Search This Blog

Saturday 5 November 2022

PENIELA (STORY YA KIJASUSI) - 4

 






Simulizi : Peniela (Story Ya Kijasusi)

Sehemu Ya Nne (4)



“ Mhh ! Anitha amenisisimua sana na macho yake.Ni mwanamke mzuri mno.Amenifanya nishindwe kukaa kwa muda mrefu pale ndani kwa jinsi alivyokuwa akinitazama.Macho yake mazuri ya kimalaika yanasisimua akikutazama” akawaza Jason akiwa ndani ya gari baada ya kuondoka nyumbani kwa Mathew

“ Kwa nini Anitha ameamua kuacha kazi zote na kuamua kuifanya kazi hii ya hatari ? Binti mzuri kama Yule hakupaswa kujihusisha kwa namna yoyote ile na kazi kama hizi za hatari.Gosh she’s so pretty.Lakini hawezi kuwa mzuri kumshinda Peniela” Akawaza Jason

“ Kwa sasa ngoja nielekee kwa Peniela.Sijamuona kwa siku kadhaa lazima nikaonane naye jioni hii.Lazima nimuulize alikwenda wapi? Na kwa nini hakuniaga? Dah ! Peniela ameniingia sana akilini.Haipiti saa bila ya kumuwaza.Ninampenda Peniela na kwa hilo siwezi kulificha.Kwa muda wa mwaka mzima nimekuwa na Peniela nikihangaika naye katika kesi na ninaamini nimemfahamu vyema.Nimejiridhisha kwamba ni mwanamke mwenye kunifaa kabisa katika maisha yangu.Ni mwanamke mzuri mwenye kila sifa.Ni mzuri kwa nje na ndani pia nadhani hii ndiyo sababu iliyomfanya hata Edson kuamua kumuacha binti wa rais na kumfuata Penny.Sitakiwi kuendelea kupoteza muda kumueleza ukweli wa moyo wangu kwani chelewa chelewa utakuta mwana si wako.Natakiwa nianze kuchukua hatua kuanzia sasa.Peniela anatakiwa afahamu kwamba ninampenda na niko tayari kufunga naye ndoa na kumsahaulisha mateso na maumivu yote aliyoyapata” akawaza Jason.

Saa mbili kasori dakika kumi na nne za usiku akawasili nyumbani kwa Penny.Akabonyeza kengele ya getini ikaita bila majibu.Takribani dakika tano aliendelea kubaki nje akibonyeza kengele bila geti kufunguliwa.Akachukua simu yake na kumpigia Penny akamfahamisha kwamba yuko pale nje.Hazikupita dakika mbili geti likafunguliwa

“ I’m so sorry Jason.Sikujua kama ni wewe ndiye uliyekuwa ukigonga.Sikuwa nikimtegemea mgeni yeyote Yule jioni hii” akasema Penny

“ Usijali Penny.Mimi ndiye mwenye makosa kwa kutokutaarifu kwamba nitakuja .Utanisamehe sana kwa kuingilia ratiba zako lakini nisingeweza kulala usiku wa leo bila kuja kukuona na kuhakikisha umerejea salama” akasema Jason

“ Usijali Jason.Hapa ni nyumbani kwako huna haja ya kunitaarifu kwamba unakuja.Muda wowote unakaribishwa” akasema Penny na kumfanya Jason atabasamu.Mezani kulikuwa na chupa kubwa ya whysky.Penny akauliza

“ Unatumia kinywaji gani Jason?

“ Wine” akasema Jason

“ Ouh Jason,tonight why cant you change? Try some whisky.I feel like I want something strong tonight.Join me” akasema Penny.Jason akatabasamu na kusema

“ Ok Penny lets have fun “ akasema Jason.Penny akammiminia whysky katika glasi wakaanza kunywa

“ Jason kwanza kabisa naomba samahani sana kwa kutokutaarifu kwamba sintakuwepo kwa siku kadhaa.” Akasema Penny

“ Usijali kuhusu hilo Penny.Nilifika hapa kwako na kukutana n makufuli.Nilipatwa na wasi wasi sana kuhusiana na usalama wako kwani hata simu yako haikuwa ikipatikana.Siku hizi zote nilikuwa nikiishi kwa wasi wasi mkubwa .Thanks God you are back” akasema Jason

“ Vipi wewe unaendeleaje ? akauliza Penny

“ Ninaendelea vizuri Penny.Just mised you”

“ I missed you too Jason.Naomba nikwambie ukweli Jason huko nilikokuwa hazikupita dakika mbili bila kukuwaza” akasema Penny.Jason akatabasamu

“ Kwani ulikwenda wapi Penny? Umerejea umebadilika sana.Umekuwa mrembo mno tofauti na Penny Yule niliyemzoea.Kama si sauti yako ningeweza hata kukupotea” akasema Jason na kumfanya Penny acheke kicheko kikubwa

“ Nilikwenda kufuatilia masuala yangu ya biashara.And you ? ,leo umetoka wapi kwa sababu umependeza mno tofauti na nilivyokuzoea ukiwa katika suti kila siku.Dont tell me you had a date” akasema Penny ambaye usiku huu alikuwa amechangamka sana

“ No ! I had to meet a friend.It wasn’t a date” akasema Jason.Penny akanywa funda moja na kuuliza

“ Jason kuna kitu nimekuwa nikitaka kukuuliza kila siku lakini sikuweza kutokana na kutingwa na kesi lakini kwa sasa kwa vile mambo yamekwisha naomba nikuulize”

“ Uliza Penny”

“ Where is your wife? Sijawahi kukusikia hata siku moja ukizungumizia masuala ya familia”

Jason akatabasamu na kusema

“ Sina mke wala familia”

“ What ?!..Huna mke? ..

“ Ndiyo sina mke.Mbona umeshangaa sana Penny?”

“ Nimeshangaa sana kwa sababu kwa kijana mzuri kama wewe tena msomi uliyebobea katka sheria huna mke.What are you waiting for Jason? Akauliza Penny.Jason akanywa funda moja la whysky akatabasamu na kusema

“ Ni kweli Peniela sina mke mpaka sasa lakini sababu kubwa iliyonifanya niwe hivi mpaka leo ni kutokana na kutingwa mno na kazi na hata kujisahau kwamba na mimi ninahitaji kuwa na maisha kama wengine.Kingine kikubwa ni kwamba bado sikuwa nimefanikiwa kumpata mwanamke Yule ambaye ataufanya moyo wangu usimame,ambaye atanifaa kuwa mke” akasema Jason .Penny akanywa funda la mvinyo na kusema

“ I’m curious.Why a handsome guy like you, you are still single up to now? Be honest with me Jason.Are you a gay? Akauliza Penny.Jason akastushwa sana kwa swali lile akashindwa kujibu akabaki amemtazama Penny .Walitazamana kwa sekunde kadhaa halafu Penny akanywa funda la whysky na kusema

“ Mbona hunijibu Jason? Is it true? Akauliza Penny.Bado Jason hakumjibu kitu.Penny akainuka toka katika sofa alilokuwa amekaa akamfuata Jason na kukaa karibu naye.

“ Jason tell me the truth.” Penny akamnong’oneza Jason sikioni.Mapigo ya moyo ya Jason yakaanza kwenda kasi baada ya Penny kumpumulia sikioni.Penny akamtazama usoni na kuwaza

“ There is only one way to find the truth”

Taratibu Penny akaupeleka mkono wake hadi katika maeneo nyeti ya Jason na ghafla akahisi kushika kitu kigumu

“ Gosh ! its serious” akasema huku akicheka.Jason hakuwa akicheka.mapigo ya moyo yalikuwa yakimuenda mbio.Penny akaendelea kuchezea maeneo nyeti ya Jason yaliyokuwa yamefura.

“ Sorry Jason nilikufikiria vibaya.Umezidi kuwa mzuri” akasema Penny kwa sauti ya kunong’ona

“ what are you doing Penny ? What do you want? Akauliza Jason

“ Please Jason,make my night beautiful” akasema Peniela.Kwa kasi ya ajabu Jason akamvuta Peniela na kuanza kumwagia mabusu mazita mazito huku akimtoa nguo

“ Jason I need you..I need you Ja…!!..” akasema Penny

“ I’ve been waiting for so long for this chance.Leo utaongea lugha kumi na mbili” akasema Jason huku akivua nguo yake ya ndani



Jason you are a real man” akasema Peniela huku akitweta baada ya kumaliza mzunguko mmoja.Jason alikuwa amejilaza sofani akitiririkwa na jasho.Shughuli aliyoifanya haikuwa ndogo.Penny akajiinua toka katika zuria alikojikuta amelala,akajimiminia whysky katika glasi na kunywa

“ Uuupphhhhh…!!!” akavuta pumzi ndefu halafu akamtazama Jason

“ You are so wonderful Jason.I swear in heaven and earth,sijwahi kukutana na mwanaume anayeyajua mapenzi kama wewe.You are amazing” akasema Penny

“ Come here Peniela” akasema Jason .Penny akamfuata pale sofani.Jason hakusema chochote akamvuta na kumkumbatia kwa nguvu huku akimporomoshea mabusu mazito mazito .Penny akajikuta hajiwezi tena na alihitaji huduma kwa mara nyingine tena.Jason alikifahamu alichokihitaji Penny naye bila kumkawiza akaanza kumpatia huduma,wakaingia katika mzunguko wa pili.Sebule ikajazwa na vilio vya mahaba toka kwa Penny kuashiria raha aliyokuwa akiipata .Jason alimchezesha gwaride la uhakika na hadi wanamaliza mzunguko wa pili Penny alikuwa hoi amechoka

“ Dah ! Jason kweli kidume.Sikutegemea kama ana uwezo mkubwa kiasi hiki.Kwa mara ya kwanza katika maisha yangu nimepata mtu ambaye amenikuna kisawa sawa.Sikuwahi mpata mtu ambaye alinikimbiza mchaka mchaka kama huyu.Huyu ndiye mwanaume ambaye nimekuwa nikimuota kila siku nimpate katika maisha yangu,mwanaume ambaye anafahamu mwanamke anahitaji nini na akamtimizia.Wanaume kama hawa ni wachache sana siku hizi.What can I do to own him? “ akawazaPenny akiwa kifuani kwa Jason

“ Sikuwahi kufikiria hata mara moja kwamba itatokea siku moja nitamvulia nguo Jason kwa namna tulivyokuwa tukiheshimiana na kuchukuliana kama kaka na dada.Amenisimamia kesi yangu na nikashinda na katika siku zote hizo takribani mwaka mzima hata siku moja hakujawahi kujitokeza hisia zozote za kimapenzi kati yetu.Kuna kitu ninajiuliza,je kama tulikuwa tunachukuliana kama kaka na dada kitendo hiki tulichokifanya leo kimetokea kwa bahati mbaya au nilidhamiria kukifanya? Akajiuliza Penny huku akihisi raha ya aina yake pale Jason alipokuwa akiupitisha mkono wake katika sehemu ya uti wa mgongo

“ Haikuwa ni bahati mbaya.I wanted this to happen.Nilihitaji kufanya hivi kwa sababu maalum.Pamoja na hayo kuna kitu nimekigundua kilichokuwa kimejificha ndani mwangu.Ni wazi ninampenda Jason.I deeply love him na kwa hilo siwezi kubishana na nafsi yangu.Jason ndiye mwanaume ambaye ninamuhitaji katika maisha yangu .Kwa bahati mbaya sana haiwezekani kuwa naye katika maisha yangu.Ouh gosh what kind of life is this? Siwezi kuipata furaha niitakayo katika maisha yangu.Kwa nini ninaishi maisha kama haya? Nimekuwa na mahusiano na wanaume kadhaa mpaka sasa lakini Jason ni wa tofauti kabisa na hao wote na ninaamini ni mwanaume ambaye atanifaa sana lakini kwa mfumo wa maisha ninaoishi haitawezekana kuwa naye.Nasikitika sana kumkosa kijana kama huyu” Akawaza Penny

“ Penny unawaza nini? Akauliza Jason

“ Ninawaza mambo mengi sana,kikubwa ni kuhusu wewe.Mambo uliyonifanyia leo yamenifanya niwaze vitu vingi sana.” Akasema Penny.Jason akatabasamu na kusema

“ Usiku wa leo utakuwa ni maalum kwa ajili yako.Nataka niung’arishe usiku huu.I’ll take you to the sky and back.Nataka kuikata kiu yako ya mwaka mzima.I know you needed this and I’m here to give you all that you want” akasema Jason na kumuangushia Peniela busu zito

“ Its true Jason .It’s true I needed this.I needed a strong man tonight.After what you’ve done to me,I don’t think that I’ll let you go.I need you to stay with me Jason,not just for tonight but forever.I need you in my life” akasema Penny na kuufanya uso wa Jason upambwe na tabasamu pana sana.

“ Siamini kama mambo yanakwenda kama nilivyokuwa nataka.Huu ndio wakati niliokuwa nautafuta sana kwa siku nyingi .Ni wakati sasa wa kuweka kila kitu wazi.Siwezi kuipoteza nafasi hii nikaja kujilaumu baadae wakati kumbe hata yeye mwenyewe alikuwa akinitamani ” akawaza Jason na kuendelea kumporomoshea Penny mabusu mfululizo

“ Peniela hufahamu ni jinsi gani nimekuwa nikiota kuipata nafasi kama hii ya mimi na wewe kuwa kama hivi watupu.Leo hii ile ndoto yangu ya muda mrefu imetimia.I’m right here with you in my arms.” Akasema Jason.Penny akainua kichwa na kumtazama Jason

“ Were you dreaming for this to happen? Akauliza

“ Ndiyo Penny.To be honest I’ve been dreaming for this to happen for so long ” akasema Jason.

“ mhh…!..” Penny akaguna

“ Penny you’ve been in my dreams since the day we met.Wewe ndiye Yule mwanamke wa ndoto zangu ambaye maisha yangu yatakamilika endapo nitakuwa nawe.Penny nafahamu hukuwa umelitegemea hili lakini naomba nikueleze ukweli kwamba ninakupenda sana.Nimekuwa nikiomba kila siku itokee siku kama ya leo ambayo nitauweka wazi ukweli wa moyo wangu.Penny wewe ni mwanamke wa pekee kabisa katika dunia hii ambaye utayafanya maisha yangu yawe na furaha na maana.Nakuhakikishia kwamba niko tayari kuutunza moyo wako zaidi ya mboni yangu ya jicho endapo utaufungua na kuniruhusu niingie ndani yake.” Akasema Jason.Peniela aliyekuwa amelalia kifua cha Jason akainuka na kumuangalia kana kwamba ni mara ya kwanza wanaonana.Alitaka kusema kitu lakini akajikuta sauti ikikwama

“ Shhhh..!!!..” Jason akamzuia kwa kumuwekea kidole mdomoni

“ Don’t say anything yet .Take your time and think about it first. This is your life, this my life, this is our life so think carefully” akasema Jason

“ Jason…..uuhhmm..” akaita Penny

“ Sema Penny”

“ Nimekosa neno la kusema.Come here.Wewe ni kijana usiyeisha utamu.I feel like I need it again and again..” akasema Penny huku akimvuta Jason na kumporomoshea mabusu



***********************



Noah na Anitha walikuwa kimya kabisa wakisubiri kusikia atakachowaeleza Mathew aliyekuwa ameegemea kabati akiwaza huku mkononi akiwa na glasi ya mvinyo.Alionekana kuzama katika mawazo mengi.

“ Whats wrong with him? Who is John Mwaulaya? Akauliza Noah

“ Sifahamu mtu huyu John Mwaulaya ni nani lakini ninachofahamu Mathew alistuka sana alipoliskia jina hili .Ngoja akitulia atatueleza namna anavyomfahamu huyu mtu” akasema Anitha

Baada ya dakika zaidi ya tatu za kuzama katika mawazo mengi,Mathew akaketi kitini

“ Sorry guyz najitahidi kulazimika kutokuwaza lakini siwezi kuyaepuka mawazo kila ninapolisikia jina John Mwaulaya. “ akasema Mathew.

“ Who is this guy ? akauliza Noah.Mathew akainama akafikri kidogo na kusema

“ Ninyi ni washirika wangu nitawaeleza kila kitu ninachokifahamu kuhusiana na John mwaulaya” akasema Mathew halafu akainama tena chini akawaza kwa sekunde na kusema

“ Sijawahi kuonana naye ana kwa ana.John Mwaulaya ni mtu ambaye ninamfahamu kwa jina na vitendo na siifahamu sura yake ikoje.” Akanyamaza kidogo akameza mate na kusema

“ Mwaka 2006 nikiwa nafanya kazi katika idara ya ujasusi ya taifa tulipata taarifa za kuingia nchini mwanamke mmoja aitwaye Faizat AbdulOmar Fayed ambaye inasemakana alikuwa mmoja kati ya wafadhili wakubwa wa mtandao wa Alqaeda.Mwanamama huyu tajiri sana aliyeingia nchini akitokea nchini Oman,anamiliki visima vya mafutta nchini Saudi Arabia,Syria na Iraq,utajiri aliourithi baada ya mume wake Omar na wanae wawili kuuawa na vikosi vya marekani vilivyokuwa vikimfuatilia kwa muda mrefu.Omar alikuwa mmoja kati ya watu waliokuwa wakitafutwa kwa muda mrefu na serikali ya marekani kwa kuufadhili mtandao wa Alqaeda.Baada ya kifo cha mumewe na wanae wawili,Faizat aliapa kuendeleza mapambano na aliendelea kuufadhili mtandao wa Alqaeda kwa pesa na kufanikisha mashambulio mengi yaliyopoteza uhai wa watu wengi.” Akanyamaza akawatazama akina Anitha halafu akaendelea.

“ Baada ya kuzipata taarifa zile tulianza mikakati ya kumtia nguvuni kwani tulikuwa na taarifa zake zote.Tulifahamu mahala alipo na tukaweka mikakati ya kuweza kumpata.Tulizisoma nyendo zake na kufahamu kwamba Faizat alikuwa na tabia ya kujibadilisha muonekano na hivyo kukwepa vizingiti mbali mbali alivyowekewa vya kumkamata .” akakaa kimya kidogo halafu akaendelea

“ Ilikuwa ni siku ya alhamisi tuliyopanga kumvamia na kumkamata Faizat mahala alikokuwa amejificha,mimi ndiye niliyeongoza timu ya watu kumi na saba wenye ujuzi wa hali ya juu wa kukabiliana na magaidi toka katika idara ya ujasusi ya taifa.Tulikuwa tumejihami kwa silaha na kila aina .Saa saba za usiku tuliivamia nyuma alimokuwamo Faizat lakini tukamkosa.Nyumba ilikuwa tupu kabisa.Wakati tukijiuliza nini kimetokea wakati taarifa tulizokuwa nazo kiintelijensia zilionyesha wazi kwamba Faizat alikuwa katika nyumba ile,ghafla tukavamiwa na watu wasiojulikana na kuanza kutushambulia kwa silaha kali sana. Hatukuwa tumetegemea shambulio kama lile lililotokea kwa kitendo cha kufumba na kufumbua kwa hiyo tulijikuta tukipoteza kikosi kizima na ni mimi peke yangu niliyefanikiwa kutoka salama.Mpaka leo ninaamini nilifanikiwa kutoka katika shambulio lile kwa maongozi ya Mungu tu. Kila mara picha ya shambulio lile ikinijia mwili wote husisimka.Siwafichi ndugu zangu ni miaka kadhaa imepita sasa lakini mpaka leo hii nikikumbuka kilichotokea usiku ule huwa ninaogopa sana.Ni picha ambayo ni ngumu hata kuielezea” Akanyamaza kidogo na kuinama halafu akasema

“ Nilipofanikiwa kutoka salama eneo lile nilikimbia moja kwa moja hadi nyumbani kwangu lakini nikakutana na kitu cha ajabu ambacho mpaka leo hii picha yake haiwezi kunitoka kichwani.Nyumba yangu ilikuwa ikiteketea kwa moto.Familia yangu yote ilikuwa imeteketea katika moto ule mkubwa” Mathew akashindwa kuvumilia akainama na kuangusha chozi







Nilichanganyikiwa baada ya kuona nyumba yangu ikiteketea kwa moto.Nilitamani hata kujitupa ndani ya moto ule ili nami niteketee pia pamoja na familia yangu.Mara walitokea watu wawili ambao sielewi walitokea wapi ambao nilidhani walikuwa ni miongoni mwa majirani zangu,wakaniingiza katika gari na kuniwekea bastora kichwani wakinitaka nisifurukute bali nifuate kila watakachonielekeza.Kwa wakati huo nilikuwa kama mtu niliyechanganyikiwa na sikuwa nikiogopa chochote,nilianza kupambana nao na walipoona nimewashinda wakaamua kunitupa nje na kukimbia huku nikiwa nimejeruhiwa kwa risasi begani.” Mathew akavua shati na kuwaonyesha akina Anitha kovu mahala alikopigwa risasi

“ Nilikimbia na kujificha chini ya daraja,nikampigia simu mkurugenzi na kumfahamisha kilichotokea.Dr Wilbert Augustino mkurugenzi wa idara ya ujasusi aliyekuwapo wakati ule alifika mara moja mahala nilipokuwa nimejificha na kunichukua akanipeleka katika nyumba fulani kubwa.Akawapigia simu rafiki zake wawili madaktari wakafika na kunitoa risasi ile niliyopigwa begani.Nilijaribu sana kumuuliza mkurugenzi kama anafahamu chochote kuhusiana na shambulio lile lakini alinieleza kwamba hafahamu chochote.Aliniambia niendelee kukaa katika nyumba ile wakati wakiendelea na uchunguzi kuhusiana na tukio lile la kustusha.” Mathew akainama na kuzama katika mawazo .Alikuwa amekumbuka mbali sana.

“ Kwa takribani siku kumi na nne “ akaendelea Mathew

“ Niliendelea kukaa ndani ya ile nyumba kubwa na nzuri ambayo haikuwa ikikaliwa na mtu mwingine yeyote zaidi yangu.Daktari alifika kila siku na kunitibu jereha.Mkurugenzi pia hakukosa hata siku moja kufika na kuniletea mahitaji mbali mbali ikiwemo chakula.Bado mkurugenzi aliendelea kunisihi nisijaribu kutoka nje kwani hali ya huko haikuwa bado nzuri kwa upande wangu.Alinieleza kwamba nilikuwa natafutwa sana lakini hakunieleza ni akina nani waliokuwa wakinitafuta.Hiki kilikuwa ni kipindi kigumu mno katika maisha yangu.Nililia mno kila siku nikiiililia familia yangu niliyoipenda kupita kitu chochote.Ilifika mahala sikutamani hata kuendelea kuishi kwani sikuona faida ya kuishi bila ya familia yangu iliyoteketezwa kikatili.” Mathew akainama kwa uchungu akikumbuka familia yake halafu akaendelea.

“ Siku moja mkurugenzi alikuja na kunikabidhi nyaraka za kusafiria na kunitaka niondoke nchini haraka sana kwa ajili ya usalama wangu kwani tayari nimekwisha julikana mahala ninakojificha.Niliondoka usiku huo kama mkimbizi nikielekea nchini japan.Tayari mkurugenzi alikuwa amekwisha suka mipango yote na nikafanikiwa kuingia nchini Japan kwa jina la Adrian Kusema nikiwa kama mtafiti wa kilimo ninayekwenda kufanya utafiti wa zao la mpunga.Mwenyeji wangu alikuwa ni mtu mmoja niliyemfahamu kwa jina moja tu la Yamazuka ambaye tayari alikwisha wasiliana na mkurugenzi wangu .Nilipelekwa katika kijiji kimoja cha wakulima wa mpunga ambako nilianza kujifunza kuhusu kilimo cha mpunga.Niliishi katika kijiji kile kwa muda wa miaka mitatu.Nilijifunza maisha ya ukulima.Watu wale walikuwa wakalimu sana.Walinifundisha mambo mengi .Yalikuwa ni maisha mazuri na niliyapenda.Nilijitahidi sana kuyazoea maisha yangu mapya na kuyasahau maisha yangu ya nyuma lakini pamoja na jitihada zote za kutaka kuyasahau maisha ya nyuma,bado picha ya usiku ule iliendelea kunitesa kila uchao.Kila nikifumba macho nilikuwa nikiwaona wenzangu namna walivyokuwa wakiuawa na mbaya zaidi ni ule moto mkubwa niliouona ukiiteketeza familia yangu.Nilishindwa kuiondoa kumbu kumbu ile kichwani kwangu hivyo kunilazimu kuondoka nchini japan nikaelekea Marekani ambako nilikutana na rafiki yangu mmoja aitwaye Jerry Washington ambaye anafanya kazi katika shrikika la ujasusi la marekani C.I.A.Huyu ndiye aliyenisaidia kufahamu kila kitu kuhusiana na kilichotokea siku ile usiku na hata mauaji ya familia yangu.” Mathew akainuka na kuchukua mvinyo akanywa kidogo na kuendelea

”Nchi ya Marekani kwa sasa ndiyo inayoongoza kwa uwekezaji mkubwa sana hapa Tanzania na katika eneo lote la afrika mashariki .Wamewekeza mabilioni ya dola katika sekta ya mafuta na gesi.Kwa sasa wanajenga kituo kikubwa kabisa cha mazoezi ya kijeshi cha wanamaji katika bahari kuu eneo la maji ya Tanzania.Hiki ni kituo kikubwa kabisa kuwahi kujengwa barani afrika.Kutokana na uwekezaji huu mkubwa ,serikali ya Marekani imelazimika kutafuta namna ambayo itayalinda maslahi yake katika eneo hili la ukanda wa afrika mashariki na ndipo walipounda kikosi kiitwacho Team SC41.Kikosi hiki kipo nchini Tanzania na kinaendeshwa kwa usiri mkubwa mno kiasi kwamba si rahisi kufahamu kama kuna kikosi kama hiki hapa nchini.Hata serikali ya Tanzania haifahamu chochote kuhusiana na uwepo wa kikosi hiki ndani ya ardhi yake.Team SC41 ni kikosi kidogo lakini hatari sana na kilichosheheni watu wenye uwezo mkubwa waliopata mafunzo ya hali ya juu nchini Marekani.Kikosi hiki kina uwezo wa kupata taarifa za kila kinachoendelea kila siku serikalini na lengo likiwa kuhakikisha maslahi ya marekani yanalindwa kwani uwekezaji huu mkubwa katika mafuta na gesi unauinua sana uchumi wa Marekani” Akanyamaza kidogo halau akaendelea

“ Makachero wa marekani walikuwa wakimfuatilia Faizat kwa siri toka alipotoka nchini Oman na kuzisoma nyendo zake.Hawakuwa na haraka ya kumkamata japokuwa uwezo huo walikuwa nao.Sisi hatukulifahamu hilo na ndiyo maana baada tu ya kupata taarifa za kuwepo kwa Faizat hapa nchini tulianza mara moja mikakati ya kumkamata bila kuishirikisha serikali ya marekani.Taarifa za mpango wetu ziliwafikia team SC41 hivyo wakawa wamejiandaa kutukabili ili tusiweze kufanikisha mpango wetu wa kumkamata Faizat.Hatukujua kilichokuwa kikiendelea hivyo wakatushambulia na lengo lao likiwa ni kuua kikosi chote kilichokwenda kumkamata Faizat. Hawakutaka siri ivuje kuhusiana kuonekana kwa Faizat hapa nchini.Ni mimi peke yangu niliyefanikiwa kutoka hai katika shambulio lile kwa hiyo ilikuwa lazima wanipate .Waliiteketeza nyumba na familia yangu wakiamini kwamba kwa kufanya vile watakuwa wamenichanganya kwa hiyo itakuwa rahisi kwao kunipata.Namshukuru sana mkurugenzi wangu Dr Wilbert Augustino ambaye alinisaidia nikatoroka nchini vinginevyo nisingekuwa hai mpaka muda huu.Kwa bahati mbaya Dr Wilbert naye alifariki dunia katika ajali tata.Hii yote ikiwa ni kazi ya Team SC41 .Mungu amrehemu sana Yule mzee” akasema Mathew na kunywa mvinyo kidogo halafu akaendelea.

“ Nikiwa nchini Marekani ,nilianza kufanya uchunguzi wa kina ili kujaribu kukifahamu kikindi hiki cha Team SC41 lakini juhudi zangu hazikufanikiwa kwa sababu kikundi hiki kinaendeshwa kwa usiri mkubwa mno na ni watu wachache hata ndani ya Pentagon wanaofahamu uwepo wa kikundi hiki hapa nchini kwa hiyo ni vigumu sana kuzipata taarifa zake.Kingine kikubwa nilichofanikiwa kukifahamu ni kwamba hapa nchini kikundi hicho kinaongozwa na mtu aitwaye John Mwaulaya Albert.Baada ya kukosa taarifa zake za kina niliamua kuachana nao na kujitahidi kuyasahau maisha yangu ya awali na ndipo nilipoanza kufanya kazi za kujtegemea.Kwa hiyo ndugu zangu naomba mtambue kwamba Team SC41 ni kikundi chenye nguvu lakini hatari sana.Ni watu wenye mafunzo na uwezo wa hali ya juu mno.” Akasema Mathew.Anitha na Noah walikuwa kimya kabisa wakisikiliza.

“ Kuna mawasli ambayo tunatakiwa tujiulize.Kwanza ni je Peniela ana mahusiano gani na kikundi hiki? Watu wale walioingia ndani mwa Penny walitoka na kuelekea moja kwa moja hospitali alikolazwa John Mwaulaya.Je wana mahusiano naye au wanamuwinda? Lakini je wanamuwinda kwa kitu gani hasa? Kama Peniela ana mahusiano yoyote na Team SC41 basi she is a very very dangerous woman.Na kama kweli ni Team SC41 basi nina hakika kabisa kwamba hata Edson aliuawa na watu hawa na kama ni hivyo basi lazima kuna sababu kubwa na ya msingi iliyopelekea kufanyika kwa mauaji hayo kwani team SC41 huwa inashughulika na masuala mazito yenye maslahi na nchi ya Marekani tu.Tuna kazi kubwa ya kufanya mbele yetu.I can say this is a victory or death.We have to get prepared for a big war” akasema Mathew.Anitha na Noah walikuwa kimya kana kwamba wamemwagiwa maji.Anitha akamtazama Mathew na kuvuta pumzi ndefu akasema

“ I’m scared.Real scared but I have to fight”

“ Me too.Hii ni mara yangu ya kwanza kuisikia Team SC41 “ akasema Noah.

“ Ndugu zangu naomba nisiwafiche hata mimi ninaogopa sana nikiwafikiria Team SC41.Tukio la siku ile usiku halitaweza katu kufutika kichwani kwangu.These people have got no souls.They are monsters.Lakini pamoja na hofu hiyo tuliyonayo sote lazima tupambane nao.Najua ni jambo la hatari kubwa sana kwani unapogusa Team SC41 unagusa taifa lenye nguvu kubwa ya kiuchumi na kijeshi duniani kwa hiyo hawako tayari siri zao zijulikane na kuvuruga uhusiano mzuri ilionao na nchi za afrika mashariki na ndiyo maana nikawaambia kwamba this is a victory or death..” Akasema Mathew.Noah akafuta jasho usoni na kusema

“ Mathew sisi tuko tayari kuingia katika mapambano na Team SC41 ,lakini kuna swali ninajiuliza .Je tunatafuta nini kwa Team SC41.Is this about revenge ?

“ Hata mimi nakubaliana na mawazo yako Noah.Lazima tunapoingia katika mapambano na hawa jamaa tufahamu tunapambana kwa ajili ya kitu gani.” akasema Anitha

Mathew akacheka kidogo na kusema

“ Mapambano haya si kwa ajili ya kulipiza . Msingi mkuu tunaoenda nao ni mauaji ya Edson.Tunatafuta nani alimuua na kwanini.Kadiri uchunguzi wetu unavyoendelea mambo mengi yanazidi kujitokeza likiwamo na hili la Team SC41 na mengine mengi ambayo yatajitokeza mbeleni,lakini naomba tusipoteze msingi mkuu wa kazi yetu yaani kuchunguza kifo cha Edson.Ndani ya mauaji ya edson kutaibuka mambo mengi mazito ndani yake.Kwa hiyo tutachunguza endapo kuna mahusiano yoyote kati ya Peniela na Team SC41,tutachunguza endapo Team SC41 walihusika katika mauaji ya Edson na kama walihusika basi tufahamu ni kwa nini.Endapo tutagundua kwamba Team SC41 walihusika katika mauaji ya Edson basi mapambano yetu na wao yataanzia hapo.” Akasema Mathew

“ Nimekuelewa Mathew lakini nina wazo moja, kwa nini basi tusianze kwanza kumchunguza Peniela na kufahamu uhusiano wake na Team SC41? Hii inaweza ikaturahishia kazi sana” Noah akauliza

“ Not yet Noah.Suala hili ni kubwa na tutalichimba hadi mzizi wake kwa hiyo suala la kumchunguza Peniela lina wakati wake.Kwa sasa tuelekeze nguvu katika suala la kesho.Tuna kazi ngumu sana kesho” akasema Mathew na majadiliano yakaendelea kuhusiana na kazi kubwa waliyokuwa nayo kesho.



*********************



Ni asubuhi nyingine tena,nchi ikiwa inaendelea na maombolezo kufuatiwa msiba mzto wa Dr Flora Johakim mke wa rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.Bado hakukuwa na taarifa rasmi zilizotolewa kuhusiana na nini kilichosababisha kifo chake cha ghafla.Salamu za rambi rambi zilimiminika toka kila pembe ya dunia,watu mbali mbali wakimpa pole Dr Joshua rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Jaji Elibariki akiwa miongoni mwa watu waliokuwa katika pilika pilika nyingi siku hii akastushwa na mlio wa simu .Akaitoa na kutazama mpigaji,alikuwa ni Peniela

“ Peniela !!...” akastuka kidogo.Hakuwa ametegemea kama angepigiwa simu na Penny

“Hallo Penny” akasema Jaji Elibariki baada ya kupokea simu ile

“ Jaji Pole sana kwa matatizo yaliyokupata.Nimestushwa sana na msiba wa mama mkwe wako” akasema Penny

“ Ahsante sana Penny.Ni mapenzi ya Mungu,yeye ndiye mwenye kutoa na kutwaa.Vipi unaendeleaje?

“ Ninaendelea vizuri Jaji Elibariki.” Akasema Penny

“ Nimekutafuta kwa siku kadhaa hukuwa ukipatikana kabisa.Nilipatwa na wasi wasi mkubwa kwamba pengine umepatwa na matatizo”

“ Naomba unisamehe sana Jaji Elibariki,nilipatwa na safari ya ghafla ikanilazimu kuondoka bila hata kuaga.”

“ Ok nashukuru kama umerudi salama.Siku nyingine usifanye hivyo.Unatupa wasi wasi sana sisi ambao tunajali usalama wako”

“ Ndiyo Jaji Elibariki.Siku nyingine sintofanya hivyo” akasema Penny halafu kikapita kimya kifupi

“ Jaji Elibariki samahani kwa kukusumbua mida hii lakini nimekupigia simu nina tatizo kidogo na ninahitaji msaada wako”

“ Una tatizo gani Penny?

“ Sintoweza kukueleza katika simu.Unaweza kupata muda sasa hivi tukaonana nikueleze?

“ Uko wapi mida hii? Akauliza Jaji Elibariki

“ kwa sasa niko nyumbani kwangu” akajibu Penny

Jaji Elibariki akafikiri kidogo na kusema

“ Ok ninapafahamu nyumbani kwako nitafika muda si mrefu.” Akasema Jaji Elibariki na kukata simu

“ Penny ana matatizo gani? akajiuliza jaji Elibariki akiwa bado amesimama katika maua

“ Yawezekana akawa na tatizo kubwa ngoja nikamuone” akawaza na bila kuaga mtu yeyote akaingia katika gari lake na kuondoka

“ Nina hakika lazima atakuwa na tatizo kubwa sana ambalo si rahisi kuelezeka simuni.Lazima nikamsikie ana tatizo gani kwani tayari nimekwisha jitolea kwa hali na mali kumsaidia ,kumlinda na kila anayetaka kumdhuru.Peniela tayari amekwisha niingia katika mishipa ya damu .Toka nilipokutana naye kwa chakula cha usiku,kichwa changu hakitulii,kila mara namfikiria yeye “ akawaza .

Penny alikuwa amejilaza kitandani wakati akiongea na jaji Elibariki

“ Mwili wote unaniuma kwa gwaride alilonichezesha Jason jana usiku.Dah ! Jason kweli ni kidume wa shoka.Mziki wake si mdogo.Anajua kuicheza ngoma na hachoki ana mapafu kama ya farasi.” Akawaza Penny halafu akainuka na kwenda kuchukua glasi ya maji ya matunda

“ Kwa kweli jana Jason amenikuna kiswa sawa na kunifikisha ninapopataka.Ni bahati mbaya sana kwamba siwezi kuwa na kijana huyu katika maisha yangu ingawa ninatamani sana kama angekuwa ni mume wangu nikaishi naye mpaka kifo kitutengenishe.Lakini haiwezekani kwa sababu tayari nimekwisha yaharibu maisha yangu na hayawezi kuwa sawa tena.Sintoweza kupata furaha kamwe..” akawaza Penny na kwenda sebuleni akajilaza sofani

Kengele ya getini ndiyo iliyomstua Penny toka katika kijiusingizi kilichoanza kumpitia.Akainuka na kwenda getini.Alikuwa ni Jaji Elibariki

“ Hallo jaji Elibariki.Karibu sana” akasema Penny na kumkaribisha ndani Elibariki kwa furaha

“ Karibu ndani Jaji Elibariki” Penny akamkaribisha sebuleni

“ Penny just call me Elibariki or Eli.Hayo mambo ya Jaji tuyaache mahakamani.” Akasema Jaji Elibariki na kumfanya Penny atabasamu

“ Ok Eli” akasema Penny huku akicheka kidogo

“ Eli unatumia kinywaji gani? akauliza Penny

“ Naomba mvinyo kidogo kama upo.” Akasema Jaji Elibariki.Penny akamtazama na kutabasamu akaenda na kuchukua chupa ya mvinyo akamminia Elibariki katika glasi

“ Pole sana Jaji Elibariki kwa matatizo yaliyowapata.Dr Flora alifariki kwa ugonjwa gani?

“ Mpaka sasa bado hakuna taarifa rasmi iliyotolewa lakini kwa muda mrefu sasa Dr Flora alikuwa akisumbuliwa na shinikizo la damu na ninaamini hicho ndicho kilichomuua”

“ Pole sana Eli”

“ Nimekwisha poa Penny.Vipi wewe unaendeleaje ?

“ Ninaendelea vizuri sana Eli.Vipi wewe unaendeleaje?

“ Ninaendelea vizuri pia.Wasi wasi wangu ulikuwa ni juu ya usalama wako”

“ Nashukuru sana Eli kwa kunijali.” Akasema Penny na kimya kifupi kikapita

“ Nimestuka sana uliponiambia kwamba una tatizo nikaona nikimbie mara moja nije nikuone.Una tatizo gani Penny? Akauliza Jaji Elibariki

“ Eli nina tatizo ambalo nataka nikueleze lakini kwanza unaonekana umechoka sana.Unaonekana hukupata usingizi wa kutosha usiku.Hii ni hatari kwako Jaji Elibariki kuendesha gari katika hali hii.You need some rest” akasema penny

“ Ni kweli nimechoka Penny.Mambo yalikuwa mengi sana msibani.”

“ Ok Jaji Elibariki,naomba kwanza kabla ya kurejea msibani upate wakati wa kupumzika walau kidogo hapa kwangu .”

“Penny nikitoka hapa nitaelekea moja kwa moja nyumbani kupumzika.”

“ Hapana Elibariki.Huwezi kuendesha gari ukiwa katika hali hii ya uchovu. Utapumzika hapa na utakapoamka utakuwa tayari kuendelea na majukumu mengine.Naomba usiogope Jaji Elibariki.Hapa ni sehemu salama” akasema Penny.Jaji Elibariki hakujibu kitu akatabasamu

“ Kabla ya kupumzika,twende nikupeleke ukaoge kwanza ili uondoe uchovu.Ninayafahamu mambo ya msiba yanavyokuwa,hutapata hata wasaa wa kujimwagia maji”

“ Kweli kabisa Penny.Mambo ya msibani ni mengi mno” akasema jaji Elibariki.Penny akainuka na kumuongoza hadi chumbani kwake akamfungulia bafu ili Jaji Elibariki aweze kujimwagia maji.

“ Dah ! Kweli Penny anajua kuchunguza watu.Ni kweli nimechoka sana na ninahitaji mapumziko.Toka jana sijapata wasaa wa kupumzika.” Akawaza Jaji Elibariki huku akivua nguo akijiandaa kujimwagia maji

“ Penny anataka kunieleza nini? Ana tatizo gani? akajiuliza

“ Sikuwahi hata mara moja kuingia katika nyumba ya Penny.Ni kubwa na nzuri.Dah ! Penny ni mzuri jamani.Ukimuangalia tu hadi unapatwa na msisimko “ akawaza Jaji Elibariki na mara mlango wa bafuni ukafunguliwa.Jaji Elibariki alipatwa na mstuko wa mwaka.Hakuamini kile alichokuwa akikiona.Macho yalimtoka pima.

“ P…pe..Pee..” akataka kusema lakini maneno hayakutoka

Mlangoni alikuwa amesimama Peniela akiwa na tabasamu usoni huku akiwa mtupu kama alivyozaliwa





Jaji Elibariki alipangusa maji usoni ili aweze kuangalia vizuri kitu alichokuwa akikiona mbele yake.Haikuwa ni ndoto,msichana aliyesimama mbele yake alikuwa ni Peniela akiwa mtupu huku akitabasamu

“ Ouh my..!!...” Jaji Elibariki akashangaa.

“ Penny..what..what are you doing here ?!! akauliza kwa sauti yenye kukwama kwama

“ Relax Eli.” Akasema Peniela kisha akafunga mlango wa bafu na kuanza kupiga hatua akimsogelea Jaji Elibariki ambaye bado aliendelea kumtumbulia macho asiamini alichokiona.Penny akamsogelea karibu

“ Aren’t you happy to have a bath with me Eli? Akaliza Penny kwa sauti laini.Jaji Elibariki alishindwa aseme nini .Mapigo ya moyo wake tayari yalikwisha anza kwenda mbio .Umbo zuri la Peniela lilimchanganya mno.

“ What do you want Penny? Akauliza Jaji Elibariki

“ What do you want from me Eli? Penny naye akauliza

“ I want you out of here” akasema Jaji Elibariki.Penny akatabasamu na kusema

“ No Eli.You don’t want me to go away.You want me so badly just like I want you.” Akasema Peniela na kumsogelea Jaji Elibariki ,akamkumbatia na kuzigusisha chuchu zake za moto katika kifua cha Elibariki na ghafla maeneo nyeti yakakasirika na kusimama.Elibariki akaanza kutweta ,mwili wote ukamsisimka .

“ Siamini kama jambo hili linatokea kweli.Nilikuwa nikitafuta sana fursa kama hii ya kujivinjari na mtoto mzuri kama huyu lakini leo imekuja yenyewe.Peniela amekuwa katika kichwa changu na kunifanya nimfikirie kila saa.Hii ni ndoto au ni kweli? Akajiuliza Jaji Elibariki.Taratibu akiinua mikono yake na kuanza kuipitisha katika mgongo wa Penny

“ Hapana si ndoto.Hii ni kweli.Niko na Peniela.Huyu mtoto ni kama mchawi amejuaje kwamba nimekuwa nikimuota usiku namchana? Amejuaje kwamba nilikuwa nikiitafuta kwa udi na uvumba fursa kama hii? Akaendelea kuwaza jaji Elibariki akiwa amefumba macho huku akisikia raha ya aina yake wakati mikono ya Penny ikichezea ikulu iliyokuwa imekasirika na kusimama kwa hasira.

“ Ouh Penny…ouh..aah...” akalalama Jaji Elibariki.Penny hakumjali akaendeleza utundu wake kwa kutumia mikono halafu taratibu akapiga magoti na kuanza manjonjo kwa kutumia mdomo wake.Jaji Elibariki nusura apige ukulele kwa raha aliyoisikia akajikaza na kubaki akilalama.

“ I’m yours Eli.I want you now so badly.Please hold me tight in your hands ” akasema penny kwa sauti lain iliyokuwa ikitokea puani.Jaji Elibariki alikuwa katika hali mbaya na hakuweza tena kuvumilia.Wakaingia mchezoni.Ulikuwa ni mpambano mkali baina ya Jaji Elibariki na Peniela.Ni Elibariki ambaye alionyesha kuutawala mchezo.Alibadili kila aina ya mfumo wa uchezaji ili mradi kujihakikishia ushindi mnono mwisho wa mchezo.Hadi wanamaliza raundi ya kwanza wote walikuwa wakitweta kama wakimbiaji wa mbio ndefu.

“ Thank you Eli.Thank you so much” akasema Peniela huku akitabasamu .Jaji Elibariki hakusema kitu alikuwa ameinama akitweta.Alionekana kuwa na mawazo mengi.

“ Unawaza nini eli? Akauliza penny

“ Ni mara yangu ya kwanza kuisaliti ndoa yangu” akasema Elibariki

“ C’mon Eli..Huna sababu ya kusikitika .You wanted this ,right? Akauliza penny.Elibariki hakujibu kitu akabaki akimuangalia

“ Yes you wanted this so badly.Toka siku ya kwanza nilipokutana nawe kwa chakula cha usiku nilibaini kwamba ulikuwa ukinihitaji sana. Sina sababu yoyote ya kunizuia kukupatia kile unachokihitaji kwa sababu wewe ni mtu muhimu sana katika maisha yangu na zaidi ya yote hata mimi nilikuwa nakuhitajipia. Hii ni ahsante yangu kwako Elibariki kwani bila ya wewe hivi sasa ningekuwa gerezani.kwa hiyo usijisikie vibaya.Hujafanya kosa lolote.” Akasema penny huku akimchezea Jaji Elibariki kifuani.

“ Penny..” Elibariki akataka kusema neno lakini Penny akamzuia.

“ Don’t say anything Eli.” Akasema Penny

“ Spend this day with me Eli.I need you so badly today”

Elibariki akambusu na kusema

“ Penny you are wonderfull woman.Unajua kuyasoma mawazo ya mtu.Ni kweli nilikuwa nakuhitaji sana lakini nilishindwa namna ya kuweza kukupata. Penny mimi nina mke wa ndoa na ninampenda lakini sielewi ni kitu gani kimenitokea kwani baada ya kuanza kusikiliza kesi yako nilijikuta nikianza kuvutiwa nawe na kila nilipokuona ndivyo moyo wangu ulivyozidi kuvutwa kwako kama sumaku.Mimi ni mtu mwenye msimamo sana hususani katika kuilinda ndoa yangu lakini kwako nimeshindwa kuwa na msimamo na kwa mara ya kwanza nimejikuta nikiisaliti ndoa yangu.Penny nakupenda sana na ndiyo maana nikafanya kila linalowezekana kukuachia huru na bado ninaendelea kufanya kila linalowezekana kuhakikisha kwamba unakuwa na maisha mazuri na yenye furaha na amani.For you I’m ready for anything”akasema Jaji Elibariki.Penny akatabasamu akambusu Elibariki na kusema

“ Eli ulichokuwa ukiwaza na ndicho mimi nilichokuwa nikikiwaza.Nilipokuona tu mara ya kwanza nilianza kuvutiwa sana nawe.I need someone like you.Wewe ni mtu mwelewa ,unayejua kupenda na unayejali.Sintajali kama una mke lakini hata mimi nakupenda sana Eli.Niko tayari kukupatia kila kitu zaidi ya anavyokupatia mkeo .Nitakupa kila aina ya raha ya dunia hii na sintahitaji kitu chochote toka kwako zaidi ya penzi lako tu.” Akasema Peniela .Elibariki akatabasamu na kusema

“ Usijali Penny.Kuanzia sasa hutanikosa muda wowote ukinihitaji.Antime you need me just call my name and I’ll be there.Kwako ninahisi furaha ya ajabu niliyoikosa kwa miaka mingi.Nikiwa nawe najiona kama niko peponi.Unajua kunichanganya sana.” Akasema Jaji Eibariki.Peniela akafurahi na kuendelea kumwagia mabusu mfululizo.Baada ya dakika kadhaa wakaingia tena katika mzunguko wa pili.Hadi wanamaliza peniela alikuwa hoi na hakutaka tena waendelee kwani simu ya elibariki ilikuwa ikipigwa sana bila kupokelewa.

“ Elibariki nashukuru sana kwa raha ulizonipa..Sijawahi kupewa raha ya namna hii na mtu yeyote Yule .Natamani kama tungeendelea lakini kwa sasa unahitajika msibani ndiyo maana hawaishi kukupigia simu.Tafadhali kama ukipata muda jioni ya leo unaweza ukatoroka na kuja kuniliwaza kidogo? I feel so lonely .I need someone by my side.Nitafarijika sana kama nikipata wasaa wa kuwa nawe jioni ya leo” akasema Penny huku Jaji Elibariki akitabsamu kila alipoendelea kuushuhudia uzuri wa kipekee wa Peniela akiwa mtu.

“ usijali penny.Nitakuja jioni ya leo.Hata mimi nahitaji faraja hususani katika kipindi hiki cha matatizo .Licha ya msiba wa mama mkwe lakini hata mimi nina matatizo yangu binafsi na ninahitaji faraja.Wewe ndiye utakayekuwa mfariji wangu Peniela kwa hiyo usihofu jioniya leo nitakuja na ikiwezekana usiku wote nitakuwa nawe.” Akasema jaji Elibariki na kumfurahisha sana Penny .Baada ya mapumziko Elibariki akaagana na Penny akaondoka kuelekea nyumbani kwake kubadili nguo kabla ya kuelekea msibani.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“ Good.Mpango wangu unakwenda vizuri kama ninavyotaka.Tayari wote nimewatia mikononi.Dah ! wanaume kukamatika ni kitu kidogo .Ni majasiri kwa nje lakini kwa ndani wana udhaifu mkubwa sana.Ninachokisubiri sasa ni boom ” Akawaza Penny baada ya jaji Elibariki kuondoka.

“ Inaniuma sana kwa ninachotaka kukifanya lakini sina budi kukifanya.Hii ni kwa faida yao wenyewe.Hakuna namna ninayoweza kuwashawishi wakaachana na mpango wao wa kuchunguza kifo cha Edson .Kuendelea kuchunguza mauaji yale ni hatari sana kwa usalama wao na mimi sitaki wadhurikike hata kidogo “ akawaza Penny

“ Ngoja nijilaze nipumzike.mwili wote hauna nguvu hata kidogo.Nimekimbizwa mchaka mchaka na Jason usikukucha na sasa hivi nimekutana na gwaride lingine la Elibariki.” Akainama akazama katika mawazo

“ lakini nitaendelea na maisha haya ya kuutumiamwili wangu kwa ajili ya kila ninachokihitaji hadi lini? Mwili wangu umekuwa ndiyo suluhisho la kila kitu.I’m tired with this kind of life.Nahitaji kuishi maisha ya kawaida kama wenzangu wanavyoishi” akawaza Penny na kujitupa kitandani



*****************




Ni saa nne za asubuhi,Mathew na wenzake tayari wamekwisha jiandaa kwa kazi kubwa waliyonayo katika siku hii.

“ Kila kitu kiko sawa? Akauliza Mathew

“ Kila kitu kiko sawa sawa.” Akajibu Noah

“ Anitha mitambo yako yote iko sawa sawa? Mathew akamuuliza Anitha

“ Ndiyo,kila kitu kiko sawasawa.”

“ Ok guyz.Kila kitu ni kama tulivyokipanga.Kama hakuna tatizo its time now” akasema Mathew halafu akaingia katika gari akaondoka.Noah na Anitha nao wakaingia katika gari lingine nao wakaondoka.Mathew alielekea moja kwa moja Mseko hospitali anakofanyia kazi Dr Michael.Noah na Anitha wakaelekea Tanganyika Internation school anakosoma Michael Jr mtoto wa Dr Michael.

“ Anitha kuna jambo ambalo nataka nikuweke wazi wewe kama rafiki yangu wa siku nyingi ila naomba usimwambie Mathew” akasema Noah wakiwa garini

“ jambo gani Noah? Akauliza Anitha aliyekuwa makini katika usukani

“ Nimefikiria sana kuhusu hatari iliyoko mbele yetu.Kuna kitu nimekigundua.Mathew is using us”

“ using us ?!Anitha akashangaa

“ yes ! he’s using us”

“ Hebu nieleweshe Noah.Mathew anatutumia kivipi?

“ Anatutumia kwa ajili ya kulipiza kisasi kwa Team SC41”

“ You are wrong Noah.”

“ Kweli nakwambia Anitha.Mathew anatutumia kulipiza kisasi.Sikufichi ningejua kama kazi ninayokuja kuifanya ni hii katu nisingekuja.Hii ni kazi ya hatari kubwa sana.”akasema Noah.Anitha akapunguza mwendo wa gari na kulisimamisha pembeni mwa barabara,akashuka na kwenda kuufungua mlango upande aliokaa Mathew

“ get out of the car “ akasema kwa ukali

“ Kwani vipi Anitha?

“ Ninasema shuka !! akafoka

“Kwani vipi Anitha?Kumetokea nini?

“ Kwa taarifa yako sisi hatukutegemei wewe katika kazi hii.Hata usipokuwepo wewe bado nitaendelea kumsaidia Mathew kuifanya kazi hii na tutafanikiwa tu.Kwa hiyo una sekunde thelathini za kufanya maamuzi.Unaendelea na sisi au unaachana nasi” akasema anitha kwa ukali

“ I’m sorry Anitha.Nilikuwa nakupima tu.Ingia garini twende tunachelewa” akasema Noah huku akicheka.Antha akamtazama kwa makini halafu akaubamiza mlango kwa hasira akarejea garini na kuwasha gari wakaendelea na safari

“ Nimeanza kuwa na wasi wasi mkubwa na huyu Noah.Sina hakika kama atavumilia kuwa nasi muda wote.Mtu huyu anaweza kuwa hatari sana kwa usalama wetu.Kuanzia sasa nitaanza kumchunguza kila anachokifanya” akawaza Anitha

“ Anitha usinielewe vibaya ndugu yangu,sikuwa nikimaanisha chochote kwa maneno yale niliyokwambia.Unajua siku nyingi sijakutania kwa hiyo nilitaka kukuchemsha kidogo.Mathew ni mtu wangu wa karibu sana na niko tayari kufa kwa ajili yake.Amenitoa mbali hadi kunifkisha hapa.It was just a joke” akasema Noah huku akicheka.Anitha hakujibu kitu akaendelea kuendesha gari kimya kimya

Waliwasili Tanganyika international school,wakasimamisha gari katika maegesho ya magari.Ilipata saa tano na dakika kumi na tatu

“ Tumejitahidi sana kwenda na wakati” akasema Anitha akachukua simu yake na kumpigia Lydie akamfahamisha kwamba tayari wamekwisha wasili pale shuleni.Baada ya dakika kama kumi hivi ,Lydie akatoka akiwa amemshika mkono mtoto mdogo .Moja kwa moja akanyoosha katika gari la akina Anitha wakaingia ndani kisha wakaondoka.

Walifika katika kituo cha mafuta cha Alnoor,Anitha akamuomba Lydie ashuke wakaelekea katika vyoo .

“Lydie,mzigo wako huu hapa.Milioni saba kamili”akasema Anitha akitoa mabunda ya noti katika mkoba wake na kumkabidhi Lydie.

“Ahsante sana Anitha”akasema Lydie huku akizipakia noti zile katika mkoba wake.

“ Ok nitakuacha hapa utachukua taksi mpaka nyumbani kwako utachukua begi lako na utaelekea ubungo.Natumai mpaka mida hii bado kuna magari ya kuelekea Arusha.Panda basi na uondoke Dar es salaam leo hii.Nenda kaanze maisha mapya.Nakutakia maisha mema” akasema Anitha

“ Ahsante Anitha”akajibu Lydie.Anitha akarejea garini na kumuachia Noah usukani yeye akakaa nyuma ya gari na Michae Jr.

“ tayari tumempata mtoto” Anitha akamtaarifu Mathew.

“ Good job Anitha.Ok sasa twende hatua ya pili.Umekwisha kamilisha kila kitu?

Akauliza Mathew

“Kila kitu tayari Mathew.Utatumia jina lile lile la Dr Emanuel kaboba.Tayari nimekwisha ingiza kila kitu .Ninaingia katika mtandao wa hospitali na muda si mrefu nitakuwa nikikuona na kukupa maelekezo.hata sisi tuko njiani tunaelekea huko” akasema Anitha

“ Where is my aunt Lydie ? akauliza Michael Jr

“ Your aunt has got an emergency .We’re taking you to your father” akajibu Anitha

Wakati akiongea na Anitha Mathew alikuwa mbali kidogo na hospitali.Alipohakikishiwa kwamba kila kitu kiko tayari,akawasha gari na kuelekea hospitali,akipita katika geti wanalopitia madaktari.Aliegesha gari katika maegesho na kwa haraka sana akaangaza macho na kuliona gari la Dr Michael.

“ Good..Dr Michael bado yupo”akasema kimoyo moyo na kupeleka kidole chake sikioni akakigusa kile kifaa cha mawasiliano kilichomo sikioni

“ Anitha nimekwishafika,sasa naingia ndani ya jengo la ofisi.Tayari mmekwisha fika? Akauliza Mathew

“ Tunakaribia kufika Mathew lakini tayari nimekwishaingia katika mtandao wa hospitali na tayari ninaziona kamera.Ok you can go in now” akasema Anitha

Taratibu Mathew akaanza kupiga hatua kuelekea katika jengo lenye ofisi za madaktari.Alipoukaribia mlango ukafunguka akajikuta ametokeza katika kijichumba Fulani ambacho kulikuwa na mashine mfano wa zile mashine za kutolea fedha.

“ Anitha niko katika ile mashine yenye kusoma alama za vidole” akasema Mathew.

“ Ok ingiza namba zile nilizokupa halafu weka mkono wako wa kulia na baada ya sekunde kumi itasoma na mlango utafunguka.” Akasema Anitha

Mathew akaisogelea mshine ile akabonyeza namba alizokuwa amepewa na Anitha halafu akaweka kiganja cha mkono mahala palipochorwa alama ya vidole.Baada ya sekunde kumi kama alivyokuwa ameambiwa na Anitha ikawaka taa ya kijani na maandishi yakatokea

“ Thank you Dr Emanuel Kaboba.Now you can go in” Mara mlango ukafunguka.Mathew akatabasamu na kuingia ndani.

“ Tayari niko ndani” akasema Mathew

“ Ok Mathew.Ofisi ya Dr Michael iko ghrofa ya pili chumba namna 35. “ akasema Anitha.Mathew hakutaka kupanda lifti akapanda kwa miguu hadi ghorofa ya pili na moja kwa moja akaelekea chumba namna 35 alichoelekezwa kwamba ndicho chumba cha Dr Michael.Alikuwa akikutana na madaktari wakati akipanda lakini hakuna aliyemtilia wasi wasi kwani huwezi kuingia ndani ya jengo lile bila kuwepo katika mfumo wa kompyuta wa pale hospitalini.

Moja kwa moja Mathew akaelekea chumba namba 35 akagonga mlango na sauti toka ndani ikamruhusu aingie

“ Dr Michael” akasema Mathew huku akitabasamu.Dr Michael akainua kichwa na kumtazama Mathew.Akastuka kidogo kwani hakuwahi kumuona.

“ Dr….” Akasema Dr Michael huku akimshangaa Mathew

“ Dr Emanuel Kaboba” akasema Mathew hukuakimpa mkono Dr Michael

“ Ouh Dr Emanuel ,are you new here? Akauliza Dr Michael

“ Yes I’m new here” akajibu Mathew halafu akatoa kitu Fulani kama simu akakiweka mezani na kubonyeza kitufe chekundu chenye maandishi Scan.Baada ya sekunde kama ishirini hivi kikatoa ukelele

“ Mathew tayari tumekwisha scan chumba chote .Hakuna kitu chochote kilichofungwa cha kumfuatilia Dr Michael.Unaweza kuendelea” Anitha akamtaarifu Mathew ambaye alikichukua kifaa kile na kukirudisha mfukoni.

“ What can I help you Dr Emanuel? Akauliza Dr Michael huku akiendelea kumshangaa Mathew.Mathew akainuka na kuchomoa bastora mfukonihttp://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“ Dr Michael mimi si daktari ila nimekuja hapa kwa sababu nina shida kubwa na wewe” akasema Mathew na Dr Michael aliyekuwa amepatwa na mstuko mkubwa akataka kusimama

“ Kaa chini Dr Michael.Kuanzia sasa utafuata kile nitakachokuelekeza.!

“ Unataka nini toka kwangu? Wewe ni nani? Akauliza Dr Michael kwa wasi wasi

“ Anitha,niko na Dr Michael hapa .Niunganishe na mwanae” Mathew akamwambia Anitha

“ Ok Mathew,angalia simu yako”

Mathew akachukua simu yake na mara picha ya Michael Jr akiwa ndani ya gari ikatokea,akampatia Dr Michael ile simu.Alistuka sana alipoiona sura ya mwanae.Mwili ukamtetemeka.

“ Huyu ni mtoto wangu Michael” akasema

“ Ndiyo ni mtoto wako lakini kwa sasa tunaye sisi “

“ Mnaye ninyi? Kivipi mko naye ninyi wakati yuko shule? Ninyi ni akina nani? Akaulzia Dr Michael kwa wasi wasi mwingi

“ Dr Michael mwanao tumemtoa shuleni,yuko nasi .Hatuna lengo baya na mwanao kama utatupa ushirikiano tunaoutaka” akasema Mathew

“ Mbona sikuelewi.Mwanangu yuko wapi? Akasema Dr Michael kwa hamaki na kutaka kuinuka

“ Shhhh..kaa hapo hapo ulipo na tafadhali usipaaze sauti.Ukitaka mwanao aendelee kuwa hai tafadhali fuata kile ninachokuelekeza kufanya” akasema Mathew kwa ukali

“ Ok Ok..niambie unataka nini? Tafadhali naomba msimuumize mwanangu wala kumfanya kitu chochote kibaya.Niko tayari kufanya unachokitaka” akasema Dr Michael kwa wasi wasi

“ Nataka unipeleke chumba PV2 – 78” akasema Mathew.Dr Michael macho yakamtoka pima.Alistuka mno.Midomo ikabaki ikimcheza.





Dr Michael alimuangalia Mathew kwa uoga mkubwa.

“ Unataka nikupeleke PV2 – 78? Akauliza

“ Ndiyo nataka unipeleke huko” akajibu Mathew.Dr Michael akamtazama kwa macho makali na kuuliza

“ Wewe ni nani? Unataka kwenda kufanya nini kule wakati si daktari?

“ Dr Michael naomba tusiendelee kupoteza wakati.Nimesema nipeleke PV2 – 78..!! Mathew akasema kwa ukali huku amemuelekezea Dr Mathew bastora.Dr Mathew akaogopa sana ,akamtazama Mathew machoni na kugundua hakuwa akihitaji masihara.Akajikaza na kusema

“ Samahani ndugu yangu ,naomba usikasirike na tunaweza tuaongea bila kunielekeza hiyo silaha mkononi.Mnaye mwanangu kwa hiyo sina ujanja tena nitafanya kila mtakachoniamuru kufanya kwa ajili ya kumuokoa .Nitakupekeka huko unakotaka lakini naomba unifahamishe mambo machache.” Akasema Dr Michael

“ Mambo gani unayohitaji kufahamu Dr Michael?

“ Ninahitaji kufahamu kuhusiana na mgonjwa aliyelazwa katika chumba unachohitaji nikupeleke kwa sababu sina mahala ninapoweza kwenda kuuliza chochote kuhusiana na mgonjwa yule.Mambo yanayotendeka mle si ya kawaida.”

“ Kwa nini unasema hivyo? Akauliza Mathew

“ Kuna mambo yanayoendelea yasiyo ya kawaida kuhusiana na Yule mgonjwa.Ni mgonjwa anayeonekana kufichwa fichwa sana na hata ugonjwa wake unatibiwa kwa siri.Matibabu yake ni ya siri na nilipewa jukumu la kumuhudumia mgonjwa Yule kwa sharti maalum kwamba mtu yeyote asifahamu kinachoendelea kuhusiana na ugonjwa wake .Katika chumba kile si rahisi kwa mtu ambaye si daktari au hafahamiki na vijana wanaomlinda mtu Yule kuingia ndani ya kile chumba.Kuna vijana wanaomlinda kwa saa ishirini na nne.Nimewachunguza vizuri sana wale vijana wana vifaa maalum vya mawasiliano na wanatembea na bastora.Naomba unieleze mtu Yule ni nani? Ni kiongozi wa serikali? Nina wasi wasi pengine ninawea kuwa ninamuhudumia mtu hatari bila kujua” Akaulzia Dr Michael

“ Dr Michael swali lako kwa sasa ni gumu kulijibu .Naomba tusiendelee kupoteza wakati nipeleke mara moja mahala ninakotaka unipeleke.” Akasema Mathew.Dr Michael akavuta pumzi ndefu na kumuangalia Mathew kwa macho makali akasema

“ Mmemteka mwanangu na kwa sasa umenielekezea silaha huku ukiniamuru nifanye unavyotaka .Naomba ufahamu kwamba mgonjwa Yule yuko chini yangu na nilikabidhiwa kwa sharti kwamba chochote kitakachomtokea kitakuwa ni juu yangu kwa hiyo nina haki ya kufahamu.Kama una jibu la swali langu tafadhali ninaomba unipatie kwa sababu hakuna mahala ninakoweza kuuliza na kupata majibu kuusiana na mgonjwa Yule.Nina mashaka mno na maisha yangu yanaweza kuwa hatarini kutokana na mazingira yaliyomzunguka Yule mgonjwa na endapo nikifanya hata kosa moja ninaweza kujikuta katika hatari kubwa.” Akasema Dr Michael,Mathew akamtazama na kusema

“ Nitakueleza kila kitu lakini kwanza nipeleke katika chumba hicho”

“ Ninaogopa sana endapo wale vijana wanaopeana zamu kumlinda Yule mgonjwa watagundua kwamba wewe si daktari,nitakuwa nimejitafutia matatizo mimi mwenyewe na wanaweza wakanifanyia kitu kibaya”

“ Dr Michael hii ni kauli yangu ya mwisho Naomba unipeleke katika chumba hicho haraka.Ninafahamu kwamba siwezi kuingia kule bila ya wewe na ndiyo maana nimekuja hapa.Usinilzimishe nitumie nguvu.Kumbuka tunaye mwanao na kauli yangu moja tu mwanao hutamuona tena.Kwa hiyo naomba tuachane na mabishano na ufanye kile ninachokitaka ukifanye !! akafoka Mathew..Dr Michael hakutaka tena mabishano akafungua kabati lake na kumpatia Mathew koti jeupe

“ Vaa koti hili uonekane kama daktari.Vijana wale hawawezi kukuruhusu uingie kama wakigundua wewe si daktari.Kitu kingine ni kwamba hautakiwi uingie na silaha mle ndani kwani kabla ya kuniruhusu nianze kumtibu mgonjwa wao huwa wananikagua kwanza na chombo maalum kuhakisha kwamba sina silaha ya aina yoyote ile na hata dawa ninazompatia huwa wanazikagua kama zina sumu au kitu chochote cha hatari.Ndiyo maana nina maswali mengi sana kuhusiana na mgonjwa Yule ni nani? Akauliza Dr Michael.Mathew hakumjibu kitu akavaa koti lile akaonekana kama daktari halisi

“ Ok twende unipeleke , na tafadhali usijaribu kluonyesha dalili zozote kama nimekulazimisha kitu.Nataka watu watuone kama ni watu tunaofanya kazi pamoja.Nakukumbusha tena kosa moja tu na mwanao hutamuona tena” akaamuru Mathew .Dr Mathew hakujibu kitu akafungua mlango na kutoka Mathew akamfuata

“ We’re on move” Mathew akawataarifu akina Anitha

“ Ok Mathew ,tunakufuatilia kwa karibu sana,mpaka sasa hatujaona bado hatari yoyote” akasema Anitha

Hakuna aliyeweza kuhisi chochote kilichokuwa kinaendelea baina ya Dr Michael na Mathew.Walionekana kama ni madaktari waliokuwa katika shughuli zao za kawaida.Walitembea kwa haraka hadi walipolifikia jengo ilimo wadi PV2 – 78

“ Tunaingia ndani ya jengo la wadi” akasema Mathew akiwapa taarifa wenzake.Walipanda lifti hadi ghorofa ya nne wakashuka na kuelekea moja kwa moja chumba PV2 – 78.Dr Michael alionekana wazi kuwa na wasi wasi mwingi sana.Mathew yeye hakuwa na wasi wasi sana na alikwisha jiandaa kwa lolote

Waliufikia mlango wa chumba PV2 – 78 wakasimama.Dr Michael akasita kidogo.Mathew akamkata jicho kali Dr Michael akaogopa na kugonga mlango mara tatu.Sekunde zilikatika bila ya mlango kufunguliwa akagonga tena na safari hii pia hakukuwa na majibu yoyote.Hakuna mtu aliyejitokeza kuufungua mlango.

“ Hii si kawaida yao.Siku zote ninapogonga mara tatu hunifungulia mlango ,sielewi leo nini kimetokea” akasema Dr Michael kwa wasi wasi

“ Gonga tena” akasema Mathew na Dr Michael akafuata maelekezo akagonga tena lakini bado hakukuwa na majibu.Kengele ya hatari ikagonga kichwani kwa Mathew,akaupeleka mkono ilipo bastora yake na kuishika.Akamwambia Dr Michael akinyonge kitasa na kuufungua mlango.Taratibu na kwa uoga mwingi akakinyonga kitasa na mlango ukafunguka wakaingia ndani.Dr Michael alipatwa na mshangao wa mwaka,alihisi miguu ikimuisha nguvu.Kitu cha ajabu kilikuwa kimetokea.John Mwaulaya hakuwepo mle chumbani.Chumba kilikuwa kitupu.

************

Kila mtu katika ofisi ile ya wanasheria aliiona furaha aliyokuwa nayo Jason.Toka amefika ofisini alikuwa mchangamfu sana na uso wake ulitawaliwa na tabasamu muda wote.Alisalimiana na kila mtu kwa furaha na utani mwingi kitu ambacho hakikuwa kawaida yake kwani siku zote Jason huwa ni mtu mwenye pilika pilika nyingi hivyo hakuwa akitaniana na wenzake.

Aliingia ofisini kwake ,akavua koti halafu akalegeza tai na kujimiminia mvinyo kidogo katika glasi akanywa na kukaa juu ya meza.Ni picha moja tu iliyokuwa imekitawala kichwa chake kwa wakati huo.Picha ya msichana mrefu wastani ,mwenye umbo la kuvutia na tabasamu la kimalaika,iliufanya uso wake usikaukiwe na tabasamu

“ peniela..!!..” akasema kwa sauti ndogo halafu akamalizia mvinyo katika glasi

“ Bado siamini kama ndoto yangu ya siku nyingi imetimia.Peniela alikuwa akilini mwangu kwa muda mrefu sana.Toka nilipoonana naye tukafahamiana nilianza kumpenda.Moyo wangu umekuwa ukiugulia ni lini nitampata malaika Yule lakini hatimaye sasa ndoto imekuwa kweli.Peniela ana kila kitu ninachokihitaji kwa mwanamke wa maisha yangu.” Akawaza halafu akainuka na kwenda kuketi kitini,bado mawazo yakiendelea kumuandama

“ Nakiri katika maisha yangu sijawahi kukutana na mwanamke aliyenipa raha na kuufanya moyo wangu uwe na furaha kama Peniela.Anayafahamu mapenzi,anajua mwanaume anahitaji nini,.Ouh gosh ! usiku wa jana ni usiku wa kihistoria kwangu .Nilijivinjari nitakavyo na Peniela mwanamke asiyeisha hamu.Kila baada ya mzunguko nilijikuta nikihitaji tena na tena.Dah !..sintausahau usiku ule” akaendelea kuwaza

Picha ya mambo waliyoyafanya na Penny usiku ikamjia kichwani na mara akahisi ikulu imeanza kukasirika na kufura .Mwili wote ulikuwa unamsisimka.

“ Peniela amekiteka kichwa changu.Akili yangu yote inamuwaza yeye tu.Sina hamu ya kufanya chochote leo,nahitaji kuwa naye tu karibu.Natamani muda huu angekuwa mikononi mwangu nikimbembeleza kama mtoto mdogo,huku nikiisikia miguno yake.Sauti yake laini anapolalama kwa raha inanichanganya mno.Natamani msisimko ule ninaoupata pale anapozigusisha chuchu zake kifuani kwangu.Peniela yuko tofauti na wanawake wengine wote,ana mvuto wa ajabu mno na amebarikiwa vitu vya kipekee ambavyo ni vigumu hata kuvielezea.Kitu kingine kinachonipa furaha ni kwamba hata yeye mwenyewe ameonekana kuwa na hisia kwangu.Nalisubiri kwa hamu sana jibu lake.Nina hakika hataweza kusema hapana.Kuna kila dalili kwamba mimi na yeye tuliumbwa tuwe pamoja .Ni kwa maongozi ya Mungu tumekutana .Ngoja kwanza nimpigie simu “ akachukua simu na kumpigia .Simu ikaita na kukatika bila kupokelewa,akapiga tena na safari hii ikapokewa

“ Hallow Jason” Sauti laini ya Penny iliyoonyesha uchovu ikasikika

“ Hallow my angel Peniela how are you? Akauliza Jason

“ I’m ok Jason.How are you?

“ I’m ok Penny.Umelala?

“ Nilikuwa nimelala .Mwili umechoka sana.Shughuli ya jana haikuwa ndogo” akasema Penny kwa sauti iliyojaa uchovu

“ Pole sana Penny

“ Pole ya nini Jason?http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“ Kwa uchovu unaousikia”

Penny akacheka kidogo na kusema

“ You don’t know how much I miss you Jason.Sijawahi kuwa na usiku mzuri kama wa jana.Naomba nikiri kwamba sijawahi kukutana na mwanaume kama wewe.Nakupigia saluti Jason wewe ni wa kipekee kabisa.Mwanamke yeyote Yule ambaye utamgusa hatakubali kamwe kukuachia kama vile ambavyo mimi sitaki kukuacha. Natamani niwe nawe kila wakati.Natamani nikichezee kifua chako ,natamani nipapaswe na mikonoyako yenye nguvu” akasema Penny.Maneno yale ya Penny yakazidi kumpandisha mzuka Jason na ikulu yake nayo ikaonekana kuzidi kuchachamaa.Akavuta pumzi ndefu na kusema

“ Penny maneno matamu uliyoniambia nayarudisha tena kwako.Wewe ni wa kipekee kabisa.Hakuna kama wewe katika hii dunia.Ni vigumu mno kuielezea raha niliyoipata jana kwa kuwa pembeni ya malaika kama wewe ,natamani usiku ule ujirudie tena na tena “

“ Usihofu Jason.Hata mimi natamani iwe hivyo.Hata mimi nakutamani sana.Naomba uje tena kwangu usiku wa leo.Please don’t say No Jason” akasema Penny .Uso wa Jason ukachanua kwa tabasamu pana

“ Peniela ,Kwako wewe ulimi wangu hauwezi kutamka neno hapana.Dakika nitakayotamka neno hilo nitakuwa nimelaaniwa.Kwako kila utakachoniambia nitakuwa na jibu moja tu la Ndiyo.Nitakuwa na matatizo ya akili endapo nitakataa kuupitisha usiku wangu nikiwa na malaika kama wewe.Nitafika Penny ,si leo tu bali kila mara utakaponihitaji”

“ Nafurahi sana kusikia kauli hiyo Jason.Ndiyo maana nikakwambia kwamba katika dunia hii hakuna mwanaume wa kulinganishwa na wewe.Nitakusubiri kuanzia mida ya saa tatu.Ukifika hauna haja ya kugonga geti litakuwa wazi,pita ndani moja kwa moja”

“ Ahsante sana Penny.Ahsante sana malaika wangu.Nitafika mida hiyo usijali” akasema Jason

“ Ahsante Jason.Kwa sasa ngoja nipumzike tutaonana baadae”

“ Penny naomba usikate simu kwanza..!! Akasema Jason

“ Unasemaje Jason?

“ Nataka tu kukukumbusha kwamba ninakupenda sana kuliko chochote katika hii dunia”

“ Nafurahi kusikia hivyo” akajibu Penny na kukata simu

Hata baada ya kumaliza kuongea na Peniela simuni ,bado uso wa Jason uliendelea kupambwa na tabasamu zito sana.

“ Nilikuwa nikisikia kwamba kuna nyakati mapenzi yanaweza kukupa uendawazimu,nahisi hata mimi ninaelekea huko.Nina haki ya kuchanganyikiwa kwa mwanamke kama Peniela.Usiku wa leo nitampeleka tena katika sayari nyingine.Dah sipati picha namna itakavyokuwa usiku wa leo” akawaza huku akiinuka na kuvaa koti lake

“ Ninaanza kuwa na matumaini kwamba hata Peniela naye ananihitaji sana.Nina hakika hata jibu atakalonipa ni zuri kwani angekuwa hana hisia zozote kwangu basi asingenikubalia kirahisi namna hii” akawaza Jason huku akitoka ofisini kwake

*********

Baada ya kutoka nyumbani kwa Peniela Jaji Elibariki akaelekea nyumbani kwake kubadili nguo.Kichwa chake kilija mawazo mengi sana kuhusiana na kile alichokifanya na Penny

“ Mmhh ! sikujua kama Peniala ni msichana mtundu kiasi kile.Aliponipigia simu nilidhani ana tatizo kubwa sana lakini kumbe alikuwa na lake jambo “ akawaza huku akitabasamu

“ Nilihisi kuchanganyikiwa pale alipofungua mlango na kuingia bafuni.Mtoto ameumbika Yule.Kila nikiikumbuka picha ile mwili wote unanisisimka. Inaonekana upweke unamsumbua Penny,nitajitahidi kwa kadiri niwezavyo niweze kumuweka karibu na kumliwaza.Anahitaji faraja na hapa amefika.Kwa sasa Flaviana hataniumiza kichwa tena kwani tayari nina sehemu ya kupata kitulizo.” Akaendelea kuwaza.

Alifika nyumbani kwake na kufululiza moja kwa moja chumbani akabadili nguo haraka haraka

“Sikutegemea hata siku moja kama nitakuja kuisaliti ndoa yangu.Pamoja na misuko suko mingi ambayo tumeipata ndani ya ndoa yangu lakini nimesimama imara na hata mara moja sijawahi kutoka nje ya ndoa.Kwa mara ya kwanza nimeshindwa kuwa jasiri wa kukitetea kiapo changu cha ndoa mbele ya Peniela.Nahisi huyu mwanamke anaweza kuwa na dawa Fulani kwa sababu sijawahi kuchanganywa kichwa changu na mtoto wa kike kama inavyonitokea sasa. Nahisi kuanza kuchanganyikiwa na mambo aliyonifanyia Penny leo.Hata mke wangu hajawahi kunifanyia mambo kama yale na ndiyo maana Penny amekitawala kichwa changu.Ninaapa nitafanya kila ninachoweza kuhakikisha kwamba Penny anakuwa ni mwanamke mwenye furaha sana .Nitampatia kila anachokihitaji na kwa kuanzia nitafanya kila linalowezekana kulisafisha jina lake kutokana na tuhuma zile za mauaji.Nitahakikisha aliyefanya mauaji yale ya Edson na kumbambikia Peniela kesi ile anapatikana na jina la Penny linasafishwa.” Jaji Elibariki akastushwa na mlio wa simu.Alikuwa ni mke wake Flaviana.Akabonyeza kitufe cha kupokelea

“ Hallo Flaviana”

“ Hallo Eli,uko wapi? Ninakutafuta hapa sikuoni na simu yako imekuwa ikiita bila kupokelewa.”Akauliza Flaviana

“ Nimekuja nyumbani mara moja kubadili nguo.” Akajibu Elibariki

“ Ok Eli ukifika naomba unitafute kuna jambo ninahitaji kuongea nawe la muhimu sana”

“ Sawa Flaviana ninakuja sasa hivi” akasema Mathew na kukata simu moja kwa moja akapanda gari lake na kuelekea msibani.Baada ya kuwasili akamtafuta mkewe wakajitenga pembeni kidogo mahala kusikokuwa na watu

“ Eli kuna jambo ambalo nataka unisaidie” akasema Flaviana

“ Jambo gani Flaviana?

“ Ni kuhusu kilichomuua mama.Mpaka sasa hivi hakuna kitu kilichowekwa wazi nini kilimuua mama.Hata sisi watoto wake hatufahamu kitu gani kilimuua ghafla namna ile.”

“ Baba yako anasemaje kuhusu hilo? Mmekwisha muuliza kma kuna taarifa yoyote aliyoipokea ? Akauliza jaji Elibariki

“ Baba hajasema chochote mpaka sasa. Kuna daktari mmoja katika hospitali ile ya jeshi ambaye ninafahamiana naye nilimpigia simu na kumuuliza kuhusiana na uchunguzi wa kifo cha mama alinipa jibu la kushangaza sana.”

“ Alisemaje?

“ Alisema kwamba wakiwa katika harakati za kufanya uchunguzi wa kifo cha mama walipokea simu kwamba wasiendelee na kufanya uchunguzi huo”

“ What ?!! Jaji Elibariki akashangaa

“ Amri hiyo walipewa na nani?

“ Sifahamu Eli,sifahamu nani aliyewapa amri hiyo na kwa nini walifanya hivyo.Daktari huyo hakuwa tayari kusema ni nani aliyewapa taarifa hiyo ya kutokuendelea na uchunguzi wa kifo cha mama”

Jaji Elibariki akainama akazama katika mawazo

“ Unajua hainiingii akilini kwamba kwa mtu mkubwa kama mke wa rais afariki ghafla halafu kusifanyike uchunguzi wowote wa kuhusiana na kifo chake.”

“ Hata mimi nimeshindwa kuelewa Eli na ndiyo maana nikakuita hapa ili unisaidie”

“ Unataja nifanye nini?

“ Naomba unisaidie kufahamu nini kilimuua mama”

“ What ? akauliza Jaji Elibariki kwa mshangao

“ Naomba unisadie kuupata ukweli wa nini kilisababisha kifo cha mama”

“ Flaviana nitawezaje kufanya hivyo wakati mimi si daktari?

“ I don’t know Eli but find a way.I know you must have a way to find the truth.”

Jaji Elibariki alihisi kama kitu kizito kimegonga kichwa chake.Flaviana akauona mstuko alioupata mumewe akamshika mkono na kusema

“ Elibariki mume wangu najua hili si suala rahisi lakini sina mwingine ambaye anaweza akanisaidia katika hili zaidi yako.Please help me.Nahitaji sana kufahamu nini kilimuua mama.Sielewi ni kwa nini moyo wangu unajikuta ukitaka kufahamu sababu ya kifo cha mama.Elibariki najua wewe una njia nyingi za kuweza kufanya ukaipata.You have many connections so please my love do it for me.Najua nimekukosea sana mambo mengi lakini tafadhali naomba tofauti zetu tuziweke kando kwa sasa na tulishughulikie suala hili.Ni muhimu sana kwangu ” Akasema Flaviana.Jaji Elibariki akainama akawaza halafu akainua kichwa na kusema

“ Ok my love.I’ll do it for you”

Wakakumbatiana na Flaviana akaondoka.Kichwa cha Jaji Elibariki kilikuwa kizito kama kimefungwa jiwe.Alihisi kuchanganyikiwa,hakujua angewezaje kuipata ripoti ile aliyoitaka mke wake.Alibaki ameegemea mti kwa dakika kadhaa akiwaza

“ How am I going to do it? Nahisi kuchanganyikiwa sielewi nitafanya vipi kufahamu nini kilimuua Dr Flora.”

Kwa takribani dakika kumi alikuwa amezama katika mawazo na mwishowe akachukua simu yake na kuzitafuta namba za simu za Mathew

“ I need Mathew.” Akasema na kumpigia.Simu ikaita bila kupokelewa.Akapiga tena lakini bado simu haikupokelewa ,akahisi kuchanganyikiwa





Mathew na Dr Michael walipigwa na butwaa wakabaki wakitazamana.Mathew alitamani iwe ni ndoto lakini haikuwa hivyo.Ni kweli chumba kilikuwa kitupu na John Mwaulaya hakuwepo mle chumbani.

“ Haya ni mazingaombwe makubwa .Mgonjwa John amekwenda wapi? Saa nne na dakika ishirini nimetoka humu na kumuacha akiwa amelala hapo kitandani sasa amekwenda wapi? Nani kamtoa? Akauliza Dr Michael.Mathew akafungua mlango wa maliwato akachunguza kila pembe akatoka na kuchungulia dirishani ,halafu akamfuata Dr Michael.Akamkaba shingoni na kumgandamiza ukutani akamuwekea bastora kichwani

“ Niambie John yuko wapi? Akasema kwa ukali .

Dr Michael alikuwa akitetemeka mwili mzima kwa namna Mathew alivyokuwa amebadilika. “ Si..s..sifahamu mahala aliko” akasema kwa woga.Jasho lilikuwa likimtoka

“ Nakupa dakika moja ya kusema ukweli ama sivyo mwanao hutamuona tena.John mwaulaya yuko wapi?!!..

“ Sifahamu aliko.Naomba uniamini sifahamu mahala aliko. Hata mimi nashangaa ni kitu gani kimetokea.Ninaapa sifahamu John yuko wapi” akasema Dr Michael na kwa mbali machozi yakimlenga kwa woga

Sura ya Mathew ilikuwa imebadilika.Alikuwa na hasira zisizomithilika.Akamtazama Dr Michael kwa macho makali na kuzidi kumuogopesha

“ Dr Michael hii ninafasi yako ya mwisho. Tafadhali niambie John Mwaulaya yuko wapi?

“ Sifahamu yuko wapi.Kama ningejua mahala aliko ningekwambia,lakini sifahamu yuko wapi” akasema Dr Michael huku akitetemeka.

“ Dr Michael nitazame vizuri machoni” akasema Mathew.

“ Unavyoniona ninafanya utani siyo?

“ Hapana hautanii!! Akasema Dr Michael kwa woga

“ Ok basi kabla ya saa moja jioni ya leo,familia yako yote itakuwa imeteketea tukianzia na mwanao mdogo Michael kama hutaweza kunieleza yuko wapi John Mwaulaya” akasema Mathew.Machozi yakamtoka Dr Michael

“ Ndugu yangu sifahamu mahala aliko huyu mgonjwa.Kama ningejua mahala aliko ningekwambia.Ta

fadhali naomba usiidhuru familia yangu.Naombeni mnidhuru mimi lakini si familia yangu” akaomba Dr Michael.Mathew akamtazama kwa sekunde kadhaa halafu akamuachia.Dr Michael akakaa chini

“Anasema ukweli,hafahamu chochote” akawaza Mathew huku akipumua kwa kasi.

“ Team SC 41 wamefahamu kwamba tuko hapa na shida yetu ni John mwaulaya na ndiyo maana wakawahi kumuondoa.Ninachojiuliza ni vipi wameweza kugundua kwamba tuko hapa na tumekuja kwa ajili ya John Mwaulaya? Akajiuliza Mathew na kushindwa kupata jibu akakumbuka kwamba hakuwa amewataarifu wenzake kile alichokikuta mle ndani.

“ Anitha,John ametoweka humu chumbani.Narudia tena John ametoweka humu chumbani”

“ Mathew hii imetokeaje?Ameruhusiwa na daktari? Akauliza Anitha

“ Hapana Anitha.John hajaruhusiwa na daktari ,ametoroshwa.They know we are here.” Akasema Mathew na kumshika mkono Dr Michael akamuinua

“Twende tuondoke” akasema Mathew

“ Unanipeleka wapi? Mwanangu yuko wapi?

“ Nasema twende tuondoke hapa haraka sana!! …Akafoka Mathew.Dr Michael akaogopa na kuanza kutembea kwa kasi akimfuata Mathew wakashuka ghorofa na moja kwa moja wakaelekea katika maegesho ya magari wakaingia katika gari la Mathew.Kabla hajawasha gari simu ya Dr Michael ikaita

“ Mke wangu ananipigia” akasema Dr Michael

“ mwambie aondoke nyumbani haraka sana kwani si sehemu salama kwa sasa.Sisi tunakwenda kwanza shuleni kuwachukua wanao wawili halafu tutampitia na yeye mahala atakapokuwa amekwenda na tutakwenda katika sehemu salama.Kwa sasa wewe na familia yako maisha yenu yako hatarini” akasema Mathew.Bila ubishi Dr Michael akabonyeza kitufe cha kupokelea

“ Hallow “ akasema Dr Michael

“ Hallow Dr Michael” ikasema sauti ya upande wa pili.Nusura Dr Michael aangushe simu kwa mstuko alioupata.Aliyekuwa akiongea upande wa pili hakuwa mkewe bali sauti nzito ya kiume.Mathew aliuona mstuko alioupata Dr Michael ,akamuelekeza abonyeze kitufe cha kuwezesha sauti kubwa kusikika ili aweze kusikia maongezi yale.Bila ubishi Dr Michael akakibonyeza.

“ Hallow Dr Michael “ akasema mtu Yule.

“ Wewe ni nani na kwa nini uko na simu ya mke wangu? Akauliza Dr Michael

“ Dr Michael nakufahamisha kwamba mkeo tunaye hapa ,tunamshikilia “

“ unasemaje?!! Dr Michael akapatwa na mstuko mkubwa

“ Mkeo tumemchukua tuko naye kwa hiyo usisumbuke kumtafuta”

“ Wewe ni nani? Akauliza Dr Michael kwa wasi wasi

“ Huna haja ya kunifahamu lakini nataka tu ufahamu kwamba mkeo tunaye,yuko salama na atakuwa salama endapo tu utakuwa msikivu na kufuata kile tutakachokuelekeza.”

“ Mungu wangu ! kitu gani hiki kinanitokea mimi na familia yangu? Akajiuliza Dr Michael

“ Dr Michael! Akaita Yule jamaa simuni

“ Tafadhalini naomba msimfanye chochote mke wangu.” Akaomba Dr Michael

“ Hatuna haja ya kumfanya chochote mke wako Dr Michael ila tutalazimika kufanya hivyo pale utakapokwenda kinyume na sisi.”

“ Mnataka nini toka kwangu? Akauliza Dr Michael

“ Nitakupigia baadae kukupa maelekezo lakini nakuonya kwamba usithubutu kupeleka suala hili polisi wala kumweleza mtu mwingine yeyote .Kufanya hivyo kutasababisha umkose mke wako.Usifanye jambo lolote la kijinga na kuhatarisha uhai wa mke wako.Kwa sasa ongea na mkeo” akasema Yule jamaa na kumpa simu mke wa Dr Michael aongee na mumewe

“ Hallow “ akasema mke wa Dr Michael

“ Hallow mpenzi,uko salama? Hawajakuumiza hawa mabazazi? Akauliza Dr Michael

“ Hapana hawajanidhuru lakini wametishia kwamba watanifanyia kitu kibaya endapo hautafanya wanachotaka ukifanye.Tafadhali mume wangu fanya chochote wakatachokuambia ufanye ili uweze kuniokoa.Ninaogopa sana” akasema mke wa Dr Michael huku akilia.

“ Usilie mke wangu,tafadhali usilie.Nakujua wewe ni mwanamke jasiri kwa hiyo usilie nitafanya kila watakachoniamuru kufanya kwa ajili ya kukuokoa wewe..Siko tayari udhurike mke wangu” akasema Dr Michael na mara simu ikakatwa.Mwili ulikuwa ukimtetemeka hakujua afanye nini.

“ Wamemteka mke wangu” akasema Dr Michael

“ Watamuua mke wangu.Watu hawa ni akina nani na wanataka nini kwangu? !!Kwa nini wamemteka mke wangu? Akauliza Dr Michael

“ Dr Michael ni vigumu kusema moja kwa moja watu hawa ni akina nani lakini ni watu wanaokufahamu vyema .Nakuahidi kwamba tutawatafuta na kuwapata pamoja na kumpata mkeo akiwa salama.Ninachoh

itaji ni ushirikiano wako”

“ Tafadhali naomba ufanye kila linalowezekana umkomboe mke wangu.Unafahamu mahala alipo? Unawafahamu waliomteka? Akauliza Dr Michael ambaye alionekana kuchanganyikiwa

“ Dr Michael sina jibu lolote la kukupa kwa sasa lakini nakuahidi kukulinda wewe na familia yako.Mimi na wenzangu tutafanya kila linalowezekana kumtafuta mkeo” akasema Mathew huku akiwasha gari na kuliondoa kwa kasi.

“ Ndugu yangu sema chochote unachohitaji nikifanye ili familia yangu iweze kuwa salama.” Akasema Dr Michael.Kabla Mathew hajamjibu Anitha akamuita

“ Mathew kuna kitu nimekigundua,mtazame vizuri Dr Michael kuna kifaa anacho ambacho kinarusha mawasiliano.Nimeona hapa kwenye kompyuta yangu kuna mawasiliano yanatoka” .Mathew akasimamisha gari na kumtazama Dr Michael

“Kuna nini mbona umesimamisha gari? Mbona unanitazama hivyo? Akauliza Dr Michael lakini Mathew hakumjibu kitu akaendelea kumkagua.Akachukua simu ya Dr Michael na kuizima.

“ Anitha vipi hapo bado unaona kitu chochote? Akauliza Mathew

“ Bado kuna kitu anacho kinachorusha mawasiliano kupeleka sehemu Fulani”

Mathew akamtoa Dr Michael nje ya gari akaanza kumkagua .Katika mfuko wake wa koti kulikuwa na kalamu mbili,akazichukua zile kalamu na kuzifungua.Katika kalamu moja akakutana na kitu kisicho cha kawaida.Akashuka na kuziweka kalamu zile mbele ya tairi halafu akawasha gari na kuzikanyaga halafu akasimamisha gari.

“ Anitha ulikuwa sahihi.Dr Michael alikuwa amewekewa kifaa kidogo sana cha mawasiliano katika kalamu yake na ndiyo maana watu wale waliweza kusikia kila tulichokuwa tunakiongea na Dr Michael hivyo kwa haraka wakamuondoa John Mwaulaya.” Mathew akamfahamisha Anitha

“ Kwa sasa naona shwari sioni kama kuna mawasiliano yanayoruka kwenda sehemu nyingine” akasema Anitha

“ Good Job anitha”

“ So whats next Mathew? Akauliza Anitha

“ Tunasubiri maelekezo atakayopewa Dr Michael na watekaji halafu tutajua nini cha kufanya lakini wakati tukisubiri hayo tunaelekea White shield international high school kuwachukua watoto wa Dr Michael na kuwaweka sehemu salama.” akasema Mathew

“ Unasema nilikuwa nimewekewa kifaa cha mawasiliano? Akauliza Dr Michael

“ Ndiyo Dr Michael.Katika kalamu yako moja kulikuwa na kifaa kidogo cha mawasiliano ambacho kazi yake ni kunasa kila utakachokiongea na kuyarusha kwa wahusika.Kifaa hiki ndicho kilinasa maongezi yetu asubuhi nilipokuwa ninakuamuru unipeleke chumba cha John na kwa kuwa walihisi kuna hatari inaweza kutokea ikawalazimu kumuondoa John haraka sana.” Akasema Mathew na kuzidi kumshangaza Dr Michael

“ Unataka kuniambia kwamba watu waliomteka mke wangu wana uhusiano na Yule mgonjwa aliyetoroka?

“ Ndiyo.” Akajibu Mathew.Dr Michael akainama chini akafikiri na kukumbuka kitu

“ Unaweza kuwa sahihi ndugu yangu.Nimekumbuka kuna siku moja nilipokuwa nikimuhudumia John,mmoja wa wale vijana aliniomba kalamu lakini hakunirudishia kalamu yangu na badala yake akanirejeshea kalamu nyingine kabisa kwa madai kwamba kalamu yangu haiandiki vyema.Nilishukuru na sikuuliza chochote na wala sikufahamu jambo lolote kuhusiana na nini kilikuwamo ndani ya kalamu ile.Kama ni wao ndio waliomteka mke wangu basi watakuwa wamefanya hivyo kwa sababu moja tu.”

“ sababu gani? Akauliza Mathew

“ John anatakiwa afanyiwe upasuaji wa kichwa na mimi ndiye daktari pekee wanayemtegemea kufanya upasuaji huo..Huyu John ni nani? Akauliza Dr Michael

“ Upasuaji huo ulitakiwa ufanyike lini?

“ Kuna dawa tulizokuwa tunazisubiri ziwasili ndani ya siku mbili hizi halafu tumfanyie upasuaji”

“ ok vizuri.Tutaongea zaidi baadae kwa sasa tusipoteze wakati tuelekee moja kwa moja shuleni kuwawahi watoto” akasema Mathew na kuwasha gari wakaondoka kuelekea White shield international high school.

“ Hii ni vita kali na inabidi kujihami kwa kila namna inavyowezekana.Team SC 41 tayari wanafahamu kwamba kuna watu wanaowafuatilia .Ninaanza kuingiwa na woga lakini sintarudi nyuma,lazima nipambane nao.Safari hii sintokubali wanishinde” akawaza Mathew.

Walifika katika shule wanakosoma watoto wa Dr Michael .

“ Usiwaeleze chochote watoto kwa sasa ili usiwasababishie mstuko .Hatutaki suala hili lisambae“Mathew akamwambia Dr Michael ambaye alishuka na kuingia ndani ya jengo la shule.Baada ya kama dakika saba akarejea akiwa na watoto wawili.Mathew akafungua mlango wakaingia ndani ya garihttp://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“ Tunaelekea wapi sasa hivi? Akauliza Dr Michael

“ Tunaelekea nyumbani kwangu” akasema Mathew na kuwasha gari wakaondoka.

Waliwasili katika makazi yake na Dr Michael alishindwa kuonyesha furaha yake kwa kukutanishwa tena na mwanae Michael Jr aliyekuwa ameongozana na akina Anitha.Watoto wote wa Dr Michael hawakuelewa kilichokuwa kinaendelea na kwa nini walikuwepo pale kwa Mathew.Mathew akamuelekeza Anitha awapeleke watoto katika chumba cha kupumzikia kilichokuwamo na runinga na michezo ya kompyuta.

“ Dr Michael pole sana kwa matatizo yaliyokupata “ akaanzisha mazungumzo Mathew

“ Nashukuru sana,lakini ningependa niwafahamu ninyi ni akina nani? Ni polisi au usalama wa taifa? Akauliza Dr Michael

“ Mimi ninaitwa Mathew,mwenzangu pale anaitwa Noah na Yule mwanadada anaitwa Anitha.Sisi si polisi wala usalama wa taifa ila kwa pamoja sisi ni kikosi cha uchunguzi tunaochunguza kuhusu tukio Fulani la mauaji tata.Uchunguzi wetu umetufikisha hadi kwa John mwaulaya mgonjwa aliyekuwa amelazwa wadi PV2 – 78 na ndiyo maana lengo langu lilikuwa ni kumuhoji na kutaka kuufahamu ukweli.” Akasema Mathew

“ Kama ni hivyo msingetumia njia ya kumteka mwanangu na kumfanya chambo ili niweze kufanya mnachokitaka.Endapo ungenieleza ukweli ningeweza kuwasaidia bila hata ya kutumia njia ile ya utekaji.” Akasema Dr Michael

“ Dr Michael ,huwa tunatumia njia kama hii kwa sababu kwa njia ya kawaida watu wengi huwa hawako tayari kutoa ushirikiano_Ok sasa tujad……” kabla hajaendelea na alichotaka kukisema simu yake iliyokuwa mezani ikatetema,akainuka na kutazama mpigaji alikuwa ni Jaji Elibariki

“ Hallo Elibariki”

“habari yako Mathew? Akasema jaji Elibariki

“ habari yangu nzuri Mheshimiwa jaji,pole sana na matatizo”

“ Tumekwisha poa Mathew,poleni na nyie “

“ Ahsante sana Eli.Ninashukuru pia kwa mzigo wa jana Jason alinifikishia na tayari tumekwisha ufanyia kazi”

“ Ok nashukuru kama ulipata ule mzigo.Muda wowote ukikwama nitaarifu ili nikukwamue” akasema Elibariki halafu kikapita kimya kifupi akasema

“ Mathew nimekutafuta sana simuni leo lakini simu imekuwa ikiita tu bila kupokelewa.” Akasema Jaji Elibariki

“ Tulikuwa tumetoka kikazi na na simu niliitoa mlio kwa hiyo sikuweza kusikia uliponipigia.Kuna habari gani?

Jaji Elibariki akavuta pumzi ndefu na kusema

“ Mathew kuna jambo lingine limeibuka ambalo sina mwingine anayeweza kunisaidia zaidi yako”

“ jambo gani Elibariki?

“ Sintoweza kuongea nawe simuni ni jambo nyeti sana ,nitakuja hapo kwako jioni kukuona na tutaongea vizuri.”

“ Elibariki nadhani ingekuwa vyema kama ungeniambia sasa hivi kwa sababu siwezi kujua baadae nitakuwa sehemu gani kwani tunapokuwa tunaifanya kazi Fulani huwa hatuna muda maalum wa kupumzika.Naomba unieleze ni tatizo gani hilo?akauliza Mathew

Elibariki akavuta pumzi defu na kusema

“Nadhani una tarifa kuhusiana na kifo cha mke wa rais Dr Flora Joshua?

“ Ndiyo Eli nina taarifa hizo aliniambia Jason jana.”

“ Dr Flora alifariki ghafla lakini mpaka sasa bado hakuna taarifa yoyote iliyotolewa kuhusiana na sababu ya kifo chake.Kitu kingine cha kushanganza ni kwamba madaktari katika hospitali ya jeshi walikwisha anza kuufanyia uchunguzi mwili wa marehemu kubaini nini kilimuua lakini walipokea taarifa kwamba waachane na zoezi hilo” akasema Jaji Elibariki na kumstua sana Mathew

“ hebu subiri kidogo Eli ,unasema madaktari Waliambiwa waache wasifanye uchunguzi kubaini kilichomuua Dr Flora?

“ Ndiyo Mathew ,kwa mujibu wa daktari anayefahamiana na mke wangu”

“ Taarifa hiyo ilitoka kwa nani?

“ Mpaka sasa hatuelewi taarifa hiyo ilitoka kwa nani .Mke wangu ambaye ni mtoto mkubwa wa marehemu ana wasi wasi mno ameanza kuingiwa na mashaka sana kuhusiana na kifo cha mama yake kwa sababu jioni ya siku ile walikuwa wakutane kuna jambo kubwa ambalo alitaka kuwaeleza watoto wake lakini hakufika jioni akafariki ghafla.”

“ Ana wasi wasi kwamba yawezekana Dr Flora akawa ameuawa?

“ Kutokana na mazingira yalivyo kuna weza kuwa na hisia hizo” akajibu Elibariki

Mathew akafikiri kidogo na kusema

“ Unataka nifanye nini mheshimiwa?

“ Sifahamu kama hili linaweza kuwa ndani ya uwezo wako lakini nataka kufanya uchunguzi kubaini nini kilimuua Dr Flora.This is for my wife.” Akasema Jaji Elibariki.

Mathew akavuta pumzi ndefu akainama na kuzama katika mawazo.

“ Mathew if this is too much for you then we can leave it…” akasema Jaji Elibariki baada ya kuona kimya kinapita na Mathew hajibu chochote

“ Hapana jaji Eli,tutaifanya hiyo kazi.Consider it done” akasema Mathew

“ Thank you so much Mathew.”

“ Ok Elibariki,let me figure out how I can do this,and then I’ll get back to you” akasema Mathew

“ Ok Mathew,thank you so much.Kama kuna tatizo lolote linalohitaji msaada usisite kunitaarifu” akasema jaji Elibariki na kukata simu

“ Dah ! nahisi nimeutua mzigo mkubwa sana uliokuwa unanielemea.Suala hili ni zito na sijui litafanyikaje lakini nilishindwa kumkatalia Flaviana.” Akawaza Elibariki baada ya kumaliza kuongea na Mathew simuni

Mathew alisimama kwa sekunde kadhaa akiwaza .Jambo aliloambiwa na jaji Elibariki lilimstua sana ingawa alishindwa kukataa

“ How am I going to do it? Akajiuliza Mathew .Akainama akafikiri kwa muda halafu akamuendea Dr Michael

“ Dr Michael ,naomba unisikilize kwa makini ” akasema Mathew

“ Nakusikiliza Mathew”

“ Kwa sasa wewe na familia yako mko hatarini na mke wako tayari yuko katika mikono ya watekaji.Ninaku

ahidi kwamba mimi na wenzangu tutafanya kila tunachoweza kumtafuta mkeo na kumuokoa mikononi mwa watekaji hao.”

“ Nitashukuru sana Mathew kama utaweza kunisaidia kwa hilo”

“ Nitakusaidia kwa hilo Dr Michael lakini kwa sharti moja”

“ Sharti gani?

“ Kuna kazi ambayo nitaomba unisaidie kuifanya”

“ kazi gani?

“ Nitakueleza baadae ni kazi gani “ akasema Mathew na kuwaita akina Anitha katika chumba kingine

“ ndugu zangu mapambano yameanza.Team SC 41 tayari wamekwisha fahamu kwamba tunamfuatilia John Mwaulaya na ndiyo maana wakamuondosha pale hospitali haraka sana.Nina hakika lazima hivi sasa watakuwa wakijiuliza sisi ni akina nani na kwa nini tunamtafuta John Mwaulaya.” Akasema Mathew akanyamaza kidogo ba kuendelea

“ John Mwaulaya anaumwa na Dr Michael ndiye mtu pekee ambaye anategemewa kumfanyia upasuaji wa kichwa na hii ndiyo sababu ambayo imewapelekea wamteke mke wa Dr Michael ili kumshinikiza afanye upasuaji huo.Mpango mkubwa ulioko mbele yetu kwa sasa ni kumkomboa mke wa Dr Michael akiwa hai.Hata ikitokea Dr Michael akimfanyia upasuaji John mwaulaya lazima watamuua tu.hawako tayari kumuacha hai mtu ambaye tayari amefahamu siri zao.Tusikubali hilo litokee.We have to save Dr Michael and his family.” Mathew akanyamaza kidogo halafu akaendelea

“ Muda mfupi uliopita nimepokea simu toka kwa jaji Elibariki.Kuna jambo ambalo ameniambia ambalo limenishangaza kidogo.Mke wa rais alifariki ghafla na mpaka sasa hakuna taarifa zozote za kuhusu nini kilisababisha kifo chake.Madaktari katika hospitali kuu ya jeshi walipewa amri ya kutokufanya uchunguzi wao.Bado haifahamiki ni nani aliyewapa amri hiyo ya kutokufanya uchunguzi wa kilichosababisha kifo cha mke wa rais.Usiku wa kuamkia siku ya kifo chake Dr Flora alizungumza na wanae wawili na kuwataka waonane jioni alikuwa na jambo muhimu sana la kuwaeleza.Kwa bahati mbaya haikufika jioni na Dr Flora akafariki dunia ghafla.Ukiunganisha mambo haya mawili kuna picha inayojengeka hapa .Tunahitaji kufanya uchunguzi wa nini kilimuua Dr Flora mke wa rais”

Anitha na Noah walikuwa kimya wakimsikiliza Mathew.Suala la kufanya uchunguzi wa kifo cha Dr Flora liliwastua sana.

“ Mathew usinielewe vibaya ndugu yangu,lakini nina mashaka kidogo na kazi hii iliyoibuka ghafla kuhusiana na kufanya uchunguzi wa kifo cha Dr Flora.Hapa unazungumzia mke wa rais,unadhani inaweza kuwa rahisi ? Sisi hatuna taaluma yoyote ya udaktari tutaweza vipi kufanya uchunguzi huo? Kifo cha mke wa rais kina mahusiano yoyote na suala tunaloendelea kulichunguza ?Noah akauliza

“ Noah usianze kuogopa angali mapema.Bado tuna kazi pevu sana mbele yetu.Kwa kufanya uchunguzi huu tutamtumia Dr Michael.Nimemuahidi kumtafuta mke wake na kumpata kwa hiyo lazima atakubali kuifanya kazi hii.Kitu kikubwa na kigumu hapa ni namna gani tutaweza kuupata mwili wa Dr Flora na kuufanyia uchunguzi.Kuhusu mahusiano ya suala hili la Dr Flora na suala tunaloendelea kulichunguza,sina hakika bado kama yana mahusiano yoyote lakini yote mawili lazima tuyafanye.Tutafanya uchunguzi wa nini kilisababisha kifo cha Dr Flora na tutamkomboa mke wa Dr Michael” akasema Mathew

“ Kuhusu Team SC 41,nataka nikaingie tena katika mtandao wa hospitali na kwa kupitia kamera iliyopo nje ya lile jengo la private ward 2 ,tutaweza kuwabaini watu ambao walimtorosha John mwaulaya.Kwa kutumia program ya kulinganisha sura tunaweza kuwafahamu watu hao ni akina nani” akasema Anitha.

“ wazo zuri sana hilo Anitha.Shughulikia suala hilo na mimi ngoja nikaongee na Dr Michael ili nione namna tunavyoweza kuufanyia uchunguzi mwili wa mke wa rais kufahamu kilichomuua.” akasema Mathew.Anitha na Noah wakaelekea katika chumba chenye mitambo mbali mbali ,Mathew akaenda kuongea na Dr Michael

“ Dr Michael muda unazidi kwenda hivi sasa ni saa kumi na moja za jioni ,wakati tunasubiri hawa jamaa wapige simu na kutoa maelekezo naomba nikufahamishe kazi ninayotaka unisaidie”

“ kazi gani unataka nikusaidie Mathew?

“ Kuna mwili wa mtu ninataka kuufanyia uchunguzi ili kubaini kilichosababisha kifo chake”

Kabla Dr Michael hajajibu chochote simu yake ikaita.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“ Wamepiga tena.Hii ni namba ya mke wangu”akasema Dr Michael.

“Usiipokee kwanza,ngoja tuifuatilie tujue inapigwa toka wapi” akasema Mathew halafu akakimbia kwenda kumchukua Anitha ambaye alifika mara moja na kompyuta yake,na kuweka chombo fulani karibu na Dr Mathew halafu akamwambia aipokee na aweke sehemu ya kuongelea kwa sauti kubwa ili wote wasikie

“ Hallow”akasema Dr Michael

“ hallow Dr Michael,uko wapi?

“ Nimetoka kazini niko mahala nimepumzika nasubiri maelekezo yenu”

“ ok vizuri.Endelea kusubiri tutakupigia tena baadae kidogo.Nakukumbusha kwamba tunakufuatilia kila unachokifanya,ukithubutu kwenda polisi au kumwambia mtu yeyote Yule basi mkeo hutamuona tena.Tumeelewana Dr Michael?

“ Tumeelewana.Tafadhalini naomba msimdh..” kabla hajamaliza alichotaka kukisema simu ikakatwa

“ Umefanikiwa Anitha? Akauliza Mathew

“ Hapana,simu imewahi sana kukatika ,sijapata chochote”

“ Ok hakuna tatizo tutaendelea kusubiri maelekezo yao.Mmepata chochote katika kamera?

“ Tumegundua kwamba kuna wakati kamera iligeuzwa na kuelekezwa sehemu nyingine.Nadhani walifanya hivi ili waweze kutoka bil akuonekana katika kamera, walipotoka kamera zilirudi kama kawaida .” akasema Anitha

“Team SC41 ni watu hatari sana,muda wote wanafanya mambo yao kwa tahadhari kubwa” akasema Mathew.





Mathew akawaacha wenzake na kuelekea chumbani kwake,akakaa juu ya kitanda akazama mawazoni.

“ Vitani tena na Team SC41” akawaza

“ Bado sijausahau usiku ule walipowaua wenzangu wote .Bado picha ya usiku ule haijafutika kichwani kwangu.Bado picha ya moto ule mkubwa ulioteketeza nyumba na familia yangu inanijia kichwani kila siku,nahisi kama ninasikia vilio vya mke wangu n wanangu wakiteketea katika moto mkubwa.Siku ile furaha yangu yote ya maisha ilipotea.Ni muda sasa wa kulipa kisasi.Damu ya watu wangu inanililia ikitaka niwalipie kisasi.Lazima nilipe kisasi.” Mathew akapatwa na uchungu sana alipoikumbuka picha ya usiku ule mbaya kuliko yote katika maisha yake.

“ Bado najiuliza sana kuhusiana na jambo alilonieleza Jaji Elibariki kuhusu kifo cha mke wa rais.Inawezekana akawa aliuawa? Kama aliuawa ni kwa nini? Na nani alimuua? Akajiuliza

“ Kuna haja ya kufanya uchunguzi wa suala hili ili kufahamu kilichomuua Dr Flora.Lakini ni namna gani tutaweza kuufanya uchunguzi huo? akajiuliza .Akainama akawaza halafu akachukua simu na kuzitafuta namba Fulani akapiga

“ Hallow Neema” akasema Mathew baada ya simu kupokelewa

“ hallow Mathew,habari ya siku nyingi? Mbona umeadimika kiasi hicho?

“ Mimi nipo Ney.Sionekani mara kwa mara nimetingwa sana na kazi.Maisha yanakwendaje?

“ Namshukuru Mungu maisha yanakwenda vizuri sana.”

“ Nafurahi kusikia hivyo.Kuna zawadi yako nimekuletea toka Ufaransa”

“ wow ! ahsante sana Mathew.Kila mara huwa husahau kunikumbuka kwa zawadi.”

“ Siwezi kukusahau Ney.Najua wewe ni mrembo na unapenda vitu vizuri kwa hiyo kila niwapo safarini na kukutana na kitu kizuri huwa nakukumbuka sana”

“ Ahsante sana Mathew,nashukuru.Nikufuate nyumbani nije niichukue zawadi yangu? Akauliza Neema

“ Nitaipeleka ofisini kwako utaikuta pale.” Akasema Mathew

“ Mhh..haya ! akasema Neema.Kikapita kimya kifupi Mathew akasema

“ Neema kuna jambo nataka kukuuliza”

“ Mhh nilijua tu,ukianza mambo ya zwadi lazima utakuwa na shida inayohitaji msaada wangu.haya sema una tatizo gani?

“ Naomba unisaidie kutafuta ni nani daktari mkuu katika hospitali kuu ya jeshi” akasema Mathew

“ Ok Mathew,naomba unipe dakika tatu nitakupigia”akasema Neema na kukata simu

“Neema ni binti ambaye amekuwa akinisaidia sana kupata taarifa mbali mbali,safari hii lazima nimtafutie mkufu wa dhahabu,anapenda sana dhahabu” akawaza Mathew.Baada ya dakika kama tano hivi simu ikaita alikuwa ni Neema

“ Mathew ,daktari mkuu wa hospitali ya jeshi ni Kanali Adolf mubaya.”

Mathew akastuka sana kwa kulisikia jina lile

“ Unasema Kanali Adolf Mubaya? Akauliza

“ Ndiyo.”akajibu Neema.Kikapita kimya kifupi

“ Mathew ,kuna nini kwani? Akauliza Neema

“ naomba unisaidie kufahamu kanali Adolf anaishi wapi?

“ Anaishi katika nyumba za maafisa wa jeshi Kigamboni.Nyumba yake ni namba 54.” Akasema Neema

“ Ok ahsante sana Neema.Nitakutumia mzigo wako baadae”

“ Ahsante sana Mathew.”akajibu Neema na kukata simu

“ Kanali adolf” akasema Mathew baada ya kumaliza kuongea na Neema,akatoka na kuelekea katika chumba walichokuwamo Anitha na Noah

“ Kuna jambo nimelipata sasa hivi.Daktari mkuu wa hospitali kuu ya jeshi ni kanali Adolf Mubaya” akasema

“ Do you know him? Akauliza Anitha

“ Yes I know him” akajibu Mathew

“Who is he? akauliza Noah

“ Simfahamu kiundani sana lakini nilimfahamu wakati nikiwa katika operesheni fulani.Kuna watu nilikuwa nikiwafuatilia ikanilazimu kufanya kazi kama meneja wa baa”

“ hahahaa..! Anitha akacheka

“ Kumbe uliwahi kuwa meneja wa baa?

“ Yah ! Ilinilazimu kuwa meneja wa baa moja maarufu sana.Baa hiyo inamilikiwa na Eva mwabukuku ambaye ni kachero wa siri wa idara ya usalama wa taifa.Wakati nikiwa katika baa ile ndipo nilipomfahamu Kanali Adolf .Alikuwa akifika pale kila siku kuanzia mida ya saa tano na kukaa hadi mida ya saa saba za usiku .Alikuwa akifika pale kufuata wanawake wanaojiuza.Si yeye tu bali hata watu wengine wakubwa wakubwa walikuwa wakifika pale kwa siri wakifuata huduma hiyo.Ninamfahamu Kanali Adolf kwa matumizi makubwa aliyokuwa akiyafanya.Kwa kuwa si yeye niliyekuwa nkimfuatilia sikutaka kumchunguza lakini kwa mujibu wa Eva,Kanali Adolf anajipatia fedha zake kutokana na miradi mbali mbali anayoifanya kwa siri.Kwa muda niliokaa pale niliwafahamu watu wengi hususani viongozi wakubwa waliokuwa wakifika pale kumwaga hela na makahaba.Eva Mwabukuku ni rafiki yangu sana na nimewahi kumsaidia sana huko nyuma ,yeye anawafahamu wakubwa wengi,anazifahamu siri zao nyingi kwani yeye ndiye ambaye huwa anawaunganishiwa wasichana wale makahaba,nina hakika hata kanali Adolf atakuwa akimfahamu kiundani.Nitaka kutafuta jambo ambalo litamfanya Kanali Adolf akubali kuifanya kazi yetu kwa usiku wa leo ”

“ Una hakika huyo Eva anaweza akakubali kukupa siri za Kanali Adolf? Akauliza Noah

“ Eva ni rafiki yangu sana ingawa kwa muda mrefu hatujaonana lakini ninazo namba zake za simu za siri katika kitabu changu cha kumbu kumbu ngoja nikazitafute nimpigie “ akasema Mathew na kurejea chumbani kwake akafungua kabati la ke analohifadhi nyaraka zake muhimu akatoa kitabu fulani ambacho huandika kumbukumbu zake mbali mbali za muhimu na kuzitafuta namba za simu za Eva Mwabukuku akazipata

Haraka haraka akaziandika namba zile katika simu yake akapiga simu ikaita

“ Hallo Zombie,are you back from hell? Ikauliza sauti ya upande wa pili na kumfanya Mathew acheke kicheko kikubwa.

“ I’m back Eva,I’m back” akasema Mathew

“ Welcome back.Umepotea sana Mathew.Its been years.How are you?” Akasema Eva

“ kweli Eva,umekuwa ni muda mrefu sana hatujaonana,maisha yanakwendaje?

“ Maisha yanakwenda vizuri sana .Vipi wewe,unaendeleaje?

“ Ninaendelea vizuri Eva.” Akasema Mathew na kukaa kimya kidogo.

“ Eva ninahitaji kukuona nina shida kidogo nahitaji msaada wako” akasema Mathew

“ Mathew hata mimi nina hamu sana ya kukuona.Uliponipigia simu sikuamini .Umekuja kwa wakati muafaka wakati ambao nakuhitaji sana.Njoo hapa pub utanikuta.” akasema Eva

“ Ok ninakuja hapo muda si mrefu” akasema Mathew na kukata simu halafu akawafuata wenzake

“ Nimeongea na Eva,amesema nimfuate katika baa yake ananisubiri.Nina hakika kwa Eva lazima kuna jambo nitalipata.Yule ana siri nyingi sana za watu wengi.Anitha jiandae twende,Noah utabaki na Dr Michael.” Akasema Mathew halafu akaingia chumbani kwake kujiandaa kisha akamfuata Dr Michale aliyekuwa amejiinamia sebuleni

“ Dr Michael ninatoka kidogo kuna sehemu ninahitaji kwenda ,nitarejea baada ya muda si mrefu sana.kama jamaa wakipiga simu utanifahamisha nini wamesema” akasema Mathew.Dr Michael akaonyesha wasi wasi

“ sasa itakuaje jamaa wakipiga simu na haujarejea? Akauliza Dr Michael.

“ Yupo Noah na chochote watakachosema atanifahamisha.Usihofu kitu Dr Michael kila kitu kitakwenda vizuri.Niamini ninachokwambia tutampata mkeo” Akasema Mathew halafu akaongozana na Anitha wakatoka na kuingia garini safari ya kuelekea kwa Eva ikaanza..

“ Mathew umenifurahisha sana leo,hukuwahi kuniambia kama uliwahi kufanya kazi baa.” Akasema Anitha Mathew akatabasamu na kusema

“ Yah ! hakukuwa na ulazima wowote wa kukueleza.Hiyo ni historia yangu ya zamani sana ambayo nimekwisha isahau.” Akasema Mathew

“ Huyu Eva,una hakika anaweza akatusaidia kupata taarifa za kanali Adolf? Akauliza Anitha

“ Nina uhakika asilimia mia moja .Kama anazo taarifa zozote za kumuhusu Kanali adolf basi atanipatia.Hakuna namna tnayoweza kufanya uchunguzi wa mwili wa Dr flora bila ya kumtumia Adolf.Ile ni hospitali ya kijeshi kwa hiyo kuingia pale na kufanya tunachokitaka si kazi rahisi ingawa tunaweza kufanya hivyo lakini hatuna muda wa kutosha hivyo inatulazimu kutafuta njia ya mkato ya kuweza kulifanikisha suala hili” akasema Mathew

“ na vipi kuhusiana na Team SC41? Bado hujatupa maelekezo yoyote ya nini kinaendelea na nini tufanye.”

“ kwa sasa tunasubiri maelekezo atakayopewa Dr Michael na ndipo tutajua nini cha kufanya.Watu hawa ni hatari kwa hiyo tunatakiwa kuwaendea kwa tahadhari kubwa sana.” Akasema Mathew

“ Mauaji ya Edson ,yanahusiana vipi na Team SC41? Usinielewe vibaya Mathew ila ninauliza hivyo kwa sababu naona kama vile tumehama katika kazi yetu ya msingi na kwa sasa tumehamia kwa team SC41” akauliza Anitha.Mathew akatabasamu na kusema

“ Bado hatujatoka katika shughuli yetu ya msingi Anitha.Bado tunaendelea kuchunguza kifo cha Edson lakini team SC41 wameingia katikati ya uchunguzi wetu baada ya kuonekana nyumbani kwa peniela hivyo lazima tuwachunguze.Tunachunguza Peniela ana mahusiano gani na Team SC41? Tukifahamu mahusiano yao tutajaribu kuangalia kama kuna muunganiko wowote kati ya mauaji ya Edson na Team Sc41” akasema Mathew.

“ Kwa nini tusimchunguze peniela moja kwa moja ili tufahamu mahusianoyake na Team Sc41? Akauliza Anitha

“ Peniela kuna namna yake ya kumchunguza.Tutamfanyia uchunguzi tu lakini ngojakwanza tushughulike na masuala mawili yaliyoko mbele yetu kwanza halafu tutarejea kwa Penny” akasema Mathew.Wakaende

lea na maongezi mengine hadi walipofika katika baa inayomilikiwa na Eva mwabukuku.Mathew akatabasamu baada ya kuiona tena baa ile.

“ Imebadilika sana baa hii.Imeboreshwa mno.” Akawaza huku akitabasamu.Alikumbuka mbali sana.

“ Ndani ya baa hii nimeshuhudia mambo mengi sana yakifanyika na mengi yakiwa ni ya aibu hata kuyasimulia” akawaza huku akifungua mlango na kushuka akampigia simu Eva akamfahamisha kwamba tayari amekwisha fika.Baada ya dakika tatu Eva akatokea.Alikuwa ni mwanamma mwenye umbo la kuvutia mno.Wakakumbatiana kwa furaha ya kutoona kwa muda mrefu

“ Ouh Mathew,karibu sana.” Akasema Eva.Mathew akamtambulisha Anitha kwa Eva halafu wakaongozana kuelekea ndani Anitha akakaribishwa katika meza ya pembeni kabisa akapewa muhudumu wa kumuhudumia,Mathew na Eva wakaelekea ofisini..

“ Mathew siwezi kukuficha nimefurahi sana kukuona tena.Wewe ni mmoja wa watu ambao nilihitaji sana kuwaona.Nimefurahi sana kwa kweli.Umenawiri mno inaonekana mambo yako si mabaya siku hizi” akasema Eva

“ hata mimi nimefurahi sana kukuona tena stone lady.Hata baada ya miaka kadhaa kupita lakini bado umenawiri na unazidi kupendeza.Hongera sana naona baa yetu inaendelea vizuri,imeboreshwa mno siku hizi” akasema Mathew

“ Kwa kweli ninamshukuru sana Mungu kwani ninaendelea vizuri sana na ndiyo maana unaona mabadiliko makubwa.” Akasema Eva

“ Eva nina mambo mengi mno ambayo nahitaji kuongea nawe lakini itahitajika siku nzima.Kwa jioni hii nimekuja kwako ninahitaji msaada wako.” Akasema Mathew

“ Karibu sana Mathew.Hapa kwangu umefika na nitakusaidia chochote unachotaka” akasema Eva

”Nafurahi kusikia hivyo “ akasema Mathew

“ Ni msaada gani unauhitaji Mathew “ akauliza Eva

“ Kuna mwili wa mtu ambao nahitaji kuufanyia uchunguzi kujua sababu za kifo chake.Mwili huo uko katika hospitali kuu ya jeshi na kama unavyojua mahala pale hapaingiliki kirahisi na kuingia pale kwa nguvu unakuwa umetangaza mgogoro na jeshi.Nahitaji kutumia njia rahisi isiyokuwana tatizo wala kuniingiza katika mgogoro wa aina yoyote na chombo hiki cha usalama” akasema Mathew

“ Nimefuatilia nimegundua kwamba kanali Adolf ndiye daktari mkuu wa ile hospitali kwa hiyo ninataka kumtumia yeye.Nimekuja kwako kwa kuwa wewe unawafahamu watu wengi,una siri za watu wengi hasa hawa wakubwa kwa hiyo ninahitaji kupata taarifa Fulani ya kanali Adolf ambayo ninaweza kuitumia kumlazimisha afanye kazi ninayoihitaji ya kuifanyia uchunguzi maiti hiyo.” Akasema Mathew

“ Mathew natamani sana kukusaidia kwa hilo lakini nasikitika kwamba sina taarifa zozote za kumhusu Kanali Adolf” akasema Eva

“ Eva nimekuja kwako kwa kuwa ninafahamu wewe hukosi kitu chochote cha kunisaidia.Tafadhali naomba unisaidie ni muhimu mno kwangu.Please Eva don’t shut me down on this.” Akaomba Mathew.Eva akainama akafikri kidogo kisha akasema

“Mathew wewe ni mtu wangu wa karibu sana.Tumefanya kazi pamoja na tumesaidiana katika mambo mengi kwa hiyo nitakusaidia lakini kwa sharti moja tu.”

“ Sharti gani Eva?

“Kuna kazi ambayo na mimi nitaomba unisaidie”

“ usijali Eva,niko tayari kukusaidia katika kazi hiyo .I give you my word.Tafadhali nisaidie kwanza katika hili”akasema Mathew

“ Ok Mathew nitakusaidia.Kanali Adolf siku hizi hafiki tena hapal,Lakini pamoja na kukata kabisa mguu baada ya mambo yake kuanza kwenda vizuri ninafahamu mambo yake mengi.Moja ninalolifahamu ambalo watu wengi hawalifahamu ni kwamba Kanali Adolf ni mshirikina wa kutupwa na Ili mambo yake yaende vizuri alikwenda kwa mganga na akaambiwa kwamba atafute viungo vya mlemavu wa ngozi.Binti mdogo wa miaka kumi na mitano alitolewa mkoani Geita akaletwa hapa Dar es salaam,akachinjwa na kuchukuliwa viungo vyake na kisha akazikwa katika nyumba yake mpya aliyohamia hivi sasa.Mahala alipozikwa kumepandwa mnazi.Ninayafahamu madhambi yake mengi lakini hilo tu linaweza kumfanya akafanya kila unachokitaka.Mathew nimekwambia siri hii kwa sababu wewe ni mtu wangu wa karibu na ninafahamu umekuja kwangu unahitaji mno msaada.Sasa na mimi ninaomba nikwambie kazi ninayohitaji unisaidie”

“ Sema Eva ni kazi gani unahitaji msaada?

“ Kuna msichana mmoja ambaye amepotea katika mazingira ya kutatanisha sana na mpaka sasa hajulikani alipo.” Akasema Eva.Mathew akatabasamu na kumtania

“ siku hizi umeanza kufanya kazi za polisi Eva? Kutafuta watu waliopotea ni kazi ya jeshi la polisi.” Akasema Mathew

“ Si hivyo Mathew,suala hili liko tofauti.Msichana huyo anaitwa Sabina .Alikuwa akija hapa mara kwa mara akiwa na mzee mmoja hivi aliyekuwa akifanya biashara.Mzee Yule alifariki katika mazingira ya kutatanisha sana na baada ya wiki moja Sabina akapotea.Hakukuwa na taarifa zozote za kupotea kwake.Jana nilipigiwa simu na namba ngeni kabisa nikapokea nikaisikia sauti ya Sabina.Alikuwa akilia na kuniambia kwamba nimsaidie kumuokoa amefungiwa ndani ya chumba kwa miezi saba sasa.Nikamuuliza yuko wapi na ni akina nani waliomfungia ndani ya chumba hicho akaniambia kwamba ametekwa na watu wasiojulikana .Kabla hajaendelea kunieleza zaidi nikasikia amenyang’anywa simu ikazimwa.Sifahamu yuko wapi na kwa nini amekamatwa na watu hao waliomfungia ndani kwa kipindi chote hicho.Nimechang

anyikiwa na sijui ni namna gani nitaweza kumuokoa kwa sababu sielewi yuko wapi .Laiti ningefahamu yuko wapi ingekuwa rahisi kidogo lakini sifahamu mahala aliko na sikuona mtu mwingine wa kumshirikisha katika suala hili ambaye anaweza kunisaidia..Uliponipigia simu nilimshukuru Mungu sana.Mathew please help me I need to save that girl.Najua kuna sababu iliyopelekea msichana Yule akakamatwa na kufungiwa ndani.We need to find her” akasema Eva

“ Ok Eva,nakuahidi nitafanya kila linalowezekana kumtafuta msichana huyo na kumpata ila kwa sasa naomba unisaidie katika suala hili nililokwambia’”

“ Nimekwisha kusaidia Mathew kama ulivyokuwa ukihitaji.Nimekupa tarifa ambayo itamfanya Adolf atii kila utakachomwambia”

“ Nashukuru sana kwa hilo Eva lakini bado naomba unisadie tena kitu kingine”

“Kitu gani Mathew? Akauliza Eva

“ Natumai una mawasiliano na Kanali Adolf.Naomba uwasiliane naye na umuombe mkutane.Najua kwako wewe hawezi kukataa.Mimi kum,pata kwa sasa itanichukua muda mrefu kidogo”

Eva akainama akafikiri kidogo halafu akachukua simu yakena kuzitafuta namba za simu za Kanali Adolf akampigia

“Hallow Adolf,habari yako? Akasema Eva baada ya Kanali Adolf kupokea simu

“ ouh Eva.habari za siku nyingi?

“ habari za siku nyingi nzuri sana,umenikimbia siku hizi.Toka mambo yako yalipokuwa mazuri hata sisi watu wako wa zamani hututaki tena”

“ Si hivyo Eva.Unajua nimetingwa sana na kazi siku hizi na ndiyo maana umeona sifiki mara kwa mara hapo kwako” akasema kanali Adolf

‘ Kanali adolf uko wapi mida hii?

“ kwa sasa niko barabarani kuna sehemu naelekea “

“ Ok ninahitaji kukuona nina shida Fulani”

“ una shida gani we mtoto? Akauliza kanali Adolf

“ Ni shida ambayo siwezi kukueleza simuni.Tafadhali naomba uje hapa ofisini kwangu au nielekeze ulipo nikufuate .Ni muhimu sana”

Kanali Adolf akakaa kimya kidogo halafu akasemahttp://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“ Ok ! siko mbali sana na hapo ofisini kwako ,nisubiri kama dakika tano hivi nitakuwa hapo lakini sintakaa sana kuna mahala ninahitajika usiku wa leo” akasema Kanali Adolf

‘ Nashukuru sana Adolf” akasema Eva na kukata simu.

“ Ndani ya dakika tano Adolf atakuwa hapa.sasa niambie utanisaidiaje kumpata msichana Yule ? akauliza Eva

“ Usihofu kuhusu kumpata huyo msichana Eva.Mimi na timu yangu tutampata tu.Tukishamaliza suala hili tutageukia suala lako.I give you my word Eva tutampata huyo msichana aliyepotea” akasema Mathew

“Nitashukuru sana kama utanisaidia kumpata.Msichana Yule anahitaji msaada na hana mtu mwingine wa kumkimbilia zaidi yangu.”akasema Eva na kuchungulia dirishani akaliona gari la kanali Adolf likiingia katika maegesho

“ kanali adolf ameingia kama alivyoahidi.Ni kweli hakuwa mbali na hapa” akasema Eva

“ Ahsante sana Eva.”akasema

Baada ya kama dakika mbili hivi mlango ukagongwa.

“ Its him”akasema Eva huku akiinuka na kwenda kuufungua mlango

“ Ouh Adolf ! karibu sana.” Akasema Eva kwa furaha

“ Ahsante sana Eva.Habari za siku nyingi? naona umefanya mabadiliko makubwa sana “

“ Ndiyo Adolf ni muhimu kufanya mabadiliko ya mara kwa mara.Umepotelea wapi siku hizi?

“ Kazi zimekuwa nyingi sana Eva ndiyo maana unaniona niko kimya sana,lakini hapa ni nyumbani na muda wowote nitakaopata nafasi nitakuja”

“ Ok vizuri.karibu sana.Adolf huyu ni rafiki yangu anaitwa Mathew.Mathew huyu ni kanali Adolf daktari mkuu wa hospitali kuu ya jeshi” Eva akafanya utambulisho.Mathew na Adolf wakapeana mikono.

“ Ndiyo Eva nimefika kama ulivyokuwa umenitaka.Nieleze shida yako kwa sababu kuna mahala ninataka kuwahi”akasema kanali Adolf

“ kanali Adolf,mimi sina shida lakini kuna huyu ndugu yangu hapa ndiye mwenye shida na wewe ya muhimu sana.Nitawaacha ninyi wawili muongee na mkisha malizana nitarejea”akasema Eva huku akiinuka na kutoka .Kanali adolf akabaki akishangaa.

“ halow Mathew,natumai hatujawahi kuonana” akasema Adolf

“Ndiyo kanali Adolf hii ni mara yetu ya kwanza tunaonana”akasema Mathew.

“ Una tatizo gani kijana wangu? Akauliza kanali Adolf

“ kanali Adolf nina tatizo moja ambalo linahitaji sana msaada wako.”

“Sema tu kijana wangu kama litakuwa ndani ya uwezo wangu nitakusaidia”

“ Kanali Adolf,kwa sasa nchi iko katika maombolezo ya kifo cha mke wa rais.Tunaambiwa kwamba kifo chake kilikuwa cha ghafla sana.Wewe kama daktari mkuu wa hospitali iliyothibitisha kifo chake unaweza ukaniambia kwamba nini sababu ya kifo chake?

Kanali Adolf akastushwa sana na swali lile akamkazia macho Mathew

“Kijana mbona sikuelewi? Wewe ni nani? Umetokea wapi?Unahusiana vipi na familia ya rais hata uniulize swali kama hilo?Wanaopaswa kuniuliza swali kaam hilo ni wafiwa na si wewe” Akauliza adolf ambaye alionekana kukerwa na swali lile

“ Naomba usikasirike kanal Adolf,si lazima niwe natokea familia ya rais ndiyo niulize swali kama hili.kama unafahamu kilichosababisha kifo cha Dr Flora tafadhali naomba uniambie”akasema Mathew.Kanali Adolf akainuka

“ I’m not having conversation with idiots”akasema na kukisukuma kiti nyuma ili aweze kupata nafasi ya kuondoka.Mathew akamtolea bastora na kumuelekezea

“kaa chini kanali Adolf..!!akasema kwa ukali Mathew.Adolf hakuogopa akacheka kidogo kana kwamba alikuwa akimdharau Mathew

“ Eva kanifanyia mambo gani haya? Mimi mtu wa kunikutanisha na wahuni kama huyu” akawaza

“ Sema unachotaka kusema kijana,usidhani nitaogopa hiyo bastora.Mimi ni kanali wa jeshi na huwezi kujua nimepitia mambo mangapi hadi hapa nilipofika” akajitapa

“ Nafahamu wewe ni kanali wa jeshi na umepitia mambo mengi sana lakini kuanzia sasa utakaa na kunisikia ninachokwambia” akasema Mathew

“ hahaahaa..vijana wa siku hizi njaa zitawaua.kama sitaki utanifanya nini?

“ I’ll destoy you “ akasema Mathew.Adolf akacheka na kusema

“ Nimekwisha zizoea kauli kama hizo za kihuni.Huna uwezo wa kunitisha mtu kama mimi.Ninaondoka na huna uwezo wa kunifanya chochote na ninakutuma nenda mwambie huyo mwanamke kahaba aliyenileta hapa kwamba mimi si mtu wa kufanyiwa mchezo na wahuni” akasema kanali Adolf huku akipiga hatua kuelekea mlango

“ Stop there Adolf” akapaaza sauti Mathew.Adolf akasimama.

“ Najua huogopi silaha lakini ukijaribu kutoa mguu wako nje ya huo mlango kesho asubuhi vichwa vya habari vya magazeti yote nchini vitapambwa na habari moja tu,ya wewe kumuua Albino ”

Kanali Adolf aligeuka ghafla kama mtu aliyepandwa na wazimu akamtazama Mathew kwa macho makali sana.Uso wake ukakunjamana kwa hasira

“ Kijana anaomba usinijaribu.Hunifahamu mimi ni nani.Nitakuondoa katika hii dunia hata nzi wasifahamu nimekupeleka wapi” akasema Adolf kwa hasira

“ Adolf huwezi kunifanya kitu.Ninakufahamu zaidi ya unavyojifahamu .Ninafahamu kila kitu unachokifanya na kubwa zaidi likiwa ni hili la kumuua mlemavu wa ngozi.Kama hutakuwa tayari kunisikiliza ninachotaka kukwambia usiku huu nitaongozana na kikosi cha askari na waandishi wa habari na kwenda kuwaonyesha mahala ulikofukia mwili wa binti Albino uliyemuiba toka Geita.Sitaki mambo haya yafike huko.”akasema Mathew.Adolf alihisi miguu ikimuisha nguvu akatoa kitambaa akafuta jasho,halafu akaketi kitini.

“ Kijana unatakiwa uwe makini sana na unayoyasema.Una ushahidi wa hayo yote unayoyasema? Ninaweza kukufungulia mashitaka kwa kunikashifu.Mimi kanali Adolf ninaweza kweli kuua mlemavu wa ngozi?

“ Nina kila ushahidi wa kukutia hatiani Adolf.Ninawafahamu vijana uliowatuma kwenda kumteka Albino Geita,ninamfahamu hata mganga aliyekuagiza ufanye hivyo.”akasema Mathew kwa kujiamini

“ Unataka nini kijana? Shida yako ni nini? Adolf akauliza taratibu huku akiendelea kujifuta jasho

“ kanali Adolf naomba tusiyafanye mambo haya yawe makubwa.Naomba unisikilze kwa makini.Mke wa rais Dr Flora Joshua alipofariki aliletwa hospitalini kwenu.Nani aliwazuia msifanye uchunguzi kubaini kifo chake? Mathew akauliza.Adolf hakujibu kitu akabaki kimya

“ kanali Adolf naomba unijibu.Mlipokea simu mkizuiwa kufanya chochote katika mwili wa Dr Flora.Ni nani aliyewapigia simu kuwaambai kwamba msimfanyie uchunguzi?

“ Hiyo ni amri iliyotoka kwa uongozi wa juu”

“ Uongozi wa juu ni nani.Nahitaji jina!!

“ Nilitaarifiwa na katibu wa rais”




ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog