kuumia.Inaonekana walikuwa wakimpiga sana.Yule jamaa tuliyemchukua leo ataomba ni bora kama angekutana na mtoa roho kuliko kukutana na mimi kwa sababu kitu nitakachomfanyia ataeleza kila kitu.Haiwezekani wamfanyie huyu binti ukatili wa namna hii.” Akawaza Mathew





********





Jaji Elibariki na Noah waliendelea na safari yao kama kawaida huku kichwa cha Elibariki kikijaa mawazo mengi sana kuhusiana na kile kilichotokea na zaidi sana picha ya Peniela ndiyo iliyokuwa ikimjia kichwani mara kwa mara na kumfanya asiache kumuwaza.Walipofika katika taa za kuongozea magari katika makutano ya barabara za Mkwavinyika na Kilimanjaro iliwalazimu wasimame baada ya taa nyekundu kuwaka.Wakati wakisubiri waruhusiwe Jaji Elibariki akamuuliza Noah.

“ Noah umeoa?

Noah akatabasamu na kusema

“Hapana bado..”

“Kama bado basi unatakiwa uw……………” kabla hajamalizia alichotaka kukisema zilizotokea piki piki mbili na Ghafla Noah aliyekuwa ameleekeza macho yake nje akapiga ukelele mkubwa



“ Elibariki get down..!!!!!!!.. akasema na kumrukia Elibariki akamgandamiza katika kiti.Milio ya risasi ikarindima mahala pale na kusababisha taharuki kubwa.Watu wakashuka katika magari na kukimbia hovyo ili kujinusuru .Kwa takribani dakika tano risasi ziliendelea kurindima eneo lile.Mara kukawa kimya halafu mlango wa gari ya jaji Elibariki ukafunguliwa na mtu mmoja aliyekuwa na bastora mkononi na usoni akiificha sura yake kwa kofia nyeusi na kuacha sehemu ya macho.

“ Elibariki….!!” Akaita mtu Yule ambaye alikuwa ni mwanamke.Elibariki aliyekuwa amegandamizwa na Noah alishindwa kuitika alikuwa amechanganyikiwa .

Yule mwanamke akamsukuma Noah aliyekuwa amemgandamiza Elibariki kitini.Hakuwa na uhai tena.Alikuwa hatazamini kwa namna alivyoharibiwa na risasi.Jaji Elibariki alikuwa ameloa damu na hakuwa na hata nguvu za kusimama.Yule mwanamke akamshika mkono na kumtoa ndani ya lile gari na kumpeleka hadi katika gari ra rangi nyeusi lililokuwa nyuma ya gari la Elibariki halafu wakaondoka kwa kasi kubwa.Eneo lote halikuwa na mtu hata mmoja.Magari yalikuwa matupu watu walikuwa wameyaacha na kukimbia kuokoa maisha yao.



Dr Kigomba akiwa katika chumba kimoja pamoja na rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr Joshua wakiwa na baadhi ya wageni waliokuja kumpa pole mheshimiwa rais,simu yake ikaita akaitoa mfukoni na kutazama mpigaji halafu akainuka na kutoka nje ya kile chumba akajitenga pembeni mahala kusikokuwa na watu akaipokea

“ Hallow Festo” akasema Dr Kigomba kwa sauti ndogo

“ Mzee nimekupigia kukupa taarifa kuhusiana na ile kazi.”

“ Enhee nipe ripoti.Mmeimaliza tayari? Kila kitu kimekwenda vizuri? Akauliza Dr Kigomba

“ Tayari mzee tumeifanikisha .Nilikuwepo eneo la tukio nikishuhudia namna vijana walivyoifanya kazi lakini kuna tatizo moja lilitokea.”

“ Tatizo gani Festo?

“ Wakati vijana wakiifanya kazi yao kuna mtu ambaye hatumfahamu alitokea na kujaribu kupambana na vijana wetu kwa kujibizana nao risasi.Vijana wetu wawili wamejeruhiwa kwa risasi zilizotoka kwa huyo mtu.”

“ C’mon Festo kwa nini hakumdhibiti ? Akauliza Dr Kigomba

“ Mzee hatukufanikiwa kumfahamu mtu huyo ni nani lakini anaonekana ni mtu aliyekuwa amejiandaa sana na ni mtaalamu hasa wa kutumia silaha kwa namna alivyokuwa akifanya mashambulizi yake.Kazi ile ilituchukua zaidi ya dakika tano kitu ambacho hatukuwa tumekipanga.Sisi tulipanga iwe ni kazi ya dakika moja au mbili lakini ilituchukua muda zaidi kwa ajili ya kupambana na mtu yule ambaye alionekana kutaka kutuzidi nguvu.”

“ Kwa hiyo hakuna hata kijana mmoja aliyepoteza maisha?

“Zaidi ya kujeruhiwa kwa risasi zilizotoka kwa yule mtu hakuna hata kijana mmoja aliyepoteza maisha.”

“ Ok vizuri.Kazi yetu ya msingi ilifanikiwa? Kwa sababu hicho ndicho kitu kikubwa kuliko vyote”

“ Kwa kiasi kikubwa ninaweza kusema kwamba kazi ilikwenda vizuri kwa sababu gari la jaji limeharibiwa vibaya sana kwa risasi.Nina hakika hakuna ambaye angeweza kutoka salama.”

“ so you didn’t confirm that he’s dead? Akauliza Dr Kigomba

“ Mzee ilitulazimu kuondoka haraka eneo lile ili kuepusha mapambano zaidi na yule jamaa tusiyemfahamu aliyekuwa akijibizana nasi kwa risasi.Tatizo ni kwamba yeye alikuwa akituona lakini sisi hatukuwa tukimuona kwa hiyo ilikuwa ni ngumu sana kwenda kuhakikisha kama mtu wetu amefariki .Lakini nina uhakika mkubwa sana kwamba kutokana na shambulio lile hataweza kutoka hai” akasema festo

“ Ouh Festo ,Festo…hilo ndilo jambo ambalo nilikuonya toka mwanzo kwamba lazima uwe makini na uhakikishe kila kitu kinakwenda vizuri.Kwa sasa hatuna uhakika kama Elibariki amekufa ama vipi.Oh Festo unazidi kuniweka katika wakati mgumu sana”

“ Mzee usihofu nina uhakika mkubwa kwamba hawezi kutoka hai ndani ya gari lile.Halikuwa shambulio dogo.Hata kama ikitokea akawa amenusurika basi ni kwa mkono wa malaika lakini ninakuhakikishiaa kwamba tutamsaka kokote na kumpata .Hawezi kutukimbia ” Akasema Festo

“ Festo unanipa wakati mgumu sana .Nitakupigia tena baadae.Nimechanganyikiwa na sijui nini cha kufanya.” akasema Dr Kigomba na kukata simu.akaegeemea mti na kuvuta pumzi ndefu

“ Dah ! NImechanganyikiwa na sijui nifanye nini.” Akawaza Dr Kigomba

“ I have to inform Dr Joshua”

Dr Kigomba akatembea kwa kasi hadi katika chumba kile alichokuwamo mheshimiwa rais na wageni wake,akamfuata na kumnong’oneza kitu sikioni halafu dr Joshua kawaomba radhi wageni wake akatoka mle chumbani na Dr Kigomba wakaelekea katika chumba cha maongezi wakajifungia

“ Dr Kigomba kuna nini? Mbona unaonekana hauko kawaida? Akauliza Dr Joshua

“ Dr Joshua kazi uliyonipa kwa ajili ya kumshughulikia Elibariki imefanyika na nimepokea simu muda si mrefu toka kwa vijana kwamba zoezi hilo limefanyika lakini kulikuwa na tatizo dogo.”

“ Tatizo gani Kigomba? Akauliza Dr Joshua

“ Kama nilivyokutarifu mapema kwamba njia ya ajali ingekuwa ngumu hivyo kwa kuwa suala lenyewe ulitaka lifanyike haraka ,ilitulazimu kutumia njia ya shambulio ili ionekane kama vile Elibariki alivamiwa na watu wasiofahamika wakamuua.Vijana waliandaa shambulio la kustukiza lakini katika shambulio hilo kulitokea upinzani.Kuna mtu ambaye bado hajafahamika ambaye alikuwa akishambuliana na vijana wetu na kuwajeruhi wawili .Kutokana na mazingira ya mahali hapo ilikuwa ni vigumu kwa vijana wetu kumfahamu mtu huyo na hivyo baada ya kutekeleza shambulio lao ikawalazimu kutoweka haraka sana eneo lile” akasema Dr Kigomba

“ Dr Kigomba bado sijakuelewa,naona unaniambia maneno mengi .Nataka neno moja tu Elibariki amekufa ama bado” akasema Dr Joshua

“ Kwa mujibu wa Festo ni kwamba hana uhakika kama amefariki ama bado lakini anadai kwamba lilikuwa ni shambulio zito ambalo Elibariki hawezi kutoka hai”

“ Ouh my God !!... akasema Dr Joshua na kushika kiuno

“ so you are not sure if he’s dead or not? Akauliza Dr Joshua

“ Mzee sina uhakika bado kama amefariki ama bado ” akasema Dr Kigomba

Dr Joshua akafikri kwa muda na kusema

“ Dr Kigomba kwa nini jambo hili limekwenda hivi? Nilikuonya toka mwanzo kwamba jambo hili linahitaji umakini mkubwa lakini kwa nini hukuliwekea uzito wa kutosha?

“ Dr Joshua suala hili tumelichukulia kwa uzito unaostahili lakini hatukujua kama kunaweza kutokea jambo kama lililotokea la huyo mtu asiyejulikana.Lakini kama kujitahidi tumejitahidi na kilichobaki ni kupata uhakika kama Elibariki amefariki au bado.”

“ You didn’t do enough Kigomba!! Akasema kwa ukali Dr Joshua.

“ Kama kazi hii ingefanyika inavyotakiwa basi tusingekuwa hapa tunakaa roho juu juu hatuelewi kama Elibariki ni mzima ama vipi.Endapo vijana hawakufanya kazi vizuri na Elibariki akawa mzima basi tutakuwa tumeharibu kila kitu.Mambo yatazidi kuwa mabaya kwa upande wetu.Ouh Kigomba umenichanganya sana ..”

“ Dr Joshua hatuna muda wa kuendelea kulaumiana .Kazi imekwisha fanyika na kinachotakiwa hivi sasa ni kupata uhakika kama ilifanikiwa ama vipi.Kwa hiyo badala ya kuendelea kunilaumu kwamba sikufanya kazi inavyotakiwa chukua simu na umpigie kamanda wa polisi na umuulize kama Elibariki ni mzima ama vipi.Nina hakika mpaka mida hii tayari atakuwa amekwisha pewa taarifa za tukio hilo” akasema Dr Kigomba.Dr Joshua akainama akafikiri halafu akachukua simu na kumpigia Kamishna John adungile kamanda wa polisi kanda maalum ya Dare s salaam

“ Hallow mzee” akasema kamishna John

“ Kamishna nimepata taarifa muda si mrefu kwamba kuna yule kijana wangu jaji Elibariki ameshambuliwa na watu wasiojulikana.Naomba unithibitishie taarifa hizi ni za kweli? Akauliza Dr Joshua

“ Mheshmiwa hizi ni taariza za kweli kabisa.Tukio hilo ni kweli limetokea katika makutano ya barabara za Mkwavinyika na Kilimanjaro.Kwa mujibu wa mashuhuda ni kwamba wakati gari zikiwa zimesima zikisubiri taa za kuongozea magari ziwaruhusu wapite zilitokea piki piki mbili zikiwa na watu wawili kila moja na kisha wakaanza kulishambulia gari la mheshimiwa jaji kwa risasi.”

“ Jaji Elibariki alikuwemo ndani ya gari hilo? Kama alikuwemo ni mzima? Akauliza Dr Joshua

“ Kwa taarifa nilizozipata toka kwa kamanda wangu aliyeko katika eneo la tuko hivi sasa ni kwamba katika gari la mheshimiwa jaji kumekutwa mtu mmoja tu na ambaye amekutwa amekwisha fariki.Lakini wameshindwa kumtambua ni nani kutokana na kuharibiwa vibaya kwa risasi.Kwa hiyo ni vigumu kuthibitisha kaam jaji Elibariki alikuwemo ndani ya hilo gari wakati wa shambulio ama vipi.Mwili wa mtu huyo aliyekutwa ndani ya gari umepelekwa katika hospitali ya taifa kwa utambuzi”

“ Ok kamishna .Mpaka sasa kuna fununu zozote za kuwafahamu watu hao waliofanya shambulio hilo?

“ Mpaka sasa bado hatujawafahamu watu hao ni akina nani lakini nakuhakikishia mzee kwamba tutawasaka watu hawa katika kila kona ya jijii na tutawapata.”

“ Ahsante sana kamishna kwa taarifa hii.Ninaomba ufanye kila linalowezekana ili uweze kuwabaini watu waliofanya kitendo hicho”

“ Tututajitahdi sana mzee na ninakuhakkishia kwamba lazima tutawapata tu” akasema Kamishna na Dr Joshua akakata simu akamgeukia Dr Kigomba

“ Kwa mujibu wa kamishna ni kwamba kuna mtu mmoja aliyekutwa ndani ya gari la jaji Elibariki lakini wameshindwa kumtambua kutokana na kuharibiwa vibaya kwa risasi.Kwa hiyo tuna uhakika kwamba kuna mtu amekufa ndani ya gari lakinihatuna uhakika kama kweli ni Elibariki.”

“ Ok Dr Joshua niachie mimi kazi hii.Ninakwenda sasa hivi hospitali kwenda kumtambua mtu huyo kama ni elibvariki.”

“ Vipi kuhusu Flaviana ? Kuna haja ya kumweleza chochote kuhusiana na jambo hili ?

“ Kwa sasa hakuna haja ya kumueleza chochote hadi hapo tutakapokuwa na uhakika kwamba aliyefariki ni mumewe.Ninakwenda huko hospitali sasa hivi kuthibitisha kama ni yeye kweli ama vipi ” akasema dr Kigomba.

“ Sawa Kigomba fanya hivyo Ili tuwe na uhakika kama zoezi letu limefanikiwa ama vipi.hata hivyo ninawas………..” kabla hajamaliza kuongea ,simu yake ikaita .Alikuwa ni Flaviana.Dr Joshua na Kigomba wakatazamana.

“ Nina hakika tayari atakuwa amekwishapata taarifa za tukio.What am I going to tell her? Akauliza Dr Joshua

“ Ongea naye mweleze kwamba hata wewe umezipata taarifa hizi sasa hivi “ akasema Dr Kigomba.Dr Joshua akabonyeza kitufe cha kupokelea simu

“ Hallow Flaviana”

“ Baba uko wapi ? Akauliza Flaviana huku akilia

“ Niko huku ndani katika chumba cha maongezi.Kuna nini Flaviana mbona unalia?

“ Baba mume wangu..Eli ame…”

“ Flaviana …” akasema Dr Joshua lakini tayari simu ilikwishakatwa

“ Tayari ana taarifa.Siku hizi taarifa huwa hazichelewi.Kigomba nenda hospitali mara moja kathibitishe ili tujue nini cha kufanya “ akasema Dr Joshua .Kabla hawajatoka ndani ya kile chumba Flaviana akafika akikimbia .Machozi yalikuwa yanamtoka.Alikuwa ameongozana na Anna mdogo wake.Alipomuona baba yake akamkumbatia huku akilia

“ Baba ! mume wangu.Elibariki amepigwa risasi....” akasema Flaviana

“ Flaviana nyamaza kulia kwanza.Hata mimi nimezipata taarifa hizo sasa hivi nimepigiwa simu na kamishna wa polisi kanda maalum na amenithibitishia kwamba ni kweli kuna watu wasiofahamika wamelishambulia gari la mumeo na kuna mtu mmoja amekutwa amekufa lakini wameshindwa kumtambua mtu aliyekuwemo ndani ya gari hilo kama ni mumeo .Hakuna mwenye uhakika kama mumeo alikuwemo ndani ya hilo gari.Elibariki ni mtu maarufu hapa mjini kama angekuwa ni yeye basi tungekwisha jua.”

“ dady its him..Ouh Eli….Nimetoka kuongea naye usiku huu” Akasema Flaviana huku akilia

“ Usilie Flaviana.Nimemtuma Dr Kigomba aende huko hospitali ili akathibitishe kama kweli ni Eli ndiye aliyekuwamo ndani ya hilo gari ama vipi” akasema Dr Joshua

“ Ninakwenda naye.Nataka nikathibitishe kama kweli mume wangu ameuawa “ akasema Flaviana.Dr Joshua alishindwa kumkatalia mwanae kwenda hospitali

“ Dr Kigomba ongozana na Flaviana kwenda hospitali.Mimi nitabaki na wageni walioko hapa.Mtanipa taarifa baada ya kuthibitisha kama kweli mtu huyo ni Elibariki” akasema Dr Joshua

Kwa haraka Dr Kigomba akaongozana na akina Flaviana wakaingia katika gari wakaelekea hospitali.Njia nzima Flaviana alikuwa analia.Walifika hospitali wakapokewa na kupelekewa katika chumba cha maiti wakaonyeshwa maiti iliyokuwa imetolewa ndani ya gari la jaji Elibariki.Ilikuwa imeharibiwa vibaya kwa risasi

“ This is not him.This is not my husband.” Akasema Flaviana.Watu wote mle ndani wakaangaliana

“ Flaviana are yousre this is not him? Akauliza Dr Kigomba

“ This is not him.Ninamfahamu mume wangu vizuri na nimetoka kuongea naye usiku huu kwanza haya si mavazi aliyokuwa amevaa,hakuwa amevaa kaptura .This is someone else.Mume wangu si huyu..” Akasema Flaviana na kuchukua simu yake akajaribu kupiga namba ya simu ya mumewe lakini hazikuwa zikipatikana.

“ Where is my husband? Akajiuliza Flaviana huku akihisi kuishiwa nguvu akakaa chini.Dr Kigomba alihisi kuchanganyikiwa.

“ Eli bariki hajafa.Yuko wapi ? Swali hili lilimuumiza sana kichwa.



*******



Mlinzi aliwafungulia geti akina Mathew wakaingia ndani .Nyumba ilikuwa kimya .Noah hakuwepo.Mathew akamtoa yule msichana ambaye hali yake iliendelea kuwa mbaya akampeleka sebuleni na kumlaza katika sofa .Akamtazama na kumuonea huruma sana

“ Hali yake inazidi kuwa mbaya.Anahitaji msaada wa haraka” akawaza Mathew na kumpigia simu Eva

“ Eva uko wapi? Ninakuhitaji haraka.Mimi tayari niko hapa nyumbani”

“ Niko njiani Mathew.Nilikwama kidogo katika foleni lakini ndani ya dakika tano nitakuwa nimefika hapo kwako” akasema Eva.

Mathew akaenda katika gari lake na kufungua buti akamtoa yule jamaa aliyekuwa amemfungia mle akambeba na kumuingiza ndani.Moja kwa moja akampeleka katika chumba alichokuwa amemfungia Arnold mchana akamlaza katika kitanda na kumfunga miguu na mikono akamuacha na kurejea sebuleni .Wakati huo huo gari la Eva likafunguliwa geti na kuingia ndani.

“ Eva karibu sana” akasema Mathew akimpokea Eva

“ Mathew ahsante sana.Kuna tatizo gani? Akauliza Eva kwa wasi wasi.Mathew hakumjibu kitu akamuongoza Eva hadi sebuleni.Mstuko alioupata Eva hauelezeki

“ We found her” akasema Mathew.Eva alishindwa kujizuia akainama na kumkumbatia msichana yule aliyekuwa amelala pale sofani huku hali yake ikionekana mbaya sana.Machozi yakamtoka

“ Mmempata wapi? Wamemfanya nini? Akauliza Eva

“ Eva ni hadithi ndefu lakini kwa sasa tunachotakiwa kukifanya ni kumpatia matibabu.Inasemekana kwamba amegoma kula chakula siku ya ya tatu leo.Hiyo ndiyo sababu kubwa iliyomfanya adhoofu namna hii.Tunatakiwa kumpatia huduma ya haraka.Unafahamiana na daktari yeyote ambaye anaweza kumuhudumia kwa haraka? Akauliza Mathew

“ Ndiyo ninafahamiana nao.Ninaombeni dakika kumi nikamchukue daktari .”akasema Eva na kutoka mbio hadi katika gari lake akamfuata daktari

“ Its time to find the truth now.” akasema Mathew na kuingia katika chumba Fulani ambacho ameweka vifaa vingi akachukua sanduku lenye rangi nyekundu halafu akaenda katika chumba alichomuweka yule jamaa ambaye tayari alikwisha zinduka .Mathew akammulika katika macho kwa kutumia tochi ndogo halafu akachukua kidude Fulani kidogo mithili ya chupa ya dawa akakifungua na kukiweka katika pua za yule jamaa na kumfanya apige chafya mfululizo.Mathew akavuta kiti na kuketi.Akamtazama yule jamaa kwa macho makali na kusema

“ Wenzio wote ulio kuwa nao wamekwisha fariki dunia umebaki wewe tu na maisha yako kwa sasa nimeyashikilia mimi.Nitakuwa na maneno machache sana ya kuongea nawe na nitaomba nitakachokuuliza unijibu kwa usahihi ama sivyo nitakufanyia kitu kibaya ambacho huajwahi kuona binadamu akimfanyia binadamu mwenzake.” Akasema Mathew kwa ukali na mara mlango ukafunguliwa akingia Anitha.

“ Anitha tafadhali naomba unipishe .Hutakiwi kukaa ndani ya chumba hiki.Hutakiwi kuona mambo yatakayofanyika humu” akasema Mathew.Anitha hakuongea kitu akaufunga mlango akatoka.Aliogopa kwa namna Mathew alivyokuwa amebadilika.Yule jamaa palekitandani alikuwa anatetemeka kwa woga.Mathew akamsogelea na kumwambia

“ Nataja uniambie ninyi ni akina nani? Mfanya kazi gani?

Yule jamaa hakutaka kumchezea Mathew alimuona namna alivyokuwa amekasirika hivyo akarekebisha koo lake na kusema kwa sauti yenye kukwaruza

“ Kusema ukweli sisi ni..” akasita .Mathew akamtazama kwa hasira halafu akaenda katika kile kisanduku chekundu akachukua kifaa cha kutobolea

“Nilikwambia kwamba nina muda mchache sana wa kuongea nawe.Sihitaji kabisa kuchezewa akili yangu.” Akasema Mathew na kukiwasha kidude kile akakichomeka katika mguu wa Yule jamaa ambaye alitoa ukulele mkubwa wa maumivu.

“ Nadhani sasa umekwisha nielewa mimi ni nani.Kwa hiyo nieleze haraka ninyi ni akina nani na nini shughuli zenu? Akasema Mathew.Yule jamaa bado aliendelea kulia kwa maumivu makali huku damu ikimtoka.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“ Naona bado hujanifahamu vizuri.” Akasema Mathew na kuchukua tena kile kifaa akakiwasha na kutaka kukizamisha katika mguu wa yule jamaa.Akapiga ukulele mkubwa akimtaka asifanye vile.

“ tafadhali usiniumize tena.Nitakueleza kila kitu” akasema yule jamaa huku akilia kwa maumivu makali aliyokuwa akiyasikia

“ Niambie haraka sana ninyi ni akina na nini kazi zenu?

“ Sisi kazi zetu ni wizi wa magari.Huwa tunaiba magari ndani na nje ya nchi.Vile vile huwa tunafanya shughuli za ujambazi ,kuvamia mabenki na kupora fedha n.k Hizo ndizo shughuli zetu” akasema yule jamaa na kuuma meno kwa maumivu makali .Bado alikuwa amefungwa miguu na mikono katika kitanda.

“ Kwa nini mnamfutilia Eva? Nani kawatuma mumfuatilie Eva? Akauliza

“ Sisi hatumjui Eva na wala hatujawahi kumuona”

‘ Kama hamumjui kwa nini mnamfuatilia? Akauliza Mathew

“ ouh kaka ninaumia sana.Naomba unifungue walau mikono .Ninasikia maumivu makali sana.Nitakueleza kila kitu unachokitaka naomba uniamini”akasema yule jamaa.Mathew akamtazama na kuamua kumfungua

“ Ukweli wako ndio utakaokuweka hai.Niambie ukweli mtupu.Kwa nini mnamfuatilia Eva ” akasema Mathew

“ Nitakueleza kila kitu ila naomba usiniue” akasema yule jamaa baada ya kufunguliwa mikono



Yule jamaa bado alikuwa katika maumivu makali na damu iliendela kumtoka sehemu ile ambayo Mathew alimtoboa na kile kifaa cha kutobolea

“ Sisi hatukuwa tukimfahamu Eva hadi wiki hii.” Akasema Yule jamaa na kuuma meno kwa maumivu makali aliyokuwa akiyasikia

“ Ilikuwaje mkafahamu Eva na kuanza kumfuatilia? Hicho ndicho kitu ambacho nahitaji kukifahamu” akasema Mathew kwa ukali

“ Ni jambo lenye mlolongo mrefu kidogo lakini nitakuweleza ila ahhgggh ! ..yule jamaa akashindwa kuendelea akagugumia kwa maumivu makali sana.Akajikaza na kusema

“Kuna mzee mmoja anaitwa mzee Kitwana.Yeye ni mzee maarufu sana hapa mjini na ni mtu mwenye uwezo mkubwa kifedha.Ana magari mengi tu ya kubeba mizigo pamoja na biashara nyinginezo nyingi.Huyu ndiye aliyekuwa mfadhili wetu mkuu wa kazi zetu.Mzee Kitwana alikuwa na mtandao mkubwa wa watu na alikuwa akipata taarifa nyingi kwa hiyo kila alipokuwa akipata taarifa Fulani kuhusiana na fedha mahala Fulani basi huwa anatutafuta na kutupa kazi hiyo ya kwenda kuvamia na kuiba.Siku moja alitufuata na kutuambia kwamba kuna kazi ambayo anataka kutupa na yenye pesa nyingi mno tofauti na ujambazi.Alisema kwamba kuna kitu Fulani kinatakiwa na watu wa kutoka nje ya nchi lakini hakututajia ni kitu gani hicho na ni akina nani hao ambao walikuwa wakikitafuta hicho kitu.” Akanyamaza akafumba macho kidogo na kusema

“ Tafadhali kaka naomba unisaidie kuzuia damu hii isiendele kutoka Nitakufa” akasema Yule jamaa.

“Nimekwambia nieleze kila kitu ,na kama usipofanya hivyo you’ll bleed to death.” Akasema Mathew

“ Ok nitakueleza kaka lakini naomba baada ya kumaliza kukueleza ukweli unitafutie dawa.Nihurumie ninasikia maumivu makali sana” akasema Yule jaama

“ Kitu hicho alichokuwa anakiongelea mzee Kitwana kilikuwa kinatakiwa kutoka Ikulu. Na ili kukipata walilazimika kujenga mtandao .Kulikuwa na yeye mzee Kitwana halafu kukawa na mzee Matiku.Huyu alikuwa ni mwanajeshi mstaafu na aliwahi kuwa mlinzi wa rais kwa miaka ya nyuma.Baada ya huyu mzee Matiku kukawa na kijana mmoja anaitwa Edson ambaye alikuwa akifanya kazi Ikulu na ndiye aliyefanikisha kila kitu hadi kitu hicho kikapatikana.

Mathew aliposikia jina Edson likitwajwa akahisi nywele zikimsimama na mwili wote ukastuka.

“ Ouh my God ! Edson “ akasema kwa sauti ndogo na kumkazia macho Yule jamaa

“ Umesema Edson? Ni Edson Kobe? Akauliza Mathew

“Ndiyo Edson Kobe.Kumbe unamfahamu aagghhhhh..! akaguugumia kwa maumivu makali

“ Dah ! Ahsante Mungu tumefika katika ukweli” akawaza Mathew

“ Endelea ! akasema

“Baada ya kukipata kitu hicho,alikabidhiwa mzee Matiku ili akihifadhi wakati wakisubiri kulipwa fedha zao na watu waliokuwa wakikihitaji . Mzee Kitwana aliungana na Edson kwa siri wakamzunguka mzee Matiku na kuikiiba kitu hicho wakimtumia mpenzi wa mzee Matiku aliyeitwa Brigita.Edson alijenga mahusiano ya siri na Brigita na hivyo wakafanikiwa kuiba kitu hicho kwa lengo la kukiuza bila kumshirikisha mzee Matiku.Mzee Matiku alifanya uchunguzi na kugundua kwambna ni washirika wake Kitwana na Edson ndio waliomzunguka na kukiiba kitu kile.Alikasirika sana na hivyo kuamua kuvujisha siri kwa wakuu wa Edson kuhusiana na wizi wa kitu kile.” Akanyamaza na kisha akaendelea

“ Edson aliuawa wiki moja tu baada ya mzee Matiku kuvujisha siri kwa wakubwa zake.”Akasema Yule jamaa na kabla hajaendelea zaidi Mathew akauliza

“ Nani alimua Edson?

Yule jamaa akamuangalia na kusema

“ White house”

“ White house ?unamaanisha nini?

“ Watu toka ndani ya Ikulu”akasema Yule jamaa .Mathew akakaa kimya kwa muda.Mambo mengi sana yakamjia kichwani .

“ Endelea” akamuamuru yule jamaa

“ Wiki mbili baada ya Edson kuuawa ,KItwana akatuamuru tumuue Brigita ambaye ndiye aliyekiiba kitu hicho kwa mzee Matiku .Matiku na Kitwana waliendelea na malumbano ya wao kwa wao na ikamlazimu Kitwana aamuru Matiku auawe,tukamuua.Baada ya hapo tukagundua njama mbaya ya mzee Kitwana.Alikuwa akitaka kuipata pesa yote peke yake kwa hiyo alipanga mpango wa kutumaliza ili abaki peke yake na kuchukua pesa yote peke yake.Kwa bahati mbaya watu aliowatafuta kwa ajili ya kutuua ni wa washirika wetu wa karibu na walipotueleza hatukukawia ikatulazimu kumuua mzee Kitwana na sisi kubaki na biashara hiyo.Tulipomuua Kitwana tuligundua kwamba kitu hicho hakikuwepo nyumbani kwake lakini baadae tuligundua kwamba alikuwa amekificha kwa msichana mmoja ambaye walikuwa na mahusiano ya kimapenzi.Tulimsaka msichana huyo na kumfungia mle ndani kwa muda wa miezi saba sasa tukitaka atuonyeshe mahala alipokificha hicho kitu.Baada ya kumpa mateso mengi hatimaye aliamua kutueleza ukweli kwamba kitu hicho amekificha kwa msichana mmoja anaitwa Eva.Kwa kuwa hatukuwa tukimfahamu Eva ni nani ilitulazimu kuanza kumtafuta ili kumfahamu ni nani na tukafanikiwa kumfahanmu kwamba ni mfanykazi wa idara ya usalama wa taifa kwa hiyo basi ikatulazimu kuanza kuzifuatilia nyendo zake ndipo tulipomtafuta mtaalamu mmoja wa program za kompyuta na kumuomba atutengenezee program yenye kuweza kumfuatilia mtu na leo hii ndiyo ametukabidhi kazi tuliyomtaka atufanyie.Kwa hiyo hivyo ndivyo ilivyokuwa hadi tukamfahamu Eva.Nimekwisha kujibu maswali yako naomba sasa unisaidie jeraha hili lisiendele kutoa damu” akasema Yule jamaa na kujaribu kuizuia damu isiendee ktoka kwa kutumia mkono wake

“ Nani mnunuzi wa hicho kitu ? Mlitaka kumuuzia nani? Akauliza Mathew

“ Mnunuzi ambaye anakitaka hicho kitu anaitwa Habib soud anatokea Saudi Arabia” akasema Yule jamaa.

“ Mna mawasiliano na huyo jamaa?

“ Ndiyo huwa tunawasiliana naye na tuliwasiliana naye hata juzi na akatuambia kwamba muda wowote tukifanikiwa kukipata tumtaarifu ili aweze kutupa maelekezo ya namna tukavyoipata pesa yetu” akasema Yule jamaa

Mathew akainama akafikiri kwa muda halafu akainua kichwa

“ Una bahati sana.Una maisha marefu zaidi ya paka.Sintakufanyia kile ambacho nilipanga kukufanyia.Nitakutibu jeraha lako lakini sintakuachia huru” akasema Mathew na kutoka mle chumbani akaenda chumbani kwake akarejea na kisanduku cha huduma ya kwanza.Akafungua kichupa Fulani kilichokuwa na unga unga akamimina unga ule katika kidonda cha yule jamaa ambaye alipiga ukele mkubwa sana na kumfanya Anitha aliyekuwa sebuleni kufika haraka mle chumbani kuangalia kuna nini.

“ Mathew whats going on? Akauliza Anitha

Mathew hakujibu kitu akaendelea na kazi ya kulifunga jeraha la Yule jamaa. Anitha aliogopa sana kwa namna damu ilivyokuwa imetapakaa mle ndani .Mathew naye alikuwa amechafuka damu

“ Eva tayari amekwisha rejea na daktari anamuangalia Yule msichana” akasema Anitha

“ Muite Yule msichana tuliyetoka naye kule kwa hawa jamaa aje afanye usafi ndani ya hiki chumba “ akaamuru Mathew na Anitha akakimbia haraka kwenda kumleta msichana Yule.Wakati akiendelea na kusaficha mle chumbani Mathew na Anitha wakatoka moja kwa moja wakaelekea sebuleni.Eva alikwisha mleta daktari na alikuwa anaendelea kumuhudumia Yule msichana.Mathew akamuita Eva pembeni

“ Eva do you trust this doctor?

“ Ndiyo ninamuamini sana.Anaifahamu kazi ninayoifanya na amekuwa akinisaidia sana kila ninapohitaji msaada wa tiba kama huu”

“ Ok Good.Sasa tuna mtu mwingine naye anahitaji matibabu anatakiwa atibiwe jeraha|” akasema Mathew halafu akaomba waongozane hadi katika chumba ambacho hupangia kazi

“ Mathew poleni sana kwa misuko suko mliyoipata.Nashukuru sana kwa msaada huu mkubwa na ninashukuru sana kwa kunisaidia kumpata Sabina”

“ Yule msichana anaitwa Sabibna? Akauliza Anitha

“ Ndiyo anaitwa Sabina.Sina cha kuwapa kwa kunisaidia kumpata.Nilikuwa naumiza kichwa sana nitampata wapi lakini nashukuru Mungu alikuleta kwangu na umenisaidia nimempata.” Akasema Eva

“ Usijali Eva hata sisi ulitusaidia sana kuweza kumpata kanali Adolf na kwa kupitia yeye tuliweza kuifanikisha kazi tuliyokuwa tunaitaka.Nilikuahidi kukusaidia na nimeitekeleza ahadi yangu.”

“ Ahsante sana Mathew.Sina neno zuri la kushukuru.By the way who are these people? Mmefahamu ni kwa nini walikuwa wananifuatilia? Kwa nini walimteka Sabina? Akauliza Eva

“ Watu hawa wanafanyakazi ya ujambazi kama alivyodai mmoja wao ambaye nimetoka kumuhoji sasa hivi.Walimteka Sabina ili awaonyeshe mahala kilipo kitu Fulani ambacho ni Sabina pekee anafahamu kilipo.Baada ya kumtesa sana Sabina aliwaambia kwamba kitu hicho alikupatia wewe umfichie na siku ile alipokupigia na kukutaka umsaidie alipewa simu ili awasiliane nawe.Baada ya hapo walianza kukufuatilia ili wakufahamu nyendo zako na ili kulifanikisha hilo wakamtumia mtaalamu mmoja wa program za kompyuta kutengeza programu itakayowawezesha wao kukufuatilia na leo hii ndiyo maana walikuwa wanakufuatilia ili waweze kutega kifaa katika gari lako cha kuweza kukufuatilia.Kwa hiyo Eva Sababu kubwa iliyowafanya wakufuatilie ni hiyo .Kuna kifaa anacho Sabina na walikuwa wakikihitaji sana.” akasema Mathew na kumuacha Eva akishangaa

“ Eva ni kweli kifaa hicho Sabina alikukabidhi umfichie? Akauliza Mathew

“ Hapana hakunipa.Yawezekana kuna mahala kwingine amekiweka kwa sababu mimi wala sina mazoea naye ya kufikia hatua hiyo.Mimi ninamfahamu kama mteja mzuri wa baa yangu.Ni kitu gani hicho wanachikitafuta hawa jamaa?

“ Eva ni hadithi ndefu sana tutaongea baadae.Kinachotakiwa kwa sasa ni kujitahidi Sabina apate fahamu na atueleze ni wapi alikokiweka kitu hicho.Kwa sasa naomba nenda kamsaidie daktari .Nina maongezi na Anitha” akasema Mathew.Alipohakikisha Eva ametoka Mathew akasema

“ White house killed Edson” akasema Mathew baada ya Eva kutoka mle chumbani.

“ Ouh my God ! Anitha akashangaa

“ Anitha suala hili si suala dogo kama tulivyokuwa tunalifikiria.Ni jambo kubwa na zito” akasema Mathew na wote wakabaki kimya.





“ Mathew I’m so scared.What real happened? Who ordered him killed? Akauliza Anitha

Mathew akamueleza kila kitu alichokipata toka kwa yule jamaa.

“ Dah ! kwa kweli suala hili si dogo kama ulivyosema.Sikufikiria kabisa kama jambo hili linaweza kuwa namna hii.Kwa maana hiyo Elibariki alikuwa sahihi kabisa kumuachia huru Peniela kwani alibambikiwa tu ile kesi.Kuna kitu alikihisi hakikuwa sawa na ndiyo maana akatutaka tufanye uchunguzi” akasema Anitha

“ Hata mimi kutoka mwanzo nilihisi kuwa lazima kuna sababu nzito iliyopelekea kifo cha Edson” akasema Mathew

“ Kwa hiyo baada ya kufahamu nani waliomua Edson,nini kinafuata? Akauliza Anitha

“ Kinachofuata ni kitu ambacho sikuwa nikitaka hata kukifikiria.”

“ Ni kitu gani Mathew?

“ We’re going to deal with white house.”

Anitha hakujbu kitu akabaki anamuangalia Mathew. hata yeye mwenyewe alitishika

“ Edson aliuawa na watu toka ndani ya Ikulu ,hilo tumekwisha lifahamu.Lakini hatuwezi kuishia hapo.Lazima twende mbali zaidi.Kwanza lazima tukipate hicho kitu alichokiiba na kilichopelekea yeye kuuawa.Nina hakika kabisa mpaka ifike hatua ya kumuua lazima kitu hicho kitakuwa ni kikubwa sana.Nina uzoefu wa kutosha na mambo ya ikulu kwani nimewahi kushughulika na kesi kadhaa kuhusiana na ikulu na ndiyo maana nina uhakika mkubwa kwamba kitu hicho hakitakuwa kidogo.”

“ Mathew unahisi kitu hicho kinachoongelewa inaweza kuwa ni siri Fulani? Akauliza Anitha

“ Inawezekana kabisa ikawa ni siri Fulani au nyaraka Fulani za siri.Ukumbuke kwamba Edson alikuwa akifanya kazi katika idara ya mawasiliano Ikulu kwa hiyo inawezekana kuna siri Fulani aliiba .Nina uhakika huo lakini tutajua kila kitu baada ya kukipata kitu hicho.Lakini tukae tukijua kwamba hatua inayofuata lazima tuingie katika lile jumba jeupe.Kule ndiko kuna majibu ya kila kitu.na tukianza kulichunguza jumba lile it’s a victory or death ” akasema Mathew

“ Vipi kuhusu Peniela na Team SC41? Akauliza anitha

“ Kwa sasa tuna hakika kwamba Peniela hakuhusika katika mauaji yale ya Edson lakini tumeshukuru kwani ametufanya tukagundua kuhusu uwepo wa Team SC41.Yeye pia tutamchunguza ili tufahamu kama anahusika na Team SC41.Tutakapopata majibu ya uchunguzi wetu tutahamia kwa Team SC41.Halafu kuna kitu ambacho tunatakiwa tukifahamu pia kuna huyu mtu ambaye ni mnunuzi wa kifaa hicho anaitwa Habib Soud toka Saudi Arabia .Tunatakiwa tumfahamu ni nani na pengine tunaweza tukagundua kitu toka kwake.Zitafute habari zake ili tumjue” Akasema Mathew na kutoa simu yake akazitafuta namba za Elibariki akapiga lakini simu yake haikuwa ikipatikana,

“ Elibariki na Noah wako wapi?Mbona simu ya Elibariki haipatikani? Inawezekana Noah akawa amemshawishi wapiti sehemu ya burudani.Ninamfahamu vizuri Noah ni mtu wa starehe sana.” Akasema Mathew

“Muache atulize akili kwa sababu tuna kazi kubwa mbele yetu” akasema anitha huku akikaa katika kompyuta yake

“ Anitha wakati unaendelea kutafuta taarifa za Habin mimi ngoja nikamsukume daktari amuamshe Sabina haraka ili aweze kutuonyesha mahala alikokificha hicho kitu.Hatuna muda wa kusubiri sana.Ukipata chochote kuhusiana na Habib utanitaarifu” akasema Mathew na kutoka akaelekea sebuleni ambako daktari alikuwa amemtundikia Sabina chupa ya maji iliyokuwa na dawa ya kuweza kumpa nguvu kwani alikuwa amedhoofu sana.

“ anaendeleaje Sabina” akauliza Mathew

“ kwa sasa nimemtundikia chupa ya maji na nimechoma dawa ya kuweza kumpa nguvu kwani hali yake ni kama unavyoiona amedhoofu sana” akasema daktari

“ Anaweza akachukua muda gani hadi kupata nafuu? Akauliza Mathew

“ Siwezi kuwa na uhakika lakini anaweza akachukua siku mbili hadi tatu ili kuweza kurejea katika hali yake ya kawaida” akasema daktari.Mathew akamuomba Eva waongee pembeni

“ Unasemaje Mathew? Akauliza Eva

“ Eva kuna jambo ambalo sikuwa nimekutaarfu.Ni kwamba nimegunduda kwamba Sabina ana uhusiano na suala ambalo nilikuwa ninalichunguza.Kwa sasa tayari tumepata mwanga Fulani lakini tunahitaji kulichimba zaidi suala hili.Kwa hiyo basi nitahita kikukifahamu kitu hicho ambacho amekificha mahala ambacho hawa jamaa walikuwa wakikihitaji”

“ Hizo ni habari njema sana Mathew.Siku nyingine usikatae kutoa msaaa ukiombwa” akasema Eva

“ Ndiyo Eva ni habari nzuri lakini kuna jambo ambalo lazima lifanyike”

‘ jambo gani Mathew?

“Sabina anatakiwa aamshwe haraka ili tuweze kumuhoji atuonyeshe ni wapi alikokihifadhi kifaa hicho” akasema Mathew

“ Sabina hajitambui na amedhoofu sana.Tutamuamshaje?

“ Kuna sindano ambayo atachomwa na itamuamsha lakini ni ya hatari sana inaweza ikamsababishia kupoteza maisha.Kwa hiyo basi lazima tufanye maamuzi magumu”

“ No Mathew.Hatuwezi kufanya jambo kama hilo kwa huyu binti.Hebu muangalie namna alivyodhoofu.Muonee huruma Mathew”

“ Eva kazi yako ni nyepesi na nina hakika haujawahi kukutana na mikiki mikiki kamahii.Kazi ninazozifanya mimi zinahitaji moyo wa chuma,na tunapokuwa katika kazi kama hizi moyo wa huruma hutoweka na tunavaa moyowa ujasiri.Lazima tufanye maamuzi magumu kwa ajili ya kupata kitu muhimu na kwa sasa kitu muhimu tunachikihitaji ni hicho alichokificha Sabina.Hakuna namna nyingine tunayoweza kufanya kukipata kitu hicho kwa haraka zaidi ya njia hiyo niliyokwambia” akasema Mathew

“ Hapana Mathew,sikubaliani nawe hata kidogo.Hatuwezi kumfanyia Sabina ukatili wa namna hii .Sabina yuko katika mikono yangu na lazima tumsubiri hadi hapo atakapopata nafuu ndipo tuweze kumuhoji taratibu na atueleze mahala alipoweka hicho kifaa.Huyu si mhalifu na hatuwezi kutumia nguvu katika kumuhoji.” Akasema Eva.Mathew akainama akafikri kidogo kisha akasema

“ Eva hebu twende huku nikuonyeshe kitu” akasema Mathew wakaongozana na Eva hadi katika chumba fulani kilichoonekana kama chumba cha kulala .Kulikuwa na kitanda cha chuma na meza moja ndogo.

“Nisubiri hapa ninakuja” Mathew akatoka na baada ya dakika mbili akarejea .

“ Kuna nini humu Mathew? Hiki chumba ni cha nini? ” akauliza Eva lakini kabla hajajibiwa akajikuta amegeuzwa na kukabwa na kutahamaki akajikuta akiwa amefungwa pingu mkononi .alipojaribu kujitetea akapigwa kofi kali linalompeleka mpaka chini na mikono yenye nguvu ya Mathew ikamuinua na kumtupa kitandani na kuifunga pingu ile katika chuma cha kitanda.

“ You will stay here” akasema Mathew

“mathew !!!!!!!..akapiga ukelele Eva

“ Mathew nifungue tafadhali!!...

Mathew hakuzijali kelele zile akatoka na kufunga mlango kwa funguo

“Ninapokuwa katika shughuli nzito kama hizi huwa sina urafiki na mtu yeyote yule.” Akawaza Mathew kisha akaoka ndani ya kile chumba na kukifunga kwa funguo akaelekea sebuleni

“ Daktari kuna jambo moja naomba tuongee” akasema Mathew

“ Jambo gani kaka? akauliza daktari

“ Msichana huyu ana taarifa nyeti sana ambayo tunaihitaji kwa haraka .Ninataka umuamshe walau kwa dakika mbili tu atueleze mahala alipoweka kitu hcho tunachokitafuta”

“ Kaka hilo haliwezekani.Hakuna namna tunayoweza kufanya ili kumuamsha.Hali yake si nzuri hata kidogo na amedhoofu sana.Ninakushauri tuendelee kusubiri hadi hapo atakapopata nafuu.Bila hivyo hakuna namna nyingine ya kufanya ili kuweza kumuamsha “akasema daktari.Mathew akatoka pale sebuleni akaelekea chumbani kwake na baada ya dakika tatu akarejea akiwa na kichupa cha dawa

“ Daktari mchome dawa hii na ataamka” akasema Mathew na kumpatia yule daktari kile kichupa cha dawa ambaye alibaki anashangaa

“Unashangaa nini ? Fanya nilivyokwambia” akasema Mathew.Daktari yule akakichukua kile kichupa cha dawa akakisoma halafu akamgeukia Mathew

“ Hapana siwezi kumchoma mgonjwa kama huyu hii dawa.Ni hatari sana.Umeitoa wapi kwanza? Akauliza yule daktari kwa mshangao

“ Daktari tafadhali usitake kufahamu nimeitoa wapi lakini fanya ninavyokueleza ufanye” akasema Mathew kwa ukali

“ Hapana siwezi kufanya hivyo” akasema yule Daktari.Mathew akakasirika sana

“ Siku zote huwa sitaki mtu yeyote anikwamishe katika kazi yangu” akawaza na kwa kasi ya ajabu akaichomoa bastora na kumuelekezea yule daktari.

“ Sitaki mabishano na wewe tena .Usiku huu tayari nimekwisha ua watu wanne kwa hiyo nihesabu mpaka tatu na kama ukikaidi basi nitakifumua kichwa chako kwa risasi..One…” akasema Mathew

“ two”…akasema huku bastora yake ikiwa imeelekezwa kwa daktari

“ Ok kaka ntafanya unavyotaka lakini naomba ufahamu kwamba ni hatari sana kufanya hivi na mgonjwa anaweza akapoteza hata maisha”

“ Go ahead do it” akasema Mathew.

Daktari akachukua dawa na kuivuta katika bomba halafu akamchoma Sabina.Baada ya dakika kama mbili hivi Sabina akafumbua macho.Mathew akasogea pale kitandani

“ Sabina,Sabina..!! akaita Mathew Sabina akamtazama halafu akafumba macho

“ Sabina ! Sabina ! akaita tena Mathew na Sabina akafumbua macho na kumtazama Mathew na kisha akaitika kwa sauti dhaifu

“ Sabina usihofu uko katika mikono salama,tumekuokoa kutoka katika mikono ya wale jamaa waliokuwa wamekuteka.Usihofu uko huru sasa” akasema Mathew

“ Niko wapi? Akauliza Sabina kwa sauti ndogo

“ Uko sehemu salama.Sabina naomba uniambie umeuficha wapi mzigo uliopewa na mzee Kitwana? Akauliza Mathew

“ Siufahamu mzigo.wo..w..”

akasema Sabina

“ Ouh my gosh this is not going to work” akawaza Mathew halafu akatoka mbio na kuelekea katika chumba alichomfungia Eva akafungua mlango na kumkuta Eva amejilaza kitandani

“ Eva,Eva..! akaita Mathew Eva akamtazama kwa macho makali

“ Eva listen to me” akasema Mathew

“Go away Mathew..You are a monster’ akasema Eva

“ Eva naomba unisikilize.Sabina ameamka.Ni wewe tu ambaye anaweza akakueleza mahala alipouweka mzigo aliopewa na mzee Kitwana.Hatuna muda mrefu.Tafadhali naomba twende ukaongee naye.This is very important”akasema Mathew huku akimfungua Eva na kumshika mkono wakaongozana hadi sebuleni.Eva akamunamia Sabina

“ Sabina..Sabina ! akaita Eva.Sabina akafumbua macho na kumtazama Eva akamtambua

“ Eva..! Umekuja…Niko wapi hapa? akasema Sabina kwa sauti dhaifu

“ Sabina naomba unisikilize.Tumekuokoa kule ulikokuwa.Uko sehemu salama.Naomba uniambie ule mzigo uliopewa na mzee Kitwana uko wapi? Akauliza Eva lakini Sabina hakujibu kitu akafumba macho.Eva akamtikingisha

“ Sabina tafadhali naomba uniambie.Mzigo uleuko wapi? Sabina akamfanyia ishara amuinamie.Eva akamuinamia Sabina akamnong’oneza kitu sikioni halafu Eva akainuka

“ Anasemaje? Mzigo uko wapi?akauliza Mathew

“ Amenielekeza mzigo huo ulipo.Ameuficha kwa bibi yake amesema nikauchukue niufiche.”

“ Ok good.Hatuna muda wa kupoteza.Tunakwenda sasa hivi kwenda kuuchukua mzigo huo kwa bibi yake.” Akasema Mathew halafu akaelekea katika chumba alimo Anitha

“ Anitha tumekwisha fahamu mahala Sabina alikouficha mzigo.Tunakwenda kuuchukua wewe utabaki hapa na kuangalia nyumba kwani Noah hayupo.Hatutakawia sana.Ukipata chochote utanifahamisha kwa simu”akasema Mathew na kurejea sebuleni

“ Eva tunaongozana wote kwenda huko alikokuelekeza “ akasema Mathew

“ Hapana siongozani nawe Mathew.Nitabaki hapa kumuangalia Sabina.” Akasema Eva

“ Eva hili si ombi.Hii ni amri.’ Akasema Mathew .Eva tayari alikwisha muogopa Mathew kwa hiyo hakuweza kukataa.

“ Nadhani na mimi nimekwisha maliza kazi yangu .Ninaondoka pia” akasema yule daktari ambaye kijasho kilikuwa kinamtoka.Kitendo cha kunyooshewa bastora na Mathew kilimuogopesha mno

“ No ! Utabaki hapa hadi tutakaporudi.Endelea kumuangalia mgonjwa na hakikisha amepata nafuu” akasema Mathew kwa ukali

“ Huyu mgonjwa hali yake si nzuri na sitaki apoteze maisha katika mikono yangu”

“ Nimekwambia utamuhudumia na utahakikisha anakuwa salama .Ukikaidi maagizo yangu hautatoka salama ndani ya nyumba hii” akasema Mathew na daktari yule hakuwa na la kusema zaidi ya kukubaliana na matakwa ya Mathew.

Mathew na Eva wakaingia garini na kuondoka

“ Mathew you are a monster.Sikutegemea hata siku moja kama unaweza ukafanya kitu kama kile.Sikutegemea kama unaweza ukawa mkatili namna hii” akasema Eva wakiwa garini

“ Ni kwa sababu hujawahi kunikuta nikiwa kazini.Ninapokuwa kazini huwa si yuleMathew unayemfahamu” akasema Mathew

“ Pamoja na hayo Mathew kwa nini ufanye vile kwa binti yule ambaye hana kosa lolote? Nimeumia sana naomba ulifahamu hilo and I’ll never trust you again”

“ Sabina ana kitu muhimu ambacho tunakihitaji kwa hiyo lazima itumike kila mbinu kukipata.kazi zetu ndivyo zilivyo.Wewe ulitaka nikusaidie kumkomboa na nimefanya hivyo kwa hiyo kwa sasa ninaendel ea na shughuli zangu.” Akasema Mathew



*******



Dr Kigomba aliwaacha Flaviana na ndugu zake wakiwa nje ya jengo la kuhifadhia maiti akasogea pembeni mahala kusikokuwa na watu akachukua simu yakena kumpigia Dr Joshua.

“ Nipe ripoti Kigomba.Ni mwenyewe ? akauliza Dr Joshua

“No Mr president.Its not him”akasema Kigomba .Dr Joshua akavuta pumzi ndefu.

“ Now its going to get ugly” akasema Dr Joshua.Kimya kifupi kikapita akasema

“ You’ve failed me once again Dr Kigomba.Kutoka na kukosa umakini katika kazi sasa inatubidi tuongie tena katika kazi nyingine ya kuanza kumtafuta Elibariki”

“ mzee hili suala la kunilaumu mimi.Kila kitu kilikwenda kutokana na mipango namna tulivyokuwa tumeipanga kwa hiyo kushindwa kufanikiwa si kwa uzembe”

“ Kigomba rudi haraka hapa tulijaridi suala hili .Hatuwezi kuongea simuni suala zito kama hili” akasema Dr Joshua

“ Ok mzee tunarudi sasa hivi” akasema dr Kigomba na kuwataka akina Flaviana waingie garini waondoke

“ Ninahisi kama akili yangu haifanyi kazi tena” akawaza Flavian akiwa garini

“ Kabla hata mama hajazikwa linatokea tena jambo lingine.Nani waliomshambulia mume wangu? Elibariki yuko wapi? Akaendelea kujiuliza maswali mengi

“ Yule mtu aliyekuwa na gari la Elibaiki ni nani ? Ouh Mungu wangu naomba unisaidie naona akili yangu imefika mwisho wake na kufikiri.Kichwa changu kimejaa maswali mengi ambayo hayana majibu.Tukio zima la kushambuliwa gari la mume wangu linachanganya sana na sijui ni wapi nitapata majibu ya kweli kuhusiana nini kilitokea na mume wangu yuko wapi ” akaendelea kuwaza Flaviana

Aliwaza mambo mengi sana na namna ambavyo wamekuwa wakigombana na mume wake machozi yakaendelea kumtiririka.

“ Sijui nitafanya nini endapo Elibariki atakuwa amekufa.Japokuwa tumekuwa tukilumbana mara kwa mara lakini toka ndani ya moyo wangu ninampenda sana Elibariki.Sijui maisha yangu yatakuwaje bila yeye.” Machozi mengi yakaendelea kumtoka ,Anna akajitahidi kumtuliza

“ lakini nini dhana ya shambulio lile? Ni mume wangu ndiye aliyekuwa akilengwa kuuawa? Kama ni hivyo ni nani basi waliotaka kumuua na kwa nini ? Kikubwa zaidi ninachotaka kukifahamu sasa hivi mume wangu yuko wapi , is he ok? Flaviana akaendelea kujiuliza maswali yaliyokosa majibu

“ Itamlazimu baba atumie vyombo vyake kumtafuta mume wangu na tujue yuko wapi na kama yuko hai ama vipi.Ninapatwa na wasiwasi sana kuhusiana na maisha ya mume wangu.” Akawaza Flaviana

Walirejea nyumbani na bila kupoteza muda Flaviana akamuomba baba yake waongee katika chumba cha maongezi ya faragha.

“ Baba ,mtu aliyeuawa ndani ya gari la mumwe wangu si Elibariki.Inasikitisha sana kwa namna walivyomchakaza kwa risasi .Wamemuua kinyama sana.Watu waliofanya shambulio lile wana roho za kishetani.Ninachohitaji kufahamu hivi sasa ni mahala alipo mume wangu.Dady nina wasi wasi sana na maisha ya Elibariki na sijui mahala aliko.Ni vigumu kuamini kwamba Elibariki hakuwemo ndani ya ile gari kwa sababu nimeongea naye mimi usiku huu na nusu saa baadae gari lake linashambuliwa.Baba nina wasi wasi sana na usalama wa maisha ya Elibariki”akasema Flaviana

“ Flaviana mstuko ulioupata hata mimi umenipata pia.Tukio hili limenistua sana lakini kitu cha kutia faraja ni kwamba hajakutwa ndani ya hilo gari .Kwa maana hiyo basi tuna uhakika kwamba atakuwa hai .Tunachotakiwa kufanya kwa sasa ni kumtafuta mahala aliko.Nina hakika kuna sehemu yupo na kama amepata taarifa kwamba gari lile limeshambuliwa basi anaweza asijitokeze mapema.Kazi anayoifanya mumeo inamfanya awe na maadui wengi ambao hawaridhishwi na hukumu anazozitoa kwa hiyo matukio kama haya kwa majaji ni kitu cha kawaida na ndiyo maana huwa tunawapatia ulinzi lakini nashangaa yeye Elibariki anaendesha gari lake mwenyewe bila ulinzi na wala bila dereva.Ninachokuomba kwa sasa kaa, tulia na uniachie mimi kazi hiyo.Sina wasi wasi kabisa kwamba Elibariki atakuwa amekufa.Lazima yuko mahala na vyombo vyangu vitafanya kazi ya kumtafuta tutampata tu.” Akasema Dr Joshua

“ Baba nitawezaje kukaa wakati sifahamu mume wangu aliko? Kwa nini mambo haya yanatutokea sasa ? kabla hatujamaliza hili linaibuka hili.Kwa nini dady?akauliza Flaviana

“ Flaviana ninakuhakikishia kwamba nitatumia vyombo vyote vya usalama unavyovifahamu kumtafuta mumeo kuwatafuta watu waliofanya kitendo kile.Nakuhakikishia kwamba hakuna ambaye ameshiriki katika shambulio lile atabaki huru.Lazima wote wapitiwe na mkono wa sheria.” Akasema Dr Joshua na kidogo Flaviana akapata faraja .

“ Dr Kigomba amefanya uzembemkubwa sana.Suala lile halikuwa la kuchukulia kirahisi rahisi kama alivyolichukulia.Kwa sasa amesababisha tatizo jingine kubwa.Ametupa tena kazi ya kumsaka Elibariki na kufahamu mahala aliko.Elibariki anaufahamu ukweli wa nini kilimuua Flora na tukio la leo litamfanya aamini kabisa kwamba anatafutwa auawe kutokana na kuufahamu ukweli. Kigomba ndiye aliyesababisha haya yote.” Akawaza Dr Joshua akiwa amekasirika sana

“ lakini inawezekanaje Elibarik i asiwemo ndani ya hilo gari ? Kuna mtu alimpa taarifa? Na huyo mtu ambaye alikuwa akipambana na vijana wetu ni nani? Akajuliza Dr Joshua

“ hapa lazima kuna jambo linaloendelea.Lazima ufanyike uchunguzi wa kina kubaini ni kitu gani ambacho kinaendelea.hainiingii akilini kwamba Elibariki asiwemo ndani ya gari wakati vijana wamemfuatilia toka alipotoka hapa.Kama hakuwemo ndani ya gari yuko wapi? Uchunguzi wa kina unahitajika katika jambo hili.” Akawaza Dr Joshua



http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Dr Joshua aliitisha kikao cha dharura na washirika wake wakubwa Dr Kigomba na Captain Amos lengo likiwa ni kujadili kile kilichotokea usiku ule..

“ Jamani nimewaiteni hapa kwa dharura ili tujadili jambo lililotokea usiku huu.Kama mnavyofahamu mambo yameanza kwenda tofauti na matarajio.Mpango wetu haukuenda kama tulivyokusudia na hii ni kwa sababu ya kukosekana kwa umakini na usimamizi madhubuti .Makosa mengi yamefanyika ambayo sasa yanatulazimisha kufanya kazi ya ziada kuyarekebisha.Niliwataarifu toka awali kwamba Elibariki ni mtu hatari sana kwetu kwa sababu tayari amekwisha nusa harufu ya kinachoendelea hapa.Amekwisha fahamu sababu ya kifo cha Flora kiyu ambachohakutakiwa mtu yeyote kukifahamu .Japokuwa tumefanikiwa kuonyesha kwamba taarifa yake haikuwa na ukweli wowote ndani yake lakini bado ni mtu hatari sana kwetu.Suluhisho peke e lilikuwa ni kuwahi kummaliza lakini kumefanyika uzembe mkubwa katika mpango huo na kushindwa kufanikiwa.” Akasema Dr Joshua

“ Shambulio limefanyika lakini amekufa mtu mwingine kabisa tofauti na mtu tuliyekuwa tunamtaka.Sijawaita hapa ili kulaumiana kwa kilichotokea lakini nimewaita hapa ili kutafuta namna ya kusahihisha makosa yaliyofanyika.Elibariki bado yuko hai na amejificha mahala.Tunatakiwa tumtafute kwa kila njia hadi apatikane.Lakini kabla ya hapo kuna maswali kadhaa ambayo lazima tuyatafutie majibu.Kwanza ni kwa nini Elibariki hakuwemo ndani ya gari lake? Ni nani aliyekuwa akishambuliana na vijana wetu ? Je ni Elibariki mwenyewe au kuna mtu wingine? Kama ni mtu mwingine ni nani? Amewafahamuje vijana wetu? Haya nimaswali ambayo Lazima tupate majibu yake..Nina wasi wasi sana yawezekana kukawa na kuvuja kwa siri na ndiyo maana Elibariki akaponyoka kwa sababu hainiingii akilini ni kwanini hakuwemo ndani ya gari lake wakati vijana walikuwa na uhakika kabisa kwamba ameingia ndani ya gari lake.” Akasema Dr Joshua

“ Mzee ninaweza kukubaliana nawe kwa sababu nimezungumza na mtu ambaye alikuwa akimfuatilia toka ameingia hapa usiku huu alisema kwamba alifika hapa na kuonana na mkewe wakaelekea bustanini wakaongea halafu akaelekea katika gari lake na kabla ya kupanda katika gari aliongea kwanza na simu na baada ya muda akaingia katika gari lake na kuondoka.Kwa mujibu kijaa huyo ni kwamba elibariki si aliyekuwa akiendesha hilo gari.Kulikuwa na mtu aliyekuwa anaendesha na ninadhani ndiye aliyekutwa amekufa.Ina shangaza sana namna alivyonusurika .Nina wasiwasi yawezekana kweli kuna uvujaji wa siri zetu.” Akasema Dr Kigomba

“ Kigomba lifanyie kazi hilo suala haraka iwezekanavyo.Tunatakiwa tufahamu kama kuna uvujaji wowote wa taarifa zetu.Vijana wetu wanatakiwa wachunguzwe kama kuna mmoja kati yao ambaye anatoa siri zetu nje.Hili ni jambo la haraka sana kulifanya vinginevyo mipango yetu yote itakawama na juhudi zote za miaka mingi zitakuwa kazi bure.Hatutaweza kuupata utajiri ule ambao tunatarajia kuupata endapo hakutakuwa na juhudi za makusudi za kuhakikisha suala hili linafika mwisho.Ndugu zangu tumeshughulika na suala hili kwa miaka mingi na tunaelekea ukingoni kwa hiyo tukifanya mchezo tunaweza kushindwa kulimaliza salama na mkumbuke kwamba endapo tukishindiwa kulimaliza salama basi ndio utakuwa mwisho wetu.” Akasema Dr Joshua

“ Ni kweli Dr Joshua kumeanza kuonekana vizingiti hasa katika hatua hizi za mwishoni.Mwanzo tulianza vizuri sana lakini baada tu ya Dr Flora kuingia na kifahamu suala lile mambo yalianza kwenda ndivyo sivyo.”akasema Captan amos.Dr Joshua akadakia

“ Usiwe na shaka kuhusu Flora .Nina hakika hakumweleza mtu yeyote.lakini alitaka kuwaeleza watoto wake ndipo tukamuwahi.Nina hakika ulimi wake haukuwahi kutamka chochote kuhusiana na jambo hili.”

“ Dr Joshua nitalisimamia suala hili la uchunguzi na nitahakikisha kila kitu kinakwenda kama ulivyoagiza.Pamoja na hayo kuna kitu Fulani ambacho ninataka kukushauri”

“ Ni kitu gani hicho Kigomba? Akauliza Dr Joshua

“ Njia nyepesi ya kumpata Elibariki kwa haraka ni kuelekeza macho yetu kwa mke wake .Nina hakika lazima atawasiliana naye na atamuelekeza mahala alipo .Flaviana ni njia rahisi sana kwetu ya kumpata Elibariki”

“ Kigomba ,tayari mmekwisha unganisha simu ya Flaviana na mnaweza mkafuatilia kila atakachoongea simuni inatosha sana lakini kama unaona kuna ulazima wa kumfuatilia basi fanya hivyo kwani kwa sasa chochote kinachoweza kutusaidia hatutakiwi kukipuuza.” Akasema Dr Joshua.

“ Sawa nimekuelewa mzee.”

“ Nataka mpaka kesho jioni nitakaporejea toka katika mazishi tayari muwe na majibu ya mambo haya niliyowaelekeza.Sitaki tena majibu ya kisisa.Ninataka matokeo mazuri” akasema Dr Joshua

“ Tumekuelewa mzee.Tutajitahidi kufanya kama ulivyotuelekeza” akasema Dr Kigomba

“ Sijui ni kwa nini kumeanza kutokea vizingiti katika hatua za mwishoni kabisa za mpango wetu.Lakini hakuna kitakachoharibika ,lazima kila kitu kitakwenda kama kinavyotakiwa.Tukishampata Elibariki roho yangu itakuwa imetulia lakini vinginevyo sintakuwa na amani kabisa.Bado naendelea kujiuliza ameponaje katika shambulio lile? Nina hakika asilimia mia moja kwamba lazima kuna mtu ambaye alimpa taarifa za kuwepo kwa shambulio .Lakini hata kama alipewa taarifa mbona vijana wetu hawakumuona akishuka sehemu yoyote toka alipotoka hapa? Alitowekaje ndani ya gari? Akajiuliza Dr Joshua baada ya akina Kigomba na Amos kuondoka



*******



Osmund alitoka ofisi kuu ya Team SC 41 akachoma mafuta hadi nyumbani kwa John Mwaulaya.Akafululiza hadi chumbani kwa John ambaye hali yake kidogo ilikuwa umeimarika

“ Hallo John” akasema Osmund

“ habari yako Ossy. Sijakuona toka asubuhi ya leo.Ulikuwa wapi?

“ John nilikuwa na mizunguko mingi sana siku ya leo.Unaendeleaje?

“Ninaendelea vizuri sana.Nyie mnaendelaje?

“ Tunaendelea vizuri .Nimeongeana mkuu toka Marekani na anakupa pole sana ila amesema kwamba anasubiri taarifa ya Dr Burke ili aweze kujua ni namna gani ya kuutibu ugonjwa wako” akasema Osmund

“ Hakusema kitu kingine? Akauliza John

“ Alikupa pole nyingi.Vile vile nimeongea na Peniela na amesema kwamba anahitaji kukuona” akasema Osmund

“ Ana matatizo gani? akauliza John

“ Hakuniambia ana matatizo gani ila alisema kwamba ni suala binafsi”

Kimya kikapita Osmund akimtazama John mwaulaya.

“ Mtaarifu kwamba nitaonana naye kesho jioni”akasema John

“ Sawa mzee” akasema Osmund akiendelea kumkodolea macho John

“ Mbona unanitazama hivyo Osmund ? Kuna kitu unataka kuniambia? Unataka kuniambia kuhusu vifo vya vijana wetu sita ? Akauliza John na kumstua sana Osmund.Hakuwa ametegemea kama John tayari anafahamu kuhusiana na vifo vile.

“ Osmund kwa nini ukanificha kuhusiana na tukio hilo? Akauliza John

“ Ulipaswa kuja kwangu na kunieleza kila kitu kuhusiana na kilichotokea .Kwa nini hukutaka ushauri wangu ? Ulifikiri kwamba sintajua kilichotokea ? Osmund usidhani kwamba kwa vile niko kitandani sijiwezi basi sina nafasi tena katika Team Sc41.Mimi bado ni mkuu wa Team SC41.Nimeianzisha mimi na ninaifahamu vizuri kuliko yeyote kati yenu kwa hiyo kabla ya kufanya jambo lolote unapaswa kwanza kuja kwangu na kunitaarifu ili nikupe ushauri.Mwili wangu hauna nguvu lakini kichwa change bado kina uwezo mkubwa wa kuongoza” Akasema John

“ John sikukueleza kutokana na haliyako lakini hupaswi kunilaumu John kwa kilichotokea kwa sababu nilifanya kila kitu kwa sababu yako.Kama isingekuwa ni kwa sababu ya ugonjwa wako nisingemteka mke wa yule daktari,”

“ Hukupaswa kufanya vile.Team SC 41 si kikundi cha watekaji.Si kikundi cha mapigano.Ungejua athari ya kitu ulichokifanya usingesimama hapa ndani na kusema kwamba ulifanya kwa ajili yangu.” Akasema John.Osmund akakaa kimya kwa muda kisha akasema

“ Dr Burke anakuja kesho kujakuona afya yako na ndiye atakayetoa mapendekezo ya namna ya kukutibu” akasema Osmund.

“ Thank you” akasema John

“ Anything you need John?

“ Nothing.Just leave me alone” akasema John.Osmund akamuangalia na na kutoka

“ Peniela ana matatizo gani? Kwa nini anataka kuniona? Akajiuliza John baada ya Osmund kutoka

“ Inawezekana kuna jambo linamsumbua hadi akataka kuja kuniona? Ninajua ana hamu sana ya kukaa name na kuongea name.Ana mambo mengi ambayo anataka kuyafahamu toka kwangu na mimi pia nina mambo mengi sana ambayo ninatamani kumweleza lakini ninashindwa namna ya kumwambia. Natamani afahamu kuhusu wazazi wake lakini sijui atanielewaje endapo nitamwambia kwamba ni mimi ndiye niliyewaua wazazi wake.Kuna mambo mengi ambayo anatakiwa ayafahamu Peniela lakini ninashindwa namna ya kumfahamisha.” Akawaza John baada ya Osmund kutoka mle chumbani

“ Laiti kama ningekuwa nina uhakika wa kuishi kwa muda mrefu kutokana na ugonjwa huu unaonisumbua ningemfanyia Peniela mambo makubwa kufidia maumivu mengi niliyomsababishia katika maisha yake,kufidia maisha yake niliyoyaharibu kwa kumuingiza katika team SC41.Ingawa bado sijachelewa sana lakini kuna mambo ambayo nikiyakumbuka kuhusu Peniela huwa yananiumza sana.Kubwa ambalo nina hakika endapo atalifahamu atakasirika sana ni kitendo cha kumuua mvulana wake wa kwanza Peter mtoto wa tajiri mmoja mkubwa hapa nchini.Mahusiano yao yalianza wakati Peniela akiwa kidato cha pili .Sikutaka Peniela awe na mahusiano ya kimapenzi kwa sababu nilikuwa na mipango tayari ya kuja kumtumia katika shughuli muhimu za Team SC41.Peniela aliumia sana kwa kifo cha Peter .Japokuwa ni muda mrefu umepita lakini bado naikumbuka siku ile .” akawaza John na kufumba macho akavuta kumbu kumbu

Ni siku ya jumamosi wanafunzi sita wa shule ya sekondari ya Hope Secondary ,shule ambayo wengi wa watoto wanaosoma hapa ni wenye uwezo mkubwa kifedha, wakiwa katika magari matatu waliamua kutoka na kwenda matembezini nje kidogo ya jiji.Kila mmoja alikuwa na mpenzi wake na walionekana kuifurahia sana safari yao.Hawakujua kama nyuma yao kulikuwa na gari inawafuatilia kila sehemu waliyokwenda.

Wanafunzi wale walifika mahala kulikokuwa na uwanda mpana wa majani mazuri wakatoa vitu walivyokuwa wamebebea kama vile vinywaji na kuanza kuburudika kila mmoja na mpenzi wake.Wakati wakiendelea na burudani yao wakiwa hawana wasi wasi wowote ghafla wakavamiwa na mtu aliyekuwa amejificha uso wake na akawalazimisha wote walale chini.Mtu yule aliyekuwa na akamuamuru Peter asimame na kumpigisha magoti mbele ya wenzake na kisha akaanza kumiminia risasi yule kijana alifariki pale pale.Yalikuwa ni mauaji ya kutisha ambayo Peniela aliyashuhudia kwa mara ya kwanza katika maisha yake.

Kumbu kumbu ile limfanya John Mwaulaya ahisi kama kuna kitu kikali kinaukata moyowake.

“ kwa nini nlikuwa mkatili namna hii ? Nilitoa uhai wa watu wengi wasio na hatia na sikujua kama siku moja na mimi nitakinusa kifo.Death is so scary “ akawaza John

*****

Mathew na Eva walisimamisha gari katika baa moja maarufu ijulikanayo kama mkombozi.

“ kwa mujibu wa Sabina ni kwamba nyuma ya baa hii kuna nyumba ya bibi yake ina vyumba vinne na kuna kilabu cha pombe za kienyeji.Alisema nimuulizie bibi Mariana.” Akasema Eva wakashuka ndani ya gari na kuzunguka nyuma ya ile baa ya mkombozi ni kweli kulikuwa na kilabu cha pombe za kienyeji na kulikuwa na idadi kubwa ya watu.Eva akamfuata mama mmoja na kumuuliza kama anaweza kumpata bibi Mariana akaelekezwa kwamba ni yule aliyekuwa akiuza pombe.Akamfuata na kumsalimu akamuomba waongee pembeni.

“ Bibi samahani kwa kukusumbua katika biashara “ akasema Eva

“ Bila samahani mwanangu.” Akasema Bibi Mariana

“ Nimekuja hapa nimeagizwa na Sabina”

“ Sabina? Bi Mariana akastuka

“ Ndiyo bibi”

“ Yuko wapi huyu mjukuu wangu? Ni muda mrefu sijamuona na hajafika hapa kwangu.”

“Bibi Sabina yuko safari .Ni rafiki yangu tulikuwa wote safari nje ya mkoa .Kuna biashara Fulani tunafanya wote na mimi nimerudi mara moja kuja kuchukua mzigo na ninaondoka kesho asubuhi sana na ndiyo maana imenilazimu kuja hapa kwako usiku huu” akasema Eva

“ Wala usijali mwanangu.Haka kajukuu kangu hakajambo?

“Sabina mzima kabisa bibi,anaendelea vizuri”akasema Eva

“ Nashukuru kama anaendelea vizuri” akasema bibi Mariana

“ Bibi Sabina amenituma nikuletee mzigo huu hapa” akasema Eva na kufungua pochi yake akatoa bunda la noti na kumpatia.

“ ouh Mungu wangu ahsante sana.Mungu awabariki sana na awazidishie mafanikio” akasema Bi Mariana

“ Amina bibi.Halafu pia amenituma kwamba unipe ule mzigo wake niende nao”

“ Sawa mwanangu ngoja nikakuletee sasa hivi .” akasema Bi Marina na kuingia ndani .Alikuwa nafuraha ya ajabu kwa kupewa bunda lile la noti.Mathew alikuwa amesimama mbali kidogo na hakutaka kuwasogelea

Baada ya kama dakika kumi hivi Bi Mariana na kurejea akiwa na mfuko wa nailon

“ Samahani kwa kuchelewa unajua mzigo wenyewe nilikuwa nimeuficha mbali kwa sababu alisema kwamba niufiche mbali “

“ Ahsante sana bibi nashukuru”

“ Hata mimi nashukuru mjukuu wangu.Msalimu sana Sabina mwambie mzigo nimeupokea na ninashukuru sana” akasema Bi Mariana akaagana na Eva akaondoka ,

“Mzigo huu hapa “ akasema Eva akimkabidhi Mathew mzigo ule.Walipofika garini Mathew akaufungua .Kulikuwa na kiboksi chenye ukubwa wa karatasi ya barua lakini kilikuwa cha chuma na kilikuwa kimefungwa kwa ufunguo .

“ hakukupa ufunguo wa kiboksi hiki?akauliza Mathew

“ Hapana hakunipa”akajibu Eva

“ Ok nitakwenda kukifungulia nyumbani.Ahsante sana Eva Umenisaidia sana” akasema Mathew na kuwasha gari wakaondoka

“Mathew wewe ni rafiki yangu na umenisaidia mambo mengi sana lakini naomba nikueleze ukweli kwamba sijafurahishwa hata kidogo na kitendo ulichokifanya leo kwa Sabina.Ule si ubinadamu hata kidogo” akasema Eva huku akionekana bado amekasirika

“ Eva,kama nilivyokwamba awali kwamba kazi yangu wakati mwingine inahitaji kufanya maamuzi magumu ili kufanikisha baadhi ya mambo.Maamuzi magumu niliyoyafanya yametusaidia tumeweza kukipata kitu ambacho ni cha muhimu sana.Jifunze kufanya maamuzi magumu katika kazi zako” akasema Mathew

“ Mathew achana na maneno hayo ya wanasiasa .Maamuzi magumu katika kuhatarisha uhai wa mtu? Unajua ni kiasi gani umehatarisha uhai wa Sabina kwa ajili ya hiki kiboksi tu? Akasema Eva.Mathew akamtazama na kusema

“ Unajua ni watu wangapi wamepoteza uhai wao kwa sababu tu ya hiki unachokidharau? Akauliza Mathew na hawakuendelea tena na maongezi .Wakati safari ikiendelea kimya kimya Anitha akapiga simu

“ Hallow anitha “ akasema Mathew

“ Mathew nimefankiwa kupata taarifa za Habid soud.Huyu ni mtoto wa tajiri mmoja mkubwa nchini Saudi Arabia anayemiliki visima vya mafuta.Habib soud anatajwa kama mmoja wa vijana wenye mafanikio makubwa sana nchini mwao.Hizo ndizo taarifa zake ambazo nimezipata lakini ninaendelea kumchimba zaidi ili niweze kuzipata taarifa zake za kina”

“ Good Job anitha.Niko njiani ninakuja .Noah amekwisha rejea?

“Hapana bado hajarejea. Umefanikiwa kuupata ule mzigo?

“ Ndiyo nimefanikiwa kuupata” akasema Mathew

“ Good job Mathew” akasema Anitha na kukata simu

Eva bado aliendelea kuonyesha kukasirika na hakutaka maongezi tena na Mathew

“ Eva najua umekasirika sana lakini nakuomba usifanye hivyo.Kazi yangu inanilizimu kufanya vile nilivyofanya” akasema Mathew

“ Nikifika sasa hivi kama Sabina yuko bado hai basi nitaondoka naye.Sitaki aendelee tena kukaa pale kwako” akasema Eva

“ Usijalie Eva.kwa sasa sina haja naye tena.Unaweza ukamchukua” akasema Mathew

Walifika nyumbani kwa Mathew na kuingia ndani.

“ Vipi hali ya mgonjwa? Mathew akauliza

“ Amepoteza fahamu tena” akasema Daktari.Eva akamuangalia Mathew kwa jicho la ukali.

“ Vipimo vinaonyeshaje?

“ Mapigo ya moyo yako juu sana isivyo kawaida na hii ni hatari sana” akasema daktari

“ Dr Evarist can we save her” akauliza eva

“ yes we stili have a chance lakini si hapa inabidi tumkimbize hospitali” akasema Dr Evarist

“ Lets go,we’re getting gher out of here” akasema Eva.Daktari akamgeukia Mathew akamtazama kana kwamba alikuwa anataka asike naye anasema nini

“ yah you can get her out of here” akasema Mathew na kusaidiana na Daktari wakambeba Sabina wakamuingiza katika gari ,Mathew akamuamuru yule msichana mwingine aliyekuwa mtumishi wa ndani aongozane na akina Eva kwani hakuwa akimuhitaji tena

“ Noah karudi ? akauliza Mathew

“ Hapana bado.Inawezekana kuna mahala wamepita” akasema Anitha

“ Ok good muache asafishe macho na yule jamaa mwingine anaendeleaje?

“ Amepewa dawa amelala”

“ Ok good.Kuna taarifa nyingine umezipata kuhusia na Habib?

“ bado ninaendelea kutafuta taarifa zake lakini hakuna taarifa zozote mbaya za kumuhusu yeye.Taarifa zake nyingi ni za utumiaji mbaya wa fedha ” Akasema Anitha

“ Ok keep searching.”akasema mathew

“Mmefanikiwa kupata kitu gani huko mlikotoka? Akauliza Anitha.Mathew akakitoa kile kiboksi katika ule mfuko akakiweka mezani

“A box? Anitha naye akashangaa

“Ndiyo ni huu mzigo ambao Sabina aliuficha kwa bibi yake

“ Watu wote hawa wamekufa kwa sababu ya hiki kiboksi? Akauliza Anitha

“ Hata mimi nilistuka kidogo lakini ngoja kwanza tukifungue tujue ndani yake kuna nini” akasema Mathew na kutoka ,halafu akarejea na kifaa cha kukatia chuma na kuanza kukikata kile kiboksi kwa kuwa hawakuwa na funguo.





Mahew na Anitha wote walionekana kuwa na shauku kubwa ya kutaka kufahamu ndani ya kile kiboksi kulikuwa na kitu gani.Alikikata kiungalifu sana ili asije haribu kilichokuwamo mle ndani.Baada ya kufanikiwa kukifungua wote wakapigwa na mshangao kwa walichokikuta ndani.Kulikuwa na bahasha.Akaitoa bahasha ile na kufungua ndani yake kulikuwa na karatasi nne ambazo zilionekana kuchorwa chorwa vitu kama vya kisayansi .Mathew na Anitha wakabaki wanaangaliana.



“ So what’s this? Akauliza Anitha baada ya kuziangalia karatasi zile na kushindwa kufahamu kilichokuwa kimeandikwa

“ Hata mimi sifahamu ni kitu gani hiki” akasema Mathew halafu akachukua tena zile karatasi akaanza kuziangalia



“ Zinaonekana ni kama formula za kisayansi lakini sina uhakika.” Akasema Mathew

“ Kwa hiyo listi yote ile ya watu wamekufa kwa sababu ya karatasi hizi? Akauliza Anitha

“Inashangaza sana lakini nina hakika lazima kuna kitu ndani ya karatasi hizi ambacho hatukifahamu na ndiyo maana kukawa na mlolongo wa vifo” akasema Mathew



“ Mathew nataka kukubaliana na wewe lakini ninasita.Ninahisi kuna kitu kingine walichokuwa wanahitaji kukiuza na si hizi karatasi.Hainiingii akilini kabisa kwamba karatasi hizi zisababishe idadi ile watu kuuawa.Edson,mpenzi wake brigita,mzee Matiku,mzee KItwana wote hawa wamekufa kwa sababu ya hizi karatasi? Ninahisi bado kuna kitu kingine kimefichwa ambacho tunatakiwa tukipate.” Akasema Anitha



“ Anitha mzigo huu tumeutoa kwa bibi yake Sabina ambao alikuwa ameuficha mbali.Sabina alipewa mzigo huu na mzee Kitwana kwamba aufiche.Nina hakika kuna kitu ndani ya karatasi hizi ambacho tunatakiwa tukifahamu.Usikate tama mapema” akasema Mathew

“Mathew una hakika kwamba hakuna kitu kingine tofauti na hizi karatasi? Unajua hainiingii akilini eti watu wote wale wafe kwa sababu tu ya hizi karatasi.Na ukumbuke kwamba hii ilikuwa ni biashara ambayo ilitakiwa kuwapatia watu hawa wote mamilioni ya fedha sasa ninashindwa kuamini kama karatasi hizi ndizo zingewaingizia watu wale millions of money.I think there is something else” akasema Anitha



“ Anitha Karatasi hizi ziliibwa toka ikulu na Edson na walipanga waziuze kwa mamilioni ya fedha kwa Habib Soud ambaye nilikwambia utafute taarifa zake .Kama ni hivyo lazima karatasi hizi zina kitu kizito ndani yake.Karatasi kama hivi kuuzwa kwa mamilioni ya fedha si kitu rahisi ,kwa hiyo basi tunachitakiwa kukifanya kwa sasa ni kujaribu kufahamu karatasi hizi ni za nini na umuhimu wake.” Akasema Mathew

“ Nani ambaye atatueleza kuhusiana na karatasi hizi? Mbona maandishi yake ni ya ajabu ajabu tu? Akauliza Anitha

“ Karatasi hizi zimeibwa toka ikulu na ili kufahamu ni za nini tunatakiwa kumpata mtu toka ndani ya Ikulu ambaye anaweza akatueleza kuhusu nini kilichomo ndani ya karatasi hizi.Zimeandikwa kisayansi sana na sisi si wanasayansi.Hakuna chochote tunachoweza kuambua ndani ya karatasi hizi” Akasema Mathew

“ Ni nani ndani ya ikulu ambaye anaweza akatusaidia Mathew? Huoni kwa kufanya hivyo tunaweza kuwa tunajitafutia matatizo mengine kwa sababu karatasi hizi zimeibwa toka ikulu?” Akasema Anitha.Mathew akafikiri kwa muda halafu akasema



“ Mr President”

“ President? Anitha akashangaa



“ Ndiyo ,tukimfuata na karatasi hizi anaweza akatusaidia kufahamu kilichomo ndani yake na umuhimu wake na kwa nini ziliibwa na kutaka kuuzwa kwa mamilioni ya fedha.Kama zimetoka ndaniya ikulu basi lazima atakuwa anafahamu ni za nini.Hakuna mwingine tunayeweza kumuanini zaidi yake” akasema Mathew



“ Kwa hiyo tutamueleza ukweli sisi ni akina nani ? akaulzia Anitha

“ Kama tubna nyaraka kama hii lazima tumueleze ukweli ili atuamini”

“ How can we meet with President? Akauliza Anitha

“ Through Elibariki.Yeye ni mkwe wake na atatusaidia sisi kuweza kuonana naye kwa urahisi.Jambo hili si la kuchelewa tunatakiwa tulifahamu vizuri na kwa haraka “ akasema Mathew na kuchukua simu yake akazitafuta namba za jaji Elibariki akapiga lakini simu ya jaji Elibariki haikuwa ikipatikana



“ Elibariki yuko wapi? Kwa nini ameizima simu yake? Akauliza Mathew



“ Nilikwambia yawezekana Noah akawa amemshawishi wakapitia sehemu Fulani kupooza koo si unajua tena Noah anavyopenda starehe” akasema Anitha



“ Ok ngoja tuwasubiri lakini ingekuwa vyema kama angewahi kuja ili tuweze kuongea naye kuhusiana na suala hili na atusadie kuweza kulipatia ufumbuzi ” Akasema Mathew na kuzishika tena zile karatasi akaanza kuziangalia



“ Dah ! pamoja na ufahamu wangu wa vitu vingi lakini kwa hili nimegonga mwamba.Nimeshindwa kuambua kitu chochote hapa.Namna vitu vilivyoandikwa andikwa inachanganya sana.” Akasema Mathew

“ Mathew unadhani labda inawezekana kuna kitu kinafichwa ndani ya maandishi haya ili kisijulikane? Yawezekana ni siri Fulani?

“ Kwa namna nilivyoziona hizi ni formula za kisayansi.Kuna mahesabu mengi ya kisayansi humu ndani kwa hiyo inatakiwa tumpate mtu ambaye anaweza akatufafanulia kuhusiana na formula hizi.Usijali Anitha tutafahamu tu ni kitu gani lakini lazima tujue kwamba kilichomo ndani ya karatasi hizi ni kitu kikubwa na ndiyo maana kimegharimu uhai wa watu.Na hata hivyo tunatak…………….” Mathew akakatishwa na simu yake ya mkononi iliyokuwa ikiita.Alikuwa ni Jason



“ Hallo Jason” akasema Mathew

“Mathew samahani kwa kuwasumbua mida hii lakini nataka kuwahamisha kuhusiana na shambulio lililotokea usiku huu”



“ Shambulio ? Mathew akastuka



“ Shambulio gani Jason?



“ Ina maana hamjapata taarifa zozote za kuhusiana na shambulio lililotokea? Akauliza Jason



“ Hapana hatuna taarifa zozote.Ni shambulio gani? akauliza Mathew kwa mshangao



“ Gari la jaji Elibariki limeshambuliwa na watu wasiojulikana usiku huu na inasemekana kuna tu ameuawa” akasema Jason.Taarifa zile zikamstua mno Mathew



“ Shambulio hilo limetokea saa ngapi?

“ Usiku huu Mathew na inasemekana kuna mtu mmoja ameuawa katika shambulio hilo”

“ Ouh my God ! “ akasema Mathew na kushindwa la kusema .Midomo yake ilikuwa inamcheza.



“ What happened Mathew? Akauliza Anitha.Mathew akashinda kuongea

“ C’mon Mathew tell me what happened? Akauliza Anitha



“ Elibariki ameshambuliwa na watu wasiojulikana” akasema Mathew huku sauti ikimtetemeka



“ Don’t tell me he’s dead” akasema Anitha na macho yake yalishindwa kuonyesha mstuko aliokuwa ameupata

“ Jason ! akaita Mathew

“ Mtu aliyekutwa amekufa ndani ya gari ni jaji Elibariki au ni nani ? Kwa sababu Elibariki alikuwa ameongozana na Noah usiku huu” Akauliza Mathew



“ Alikuwa na Noah? Akauliza Jason

“ Ndiyo alikuwa na Noah “ akajibu Mathew



“Mpaka sasa hakuna taarifa kamili kwamba aliyekutwa amekufa ndani ya gari hilo ni nani lakini taarifa zinadai kwamba ni mtu mmojandiye aliyekutwa amekufa.Hivi sasa ninaelekea katika hospitali kuu ya taifa kwa ajili ya kwenda kumtambua kama ni Elibariki ama vipi.” Akasema Mathew

“Jason ahsante sana hata sisi tunaelekea huko sasa hivi” akasema Mathew na kukata simu.Alihisi mwili wake kukosa nguvu

“ Jason anasemaje? Akauliza Anitha



“ Hakuna mpaka sasa taarifa kamili iliyotoka kama aliyekufa ni jaji Elibariki ama si yeye.Kwa sasa Jason anaelekea hospitali kuu ya Taifa ili kwenda kuutambua mwili wa mtu huyo aliyekutwa amekufa ndani ya gari la jaji Elibariki” akasema Mathew



“ Mathew I’m so scared.Elibariki alikuwa na Noah ndani ya gari.Una hakika Noah yuko salama? Akauliza Anitha



“ Siwezi kuwa na uhakika kama aliyefariki takuwa nani lakini lazima tujiandae kwa lolote.Tunaelekea hospitali tukathibitishe.” Akasema Mathew na kuingia chumbani kwake akabadili mavazi halafu wakaingia garini na kuanza safari ya kuelekea hospitali kuu ya taifa kwa ajili ya kwenda kuutambua mwili wa mtu aliyeuaa kwa risasi ndani ya gari la jaji Elibariki.

“ Mathew unadhani ni nani ambaye anaweza kuwa amefanya shambulio hili ? Akauliza Anitha kwa sauti yenye kitetemeshi.



“ hapana siwezi kujua kwa sasa.Ni vigumu kufahamu kwa sababu majaji huwa ni watu wenye maadui wengi.Inawezekana wakawa ni watu ambao hawakuridhishwa na mojawapo ya maamuzi yake kwa hiyo wakaamua kulipiza kisasi.”akasema Mathew ambaye alionekana kuwa na mawazo mengi sana.Anitha alikuwa ameifunga mikono yake na kuiweka kifuani akiomba kimoyo moyo.

“Mungu wangu ninaomba Noah awe mzima kwa sababu naye alikuwamo ndani ya gari la jaji Elibariki.”

Waliwasili katika hospitali kuu ya taifa na kuelekea moja kwa moja katika chumba cha kuhifadhia maiti .Nje ya jengo lile wakakutana na Jason ambaye tayari alikwisha fika

“ Jason tupe taarifa.Umefanikiwa kumtambua mtu huyo? Akauliza Mathew



“ Nimefanikiwa kumuona lakini si jaji Elibariki..” akasema Jason na huku akionekana kuogopa .Anitha alikuwa ameiweka mikono kichwani aliogopa sana.Mathew Anitha na Jason wakaingia ndani ya chumba cha maiti kwa ajili ya kuitambua maiti ya mtu Yule.Anitha akaanguka na kupoteza fahamu baada ya kugunudua kwamba mtu Yule aliyekuwa amefariki ni Noah.Mathew na Jason wakisaidiana na watu wengine waliokuwapo pale wakambeba na kumtoa nje kwa ajili ya kumsadia ili aweze kurejewa na fahamu zake.Alipatwa na mstuko mkubwa sana.Wakati Anitha akiendelea kupatiwa huduma ya kwanza Mathew alisogea pembeni akatoa kitambaa na kujifuta machozi.Aliumizwa sana na tukio lile.



“ Ni nani lakini aliyefanya jambo kama hili? Ni nani aliyemuua Noah? Akajiuliza huku machozi yakiendelea kumtoka



“ Masikini Noah amekufa bado kijana mdogo tu.Nitawaeleza nini familia yake? Bado Mathew aliendelea kuangusha machozi na mara akashikwa bega na Jason



“ Mathew ,Anitha ameamka” akasema Jason



“Jason I’m deeply hurt.Sijawahi kuumia namna hii kwa miaka mingi.Machozi ya mwisho niliyatoa wakati familia yangu ilipoteketea kwa moto lakini leo nimeshindwa kujizuia na kuangusha machozi.Nimeumia sana Jason kwa kifo hiki cha Noah.Nimemfahamu Noah kwa muda mrefu na ni mimi niliyemjenga hadi hapa alipofika.Nilimuita aje anisaidie katika kazi mliyotukabnidhiya kumtafuta muuaji wa Edson na sikjua kama nilikuwa namuita aje kufa.Laiti kama ningejua kijana Yule anakuja kufa wala nisingemuita aje anisaidie kazi” akasema Mathew na kushindwa kujizuia kudondosha chozi



“ Pole sana Mathew.Pole sana” akasema Jason



“ Ahsante sana Jason.Japokuwa kifo tumeumbiwa wanadamu lakini kwa kweli nimeumizwa mno na mauaji haya ya kikatili ya Noah.Sikutegenmea hata siku moja kama Noah angeweza kuawa kikatili namna hii” akasema Mathew kwa ucungu



“ Ilikuwaje Noah akawa katika gari la jaji Elibariki? Akauliza Jason.Mathew akafuta machozi na kusema

“ Noah alikuwa anajeraha katika mguu wake kwa hiyo tulimuacha nyumbani wakati sisi tukielekea katika kazi Fulani usiku huu.Wakati hatupo alifika Elibariki kwa kuwa nilihitaji kuonana naye usiku wa leo.Aliponikosa aliamua kuondoka na kwenda kuonana na mke wake halafu arejee.Alinipiga simu na kunitaarifu kwamba atarejea baada ya muda na anaongozana na Noah ambaye alisema kwamba anataka kwenda kuufanyisha mazoezi mguu wake na alikuwa ameboreka pale ndani peke yake.Ningejua kama anakwenda kufa wala nisingemruhusu aondoke pale nyumbani” akasema Mathew na kufuta machozi.Kikapita kimya cha sekunde kadhaa Jason akauliza



“ Jaji Elibariki yuko wapi? Si umesema kwamba walikuwa wote ndani ya gari? Akauliza Jason

“ Ni kweli walikuwa wote ndani ya gari lakini hata mimi sifahamu Elibariki yuko wapi “ akasema Mathew



“ Hili ni jambo la kushangaza sana kama walikua wote garini yeye yuko wapi? Kwa nini afariki Noah peke yake? Ina maana wakati shambulio hilo linafanyika Elibariki hakuwamo garini? Akauliza Jason



“ Jason jambo hili linashangaza sana.Hata mimi nashindwa kuelewa kwamba ndani ya hilo gari alikuwepo Noah peke yake? Kuna maswali mengi ya kujiuliza hapa lakini kwa sasa inatubidi tuachane kwanza na hayo ili tushughulikie suala la msiba wa Noah.Siwezi kufanya jambo lolote kwa sasa hadi kwanza akili yangu itakapotulia .Elibariki yuko wapi ,amekufa ama hajafa ni suala ambalo nitalishughulikia baadae.” Akasema Mathew ambaye ni wazi alionekana kuchanganyikiwa

“Sawa Mathew ,basi tuanze taratibu zinazotakiwa ili tuweze kukabidhiwa mwili wa Noah.Niachie mimi nitalishughulikia suala hili .Kwani Noah ni mtu wa wapi? Ndugu zake wako wapi?



“Kwa sasa familia yake inaishi jijini Harare Zimbabwe.Mama yake ni mtanzania na baba yake ni raia wa Zimbabwe.Nitafanya utaratibu wa kuwasiliana na familia yake na kuwataarifu kuhusiana na msiba huu na kwa pamoja tujadiliane namna ya kufanya kama Noah azikwe hapa Tanzania au asafiriswe kwenda Zimbabwe.” akasema Mathew



“ Sawa Mathew mimi nitalishughulikia suala hilo .Kwa sasa unaweza kwenda kupumzika mimi nitalishuhulikia jambo hili kwa sababu lina taratibu zake na nitakupa majibu kesho asubuhi.” Akasema Jason .

Tayari Anitha alikwisha rejewa na fahamu zake lakini hakuwa na nguvu kabisa.Machozi mengi yalikuwa yanamtoka.Jason akamshika mkono akamsaidia kutembea hadi katika gari akiwa ameongozana na Mathew

“ Mathew are you sure you can drive? Akauliza Jason

“ Yes I can.Shughulikia suala hilo na nitakufahamisha baada ya kuwasiliana na familia ya Noah” akasema Mathew na kuwasha gari kisha wakaondoka.Anitha alikuwa ameinama akilia.Mathew naye alikuwa akiendesha gari huku machozi yakimtiririka.Kifo cha Noah kilimuumiza sana.

Walifika numbani na Anitha akajitupa sofani akaendelea kulia



“ Anitha najua ni kwa namna gani kifo cha Noah kimekuumiza,hata mimi nimeumia sana na siwezi kueleza ni kwa namna gani ninaumia moyoni lakini pamoja na maumivu yote tuliyonayo kwa sasa tunatakiwa tusimame imara katika suala hili hadi hapo tutakapo hakikisha kwamba Noah amepumzishwa.Sisi ndiyo ndugu zake wa karibu na tunatakiwa tuwe na nguvu na ujasiri tuubebe msiba huu hadi mwisho .Tafadhali Anitha nakuhitaji sana katika hili.Nahitaji sana ushirikiano wako” akasema Mathew

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“ Mathew I’m sorry I cant…Ninashindwa kabisa kujizuia kulia.NImeumia sana..Ouh Noah !..Anitha akashindwa kujiuzia na kuangua kilio.Mathew akamfuata akamkumbatia na kumfuta machozi.



“ We need to be strong for him” akasema Mathew halafu akainuka na kwenda chumbani kwake akakaa kitandani nz kuanza kulia.Baada ya kama dakika kumi hivi za kulia akainuka na kujifuta machozi halafu akafungua kabati lake na kutoa kitabu Fulani ambacho huwa anaandika kumbu kumbu kadhaa.Akazitafuta namba Fulani akaziandika katika simu yake na kupiga lakini namba zile hazikuwa zikipatikana.Akaandika tena namba nyingine na kupiga.Simu ikaanza kuita.Mathew alikuwa anampigia simu dada wa Noah anayefanya kazi katika benki moja nchini Zimbabwe.Baada ya kuzipata taarifa zile dada wa Noah akaumuunganisha Mathew na wazazi wake akawataarifu kuhusiana na kilichotokea.Kila aliyeipata taarifa ile alipatwa na mstuko mkubwa sana.Baba wa Noah akamuahidi Mathew kumpigia simu asubuhi ili kumtaarifu ni kitu gani watakuwa wameamua kuhusiana na mazishi ya mtoto wao

Mathew alikaa tena kitandani an kukumbuka mbali sana toka alipokutana na Noah na kujenga urafiki na hatimaye akamtoa katika kazi aliyokuwa anaifanya na kumuingiza katika kufanya kazi binafsi na ambazo zilimletea mafanikio makubwa .



“ Alikuwa ni kijana mchapa kazi na ambaye alikuwa uwezo ajabu.Nimekwisha fanya naye kazi nyingi na kila kazi niliyofanya naye ilifanikiwa kwa kiasi kikubwa.Yeye na Anitha hawakuwa tu ni marafiki zangu bali ndugu zangu” akawaza Mathew

“ Yeyote aliyefanya kitendo hiki nitamtafuta hadi nimpate.Kila risasi iliyoingia mwilini mwa Noah haitakwenda bure lazima itaondoka na mtu. I swear in heaven and earth yeyote aliyefanya ukatili huu hawezi kujificha sehemu yoyote nisimtambua.Nitawasaka kila mahala na nitawapata.” Akawaza Mathew akiwa na hasira kali



*******





Mwili wa jaji Elibariki ulikuwa umeloa damu na alikuwa na jeraha katika mkono wake wa kulia lililokua linatoa damu.Alikuwa amekaa ndani ya gari huku pembeni yake kukiwa na mwanamke aliyekuwa anaendesha gari kwa umahiri mkubwa sana.Mwili wote bado ulikuwa unamteteteka.Alikumbuka kilichotokea muda mfupi uliopita akaogopa sana.



“ Wamemuua Noah !! akawaza huku machzi yakimtoka

“ Ni akina nani wale waliofanya kitendo kile cha kinyama? Nilifanya kosa kubwa sana kulipuuza onyo lile nililopewa na Yule mwanamke aliyenipigia simu na kunitaka nisiingie katika gari.Inaonekana kuna mpango ulikuwa umekwisha pangwa ili niuawe.Lakini kwa nini watake kuniua? Ni nani wanaotaka kuniua? Mwanamke Yule aliyenipigia simu na kunipa onyo ni nani? Ni huyu pembeni yangu ama ni nani? Huyu mwanamke naye ni nani? Amenifahamuje? Mbona mimi simfahamu? Ananipeleka wapi? Akajiuliza Jaji Elibariki maswali mfululizo bila kupata majibu

“Mpaka sasa hivi sifahamu nimeponaje katika lile shambulio.Dah ! Toka nimezaliwa sijawahi kushuhudia shambulio baya kama lile.Risasi zilikuwa zinavuma kama vitani.Nimeponyoka toka mdomoni mwa kifo.” Akawaza Jaji Elibariki na kuvuta kumbu kumbu kuhusiana na namna tukio lile llilivyotokea.Alikumbuka namna Noah alivyoruka na kumkinga na risasi akaumia sana na machozi yakamtoka

“ Noah aliniokoa.Bila yeye hivi sasa ningekuwa tayari marehemu.Shambulio lile lilinilenga mimi na amekufa kifo nilichostahili kufa mimi.Ninaamini haikuwa ni mipango ya Mungu nifariki leo.Nadhani Mungu ana makusudi yake kwa nini nimepona leo hii.” Akawaza Jaji Elibariki halafu akajaribu kunyoosha mkono akagugumia kwa maumvu makali



“ Elibariki ! akaita Yule mwanamke ambaye alikuwa makini sana katika usukani.Elibariki akageuza shingo na kumtazama.Hakuwa na kumbu kumbu kama amewahi kumuona sehemu mwanamke sehemu yoyote.

“Unajisikiaje? Akauliza Yule mwanamke



“ Sijielewi elewi bado.I feel like I’m dead” akasema Elibariki na Yule mwanamke akatabsamu na kusema



“ You are not dead Elibarki .You are alive.Kuna sehemu yoyote umeumia? Akauliza



“ Ninasikia maumivu makali hapa katika mkono wa kulia na chini ya mguu wa kushoto” akasema Elibariki



“ Pole sana.” Akasema Yule mwanamke



“ Wewe ni nani? Akauliza Elibariki.Yule mwanamke akatabasamu na kusema



“ Mtu ambaye hupaswi kumfahamu”



“ Mtu ambaye sipaswi kukufahamu? Una maana gani kusema hivyo? Wewe ndiye uliyenipigia simu? Akauliza Elibariki

“ Elibariki kitu cha msingi cha kushukuru kwa sasa ni kwamba uko salama.”



“ Nani waliotaka kuniua? Unawafahamu? Akauliza jaji Elibariki



“ Elibariki huu si muda wa maswali mengi” akasema Yule mwanamama.Elibariki akakaa kimya kidogo halafu akauliza



“ Unanipeleka wapi?

“ Somewhere safe.Kuna sehemu yoyote ambayo unahisi inaweza kuwa salama kwa sasa kwa wewe kwenda kujificha? Kwa sababu hutakiwi kabisa kuonekana.”Akauliza Yule mwanamama.Jaji Elibariki akafikiri kwa muda halafu akasema



“ Ndiyo”



“ Ni wapi nikupeleke ? Akauliza Yule mwanamke



“ Kwa rafiki yangu”

“ Unafahamu anakokaa? Akauliza

“ Ndiyo ninapafahamu”



“ Unazifahamu namba zake za simu kwa kichwa ? kwa sababu sitaki uwashe simu yako” Akauliza



“ Ninazikumbuka “ akasema jaji Elibariki na kumtajia Yule mwanamke akaziandika katika simu yake akapiga na simu ikaanza kuita

“ Hallow” akasema Yule mwanamke baada ya simu kupokelewa



“ Hallow” ikasema sauti ya upande wa pili



“ Samahani ninaongea na nani?

“ Unaongea na Peniela” ikasema sauti ya upande wa pili.Yule mwanamke akamgeukia jaji Elibariki

“ Anasema anaitwa Peniela ndiye rafiki yako? Akauliza



“ Ndiyo”



“ Do you trust her? Akauliza tena

“ Ndiyo ninamuamini sana” akasema jaji Elibariki



“ Ok ongea naye” akasema Yule mwanamke na kumpatia Elibariki simu

“ Hallow Peniela Elibariki hapa ninaongea”

“Elibariki?



“Ndiyo ni mimi?



“ Mbona unanishangaza Elibariki? Mbona unanipigia kwa kutumia simu nyingine? Uko wapi ? Uko na nani?

“ Niko katika gari na ….” Elibariki akasita.Yule mwanamke aliyekuwa akiendesha gari akaachia usukani wa gari na kumnyang’anya Elibariki simu

“ Hallow Peniela.Una gari? Akauliza

“ Ndiyo ninalo”



“ Ok vizuri basi washa gari lako sasa hivi na uje pale Kisulo restaurant uje umchukue rafiki yako .He’s in trouble na anahitaji sehemu salama.Tafadhali usimwambie mtu yeyote kuhusiana na jambo hilina uwe na uhakika hakuna mtu anayekufuatilia” Akasema Yule mwanamke na kukata simu.



Kisulo Restaurant ni moja ya hoteli kubwa na nzuri jijini Dar es salaam ambayo kwa masaa yote huwa imejaa watu kutokana na huduma nzuri wanazozitoa pamoja na chakula kizuri kinachopika hapa.Kila aina ya chakula unachokihitaji basi unaweza ukakipata hapa.Eneo la maegesho la hoteli hii ni kubwa kutokana na idadi kubwa ya watu wanaofika hapa.Gari alilokuwa amepanda jaji Elibariki lililokuwa linaendehshwa na mwanamke ambaye hakumfahamu lilivuka hoteli kidogo na kwenda kusimama mbele yake,yule mwanamke akalizima akatoa bastora yake na kuiweka tayari.Alikuwa na wasiwasi sana yawezekana walikuwa wakifuatiliwa.

“Peniela ! do you trust her? Akarudia tena kuuliza yule mwanamke

“ Yes I do “ akasema Jaji Elibariki

“ kwa nini unaniuliza hivyo? Akaulizia

‘ Ninakuuliza hivyo kwa sababu maisha yako ya sasa hivi yanategemea sana watu unaowaamini.” Akasema yule mwanamke

“ kwani wewe ni nani? Umenifahamuje? Kwa nini umeniokoa? Unawafahamu waliotaka kuniua? Akauliza jaji Elibariki

“ Eliariki nimekwisha kwambia kwamba usitake kunifahamu.Kukuweka sehemu salama ni jukumu langu la kwanza .Nitakutafuta tena baadae.Ila ninachokuonya ni kwamba hutakiwi kabisa kuonekana kwa sasa.Hutakiwi kutoka hadi hapo nitakapokuamuru.” Akasema yule mwanamke.Jaji Elibariki akamtazama na kusema

“ Ninashukuru sana kwa kuniokoa lakini bado ninashauku kubwa ya kutaka kukufahamu wewe ni nani ,na kwa nini umeniokoa? Akauliza .Yule mwanamke hakujibu kitu akatoa simu yake na kuzitafuta namba za simu za Peniela akampigia

“ Hallow Peniela umefika wapi?

“ Nimekaribia sana kufika.” Akajibu Peniela

“ Ok good.Ukifika utalifuata gari Fulani limeegeshwa mbele ya kibanda kile cha kuuza vocha za simu .” akasema Yule mwanamke na kukata simu

“ Elibariki are you sure you’ll be in safe hands? Akauliza yule mwanamke

“ Yes I’m sure” akasema Elibariki

“ Kitu kingine usithubutu kumpigia simu mtu yeyote yule na kumweleza kwamba uko hai na mahala uliko.Si mke wako wala yeyote unayemfahamu mpaka hapo nitakapokuruhusu kufanya hivyo.Tumeelewana Elibariki?

“ Tumeelewana”akajibu jaji Elibariki ambaye bado kila kitu kilichotokea kwake ilikuwa ni kama sinema

“ This woman Peniela ,who is she to you? Akauliza yule mwanamke

“ What ? akauliza jaji Elibariki ambaye alionekana kuwa mbali sana kimawazo

“ nakuuliza huyu Peniela ni nani wako?Ndugu yako,rafiki yako au ni nani wako?

“ Ni rafiki yangu.” Akajibu Jaji Elibariki

“ Unamfahamu? Akauliza jaji Elibariki

“ Hapana simfahamu ila ninahitaji kumfahamu ili nihakikishe kwamba niko katika mikono salama”akasema yule mwanamama

“ Kwa nini umeniokoa? Kwa nini unataka kuhakikisha kwamba niko katika mikono salama? Akauliza jaji Elibariki na mara gari moja ndogo nyeusi ikawapita na kwenda kusimama mbele yao akashuka msichana mmoja ambaye jaji Elibariki akamtambua

“ Thats Peniela” akasema

“ wow she’s so beautiful” akasema yule mwanamke huku akitabasamu na kufungua mlango wa gari akashuka

“ Peniela ! akaita yule mwanamke na Peniela akamsogelea.Alikuwa na wasi wasi mwingi

“ Habari yako” yule mwanamke akamsalimu Peniela

“Nzuri .Elibariki yuko wapi? Is he ok? Akauliza Peniela akiwa na hamu ya kutaka kujua hali ya Elibariki

“ Usihofu Elbariki ni mzima na anaendelea vizuri .Kumefanyika shambulio usiku huu kuna watu waliotaka kumuua lakini nimefanikiwa kumuokoa. Elibariki anatafutwa auawe kwa hiyo anatakiwa apate sehemu ya kujificha hadi hapo mambo yatakapokaa vizuri Kwa sasa wewe pekee ndiye mtu ambaye anakuamini na anaamini katika mikono yako atakuwa salama.”akasema yule mwanamke

“ Ni akina nani wanaotaka kumuua? Akauliza Peniela akiwa na wasi wasi mwingi

“ Ni mapema mno kusema ni akina nani lakini naomba tu ufahamu hilo kwamba roho ya Elibariki inatafutwa kwa gharama yoyote ile kwa hiyo basi hakikisha kwa kila namna utakavyoweza Elibariki anakuwa salama.Muda wowote ule ukihisi hatari yoyote ile utanipigia simu yangu na kunifahamisha na nitakusaidia.”akasema yule mwanamke

“ kwani wewe ni nani? Akauliza Peniela lakini yule mwanamama hakujibu akaufungua mlango wa gari na kumtoa Jaji Elibariki kwa haraka haraka akaingia katika gari la Peniela kisha yule mwanamke akaondoa gari lake kwa kasi.Kwa muda wa sekunde kadhaa jaji Elibariki na Peniela walibaki wanaangaliana.Peniela aliogopa sana kwa namna Elibariki alivyokuwa ameloa damu

“ Pole sana Elibariki” akasema Penny

“ Ahsante sana Penny”

“ Umeumia mahala kokote?akauliza Peniela

“ Nina jereha hapa katika mkono wa kulia nahisi nimekwaruzwa na risasi na katika mguu ninahisi kuna maumivu makali”

“ Pole sana Elibariki.Nani lakini waliofanya kitu hiki? Unaweza kuwafahamu? Akauliza Peniela

“ Hapana Penny siwezi kuwafahamu ni akina nani lakini nia yao ilikuwa ni kuniua” akasema Elibariki.Penny akawasah gari wakaondoka

“ Nani ametaka kumuua Elibariki? Yawezekana akawa ni Jason akitaka kulipiza kisasi ? Ninaanza kuwa na wasi wasi sana yawezekana kabisa akawa ni Jason huyu ndiye aliyepanga njama hizi.Jason alichukia sana siku ile na nilimuona kabisa kwamba alikuwa na dhamira ya kuua na ndiyo maana alimpiga Elibariki na chupa kichwani.Sioni mwingine anayeweza kufanya jambo kama hili zaidi yake.” Akawaza Peniela

“ Kwa mujibu wa yule mwanamke Elibariki yuko katika hatari kubwa sana ya kuuawa.Lazima nitafute sehemu salama ya kwenda kumuweka.Sehemu ipi ni salama zaidi kumuweka kwa sasa?akajiuliza Peny

“Nyumbani kwangu sina hakika kama ni salama na nina ogopa anaweza akajulikana .Katika ile nyumba mpya niliyohamia leo ni sehemu salama na anaweza akaishi pale muda mrefu bila ya mtu yeyote kufahamu lakini tataizo ni kwamba lengo la rais kunitaka nikaishi pale ni ili awe na uwezo wa kufika muda wowote anaotaka .Itakuwaje iwapo atakuja na kumkuta Elibariki yuko pale? Hapana sehemu ile si muafaka kumuweka Elibariki.Itanibidi nimpeleke nyumbani kwangu halafu kesho nitaangalia namna nzuri ya kufanya. Lazima nipate sehemu salama kabisa ya Elibariki kuishi kwa muda wowote anaoutaka” akawaza Peniela

“ Nimefurahi kwa Elibariki kutua tena katika mikono yangu.Nilikuwa naitafuta sana nafasi hii ya kuweza kuutengeneza upya uhusiano wangu na Elibariki.Ni mtu ambaye amenisaida sana katika kuniweka huru .Lazima na mimi nimsaidie katika kipinid hiki ambacho anahitaji sana msaada ” akawaza Peniela na hawakuongea kitu chochote hadi walipofika nyumbani kwake akashuka na kufungua geti akaingiza gari ndani halafu akaufungua mlango wa gereji na kuliingiza gari katika gereji na ndipo alipomruhusu Jaji Elibariki kushuka.Akamsaidia kutembea hadi sebuleni akamkalisha sofani.Bado jeraha alilokuwa amelipata jaji Elibariki katika mkono wake liliendelea kutoa damu.Peniela akaenda chumbani kwake na kurejea na kiboksi chenye vifaa vya huduma ya kwanza na kulisafisha jeraha lile na kisha kupata dawa na kulifunga ili lisiendelee kutoa damu.

“ Pole sana Elibariki,usijali hapa uko sehemu salama na nitafanya kila linalowezekana kuhakikisha kwamba unakuwa salama.Kwa sasa ngoja nizuie hii damu halafu nitamuita daktari atakuja kukuangalia “ akasema Peniela na Elibariki akaonyesha wasi wasi Fulani

“usiogope Elibariki.Daktari huyo ni rafiki yangu mkubwa tumesoma wote toka shule ya msingi “ akasema Peniela.Baada ya kumfunga jeraha lile akamshika mkono na kumuongoza hadi bafuni ambako alimsaidia kuoga halafu akampeleka kitandani .

“ Peniela nashukuru sana “ akasema Jaji Elibariki

“ Usijali Elibariki.Wewe ni mtu wa muhimu sana kwangu kwa hiyo nitafanya kila linalotakiwa kufanywa kuhakikisha kwamba uko salama.” Akasema Peniela wakatazamana kwa muda halafu Peniela akasema

“ Elibariki ninaomba samahani sana kwa jambo lililotokea siku ile.Ni jambo la aibu sana lakini naomba tusahau yote yaliyotokea.Najua ulikasirika sana kwa tukio lile lakini nina hakika tutakaa na kuliongelea “ akasema Peniela .Jaji Elibariki akatabasamu kidogo na kusema

“Peniela naomba kwa sasa usiwaze kuhusiana na mambo hayo.Yamekwisha pita na kwa sasa tuko katika mambo mengine kabisa.Tushughulike na lili liko mbele yetu yaliyopita yamekwisha pita tusihangaike nayo.Tell me anything and I believe you”akasema jaji Elibariki na kumfanya Peniela atabasamu

“ Nashukuru sana Elibariki.Ngoja kwanza niwasiliane na daktari” akasema Penny na kumpigia daktari rafiki yake waliongea kwa dakika kama mbili hivi halafu akamfuata Elibariki

“ Daktari anakuja muda si mrefu” akasema

“ nashukuru sana Penny.Ahsante sana kwa kunijali ” akasema Elibariki na Penny akatabasamu na kusema

“ Elibariki nilistuka sana uliponipigia simu.Baada ya tuko lile la siku ile nilikuwa naogopa hata kukupigia simu na kukujulia hali yako.Kila nilipotaka kukupigia nilijikuta nikishindwa.Uliponipigia leo nilistuka sana na kujiuliza ni kwa nini mimi? Kwa nini katika watu wote hawa waliokuzunguka ukanichagua mimi? Am I that important to you?akauliza Peniela .Jaji Elibariki akamtazama na kusema

“ Peniela ,jina lako lilikuwa la kwanza kulifikiria mara tu nilipofikiria kama kuna sehemu salama ninaweza kwenda kukaa kwa usiku huu.Sikuwaza mtu mwingine yeyote zaidi yako kwa hiyo nina amini kwamba hapa niko sehemu sahihi “ akasema jaji Elibariki.

“ Mkeo ana taarifa ya kilichotokea? Akauliza Peniela

“ Nina hakika lazima atakuwa na taarifa mpaka hivi sasa.Siku hizi taarifa hazichelewi kusambaa.Nina hakika baada ya kuzipata taarifa hizi atakuwa katika wakati mgumu sana ”

“ Elibariki najua bado uko katika mstuko lakini unaweza ukanieleza hasa nini kilitokea? Akaulizia Peniela

Jaji Elibariki akafumba macho na kuvuta picha ya tukio lile kisha akasema

“ Usiku huu mke wangu alinipigia simu na kunitaka niende nikaonane naye kuna suala ambalo alitaka kunieleza.Siwezi kukuficha Peny kwa siku za hivi karibuni mimi na mke wangu tumekuwa katika mikwaruzano kidogo.Hata usiku huu tulipoonana tulishindwa kuelewana ikanilazimu kuondoka kwani nilikuwa na miadi ya kuonana na rafiki yangu mmoja anaitwa Mathew.Kabla sijafungua mlango wa gari langu nilipigiwa simu na mtu ambaye simfahamu.Alikuwa ni mwanamke na akaniambia kwamba nisiingie katika gari.Nikamuuliza yeye ni Nani na kwa nini nisiingie katika gari langu akaniambia kwamba kuna mpango wa kuniua.Nikampuuza na kuingia garini.Nilikuwa na mtu mmoja anaitwa Noah ambaye ndiye aliyekuwa akiendesha gari langu usiku huu.Tuliendelea na safari hadi tulipofika katika makutano ya barabara za Mkwavinyika na Kilimanjaro pale kwenye taa za kuongozea magari tukakuta kuna msururu mrefu wa magari.Wakati tukisubiri taa ziwake ghafla zilitokea piki piki mbili na kuanza kutuvurumishia risasi.Yule jamaa niliyekuwa naye garini Noah aliniwahi na kunikinga na zile risasi zikampata yeye na kumuua pale pale.Bila Noah hivi sasa tayari ningekuwa nimekufa.Alijitolea hai wake kwa ajili yangu” akasema jaji Elibariki

“ Pole sana Elibariki.Pole sana” akasema Peniela na kumfuta machozi yaliyokuwa yakimtoka.

“ Ahsante sana Peniela.”

“ Lakini ni akina nani waliotaka kufanya jambo hili? Ni kwa nini walitaka kukuua? Akauliza Peniela huku naye machozi yakimtoka

“ Sifahamu Peniela.Sifahamu ni akina nani wanaoitafuta roho yangu .Kwa sasa baada ya kunusurika inanibidi nichukue tahadhari kubwa sana kwani watu hawa wakijua wamenikosa hawatalala usingizi wataendelea kunisaka usiku na mchana hadi wahakikishe wametimiza lengo lao.lakini nakuhkikishia Peniela kwamba lazima watu hawa watapatikana tu” ” akasema jaji Elibariki na Kengele ya getini ikalia kuashiria kwamba kuna mtu.

“Huyo atakuwa ni daktari wangu” akasema Peniela na kuinuka akaelekea getini.Ni kweli alikuwa ni daktari aliyemuita Dr Jonesia.Peniela akampokea na kumpeleka moja kwa moja hadi chumbani kwake ambako alikuwepo jaji Elibariki.Dr Jonesia akasalimiana na jaji Elibariki halafu akaanza kumuangalia mahala alikoumia.Alimchunguza kwa muda wa kama nusu saa hivi kila sehemu ya mwili ambayo kulionekana kuwa na damu halafu akasema

“ Mungu ni mkubwa majeraha haya yote ni ya michubuko tu na hakuna risasi hata moja iliyoingia mwilini mwake” akasema Dr Jonesia na kuyatibu majeraha yote ya jaji Elibariki halafu akamchoma sindano na kumtaka apumzike.Peniela akamshukuru na kumsindikiza akaondoka

“ Peniela nashukuru tena kwa mara nyingine kwa msaada wako .Kama nilivyosema awali kwamba sikukosea kabisa kuja hapa.Ninaamini nimefika sehemu sahihi ninakotakiwa kuwapo kwa sasa”akasema jaji Elibariki na Penny akatabasamu kidogo

“Usijali Elibariki nitafanya kila linalowezekana kwa ajili yako “ akasema Peniela na mara simu ambayo huwa anaitumia kuwasiliana na Dr Joshua ikaita

“ Sorry Elibariki I need to take this call in Private .Its important’akasema Peniela na kuichukua simu ile akatoka mle chumbani

“hallow Dr Joshua’akasemaPeniela

“hallow Peniela,hujambo? habari za makazi mapya? Kareem aliniambia kwamba ila kitu kimekwenda vizuri kama ulivyotaka”

“Ndiyo Dr Joshua kila kitu kimekwenda vizuri na ninashukuru sana.Vipi wewe unaendeleaje? Akauliza Penny

“Hata mimi ninaendlea vizuri sana Penielea.Leo tulikuwa na zoezi la kuuaga mwili wa Flora na kesho tunalekea kijijini alikozaliwa kwa ajili ya mazishi.”

“ Pole sana Dr Joshua.” Akasema Peniela

‘ Ahsante sana Peniela.lakini yote hii ni mipango ya Mungu .Yeye ndiye mwenye kupanga mambo yote yatokee na hata kwa hili ana makusudi yake kwa nini litokee sasa.Nadhani ana mpango mkubwa wa nchi kumpata first lady mpya” akasema Dr Joshua huku akicheka kidogo

“Dr Joshua achana na mawazo hayo kwanza.Subiri kwanza hadi mkeo atakapozikwa”

“ Hahaha Peniela unanifurahisha sana,Flora is gone and she’ll never come back.Maisha lazima yaendelee “akasema Dr Joshua akatulia kidogo halafu akaendelea

“ Peniela nimekupiga simu kukutakia tu usiku mwema na kukumbusha ni namna gani ninavyokupenda.Endapo kama kusingekuwa na watu wengi hapa msibani nigekuja sasa hivi kujaku kuangalia na kupata faraja.Wewe ndiye furaha yangu”

“ Dr Joshua kwa sasa siko katika ile nyumba mpya .Nimerejea kwanza nyumbani kwangu kwa muda.” Akasema Penny na kumstua Dr Joshua

“kwa nini penny? Kuna tatizo lolote?akauliza Dr Joshua

“hapana Dr Joshua hakuna tatizo lolote ila kuna mambo ambayo nataka niyaweke sawa kwanza kabla ya kuanza kuishi katika nyumba mpya.” Akasema Peniela

“ Sawa Peniela tutaongea vizuri nikisharudi kesho.Endapo kuna kitu chochote unakihitaji utawasiliana na Kareem moja kwa moja” akasema Dr Joshua

“ Usiku mwema Dr Joshua”

“ Usiku mwema Peniela.I love you”akasema Dr Joshua na kukata simu

“ Huyu mzee hana akili nzuri.Yaani hata mke wake bado hajazikwa tayari amekwisha anza kuwaza mambo mengine kabisa.Laiti angenifahamu wala asingethubutu kunitamkia maneno yale ya kipuuzi.” Akawaza peniela na kurejea tena chumbani.

“ Peniela kuna jambo nataka nikuombe”

“ Omba chochote Elibariki”akasema Peniela

“Kuna mtu wa muhimu sana ambaye nataka niwasiliane naye”

“ Mke wako? Akauliza Peniela

“hapa sitaki kuwasiliana na mke wangu.Ni rafiki yangu tu ila ni wa muhimu mno ” akasema jaji Elibariki.Peniela akachukua simu yake na kuziandika namba alizotajiwa na Elibariki halafu akapiga.

“ Simu inaita”akasema Penny na kumpatia Elibariki simu

‘ Hallow” ikasema sauti ya upande wa pili

“ Hallow Mathew.Elibariki hapa ninaongea” akasema

“ Elibariki ? ! ..Mathew akastuka

“Ndiyo Mathew ni mimi”

“ Uko wapi Elibariki ? akauliza Mathew

“ Niko sehemu salama kwa sasa.Tayari mmepata taarifa za kilichotokea?

“ Ndiyo Elibariki.Tayari tumekwisha zipata taarifa na muda si mrefu tumetoka hospitali kuutambua mwili wa Noah.Pole sana kwa kilichotokea.”

“ Ahsante sana Mathew.Kwa kweli lilikuwa ni tukio baya sana na sikuwahi kutegemea kama siku moja tukio kama lile linaweza kunitokea.Ilikuwa nife lakini Noah ameniokoa .Amekufa kishujaa .He saved me.He saved my life” akasema Jaji Elibariki huku akilengwa na machozi

“ Kifo cha Noah kimeniumiza sana Elibariki.Lakini hatuna namna ya kufanya imeshatokea imetokea.Kwa sasa uko wapi? Akauliza Mathew

“ Kuna sehemu nimejificha”

“ Is it a safe place? Are you sure you are safe? Akauliza Mathew

“ Yes I’m sure.I’m safe”

“ Ok good.Endelea kujificha hapo hapo .Kwa sasa tunashughulikia msiba wa Noah.Nimewasiliana na wazazi wake tayari nchini Zimbabwe na wamesema kwamba tutawasiliana tena asubuhi ili wanitaarifu kuhusiana na walichokipanga.Noah alikuwa ni kama mdogo wangu kwa hiyo nitaweka kila kitu pembeni kwa sasa na baada tu ya kumzika ndipo nitaanza tena kazi.Ninakuahidi kwamba yeyote aliyehusika katika tukio hili hatabaki salama.Nitakaporejea utashuhudia nitakachokifanya.Kila risasi iliyoingia mwilini mwa Noah italipwa.Kwa sasa endelea kukaa hapo hapo hadi nitakaporejea.Endapokukiwa na tatizo lolote unitaarifu mara moja.Lakini mpaka hapo tutakapoonana tena please stay safe” akasema Mathew na kukata simu



“ Mathew ameumizwa sana na kifo cha Noah .Nimeisikia sauti yake na anaonekana wazi kwamba ana nia ya dhati ya kulipiza kisasi.Hata mimi ninamuunga mkono kwa hilo.Lazima watu wote waliofanya kitendo kile wapatikane .Watu wale walikuwa na lengo la kuniua lazima niwafahamu ni akina nani kwa nini wanataka kuniua? Akawaza jaji Elibariki.Mawazo mengi yakamjia kichwani kutafakari kuhusiana na tukio lile .



“ Ama kweli maisha ya mwanadamu ni mafupi sana.Dakika chache zilizopita nilikuwa naongea na kucheka na Noah lakini ghafla tu watu wameukatili uhai wake.Tukio lile litaendelea kukaa katika kumbukumbu zangu kwa miaka mingi sana .Ni tukio baya sana kuwahi kunitokea lakini kwa msaada wa Mathew nina hakika nitawafahamu waliofanya tukio lile.” Akawaza na kukumbuka toka alipopigiwa simu na Yule mwanamke na kumzuia asiingie katika gari



“ Mawazo yananijia kwamba yawezekana kabisa sababu ya kutaka kuniua chanzo chake kikawa ni kifo cha Dr Flora ambaye akifo chake kimetawaliwa na utata mwingi. Nilifanikiwa kuufahamu ukweli wa kilichomuua Dr Flora lakini nilishangaa baadaya taarifa yangu kutupwa mbali kwamba ni taarifa ya uongo na ya kuunga unga.Ninamuamini Mathew na hawezi kunipa taarifa ya uongo.Ninahisi kitendo changu cha kuufahamu ukweli wa kifo cha Dr Flora kimewapa mashaka sana watu waliomuua na hivyo ili kuendelea kuificha siri hii wakaona njia bora ni kuniua na mimi pia.Ni akina nani watu hawa? Kwa nni walimuua Dr Flora? Kuna mambo mengi hapa ya kujiuliza na kuyatafutia majibu “ akawaza na taratibu kijiusingizi kikaanza kumpitia kutokana na dawa alizokuwa amepewa .Peniela akamfunika vizuri na kulala pembeni yake.

“ Lini na mimi nitampata mwanaume wa kulala naye kitandani kama hivi ambaye nitakuwa na uhakika kwamba ni mwanaume wangu? Nitakuwa nikilala na wanaume wa wenzangu hadi lini? Nimekwisha anza kuchoshwa na maisha haya.Sitaki tena kuwa sehemu ya Team SC41.Nataka niishi maisha ya kawaida kama wanawake wenzangu.Lakini yote haya mwisho wake umekaribia sana.Nikishaikamilisha operesheni 26B lazima nirejee katika maisha ya kawaida.” akawaza Peniela akiwa ameuweka mkono wake kifuani kwa jaji Elibariki





********



Kumepambazuka na nchi ikia imeamshwa na taarifa kubwa ya kushambuliwa kwa jai wa mahakama kuu.Vyombo vyote vya habari hii ndiyo ilikuwa habari yao kubwa siku hii.Hakuna aliyeweza kufahamu mahal aliko jaji Elibariki japokua kulikuwa na juhudi kubwa za jeshi la polisi katikakumtafuta mahala aliko.Flaviana Hakuweza kabisa kupata usingizi kutokana na hofu aliyokuwa nayo.Mpaka kunapambazuka hakuwa amepata taarifa zzote kuhusiana na wapi alipo mume wake.Akampigia smu baba yake na kumuuliza kama kuna taarifa zzote za kuhsu mahala aliko mume wake lakini mheshimiwa rais akamuhakikishia kwamba vypmbo vya uslama vinaendelea kmtafuta kila mahala .

“Nakuomba baba tafadhali fanya kila linalowezekana ili mume wangu aweze kupatikana.” Kasema Flaviana

“ Flaviana nimekwisha kuahidfi kwamba nitafanay akila linalowezekana ilikuhakkisha kwamba Elibariki anapatikana tena akiwa hai” akasema DrJoshua na kuwaomba wajiandae kwa ajiliya safari ya kueleka mazishini kijijini alikozaliwa mama yao





*******





Mlio wa simu ukamstua Mathew aliyekuwa amejilaza sofani.Akainuka na kuichukua simu yake.Alikuwa ni baba yake Noah ambaye alimfahamisha kwamba wamekaa kikao cha familia na wameafikiana kwamba Noah azikwe jijini Dar es salaam kwa hiyo familia nzima itakuja jijini Dar kwa mazishi.Baada ya kuongea na baba yake Noah Mathew akampigia simu Jason na kumfahamisha mambo aliyoongea na baba yake Noah.Hakumueleza chochote kuhusiana na Ebariki.Kisha ongea na Jason akaenda kumgongea Anitha ambaye macho yake yalikuwa yamevimba kwa kulia akamfahamisha kilichokuwa kinaendelea



“ Anitha there is one more thing” akasema Mathew

“ Kitu gani Mathew?



“ Nimeongea na Elibariki jana usiku”

“ Elibariki?! Anitha akastuka



“ Ndiyo nimeongea naye jana usiku “



“ Kwa nini hukuniambia usiku ule kama uliongea na Elibariki ili nisiwe na mawazo kama amekufa?



“ Usingeweza kunisikia kwa namna ulivyokuwa na uchungu ” akasema Mathew

“ Yuko wapi ? Is he ok? Is he safe? Akauliza Anitha



“ Hakuniambia kama yuko wapi lakini alinihakikishia kwamba yuko salama.”



“ Are you sure he’s safe? Akauliza Anitha



“ Sina hakika sana kama yuko salama lakini yeye mweyewe alinihakikishia kwamba yuko salama”



“ Nina wasi wasi asije kuwa ametekwa na watu na wakamlazimisha apige simu ili kuwaondoa watu wasi wasi” akasema Anitha



“ Hilo linawezekana kabisa .Unajua kwa wakati ule hata mimi kichwa changu hakikuwa sawa.Nilikuwa na mambo mengi sana” akasema Mathew

“ Namba alizokupigia unazo? Akauliza

“ Ndiyo ninazo “ akasema Mathew



“ Tunatakiwa tuzifuatilie namba hizo tuzifahamu ni za nani ili tujue ni wapi tunaweza kuanza kumtafutia jaji Elibariki.We need to find him Mathew.We need to bring him here.This is the only place we can be sure he’s safe” akasema Anitha. Mathew akamtajia namba alizotumia jaji Elibarki kumpigia simu usiku ,Anitha akainuka na kuchukua kompyuta yake ndogo akafungua program Fulani na kuziandika zile namba alizotumia Elibariki kumpigia Mathew.Baada ya kama sekunde ishirini hivi akamgeukia Mathew



“ What ! Umegundua nini? Akauliza Mathew



“ Peniela !..



“ Peniela? Akauliza Mathew



“ Ndiyo.Namba aliyoitumia Elibariki jana kukupigia ni namba ya simu ya Peniela”



“ Are you sure? Akauliza Mathew



“ Yes I’m sure.Ni namba ya Peniela.Are you sure he’s safe there?

“ I think he’s safe.” Akasema Mathew



“ Amefikaje kwa Peniela? Akauliza Anitha



“ Hata mimi sifahamu bado amefikaje lakini nina hakika ni sehemu ambayo amechagua kuwepo kwa sasa.Ukumbuke niliwaambia mapema kwamba Elibariki na Peniela wana mahusiano kwa hiyo atakuwa ameamua kwenda kujificha kule”

“ What about Team SC41? Akauliza Anitha

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“ Anitha kwa sasa kilichopo mbele yetu ni kwanza kushughulika na msiba wa Noah na baada ya hapo tutarejea tena kazini na safari hii tutakuwa na kazi kubwa ya kuweza kuwatafuta wale wote waliomuua Noah ,vile vile tuna kazi kubwa ya kufahamu kuhusiana na zile karatasi,na mwisho tuna kazi kubwa ya …” Mathew akasita

“ Kazi kubwa ya nini? Akauliza Anitha



“ Ouh sorry forget about that.Inuka ujiandae leo tuna siku ndefu sana” akasema Mathew na kutoka.

“ Kazi yangu ya mwisho ni kupambana na Team SC41.Sikutaka Anitha afahamu hili kwa sababu hiki ni kisasi changu peke yangu na sitaki yeyote ahatarishe maisha yake kwa sababu ya kazi hii.Nitapambana peke yangu” akawaza Mathew na kuingia chumbani kwake.





********



ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog